Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Sehemu ya 58


ILIPOISHIA:

Sikuyaamini macho yangu kugundua kwamba tulikuwa Mlandizi, tena jirani kabisa na pale ile ajali ilipotokea. Nilipotazama upande wa pili wa barabara, niliwaona watu wengi wakiwa wamekaa na kuuzunguka moto, pale kwenye ile nyumba iliyokuwa na msiba wa kwanza wa yule mtoto, moyo ukashtuka sana nikikumbuka kilichotokea.

“Mbona umeshtuka,” baba aliniuliza.

SASA ENDELEA…

Sikumjibu zaidi ya kumuonesha kidole kwenye ile nyumba ambapo bado watu walikuwa wakiendelea kuota moto huku wakipiga stori za hapa na pale msibani. Baba wala hakuhangaika hata kugeuka, akanitaka kuelekeza akili zangu kwenye jambo lililotupeleka pale kwani muda ulikuwa umetutupa mkono.

Ilionesha baba alikuwa anaelewa kila kitu kilichokuwa kikiendelea, nikawa najiuliza ameyajuaje yote hayo? Kiukweli sikupata jibu, baba Rahma naye wala hakujishughulisha na chochote na wale watu kama baba.

“Onesha aliangukia wapi? Unatupotezea muda,” alisema baba, nikawa najaribu kuvuta kumbukumbu, nikawa natembea pembeni ya barabara kuelekea pale yule dereva wa bodaboda alipodondokea, wakawa wananifuata kwa nyuma.

“Nadhani ni hapa.”

“Unadhani? Kwani huna uhakika?”

“Nilipomgonga aliyumbayumba kwa mita kadhaa, akaja kudondokea hapa, sina uhakika kwa sababu mimi nilikuwa nimesimama kule mbali.

“Hebu nenda ulipokuwa umesimama,” alisema baba. Ilionesha hakuwa akitaka majibu ya kubahatisha, nikageuka na kutazama tena kule msibani. Bado moyo wangu ulikuwa na hofu, nikiamini wale wazee wanaweza kuwa miongoni mwa watu waliokesha pale msibani halafu nikayazua mengine tena.

Nilirudi kwa hofu mpaka pale nilipokatiza barabara nikiwa spidi kali kama kiberenge, nikasimama na kuwageukia akina baba. Niliweza kupata ramani halisi, nikatembea harakaharaka kuelekea mpaka pale nilipokuwa nimewaacha.

“Ni hapa,” nilisema huku nikioneshea kidole katikati ya barabara. Ni kweli nilipatia kwa sababu bado palikuwa na alama za damu na vioo vya ile bodaboda, baba akainama pale katikati ya lami kisha akawa ni kama anaokota vitu fulani hivi.

Baada ya hapo alikuja upande wa pili tulipokuwa tumesimama, akawa anatazama chini kisha akainua uso na kunitazama:

“Walipomtoa pale katikati ya barabara walimlaza hapa,” alisema huku akionesha, ni kweli pale pembeni napo palikuwa na alama za damu nyingi zilizokaukia, kwa kutumia mikono miwili, alizoa udongo uliokaukia damu, kisha akapiga magoti na kuuinua juu, akazungumza maneno fulani kama anayenuiza jambo kisha akausogeza ule udongo puani kwake, akaunusa kisha akapiga chafya mfululizo.

Hakusema chochote baada ya hapo zaidi ya kuinuka na kuanza kutembea kwa haraka kuelekea upande wa kusini, kama anayetafuta kitu, baba yake Rahma alinipa ishara kwamba tumfuate, akawa anatembea kwa kasi huku akiongea maneno ambayo sikuwa nayaelewa.

Alivuka barabara, na sisi tukawa tunamfuata, akawa anazidi kuongeza kasi kiasi kwamba nililazimika kuwa nakimbia ili kwenda nao sawa. Bahati nzuri ni kwamba tulikuwa tukielekea upande tofauti kabisa na kule kulikokuwa na msiba.

Ilifika mahali akachepuka na kuingia vichakani, safari hii akaanza kutimua mbio, sote tukawa tunakimbia kumfuata. Japokuwa ilikuwa ni usiku, tulikimbia vichakani kwa muda mrefu sana, baadaye tukatokezea kwenye makaburi mengi, baba akawa anazunguka huku na kule na mwisho aliishia kwenye kaburi moja lililoonesha kuwa jipya.

“Amezikwa hapa,” alisema baba huku akigeuka huku na kule, nikawa natetemeka kwa hofu, sikujua nini kinachoenda kutokea.

“Simama kwa kule,” alisema baba huku akinielekeza kusimama upande uliokuwa na msalaba ambapo kimsingi ndiyo kichwani. Nilifanya hivyo, baba yake Rahma akasimama upande wa miguuni na baba akasimama katikati, juu ya kaburi.

Baada ya kusimama hapo, aligeuka huku na kule kama anayetafuta kitu kisha akashuka kutoka pale juu ya kaburi na kunifuata, akawa ananiongelea sikioni.

“Huyu amezikwa leo, katika sheria za jamii yetu, anaruhusiwa kutolewa kafara kwa hiyo tutamchukua huyu badala ya Sadoki, kule tutarudi siku nyingine kwa sababu kuna mambo hayakwenda sawa kwa sababu yako, sasa ukifanya ujinga tena na hapa, hakuna wa kumlaumu,” alisema baba.

Hofu ikazidi kuongezeka kwenye moyo wangu. Kama nilivyoeleza, hakuna sehemu niliyokuwa naiogopa kama makaburini, nikawa nahisi kama mwili na akili vinatengana. Kibaya zaidi ilikuwa ni usiku na nimeshawahi kusikia kwamba makaburini nyakati za usiku kunakuwa na mambo mengi sana ya ajabu, sikuelewa baba anavyosema tunamchukua yule dereva bodaboda aliyefariki kwenye ajali, alimaanisha nini.

Ninavyojua mimi, huwezi kufukua kaburi na kutoa maiti kwa sababu kwanza siyo kazi nyepesi lakini pia, lazima watu watakuona ukiwa unalifukua kwa sababu makaburi mengi huwa yanakuwa na ulinzi, na kama si hivyo, mizimu mibaya iliyopo makaburini lazima itakudhuru tu. Sikuelewa malengo ya baba ni nini lakini kama mwenyewe alivyokuwa anasisitiza kwamba lengo ni kunisaidia mimi, ilibidi nitulie kuona mwisho wake.

Baada ya kuzungumza na mimi, alimfuata baba yake Rahma, wakawa wanajadiliana jambo pale, wakazungumza kwa zaidi ya dakika mbili kwa sauti ya chini kiasi kwamba sikuwa nikisikia walichokuwa wanakisema.

Baada ya hapo, baba yake Rahma alinifuata na kuniambia natakiwa kuvua nguo zote na kukaa juu ya kaburi kwa sababu kazi iliyokuwa inaenda kufanyika, si ya kitoto. Nilishtuka, yaani nivue nguo halafu nikae juu ya kaburi? Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio tena.

Ni kama baba yake Rahma alinielewa jinsi nilivyokuwa na hofu, akaniambia sitakiwi kuwa na hofu yoyote kwa sababu kwenye jamii yao, kukaa bila nguo ni kitu cha kawaida kabisa, isitoshe wao ni baba zangu ambao wananijua tangu nikiwa mtoto mchanga, kwa hiyo lazima nifanye walichoniambia.

