Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Sehemu ya ishirini na tatu_______23



ILIPOISHIA:

“Tupeleke Coco Beach, kule wanakouza mihogo,” alisema Rahma, safari ikaanza lakini mita chache mbele, nilishtuka baada ya kusikia mtu akiliita jina langu kwa nguvu, tena sauti yenyewe ilikuwa ya kike, ilibidi Rahma amwambie dereva asimame, tukageuka nyuma kutazama ni nani aliyekuwa ananiita kwa sababu mimi nilikuwa mgeni na hakuna mtu yeyote aliyekuwa akilifahamu jina langu zaidi ya wale tuliokuwa tukiishi pamoja.

SASA ENDELEA…

Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kushuka kwenye Bajaj, Rahma naye akafuatia, nikawa na shauku kubwa ya kumjua aliyeniita kwa bashasha kiasi kile.

“Togo, ni wewe! Ooh siamini macho yangu, sikujua kama nitakupata!” alikuwa ni yule msichana ambaye tulikaa naye siti moja kwenye basi wakati tukisafiri kutoka Mbeya kuja Dar es Salaam. Alikuwa amevaa sketi fupi na nyepesi ambayo ilimfanya maungo yake yajichore vizuri.

Juu alikuwa amevaa blauzi ndogo ambayo iliacha sehemu kubwa ya kifua chake wazi, akawa anatembea kwa maringo akinifuata huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake. Kiukweli na mimi nilishindwa kujizuia kutabasamu, hasa nilipokumbuka wakati mzuri tuliokuwa nao kwenye basi mpaka tulipoachana Ubungo.

“Jamani mbona ile simu niliyokupa hupatikani hewani? Nimehangaika sana kwa kweli,” alisema akiwa tayari ameshanifikia, kufumba na kufumbua nikashtukia amenikumbatia kimahaba na kunibusu mdomoni.

“Dada mambo!” alimsalimia Rahma ambaye alikuwa amesimama pembeni yake, akiwa ni kama haamini kile alichokuwa anakiona. Ilibidi nianze kuvungavunga pale maana kila kitu kilikuwa kikitokea kwa kasi kubwa mno.

“Umepajuaje hapa?”

“Ilibidi nimtafute dereva teksi aliyewabeba wakati mnatoka pale Ubungo, kwa bahati nzuri akawa anakumbuka sehemu alipowaleta, ndiyo amenileta, yule pale kwenye gari,” alisema huku akigeuka nyuma na kuonesha upande teksi alityokuja nayo ilipokuwa imepaki.

“Mnaenda wapi kwani?”

“Tunaenda bichi,” nilimjibu harakaharaka huku nikigeuka na kumtazama Rahma usoni ambaye bado alionesha kutoelewa kinachoendelea.

“Kwa nini tusipande kwenye ile teksi, mi nimeshalipa.”

“Hapana, ahsante,” Rahma alidakia na kunishika mkono, naona uzalendo ulishafika kikomo, akatangulia kuingia kwenye Bajaj na kunivuta mkono na mimi niingie.

‘Kwani mnaenda bichi gani?” aliuliza huku akionesha bado kuwa na shauku kubwa ya kuzungumza na mimi.

Sikuwa nakujua Coco lakini kwa sababu nilimsikia Rahma akimueleza dereva wa Bajaj kuwa atupeleke wanakouza mihogo, na mimi nilijikuta nikijibu hivyohivyo.

“Coco wanakouza mihogo,” baada ya kumjibu hivyo, nilimuona haraka akigeuka na kurudi kwenye teksi aliyokuja nayo. Watu kadhaa waliokuwa eneo lile, waliacha kila walichokuwa wanakifanya na kugbaki wakishangaa muvi iliyokuwa inaendelea.

“Togo, yule ni nani?”

“Mh! Jina lake simjui lakini tulikaa naye siti moja kwenye basi wakati tunakuja.”

“Muongo! Yaani mtu uliyekaa naye siti moja tu ndiyo akuzoee kiasi hiki? Angalia amekupaka lipstiki yake mdomoni,” alisema Rahma huku akionesha kuanza kulengwalengwa na machozi.

“Kweli tena, hata ukimuuliza atakwambia hivyohivyo, hata hatujuani vizuri,” nilisema huku nikijifuta mdomoni, kweli kulikuwa na mabaki ya lipstiki aliyoniachia aliponibusu mdomoni.

“Yeye amenizoea tu lakini hakuna chochote kati yetu.”

‘Mbona nimemsikia akisema alikupa simu? Yaani inawezekanaje mtu akupe simu tu? Halafu umeona alivyovaa, kwa nje tu anaonekana changudoa, ka hiyo kumbe wewe unatembea na machangudoa? Si nakuuliza?” Rahma alizidi kunibana kwa maswali mengi. Sikuwahi kumsikia Rahma anavyozungumza akikasirika lakini siku hiyo alikasirika kwelikweli, akawa anaendelea kufoka na muda mfupi baadaye alianza kulia.

Ilibidi nianze kazi ya kumbembeleza, nikamkumbatia kifuani kwangu na kumbusu sehemu mbalimbali za mwili wake, kidogo nikamuona akianza kutulia, na yeye akanikumbatia kwa nguvu kifuani huku Bajaj ikizidi kukata mitaa.

“Halafu umemuelekeza mpaka sehemu tunapoenda, hujui anaweza kukufuata? Dereva nimebadilisha mawazo, hebu tupeleke Msasani Beach na siyo Coco tena, nitakuongeza hela,” alisema Rahma, dereva akatingisha kichwa kuonesha kwamba amemueleza.

“Unajua mimi nakupenda, kwa nini unanifanyia makusudi lakini?”

“Nisamehe Rahma, hayakuwa makusudio yangu, nimejikuta tu mambo ya ajabu yametokea, nisamehe,” niliendelea kumbembeleza na kumbusu, cha ajabu alitulia kabisa na hakusema neno lingine lolote mpaka tulipofika Msasani Beach. Sikuwa naijua mitaa lakini kiukweli nilifurahia sana mandhari ya Jiji la Dar es Salaam.

Alimlipa dereva kisha tukashuka, tukawa tunatembea kuelekea baharini huku nikiwa na shauku kubwa ya kuiona bahari maana nilikua nikisikia tu. Nilitaka pia nikaonje maji yake nihakikishe kama kweli yana chumvi kama ambavyo watu huwa wanasema.

Tulipita sehemu ambapo kuna viti vya kupumzikia, tukawaona watu mbalimbali wakiwa wanapunga upepo, wengine wakila na kunywa. Tulipitiliza mpaka baharini kama nilivyomuomba Rahma na kitu cha kwanza nilichokifanya, ilikuwa ni kunawa usoni na kichwani kwa kutumia maji ya baharini.

Niliwahi kusikia pia kwamba maji ya baharini huondoa mikosi, nikanawa kwa maji mengi na hapo ndipo nilipogundua kuwa ni kweli maji hayo yalikuwa na chumvi, tena nyingi kiasi kwamba huwezi hata kuyanywa. Kiukweli nilifurahi sana kuiona bahari na kuyagusa maji ya bahari, nikawa najisikia kama nimetua kwenye ulimwengu mwingine tofauti.

Rahma muda wote alikuwa akicheka kwa furaha, hasa kwa jinsi nilivyokuwa ‘najitoa ufahamu’ na bahari. Nilifurahi kumuona akicheka mpaka kukaukia, akiwa amekaa kwenye mchanga, jirani na pale nilipokuwa.

Baada ya kucheza sana kwenye maji, nilirudi pale alipokuwa amekaa Rahma, nikakaa pembeni yake na kumuegamia, akanibusu kwenye paji la uso na kuniambia kuwa nimemfurahisha sana. Tuliendelea kupiga stori za hapa na pale lakini mra kwa mara Rahma alikuwa akipenda zaidi tuzungumze mambo ya kikubwa.

Alikuwa anataka kusikia nina mal;engo gani naye siku za usoni, alitaka kujua napenda kuwa na familia ya watoto wangapi au nitakuwa baba wa aina gani kwa wanangu. Aliniuliza pia kama nina mpango wa kujiendelea kwenye fani yoyote ili mwisho na mimi nije kuwa na uwezo wa kutunza familia.

Kwangu mazungumzo hayo si tu kwamba yalikuwa mageni kwangu, lakini pia mambo mengi sikuwahi kuyawaza. Nadhani hili ndiyo tatizo linalowakumba watu wengi wanaopishana umri wa wenzi wao, hasa kama mwanamke akiwa mkubwa. Kwangu Rahma alikuwa mkubwa, kama nilivyowahi kusema siku za nyuma, alikuwa akilingana na dada yetu mkubwa, Sabina.

Hata mazungumzo yake, alikuwa ni mdada anayejiheshimu, mwenye busara na anayewaza mbali, alionesha kweli kwamba ameanza kukomaa kiakili. Hali ilikuwa tofauti kwangu kwa sababu hata mwanamke mwenyewe, yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kwangu, kwa maana sikuwahi kuwa na mpenzi wala kushiriki sanaa za kikubwa kabla ya kukutana naye.

Sikuwa nikiwaza chochote kuhusu familia, au mke au maisha ya ndoa, nadhani ni kwa sababu ya umri. Hata hivyo, kwa sababu Mungu alinipa uwezo wa kumsoma mtu haraka, sikutaka kumkasirisha mawazo Rahma, kwa hiyo ikabidi na mimi nianze kuzungumza kama mtu mzima flani hivi, tukawa tunaenda sawa.

“Mh, hebu naomba simu yangu mara moja, sijaigusa tangu tumefika,” alisema rahma, nikamsogezea pochi yake ndogo ambapo alifungua na kutoa simu.

“Mh! Baba amepiga sana, sijui alikuwa anasemaje,” alisema Rahma huku akiendelea kubonyezabonyeza simu yake, mara akanigeukia na kunitazama usoni.

“Kulikuwa na ujumbe wako hapa lakini tumechelewa sana, hata sijui itakuwaje,” alisema, hali iliyonifanya na mimi nishtuke kwa sababu ya jinsi yeye mwenyewe alivyoonekana kushtuka.

“Kuna nini kwani?” nilimuuliza, akaniambia baba alikuwa amempigia simu kwa lengo la kutaka kuzungumza na mimi na kubwa alilokuwa anataka kuniambia ni kwamba wamesahau kuniambia kwamba nikienda ufukweni nisiguse kabisa maji ya bahari. Nilishangazwa sana na maelezo hayo, nikajiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.

