Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Sehemu ya kumi na mbili----12



ILIPOISHIA:

Alikuwa ni msichana mzuri sana, upande wa nyuma alikuwa amejazia huku kiuno chake kikiwa kimegawanyika, kama nyigu ambao kule kijijini tulikuwa tukiwaogopa kutokana na sumu yao wanapokung’ata.

Suruali ya jeans aliyovaa, ililifanya umbo lake lijichonge vizuri, ghafla akageuka, akanibamba nikiwa namtazama kwa nyuma, nikazidi kujisikia aibu.

SASA ENDELEA…

“Mbona unaniangalia hivyo?”

“Mimi?” Nilijifanya kuvunga, akanisogelea na kunipiga kakibao kepesi begani huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye kwenye uso wake. Na mimi nikawa nacheka huku aibu zikiwa zimenijaa.”

“Dar es Salaam unaishi sehemu gani?” aliniuliza swali ambalo lilikuwa gumu sana kulijibu kwani ukweli ni kwamba sikuwa naijua Dar wala sikuwahi kufika kabla. Nikawa nababaika mwenyewe, akajiongeza na kuniuliza:

“Kwani hii ndiyo mara yako ya kwanza kufika Dar?”

“Ndiyo,” nilijibu harakaharaka kwa sababu alikuwa amenipunguzia sana kazi ya kumjibu. Akaniambia kwamba yeye anaishi na wazazi wake Kijitonyama. Akaniambia kwamba alikuwa amemaliza chuo akisomea uhasibu na alikuwa anatoka Mbeya kuwasalimu bibi na babu yake wa upande wa mama.

“Wanaishi Mbeya sehemu gani?” nilimuuliza, akaniambia wanaishi Katumba, njia panda ya kwenda Mwakaleli. Maeneo hayo sikuwa nimewahi kufika zaidi ya kusikia tu kwa watu, nikawa natingisha kichwa kumkubalia. Akaendelea kunieleza kwamba mama yake alikuwa Mnyakyusa lakini baba yake alikuwa ni mtu kutoka Mkoa wa Pwani ingawa hakunieleza ni kabila gani.

Hatimaye dakika kumi ziliisha, dereva akaanza kupiga honi akitupa ishara kwamba muda wa kuingia kwenye basi umefika. Kwa hizo dakika chache nilizokaa na msichana huyo, niligundua kwamba alikuwa mcheshi, mchangamfu na asiye na maringo kama walivyo wasichana wengi warembo kama yeye.

“Lakini hujaniambia unaitwa nani.”

“Unataka kujua jina langu?”

“Ndiyo.”

“Sitaki,” alisema huku akinipiga tena begani, akaanza kukimbia kuelekea kwenye basi. Sikuelewa kitendo hicho kilikuwa na maana gani, wakati anakimbia nilishuhudua kitu kingine ambacho kiliusisimua sana moyo wangu, mpaka nikawa najiuliza zile hisia nilizokuwa nazisikia kwa wakati huo zilikuwa na maana gani?

Kwa kifupi nilijisikia raha sana kufahamiana na msichana huyo. Niliendelea kumtazama akikimbia mpaka alipofika kwenye ngazi za kupanga kwenye basi, akageuka na kunitazama kisha akapanda ngazi. Na mimi nilitembea harakaharaka huku nikiendelea kuchekacheka mwenyewe, mkononi nikiwa na kopo la soda ambayo nilikua nimeinywa nusu.

Nilipopanda na kuingia ndani ya gari, ndugu zangu wote walishangaa kuniona nikiwa na soda ya kopo, tena nikinywa kwa mrija.

Niliwaona wote walivyomeza mate, wakawa wanaulizana nimeipata wapi soda hiyo? Sikuwajali kwa sababu bado nilikuwa na hasira nao, nikakaa kwenye siti yangu, nikageuka na kumtazama yule msichana ambaye mpaka muda huo hakuwa amenitajia jina lake, nikashtuka tena kugundua kwamba kumbe alikuwa ametulia akinitazama kila nilichokuwa nakifanya.

Macho yangu na yake yalipogongana, aliachia tabasamu hafifu halafu eti na yeye akakwepesha macho yake kwa aibu, yaani mwanzo mimi ndiyo nilikuwa nakwepesha macho yangu lakini ghafla na yeye alianza kukwepesha macho yake kwa aibu. Dereva aliondoa gari na safari ikaendelea.

Safari hii umakini ulikuwa ukinipungua sana kichwani mwangu kwani mara kwa mara tulikuwa tukitazamana na yule msichana na kuishia kuchekacheka tu. Nashukuru hakuna jambo lolote baya lililotokea mpaka tulipoanza kuingia mjini.

Tulipofika Kibaha, gari lilisimama na yule abiria aliyekuwa amekaa pembeni yangu, alisimama na kushuka, harakaharaka nikamuona yule msichana akikusanya kila kitu chake na kuja kukaa pembeni yangu. Aliponisogelea tu, nilianza tena kusikia harufu ya manukato aliyojipulizia, ambayo kiukweli yalinivutia sana.

Akakaa pembeni yangu na kuniegamia kimtindo kabla ya kujiweka vizuri kwenye siti yake.

“Yule niliyekaa naye hata stori hana, muda wote analala tu bora nikae na wewe,” alisema huku akinipigapiga begani, nikawa natabasamu tu kwani kiukweli hata mimi nilikuwa napenda kukaa naye siti moja.

“Ulisema unataka kujua jina langu?” alianzisha mazungumzo, niikamjibu kwa kutingisha kichwa, akaniambia ananipa mtihani nitafute mwenyewe jina lake. Kiufupi ni kwamba, kwa muda mfupi tu niliokaa naye, alionesha kupenda sana urafiki wetu uendelee, jambo ambalo hata mimi nilikuwa nalipenda ingawa mara kwa mara nilikuwa najishtukia.

Hata nilipokuwa nacheka, sikuwa napenda ayaone meno yangu kwani ya kwake yalikuwa meupe sana na masafi lakini kwangu mimi, hata sikuwa nakumbuka mara ya mwisho kupiga mswaki ni lini, si unajua tena maisha ya kijijini.

