Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Cha ajabu sasa, wakati nageuka kutazama kule zile damu zilikokuwa zikimwagika, nilishangaa kuona kinachotoka si damu bali maji na wala hakuna dalili yoyote ya damu. Tayari kaka zangu walishafika na kunikuta nikihangaika kujifunga ile khanga niliyopewa, wakataka kujua nini kimetokea

Kelele hizo kumbe hata baba na yule mwenzake walizisikia, nao wakaja haraka kutaka kujua nini kimetokea.

Je, nini kitafuatia?
Mbona hamna connection? Imekuwaje kuwaje hadi wamefika kudinyana?
SASA ENDELEA…

ALINIACHIA huku naye akionyesha kushtuka, akashuka kitandani na kuokota khanga yake, akajifunga kivivu na kunionyesha ishara kwamba niingie kwenye kabati la nguo, nilifanya hivyo haraka, nikamsikia akifungua mlango.

“Baba amesema usije ukafunga mlango mkubwa wa nje, watachelewa kuingia ndani kwani kuna kazi wanaifanya.”
 
Sehemu ya kumi na sita______16



ILIPOISHIA:

“TOGO,” nilisikia sauti nzito ya baba ikiniita, harakaharaka nikamtoa Rahma, kila mmoja akawa anahaha kujiweza vizuri.

“Togooo,” alirudia kuniita, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio mno huku mdomo ukiwa mzito kufunguka.

SASA ENDELEA…

“NAAM!”

“Hebu sogea hapa dirishani,” alisema baba, harakaharaka nikavaa nguo zangu, Rahma naye akawa ameshavaa nguo zake na bila kujali atakutana na nani nje, alitoka kwa kasi.

“Wewe Togo, si nimekwambia sogea hapa?” alisema baba, safari hii akigonga kioo cha dirisha. Kwa kuwa tayari nilishavaa, nilisogea pale dirishani na kufunua pazia pamoja na dirisha moja, nikamuona baba amenikazia macho.

“Unafanya nini?”

“Nilikuwa nafanya mazoezi ya kupiga pushapu.”

“Kweli?”

“Kweli baba.”

“Hebu funua pazia lote,” alisema baba, kwa kuwa nilikuwa na uhakika Rahma ameshatoka, nilifunua pazia lote, akatazama huku na kule kisha akarudi kunitazama usoni.

“Mwanangu Togo, mbona tangu tumeanza safari umekuwa ni mtu wa kututia aibu kila sehemu? Una nini kwani wewe?”

“Mama sasa kwani mi nimefanya nini? Ina maana hata kufanya mazoezi ndani nako ni makosa?” nilimjibu mama ambaye kumbe alikuwa na baba kule nje, nikavaa uso wa huruma ili kuwafanya waniamini kile nilichokuwa nakisema.

“Hivi unatufanya sisi wote ni watoto wadogo kama wewe?” alisema baba huku akiwa amekazia macho suruali niliyokuwa nimevaa, ikabidi na mimi nijiangalie. Cha ajabu, suruali niliyokuwa nimevaa nilikuwa nimeigeuza nje ndani, aibu niliyoihisi ilikuwa kubwa mno, ikabidi niliachie pazia na kurudi kitandani huku nikikosa cha kujibu.

“Nitasema wakati wa kuvaa nimevaa harakaharaka, bado nitaendelea kukataa kwamba sijafanya chochote,” nilijisemea huku nikiivua ile suruali na kuivaa vizuri. Kwa kuwa mwanzo Rahma alipokuja aliniambia kwamba chai ipo tayari, ili kuzidi kupoteza ushahidi, niliamua kupitia kwanza bafuni kabla sijaenda sebuleni.

Nikanawa uso harakaharaka na kutoka kuelekea sebuleni, bado wale mafundi walikuwa wakiendelea kutengeneza mlango na nahisi walikuwa wanajua kilichokuwa kinaendelea kati yangu na Rahma kwa sababu wakati natoka bafuni, wote waliacha kila walichokuwa wanakifanya na kunitazama usoni, wakionyesha dhahiri kwamba walikuwa na shauku ya kunijua.

Sikuwasemesha kitu, hata salamu sikuwapa, nikapitiliza moja kwa moja mpaka sebuleni ambako niliwakuta karibu watu wote wakiwa wanakunywa chai isipokuwa wazazi wa pande zote mbili, kwa maana ya baba na mama yetu na baba na mama yao akina Rahma, kila mmoja akiwa na kikombe chake na vitafunwa vyake.

Kabla hata sijakaa, Rahma aliinuka na kunichukulia kikombe, akanimiminia chai na kunisogezea pale nilipokuwa nimekaa pamoja na vitafunwa. Watu wote walikuwa kimya kabisa, macho yakiwa kwenye runinga kubwa ya kisasa.

Wakati akinisogezea chai, Rahma alinitazama kwa macho ya kuibia, na mimi nikamtazama, macho yetu yakagongana ambapo nilimuona akiachia tabasamu pana huku aibu za kikekike zikiwa zimetawala kwenye uso wake.

Hakutaka kurudi kukaa pale alipokuwa amekaa awali, alichukua kikombe chake cha chai na kuja kukaa pembeni yangu, nikawaona ndugu zangu, akiwemo dada Sabina wakinitazama kwa macho ya chinichini.

Ukimya uliendelea kutawala, tukaendelea kunywa chai na baada ya kumaliza, Rahma na dada Sabina waliinuka na kuanza kutoa vyombo, tayari kwa ajili ya kwenda kuviosha lakini ghafla mama aliingia akiwa ameongozana na mama yake Rahma. Kwa kuwatazama tu sura zao, ilionyesha kuna jambo halikuwa sawa.

“Togo, njoo huku,” alisema mama, mama yake Rahma naye akamuita Rahma, ikabidi aache kutoa vyombo, wote tukaelekea kule nje ambako tulikuta wazazi wetu wakiwa wamekaa kwenye viti vilivyokuwa pale nje, wote wakionyesha kutokuwa na furaha kwenye nyuso zao.

“Hebu tumbieni, hivi Togo na Rahma mlikuwa mnafahamiana kabla?” aliuliza baba yake Rahma, muda mfupi tu baada ya sisi kufika.

“Hapana,” nilisema huku nikitingisha kichwa.

“Mbona ndani ya muda mfupi tu tangu mkutane mmekuwa na nyendo zinazotutia mashaka? Hivi mnajua kama nyie ni ndugu?” alisema baba yake Rahma na kunifanya nishtuke.

Alichokuwa ametuambia baba, ni kwamba baba yake Rahma alikuwa ni rafiki yake wa siku nyingi ambaye walishirikiana vitu vingi pamoja na ndiyo maana hata alipoona mambo hayaendi vizuri kule Chunya, majirani na wanakijiji wakiituhumu familia yetu kuwa inajihusisha na Imani za kishirikina aliamua kuondoka na sisi mpaka jijini Dar es Salaam.

“Sikuwa nimewafafanulia mwanzo lakini ukweli ni kwamba ukiacha urafiki wetu, sisi ni ndugu, mama yangu kwa maana ya bibi yenu na mama mzazi wa baba Rahma ni mtu na mdogo wake, kwa hiyo sisi ni ndugu na nyie ni ndugu, tena wa damu kabisa,” alisema baba, kauli ambayo ilinishtua mno.

“Msije mkatuletea aibu ya mwaka hapa maana naona mmeshaanza kuonyesha kupendana, nyie ni ndugu na kwa ukoo wetu sisi ndugu wakifanya dhambi kama hiyo, husababisha mabalaa makubwa sana kwenye ukoo mzima,” baba yake Rahma alizidi kupigilia msumari.

Japokuwa ilikuwa ni asubuhi, nilijikuta kijasho chembamba kikinitoka, lilikuwa ni jambo ambalo sikulitegemea kabisa, nikageuka na kumtazama Rahma, nikamuona akiwa amejiinamia kwa aibu.

Sikuwahi kuwa na skendo yoyote ya mapenzi na hata wazazi wangu hawakuwahi kusikia jambo lolote baya kuhusu mimi lakini cha ajabu, ndani ya muda mfupi tu niliokutana na Rahma na kunionjesha ulimwengu wa kikubwa, tayari kila mtu alikuwa na wasiwasi na mimi. Nilijisikia aibu sana.

“Mmeelewa?” alihoji baba, nikajibu kwa kutingisha kichwa, wakatuambia tukaendelee na tulichokuwa tukikifanya, wakati tukiondoka tukawasikia wakipiga stori na kucheka, nadhani baba alizungumza kitu kuhusu mimi kilichowavunja mbavu wote.

Tulipoingia sebuleni, tulikuwa kama tumemwagiwa maji ya baridi, afadhali mimi kidogo niliweza kujikaza, Rahma alionyesha kuchoka mno, macho yakawa mekundu kama anayetaka kulia.

Hakuweza kuendelea kukaa pale sebuleni, nilimuona akiinuka kwa unyonge, akaelekea chumbani kwake ambapo tayari mafundi walikuwa wamemaliza kutengeneza mlango wa chumba chake, akaingia ndani na kujifungia.

Sikumuona tena akitoka mpaka muda wa chakula cha mchana, mimi na ndugu zangu tukawa tunaendelea kushangaa runinga na vitu vingine vya kisasa vilivyokuwa mle ndani.

Baada ya chakula cha mchana kuiva, mama yake Rahma alimtuma mdogo wake kwenda kumuita chumbani kwake wakati chakula kikipakuliwa. Muda mfupi baadaye, alikuja na majibu kwamba dada yake alikuwa amelala chumbani lakini alipojaribu kumuamsha, hakuamka.

“Unasema?” mama yake Rahma aliuliza kwa mshtuko, huku akiacha kila alichokuwa anakifanya. Haraka akakimbilia chumbani kwa mwanaye, huku akionyesha kuwa na wasiwasi mkubwa moyoni mwake, mama naye akamfuata, na mimi uzalendo ukanishinda, nikainuka na kuwafuata.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na saba_______17



ILIPOISHIA:

“UNASEMA?” Mama yake Rahma aliuliza kwa mshtuko, huku akiacha kila kitu alichokuwa akifanya. Haraka akakimbilia chumbani kwa mwanaye huku akionyesha wasawasi mkubwa moyoni mwake, mama naye akamfuata, na mimi uzalendo ukanishinda, nikainuka na kuwafuata.

SONGA MBELE…

TULIPOINGIA chumbani, mama yake Rahma akaanza kumuamsha kwa kumwita lakini hakuitika wala kutikisika, akasema; “mwanangu umepatwa na nini?” Hata hivyo, Rahma hakuitika wala kufumbua macho, jambo hilo lilitushtua sana, mama naye alipojaribu kumwita hali ikawa vilevile, Rahma alitulia kimya.

