Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA TATU
"Kama nilivyokwambia haya mazungumzo hayajawahi kufanyika wala hii siku haijawahi kutokea. Asante sana Gabriel" walipeana mikono na kuondoka kwa sababu alijua kwamba angetumiwa taarifa zote za namna ya kukutana na watu hao ili awape majukumu ya kuyafanya. Cleopatra Gambo aliyafanya hayo yote kuwatumia makomando ya jeshi ili kulinda mahusiano yake yeye na mdogo wake kwani misheni ambayo ilikuwa mbele yake ilikuwa ni kumfuta Ashrafu kwenye macho ya watu kwa kumkamata na kumfunga sehemu ambayo aliahidi kwamba hakuna mwanadamu angekuja kujua kwamba mwanaume huyo aliwahi kutokea.

Kama angewatumia vijana wake mdogo wake angekuja kujua pale ambapo Ashrafu angepotea lakini kuwatumia makomando lingeonekana kuwa suala la kitaifa ndiyo maana wametumika makomando hivyo yeye angejiweka nje ya lawama lakini kiuhalisia hakuwa tayari kuendelea kumuona Ashrafu kuendelea kufanya yale ambayo alikuwa anayafanya nchini.

Wakati amefika kwenye gari na gari hizo zinaanza kuondoka, alipokea simu kutoka kwenye namba ambayo ilikuwa ni ngeni.
"Kwanini umefanya hivi dada? Ndiyo maana niliishi maisha yangu yote nikiwa nakuchukia sana kwa sababu hata siku moja haukuwahi kuijali furaha yangu. Unakuja kumpa taarifa zangu binti wa kawaida kama yule mpaka akapajua ninapo ishi?"
"Maria nisikilize kwanza"

"Hakuna mazungumzo ambayo mimi nitakuwa nayo na wewe kwa sasa kwenye maisha yangu ila nataka nikwambie jambo moja kwamba kile ambacho wewe ulikuwa unakitafuta na watu wako ndicho kinaenda kutokea kuanzia sasa" simu ilikatwa. Alibaki anaongea mwenyewe hivyo ikamlazimu kuipiga tena namba hiyo lakini haikuwa ikipatikana kabisa na baada ya muda akaambiwa kwamba kwenye usajili hakukuwa na namba kama hiyo ilikuwa imekosewa hivyo alitakiwa kuangalia kwa umakini kabla ya kupiga. Alibaki kwenye hali ya mawazo sana lakini kutokana na uchovu ambao alikuwa nao alilazimika kwenye kupumzika kwanza ndipo kesho yake angejua ni kipi ambacho alitakiwa kukifanya.

Wakati huo ambao Anelia alikuwa ametoka kumfuatilia Suzane alipitiliza moja kwa moja mpaka Kawe kwa raisi kwa sababu alimwambia kwamba ilikuwa ni mhimu sana kwa wao kukutana wakati huo. Alikuwa anaendesha gari kwa spidi kubwa sana ili kuweza kuwahi huko kwani aliahidiwa kwamba kama akiifanikisha kazi hiyo basi naye raisi angeweza kumsaidia kwa kile ambacho alikuwa anakihitaji yeye. Alitumia muda mchache sana kuweza kufika huko ambako alimkuta mheshimiwa raisi akiwa anamsubiri.

"Umenitisha sana kuniambia kuna habari ambazo hazitakiwi kulala. Unaweza ukanipa hizo taarifa mapema?" walikuwa wamekaa kwenye Balcony wakati anahitaji mrembo huyo aweze kumpatia hizo taarifa.
"Nimefanikiwa kumjua mtu ambaye huenda ana uhusiano wa moja kwa moja na hili jambo"
"Unaweza kuniambia ni nani?"
"Brigedia Mariana Amboni"
"Unaweza ukanikumbusha kwamba ndiye nani huyo?"
"Ni moja kati ya wanajeshi ambao waliifanya kazi kubwa sana kwenye taifa hili ila kwa sasa amestaafu"
"Umeyajuaje haya mambo?"

"Nadhani wewe mwenyewe ulinipa kazi kwa ajili ya kuwachunguza Holy Trinity kwa kila hatua wanayo ipiga hivyo nilikuwa namfuatilia kiongozi wao kwa ukaribu sana mpaka anafika ndani ya ile sehemu ambayo nadhani hata yeye alielekezwa tu maana alionekana kuwa mgeni na ilikuwa mara yake ya kwanza kuweza kufika kule"
"Unamaanisha kwamba huenda kuna mtu mwingine ambaye anaweza kuwa na hizi taarifa sio?"
"Ndiyo mheshimiwa"
"Enhe endelea"

"Kitu ambacho kimenishtua sana kuhusu yule mama ni jinsi anavyo lindwa, nyumba yake inalindwa sana kiasi kwamba sio bure lazima kuna siri kubwa sana anayo na ni kwanini aweze kujificha sehemu kama ile na sio mjini?"
"Maana yako ni ipi labda?"
"Kuna kitu atakuwa anakijua kuhusu Remy Claude"
"Whaaaat?"

"Kwenye taarifa zangu ambazo nilizifuatilia ni kwamba kikosi cha siri cha mkurugenzi cha Holy Trinity kilimvamia mwanaume huyo ili wamkamate lakini baadae aliwafanya kitu kibaya sana kisha akamuacha kiongozi wao tu akiwa salama na inaonekana kwamba kuna onyo alimpatia kuhusu kumfuatilia na jambo hilo akawa amelifikisha kwa mkurugenzi ambaye baada ya pale alienda kuwaona kwenye kambi yao ila sina uwezo wa kuingia kule hivyo sikufanikiwa kujua kilicho endelea na baadae ndipo Suzane akawa amefanya uamuzi wa kwenda ile sehemu" raisi alitabasamu kwa sababu alikuwa na uhakika kwamba mwanamke huyo hakuwa anamwambia kila kitu.