“Una simu?” aliniuliza swali ambalo lilinifanya nijisikie tena aibu. Sikuwa na simu, sikuwahi kumiliki wala sikuwa najua namna ya kuitumia, nikawa natingisha kichwa kukataa, akaniambia alikuwa na simu mbili lakini hiyo nyingine hakuwa akiitumia kwa sababu ilikuwa ya kizamani.

“Basi nipe mimi,” nilisema kwa utani kwani nilijua ni jambo ambalo haliwezekani, akacheka na kufungua kibegi chake kidogo, akatoa simu ndogo aina ya Nokia ya tochi na kunipa.

“Chukua utakuwa unatumia,” alisema. Nikapigwa na butwaa nikiwa ni kama siamini. Kuna wakati nilihisi kwamba pengine alikuwa akinitania lakini mwenyewe alisisitiza kwamba ni kweli amenipa. Muda huo, tayari gari lilikuwa limeshawasili Ubungo, sikuwa napajua zaidi ya kusikia tu watu wakisema hapo ndiyo ubungo.

Tayari giza lilishaanza kuingia, taa nyingi zilizokuwa zinawaka kila upande zikanifanya nijihisi kama nilikuwa kwenye ndoto.

Waliosema mjini kuzuri hawakukosea, Dar ilikuwa na tofauti kubwa sana na kule kijijini nilikozaliwa na kukulia, kila kitu kilikuwa kigeni kwangu. Wakati nikiendelea kushangaashangaa, nilisikia mama akiniambia kwamba natakiwa kuwa makini kuchukua mizigo iliyokuwa imewekwa kwenye buti.

Harakaharaka nikateremka na abiria wengine, hata sikukumbuka nilipotezana saa ngapi na yule dada, ushamba wa mjini ulinipa mchecheto mkubwa ndani ya moyo wangu, nikaenda mpaka kwenye buti nikiwa na wale ndugu zangu wengine ambao nao walikuwa wakishangaashangaa, tukafanikiwa kushusha mizigo yetu yote na kuiweka pembeni.

“Twendeni nilisikia sauti ya baba akizungumza, kugeuka pembeni, sote tulipigwa na butwaa kumuona baba akiwa anafungua milango ya teksi. Hakuna aliyejua baba alifika saa ngapi Dar es Salaam kwa sababu kama aliweza mpaka kuzungumza na dereva wa teksi na kukaa pale wakitusubiri, maana yake ni kwamba aliwahi sana kufika.

“Unajua wewe huna akili kabisa,” baba alianza kunifokea baada ya kumaliza kupakiza mizigo kwenye teksi, nikawa nashangaa kwa nini baba ananiambia maneno hayo.

“Yule uliyekuwa umekaa naye kwenye basi ni nani?”

“Ni rafiki yangu.”

“Unamjua wewe? Na hicho alichokupa una uhakika gani kama ni simu? Ujinga wako utaiponza familianzima,” alisema maneno ambayo yalinishangaza sana.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na tatu_______13




ILIPOISHIA:

“YULE uliyekuwa umekaa naye kwenye basi ni nani?”

“Ni rafiki yangu.”

“Unamjua wewe? Na hicho alichokupa una uhakika gani kama ni simu? Ujinga wako utaiponza familia nzima,” alisema maneno ambayo yalinishangaza sana.

SASA ENDELEA…

“NI simu baba!”

“Sitaki kukuona naye tena na hiyo simu lete,” alisema huku akinipokonya ile simu. Nilizidi kumshangaa baba, nikaona kama anataka kunikosesha bahati ya bure. Kwa mara ya kwanza nilijikuta nikipandwa sana na hasira juu yake. Hata hivyo sikuwa na cha kufanya, tuliondoka Ubungo huku kila mmoja ndani ya gari tulilokuwa tumepanda, akiwa anashangaa mandhari ya Jiji la Dar es Salaam.

Japokuwa tulikuwa tumebanana sana kwenye ile teksi kwa sababu ya wingi wetu, kila mmoja alikuwa akitamani yeye ndiyo akae dirishani. Tulikatiza mitaa mingi na hatimaye tukaiacha barabara ya lami na kuingia kwenye barabara ya vumbi. Baada ya muda, tulitokeza kwenye nyumba moja nzurinzuri, baba akawa wa kwanza kuteremka kwenye gari, na sisi wengine tukafuatia na kuanza kushusha mizigo.

Wakati tukiendelea kushusha mizigo, geti kubwa lilifunguliwa, mwanaume wa makamo aliyeonekana wanafahamiana vizuri na baba, alimuita kwa jina lake, baba akaacha kila alichokuwa anakifanya na kwenda kumkumbatia, wote wawili wakionyesha kuwa na furaha kubwa kwa kukutana.

“Hii ndiyo familia yangu, shemeji yako na watoto,” alisema baba huku akituonyeshea sisi, akatusogelea na kusalimiana na mama, kisha akaanza kutupa mikono, mmoja baada ya mwingine huku akituuliza majina.

“Naitwa Togolai,” nilimwambia aliponifikia, akanitazama usoni.

“Wewe ndiyo Togo?”

“Ndiyo,” nilisema huku na mimi nikiachia tabasamu hafifu kwa sababu na yeye alikuwa akitabasamu. Baada ya hapo, alitukaribisha ndani, wakati tunabeba mizigo kuingiza, walikuja watu wengine watatu, wasichana wawili na mwanaume mmoja ambao kwa kuwatazama tu, walionyesha dhahiri kwamba ni wanaye kwa jinsi walivyokuwa wamefanana na kupishana umri.

Mkubwa alikuwa wa kike, aliyemfuatia alikuwa wa kiume na mdogo kabisa naye alikuwa wa kike. Hawakupishana sana umri, yule mkubwa alikuwa akilinganalingana na dada yetu Sabina.

Tofauti yao na sisi, ilikuwa kubwa sana, kuanzia jinsi walivyokuwa wamevaa na mpaka muonekano wa miili yao. Walikuwa na mwonekano wa kimjini haswaa wakati sisi tulikuwa na mwonekano wa ‘bushi’, kuanzia sura zetu, mavazi yetu mpaka jinsi tulivyokuwa tukizungumza.

Walitukaribisha mpaka ndani, tukaenda kukaa kwenye sebule kubwa na ya kisasa. Japokuwa tulikuwa wengi, lakini wote tulitosha kwenye masofa ya kisasa. Ushamba wetu uliendelea kujidhihirisha mle ndani kwani tulikuwa tukishangaa kila kitu, kuanzia taa za umeme, feni, mapazia, kuta zilizokuwa zimenakshiwa kwa rangi nzuri na marumaru, kila kitu kilikuwa kigeni kwetu.

