Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
Safari yake usiku huo ilienda kuishia yalipo makao makuu ya usalama wa taifa, haikuwa kawaida yake kufika hiyo sehemu lakini siku hiyo alienda yeye mwenyewe tena bila uwepo wa mkurugenzi wa usalama wa taifa. Walinzi waliuzuia msafara huo lakini baada ya kugundua kwamba alikuwa ni mheshimiwa raisi walimfungulia haraka sana ambapo alikutana moja kwa moja na mlinzi mkuu wa eneo hilo.
"Mheshimiwa karibu sana"
"Nataka kukutana na Bruno Josephat"
"Utaniruhusu nimpe taarifa bosi mheshimiwa?"
"Yaani kwenye taifa langu kumuona mateka mpaka nipate ruhusa kwa mtu? sihitaji mtu apewe taarifa kwani unahisi mimi sina namba yake nimeshindwa kumpigia mwenyewe?"
"Nisamehe sana mheshimiwa"
"Muda mwingine angalia sana maneno yanayotoka kwenye mdomo wako"
"Hili halitajirudia tena mheshimiwa" mwanaume huyo alijibu kinyonge kwa sababu huyo ndiye alikuwa anahakikisha wao wanapata mishahara kama angemtibua huenda hata kazi yenyewe angeikosa au hata kuishia kufa hivyo aliongoza njia kumpeleka mpaka alipokuwepo mtu huyo kisha akahitaji waachwe wao wawili tu humo ndani.

Bruno Josephat alikuwa amelala usingizi wakati huo baada ya kuchapika kwa kipigo kikali kwa muda mrefu sana. Raisi huyo alimzunguka mtu huyo na kumwangalia kwa umakini sana, akasikitika kwa jinsi alivyokuwa amesulubiwa majeraha kila kona. Alisogeza kiti karibu na alipokuwa ameketi bruno na kuitoa sigara yake ya gharama kwenye mfuko wa koti kisha akaiwasha na kuanza kuivuta taratibu. Moshi wa sigara hiyo ulikuwa unamuingia moja kwa moja Bruno puani hali ambayo ilimfanya kuanza kupaliwa na kukohoa mpaka akawa amekurupuka kutoka kwenye usingizi akiwa anaona nyota nyota mbele yake.

"Usiniue tafadhali, usiniue, nitakwambia kila kitu, naahidi" aliweweseka huku akiwa anatamka maneno hao baada ya kuona mtu mbele yake maana bado alikuwa na mawenge kwenye macho ila baada ya kutulia moyo wake ulipiga kwa nguvu baada ya kugundua kwamba aliyekuwa mbele yake alikuwa ni raisi wa nchi.
"Kiongozi!!" aliita kwa wasiwasi sana akiwa anachangamka kiasi baada ya kumuona mtu huyo mbele yake lakini raisi alikuwa anamwangalia tu akiwa anaivuta sigara yake kisha akaizimia kwenye kidonda cha mguuni mwa Bruno na kumpatia maumivu makali ambayo yalimfanya agune sana akiikaza mishipa yake ya shingo.

"Hivi kwenye maisha mtu unatakiwa upewe nafasi ngapi ili uelewe thamani ya maisha yako?" raisi alimuuliza Bruno akiwa anajifuta mikono kwa kitambaa chake baada ya sigara kumchafua.
"Nafasi moja tu lakini kila mtu anastahili nafasi ya pili pia"
"Hapana Bruno maisha hayako hivyo, maisha yanakupa nafasi moja tu pekee ukishindwa kuitumia basi habari yako inakuwa inaishia hapo. Hakuna watu ambao huwa ni wajinga na wapuuzi sana kama watu wanaopewa nafasi nyingi kwenye maisha kwa sababu huwa inafikia hatua wanajiona kama wao hata wakikosea bado ulimwengu utawapendelea tena kwa kuwapa nafasi zingine kitu ambacho kinafanya kunakuwa na kizazi cha hovyo sana lakini ukikutana na mtu ambaye anajua kabisa kwamba ana nafasi moja tu kwenye maisha yake siku zote hawezi kuichezea nafasi moja ambayo anaipata"

