feisal firdaus
JF-Expert Member
- Apr 6, 2022
- 424
- 675
Ww Soma tu kwa kujifurahisha kuongea sikuHivi hii story ni kweli au ya kutunga??
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ww Soma tu kwa kujifurahisha kuongea sikuHivi hii story ni kweli au ya kutunga??
>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Sehemu ya tatu -- 3
Tena ni mateso makubwaAsee, ulimwengu wa giza ni full mateso.
Kwa yesu ni maombi tu, sio upuuzi tu
Togo ashakuwa mwanga duh.Tusali ndio tulale mtu kahama kambi[emoji38][emoji38][emoji38]Sehemu ya 40
ILIPOISHIA:
Nilipokisogeza kibuyu hicho karibu na pua, nilikumbana na harufu kali kwelikweli, ikabidi nizibe pua, nikanywa huku nikiwa nimefumba macho. Kabla sijameza, nilisikia vitu vikinitembea mdomoni, nilipotazama vizuri kile kibuyu, pale kwenye mdomo wa kunywea, sikuyaamini macho yangu, nikataka kutema lakini tayari nilishachelewa, vitu vyote vilikimbilia tumboni vyenyewe.
SASA ENDELEA…
Pale kwenye sehemu ya kunywea, ndipo paliponipa picha kwamba nilichokunywa kilikuwa ni kitu gani. Minyoo mingi ya rangi mbalimbali, ilikuwa imechanganywa na maji machungu yenye harufu mbaya mno. Jambo lile, la kugundua kwamba nilikuwa nimekunywa minyoo, lilinifanya nisisimke sana, nilijaribu kujitapisha lakini ilikuwa sawa mna kazi bure.
Kwa jinsi minyoo yenyewe ilivyokuwa imechangamka, muda mfupi tu baadaye, nilisikia tumbo likianza kutibuka, hofu kubwa ikanitanda ndani ya moyo wangu. Sikujua nini itakuwa hatma yangu.
Yule babu alikichukuaa kibuyo na kukifunga, akakirudisha pale chini, nikamuona akichaguachagua na muda mfupi baadaye, alichukua kibuyu kingine lakini hiki kilikuwa kidogo kuliko kile cha awali. Akawatazama wale watu wengine waliokuwa wamekaa pembeni na kutulia kisha akawapa ishara fulani, nikaona wanaume wawili wakiinuka.
Wakatembea harakaharaka kusogea mpaka pale nilipokuwa nimekalishwa. Sikutaka kuyaamini macho yangu, ilibidi nijifikiche macho nikidhani labda nipo ndotoni.
Haikuwa ndoto, ilikuwa ni kweli kabisa. Mbele yangu walikuwa wamesimama baba na baba yake Rahma. Niliwatazama mmoja baada ya mwingine, bado nikawa siamini. Nao walikuwa wamevaa kama wale watu wengine, walijistiri kidogo tu lakini sehemu kubwa ya miili yao ilikuwa wazi.
Ni hapo ndipo nilipoielewa kauli ya baba yake Rahma aliyoitoa muda mfupi kabla ya yale mauzauza hayajanitokea, kwamba eti utii ni jambo muhimu sana na la lazima kwa jamii yao. Kumbe urafiki au ukaribu wa baba na baba yake rahma ulikuwa zaidi ya vile kila mmoja alivyokuwa akiamini.
Yule mzee alimtazama baba, baba naye akamtazama kisha kichwa chake akakiinamisha kwa utii, yule babu akawa anaongea kwa lugha ambayo hata sikuwa naielewa, baba naye akawa anamfuatisha anachokisema, muda mfupi baadaye baba yake Rahma naye alikuwa akifuatisha walichokuwa wanakisema.
Muda mfupi baadaye, walinizunguka na kutengeneza kama duara jingine hivi, wakawa wanaendelea kuzungumza yale maneno kwa sauti ya juu, muda mfupi baadaye wale watu wengine nao walidakia, wakawa wanawafuatisha. Ilivyoonesha, wote walikuwa wakiielewa vizuri lugha ile maana hakuna aliyekuwa akibabaika.
Baadaye, yule mzee alitoa ishara, watu wote wakanyamaza, akaanza kuzungumza lakini safari hii, alikuwa akiongea Kiswahili japo ilionesha hakuwa akikielewa vizuri. Akawaambia watu wote kwamba anayo furaha kubwa kukutana nao usiku huo na furaha yake iliongezwa zaidi na tukio lililokuwa likifanyika usiku huo.