Tuliandaliwa chakula na mama wa familia ile ambaye alikuwa mchangamfu na anayependeza kimwonekano kuliko mama yetu. Kilikuwa ni chakula kizuri mno, ambacho ama kwa hakika tulikifurahia. Tukala mpaka kumaliza, mwenzetu mmoja akawa anataka kulamba bakuli la mboga, mama akamkata jicho la ukali na kumfanya aogope.

Baada ya chakula, tulianza kushangaa runinga maana kule hakukuwa kuangalia, ilikuwa ni mara yetu ya kwanza kuona runinga lakini achilia mbali runinga ya kawaida, ile iliyokuwa mle ndani ilikuwa kubwa sana, tena ya kisasa kabisa iliyounganishwa na spika ndogo za kisasa zilizokuwa zinatoa mdundo mzito.

Mpaka muda wa kulala unafika, hakuna aliyekuwa tayari kubanduka pale sebuleni, kila mmoja alikuwa anatamani kama akeshe palepale akitazama vipindi vizuri vilivyokuwa vinaonyeshwa. Ilibidi mama atumie ukali, kwani kwa muda huo baba ambaye ndiyo tunayemwogopa sana, alikuwa nje kwa mazungumzo na yule rafiki yake.

Kabla ya kwenda kulala, ilibidi kwanza tuende kuoga mmojammoja kuondoa vumbi na uchafu tuliotoka nao kijijini. Mimi ndiye niliyekuwa wa mwisho kwenda kuoga ambapo nilipoingia kwenye bafu hilo la kisasa, nilishangazwa kwa jinsi lilivyokuwa safi. Yaani hata kama ningeambiwa nikae mle ndani kwa siku nzima na kuletewa chakula nilie humohumo ningekubali kwa sababu ya usafi wake.

Kule kijijini tulizoea kwenda kuoga mtoni, wakati mwingine kuogelea lakini mjini mambo yalikuwa tofauti. Nilivua nguo zangu na kuzikung’uta kwanza kwa sababu zilikuwa na vumbi jingi. Kwa bahati mbaya, wakati nikiikung’uta suruali niliyokuwa nimevaa, nilisahau kwamba ile dawa niliyopewa na baba nilikuwa nimeiweka kwenye mfuko, nilipokung’uta ikadondoka chini na kwa kuwa choo na bafu vilikuwa vimeungana, yaani upande mmoja kuna bafu na upande wa pili kuna choo, iliteleza mpaka kwenye sinki la choo.

*(Simulizi za Majonzi)

Kutokana na umuhimu wa dawa hiyo, ilibidi niende kuiokota haraka lakini kabla sijafanya hivyo, niliitundika ile suruali kwenye bomba lililokuwa pembeni. Nikashtuka kuona maji yakianza kumwagika, yakaisomba ile dawa na kuipeleka kwenye shimo la choo, ikapotelea kwenye bomba la kutolea maji machafu.

Nilishangaa sana yale maji nani ameyafugulia lakini nilipotazama vizuri, niligundua kuwa kumbe pale nilipokuwa nimetundika suruali ile ilikuwa ni koki ya bomba ambayo kwa jinsi ilivyokuwa ya kisasa nilishindwa kuitambua.

“Ayaaa!” nilisema kwa sauti kubwa kwa sababu sikutegemea kabisa kile kilichotokea na hata sikujua nitamwambia nini baba kwa sababu wakati ananipa, alinisisitiza kuitunza sana dawa hiyo. Ilibidi nifunge maji kwanza, nikaegamia kwenye marumaru za bafuni, nikiwa na mawazo mengi juu ya nini cha kufanya.

Mwisho nilipiga moyo konde na kujiambia kwamba nitaenda kumweleza baba hali halisi na kwa sababu ananipenda na ananiamini. Nilimalizia kuvua nguo, nikawa nataka nioge maji kwa kutumia bomba linalomwaga maji kama mvua, kama nilivyokuwa nimeona kwenye runinga muda mfupi uliopita.

Kwa umakini mkubwa nilichunguza mahali ilipo koki yake, nilipoiona niliifungua, maji yakaanza kumwagika, harakaharaka nikaingia katikati yake na kuanza kujimwagia.

Ilibidi nifumbe macho wakati najipaka sabuni lakini taratibu nilianza kuona maji yanaanza kuwa ya uvuguvugu kidogo halafu yanakuwa kama mazito kidogo na yana chumvichumvi. Nikawa nikipaka sabuni haiishi mwilini, ikabidi nisogeze kichwa pembeni kidogo na kufumbua macho.

“Mungu wangu,” nilipiga kelele kwa nguvu baada ya kugundua kwamba kumbe kile nilichokuwa nikiamini kwamba ni maji, zilikuwa ni damu zikimwagika kama maji. Uda mfupi baadaye tayari nilikuwa kwenye mlango wa bafuni lakini cha ajabu, licha ya kutoa loki niliyoiweka wakati nikiingia, mlango uligoma kufunguka, nikawa nagongagonga kwa nguvu huku nikiendelea kupiga kelele.

Wa kwanza kufika alikuwa ni yule msichana ambaye alionyesha kuwa ndiyo mtoto mkubwa wa yule mzee, akasukuma mlango kwa nguvu kutokea nje. Nguvu alizotumia, ukichanganya na kwamba miguu yangu ilikuwa na majimaji, nilijikuta nikiteleza na kuanguka chini kama mzigo akaingia na kupigwa na butwaa kutokana na hali aliyonikuta nayo kwani sikuwa na nguo hata moja na bado nilikuwa nikipiga mayowe ya kuomba msaada.

Alichokifanya, haraka alivua khanga aliyokuwa amejifunga juu ya gauni lake na kunirushia ili nijisitiri kisha haraka akageuka na kutoka, nikamsikia akijifungia mlango wa chumbani kwake, nadhani alijisikia aibu sana kwa hali aliyonikuta nayo.

