Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Sehemu ya 38


ILIPOISHIA:

“Wewe sasa hivi una mambo ya kikubwa, hutakiwi kuwa unachanganyikana na wenzako, inabidi uanze kukaa na sisi baba zako, vuta kiti kaa hapa,” alisema baba, akawa ametibua shoo nzima, nilitaka kutoa visingizio lakini hakutaka kusikia chochote kutoka kwangu, ikabidi nikae na kujiinamia, wote wakawa wananitazama.

SASA ENDELEA…

“Una matatizo gani?” baba aliniuliza baada ya kuniona nikiwa nimekaa huku uso wangu nikiwa nimeukunja.

“Unajua hata sisi wote unaotuona hapa, kuna kipindi tulikuwa kama wewe, sote tulikuwa vijana hapa na tulipitia yote unayoyapitia, kwa hiyo usitake kujifanya mjanja, umenisikia?” baba alisema kwa msisitizo.

“Na nyie mlipitia mauzauza kama yangu? Kwa nini kila siku huniambii ukweli mimi ni nani?” kwa mara ya kwanza nilimpandishia baba sauti mbele ya baba yake Rahma, nikaona wameacha kucheza karata, wakawa wanatazamana kisha wote wakanigeukia.

“Sisi ni baba zako, hutakiwi kuzungumza kwa namna hiyo, umesikia mwanangu,” alisema baba yake Rahma huku akinipigapiga begani. Tofauti kati ya baba na baba yake Rahma, yeye alikuwa na busara na mpole lakini baba yeye alizoea kufokafoka tu.

“Hapana mimi nimechoka, kila siku nikimuuliza baba aniambie ukweli hataki, mauzauza yanazidi kunitokea kila siku, mambo ya ajabu yananikumba mimi tu, mbona ndugu zangu hakuna anayepata shida kama mimi,” nilisema kwa uchungu huku machozi yakianza kunilengalenga.

Baada ya kusema ya moyoni, niliegamia meza na kujilaza huku machozi yakinitoka, kiukweli nilikuwa na dukuduku kubwa sana moyoni. Hakuna kitu ambacho kilikuwa kikinikasirisha kama kitendo cha baba kuwa ‘ananikontroo’ kama roboti bila kunieleza ukweli uliokuwa nyuma ya maisha yangu.

“Najua kwamba mimi ni mwanaye, tena anayenipenda kuliko watoto wengine wote lakini kwa nini nipo tofauti? Kwa nini haniambii ukweli?” nilisema kwa kulalama, machozi yakiwa yanaendelea kunitoka.

“Kama anaweza kufikiria haya maana yake ni kwamba ameshapevuka kiakili, nafikiri ni muda muafaka wa yeye kuujua ukweli.”

“Hapana, bado hajakua huyu, ana mambo ya kitoto sana, mimi ndiyo namjua,” baba alisema, kauli ambayo ilinifanya niinuke pale mezani na kumkodolea baba macho. Yaani kumbe alikuwa anashindwa kunieleza ukweli kwa kipindi chote hicho kwa sababu tu alikuwa anahisi kwamba mimi bado nina akili za kitoto?

Kauli ile ilinifanya nijiulize maswali mengi yaliyokosa majibu. Kwa nini baba alikuwa ananiona mimi kama bado mtoto wakati tayari nilishapevuka na kuwa mwanaume kamili? Hata Rahma aliniambia kwamba mimi ni kidume cha mbegu, achilia mbali Isri aliyekuwa akinisifia sana. Na kama ni hivyo, mbona pale aliponiita alisema nimeshakua mkubwa kwa hiyo natakiwa kukaa nao?

“Kwa nini unaniona bado mdogo?”

“Kwa sababu huwezi kuelewa kitu kwa kuelezwa mara moja. Kila unachokatazwa kufanya wewe unafanya,” alisema baba na kurudia kauli yake kwamba hawezi kuniamini kwa asilimia mia moja mpaka nitakapomuonesha ukomavu wangu wa akili.

Kiukweli kwa kipengele hicho baba alikuwa amenishinda kwa pointi na udhaifu wangu mkubwa nilikuwa nimeuonesha kwenye suala zima la mapenzi. Nakumbuka tulianza kutofautiana na baba baada ya kukutana na Isri kwenye basi, akawa ananikataza kuwa naye karibu lakini nikampuuza.

Pia hata tulipofika kwa akina Rahma, mara kadhaa alishagundua kwamba tulikuwa na ukaribu usiofaa na akanikataza kwa msisitizo kwamba nisijaribu kukutana kimwili na Rahma, tena mpaka wakatumia kigezo kwamba sisi tulikuwa ndugu lakini bado tuliangukia dhambini, tena siyo mara moja.

Kubwa zaidi, hata hapo tulipokuwa tukizungumza, licha ya baba kunikataza kwamba endapo nitakutana kimwili tena na Rahma basi atakufa, kama wasingeniita na kunizuia, pengine muda huo ningekuwa ‘nikilitafunilia mbali tunda la mti uliokatazwa’ na Rahma.

Kama kigezo hicho pekee ndicho kilikuwa kinaonesha kwamba mtu amekuwa mkubwa, basi ni kweli nilikuwa nimefeli mtihani uliokuwa mbele yangu, nikawa mdogo kama ‘piriton’.

“Eti ni kweli anachokisema baba yako?” aliniuliza baba yake Rahma, nikakosa cha kujibu.

“Unajua kwa jinsi sisi baba zako tulivyo, na pengine wewe ukija kupata nafasi hiyo, hakuna kitu ambacho kinaheshimika kwenye jamii yetu kama utii. Ukiambiwa jambo ni lazima ufanye vilevile ulivyoambiwa na si vinginevyo, kosa dogo tu linaweza kusababisha matatizo makubwa mno ndiyo maana baba yako anakuwa mkali,” alisema baba yake Rahma.

>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Kauli hiyo ilinifanya nijiulize maswali mengine mengi zaidi. Aliposema ‘jamii yetu’, baba yake Rahma alikuwa akimaanisha nini? Nilianza kupata picha kwamba huenda naye alikuwa anafahamu kila kitu kinachoendelea na kama alikuwa jamii moja na baba, basi moja kwa moja na yeye alikuwa akishughulika na mambo kama yale ya baba.

Tangu tumefika, baba yake Rahma hakuwahi kutoka kwamba labda anaenda kazini au kwenye biashara zake, muda wote alikuwa nyumbani tu lakini alikuwa na maisha ya hali ya juu sana. Nikiwa bado naendelea kujiuliza maswali mengi, baba yake Rahma alinisogelea.

“Baba yako anasema hakuamini kwa sababu bado una akili za kitoto lakini mimi nikikutazama nakiona kitu kikubwa sana ndani yako, tucheze dili?” aliniuliza kwa sauti ya chini huku akinikonyeza kwa jicho moja. Sikujua ni dili gani ila kwa sababu nilikuwa nataka kujua ukweli wa maisha yangu, nilitingisha kichwa kuonesha kumkubalia.

“Inatakiwa mimi na wewe tukazungumze lakini hatuwezi kuzungumzia humu ndani, inabidi tutoke nje! Lakini hapohapo, baba yako ameniambia kwamba kuna ‘madhambi’ mengine umeyafanya kiasi kwamba wewe na yeye hamuwezi kutoka mpaka giza liingie, ni kweli au si kweli?”

“Ni kweli.”

“Sasa mtihani wa kwanza, unatakiwa ukazivunje hizo nguvu zako za giza ulizozitega pale mlangoni.”

“Mimi sina nguvu zozote za giza wala sijatega chochote…” nilimkatisha lakini alinitazama usoni na kunikumbusha kwamba utii ni jambo muhimu sana, nikaufyata mkia.

“Unauona ule mlango, inatakiwa utembee kinyumenyume mpaka pale, ukiukaribia, unaugeukia lakini unatakiwa kufumba macho, kisha unakojoa mkojo wa kutosha kulowanisha eneo lote la mlango,” alisema baba yake Rahma, macho yakanitoka kama mjusi aliyebanwa na mlango.

“Hakuna kitu kinachoweza kuvunja na kumaliza kabisa nguvu za giza kama mkojo, haya fanya kama nilivyokwambia,” alisema baba yake Rahma. Ama kweli huo ulikuwa mtego mkali sana kwangu, yaani nikakojoe mlangoni, tena mahali ambapo watu wote waliokuwa sebuleni wangeweza kuniona?

Sikujua ndugu zangu watakichukuliaje kitendo hicho, wala sikujua Rahma na wadogo zake nao watanichukuliaje ila kwa sababu nilikuwa na shauku ya kuujua ukweli, nilipiga moyo konde.

>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Wakati nikijiandaa kwenda, nilimsikia Rahma akiimba huku akitoka koridoni na kwenda kule sebuleni, nadhani alishachoka kusubiri na kuamua kunifuata, mtihani ukazidi kuwa mgumu. Ningemjibu nini Rahma endapo angeniuliza kwa nini nakojoa mlangoni wakati choo kipo, tena siyo kwamba nimelewa au naumwa, nina akili zangu timamu kabisa!

Baba na baba yake Rahma walikuwa wametulia wananitazama huku nikimuona baba uso wake ukionesha ishara kama anayesema ‘hawezi huyu, akili zake bado za kitoto’. Niliamua kujilipua, nikasema liwalo na liwe, nilisogea usawa wa mlango, nikageuka na kuupa mgongo, nikaanza kutembea kinyumenyume kuuelekea kisha nikafumba macho, nilipoukaribia, niligeuka, macho nikiwa nimeyafumba.

Nilifungua zipu kisha nikaanza kufanya kama vile nilivyoelekezwa. Nikiwa naendelea na kitendo kile cha aibu na cha aina yake, nilisikia watu wote waliokuwa sebuleni wakishtuka, nadhani waliniona nilichokuwa nakifanya, sikuwajali, nikaendelea kuumwaga, mara kilisikika kishindo kikubwa ambacho kilinifanya nishindwe kuendelea kufumba macho, nikayafumbua.

“Mungu wangu!” nilisema kwa sauti ya juu.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 39




ILIPOISHIA:

Nilifungua zipu kisha nikaanza kufanya kama vile nilivyoelekezwa. Nikiwa naendelea na kitendo kile cha aibu na cha aina yake, nilisikia watu wote waliokuwa sebuleni wakishtuka, nadhani waliniona nilichokuwa nakifanya, sikuwajali, nikaendelea kuumwaga, mara kilisikika kishindo kikubwa ambacho kilinifanya nishindwe kuendelea kufumba macho, nikayafumbua.

“Mungu wangu!” nilisema kwa sauti ya juu.

SASA ENDELEA…

Kile kilichokuwa kikinitoka, hakikuwa haja ndogo kama mwenyewe nilivyokuwa nadhani, ilikuwa ni damu, tena nzito kabisa yenye wekundu uliokolea kisawasawa, na kile kishindo kilichosikika, kilikuwa ni cha dude kubwa lililoanguka kutoka angani.

Sijui niliiteje dude hilo kwa sababu kwanza lilikuwa na miiba kama nungunungu, lakini pia lilikuwa na mabawa yenye kucha kama popo, ukubwa wake ulikuwa kama ng’ombe mdogo.

Usoni lilikuwa na pembe zilizojikunja na sehemu ya macho, kulikuwa kumezibwa kabisa, kwa kifupi halikuwa na macho. Ile damu iliendelea kunitoka, hata pale nilipotaka kuikata haja ndogo, iliendelea kunitoka kwa wingi utafikiri inavutwa na bomba.

Lile dude la ajabu, lilijiburuta chini na kusogea mpaka pale nilipokuwa natolea haja ndogo, kwenye vizingiti vya milango, likafumbua mdomo kidogo na kutoa ulimi mrefu uliokuwa umegawanyika katikati kama wa nyoka, likaanza kulamba kile nilichokuwa nakitoa.