Tayari nilishayagusa na siyo kuyagusa tu bali niliyachezea vya kutosha na kama Rahma asingenizuia au kama siyo woga wa bahari, nilitaka hata niogelee. Tukiwa bado tunashauriana cha kufanya, mara simu ya Rahma ilianza tena kuita, harakaharaka akaipokea.

“Samahani simu ilikuwa kwenye mkoba baba,” nilimsikia Rahma akijitetea, bila shaka aliulizwa kwa nini hakupokea simu.

“Eeeh niko naye,” alijibu tena, nikajua lazima ameulizwa kama yupo na mimi, nikamuona akinipa simu, akaniambia baba anataka kuzungumza na mimi.

“Haloo Togo.”

“Haloo baba.”

“Hebu ongea na mzee,” alisema baba yake Rahma akimaanisha nizungumze na baba, akampa simu. Alimpa simu baba na swali lake la kwanza lilikuwa ni kama nimeshayagusa maji ya bahari. Ilibidi nimjibu kwamba nimeshayagusa kwani sikuwa najua chochote.

“Mungu wangu, kuna mtu anaenda kufa,” alisema baba kisha akakata simu, nikashtushwa mno na kauli yake hiyo. Sikuelewa nini kimetokea au kosa langu lilikuwa ni nini.

“Mbona watu wanachezea maji, wengine wanaogelea bila tatizo, mimi kosa langu nini,” nilijikuta nikijisemea, Rahma akanishika na kunituliza pale chini kwani nilishaanza kuchanganyikiwa kutokana na kile alichokisema baba.

“Amesemaje kwani?” aliniuliza Rahma, nikashusha pumzi ndefu na kumtazama usoni, sikutaka kumwambia ukweli wa nilichoambiwa na baba, nikamdanganya kwamba baba amenifokea sana kwa sababu nimegusa maji hayo. Aliupokea uongo wangu, akanikumbatia na kunipa pole, nikatulia kifuani kwake.

Ghafla tulishtushwa na kishindo kikubwa ambacho hata sikuelewa kimetokea wapi.

Je, nini kimetokea?
 
Sehemu ya pili - 2

ILIPOISHIA:
Tulipokaribia nyumbani kwa mzee huyo, baba alinionesha ishara kwamba nisimame, nikafanya hivyo, tukawa tunasikia sauti za watu wengi wakilia kutoka nyumbani kwa mzee huyo, baba akanionesha ishara kama anayesema ‘unaona?’, nikashika mdomo kwa mshangao. Sikutaka kuamini kwamba kweli mzee Mwankuga alikuwa amefariki dunia.

SASA ENDELEA...
Nilijikuta nikishusha lile furushi la dawa na panga, nikawa nataka niende kushuhudia mwenyewe kama ni kweli lakini baba aliniambia nisithubutu kufanya hivyo, hasa kutokana na uhasama uliokuwepo kati yetu na familia hiyo. Bado niliendelea kuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kama ni kweli yule mzee amekufa.

Ilibidi baba anishike mkono, tukaenda mpaka nyumbani ambapo baba aliingia kwenye chumba chake cha uganga na kuanza kuchambua zile dawa tulizotoka nazo porini. Ni kama alijua kwamba nitamtoroka na kurudi kule msibani kwenda kushuhudia kilichotokea kwani aliniambia nikae palepale, nimuangalie jinsi alivyokuwa akichambua dawa.

Kweli nilitii maagizo yake, nikakaa pale lakini bado nilikuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kilichoendelea. Nilipomuona baba amezama kwenye kazi yake hiyo, niliinuka na kuanza kuelekea mlangoni, akaniwahi na kuniuliza ninakokwenda.

“Naenda kujisaidia baba,” nilimdanganya baba, akanitazama usoni kisha akaendelea na kazi yake. Nilitoka na kwenda chooni ambako nako nilizunguka nyuma, nikatokomea huko na kwenda kutokea upande wa pili, nyumbani kwa mzee Mwankuga.

Kwa kuwa watu walikuwa wengi, hakuna aliyenitazama vizuri, kwa hiyo nikapata nafasi ya kujichanganya na waombolezaji ambao kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo walivyokuwa wakizidi kuongezeka.
“Kwani alikuwa anaumwa?”

“Hapana alikuwa mzima wa afya kabisa na alikuwa akiendelea na kazi zake, mara akaanza kulalamika kwamba kichwa kinamuuma sana, damu zikawa zinamtoka puani na mdomoni, ghafla akadondoka na kugeuza macho, muda mfupi baadaye moyo wake ukasimama,” nilimsikia ndugu mmoja wa Mwankuga akimuelezea mmoja wa waombolezaji.

Ni hapo ndipo nilipoamini kwamba kweli Mwankuga alikuwa amekufa, kwa kuhofia kuonekana na watu, hasa ndugu zake ambao kama nilivyosema tangu awali hatukuwa na uhusiano nao mzuri, nilirudi kinyumenyume, kisha nikaondoka haraka kurudi nyumbani.

Nilimkuta baba akiwa amesimama nje ya nyumba yetu, akinitazama, nadhani alishashtukia kwamba nimemtoroka, aliponiona tu natokeza, akanibana kwa maswali magumu.

“Ulikuwa wapi?”
Nilikosa cha kujibu, nikawa najiumauma, baba akaniambia nina bahati sana vinginevyo angenifunza adabu, tukaingia ndani ambapo tulienda mpaka kule kwenye chumba cha uganga, baba akanikalisha chini na kuanza kuzungumza na mimi.

“Unajua wewe ndiyo mwanangu kipenzi na sasa umeshakuwa mkubwa, sina sababu ya kuendelea tena kukuficha mambo yangu ndiyo maana leo nimekuonesha baadhi ya mambo.

“Dunia imebadilika sana mwanangu, binadamu tunaishi kwa ubaya sana, hakuna anayemtakia mwenzake mema, watu wanawaonea wengine bila sababu, watu wasio na hatia wanakufa kila siku, ukienda makaburini, yaliyojaa ni makaburi ya watu wasio na hatia! Kila mmoja lazima ajilinde mwenyewe na ukishaweza kujilinda mwenyewe, unaweza pia kuwalinda wenzako,” alisema baba, maneno ambayo yaliniingia lakini bado sikuwa naelewa kile alichokuwa anakimaanisha.

Bado nilikuwa nataka ufafanuzi wa kifo cha mzee Mwankuga kwa sababu kwa akili yangu, niliona kama hakuwa amefanya jambo lolote kubwa kustahili adhabu ya kifo. Ni kama baba aliyaona mawazo yangu, akaniambia anajua najiuliza maswali mengi yasiyo na majibu kuhusu kilichotokea kule msituni.

“Kuna yule rafiki yako aliyekufa kwa kutumbukia kwenye kisima mwaka jana, unamkumbuka?”

“Alfred? Ndiyo namkumbuka,” nilimjibu baba huku nikiwa na shauku ya kutaka kusikia anachotaka kukisema.

Akaniambia mazingira ya kifo cha Alfred, yalikuwa yamejaa utata wa hali ya juu na kwamba baada ya kuchunguza kwa kina, aligundua kwamba Alfred hakufa kifo cha kawaida, bali aliuawa.

Akaendelea kuniambia kwamba hata huko kuuawa kwenyewe, japokuwa kila mtu alikuwa anajua ni kweli amekufa na kuzikwa, lakini ukweli ni kwamba hakuwa amekufa bali alichukuliwa msukule.

“Kwani kuna tofauti gani kati ya mtu aliyekufa na mtu aliyechukuliwa msukule?” Nilimuuliza baba, akaniambia kwamba mtu aliyekufa kwa kifo cha amri ya Mungu, huwa mwili unatengana na roho, mwili unaenda kuzikwa kaburini na huo ndiyo unakuwa mwisho wa maisha ya kawaida ya hapa duniani.

Akaniambia pia kwamba kwa kawaida, nafsi au roho ya mtu huwa haiishi ila baada ya kutengana na mwili, huhama kutoka kwenye ulimwengu wa kawaida na kwenda kwenye ulimwengu mwingine. Nilipotaka kumuuliza kuhusu huo ulimwengu mwingine, aliniambia kwamba atanifafanulia siku nyingine.

Akaendelea kunieleza kwamba mtu anayechukuliwa msukule, huwa hafi bali anabadilishwa kichawi kiasi cha kila mmoja kuamini kwamba ni kweli amekufa lakini kinachotokea, huwa anachukuliwa na wachawi na kwenda kutumikishwa kichawi kwenye kazi mbalimbali, mpaka siku ambayo atakufa kwa amri ya Mungu lakini kwa kipindi chote hicho, huwa anaishi kama msukule.

“Sasa mbona Alfred alipokufa tulienda kumzika makaburini na hata siku ya kuaga mwili wake, wote tulipita kwenye jeneza lake na mimi mwenyewe nilimshuhudia akiwa amelala ndani ya jeneza?”

“Ni vigumu sana kunielewa hiki ninachokisema kwa maneno, lakini nataka nikuhakikishie kwamba rafiki yako hakufa na aliyefanya yote hayo ni huyu mshenzi Mwankuga,” alisema baba akionesha kuwa na jazba, akaendelea kunieleza kwamba, licha ya Alfred, walikuwepo watu wengine wengi tu ambao wengine waliuawa kwelikweli lakini kwa ushirikina, ikiwa ni uonevu unaofanywa na wachawi hasa wanapokaribia kutoa makafara yao, na wengine huchukuliwa misukule.

Bado sikuwa namuelewa anachokisema, akaniambia anataka akanithibitishie kwamba Alfred hakufa. Aliacha kila alichokuwa anakifanya, tukatoka nje ambapo watu walikuwa wakizidi kufurika kwenye msiba wa Mwankuga na sasa vilio vya wanawake vilikuwa vikizidi kuongezeka.

Wala baba hakujali chochote, tukatoka na kuelekea makaburini ambayo yalikuwa eneo maarufu linalofahamika kama msalabani, nilikuwa na shauku kubwa ya kutaka kujionea mwenyewe kile alichokuwa anakisema baba kama ni kweli.

“Unakumbuka alizikwa kwenye kaburi gani?” baba aliniuliza, nikamwambia nakumbuka vizuri kwa sababu enzi za uhai wake, Alfred alikuwa rafiki yangu mkubwa na kifo chake cha ghafla, kiliniumiza mno moyo wangu. Kwa kuwa hata siku ya mazishi yake nilikuwepo mpaka makaburini, nilikuwa nalikumbuka vizuri kaburi lake.

Nikamuongoza baba mpaka kwenye kaburi la Alfred ambalo juu yake kulikuwa na msalaba ulioandikwa jina lake kamili, tarehe ya kuzaliwa na tarehe ya kufa kwake.