Ilibidi nikubaliane naye maana baba alikuwa akisisitiza kwamba muda unakwenda. Nikasogea pembeni na kuvua nguo zote, nikajiziba sehemu ya mbele kwa mikono yangu na kupanda kwenye tuta la lile kaburi, nikawa natetemeka mno.

Baada ya kukaa juu ya tuta la kaburi, nikiwa nimeupa msalaba mgongo kama nilivyoelekezwa, baba na baba Rahma, mmoja akiwa amesimama upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni, walianza kuimba nyimbo za kutisha kwa kupokezana, akiimba baba, baba yake Rahma anaitikia, wakaendelea hivyo kwa dakika kadhaa kisha wakaanza kulizunguka lile kaburi, kutoka kulia kwenda kushoto.

Walifanya hivyo kwa dakika kadhaa, baadaye baba akaniambia nisimame. Nilifanya hivyo huku nikijiziba kwa soni, akanielekeza kuelekea upande ule wa kichwani niliokuwa nimesimama awali, kisha akaniambia niwe makini kutazama anachokifanya.

Milio ya bundi na ndege wengine wa usiku, iliendelea kusikika na kufanya hali iwe ya kutisha mno pale makaburini. Baba alionesha kwa ishara kwamba natakiwa kupiga makofi na kupiga mguu wangu wa kushoto chini kwa nguvu, na vyote vifanyike kwa wakati mmoja.

Alinihesabia kwa alama za vidole kisha akaniruhusu, nikapiga makofi kwa nguvu na wakati huohuo nikapiga kishindo cha nguvu. Alinionesha kwa ishara kwamba natakiwa kufanya hivyo mara tatu, nikarudia mara ya pili, kisha nikafanya kwa mara ya tatu.

Kilichotokea baada ya kufanya hivyo kwa mara ya tatu, kilinifanya nihisi kama mwili wangu unakufa ganzi kwa hofu, sijawahi kushikwa na hofu kama niliyoipata siku hiyo na kama baba asingeniwahi, huenda ningedondoka kama mzigo chini maana mwili wote uliisha nguvu.

Japokuwa ilikuwa ni usiku, tena nikiwa sina nguo na kulikuwa na baridi kali, nilihisi kijasho chembamba kikinitoka, ama kweli duniani kuna mambo na ukishangaa ya Musa, utayaona ya Firauni.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 59


