feisal firdaus
JF-Expert Member
- Apr 6, 2022
- 424
- 675
Sema ni kusadikika tunaishi nayo hivyo hivyo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
[emoji38][emoji38][emoji38]Hilo toto si angebadilishana kwa gunia mbili za mkaa tu.
NarudiSehemu ya Saba ----07
ILIPOISHIA:
Wale wageni waliaga na kuondoka, baba akatuita tena ndani na kuanza kuhesabu fedha zilizopatikana. Zilikuwa ni shilingi milioni mbili na laki tatu, akasema zingetosha kabisa kwa safari yetu. Tukakubaliana kwamba tumalizie maandalizi na asubuhi ya siku ya pili tuianze safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam.
SASA ENDELEA…
Kweli usiku huo hakuna hata aliyepata lepe la usingizi, ‘kimuhemuhe’ cha safari kilitufanya tukae macho mpaka jogoo la kwanza lilipokuwa linawika. Baba alituagiza kwamba tubebe vile vitu vya muhimu tu kwa sababu maisha ya kijijini yalikuwa tofauti sana na maisha ya mjini.
Akatuambia vitu vingine tuviache palepale na vitakuwa salama kwa sababu kuna walinzi anawaacha kwa ajili ya kutulindia mji wetu. Aliposema walinzi sikumuelewa kwa haraka anamaanisha nini, akili nyingine zikanituma kuamini kwamba labda watakuwa ni mgambo lakini nilijiuliza anaweza kuwaacha mgambo ndiyo walinde nyumba yetu wakati hawakuwa wakielewana? Sikupata majibu.
Saa kumi na nusu za usiku, tulitoka na kuanza kutembea kuelekea stendi, kila mmoja akiwa na mzigo wake. Tukaenda mpaka stendi ambapo tulipanda gari la kwanza kabisa ambalo lilikuwa likielekea Mbeya mjini, lakini cha ajabu, wakati wote tumeshapanda kwenye gari, baba yeye alibaki chini.
Tukawa tunasubiri na yeye apande lakini hakufanya hivyo, sanasana tukamuona akiwa anazungumza na mama, kupitia dirisha la gari lile tulilokuwa tumepanda, nadhani alikuwa akimpa maelekezo muhimu sana kwa sababu muda wote mama alikuwa akitingisha kichwa kuashiria kuelewa kile alichokuwa akiambiwa.
Baada ya kumaliza kuzungumza na mama, baba alikuja moja kwa moja pale nilipokuwa nimekaa mimi, akanipa mkono na kuniambia kwamba tutangulie yeye atafuata, akaniambia ananiamini mimi zaidi kwa hiyo lazima niwe makini kuwalinda ndugu zangu.
Nilijisikia fahari sana kwa jinsi baba alivyokuwa akinipa kipaumbele kwenye mambo ya msingi japokuwa nilikuwa na kaka zangu na mimi ndiyo nilikuwa mdogo. Baada ya dakika chache, dereva aliingia ndani ya gari, akawasha na safari ya kutoka Makongorosi kuelekea Mbeya mjini ikaanza.
Safari haikuwa nyepesi, kwa sababu sehemu kubwa ya njia ya kutokea Chunya kuelekea Mbeya mjini, ni milima na mabonde makubwa, ikiambatana na miteremko ambayo kama dereva hayupo makini hamuwezi kufika salama. Ukizingatia na lile giza la alfajiri ile, kila mmoja alikuwa akiomba moyoni tufike salama. Baada ya safari ndefu, hatimaye tuliwasili Mbalizi, gari likashusha baadhi ya abiria na kuingia Barabara Kuu ya Mbeya-Tunduma ambayo ni ya lami, likaendelea na safari ya kuelekea Mbeya Mjini.
Nikiri kwamba hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika mjini na kila kitu kwangu kilikuwa kigeni. Sikuwahi kuona barabara ya lami, sikuwahi kuona magari mengi ya kila aina wala sikuwahi kuona nyumba nzuri na za kisasa, nyingine zikiwa na maghorofa.
Ilikuwa ni safari ambayo iliufurahisha mno moyo wangu, nikawa nachekacheka tu mwenyewe. Hali ilikuwa hivyohivyo kwa ndugu zangu wengine ambao nao walikuwa na ushamba ulioonekana waziwazi kwenye sura zao. Safari yetu ilienda kuishia kwenye Stendi Kuu ya Mabasi ya Mbeya au maarufu kama Mbeya Terminal.
Cha ajabu, wakati gari likikata kona kuelekea sehemu ya kushushia abiria, nilimuona baba akiwa chini, akilitazama gari tulilokuwa tumepanda. Nikabaki na maswali mengi yasiyokuwa na majibu, kwamba alifikaje kabla yetu? Kumbukumbu zangu zilinionesha kwamba kule Chunya, stendi kulikuwa na gari moja tu ambalo ndiyo hilo ambalo sisi tulipanda.
Na safari nzima, hatukupitwa na gari lingine lolote, wala chombo kingine cha usafiri, si bodaboda wala Bajaj, sasa baba alifikaje pale kabla yetu? Yalikuwa ni maswali ambayo sikuwa na majibu yake. Lakini cha ajabu, nilipomgeukia mama wala hakuonesha kushtushwa na uwepo wa baba eneo lile, nikamuona akimpungia mkono kama anayemwambia ‘tuko hapa’.
Gari liliposimama, baba ndiye aliyekuwa akitupokea mizigo, ndugu zangu wote walionekana kuchukulia uwepo wa baba eneo lile kama kitu cha kawaida, kwa kifupi hakuna aliyekuwa na akili ya udadisi kama niliyokuwa nayo mimi, nadhani ndiyo maana baba alikuwa akinipenda zaidi yao.
Alitupokea mizigo na kutusaidia kushuka, tukasimama pembeni ya gari, mimi nikawa namtazama nikiwa sina majibu ya maswali yangu kabisa. Mimi na ndugu zangu wote tulikuwa tumechafuka miili yetu kwa sababu ya kusafiri kwenye barabara ya vumbi kutoka Chunya lakini baba yeye alikuwa msafi kabisa.
“Tunasafiri na basi lile pale,” alisema baba kwa sauti ambayo wote tuliisikia vizuri, akatuonesha kwenye basi kubwa lililokuwa limeinama upande wa mbele kama ndege ya kijeshi, wote tukawa tunalitazama basi lile kwani muundo wake ulikuwa wa aina yake na sidhani kama kuna yeyote kati yetu ambaye aliwahi kuliona basi kama hilo kwa macho.
Basi tulibeba vifurushi vyetu na kuanza kumfuata baba ambaye alitupeleka mpaka kwenye lile basi, yeye akawa wa kwanza kuingia, akawa anatusaidia kupanda ngazi mmoja baada ya mwingine. Wa mwisho alikuwa mama ambaye alikuwa na mzigo mkubwa, baada ya kuingia, baba alianza kusoma namba za siti zilizokuwa zimeandikwa upande wa juu wa basi hilo kubwa, mpaka alipozipata.
Kila mtu alikuwa na siti yake, akawa anatuelekeza sehemu za kukaa, akampa mama tiketi zetu wote kisha nikamuona akizungumza naye mambo fulani, akaingiza mkono mfukoni na kutoa noti kadhaa za shilingi elfu kumikumi, mama akamshukuru, kisha akamuinamia sikioni na kumuongelesha mambo ambayo hakuna aliyesikia.
Wakati akimnong’oneza mama, macho ya baba yalikuwa kwangu, nilipoona ananiangalia, ikabidi nikwepeshe macho yangu kwani tulifundishwa kwamba siyo heshima kuwatazama baba na mama wanapokuwa na mazungumzo yao ya siri.
Baada ya hapo, alikuja pale nilipokuwa nimekaa, akaniinamia na kurudia kuniambia maneno yaleyale aliyoniambia wakati tukiondoka kule Chunya. Aliniambia kwamba ukimtoa mama, mimi ndiye niliyepaswa kuwa mkuu wa msafara na lazima nihakikishe tunafika salama salmini tuendako, akanipigapiga mgongoni kisha akanipa mkono.