"Nisamehe sana kwa hili kosa ambalo nimelifanya kiongozi"
"Sijajua ni mtu gani ambaye aliwapa hii mbinu, nachukia sana mtu akifanya ujinga kupenda kulitumia neno samahani kama msaada kwake. Huwa narudia kwa watu wengi sana, usifanye kosa kwa sababu tu unajua kuna neno samahani. Kuna wakati hilo neno huwa halina maana sana hasa kwa wale watu ambao wanakuona wewe hiyo ndiyo tabia yako, sasa na wewe sijakuuliza hata maswali unaanza kuniomba msamaha, au unahisi mimi ni jaji wa mahakama sio"

"Hapana kiongozi"
"Kwanini ulienda kwenye lile gereza?"
"Mheshimiwa"
"Nadhani unanifahamu vizuri huwa sipendi kuuliza kitu kimoja mara mbili"
"Kwa sababu binti yangu ametekwa"
"Na nani?"
"Ulimboka"

"Ulimboka amteke binti yako kwa sababu ipi na ina uhusiano gani na wewe kwenda kujificha gerezani?"
"Miaka miwili iliyo pita Ulimboka alimpoteza mwanae wa kiume James ambaye alikutwa ameuawa lakini ukweli ni kwamba James ni mimi ndiye nilimuua kwa mkono wangu kwa sababu alikuwa amekuja kwenda kiwanda changu akihitaji kubeba pesa na nyaraka za umiliki wa baadhi ya mali zangu. Nilimuuliza kama ni baba yake alimtuma, baada ya mateso makali akakiri kwamba ni yeye mwenyewe alikuwa hanipendi tangu muda mrefu sana hivyo alifanya vile ili kunikomoa na baba yake hakuwa akihusika kabisa. Kwa sababu msaliti sikuwahi kuweka mazingira ya kumsamehe nikaamua kumuua kwa kumpiga risasi nikaiweka hiyo siri kwenye kifua changu. Baada ya muda kupita nadhani kuna kijana wangu aliamua kunisaliti na kumpa ile siri Ulimboka hali ambayo ilimfanya kuja kumuua mke wangu na kumteka binti yangu kwa sababu alidai kwamba mwanae wa kiume ndiye alikuwa mrithi wake hivyo kwenda naye sawa ilitakiwa kumuua mwanangu na mke wangu hapo ndipo tungekuwa sawa"

"Mimi nilimuomba sana asimuue binti yangu hivyo akanipa sharti ili binti yangu aendelee kuwa hai. Nilitakiwa kwenda sehemu ambayo sitaonekana tena mtaani ili nikateseke huko na ikiwezekana niweze kuuawa kwa mateso ya gereza na ndipo alinichagulia lile gereza la Dominic ambako anaamini kwamba kuna maisha magumu sana. Alinipa onyo kwamba kama ningeonekana popote pale au kutuma watu wangu kufanya jambo lolote lile basi alikuwa anamuua mwanangu hivyo nilitakiwa kuishi nalo moyoni pekeyangu na ndipo hapo nilipo mtafuta Luka Gambino na kuamua kuanza kuishi ndani ya lile gereza" maelezo yake yalimfanya kiongozi huyo kuanza kucheka.

"Sasa nimeanza kukuelewa, kwahiyo wewe ndiye umemtorosha Remy ili akamsaidie mwanao sio?"
"Ndiyo kiongozi"
"Oooooh maskini Bruno ulikuwa moja kati ya vijana ambao niliwahi kuwaona wana akili sana ndani ya hili taifa, uliwaza vipi kitoto sana namna hiyo bila kufikiri? Ulishindwa kunifikishia hizo habari jambo ambalo ningelishughulikia ndani ya dakika kumi tu likaisha?"