ILIPOISHIA:
Kilichotokea baada ya kufanya hivyo kwa mara ya tatu, kilinifanya nihisi kama mwili wangu unakufa ganzi kwa hofu, sijawahi kushikwa na hofu kama niliyoipata siku hiyo na kama baba asingeniwahi, huenda ningedondoka kama mzigo chini maana mwili wote uliisha nguvu.
Japokuwa ilikuwa ni usiku, tena nikiwa sina nguo na kulikuwa na baridi kali, nilihisi kijasho chembamba kikinitoka, ama kweli duniani kuna mambo na ukishangaa ya Musa, utayaona ya Firauni.
SASA ENDELEA…
Kitendo cha kufuata maelekezo yale tu, mara kaburi lilifunuka lote, yaani ule udongo wote uliokuwa umetumika kulifukia, ukapotea kiasi kwamba kila kitu kilichokuwa ndani ya kaburi kilikuwa kikionekana.
“Ingia tukasaidiane kumtoa kwenye jeneza,” alisema baba, nikajikuta nguvu za kuendelea kusimama zimeniisha maana miguu ilikuwa ikitetemeka kuliko kawaida, nikakaa kwenye kaburi lililokuwa pembeni, uso wote ukiwa umelowa kwa machozi.
Ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba alikuwa akiniambia kwamba bado sijakomaa kiakili na sitakiwi kuingizwa kwenye hayo mambo.
“Inuka acha kuleta mambo ya kijinga hapa, upumbavu wako ndiyo uliotufikisha hapa,” alisema baba kwa ukali, nikajikakamua na kusimama huku nikiwa bado natetemeka. Alichokifanya baba baada ya kuona kama nasuasua, alinisukumia ndani ya lile kaburi, nikaporomoka na kwenda kujibamiza kwenye jeneza.
Nilijikuta nikipiga kelele kwa sauti kubwa huku nikitafuta sehemu ya kutokea, kwa kuwa ilikuwa ni ndani ya shimo kelele zangu hata hazikufika mbali, zikawa zinajirudia na kusababishwa mwangwi. Tayari baba naye alishaingia mle kaburini, akaninyamazisha kwa ukali kama kawaida yake.
“Wewe ndiyo unatakiwa uifanye hii kazi, mimi nakusaidia tu,” alisema huku akihangaika kulifungua jeneza lililokuwa na ule mwili.
Nisingependa sana kueleza kuhusu kipengele hiki kwa sababu hata mwenyewe nikikumbuka huwa naogopa sana, lakini kwa kifupi, nilisaidiana na baba kuutoa ule mwili kwenye jeneza, sanda yote ikiwa imelowa damu hasa maeneo ya kichwani inakoonesha marehemu aliumia sana kwenye ile ajali.
Tukautoa na kuulaza pembeni ya kaburi huku lile jeneza baba akilirudishia kama lilivyokuwa mwanzo. Huku nikitetemeka kuliko kawaida, baba aliniamuru tena kufanya kama nilivyofanya mwanzo, nikafanya mara ya kwanza, ya pili, kisha nikafanya mara ya tatu.
Cha ajabu kaburi lilijifukia vilevile na kurudi kama lilivyokuwa mwanzo, tofauti yake ni kwamba kidogo lilikuwa limetitia. Ni hapo ndipo nilipoamini kauli niliyokuwa nikiisikia kwa muda mrefu, kwamba ukiona kaburi jipya limetitia sana, kuna uwezekano mkubwa kwamba kilichozikwa ndani siyo mtu au kama ni maiti, basi imechukuliwa na wachawi.
Baada ya zoezi hilo kukamilika, baba aliniamuru niibebe ile maiti huku baba yake Rahma akinitoa hofu kwamba mtu akishakufa hana madhara yoyote, hawezi kunidhuru kwa namna yoyote, nikajikakamua na kuiweka begani, tukaanza kuondoka makaburini hapo huku ikichuruzika vitu ambavyo hata bila kutazama nilijua ni damu.
Unajua baadaye nilikuja kujifunza kitu kingine, kwamba watu wanaofariki katika mazingira ya kishirikina, unaweza kutambua maiti zao kwa haraka kama na wewe una uelewa kuhusu mambo hayo, kwa sababu kwanza imezoeleka kwamba mtu akifa mwili wake hupoa na kuwa wa baridi sana lakini kama amekufa kwa mipango ya watu, mwili huendelea kuwa na joto kwa muda mrefu.
Pia maiti za namna hii zinakuwa na kawaida ya kutoka damu. Inafahamika kwamba mtu akifa, moyo unakuwa umeacha kusukuma damu kwa hiyo hata mzunguko mzima wa damu nao unasimama lakini kwa watu waliochukuliwa kabla ya muda wao, japo kwa nje anaonekana amekufa, bado mzunguko wa damu unakuwa unaendelea japo kwa kasi ndogo sana na ndiyo maana, utakuta maiti inatoka damu puani, mdomoni, masikioni au kama ni ya ajali kama hiyo, majeraha yanakuwa yanaendelea kuchuruzika damu.
Tulitoka huku nikijikaza kiume na ule mwili begani kwa sababu ulikuwa mzito sana lakini kwa kuwa na mimi kidogo nilikuwa na ubavu, niliweza kuhimili uzito huo mpaka kwenye mti mkubwa uliokuwa pembeni ya makaburi hayo, kama kawaida, maandalizi ya safari yakaanza kufanyika ambapo baba aliniambia niulaze ule mwili chini.
Mchakato ulifanyika na kama kawaida, muda mfupi baadaye, akili ilinitoka, nilipokuja kuzinduka, tulikuwa tayari kwenye lile eneo letu tunalokutania, watu wengi wakiwa wamezunguka na kutengeneza duara kama kawaida huku nyimbo za ajabuajabu zikiendelea kuimbwa na kuifanya hali iwe ya kutisha sana.
“Mkuu akikusogelea, inabidi uinamishe kichwa chako chini na kuweka mikono hivi maana umefanya makosa,” baba aliniambia kwa sauti ya chini, akinielekeza nini cha kufanya. Kwa mbali nikawa namuona Mkuu akija huku kama kawaida yake, vishindo vyake vikisikika eneo lote hilo.
Baba na baba Rahma walimsogelea na kuinamisha vichwa vyao kwa utii, akawa anawagusa na mkia wa mnyama ambaye simjui, aliokuwa ameushika, harakaharaka wakaondoka na kwenda kukaa kule walikokuwa wamekaa wale watu wengine.
Mkuu akanisogelea mpaka pale nilipokuwa nimepiga magoti huku uso wake akiwa ameukunja, nilipomtazama mara moja sikurudia tena kumtazama kwa sababu alikuwa anatisha sana. Nilizoea kumtazama akiwa hajakasirika lakini siku hiyo alikuwa kama mnyama mkali wa porini kwa jinsi alivyokuwa anatisha, midomo ikimchezacheza kwa hasira.
Ilibidi niinamishe kichwa kama baba alivyonifundisha, mikono nikaiweka kifuani kwa unyenyekevu, aliendelea kunitazama bila kusema chochote kwa sekunde kadhaa kisha nikasikia akinipigapiga na ule mkia.
“Sirudie masiku mengine,” alisema Mkuu kwa Kiswahili kibovu huku akiendelea kunipigapiga, kidogo kamoyo kalitulia ila nilichojifunza ni kwamba kumbe nilikuwa nimefanya kosa kubwa sana na pengine bila kufanya kile tulichokifanya kwa msaada wa baba na baba yake Rahma, huenda huo ndiyo ungekuwa mwisho wangu.
Kumbe ndiyo maana ni rahisi sana kusikia wachawi wamekufa ghafla vifo vya kutatanisha, wakati mwingine inakuwa ni kukosea masharti kama kilichotaka kunitokea mimi na adhabu inayomfaa mtu anayekiuka masharti, ni kuuawa na kuliwa nyama, kama siyo yeye basi mtu wake wa karibu.
Baada ya kupitisha msamaha kwangu, niliinua uso wangu, mkuu akaugeukia ule mzigo niliokuwa nao ambapo kwa kutumia kisu kikali alikata ile sanda kisha akanigeukia na kutingisha kichwa, akainua ule mkia wake juu na watu wote wakapaza sauti zao kutamka maneno ambayo hata sikuwa nayaelewa.
Basi kilichoendelea hapo ni utaratibu wa kawaida, watu wakala na kucheza ngoma huku mara kwa mara Mkuu akinikata jicho kama anayenichunga kuhakikisha siharibu kitu kingine.
“Amefurahishwa na kazi uliyoifanya, amesema anataka kukuongeza nguvu maana japikuwa umefanya makosa, lakini kupitia makosa hayo umeweza kuonesha ushujaa ambao wengine huwa wanashindwa, mshukuru sana baba yako,” baba Rahma aliniambia kwa sauti ya chini, nikageuka kumtazama Mkuu, macho yake na yangu yakagongana, nikamuona akiachia tabasamu hafifu.
“Akikupa nafasi ya kuchagua akuongezee uwezo gani utachagua nini?”
“Nataka niwe na uwezo wa kupata hela kirahisi, nataka kuwa tajiri.”
“Tajiri? Utajiri wa kichawi ni mbaya sana, jaribu uone mwenyewe, bora hata uombe kitu kingine chochote,” alisema baba yake Rahma lakini maneno yake wala hayakuwa yakiniingia akilini. Kiukweli na mimi nilikuwa natamani kuwa tajiri kwa sababu tangu nizaliwe, maisha yetu yalikuwa ya kimaskini kule kijijini na umuhimu hasa wa kuwa tajiri, niliuona baada ya kufika mjini.
Vijana wadogo tu kama mimi, wengine hata nawazidi lakini wanaendesha magari ya kifahari barabarani, kwa nini na mimi nisionje kidogo hata kama ni mbaya? Wakati akiendelea kunipa nasaha zake, Mkuu alinipa ishara kwamba nimfuate, harakaharaka nikainuka na kumuacha baba yake Rahma akiendelea kuongea.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 60



ILIPOISHIA:

Vijana wadogo tu kama mimi, wengine hata nawazidi lakini wanaendesha magari ya kifahari barabarani, kwa nini na mimi nisionje kidogo hata kama ni mbaya? Wakati akiendelea kunipa nasaha zake, Mkuu alinipa ishara kwamba nimfuate, harakaharaka nikainuka na kumuacha baba yake Rahma akiendelea kuongea.

SASA ENDELEA…

Alinishika mkono na kusogea pembeni na mimi, mawasiliano kati yetu kidogo yalikuwa magumu kwa sababu alikuwa akiongea maneno ya Kiswahili machache, tena yaliyopindapinda lakini muda mwingi alikuwa akizungumza lugha ambayo siielewi.

Katika yale machache niliyomuelewa, alionesha kufurahishwa na ujasiri wangu, na kuniambia kwamba japokuwa ndiyo kwanza nilikuwa nimejiunga, nilikuwa na kasi nzuri ya kujifunza. Kama alivyoniambia baba yake Rahma, kweli Mkuu aliniuliza ni zawadi gani akinipa nitafurahi?

Sikupepesa macho wala kumung’unya maneno, nikamwambia kwamba nataka dawa za kunifanya niwe tajiri. Alicheka sana, mapengo yake yakawa yanaonekana, ni hapo ndipo nikagundua kwamba kumbe naye huwa anacheka na kufurahi, ingawa sikuelewa nini hasa kilichomfurahisha.



Aliniambia kitu nilichokichagua ni kikubwa sana kuliko uwezo wangu, akaniambia atanipa dawa lakini haitakuwa ya kupata utajiri mkubwa kwa sababu utajiri una masharti magumu na nikipata pesa nikiwa bado mdogo, naweza kufa siku si zangu.

Tulirudi pale katikati alipokuwa ameweka vifaa vyake, akatoa kimkoba chake cha ngozi na kutoa kichupa kilichokuwa na dawa, akatoa na wembe kisha akaniambia nimfuate. Tulitoka pale na kupotelea vichakani kwenye giza, nikiwa namfuata nyumanyuma.