Alifanya hivyohivyo kwa ndugu zangu wengine pia, akawapa mkono mmoja baada ya mwingine kisha akarudi kwangu na kuniambia kwamba tutangulie yeye anafuata.
“Lakini baba… sisi wote ni wageni huko tunakoenda, kwa nini usikae na sisi kwenye hili basi? Tukipotea je?” nilimuuliza, swali lililomfanya anitazame usoni kwa makini, nikakwepesha macho yangu kwa sababu baba alikuwa na hali fulani ambayo akikukazia macho lazima utazame pembeni.
“Kwani kutoka Chunya kuja hapa nani alikuwa wa kwanza kufika?” aliniuliza, swali lililonifanya nipate nafasi ya kutoa dukuduku nililokuwa nalo moyoni.
“Tena nilitaka kukuuliza, kwani ulikuja na usafiri gani na kwa nini wewe hujachafuka kama sisi?”
‘Wewe ni mwanaume, lazima ujifunzwe kuwa na akiba ya maneno, siyo kila unachokiona ukizungumze au uulize, sijakuzaa kuja kuwa msindikizaji maishani mwako,” alisema kwa sauti ya chini ambayo ni mimi tu niliyeisikia lakini ilityokuwa imebeba ujumbe mzito sana ndani yake, nikashusha pumzi na kukaa vizuri kwenye sitio yangu.
Tayari dereva alishaanza kupiga ‘resi’ nyingi na kupiga honi, kuoneshakwamba muda mfupi baadaye safari ingeanza. Baba akatenbea harakaharaka kuelekea kwenye mlango wa kushukia, akateremka mpaka chini na akusimama upande ule tuliokuwa tumekaa, gari likaanza kuondoka ambapo alitupungua mikono, na sisi tukafanya hivyo.
Safari ikaanza, hiyo ilikuwa ni karibu saa kumi na mbili na nusu, basi likaanza kuchanja mbuga kuelekea Dar es Salaam.
Baada ya kusafiri umbali mfupi, tukiwa tumefika eneo maarufu liitwalo Mlima Nyoka, lililokuwa kilometa chache kutoka Uyole mjini, tulishangaa kuanza kuona gari likiyumbayumba. Nilikuwa nikisikia sifa za eneo hilo mara kwa mara kwamba magari mengi, hasa ya abiria yalikuwa yakipata ajali na kuua abiria wengi, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Kulikuwa na mteremko mkali wenye kona za hatari, na baada ya kuvuka daraja kulikuwa na mlima mkali pia, jambo ambalo lilimaanisha kama dereva akishindwa kulimudu gari, ajali yake ingekuwa si ya mchezo. Dereva alizidi kuyumba huku gari likiongeza kasi, hali iliyofanya abiria waanze kupiga kelele kwa nguvu, wengi wakilitaja jina la Mungu.
Gari lilizidi kuongeza kasi, likawa linashuka kwenye mteremko huo kwa kasi kubwa huku likiendelea kuyumba huku na kule, kelele ndani ya basio zikazidi kuongezeka.
Je, nini kitafuatia?
OkSehemu ya kumi na mbili----12
ILIPOISHIA:
Alikuwa ni msichana mzuri sana, upande wa nyuma alikuwa amejazia huku kiuno chake kikiwa kimegawanyika, kama nyigu ambao kule kijijini tulikuwa tukiwaogopa kutokana na sumu yao wanapokung’ata.
Suruali ya jeans aliyovaa, ililifanya umbo lake lijichonge vizuri, ghafla akageuka, akanibamba nikiwa namtazama kwa nyuma, nikazidi kujisikia aibu.
SASA ENDELEA…
“Mbona unaniangalia hivyo?”
“Mimi?” Nilijifanya kuvunga, akanisogelea na kunipiga kakibao kepesi begani huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye kwenye uso wake. Na mimi nikawa nacheka huku aibu zikiwa zimenijaa.”
“Dar es Salaam unaishi sehemu gani?” aliniuliza swali ambalo lilikuwa gumu sana kulijibu kwani ukweli ni kwamba sikuwa naijua Dar wala sikuwahi kufika kabla. Nikawa nababaika mwenyewe, akajiongeza na kuniuliza:
“Kwani hii ndiyo mara yako ya kwanza kufika Dar?”
“Ndiyo,” nilijibu harakaharaka kwa sababu alikuwa amenipunguzia sana kazi ya kumjibu. Akaniambia kwamba yeye anaishi na wazazi wake Kijitonyama. Akaniambia kwamba alikuwa amemaliza chuo akisomea uhasibu na alikuwa anatoka Mbeya kuwasalimu bibi na babu yake wa upande wa mama.
“Wanaishi Mbeya sehemu gani?” nilimuuliza, akaniambia wanaishi Katumba, njia panda ya kwenda Mwakaleli. Maeneo hayo sikuwa nimewahi kufika zaidi ya kusikia tu kwa watu, nikawa natingisha kichwa kumkubalia. Akaendelea kunieleza kwamba mama yake alikuwa Mnyakyusa lakini baba yake alikuwa ni mtu kutoka Mkoa wa Pwani ingawa hakunieleza ni kabila gani.
Hatimaye dakika kumi ziliisha, dereva akaanza kupiga honi akitupa ishara kwamba muda wa kuingia kwenye basi umefika. Kwa hizo dakika chache nilizokaa na msichana huyo, niligundua kwamba alikuwa mcheshi, mchangamfu na asiye na maringo kama walivyo wasichana wengi warembo kama yeye.
“Lakini hujaniambia unaitwa nani.”
“Unataka kujua jina langu?”
“Ndiyo.”
“Sitaki,” alisema huku akinipiga tena begani, akaanza kukimbia kuelekea kwenye basi. Sikuelewa kitendo hicho kilikuwa na maana gani, wakati anakimbia nilishuhudua kitu kingine ambacho kiliusisimua sana moyo wangu, mpaka nikawa najiuliza zile hisia nilizokuwa nazisikia kwa wakati huo zilikuwa na maana gani?
Kwa kifupi nilijisikia raha sana kufahamiana na msichana huyo. Niliendelea kumtazama akikimbia mpaka alipofika kwenye ngazi za kupanga kwenye basi, akageuka na kunitazama kisha akapanda ngazi. Na mimi nilitembea harakaharaka huku nikiendelea kuchekacheka mwenyewe, mkononi nikiwa na kopo la soda ambayo nilikua nimeinywa nusu.
Nilipopanda na kuingia ndani ya gari, ndugu zangu wote walishangaa kuniona nikiwa na soda ya kopo, tena nikinywa kwa mrija.
Niliwaona wote walivyomeza mate, wakawa wanaulizana nimeipata wapi soda hiyo? Sikuwajali kwa sababu bado nilikuwa na hasira nao, nikakaa kwenye siti yangu, nikageuka na kumtazama yule msichana ambaye mpaka muda huo hakuwa amenitajia jina lake, nikashtuka tena kugundua kwamba kumbe alikuwa ametulia akinitazama kila nilichokuwa nakifanya.
Macho yangu na yake yalipogongana, aliachia tabasamu hafifu halafu eti na yeye akakwepesha macho yake kwa aibu, yaani mwanzo mimi ndiyo nilikuwa nakwepesha macho yangu lakini ghafla na yeye alianza kukwepesha macho yake kwa aibu. Dereva aliondoa gari na safari ikaendelea.
Safari hii umakini ulikuwa ukinipungua sana kichwani mwangu kwani mara kwa mara tulikuwa tukitazamana na yule msichana na kuishia kuchekacheka tu. Nashukuru hakuna jambo lolote baya lililotokea mpaka tulipoanza kuingia mjini.
Tulipofika Kibaha, gari lilisimama na yule abiria aliyekuwa amekaa pembeni yangu, alisimama na kushuka, harakaharaka nikamuona yule msichana akikusanya kila kitu chake na kuja kukaa pembeni yangu. Aliponisogelea tu, nilianza tena kusikia harufu ya manukato aliyojipulizia, ambayo kiukweli yalinivutia sana.