Cha ajabu sasa, wakati nageuka kutazama kule zile damu zilikokuwa zikimwagika, nilishangaa kuona kinachotoka si damu bali maji na wala hakuna dalili yoyote ya damu. Tayari kaka zangu walishafika na kunikuta nikihangaika kujifunga ile khanga niliyopewa, wakataka kujua nini kimetokea

Kelele hizo kumbe hata baba na yule mwenzake walizisikia, nao wakaja haraka kutaka kujua nini kimetokea.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na nne__________14



ILIPOISHIA:

“MUNGU wangu,” nilijisemea, mapigo ya moyo yakiwa yananienda mbio kuliko kawaida, nikiwa sijui nini kitatokea, hasa ukizingatia kwamba nilikuwa ugenini na ndiyo kwanza tulikuwa tumewasili.

SASA ENDELEA…

ALINIACHIA huku naye akionyesha kushtuka, akashuka kitandani na kuokota khanga yake, akajifunga kivivu na kunionyesha ishara kwamba niingie kwenye kabati la nguo, nilifanya hivyo haraka, nikamsikia akifungua mlango.

“Baba amesema usije ukafunga mlango mkubwa wa nje, watachelewa kuingia ndani kwani kuna kazi wanaifanya.”

“Haya poa,” nilimsikia akizungumza na mdogo wake, akashusha pumzi ndefu na kuufunga mlango, nikamsikia safari hii akifunga kwa funguo kabisa, akaja pale kabatini na kufungua mlango, akanionyesha ishara kwamba nitoke.

Sikulaza damu, nilitoka harakaharaka nikiwa kama nilivyo, na yeye akauachia ule upande wa khanga, ukadondoka chini, tukawa tunatazama kama majogoo yanayotaka kupigana. Alipiga hatua moja mbele, miili yetu ikagusana, akazungusha mikono yake kwenye shingo yangu, na mimi nikiwa sijiaminiamini, nikaukumbatia ‘mlima’ wake.

Nikiri kwamba hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuwa kwenye hali kama hiyo na nilichokihisi kwenye mwili wangu, sikuwahi kukihisi kabisa tangu napata akili zangu. Ni hapo ndipo nilipoanza kuelewa kwa nini watu wengi huwa wanayasifia sana mapenzi kwamba ni matamu kuliko asali.

Ni hapo pia ndipo nilipoelewa kwa nini watu wengine hufikia hatua hata ya kutoana roho, baada ya mmoja kugundua kwamba anatembea na mkewe au mpenzi wake. Dakika chache baadaye, nilikuwa nahema kama nataka kukata roho, ufundi wa mikono yake kuvinjari kwenye mwili wangu, ulinifanya mara kwa mara niwe natoa miguno ambayo sikuwahi kuitoa kabla.

Hata sikukumbuka nilifikaje kwenye uwanja wake wa fundi seremala, nilikuja tu kushtukia yeye yuko juu yangu nikiwa nimelala chali, huku nikiendelea kupumua kwa fujo, mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana na ‘Togolai’ akiwa anazidi kuongeza hasira kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele.

Kwa ufundi wa hali ya juu, alimuelekeza njia ya kupita, nikajikuta nikianza kuzungumza kama bubu, maneno hayatoki wala hayaeleweki, kucheka natamani lakini muda huohuo natamani kupiga chafya, ilikuwa ni hali ya ajabu mno. Safari iliendelea, mwanzo alikuwa akipiga hatua fupifupi lakini baadaye nikaanza kumuona akinogewa na kuongeza huku akitoa ukelele fulani ulioongeza raha kubwa kwenye masikio yangu.

Baadaye ilibidi tubadilishane magoli kwenye mechi ile ya kirafiki isiyo na refa wala jezi, yeye akawa anapeleka mashambulizi Kaskazini mwa uwanja na mimi napeleka Kusini.

Japokuwa hata danadana sikuwa najua kupiga na siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza, nilijitahidi kuonyesha kiwango kwa sababu nimewahi kusikia kwamba ukicheza chini ya kiwango, huwa unadharaulika mbele ya viumbe hawa.

Akaongeza mno kasi ya mashambulizi kisha akanikaba kwa nguvu shingoni kama wanavyofanya wale watu wanaopora simu au fedha, akanishikilia kwa nguvu na kunibana, na mimi nikaongeza kasi, nikajisikia hali fulani hivi nzuri sana, akazidi kunibana kisha akaniachia na kudondokea upande wa pili, jasho likiwa limemlowanisha chapachapa na mimi nikiwa hoi bin taaban, nilijikuta nikicheka mwenyewe kwa furaha.

Hakuzungumza jambo lolote kwa dakika kadhaa, baadaye aliinuka na kukaa kitandani, akawa ananitazama kama ambaye haamini kitu fulani.

“Una miaka mingapi?”

“Kwa nini unaniuliza hivyo?”

“Kwa nje unaonekana mdogo lakini wewe ni zaidi ya mwanaume,” alisema na kunikumbatia tena, akaanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu huku akiniambia kwamba ananipenda na anaomba nisimuache ila uhusiano wetu uwe wa siri.

Bado sikuwa naelewa alichokimaanisha, akaendelea na uchokozi wake na hata sijui nini kilitokea lakini muda mfupi baadaye, nilishtukia tukiwa tena dimbani, safari hii kidogo nikawa sina ugeni na uwanja pamoja na mchezo wenyewe.

Mpambano mkali uliendelea mpaka baadaye ambapo ile hali iliyotutokea mwanzo ilitokea tena, tena kwa kila mtu. Safari hii, alipoangukia upande wa pili, haukupita muda mrefu akaanza kukoroma.

Kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, harakaharaka niliinuka na kuvaa nguo zangu nikaenda kufungua mlango na kutoka huku nikinyata, nikaenda mpaka kwenye mlango wa kile chumba ambacho nitalala na ndugu yangu mmoja.

Kwa bahati nzuri, mlango haukuwa umefungwa, nikaingia mpaka ndani, tayari ndugu yangu naye alikuwa akikoroma, nikajilaza kitandani huku nikisikia uchovu wa kiwango cha juu, karibu kila sehemu kwenye mwili wangu ilikuwa inauma.

Tabasamu pana lilikuwa limechanua kwenye uso wangu, hasa kumbukumbu ya nilichotoka kukifanya ilipokuwa inanijia. Sasa na mimi nilijihisi kuwa mwanaume niliyekamilika. Bado nilikuwa siamini jinsi nilivyoweza kuuangusha mbuyu kwa shoka moja, haukupita muda mrefu nilipitiwa na usingizi.