Tulitokezea kwenye eneo ambalo lina uwazi, akanielekeza kwa ishara kwamba nivue shati kisha nikae chini na kukunja miguu, kweli nilifanya hivyo, akanishika kichwani na kuanza kuzungumza maneno nisiyoyaelewa, akayaongea kwa muda mrefu kisha akachukua ule wembe na kuanza kunichanja chale kuanzia kwenye utosi kurudi mgongoni.

Aliponipaka ile dawa, nilisikia maumivu makali sana lakini nikajikaza kisabuni, alipomaliza, aliniambia nitulie hivyohivyo, akapotelea vichakani. Muda mfupi baadaye, aliibuka kutoka vichakani akiwa amembeba nyoka mkubwa, nikashtuka sana na kutaka kusimama nitimue mbio lakini akanionesha ishara kwamba nitulie.

Huku nikitetemeka kuliko kawaida, alimsogeza yule nyoka mkubwa kwenye zile chale, akawa anamlambisha damu zangu huku akiendelea kuzungumza maneno nisiyoyaelewa. Alipomaliza, aliamuachia, yule nyoka akatambaa kwa kasi na kupotelea vichakani.

Mshangao niliokuwa nao, ulikuwa hauelezeki. Akanipa ishara kwamba nisimame, nikafanya hivyo na kuvaa shati langu kisha tukarudi kule walipokuwa wenzetu, akaniambia kwamba baada ya siku saba dawa itaanza kufanya kazi lakini natakiwa kuwa naenda kutoa sadaka kwa yule nyoka mara kwa mara.

Baba alikuwa akifuatilia kila kilichokuwa kikiendelea na Mkuu alipomaliza tu kuzungumza na mimi, harakaharaka baba alinifuata. Ile furaha yote niliyokuwa nayo ndani ya moyo wangu ilitibuka kwani baba alipofika tu, alianza kunifokea kwa sauti ya chinichini na kuniambia kwamba nilichokifanya ni upumbavu wa hali ya juu na yeye hatahusika na chochote kitakachonipata nitakapokosea masharti.

“Masharti gani tena baba?” nilimuuliza kwa mshangao kwa sababu Mkuu hakuwa amenipa masharti yoyote, akaniambia kwamba siyo kwamba yeye hatamani utajiri lakini masharti yake yalivyo magumu, ndiyo maana wengi walikuwa wanaona ni bora waendelee kuishi kimaskini tu.

“Kama hajakwambia basi mimi nakwambia, kuna masharti magumu sana tena usipokuwa makini unaweza kusababisha hata sisi wazazi wako na ndugu zako wa tumbo moja wakawa kwenye hatari kubwa sana, kwa nini hukuuliza kabla?” baba aliendelea kuniwakia kwa sauti ya chini huku mara kwa mara akigeuka na kumtazama Mkuu. Nadhani alikuwa hataki asikie chochote.

Maelezo aliyonipa baba yaliniogopesha sana, japokuwa hakuwa amenifafanulia, ilivyoonesha kulikuwa na masharti magumu kwa sababu hata mimi siku nyingi nilikuwa najiuliza, kwamba kwa nini unakuta mganga anasaidia watu kupata utajiri kwa njia za kishirikina wakati yeye anaishi kwenye kijumba cha nyasi?

Nilikuwa pia najiuliza kwa nini wachawi wengi wanakuwa na maisha ya dhiki sana? Nilitamani kuyajua hayo masharti kwa sababu kama ni maji, yalishamwagika. Baba aliniambia hawezi kuniambia, kama nataka nirudi kwa Mkuu kwenda kumuuliza.

Ile furaha yote niliyokuwa nayo moyoni iliyeyuka, kurudi kwa Mkuu kumuuliza nikashindwa kwani muda nao ulikuwa umeenda sana. Nikiwa bado nimetulilia nikitafakari, yule msichana, Isrina alinifuata, hata sijui alitokea wapi, nilishtukia tu yupo pembeni yangu.

“Hongera,” alisema huku akinipa mkono, tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake, nilimpa mkono lakini sikuwa nimechangamka.

“Mbona siku hizi huna taimu na mimi? Kuna jambo nimekuudhi?” aliniuliza, nikatingishwa kichwa kukataa lakini ukweli ni kwamba nilikuwa na kinyongo kikali sana dhidi yake.

“Basi nitakutafuta tuzungumze, nakuomba ukubali,” alisema huku akiinuka, nikatingisha kichwa kwa sababu nilikuwa nataka aondoke haraka.

Mpaka muda wa kutawanyika unafika, bado nilikuwa sielewi nini itakuwa hatma yangu na nifanye nini kwa wakati huo. Tulirudi nyumbani kama kawaida ambapo nilijipa muda wa kutafakari mambo yote yaliyotokea kwa siku hiyo maana kiukweli kwenye ulimwengu wa giza, dunia inakwenda kasi sana kuliko unavyoweza kudhani. Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilipitiwa na usingizi mzito, nikiwa na maswali mengi ndani ya kichwa changu ambayo yote hayakuwa na majibu.

Kesho yake nilichelewa sana kuamka kwa sababu ya uchovu, nilipoamka, majira kama ya saa nne hivi, nilimfuata baba yake Rahma nikitaka ufafanuzi zaidi. Tulizungumza mambo mengi lakini kubwa aliniambia utajiri wa kishirikina, huwa unahitaji makafara ya damu mara kwa mara.

Akaniambia kwamba bahati mbaya ni kwamba, sina uwezo wa kuchagua nani atolewe kafara muda wa kufanya hivyo unapofika bali nitakuwa nachaguliwa, kwa hiyo natakiwa kuwa makini sana.

Maelezo hayo yalinitisha sana, nikawa najaribu kuunganisha matukio, ni kweli watu wenye utajiri wa kishirikina, huwa wanasumbuliwa sana na kashfa ya kuwatoa kafara watoto wao, wazazi wao au watu wao wa karibu.

Nilijaribu kujitazama kwa upande wangu, nikawafikiria wazazi wangu na ndugu zangu tuliozaliwa nao tumbo moja, nikawa najiuliza kama siku nitatakiwa kumtoa yeyote kafara nitaweza kweli? Ulikuwa ni mtihani mgumu sana kwangu.

Ila aliniambia jambo ambalo kidogo lilinipa faraja, akaniambia kwamba makafara yanakuwa ni lazima pale utajiri unapokuwa mkubwa sana, lakini kwa mambo ya fedha ndogondogo hakuna ulazima wa kufanya kafara lolote.

Maelezo hayo yalinifurahisha sana ndani ya moyo wangu, nikawa nasubiri kwa hamu hizo siku saba ziishe nikapewe maelekezo ya nini cha kufanya. Nilichojiapiza ni kwamba sitataka utajiri mkubwa, fedha ndogondogo tu za kutesea mitaani zilikuwa zinanitosha sana, hasa ukizingatia kwamba sikuwa na majukumu ya moja kwa moja.

Wakati nikiendelea kusubiri hizo siku saba, niliona huo ndiyo muda muafaka wa kuanza kushughulikia suala la Rahma. Kama nilivyoeleza, kuna ukuta mkubwa ulikuwa umejengeka kati yetu, na kama nisingefanya jambo, huenda huo ndiyo ungekuwa mwisho wetu, jambo ambalo lilikuwa likituumiza sana sote wawili, hasa Rahma.