Aliwaambia watu wote kwamba kulikuwa na utambulisho wa mwanachama mpya, akanitaka nisimame. Nilishtuka sana, mwanachama mpya? Wa nini? Ina maana kile ni chama? Kinahusika na nini? Sikuwa na majibu. Nilimgeukia baba, naye akanigeukia, akanipa ishara kwamba nitulie.
Yule babu alimkabidhi baba kile kibuyu, nikamuona akirudi tena pale palipokuwa na vifaa vingine, akachaguachagua kisha nikamuona akichukua kitambaa cheusi, au wengine wanapenda kuita kaniki. Alimpa baba, akainamisha kichwa chake kama ishara ya utii, kisha yule babu akaendelea kuzungumza na kila mtu.
Alisema hatua ya kwanza natakiwa kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kazi kisha baada ya hapo, nitatawazwa rasmi kuwa mwanachama kamili, watu wote wakalipuka kwa shangwe za kila namna. Zilikuwa ni kelele kubwa sana, kila mtu akionesha kuwa na furaha sana.
Baba aliniinamia, akaongea kwa sauti ya chini akiniambia nivue suruali niliyokuwa nimevaa maana mpaka muda huo nilikuwa kifua wazi. Niliona kama ni jambo lisilowezekana, yaani nivue nguo wakati watu wote wananitazama? Macho yakanitoka.
Ni kama baba alinielewa, alinipa na ile kaniki, akanionesha kwa ishara kwamba nijifunge juu ya suruali kisha ndiyo niiteremshe. Nilifanya hivyo, muda mfupi baadaye, nilikuwa nimeshaivua na kujifunga kaniki. Sasa na mimi nilikuwa nikifanana na wale watu isipokuwa mimi nilijifunga kaniki ndefu wakati wengine wote walikuwa wamejifunika kwa vipande vidogo.
Nilikalishwa chini, yule babu akampa ishara baba, akanisogelea na kupiga magoti, akanikabidhi kile kibuyu kilichokuwa kimevalishwa shanga, kisha akaongea kwa sauti ya chini akinitaka nisiogope chochote na nimthibitishie kwamba kweli nimekuwa mtu mzima na si mtoto kama alivyokuwa akiamini. Nilitingisha kichwa, japokuwa hakuwa ameniambia chochote, tayari nilishaelewa kilichokuwa kinaendelea.
Nilipokabidhiwa kile kibuyu, baba na baba yake Rahma waliondoka na kurudi kwenye sehemu zao, yule babu akaniambia nishike kibuyu hicho kwa mikono miwili kisha nikiinue mbele ya uso wangu.
Nilifanya kama alivyoniambia, nikamuona akichukua karai la chuma lenye maji meusi ndani yake, akanimwagia kichwani kisha kwa kutumia kisu kikali, alianza kuninyoa nywele. Sikuwahi kuona mtu akinyolewa nywele kwa siku, hata kule kijijini kwetu ambako saluni zilikuwa chache, tulikuwa tukinyolewa kwa wembe au mkasi.
Kwa kawaida nywele zangu huwa ni nguvu na wakati wa kunyoa huwa ni shughuli kwelikweli lakini huwezi kuamini, yule babu alipitisha mara kadhaa tu, kichwa kikawa cheupe kabisa. Alichukua dawa kutoka kwenye kichupa kimoja kisha akanisogelea, akarudia kunisisitiza kwamba sitakiwi kuachia kibuyu hicho kwani ndiyo maisha yangu.
Alichokifanya, kwa kutumia kilekile kisu, alianza kunichanja chake, kuanzia kichwani, akaja shingoni upande wa nyuma, akashuka mgongoni mpaka miguuni. Kiukweli maumivu niliyokuwa nayasikia yalikuwa makali sana, yote tisa, kumi ni pale alipoanza kunisugua sehemu alizonichanja kwa kutumia ile dawa iliyokuwa kwenye kile kichupa.
Maumivu ya kuchanjwa ukijumlisha na ukali wa ile dawa, nilishindwa kujizuia, nikawa nalia kwa maumivu.
“Kumbe hujakuwa mrume wewe,” alisema yule babu kwa Kiswahili kibovu lakini ambacho kilinifanya nimuelewe. Alimaanisha kwamba eti bado nilikuwa mtoto ndiyo maana nilikuwa nalia. Hakuna kitu ambacho nilikuwa nakichukia kama kuitwa mtoto. Japokuwa nilikuwa nikijisikia maumivu makali, ilibidi nijikaze, akaendelea kunisugua na ile dawa huku nikigugumia kwa maumivu.