Akakaa pembeni yangu na kuniegamia kimtindo kabla ya kujiweka vizuri kwenye siti yake.
“Yule niliyekaa naye hata stori hana, muda wote analala tu bora nikae na wewe,” alisema huku akinipigapiga begani, nikawa natabasamu tu kwani kiukweli hata mimi nilikuwa napenda kukaa naye siti moja.
“Ulisema unataka kujua jina langu?” alianzisha mazungumzo, niikamjibu kwa kutingisha kichwa, akaniambia ananipa mtihani nitafute mwenyewe jina lake. Kiufupi ni kwamba, kwa muda mfupi tu niliokaa naye, alionesha kupenda sana urafiki wetu uendelee, jambo ambalo hata mimi nilikuwa nalipenda ingawa mara kwa mara nilikuwa najishtukia.
Hata nilipokuwa nacheka, sikuwa napenda ayaone meno yangu kwani ya kwake yalikuwa meupe sana na masafi lakini kwangu mimi, hata sikuwa nakumbuka mara ya mwisho kupiga mswaki ni lini, si unajua tena maisha ya kijijini.
“Una simu?” aliniuliza swali ambalo lilinifanya nijisikie tena aibu. Sikuwa na simu, sikuwahi kumiliki wala sikuwa najua namna ya kuitumia, nikawa natingisha kichwa kukataa, akaniambia alikuwa na simu mbili lakini hiyo nyingine hakuwa akiitumia kwa sababu ilikuwa ya kizamani.
“Basi nipe mimi,” nilisema kwa utani kwani nilijua ni jambo ambalo haliwezekani, akacheka na kufungua kibegi chake kidogo, akatoa simu ndogo aina ya Nokia ya tochi na kunipa.
“Chukua utakuwa unatumia,” alisema. Nikapigwa na butwaa nikiwa ni kama siamini. Kuna wakati nilihisi kwamba pengine alikuwa akinitania lakini mwenyewe alisisitiza kwamba ni kweli amenipa. Muda huo, tayari gari lilikuwa limeshawasili Ubungo, sikuwa napajua zaidi ya kusikia tu watu wakisema hapo ndiyo ubungo.
Tayari giza lilishaanza kuingia, taa nyingi zilizokuwa zinawaka kila upande zikanifanya nijihisi kama nilikuwa kwenye ndoto.
Waliosema mjini kuzuri hawakukosea, Dar ilikuwa na tofauti kubwa sana na kule kijijini nilikozaliwa na kukulia, kila kitu kilikuwa kigeni kwangu. Wakati nikiendelea kushangaashangaa, nilisikia mama akiniambia kwamba natakiwa kuwa makini kuchukua mizigo iliyokuwa imewekwa kwenye buti.
Harakaharaka nikateremka na abiria wengine, hata sikukumbuka nilipotezana saa ngapi na yule dada, ushamba wa mjini ulinipa mchecheto mkubwa ndani ya moyo wangu, nikaenda mpaka kwenye buti nikiwa na wale ndugu zangu wengine ambao nao walikuwa wakishangaashangaa, tukafanikiwa kushusha mizigo yetu yote na kuiweka pembeni.
“Twendeni nilisikia sauti ya baba akizungumza, kugeuka pembeni, sote tulipigwa na butwaa kumuona baba akiwa anafungua milango ya teksi. Hakuna aliyejua baba alifika saa ngapi Dar es Salaam kwa sababu kama aliweza mpaka kuzungumza na dereva wa teksi na kukaa pale wakitusubiri, maana yake ni kwamba aliwahi sana kufika.
“Unajua wewe huna akili kabisa,” baba alianza kunifokea baada ya kumaliza kupakiza mizigo kwenye teksi, nikawa nashangaa kwa nini baba ananiambia maneno hayo.
“Yule uliyekuwa umekaa naye kwenye basi ni nani?”
“Ni rafiki yangu.”
“Unamjua wewe? Na hicho alichokupa una uhakika gani kama ni simu? Ujinga wako utaiponza familianzima,” alisema maneno ambayo yalinishangaza sana.
Je, nini kitafuatia?
Aisee togo wewe ni bonge la kiaziSehemu ya ishirini na nane________28
ILIPOISHIA:
Baba alitoa kichupa kilichokuwa na unga mweusi lakini kabla hajafanya chochote, aliniambia nikajitazame kwenye kioo kilichokuwa humo chumbani.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko usio wa kawaida.
SASA ENDELEA...
Uso wangu ulikuwa umebadilika na kuwa mweusi tii kama mkaa. Kilichoonekana ilikuwa ni macho na meno tu. Nilishindwa kuelewa kwa nini mimebadilika na kuwa vile, sikujua kama ni yale makofi ya nguvu niliyopigwa au ni nini.
“Usishtuke, na huo mchezo wako ukiendelea nao yatakufika makubwa zaidi, yaani unaonekana umeonja asali na sasa unataka kuchonga mzinga kabisa. Hukuwa na mambo ya kupenda wanawake, nini kimekusibu?” alisema baba lakini maneno yake yaliingilia sikio moja na kutokea jingine.
Akili yangu ilikuwa ikiwaza kuhusu mabadiliko yaliyotokea kwenye uso wangu. Nilishindwa kuelewa itakuwaje kama nitaendelea kuwa hivyo, nilijikuta nikiishiwa nguvu kabisa, nikakaa chini huku hofu kubwa ikiwa imetanda moyoni mwangu.
“Si naongea na wewe?” alinihoji baba huku akiwa amekishika kile kichupa, sikumjibu chochote kwa sababu akili yangu ilikuwa ikiwaza mambo mengine tofauti kabisa. Suala la kuacha kufaidi penzi la Rahma halikuwepo kabisa kichwani mwangu, kwa sababu hata wao wenyewe walijaribu kulizuia lakini kilichotokea kila mmoja akawa shahidi.
“Hebu inuka,” alisema baba kwa jazba, nadhani ni baada ya kuona simpi ushirikiano. Nilisimama, akatoa wembe kwenye mfuko wa mbele wa shati yake, akanichanja kwenye paji la uso, juu kidogo ya sehemu nywele zinapoanzia.
Akanipaka ile dawa, yaani kwa jinsi ilivyokuwa inauma, nilishindwa kujizuia, nikawa napiga kelele, baba akanikamata na kuniziba mdomo huku akinionesha ishara ya kunyamaza.
“Inatakiwa ujikaze, halafu hakikisha asubuhi hakuna mtu yeyote anayejua kilichotokea, ni mambo ya aibu sana na yatatusababishia matatizo makubwa, si unajua ndiyo kwanza tumefika na hapa ni kwa watu?”
“Nataka kujua wale ni akina nani na wametoka wapi? Kwa nini wameingia chumbani kwa Rahma?”
“Nitakujibu lakini siyo leo,” alisema baba huku akinisisitiza kwamba nilale na nisiende tena chumbani kwa Rahma. Hakuna jambo ambalo lilikuwa likinikera kwa baba kama kila ninapomuuliza kuhusu mauzauza yanayonitokea yeye anakimbilia tu kusema kwamba atanijibu. Alitoka na kurudia kunisisitiza kwamba nisitoke na asubuhi nisimwambie yeyote kuhusu kilichotokea.
“Na huu uso itakuwaje?”
“Hiyo dawa niliyokupaka itakusaidia, mtu yeyote akikuuliza mwambie umeamka tu asubuhi na kujikuta ukiwa hivyo,” alisema. Nikasogea tena kwenye kioo na kujitazama. Yaani hata sikujua kama asubuhi kukipambazuka halafu nikawa bado kwenye hali hiyo itakuwaje maana kiukweli nilikuwa natisha.
Kwenye upande wa shavu la kushoto na kulia, kulikuwa na alama za vidole za yule bibi kizee sehemu aliponipiga makofi, nikaapa siku nitakayomjua halafu nikakutana naye barabarani, lazima na mimi nimlipizie.
Nilijaribu kujilaza kitandani lakini usingizi haukuja kabisa, mara kwa mara nilikuwa nikisikia vishindo vikubwa juu ya bati kama kuna watu wanapigana, huku wakati mwingine sauti za ajabu zikisikika. Nilikuja kupata usingizi wakati kumeshaanza kupambazuka kabisa.