Akaniambia niwe makini kwa kila atakachokuwa anakifanya, nikatingisha kichwa huku hofu kubwa ikiwa imetanda ndani ya moyo wangu kwani kiukweli nilikuwa nikiogopa sana makaburi na maiti.

Je, nini kitafuatia?
Hii episode ya kwanza Nimekariri 'Makongorosi Chunya mkoani Mbeya!'

Naendelea kusoma🙇
 
Sehemu ya ishirini na nne_____24



ILIPOISHIA:

Ghafla tulishtushwa na kishindo kikubwa ambacho hata sikuelewa kimetokea wapi. Watu walianza kupiga kelele kwa nguvu huku wale waliokuwa baharini wakianza kukimbia kuokoa maisha yangu. Ilibidi tugeuke kutazama kule kishindo kile kilichotokea ambako bado zile kelele zilikuwa zikitokea.

SASA ENDELEA…

Lahaula! Samaki mkubwa ambaye sikuwahi kumuona ingawa baadaye nilisikia kwamba anaitwa papa, akiwa na meno makali yaliyochongoka, aliipiga kikumbo boti ndogo ya uvuvi iliyokuwa eneo hilo na kusababisha kishindo kikubwa, wavuvi waliokuwa ndani ya boti hiyo wote wakarukia majini na kuanza kuhaha kuokoa maisha yao.

Nikiwa bado namshangaa samaki yule ambaye alijirusha kwa nguvu kutoka majini na sasa akawa anaonekana mzimamzima, wote tulishtukia akimfuata mmoja kati ya wale wavuvi, akafunua mdomo wake uliokuwa na meno makali kama msumeno, akamkamata kiunoni, kufumba na kufumbua akaubana mdomo wake kwa nguvu, yule mvuvi akagawanyika vipande viwili.

Sijui nilipata wapi ujasiri, nilijikuta nikiinuka kwa kasi kubwa pale tulipokuwa tumekaa na Rahma, akabaki anapiga kelele za kuniita huku akiniuliza nakwenda wapi na kufanya nini? Sikuelewa swali lake lilimaanisha nini kwa sababu kila kitu kilikuwa wazi, nilikuwa nakwenda kutoa msaada kwa wale wavuvi.

Nilikimbia mpaka eneo ambalo maji yalianza kunifika kiunoni, kwa kuwa nilikuwa na uzoefu wa kutosha wa kupiga mbizi, nilianza kuelekea eneo la tukio. Kadiri nilivyokuwa nazidi kusonge mbele ndivyo kelele zilivyokuwa zikizidi kuongezeka. Sikuwahi kudhani kwamba samaki ana sauti ya kutisha kiasi kile maana alikuwa akitoa milio ya ajabu.

Nikiwa naendelea kupiga mbizi, nilimshuhudia akikifuata kile kipande cha kichwa cha yule mvuvi, akaanza kukichanachana kwa meno yake makali, akararua minofu yote na kubakiza mifupa michache tu, akahamia kile kipande kingine cha kichwa, akakitafuna na kuacha kichwa tu. Nilijikuta nikipatwa na hofu ya ajabu, hakika sikuamini nilichokuwa nakiona.

Maji yote ya eneo lile yalibadilika rtangi na kuwa mekundu, mimi nikawa nazidi kupiga mbizi nikiwa hata sijui naenda kufanya nini maana uwezo wa kupambana na samaki yule kwenye maji, hakika sikuwa nao, nikasikia kelele za watu wakinizuia na kunitaka nirudi maana tayari wale wavuvi wengine walishapotea kwenye upeo wa macho yangu.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Ghafla nilihisi kama kuna kitu kimenishika kwenye mguu wangu wa kushoto na kuanza kunivutia chini, tayari nilishafika kwenye kina kirefu, nikatumia nguvu kubwa kujaribu kupambana na kile kitu kilichokuwa kimeninasa ambacho bado sikuwa najua ni nini, ghafla nikajikuta nikizama.

Nilipoibuka, nilikuwa nimemeza kiasi kikubwa cha maji ya chumvi na nikiri kwamba unaweza kuwa unajua sana kuogelea kwenye maji baridi lakini maji chumvi ni hatari sana maana yakikuingia puani au ukiyanywa, ile chumvi inakufanya uzidi kuwa kwenye hali mbaya.

Nilijaribu kupiga mbizi kwa nguvu lakini bado kile kitu kilikuwa kimenibana mguu na kuzidi kunivuta, nilitamani nigeuke niangalie ni nini lakini sikuweza kutokana na jinsi nilivyokuwa napambana na mawimbi makali. Nikajikuta nikizama tena na kunywa maji mengi zaidi ya mwanzo, nikaibuka na kuendelea kutapatapa, safari hii mwili ukiwa umeishiwa kabisa nguvu kiasi cha kuanza kuhisi giza nene machoni.

Sikuelewa tena kilichoendelea kwani giza nene lilinizingira usoni huku nikianza kuona picha za majinamizi ya kutisha.

***

“Nisaidieni jamani mchumba wangu anakufaaaa, msaada?” Rahma alipiga kelele kwa nguvu na kuwafanya watu wote waliokuwa ufukweni hapo, wakiwemo wavuvi waliokuwa wakivuta nyavu zao, kuacha kila walichokuwa wakikifanya na kukimbilia kule baharini kwenye kina kirefu.”

“Imekuwaje tena jamani?”

“Mh hata sijui nini kimetokea, hawa walikuwa wamekaa pale ufukweni na mwenzake, mara mwanaume akaanza kukimbilia baharini, tena akiwa na nguzo zake zote.”

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Mimi mwenyewe nimemuona, nikasema huyu jamaa kachanganyikiwa nini? Unaambiwa kakimbia mpaka kule, akaanza kupiga mbizi kwa kasi kubwa kama samaki, mara tunashangaa anaanza kutapatapa, mwisho maji yanamzidi anazama,” alisema mwanaume mmoja, shuhuda wa tukio lile.

“Binti kwani amepatwa na nini?”

“Nisaidie kwanza kumsaidia, mengine tutajua baadaye,” alijibu Rahma huku akilia na kurusharusha miguu kama amekanyaga siafu. Muda mfupi baadaye, wavuvi watatu tayari walikuwa wameshamfikia pale alipokuwa ambapo kwa sababu alishazama na kuibuka kwa mara ya tatu, ilibidi wazame chini kumtafuta.

Kwa bahati nzuri, walifanikiwa kumpata, wakaibuka naye na kupiga mbizi mpaka ufukweni kwenye mchanga ambapo watu wengi walikuwa tayari wameshakusanyika, zoezi la kumsaidia kurejesha pumzi zake likaanza ambapo wale wavuvi walianza kumkandamiza tumboni kwa nguvu.

***

“Kwani ilikuwaje Rahma?”

“Hata sijui baba, siwezi kuelezea maana naona ni zaidi ya maajabu,” nilisikia sauti za watu wakizungumza kwa mbali ambapo nilizitambau vyema sauti hizo kuwa ni Rahma na baba. Bado macho yangu nilikuwa nimeyafumba, nikihisi kila kiungo kwenye mwili wangu kikiwa kizito na kilichokosa nguvu kabisa.

Nilijaribu kufumbua macho mara kadhaa lakini nilikuwa nashindwa, nikawa nimelala tu lakini nikiwa na uwezo wa kusikia kila kilichokuwa kinaendelea.

“Tueleze ili angalau tupate mwanga maana mpaka sasa sote tupo gizani na wewe ndiye uliyekuwa naye kabla hajafikwa na haya matatizo.”

“Tulikuwa salama tu lakini baada ya ile simu mliyopiga ndiyo mambo yalipoharibika, kwa sababu mwanzo tulikuwa tumekaa kwenye mchanga baada ya kuwa Togo ameshacheza sana na maji ya bahari, tena akawa ananichekesha kwa kuniambia eti ukipia chakula hakuna haja ya kuweka chumvi.

“Muda mfupi baada ya kumaliza kuzungumza na simu, nilishangaa kusikia akiniambia kama nimesikia hicho kishindo kikubwa, nikawa nashangaa maana hakukuwa na kishindo chochote, mara akasimama huku akitazama baharini, akawa ni kama ameona kitu ambacho mimi hata sijui ni nini.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, nilishangaa akianza kukimbilia baharini, alipofika kwenye maji mengi alipiga mbizi kwa kasi kubwa mpaka alipofika kwenye kina kirefu, mara akaanza kutapatapa mpaka akazama, wavuvi wakaenda kumuokoa akiwa hajitambui, tumbo likiwa limejaa maji,” nilimsikia Rahma akitoa ufafanuzi ambao ulinishangaza sana.

Nilijikuta nikipata nguvu za ghafla, nikafumbua macho na mimi nikitaka kutoa ufafanuzi wa kilichotokea. Kitendo cha mimi kufumbua tu macho, kiliwafanya wote waache kila walichokuwa wanakifanya, wakanisogelea na kuzunguka pale kitandani huku nikimsikia Rahma akimuita nesi.

Wakati wao wananishangaa na kuniuliza nilikuwa najisikiaje, mimi bado nilikuwa nikitafakari maelezo aliyoyatoa Rahma ambayo niliyasikia vyema kabisa. Nilishangaa kwa nini akwepeshe ukweli wa kilichotokea? Yaani alibadilisha maelezo kwa faida ya nani?

Kwani yeye hakumuona yule papa mkubwa aliyekuwa akimla mvuvi huku wenzake wakiponea kwenye tundu la sindano? Ina maana hakusikia kile kishindo cha samaki yule mkubwa anayetisha alipoipiga kikumbo kikubwa boti ile ya wavuvi? Kwa nini hawaambii kwamba nilikuwa naenda kuwaokoa wavuvi? Nilijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.

Nilianza kuwatazama mmoja baada ya mwingine, kuanzia mama ambaye uso wake ulikuwa na huzuni kubwa, baba ambaye alionesha kuwa katika tafakuri nzito na ndugu zangu wote ambao walikuwa wamekodolea macho, kila mmoja akiwa na maswali mengi yasiyo na majibu.

Mara mlango wa wodi ulifunguliwa, watu wote wakageuka kutazama ni nani aliyekuwa akiingia kwa kasi kiasi kile.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya ishirini na tano________25




ILIPOISHIA:

Nilianza kuwatazama mmoja baada ya mwingine, kuanzia mama ambaye uso wake ulikuwa na huzuni kubwa, baba ambaye alionesha kuwa katika tafakuri nzito na ndugu zangu wote ambao walikuwa wamenikodolea macho, kila mmoja akiwa na maswali mengi yasiyo na majibu. Mara mlango wa wodi ulifunguliwa, watu wote wakageuka kutazama ni nani aliyekuwa akiingia kwa kasi kiasi kile.