"Kwanini hauniambii taarifa iliyo kamili Anelia?" Anelia alimgeukia mheshimiwa raisi
"Kwa sababu bado haujaitimiza ahadi yangu hata moja"
"Unataka nini?"
"Uliniahidi kwamba ungenisaidia kuufahamu ukweli wa wazazi wangu"
"Nilikuahidi na hilo nitalitekeleza kwa sababu lipo ndani ya uwezo wangu ila unatakiwa kuwa mpole kwa sababu hili sio zoezi la siku moja. Halafu ngoja nikuulize kitu"

"Unataka kufanya nini ukishamfahamu mtu ambaye alihusika na kupotea kwa wazazi wako?"
"Nadhani kama yupo hai mtu huyo basi sitaishi kwa amani maisha yangu yote inatakiwa alipe kwa kila ambacho alikifanya"
"Vipi kama huenda ni miongoni mwa watu ambao unawapenda sana?"
"Sijali kuhusu hilo tena kwenye maisha yangu"
"Kuna watu ambao tayari nimewaagiza kuifanya hiyo kazi muda wowote wananiletea ripoti hivyo unaweza ukaniambia hicho ambacho unazungusha maelezo ili kunificha"
"Kabla Suzane hajaingia kwenye ile gari nilifanikiwa kuweka kifaa cha mawasiliano"
"Enhe!"
"Hivyo baada ya kutoka pale kuna mawasiliano aliyafanya na mtu na nilikuwa nayasikia moja kwa moja"

"What is it?" Anelia hakuongeza neno lolote lile zaidi ya kumsikilizishia mheshimiwa sauti ya Suzane ikiwa inasikika wakati anampigia mkurugenzi wa usalama wa taifa.
"Whaaaat? Unataka kuniambia huyo brigedia ni mdogo wa damu kabisa wa mkurugenzi wa usalama wa taifa?"
"Ndiyo"
53 INAFIKA MWISHO.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA NNE
"Hahahah hahahah hahah noooo hili haliwezekani"
"Na huyo brigedia ndiye njia pekee ya kumpatia Remy" mheshimiwa alisimama na kucheka sana baada ya kuambiwa hayo maneno.
"Haya mambo yanawezekanaje?"

"Bosi anaonekana ana mambo mengi sana ambayo anayajua ila hataki kuutoa ukweli wote ambao anao. Nimetambua kwamba huyo brigedia ni ndugu yake wa damu na huyo brigedia anaonekana kuwa mtu wa mhimu sana kwa Remy na huenda ndiye ambaye amemlea na kumtengeneza kwa mikono yake mwenyewe"
"Are you sure about this Anelia?"
"Yes sir!"
"Unaweza kwenda kwa sasa, hapa palipo bakia niachie mwenyewe nipamalizie, asante sana kwa hili muda mfupi tu utapatiwa ripoti nzima ya kifo cha wazazi wako"

"Nitashukuru sana mheshimiwa" waliagana huku raisi akionekana kama kuchanganyikiwa sana kwa sababu ilikuwa ni hatari kubwa mno kama hata mkurugenzi wa usalama wa taifa alikuwa ana siri nyingi sana ambazo mheshimiwa hakuwa akizifahamu kabisa. Aliichukua simu yake na kuipiga kwa CDF ambaye alimtaka afike haraka sana Ikulu wakati huo huku naye akitoka ndani ya jumba lake hilo na kurudi Ikulu usiku huo huo.

CDF alifika haraka sana ndani ya Ikulu ambapo alipewa maelekezo kwamba mheshimiwa alikuwa akimsubiri ndani ya ofisi yake. Alitembea haraka haraka sana maana lilionekana kuwa jambo la mhimu mno ambalo lilipaswa kufanyika wakati huo.
"Unamfahamu brigedia Mariana Amboni?" lilikuwa swali la kwanza hata kabla hajapewa salamu CDF kitu ambacho kilimshangaza sana.
"Ndiyo mheshimiwa"
"Yuko wapi?"
"Kwa sasa amestaafu"
"Alifikisha umri wa kustaafu?"
"Hapana"
"Sasa alistaafu vipi?"

"Alikuwa na matatizo ya kiafya hivyo kutokana na kazi kubwa sana ambazo alilifanyia taifa ikatoka ruhusa kwamba akapumzike mpaka pale ambapo atataka yeye mwenyewe kurudi jeshini na kama hatataka basi anapewa nafasi ya kustaafu moja kwa moja"
"Unaweza kunipa taarifa zake baada ya yeye kustaafu?"
"Hapana, baada ya kutoka jeshini alipotea kwa muda mrefu sana na mpaka leo hajawahi kuonekana tena"
"Kwanini haukuwahi kulifuatilia hili jambo?"

"Kwa sababu wakati anastaafu ripoti zilizopo ni kwamba aliomba usiri juu ya maisha yake kwani alihitaji kuyaishi maisha ya kawaida tu hivyo hakuhitaji mtu yeyote yule kuweza kumfuatilia tena"
"Wewe ulikuwepo wakati anastaafu?"
"Hapana, wakati huo sikuwa kwenye hii nafasi ila nilikuwa namfahamu sana kwa sababu sifa zake zilikuwa zimetapakaa kila sehemu ya jeshi na jina lake lilikuwa likichukuliwa kama alama ya ujasiri jeshini"
"Na kuhusu yeye ulipataje taarifa?"

"Taarifa zake zipo kwenye kila kambi ya jeshi nchini na ni miongoni mwa taarifa ambazo ukipata nafasi ya kuwa mkuu wa majeshi lazima uzisome ili kuzitumia kuwahimiza vijana kulipambania taifa lao ila baada ya kustaafu hakuna taarifa yake yoyote ambayo imewahi kuonekana wala kupatikana"
"Unaweza ukanipa taarifa zake chache?"

"Ndiyo, ni mwanajeshi wa zamani wa taifa hili ambaye alifanikiwa kuyapata mafunzo kwenye kambi tatu tofauti za kikomando ikiwemo ya Morogoro hapa Tanzania lakini baadae baada ya kufanya vizuri alipelekwa nje ya nchi ambako alimaliza miaka mitatu na baada ya kurudi ndipo alifanikiwa kupewa nafasi ya kuwa brigedia ambapo alianza kuongoza vikosi kadhaa ambavyo vimezalisha wanajeshi bora zaidi kwenye hiki kizazi ambao wengi mpaka leo ndio wana nafasi kubwa jeshini na wanaifanya kazi kwa weledi sana na hii yote ni kwa ajili ya mchango wake mkubwa ndiyo maana jina lake huwezi ukakuta hata mtu mmoja analitamka vibaya kwani ni mtu mwenye heshima kubwa sana ndani ya jeshi" mheshimiwa alibaki anashangaa wakati anapewa taarifa nzito sana za mwanamke huyo.

"Je amewahi kuwa na ndugu kwenye maisha yake?"
"Hapana, kwa taarifa zilizopo ni kwamba walizaliwa wawili lakini kwa bahati mbaya mwenzake na wazazi wake walikufa kwenye ajali mbaya akafanikiwa kubakia yeye mwenyewe tu hivyo hana ndugu yeyote yule"
"Na kuhusu familia yake binafsi?"