"Nilihofia maisha ya mwanangu kiongozi"
"Kwahiyo maisha ya mwanao ni ya mhimu sana kuliko yangu?"
"Sijamaanisha hivyo"
"Kwahiyo mkuu wa gereza analijua hili vizuri sio?"
"Ndiyo"
"Ni wapi na wapi ambako umemuelekeza Remy kwenda ili kumpata mwanao?"
"Nimempa maelezo ya kufika kwa Benard Taradadi kwa sababu nimemwambia huyo ndiye angempa maelezo zaidi juu ya wapi anapotakiwa kumpata binti yangu"
"Kwahiyo naye alikuwa analijua hili?"
"Ndiyo"

35 INAFIKA TAMATI.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA SITA
"Hii ni mbaya sana mtu kama wewe unapo amua kuwa mnafiki, je kuna mtu yeyote ambaye umemwambia kuhusu haya mambo kwa undani labda?"
"Hapana mheshimiwa"
"Una uhakika?"
"Ndiyo"

"Haya mambo yanatakiwa kuishia kwako tu pekee kwa sababu umeshindwa kuwa na kifua kipana na akili za kufanya maamuzi, hata hapo ulipokuwa umelala nimekusikia ukiomba useme ukweli maana yake kama hujatoa taarifa za maana ni suala la muda tu kuweza kuzitoa. Ujinga wako unaweza ukalipelekea taifa hili kuingia kwenye hali mbaya sana na mtu wa kwanza kulaumiwa ni mimi hapa sio mtu mwingine hivyo mimi sipo tayari kuzipokea lawama kwa ajili ya upumbavu wako wewe"

"Naomba nisamehe mheshimiwa, nipe nafasi nyingine ya mwisho nitalirekebisha hili"
"Nimekwambia mapema maisha yanakuchagulia nafasi moja tu pekee. Chaguo ni lako aishi mwanao au afe, wewe hautakiwi kuishi tena kwa sababu kazi yako ambayo ilikuwa inakufanya uwe hai umeshindwa kuitekeleza hivyo unatakiwa ufe. Kufa kwako kutanifanya mimi nimlinde mwanao na awe salama kama tu utaamua kuyatoa maisha yako mwenyewe ila kama hautataka basi nitakuua kwa lazima kisha huyo binti yako naye nimuue"

"Mheshimiwa" aliongea Bruno machozi yakiwa yanamtoka.
"Kuna muda maisha ni kuhusu maamuzi magumu Bruno, unatakiwa kufanya maamuzi magumu pale ambapo faida za kufanya hivyo zikiwa ni nyingi kuliko kutofanya hivyo hata maadili yanatupa hilo somo. Kufa kwako itakuwa ni nafasi bora sana ya mwanao kuweza kuyaishi maisha mazuri"
"Naomba niahidi kama mwanangu ataishi vizuri mheshimiwa"
"Mimi ndiye bosi wa taifa, japo huwa sio mzuri sana kwenye ahadi zangu maana kuna muda ahadi inaweza kukwamisha mambo mengi ila kwa mwanao nitajitahidi sana kwa sababu ni mtoto wa kike" raisi alimpa Bruno hayo maelezo huku akiwa anakitoa kidonge kwenye mfuko wake na kumpatia.

"Ukikila itachukua dakika tano tu wewe kuwa hai, mwili utaanza kukoka nguvu, utapata maumivu makali sana ya kichwa kwa dakika moja na baada ya hapo utaanza kupooza mpaka moyo utaacha kufanya kazi. Ni dakika tano tu zinatosha" Bruno alikipokea akiwa anatetemeka sana.
"Kwaheri Bruno japo umeamua kufa kipumbavu sana" alitamka akiwa anasikitika na kumpiga piga mwanaume huyo begani kisha akaondoka taratibu humo ndani bila haraka yoyote ile.











Watu hao watano walikuwa mbele ya Ashrafu tena ghafla sana kwa sababu hakutegemea kama anaweza kukutana nao usiku huo huku wakionekana kabisa kwamba walikuwa na usongo nae isivyo kawaida. Jambo hilo lilimshangaza sana hivyo akaitoa simu yake mfukoni na kuipiga kwa mtu ambaye binafsi alikuwa anajua yeye kwamba anataka kuongea na nani wakati huo. Simu hiyo moja kwa moja ilikuwa ni kwenda kwa mkurugenzi wa usalama wa taifa mwanamama Cleopatra Gambo, simu hiyo iliita kwa muda mfupi sana na kupokelewa;