Naomba nieleze vizuri kilichotokea na ambacho huwa kinatokea pale mtu anapokumbwa na nguvu za uchawi. Yaani tukio unaliona, na ile hatari iliyopo mbele yako unaiona kabisa lakini mwili unakufa ganzi, unakuwa huwezi kufanya chochote zaidi ya kile ambacho unakuwa umeshaanza kukifanya na akili zako zinakosa maamuzi, kwa kifupi unakuwa siyo wewe.

>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Hicho ndicho kilichotokea, sikuwa na uwezo wa kuikatisha ile haja ndogo ya damu, sikuwa na uwezo wa kwenda mbele, wala sikuwa na uwezo wa kurudi nyuma, nilitamani kupiga kelele za kuomba msaada lakini pia sikuweza kufanya hivyo, nikabaki nimeduwaa tu.

Lile dude lililamba ile damu yote pale mlangoni, likaona haitoshi, likafumbua mdomo wake ambao ulikuwa na meno mengi na kukinga ile iliyokuwa ikiendelea kunitoka kupitia haja ndogo, nikasikia kitu kama ganzi ikinipata kwenye maeneo yangu nyeti kisha ile damu ikakata.

Lile dude ambalo ama kwa hakika lilikuwa linatisha, likajilamba na kugeuka, likajikung’uta kwa nguvu kwenye mabawa yake yenye kucha kubwa na kali, likawa kama linataka kuruka kwani lilipigapiga mbawa zake, kufumba na kufumbua, likayeyuka na kupotea.

Lilipopotea tu, nilihisi kichwa kikiwa kizito, nikaanza kuona giza machoni mwangu, nikawa nasikia sauti za ajabuajabu masikioni, nikadondoka chini kama mzigo. Sikuelewa tena kilichoendelea.

***

Nilipokuja kuzinduka, nilijikuta nimelala chini kwenye majani, mwili wangu ukiwa unahisi baridi kali kuliko kawaida. Kilichonizindua zilikuwa ni kelele za ngoma na manyanga na sauti za ajabuajabu za watu wakiimba nyimbo kwa lugha ambayo sikuwa naielewa.

Nilifumbua macho, huku mapigo yangu ya moyo yakiwa yananienda mbio kuliko kawaida, macho yangu yalitazama juu moja kwa moja. Nikawa naziona nyotanyota kwa mbali kuashiria kwamba ni usiku sana, lakini pia upande wangu wa kushoto, kulikuwa kumewashwa moto mkubwa ambao ulipafanya pale nilipolala, pawe na mwanga.

Niligeuza shingo kutazama pale ni wapi, nilishtuka kugundua kwamba kumbe nilikuwa katikati ya duara, watu wengi waliokuwa hawana kitu mwilini zaidi ya kujiziba kidogo na nguo nyeusi au nyekundu kwenye maeneo nyeti walikuwa wamenizunguka. Wengine ambao ni wanawake, walikuwa wamejiziba pia vifuani mwao.

>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Walikuwa wakiimba na kucheza kwa kuzunguka duara ambalo ndani yake nilikuwa nimelazwa mimi na pia kulikuwa na moto mkubwa jirani kidogo na pale nilipokuwa nimelala. Walikuwa wakiimba na kucheza, huku kila mmoja akionesha kuwa na furaha kubwa.

Nilishtuka mno, nikawa sielewi pale ni wapi na nimefikaje, nilijaribu kuwatazama watu hao kwenye nyuso zao kama kuna yeyote ninayeweza kumtambua lakini macho yangu hayakuwa na nguvu za kutosha kuona. Nilitaka kusimama lakini nilishtuka zaidi kugundua kwamba kumbe nilikuwa nimefungwa mikono na miguu kwa kamba za miti.

Zile purukushani zangu, ziliwafanya wale watu waache kila walichokuwa wanakifanya, wote wakawa wananitazama. Niligeuka huku na kule, wote walikuwa wamenikazia macho. Kilichozidi kunitisha, macho yao yalikuwa yakiwaka kama wanyama wakali wa porini.

Nikamsikia mmoja kati yao akizungumza kwa lugha ambayo sikuwa naielewa, watu wote wakainua mikono juu kisha taratibu wakaishusha chini, wakati wakishusha mikono, nao walishuka mpaka wakapiga magoti, wakapeleka vichwa vyao mpaka chini kisha wakainuka na kusimama kama mwanzo.

Yule mwanaume ambaye sikuwa najua yupo upande gani, aliyarudia tena maneno yale, wakafanya hivyo tena mpaka chini, wakarudia mara tatu kisha wote wakakaa chini na kukunja miguu.

Kizee kimoja kilichokuwa kimepinda mgongo, kiliibuka kutoka kusikojulikana, kikiwa kinatembelea mkongojo. Kikawa kinajikongoja kuja pale nilipokuwa nimefungwa, kadiri kilivyokuwa kinanikaribia ndivyo mapigo ya moyo wangu yalivyokuwa yakizidi kuongezeka.

Sikujua kinataka kunifanya nini, kilisogea mpaka pale nilipokuwa nimefungwa, nikakiona kikitoa kisu kikali, kikaniinamia huku kikiyumbayumba, nikajua nimekwisha. Nimewahi kusikia kwamba wachawi wana mchezo wa kuchinja watu na kuwala nyama, nikajua na mimi ndiyo siku yangu ya kuliwa imewadia.

Tofauti na nilivyotegemea, wala hakunidhuru mwilini, badala yake alikitumia kile kisu kukata kamba nilizofungwa mikononi na miguuni. Kilichonishangaza zaidi, kumbe alikuwa akinijua mpaka jina langu kamili.

“Togolai!”

“Naam, shikamoo babu,” niliitikia kwa kutetemeka. Hakujibu salamu yangu, badala yake alinionesha sehemu ya kukaa, akaniambia kwa ishara nikunje miguu kama watu wengine wote walivyokuwa wamekaa. Nilitii agizo hilo haraka.

Kumbe pembeni ya pale nilipokuwa nimelazwa, kulikuwa na vifaa mbalimbali, nikamuona akichukua kibuyu kimoja, akakitingisha kisha akanipa na kunionesha kwa ishara kwamba ninywe kilichomo ndani.

Huku nikitetemeka, nilikishika kibuyu hicho, nikawa nakipeleka mdomoni huku nikimtazama kwa kina mzee huyo, pamoja na watu wengine waliokuwa wamenizunguka kwa mbali.

“Nwa, ulogoleza shoni, nwa!” aliongea kwa kilugha ambacho sikuwa nakielewa lakini kwa jinsi matamshi yake yalivyokuwa, nilihisi ananiambia, ‘kunywa, unaogopa nini, kunywa’.

Nilipokisogeza kibuyu hicho karibu na pua, nilikumbana na harufu kali kwelikweli, ikabidi nizibe pua, nikanywa huku nikiwa nimefumba macho. Kabla sijameza, nilisikia vitu vikinitembea mdomoni, nilipotazama vizuri kile kibuyu, pale kwenye mdomo wa kunywea, sikuyaamini macho yangu, nikataka kutema lakini tayari nilishachelewa, vitu vyote vilikimbilia tumboni vyenyewe.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 40




ILIPOISHIA:

Nilipokisogeza kibuyu hicho karibu na pua, nilikumbana na harufu kali kwelikweli, ikabidi nizibe pua, nikanywa huku nikiwa nimefumba macho. Kabla sijameza, nilisikia vitu vikinitembea mdomoni, nilipotazama vizuri kile kibuyu, pale kwenye mdomo wa kunywea, sikuyaamini macho yangu, nikataka kutema lakini tayari nilishachelewa, vitu vyote vilikimbilia tumboni vyenyewe.

SASA ENDELEA…

Pale kwenye sehemu ya kunywea, ndipo paliponipa picha kwamba nilichokunywa kilikuwa ni kitu gani. Minyoo mingi ya rangi mbalimbali, ilikuwa imechanganywa na maji machungu yenye harufu mbaya mno. Jambo lile, la kugundua kwamba nilikuwa nimekunywa minyoo, lilinifanya nisisimke sana, nilijaribu kujitapisha lakini ilikuwa sawa mna kazi bure.

Kwa jinsi minyoo yenyewe ilivyokuwa imechangamka, muda mfupi tu baadaye, nilisikia tumbo likianza kutibuka, hofu kubwa ikanitanda ndani ya moyo wangu. Sikujua nini itakuwa hatma yangu.

Yule babu alikichukuaa kibuyo na kukifunga, akakirudisha pale chini, nikamuona akichaguachagua na muda mfupi baadaye, alichukua kibuyu kingine lakini hiki kilikuwa kidogo kuliko kile cha awali. Akawatazama wale watu wengine waliokuwa wamekaa pembeni na kutulia kisha akawapa ishara fulani, nikaona wanaume wawili wakiinuka.

Wakatembea harakaharaka kusogea mpaka pale nilipokuwa nimekalishwa. Sikutaka kuyaamini macho yangu, ilibidi nijifikiche macho nikidhani labda nipo ndotoni.

Haikuwa ndoto, ilikuwa ni kweli kabisa. Mbele yangu walikuwa wamesimama baba na baba yake Rahma. Niliwatazama mmoja baada ya mwingine, bado nikawa siamini. Nao walikuwa wamevaa kama wale watu wengine, walijistiri kidogo tu lakini sehemu kubwa ya miili yao ilikuwa wazi.

Ni hapo ndipo nilipoielewa kauli ya baba yake Rahma aliyoitoa muda mfupi kabla ya yale mauzauza hayajanitokea, kwamba eti utii ni jambo muhimu sana na la lazima kwa jamii yao. Kumbe urafiki au ukaribu wa baba na baba yake rahma ulikuwa zaidi ya vile kila mmoja alivyokuwa akiamini.

>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Yule mzee alimtazama baba, baba naye akamtazama kisha kichwa chake akakiinamisha kwa utii, yule babu akawa anaongea kwa lugha ambayo hata sikuwa naielewa, baba naye akawa anamfuatisha anachokisema, muda mfupi baadaye baba yake Rahma naye alikuwa akifuatisha walichokuwa wanakisema.

Muda mfupi baadaye, walinizunguka na kutengeneza kama duara jingine hivi, wakawa wanaendelea kuzungumza yale maneno kwa sauti ya juu, muda mfupi baadaye wale watu wengine nao walidakia, wakawa wanawafuatisha. Ilivyoonesha, wote walikuwa wakiielewa vizuri lugha ile maana hakuna aliyekuwa akibabaika.

Baadaye, yule mzee alitoa ishara, watu wote wakanyamaza, akaanza kuzungumza lakini safari hii, alikuwa akiongea Kiswahili japo ilionesha hakuwa akikielewa vizuri. Akawaambia watu wote kwamba anayo furaha kubwa kukutana nao usiku huo na furaha yake iliongezwa zaidi na tukio lililokuwa likifanyika usiku huo.

Aliwaambia watu wote kwamba kulikuwa na utambulisho wa mwanachama mpya, akanitaka nisimame. Nilishtuka sana, mwanachama mpya? Wa nini? Ina maana kile ni chama? Kinahusika na nini? Sikuwa na majibu. Nilimgeukia baba, naye akanigeukia, akanipa ishara kwamba nitulie.

Yule babu alimkabidhi baba kile kibuyu, nikamuona akirudi tena pale palipokuwa na vifaa vingine, akachaguachagua kisha nikamuona akichukua kitambaa cheusi, au wengine wanapenda kuita kaniki. Alimpa baba, akainamisha kichwa chake kama ishara ya utii, kisha yule babu akaendelea kuzungumza na kila mtu.

Alisema hatua ya kwanza natakiwa kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kazi kisha baada ya hapo, nitatawazwa rasmi kuwa mwanachama kamili, watu wote wakalipuka kwa shangwe za kila namna. Zilikuwa ni kelele kubwa sana, kila mtu akionesha kuwa na furaha sana.