"Hii ni habari mbaya kidogo ambayo huwa haitakiwi kusambazwa sana ila ni kwamba kwa vipimo vya madaktari hakuwa na uwezo wa kuzalisha kitu ambacho kilimfanya awe na chuki sana na watoto kwani kila anapo waona alikuwa anakumbuka kuhusu tatizo lake na kujikuta akiwa na simanzi kila wakati hivyo akaamua kuishi kipweke na ndiyo sababu kuna watu huwa wanahisi kwamba huenda aliamua kwenda mbali kujitenga na watu ili aishi mwenyewe bila kuwa na mawazo mengi"
"Na kuhusu mpenzi?"
"Kuna taarifa ambazo sio za kweli kwa sababu kuna watu huwa wanahisi zinazushwa tu ili kutaka kulichafua jina lake. Inasemekana kwamba aliwahi kuonekana mara moja na Dominic Sawa sawa"
"Umesema Dominic Sawa sawa?"
"Ndiyo mheshimiwa japo hazikuwa taarifa za kuaminika sana kwani ni kama zilitengenezwa ili kuweza kumchafulia jina"

"Asante kwa maelezo yako na kukusumbua usiku huu, nililisikia hili jina kwa mtunza historia wetu sasa sikutaka kuamini kama taifa letu limebahatika kupata shujaa mkubwa kama huyu hivyo nilitaka nipate uhakika kutoka kwako maana najua hizi taarifa za wanajeshi wewe ndiye unazo kwa wingi. Kwa sasa unaweza kwenda ila nahitaji file zima la maisha yake hapa asubuhi niweze kuzipitia habari hizi kwa umakini huenda kuna siku nitahitaji kukutana naye"

"Sawa mheshimiwa, uwe na usiku mwema" CDF aliaga na kutoka nje, alisimama na kugeuka nyuma akiwa na maswali mengi sana. Ilikuwa ni ghafla sana mkuu wa nchi kuzihitaji taarifa za mwanamke huyo na alijua kabisa kwamba haikuwa bure lazima kulikuwa kuna kitu nyuma yake. Alianza kuunganisha doti kuhusu mtu huyo na maswali ya raisi kisha akawa anakumbuka jinsi mkurugenzi wa usalama wa taifa alivyodai kuanza kumchunguza mheshimiwa raisi pamoja na kuhitaji watu ambao wangeifanya kazi hiyo bila yeye kujulikana, hisia zilianza kumjia kwamba huenda brigedia Mariana Amboni akawa kati kati ya huo mchezo maana yake kama hisia zake zitakuwa sawa huyo mwanamke ndiye alikuwa mtu wa mhimu zaidi kwenye huo mchezo.

54 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA TANO
Raisi alibaki kwenye ofisi yake ambapo alisimama na kuifungua simu yake, aliifungua picha ya mwanamke huyo Mariana Amboni kisha pembeni akawa anaiangalia picha kubwa ya mkurugenzi Cleopatra Gambo. Alicheka sana mheshimiwa, wanawake hao walikuwa wanaicheza karata moja ngumu sana ambayo huenda bila msaada mkubwa wa Anelia Baton asingeweza kuing'amua haraka kisha akaitoa simu yake.

"Mpango umebadilika, vijana utakutana nao kesho lakini mimi na wewe tunatakiwa kukutana muda huu ndani ya Kilimanjaro Hotel kwenye chumba namba 101 haraka sana" hakutaka hata kusubiri jibu upande wa pili akaikata simu hiyo na kutoka ndani ya ofisi yake.

Ndani ya nusu saa baadae usiku wa manane sana mheshimiwa alikuwa ndani ya chumba ambacho alikuwa ameahidi kuwepo, alikuwa upande wa dirishani akiwa anaangalia chini ya jengo hilo kubwa ambapo aliona msafara wa gari mbili ukiwa unaingia ndani ya eneo hilo, alitabasamu.

Ulinzi ulikuwa ni mkali sana ndani ya hilo eneo ambapo mwanaume ambaye alikuwa anafika hapo alikaguliwa sana na walinzi wake ambao alikuja nao walibaki nje kisha yeye akaingia ndani kukutana na bosi wake akiwa na begi ya laptop mkononi.

Walikumbatiana na kusogea kwenye meza kubwa kisha wakakaa hapo. Mwanaume ambaye alifanikiwa kufika ndani ya hiyo sehemu ndiye yule ambaye alipigiwa simu na mheshimiwa kwamba anamhitaji haraka sana aweze kufika Tanzania na ndiye ambaye kesho yake alitakiwa kuwepo kwenye kikao na wanaume watano ambapo mmoja alipotea ambaye ni ULIMBOKA.
"Bosi ni usiku sana saivi, kuna usalama kweli?"
"Hapana kungekuwa na usalama ningehitaji tuonane asubuhi. Kuna kazi ambayo inatakiwa kufanyika haraka sana kabla hakujapambazuka" mheshimiwa aliongea akiwa anaitoa karatasi ndogo kwenye mfuko wake na mwanaume yule aliipokea kwa mashaka sana akiwa anamwangalia mheshimiwa.

"Hiyo ni address na namba ya nyumba najua kupitia hiyo unaweza kuidukua nyumba hiyo ukapata taarifa za siri za mmiliki na kila kinacho endelea hapo sio?"
"Ndiyo mheshimiwa kama tu mmiliki wa nyumba aliweka taarifa zake hata kama ni kwa siri sana inawezekana kuzipata"
"Itachukua dakika ngapi?"
"Tatu tu"
"Do it" huyo mwanaume licha ya kuwa mtu hatari sana lakini pia alikuwa ni mdukuzi wa kutisha mno ambaye alikuwa amefanya kazi nyingi sana za hatari ila ni wanadamu wachache sana ambao walikuwa wanalifahamu hilo au kuufahamu ukweli kuhusu mtu huyo.

"Mmiliki wa hili eneo anaitwa Mariana Amboni, ni mwanajeshi mstaafu kwa sasa na ni mama wa mtoto mmoja ambaye hakuna taarifa yake yoyote"
"Umesema ana mtoto mmoja?"
"Ndiyo bosi na huyo mtoto ndiye ameandikwa kama mmiliki wa hiyo nyumba" mwanaume huyo aligeuza laptop yake ili mheshimiwa aweze kujionea mwenyewe.
"oooooh fu**k na kuhusu familia?"
"Ana ndugu mmoja japo kwenye hiyo sehemu ambayo inaonyesha family tree pamewekwa kivuli, hii ina maana kwamba taarifa za huyu ndugu yake zimefichwa"

"Hahaha hahahah hahahah kwenye nchi hii ni nani ambaye anajiamini kuweze kunifanya mimi mpuuzi kiasi hiki?" mheshimiwa alicheka na kuongea kwa jazba sana huku akiendelea yeye mwenyewe.
"Oooooh Cleopatra son of a b***" alitukana tusi zito sana kwenda kwa mkurugenzi. Huyo mwanamke hapo taarifa za CDF zilionyesha kwamba hakuwa na uwezo wa kuzaa na wala hakuwa na ndugu yeyote lakini taarifa za siri zilikuwa zina eleza kwamba mwanamke huyo alikuwa mama wa mtoto mmoja na alikuwa na ndugu mmoja ambapo wote walikuwa ni siri nzito sana.

kisha akakumbuka tena CDF alimwambia kwamba kuna taarifa zilikuwa zinadai kwamba mwanamke huyo aliwahi kuonekana na Domimic Sawa Sawa. Maana yake ni kwamba kulikuwa na mawili, kama sio kuzaa na Dominic Sawa Sawa basi alikuwa amemlea mtoto wa Dominic Sawa Sawa kwa siri kubwa sana na huenda ndiyo sababu ya yeye kuweza kustaafu jeshi na kutohitaji maisha yake yaje kuwa wazi tena.