"Mara ya mwisho mimi kuongea na wewe nilikwambia kabisa kwamba sitaki mtu yeyote ayafuatilie maisha yangu kwa sasa. Kwanini unawatuma hawa vijana wako ambao hawana hatia kwangu? Inamaanisha ulikichukulia kile kitu kama naimba kwaya bila watazamaji?" ni swali ambalo aliliuliza kwenda kwa mkurugenzi wa usalama wa taifa
"Naongea na nani?" ilisikika sauti upande wa pili ambayo ilikuwa ni ya Cleopatra Gambo.
"Usijifanye haunifahamu, acha kucheza michezo ya kitoto namna hiyo ambayo haiendani kabisa na umri wako"

"Nikurahisishie maelezo yako tu bwana mdogo mimi siwezi kukuacha ukaenda kufanya kile ambacho unakitaka wewe, hilo ni jambo ambalo halitakuja kuwezekana hata siku moja"
"Upo tayari kuyabeba madhara ambayo yatatokea?"
"Nafikiri wakikuleta ndipo tutaongea kwa mapana na utanielewa ninacho kimaanisha kwa sasa kwa sababu unatembea kwa miguu yako ndiyo maana unakuwa na kiburi sana. Nakusubiria Ashrafu" mwanamama huyo aliongea kijasiri sana huku akimkatia mwanaume huyo simu. Aliitazama simu hiyo haikuwa na kazi tena, aliibamiza chini ikapasuka kisha akawa anasogea ile sehemu ambayo watu wale watano walikuwa wamesimama kumsubiri maana ndiyo ilikuwa njia ya kuelekea getini. Utano mtakatifu au waweza kuwaita Waliokufa Wakiwa Hai ndio waliokuwa wana hamu kubwa sana na Ashrafu.

"Ni mara ya kwanza kwenye maisha yangu kuchezewa mchezo wa akili na mtu mmoja na akashinda mbele yangu. Sikuamini baada ya kupata taarifa na uthibitisho kwamba maisha yako yote yalikuwa ni ya maigizo Ashrafu, unajikuta nani labda kutaka kushindana na serikali?" Kai aliuliza kwa hasira sana akiwa na kisu chake mkononi anamsogelea taratibu Ashrafu ambaye alikuwa amesimama lakini kwenye mapaja yake damu ilionekana ikiwa inachuruzika kwenye suruali yake bila shaka alikuwa ameyatonesha yale majeraha ambayo alipigwa risasi na mkuu wa gereza Luka Gambino.

"Una akili fupi sana bwana mdogo sidhani hata kama ulikuwa unastahili kuifanya hiyo kazi yako ya kipelelezi. Nani amefanikiwa kuwapatia taarifa zangu?" alimjibu Kai kwa jeuri sana kiasi kwamba alitamani kumkimbilia mwanaume huyo lakini Suzane aliwahi na kumdaka mkono wake kwanza, hakutakiwa kutumia mihemko sehemu kama hiyo kwani wangeiharibu kazi yenyewe ambayo walitumwa kuifanya.

"Ashrafu haina haja ya sisi kukuumiza kwa mara nyingine tena, tuongozane pamoja ili ukajibu kila ambacho unatakiwa kukitolea taarifa huenda tukapata namna ya kukusaidia kwa kuipoteza familia yako ila hii njia ambayo unaitumia unatulazimisha tukufanyie jambo baya sana kwenye maisha yako" Suzane aliongea kwa busara sana kama mwanamke kwa sababu jambo ambalo lilimkuta mwanaume huyo kuwapoteza watu kumi na watano kwenye familia yake yeye alilichukulia kwa uzito mkubwa sana.

"Hahaha sitaki kuamini Suzane leo unambembeleza huyu mjinga kama amekuwa mwanamke anayekwenda kuolewa? No, hii haiwezi kwenda hivi huyu boya ni lazima twende naye kwa nguvu na sio kumbembeleza" Kai aliongea kwa jazba maana mpaka wakati huo ni hasira ndizo zilikuwa zinamuendesha.