Kwa kuhofia kwamba ndugu yangu akiamka anaweza kuniona nilivyokuwa natisha usoni, nilijifunika ‘gubigubi’. Nilimsikia akijiongelesha kama aliyeshtuka kuniona nimelala pembeni yake wakati hakumbuki usiku niliingia saa ngapi.
“Unaendeleaje Togo,” aliniuliza lakini nilijikausha na kujifanya nimepitiwa na usingizi.
“Togoo!” aliniita huku akivuta shuka kwa nguvu. Kwa kuwa sikutegemea tukio hilo, alifanikiwa kunifunua na mimi bila hata kufikiri mara mbili, nikaamka kwa hasira, tukawa tunatazamana.
“Mbonaunapenda kunisumbua wakati unajua mwenzio naumwa?”
“Hee... huko usoni umefanya nini?” aliniuliza huku akirudi nyuma kwa hofu, akafungua mlango na kutoka mbio. Nilijikuta nikikosa amani mno, ikabidi nisogee na kujitazama tena kwenye kioo. Bado uso wangu haukuwa umerudi kwenye hali yake.
Japokuwa ule weusi kidogo ulikuwa umepungua lakini bado mtu yeyote asingeweza kunitazama usono bila kushtuka. Pia mashavu yote mawili yalikuwa yamevimba huku damu ikiwa imevilia kwenye zile alama za vidole na kwenye jicho langu la kushoto.
“Eti kuna nini,” baba alisema huku akifungua mlango. Kumbe kutokana na mshtuko alioupata alikuwa amekimbia na kwenda kumuita baba.
“Huyu mjinga eti mimi nimelala yeye ananivuta shuka,” nilisema huku nikikwepa kutazamana usoni na baba. Aliligundua hilo, akanilazimisha nimuangalie.
“hebu ngoja nakuja, na wewe acha ujinga wa kupigapiga kelele, inamaana hujui kama mwenzenu anaumwa,” alisema baba kwa kumkaripia yule ndugu yangu, nikamuona ‘limemshuka’ maana alitegemea baba atashtuka kama yeye.
“Kwanza ondoka muache apumzike,” alisema baba, ikabidi atoke naye, nikajilaza tena kitandani nakujifunika vizuri. Nikawa naendelea kutafakari mambo mengi yasiyo na majibu. Muda mfupi baadaye, baba alirejea akiwa na kimkoba chake kidogo, akaniamcha na kunitaka nifanye kama anavyoniambia.
Kuna kimzizi fulani alikitoa kwenye mkoba wake, akipa na kuniambia nikitafune lakini nisimeze mate. Nilipokitia mdomoni, niligundua kwamba kilikuwa kichungu sana, nikakitafuna huku nikiwa nimekunja sura.
‘Temea mate kwenye mkono wako wa kushoto na ujipake kwenye shavu la kulia,” alisema huku akinisisitiza kuwa makini. Nilifanya hivyo, nikajipaka kwenye shavu na kuhisi kama moto unawaka. Tema mengine kwenye mkono wa kulia na ujipake kwenye shavu la kushoto,” aliniambia, nikafanya hivyo, maumivu yakazidi ikuongezeka, nikawa nahisi kama ngozi ya sura inajaa kama puto.
“Nifuate,” alisema, akafungua mlango na kuelekea bafuni, nikamfuata ambapo alinielekeza namna ya kusimama kisha akafungulia maji na kuanza kunimwagia kichwa kizima huku akinisugua na kunipaka ungaunga mwingine uliokuwa na ladha kama magadi.
Alinisafisha kwa muda mrefu kisha akatoa kipande cha kitambaa na kunifuta, akaniambia nisifumbue macho mpaka atakaponiambia. Alinishika mkono na kunirudisha chumbani, akanilaza kitandani na kuniambia nifumbue macho.
“Inabidi ulale hivyo kwa dakika saba, zikiisha amka halafu ujitazame tena kwenye kioo,” aliniambia baba, akakusanya vitu vyake na kuondoka. Nikawa nasubiri hizo dakika saba ziishe maana aliniambia atakuja mwenyewe kuniambia. Baba alikuwa na mambo mengi sana yenye utata, hasa huo ujuzi wake wa mitishamba na dawa za kiganga.
Nililala pale kitandani lakini kwa mbali nilianza kujihisi hali fulani hivi isiyo ya kawaida. Sikutaka kuitilia maanani kwani bado uso wangu ulikuwa ukiwaka moto kwa maumivu. Dakika saba baadaye, kweli baba alirudi na kuniamsha, nikasogea na kujitazama kwenye kioo. Huwezi kuamini, uso wangu ulikuwa umerudi kwenye hali yake ya kawaida ingawa jicho moja bado lilibaki limevilia damu na zile alama za vidole mashavuni zenyewe hazikufutika.
Alitoka na kuniacha mwenyewe, angalau moyo wangu ukawa na amani. Nilisimama kwa muda pale mbele ya kioo nikiendelea kujitazama. Ile hali sasa ilizidi kunisumbua na kunifanya nijisikie vibaya. Yaani kwa jinsi nilivyokuwa najisikia, ilikuwa ni kama nimeshikwa na kiu kali lakini tofauti na kiu ya kawaida, ilikuwa ni kiu ya kukutana kimwili na mwanamke.
Nilibaki nikijishangaa mwenyewe kwani kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele ndivyo nilivyokuwa nikizidi kuteseka. Wakati nikiendelea kuugulia ndani kwa ndani, nilishangaa kwa nini rahma mpaka muda huo hakuwa amekuja kuniuliza nimeamkaje na hata sauti yake sikuisikia. Japokuwa baba alikuwa amenikanya sana, kwa jinsi hali ilivyokuwa, niliamini yeye ndiye anayeweza kuwa msaada kwangu kwa sababu tunapendana.
Nilitoka na kusogea kwenye mlango wa chumbani kwake lakini kabla sijashika kitasa, nilisikia sauti ya mdogo wake wa kiume akiniambia kwamba hakuwepo, alikuwa ameondoka na mama yake asubuhi na mapema kufuatilia mambo ya chuo. Ni kweli jana yake alikuwa amenidokeza kuhusu suala hilo lakini sijui kwa nini sikukumbuka. Nilijikuta nikiishiwa nguvu kwani sikujua nini kitafuatia.
Nilirudi chumbani kwangu huku hali ikizidi kuwa mbaya, sijui ni machale gani yalimcheza baba, mara akafungua mlango na kunikuta nikiwa kwenye hali ambayo haielezeki.
“Ule mzizi niliokupa na kukwambia uutafune lakini usimeze, ulifanya kama nilivyokwambia?” baba aliniuliza. Kiukweli baada ya kutema mate kwenye mkono wa kushoto na kulia, mengine yaliyobakia, pamoja na mabaki ya mzizi wenyewe, nilivimeza vyote. Nilipomwambia hivyo baba, alishtuka kuliko kawaida. Sikujua kwa nini ameshtuka kiasi hicho, akatoka haraka.
Nikiwa bado naendelea kuugulia, nilisikia ndugu yangu mmoja akiniita kutokea dirishani, nikafunua pazia na kuchungulia nje. Sikuyaamini macho yangu baada ya kumuona akiwa na yule msichana tuliyesafiri naye, harakaharaka nikafungua dirisha huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.
Je, nini kitafuatia? Usikose
Hata mimi nimeshindwa kuunganisha matukio itakua kajisahauHiyo 31 siyo muendelezo wa 30.
Haziendani kabisa...kuna kipande umeruka boss.
Hicho kidevice cha mfukoni ni unyama mwaisa [emoji38][emoji38][emoji38]Sehemu ya 31
ILIPOISHIA:
Nikiwa bado naendelea kumtazama kwa jicho baya, mara nilishtuka kusikia vishindo viwili vikubwa juu ya bati, kama vile nilivyokuwa navisikia usiku uliopita, moyo wangu ukapatwa na mshtuko mkubwa mno. Mara nilisikia vishindo vingine vitatu mfululizo, nikawa nimepigwa na butwaa huku macho yangu yote yakiwa juu.