“Motooo! Jamani moto… nakufaaaa,” sauti za mtu aliyekuwa akipiga kelele kuomba msaada, ndizo zilizonishtua kutoka kwenye usingizi mzito, nikakurupuka huku mapigo yangu ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida, nikatoka mpaka koridoni.

Sikuamini macho yangu kusikia sauti ile ilikuwa ikitoka kwenye kile chumba ambacho usiku huo mimi na yule dada tulilambishana asali. Moto ulikuwa umekolea kiasi kwamba hata sehemu ya kupita haikuwa ikionekana.

Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kufika eneo hilo kwa sababu sikumkuta mtu mwingine yeyote, nikaona nikisema niende kuwaamsha baba na mama, dada wa watu anaweza kufa bure, nikapiga moyo konde na kuukanyaga mlango ambao ulikuwa ukiwaka moto, ukaangukia ndani.

Sikujali kuhusu moshi mzito uliokuwa umetanda kwani tayari nilikuwa na uzoefu wa kucheza kwenye moshi kwani kule kijijini ilikuwa kama tunataka kwenda kupakua asali kwenye mzinga, lazima tuwashe moto kwa kutumia miti inayotoa moshi mzito. Nilibana pumzi, nikaenda mpaka pale kitandani ambapo nilimkuta akiwa ameanza kuishiwa pumzi kutokana na kuvuta moshi mwingi.

Kwa kuwa mwili wangu ulikuwa na nguvu, si unajua tena maisha ya kijijini yanakufanya uwe ‘ngangari’ kutokana na kazi ngumu, nilimbeba na kutoka naye mpaka koridoni, moto ukawa unazidi kuwaka lakini kilichonishangaza sana ni kwamba haukuwa ukisambaa kwenye vyumba vingine.

Nikiwa koridoni, mikononi nikiwa nimembeba yule dada ambaye alishapoteza fahamu, nilikutana na baba na mwenyeji wake pamoja na mama na mwenyeji wake.

“Kuna nini tena? Rahma kapatwa na nini?” aliuliza baba yake, ni hapo ndipo nilipojua kwamba kumbe jina lake anaitwa Rahma. Sikuweza kuwajibu kwa sababu walikuwa wanamuona hali aliyokuwa nayo, baba yake na baba wakanipokea na kumkimbiza mpaka sebuleni, feni zote zikawashwa.

*(Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi)

“Kumetokea nini?”

“Moto.”

“Motoo?”

“Ndiyo, chumbani kwake kunawaka moto,” nilisema huku nikishangaa kwa nini walikuwa wakiniuliza mara mbilimbili jambo ambalo lilikuwa wazi. Harakaharaka walielekea kule chumbani wakati mama yake akihangaika kumpa huduma ya kwanza lakini muda mfupi baadaye, walirudi mbiombio.

“Umesema chumbani kwake kunawaka moto?”

“Ndiyo, alikuwa anapiga kelele za kuomba msaada ndiyo nikaamka na kwenda kumsaidia, nilisema, nikaona baba na mwenyeji wake wakitazamana, sikuelewa walikuwa wanamaanisha nini. Ilibidi haraka nirudi kule chumbani kwake ili kuangalia moto umefikia wapi.

Cha ajabu, mpaka nafika mlangoni hakukuwa na moto wala dalili za moto isipokuwa mlango ulikuwa umevunjwa na nakumbuka vizuri mimi ndiye niliyeukanyaga kwa nguvu ukavunjika.

Huku nikiwa nimepigwa na butwaa, niliingia ndani ambako muda mfupi uliopita moto mkubwa ulikuwa umetanda kila sehemu lakini cha ajabu kila kitu kilikuwa sehemu yake, nikageuka huku nikiwa siamini, nikakutana na baba na mwenyeji wake ambao kumbe walikuwa nyuma yangu wakinitazama.

“Ulimaanisha chumba hiki au kingine?”

“Hikihiki, nashangaa sijui imekuwaje, kwani nyie hamjasikia kelele za kuomba msaada?”

“Mimi nimesikia kelele za mlango kuvunjwa tu, basi.”

“Mungu wangu,” nilisema kwa hofu kubwa, nikijihisi kama nipo kwenye ndoto ya kutisha.

“Na vipi kuhusu hii?” baba aliniuliza, huku akinionyeshea nguo yangu ya ndani iliyokuwa pale chini ya kitanda cha Rahma. Kumbe wakati muda ule navaa nguo zangu, niliisahau si unajua tena maisha ya kijijini kuvaa hiyo kitu hasa kwa sisi wanaume siyo kitu cha lazima sana? Aibu ya mwaka ilikuwa imenifika.

“Eti kumetokea nini kwani?” sauti ya mama yake Rahma ilisikika, akiwa ameongozana na binti yake ambaye sasa fahamu zilikuwa zimemrudia, wakiwa pamoja na mama. Nilishindwa hata cha kujibu, mate yakanikauka ghafla mdomoni.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na tano_______15




ILIPOISHIA:

“ETI kumetokea nini kwani?” sauti ya mama yake Rahma ilisikika, akiwa ameongozana na binti yake ambaye sasa fahamu zilikuwa zimemrudia, wakiwa pamoja na mama. Nilishindwa hata cha kujibu, mate yakanikauka ghafla mdomoni.

SASA ENDELEA…

“ETI Rahma, nini kimetokea?” “Nilikuwa nimelala, ghafla nikaanza kuhisi kama naungua hivi, sijui tena kilichotokea mpaka nilipokuja kuzinduka kule sebuleni,” alisema na kunifanya nimtazame kwa macho ya mshangao.

Ni yeye pekee ndiye ageweza kuthibitisha kilichotokea lakini kwa maelezo yale, japo alizungumzia kidogo kuhusu kuhisi anaungua, bado yasingetosha kumfanya mtu aamini nilichokuwa nakizungumza. “Na hii nguo imefikaje huku?”

“Niliposhtuka usingizini, sikuwa nimevaa nguo kwa hiyo katika zile purukushani za kuwahi kuja kumuokoa dada nikasahau kuivaa na nadhani ilikuwa kwenye nguo zangu ndiyo maana ikaja kuangukia humu ndani,” nilisema.