"Ina maana mtoto mmoja wa Dominic Sawa Sawa yupo hai? Oooooh shiiiiiit!" alitamka huku akiwa anabamiza chupa kubwa ya wine chini kwa hasira sana. Alikuja kulitambua hilo akiwa amechelewa sana mheshimiwa na ndio wakati ambao alianza kuelewa kwamba ni kwanini ilitoka taarifa kama ile kwenye gazeti ili kumtaka kupiga goti hadharani na kuomba msamaha, ilikuwa ni kwa sababu mtu huyo alikuwa amerudi kuchukua kile ambacho wao walimbebea. Mwanaume aliyekuwa kwenye laptop yake hata yeye baada ya kusikia jambo hilo lilimshtua sana.

"Bosi hili jambo haliwezekani kabisa"
"You fAILED ME BIG TIME BOY" alimgeukia mwanaume huyo na kumkwida shingoni akiwa anamtamkia kwa hasira sana kwamba alimfelisha sana.
"Bosi kila kitu kilifanyika kama ilivyokuwa inatakiwa"
"Mpaka leo tusingekuwa hapa mpuuzi mkubwa wewe kama kazi ilifanyika kwa usahihi kama unavyotaka kuanza kunidanganya hapa. Mimi na wewe tutalizungumza hili kwa marefu ili unipe sababu za msingi za mimi kutowaua ninyi nyote wapuuzi wakubwa, for now huyo mwanamke nakupa masaa mawili awe kwenye mkono wako vinginevyo nakuua wewe" alitamka kwa msisitizo mkubwa sana mheshimiwa huku akiwa anabeba kofia yake na kutoka ndani ya chumba hicho kwa hasira kali sana kwa sababu vijana wake walionekana kufanya kazi kipumbavu sana kitu ambacho hakukubaliana nacho hivyo kabla ya asubuhi alitoa amri kwamba mwanamke huyo awe amepatikana vinginevyo kijana wake huyo ndiye alitakiwa kufa kwenye mikono yake hivyo ilikuwa ni kwake kuchagua cha kufanya.

Mkurugenzi baada ya kushindwa kuelewana na mdogo wake wakati ambao alipigiwa simu akiwa anatoka kwenye kambi kuu ya jeshi la nchi alirudi nyumbani kwake kuweza kulala lakini hakupata hata lepe la usingizi kwa sababu moyo wake ulikuwa unamuenda mbio sana na alikuwa anaumia sana kwa kile ambacho alikuwa amekifanya, alijihisi hatia kubwa sana ndani ya moyo wake na kuona amemkosea sana mdogo wake hivyo alitamani kumpigia simu ili amuombe msamaha.

Aliamka kutoka kitandani na kuipiga namba nyingine ya siri sana ambayo ilikuwa ni ya chumbani kwa mdogo wake. Simu iliita mpaka ikakata, alipiga kwa mara ya pili lakini bado haikupokelewa. Moyo wake ulianza kwenda mbio sana asijue kwamba shida ilikuwa wapi hivyo akalazimika kupiga simu kwa walinzi wa mdogo wake lakini hakuna hata mmoja ambaye alikuwa anapokea simu. Alishtuka sana Cleopatra Gambo, hilo halikuwa jambo la kawaida bali kulikuwa na hatari ambayo ilikuwa inajieleza mbele ya macho yake na kwenye moyo wake. Alivaa haraka sana na kuchukua silaha kisha akatoka nje na kuwataka vijana wake waondoke naye kwani kulikuwa na dharura ya mhimu sana wakati huo hivyo msafara wa gari tatu ukaingia barabarani ukiwa kwenye kasi mno.

55 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA SITA
Wakati msafara wake unafika Chalinze, walipishana na gari ambazo zilikuwa zinaenda njia ambayo wao walikuwa wametokea, zilikuwa ni gari mbili za gharama na zenye vioo vyeusi tii zikiwa kwenye mwendo mkali kuliko hata msafara wake lakini hawakuzitiilia sana maanani kwa sababu ulikuwa ni usiku ni watu wengi sana walikuwa wanapenda kuutumia wakati huo kuyakamilisha yale ambayo hawakutaka ulimwengu uyajue.

Mida ya saa kumi na moja kasoro alikuwa anaingia ndani ya eneo hilo akiwa na haraka sana kwa sababu hata kama hawakuwa sawa kwenye maelewano ila uhalisia ni kwamba alikuwa anampenda mdogo wake kuliko kitu chochote kile kwenye maisha yake. Aliruka kwenye gari na kuanza kukimbilia kwenye geti la nje la senyenge ambalo lilikuwa wazi na chini kulikuwa na wanaume wawili ambao walikuwa wamekufa tayari kwa kukatwa na visu. Hofu ilianza kuzidi kumtanda kwenye nafsi yake maana hakuwa tayari kuona kile ambacho angekutana nacho mbele yake

Kwenye geti kubwa la kuingilia ndani wanaume watatu walikuwa wametandikwa risasi za kichwa na kufa hapo hapo. Walinzi wake waliizunguka nyumba hiyo kwa nje lakini hakuna mtu hata mmoja ambaye alikuwa hai. Baada ya kupewa taarifa hiyo ulikuwa ni wakati sasa wa yeye kuingia ndani mwenyewe ambapo hakutaka kuongozana na mtu yeyote yule, baada ya kufika sebuleni, mlinzi mkuu wa mdogo wake alikuwa amekufa kikatili kwa kuchomwa chomwa visu vingi sana kisha mwili wake ukalazwa juu ya meza. Alipandisha ngazi taratibu mwili ukiwa unamtoka jasho sana, alipofika mlangoni alihema na kusali kabla ya kuingia kwenye chumba cha mdogo wake ambacho alikuwa ana uhakika kwamba ndicho alikuwa anakitumia kulala.