SASA ENDELEA…
Kwa jinsi vishindo hivyo vilivyokuwa vikisikika, ilikuwa ni kama kuna watu wanaruka kutoka angani na kudondokea juu ya bati kwani vilikuwa vizito mno. Safari hii nilitaka kuwa makini kushuhudia je, kile ninachokisikia mimi, kila mtu anasikia hivyohivyo maana nilishahisi kuna kitu hakipo sawa kwangu lakini baba hataki kuniambia ukweli.
Baada ya vishindo vile vya kama watu au vitu kutua juu ya bati, mara vilianza kusikika vishindo vya mtu akitembea juu ya bati.
Unajua haya matukio kama hujawahi kutokewa nayo, huwezi kuelewa ile hofu unayokuwa nayo lakini kiukweli, ni bora tu uwe unasikia lakini yasikutokee. Hakuna hofu inayotesa kama hofu ya matukio kama haya yanapokutokea, hasa usiku kama huo.
Nilijikuta nywele zikisisimka vibaya mno, mapigo ya moyo yakawa yananienda kwa kasi maana sikujua safari hii wanakuja kwa mtindo gani. Vishindo viliendelea kusikika kisha kikasikika kishindo kingine ambacho kwa makadirio yangu ya haraka, kilikuwa ni kwenye sakafu ya mle mahabusu.
Nilishindwa kuelewa, inawezekanaje usikie mtu anatembea juu ya bati, tena kwa nje halafu muda mfupi baadaye umsikie akirukia na kudondokea kwa ndani, tena jirani kabisa na pale ulipo! Inatisha sana.
“Humu ndani kuna wanga eeh! Mbona nywele zinanisisimka? Sasa ole wake mtu aniguse,” mmoja kati ya wale mahabusu tuliokuwa nao mle ndani, aliyekuwa amekaa kwenye kona nyingine, alisikika akiongea kilevilevi, akawa anaporomosha matusi mazitomazito.
Kitendo kile kilinifanya niamini kwamba hatimaye sasa sikuwa peke yangu ambaye nilikuwa nikishuhudia mchezo uliokuwa ukiendelea. Niliamini hivyo kwa sababu kwenye kona aliyokuwa amekaa yule mahabusu ambaye alikuwa akiendelea kutukana, ndiko ambapo makadirio yangu yalinionesha kwamba yule mtu aliyekuwa akitembea juu ya bati alidondokea palepale.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Matusi aliyokuwa akitukana, yalisababisha mahabusu wengine ambao bado hawakuwa wamelala, waanze kucheka kwa nguvu na kumtania kwamba amelewa lakini kelele zote zilizimika ghafla bila mtu yeyote kutoa amri, ikatokea tu kwamba watu wote wapo kimya.
Katika ukimya huo, ulisikika msonyo mkali ambao japokuwa wale mahabusu wengine waliamini kwamba umetolewa na yule mahabusu aliyekuwa akitoa matusi mazito kwa wale aliowaita wanga, mimi nililitazama tukio hilo katika sura nyingine tofauti.
Haikuwa mara ya kwanza kusikia msonyo wa namna hiyo ingawa safari hii ulionekana kutoka kwa mtu tofauti ambaye sijawahi kuisikia sauti yake. Unajua kuna watu wamezaliwa wakiwa na uwezo fulani wa kipekee, sijui niuiteje lakini kwa kifupi mtu anakuwa na uwezo wa kufikiri na kuyaona mambo kwa utofauti na wengine.
Yaani kuna baadhi ya watu, nyie wengine wote mnaweza kuamini kwa mfano ajali iliyotokea barabarani imesababishwa na uzembe wa dereva kukimbia kwa mwendo kasi akiwa hajafunga mkanda, lakini mtu mwingine hapohapo akalitazama tukio na kutoa jibu tofauti kabisa ambalo pengine halikutegemewa.
Baba amewahi kunifundisha kwamba japokuwa watu wa namna hii huwa wanachekwa au kuzomewa na kuonekana wanaishi kwenye ulimwengu wa ndoto, lakini wao ndiyo huwa sahihi kwa sababu wanautazama ulimwengu kwa jicho tofauti na watu wengine wote.
Ndicho kilichotokea mle mahabusu, wakati watu wote wakilichukulia tukio la yule mahabusu kudai kule ndani kuna wachawi kisha akaanza kuporomosha matusi, wengi walimuona kama mlevi tu lakini mimi nilimtazama kwa jicho tofauti.
Hata uliposikika ule msonyo na watu kuanza kumtuhumu kwamba anawavurugia usingizi wao, mimi nilikuwa nikiamini kwamba hakuutoa yeye na alichokuwa akikisema kwamba mle ndani kulikuwa na wanga, ulikuwa ni ukweli mtupu.
“Sikilizeni, sikilizeni,” alisema yule mahabusu, kwa msaada wa mwanga hafifu uliokuwa ukipenya kutokea nje, nilimuona akiinua kichwa chake juu kutazama darini, lakini kelele za mahabusu wengine zikamfanya ashindwe kusikia alichokuwa akitaka kukisikia.
“Au naye ana nguvu kama mimi?” nilijiuliza kwa sababu wakati akiwataka watu wote watulie ili wasikie, ni kweli juu ya bati kuna mtu alikuwa akitembea kwa vishindo kabisa kisha naye akasikika akidondokea ndani ya ile mahabusu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Baada ya hapo, vilianza kusikika vishindo vya watu wakirukia mle mahabusu mfululizo, nikawa natetemeka nikiwa sijui nini kitatokea maana kama unavyojua, milango ya mahabusu huwa muda wote imefungwa na haiwezekani ikafunguliwa kwa muda ule. Nilichokuwa nakiomba, ni wachawi hao wasije wakawa wamekuja kwa shari kama ilivyotokea kwangu na safari hii, nilijifunza kuufyata mkia, sikutaka kuzungumza chochote zaidi ya kuzidi kukodoa macho yangu gizani kama nitaona kitu chochote.
Nilishangaa mfuko wa suruali yangu ukianza kutetemeka kama ndani kulikuwa na kitu ‘kinacho-vaibreti’, sikukumbuka kama niliweka kitu chochote mfukoni na hata kama ni simu, wala sikuwa nikimiliki baada ya baba kunipokonya ile niliyopewa na yule dada ambaye ndiye aliyesababisha muda huo nikawa nyuma ya nondo.
Kwa hofu kubwa niliingiza mkono mfukoni huku nikiwa bado nimekodoa macho, nikagundua kwamba kulikuwa na kitu kwenye mfuko wangu ambacho sikuwa najua ni kitu gani.
Mbaya zaidi, sikujua ni nani aliyekiweka kwenye mfuko wa nguo yangu kwa sababu wakati naingizwa na wale askari, waliniambia pale kaunta nitoe kitu chochote nilichokuwa nacho mfukoni na wala sikuhitaji kujisachi kwa sababu nilikuwa najua sina chochote.
Cha ajabu, nilipokigusa kitu hicho tu, kiliacha kutetemeka lakini yote tisa, kumi ni kwamba nilianza kuona vitu vya ajabu mno. Japokuwa mle ndani kulikuwa na giza, niliweza kuwaona watu wote vizuri, mpaka sura zao utafikiri ilikuwa mchana, ila tofauti yake ni kwamba hakukuwa na mwanga wenye uangavu kama wa mchana bali ulifanana kwa mbali na nuru ya mbalamwezi.
Kwa wale tuliokulia vijijini nadhani wanaelewa vizuri usiku wa mbalamwezi unavyokuwa, yaani unaweza kusema ni mchana kabisa kwani vitu vyote vinaonekana japo siyo vizuri kama vile nilivyokuwa naona mimi.
Nilianza kuwatazama mahabusu wenzangu mmoja baada ya mwingine maana kama unavyojua, niliingizwa giza likiwa limeshaingia na kwa sababu mle ndani hakukuwa na taa, watu pekee niliowaona vizuri ni wale waliokuwa jirani na mimi.