Alikuwa hanielewi kwa nini nimebadilika ghafla, nimekuwa na mambo mengi ya ajabuajabu, sioneshi kumhitaji tena kama siku za mwanzo na wala sijali hisia zake. Ukweli ni kwamba nilikuwa namlinda na ndiyo maana ilikuwa lazima nifanye hivyo na njia pekee, ilikuwa ni kumshawishi naye ajiunge nasi, kazi ambayo isingekuwa nyepesi lakini nilishajipanga kumkabili.

Je, nini kitafuatia?
 
Haya bana,
Natamani kafara la kwanza tu liwe ni la kutaka damu ya baba yako.
 
Sehemu ya 61



ILIPOISHIA:

Alikuwa hanielewi kwa nini nimebadilika ghafla, nimekuwa na mambo mengi ya ajabuajabu, sioneshi kumhitaji tena kama siku za mwanzo na wala sijali hisia zake. Ukweli ni kwamba nilikuwa namlinda na ndiyo maana ilikuwa lazima nifanye hivyo na njia pekee, ilikuwa ni kumshawishi naye ajiunge nasi, kazi ambayo isingekuwa nyepesi lakini nilishajipanga kumkabili.

SASA ENDELEA…

“Rahma!” nilimuita msichana huyo baada ya kukutana naye koridoni, mimi nikitoka bafuni kuoga na yeye akitoka chumbani kwake. Tofauti na siku zote ambazo alikuwa akinichangamkia sana anaponiona, wakati mwingine hata akinifuata chumbani kwangu, siku hiyo Rahma alikuwa tofauti kabisa, alipooza na alionesha kutotaka kuzungumza chochote na mimi.

“Rahma si nakuita jamani,” nilisema baada ya kumuona amenipa mgongo, akitembea haraka kuelekea sebuleni. Licha ya kutamka maneno hayo, bado hakutaka kusimama, ikabidi nitumia nguvu kumshika mkono na kumgeuza.

“Samahani nina mazungumzo na wewe, naomba unisikilize tafadhali,” nilimwambia kwa upole, akanitazama usoni, macho yake na yangu yakagongana, nikashtuka kumuona akilia.

“Unalia nini Rahma?” nilimuuliza lakini hakunijibu kitu zaidi ya kuendelea kunitazama kwa huzuni. Ilibidi nianze kumbembeleza lakini kwa kuwa tulikuwa tumesimama koridoni, niliona haiwezi kuwa picha nzuri kwani mtu yeyote angetuona tukibembelezana hapo angeweza kutufikiria vibaya.

“Naomba tutoke tukanywe japo soda pale dukani, nina mazungumzo ya muhimu sana na wewe,” nilimwambia Rahma, akatingisha kichwa bila kunijibu chochote kisha akarudi chumbani kwake.

Ilibidi na mimi nirudi chumbani kwangu, nikachukua nauli iliyokuwa imebaki siku nilipoenda Mlandizi na kuitia mfukoni, nikajiweka vizuri na kutoka nje. Nilizugazuga pale nje, nilipoona hakuna anayenifuatilia, nilifungua geti kubwa na kutoka nje. Ile kutoka tu, madereva Bajaj na bodaboda waliokuwa wanapaki pale nje, waliacha kila walichokuwa wanakifanya na kuanza kunitazama.

Kibaya ni kwamba upande ule waliokuwa wakipaki, kwa mbele kidogo ndiyo kulikuwa na duka ambalo nilipanga tukae pale na Rahma kwa sababu kulikuwa na viti upande wa nyuma, kwa hiyo ilikuwa ni lazima niwapite palepale walipopaki.

Nimewahi kusikia matukio kadhaa ya madereva hao wa Bajaj na bodaboda kushirikiana kufanya uhalifu, hasa pale inapoonekana mmoja wao ameonewa, nikajua lazima watakuwa wamenipania kwa jinsi nilivyomsulubu mwenzao. Hata hivyo, kwa sababu nilikuwa na nguvu za giza, tena za kutosha kabisa, sikuogopa chochote, ndiyo kwanza nikawa napiga mluzi huku nikielekea kule walikokuwa.

Cha ajabu, nilishangaa kuona kila mmoja akikimbilia kwenye chombo chake na kukiwasha, wakaanza kuondoka mmoja baada ya mwingine wakikimbia kwa kasi, sekunde chache baadaye eneo lote likawa tupu.

Hakukuwa na mashaka kwamba walikuwa wakinikimbia mimi, kwa sababu hata kama wanawahi abiria, wasingeweza kuondoka wote kwa mkupuo, tena kwa kasi kubwa wengine wakinusurika kugongana wao kwa wao.

Sikuelewa nini kimetokea mpaka wawe wananiogopa kiasi hicho lakini sikuwajali maana na mimi nilikuwa na majanga yangu mengi kichwani. Nilienda mpaka pale dukani, nikamsalimia muuza duka ambaye aliponiona tu, alishtuka sana, akaitikia kwa woga.

“Naomba Fanta,” nilisema huku nikimeza mate kwani mara ya mwisho kunywa soda, ilikuwa ni siku ile tuliposafiri kuja jijini Dar es Salaam.”

“Hatuuzi soda hapa!” alisema yule muuzaji, kauli ambayo nilishindwa kuielewa ina maana gani. Juu ya meza kulikuwa na chupa tupu za soda kuonesha kwambamuda si mrefu kuna watu walikuwa wakinywa soda, na mara kadhaa nilipita pale na kuona watu wakipata vinywaji, kwa nini aniambie kwamba hawauzi soda?

Nikiwa bado nimeduwaa, nikishindwa nimuulizeje, mara Rahma aliwasili, kumbe hatukuwa tumeachana umbali mrefu, akamsalimia yule muuzaji. Alimuita kwa jina lake na ilionesha wanafahamiana.

“Kumbe anaitwa Vero,” nilijisemea moyoni, alikuwa mwanamke ambaye kwa kumkadiria alionesha kuwa bado mdogo lakini mwenye uso uliokomaa na kupoteza nuru kama walivyo wanawake wengi wa vijijini kama kule kwetu Chunya.

“Huyu ni kaka yangu, unamjua? Anaitwa Togo,” Rahma alisema huku akinishika begani, nikamuona yule mwanamke akijaribu kuvaa tabasamu la uongo usoni.

“Tuletee soda, Togo unakunywa nini?” alisema Rahma, yule mwanamke akawa anababaika, kama anayeshindwa ajibu nini maana mimi aliniambia hawauzi soda. Rahma alinishika mkono huku akionesha kabisa kwamba anailazimisha furaha, tukaenda mpaka kwenye viti na kukaa, tukawa tunatazamana huku tukisubiri yule mwanamke aje atuhutubie.

“Unataka kuniambia nini?” alisema Rahma huku akikwepesha macho yake pembeni.

“Rahma! Najua unanifikiria vibaya sana kwa sasa, najua unaona kama nakufanyia makusudi kwa sababu sikupendi lakini ukweli ni kwamba ni matatizo makubwa sana na badala ya kunichukia, unatakiwa unionee huruma mwenzio,” nilianza kumbembeleza Rahma.