36 INAFIKA MWISHO.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
"Bwana mdogo una mihemko sana sidhani hata kama unaweza kumpa furaha mwanamke wako. Huo mdomo wako unaonekana kabisa kwamba haujapata mtu wa kuufundisha namna ya kuutumia vizuri, sio kwa lazima tu hata kwa kubembelezwa bado nisingeweza kwenda na nyie hivyo ondokeni hapa taifa linaweza kuja kuwatumia kwa namna nyingine ambayo inaweza kuwa bora zaidi. Sitaki kumwaga damu ya watu ambao bado naamini mnaweza kuja kuwasaidia raia maskini ambao hawana mtu wa kuwasemea wala kuzipigania haki zao hivyo kama ukija kurudia tena kuutumia huo mdomo wako mbele yangu kama hivyo nitakuua" Aliongea kwa msisitizo na sauti kali sana ambayo ilipenya vizuri kabisa kwa wote lakini Kai aliichukulia kama kukosewa heshima, hakusubiri tena kupewa ruhusa na kiongozi wake ambaye alikuwa ni Suzane.

Alimpita Suzane juu kwa sarakasi maridadi sana akiwa ameitanguliza mikono yale mbele kwa pamoja, mkono mmoja ukiwa na kisu ambacho kilikuwa kinazungushwa kwa nguvu sana. Ashrafu alifanikiwa kurudi nyuma kidogo kisu kikamkosa kwenye kifua chake hata hivyo wakati Kai anatua chini alijibetua kwa sarakasi ya pembeni akalizungusha teke lake ambalo lilikita kwenye paja la Ashrafu. Mwanaume aliuma meno kwa maumivu makali kwa sababu teke hilo lilitua sehemu ambayo ilikuwa na kidonda, teke hilo lilimbeba mpaka hatua kadhaa nyuma ambapo mguu wake mmoja ulikita kwenye gari ambayo ilikuwa imepakiwa hapo na kuifanya kubonyea sehemu ambayo aliikanyaga akiwa anaitafuta balansi ili asiangukie nyuma.

Paja lilionyesha dalili za kujeruhiwa vibaya hivyo Kai alitabasamu akiwa anakuja kwa mara nyingine tena kuweza kushambulia maana hiyo kazi aliona kwamba anaweza kuimaliza hata mwenyewe. Buti lake lilitua kwenye gari baada ya Ashrafu kubinukia chini akiwa analikwepa buti ambayo lilipasua kioo cha gari hiyo lakini hakutua hata chini Kai aligeuka tena kwa nguvu sana ila wakati anageuka hivyo Ashrafu alimpitia pembeni kwa kasi sana ambapo alimgonga na kiganja cha mkono kwenye bega kiasi kwamba mwanaume huyo aliinama kidogo kwa maumivu makali ambayo aliyapokea kwenye hilo bega lake akiwa anaguna. Hakupewa nafasi sana baada ya kutishiwa kupigwa goti la kifua wakati anaituma mikono yake kupangua goti hilo Ashrafu aligeuka na teke ambalo lilitua kwenye uso wa Kai na kwenda kumtupa kwenye miguu ya Suzane.

Kai hakuweza kukubali hilo jambo licha ya kuwa kwenye maumuvu alichomeka kisu chake chini kwa nguvu akiwa amepiga goti moja chini akiwa anamwangalia Ashrafu kwa hasira, alipo kichomoa kisu hicho alitembea kwa mikono kuelekea pale alipokuwepo mwanaume huyo, alipo karibia kumfikia alikiachia kisu chake kwa nguvu huku akiwa anazunguka kwa kasi na mateke ya chini ambayo lengo lilikuwa ni kumzoa Ashrafu lakini ni kama alikuwa anampigia mbuzi gitaa kwani sio kisu chake wala miguu yake ambayo ilifanikiwa kutua kwa Ashrafu.

Alisimama kwa teke moja huku akizungusha lingine hewani ambalo lilidakwa kwa nguvu mpaka akahisi mguu unaenda kuvunjika, ilimpotezeshea balansi hivyo akavutwa kuelekea kule alipokuwepo Ashrafu, alipigwa na ngumi sita kwenye mbavu yake kisha alishindiliwa buti kali la kifua ambalo lilimfanya kumwaga damu nyingi sana kutoka kwenye mdomo wake na kumfanya atake kudondokea nyuma hata hivyo hakuipata nafasi hiyo kwani alidakwa na kuzungushwa kisha mwanaume akiishika shingo yake na kuhitaji kuizungusha ambapo angemnyonga na kumuua kabisa mwanaume huyo lakini alisikia sauti kali sana kutoka kwa Suzane.
"Stop Ashrafu" mwanaume sauti hiyo ilimfanya kuvikaza vidole vyake viwili na kuvipitisha kwa nguvu sana kwenye shingo ya Kai ambaye alipoteza fahamu hapo hapo kisha akamtupia pembeni.