Cha ajabu, wakati nikiendelea kuwatazama mahabusu hao ambao wengi walishaanza kusinzia kutokana na uchovu, niligundua kwamba kulikuwa na watu wengine wasio wa kawaida mle ndani, nao wakiwa wamejichanganya na mahabusu lakini tofauti yao ilikuwa moja.
Karibu wote walikuwa na macho mekundu sana na walikuwa wakinitazama kama wanaosubiri kuona nitafanya nini lakini kubwa, wote walikuwa watupu kabisa. Nilipopiga jicho harakaharaka na kujaribu kuwahesabu, walikuwa kama saba hivi, tena wengine wawili walikuwa ni wanawake na kama unavyojua mahabusu huwa hawachanganywi wanawake na wanaume.
Wote waliacha kila walichokuwa wanakifanya, wakawa wananitazama kwa macho makali. Sikuelewa nini hasa kimetokea, wakati nikiendelea kuwatazama vizuri kwa mara ya pili, kuna jambo moja lilinishtua mno mpaka nikajikuta nimetoa mkono mfukoni, giza likarudi kama lilivyokuwa mwanzo.
Je, nini kitafuatia?
We jamaa mbona una roho mbaya hata kunitag mwanangu? Poa ntakuja kuishi hapaMAKABURI YA WASIO NA HATIA (GRAVES OF THE INNOCENTS)- 1
JINA langu naitwa Togolai Mahimba, ni mtoto wa mwisho kati ya watoto saba wa baba yetu, Sinai Mahimba ambaye kwa sasa ni marehemu. Baba yetu alifariki miaka mitatu iliyopita baada ya kuugua ghafla.
Kifo chake kilitawaliwa na utata mkubwa na hata siku ya mazishi yake, kulitokea mambo mengi ya ajabu ambayo mpaka leo siwezi kuyaeleza. Ninayo mambo mengi ambayo ningependa kukusimulia ndugu msomaji lakini kwa kuanzia, naomba nikueleze mambo machache yaliyotokea kabla ya kifo cha baba yetu ambaye mimi ndiye nilikuwa mtoto anayenipenda zaidi.
Kabla hajafikwa na mauti, baba yetu alikuwa mtu maarufu sana kijijini kwetu, Makongorosi, Chunya mkoani Mbeya tulikokuwa tukiishi. Kilichofanya awe maarufu kiasi hicho, ni kazi yake ya uganga aliyokuwa anaifanya ambapo mbali na mambo mengine, alikuwa akiwafanyia matambiko wachimbaji wengi wa dhahabu ili wakiingia mgodini, wapate dhahabu kwa urahisi sambamba na wafanyabiashara wengine.
Umaarufu wa baba ulisababisha hata sisi watoto wake tuwe maarufu sana, hasa mimi ambaye muda mwingi nilikuwa nikiongozana naye kila alikokuwa anakwenda, kuanzia kwenye matambiko maporini, kwenye mazindiko migodini, kuchimba dawa msituni mpaka kilingeni kwake alikokuwa akifanyia shughuli zake za uganga.
Wengi walikuwa wakifupisha jina langu kwa kuniita Togo na hilo ndiyo lililokuwa maarufu kuliko hata jina langu halisi. Nakumbuka maisha yangu ya utotoni yalikuwa ya raha sana kutokana na jinsi baba alivyokuwa akinipenda. Hata ndugu zangu wengine tuliozaliwa pamoja, walikuwa wakinionea gere kwa jinsi nilivyokuwa nikipendwa.
Maisha yaliendelea vizuri, nikawa naendelea kukua huku pia nikijifunza mambo mengi aliyokuwa akiyafanya baba katika kazi zake. Mambo yalianza kubadilika siku moja tukiwa msituni na baba kutafuta dawa.
Baba akiwa ameinama akichimba mizizi ya mti wa mtangetange ambao ulikuwa ukitumika kwa kutibu magonjwa mengi, hata yale yaliyoshindikana hospitalini, ghafla alivamiwa na kundi la popo waliokuwa wanapiga kelele kwa nguvu. Baba akawa anahangaika kujaribu kuwazuia popo hao ambao waliendelea kumzonga hasa sehemu za kichwani.
Akiwa anaendelea kupambana nao, nilimshuhudia akifanya tukio ambalo sikuwahi kumuona baba akilifanya hata mara moja. Kwa kasi ya kimbunga, aliyeyuka na kupotea eneo hilo, nikabaki nimepigwa na butwaa, nikiwa ni kama siamini.
Ghafla wale popo baada ya kuona baba amepotea kimiujiza, walitawanyika na kupotea eneo hilo huku wakiendelea kupiga kelele kwa nguvu. Nikawa nageuka huku na kule kumtazama baba bila mafanikio, hofu kubwa ikatanda kwenye moyo wangu.
“Unashangaa nini Togolai,” sauti ya baba ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye lindi la mawazo, nikashtuka kwa nguvu. Cha ajabu, baba alikuwa amesimama palepale alipokuwepo, akiendelea na kazi yake ya kuchimba mizizi ya mtangetange kama hakuna kilichotokea.
“Baba mbona sielewi?”
“Huelewi nini tena?”
“Popo.”
“Popo? Wamefanya nini?”
“Hawajakuumiza?”
“Mbona sikuelewi Togo?” alisema baba huku akiacha kazi aliyokuwa anaifanya na kunisogelea. Sikutaka kuamini kama kweli baba alikuwa haelewi nilichokuwa nakizungumza, akanisogelea na kunishika begani.
“Uko sawa?”
“Ndi..yo baba, niko sawa,” nilibabaika kidogo, nikamuona baba akigeuka huku na kule kama anayeangalia kitu fulani. Na mimi nikawa nageuka kufuata usawa wa macho yake, ghafla macho yetu yakaganda eneo moja, nilipigwa na butwaa kubwa kwa nilichokuwa nakiona, nikajikuta nikianza kutetemeka.
Wanaume wawili waliokuwa uchi wa mnyama, walikuwa wakining’inia kwenye tawi la mti mkubwa uliokuwa mita chache kutoka pale tulipokuwa, wote wakitukodolea macho yao mekundu.
“Unawaona wale washenzi?” baba alisema huku akionyesha kutokuwa na hata chembe ya wasiwasi. Nikatingisha kichwa kama ishara ya kumjibu ‘ndiyo nawaona’.
“Wale ni wachawi wanaosumbua watu kijijini kwetu, naona wametangaza vita na mimi, hawanijui hawa,” alisema baba na kama ilivyotokea mara ya kwanza, aliyeyuka na kupotea eneo lile, wale wachawi nao wakapotea kwenye upeo wa macho yangu, nikasikia kelele za watu waliokuwa wakilia kwa sauti kubwa kama wanaolalamikia maumivu makali.
“Ndiyo dawa yao, na siku nyingine wakirudia watanikoma,” alisema baba, nikashtuka tena baada ya kumuona amesimama palepale alipokuwa mara ya kwanza, pembeni yangu lakini safari hii alikuwa akihema kwa nguvu kama mtu aliyetoka kukimbia. Nilijihisi kama nipo ndotoni.
“Baba mbona sielewi kinachotoke…” nilisema lakini kabla sijamalizia kauli yangu, macho yangu yalitua kwenye mkono wa baba uliokuwa na jeraha na alama kama ameng’atwa na mnyama mkali, huku damu nyeusi zikimtoka kwa wingi.
“Ninii!” baba alinihoji baada ya kuona macho yangu yameganda kwenye mkono wake.
“Umeumia baba, pole,” nilisema lakini baba hakunijibu kitu zaidi ya kuusogeza ule mkono wenye jeraha karibu na uso wake, akawa analichunguza vizuri lile jeraha.
Akasogea pale kwenye mti wa mtangetange na kuchuma majani yake, akayatia mdomoni na kuanza kuyatafuna kisha muda mfupi baadaye, aliyatoa mdomoni na kuyabandika juu ya kidonda chake, nikamuona akifumba macho kama ishara ya kuonyesha jinsi alivyokuwa akihisi maumivu.