Damu nyingi ilikuwa ikinitoka kwenye majeraha yangu lakini safari hii sikujali, sikutaka kuonekana mtoto, yule babu akaendelea mpaka alipomaliza. Baada ya kumaliza, alinishika mkono na kunisimamisha, akanisogeza kwenye ule moto.
Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe pale kulikuwa na nyama nyingi ya kutosha imewekwa pembeni ya moto. Yule babu aliinama pale kwenye nyama, akatoka na kipande kimoja, akanifuata na kunipa.
Kwa akili yangu nilielewa kwamba ananipa ili niichome kwenye moto ikiiva ndiyo niile, nikashangaa ananiambia eti niile vilevile ikiwa mbichi. Nilishtuka sana maana ilikuwa bado na damudamu kabisa.
Nilitamani kumuuliza kwanza ile ni nyama ya nini lakini nilikumbuka kauli ya baba yake rahma na aliyoniambia baba muda mfupi uliopita kwamba natakiwa kuwa mtiifu, ikabidi nifumbe macho, nikaitia mdomoni na kutaka kuimeza bila kutafuna lakini ilikuwa kubwa, ikabidi nipige moyo konde, nikaanza kuitafuna kisha harakaharaka nikameza.
“Twive umile,” alisema yule mzee huku akinionesha kwa ishara kwamba nifumbue mdomo. Sijui kile ni kilugha alichokuwa akizungumza, nilifanya kama alivyoniambia, nikafumbua mdomo. Nadhani alitaka kuhakikisha kama nimemeza, alipohakikisha, alinishika mkono na kuuinua juu kama wanavyofanya waamuzi wa mapambano ya ndondi wanapomtangaza msshi ulingoni.
Watu wote walishangilia kwa nguvu, wengine nikawaona wakirukaruka kwa furaha, ikabidi na mimi nifurahi ingawa bado nilikuwa gizani. Yule mzee aliniachia mkono na kuanza kuzungumza na wale watu, akiwataka wanipe ushirikiano na kunifundisha yale nisiyoyajua.
Wakati anaongea hayo, sijui nini kilinituma nitazame pale zilipokuwepo zile nyama, nikashtuka kuliko kawaida kuona kuna viungo vya binadamu, viganja vya mikono na miguu. Ile nyama aliyonipa aliichukua palepale, kwa hiyo alikuwa amenipa nyama ya mtu? Macho yalinitoka nikiwa siamini macho yangu.
Nikiwa bado nashangaa, mwili ukiwa unatetemeka kwa hofu, nilishtukia wale watu wakikimbilia pale kwenye moto na kujipanga foleni, yule babu akasogea kwenye zile nyama, akawa anagawa, kila mmoja anapita na kupewa kipande chake kisha anatafuta sehemu ya kwenda kukaa na kuanza kula. Nilihisi kama nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo.
“Hongera, umekuwa sasa,” alisema baba huku akinikumbatia, akanishika mkono na kunipeleka kwenye foleni, akaniingiza kwenye foleni.
Je, nini kitafuatia?
>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
>> Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
>> Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Daah Rahma ananyanduliwa balaa aiseeSehemu ya ishirini na sita______26
ILIPOISHIA:
Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.
SASA ENDELEA…
Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
“Sasa baba, unajua mimi kuna mambo mengi sana sielewi, halafu nikikuuliza hata hunipi majibu ya kuridhisha.”
“Hilo siyo jibu, umeanza kuwa na kiburi,” alisema baba kwa sauti ya chini lakini akionesha kama alikuwa amepania kuniadhibu. Sikumjibu chochote, akauma meno kwa hasira na kuelekea pale alipokuwa amesimama baba yake rahma, wakawa wanazungumza jambo. Nadhani walikuwa wananijadili.
Kiukweli, uhusiano wangu na baba ulikuwa umeingia doa kubwa na sababu ya yote, ni mambo ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea ambayo yeye alionesha kwamba anajua kila kitu na pengine ndiyo chanzo cha yote. Bado nilikuwa na maswali mengi ambayo alipaswa kunijibu.
Swali la kwanza, nilitaka aniambie kwa nini wanakijiji wenzake kule kijijini kwetu, Chunya walikuwa wakimtuhumu kwamba ni mchawi na ndiye aliyeshiriki kwenye vifo vya watu wawili katika mazingira ya kutatanisha. Kwa macho yangu nilishuhudia akipambana na watu hao kabla ya baadaye kubainika kwamba wamekufa vifo vya ghafla.