Sijui nilipata wapi akili za kutunga uongo mkubwa kiasi hicho. Baba alinitazama usoni, nikakwepesha macho yangu kwa sababu baba alikuwa na uwezo wa kumgundua mtu anayezungumza uongo kwa kumtazama na kwa sababu sikuwa na kawaida ya kudanganya, nilijua anaweza kunigundua kwa haraka.

Namshukuru Mungu uongo wangu ulipita, baba akaisukumia ile nguo kwangu kwa kutumia mguu wake wa kushoto. Niliinama haraka na kuiokota, nikaisunda mfukoni, kiukweli nilijisikia aibu sana kwa sababu mama alikuwepo, mama yake Rahma alikuwepo na hata Rahma mwenyewe.

Licha ya kulimaliza hilo la kwanza kwa kuongea uongo, bado mjadala mkubwa ulibaki kwenye ishu ya mimi kusema chumba cha Rahma kilikuwa kikiwaka moto huku kukiwa hakuna dalili zozote za moto. Niliwaona baba na baba yake Rahma wakinong’onezana jambo, kisha baba yake Rahma akamnong’oneza mkewe, baba akanishika mkono na kunitoa nje, baba Rahman naye akafuatia, kwa lugha nyepesi wanaume tukatoka na kuwaacha mama Rahma, mwanaye na mama.

Tulienda mpaka nje kabisa, tukakaa kibarazani mimi nikiwa katikati, baba akanigusa begani na kunipigapiga. “Hebu sema ukweli, nini kilichotokea mpaka ukaenda kuvunja mlango na kumtoa dada yako mzobemzobe.” “Moto ulikuwa unawake, tena moto mkubwa kwelikweli.”

“Lakini wewe si unafahamu kwamba moto ukiwaka lazima uache ishara yoyote na unavyosema kwamba ulikuwa ni moto mkubwa, inawezekanaji muda huohuo sisi tuende chumbani na tusikute moto wala dalili zozote za moto?” “Aaah… eeh hata mimi ndiyo nasha…ngaa,” nilisema kwa kubabaika, maji yalikuwa yamenifika shingoni na hata sijui ningetumia lugha gani ili nieleweke.” “Umeanza kuvuta bangi kama kaka zako?” baba aliniuliza swali ambalo lilinifedhehesha sana.

Sikuwahi kutumia kilevi cha aina yoyote tofauti na kaka zangu ambao kule kijijini walikuwa na tabia ya kutembea na vijana wahuni wa kijiji ambao ilikuwa inaaminika kwamba wanavuta bangi ndiyo maana walikuwa na uwezo wa kulima mashamba makubwa bila kuchoka au kufanya kazi ngumu za migodini kwa muda mrefu. Nilitingisha kichwa kukataa, akaniambia kwamba ananiamini sana ndiyo maana ananipa upendeleo kuliko mtu yeyote kwenye familia yetu, akanitaka nisimuangushe na kama nina tatizo lolote nimwambie kuliko kumficha. Baba yake Rahma naye aliongeza kwamba wananiamini na kuna kazi kubwa mbele yetu ambayo walishakubaliana kwamba watashirikiana na mimi kwa hiyo lazima niwe makini sana.

*(Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi)

“Haya nenda kalale,” alisema baba, nikainuka kinyonge na kuanza kutembea kuelekea ndani, huku nikijisikia vibaya sana kwa sababu niliamini nilichokifanya ilikuwa ni kwa nia njema kabisa lakini kibao kilinigeukia, nikaonekana eti mimi ni mvuta bangi! Nilijisikia vibaya sana kiukweli.

Nilipitiliza moja kwa moja mpaka chumbani, nikaingia na kujitupa kitandani na kuanza kutafakari kwa kina juu ya kilichotokea. Mambo yalikuwa yametokea kwa kasi mno, yaani siku moja ilikuwa na matukio chungu nzima, yaani kama ingekuwa ni filamu, basi nina hakika ingependwa sana.

Kutokana na uchovu wa safari na matukio yote yaliyotokea kutwa nzima, kuanzia alfajiri tulipoianza safari ya kutoka Makongorosi mpaka muda huo, tukiwa tayari ndani ya Jiji la Dar es Salaam, nilipitiwa tena usingizi mzito. Safari hii sikushtuka mpaka asubuhi na kilichoniamsha zilikuwa ni kelele za mafundi waliokuwa wakitengeneza mlango wa chumba cha Rahma.

Nikaamka na kukaa kitandani, kumbukumbu za matukio yaliyotokea jana yake zikaanza kurudi kichwani mwangu, ndugu yangu niliyelala naye alishaamka muda mrefu tu na hakuwepo chumbani kwa hiyo nilikuwa peke yangu.

“Kaka Togo! Kaka Togo,” sauti ya kike ilisikika nje ya mlango wa chumba kile, kabla sijajua cha kufanya mlango ulifunguliwa, nikakutana na sura nzuri ya Rahma, tabasamu pana likiwa limechanua usoni mwake. Aligeuka nyuma kama anayetazama kama kuna mtu anayemuangalia kisha nikamuona akiingia na kufunga mlango kwa ndani.

“Nimekuja kukuita tukanywe chai lakini pia nimekuletea zawadi,” alisema huku akinipa ‘apple’ la rangi ya kijani. Niliachia tabasamu na kulipokea, nikaanza kulila kuchangamsha mdomo kwani tangu nimeamka hata mswaki sikuwa nimepiga. Alikuja na kukaa pembeni yangu pale juu ya kitanda, akawa ananitazama kwa macho yake mazuri wakati nikilila lile tunda alilonipa.

“Samahani, eti kwani jana usiku kulitokea nini? Naomba nisamehe kama nimekusababishia matatizo.”

“Aah, kawaida tu wala usijali.” nilimjibu kwa mkato, sikutaka kujadiliana naye sana kuhusu kilichotokea, akaendelea kuniuliza maswali lakini nikawa namkatisha, nikamwambia tutazungumza vizuri kuhusu suala hilo muda muafaka ukifika.

“Samahani kama nimekuudhi,” alisema huku akiinuka na kunibusu kwenye shavu langu kisha akanikumbatia na kunibusu tena. “Usijali kabisa, wala hujaniudhi,” nilisema huku mapigo ya moyo wangu yakianza kwenda mrama.