“Nitakuwa sawa usijali, nimeshazoea kusumbuana na hawa wachawi. Inabidi na wewe uwe jasiri,” alisema baba huku akiendelea kujisafisha pale kwenye jeraha lake. Zile damu nyeusi zilizokuwa zinamtoka zikakata, akashusha pumzi ndefu na kuendelea na kazi ya kuchimba dawa.
Kwa kweli matukio yale niliyoyashuhudia yaliufanya moyo wangu uingiwe na hofu kubwa mno. Sikuwahi kudhani baba anaweza kuwa na nguvu za giza kiasi kile, siku zote niliamini alichokuwa anakifanya ni kutibu watu kwa mitishamba tu, basi! Hata hivyo, nilijikaza kiume na kuuficha mshtuko nilioupata, nikaendelea kumsaidia baba na hatimaye tukamaliza kazi yetu.
Wakati tunarudi kutoka msituni, baba alinisisitiza njiani kwamba sitakiwi kumwambia mtu yeyote kuhusu nilichoshuhudia, hata ndugu zangu wa tumbo moja. Akaniambia kwa kilichotokea, anahisi kuna madhara makubwa yatakuwa yametokea kijijini kwetu.
“Unamaanisha nini baba?”
“Wale wachawi waliotuvamia kule msituni, mmoja nimemuumiza sana sijui kama anaweza kuwa yupo hai mpaka muda huu.”
“Kwani ni akina nani wale?”
“Kwani wewe huwajui wale? Au hujawatazama vizuri?” baba alinihoji na kuanza kunifafanulia, akaniambia yule mmoja ni mzee wa kanisa pale kijijini kwetu, aliponitajia jina lake ndiyo nikamtambua vizuri. Alikuwa ni mzee Mwankuga, ambaye mara kwa mara alikuwa akiingia kwenye migogoro na baba kutokana na kugombea mpaka wa shamba kwa sababu shamba letu na lake yalikuwa yemepakana.
Nakumbuka kuna kipindi waliwahi kupelekana mpaka kwa balozi kutokana na ugomvi wao huo. Hata familia zetu hazikuwa na uhusiano mzuri, sisi tulikatazwa kabisa kuongea wala kucheza na watoto wa mzee Mwankuga na yeye hali kadhalika.
“Kwa hiyo unataka kusema mzee Mwankuga naye ni mchawi? Si mtumishi wa Mungu yule na kila Jumapili anaenda kanisani tena anakaa siti za mbele?”
“Mwanangu dunia ina mengi hii! Hutakiwi kumuamini mtu, pale kanisani waumini karibu wote huwa wanakuja kutafuta dawa kwangu, wengine wanataka wapandishwe vyeo, wengine wanataka kujikinga na wengine wana shida mbalimbali, usiwaamini binadamu,” alisema baba, nikabaki nimeduwaa. Hizo zikawa ni habari nyingine za kushangaza sana kwangu.
“Sasa pale si walikuwa wawili? Huyo mwingine ni nani?”
“Si yule mwalimu wenu, Mwashambwa?”
“Mwalimu wetu Mwashambwa anayetufundisha hesabu naye ni mchawi?” niliuliza kwa mshangao mkubwa huku mdomo nikiwa nimeuacha wazi.
“Ndiyo, hata ule mguu wake anaochechemea nasikia alikutana na kombora la kichawi ndiyo likampa ulemavu wa kudumu, siyo mtu mzuri kabisa, we turudi nyumbani utasikia chochote kuhusu watu hao wawili,” baba alisema kwa kujiamini, ukimya mrefu ukatanda kati yetu, hakuna aliyezungumza chochote.
Niliendelea kutembea huku nikiwa na furushi langu la dawa kichwani pamoja na panga, baba yeye alikuwa ametangulia mbele, naye akiwa amebeba dawa na jembe tulilokuwa tunalitumia kuchimbia dawa.
Ili kufika nyumbani kwetu, ilikuwa ni lazima upite nyumba kadhaa za nyasi na nyingine za bati zilizokuwa pembezoni mwa kijiji ndiyo uelekee nyumbani. Miongoni mwa nyumba hizo, ilikuwepo pia na nyumba ya mzee Mwankuga ambaye muda mfupi uliopita baba alikuwa akinisimulia mambo yake kwamba ni mchawi.
Tulipokaribia nyumbani kwa mzee huyo, baba alinionyesha ishara kwamba nisimame, nikafanya hivyo, tukawa tunasikia sauti za watu wengi wakilia kutoka nyumbani kwa mzee huyo, baba akanionyesha ishara kama anayesema ‘unaona?’, nikashika mdomo kwa mshangao. Sikutaka kuamini kwamba kweli mzee Mwankuga alikuwa amefariki dunia.
Je, nini kitafuatia?
Naweka kambi hapaMAKABURI YA WASIO NA HATIA (GRAVES OF THE INNOCENTS)- 1
JINA langu naitwa Togolai Mahimba, ni mtoto wa mwisho kati ya watoto saba wa baba yetu, Sinai Mahimba ambaye kwa sasa ni marehemu. Baba yetu alifariki miaka mitatu iliyopita baada ya kuugua ghafla.
Kifo chake kilitawaliwa na utata mkubwa na hata siku ya mazishi yake, kulitokea mambo mengi ya ajabu ambayo mpaka leo siwezi kuyaeleza. Ninayo mambo mengi ambayo ningependa kukusimulia ndugu msomaji lakini kwa kuanzia, naomba nikueleze mambo machache yaliyotokea kabla ya kifo cha baba yetu ambaye mimi ndiye nilikuwa mtoto anayenipenda zaidi.
Kabla hajafikwa na mauti, baba yetu alikuwa mtu maarufu sana kijijini kwetu, Makongorosi, Chunya mkoani Mbeya tulikokuwa tukiishi. Kilichofanya awe maarufu kiasi hicho, ni kazi yake ya uganga aliyokuwa anaifanya ambapo mbali na mambo mengine, alikuwa akiwafanyia matambiko wachimbaji wengi wa dhahabu ili wakiingia mgodini, wapate dhahabu kwa urahisi sambamba na wafanyabiashara wengine.
Umaarufu wa baba ulisababisha hata sisi watoto wake tuwe maarufu sana, hasa mimi ambaye muda mwingi nilikuwa nikiongozana naye kila alikokuwa anakwenda, kuanzia kwenye matambiko maporini, kwenye mazindiko migodini, kuchimba dawa msituni mpaka kilingeni kwake alikokuwa akifanyia shughuli zake za uganga.
Wengi walikuwa wakifupisha jina langu kwa kuniita Togo na hilo ndiyo lililokuwa maarufu kuliko hata jina langu halisi. Nakumbuka maisha yangu ya utotoni yalikuwa ya raha sana kutokana na jinsi baba alivyokuwa akinipenda. Hata ndugu zangu wengine tuliozaliwa pamoja, walikuwa wakinionea gere kwa jinsi nilivyokuwa nikipendwa.
Maisha yaliendelea vizuri, nikawa naendelea kukua huku pia nikijifunza mambo mengi aliyokuwa akiyafanya baba katika kazi zake. Mambo yalianza kubadilika siku moja tukiwa msituni na baba kutafuta dawa.
Baba akiwa ameinama akichimba mizizi ya mti wa mtangetange ambao ulikuwa ukitumika kwa kutibu magonjwa mengi, hata yale yaliyoshindikana hospitalini, ghafla alivamiwa na kundi la popo waliokuwa wanapiga kelele kwa nguvu. Baba akawa anahangaika kujaribu kuwazuia popo hao ambao waliendelea kumzonga hasa sehemu za kichwani.
Akiwa anaendelea kupambana nao, nilimshuhudia akifanya tukio ambalo sikuwahi kumuona baba akilifanya hata mara moja. Kwa kasi ya kimbunga, aliyeyuka na kupotea eneo hilo, nikabaki nimepigwa na butwaa, nikiwa ni kama siamini.
Ghafla wale popo baada ya kuona baba amepotea kimiujiza, walitawanyika na kupotea eneo hilo huku wakiendelea kupiga kelele kwa nguvu. Nikawa nageuka huku na kule kumtazama baba bila mafanikio, hofu kubwa ikatanda kwenye moyo wangu.