"Nimewaambia muondoke hili eneo sitaki kuua mtu" aliongea kwa sauti kali sana huku akiwa anachechemea kwa maumivu ambayo mguu wake ulikuwa unayapitia.
"Jisalimishe Ashrafu, wote tunajua kwamba sisi hapa huwezi ukatushinda hata iweje na hali hiyo ambayo upo nayo" Suzane alitamka maneno yake akiwa anawaangalia wenzake ambapo wote walikuwa wamemkazia macho Ashrafu.

"Hahaha hahaha hahaha, sijaona ngumi yenye uzito wa kunifanya mimi nishindwe kuondoka ndani ya hii sehemu. Huwa sipigani na wanawake kwenye maisha yangu kwa heshima ya mama yangu ambaye amelala kaburini ila kama ukinilazimisha nitakufanyia jambo ambalo hautalisahau kamwe kwenye maisha yako yote"
"Namhitaji akiwa hai" aliongea akiwa anauma meno kwa vijana wake watatu, kuhusishwa kuwa wa kike ni kama alichukuliwa poa sana likiwa ni jambo ambalo lilikuwa linamkera sana kwenye maisha yake hivyo alihitaji kwanza kuipata heshima ambayo aliona kwamba alikuwa anaistahili na sio hizo dhihaka. Ashrafu alisikitika sana akiwa anaiangalia damu yake ambayo ilikuwa inamtoka kwa wingi sana mguuni kisha akakitoa kisu na kukishika mkononi.

Luqman, Lukas na Venance ndio wanaume ambao walimsogelea mwanaume huyo kwa nguvu mno baada ya kupewa kibali na kiongozi wao. Wanaume hao walikuwa wanakuja kwa kasi isivyo kawaida, walimshambulia sana Ashrafu ambaye alipigwa mpaka ukutani ambako alibaki anahema sana, aliinyosha shingo yake na kufumba macho yake kwa hasira ambayo yalikuwa mekundu sana, alipiga makelele sana kabla ya kuwajia yeye mwenyewe wanaume hao.

Luqman alikuwa mbele, alishangaa jinsi mtu huyo alivyokuwa anakuja huku kisu kikiwa kinazungushwa kwa namna ambayo hakuamini kama ni kasi ya binadamu ilikuwa inafanya hayo yote na aliona kabisa kwamba asingeweza kukizuia kisu hicho hivyo alitaka kurukia pembeni ila alichelewa kidogo mguu wake ulidakwa kwa nguvu sana, alifanikiwa kukikwepa kisu ndiyo lakini goti lilipiga kwenye mguu wake ambao ulivunjika vibaya sana. Wakati anaachiwa alikuwa anajivuta kwenda pembeni wakati huo Ashrafu alikiachia kisu chake ambacho kilizama kwenye mbavu ya Lukas lakini wakati huo alirudi na sarakasi ya nyuma ambapo mguu wake ulitua kwenye paji la uso la Luqman ambaye alijipigiza chini vibaya sana akatulia hapo hapo.

Lukas alifanikiwa kukichomoa kisu chake ambacho kilikuwa kimezama ndani sana akiwa anamwaga damu yake. Ndio wakati ambao Venance alikuwa anahangaika kuikoki bunduki yake ili kumshambulia mtu huyo maana aliona kama kupigana naye kawaida isingewezekana ila bastola hiyo ilikuja kukaa sawa wakati mhusika amefika ambapo aliikita na teke bastola hiyo ikaruka juu kisha alikwepa ngumi tatu za Venance ambapo moja ilitua kwenye tumbo lake sehemu ambayo ilionekana kutoa damu nyingi lakini hakujali hata hivyo na yeye alifanikiwa kupeleka ngumi yake usoni kwa Venance ambaye alianza kuona nyota nyota nyingi sana akawa anayumba yumba.