Baba aliniinamia, akaongea kwa sauti ya chini akiniambia nivue suruali niliyokuwa nimevaa maana mpaka muda huo nilikuwa kifua wazi. Niliona kama ni jambo lisilowezekana, yaani nivue nguo wakati watu wote wananitazama? Macho yakanitoka.

>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Ni kama baba alinielewa, alinipa na ile kaniki, akanionesha kwa ishara kwamba nijifunge juu ya suruali kisha ndiyo niiteremshe. Nilifanya hivyo, muda mfupi baadaye, nilikuwa nimeshaivua na kujifunga kaniki. Sasa na mimi nilikuwa nikifanana na wale watu isipokuwa mimi nilijifunga kaniki ndefu wakati wengine wote walikuwa wamejifunika kwa vipande vidogo.

Nilikalishwa chini, yule babu akampa ishara baba, akanisogelea na kupiga magoti, akanikabidhi kile kibuyu kilichokuwa kimevalishwa shanga, kisha akaongea kwa sauti ya chini akinitaka nisiogope chochote na nimthibitishie kwamba kweli nimekuwa mtu mzima na si mtoto kama alivyokuwa akiamini. Nilitingisha kichwa, japokuwa hakuwa ameniambia chochote, tayari nilishaelewa kilichokuwa kinaendelea.

Nilipokabidhiwa kile kibuyu, baba na baba yake Rahma waliondoka na kurudi kwenye sehemu zao, yule babu akaniambia nishike kibuyu hicho kwa mikono miwili kisha nikiinue mbele ya uso wangu.

Nilifanya kama alivyoniambia, nikamuona akichukua karai la chuma lenye maji meusi ndani yake, akanimwagia kichwani kisha kwa kutumia kisu kikali, alianza kuninyoa nywele. Sikuwahi kuona mtu akinyolewa nywele kwa siku, hata kule kijijini kwetu ambako saluni zilikuwa chache, tulikuwa tukinyolewa kwa wembe au mkasi.

Kwa kawaida nywele zangu huwa ni nguvu na wakati wa kunyoa huwa ni shughuli kwelikweli lakini huwezi kuamini, yule babu alipitisha mara kadhaa tu, kichwa kikawa cheupe kabisa. Alichukua dawa kutoka kwenye kichupa kimoja kisha akanisogelea, akarudia kunisisitiza kwamba sitakiwi kuachia kibuyu hicho kwani ndiyo maisha yangu.

Alichokifanya, kwa kutumia kilekile kisu, alianza kunichanja chake, kuanzia kichwani, akaja shingoni upande wa nyuma, akashuka mgongoni mpaka miguuni. Kiukweli maumivu niliyokuwa nayasikia yalikuwa makali sana, yote tisa, kumi ni pale alipoanza kunisugua sehemu alizonichanja kwa kutumia ile dawa iliyokuwa kwenye kile kichupa.

Maumivu ya kuchanjwa ukijumlisha na ukali wa ile dawa, nilishindwa kujizuia, nikawa nalia kwa maumivu.

“Kumbe hujakuwa mrume wewe,” alisema yule babu kwa Kiswahili kibovu lakini ambacho kilinifanya nimuelewe. Alimaanisha kwamba eti bado nilikuwa mtoto ndiyo maana nilikuwa nalia. Hakuna kitu ambacho nilikuwa nakichukia kama kuitwa mtoto. Japokuwa nilikuwa nikijisikia maumivu makali, ilibidi nijikaze, akaendelea kunisugua na ile dawa huku nikigugumia kwa maumivu.

Damu nyingi ilikuwa ikinitoka kwenye majeraha yangu lakini safari hii sikujali, sikutaka kuonekana mtoto, yule babu akaendelea mpaka alipomaliza. Baada ya kumaliza, alinishika mkono na kunisimamisha, akanisogeza kwenye ule moto.

Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe pale kulikuwa na nyama nyingi ya kutosha imewekwa pembeni ya moto. Yule babu aliinama pale kwenye nyama, akatoka na kipande kimoja, akanifuata na kunipa.

Kwa akili yangu nilielewa kwamba ananipa ili niichome kwenye moto ikiiva ndiyo niile, nikashangaa ananiambia eti niile vilevile ikiwa mbichi. Nilishtuka sana maana ilikuwa bado na damudamu kabisa.

Nilitamani kumuuliza kwanza ile ni nyama ya nini lakini nilikumbuka kauli ya baba yake rahma na aliyoniambia baba muda mfupi uliopita kwamba natakiwa kuwa mtiifu, ikabidi nifumbe macho, nikaitia mdomoni na kutaka kuimeza bila kutafuna lakini ilikuwa kubwa, ikabidi nipige moyo konde, nikaanza kuitafuna kisha harakaharaka nikameza.

“Twive umile,” alisema yule mzee huku akinionesha kwa ishara kwamba nifumbue mdomo. Sijui kile ni kilugha alichokuwa akizungumza, nilifanya kama alivyoniambia, nikafumbua mdomo. Nadhani alitaka kuhakikisha kama nimemeza, alipohakikisha, alinishika mkono na kuuinua juu kama wanavyofanya waamuzi wa mapambano ya ndondi wanapomtangaza msshi ulingoni.

Watu wote walishangilia kwa nguvu, wengine nikawaona wakirukaruka kwa furaha, ikabidi na mimi nifurahi ingawa bado nilikuwa gizani. Yule mzee aliniachia mkono na kuanza kuzungumza na wale watu, akiwataka wanipe ushirikiano na kunifundisha yale nisiyoyajua.

Wakati anaongea hayo, sijui nini kilinituma nitazame pale zilipokuwepo zile nyama, nikashtuka kuliko kawaida kuona kuna viungo vya binadamu, viganja vya mikono na miguu. Ile nyama aliyonipa aliichukua palepale, kwa hiyo alikuwa amenipa nyama ya mtu? Macho yalinitoka nikiwa siamini macho yangu.

Nikiwa bado nashangaa, mwili ukiwa unatetemeka kwa hofu, nilishtukia wale watu wakikimbilia pale kwenye moto na kujipanga foleni, yule babu akasogea kwenye zile nyama, akawa anagawa, kila mmoja anapita na kupewa kipande chake kisha anatafuta sehemu ya kwenda kukaa na kuanza kula. Nilihisi kama nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo.

“Hongera, umekuwa sasa,” alisema baba huku akinikumbatia, akanishika mkono na kunipeleka kwenye foleni, akaniingiza kwenye foleni.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 40




ILIPOISHIA:

Nilipokisogeza kibuyu hicho karibu na pua, nilikumbana na harufu kali kwelikweli, ikabidi nizibe pua, nikanywa huku nikiwa nimefumba macho. Kabla sijameza, nilisikia vitu vikinitembea mdomoni, nilipotazama vizuri kile kibuyu, pale kwenye mdomo wa kunywea, sikuyaamini macho yangu, nikataka kutema lakini tayari nilishachelewa, vitu vyote vilikimbilia tumboni vyenyewe.

SASA ENDELEA…

Pale kwenye sehemu ya kunywea, ndipo paliponipa picha kwamba nilichokunywa kilikuwa ni kitu gani. Minyoo mingi ya rangi mbalimbali, ilikuwa imechanganywa na maji machungu yenye harufu mbaya mno. Jambo lile, la kugundua kwamba nilikuwa nimekunywa minyoo, lilinifanya nisisimke sana, nilijaribu kujitapisha lakini ilikuwa sawa mna kazi bure.

Kwa jinsi minyoo yenyewe ilivyokuwa imechangamka, muda mfupi tu baadaye, nilisikia tumbo likianza kutibuka, hofu kubwa ikanitanda ndani ya moyo wangu. Sikujua nini itakuwa hatma yangu.

Yule babu alikichukuaa kibuyo na kukifunga, akakirudisha pale chini, nikamuona akichaguachagua na muda mfupi baadaye, alichukua kibuyu kingine lakini hiki kilikuwa kidogo kuliko kile cha awali. Akawatazama wale watu wengine waliokuwa wamekaa pembeni na kutulia kisha akawapa ishara fulani, nikaona wanaume wawili wakiinuka.

Wakatembea harakaharaka kusogea mpaka pale nilipokuwa nimekalishwa. Sikutaka kuyaamini macho yangu, ilibidi nijifikiche macho nikidhani labda nipo ndotoni.

Haikuwa ndoto, ilikuwa ni kweli kabisa. Mbele yangu walikuwa wamesimama baba na baba yake Rahma. Niliwatazama mmoja baada ya mwingine, bado nikawa siamini. Nao walikuwa wamevaa kama wale watu wengine, walijistiri kidogo tu lakini sehemu kubwa ya miili yao ilikuwa wazi.

Ni hapo ndipo nilipoielewa kauli ya baba yake Rahma aliyoitoa muda mfupi kabla ya yale mauzauza hayajanitokea, kwamba eti utii ni jambo muhimu sana na la lazima kwa jamii yao. Kumbe urafiki au ukaribu wa baba na baba yake rahma ulikuwa zaidi ya vile kila mmoja alivyokuwa akiamini.



Yule mzee alimtazama baba, baba naye akamtazama kisha kichwa chake akakiinamisha kwa utii, yule babu akawa anaongea kwa lugha ambayo hata sikuwa naielewa, baba naye akawa anamfuatisha anachokisema, muda mfupi baadaye baba yake Rahma naye alikuwa akifuatisha walichokuwa wanakisema.

Muda mfupi baadaye, walinizunguka na kutengeneza kama duara jingine hivi, wakawa wanaendelea kuzungumza yale maneno kwa sauti ya juu, muda mfupi baadaye wale watu wengine nao walidakia, wakawa wanawafuatisha. Ilivyoonesha, wote walikuwa wakiielewa vizuri lugha ile maana hakuna aliyekuwa akibabaika.

Baadaye, yule mzee alitoa ishara, watu wote wakanyamaza, akaanza kuzungumza lakini safari hii, alikuwa akiongea Kiswahili japo ilionesha hakuwa akikielewa vizuri. Akawaambia watu wote kwamba anayo furaha kubwa kukutana nao usiku huo na furaha yake iliongezwa zaidi na tukio lililokuwa likifanyika usiku huo.

Aliwaambia watu wote kwamba kulikuwa na utambulisho wa mwanachama mpya, akanitaka nisimame. Nilishtuka sana, mwanachama mpya? Wa nini? Ina maana kile ni chama? Kinahusika na nini? Sikuwa na majibu. Nilimgeukia baba, naye akanigeukia, akanipa ishara kwamba nitulie.

Yule babu alimkabidhi baba kile kibuyu, nikamuona akirudi tena pale palipokuwa na vifaa vingine, akachaguachagua kisha nikamuona akichukua kitambaa cheusi, au wengine wanapenda kuita kaniki. Alimpa baba, akainamisha kichwa chake kama ishara ya utii, kisha yule babu akaendelea kuzungumza na kila mtu.

Alisema hatua ya kwanza natakiwa kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kazi kisha baada ya hapo, nitatawazwa rasmi kuwa mwanachama kamili, watu wote wakalipuka kwa shangwe za kila namna. Zilikuwa ni kelele kubwa sana, kila mtu akionesha kuwa na furaha sana.

Baba aliniinamia, akaongea kwa sauti ya chini akiniambia nivue suruali niliyokuwa nimevaa maana mpaka muda huo nilikuwa kifua wazi. Niliona kama ni jambo lisilowezekana, yaani nivue nguo wakati watu wote wananitazama? Macho yakanitoka.



