Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Hii story Facebook imekwenda mbele zaidi Ingawa umesitisha kupost@FEBIANI BABUYA
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA NNE
Aliisogelea self ya kuhifadhia silaha yake na kuitoa kisha akaielekeza kwenye sofa moja kubwa ambalo alihisi kulikuwa na mtu kwani kwa ukubwa wake ukiwa nyuma usingeweza kumkuona kabisa mtu ambaye alikuwa mbele yake.
“Clara, sijui nikuite Anelia?” aliisikia sauti nzito ambayo alikuwa anaijua sana kwenye maisha yake. Haikuwa sauti ngeni kabisa kwake hivyo haraka sana alimjua mhusika na mmiliki wa hiyo sauti.

“Unatafuta nini kwangu na umeingiaje hapa Remy?’’
“Hiyo ndiyo salamu?”
“Usijifanye unajali salamu wakati hauna hata muda nazo. Nilipo sikia kwamba kuna mambo unayafanya kihuni nilishangaa sana lakini nilipo sikia umefanikiwa kutoroka kwenye gereza nilishangazwa zaidi na hizo taarifa kwa sababu sikuamini wala kufikiri mtu kama wewe unaweza kuwa zaidi ya vile nilivyokuwa nimekutegemea”

“Ulitamani sana kuniona nikifia gerezani kwa ile miaka sitini niliyo hukumiwa sio? Hilo nalijua, hakuna kitu ulikuwa unajali kuhusu mimi” mwanaume huyo aliongea akiwa anasimama na kuanza kusogea kule alikokuwepo Anelia ambaye alikuwa bado amemnyooshea bastola yake.
“Usisogee nitakuua Remy”

“Najua huwezi kufanya hivyo, hauna huo ujasiri” mwanaume alimjibu akiwa anaendelea kumsogelea taratibu.
“Stoooooop!” aliongea kwa nguvu lakini bado mwanaume aliendelea kumsogelea tu hali ambayo ilimfanya kuruhusu risasi zitoke kuelekea kwa Remy ila aligundua kwamba bastola hiyo haikuwa na risasi, alihisi labda ni presha ilimfanya asifanye hilo jambo kwa usahihi lakini hata baada ya kuikagua na kuziruhusu tena ndipo aligundua kwamba bastola hiyo haikuwa na risasi hata moja.

Mwanaume aliunyoosha mkono wake na kuzimwaga risasi sita sakafuni akiwa ameunyoosha mkono wake.
“Hili nilikuwa nalijua kwamba unahitaji sana kuweza kuniua hasa baada ya kuthibitisha kwamba kila kitu kuhusu mimi na wewe kilikuwa ni maigizo kama wewe mwenyewe ulivyokuwa unaniigizia mwanzo. Sijaja hapa ili kupoteza muda wangu kujadili mapenzi ya uongo ambayo yalikuwepo baina yetu hivyo njoo ukae unisikilize kisha mimi niondoke zangu” alitamka akiwa anasogea kwenye sofa akaketi na kuitoa bastola yake akaiweka mezani hali ambayo ilimfanya Anelia kusita sita sana kusogea kukaa lakini mwanaume huyo aliligundua jambo hilo.

“Kama ningekuwa nahitaji kukuua, ningekuua muda mrefu tu mpaka sasa hata mwili wako ungekuwa umepoa, nina muda mfupi mno wa kukaa hapa” ikamlazimu mwanamke huyo kusogea kwenye sofa akiwa na wasiwasi sana kwenye nyumba yake mwenyewe.
“Wewe ni nani Remy?”
“Unalitaja jina langu halafu unaniuliza mimi ni nani?”
“Najua hili sio jina lako”
“Hahahah hahaha inanishangaza sana, haunijui jina langu wakati bosi wako anayajua majina yangu yote matatu?”
“Whaaaat?”