Sikukubaliana na hali hiyo, nilijongea kitandani alipolala Rahma, nikamshika begani na kuanza kumtikisa huku nikimwita, kama ilivyokuwa kwa mama yake na mama, kipenzi changu Rahma hakuitika. Kilichofuatia ni kila mmoja wetu kuanza kulia kwani tulijua alikuwa ametutoka, kufuatia vilio vyetu baba yake Rahma alisikia akaja mbio kujua kilitokea nini, akina mama wakiwa wanalia walishindwa kumweleza chochote zaidi ya kulia.

“Eti Togo, kimetokea nini?” akaniuliza. Nilimfahamisha kilichotokea, akiwa amepata mshtuko, mzee huyo alimshika Rahma kifuani akagundua mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa mbali, akawauliza akina mama alipatwa na nini. Mama ya Rahma akamweleza kila kitu, mzee huyo aliwaambia wanyamaze kwani Rahma alikuwa hajafa, mzee huyo aliniambia niende haraka kwa jirani aliyekuwa na usafiri ili amkimbize Rahma hospitali.

Nikiwa nimechanganyikiwa na tukio hilo, nilikwenda kwa jirani huyo ambaye alikuja na gari lake tukampakiza Rahma na kumkimbiza hospitali, alipofikishwa huko alifanyiwa uchunguzi na kuibainika alikunywa dawa mchanganyiko ili ajiue. Madaktari walimuwekea dripu ya maji kisha antpoison kuondoa sumu hiyo, wakati akipewa matibabu hayo alikuwa hajitambui, madaktari walituambia tusiwe na wasiwasi kwani baada ya muda mfupi hali yake ingetengemaa.

“Kati yenu ni nani wazazi wa huyu binti?” Daktari aitwaye Jason aliwauliza akina mama na akina baba! “Mimi mama yake na huyu hapa ndiye baba yake,” mama ya Rahma alimjibu daktari huyo huku akimuonyeshea mumewe. “Oke, naomba twendeni ofisini kwangu tukazungumze kuhusiana na tatizo la binti yenu,” daktari huyo aliwaambia.

“Hakuna shida daktari,” baba ya Rahma alimwambia. “Kwanza nawapeni pole kwa jambo lilitokea kwani najua ni kwa kiasi gani mmepata mshtuko,” daktari aliwaambia. “Tunashukuru dokta, pia tunashukuru kwa jinsi ulivyompokea na kumhudumia kwa wakati,” mama yake Rahma alimwambia daktari. Alipoambiwa, daktari aliwaambia wasijali kwani huo ndiyo wajibu wao kwa wagonjwa kisha akawauliza kilitokea nini nyumbani kilichosababisha Rahma kutaka kujiua!

“Kwa kweli hata sisi tumeshangazwa sana na uamuzi wake, ameamka akiwa mukheri wa afya, tumeshinda naye vizuri hadi mchana mama yake alipomtuma ndugu yake akamuamshe kwa ajili ya kula ndipo akarudi mbio na kumweleza alimwita hakuitika na alipojaribu kumtikisa alitulia tu!” baba ya Rahma alimweleza daktari.

“Oh poleni sana, lakini lazima kutakuwa na sababu kwani katika hali ya kawaida siyo rahisi kwa mtu kuchukua uamuzi wa kutaka kujiua bila ya kukwazwa na jambo f’lani, je, yupo katika uhusiano wa kimapenzi na mtu yeyote?” Daktari aliwauliza. “Hatuelewi maana hatujawahi kumuona na mwanaume yeyote,” mama Rahma alimwambia.

Alipotoa kauli hiyo, daktari Jason aliwauliza tena kama binti yao alikuwa na ugomvi na mtu yeyote hasa marafiki zake, wazazi wake wakamwambia hakuwa na ugomvi. “Labda aliomba mnunulie kitu f’lani mkamkatalia kwa ukali?”

Daktari huyo alizidi kuwabana kwa maswali ili tu kujua sababu ya Rahma kutaka kujiua. “Kwa upande wangu hajaniomba chochote labda mwenzangu,” mama yake alimjibu daktari. “Eh! Baba au alikuomba fedha ukamnyima,” daktari akamwuliza. “Hapana daktari, tena juzi tu nimempatia fedha za kutosha kwa ajili ya matumizi yake,” mzee huyo alimwambia.

Baada ya maswali hayo na majibu, daktari aliwaambia lazima kuna jambo ambalo wazazi hawalifahamu lililosababisha Rahma kutaka kujiua, akawashauri wawe wanachunguza nyendo za watoto wao hasa mabinti kwa sababu wana mambo mengi sana.

***

Wakati kule ofisini kwa daktari Jason akiendelea kuzungumza na wazazi wa Rahma, nje baba yake Togo na mama yake ambao hawakuwa na furaha walikuwa wakizungumza kuhusu tukio hilo. “Hivi mama Togo, kitendo cha kuwauliza hawa watoto kama wanafahamiana tangu zamani na kwamba ukaribu wao unatutia shaka inaweza kuwa sababu ya Rahma kutaka kujiua?” baba Togo alimwuliza mkewe.

“Sidhani, nahisi kutakuwa na jambo lingine tu mume wangu,” mama huyo alimwambia mumewe. Alipoambiwa hivyo, mumewe alimweleza mkewe kwamba huenda tayari walishaanza kufanya utundu na sababu ya kutaka kujiua ni baada ya kuwaambia walikuwa ndugu!

“Ila unachosema naona umenifungua kichwani, huenda ikawa hivyo ili kuficha aibu ya kutembea na kaka yake, lakini tusiwaze sana kuhusu hilo tutajua tu ukweli!” mama Togo alimwambia mumewe.

Hata hivyo, baba Togo alimwambia mkewe kwamba ngoja wamsubiri Togo aliyekuwa amekwenda kununua maji ya kunywa arejee ili wambane kwani walihisi alikuwa anajua sababu za mwenzake kutaka kujiua. “Nakuunga mkono, atakuwa anajua japo anajifanya hajui chochote,” mama Togo alimwambia mumewe. “Mh! Huyu mtoto ana hatari sana, hata kama wameshafanya utundu na kaka yake uamuzi aliochukua siyo mzuri hata kidogo,” baba Togo alimwambia mkewe kwa huzuni.

“Ila mke wangu kama kweli hawa watoto watakuwa wamefanya utundu itakuwa dhambi kubwa ambayo italeta balaa na tutakuwa tumesababisha sisi kushindwa kuwaambia mapema kwamba walikuwa ndugu,” baba Togo alimwambia mkewe.

“Sijui itakuwaje sasa mume wangu, lazima balaa litokee tuombe tu Mungu Togo atuhakikishie kwamba hawafanyi mapenzi na ndugu yake,” mama Togo alimwambia mumewe. Wakati wakizungumza hayo, mara wakawaona baba na mama Rahma wanakwenda walipokuwa wakitokea ofisini kwa daktari, wakaacha mazungumzo yao.

Je, kilifuatia nini? Usikose next issue.
 
Sehemu ya kumi na nane_______18


ILIPOISHIA:

“SIJUI itakuwaje sasa mume wangu, lazima balaa litokee tuombe tu Mungu Togo atuhakikishie kwamba hawajafanya mapenzi na ndugu yake,” mama Togo alimwambia mumewe.

Wakati wakizungumza hayo, mara wakawaona baba na mama Rahma wanakwenda walipokuwa wakitokea ofisini kwa daktari, wakaacha mazungumzo yao.



SASA ENDELEA…

“VIPI anaendeleaje?”

“Anaendelea vizuri, mtoto mjinga sana huyu.”

“Mh! Usimuite mjinga, huu siyo muda wake, uchungu wake naujua mimi, nimembeba kwenye tumbo langu kwa miezi tisa,” alisema mama yake Rahma akionyesha kutofurahishwa na kauli ya mumewe. Walitoka pamoja na kwenda kukaa kwenye benchi lililokuwa nje ya jengo hilo la hospitali, mimi nikaenda kukaa upande wa pili.

“Hivi, mnajua mimi bado sina majibu juu ya haya maswali niliyonayo.”

“Maswali gani yanayokusumbua?”

“Ni kwa sababu gani Rahma amechukua uamuzi wa kuyakatisha maisha yake?”

“Mh! Hawa watoto wetu wa siku hizi, mimi nahisi alikuwa anampenda Togo sasa kitendo cha kuwaambia kwamba ni ndugu ndiyo maana ameamua kufanya aliyoyafanya, tumshukuru Mungu bado yupo hai.”

“Unachokisema ni sawa lakini nahisi kuna kitu zaidi ya hicho, nahisi hawa watoto walikuwa wameshaanza kufanya mapenzi.”

“Mh! Ninavyomjua Togo huwa hana kawaida ya kuwa karibu na wasichana kabisa, ni muoga sana wa wasichana, sidhani kama hilo linawezekana.”

“Hata Rahma naye si mcharuko kiasi hicho, sijawahi hata kumuona akiwa na mwanaume kichochoroni, kama mambo hayo anayafanya basi anafanya kwa siri sana, kwa ufupi anajiheshimu.”

“Sasa kama tatizo siyo hilo, mnafikiri nini kinaweza kuwa chanzo?”

“Mh! Mimi nakuunga mkono rafiki yangu, kuna kitu nimekihisi na kwa kuunganisha matukio, inawezekana ni kweli wakawa wameshaanza kukutana kimwili,” alisema baba na kusimama, akageuka huku na kule, nilishajua ananitafuta mimi na hakuwa akijua kwamba kumbe nilikuwa palepale jirani yao, nikisilikiza kila kilichokuwa kinaendelea.

“Hebu njoo hapa,” alisema huku uso wake ukiwa na jazba, nikasogea huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha chini.

Pale kulikuwa na makundi mawili, baba yake Rahma na baba, wao walikuwa waking’ang’ania kwamba lazima mimi na Rahma tayari tumeshavunja amri ya sita wakati mama na mama yake Rahma, wao walikuwa wakitutetea, kila mmoja na mwanaye.

“Ule mzigo niliokupa safarini uko wapi?” nilishangaa baba akiniuliza swali tofauti kabisa na nililolitegemea. Nikaanza kuvuta kumbukumbu anazungumzia mzigo gani, kwa kutumia tafsida akanifafanulia mpaka nikaelewa kwamba kumbe alikuwa akimaanisha ile dawa aliyonipa pale Mlima Nyoka, Mbeya baada ya kunusurika kwenye ajali mbaya ya gari.

“Ipo nyumbani,” nilimdanganya lakini ukweli ni kwamba licha ya kunisisitiza sana niitunze dawa hiyo, ilikuwa imeniponyoka na kutumbukia kwenye shimo la choo, nyumbani kwa akina Rahma wakati nikioga.