Nikiri wazi kwamba Rahma alikuwa mzuri sana, kitendo cha kunikumbatia, kumbukumbu za tulichokifanya jana yake zilianza kujirudia ndani ya kichwa changu. Na mimi nilimkumbatia na kushika kiuno chake, nikamuona akijinyonganyonga huku akinitazama kwa macho kama vile bado alikuwa na usingizi. Hamasa niliyokuwa naipata, ilinifanya nisiogope chochote, nikaamua kuyavulia tena maji nguo, tayari kwa kuyaoga.

Muda mfupi baadaye, tulikuwa msambweni na Rahma lakini safari hii tulikuwa tukijizuia kutoa aina yoyote ya kelele kwani tulikuwa tunajua kwamba watu wote wameshaamka. Yaani ndani ya muda mfupi tu, Rahma alishaingia ndani ya moyo wangu na kunifanya nimpende sana na kuwa tayari kwa chochote.

Tuliendelea kupigiana pasi fupifupi, wakati mwingine Rahma akawa anashindwa kujizuia na kutoa miguno ya hapa na pale, tukiwa tunaendelea, tulishtuka baada ya kusikia minong’ono dirishani kwa upande wa nje. Kwa ilivyoonyesha, kuna watu walikuwa wakifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea.

“Togo,” nilisikia sauti nzito ya baba ikiniita, harakaharaka nikamtoa Rahma, kila mmoja akawa anahaha kujiweza vizuri. “Togooo,” alirudia kuniita, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio mno huku mdomo ukiwa mzito kufunguka.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na nne__________14



ILIPOISHIA:

“MUNGU wangu,” nilijisemea, mapigo ya moyo yakiwa yananienda mbio kuliko kawaida, nikiwa sijui nini kitatokea, hasa ukizingatia kwamba nilikuwa ugenini na ndiyo kwanza tulikuwa tumewasili.

SASA ENDELEA…

ALINIACHIA huku naye akionyesha kushtuka, akashuka kitandani na kuokota khanga yake, akajifunga kivivu na kunionyesha ishara kwamba niingie kwenye kabati la nguo, nilifanya hivyo haraka, nikamsikia akifungua mlango.

“Baba amesema usije ukafunga mlango mkubwa wa nje, watachelewa kuingia ndani kwani kuna kazi wanaifanya.”

“Haya poa,” nilimsikia akizungumza na mdogo wake, akashusha pumzi ndefu na kuufunga mlango, nikamsikia safari hii akifunga kwa funguo kabisa, akaja pale kabatini na kufungua mlango, akanionyesha ishara kwamba nitoke.

Sikulaza damu, nilitoka harakaharaka nikiwa kama nilivyo, na yeye akauachia ule upande wa khanga, ukadondoka chini, tukawa tunatazama kama majogoo yanayotaka kupigana. Alipiga hatua moja mbele, miili yetu ikagusana, akazungusha mikono yake kwenye shingo yangu, na mimi nikiwa sijiaminiamini, nikaukumbatia ‘mlima’ wake.

Nikiri kwamba hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuwa kwenye hali kama hiyo na nilichokihisi kwenye mwili wangu, sikuwahi kukihisi kabisa tangu napata akili zangu. Ni hapo ndipo nilipoanza kuelewa kwa nini watu wengi huwa wanayasifia sana mapenzi kwamba ni matamu kuliko asali.

Ni hapo pia ndipo nilipoelewa kwa nini watu wengine hufikia hatua hata ya kutoana roho, baada ya mmoja kugundua kwamba anatembea na mkewe au mpenzi wake. Dakika chache baadaye, nilikuwa nahema kama nataka kukata roho, ufundi wa mikono yake kuvinjari kwenye mwili wangu, ulinifanya mara kwa mara niwe natoa miguno ambayo sikuwahi kuitoa kabla.

Hata sikukumbuka nilifikaje kwenye uwanja wake wa fundi seremala, nilikuja tu kushtukia yeye yuko juu yangu nikiwa nimelala chali, huku nikiendelea kupumua kwa fujo, mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana na ‘Togolai’ akiwa anazidi kuongeza hasira kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele.

Kwa ufundi wa hali ya juu, alimuelekeza njia ya kupita, nikajikuta nikianza kuzungumza kama bubu, maneno hayatoki wala hayaeleweki, kucheka natamani lakini muda huohuo natamani kupiga chafya, ilikuwa ni hali ya ajabu mno. Safari iliendelea, mwanzo alikuwa akipiga hatua fupifupi lakini baadaye nikaanza kumuona akinogewa na kuongeza huku akitoa ukelele fulani ulioongeza raha kubwa kwenye masikio yangu.

Baadaye ilibidi tubadilishane magoli kwenye mechi ile ya kirafiki isiyo na refa wala jezi, yeye akawa anapeleka mashambulizi Kaskazini mwa uwanja na mimi napeleka Kusini.

Japokuwa hata danadana sikuwa najua kupiga na siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza, nilijitahidi kuonyesha kiwango kwa sababu nimewahi kusikia kwamba ukicheza chini ya kiwango, huwa unadharaulika mbele ya viumbe hawa.

Akaongeza mno kasi ya mashambulizi kisha akanikaba kwa nguvu shingoni kama wanavyofanya wale watu wanaopora simu au fedha, akanishikilia kwa nguvu na kunibana, na mimi nikaongeza kasi, nikajisikia hali fulani hivi nzuri sana, akazidi kunibana kisha akaniachia na kudondokea upande wa pili, jasho likiwa limemlowanisha chapachapa na mimi nikiwa hoi bin taaban, nilijikuta nikicheka mwenyewe kwa furaha.

Hakuzungumza jambo lolote kwa dakika kadhaa, baadaye aliinuka na kukaa kitandani, akawa ananitazama kama ambaye haamini kitu fulani.

“Una miaka mingapi?”

“Kwa nini unaniuliza hivyo?”

“Kwa nje unaonekana mdogo lakini wewe ni zaidi ya mwanaume,” alisema na kunikumbatia tena, akaanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu huku akiniambia kwamba ananipenda na anaomba nisimuache ila uhusiano wetu uwe wa siri.

Bado sikuwa naelewa alichokimaanisha, akaendelea na uchokozi wake na hata sijui nini kilitokea lakini muda mfupi baadaye, nilishtukia tukiwa tena dimbani, safari hii kidogo nikawa sina ugeni na uwanja pamoja na mchezo wenyewe.