“Kama kiongozi wako anakutuma kufanya kazi za hatari za kumtafuta mtu kama mimi basi anatakiwa pia kukupatia maelekezo yote ya mhimu kwa sababu wakati mwingine sitakupa nafasi nyingine ya kuishi”
“Unamaanisha kwamba bosi anajua kila kitu kuhusu wewe?”
“Nikisema kila kitu nitakuwa namuonea kwa sababu ni mtu mmoja tu ambaye anajua kila kitu kuhusu mimi kwenye dunia hii kwa watu ambao wapo hai ila bosi wako anajua ukweli wa maisha yangu kwa kiasi kidogo na hata sababu ya msingi ya mimi kufanya haya anaijua, ni kwa sababu tu hataki kukubaliana na ukweli kwamba hawezi kunizuia kukamilisha kile ninakitaka mimi”
“Unahisi kwamba unaweza kufanya lolote kwenye hili taifa sio?”
“Huenda jibu likawa ndio”
“Kwa mkono wangu nitakuua Remy, hii ni ahadi ambayo nimejiwekea kwenye maisha yangu na siwezi kufa kabla sijaitimiza”

“Kila kinywa huwa kinajiwekea ahadi nyingi sana ila ni ngumu sana kuweza kuzitimiza. Labda nikuulize swali rahisi sana, kwangu ulikuja kunipeleleza na sio kwa mapenzi kama ulivyo nidanganya sasa ni sababu gani inayokufanya uhitaji kuniua?”
“Kwahiyo unajifanya haujui Remy?”
“Ningekuwa naijua basi nisingekuuliza”
“Hivi uliwahi hata mara moja kunifikiria kama mwanamke wako kwenye moyo wako?”
“Punguza kuwa mwigizaji, you don’t give a damn about that love, haya yote yanatoka wapi?”
“Hilo unalisema wewe, lakini haujui ni kipi mimi nimekipitia kipindi nipo mwenyewe”

“Wewe ni bora sana kwenye upande wa maigizo na naona umeasha anza tena kuniigizia. Jambo unalotakiwa kulifahamu ni kwamba kila kitu nilikuwa nakijua tokea mwanzo na nilijua kabisa kwa hali yangu lazima wangehitaji kumtumia mwanamke kama wewe. Kukuruhusu wewe kuwa daktari wangu na baadae kuwa mpenzi wangu huo ulikuwa ni mpango wangu mwenyewe kwa sababu mtu ambaye nilikuwa namtaka nilipata taarifa kwamba yupo gerezani na anahitaji msaada ila mtu wa kumsaidia hakuwepo. Ilikuwa ni nafasi yangu bora sana kuweza kukutana na huyo mtu ili niweze kuujua uhalisia wake na umoja wao ambao mimi nimekua nikilala na kuota ndoto mbaya sana nikitamani siku moja kuweza kukutana nao”

“Njia pekee ya mimi kuweza kufika kule gerezani ilikuwa ni kuwa mhalifu ili nikamatwe na makosa makubwa ili nifanikiwe kuingia jela ambako nilifanya matukio ya kutisha yaliyo nipeleka kwenye lile gereza na nimefanikiwa kukutana na huyo mtu tayari hivyo sikuona haja ya kuendelea na maisha ya kuishi gizani kama zamani tena kwa sababu naanza kumpoteza mmoja mmoja. Kwahiyo kama ulijiona mjanja sana kwa kuona umeniingiza mtegoni basi nikupe pole na asante sana kwa kufanikisha kunisaidia mimi kulikamilisha zoezi hili kwa wepesi sana tofauti hata na nilivyokuwa nimetegemea”

“Je mpaka hapo bado unatamani kunifahamu kwamba mimi ni nani Anelia?” mwanamke huyo alikuwa anashangaa namna mwanaume huyo alivyokuwa bingwa kwa kamari ngumu kama hizo kwenye huu ulimwengu.
“Kwahiyo umekuja kuniua?”
“Nimekwambia mapema ningehitaji kukuua kwangu ilikuwa ni kazi rahisi sana hivyo mpaka sasa ungekuwa umekufa ila halijanileta hilo hapa leo. Kuna kitu kimenileta mbali na haya” alikuwa anaonyesha hasira za wazi Anelia ila hakuwa na la kufanya hivyo Ashrafu aliendelea;

“Kwenye haya maisha ya mimi na wewe, hesabia kwamba hatujawahi kukutana, yaani wakati ambao ulikuwepo baina yangu mimi na wewe ufute kwenye kumbukumbu za maisha yako. Usije ukajitokeza tena kwenye njia zangu hata siku moja kwa sababu nitakuua mwenyewe kwa mkono wangu”