“Una uhakika?”

“Ndi… ndi…yo,” nilibabaika. Baba alikuwa akinijua vizuri, nadhani kwa kubabaika huko, alielewa kwamba dawa hiyo haipo salama, akasimama na kunishika mkono, akanivuta kwa nguvu pembeni.

“Nakuuliza kwa mara ya mwisho, dawa yangu iko wapi?”

“Baba nisamehe, ilitumbukia chooni.”

“Unasemajee?” baba alishtuka kuliko kawaida. Mshtuko aliouonyesha ulinifanya nielewe kwamba kumbe dawa ile kutumbukia chooni halikuwa jambo la kawaida.

“Kwa nini umeniangusha mwanangu? Kwa nini umewapa ushindi?” alisema baba huku akiwa anatingisha kichwa chake kwa masikitiko, nikawa sielewi anamaanisha nini.

“Halafu kwa nini usiniambie mapema ili tujue nini cha kufanya?”

“Nisamehe baba.”

“Nataka uniambie ukweli, wewe umeshafanya mapenzi na Rahma, kweli si kweli?” baba alinihoji, safari hii akiwa amenikazia macho usoni, nikawa nashindwa kama nikubali au nikatae.

“Unaona upumbavu wako? Yaani hili halijaisha umeanzisha jingine, hivi una nini wewe?” alisema baba, akiwa tayari ameshajipa majibu kuhusu swali alilouliza. Nilishindwa cha kusema, nikajiinamia chini kwa aibu, masikitiko na huzuni vyote kwa wakati mmoja.

“Upumbavu ulioufanya utasababisha matatizo makubwa sana kwa watu wasio na hatia, hata sijui itakuwaje,” alisema baba huku akionyesha kuchanganyikiwa kabisa, akaondoka na kuniacha palepale nikiwa nimesimama, na mimi nikiwa nimechanganyikiwa.

Alienda pale alipokuwa amemuacha mama na wazazi wa Rahma, wakawa wanazungumza kitu kisha nikaona wote wamegeuka na kunitazama, hata sijui walikuwa wakizungumza nini.

“Wakiwa bado wananitazama, nesi mmoja alifungua mlango wa wodi aliyokuwemo Rahma na kutoka mbiombio mpaka kwenye ofisi ya madaktari iliyokuwa hapohapo jirani, muda mfupi baadaye akatoka tena mbiombio lakini safari hii alikuwa ameongozana na madaktari wawili ambao nao walikuwa wakikimbia.

Niliwaona akina baba wakikatisha mazungumzo yao na kusimama, huku macho yao yakiwa kwenye ule mlango wa wodi. Mle wodini kulikuwa na wagonjwa kadhaa ila sijui kwa nini akili yangu ilinituma kuamini kwamba walikuwa wakimkimbilia Rahma. Hata akina baba nao nadhani walishajua kwamba mwenye tatizo ni Rahma.

Sikutaka kuandikia mate wakati wino upo, nilitimua mbio kutoka pale nilipokuwa na kukimbilia kwenye mlango wa ile wodi, nikaupiga kikumbo mlango na kuingia mpaka ndani, macho yakiwa pale kwenye kitanda alichokuwa amelazwa Rahma.

Madaktari na manesi walikuwa wamemzunguka, nikasogea kutaka kujionea amepatwa na nini? Nilichokiona sikukiamini. Rahma alikuwa akitapatapa kama anayetaka kukata roho, kibaya zaidi damu nyingi zilikuwa zikimtoka mdomoni na puani, kiasi cha kusababisha mashuka meupe aliyokuwa amelalia yalowe damu.

“Aisee, huruhusiwi kuingia humu, muda wa kuona wagonjwa haujafika,” mlinzi ambaye mkononi alikuwa na rungu kubwa, aliniambia huku akilitingisha lile rungu, akanionyesha ishara kwamba nitoke nje vinginevyo ataniadhibu.

Ilibidi nitoke tu kwani sikutaka matatizo zaidi, ukizingatia na hali niliyomuona nayo Rahma ndiyo nilizidi kuchanganyikiwa.

“Vipi kuna nini?” baba aliniuliza nilipotoka tu, ikabidi nimueleze hali halisi, nikamuona na yeye akishusha pumzi ndefu na kushika kiuno.

“Haya yote ni kwa sababu yako na hawezi kupona kwa kutibiwa hospitali, dawa yake unayo wewe,” alisema baba huku akinitazama kwa macho ya ukali.

“Mimi? Dawa gani?”

“Inabidi ufute makosa ya upumbavu wako wote ulioufanya, hiyo ndiyo itakuwa ponapona yake, mtoto mshenzi sana wewe, wala sikukutegemea,” alisema baba huku akinisogelea mwilini, nikahisi lazima atanizabua makofi kwa sababu anapokasirika sana huwa hawezi kudhibiti hasira zake.

“Itabidi tuwaombe tuondoke naye mpaka nyumbani, nitaenda kukuelekeza nini cha kufanya kumsaidia,” alisema kwa sauti ya kunong’ona, nikahisi kama amechanganyikiwa akili. Yaani kwa hali aliyokuwa nayo, halafu eti akawaombe madaktari tuondoke naye kurudi nyumbani? Niliona ni kitu kisichowezekana.

Baba aligeuka na kuondoka, akasogea pembeni na kuanza kuzungumza na baba yake Rahma. Akina mama wao niliwaona wameshaanza kuchanganyikiwa, mama yake Rahma akawa analia. Nilijisikia vibaya sana ndani ya moyo wangu, hasa kwa jinsi baba alivyokuwa ananishutumu kwamba mimi ndiyo chanzo cha yote yale.

Mara mlango wa wodi ulifunguliwa, daktari mmoja akachungulia nje na kuwaonyesha ishara ya kuwaita baba na baba yake Rahma, mapigo ya moyo wangu yakalipuka mno, sikujua anaenda kuwaambia nini, akilini nikawa nahisi kabisa kwamba mambo yameshaharibika.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na tisa_________19




ILIPOISHIA:

MARA mlango wa wodi ulifunguliwa, daktari mmoja akachungulia nje na kuwaonesha ishara ya kuwaita baba na baba yake Rahma, mapigo ya moyo wangu yakalipuka mno, sikujua anaenda kuwaambia nini, akilini nikawa nahisi kabisa kwamba mambo yameshaharibika.

SASA ENDELEA… “Kuna tatizo.” “Nini tena daktari?” “Mgonjwa wenu anaishiwa damu kwa kasi kubwa mno, isitoshe anatapika damu, hatujui tatizo ni nini kwani vipimo havioneshi tatizo lingine lolote zaidi ya kwamba alikunywa sumu kwa lengo la kujiua.”

“Sasa tutafanyaje dokta?” “Inabidi kwanza tushughulikie hili suala la kupungukiwa damu, inabidi wanandugu muitane kwa ajili ya kuchangia damu, mkiwa tayari mniambie ngoja nizungumze na watu wa kitengo cha damu waandae vifaa,” alisema yule daktari na kuingia wodini, nikawaona baba na baba yake Rahma wakitazamana.

“Nahisi kuna nguvu za giza nyuma ya hili suala na kama tusipotumia nguvu za ziada, tunaweza kumpoteza binti yetu,” alisema baba, mwenzake akawa anatingisha kichwa kuonesha kuunga mkono alichokuwa anakisema. “Mimi nina wazo, unaonaje tukiondoka na mgonjwa wetu tukamtibu nyumbani. Kuna kitu tukikifanya mara moja anapona huyu.”

Nilishangazwa sana na uamuzi walioufikia, yaani mgonjwa ana hali mbaya kiasi kile halafu wamuondoe hospitali na kwenda naye nyumbani? Akifa je? Nilijiuliza bila kupata majibu. Muda mfupi baadaye, baba aligonga tena mlango wa wodi, yule daktari akafungua mlango kwa lengo la kusikiliza walichokiamua. “Mmeshakubaliana kuhusu kuchangia damu?”

“Hapana, imani yetu hairuhusu kuchangia damu, tunamuomba mgonjwa wetu tuondoke naye tukajaribu sehemu nyingine,” alisema baba kwa kujiamini, nikamuona yule daktari akiwatazama wote wawili usoni kwa mshtuko. “Ndivyo mlivyokubaliana?”



“Ndiyo,” alisema baba, nikamuona akishusha pumzi ndefu na kuonesha ishara kwamba wasubiri, akaingia ndani nadhani kwa lengo la kwenda kujadiliana na wenzake, muda mfupi baadaye alipotoka, aliwaambia madaktari wenzake wamekataa wazo hilo, wakawaambia afadhali kama wangekuwa wanaomba rufaa kwenda hospitali kubwa lakini kama ni kumrudisha nyumbani, hilo suala haliwezekani.

“Hawa washenzi sana, kwa hiyo wanaamini hatuwezi kumchukua mgonjwa wetu bila ridhaa yao?” alisema baba huku akimshika mkono baba yake Rahma na kuondoka naye, walitoka mpaka nje kabisa ya eneo la hospitali. Nilikuwa na shauku kubwa ya kumsaidia Rahma, nilipohakikisha akina baba wametoka nje, na nilipowatazama mama na mama Rahma kwa mbali ambao walikuwa wakibembelezana pale kwenye

benchi, harakaharaka nilitembea kuelekea kule wodini. “Unasemaje kijana?” “Huyu ni dada yangu, nataka kumtolea damu.” “Ooh! Umefanya jambo la maana sana, twende huku,” alisema yule daktari huku akinishika mkono, tukatoka wodini na kuanza kutembea harakaharaka kwenye korido, tukaelekea mpaka kwenye chumba maalum cha kutolea damu ambapo niliwakuta watu wengine watatu wakiwa wamekaa kwenye vitanda maalum, wakiwa wanajitolea damu.

“Kaa hapo,” alisema yule daktari huku akinionesha sehemu ya kukaa, akapitiliza na kwenda kuzungumza na mwenzake ambaye alikuwa bize akishughulika na mmoja kati ya wale watu waliokuwa wakitoa damu. Akazungumza naye kisha nikaona wote wawili wamegeuka na kunitazama. Muda mfupi baadaye, yule daktari alitoka na kuniaga, akaniambia nikishamaliza niende nikamuone. Alipotoka, yule daktari mwingine ambaye yeye alikuwa amevalia sare za rangi tofauti, alikuja pale nilipokuwa nimekaa, tukasalimiana kisha akaniuliza kama nilikuwa nataka kujitolea damu, nikamjibu kwamba ni kweli.