Aliusukuma mlango huo akiwa ameyafumba macho yake ila baada ya kuyafumbua chumba kilikuwa cheupe, alikagua kila sehemu lakini hakuona dalili ya uwepo wa mtu yeyote yule. Hakuona sababu ya kuendelea kukaa hapo alimshukuru tu Mungu kwa sababu hakuikuta maiti ya mdogo wake ila wakati anatoka alikiona kidani kimoja kidogo sana ambacho kilikuwa chini ya sakafu kikiwa kimekatika.

Aliinama na kukiokota kwa hisia kali sana, alifunua suti yake shingoni, hata yeye alikuwa nacho kama hicho. Vilikuwa ni vidani ambavyo vilikuwa vinawatambulisha wao kama ndugu na wasingekuja kutengana kamwe, maana yake kama mdogo wake alikuwa amekitunza bado alikuwa anamtambua yeye kama dada yake na kumpenda vinginevyo angelikuwa ameshakitupa. Chozi lilimshuka taratibu kwenye shavu lake akiwa amepiga goti pale chini na kidani chake mkononi na hapo ndipo akili yake ilifunguka akazikumbuka zile gari ambazo alipishana nazo akajua basi ndio wale ambao walifanya yote hayo.

"Nisamehe sana mdogo wangu, kwa gharama yoyote ile mimi nitakutafuta sehemu yoyote ile na utakuwa salama. Dada anakupenda sana" alitamka kwa hisia sana akiwa anatoka ndani na kuwataka wanaume kadhaa wabaki wakiliweka eneo hilo sawa lakini wengine aliwahitaji warudi Dar es salaam haraka sana na msafara wa gari mbili na wakati huo ilikuwa ni saa kumi na mbili asubuhi ambapo watu barabarani walikuwa wakizishangaa gari hizo ambazo zilikuwa zinapita kwa mwendo mkali kana kwamba zilikuwa kwenye mashindano ya formula 1.

Robert vijana wake wote walikuwa wamefika ndani ya jiji la Dar kama alivyokuwa amewapa maagizo watoke Arusha kwani ni wakati wa kumtafuta mtoto wa bosi wake ulikuwa umewadia kama alivyokuwa amewapa taarifa vijana wake hao. Msafara wa watu saba ulikuwa umefika ndani ya jiji na kuwafanya jumla kuwa na watu tisa.

Huyo ndiye mwanaume ambaye aliwahi kuwa mlinzi mkuu wa tajiri Dominic Sawa sawa hivyo alikuwa na mengi sana ambayo alikuwa anayajua kwenye moyo wake, mambo ambayo yalimtesa sana kwenye maisha yake mpaka inafikia kipindi kile ambacho alikuwa mtu mzima haswa lakini bado hakuwahi kukata tamaa ya kuweza kuwalipizia kisasi wale wote ambao walihusika moja kwa moja na kupotea kwa bosi wake japo hakuwahi kuwapata moja kwa moja kuweza kuwajua kwamba ni akina nani. Watu hao baada ya kufika ndani ya jiji, Robert na Hezroni walikuwa tayari wamesha ondoka Downtown na kuhamia maeneo ya Kimara Suka kwenye nyumba ambayo ilikuwa imejengwa barabara ya kuelekea Golani. Wakiwa ndani ya jumba hilo walikuwa kwenye chumba ambacho kilikuwa kimetengwa kwa ajili ya mikutano ili kuuchora mchezo mzima na namna unavyo takiwa kuchezwa mpaka dakika ya tisini.

"Boss ni muda mrefu sana tangu sasa umekuwa ukitupatia taarifa nusu nusu, tunafanya kazi kwa pamoja ni vizuri zaidi kama ukituweka wazi kwa sababu sisi sote ni wamoja humu ndani na tupo tayari kuifanya kazi hii kama yetu. Licha ya kwamba unatulipa kuifanya kazi hii lakini imefikia hatua sisi tumekuwa kama familia hivyo tunahitaji utuambie ukweli kwamba ni kipi kinaendelea kwenye maisha yako na huyo mtu" Nicole ambaye alikuwa ni moja kati ya wadukuzi mahiri sana akiwa anasaidiana kwa ukaribu na Hezroni ndiye ambaye alikuwa anamuuliza Robert swali hilo huku wenzake nao wakiitikia kuonyesha kwamba wanakubaliana na jambo hilo. Mzee huyo alisogea upenuni mwa hiyo sehemu eneo ambalo lilikuwa linapitisha hewa safi sana, aliufunga mlango na kuvuta sigara yake kwa dakika mbili kabla ya kurudi ndani ambako aliamini moshi huo ungewakera vijana wake kisha akarejea akiwa anajikohoza.

"Ni jambo ambalo nimewaahidi kwa muda mrefu sana na hata bila kunikumbusha nilikuwa naenda kuwaambia kwa namna moja au nyingine na naenda kuwaambia kuhusu hili ila sina imani sana nahisi kwamba kuna mtu anatusaliti" kauli yake iliwashtua wote humo ndani kwa sababu hawakuelewa kwamba ni kwanini kiongozi wao angeweza kuongea kauli kama hiyo.
"Kivipi bosi?" aliuliza mwanaume mmoja ambaye alikuwa amevaa suti nyeusi.
"Kwa sababu hakuna mtu ambaye alikuwa anajua kwamba mimi nipo hai maana nilipotea kwenye maisha ya kawaida kwa miaka ishirini huu unaenda wa ishirini na moja lakini ghafla sana nikavamiwa na mwanaume ambaye tuliwahi kujuana miaka ya zamani sana akiwa anahitaji kuniua. Kuna ambaye anaweza kunisaidia labda kufikiri kwamba mtu yule alijuaje kwamba mimi ningekuwa ndani ya lile eneo? Huenda mimi nimeanza kuzeeka vibaya sana" wote walibaki wanaangaliana kila mmoja akiwa anaonekana kuwa na maswali mengi sana kichwani mwake. Mzee huyo alitabasamu na kuendelea.