44 NAWEKA NUKTA HAPA.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA SITA
Akiwa anatembea na gari yake alishtuka baada ya gari hiyo kuyumba nusura idondoke na kama ingekuwa kwenye mwendo mkali basi ingedondoka kabisa chini. Alishuka na kuangalia akagundua kwamba upepo ulikuwa umeisha upande mmoja ila wakati anashangaa aligundua kwamba ni risasi ilikuwa imepita kwenye hilo tairi. Alijishika kiunoni ili kutoa bastola yake ila alikuwa amechelewa kwani alihisi kuna kitu cha baridi kimeigusa shingo yake hivyo akawa mpole maana kama angecheza vibaya basi angeyapoteza maisha yake na hakuna mtu hata mmoja ambaye angekuja kujua kuhusu uwepo wake.

"Nani wewe?" sauti nzito ya kiume ilisikika vizuri kwenye masikio yake.
"Naomba kuongea na brigedia mstaafu Mariana Amboni" alitamka mwili ukiwa unatetemeka maana yake hiyo kamari ambayo alikuwa anaicheza ilikuwa ni ngumu sana kama angekosea hatua hata moja tu ilikuwa inakula kwake.

Mwanaume mmoja aliongoza mbele na mwingine akiwa nyuma yake ambaye alikuwa amemuwekea bastola kichwani. Walitembea kwa dakika kumi akagundua kwamba sehemu hiyo ilikuwa na senyenge kubwa mbele yao. Walifungua sehemu hiyo kwa rimoti kisha wakatembea kwa dakika zingine tano ndipo walikutana na lango kubwa la geti ambalo lilionyesha wazi kwamba ndani yake kulikuwa na jengo la gharama sana.

Mwanaume mmoja aliscan jicho lake ndipo geti hilo likafunguka ambapo alisachiwa na kuchukuliwa kila kitu alichokuwa nacho mwilini kabla ya kupata nafasi ya kuingia ndani na baada ya hapo aliruhusiwa ambapo baada ya kugeuka hakuwaona tena wanaume wale ambao walimsindikiza zaidi zaidi aliwaona wengine ambao walikuja kumchukua na kumpeleka alipokuwa mama huyo.

Walimpeleka mpaka nyuma ya jumba hilo sehemu ambako kulikuwa na bustani nzuri sana na makabati ya shaba ndani yake kukiwa na samaki. Pembeni mwa kabati moja alionekana mama mmoja wa makamo kidogo ambaye alikuwa na mwili mnene kiasi akiwa anawalisha samaki ambao bila shaka walikuwa ni wake, Suzane akili yake ilijua imempata mtu sahihi ambaye alikuwa amekuja kuonana naye.

"Suzane Gulamo, umekua sana siku hizi. Umekuja wakati ambao sio sahihi ila karibu nyumbani binti yangu" alipigwa na butwaa baada ya kukaribishwa na mwanamama huyo.
"Unanifahamu mimi?"
"Hahahah mwanangu kufanya kazi ndani ya usalama wa taifa basi unahisi kwamba wewe utakuwa wa siri kwa kila mtu"

"Sishangai sana kwa sababu dada yako ndiye bosi wangu" mama huyo alitabasamu.
"Amefanya kosa kubwa sana kukuonyesha wewe kuhusu mimi hili ni jambo ambalo litakuwa na matokeo mabaya sana hapo baadae. Karibu ndani uniambie kipi kimekuleta hapa" mama huyo aliongea jambo ambalo Suzane hakulielewa kwa wakati huo ila alitakiwa kuingia ndani kwanza ili kama ana maswali au kuna mambo anahitaji kuuliza akajibiwe huko na mama huyo ambaye kukutana naye kwake ilikuwa kama bahati na hatua kubwa sana kwenye maisha yake ya kazi.