Alinisogelea na kuanza kunitazama kwenye mkono wangu wa kushoto, akachukua pamba iliyokuwa na spirit, akanipaka sehemu ya ndani ya mkono wangu kisha akanifunga kwa mpira maalum upande wa juu wa mkono, mishipa ikatokeza kwa wingi mkononi. “Huwa unafanya mazoezi?” aliniuliza.

Nilielewa kwa nini ameniuliza swali lile, kazi ngumu za kijijini, ikiwemo kulima na kupasua kuni zilinifanya mimi na ndugu zangu tuwe na nguvu sana mithili ya watu wanaonyanyua vyuma. “Hapana, ni kazi za kawaida tu,” nilimjibu, akatabasamu na kusema wanaume wengi huwa na miili legelege kwa hiyo linapokuja suala la kuchangia damu, inakuwa vigumu kuuona mshipa mkuu wa damu lakini kwangu mimi ulikuwa ukionekana vizuri na ulikuwa mkubwa kama mtu anayefanya mazoezi.

Nikamuona akichukua sindano moja nene iliyounganishwa na mrija kwa nyuma ulioenda hadi kwenye kibegi kidogo cha plastiki cha kuhifadhia damu. Kiukweli sikuwahi kuchomwa sindano hata mara moja kwenye maisha yangu, kule kijijini kwetu mtu ukiumwa zipo dawa za mitishamba kibao. Ukizingatia baba alikuwa mtaalamu wa mambo hayo, alikuwa akizijua dawa za magonjwa karibu yote. Hata hivyo, sikutaka kuonekana mshamba, ikabidi nijikaze kiume, akanichoma taratibu na kuiingiza ile sindano kwenye mshipa, akanifunga na

bandeji kwa juu kisha akafungua ule mpira, damu ikaanza kutiririka kwa kasi kufuata ule mrija mpaka kwenye kile kimfuko. “Mh! Hii damu yako ikoje?” alisema huku akikiinua kile kimfuko cha damu na kuanza kukitazama kwa karibu. Tofauti na damu za watu wengine mle ndani, yangu ilionesha kuwa nyeusi sana mpaka nikawa najishtukia.

“Ina nini kwani?”

“Ni nyeusi sana na inaganda humu kwenye huu mfuko, sijawahi kukutana na hali kama hii,” alisema huku akinitaka nitulie, akaenda kuwaita wenzake na muda mfupi baadaye, walinizunguka, kila mmoja akiwa ananishangaa. “Unaitwa nani?” “Togo.” “Umewahi kuchangia damu kabla ya leo?” “Hapana, leo ndiyo mara ya kwanza.” “Mbona damu yako iko hivi?” aliniuliza daktari mmoja, ikabidi amuelekeze yule aliyenichomeka ile sindano, harakaharaka wakanitoa ile sindano, wakawa wanaendelea kujadiliana kuhusu damu yangu.

“Tunaomba utusubiri pale nje tutakuita,” alisema yule daktari ambaye ndiye aliyenipeleka kwenye chumba kile, nikainuka huku na mimi nikiwa na maswali mengi kuliko kawaida, nikatoka huku nikiwa nimebana pamba pale kwenye jeraha la sindano ili damu isiendelee kutoka. “Ulikuwa wapi tunakutafuta huku?” baba alinidaka juujuu, macho yake yakatua kwenye pamba niliyokuwa nimeikandamiza pale kwenye jeraha la sindano.



“Na hiki ni nini?” alisema huku akinishika mkono kwa nguvu. “Nilikuwa natoa damu.” “Mungu wangu, hivi wewe mtoto una akili timamu kweli?” alisema baba huku akionesha kushtuka mno, akageuka na kumuonesha ishara baba yake Rahma kwamba aje, harakaharaka akaja mpaka pale tulipokuwa tumesimama.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya ishirini_______20




ILIPOISHIA

“MUNGU wangu, hivi wewe mtoto una akili timamu kweli?” alisema baba huku akionyesha kushtuka mno, akageuka na kumuonyesha ishara baba yake Rahma kwamba aje, harakaharaka akaja mpaka pale tulipokuwa tumesimama.

SASA ENDELEA…

“UNASIKIA majanga ya huyu mtoto aliyoyazua tena?”

“Kuna nini?”

“Eti alikuwa kujitolea damu.”

“Mungu wangu, kwani hujawahi kumwambia ukweli?”

“Ukweli? Ukweli gani?” niliuliza kwa mshtuko.

“Wewe ni mpuuzi sana, yaani hili halijaisha unaanzisha jingine, kwa hiyo tutakuwa na kazi ya kurekebisha makosa yako tu muda wote,” baba alisema kwa kufoka, baba yake Rahma akawa anamtuliza na kumkumbusha kwamba kuna kazi hawajaimaliza.

“Huyu ndiyo ilitakiwa akaifanye hiyo kazi lakini ameshaharibu tena, unafikiri itakuwaje?”

“Twende tu tutajua hukohuko,” alisema baba Rahma huku akinishika mkono, akanipeleka mpaka kwenye gari aina ya Toyota Noah lililokuwa limepaki jirani na geti la kutokea. Kumbe tayari Rahma alishatolewa wodini na alikuwa ameshaingizwa ndani ya gari, mama na mama Rahma wakawa wamempakata.

Tulipoingia tu, gari liliwashwa na kuondoka, mama akageuka na kunitazama kwa uso wa huzuni kama anayeniuliza ‘ulikuwa wapi?’

Nilikaa na kutulia kimya, safari ikaendelea. Watu wote walikuwa kimya kabisa ndani ya gari, sauti pekee iliyokuwa inasikika, ilikuwa ni ya Rahma aliyekuwa anakoroma. Dereva aliendesha gari kwa kasi na baada ya takribani dakika thelathini, tayari tulikuwa tumefika nyumbani.

Siku hiyo hata sikuwa na hamu ya kulishangaa jiji, maghorofa yote ambayo awali nilikuwa na hamu ya kuyatazama jinsi yalivyo marefu na yenye kuvutia, hayakuwa na maana tena kwangu.

Baba na baba yake Rahma walisaidiana kumshusha mgonjwa na moja kwa moja wakampeleka chumbani kwake.

“Nenda bafuni kaoge, usitumie sabuni, utatumia hii badala ya sabuni,” alisema baba huku akinipa kitu kama jiwe laini lenye rangi nyekundu.

Nikageuka na kuanza kuelekea chumbani kwangu kwa lengo la kubadilisha nguo kwanza.

“Unaenda wapi tena? Nimekwambia kaoge, moja kwa moja bafuni nakuja hukohuko,” alisema baba kwa sauti iliyoonyesha kutokuwa na masihara hata chembe. Nilitii alichoniambia, kauli yake kwamba ‘dawa’ ya kumtibu Rahma nilikuwa nayo mimi, ikaanza kujirudia kichwani.

Nilipofika mlangoni, nilivua mabuti yangu, maana siwezi kuita viatu bali mabuti kutokana na jinsi muundo wake ulivyokuwa. Kule kwetu kijijini mabuti hayo yalikuwa yakivaliwa siku za sikukuu au kunapotokea safari kama hiyo tu lakini siku nyingine zote, mimi na wenzangu tulikuwa tukitembea pekupeku, si unajua maisha ya kijijini tena.

Basi niliyavua pale mlangoni na kuvaa ndala, nikaingia bafuni na kuvua nguo, nazo nikazitundika kwenye misumari maalum na kusogea kwenye bomba. Safari hii sikutaka kutumia bomba la mvua kwani tangu niliposhtukia nikioga damu badala ya maji, nilikuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wangu.

Nilichoamua ni kuoga kwa kutumia maji yaliyokuwa kwenye ndoo ya kuogea, nikajimwagia mwilini kwa kutumia kopo kisha nikaanza kujipaka ile dawa aliyonipa baba. Cha ajabu, nilipokuwa nikijipaka, ilikuwa ikitoa povu kama sabuni na ilikuwa na harufu fulani isiyo ya kawaida.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Yote tisa, kumi ni kwamba nilipojimwagia maji tena juu ya ile dawa, nilishangaa maji yaliyokuwa yakitoka mwilini mwangu yakiwa meusi kama maji yaliyochanganywa na mkaa au masizi. Mara ya kwanza nilihisi kama nipo ndotoni, nikakodoa macho lakini ndiyo ulikuwa ukweli.

Ilibidi niendelee kujimwagia maji kwa wingi na kadiri nilivyokuwa nazidi kujimwagia, ndiyo ule weusi ulivyokuwa ukizidi kupungua. Nilijipaka kwa mara ya pili na kujimwagia maji, bado uchafu mweusi ukawa unanitoka kwa wingi, nikawa najimwagia maji kwa wingi mpaka ulipoisha kabisa.

“Ina maana mimi ndiyo nilikuwa mchafu kiasi hiki? Halafu huu ni uchafu gani unakuwa mweusi kiasi hiki?” nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu. Wakati naendelea kuoga, nilisikia mlango ukigongwa, ukafuatiwa na sauti ya baba.

Iweje baba anifuate bafuni? Alikuwa anataka kufanya nini? Nikiwa bado najiuliza maswali, nilisikia tena sauti ya baba akinilazimisha nifungue mlango. Ikabidi nifungue kidogo na kumchungulia.

“Umetumia hiyo dawa?”

“Ndiyo.”

“Umeona nini?”

“Maji meusi kama ya mkaa yalikuwa yananitoka.”

“Safi, sasa vaa hii,” alisema baba huku akinyoosha mkono na kupenyeza kitambaa cheupe kupitia ule upenyo mdogo niliouacha. Akanisisitiza kwamba nisiziguse kabisa nguo zangu, nijifunge na yeye ananisubiri nje.

Nilirudisha mlango na kuufunga vizuri, nikawa nakitazama kile kitambaa alichonipa. Japokuwa sikuwa mzoefu wa shughuli za mazishi kiasi hicho, niliweza kukitambua vizuri kitambaa hicho kwamba kilikuwa ni sanda. Ninavyofahamu mimi, sanda huvalishwa maiti, sasa baba alikuwa na maana gani kuniambia nivae sanda?

Sikupata majibu. Nikawa naendelea kuishangaa sanda hiyo huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida. Nikiwa bado katika hali ile, nilisikia baba akigonga tena mlango kwa nguvu, akaniambia ananisubiri.