"Hiyo simulizi ya maisha yangu na huyo mtu ambayo mnataka kuisikia mnaweza mkaisikia kidogo sana ila sehemu nyingine mnaweza mkaipata kwa masharti maalumu ila kabla ya huko nataka niwape mkasa wangu mimi na huyo mwanaume aitwaye Justin ambaye ndiye alinivamia kule Arusha"

"Mimi sio Robert kama wote humu ndani mnavyo nijua wala mimi sio mzee kama ambavyo naonekana nipo wala mimi sio mzaliwa wa Uganda kama ambavyo wote mnajua humu ndani. Jina langu mimi ninaitwa Shinji Salumu, mzaliwa wa kisiwa cha pemba ila kwa bahati mbaya sana jina langu ukienda mahali popote pale huwezi ukalikuta kwa sababu niliufuta na kuupoteza utambulisho wangu kiasi kwamba imebakia kwamba hajawahi kutokea mtu kama mimi kwenye haya maisha kabisa"

"Najua hili litakuwa linaonekana jambo la ajabu kwenu kwa sababu huenda hamkuwahi kabisa kulitarajia ila huo ndio uhalisia, niliamua kuishi hivi ili niendelee kuwa hai kwa sababu kama ningeishi kwenye maisha yale ya zamani ningekuwa nimekufa muda mrefu sana kwani nakumbuka baada ya lile sakata la bosi kufa ulipitishwa msako mkali sana kimya kimya kuona kama kuna mtu anaishi hususani baada ya baadhi ya miili kutoonekana ambayo ni mwili wangu na wa Ashrafu ila baadae walikuja kukata tamaa baada ya kutoonekana kwa dalili zozote zile kwamba tupo hai. Hiyo ndiyo sababu ambayo ilinifanya niendelee kumtafuta Ashrafu kwa sababu baadae nilikuja kugundua kwamba mwili wake haukupatikana licha ya kuona kuna mtu siku ile ameielekezea bastola kwake wakati nikiwa kwenye hali mbaya sana"

56 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA SABA
"Mnaweza kujiuliza kwamba inakuwaje niwe hivi na bado Justin aweze kunitambua? Jibu ni rahisi sana kwanza ni kwa sababu jina langu halisi mpaka hili ambalo nilikuwa nalitumia kwenye kazi alikuwa analijua lakini pia yeye ndiye ambaye alinifundisha hii michezo ya kuweza kubadili sura"

"Bosi unamaanisha huyu mtu mnafahamiana kabla ya hapa?" mwanaume mmoja aliuliza kwa mshangao

"Sio tumefahamiana bali tulikuwa marafiki wakubwa sana tena zaidi hata ya neno sana ndiyo maana hata niweje kwenye maisha yake yeye kunitambua mimi ni kazi rahisi sana. Kwenye shingo yangu nina alama nyeusi hapa ambayo kwa bahati mbaya sana ni yeye mwenyewe ndiye aliniumiza hivyo mimi siwezi kujificha mbele yake hata nikiwa vipi lakini je mnataka kujua pia kwamba alifanikiwaje kujua kwamba mimi bado nipo hai na bado ninaishi?" Robert aliongea huku akiwa anacheka na kumpiga piga mgongoni Nicole kwa sababu alikuwa karibu na alipokuwepo. Hakuna hata mmoja ambaye alijibu chochote kwa sababu kila mmoja alibakia anamwangalia mwenzake usoni, Robert alisogea mbele yao wote na kujichoma sindano ndogo shingoni ambapo ngozi ilijitanua kidogo akaivuta kwa nje na kuivua ile sura ambao alikuwa anaonekana nayo kwa muda mrefu sana kitu ambacho kiliwashangaza sana wote ambao walikuwa humo ndani wasiamini kile ambacho walikuwa wanakiona kwani mbele yao hakuwa mzee kama walivyokuwa wanamuona bali alikuwa na umri wa takribani miaka arobaini sita hivi.

"Justin alifanikiwa kunipata kwa sababu kuna msaliti humu ndani na ananisikiliza mpaka wakati huu ambao mnanisikiliza aliamua kuuza taarifa zangu" alikuwa anaongea akiwa siriasi sana huku akiwa amemkazia macho Hezroni ambapo bwana mdogo alianza kujitetea mapema.

"Bosi mimi siwezi kufanya jambo kama hili na unalijua hilo" kijana huyo alikuwa anatetemeka sana wakati huo Robert aliitoa bastola na kuielekezea kwa bwana mdogo huyo na kuwafanya wote wabaki wameduwaa.
"Najua Hezroni wewe hauwezi kunisaliti kwa namna yoyote ile lakini je ni nani unahisi ambaye ananisaliti mimi?" aliongea kwa sauti kali akiwa anawasogelea watu hao mbele yao huku akiwa anaikoki bastola yake. Aliigeuza ghafla sana na kuielekezea pale alipokuwepo Nicole na kumpiga risasi mkononi, mkono ambao Nicole aliutumia kuitoa bastola moja kwenye droo lakini aliwahiwa kwa sababu Robert alikuwa anajua muda sana kila alichokuwa anakifanya. Alicheka sana huku akiwa anamsogelea Nicole akiwa ameegamia meza anavuja damu kwa maumivu makali sana bastola ikiwa chini.

"Hili jambo nilikuwa nalijua mapema sana Nicole kwamba wewe ni msaliti na hapa nilitaka kuwadhihirishia wenzako kwamba wewe unatusaliti sisi kwani kama ningefanya maamuzi bila wao kuona unacho kifanya basi wangepoteza imani na mimi kwa kuhisi siwaamini kabisa lakini sio kweli kwa sababu hata baadhi ya akaunti zangu za benki wote mna uwezo wa kuingia na kutoa pesa sasa utasema vipi siwaamini?"

"Kitu kimoja ambacho ulifanya makosa kwenye kazi yako ni kushindwa kujua kwamba server za hiyo mitambo ambayo mlikuwa mnaitumia nilikuwa na mifumo yake yote kwenye simu yangu hivyo kila ambacho mlikuwa mnakifanya ilikuwa ni lazima mimi niipate taarifa mapema sana kwenye simu yangu. Kwa muda mrefu sana kwenye dark web kuna picha zangu zilisambazwa na aina mbali mbali za sura za kufake ikiwemo hii ambayo huwa naitumia kwamba kama kuna mtu atakuja kuniona mahali basi aripoti kwa watu hao atajipatia pesa za kitanzania taslimu Bilioni moja. Je unahisi nilikuwa sijui Nicole?"