Baada ya kufika ndani mama huyo alikuja na kahawa mezani ambapo moja alijiwekea mwenyewe na nyingine aliiweka kwa ajili ya Suzane na kuwataka walinzi wote watoke hapo maana alikuwa anahitaji kuongea pekeyake na binti huyo.
"Samahani sana hapo nje umesema kwamba jambo hili litakuwa na matokeo mabaya hapo baadae bado sijakuelewa vizuri"

"Unahisi kwanini umekuja kuniona Suzane?"
"Kwa sababu nataka amani"
"Hiyo amani ulitakiwa uitafute kwa namna nyingine, hii njia ambayo bosi wako amekuonyesha ni mbaya kuliko ambavyo akili yako inafikiria"

"Kama unajua kilicho nileta hapa basi nina imani pia kwamba wewe ndiye mtu pekee ambaye unaweza ukafanya haya mambo yote yakaisha"
"Kwa sababu umekutana na dada yangu na kuijua hii siri unahisi unanifahamu sana mimi?"
"Hapana sina maana hiyo"

"Hivi unajua mwanadamu yeyote yule huwa anaanza kufeli wapi pale ambapo anakuwa anashindana na maadui zake?"
"Nadhani anapokuwa ameishiwa uwezo na mbinu"
"Hizo ni kwa wanajeshi tu labda ila kwenye maisha sio kweli binti yangu, mtu yeyote kwenye maisha yake huwa anaanza kufeli pale maadui zake wanapofanikiwa kuujua udhaifu wake lakini huo huo udhaifu wake ndio ambao unaweza ukamfanya akiwa kiumbe wa ajabu sana mpaka akaishangaza dunia kwa mambo ambayo anaweza kuyafanya"

"Unamaanisha nini kusema hivyo?"
"Acha kuzunguka Suzane, unataka nini?"
"Matatizo yameanza kutokea mjini hali ambayo inaanza kuleta mashaka kwa taifa na kwa wananchi pia na baada ya uchunguzi kufanyika nimegundua kwamba mwanao ndiye mtu ambaye yupo nyuma ya kila kitu na ndiye ambaye anaanza mpaka kumtisha mheshimiwa raisi. Hii ni hatua mbaya sana ambayo inaweza kumfanya akaishia kuuawa muda wowote ule hivyo unayo nafasi ya kumfanya aache kufanya haya anayo yafanya kwa kuwa nimesikia kwamba wewe ndiye pekee ambaye anaweza kukusikiliza na kukutii ndani ya hii dunia"

"Kwahiyo umekuja kwangu kunionya au kunipa ushauri? Mbona unaongea kama unamuonea huruma mwanangu binti?"
"Baada ya kuisikia historia ya maisha yake imeniuma kwa sababu alikutwa na jambo baya sana lakini sio sababu ya yeye kuweza kuleta machafuko ambayo yanaweza kuwaumiza mpaka wasio na hatia"
"Binti haujaja hapa kwa sababu unayajali maisha ya mwanangu ila ni kwa sababu unaogopa baada ya kuanza kumjua alivyo na yale ambayo anaenda kuyafanya. Nafikiri ulitakiwa kujali kwanza afya ya vijana wako ambao juzi ilibakia kidogo uwapoteze"

"Umejuaje kuhusu hili?"
"Hii dunia ni ndogo sana, mwanangu ndiye tumaini langu la pekee hivyo kila hatua anayo ipiga nakuwa makini kuhakikisha namlinda ndiyo maana kujua hayo ni jukumu langu mimi. Sasa nataka nikukumbushe kitu kwamba ni kwanini nimekwambia kwamba huu utakuwa mwanzo wa mambo mabaya sana kutokea Suzane huenda umehisi ni mwanzo wa ushindi kwenu ila mmekosea sana" mama huyo alimeza funda la kahawa na kuendelea;

"Unajua unaweza ukawa unafanya mambo yako kwa amani sana bila ubaya na mtu pale ambapo unakuwa unajua kwamba hakuna mtu wa kukudhoofisha kwa namna yoyote ile ila unapokuwa unajua kwamba kuna mtu anaweza kukudhoofisha kwenye kila unacho kifanya basi mambo huwa ni ya tofauti sana kwani unakuwa unafanya mambo kwa tahadhari kubwa hasa kumpoteza yule ambaye anataka kukutesa kwa sababu ya udhaifu ambao unakuwa unao. Mpaka sasa umeshajua kwamba udhaifu mkubwa wa mwanangu ni mimi hapa hivyo pale mambo yatakapokuwa magumu kwa upande wenu umeshajua kwamba kete yako ya mhimu utakuwa ni kudili na mimi ili kumpata Ashrafu ila nikupe ushauri na kukuonya mapema"