Ilibidi niivae harakaharaka, kisha nikafungua mlango. Baba alinitazama kuanzia juu hadi chini, akanirekebisha sehemu ambazo sikuwa nimejifunga vizuri, akatoa kipande kingine na kunifunga kichwani, akanisogelea sikioni na kuniambia:

“Upumbavu uliofanya ndiyo uliotufikisha hapa tulipo. Lazima ufanye kila kinachowezekana kuokoa maisha ya Rahma. Kwa hiyo, utalazimika kufanya kile nitakachokwambia bila kuhoji chochote, ukikosea masharti Rahma atakufa na wewe ndiyo utakuwa umemuua, hutakiwi kuzungumza chochote mpaka tutakapomaliza hii kazi,” alisema baba kwa sauti isiyokuwa na masihara hata kidogo.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Nilizidi kutetemeka, yaani mimi ndiyo niwe nimemuua Rahma? Kwa lipi? Hata hivyo, kwa kuwa ndani ya moyo wangu, licha ya yote yaliyotokea nilishatokea kumpenda mno Rahma, nilichojiapiza ni kwamba nitafanya kila kinachowezekana kuhakikisha naokoa maisha yake.

“Nifuate,” alisema baba huku akigeuka, akawa anatembea kwa hatua ndefundefu, alipofika kwenye mlango wa chumba cha Rahma, aliniambia nigeuke na kuupa mlango mgongo.

“Utaingia kinyumenyume mpaka ndani,” alisema baba, bado kidogo nimuitikie ‘sawa’ lakini nikakumbuka alichoniambia kwamba sitakiwi kuzungumza chochote. Alitangulia, akafungua mlango, nikamfuata kinyumenyume kama alivyonielekeza.

“Chumba kizima kilikuwa kimefukizwa ubani wenye harufu kali, alinipa ishara kwamba niendelee kutembea kinyumenyume mpaka aliponipa ishara kwamba nisimame, nikageuka na kutazama pale kitandani. Rahma alikuwa amelala, damu nyingi zikiendelea kumtoka na kulowanisha kitanda kizima.

Hakuwa na nguo yoyote mwilini zaidi ya kipande cha sanda alichokuwa amefunikwa kuanzia juu kidogo ya mapaja mpaka kifuani ambacho nacho kilikuwa na damudamu.

Baba akanitazama usoni, na mimi nikamtazama nikiwa na shauku kubwa ya kusikia kile atakachoniambia. Nilikuwa tayari kwa chochote ilimradi Rahma apone.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya kumi na nane_______18


ILIPOISHIA:

“SIJUI itakuwaje sasa mume wangu, lazima balaa litokee tuombe tu Mungu Togo atuhakikishie kwamba hawajafanya mapenzi na ndugu yake,” mama Togo alimwambia mumewe.

Wakati wakizungumza hayo, mara wakawaona baba na mama Rahma wanakwenda walipokuwa wakitokea ofisini kwa daktari, wakaacha mazungumzo yao.



SASA ENDELEA…

“VIPI anaendeleaje?”

“Anaendelea vizuri, mtoto mjinga sana huyu.”

“Mh! Usimuite mjinga, huu siyo muda wake, uchungu wake naujua mimi, nimembeba kwenye tumbo langu kwa miezi tisa,” alisema mama yake Rahma akionyesha kutofurahishwa na kauli ya mumewe. Walitoka pamoja na kwenda kukaa kwenye benchi lililokuwa nje ya jengo hilo la hospitali, mimi nikaenda kukaa upande wa pili.

“Hivi, mnajua mimi bado sina majibu juu ya haya maswali niliyonayo.”

“Maswali gani yanayokusumbua?”

“Ni kwa sababu gani Rahma amechukua uamuzi wa kuyakatisha maisha yake?”

“Mh! Hawa watoto wetu wa siku hizi, mimi nahisi alikuwa anampenda Togo sasa kitendo cha kuwaambia kwamba ni ndugu ndiyo maana ameamua kufanya aliyoyafanya, tumshukuru Mungu bado yupo hai.”

“Unachokisema ni sawa lakini nahisi kuna kitu zaidi ya hicho, nahisi hawa watoto walikuwa wameshaanza kufanya mapenzi.”

“Mh! Ninavyomjua Togo huwa hana kawaida ya kuwa karibu na wasichana kabisa, ni muoga sana wa wasichana, sidhani kama hilo linawezekana.”

“Hata Rahma naye si mcharuko kiasi hicho, sijawahi hata kumuona akiwa na mwanaume kichochoroni, kama mambo hayo anayafanya basi anafanya kwa siri sana, kwa ufupi anajiheshimu.”

“Sasa kama tatizo siyo hilo, mnafikiri nini kinaweza kuwa chanzo?”

“Mh! Mimi nakuunga mkono rafiki yangu, kuna kitu nimekihisi na kwa kuunganisha matukio, inawezekana ni kweli wakawa wameshaanza kukutana kimwili,” alisema baba na kusimama, akageuka huku na kule, nilishajua ananitafuta mimi na hakuwa akijua kwamba kumbe nilikuwa palepale jirani yao, nikisilikiza kila kilichokuwa kinaendelea.

“Hebu njoo hapa,” alisema huku uso wake ukiwa na jazba, nikasogea huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha chini.

Pale kulikuwa na makundi mawili, baba yake Rahma na baba, wao walikuwa waking’ang’ania kwamba lazima mimi na Rahma tayari tumeshavunja amri ya sita wakati mama na mama yake Rahma, wao walikuwa wakitutetea, kila mmoja na mwanaye.

“Ule mzigo niliokupa safarini uko wapi?” nilishangaa baba akiniuliza swali tofauti kabisa na nililolitegemea. Nikaanza kuvuta kumbukumbu anazungumzia mzigo gani, kwa kutumia tafsida akanifafanulia mpaka nikaelewa kwamba kumbe alikuwa akimaanisha ile dawa aliyonipa pale Mlima Nyoka, Mbeya baada ya kunusurika kwenye ajali mbaya ya gari.

“Ipo nyumbani,” nilimdanganya lakini ukweli ni kwamba licha ya kunisisitiza sana niitunze dawa hiyo, ilikuwa imeniponyoka na kutumbukia kwenye shimo la choo, nyumbani kwa akina Rahma wakati nikioga.

“Una uhakika?”

“Ndi… ndi…yo,” nilibabaika. Baba alikuwa akinijua vizuri, nadhani kwa kubabaika huko, alielewa kwamba dawa hiyo haipo salama, akasimama na kunishika mkono, akanivuta kwa nguvu pembeni.

“Nakuuliza kwa mara ya mwisho, dawa yangu iko wapi?”

“Baba nisamehe, ilitumbukia chooni.”

“Unasemajee?” baba alishtuka kuliko kawaida. Mshtuko aliouonyesha ulinifanya nielewe kwamba kumbe dawa ile kutumbukia chooni halikuwa jambo la kawaida.

“Kwa nini umeniangusha mwanangu? Kwa nini umewapa ushindi?” alisema baba huku akiwa anatingisha kichwa chake kwa masikitiko, nikawa sielewi anamaanisha nini.

“Halafu kwa nini usiniambie mapema ili tujue nini cha kufanya?”

“Nisamehe baba.”

“Nataka uniambie ukweli, wewe umeshafanya mapenzi na Rahma, kweli si kweli?” baba alinihoji, safari hii akiwa amenikazia macho usoni, nikawa nashindwa kama nikubali au nikatae.

“Unaona upumbavu wako? Yaani hili halijaisha umeanzisha jingine, hivi una nini wewe?” alisema baba, akiwa tayari ameshajipa majibu kuhusu swali alilouliza. Nilishindwa cha kusema, nikajiinamia chini kwa aibu, masikitiko na huzuni vyote kwa wakati mmoja.

“Upumbavu ulioufanya utasababisha matatizo makubwa sana kwa watu wasio na hatia, hata sijui itakuwaje,” alisema baba huku akionyesha kuchanganyikiwa kabisa, akaondoka na kuniacha palepale nikiwa nimesimama, na mimi nikiwa nimechanganyikiwa.

Alienda pale alipokuwa amemuacha mama na wazazi wa Rahma, wakawa wanazungumza kitu kisha nikaona wote wamegeuka na kunitazama, hata sijui walikuwa wakizungumza nini.

“Wakiwa bado wananitazama, nesi mmoja alifungua mlango wa wodi aliyokuwemo Rahma na kutoka mbiombio mpaka kwenye ofisi ya madaktari iliyokuwa hapohapo jirani, muda mfupi baadaye akatoka tena mbiombio lakini safari hii alikuwa ameongozana na madaktari wawili ambao nao walikuwa wakikimbia.

Niliwaona akina baba wakikatisha mazungumzo yao na kusimama, huku macho yao yakiwa kwenye ule mlango wa wodi. Mle wodini kulikuwa na wagonjwa kadhaa ila sijui kwa nini akili yangu ilinituma kuamini kwamba walikuwa wakimkimbilia Rahma. Hata akina baba nao nadhani walishajua kwamba mwenye tatizo ni Rahma.

Sikutaka kuandikia mate wakati wino upo, nilitimua mbio kutoka pale nilipokuwa na kukimbilia kwenye mlango wa ile wodi, nikaupiga kikumbo mlango na kuingia mpaka ndani, macho yakiwa pale kwenye kitanda alichokuwa amelazwa Rahma.

Madaktari na manesi walikuwa wamemzunguka, nikasogea kutaka kujionea amepatwa na nini? Nilichokiona sikukiamini. Rahma alikuwa akitapatapa kama anayetaka kukata roho, kibaya zaidi damu nyingi zilikuwa zikimtoka mdomoni na puani, kiasi cha kusababisha mashuka meupe aliyokuwa amelalia yalowe damu.

“Aisee, huruhusiwi kuingia humu, muda wa kuona wagonjwa haujafika,” mlinzi ambaye mkononi alikuwa na rungu kubwa, aliniambia huku akilitingisha lile rungu, akanionyesha ishara kwamba nitoke nje vinginevyo ataniadhibu.

Ilibidi nitoke tu kwani sikutaka matatizo zaidi, ukizingatia na hali niliyomuona nayo Rahma ndiyo nilizidi kuchanganyikiwa.

“Vipi kuna nini?” baba aliniuliza nilipotoka tu, ikabidi nimueleze hali halisi, nikamuona na yeye akishusha pumzi ndefu na kushika kiuno.

“Haya yote ni kwa sababu yako na hawezi kupona kwa kutibiwa hospitali, dawa yake unayo wewe,” alisema baba huku akinitazama kwa macho ya ukali.

“Mimi? Dawa gani?”

“Inabidi ufute makosa ya upumbavu wako wote ulioufanya, hiyo ndiyo itakuwa ponapona yake, mtoto mshenzi sana wewe, wala sikukutegemea,” alisema baba huku akinisogelea mwilini, nikahisi lazima atanizabua makofi kwa sababu anapokasirika sana huwa hawezi kudhibiti hasira zake.