SASA ENDELEA…

“Shikamooni! Samahani naomba kuuliza eti hii ndiyo wodi aliyolazwa Togo?” alisema mtu huyo lakini kabla hajajibiwa, tayari alikuwa ameshasimama sehemu ambayo ilinifanya mimi na yeye tutazamane.

Moyo wangu ulinilipuka mno kugundua kuwa kumbe alikuwa ni yule msichana tuliyekutana naye kwenye basi na kujenga naye urafiki utafikiri tumejuana miaka kumi iliyopita.

Sikuelewa amejuaje kwamba nilikuwa hospitalini hapo kwa sababu mara ya mwisho alipokuja nyumbani na kunikuta nikiwa na Rahma, tukiondoka kuelekea ufukweni, nilimueleza kwamba tunaenda Coco lakini baadaye tukabadili uelekeo na kuelekea Msasani Beach kwa lengo la kumkwepa.

Kwa harakaharaka, isingewezekana mtu ambaye ametufuata Coco ajue kwamba kumbe tulienda Msasani na kama hiyo haitoshi, ajue kwamba kuna tatizo limetokea na kujua mpaka wodi niliyokuwa nimelazwa. Kengele ya hatari ililia ndani ya kichwa changu.

“Ooh! Ahsante Mungu, Togo… umepatwa na nini baba?” alisema huku akinisogelea pale kitandani lakini baba alimzuia.

“Binti, sidhani kama nakujua. Wewe ni nani?”

“Togo alisema hawafahamiani ila walikaa siti moja kwenye basi tu, hata sijui amefuata nini,” alidakia Rahma na kuzungumza kwa chuki, moyoni nikajisikia vibaya sana kwa sababu kama mtu alikuwa amekuja kwa ajili ya kuniona, achilia mbali utata mkubwa uliokuwa nyuma ya tukio la yeye kujua mahali nilipo, hakupaswa kufanyiwa vile.

“Mruhusuni. Ni rafiki yangu!” nilitamka kwa sauti dhaifu ya kukwamakwama, yakiwa ndiyo maneno yangu ya kwanza kuyatamka tangu niliporejewa na fahamu. Baba akageuka na kunitazama kwa sekunde kadhaa, akageuka na kumtazama yule dada usoni, akageuka na kumtazama Rahma ambaye utulivu ulimuisha.

Akamruhusu anisogelee pale kitandani, huku uso wake ukilengwalengwa na machozi, aliniinamia pale chini kwa heshima.

“Pole baba, nimeona picha ya tukio la wewe kuokolewa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, nikajaribu kuulizia ndiyo nikaambiwa umelazwa hapa. Pole sana,” alisema huku safari hii machozi yakiwa yanamtoka. Nadhani kwa jinsi alivyoonesha kuguswa na hali yangu, hata baba alianza kumkubali kwani nilimsikia akishusha pumzi ndefu.

“Najua hakuna anayeweza kukuelewa ukieleza kilichotokea, nakuombea upone haraka,” alisema msichana huyo na kunifanya nikodoe macho kama fundi saa aliyepoteza nati. Alijuaje kwamba hakuna atakayenielewa nikieleza kilichotokea? Alijuaje kwamba maelezo ya Rahma yalikuwa tofauti kabisa na kile nilichoamini kwamba ndiyo ukweli? Nilijikuta nikichanganyikiwa.

Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, alinibusu kwenye mkono wangu uliokuwa na sindano ya dripu, akageuka na kuwashukuru watu wote kisha kwa heshima kubwa akaondoka zake. Japokuwa mavazi aliyokuwa amevaa yalimtafsiri katika picha nyingine tofauti kabisa, alionesha nidhamu ya hali ya juu mno.

“Huyu ni nani?” swali la baba lilinizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo, akanikazia macho akionesha kuwa na shauku ya kutaka kusikia nitamjibu nini.

“Ni rafiki yangu.”

“Huyu ndiyo mliyekuwa naye kwenye basi?”

“Ndiyo.”

“Na ndiyo aliyekupa simu si ndiyo?”

“Ndiyo.”

“Amejuaje kama umelazwa hapa?”

“Anasema kuwa ameniona kwenye mitandao.”

“Mitandao? Wewe umefikaje kwenye mitandao?” baba alinihoji, huku na yeye akionesha kutokuwa na uelewa wa mambo ya teknolojia kama mimi. Nilimuona baba yake Rahma naye akisogea na kuja kuungana na baba pale pembeni ya kitanda changu.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

“Eti anasema amemuona kwenye mitandao,” alisema baba huku akimgeukia baba yake Rahma.

“Inawezekana, unajua hawa vijana wa siku hizi ni wepesi sana wa kutumia mitandao ya kijamii kama Facebook, WhatsApp na Instagram kwa hiyo tukio lisilo la kawaida likitokea tu, haraka wanapiga picha kwa kutumia simu zao na kuliweka mtandaoni kwa hiyo habari zinasambaa kwa kasi,” alisema baba yake Rahma.

Na mimi nikawa nimepata elimu kidogo maana kiukweli sikuwa najua chochote kuhusu hayo mambo maana kule ‘bush’ kwetu tulichokuwa tunakijua ni redio tu. Muda mfupi baadaye, madaktari waliingia na kuwataka watu wote wawapishe ili waweze kuendelea kunipa huduma.

Madaktari walifurahi kuniona nikiwa na hali ile, wakaanza kuniuliza jinsi nilivyokuwa najisikia. Niliwaambia kwamba nahisi mwili wote umekuwa mzito, kila kiungo hakina nguvu. Waliniambia ni kwa sababu ya kiwango kikubwa cha chumvi nilichokuwa nimekula na mwili kukosa hewa safi kwa muda.

Hata hivyo, waliniambia kwamba hali hiyo ni ya muda tu, mwili utapata nguvu hasa baada ya kumaliza kiwango cha dripu walichonipangia, ambazo zilikuwa zikiendelea kutiririka kwa kasi kuingia mishipani mwangu.

“Kwa hiyo leo naweza kuruhusiwa kutoka?”

“Leoleo utatoka wala usiwe na wasiwasi.”

“Kwani saizi ni saa ngapi?”

“Ni saa moja za jioni,” alisema daktari huku akinipima mapigo ya moyo kwa kutumia kifaa maalum, akarekebisha kasi ya dripu kuingia mwilini mwangu kisha akawa anaandika jambo kwenye faili huku akijadilianana wenzake.

“Kwani wewe hujui kuogelea.”

“Najua vizuri tu.”

“Sasa mbona maji yalikuzidi nguvu? Si vizuri kucheza na maji kama hujui kuogelea vizuri, sawa kijana?” alisema daktari huku akinitazama. Niliamua kukaa kimya maana hata ningeeleza kilichotokea, hakuna ambaye angenielewa. Kwa kifupi ni kwamba ilionesha eti mimi nilikuwa nachezea maji ya baharini ndiyo maana nikazama na kutaka kupoteza maisha.

Hicho ndicho walichokuwa wakikiamini watu wote lakini ukweli nilikuwa nao moyoni mwangu, nikaona njia nzuri ni kunyamaza tu kwa sababu sikuwa napenda kukaa hospitalini, isitoshe hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kulazwa. Kule kijijini kwetu, mtu ukiumwa ilikuwa hakuna kwenda hospitali, baba anamaliza kila kitu yeye mwenyewe.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Kwenye majira ya kama saa tatu za usiku, nilimuona baba na baba yake Rahma wakiingia wodini wakiwa wameongozana na wale madaktari waliokuwa wakinitibu, wakapewa baadhi ya maelekezo kisha wakaja pale kitandani kwangu, daktari mmoja akanichomoa dripu na kuniambia nijaribu kusimama.

Nilifanya hivyo, japokuwa kwa mbali nilikuwa nasikia kizunguzungu, niliweza kusimama vizuri. Wakaniambia nijaribu kutembea hatua chache, nilifanya hivyo na wote waliridhishwa na maendeleo yangu. Yule daktari akawaelekeza akina baba sehemu ya kwenda kulipia, baba yake Rahma akanishika mkono na kuanza kuniongoza kuelekea nje.

Nguo nilizokuwa nimevaa hazikuwa zile nilizovaa wakati nilipotokewa na tukio lile, hata sikukumbuka nani alinibadilisha na alinibadilisha saa ngapi. Nilipotoka nje, niliwakuta ndugu zangu wote wakiwa wamekusanyika, wote wakainuka baada ya kuniona nikitembea kwa kujivuta, wakaja na kunizunguka.

“Unaendeleaje mwanangu,” alisema mama huku akija na kunikumbatia, nikamwambia naendelea vizuri, akaja mama yake Rahma ambaye naye alinikumbatia, akaja dada Sabina, Rahma na wengine wote, kila mtu akawa ananikumbatia na kunipa pole kwa kilichotokea.

Wote wakageuka na kuanza kuniongoza kwenye gari aina ya Toyota Noah lililokuwa eneo la mapokezi, mimi nikasaidiwa kukaa siti ya mbele, pembeni ya dereva, ndugu zangu wengine wote wakakaa nyuma. Kwa sababu ya wingi wao, hawakutosha, ikabidi mama na mama Rahma pamoja na baba zetu wao wapande kwenye teksi iliyokuwa imepaki mbele ya ile Noah tuliyopanda.

Muda mfupi baadaye, dereva aliingia, akanisabahi na kunisaidia kufunga mkanda, kabla hajaondoka nilimuona yule msichana akitokea upande wa pili, akamuonesha dereva ishara kwamba asiondoe kwanza gari, akaja pale kwenye dirisha la siti niliyokuwa nimekaa.

“Togo, vipi unaendeleaje?”

“Naendelea vizuri, namshukuru Mungu.”

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

“Pole sana mpenzi wangu,” alisema, nikiwa bado nashangaa kwa nini ameniita hivyo, alinivuta na kugusanisha mdomo wake na wangu, nikabaki nimeganda kama nimepigwa na shoti ya umeme. Aliponiachia, harakaharaka niligeuka kuangalia kama Rahma hakuwa ameona kitendo hicho, kwa bahati nzuri alikuwa akipiga stori na dada Sabina, kiufupi hakuna aliyeona zaidi ya dereva ambaye naye alizuga kama hajaona kitu.

“Hii ni zawadi maalum kutoka kwako,” alisema huku anikipa bahasha kubwa ya rangi ya pinki, akanibusu kwenye paji la uso kisha akaniachia na kunipungia mkono, akampa ishara dereva kwamba aondoke. Wakati hayo yakiendelea, kumbe baba aliyekuwa amekaa siti ya mbele ya ile teksi iliyokuwa imeshaanza kutoka pale eneo la maegesho, alikuwa akishuhudia kila kilichokuwa kinaendelea.

Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.

Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.

Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”

Je, nini kitafuatia? Usikose Ijumaa kwenye Championi Ijumaa.

Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”

Itaendelea......
 
Sehemu ya ishirini na sita______26




ILIPOISHIA:

Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.

SASA ENDELEA…

Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.

Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”

Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”

“Sasa baba, unajua mimi kuna mambo mengi sana sielewi, halafu nikikuuliza hata hunipi majibu ya kuridhisha.”

“Hilo siyo jibu, umeanza kuwa na kiburi,” alisema baba kwa sauti ya chini lakini akionesha kama alikuwa amepania kuniadhibu. Sikumjibu chochote, akauma meno kwa hasira na kuelekea pale alipokuwa amesimama baba yake rahma, wakawa wanazungumza jambo. Nadhani walikuwa wananijadili.

Kiukweli, uhusiano wangu na baba ulikuwa umeingia doa kubwa na sababu ya yote, ni mambo ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea ambayo yeye alionesha kwamba anajua kila kitu na pengine ndiyo chanzo cha yote. Bado nilikuwa na maswali mengi ambayo alipaswa kunijibu.

Swali la kwanza, nilitaka aniambie kwa nini wanakijiji wenzake kule kijijini kwetu, Chunya walikuwa wakimtuhumu kwamba ni mchawi na ndiye aliyeshiriki kwenye vifo vya watu wawili katika mazingira ya kutatanisha. Kwa macho yangu nilishuhudia akipambana na watu hao kabla ya baadaye kubainika kwamba wamekufa vifo vya ghafla.

Nilitaka aniambie ukweli, yeye ni mganga kama mwenyewe alivyokuwa akijinadi au alikuwa ni mchawi? Nilitaka pia anieleze, aliwezaje kusafiri kutoka Chunya mpaka Dar es Salaam bila kuwemo kwenye basi tulilokuwa tumepanda lakini muda wote akawa anatoke apale panapotokea tatizo, kama alivyotusaidia kuepukana na ajali mbaya zilizotaka kutokea wakati tukisafiri kutoka Chunya kuja Dar, ya kwanza ikiwa ni kwenye eneo hatari la Mlima Nyoka na la pili likiwa ni kwenye Mlima Kitonga.

Nilitaka anieleze vizuri aliwezaje kuniokoa nisigongwe na gari, lakini wakati huohuo watu wengine wote wakawa hawamuoni wala kumsikia zaidi yangu. Nilitaka aniambie, ile dawa aliyonipa niwe namnyunyizia dereva, ilikuwa na maana gani na iliwezaje kutuepusha na ajali?

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Nataka kujua nini kimetokea hapa kwa akina Rahma maana nasikia kabla sisi hatujafika walikuwa wakiishi kwa amani, mbona tangu tuingie, japo ni muda mfupi tu lakini tayari kuna mambo mengi ya ajabu yametokea? Kwa nini naona mambo ambayo watu wengine hawayaoni?”

“Mbona unaongea peke yako Togo?” sauti ya Rahma ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo machungu, nikashtuka sana kugundua kwamba kumbe nilikuwa nikizungumza kwa sauti huku mwenyewe nikidhani nawaza.

“Umesikia nini kwani?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana. Kwa bahati nzuri, kumbe sikuwa nimetamka kwa sauti mambo mengi zaidi ya kujiuliza kwa nini tangu tufike nyumbani kwa akina Rahma mambo mengi ya ajabu yalikuwa yakitokea.

“Kwani unafikiri ujio wenu ndiyo chanzo cha haya yote?” aliniuliza Rahma kwa upole huku akinishika mkono na kunielekeza tuelekee ndani maana nilikuwa nimesimama, nikiwa nimepoteza kabisa mwelekeo.

“Sisi ndiyo chanzo na pengine mimi ndiyo chanzo hasa,” nilisema kwa sauti ya unyonge, Rahma akaniambia kuna jambo zuri anataka tukazungumze chumbani kwake. Nilimkubalia, tulipoingia ndani tulipitiliza mpaka chumbani kwake.

Akina mama ilibidi waanze kuchakarika kwa sababu hata chakula cha usiku hakikuwa kimepikwa siku hiyo kwa sababu ya majanga yaliyonitokea ambapo baada ya kupata taarifa kwamba nipo hospitali nikiwa sijitambui, ilibidi nyumba nzima ije kunijulia hali. Waliingia jikoni huku ndugu zangu na wadogo zake Rahma wakikaa sebuleni kutazama runinga.

Baba na baba Rahma, kama kawaida yao wao walibaki nje wakiendelea na mazungumzo yao.

“Unataka kuniambia nini Rahma,” nilimuuliza kwa upole baada ya kumuona akifunga mlango wa chumbani kwake kwa komeo. Hakujibu kitu zaidi ya kuvua blauzi yake kisha ‘bra’, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, nilijikuta nikisisimka mno. Rahma alikuwa amejaliwa kifua kizuri mno, ambacho kwa mwanaume yeyote aliyekamilika, ilikuwa ni lazima atokwe na udenda kama fisi aliyeona mfupa.

Rahma aliendelea kunikumbatia huku akinibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu kimahaba, hali ambayo ilinichanganya kabisa kichwa changu. Taratibu alinirudisha nyuma mpaka tulipofika kwenye uwanja wa fundi seremala, akanisukumia juu yake kisha akamalizia na za chini zilizokuwa zimesalia.

Akionesha kuwa na papara za hali ya juu, alihamia kwangu na kuitoa ya juu, nikabaki kifua wazi, akahamia na ile ya chini na muda mfupi baadaye, tulikuwa ‘saresare’ maua. Bado mwili wangu haukuwa na nguvu kwa hiyo nilimuachia yeye ndiye awe ‘dairekta’ wa filamu ile ya kusisimua na kweli alikitendea haki cheo nilichompa.

Kwa ufanisi wa hali ya juu, Rahma aliitii kiu yangu, mpaka anashuka kutoka juu ya mnazi, alikuwa ameshaangua madafu kadhaa, akajitupa upande wa pili huku akinishukuru, na mimi nikawa namshukuru. Hatukuchukua raundi, kila mmoja akapitiwa na usingizi mzito.

Nadhani wangu ulikuwa mzito zaidi kwa sababu kuichwa changu kilikuwa kimebeba mambo mazito mno na alichonipa rahma ilikuwa sawa na dawa ya usingizi. Tulikuja kushtuka baadaye baada ya kusikia mlango wa chumba cha Rahma ukigongwa. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikamuamsha Rahma ambaye aliamka kichovu na kusogea karibu na mlango.

Safari hii hatukuwa na hofu tena kwani tulikuwa na ruhusa ya kukaa pamoja karibu, mimi kazi yangu ikiwa ni kuhakikisha rahma harudii tena kujaribu kuyakatisha maisha yake na Rahma kuhakikisha ananisaidia mimi mgonjwa.

“Unasemaje?”

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Mama anauliza kama mtakula na sisi au mletewe chakula chenu huku.”

‘Ngoja nakuja mwenyewe,” alijibu Rahma wakati akizungumza na mdogo wake aliyetumwa na mama yao kuwaulizia.

‘Eti mpenzi wangu, we unapenda tukakae sebuleni au tulie hukuhuku chumbani.”

‘Utakavbyosema wewe hamna shida ila napenda zaidi tukikaa peke yetu,” nilimjibu, akanitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yameelemewa na usingizi kisha akaachia tabasamu la kichovu.

“Ngoja nikaonge kwanza,” alisema na kuchukua kitenge, akaelekea bafuni na muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amechangamka kidogo. Ilibidi na mimi niende kuoga wakati yeye akihangaikia chakula.

Niliporudi kutoka bafuni, tayari rahma alikuwa ameleta chakula kizuri kule chumbani. Tofauti ya vyakula tulivyozoea kula kijijini na mjini ilikuwa kubwa mno. Chakula kilipikwa vizuri, yaani kwa kukitazama tu ilikuwa ni lazima mate yakutoke. Tulinawa vizuri lakini nilipotaka kuanza kula, Rahma alinikatazana na kusema anataka anilishe kidogo.

Yalikuwa ni mambo mageni kabisa, nilizoea kuona watoto wadogo au wagonjwa ambao wako mahtuti ndiyo wanalishwa, lakini eti dume mimi nilishwe? Hata hivyo sikumkatalia. Akaanza kunilisha kwa upole, huku mara kwa mara akinitazama machoni. Sijui nini kilimtokea Rahma lakini alionesha kunipenda sana, tena sana.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Mara kwa mara alikuwa akinibusu na kuniambia kwamba ananipenda sana, mpaka nikawa najisikia aibu. Sikuwa najua kabisa mambo ya kikubwa na wala sikuwa na uelewa wowote wa mahaba. Nilikuwa nikisikiasikia kwamba watu wa pwani ndiyo wataalamu wa hayo mambo.

Japo Rahma alikuwa akinilisha matonge madogo tofauti na niliyozoea lakini kiukweli nikiri kwamba nilijisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu. Tulipomaliza kula, alitoa vyombo, akaja kufanya usafi kisha akafunga tena mlango.

“Itabidi mimi nikalale chumbani kwangu,” nilimwambia Rahma lakini akakataa katakata, akaniambia tutalala wote humo chumbani kwake na tutajifunika shuka moja. Japokuwa kwa nje nilikuwa navunga, ukweli ni kwamba hata mimi nilikuwa napenda sana kuwa karibu na Rahma hasa kutokana na mapenzi ya dhati aliyokuwa ananionesha.

Ile tofauti ya umri kati yetu sikuiona tena, namimi nikawa najiona mkubwa kama yeye, hata ile harufu ya undugu kati yetu nayo ilitoweka kabisa, ndani ya muda mfupi tu tuliokaa pamoja ikawa utafikiri tumeishi pamoja kwa miaka mingi tangu zamani.

Tulipiga stori za hapa na pale, baadaye muda wa kulala ulipofika, kama ilivyokuwa mara ya kwanza, Rahma aliniganda kama ruba, tukapeana tende na halua kwa mara nyingine kabla ya kupitiwa na usingizi mzito, akiwa ameniganda kifuani kama ruba.

Nilikuja kuzinduka usiku wa manane baada ya kuhisi hali isiyo ya kawaida. Kilichoniamsha, zilikuwa ni kelele za paka waliokuwa wakipigana juu ya paa, huku wakitoa milio ya ajabu kama watoto wachanga.

Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya ishirini na Saba_______27




ILIPOISHIA:

Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.