Ni kama baba alinielewa, alinipa na ile kaniki, akanionesha kwa ishara kwamba nijifunge juu ya suruali kisha ndiyo niiteremshe. Nilifanya hivyo, muda mfupi baadaye, nilikuwa nimeshaivua na kujifunga kaniki. Sasa na mimi nilikuwa nikifanana na wale watu isipokuwa mimi nilijifunga kaniki ndefu wakati wengine wote walikuwa wamejifunika kwa vipande vidogo.

Nilikalishwa chini, yule babu akampa ishara baba, akanisogelea na kupiga magoti, akanikabidhi kile kibuyu kilichokuwa kimevalishwa shanga, kisha akaongea kwa sauti ya chini akinitaka nisiogope chochote na nimthibitishie kwamba kweli nimekuwa mtu mzima na si mtoto kama alivyokuwa akiamini. Nilitingisha kichwa, japokuwa hakuwa ameniambia chochote, tayari nilishaelewa kilichokuwa kinaendelea.

Nilipokabidhiwa kile kibuyu, baba na baba yake Rahma waliondoka na kurudi kwenye sehemu zao, yule babu akaniambia nishike kibuyu hicho kwa mikono miwili kisha nikiinue mbele ya uso wangu.

Nilifanya kama alivyoniambia, nikamuona akichukua karai la chuma lenye maji meusi ndani yake, akanimwagia kichwani kisha kwa kutumia kisu kikali, alianza kuninyoa nywele. Sikuwahi kuona mtu akinyolewa nywele kwa siku, hata kule kijijini kwetu ambako saluni zilikuwa chache, tulikuwa tukinyolewa kwa wembe au mkasi.

Kwa kawaida nywele zangu huwa ni nguvu na wakati wa kunyoa huwa ni shughuli kwelikweli lakini huwezi kuamini, yule babu alipitisha mara kadhaa tu, kichwa kikawa cheupe kabisa. Alichukua dawa kutoka kwenye kichupa kimoja kisha akanisogelea, akarudia kunisisitiza kwamba sitakiwi kuachia kibuyu hicho kwani ndiyo maisha yangu.

Alichokifanya, kwa kutumia kilekile kisu, alianza kunichanja chake, kuanzia kichwani, akaja shingoni upande wa nyuma, akashuka mgongoni mpaka miguuni. Kiukweli maumivu niliyokuwa nayasikia yalikuwa makali sana, yote tisa, kumi ni pale alipoanza kunisugua sehemu alizonichanja kwa kutumia ile dawa iliyokuwa kwenye kile kichupa.

Maumivu ya kuchanjwa ukijumlisha na ukali wa ile dawa, nilishindwa kujizuia, nikawa nalia kwa maumivu.

“Kumbe hujakuwa mrume wewe,” alisema yule babu kwa Kiswahili kibovu lakini ambacho kilinifanya nimuelewe. Alimaanisha kwamba eti bado nilikuwa mtoto ndiyo maana nilikuwa nalia. Hakuna kitu ambacho nilikuwa nakichukia kama kuitwa mtoto. Japokuwa nilikuwa nikijisikia maumivu makali, ilibidi nijikaze, akaendelea kunisugua na ile dawa huku nikigugumia kwa maumivu.

Damu nyingi ilikuwa ikinitoka kwenye majeraha yangu lakini safari hii sikujali, sikutaka kuonekana mtoto, yule babu akaendelea mpaka alipomaliza. Baada ya kumaliza, alinishika mkono na kunisimamisha, akanisogeza kwenye ule moto.

Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe pale kulikuwa na nyama nyingi ya kutosha imewekwa pembeni ya moto. Yule babu aliinama pale kwenye nyama, akatoka na kipande kimoja, akanifuata na kunipa.

Kwa akili yangu nilielewa kwamba ananipa ili niichome kwenye moto ikiiva ndiyo niile, nikashangaa ananiambia eti niile vilevile ikiwa mbichi. Nilishtuka sana maana ilikuwa bado na damudamu kabisa.

Nilitamani kumuuliza kwanza ile ni nyama ya nini lakini nilikumbuka kauli ya baba yake rahma na aliyoniambia baba muda mfupi uliopita kwamba natakiwa kuwa mtiifu, ikabidi nifumbe macho, nikaitia mdomoni na kutaka kuimeza bila kutafuna lakini ilikuwa kubwa, ikabidi nipige moyo konde, nikaanza kuitafuna kisha harakaharaka nikameza.

“Twive umile,” alisema yule mzee huku akinionesha kwa ishara kwamba nifumbue mdomo. Sijui kile ni kilugha alichokuwa akizungumza, nilifanya kama alivyoniambia, nikafumbua mdomo. Nadhani alitaka kuhakikisha kama nimemeza, alipohakikisha, alinishika mkono na kuuinua juu kama wanavyofanya waamuzi wa mapambano ya ndondi wanapomtangaza msshi ulingoni.

Watu wote walishangilia kwa nguvu, wengine nikawaona wakirukaruka kwa furaha, ikabidi na mimi nifurahi ingawa bado nilikuwa gizani. Yule mzee aliniachia mkono na kuanza kuzungumza na wale watu, akiwataka wanipe ushirikiano na kunifundisha yale nisiyoyajua.

Wakati anaongea hayo, sijui nini kilinituma nitazame pale zilipokuwepo zile nyama, nikashtuka kuliko kawaida kuona kuna viungo vya binadamu, viganja vya mikono na miguu. Ile nyama aliyonipa aliichukua palepale, kwa hiyo alikuwa amenipa nyama ya mtu? Macho yalinitoka nikiwa siamini macho yangu.

Nikiwa bado nashangaa, mwili ukiwa unatetemeka kwa hofu, nilishtukia wale watu wakikimbilia pale kwenye moto na kujipanga foleni, yule babu akasogea kwenye zile nyama, akawa anagawa, kila mmoja anapita na kupewa kipande chake kisha anatafuta sehemu ya kwenda kukaa na kuanza kula. Nilihisi kama nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo.

“Hongera, umekuwa sasa,” alisema baba huku akinikumbatia, akanishika mkono na kunipeleka kwenye foleni, akaniingiza kwenye foleni.

Je, nini kitafuatia?
Togo ashakuwa mwanga duh.Tusali ndio tulale mtu kahama kambi[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Sehemu ya 41



ILIPOISHIA:

Nikiwa bado nashangaa, mwili ukiwa unatetemeka kwa hofu, nilishtukia wale watu wakikimbilia pale kwenye moto na kujipanga foleni, yule babu akasogea kwenye zile nyama, akawa anagawa, kila mmoja anapita na kupewa kipande chake kisha anatafuta sehemu ya kwenda kukaa na kuanza kula. Nilihisi kama nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo.

“Hongera, umekuwa sasa,” alisema baba huku akinikumbatia, akanishika mkono na kunipeleka kwenye foleni, akaniingiza kwenye foleni.

SASA ENDELEA…

“Hapana baba, siwezi! Siwezi…” nilisema huku nikitaka kutoka kwenye foleni lakini baba alinishika mkono kwa nguvu. Nilikuwa natafuta upenyo ili nijitie vidole mdomoni kujitapisha ile nyama lakini ni kama baba alinishtukia.

Hakunipa upenyo hata kidogo, nikawa naendelea kutetemeka kwa hofu kubwa, nikiwa sielewi hatima ya yote yale itakuwa nini. Tofauti na mimi, watu wengine wote waliokuwepo eneo lile, akiwemo baba, baba yake Rahma na wale watu wengine wote, walikuwa na furaha kubwa ndani ya mioyo yao.

Kingine kilichonishangaza na kuniacha na maswali mengi, kila mtu aliyekuwa akifika pale mbele kwa yule babu aliyekuwa akigawa nyama, akikabidhiwa yake alikuwa akifurahi sana na kwenda kukaa pembeni na kuanza kuila bila wasiwasi wowote.

Nimewahi kusikia sana kuhusu stori za watu wanaokula nyama za watu lakini siku zote nilikuwa naona kama ni mambo ya kutunga, iweje mtu amle mwenzake? Ni hapo ndipo nilipoelewa kwamba kumbe siyo stori za kusadikika tu bali ni mambo ambayo yapo na yanafanyika kwa wingi.

Nilijiuliza sana, wale waliokuwa wakiliwa nyama ni akina nani? Walifanya makosa gani mpaka waliwe? Walikuwa wanaishi wapi na nyama zao zilifikishwaje pale? Je, walikuwa wanaume au wanawake, wakubwa au wadogo? Sikuwa na majibu.

Foleni ikawa ikazidi kusogea mbele, mwili wangu ulikuwa na maumivu sehemu mbalimbali, hasa yale maeneo ambayo yule babu alikuwa amenichanja lakini huwezi amini, kwa jinsi nilivyokuwa na hofu, wala sikuwa nasikia chochote.

Foleni iliendelea kusogea mbele, hofu ikazidi kunijaa lakini sikuwa na cha kufanya. Mara nilipata wazo, kwamba nikifika na kupewa nyama yangu, nijifanye naenda pembeni kuila lakini nikifika pembeni niitupe na tukirudi nyumbani, nitoroke na kurudi Chunya maana sikuwa tayari kwa kile kilichokuwa mbele yangu.

>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Ni kweli mara kadhaa nilijikuta nikitamani kuzijua mbinu mbalimbali za kichawi, kama kuweza kujilinda kwenye nyakati za hatari au kumuadhibu anayekuudhi lakini sikuwa tayari kuona nakuwa sehemu ya jamii hiyo iliyokuwa na mambo ya kutisha kiasi hicho.

Hatimaye zamu yangu iliwadia, yule mzee mgawaji, huku akijitafuna na damudamu zikiwa zimelowanisha mdomo wake, alinitazama usoni huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.

Kuna kipande alikuwa amekishika mkononi lakini alipoona ni mimi, nilimuona akikirudisha pale chini palipokuwa na nyama nyingine nyingi, zikiwa zimewekwa juu ya majani ya migomba, akachaguachagua na muda mfupi baadaye, aliibuka na mnofu mkubwa wenye damudamu, akanipa huku akiinamisha kichwa kama ishara ya heshima.

Huku nikitetemeka nilipokea, macho yangu yakiwa hayatulii, nilikuwa nikilichunguza kwa umakini lile rundo la nyama pale chini ambalo sasa lilikuwa limepungua sana. Nilichokiona awali ndicho nilichokiona tena, kulikuwa na miguu iliyokatwa, viganja vya mikono na viungo vingine vya mwili.

Nikiri kwamba moyo wangu haujawahi kupatwa na hofu kama niliyoipata siku hiyo na kilichonitisha zaidi, ni pale nilipogundua kwamba katika rundo lile, kulikuwa na miguu na mikono ya watoto wadogo kabisa. Maskini… hawakuwa na hatia yoyote!

Baba naye alipewa kipande chake, akanishika mkono huku akiniongelesha kwa sauti ya chini. Aliniambia kwamba nina bahati sana kupewa heshima kubwa kama hiyo na mzee huyo ambaye baba aliniambia huwa wanamuita Mkuu kwa sababu ndiye kiongozi wao wa kanda. Akaniambia kwamba kitendo cha yeye kuinamisha kichwa chake tu, ilikuwa ni ishara kwamba amenikubali mno.

Hatukwenda mbali, tulikaa chini huku baba akinielekeza namna ya kukaa. Haukuwa ukaaji wa kawaida, mguu wa kushoto ulikuwa ukitangulia chini, kisha unakuja wa kulia halafu unakaa juu ya vifundo vya miguu yote miwili huku ukiwa umeikunja na kutengeneza alama ya V mbili.

Nilijaribu lakini miguu ikawa inaniuma sana, nilipowatazama watu wengine, wote walikuwa wamekaa kwa mtindo huo na wala hakukuwa na aliyekuwa akibabaika kama mimi, walikuwa wakiendelea kupiga stori za hapa na pale huku wakifurahia ‘kitoweo’, baba akaniambia atanifundisha taratibu.