“Itabidi tuwaombe tuondoke naye mpaka nyumbani, nitaenda kukuelekeza nini cha kufanya kumsaidia,” alisema kwa sauti ya kunong’ona, nikahisi kama amechanganyikiwa akili. Yaani kwa hali aliyokuwa nayo, halafu eti akawaombe madaktari tuondoke naye kurudi nyumbani? Niliona ni kitu kisichowezekana.

Baba aligeuka na kuondoka, akasogea pembeni na kuanza kuzungumza na baba yake Rahma. Akina mama wao niliwaona wameshaanza kuchanganyikiwa, mama yake Rahma akawa analia. Nilijisikia vibaya sana ndani ya moyo wangu, hasa kwa jinsi baba alivyokuwa ananishutumu kwamba mimi ndiyo chanzo cha yote yale.

Mara mlango wa wodi ulifunguliwa, daktari mmoja akachungulia nje na kuwaonyesha ishara ya kuwaita baba na baba yake Rahma, mapigo ya moyo wangu yakalipuka mno, sikujua anaenda kuwaambia nini, akilini nikawa nahisi kabisa kwamba mambo yameshaharibika.

Je, nini kitafuatia?
Litoto Likiazi sana hili...
 
Sehemu ya ishirini na moja______21


ILIPOISHIA:

Hakuwa na nguo yoyote mwilini zaidi ya kipande cha sanda alichokuwa amefunikwa kuanzia juu kidogo ya mapaja mpaka kifuani ambacho nacho kilikuwa na damudamu. Baba akanitazama usoni, na mimi nikamtazama nikiwa na shauku kubwa ya kusikia kile atakachoniambia. Nilikuwa tayari kwa chochote ilimradi Rahma apone.

SASA ENDELEA…

“Mlichokifanya mkidhani ni siri yenu ndicho unachotakiwa kukifanya hapa,” alisema baba huku akigeuka na kuanza kutoka. Ilibidi nimshike mkono na kumvuta, sikuwahi kumfanyia baba hivyo hata siku moja lakini siku hiyo nilijikuta tu nikifanya hivyo.

“Baba!”

“Ambacho huelewi ni nini? Kama unataka apone fanya nilichokwambia na wakati wa tendo hakikisha hiyo sanda huivui,” alisema baba kisha akatingisha kichwa kuonesha kwamba niendelee, akanifinjia kijicho na kuachia tabasamu hafifu. Nilijikuta nikiogopa pengine kuliko kipindi chochote maishani mwangu.

Yaani mtu anaumwa kiasi kile, yupo kwenye hatua za mwisho za kukata roho, halafu eti naambiwa nifanye naye mapenzi, tena mwili wake ukiwa umelowa damu na mimi nikiwa nimevalishwa sanda! Moyo wangu ulipigwa na ganzi.

“Nakupenda Rahma na sinba cha kufanya zaidi ya kukusaidia, namuomba Mungu anisamehe na akusamehe pia na wewe,” nilisema huku machozi yakinilengalenga. Hali aliyokuwa nayo Rahma pale kitandani ilikuwa ya kuhuzunisha mno, nikaamua kupiga moyo konde na kuivaa roho ya kinyama.

Ilikuwa ni lazima niivae roho ya kinyama kwa sababu vinginevyo ningemuonea huruma Rahma kutokana na hali aliyokuwa nayo na pengine huruma yangu ndiyo ingekuwa tiketi yake ya kuendelea kuzimu.

Niliifunua ile sanda kwa mbele na kuacha uwazi, nikafumba macho na kuanza kuvuta hisia za jinsi mimi na Rahma tulivyokuwa tukiogelea kwenye dimbwi la mahaba, kwa mbali hisia zikaanza kunijia. Sikutaka kufumbua macho kabisa, niliendelea kufumba macho, nikapapasa na kupanda juu ya kile kitanda, mapigo ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida.

Nilipiga magoti na kumuweka rahma katikati yangu, nikakisogeza kile kitambaa cha sanda pembeni, nikaendelea kuvuta hisia huku machozi mengi yakinitoka na muda mfupi baadaye, tayari nilikuwa nikiogelea kwenye dimbwi la damu. Niliendelea kujikaza kisabuni, nikawa napiga mbizi hivyohivyo huku nikiendelea kulia.

Katika hali ambayo sikuitegemea, nilishtuka baada ya Rahma kuzinduka na kunikamata mikono yangu kwa nguvu, ikabidi nifumbue macho, nikamuona amefumbua macho yake huku akijiuma midomo kama aliyekuwa akitaka kuzungumza kitu.

‘Ongeza spidi, dawa inakaribia kufanya kazi,” nilisikia sauti ya baba, sijjui hata ilitokea wapi kwani chumba kilikuwa kimefungwa na hata pazia lilikuwa limefunikwa. Nilijisikia aibu sana lakini sikuwa na cha kufanya, nilizidisha kasi ya kile nilichokuwa nakifanya, nikashangaa Rahma akiniachia mikono na kunikumbatia kifuani huku akianza kuangua kilio.

Sikujali damu zilizokuwa zimeulowanisha karibu mwili wake wote na pale kitandani, niliendelea kufanya kile nilichoagizwa na ghafla, nilimuona Rahma akianza kukakamaa mwili wake, nikazidi kuongeza kasi.

“Kuna kitu kitamtoka mdomoni, hakikisha unakikamata,” alisema baba, nikashtuka maana kauli yake ilimaanisha hicho kitakachomtoka kitakuwa na uhai, sasa tangu lini mtu akatoa kiumbe chenye uhai kutoka mdomoni?

Ghafla rahma alifumbua mdomo huku mwili wake wote ukiwa umekakamaa, nikashtukia kiumbe cha ajabu kama panya mweusi lakini asiye na manyoya mwilini akichungulia kutoka mdomoni, nilishtuka mno kiasi cha kunifanya nishindwe kuendelea kufanya kile nilichokuwa.

Ghafla kile kiumbe kiliruka kutoka mdomoni na kuangukia juu ya kitanda, nikasikia sauti ya baba akinisisitiza kwamba lazima nihakikishe nakikamata. Ilikuwa panya siyo panya, chura siyo chura yaani hata sijui nikielezeeje maana kichwa na kiwiliwili kilikuwa kama panya lakini hakuwa na manyoya wala mkia na hata kutembea kwake hakikuwa akikimbia kama panya bali kilikuwa kikiruka kama chura.

Nilijikuta nikipiga moyo konde, moyo wa kijasiri ukanivaa, nikaruka kutoka pale kitandani mpaka chini, nikakirukia kile kiumbe na kufanikiwa kukidaka kwenye mikono yangu lakini cha ajabu, kilipasukia mikononi mwangu, nikashtukia nimeshika mabonge ya damu.

“Safi sana!” baba alisema huku akiingia akiwa ameongozana na baba yake Rahma ambaye naye alianza kunipongeza, wakawa wananipigia makofi. Bado nilijihisi kama nipo ndotoni, sikuelewa kile kiumbe kimepotelea wapi tena na kuniacha na mabonge ya damu mikononi, nikawa natetemeka kuliko kawaida.

“Harakaharaka baba alitoa kitambaa cheupe, akanifuta yale mabonge ya damu na kukiweka kile kitambaa kwenye mfuko mweusi, akatoa wembe, akanichanja kwenye paji la uso, eneo nywele zinapoanzia na kutoa dawa kwenye kichupa, akanipaka na kuisugua kwa nguvu. Dawa ilikuwa ikiuma mno, akarudia kunipongeza kisha akaniambia kazi imekwisha, nimsaidie rahma kumsafisha na kusaficha chumba chote, wakatoka tena huku wote wakionesha kuwa na furaha kubwa mioyoni mwao.

“Togo!”

“Naam Rahma!”

“Nini kimetokea?” alisema Rahma huku akiinuka kitandani, akawa anashangaa kila kitu.

“Ni stori ndefu, naomba twende kwanza ukaoge,” nilimwambia, harakaharaka nikamuona akiinuka na kukimbilia khanga yake, akajifunga huku akionekana kunionea aibu. Hakuwa Rahma yule ambaye muda mfupi uliopita alikuwa akikaribia kukata roho, alishabadilika na kuchangamka utafikiri hakuna kilichotokea.

Baada ya kujifunga khanga, alisogea kwenye dressing table na kujitazama, nikamuona jinsi alivyoshtuka.

“Mungu wangu, mbona nimelowa damu hivi? Halafu mbona na wewe umelowa damu? Kwani nini kimetokea?” alihoji Rahma, ikabidi nivae tabasamu la uongo ili kumuondolea hofu moyoni. Nakumbuka baba amewahi kunifundisha kwamba njia nzuri ya kuishi na wanawake, ni pale wanapoonekana kulichukulia tatizo kwa ukubwa, wewe lirahisishe.

Hatua hiyo kweli ilifanikiwa sana, kwani licha ya mshtuko aliokuwa nao, aliponiona mimi nikitabasamu, Rahma aliamini kwamba kilichotokea hakikuwa tatizo kubwa, nikamshika mkono na kutaka kutoka naye tuelekee bafuni.

“Hiki nini ulichovaa?” aliniuliza, nikamtazama usoni na kumuomba anipe khanga nyingine na mimi nijifunge.

“Hujanijibu lakini.”

“Mbona una haraka ya kujua mambo yote mara moja? Nimekwambia nitakueleza kila kitu, kuwa mpole.”

“Halafu mimi si nilitaka kujiua?” alisema akiwa ni kama ameanza kurudiwa na fahamu zake, nikachukua khanga mwenyewe na kumshika mkono kumpeleka bafuni maana niliona akili yake bado ina mawenge.

“Utumie ile sabuni niliyokuwa kuogea wewe na yeye,” baba alisema, wote tukageuka na kuwatazama, kumbe walikuwa wakituangalia, wakiwa ni kama hawaamini kama Rahma yule aliyekuwa akikaribia kunusa umauti, ndiyo yule aliyekuwa akitembea mwenyewe.

“Nilifungua mlango wa bafuni, nikamtanguliza Rahma, nikamuona akitaka kujifungia mlango lakini nilisukuma na kuingia.

“Wanatuona, unafikiri baba na mama watatuelewaje?”

“Wao ndiyo wamenipa kazi ya kukusaidia kwa hiyo usiwe na wasiwasi,” nilisema huku nikifunga mlango kwa ndani, rahma akawa ananitazama kwa macho yenye maswali mengi bila majibu.

“Unatakiwa kuoga kwa kutumia hii sabuni,” nilisema huku nikimpa kile kijiwe cha ajabu nilichopewa an baba, ambacho nilikiacha humohumo bafuni, Rahma akawa bado anashangaashangaa, ilibidi nimdogeze kwenye bomba, nikafungulia maji, yakaanza kumwagikia ambapo alionekana kama kuanza kuzinduka.