SASA ENDELEA…

Nilikaza macho kwenye giza kujaribu kuangalia ni kitu gani hicho kilichodondoka, kwa mbali nikaanza kuona kama mtu amepiga magoti kwenye kona ya chumba hicho, taratibu akaanza kuinuka, nikazidi kumkazia macho na kadiri muda ulivyokuwa ukizonga ndivyo nilivyozidi kuiona vizuri taswira yake.

Nilimtambua kwamba ni mwanamke kutokana na maumbile yake ingawa alionesha kuwa ni mzee kwani niliweza kuiona ngozi yake ilivyokuwa imekunjamana, nikamkazia macho usoni nikitaka niione sura yake. Hata hivyo eneo la usoni lilikuwa na giza sana, nikamuona akiinua mikono juu kama anayetoa ishara fulani, akageuka na kuanza kujisugua makalio yake ukutani.

Mara nilisikia kishindo kingine, hofu ikazidi kutanda ndani ya moyo wangu, kijasho chembamba kikawa kinanitoka huku nikiwa nimekodoa macho kwa nguvu zote.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Nilitamani niamke nikawashe taa lakini ujasiri huo sikuwa nao, nilitamani niingie chini ya kitanda lakini mwili wote haukuwa na nguvu, nilitamani kupiga kelele kuwaamsha nyumba nzima lakini sikuwa na uwezo huo, nikawa natetemeka kuliko kawaida.

Nilipotazama kwa makini pale chini, nilimuona mtu mwingine kama yule wa kwanza naye akiinuka taratibu lakini tofauti yake, huyu alikuwa mwanaume kutokana na jinsi mwili wake ulivyokuwa na alionesha pia kuwa mzee zaidi maana mpaka mgongo wake ulikuwa umepinda.

Alipoinuka, naye alisogea ukutani na kuanza ‘kusonta’ ukutani kwa kutumia makalio yake kisha akasogea mbele na kushikama mikono na yule mwanamke wa kwanza, wakaiinua juu na kutoa ishara ambayo sikuielewa, mara nikasikia vishindo mfululizo.

Vilisikika vishindo kama sita hivi, ikimaanisha kwamba watu wengine sita walikuwa wameingia, uzalendo ukanishinda. Sijui nilipata wapi ujasiri, nikasimama wima kisha nikapaza sauti, ‘tokeni hapa washenzi nyie, hata mimi baba yangu ni mchawi vilevile’.

Kauli yangu ni kama iliwashtua watu wale wa ajabu ambao hata sielewi niwaelezeeje, wote wakashtuka na kunitazama, nikazidi kushtuka baada ya kuona wote macho yao yalikuwa yakiwaka kama mnyama mkali gizani.

Kwa wale ambao wameishi maeneo ya maporini watakuwa wananielewa kwamba mida ya usiku, wanyama kama simba, chui, mbwa mwitu au hata mbwa wa kawaida na paka, wakiwa kwenye giza totoro kisha wakakukodolea macho yao, huwa yanatoa mwanga fulani wa kutisha.

Kwa jinsi walivyonitazama, hofu ilinizidi maradufu lakini nikaona hakuna kingine cha kufanya zaidi ya kuendelea ‘kugangamala’. Sikuwa najua kama wakinigeukia nitafanya nini, sikuwa najua mbinu zozote za kupambana nao na eti nilijikuta nikijilaumu kwa nini baba hakunifundisha au hakunipa mbinu yoyote ya kukabiliana na wachawi.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Yule mwanamke aliyekuwa wa kwanza kuingia mle ndani, nilimuona akinisogelea huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya woga. Nilihisi haja ndogo ikitaka kunitoka lakini nilijikaza kiume na kusema liwalo na liwe, akanisogelea jirani kabisa huku akiendelea kunitazama kwa macho yake makali, cha ajabu, licha ya kunisogelea, sikuweza kabisa kuitambua sura yake.

Nimewahi kusikia kwamba wachawi wana kawaida ya kula nyama za watu, nikahisi na mimi usiku huo nakwenda kuliwa huku nikijiona. Niliujutia uamuzi wangu wa kusimama na kuwafokea watu hao, nikiwa bado natetemeka, nilisikia kofi moja zito likitua kwenye shavu langu la kushoto, maumivui niliyoyasikia yalikuwa hayaelezeki, nikapiga kelele kwa nguvu nikimuita baba.

Sikumbuki kama nimewahi kutoa sauti kubwa kama hiyo maishani mwangu, mara mlango ukaanza kugongwa kwa nguvu nje, nikasikia kibao kingine kikitua kwenye shavu la upande wa pili, likafuatiwa na misonyo mingi kisha wale watu wakayeyuka wote na kupotea kama moshi upoteavyo angani.

“Togo! Nini kimetokea?” alisema baba baada ya kuwa amefanikiwa kufungua mlango na kuwasha taa. Jambo la aibu ni kwamba baada ya ule mchezo wa kikubwa niliocheza na Rahma, hakuna aliyekumbuka tena kuvaa nguo zake kwa hiyo nilikuwa kama nilivyozaliwa, baba akanitazama kwa mshangao.

Najua alishangazwa na mambo mengi kwa wakati mmoja, kwanza kwa nini nilikuwa chumbani kwa Rahma mpaka usiku huo wakati makubaliano yalikuwa ni kwamba kila mmoja atalala kwake, kwa maana kwamba baada ya c hakula ilitakiwa mimi nitoke na kwenda kwenye chumba nilichopangiwa lakini sikufanya hivyo. Yote tisa, kumi ni kwamba nilikuwa kama nilivyozaliwa, na Rahma naye ambaye bado alikuwa kwenye usingizi mzito, akikoroma bila kujua chochote kilichokuwa kinaendelea, hakuwa na chochote mwilini, nikamuona baba akishusha pumzi ndefu na kunipa ishara kwamba nivae kwanza nguo, akatoka na kuurudisha mlango.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Kumbe sekeseke hilo lilisababisha nitokwe na haja ndogo bila kujua, ikabidi nichukue tambara la kufanyia usafi na kufuta harakaharaka huku nikigeuka kumtazama Rahma asije kuwa ameamka na kuona nilichokifanya. Nilipomaliza kufuta, harakaharaka nilivaa nguo zangu huku nikitetemeka kuliko kawaida.

Baba alikuwa pale mlangoni akinisubiri, nilipomaliza aliingia na kunionesha ishara kwamba nisizungumze kwa sauti ya juu, akaniuliza nini kilichotokea.

“Wachawi baba, wachawi wengi wamekuja, angalia walivyonifanya,” nilisema huku nikimuonesha mashavu yangu ambayo nilikuwa nahisi kama yanawaka moto. Awali niliona baba hataki kuamini kama ambavyo imekuwa kawaida yake mara kwa mara ninapotokewa na mambo kama hayo lakini nashukuru safari hii kulikuwa na ushahidi wa moja kwa moja.

“Mungu wangu, umefanya nini?”

“Wamenipiga,” nilisema huku nikianza kutokwa na machozi.

“Hebu niambie ukweli, umefanya tena mapenzi na Rahma?”

“Ndiyo.”

“Lakini si tumeshawakataza nyie na kuwasisitiza kwamba msirudie ujinga wenu?” baba alizungumza kwa hasira lakini kwa sauti ya chini. Sikujua kwa nini alikuwa akizungumza kwa sauti ya chini, akanishika mkono na kufungua mlango, akatazama huku na kule na alipojiridhisha, alinipeleka mpaka kwenye chumba ambacho ndicho nilichotakiwa kulala.

“Hutakiwi kumwambia yeyote kuhusu hiki kilichotokea, umenielewa?” baba aliniambia, nikatingisha kichwa lakini nilijiuliza, kama yeye ameweza kusikia zile kelele nilizopiga, si ina maana nyumba nzima wamesikia? Na kama wamesikia, kwa nini wengine wote hawakuamka isipokuwa yeye tu?

“Lakini kwa nini haya yanatokea?” utajua tu lakini unachoniudhi ni kwamba ukiambiwa jambo fulani usilifanye, wewe ndiyo unalifanya. Hukuwa na mambo ya wanawake kabisa lakini tangu tumefika hapa ndiyo umekuwa mchezo wako… utasababisha vifo vya wasio na hatia kwa nini unakuwa mgumu kuelewa?” baba alisema, safari hii siyo kwa ukali bali kwa hisia za ndano kabisa, kauli yake ikanishtua mno.

Yaani mimi ndiyo nisababishe vifo vya wasio na hatia? Kivipi? Halafu kulikuwa na uhusiano gani wa mimi kulala na Rahma na hayo yaliyokuwa yanatokea? Katika yote, jambo ambalo nilijiapiza, ni kwamba kamwe sitamuacha Rahma maana alikuwa amenionesha dunia ya tofauti mno.

Baba alitoa kichupa kilichokuwa na unga mweusi lakini kabla hajafanya chochote, aliniambia nikajitazame kwenye kioo kilichokuwa humo chumbani.

“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko usio wa kawaida.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya ishirini na nane________28




ILIPOISHIA:
Baba alitoa kichupa kilichokuwa na unga mweusi lakini kabla hajafanya chochote, aliniambia nikajitazame kwenye kioo kilichokuwa humo chumbani.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko usio wa kawaida.
SASA ENDELEA...
Uso wangu ulikuwa umebadilika na kuwa mweusi tii kama mkaa. Kilichoonekana ilikuwa ni macho na meno tu. Nilishindwa kuelewa kwa nini mimebadilika na kuwa vile, sikujua kama ni yale makofi ya nguvu niliyopigwa au ni nini.
“Usishtuke, na huo mchezo wako ukiendelea nao yatakufika makubwa zaidi, yaani unaonekana umeonja asali na sasa unataka kuchonga mzinga kabisa. Hukuwa na mambo ya kupenda wanawake, nini kimekusibu?” alisema baba lakini maneno yake yaliingilia sikio moja na kutokea jingine.
Akili yangu ilikuwa ikiwaza kuhusu mabadiliko yaliyotokea kwenye uso wangu. Nilishindwa kuelewa itakuwaje kama nitaendelea kuwa hivyo, nilijikuta nikiishiwa nguvu kabisa, nikakaa chini huku hofu kubwa ikiwa imetanda moyoni mwangu.
“Si naongea na wewe?” alinihoji baba huku akiwa amekishika kile kichupa, sikumjibu chochote kwa sababu akili yangu ilikuwa ikiwaza mambo mengine tofauti kabisa. Suala la kuacha kufaidi penzi la Rahma halikuwepo kabisa kichwani mwangu, kwa sababu hata wao wenyewe walijaribu kulizuia lakini kilichotokea kila mmoja akawa shahidi.