Lile wazo langu la kwenda kuitupa ile nyama liliyeyuka kutokana na baba alivyonibana, ambapo muda mfupi baadaye, baba yake Rahma naye alikuja na kuungana na sisi pamoja na wanaume wengine watatu ambao sikuwa nawafahamu.

Kwa muda wote huo nilikuwa nikizugazuga tu kwani kiukweli sikuwa tayari kuila ile nyama ambayo ilikuwa ikichuruzika damu, mara kwa mara nilikuwa nikiitazama kwa woga, nikitamani hata niirushe mbali na kupiga kelele kwa hofu lakini haikuwezekana.

“Kula, muda unaenda,” baba aliniambia kwa kunihimiza, wale watu wengine ambao sikuwa nawafahamu, wakawa wanamuuliza baba mimi ni nani.

“Ni mwanangu, hamuoni tunavyofanana,” aliwajibu na wote wakawa wanampongeza kwa hatua ya kunisajili rasmi, wakawa wananipongeza na mimi wakiniambia kwamba sitajuta kujiunga na jamii yao. Kwa kuwa wote sasa walikuwa wakinitazama huku wakiendelea kunisifia, ilibidi nijikaze kiume maana baba alikuwa akinitazama kwa jicho kama la kunidharau hivi au kuonesha kwamba zile sifa nilizokuwa napewa sistahili.

>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Umekua sasa si ndiyo?” baba yake Rahma aliniambia huku akinipigapiga begani na mkono wake uliokuwa na damu, mdomoni akiendelea kujitafuna. Nadhani aliongea hivyo kama kunikumbusha kile tulichokuwa tukitofautiana mara kwa mara na baba, akidai kwamba mimi bado nina akili za kitoto.

“Ndiyo,” nilimjibu kwa msisitizo, nikafumba macho na kupeleka ule mnofu mdomoni, nikaziba pua ili nisisikie hata harufu nikaanza kutafuna huku nikijikaza kisawasawa, sikuwa nataka kuonekana bado nina akili za kitoto kwa hiyo nilijikuta nikifanya kitu nisichopenda kukifanya ilimradi tu nimdhihirishie baba na baba yake Rahma kwamba sikuwa mtoto tena.

Mara kadhaa nilikuwa nikitaka kutapika lakini mwisho, hatimaye nilifanikiwa kuitia yote tumboni mwangu na kuufanya mwili wangu usisimke sana.

“Tafuna hii,” alisema baba yake Rahma huku akinipa vitu kama mizizi fulani hivi, nikavitafuna haraka na kuvimeza. Cha ajabu, mpaka muda huo, kumbe mimi ndiye niliyekuwa wa mwisho kumaliza ‘shea’ yangu, watu wote walikuwa wameshamaliza na sasa walikuwa wakipiga stori za hapa na pale.

“Vipi una swali lolote kwa kijana?” baba yake Rahma alimwambia baba kwa kejeli, nilishaelewa kwa nini amesema vile. Kwamba kwa sababu baba alikuwa ananiona kama nina akili za kitoto, je alikuwa na swali lingine lolote baada ya mimi kuonesha kile nilichokionesha pale mbele yao?

“Umenitoa aibu mwanangu, zawadi nitakayokupa hautakuja kuisahau maishani mwako,” aliniambia baba akionesha kuwa na furaha kubwa.

Mara sauti ya kama pembe la ng’ombe lililopulizwa kwa nguvu ilisikika, watu wote wakainuka walipokuwa wamekaa na kuanza kujipanga kwa mtindo wa duara kama ilivyokuwa mwanzo.

“Sasa hivi unaenda kukabidhiwa rasmi nguvu za giza ili uwe kama sisi, naomba ujasiri uliouonesha kwenye kula uuoneshe hapa pia, nenda pale ulipokuwa umekaa mwanzo,” baba aliniambia huku akinipigapiga begani kwa upole.

Kwa akili yangu nilijua kwamba tayari kazi imekwisha, kumbe kulikuwa na kazi nyingine, nikaanza kutetemeka tena huku nikigeuka huku na kule kuwatazama wale watu ambao wote walikuwa na nyuso za furaha. Nilipogeuka upande wa kushoto, nilimuona mtu aliyenifanya nishtuke mno, nilifikicha macho nikiwa ni kama siamini.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 42




ILIPOISHIA:

Kwa akili yangu nilijua kwamba tayari kazi imekwisha, kumbe kulikuwa na kazi nyingine, nikaanza kutetemeka tena huku nikigeuka huku na kule kuwatazama wale watu ambao wote walikuwa na nyuso za furaha. Nilipogeuka upande wa kushoto, nilimuona mtu aliyenifanya nishtuke mno, nilifikicha macho nikiwa ni kama siamini.

SASA ENDELEA…

Alikuwa na Isrina, naye akiwa amevaa kama wale watu wengine wote waliokuwepo eneo lile. Alikuwa ametulia akinitazama kwa makini, ilionesha kwamba kumbe naye muda wote wakati yale mambo yakiendelea alikuwepo na alikuwa akinifuatilia hatua kwa hatua.

Nilishtuka kupita kiasi, nikageuka na kumtazama baba, naye akanitazama huku akitingisha kichwa kama ishara ya kuniambia ninachokiona ni kweli. Ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini mara kwa mara baba alikuwa akinikanya kuwa karibu na msichana huyo huku akiniuliza mara kwa mara kama najua ana malengo gani na mimi.

Nilijikuta kama kichwa kikiwa kizito, kwa tafsiri nyepesi, Isrina au Isri kama mwenyewe alivyokuwa akipenda kuitwa, alikuwa akifahamiana vizuri na baba kwa sababu wote walikuwa jamii moja. Bado sikutaka kuamini kama Isrina naye anahusika na hayo mambo, nilijaribu kuvuta kumbukumbu ya siku niliyokutana naye kwa mara ya kwanza.

Bado sikuwa na majibu ilikuwaje mpaka tukapanda basi moja, ilivyoonesha ni kama kukutana kwetu hakukuwa bahati mbaya bali ni jambo ambalo lilipangwa. Sasa kama anafahamiana na baba, kwa nini hataki kabisa niwe karibu naye? Kwa nini anamchukia? Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.

Nikiwa bado naendelea kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu, yule babu ambaye baba aliniambia anaitwa Mkuu, alinishika mkono baada ya kuona nimepigwa na butwaa. Licha ya uzee wake na mwili wake kuchoka, Mkuu alikuwa na nguvu kwelikweli, akanivutia kwake na kuanza kutembea na mimi kuelekea pale katikati nilipokuwa nimelazwa kwa mara ya kwanza.

Mara nilishtuka kuona wanaume wanne, wakitoka kule pembeni na kusogea mpaka pale tulipokuwa, wakiwa wamebeba jeneza. Sikuelewa lile jeneza ni la nini lakini kwa jinsi walivyolibeba, ilionesha kama lipo tupu.

>> Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Walilisogeza mpaka pale jirani na kuliweka chini, wakasimama wakiwa ni kama wanasubiri maagizo kutoka kwa Mkuu huku wote wakinitazama. Niligeuka na kumtazama baba, akawa ni kama ananipa ishara kwamba nisiogope, nikageuka na kumtazama Isri, bado alikuwa amenikazia macho muda wote, nikashusha pumzi ndefu na kumgeukia Mkuu.

Alitoa kichupa kutoka kwenye mkoba wake wa ngozi aliokuwa ameuvaa kiunoni, akakitingisha kisha akakifungua na kunipa ishara kwamba ninuse kilichokuwemo ndani. Nilipofanya hivyo tu, nilianza kupiga chafya mfululizo kutokana na ukali wa ile dawa iliyokuwa mle ndani ya kichupa.

Nikapiga chafya zisizo na idadi, mara nikaanza kuhisi kizunguzungu kikali, nikawa napepesuka, wale wanaume wakanishika ili nisianguke, Mkuu akanisogelea pale nilipokuwa nimeshikwa, akaninusisha tena na safari hii, hakukitoa haraka kile kichupa puani, nikaendelea kupiga chafya nyingi, mwisho giza nene likatanda kwenye uso wangu na mwili wote ukawa ni kama umekufa ganzi.

Licha ya hali hiyo, bado nilikuwa naweza kuelewa kinachoendelea ingawa sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, nikasikia wakinilaza chini kisha lile jeneza likagongwagongwa na kitu kizito, nadhani walikuwa wakilifungua.

Nikiwa bado sielewi hatma yangu, nilishtukia wakininyanyua na kunilaza ndani ya jeneza. Sikuwa hata na uwezo wa kufumbua macho ingawa bado nilikuwa na fahamu zangu. Baada ya hapo, nilisikia tena jeneza likigongwagongwa juu yangu, nikajua mimi ndiyo nimewekwa kwenye jeneza.

Mara nilisikia tena lile pembe la ng’ombe likipulizwa kisha Mkuu akapaza sauti na kutamka haraka maneno ambayo sikuyaelewa, wale watu wengine wakaanza kuimba nyimbo kama za maombolezo, nikahisi lile jeneza nililowekwa ndani yake likinyanyuliwa na waliolibeba wakaanza kutembea.

Ilikuwa ni kama nipo kwenye ndoto lakini tofauti yake ni kwamba nilikuwa najielewa. Wale watu waliendelea kuimba huku nao wakionesha kuwafuata wale walionibeba kwenye jeneza. Wakatembea umbali fulani kisha nikahisi jeneza likishushwa chini huku wale watu wakiendelea kuimba.

Nikiwa sielewi nini hatima yangu, nilihisi kama jeneza linahamishwa tena na safari hii, lilikuwa kama linaingizwa kwenye shimo, mara nikashtukia vitu vizito vikianza kuangushiwa juu ya jeneza.

>> Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Kwa jinsi vilivyokuwa vikidondoka kwa vishindo, nilielewa moja kwa moja kwamba ulikuwa ni udongo, nikajiuliza ina maana wamenipeleka makaburini? Ina maana wananizika nikiwa hai? Sikupata majibu.

Vile vishindo viliendelea na muda mfupi baadaye, zile sauti za watu waliokuwa wakiimba nazo zilianza kufifia na baadaye zikatoweka kabisa, ukimya mkubwa ukiwa umetanda kila sehemu. Sikuelewa tena kilichoendelea kwani hata zile fahamu zangu, sasa zilinitoka kabisa.

Nilipokuja kushtuka, ilikuwa tayari kumepambazuka na licha ya yote yaliyotokea, nilijikuta nikiwa kwenye chumba changu, nikiwa nimelala kitandani, mwili wangu ukiwa hauna nguvu kabisa.

“Vipi unajisikiaje?” sauti ya baba ilinishtua, nikageuza shingo na kumtazama, alikuwa amekaa pembeni yangu, mkononi akiwa na bakuli la uji. Hata nguvu za kumjibu sikuwa nazo, pembeni pia alikuwepo baba yake Rahma ambaye uso wake ulikuwa na furaha.

Walisaidiana kuniinua kidogo upande wa shingoni, wakaniwekea mto na baba akaanza kuninywesha ule uji.

“Jitahidi kunywa ili upate nguvu,” alisema baba, nikajilazimisha hivyohivyo, kweli nikamaliza lile bakuli maana ni kweli tumbo nalo lilikuwa tupu kabisa.

“Inabidi uendelee kupumzika, leo hutakiwi kufanya shughuli yoyote mpaka utakapopewa maagizo na Mkuu,” aliniambia baba, nikatingisha kichwa kuashiria kukubaliana na alichokisema ingawa sikuelewa huyo Mkuu atanipaje hayo maagizo. Yaani nilivyokuwa nikijisikia, ni kama mtu aliyeumwa kwa kipindi kirefu sana na kusababisha mwili uishiwe nguvu kabisa kiasi cha kushindwa hata kujigeuza pale kitandani.