"Hayo yote niliyafahamu mapema ndiyo maana baadae baada ya kufanya na mimi kazi kwa muda ukaamua kuanza kuuza siri zangu huku ukiwaambia kwamba unanifahamu na muda wowote unaweza ukanikamatisha kwao lakini ukawa unahitaji malipo kwanza ila nao waligoma kwa kutaka kwanza uthibitisho na ndiyo sababu siku ile ulilazimisha sana kupiga picha na mimi ambapo picha hiyo uliitumia kuwatumia kama ushahidi na baada ya hapo wakakuahidi kukupatia milioni mia tano kwanza ambayo kweli walikulipa na milioni miatano nyingine wangekupa ukinikamatisha kwenye mikono yao. Hivyo uliwapa taarifa za namna ya kunipata lakini kwenye ile nyumba kubwa hukutaja kwamba ndipo tunaishi kwa sababu ulijua wazi kwamba ningejua mhusika ni wewe lakini hata wewe mwenyewe bado ulikuwa na wasiwasi ukiamini kwamba wanaweza kukuua wakikukuta hivyo ukataka kujitoa nje ya msala na kunipakazia mimi"

"Mimi sishangaia sana kwa sababu naelewa pesa inaweza kununua nafsi ya mtu ila kitu ambacho kilinikera sana ni kuhatarisha maisha ya Hezroni kwa sababu kama mtu yule wakati anarudi angemkuta basi alikuwa anamuua moja kwa moja na hata wewe mwenyewe angekutafuta kuja kukuua. Huwezi ukala pesa ya Justin halafu ukaishi hata kama umemfanyia ni kazi, yule mchaga anaipenda pesa kuliko hata maisha yake yeye mwenyewe"

"Lakini licha ya hayo yote Nicole bado nilichagua kukupa nafasi nyingine bila kukuuliza wala kukuchukulia hatua yoyote ile nikiamini kwamba huenda ungeweza kubadilika lakini ni wazi kwamba haukuwa kabisa tayari kubadilika hata tulipo fika hapa bado umeamua kutuuza tena kwa mara nyingine, je bado unahitaji mimi nikuache hai?" Robert alimpatia mwanamke huyo maelezo kumuonyesha kwamba alikuwa na uhakika sana na taarifa zake wala hakuwa anabahatisha hivyo mrembo huyo alitakiwa sana kulielewa jambo hilo kwamba wenzake waliamkia pale ambapo yeye anakilaza kichwa chake ili kupumzika.

"Bosi unamaanisha nini kusema kwamba ametuuza na hapa?" mwanaume mmoja aliuliza akiwa anaanza kupata mashaka.
"Ametoa taarifa kuna watu wanakuja hapa muda huu kutuchukua"

"Oooooh nooooooooo" mwingine alipingana na hilo jambo akiwa anafunua pazia kuangalia nje, kwa mbali sana aliona msafara ukiwa unakuja kwa kasi sana kuelekea kwenye jengo hilo. Walipatwa na hasira sana, mwanaume mmoja alimsogelea mwanamke huyo na kuitoa bastola ambapo alimtandika risasi nyingi sana mwilini huku akiwa anaomba msamaha kwamba asingeweza kurudia tena juu ya jambo hilo lakini alikuwa amechelewa sana hivyo walitakiwa kupotea haraka sana na ndicho walicho kifanya hata ile simulizi ya historia ya maisha ya Robert kabla ya siku ile hakuna mtu hata mmoja ambaye alikuwa anaihitaji tena maisha yao yalikuwa ya mhimu kwanza.

Walitokea upande wa pili na kutokomea eneo hilo huku Hezroni akiwa amekaa kwenye komputa mpakato yake wakiwa kwenye gari na kusababisha shoti kubwa sana ndani ya ile sehemu na wakati watu wale wanafika pale ulitokea mlipuko mkubwa sana ambao uliliteketeza jengo hilo kazi nzuri iliyokuwa imefanywa na Hezroni hivyo hata wavamiaji ambao walikuwa wanaongozwa na Justin hawakusimama tena eneo hilo wakawa wametoweka haraka sana maana polisi wangeingia sehemu hiyo muda wowote ule.

Kikao kizito kiliitishwa usiku sana ndani ya WE ARE BROTHER'Z TECH COMPANY. Ethan Kamau ndiye alikuwa bosi wa kampuni hiyo kubwa sana ya teknolojia, alikuwa na uraia wa nchi ya Kenya na hakuna hata mmoja ambaye alikuwa anamfahamu hata katibu mkuu kiongozi hakuwahi kumuona mwanaume huyo hata siku moja zaidi ya kuishia kuwasiliana naye kwenye simu tu.

57 sina la ziada.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA SABA
"Mnaweza kujiuliza kwamba inakuwaje niwe hivi na bado Justin aweze kunitambua? Jibu ni rahisi sana kwanza ni kwa sababu jina langu halisi mpaka hili ambalo nilikuwa nalitumia kwenye kazi alikuwa analijua lakini pia yeye ndiye ambaye alinifundisha hii michezo ya kuweza kubadili sura"

"Bosi unamaanisha huyu mtu mnafahamiana kabla ya hapa?" mwanaume mmoja aliuliza kwa mshangao

"Sio tumefahamiana bali tulikuwa marafiki wakubwa sana tena zaidi hata ya neno sana ndiyo maana hata niweje kwenye maisha yake yeye kunitambua mimi ni kazi rahisi sana. Kwenye shingo yangu nina alama nyeusi hapa ambayo kwa bahati mbaya sana ni yeye mwenyewe ndiye aliniumiza hivyo mimi siwezi kujificha mbele yake hata nikiwa vipi lakini je mnataka kujua pia kwamba alifanikiwaje kujua kwamba mimi bado nipo hai na bado ninaishi?" Robert aliongea huku akiwa anacheka na kumpiga piga mgongoni Nicole kwa sababu alikuwa karibu na alipokuwepo. Hakuna hata mmoja ambaye alijibu chochote kwa sababu kila mmoja alibakia anamwangalia mwenzake usoni, Robert alisogea mbele yao wote na kujichoma sindano ndogo shingoni ambapo ngozi ilijitanua kidogo akaivuta kwa nje na kuivua ile sura ambao alikuwa anaonekana nayo kwa muda mrefu sana kitu ambacho kiliwashangaza sana wote ambao walikuwa humo ndani wasiamini kile ambacho walikuwa wanakiona kwani mbele yao hakuwa mzee kama walivyokuwa wanamuona bali alikuwa na umri wa takribani miaka arobaini sita hivi.

"Justin alifanikiwa kunipata kwa sababu kuna msaliti humu ndani na ananisikiliza mpaka wakati huu ambao mnanisikiliza aliamua kuuza taarifa zangu" alikuwa anaongea akiwa siriasi sana huku akiwa amemkazia macho Hezroni ambapo bwana mdogo alianza kujitetea mapema.