46 INAFIKA MWISHO.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
"Usije ukajaribu kuwaza wala kulitekeleza hilo jambo kwa sababu kitakacho tokea baada ya hapo yatakuwa ni mambo ya kutisha sana ndani ya hii nchi. Ni kweli kabisa kwamba ukinipata mimi utakuwa umemdhoofisha sana Ashrafu ila matokeo yake ni mabaya zaidi ya faida ambazo mtazipata. Dada yangu niliwahi kumshauri sana kuhusu hili jambo kwamba akae mbali sana na huyu mtoto na asije akamfuatilia kwenye maisha yake yote ila naona kwamba ana kichwa kigumu kuelewa mpaka ameamua kukupatia siri nzito kama hii ambayo nilimuomba aitunze kwenye maisha yake yote. Kwa kifupi ni kwamba mimi siwezi kumzuia kufanya kile ambacho anatakiwa kukifanya, samahani sana kwa hilo" darasa lilikuwa huru sana kwa Suzane, ilikuwa ni juu yake kuamua kulielewa au kuto lielewa.

"Mama hili ni suala la nchi sasa, hauogopi kama unaweza ukampoteza huyo mtoto ambaye naye yupo mmoja tu" Maelezo ya Suzane yalimfanya mama huyo acheke kwanza.
"Unamaanisha kwamba unataka kulifanya hili sio?"
"Nitakuwa sina namna kwa sababu siwezi kumuacha aendelee kufanya kile ambacho anataka kukifanya"

"Kwa kuijua hii siri nilitakiwa kukuua ili isije ikafika mahali kwingine ila kwa sababu naona unataka kuanzisha vita basi leo nitakuacha uishi ili ujionee kwa macho yako kile ambacho kitawatokea. Kama ulimshuhudia akiwaadhibu vibaya vijana wako na kukupa wewe nafasi ya kuishi ulitakiwa kumshukuru sana Mungu kwa sababu bado haujamshuhudia yule Ashrafu mwenyewe ambaye anakuwa hana ubinadamu akikutana na watu hususani wanafiki kama wewe. Mimi na wewe tumemalizana hapa naona umekuja kwenye nyumba yangu kujaribu kuwatishia watu ambao huwajui ila unahisi unawajua kwa sababu umesimuliwa tu kuhusu maisha yao ya huko nyuma" mama huyo aliongea tena akiwa anaangalia saa yake na kumgeukia Suzane.

"Kwa sasa wahi mjini kwa sababu mwanaume ambaye anaitwa Ulimboka huenda atakuwa amekufa tayari.
"Whaaaaat?"
"Nakusubiri hiyo siku ambayo utakuja kunichukua na wenzako ili uifahamu sura halisi ya mwanangu" Maelezo yalikuwa yanamchanganya sana Suzane lakini akiwa bado amekaa, wanaume walikuja kumbeba na kwenda kumtupia nje ambapo alitembea kwa haraka sana kuelekea lilipokuwa gari lake akiwa anawaza namna sahihi ya kuweza kurudi tena Dar maana tairi ilipigwa risasi.

Lakini baada ya kufika pale alishangaa sana, tairi ilikuwa mpya kabisa kwa maana hiyo wale wanaume ambao mara ya kwanza walimsindikiza mpaka getini walikuwa wameirekebisha gari hiyo na alipo ingia ndani alivikuta vitu vyake vyote ambavyo vilibebwa wakati anaingia, aliiwasha gari hiyo na kuondoka kwa kasi kubwa sana huku akiwa anaipiga simu kwa bosi wake maana walishindwa kuelewana na mama huyo ambaye alidaiwa kuwa mama mlezi wa Ashrafu.

Simu ambayo alikuwa anaipiga Suzane ilikuwa ni kuelekea kwa bosi wake, licha ya mwanamke huyo kumkera sana kwa kile ambacho aliamua kuwaficha yeye na wenzake lakini bado ndiye alikuwa bosi wake ambaye alikuwa anamuamuru kipi cha kukifanya na kipi cha kuto kukifanya hivyo alikuwa anatakiwa kumtii kwa namna yoyote ile. Simu hiyo alikuwa anampigia ili kumpa taarifa kwamba kuna mtu alikuwa anaitwa Ulimboka ndiye alikuwa anatakiwa kufa usiku huo kwenye mkono wa Ashrafu taarifa ambayo aliipata kutoka kwa mama yake mlezi hivyo alitakiwa kutoa taarifa mapema ili kama inawezekana waweze kuwahi huko.