Waliinuka na kutoka, mimi nikapitiwa tena na usingizi mzito. Nikiwa usingizini, nilianza kuota ndoto ya kutisha, nilijiona nipo kulekule porini lakini tofauti na mara ya kwanza, safari hii tulikuwa tumebaki wawili tu, mimi na Mkuu. Akawa ananiambia ili nguvu zangu nilizopewa zianze kufanya kazi, ni lazima nitoe kafara na kafara hilo ndiyo utakuwa mtihani wangu wa kwanza.

Aliniambia kwamba wachawi wote, sifa ya kwanza ni lazima wawe na uwezo kuua na kwamba kadiri mtu anavyoua watu wengi zaidi ndivyo anavyopanda ngazi. Alisema maneno hayo kwa msisitizo kisha baada ya kumaliza, alicheka kicheko cha nguvu kilichokuwa kinasikika kama mwangwi kisha akayeyuka.

Kwa jinsi ndoto ile ilivyokuwa inatisha nilijikuta nikishtuka, kutazama nje bado ilikuwa mchana, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio kuliko kawaida. Kumbe pale wakati nashtuka, nilipiga kelele zilizomfanya baba na baba yake Rahma waje haraka kule chumbani kwangu.

Cha ajabu, nilipowahadithia nilichoota, hakuna aliyeonesha kushtuka, sanasana baba akapigilia msumari kwa kusema kwamba ile haikuwa ndoto bali ni Mkuu alikuwa akiwasiliana na mimi.

“Baba!” nilisema kwa mshtuko nikiwa bado palepale kitandani.

“Nini sasa.”

“Mimi niue mtu?” nilipotamka maneno hayo, baba alinionesha ishara kwamba nisipige kelele, wote wakanisogelea pale kitandani na kuniambia kwa sauti ya chini kwamba Mkuu akishatoa maagizo kwa mtu, kinachofuatia huwa ni utekelezaji tu na endapo mtu akishindwa kutekeleza alichoambiwa, anakufa yeye. Nilishtuka mno, nikamtazama baba, nikamtazama baba yake Rahma, wote walionesha kumaanisha kile walichokisema.

“Hapana! Hapanaaa,” nilisema kwa sauti ya juu, ikabidi baba anizibe mdomo maana alihisi naweza kuropoka mambo mengine na kuwafanya wasiohusika wajue.

“Huna haja ya kuogopa, zipo njia za kutimiza hicho ulichoambiwa bila kuonekana kama wewe ndiyo umefanya moja kwa moja, mbona sisi huwa tunafanya sana tu” alisema baba, macho yakanitoka.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya ishirini na sita______26




ILIPOISHIA:

Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.

SASA ENDELEA…

Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.

Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”

Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”

“Sasa baba, unajua mimi kuna mambo mengi sana sielewi, halafu nikikuuliza hata hunipi majibu ya kuridhisha.”

“Hilo siyo jibu, umeanza kuwa na kiburi,” alisema baba kwa sauti ya chini lakini akionesha kama alikuwa amepania kuniadhibu. Sikumjibu chochote, akauma meno kwa hasira na kuelekea pale alipokuwa amesimama baba yake rahma, wakawa wanazungumza jambo. Nadhani walikuwa wananijadili.

Kiukweli, uhusiano wangu na baba ulikuwa umeingia doa kubwa na sababu ya yote, ni mambo ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea ambayo yeye alionesha kwamba anajua kila kitu na pengine ndiyo chanzo cha yote. Bado nilikuwa na maswali mengi ambayo alipaswa kunijibu.

Swali la kwanza, nilitaka aniambie kwa nini wanakijiji wenzake kule kijijini kwetu, Chunya walikuwa wakimtuhumu kwamba ni mchawi na ndiye aliyeshiriki kwenye vifo vya watu wawili katika mazingira ya kutatanisha. Kwa macho yangu nilishuhudia akipambana na watu hao kabla ya baadaye kubainika kwamba wamekufa vifo vya ghafla.

Nilitaka aniambie ukweli, yeye ni mganga kama mwenyewe alivyokuwa akijinadi au alikuwa ni mchawi? Nilitaka pia anieleze, aliwezaje kusafiri kutoka Chunya mpaka Dar es Salaam bila kuwemo kwenye basi tulilokuwa tumepanda lakini muda wote akawa anatoke apale panapotokea tatizo, kama alivyotusaidia kuepukana na ajali mbaya zilizotaka kutokea wakati tukisafiri kutoka Chunya kuja Dar, ya kwanza ikiwa ni kwenye eneo hatari la Mlima Nyoka na la pili likiwa ni kwenye Mlima Kitonga.

Nilitaka anieleze vizuri aliwezaje kuniokoa nisigongwe na gari, lakini wakati huohuo watu wengine wote wakawa hawamuoni wala kumsikia zaidi yangu. Nilitaka aniambie, ile dawa aliyonipa niwe namnyunyizia dereva, ilikuwa na maana gani na iliwezaje kutuepusha na ajali?

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Nataka kujua nini kimetokea hapa kwa akina Rahma maana nasikia kabla sisi hatujafika walikuwa wakiishi kwa amani, mbona tangu tuingie, japo ni muda mfupi tu lakini tayari kuna mambo mengi ya ajabu yametokea? Kwa nini naona mambo ambayo watu wengine hawayaoni?”

“Mbona unaongea peke yako Togo?” sauti ya Rahma ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo machungu, nikashtuka sana kugundua kwamba kumbe nilikuwa nikizungumza kwa sauti huku mwenyewe nikidhani nawaza.

“Umesikia nini kwani?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana. Kwa bahati nzuri, kumbe sikuwa nimetamka kwa sauti mambo mengi zaidi ya kujiuliza kwa nini tangu tufike nyumbani kwa akina Rahma mambo mengi ya ajabu yalikuwa yakitokea.

“Kwani unafikiri ujio wenu ndiyo chanzo cha haya yote?” aliniuliza Rahma kwa upole huku akinishika mkono na kunielekeza tuelekee ndani maana nilikuwa nimesimama, nikiwa nimepoteza kabisa mwelekeo.

“Sisi ndiyo chanzo na pengine mimi ndiyo chanzo hasa,” nilisema kwa sauti ya unyonge, Rahma akaniambia kuna jambo zuri anataka tukazungumze chumbani kwake. Nilimkubalia, tulipoingia ndani tulipitiliza mpaka chumbani kwake.

Akina mama ilibidi waanze kuchakarika kwa sababu hata chakula cha usiku hakikuwa kimepikwa siku hiyo kwa sababu ya majanga yaliyonitokea ambapo baada ya kupata taarifa kwamba nipo hospitali nikiwa sijitambui, ilibidi nyumba nzima ije kunijulia hali. Waliingia jikoni huku ndugu zangu na wadogo zake Rahma wakikaa sebuleni kutazama runinga.

Baba na baba Rahma, kama kawaida yao wao walibaki nje wakiendelea na mazungumzo yao.

“Unataka kuniambia nini Rahma,” nilimuuliza kwa upole baada ya kumuona akifunga mlango wa chumbani kwake kwa komeo. Hakujibu kitu zaidi ya kuvua blauzi yake kisha ‘bra’, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, nilijikuta nikisisimka mno. Rahma alikuwa amejaliwa kifua kizuri mno, ambacho kwa mwanaume yeyote aliyekamilika, ilikuwa ni lazima atokwe na udenda kama fisi aliyeona mfupa.

Rahma aliendelea kunikumbatia huku akinibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu kimahaba, hali ambayo ilinichanganya kabisa kichwa changu. Taratibu alinirudisha nyuma mpaka tulipofika kwenye uwanja wa fundi seremala, akanisukumia juu yake kisha akamalizia na za chini zilizokuwa zimesalia.

Akionesha kuwa na papara za hali ya juu, alihamia kwangu na kuitoa ya juu, nikabaki kifua wazi, akahamia na ile ya chini na muda mfupi baadaye, tulikuwa ‘saresare’ maua. Bado mwili wangu haukuwa na nguvu kwa hiyo nilimuachia yeye ndiye awe ‘dairekta’ wa filamu ile ya kusisimua na kweli alikitendea haki cheo nilichompa.

Kwa ufanisi wa hali ya juu, Rahma aliitii kiu yangu, mpaka anashuka kutoka juu ya mnazi, alikuwa ameshaangua madafu kadhaa, akajitupa upande wa pili huku akinishukuru, na mimi nikawa namshukuru. Hatukuchukua raundi, kila mmoja akapitiwa na usingizi mzito.

Nadhani wangu ulikuwa mzito zaidi kwa sababu kuichwa changu kilikuwa kimebeba mambo mazito mno na alichonipa rahma ilikuwa sawa na dawa ya usingizi. Tulikuja kushtuka baadaye baada ya kusikia mlango wa chumba cha Rahma ukigongwa. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikamuamsha Rahma ambaye aliamka kichovu na kusogea karibu na mlango.

Safari hii hatukuwa na hofu tena kwani tulikuwa na ruhusa ya kukaa pamoja karibu, mimi kazi yangu ikiwa ni kuhakikisha rahma harudii tena kujaribu kuyakatisha maisha yake na Rahma kuhakikisha ananisaidia mimi mgonjwa.

“Unasemaje?”

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Mama anauliza kama mtakula na sisi au mletewe chakula chenu huku.”

‘Ngoja nakuja mwenyewe,” alijibu Rahma wakati akizungumza na mdogo wake aliyetumwa na mama yao kuwaulizia.

‘Eti mpenzi wangu, we unapenda tukakae sebuleni au tulie hukuhuku chumbani.”

‘Utakavbyosema wewe hamna shida ila napenda zaidi tukikaa peke yetu,” nilimjibu, akanitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yameelemewa na usingizi kisha akaachia tabasamu la kichovu.

“Ngoja nikaonge kwanza,” alisema na kuchukua kitenge, akaelekea bafuni na muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amechangamka kidogo. Ilibidi na mimi niende kuoga wakati yeye akihangaikia chakula.

Niliporudi kutoka bafuni, tayari rahma alikuwa ameleta chakula kizuri kule chumbani. Tofauti ya vyakula tulivyozoea kula kijijini na mjini ilikuwa kubwa mno. Chakula kilipikwa vizuri, yaani kwa kukitazama tu ilikuwa ni lazima mate yakutoke. Tulinawa vizuri lakini nilipotaka kuanza kula, Rahma alinikatazana na kusema anataka anilishe kidogo.

Yalikuwa ni mambo mageni kabisa, nilizoea kuona watoto wadogo au wagonjwa ambao wako mahtuti ndiyo wanalishwa, lakini eti dume mimi nilishwe? Hata hivyo sikumkatalia. Akaanza kunilisha kwa upole, huku mara kwa mara akinitazama machoni. Sijui nini kilimtokea Rahma lakini alionesha kunipenda sana, tena sana.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Mara kwa mara alikuwa akinibusu na kuniambia kwamba ananipenda sana, mpaka nikawa najisikia aibu. Sikuwa najua kabisa mambo ya kikubwa na wala sikuwa na uelewa wowote wa mahaba. Nilikuwa nikisikiasikia kwamba watu wa pwani ndiyo wataalamu wa hayo mambo.

Japo Rahma alikuwa akinilisha matonge madogo tofauti na niliyozoea lakini kiukweli nikiri kwamba nilijisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu. Tulipomaliza kula, alitoa vyombo, akaja kufanya usafi kisha akafunga tena mlango.

“Itabidi mimi nikalale chumbani kwangu,” nilimwambia Rahma lakini akakataa katakata, akaniambia tutalala wote humo chumbani kwake na tutajifunika shuka moja. Japokuwa kwa nje nilikuwa navunga, ukweli ni kwamba hata mimi nilikuwa napenda sana kuwa karibu na Rahma hasa kutokana na mapenzi ya dhati aliyokuwa ananionesha.