Ile bastola ambayo ilikuwa imerushwa juu ilidakwa na Ashrafu na wakati huo aligeuka na double kick ambayo iliishia kwenye kifua cha Venance na kwenda kujibamiza vibaya ukutani akawa ametulia kimya sana maana hakujulikana kama alikuwa amekufa au bado alikuwa yupo hai. Lukas alifanikiwa kukitupa chini kile kisu ambacho Ashrafu alimkutanisha nacho mbavuni na kuanza kumsogelea mwanaume huyo ambaye alimtandika risasi mbili kwenye kifua chake kisha akaigeuzia bastola hiyo kwa Suzane ila ni kama alichelewa wakati anaigeuza bastola hiyo Suzane alikuwa ameachia risasi yake ambayo ilitua kwenye mbavu ya Ashrafu na wakati huo walikuwa wanaangaliana kila mtu akiwa ameishika bastola na kumuelekezea mwenzake.

"Sitaki kukuua bibie ila kwa leo siwezi kuruhusu unikamate, naweza kukupa hata ruhusa ya kuniua kama ukitaka ila subiri kwanza nimalize kazi yangu. Kwa sasa wawahishe wenzako wakapate matibabu kwa sababu kuna wengine wanaweza kufa kwa muda mchache ujao, leo sikuja kwa ajili yenu" mwanaume aliongea kama utani lakini wakati huo huo aliiachia bastola hiyo na kumuachia nafasi Suzane kama anataka kumuua basi nafasi ilikuwa ni yake lakini wakati huo yeye alisogea pale chini kilipokuwepo kisu akakiokota na kuanza kuondoka eneo hilo huku damu ikiwa inamtoka kwenye mwili wake akimwacha Suzane akiwa anamtafakari na bastola yake mkononi asijue hata ni kipi ambacho alikuwa anatakiwa kukifanya wakati huo.

37 INAFIKA MWISHO.
 
SITAKI NIUAWE!!!!!!

Yes, ni taarifa njema kwako mpenzi msomaji.

Lile andiko bora ambalo ulikuwa unalisubiri kwa hamu kubwa, lile andiko lililo ahidiwa la IDAIWE MAITI YANGU, Leo limetoka rasmi.

Inatakiwa IDAIWE MAITI YA NANI na Kwa sababu ZIPI? Maandishi hayo hapo ✍️

Unalipata kwa pesa za kitanzania shilingi 6000 kamili tu ili uweze kutuliza akili yako na mzigo huu hapa.

Lipia 6000 yako kwa namba hizi hapa chini👇

0621567672 (HALOPESA)

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

FEBIANI BABUYA
 

Attachments

  • FB_IMG_1724231246332.jpg
    FB_IMG_1724231246332.jpg
    189.5 KB · Views: 13
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
Baada ya kufika ndani ya chumba hicho ni kweli mkuu wa gereza la Dominic, Luka Gambino alikuwa ameuliwa kwa kuchomwa na visu vitatu kwenye shingo huku kimoja akiwa amechomwa kwenye mbavu yake ya kushoto. Cleopatra Gambo alimwangalia sana mzee huyo mwenye kitambi chake, hakufanikiwa kuendelea kuwa mmoja kati ya wanadamu ambao walikuwa wanendelea kuivuta pumzi mpaka wakati huo.

"Nipeleke aliko Michael haraka sana"
"Sawa bosi" amri yake ilifuatiwa na wao kutoka ndani ya hicho chumba huku akitoa amri maiti hiyo ilitakiwa kutolewa humo na chumba hicho kuweza kufanyiwa utafiti.

Ndani ya chumba kimoja ambacho kilikuwa kipo ndani ya floor za chini sana za sehemu hiyo ndiko ambako kijana aliye fahamika kwa jina la Michael alikuwa amehifadhiwa akiwa amefungwa minyororo huku na huko yeye akiwa amesimamishwa katikati hata miguu yake ikiwa imefungwa pia. Mkurugenzi baada ya kuingia humo ndani aliitoa bastola kwenye koti lake na kummiminia kijana huyo risasi zote kwenye mguu wake mmoja mpaka zilipokuja kuishi huo mguu haukuwa unatamanika kabisa hata kuweza kuutazama tena kwa macho ya kawaida.