“Hebu inuka,” alisema baba kwa jazba, nadhani ni baada ya kuona simpi ushirikiano. Nilisimama, akatoa wembe kwenye mfuko wa mbele wa shati yake, akanichanja kwenye paji la uso, juu kidogo ya sehemu nywele zinapoanzia.
Akanipaka ile dawa, yaani kwa jinsi ilivyokuwa inauma, nilishindwa kujizuia, nikawa napiga kelele, baba akanikamata na kuniziba mdomo huku akinionesha ishara ya kunyamaza.
“Inatakiwa ujikaze, halafu hakikisha asubuhi hakuna mtu yeyote anayejua kilichotokea, ni mambo ya aibu sana na yatatusababishia matatizo makubwa, si unajua ndiyo kwanza tumefika na hapa ni kwa watu?”
“Nataka kujua wale ni akina nani na wametoka wapi? Kwa nini wameingia chumbani kwa Rahma?”
“Nitakujibu lakini siyo leo,” alisema baba huku akinisisitiza kwamba nilale na nisiende tena chumbani kwa Rahma. Hakuna jambo ambalo lilikuwa likinikera kwa baba kama kila ninapomuuliza kuhusu mauzauza yanayonitokea yeye anakimbilia tu kusema kwamba atanijibu. Alitoka na kurudia kunisisitiza kwamba nisitoke na asubuhi nisimwambie yeyote kuhusu kilichotokea.
“Na huu uso itakuwaje?”
“Hiyo dawa niliyokupaka itakusaidia, mtu yeyote akikuuliza mwambie umeamka tu asubuhi na kujikuta ukiwa hivyo,” alisema. Nikasogea tena kwenye kioo na kujitazama. Yaani hata sikujua kama asubuhi kukipambazuka halafu nikawa bado kwenye hali hiyo itakuwaje maana kiukweli nilikuwa natisha.
Kwenye upande wa shavu la kushoto na kulia, kulikuwa na alama za vidole za yule bibi kizee sehemu aliponipiga makofi, nikaapa siku nitakayomjua halafu nikakutana naye barabarani, lazima na mimi nimlipizie.
Nilijaribu kujilaza kitandani lakini usingizi haukuja kabisa, mara kwa mara nilikuwa nikisikia vishindo vikubwa juu ya bati kama kuna watu wanapigana, huku wakati mwingine sauti za ajabu zikisikika. Nilikuja kupata usingizi wakati kumeshaanza kupambazuka kabisa.
Kwa kuhofia kwamba ndugu yangu akiamka anaweza kuniona nilivyokuwa natisha usoni, nilijifunika ‘gubigubi’. Nilimsikia akijiongelesha kama aliyeshtuka kuniona nimelala pembeni yake wakati hakumbuki usiku niliingia saa ngapi.
“Unaendeleaje Togo,” aliniuliza lakini nilijikausha na kujifanya nimepitiwa na usingizi.
“Togoo!” aliniita huku akivuta shuka kwa nguvu. Kwa kuwa sikutegemea tukio hilo, alifanikiwa kunifunua na mimi bila hata kufikiri mara mbili, nikaamka kwa hasira, tukawa tunatazamana.
“Mbonaunapenda kunisumbua wakati unajua mwenzio naumwa?”
“Hee... huko usoni umefanya nini?” aliniuliza huku akirudi nyuma kwa hofu, akafungua mlango na kutoka mbio. Nilijikuta nikikosa amani mno, ikabidi nisogee na kujitazama tena kwenye kioo. Bado uso wangu haukuwa umerudi kwenye hali yake.

Japokuwa ule weusi kidogo ulikuwa umepungua lakini bado mtu yeyote asingeweza kunitazama usono bila kushtuka. Pia mashavu yote mawili yalikuwa yamevimba huku damu ikiwa imevilia kwenye zile alama za vidole na kwenye jicho langu la kushoto.
“Eti kuna nini,” baba alisema huku akifungua mlango. Kumbe kutokana na mshtuko alioupata alikuwa amekimbia na kwenda kumuita baba.
“Huyu mjinga eti mimi nimelala yeye ananivuta shuka,” nilisema huku nikikwepa kutazamana usoni na baba. Aliligundua hilo, akanilazimisha nimuangalie.
“hebu ngoja nakuja, na wewe acha ujinga wa kupigapiga kelele, inamaana hujui kama mwenzenu anaumwa,” alisema baba kwa kumkaripia yule ndugu yangu, nikamuona ‘limemshuka’ maana alitegemea baba atashtuka kama yeye.
“Kwanza ondoka muache apumzike,” alisema baba, ikabidi atoke naye, nikajilaza tena kitandani nakujifunika vizuri. Nikawa naendelea kutafakari mambo mengi yasiyo na majibu. Muda mfupi baadaye, baba alirejea akiwa na kimkoba chake kidogo, akaniamcha na kunitaka nifanye kama anavyoniambia.
Kuna kimzizi fulani alikitoa kwenye mkoba wake, akipa na kuniambia nikitafune lakini nisimeze mate. Nilipokitia mdomoni, niligundua kwamba kilikuwa kichungu sana, nikakitafuna huku nikiwa nimekunja sura.
‘Temea mate kwenye mkono wako wa kushoto na ujipake kwenye shavu la kulia,” alisema huku akinisisitiza kuwa makini. Nilifanya hivyo, nikajipaka kwenye shavu na kuhisi kama moto unawaka. Tema mengine kwenye mkono wa kulia na ujipake kwenye shavu la kushoto,” aliniambia, nikafanya hivyo, maumivu yakazidi ikuongezeka, nikawa nahisi kama ngozi ya sura inajaa kama puto.

“Nifuate,” alisema, akafungua mlango na kuelekea bafuni, nikamfuata ambapo alinielekeza namna ya kusimama kisha akafungulia maji na kuanza kunimwagia kichwa kizima huku akinisugua na kunipaka ungaunga mwingine uliokuwa na ladha kama magadi.
Alinisafisha kwa muda mrefu kisha akatoa kipande cha kitambaa na kunifuta, akaniambia nisifumbue macho mpaka atakaponiambia. Alinishika mkono na kunirudisha chumbani, akanilaza kitandani na kuniambia nifumbue macho.
“Inabidi ulale hivyo kwa dakika saba, zikiisha amka halafu ujitazame tena kwenye kioo,” aliniambia baba, akakusanya vitu vyake na kuondoka. Nikawa nasubiri hizo dakika saba ziishe maana aliniambia atakuja mwenyewe kuniambia. Baba alikuwa na mambo mengi sana yenye utata, hasa huo ujuzi wake wa mitishamba na dawa za kiganga.
Nililala pale kitandani lakini kwa mbali nilianza kujihisi hali fulani hivi isiyo ya kawaida. Sikutaka kuitilia maanani kwani bado uso wangu ulikuwa ukiwaka moto kwa maumivu. Dakika saba baadaye, kweli baba alirudi na kuniamsha, nikasogea na kujitazama kwenye kioo. Huwezi kuamini, uso wangu ulikuwa umerudi kwenye hali yake ya kawaida ingawa jicho moja bado lilibaki limevilia damu na zile alama za vidole mashavuni zenyewe hazikufutika.
Alitoka na kuniacha mwenyewe, angalau moyo wangu ukawa na amani. Nilisimama kwa muda pale mbele ya kioo nikiendelea kujitazama. Ile hali sasa ilizidi kunisumbua na kunifanya nijisikie vibaya. Yaani kwa jinsi nilivyokuwa najisikia, ilikuwa ni kama nimeshikwa na kiu kali lakini tofauti na kiu ya kawaida, ilikuwa ni kiu ya kukutana kimwili na mwanamke.

Nilibaki nikijishangaa mwenyewe kwani kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele ndivyo nilivyokuwa nikizidi kuteseka. Wakati nikiendelea kuugulia ndani kwa ndani, nilishangaa kwa nini rahma mpaka muda huo hakuwa amekuja kuniuliza nimeamkaje na hata sauti yake sikuisikia. Japokuwa baba alikuwa amenikanya sana, kwa jinsi hali ilivyokuwa, niliamini yeye ndiye anayeweza kuwa msaada kwangu kwa sababu tunapendana.
Nilitoka na kusogea kwenye mlango wa chumbani kwake lakini kabla sijashika kitasa, nilisikia sauti ya mdogo wake wa kiume akiniambia kwamba hakuwepo, alikuwa ameondoka na mama yake asubuhi na mapema kufuatilia mambo ya chuo. Ni kweli jana yake alikuwa amenidokeza kuhusu suala hilo lakini sijui kwa nini sikukumbuka. Nilijikuta nikiishiwa nguvu kwani sikujua nini kitafuatia.
Nilirudi chumbani kwangu huku hali ikizidi kuwa mbaya, sijui ni machale gani yalimcheza baba, mara akafungua mlango na kunikuta nikiwa kwenye hali ambayo haielezeki.
“Ule mzizi niliokupa na kukwambia uutafune lakini usimeze, ulifanya kama nilivyokwambia?” baba aliniuliza. Kiukweli baada ya kutema mate kwenye mkono wa kushoto na kulia, mengine yaliyobakia, pamoja na mabaki ya mzizi wenyewe, nilivimeza vyote. Nilipomwambia hivyo baba, alishtuka kuliko kawaida. Sikujua kwa nini ameshtuka kiasi hicho, akatoka haraka.
Nikiwa bado naendelea kuugulia, nilisikia ndugu yangu mmoja akiniita kutokea dirishani, nikafunua pazia na kuchungulia nje. Sikuyaamini macho yangu baada ya kumuona akiwa na yule msichana tuliyesafiri naye, harakaharaka nikafungua dirisha huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.
Je, nini kitafuatia? Usikose
 
Sehemu ya ishirini na nane________28




ILIPOISHIA:
Baba alitoa kichupa kilichokuwa na unga mweusi lakini kabla hajafanya chochote, aliniambia nikajitazame kwenye kioo kilichokuwa humo chumbani.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko usio wa kawaida.
SASA ENDELEA...
Uso wangu ulikuwa umebadilika na kuwa mweusi tii kama mkaa. Kilichoonekana ilikuwa ni macho na meno tu. Nilishindwa kuelewa kwa nini mimebadilika na kuwa vile, sikujua kama ni yale makofi ya nguvu niliyopigwa au ni nini.
“Usishtuke, na huo mchezo wako ukiendelea nao yatakufika makubwa zaidi, yaani unaonekana umeonja asali na sasa unataka kuchonga mzinga kabisa. Hukuwa na mambo ya kupenda wanawake, nini kimekusibu?” alisema baba lakini maneno yake yaliingilia sikio moja na kutokea jingine.
Akili yangu ilikuwa ikiwaza kuhusu mabadiliko yaliyotokea kwenye uso wangu. Nilishindwa kuelewa itakuwaje kama nitaendelea kuwa hivyo, nilijikuta nikiishiwa nguvu kabisa, nikakaa chini huku hofu kubwa ikiwa imetanda moyoni mwangu.
“Si naongea na wewe?” alinihoji baba huku akiwa amekishika kile kichupa, sikumjibu chochote kwa sababu akili yangu ilikuwa ikiwaza mambo mengine tofauti kabisa. Suala la kuacha kufaidi penzi la Rahma halikuwepo kabisa kichwani mwangu, kwa sababu hata wao wenyewe walijaribu kulizuia lakini kilichotokea kila mmoja akawa shahidi.