Kama nilivyosema awali, sikuw anajua mambo ya mapenzi kwa hiyo hata kubembeleza kwangu, nilikuwa naungaunga tu ilimradi Rahma anielewe. Niliendelea kushuka mistari kwa kuzunguka, nikamwambia kuna jambo zito ambalo halijui nataka kumweleza.

Maneno yangu yalimbadilisha kabisa Rahma, akawa ananitazama kwa shauku huku ile huzuni aliyokuwa nayo, ikiyeyuka ghafla. Ili kumuweka sawa, ilibidi nibadilishe mada kwanza, nikamuuliza vipi yule muuzaji mbona haleti hizo soda?

“Una kiu? Ngoja nimfuate,” alisema huku akiinuka lakini alipofika pale dukani, yule mhudumu alikataa katakata kutoka, akampa Rahma funguo ya friji na kutaka ajihudumie mwenyewe. Rahma aliichukua, akaniuliza nakunywa soda gani, akatoambili pamoja na yake, akaja mpaka pale tulipokuwa tumekaa, akazifungua zote na kurudisha funguo kwa mwenyewe.

“Kwa nini amekataa kuja kutuhudumia mwenyewe?”

“Hata mimi nashangaa! Achana naye tuendelee na yetu,” alisema Rahma, nikapiga funda moja kisha nikaendelea kuzungumza. Lengo langu lilikuwa ni kumpasulia ukweli kwamba baba yake alikuwa mwanachama wa jamii ya siri, vilevile baba yangu na mimi pia wameniingiza bila ridhaa yangu.

Niliona hiyo ndiyo gia nzuri ya kumuingia kwa sababu kama ningesema mimi mwenyewe ndiye niliyetaka kujiunga, angenishangaa sana na pengine nisingeweza kumshawishi. Nilianza kwa kumdadisi kwa kina kuhusu baba yake, nikitafuta sehemu ya kuanzia.

“Mbona unaniuliza kama una kitu unataka kuniambia? Tatizo langu wala halimhusu baba, ni mimi na wewe.”

“Ni stori ndefu Rahma ila naomba unielewe nitakachokwambia,” nilisema, nikashusha pumzi ndefu na kuamua liwalo na liwe. Nilitaka kwenda moja kwa moja, kwamba baba yake na baba yangu walikuwa wachawi. Cha ajabu, kila nilipotaka kusema hivyo, mdomo ulikuwa mzito, nikawa naumauma maneno, hali iliyosababisha anikazie macho.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 61



ILIPOISHIA:

Alikuwa hanielewi kwa nini nimebadilika ghafla, nimekuwa na mambo mengi ya ajabuajabu, sioneshi kumhitaji tena kama siku za mwanzo na wala sijali hisia zake. Ukweli ni kwamba nilikuwa namlinda na ndiyo maana ilikuwa lazima nifanye hivyo na njia pekee, ilikuwa ni kumshawishi naye ajiunge nasi, kazi ambayo isingekuwa nyepesi lakini nilishajipanga kumkabili.

SASA ENDELEA…

“Rahma!” nilimuita msichana huyo baada ya kukutana naye koridoni, mimi nikitoka bafuni kuoga na yeye akitoka chumbani kwake. Tofauti na siku zote ambazo alikuwa akinichangamkia sana anaponiona, wakati mwingine hata akinifuata chumbani kwangu, siku hiyo Rahma alikuwa tofauti kabisa, alipooza na alionesha kutotaka kuzungumza chochote na mimi.

“Rahma si nakuita jamani,” nilisema baada ya kumuona amenipa mgongo, akitembea haraka kuelekea sebuleni. Licha ya kutamka maneno hayo, bado hakutaka kusimama, ikabidi nitumia nguvu kumshika mkono na kumgeuza.

“Samahani nina mazungumzo na wewe, naomba unisikilize tafadhali,” nilimwambia kwa upole, akanitazama usoni, macho yake na yangu yakagongana, nikashtuka kumuona akilia.

“Unalia nini Rahma?” nilimuuliza lakini hakunijibu kitu zaidi ya kuendelea kunitazama kwa huzuni. Ilibidi nianze kumbembeleza lakini kwa kuwa tulikuwa tumesimama koridoni, niliona haiwezi kuwa picha nzuri kwani mtu yeyote angetuona tukibembelezana hapo angeweza kutufikiria vibaya.

“Naomba tutoke tukanywe japo soda pale dukani, nina mazungumzo ya muhimu sana na wewe,” nilimwambia Rahma, akatingisha kichwa bila kunijibu chochote kisha akarudi chumbani kwake.

Ilibidi na mimi nirudi chumbani kwangu, nikachukua nauli iliyokuwa imebaki siku nilipoenda Mlandizi na kuitia mfukoni, nikajiweka vizuri na kutoka nje. Nilizugazuga pale nje, nilipoona hakuna anayenifuatilia, nilifungua geti kubwa na kutoka nje. Ile kutoka tu, madereva Bajaj na bodaboda waliokuwa wanapaki pale nje, waliacha kila walichokuwa wanakifanya na kuanza kunitazama.

Kibaya ni kwamba upande ule waliokuwa wakipaki, kwa mbele kidogo ndiyo kulikuwa na duka ambalo nilipanga tukae pale na Rahma kwa sababu kulikuwa na viti upande wa nyuma, kwa hiyo ilikuwa ni lazima niwapite palepale walipopaki.

Nimewahi kusikia matukio kadhaa ya madereva hao wa Bajaj na bodaboda kushirikiana kufanya uhalifu, hasa pale inapoonekana mmoja wao ameonewa, nikajua lazima watakuwa wamenipania kwa jinsi nilivyomsulubu mwenzao. Hata hivyo, kwa sababu nilikuwa na nguvu za giza, tena za kutosha kabisa, sikuogopa chochote, ndiyo kwanza nikawa napiga mluzi huku nikielekea kule walikokuwa.

Cha ajabu, nilishangaa kuona kila mmoja akikimbilia kwenye chombo chake na kukiwasha, wakaanza kuondoka mmoja baada ya mwingine wakikimbia kwa kasi, sekunde chache baadaye eneo lote likawa tupu.

Hakukuwa na mashaka kwamba walikuwa wakinikimbia mimi, kwa sababu hata kama wanawahi abiria, wasingeweza kuondoka wote kwa mkupuo, tena kwa kasi kubwa wengine wakinusurika kugongana wao kwa wao.

Sikuelewa nini kimetokea mpaka wawe wananiogopa kiasi hicho lakini sikuwajali maana na mimi nilikuwa na majanga yangu mengi kichwani. Nilienda mpaka pale dukani, nikamsalimia muuza duka ambaye aliponiona tu, alishtuka sana, akaitikia kwa woga.

“Naomba Fanta,” nilisema huku nikimeza mate kwani mara ya mwisho kunywa soda, ilikuwa ni siku ile tuliposafiri kuja jijini Dar es Salaam.”

“Hatuuzi soda hapa!” alisema yule muuzaji, kauli ambayo nilishindwa kuielewa ina maana gani. Juu ya meza kulikuwa na chupa tupu za soda kuonesha kwambamuda si mrefu kuna watu walikuwa wakinywa soda, na mara kadhaa nilipita pale na kuona watu wakipata vinywaji, kwa nini aniambie kwamba hawauzi soda?