"Bosi mimi siwezi kufanya jambo kama hili na unalijua hilo" kijana huyo alikuwa anatetemeka sana wakati huo Robert aliitoa bastola na kuielekezea kwa bwana mdogo huyo na kuwafanya wote wabaki wameduwaa.
"Najua Hezroni wewe hauwezi kunisaliti kwa namna yoyote ile lakini je ni nani unahisi ambaye ananisaliti mimi?" aliongea kwa sauti kali akiwa anawasogelea watu hao mbele yao huku akiwa anaikoki bastola yake. Aliigeuza ghafla sana na kuielekezea pale alipokuwepo Nicole na kumpiga risasi mkononi, mkono ambao Nicole aliutumia kuitoa bastola moja kwenye droo lakini aliwahiwa kwa sababu Robert alikuwa anajua muda sana kila alichokuwa anakifanya. Alicheka sana huku akiwa anamsogelea Nicole akiwa ameegamia meza anavuja damu kwa maumivu makali sana bastola ikiwa chini.

"Hili jambo nilikuwa nalijua mapema sana Nicole kwamba wewe ni msaliti na hapa nilitaka kuwadhihirishia wenzako kwamba wewe unatusaliti sisi kwani kama ningefanya maamuzi bila wao kuona unacho kifanya basi wangepoteza imani na mimi kwa kuhisi siwaamini kabisa lakini sio kweli kwa sababu hata baadhi ya akaunti zangu za benki wote mna uwezo wa kuingia na kutoa pesa sasa utasema vipi siwaamini?"

"Kitu kimoja ambacho ulifanya makosa kwenye kazi yako ni kushindwa kujua kwamba server za hiyo mitambo ambayo mlikuwa mnaitumia nilikuwa na mifumo yake yote kwenye simu yangu hivyo kila ambacho mlikuwa mnakifanya ilikuwa ni lazima mimi niipate taarifa mapema sana kwenye simu yangu. Kwa muda mrefu sana kwenye dark web kuna picha zangu zilisambazwa na aina mbali mbali za sura za kufake ikiwemo hii ambayo huwa naitumia kwamba kama kuna mtu atakuja kuniona mahali basi aripoti kwa watu hao atajipatia pesa za kitanzania taslimu Bilioni moja. Je unahisi nilikuwa sijui Nicole?"

"Hayo yote niliyafahamu mapema ndiyo maana baadae baada ya kufanya na mimi kazi kwa muda ukaamua kuanza kuuza siri zangu huku ukiwaambia kwamba unanifahamu na muda wowote unaweza ukanikamatisha kwao lakini ukawa unahitaji malipo kwanza ila nao waligoma kwa kutaka kwanza uthibitisho na ndiyo sababu siku ile ulilazimisha sana kupiga picha na mimi ambapo picha hiyo uliitumia kuwatumia kama ushahidi na baada ya hapo wakakuahidi kukupatia milioni mia tano kwanza ambayo kweli walikulipa na milioni miatano nyingine wangekupa ukinikamatisha kwenye mikono yao. Hivyo uliwapa taarifa za namna ya kunipata lakini kwenye ile nyumba kubwa hukutaja kwamba ndipo tunaishi kwa sababu ulijua wazi kwamba ningejua mhusika ni wewe lakini hata wewe mwenyewe bado ulikuwa na wasiwasi ukiamini kwamba wanaweza kukuua wakikukuta hivyo ukataka kujitoa nje ya msala na kunipakazia mimi"

"Mimi sishangaia sana kwa sababu naelewa pesa inaweza kununua nafsi ya mtu ila kitu ambacho kilinikera sana ni kuhatarisha maisha ya Hezroni kwa sababu kama mtu yule wakati anarudi angemkuta basi alikuwa anamuua moja kwa moja na hata wewe mwenyewe angekutafuta kuja kukuua. Huwezi ukala pesa ya Justin halafu ukaishi hata kama umemfanyia ni kazi, yule mchaga anaipenda pesa kuliko hata maisha yake yeye mwenyewe"

"Lakini licha ya hayo yote Nicole bado nilichagua kukupa nafasi nyingine bila kukuuliza wala kukuchukulia hatua yoyote ile nikiamini kwamba huenda ungeweza kubadilika lakini ni wazi kwamba haukuwa kabisa tayari kubadilika hata tulipo fika hapa bado umeamua kutuuza tena kwa mara nyingine, je bado unahitaji mimi nikuache hai?" Robert alimpatia mwanamke huyo maelezo kumuonyesha kwamba alikuwa na uhakika sana na taarifa zake wala hakuwa anabahatisha hivyo mrembo huyo alitakiwa sana kulielewa jambo hilo kwamba wenzake waliamkia pale ambapo yeye anakilaza kichwa chake ili kupumzika.

"Bosi unamaanisha nini kusema kwamba ametuuza na hapa?" mwanaume mmoja aliuliza akiwa anaanza kupata mashaka.
"Ametoa taarifa kuna watu wanakuja hapa muda huu kutuchukua"

"Oooooh nooooooooo" mwingine alipingana na hilo jambo akiwa anafunua pazia kuangalia nje, kwa mbali sana aliona msafara ukiwa unakuja kwa kasi sana kuelekea kwenye jengo hilo. Walipatwa na hasira sana, mwanaume mmoja alimsogelea mwanamke huyo na kuitoa bastola ambapo alimtandika risasi nyingi sana mwilini huku akiwa anaomba msamaha kwamba asingeweza kurudia tena juu ya jambo hilo lakini alikuwa amechelewa sana hivyo walitakiwa kupotea haraka sana na ndicho walicho kifanya hata ile simulizi ya historia ya maisha ya Robert kabla ya siku ile hakuna mtu hata mmoja ambaye alikuwa anaihitaji tena maisha yao yalikuwa ya mhimu kwanza.

Walitokea upande wa pili na kutokomea eneo hilo huku Hezroni akiwa amekaa kwenye komputa mpakato yake wakiwa kwenye gari na kusababisha shoti kubwa sana ndani ya ile sehemu na wakati watu wale wanafika pale ulitokea mlipuko mkubwa sana ambao uliliteketeza jengo hilo kazi nzuri iliyokuwa imefanywa na Hezroni hivyo hata wavamiaji ambao walikuwa wanaongozwa na Justin hawakusimama tena eneo hilo wakawa wametoweka haraka sana maana polisi wangeingia sehemu hiyo muda wowote ule.

Kikao kizito kiliitishwa usiku sana ndani ya WE ARE BROTHER'Z TECH COMPANY. Ethan Kamau ndiye alikuwa bosi wa kampuni hiyo kubwa sana ya teknolojia, alikuwa na uraia wa nchi ya Kenya na hakuna hata mmoja ambaye alikuwa anamfahamu hata katibu mkuu kiongozi hakuwahi kumuona mwanaume huyo hata siku moja zaidi ya kuishia kuwasiliana naye kwenye simu tu.

57 sina la ziada.
Ngoja niamie huku kupunguza arosto ZA KULE KWINGINE fabiani BABUYA
 
Back
Top Bottom