“Kile nilichokiona mle bafuni na kuhisi kama naoga damu, ndicho kilichokuwa kinatokea muda huo kwani maji yaliyokuwa yakichuruzika kutoka kwenye mwili wa Rahma, yalikuwa damu tupu, nikavuta kumbukumbu na kuhisi labda kile kilichonitokea kilikuwa na uhusiano na tukio hilo.

Nilijifungua ile sanda, na mimi nikabaki kama Rahma, nikasogea pale kwenye bomba, maji yakawa yanatumwagikia, chini damu zikawa zinaendelea kutiririka kuelekea kwenye bomba la kutolea maji machafu. Nilimshika mikono Rahma, nikamvutia kwenye kifua changu, tukawa tunatazamana huku maji yakiendelea kutumwagikia, nikajikuta nikitamani kumbusu mdomoni.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya ishirini na moja______21


ILIPOISHIA:

Hakuwa na nguo yoyote mwilini zaidi ya kipande cha sanda alichokuwa amefunikwa kuanzia juu kidogo ya mapaja mpaka kifuani ambacho nacho kilikuwa na damudamu. Baba akanitazama usoni, na mimi nikamtazama nikiwa na shauku kubwa ya kusikia kile atakachoniambia. Nilikuwa tayari kwa chochote ilimradi Rahma apone.

SASA ENDELEA…

“Mlichokifanya mkidhani ni siri yenu ndicho unachotakiwa kukifanya hapa,” alisema baba huku akigeuka na kuanza kutoka. Ilibidi nimshike mkono na kumvuta, sikuwahi kumfanyia baba hivyo hata siku moja lakini siku hiyo nilijikuta tu nikifanya hivyo.

“Baba!”

“Ambacho huelewi ni nini? Kama unataka apone fanya nilichokwambia na wakati wa tendo hakikisha hiyo sanda huivui,” alisema baba kisha akatingisha kichwa kuonesha kwamba niendelee, akanifinjia kijicho na kuachia tabasamu hafifu. Nilijikuta nikiogopa pengine kuliko kipindi chochote maishani mwangu.

Yaani mtu anaumwa kiasi kile, yupo kwenye hatua za mwisho za kukata roho, halafu eti naambiwa nifanye naye mapenzi, tena mwili wake ukiwa umelowa damu na mimi nikiwa nimevalishwa sanda! Moyo wangu ulipigwa na ganzi.

“Nakupenda Rahma na sinba cha kufanya zaidi ya kukusaidia, namuomba Mungu anisamehe na akusamehe pia na wewe,” nilisema huku machozi yakinilengalenga. Hali aliyokuwa nayo Rahma pale kitandani ilikuwa ya kuhuzunisha mno, nikaamua kupiga moyo konde na kuivaa roho ya kinyama.

Ilikuwa ni lazima niivae roho ya kinyama kwa sababu vinginevyo ningemuonea huruma Rahma kutokana na hali aliyokuwa nayo na pengine huruma yangu ndiyo ingekuwa tiketi yake ya kuendelea kuzimu.

Niliifunua ile sanda kwa mbele na kuacha uwazi, nikafumba macho na kuanza kuvuta hisia za jinsi mimi na Rahma tulivyokuwa tukiogelea kwenye dimbwi la mahaba, kwa mbali hisia zikaanza kunijia. Sikutaka kufumbua macho kabisa, niliendelea kufumba macho, nikapapasa na kupanda juu ya kile kitanda, mapigo ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida.

Nilipiga magoti na kumuweka rahma katikati yangu, nikakisogeza kile kitambaa cha sanda pembeni, nikaendelea kuvuta hisia huku machozi mengi yakinitoka na muda mfupi baadaye, tayari nilikuwa nikiogelea kwenye dimbwi la damu. Niliendelea kujikaza kisabuni, nikawa napiga mbizi hivyohivyo huku nikiendelea kulia.

Katika hali ambayo sikuitegemea, nilishtuka baada ya Rahma kuzinduka na kunikamata mikono yangu kwa nguvu, ikabidi nifumbue macho, nikamuona amefumbua macho yake huku akijiuma midomo kama aliyekuwa akitaka kuzungumza kitu.

‘Ongeza spidi, dawa inakaribia kufanya kazi,” nilisikia sauti ya baba, sijjui hata ilitokea wapi kwani chumba kilikuwa kimefungwa na hata pazia lilikuwa limefunikwa. Nilijisikia aibu sana lakini sikuwa na cha kufanya, nilizidisha kasi ya kile nilichokuwa nakifanya, nikashangaa Rahma akiniachia mikono na kunikumbatia kifuani huku akianza kuangua kilio.

Sikujali damu zilizokuwa zimeulowanisha karibu mwili wake wote na pale kitandani, niliendelea kufanya kile nilichoagizwa na ghafla, nilimuona Rahma akianza kukakamaa mwili wake, nikazidi kuongeza kasi.

“Kuna kitu kitamtoka mdomoni, hakikisha unakikamata,” alisema baba, nikashtuka maana kauli yake ilimaanisha hicho kitakachomtoka kitakuwa na uhai, sasa tangu lini mtu akatoa kiumbe chenye uhai kutoka mdomoni?

Ghafla rahma alifumbua mdomo huku mwili wake wote ukiwa umekakamaa, nikashtukia kiumbe cha ajabu kama panya mweusi lakini asiye na manyoya mwilini akichungulia kutoka mdomoni, nilishtuka mno kiasi cha kunifanya nishindwe kuendelea kufanya kile nilichokuwa.

Ghafla kile kiumbe kiliruka kutoka mdomoni na kuangukia juu ya kitanda, nikasikia sauti ya baba akinisisitiza kwamba lazima nihakikishe nakikamata. Ilikuwa panya siyo panya, chura siyo chura yaani hata sijui nikielezeeje maana kichwa na kiwiliwili kilikuwa kama panya lakini hakuwa na manyoya wala mkia na hata kutembea kwake hakikuwa akikimbia kama panya bali kilikuwa kikiruka kama chura.

Nilijikuta nikipiga moyo konde, moyo wa kijasiri ukanivaa, nikaruka kutoka pale kitandani mpaka chini, nikakirukia kile kiumbe na kufanikiwa kukidaka kwenye mikono yangu lakini cha ajabu, kilipasukia mikononi mwangu, nikashtukia nimeshika mabonge ya damu.

“Safi sana!” baba alisema huku akiingia akiwa ameongozana na baba yake Rahma ambaye naye alianza kunipongeza, wakawa wananipigia makofi. Bado nilijihisi kama nipo ndotoni, sikuelewa kile kiumbe kimepotelea wapi tena na kuniacha na mabonge ya damu mikononi, nikawa natetemeka kuliko kawaida.

“Harakaharaka baba alitoa kitambaa cheupe, akanifuta yale mabonge ya damu na kukiweka kile kitambaa kwenye mfuko mweusi, akatoa wembe, akanichanja kwenye paji la uso, eneo nywele zinapoanzia na kutoa dawa kwenye kichupa, akanipaka na kuisugua kwa nguvu. Dawa ilikuwa ikiuma mno, akarudia kunipongeza kisha akaniambia kazi imekwisha, nimsaidie rahma kumsafisha na kusaficha chumba chote, wakatoka tena huku wote wakionesha kuwa na furaha kubwa mioyoni mwao.

“Togo!”

“Naam Rahma!”

“Nini kimetokea?” alisema Rahma huku akiinuka kitandani, akawa anashangaa kila kitu.

“Ni stori ndefu, naomba twende kwanza ukaoge,” nilimwambia, harakaharaka nikamuona akiinuka na kukimbilia khanga yake, akajifunga huku akionekana kunionea aibu. Hakuwa Rahma yule ambaye muda mfupi uliopita alikuwa akikaribia kukata roho, alishabadilika na kuchangamka utafikiri hakuna kilichotokea.

Baada ya kujifunga khanga, alisogea kwenye dressing table na kujitazama, nikamuona jinsi alivyoshtuka.

“Mungu wangu, mbona nimelowa damu hivi? Halafu mbona na wewe umelowa damu? Kwani nini kimetokea?” alihoji Rahma, ikabidi nivae tabasamu la uongo ili kumuondolea hofu moyoni. Nakumbuka baba amewahi kunifundisha kwamba njia nzuri ya kuishi na wanawake, ni pale wanapoonekana kulichukulia tatizo kwa ukubwa, wewe lirahisishe.

Hatua hiyo kweli ilifanikiwa sana, kwani licha ya mshtuko aliokuwa nao, aliponiona mimi nikitabasamu, Rahma aliamini kwamba kilichotokea hakikuwa tatizo kubwa, nikamshika mkono na kutaka kutoka naye tuelekee bafuni.

“Hiki nini ulichovaa?” aliniuliza, nikamtazama usoni na kumuomba anipe khanga nyingine na mimi nijifunge.

“Hujanijibu lakini.”

“Mbona una haraka ya kujua mambo yote mara moja? Nimekwambia nitakueleza kila kitu, kuwa mpole.”

“Halafu mimi si nilitaka kujiua?” alisema akiwa ni kama ameanza kurudiwa na fahamu zake, nikachukua khanga mwenyewe na kumshika mkono kumpeleka bafuni maana niliona akili yake bado ina mawenge.

“Utumie ile sabuni niliyokuwa kuogea wewe na yeye,” baba alisema, wote tukageuka na kuwatazama, kumbe walikuwa wakituangalia, wakiwa ni kama hawaamini kama Rahma yule aliyekuwa akikaribia kunusa umauti, ndiyo yule aliyekuwa akitembea mwenyewe.

“Nilifungua mlango wa bafuni, nikamtanguliza Rahma, nikamuona akitaka kujifungia mlango lakini nilisukuma na kuingia.

“Wanatuona, unafikiri baba na mama watatuelewaje?”

“Wao ndiyo wamenipa kazi ya kukusaidia kwa hiyo usiwe na wasiwasi,” nilisema huku nikifunga mlango kwa ndani, rahma akawa ananitazama kwa macho yenye maswali mengi bila majibu.

“Unatakiwa kuoga kwa kutumia hii sabuni,” nilisema huku nikimpa kile kijiwe cha ajabu nilichopewa an baba, ambacho nilikiacha humohumo bafuni, Rahma akawa bado anashangaashangaa, ilibidi nimdogeze kwenye bomba, nikafungulia maji, yakaanza kumwagikia ambapo alionekana kama kuanza kuzinduka.