Nikiwa bado nimeduwaa, nikishindwa nimuulizeje, mara Rahma aliwasili, kumbe hatukuwa tumeachana umbali mrefu, akamsalimia yule muuzaji. Alimuita kwa jina lake na ilionesha wanafahamiana.

“Kumbe anaitwa Vero,” nilijisemea moyoni, alikuwa mwanamke ambaye kwa kumkadiria alionesha kuwa bado mdogo lakini mwenye uso uliokomaa na kupoteza nuru kama walivyo wanawake wengi wa vijijini kama kule kwetu Chunya.

“Huyu ni kaka yangu, unamjua? Anaitwa Togo,” Rahma alisema huku akinishika begani, nikamuona yule mwanamke akijaribu kuvaa tabasamu la uongo usoni.

“Tuletee soda, Togo unakunywa nini?” alisema Rahma, yule mwanamke akawa anababaika, kama anayeshindwa ajibu nini maana mimi aliniambia hawauzi soda. Rahma alinishika mkono huku akionesha kabisa kwamba anailazimisha furaha, tukaenda mpaka kwenye viti na kukaa, tukawa tunatazamana huku tukisubiri yule mwanamke aje atuhutubie.

“Unataka kuniambia nini?” alisema Rahma huku akikwepesha macho yake pembeni.

“Rahma! Najua unanifikiria vibaya sana kwa sasa, najua unaona kama nakufanyia makusudi kwa sababu sikupendi lakini ukweli ni kwamba ni matatizo makubwa sana na badala ya kunichukia, unatakiwa unionee huruma mwenzio,” nilianza kumbembeleza Rahma.

Kama nilivyosema awali, sikuw anajua mambo ya mapenzi kwa hiyo hata kubembeleza kwangu, nilikuwa naungaunga tu ilimradi Rahma anielewe. Niliendelea kushuka mistari kwa kuzunguka, nikamwambia kuna jambo zito ambalo halijui nataka kumweleza.

Maneno yangu yalimbadilisha kabisa Rahma, akawa ananitazama kwa shauku huku ile huzuni aliyokuwa nayo, ikiyeyuka ghafla. Ili kumuweka sawa, ilibidi nibadilishe mada kwanza, nikamuuliza vipi yule muuzaji mbona haleti hizo soda?

“Una kiu? Ngoja nimfuate,” alisema huku akiinuka lakini alipofika pale dukani, yule mhudumu alikataa katakata kutoka, akampa Rahma funguo ya friji na kutaka ajihudumie mwenyewe. Rahma aliichukua, akaniuliza nakunywa soda gani, akatoambili pamoja na yake, akaja mpaka pale tulipokuwa tumekaa, akazifungua zote na kurudisha funguo kwa mwenyewe.

“Kwa nini amekataa kuja kutuhudumia mwenyewe?”

“Hata mimi nashangaa! Achana naye tuendelee na yetu,” alisema Rahma, nikapiga funda moja kisha nikaendelea kuzungumza. Lengo langu lilikuwa ni kumpasulia ukweli kwamba baba yake alikuwa mwanachama wa jamii ya siri, vilevile baba yangu na mimi pia wameniingiza bila ridhaa yangu.

Niliona hiyo ndiyo gia nzuri ya kumuingia kwa sababu kama ningesema mimi mwenyewe ndiye niliyetaka kujiunga, angenishangaa sana na pengine nisingeweza kumshawishi. Nilianza kwa kumdadisi kwa kina kuhusu baba yake, nikitafuta sehemu ya kuanzia.

“Mbona unaniuliza kama una kitu unataka kuniambia? Tatizo langu wala halimhusu baba, ni mimi na wewe.”

“Ni stori ndefu Rahma ila naomba unielewe nitakachokwambia,” nilisema, nikashusha pumzi ndefu na kuamua liwalo na liwe. Nilitaka kwenda moja kwa moja, kwamba baba yake na baba yangu walikuwa wachawi. Cha ajabu, kila nilipotaka kusema hivyo, mdomo ulikuwa mzito, nikawa naumauma maneno, hali iliyosababisha anikazie macho.

Je, nini kitafuatia?
Leo fupi sana

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Sehemu ya 62



“Ni stori ndefu Rahma ila naomba unielewe nitakachokwambia,” nilisema, nikashusha pumzi ndefu na kuamua liwalo na liwe. Nilitaka kwenda moja kwa moja, kwamba baba yake na baba yangu walikuwa wachawi. Cha ajabu, kila nilipotaka kusema hivyo, mdomo ulikuwa mzito, nikawa naumauma maneno, hali iliyosababisha anikazie macho.
SASA ENDELEA...

“Mbona sikuelewi Togo?”
“Ni kuhusu wazazi wetu.”
“Wamefanya nini?”
“Wanajihusisha na...” kabla sijamalizia nilichotaka kukisema, jambo la ajabu lilitokea. Yule muuzaji wa lile duka, alifungua mlango na kutoka huku akikimbia, cha ajabu, hakuwa amevaa nguo hata moja.
“Vipi kwani mbonaumeshtuka?”
“Umemuona?”
“Nani? Vero? Nini cha ajabu kwani?” Rahma alinishangaa sana, na mimi nikawa namshangaa. Yaani mtu atoke dukani akiwa mtupu, halafu aanze kukimbia mitaani, siyo jambo la kushangaza hilo?”