Nilitaka aniambie ukweli, yeye ni mganga kama mwenyewe alivyokuwa akijinadi au alikuwa ni mchawi? Nilitaka pia anieleze, aliwezaje kusafiri kutoka Chunya mpaka Dar es Salaam bila kuwemo kwenye basi tulilokuwa tumepanda lakini muda wote akawa anatoke apale panapotokea tatizo, kama alivyotusaidia kuepukana na ajali mbaya zilizotaka kutokea wakati tukisafiri kutoka Chunya kuja Dar, ya kwanza ikiwa ni kwenye eneo hatari la Mlima Nyoka na la pili likiwa ni kwenye Mlima Kitonga.
Nilitaka anieleze vizuri aliwezaje kuniokoa nisigongwe na gari, lakini wakati huohuo watu wengine wote wakawa hawamuoni wala kumsikia zaidi yangu. Nilitaka aniambie, ile dawa aliyonipa niwe namnyunyizia dereva, ilikuwa na maana gani na iliwezaje kutuepusha na ajali?
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Nataka kujua nini kimetokea hapa kwa akina Rahma maana nasikia kabla sisi hatujafika walikuwa wakiishi kwa amani, mbona tangu tuingie, japo ni muda mfupi tu lakini tayari kuna mambo mengi ya ajabu yametokea? Kwa nini naona mambo ambayo watu wengine hawayaoni?”
“Mbona unaongea peke yako Togo?” sauti ya Rahma ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo machungu, nikashtuka sana kugundua kwamba kumbe nilikuwa nikizungumza kwa sauti huku mwenyewe nikidhani nawaza.
“Umesikia nini kwani?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana. Kwa bahati nzuri, kumbe sikuwa nimetamka kwa sauti mambo mengi zaidi ya kujiuliza kwa nini tangu tufike nyumbani kwa akina Rahma mambo mengi ya ajabu yalikuwa yakitokea.
“Kwani unafikiri ujio wenu ndiyo chanzo cha haya yote?” aliniuliza Rahma kwa upole huku akinishika mkono na kunielekeza tuelekee ndani maana nilikuwa nimesimama, nikiwa nimepoteza kabisa mwelekeo.
“Sisi ndiyo chanzo na pengine mimi ndiyo chanzo hasa,” nilisema kwa sauti ya unyonge, Rahma akaniambia kuna jambo zuri anataka tukazungumze chumbani kwake. Nilimkubalia, tulipoingia ndani tulipitiliza mpaka chumbani kwake.
Akina mama ilibidi waanze kuchakarika kwa sababu hata chakula cha usiku hakikuwa kimepikwa siku hiyo kwa sababu ya majanga yaliyonitokea ambapo baada ya kupata taarifa kwamba nipo hospitali nikiwa sijitambui, ilibidi nyumba nzima ije kunijulia hali. Waliingia jikoni huku ndugu zangu na wadogo zake Rahma wakikaa sebuleni kutazama runinga.
Baba na baba Rahma, kama kawaida yao wao walibaki nje wakiendelea na mazungumzo yao.
“Unataka kuniambia nini Rahma,” nilimuuliza kwa upole baada ya kumuona akifunga mlango wa chumbani kwake kwa komeo. Hakujibu kitu zaidi ya kuvua blauzi yake kisha ‘bra’, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, nilijikuta nikisisimka mno. Rahma alikuwa amejaliwa kifua kizuri mno, ambacho kwa mwanaume yeyote aliyekamilika, ilikuwa ni lazima atokwe na udenda kama fisi aliyeona mfupa.
Rahma aliendelea kunikumbatia huku akinibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu kimahaba, hali ambayo ilinichanganya kabisa kichwa changu. Taratibu alinirudisha nyuma mpaka tulipofika kwenye uwanja wa fundi seremala, akanisukumia juu yake kisha akamalizia na za chini zilizokuwa zimesalia.
Akionesha kuwa na papara za hali ya juu, alihamia kwangu na kuitoa ya juu, nikabaki kifua wazi, akahamia na ile ya chini na muda mfupi baadaye, tulikuwa ‘saresare’ maua. Bado mwili wangu haukuwa na nguvu kwa hiyo nilimuachia yeye ndiye awe ‘dairekta’ wa filamu ile ya kusisimua na kweli alikitendea haki cheo nilichompa.
Kwa ufanisi wa hali ya juu, Rahma aliitii kiu yangu, mpaka anashuka kutoka juu ya mnazi, alikuwa ameshaangua madafu kadhaa, akajitupa upande wa pili huku akinishukuru, na mimi nikawa namshukuru. Hatukuchukua raundi, kila mmoja akapitiwa na usingizi mzito.