“Hebu inuka,” alisema baba kwa jazba, nadhani ni baada ya kuona simpi ushirikiano. Nilisimama, akatoa wembe kwenye mfuko wa mbele wa shati yake, akanichanja kwenye paji la uso, juu kidogo ya sehemu nywele zinapoanzia.
Akanipaka ile dawa, yaani kwa jinsi ilivyokuwa inauma, nilishindwa kujizuia, nikawa napiga kelele, baba akanikamata na kuniziba mdomo huku akinionesha ishara ya kunyamaza.
“Inatakiwa ujikaze, halafu hakikisha asubuhi hakuna mtu yeyote anayejua kilichotokea, ni mambo ya aibu sana na yatatusababishia matatizo makubwa, si unajua ndiyo kwanza tumefika na hapa ni kwa watu?”
“Nataka kujua wale ni akina nani na wametoka wapi? Kwa nini wameingia chumbani kwa Rahma?”
“Nitakujibu lakini siyo leo,” alisema baba huku akinisisitiza kwamba nilale na nisiende tena chumbani kwa Rahma. Hakuna jambo ambalo lilikuwa likinikera kwa baba kama kila ninapomuuliza kuhusu mauzauza yanayonitokea yeye anakimbilia tu kusema kwamba atanijibu. Alitoka na kurudia kunisisitiza kwamba nisitoke na asubuhi nisimwambie yeyote kuhusu kilichotokea.
“Na huu uso itakuwaje?”
“Hiyo dawa niliyokupaka itakusaidia, mtu yeyote akikuuliza mwambie umeamka tu asubuhi na kujikuta ukiwa hivyo,” alisema. Nikasogea tena kwenye kioo na kujitazama. Yaani hata sikujua kama asubuhi kukipambazuka halafu nikawa bado kwenye hali hiyo itakuwaje maana kiukweli nilikuwa natisha.
Kwenye upande wa shavu la kushoto na kulia, kulikuwa na alama za vidole za yule bibi kizee sehemu aliponipiga makofi, nikaapa siku nitakayomjua halafu nikakutana naye barabarani, lazima na mimi nimlipizie.
Nilijaribu kujilaza kitandani lakini usingizi haukuja kabisa, mara kwa mara nilikuwa nikisikia vishindo vikubwa juu ya bati kama kuna watu wanapigana, huku wakati mwingine sauti za ajabu zikisikika. Nilikuja kupata usingizi wakati kumeshaanza kupambazuka kabisa.
Kwa kuhofia kwamba ndugu yangu akiamka anaweza kuniona nilivyokuwa natisha usoni, nilijifunika ‘gubigubi’. Nilimsikia akijiongelesha kama aliyeshtuka kuniona nimelala pembeni yake wakati hakumbuki usiku niliingia saa ngapi.
“Unaendeleaje Togo,” aliniuliza lakini nilijikausha na kujifanya nimepitiwa na usingizi.
“Togoo!” aliniita huku akivuta shuka kwa nguvu. Kwa kuwa sikutegemea tukio hilo, alifanikiwa kunifunua na mimi bila hata kufikiri mara mbili, nikaamka kwa hasira, tukawa tunatazamana.
“Mbonaunapenda kunisumbua wakati unajua mwenzio naumwa?”
“Hee... huko usoni umefanya nini?” aliniuliza huku akirudi nyuma kwa hofu, akafungua mlango na kutoka mbio. Nilijikuta nikikosa amani mno, ikabidi nisogee na kujitazama tena kwenye kioo. Bado uso wangu haukuwa umerudi kwenye hali yake.

Japokuwa ule weusi kidogo ulikuwa umepungua lakini bado mtu yeyote asingeweza kunitazama usono bila kushtuka. Pia mashavu yote mawili yalikuwa yamevimba huku damu ikiwa imevilia kwenye zile alama za vidole na kwenye jicho langu la kushoto.
“Eti kuna nini,” baba alisema huku akifungua mlango. Kumbe kutokana na mshtuko alioupata alikuwa amekimbia na kwenda kumuita baba.
“Huyu mjinga eti mimi nimelala yeye ananivuta shuka,” nilisema huku nikikwepa kutazamana usoni na baba. Aliligundua hilo, akanilazimisha nimuangalie.
“hebu ngoja nakuja, na wewe acha ujinga wa kupigapiga kelele, inamaana hujui kama mwenzenu anaumwa,” alisema baba kwa kumkaripia yule ndugu yangu, nikamuona ‘limemshuka’ maana alitegemea baba atashtuka kama yeye.
“Kwanza ondoka muache apumzike,” alisema baba, ikabidi atoke naye, nikajilaza tena kitandani nakujifunika vizuri. Nikawa naendelea kutafakari mambo mengi yasiyo na majibu. Muda mfupi baadaye, baba alirejea akiwa na kimkoba chake kidogo, akaniamcha na kunitaka nifanye kama anavyoniambia.
Kuna kimzizi fulani alikitoa kwenye mkoba wake, akipa na kuniambia nikitafune lakini nisimeze mate. Nilipokitia mdomoni, niligundua kwamba kilikuwa kichungu sana, nikakitafuna huku nikiwa nimekunja sura.
‘Temea mate kwenye mkono wako wa kushoto na ujipake kwenye shavu la kulia,” alisema huku akinisisitiza kuwa makini. Nilifanya hivyo, nikajipaka kwenye shavu na kuhisi kama moto unawaka. Tema mengine kwenye mkono wa kulia na ujipake kwenye shavu la kushoto,” aliniambia, nikafanya hivyo, maumivu yakazidi ikuongezeka, nikawa nahisi kama ngozi ya sura inajaa kama puto.

“Nifuate,” alisema, akafungua mlango na kuelekea bafuni, nikamfuata ambapo alinielekeza namna ya kusimama kisha akafungulia maji na kuanza kunimwagia kichwa kizima huku akinisugua na kunipaka ungaunga mwingine uliokuwa na ladha kama magadi.
Alinisafisha kwa muda mrefu kisha akatoa kipande cha kitambaa na kunifuta, akaniambia nisifumbue macho mpaka atakaponiambia. Alinishika mkono na kunirudisha chumbani, akanilaza kitandani na kuniambia nifumbue macho.
“Inabidi ulale hivyo kwa dakika saba, zikiisha amka halafu ujitazame tena kwenye kioo,” aliniambia baba, akakusanya vitu vyake na kuondoka. Nikawa nasubiri hizo dakika saba ziishe maana aliniambia atakuja mwenyewe kuniambia. Baba alikuwa na mambo mengi sana yenye utata, hasa huo ujuzi wake wa mitishamba na dawa za kiganga.
Nililala pale kitandani lakini kwa mbali nilianza kujihisi hali fulani hivi isiyo ya kawaida. Sikutaka kuitilia maanani kwani bado uso wangu ulikuwa ukiwaka moto kwa maumivu. Dakika saba baadaye, kweli baba alirudi na kuniamsha, nikasogea na kujitazama kwenye kioo. Huwezi kuamini, uso wangu ulikuwa umerudi kwenye hali yake ya kawaida ingawa jicho moja bado lilibaki limevilia damu na zile alama za vidole mashavuni zenyewe hazikufutika.
Alitoka na kuniacha mwenyewe, angalau moyo wangu ukawa na amani. Nilisimama kwa muda pale mbele ya kioo nikiendelea kujitazama. Ile hali sasa ilizidi kunisumbua na kunifanya nijisikie vibaya. Yaani kwa jinsi nilivyokuwa najisikia, ilikuwa ni kama nimeshikwa na kiu kali lakini tofauti na kiu ya kawaida, ilikuwa ni kiu ya kukutana kimwili na mwanamke.

Nilibaki nikijishangaa mwenyewe kwani kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele ndivyo nilivyokuwa nikizidi kuteseka. Wakati nikiendelea kuugulia ndani kwa ndani, nilishangaa kwa nini rahma mpaka muda huo hakuwa amekuja kuniuliza nimeamkaje na hata sauti yake sikuisikia. Japokuwa baba alikuwa amenikanya sana, kwa jinsi hali ilivyokuwa, niliamini yeye ndiye anayeweza kuwa msaada kwangu kwa sababu tunapendana.
Nilitoka na kusogea kwenye mlango wa chumbani kwake lakini kabla sijashika kitasa, nilisikia sauti ya mdogo wake wa kiume akiniambia kwamba hakuwepo, alikuwa ameondoka na mama yake asubuhi na mapema kufuatilia mambo ya chuo. Ni kweli jana yake alikuwa amenidokeza kuhusu suala hilo lakini sijui kwa nini sikukumbuka. Nilijikuta nikiishiwa nguvu kwani sikujua nini kitafuatia.
Nilirudi chumbani kwangu huku hali ikizidi kuwa mbaya, sijui ni machale gani yalimcheza baba, mara akafungua mlango na kunikuta nikiwa kwenye hali ambayo haielezeki.
“Ule mzizi niliokupa na kukwambia uutafune lakini usimeze, ulifanya kama nilivyokwambia?” baba aliniuliza. Kiukweli baada ya kutema mate kwenye mkono wa kushoto na kulia, mengine yaliyobakia, pamoja na mabaki ya mzizi wenyewe, nilivimeza vyote. Nilipomwambia hivyo baba, alishtuka kuliko kawaida. Sikujua kwa nini ameshtuka kiasi hicho, akatoka haraka.
Nikiwa bado naendelea kuugulia, nilisikia ndugu yangu mmoja akiniita kutokea dirishani, nikafunua pazia na kuchungulia nje. Sikuyaamini macho yangu baada ya kumuona akiwa na yule msichana tuliyesafiri naye, harakaharaka nikafungua dirisha huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.
Je, nini kitafuatia? Usikose
Hilo toto si angebadilishana kwa gunia mbili za mkaa tu.
 
Back
Top Bottom