Ile tofauti ya umri kati yetu sikuiona tena, namimi nikawa najiona mkubwa kama yeye, hata ile harufu ya undugu kati yetu nayo ilitoweka kabisa, ndani ya muda mfupi tu tuliokaa pamoja ikawa utafikiri tumeishi pamoja kwa miaka mingi tangu zamani.

Tulipiga stori za hapa na pale, baadaye muda wa kulala ulipofika, kama ilivyokuwa mara ya kwanza, Rahma aliniganda kama ruba, tukapeana tende na halua kwa mara nyingine kabla ya kupitiwa na usingizi mzito, akiwa ameniganda kifuani kama ruba.

Nilikuja kuzinduka usiku wa manane baada ya kuhisi hali isiyo ya kawaida. Kilichoniamsha, zilikuwa ni kelele za paka waliokuwa wakipigana juu ya paa, huku wakitoa milio ya ajabu kama watoto wachanga.

Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.

Je, nini kitafuatia?
Daah Rahma ananyanduliwa balaa aisee
 
Sehemu ya 43




ILIPOISHIA:

“Hapana! Hapanaaa,” nilisema kwa sauti ya juu, ikabidi baba anizibe mdomo maana alihisi naweza kuropoka mambo mengine na kuwafanya wasiohusika wajue.

“Huna haja ya kuogopa, zipo njia za kutimiza hicho ulichoambiwa bila kuonekana kama wewe ndiyo umefanya moja kwa moja, mbona sisi huwa tunafanya sana tu,” alisema baba, macho yakanitoka.

SASA ENDELEA…

Aliondoa mkono wake mdomoni mwangu, akaniambia wameniamini ndiyo maana wameniunganisha kwenye jamii yao, akaniambia faida nitakazozipata ni nyingi na kubwa sana kwa hiyo sina sababu ya kuogopa kutimiza sharti lile dogo nililopewa.

“Sijawahi kuua mtu hata siku moja, nitaanzaje,” nilisema, baba akatabasamu na kumgeukia baba yake Rahma, wakacheka na kugongesheana mikono. Sikuelewa kwa nini wao wacheke wakati mimi nilikuwa kwenye hali mbaya kiasi hicho, hofu kubwa ikiwa imetanda kwenye moyo wangu.

“Unatakiwa ujue namna ya kudhibiti hofu yako, ukiwa mwoga hivi huwezi kufanya chochote,” alisema baba, baba yake Rahma akamuunga mkono, wakawa wananieleza kwamba mtihani niliopewa ni mdogo sana na endapo nitashindwa nitakuwa nimewaangusha sana na kila mtu atanicheka.

“Utathibitisha kwamba kauli yangu niliyoitoa juu yako ni sahihi.”

“Kauli gani?”

>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Kwamba wewe bado una akili za kitoto,” baba alisema. Hakuna kitu nilichokuwa sikipendi kama kusikia kauli za namna hiyo kutoka kwa baba, nikajikuta morali fulani ukinipanda ndani kwa ndani, nikajisemea kwamba nitamuonesha kwa vitendo kama mimi siyo mtoto.

“Endelea kupumzika mpaka mwili upate nguvu, tutakuja baadaye kukuelekeza nini cha kufanya,” alisema baba, wakatoka na kuniacha nimelala palepale kitandani. Kwa nje nilisikia wakifunga mlango kwa funguo, nikabaki nashangaa kwa nini wananifungia?

Sikuwaza sana kuhusu hilo la mlango, bado nilikuwa na mawazo mengi juu ya hatma yangu na ile kazi niliyokuwa nimepewa. Sikuwahi kudhani hata siku kwamba eti na mimi naweza kuwemo kwenye orodha ya wachawi, tena wanaoua na kula nyama za watu wasio na hatia.

Ni kweli kuna kipindi nilikuwa nikitamani kuwa na nguvu kama za baba lakini nilichokuwa nikikijua ni kwamba nguvu zake zilikuwa ni za kutibu watu na kufanya yale yasiyowezekana tu, sikujua kuwa gharama zake ni kubwa kiasi hicho.

Sikupata jibu mtihani mkubwa uliokuwa mbele yangu ningeuvuka vipi, sikujua ni kwa kiasi gani moyo wangu utakuwa na hatia kwa kuyakatisha maisha ya mtu asiye na hatia. Kuna wakati nilikuwa nikitamani kama nitoroke na kuelekea kusikojulikana lakini kila nilipokuwa nikifikiria vile vitisho nilivyokuwa napewa, nilijikuta nikikosa ujanja.

Nilipokumbuka na kauli za baba za kunidharau, nilijikuta nikizidi kuchanganyikiwa, sikuelewa nini itakuwa hatma yangu. Basi niliendelea kuwaza na kuwazua pale kitandani, mwili ukaanza kupata nguvu taratibu, saa zikawa zinazidi kuyoyoma.

Mida ya jioni baba alikuja tena, akafungua mlango na kuingia akiwa na bakuli lililokuwa na supu ya kuku wa kienyeji. Akaniwekea vizuri na kuniambia niinuke mwenyewe pale kitandani. Kwa kuwa safari hii nilikuwa na nguvu, niliinuka mwenyewe na kukaa kitako.

Akanisogezea lile bakuli na kunipa. Nililipokea huku mikono ikitetemeka, nikaanza kuinywa supu ile kwa pupa. Muda mfupi tu baadaye, bakuli lilikuwa tupu. Ile njaa niliyokuwa nayo sasa ilikuwa imepungua na nilijihisi kuwa na nguvu kama zamani.

“Hebu jaribu kusimama mwenyewe,” baba aliniambia wakati akikusanya mifupa na kuiweka kwenye lile bakuli, nikajishikilia kwenye kingo za kitanda na kusimama. Bado miguu haikuwa na nguvu vizuri lakini niliweza kusimama, akaniambia nizunguke mle ndani, kweli nikaweza.

“Safi sana, sasa umekuwa mwanaume kamili,” aliniambia huku akinielekeza kuendelea kupumzika mpaka usiku. Nilirudi kitandani na kujilaza, kidogo nikawa najisikia vizuri, baba akatoka na kufunga tena mlango kwa ndani.

Kiukweli nilikuwa nimemkumbuka sana Rahma, sikujua anawaza nini juu yangu maana siyo kawaida tukae wote nyumba moja halafu tusionane siku nzima. Nilitamani japo nipate muda mfupi wa kuonana naye, nimweleze kinachonitokea maishani mwangu maana angeweza kuhisi kama labda simpendi tena na ndiyo maana nimebadilika.

Muda ulizidi kuyoyoma na hatimaye giza likaingia, mara nikasikia mlango ukifunguliwa. Walikua ni baba na baba yake Rahma, waliingia na kuwasha taa, wakanisogelea mpaka pale kitandani.

“Vipi unaendeleaje?”

“Naendelea vizuri.”

“Safi, sasa inatakiwa tuondoke kuna mahali tunaenda kukuonesha sehemu tunapochimba dawa zetu za kufanyia kazi,” baba aliniambia, nikainuka na kukaa vizuri.

“Kwa mfano hiyo kazi uliyopewa, huwezi kuifanikisha kwa urahisi mpaka uwe na dawa na inabidi dawa hizo ukachimbe wewe mwenyewe, kwa hiyo sisi tunachokifanya ni kukuelekeza tu, mambo mengine utafanya mwenyewe ikiwa ni pamoja na kujifunza kwa vitendo,” alisema baba.

Sikuwa na cha kujibu zaidi ya kuinuka, nikataka kwenda kuoga lakini baba alinikataza, akasema sitakiwi kuoga kwa muda wa siku saba, nikashangaa sana. Aliniambia nivae nguo zangu tuondoke haraka maana tulikokuwa tukienda ni mbali.

Ilibidi nifanye kama walivyoniambia, nilivaa nguo zangu vizuri, baba akafungua mlango na kutangulia, kabla hajatoka aliniambia kwamba kila tunakoenda, sitakiwi kutangulia mbele wala kubaki nyuma, muda wote niwe katikati yao.

Sikuelewa maana ya maelekezo yake hayo ila nilitii, akatangulia, nikafuata halafu baba Rahma akafuatia nyuma. Nikiri kwamba baada ya yale yote yaliyotokea, nilikuwa nikiwatazama baba na baba yake Rahma kwa jicho tofauti kabisa. Hata sijui nieleze vipi lakini kwa kifupi nilikuwa nikiwatazama kwa jicho la tofauti.

Tulitoka moja kwa moja mpaka nje na nadhani hakuna mtu yeyote aliyetuona, tulitoka mpaka pale nje kabisa palipokuwa na maegesho ya Bajaj na bodaboda.

“Yule jamaa aliyekamatwa kwa mauaji ameachiwa? Sijui kama tutapona mtaa huu,” nilimsikia dereva bodaboda mmoja akiwaambia wenzake, akimaanisha mimi. Nilijua kwamba ananizungumzia mimi maana hata siku ile nilipokuja kuchukuliwa na polisi pale nyumbani, yeye ndiyo alikuwa kiherehere wa kuwasimulia wenzake kwamba eti mimi nimemuua mtu gesti.

Nilijikuta nimepandwa na jazba, nikatamani kama nimrukie na kumtandika makofi kwa hasira. Hakuna kitu ambacho huwa sikipendi kama dharau. Kumbe wakati nikifikiria nini cha kufanya, baba na baba yake Rahma walishajua ninachowaza.

“Hutakiwi kuwa na hasira zisizo na msingi, muache afurahishe mdomo wake,” alisema baba yake Rahma huku akinipigapiga begani. Nilishusha pumzi ndefu, baba akazungumza na dereva mmoja wa Bajaj, tukaingia na mimi nikakaa katikati.

>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Tupeleke Ubungo,” alisema baba, safari ikaanza. Ubungo hapakuwa pageni kwangu kwani ndiyo sehemu ya kwanza kukanyaga tuliposhuka kwenye basi tukitokea Chunya. Basi tulienda mpaka Ubungo, tulipofika baba alimlipa dereva, tukavuka kwenye mataa ya kuongozea magari na kwenda upande wa pili mpaka kwenye stendi ya daladala.

Tulipanda kwenye gari moja, hata sijui linaelekea wapi, tukaenda kukaa siti ya nyuma kabisa, mimi nikiwa katikati.

“Kwani tunaenda wapi?”

“Tunaenda Kibaha,” alisema baba, nikashindwa kumhoji chochote maana hata huko kibaha kwenyewe sikuwa nakujua.

Baadaye gari liliondoka, ikiwa ni majira ya kama saa tatu za usiku, tukaenda mpaka tulipofika Kibaha, tukashuka na kuanza kutembea kwa miguu. Tulivuka barabara, nikaona kuna kibao kimeandikwa Tumbi Hospital, nimewahi sana kuisikia hii hospitali kwani mara nyingi ajali nyingi zinazotokea mkoa wa Pwani majeruhi au maiti huwa zinapelekwa Tumbi.

Basi tulianza kutembea kuifuata barabara hiyo, giza nalo likawa linazidi kuwa nene, tukatembea umbali mrefu, tulipofika kule juu kabisa, tuliiacha barabara ya lami na kuingia vichakani, nako tukatembea umbali mrefu sana, hatimaye tukatokezea kwenye eneo lililokuwa na vichana vifupivifupi.

Kwa kutumia tochi aliyokuwa nayo, baba alianza kumulika kwenye vile vichaka kama anayetafuta kitu, mimi na baba yake Rahma tukawa tunamfuata kwa nyumanyuma maana kama nilivyosema, mimi sikutakiwa kutangulia mbele wala kubaki nyuma kwa hiyo ilikuwa ni lazima tutembee watatuwatatu.