“Itakuwa labda kuna anaenda kuomba chenji, tuendelee na mazungumzo yetu,” Rahma alizidi kunishangaza. Sikuelewa kwamba alikichukuliaje kitendo kile kiasi cha kutokipa uzito hata kidogo, hata baadhi ya wateja waliokuwa wamekaa upande wa pili, nao wakipata vinywaji, hawakuonesha kushtuka kabisa.
“Ndiyo atoke bila nguo?”
“Togo, umeanza kuchanganyikiwa nini?”
“Rahma, ina maana huoni kama hajavaa nguo yule? Kwa hiyo kumbe ndiyo maana alikuwa anajificha dukani?”
“Nani hajavaa nguo? Una matatizo gani Togo? Usije kunitia aibu hapa, hebu maliza twende,” alisema Rahma huku akimalizia soda yake. Nadhani alihisi huenda nikatokewa na maruweruwe kama yale yaliyokuwa yakinitokea.
“Basi Rahma, tuendelee na mazungumzo yetu,” nilijaribu kumsihi lakini alishaonesha kama ameingiwa na hofu ndani ya moyo wake, hakutaka kukaa tena eneo lile, ikabidi nimalizie soda yangu na kusimama.
Sikuwa nimemlipa yule muuzaji, lakini Rahma aliniambia kwamba nisijali yeye atampa hata baadaye. Nilijisikia vibaya sana ndani ya moyo wangu kwa jinsi Rahma alivyonipuuza ila sikutaka kumuonesha.
Kwa jinsi alivyonichukulia, hata kama ningemweleza kile kilichofanya nikakutana naye pale, huenda pia angenipuuza kwa hiyo nilichokifanya, niliamua kunyamaza na dukuduku langu moyoni.
“Hujamalizia ulichotaka kuniambia,” alisema Rahma wakati tukitembea kurudi ndani, nikamwambia asiwe na wasiwasi nitamueleza siku nyingine.
“Kwani siku hizi umeshapata mwanamke mwingine anayekuzuzua?”
“Hapana Rahma, na ndiyo maana nilitaka kuzungumza na wewe, lakini basi tuyaache.”
“Sikuelewi Togo na kama unaona ulichokifanya kwangu ni sawa, wala mimi sina cha kusema ila kumbuka chozi langu haliwezi kwenda bure,” alisema Rahma, nikajaribu kumbembeleza lakini ilikuwa sawa na kazi bure.
Mpaka tunaingia ndani, Rahma alikuwa akiendelea kulalamika tu, akaniambia anashukuru kwa yote niliyomfanyia na kumuumiza moyo wake. Nilishindwa cha kusema, ikabidi ninyamaze tu, bado wale madereva bodaboda na Bajaj pale nje hawakuwa wamerejea.
Tuliingia ndani lakini Rahma hakutaka kabisa kujishughulisha na mimi, alienda moja kwa moja sebuleni, mimi nikaenda chumbani huku nikiwa nimekosa kabisa furaha. Nilijilaza kitandani, nikaanza kutafakari tukio la yule muuzaji wa lile duka.
Nilichokihisi kwa harakaharaka, huenda alikuwa akitumia nguvu za kishirikina kwenye biashara yake maana nimewahi kusikia kwamba kuna wafanyabiashara ambao ukiingia kwenye duka lake au sehemu anayofanyia biashara, hata kama umevaa nguo, anakuona kila kitu lakini wapo wengine ambao inakuwa kinyume chake, kwamba muuzaji anakaa kwenye biashara akiwa hana nguo hata moja ingawakwa macho ya kawaida anaonekana amevaa nguo.
Lengo la kufanya hivyo inakuwa ni kuvutia wateja na kiukweli hata kwenye lile duka la pale nje, lilikuwa kubwa lenye kila kitu unachokihitaji na kiukweli alikuwa akifanya sana biashara kwa sababu kwa muda mfupi tu tuliokaa pale, wateja walikuwa hawakauki.
“Ulitaka kumwambia nini Rahma,” sauti ya baba ilinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo. Alikuwa amesimama pembeni ya kitanda changu, hata sikukumbuka ameingia saa ngapi, nilichoshtuka ni kumuona akiwa ndani.
“Mimi?” niliongea kwa kubabaika huku nikiinuka pale kitandani.
“Kwani nazungumza na nani?” baba aliniuliza akionesha kuwa na jazba, nikawa nababaika. Kwa jinsi ilivyoonesha, alikuwa anajua kwamba nilitaka kumweleza Rahma ukweli, jambo ambalo walinionya sana kwamba sitakiwi kutoa siri za jamii yetu kwa mtu yeyote asiyehusika.
“Tulikuwa tunapiga stori za kawaida tu.”
“Stori za kawaida ndiyo muende dukani?” baba alinihoji huku akinitazama kwa macho ya ukali, sikuwa na cha kujibu na kwa jinsi baba alivyo, nilitegemea kabisa kwamba pale lazima angenizibua makofi, nikawa nimekaa attention’.
“Kuna maagizo yako kutoka kwa Mkuu, usiku itabidi tukupeleke sehemu, umeyaanza mwenyewe lazima uyamalize,” baba alisema huku akigeuka na kuanza kuondoka, nikabaki na mshangao mkubwa, nikiwa sijui alichokimaanisha. Akiwa anamalizikia kutoka, aligeuka na kunitazama kwa macho makali.
“Ole wako ufumbue domo lako!” Nilishusha pumzi ndefu, mambo yalianza kuwa mengi na kunielemea kwa sababu kabla moja halijaisha, lingine lilikuwa likiibuka. Kwa jinsi nilivyozungumza na baba yake Rahma, nilitambua kwamba hizo salamu kutoka kwa Mkuu lazima zitakuwa zinahusu masharti ya uamuzi nilioufanya.
Niliona kama muda unaenda taratibu sana, sikutoka chumbani, hata chakula nililetewa kulekule na Rahma ingawa safari hii alionesha kuwa na chuki za waziwazi kwangu maana hakutaka hata kunisemesha wala kunitazama usoni.
Hatimaye jioni iliwadia, baba na baba yake Rahma, wakiwa tayari wameshajiandaa, walinifuata chumbani na kuniambia muda wa safari umewadia, wakanitaka nijiandae, baba Rahma akanipa koti kubwa jeusi.
“Kwani tunaenda wapi?”
“Jiandae bwana, maswali mengi ya nini?” alisema baba kama kawaida yake, nikajiandaa na muda mfupi baadaye, safari ilianza. Kwa jinsi nilivyokuwa nimevaa, haikuwa rahisi kwa mtu yeyote kunitambua, lile koti lilinibadilisha kabisa. Tulitoka na kuelekea moja kwa moja kwenye stendi ya mabasi ya Makumbusho, tukapanda kwenye ‘coaster’ moja ambayo mbele ilikuwa imeandikwa kwamba inaenda Bagamoyo. Sikuwa nimewahi kufika Bagamoyo zaidi ya kusoma tu darasani kuhusu mji huo wa kihistoria.
Basi tulienda mpaka tulipofika sehemu moja iitwayo Mlingotini, tukateremka kwenye gari na kuvuka barabara, tukaanza kutembea kwa miguu. Tulienda umbali mrefu sana maana mpaka inafika saa tano za usiku, bado tulikuwa tukitembea.
Hatimaye tuliwasili kwenye eneo lililokuwa na nyumba kama tatu hivi, moja ikiwa imeezekwa kwa bati na zile nyingine kwa makuti, baba akabisha hodi ambapo sauti ya mwanamke ilisikika ikitukaribisha.
Muda mfupi baadaye, mwanamke mmoja mzee alitoka, ilionesha alikuwa akifahamiana vizuri na baba na baba yake Rahma kwani aliwakaribisha kwa uchangamfu, tukaingia ndani na kukaa kwenye jamvi lililokuwa pale sebuleni.
“Ndiyo huyu?” aliuliza yule mwanamke, baba akamjibu kwamba ndiyo mimi, sikuelewa kwamba ndiyo mimi nimefanyaje na kwa nini ameniuliza, ikabidi niwe mpole.
“Mchumba hujambo? Ukifanikiwa na mimi nataka uninunulie gari,” alisema yule mwanamke huku akitabasamu, mapengo yake yakaonekana. Sikuelewa kwa nini amesema vile, nikazidi kuwa gizani. Alinishika mkono na kuwapa ishara akina baba kwamba wamsubiri, tukatoka nje na kwenda kwenye kibanda cha makuti.
Wakati tunatoka, nilimsikia baba akimwambia baba Rahma kwamba kuwana mtoto kama mimi ni hasara, wakacheka. Sikuelewa kwa nini baba amesema vile lakini sikujisikia vibaya maana mimi na baba kukwaruzana ni jambo la kawaida kabisa, ingawa mimi ndiyo nilikuwa mwanaye kipenzi.
“Nimepata salamu zako kwamba umechagua kuwa tajiri, ombi lako limekubaliwa lakini kuna masharti inatakiwa kabla siku zako saba hazijaisha, uwe umeshaanza kuyafuata, vinginevyo utakufa,” alisema yule mwanamke, macho yakanitoka pima.
Je, nini kitafuatia?
 
Back
Top Bottom