“Kile nilichokiona mle bafuni na kuhisi kama naoga damu, ndicho kilichokuwa kinatokea muda huo kwani maji yaliyokuwa yakichuruzika kutoka kwenye mwili wa Rahma, yalikuwa damu tupu, nikavuta kumbukumbu na kuhisi labda kile kilichonitokea kilikuwa na uhusiano na tukio hilo.

Nilijifungua ile sanda, na mimi nikabaki kama Rahma, nikasogea pale kwenye bomba, maji yakawa yanatumwagikia, chini damu zikawa zinaendelea kutiririka kuelekea kwenye bomba la kutolea maji machafu. Nilimshika mikono Rahma, nikamvutia kwenye kifua changu, tukawa tunatazamana huku maji yakiendelea kutumwagikia, nikajikuta nikitamani kumbusu mdomoni.

Je, nini kitafuatia?
Usije kushangaa alivyo kiazi akamgonga tena bila maelekezo.
 
Sehemu ya ishirini na mbili ______22



ILIPOISHIA:

Nilijifungua ile sanda, na mimi nikabaki kama Rahma, nikasogea pale kwenye bomba, maji yakawa yanatumwagikia, chini damu zikawa zinaendelea kutiririka kuelekea kwenye bomba la kutolea maji machafu. Nilimshika mikono Rahma, nikamvutia kwenye kifua changu, tukawa tunatazamana huku maji yakiendelea kutumwagikia, nikajikuta nikitamani kumbusu mdomoni.

SASA ENDELEA…

“Mbona najisikia hivi?”

“Unajisikiaje?”

“Hata sijui nisemeje lakini najisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu,” alisema Rahma na kabla hata sijafanya kile nilichokuwa nakitamani, yeye alinianza akanibusu kwa midomo yake milaini huku akinikumbatia kwa nguvu, na mimi nikamuonesha ushirikiano.

“Kwa nini ulitaka kujiua?” nilimuuliza, akafumbua macho yake ambayo kwa muda wote alikuwa ameyafumba, akanitazama usoni bila kusema chochote, akajiinamia. Niligundua kwamba hakulipenda swali hilo, nikaamua kubadilisha mada lakini bado hakuzungumza chochote.

Nilimsaidia kumsafisha mwili wake wote mpaka damu zote zikaisha kwenye miili yetu, nikafunga maji na kumpa khanga yake lakini aliikataa kwa sababu nayo ilikuwa na damu.

“Vaa tu kwanza tutaoga tena kwa mara nyingine, inabidi tukafanye usafi chumbani kwako,” nilimwambia, akakubali. Tulichukua ndoo za maji na vifaa vya kufanyia usafi, tukaelekea chumbani kwake ambako kila sehemu ilikuwa imechafuka kwa damu.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Tukaanza kufanya usafi lakini bado Rahma hakuzungumza chochote, muda wote alikuwa kimya kabisa na pale alipohitaji kunielekeza jambo, alikuwa akitumia zaidi ishara.

“Mbona umebadilika ghafla? Nisamehe kama kuna kitu nimekukwaza,” nilimwambia, akanitazama tena.

“Kwani nini kilitokea?”

“Wewe unakumbuka nini?”

“Nakumbuka niliamua kunywa sumu ili nife.”

“Kwa nini?”

“Kwa sababu nakupenda.”

“Sasa ukimpenda mtu ndiyo ujiue?”

“Kwa sababu walituambia kwamba sisi ni ndugu,” alisema Rahma huku akiacha kila alichokuwa anakifanya, machozi yakaanza kumtoka.

“Kumbe walisema vile kututishia kwamba tusije tukaanza kufanya mapenzi lakini siyo kweli, hatuna undugu ila baba yangu na baba yako ni marafiki tangu wakiwa vijana wadogo kwa hiyo ni kama ndugu tu,” nilimwambia.

Hata mimi maneno hayo niliwasikia mama na mama yake Rahma wakiongea kule hospitalini, wakilaumiana kwa maneno waliyotuambia ambayo ndiyo yaliyosababisha Rahma achukue uamuzi wa kuyakatiza maisha yake.

Nilipomueleza maneno hayo, alinitolea macho akiwa ni kama haamini, akanisogelea na kunishika mkono, akawa ananitingisha kwa nguvu akitaka nimhakikishie kwamba ni kweli. Nikarudia tena kumueleza vilevile, jambo lililosababisha anikumbatie na kuanza upya kulia.

“Nisamehe! Niliona bora nife tu kuliko kuishi bila wewe, nimejikuta nikikupenda mno mwenzako, utafikiri tulijuana miaka mingi nyuma,” alisema huku akiendelea kulia.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

“Na hizi damu imekuwaje?” aliniuliza, kama nilivyokuwa nikimjibu mwanzo, nikamwambia asiwe na haraka atajua kila kitu kilichotokea. Alinibusu tena, tukaendelea kufanya usafi. Ilibidi nguo zote zilizokuwa zimechafuka kwa damu, tuzikusanye kwa ajili ya kwenda kuzifua, tulitoa kuanzia mashuka mpaka foronya.

Tukasaidiana kupiga deki kwa kutumia sabuni maalum, chumba chote kikawa kisafi kabisa. Baada ya kumaliza, tulibeba furushi la nguo chafu kwa ajili ya kwenda kuzifua kule bafuni lakini wakati tukitoka, baba alikuja kutuambia kwamba nguo hizo hazikutakiwa kwenda kufuliwa bali inabidi zikachomwe moto.

Itabidi mvue hata hizo mlizovaa, zote hizi ni za kuchoma moto, tena inabidi nyie wenyewe kwa mikono yenu. Tulifanya kama baba alivyotuelekeza na muda mfupi baadaye, tulikuwa tumemaliza kila kitu, ikabidi tukaoge tena na safari hii, kila mtu alienda kuoga peke yake. Rahma alinipa fulana yake moja niivae kwani sikuwa na nguo zozote za maana nilizobeba kutoka kule kijijini.

“Baba yako amenipa hii pesa anasema muende sehemu yoyote nzuri mkatembee na Togo, hata kama ni ‘beach’ ila msichelewe kurudi,” alisema mama yake Rahma huku akitoa noti mbili nyekundu na kumpa Rahma.

“Lakini mama, naomba unisamehe!”

“Usijali, tumeshakusamehe Rahma, tunamshukuru Mungu kwa kukuokoa kutoka kwenye bonde la mauti. Jioni mtapenda kula nini?” alisema mama yake Rahma kwa upole wa ajabu.

Hata mimi nilishangaa sana, nilitegemea kwamba baada ya kila kitu kutulia, lazima mimi na Rahma tulikuwa na kesi ya kujibu lakini mambo yakawa tofauti kabisa.

“Nataka tule pilau, si ndiyo Togo,” alijibu Rahma, na mimi nikatingisha tu kichwa. Kule kijijini kwetu, pilau lilikuwa likipikwa sikukuu tu, tena Krismasi, nikajikuta nikijilamba midomo yangu kwa uchu. Baada ya hapo, mama yake Rahma alitoka na kututakia matembezi mema.

“Twende wapi kutembea,” alisema Rahma huku akinikumbatia na kunibusu, nikamwambia mimi sijui sehemu yoyote kwa hiyo yeye ndiyo aniongoze, akacheka sana na kunipiga mgongoni. Yaani kama kuna mtu alimuona Rahma saa chache zilizopitahali aliyokuwa nayo, asingeamini kwamba ndiye yeye.

Harakaharaka alianza kujiandaa, akaenda tena kuoga na kurudi chumbani kwake, mimi nikawa nimekaa kwenye kiti cha pembeni. Niweke wazi kwamba safari hii sikuwa naogopa chochote ikwa sababu baba na baba yake Rahma ndiyo walioniruhusu kuwa karibu na Rahma wakihofia kwamba kama wataendelea ukali juu yetu, anaweza kujidhuru tena.

Na waliniambia natakiwa nisimuache peke yake kule chumbani kwake kwa hiyo nilikuwepo pale kihalali kabisa ingawa waliniambia kwamba sitakiwi kufanya chochote naye kwa sababu kulikuwa na mambo yasiyo ya kawaida wameyabaini na chanzo cha yote ilikuwa ni mimi kufanya naye mapenzi.

“Hebu niambie Togo, unanipenda kweli kama mimi ninavyokupenda?”

“Nakupenda tena sana,” nilimwambia, nikamuona akiachia tabasamu pana, akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa, akanishika mkono na kunivuta ili nisimame, nikatii, alinivutia kifuani kwake na kunibusu kimahaba, na mimi nikafanya kama yeye.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

“Kama kweli unanipenda nataka unioe,” alisema Rahma kwa sauti ya kunong’ona, akanibusu tena.

“Usijali kabisa, kwako nipo tayari kwa chochote,” nilimwambia. Kiukweli nilimjibu tu kwa lengo la kumfurahisha maana niliambiwa sitakiwi kumuudhi kwa chochote. Baada ya hapo, aliniachia na kwenda kufungua kabati, akaniambia nimsaidie kuchagua nguo ya kuvaa.

Kwangu ulikuwa mtihani mkubwa sana kwani wakati mwingine alikuwa akiiachia ile khanga aliyotoka nayo bafuni na kuufanya mwili wake wenye mvuto wa kipekee ubaki wazi, nikawa na kazi ya ziada. Baadaye aliipata nguo aliyoitaka mwenyewe, akavaa gauni zuri lililompendeza na kujitanda ushungi.

Kwenye suala la mavazi, Rahma alikuwa akijitahidi sana, alikuwa akivaa mavazi ya heshima tofauti na wasichana wengi wa mjini. Mimi sikuwa na cha kubadilisha, vilevile nilivyokuwa nimevaa, tulitoka, nikataka kuvaa mabuti yangu lakini akaniambia kuna raba nzuri huwa anafanyia mazoezi, akaingia tena ndani na kutoka nazo.

Zilinipendeza vizuri, nikawa nachekacheka tu, tulienda sebuleni na kuaga, ndugu zangu waliokuwa wamenogewa na tivii, walinitazama kwa macho ya wivu, tukatoka mpaka nje ambapo Rahma alipunga mkono upande kulipokuwa kumepaki Bajaj, ikaja moja, tukaingia na kukaa.

“Tupeleke Coco Beach, kule wanakouza mihogo,” alisema Rahma, safari ikaanza lakini mita chache mbele, nilishtuka baada ya kusikia mtu akiliita jina langu kwa nguvu, tena sauti yenyewe ilikuwa ya kike, ilibidi Rahma amwambie dereva asimame, tukageuka nyuma kutazama ni nani aliyekuwa ananiita kwa sababu mimi nilikuwa mgeni na hakuna mtu yeyote aliyekuwa akilifahamu jina langu zaidi ya wale tuliokuwa tukiishi pamoja.

Je, nini kitafuatia?
 
Back
Top Bottom