Mpambano mkali uliendelea mpaka baadaye ambapo ile hali iliyotutokea mwanzo ilitokea tena, tena kwa kila mtu. Safari hii, alipoangukia upande wa pili, haukupita muda mrefu akaanza kukoroma.

Kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, harakaharaka niliinuka na kuvaa nguo zangu nikaenda kufungua mlango na kutoka huku nikinyata, nikaenda mpaka kwenye mlango wa kile chumba ambacho nitalala na ndugu yangu mmoja.

Kwa bahati nzuri, mlango haukuwa umefungwa, nikaingia mpaka ndani, tayari ndugu yangu naye alikuwa akikoroma, nikajilaza kitandani huku nikisikia uchovu wa kiwango cha juu, karibu kila sehemu kwenye mwili wangu ilikuwa inauma.

Tabasamu pana lilikuwa limechanua kwenye uso wangu, hasa kumbukumbu ya nilichotoka kukifanya ilipokuwa inanijia. Sasa na mimi nilijihisi kuwa mwanaume niliyekamilika. Bado nilikuwa siamini jinsi nilivyoweza kuuangusha mbuyu kwa shoka moja, haukupita muda mrefu nilipitiwa na usingizi.

“Motooo! Jamani moto… nakufaaaa,” sauti za mtu aliyekuwa akipiga kelele kuomba msaada, ndizo zilizonishtua kutoka kwenye usingizi mzito, nikakurupuka huku mapigo yangu ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida, nikatoka mpaka koridoni.

Sikuamini macho yangu kusikia sauti ile ilikuwa ikitoka kwenye kile chumba ambacho usiku huo mimi na yule dada tulilambishana asali. Moto ulikuwa umekolea kiasi kwamba hata sehemu ya kupita haikuwa ikionekana.

Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kufika eneo hilo kwa sababu sikumkuta mtu mwingine yeyote, nikaona nikisema niende kuwaamsha baba na mama, dada wa watu anaweza kufa bure, nikapiga moyo konde na kuukanyaga mlango ambao ulikuwa ukiwaka moto, ukaangukia ndani.

Sikujali kuhusu moshi mzito uliokuwa umetanda kwani tayari nilikuwa na uzoefu wa kucheza kwenye moshi kwani kule kijijini ilikuwa kama tunataka kwenda kupakua asali kwenye mzinga, lazima tuwashe moto kwa kutumia miti inayotoa moshi mzito. Nilibana pumzi, nikaenda mpaka pale kitandani ambapo nilimkuta akiwa ameanza kuishiwa pumzi kutokana na kuvuta moshi mwingi.

Kwa kuwa mwili wangu ulikuwa na nguvu, si unajua tena maisha ya kijijini yanakufanya uwe ‘ngangari’ kutokana na kazi ngumu, nilimbeba na kutoka naye mpaka koridoni, moto ukawa unazidi kuwaka lakini kilichonishangaza sana ni kwamba haukuwa ukisambaa kwenye vyumba vingine.

Nikiwa koridoni, mikononi nikiwa nimembeba yule dada ambaye alishapoteza fahamu, nilikutana na baba na mwenyeji wake pamoja na mama na mwenyeji wake.

“Kuna nini tena? Rahma kapatwa na nini?” aliuliza baba yake, ni hapo ndipo nilipojua kwamba kumbe jina lake anaitwa Rahma. Sikuweza kuwajibu kwa sababu walikuwa wanamuona hali aliyokuwa nayo, baba yake na baba wakanipokea na kumkimbiza mpaka sebuleni, feni zote zikawashwa.

*(Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi)

“Kumetokea nini?”

“Moto.”

“Motoo?”

“Ndiyo, chumbani kwake kunawaka moto,” nilisema huku nikishangaa kwa nini walikuwa wakiniuliza mara mbilimbili jambo ambalo lilikuwa wazi. Harakaharaka walielekea kule chumbani wakati mama yake akihangaika kumpa huduma ya kwanza lakini muda mfupi baadaye, walirudi mbiombio.

“Umesema chumbani kwake kunawaka moto?”

“Ndiyo, alikuwa anapiga kelele za kuomba msaada ndiyo nikaamka na kwenda kumsaidia, nilisema, nikaona baba na mwenyeji wake wakitazamana, sikuelewa walikuwa wanamaanisha nini. Ilibidi haraka nirudi kule chumbani kwake ili kuangalia moto umefikia wapi.

Cha ajabu, mpaka nafika mlangoni hakukuwa na moto wala dalili za moto isipokuwa mlango ulikuwa umevunjwa na nakumbuka vizuri mimi ndiye niliyeukanyaga kwa nguvu ukavunjika.

Huku nikiwa nimepigwa na butwaa, niliingia ndani ambako muda mfupi uliopita moto mkubwa ulikuwa umetanda kila sehemu lakini cha ajabu kila kitu kilikuwa sehemu yake, nikageuka huku nikiwa siamini, nikakutana na baba na mwenyeji wake ambao kumbe walikuwa nyuma yangu wakinitazama.

“Ulimaanisha chumba hiki au kingine?”

“Hikihiki, nashangaa sijui imekuwaje, kwani nyie hamjasikia kelele za kuomba msaada?”

“Mimi nimesikia kelele za mlango kuvunjwa tu, basi.”

“Mungu wangu,” nilisema kwa hofu kubwa, nikijihisi kama nipo kwenye ndoto ya kutisha.

“Na vipi kuhusu hii?” baba aliniuliza, huku akinionyeshea nguo yangu ya ndani iliyokuwa pale chini ya kitanda cha Rahma. Kumbe wakati muda ule navaa nguo zangu, niliisahau si unajua tena maisha ya kijijini kuvaa hiyo kitu hasa kwa sisi wanaume siyo kitu cha lazima sana? Aibu ya mwaka ilikuwa imenifika.

“Eti kumetokea nini kwani?” sauti ya mama yake Rahma ilisikika, akiwa ameongozana na binti yake ambaye sasa fahamu zilikuwa zimemrudia, wakiwa pamoja na mama. Nilishindwa hata cha kujibu, mate yakanikauka ghafla mdomoni.

Je, nini kitafuatia?
Kutoka sehemu ya 13 kuja 14 kuna muendelezo umekosekana
 
Back
Top Bottom