Nadhani wangu ulikuwa mzito zaidi kwa sababu kuichwa changu kilikuwa kimebeba mambo mazito mno na alichonipa rahma ilikuwa sawa na dawa ya usingizi. Tulikuja kushtuka baadaye baada ya kusikia mlango wa chumba cha Rahma ukigongwa. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikamuamsha Rahma ambaye aliamka kichovu na kusogea karibu na mlango.
Safari hii hatukuwa na hofu tena kwani tulikuwa na ruhusa ya kukaa pamoja karibu, mimi kazi yangu ikiwa ni kuhakikisha rahma harudii tena kujaribu kuyakatisha maisha yake na Rahma kuhakikisha ananisaidia mimi mgonjwa.
“Unasemaje?”
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Mama anauliza kama mtakula na sisi au mletewe chakula chenu huku.”
‘Ngoja nakuja mwenyewe,” alijibu Rahma wakati akizungumza na mdogo wake aliyetumwa na mama yao kuwaulizia.
‘Eti mpenzi wangu, we unapenda tukakae sebuleni au tulie hukuhuku chumbani.”
‘Utakavbyosema wewe hamna shida ila napenda zaidi tukikaa peke yetu,” nilimjibu, akanitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yameelemewa na usingizi kisha akaachia tabasamu la kichovu.
“Ngoja nikaonge kwanza,” alisema na kuchukua kitenge, akaelekea bafuni na muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amechangamka kidogo. Ilibidi na mimi niende kuoga wakati yeye akihangaikia chakula.
Niliporudi kutoka bafuni, tayari rahma alikuwa ameleta chakula kizuri kule chumbani. Tofauti ya vyakula tulivyozoea kula kijijini na mjini ilikuwa kubwa mno. Chakula kilipikwa vizuri, yaani kwa kukitazama tu ilikuwa ni lazima mate yakutoke. Tulinawa vizuri lakini nilipotaka kuanza kula, Rahma alinikatazana na kusema anataka anilishe kidogo.
Yalikuwa ni mambo mageni kabisa, nilizoea kuona watoto wadogo au wagonjwa ambao wako mahtuti ndiyo wanalishwa, lakini eti dume mimi nilishwe? Hata hivyo sikumkatalia. Akaanza kunilisha kwa upole, huku mara kwa mara akinitazama machoni. Sijui nini kilimtokea Rahma lakini alionesha kunipenda sana, tena sana.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Mara kwa mara alikuwa akinibusu na kuniambia kwamba ananipenda sana, mpaka nikawa najisikia aibu. Sikuwa najua kabisa mambo ya kikubwa na wala sikuwa na uelewa wowote wa mahaba. Nilikuwa nikisikiasikia kwamba watu wa pwani ndiyo wataalamu wa hayo mambo.
Japo Rahma alikuwa akinilisha matonge madogo tofauti na niliyozoea lakini kiukweli nikiri kwamba nilijisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu. Tulipomaliza kula, alitoa vyombo, akaja kufanya usafi kisha akafunga tena mlango.
“Itabidi mimi nikalale chumbani kwangu,” nilimwambia Rahma lakini akakataa katakata, akaniambia tutalala wote humo chumbani kwake na tutajifunika shuka moja. Japokuwa kwa nje nilikuwa navunga, ukweli ni kwamba hata mimi nilikuwa napenda sana kuwa karibu na Rahma hasa kutokana na mapenzi ya dhati aliyokuwa ananionesha.
Ile tofauti ya umri kati yetu sikuiona tena, namimi nikawa najiona mkubwa kama yeye, hata ile harufu ya undugu kati yetu nayo ilitoweka kabisa, ndani ya muda mfupi tu tuliokaa pamoja ikawa utafikiri tumeishi pamoja kwa miaka mingi tangu zamani.
Tulipiga stori za hapa na pale, baadaye muda wa kulala ulipofika, kama ilivyokuwa mara ya kwanza, Rahma aliniganda kama ruba, tukapeana tende na halua kwa mara nyingine kabla ya kupitiwa na usingizi mzito, akiwa ameniganda kifuani kama ruba.
Nilikuja kuzinduka usiku wa manane baada ya kuhisi hali isiyo ya kawaida. Kilichoniamsha, zilikuwa ni kelele za paka waliokuwa wakipigana juu ya paa, huku wakitoa milio ya ajabu kama watoto wachanga.
Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia?
>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
>>Usiache kutembelea… Simulizi za Majonzi
>>Usiache kutembelea… Simulizi za Majonzi