“Unashangaa nini Togolai,” sauti ya baba ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye lindi la mawazo, nikashtuka kwa nguvu. Cha ajabu, baba alikuwa amesimama palepale alipokuwepo, akiendelea na kazi yake ya kuchimba mizizi ya mtangetange kama hakuna kilichotokea.
“Baba mbona sielewi?”
“Huelewi nini tena?”
“Popo.”
“Popo? Wamefanya nini?”
“Hawajakuumiza?”
“Mbona sikuelewi Togo?” alisema baba huku akiacha kazi aliyokuwa anaifanya na kunisogelea. Sikutaka kuamini kama kweli baba alikuwa haelewi nilichokuwa nakizungumza, akanisogelea na kunishika begani.
“Uko sawa?”
“Ndi..yo baba, niko sawa,” nilibabaika kidogo, nikamuona baba akigeuka huku na kule kama anayeangalia kitu fulani. Na mimi nikawa nageuka kufuata usawa wa macho yake, ghafla macho yetu yakaganda eneo moja, nilipigwa na butwaa kubwa kwa nilichokuwa nakiona, nikajikuta nikianza kutetemeka.
Wanaume wawili waliokuwa uchi wa mnyama, walikuwa wakining’inia kwenye tawi la mti mkubwa uliokuwa mita chache kutoka pale tulipokuwa, wote wakitukodolea macho yao mekundu.
“Unawaona wale washenzi?” baba alisema huku akionyesha kutokuwa na hata chembe ya wasiwasi. Nikatingisha kichwa kama ishara ya kumjibu ‘ndiyo nawaona’.
“Wale ni wachawi wanaosumbua watu kijijini kwetu, naona wametangaza vita na mimi, hawanijui hawa,” alisema baba na kama ilivyotokea mara ya kwanza, aliyeyuka na kupotea eneo lile, wale wachawi nao wakapotea kwenye upeo wa macho yangu, nikasikia kelele za watu waliokuwa wakilia kwa sauti kubwa kama wanaolalamikia maumivu makali.
“Ndiyo dawa yao, na siku nyingine wakirudia watanikoma,” alisema baba, nikashtuka tena baada ya kumuona amesimama palepale alipokuwa mara ya kwanza, pembeni yangu lakini safari hii alikuwa akihema kwa nguvu kama mtu aliyetoka kukimbia. Nilijihisi kama nipo ndotoni.
“Baba mbona sielewi kinachotoke…” nilisema lakini kabla sijamalizia kauli yangu, macho yangu yalitua kwenye mkono wa baba uliokuwa na jeraha na alama kama ameng’atwa na mnyama mkali, huku damu nyeusi zikimtoka kwa wingi.
“Ninii!” baba alinihoji baada ya kuona macho yangu yameganda kwenye mkono wake.
“Umeumia baba, pole,” nilisema lakini baba hakunijibu kitu zaidi ya kuusogeza ule mkono wenye jeraha karibu na uso wake, akawa analichunguza vizuri lile jeraha.
Akasogea pale kwenye mti wa mtangetange na kuchuma majani yake, akayatia mdomoni na kuanza kuyatafuna kisha muda mfupi baadaye, aliyatoa mdomoni na kuyabandika juu ya kidonda chake, nikamuona akifumba macho kama ishara ya kuonyesha jinsi alivyokuwa akihisi maumivu.
“Nitakuwa sawa usijali, nimeshazoea kusumbuana na hawa wachawi. Inabidi na wewe uwe jasiri,” alisema baba huku akiendelea kujisafisha pale kwenye jeraha lake. Zile damu nyeusi zilizokuwa zinamtoka zikakata, akashusha pumzi ndefu na kuendelea na kazi ya kuchimba dawa.
Kwa kweli matukio yale niliyoyashuhudia yaliufanya moyo wangu uingiwe na hofu kubwa mno. Sikuwahi kudhani baba anaweza kuwa na nguvu za giza kiasi kile, siku zote niliamini alichokuwa anakifanya ni kutibu watu kwa mitishamba tu, basi! Hata hivyo, nilijikaza kiume na kuuficha mshtuko nilioupata, nikaendelea kumsaidia baba na hatimaye tukamaliza kazi yetu.
Wakati tunarudi kutoka msituni, baba alinisisitiza njiani kwamba sitakiwi kumwambia mtu yeyote kuhusu nilichoshuhudia, hata ndugu zangu wa tumbo moja. Akaniambia kwa kilichotokea, anahisi kuna madhara makubwa yatakuwa yametokea kijijini kwetu.
“Unamaanisha nini baba?”
“Wale wachawi waliotuvamia kule msituni, mmoja nimemuumiza sana sijui kama anaweza kuwa yupo hai mpaka muda huu.”
“Kwani ni akina nani wale?”
“Kwani wewe huwajui wale? Au hujawatazama vizuri?” baba alinihoji na kuanza kunifafanulia, akaniambia yule mmoja ni mzee wa kanisa pale kijijini kwetu, aliponitajia jina lake ndiyo nikamtambua vizuri. Alikuwa ni mzee Mwankuga, ambaye mara kwa mara alikuwa akiingia kwenye migogoro na baba kutokana na kugombea mpaka wa shamba kwa sababu shamba letu na lake yalikuwa yemepakana.
Nakumbuka kuna kipindi waliwahi kupelekana mpaka kwa balozi kutokana na ugomvi wao huo. Hata familia zetu hazikuwa na uhusiano mzuri, sisi tulikatazwa kabisa kuongea wala kucheza na watoto wa mzee Mwankuga na yeye hali kadhalika.
“Kwa hiyo unataka kusema mzee Mwankuga naye ni mchawi? Si mtumishi wa Mungu yule na kila Jumapili anaenda kanisani tena anakaa siti za mbele?”
“Mwanangu dunia ina mengi hii! Hutakiwi kumuamini mtu, pale kanisani waumini karibu wote huwa wanakuja kutafuta dawa kwangu, wengine wanataka wapandishwe vyeo, wengine wanataka kujikinga na wengine wana shida mbalimbali, usiwaamini binadamu,” alisema baba, nikabaki nimeduwaa. Hizo zikawa ni habari nyingine za kushangaza sana kwangu.
“Sasa pale si walikuwa wawili? Huyo mwingine ni nani?”
“Si yule mwalimu wenu, Mwashambwa?”
“Mwalimu wetu Mwashambwa anayetufundisha hesabu naye ni mchawi?” niliuliza kwa mshangao mkubwa huku mdomo nikiwa nimeuacha wazi.
“Ndiyo, hata ule mguu wake anaochechemea nasikia alikutana na kombora la kichawi ndiyo likampa ulemavu wa kudumu, siyo mtu mzuri kabisa, we turudi nyumbani utasikia chochote kuhusu watu hao wawili,” baba alisema kwa kujiamini, ukimya mrefu ukatanda kati yetu, hakuna aliyezungumza chochote.
Niliendelea kutembea huku nikiwa na furushi langu la dawa kichwani pamoja na panga, baba yeye alikuwa ametangulia mbele, naye akiwa amebeba dawa na jembe tulilokuwa tunalitumia kuchimbia dawa.
Ili kufika nyumbani kwetu, ilikuwa ni lazima upite nyumba kadhaa za nyasi na nyingine za bati zilizokuwa pembezoni mwa kijiji ndiyo uelekee nyumbani. Miongoni mwa nyumba hizo, ilikuwepo pia na nyumba ya mzee Mwankuga ambaye muda mfupi uliopita baba alikuwa akinisimulia mambo yake kwamba ni mchawi.
Tulipokaribia nyumbani kwa mzee huyo, baba alinionyesha ishara kwamba nisimame, nikafanya hivyo, tukawa tunasikia sauti za watu wengi wakilia kutoka nyumbani kwa mzee huyo, baba akanionyesha ishara kama anayesema ‘unaona?’, nikashika mdomo kwa mshangao. Sikutaka kuamini kwamba kweli mzee Mwankuga alikuwa amefariki dunia.
Je, nini kitafuatia?