“Unauona huu mti, unaitwa mtunguja, huu ndiyo hutumika sana kutengeneza ajali za kichawi na unapatikana kwa wingi eneo hili na ndiyo maana huku kila siku unasikia ajali mbayambaya zinatokea maana wanafunzi kama wewe, huku ndiyo eneo la kujifunza kwa vitendo,” alisema baba huku akianza kufukua kwenye shina la mti huo mdogo.

“Sifa yake moja, huu mtu huwa unatoa damu,” alisema baba, akatoa kisu na kubandua sehemu ndogo ya ganda lake, nikashangaa kweli mti ukitoa vitu vilivyokuwa vikifanana kabisa na damu.

“Niangalie vizuri namna ya kuchimba maana tukitoka hapa inabidi na wewe ukafanye majaribio kama wenzako,” alisema baba. Muda huo ulikuwa ni kama saa sita hivi za usiku, giza nene likiwa limetanda kila sehemu.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 44




ILIPOISHIA:

“Niangalie vizuri namna ya kuchimba maana tukitoka hapa inabidi na wewe ukafanye majaribio kama wenzako,” alisema baba. Muda huo ulikuwa ni kama saa sita hivi za usiku, giza nene likiwa limetanda kila sehemu.

SASA ENDELEA…

Huku nikitetemeka, nilianza kumtazama vizuri baba alivyokuwa akichimba, alikuwa akifukua shina la ule mti huku akiuzunguka, akitamka maneno fulani ambayo sikuwa nayaelewa. Baada ya kuuzunguka karibu mara saba, tayari alishakuwa ameifikia mizizi, akatoa kisu na kuanza kuichambua na kuikata mmoja baada ya mwingine.

“Hutakiwi kukata mizizi zaidi ya saba kwenye mti mmoja, na hutakiwi kuchimba mti ambao unaonekana tayari umeshachimbwa katika siku za hivi karibuni,” alisema baba, nikawa natingisha kichwa kumkubalia. Baada ya kumaliza, alinikabidhi tochi, akaniambia niutazame vizuri ule mti, nikaumulika vizuri.

“Sasa na wewe unatakiwa kutafuta mti kama huuhuu, ipo mingi lakini lazima uwe makini kutafuta wa kuchimba dawa,” aliniambia baba, basi nikaanza kumulika huku na kule, baba akiwa upande wa kushoto na baba yake Rahma upande wa kulia.

Muda mfupi baadaye, kweli nilifanikiwa kuupata lakini ulikuwa umezongwa na miiba mingi, baba akaniambia ni lazima niitoe kwanza miiba yote ndiyo nianze kuchimba, nilifanya hivyo na baada ya muda, nilikuwa nimepasafisha pale kwenye shina la mti huo.

>>Usiache kutembelea… Simulizi za Majonzi

Nikaanza kuchimba huku baba akinielekeza hatua kwa hatua, akaniambia kwa kuwa ndiyo kwanza naanza hakuna umuhimu wa kunuiza maneno kama alivyokuwa akifanya yeye bali natakiwa kuweka nia moyoni kwamba nahitaji damu kwa ajili ya kafara.

Nilifanya hivyo, nikawa naufukua ule mti na nilipozunguka mara ya saba, tayari mizizi ilikuwa ikionekana, baba akanipa kisu na kuniambia kwamba natakiwa kuchagua mizizi ya katikati, yaani isiwe mikubwa sana wala midogo sana na isizidi saba.

Nikakata wa kwanza, pale nilipokata pakawa panatoka yale majimaji kama damu, nikakata wa pili, wa tatu mpaka saba ilipotimia, shina lote likawa limelowa na yale majimaji ya ule mti kama damu.

“Haya fukia lakini hakikisha hiyo mizizi hauiweki chini, ishike vizuri,” aliniambia na kunielekeza kwamba wakati wa kufukia, natakiwa kwenda kinyume na vile nilivyokuwa nafukua, yaani kama wakati wa kufukua nilikuwa nauzunguka mti kwa kuelekea upande wa kulia, ninapofukia natakiwa kuanzia upande wa kushoto na hivyo ndivyo nilivyofanya.

Baada ya kumaliza, baba alisema tunapaswa kwenda kuziosha dawa zetu mtoni na kuzitengeneza vizuri. Sikuwa mwenyeji wa Kibaha na hata sikuwa najua kama kuna mto, nikawa kama bendera fuata upepo.

Tulitembea tukikatiza vichaka na mapori, hatimaye tukatokezea mahali palipokuwa na kama chemchemi hivi, pembeni kukiwa na bustani za mbogamboga nyingi, baba akatangulia mpaka pale kwenye chemchemi, kabla ya yote, alitoa kisu chake na kukata jani kubwa la mgomba, akalikata vipande vitatu, kimoja akanipa, kingine akampa baba Rahma na kingine akabaki nacho yeye.

Alitoa ile mizizi aliyoichimba, akaniambia nimtazame kwa makini anachokifanya, ilikuwa imebadilika rangi na kuwa nyekundu kama damu, akaanza kuiosha ikiwa juu ya jani la mgomba, akafanya hivyo kwa dakika kadhaa mpaka ilipobadilika rangi na kurejea kwenye rangi yake halisi ambayo ni kama kahawia fulani hivi.

Ilifika zamu yangu, na mimi nikafanya vilevile, nikaitoa mfukoni na kuiosha vizuri, kisha ikafika zamu ya baba yake Rahma ambapo baba alimtolea na kumpa mizizi yake, akaiosha kwa uzoefu wa hali ya juu kisha tukaondoka eneo hilo.

Hapakuwa mbali sana na barabara kwani hata kelele za magari yaliyokuwa yakipita kwa kasi kubwa tuliweza kuzisikia. Kadiri tulivyokuwa tukisonga mbele ndivyo hofu ilivyozidi kutanda kwenye moyo wangu.

Tulikatiza vichaka, mapori na mashamba ya watu na hatimaye tukawa tumetokezea barabara ya lami. Sikujua eneo lile linaitwaje lakini kwa mzunguko tulioupiga, kuanzia pale tuliposhuka kwenye gari, tulivyoelekea njia ya Tumbi na baadaye kuingia porini kisha kurudi barabarani, nilijua kwamba si mbali sana na pale tuliposhukia.

“Mtu yeyote akikusemesha hutakiwi kujibu chochote, eneo hili lina watu kutoka jamii mbalimbali ambao huwa wanapenda kupimana nguvu, umenielewa?” baba aliniambia, nikatingisha kichwa kuonesha kumkubalia.

“Leo ni zamu yako, kwa hiyo inatakiwa unisikilize kwa makini,” baba aliniambia, akasema kati ya ile mizizi saba, mmoja natakiwa kwenda kuufunga kwenye mti au jani lolote upande wa pili wa barabara, mwingine natakiwa kuuweka katikati ya barabara, mwingine natakiwa kuufunga upande ule tuliokuwepo, mmoja natakiwa kuutafuna na kuumeza na miwili natakiwa kubaki nayo mwilini, mmoja niweke kwenye mfuko wa kushoto wa suruali na mwingine niubane kwenye kwapa langu la kushoto kama kipima joto.

Yalikuwa ni maelezo marefu lakini nilijitahidi kuwa mwelewa maana nilikuwa na shauku kubwa ya kuona nini kitatokea. Kweli baada ya hali kutulia, kwa maana kukiwa hakuna gari kutoka upande wowote, nilivuka barabara kinyumenyume mpaka upande wa pili.

Kwa kutumia uzi mweusi alionipa baba, niliufunga ule mzizi kwenye tawi moja la mti mdogo uliokuwa pale pembeni ya barabara, nikarudi tena kinyumenyume mpaka katikati ya barabara na kukaa chini kabisa, nikaweka ule mzizi kisha nikajiburuza kwa makalio kinyumenyume mpaka pale baba na baba yake Rahma walipokuwa wamesimama.

Nikasimama na kusogea kwenye kimti kingine kidogo kilichokuwa kando ya barabara, usawa wa kile nilichokifunga, nikaenda kufunga ule mzizi kwa kutumia ule uzi kisha kinawasogelea akina baba ambao walikuwa wakinitazama kwa makini kuhakikisha sikosei hatua hata moja.

“Safi sana,” alisema baba kisha akaanza kuniuliza kama mpaka hapo nimeshaelewa ni gari linalotokea upande gani ndiyo litapata ajali. Sikuwa naelewa chochote. Akaniambia kwa sababu nimesota kwa makalio kutokea katikati ya barabara kuelekea upande wa kushoto wa Barabara ya Morogoro, gari litakalopata ajali litakuwa ni linalotoka Dar es Salaam kuelekea upande wa Morogoro.

>>Usiache kutembelea… Simulizi za Majonzi

Sikuelewa anamaanisha nini, ikabidi nitulie kuona nini kinachoenda kutokea. Tulisogea pembeni kabisa, umbali wa kama mita mia moja hivi, vichakani kabisa, tukakaa kwa kukunja miguu na kutengeneza duara. Kulikuwa na mbu wengi lakini wote walikuwa wakiishia kutuzunguka tu, hata sijui kwa nini hawakuwa wakituuma.

“Nataka ufumbe macho halafu utulie huku ukitafuna huo mzizi mmoja, nitakachokuuliza unijibu,” baba aliniambia, nikafanya kama alivyoniambia. Cha ajabu, nilipofumba macho tu, japokuwa tulikuwa mbali kidogo na barabara, niliweza kusikia sauti za magari na pikipiki vikipita kwa kasi, cha kushangaza zaidi, niliweza kusikia hata sauti za madereva na abiria, nikashtuka sana.

Nikiwa nimeendelea kutulia, japokuwa nilikuwa nimefumba macho, kadiri nilivyokuwa nikizidi kutafuna ule mzizi ndivyo nilivyoanza kuona taswira ya kila kilichokuwa kikiendelea barabarani utafikiri nilikuwa nimesimama pembeni ya barabara, tena nikiwa nimefumbua macho.

“Unaona magari mangapi?”

“Mengi tu.”

“Yanayoelekea upande wa Morogoro ni mangapi?”

“Ni matatu.”

“Ambalo lipo nyuma kabisa lina abiria wangapi?”

“Abiria mmoja ambaye ni mtoto na dereva mwanamke.”

“Safi, hiyo ndiyo kazi yako ya leo, likazie macho hilo gari kwa nguvu na likikaribia hapo ulipo fumbua macho ghafla halafu tena hicho kilichopo mdomoni mwako,” alisema baba, kweli nikawa nalitazama gari hilo.

Lilikuwa ni gari dogo na ndani yake kulikuwa na watu wawili tu, dereva mwanamke na mtoto, ilionesha ni kama ni wanafamilia wanarudi makwao. Sikuelewa nini kitawapata lakini kwa sababu ya shauku niliyokuwa nayo, nilijikuta nikifanya kile baba alichoniambia, nikafumbua macho ghafla na kutema mabaki ya ule mzizi, nikashtukia nimemtemea baba usoni.

Mara kikasikika kishindo kikubwa kule barabarani, kilichonishtua mno. Sikuelewa nini kimetokea pale kwa sababu nilipokuwa nimefumbamacho, nilikuwa najiona kabisa kwamba nipo barabarani lakini nilipofumbua tu, nilijikuta nikiwa nimekaa palepale tulipokuwa tumekaa na baba na baba yake Rahma.

Kitu cha mwisho nilichokumbuka, wakati nataka kufumbua machom nilimuona yule mwanamke aliyekuwa kwenye usukani, akikunya usukani gahfla kama aliyeona kitu cha hatari mbele na sasa anataka kukikwepa, ndipo kikafuatia kile kishindo.

“Nenda haraka, hakikisha unamtoa mtoto kwenye gari na kuja naye hapa, pale kwenye gari ulipomtoa utaweka hiki,” alisema baba huku akinipa kipande cha mgomba.

Je, nini kitafuatia?
 
Back
Top Bottom