"Bosi Ulimboka ndiye mtu ambaye anafuatia kufa kwa sasa hivyo inatakiwa watu watumwe haraka sana wakamchukue kabla hajampata"
"Hizo taarifa umezipatia wapi?"
"Kwa mdogo wako"
"Whaaaaaat?"

"Najua huenda unahitaji kunilaumu au kuniadhibu lakini sio kwa wakati huu, ni mhimu zaidi mtu huyu awahiwe haraka sana kabla hajapata tatizo maana yake kama tukimpata huyu anaweza kutusaidia kuwajua hawa watu na umoja wao kwa ujumla" mkurugenzi aliikata simu ya mwanamke huyo ili kulishughulikia jambo hilo ambalo lilikuwa ni la ghafla sana.

Kitu kimoja ambacho Suzane alikifanyia kosa kubwa la maisha bila kujua, ni kwamba wakati wote tangu anaondoka Dar alikuwa anafuatiliwa kwa ukaribu sana na mtu ambaye alikuwa kwenye piki piki yake kubwa. Kila hatua ambayo alikuwa anaipiga mtu huyo alikuwa naye kwa ukaribu sana mpaka anaanza kugeuza kurudi Dar bado alikuwa naye ila baada ya kufika Mlandizi mtu huyo alipotea.

Anelia Baton ndiye mtu ambaye alikuwa anamfuatilia Suzane kwa ukaribu sana. Baada ya kuhakikisha amezipata taarifa kama zilivyokuwa zinahitajika alipiga simu mahali Anelia.
"Naomba tukutane mheshimiwa"
"Nipo kwenye mkutano saivi nitakutafuta"
"Ni kwa ajili ya ile kazi ambayo umenituma niifanye, kuna kitu kipya nimekigundua"
"Njoo sasa hivi" simu ilikatwa baada ya kupewa ruhusa kwa sababu lilionekana kuwa jambo kubwa na la mhimu sana. Anelia alikuwa kwenye mpango wake wa kuweza kuwatafuta watu ambao waliiteketeza familia yake huku akigundua kwamba hata bosi wake kuna mambo mengi sana alikuwa anamficha hivyo alipoteza kabisa imani naye na kuamua kuyafanya mambo yake kwa namna ambayo alikuwa anaona kwamba inamfaa yeye hali ambayo ilimfanya kujikuta kwenye mikono ya raisi ambaye ndiye alimpa kazi ya kuwafuatilia watu hao ili kujua kila wanacho kifanya.

Msafara wa wanaume saba ulikuwa umefika JNIA, wanaume hao waliingia nchini kama wafanya biashara wakubwa sana. Kiongozi wa wanaume hao ndiye ambaye alipigiwa simu na raisi kwamba alikuwa anamhitaji haraka sana aweze kuingia nchini. Baada ya kutoka nje, kuna msafara wa magari kadhaa waliukuta unawasubiri ambapo uliwabeba mpaka Upanga ambako waliingizwa kwenye jengo moja kubwa lililokuwa limesheheni vitu vya thamani sana. Mwanaume huyo kwa mtazamo alikuwa na asili ya nchi ya Kenya pamoja na wenzake.

Aliichukua simu yake na kupiga sehemu ambako alikuwa anategemea simu hiyo iweze kufika, ilimkuta raisi wa Tanzania ambaye alikuwa kwenye chumba chake akiwa anapiga wine taratibu na kusoma gazeti la asubuni ambalo hakuwa amelisoma.
"Bosi"
"Umefika?"
"Ndiyo"

"Vijana umekutana nao?"
"Hapana ndo naingia saivi nahisi kwa mara ya kwanza kesho nakutana na katibu mkuu kiongozi"
"Safi, hakikisha hajui lolote kuhusu mimi"
"Hilo nalielewa vizuri bosi"
47 BYE.
 
Mkuu mpaka saa ngapi, na utaratibu wa kupata story yote kwa mkupouuu
 
Back
Top Bottom