"Nilikuchukulia kama mwanangu wakati unaishi hapa, nilikusikiliza na kukupatia kila ambacho ulikuwa unakitaka wewe, kwanini umekuja kufanya haya mwanangu" alikuwa anaongea kwa uchungu sana ila hasira ambayo ilikuwa ndani yake ilikuwa haielezeki kwa sababu kijana huyo alikuwa ni moja kati ya vijana ambao aliwalea kwa unyenyekevu na mapenzi makubwa sana walipokuwa chini yake. Licha ya kuongea kwa uchungu sana kijana huyo hakuongea lolote zaidi ya kutoa chozi ambapo haikueleweka kama alikuwa anatoa kwa ajili ya maumivu ambayo aliyapokea hapo au alikuwa anayatoa machozi kutokana na uchungu mkubwa ambao alikuwa nao kwenye moyo wake.

Cleopatra alilivua koti lake na kwenda kwenye box kubwa la chuma ambalo liliwekwa juu ya meza, alivaa gloves na kuchukua mkasi mkubwa sana pamoja na bisibisi ndefu. Aliinama alipokuwa amesimama kijana huyo akiwa anavuja damu nyingi sana na kama sio minyororo ambayo alifungwa basi huenda asingeweza hata kuendelea kusimama tena.

Mwanamama huyo aliinama na kuulengesha mkasi huo kwenye vidole vya miguu vitatu ambapo alivibana kwa nguvu na kuvikata vyote kisha alizamisha bisi bisi kwa nguvu kwenye kidole kikubwa. Michael pua ililoa kwa kutoa maji maji huku mkojo ukiwa unashika nafasi yake kushuka kwa kasi kwa sababu maumivu ambayo aliyapata ilikuwa ni ngumu sana kwa mwili wake kuweza kuyahimili. Bisi bisi hiyo ilikuwa inaendelea kutekenywa na kumfanya ajutie sana kuwepo hapo hivyo alitoa kilio kama mtoto mdogo.

"Kwahiyo unahisi unaweza kuendelea kuvumilia sio?" Mwanamama huyo aliongea akiwa anamsogelea kijana huyo mdomoni maana alionekana kujifanya kuwa mgumu kushindwa kutaja kwamba ni nani alimtuma kuifanya kazi hiyo na kwanini aliweza kufanya jambo la kipuuzi kama hilo.

"Kuna maswali manne ambayo unatakiwa kunijibu hapa sasa hivi. Kwanza nambie nani amekutuma, pili uniambie ni kwanini unakubali kufanya jambo kama hili lakini tatu ni wewe umemuua na Bruno pia? Mwisho kabisa ni raisi amekutuma wewe kufanya haya?" maswali yalikuwa ni magumu sana kitu ambacho kilimfanya Michael kutamka kwa uchungu sana.

"Naomba unisamehe sana bosi, sikuwa na chaguo lingine" jibu lake ndilo lilimsogeza mama huyo karibu kutaka kusikia zaidi kwamba alitaka kuongea nini ila kwa bahati mbaya sana alianza kutoa povu mdomoni. Alimuwahi na kumbana mdomo wake lakini alikuwa amechelewa, mtu huyo alikuwa na kidonge chenye sumu kwenye ulimi wake hivyo alijing'ata kwenye ulimi na kumeza kidonge hicho ambacho kilikuwa tayari kimeisambaza sumu mwilili.
"Michael usife tafadhani, nijibu maswali yangu" alikuwa anafoka huku akiwa anautikisa mwili wa Michael kwa nguvu akiwa ameushika mdomo lakini hakuna kitu angeweza kukiokoa hata asili ilimsaliti.

"Una bastola hapo?" alimuuliza kijana wake akiwa anamwangalia kwa macho ya hasira sana, kijana huyo hakuwa na namna zaidi ya kumpa bosi wake bastola ambayo ilikuwa kwenye kiuno chake. Alisogea pale alipokuwepo Michael akiwa anaweweseka na kumpiga risas nyingi sana kwenye eneo lake la moyo kiasi kwamba hata yule kijana aliyekuwa naye alianza kuogopa sana maana bosi kuwa kwenye hali kama hiyo halafu yeye ndiye alikuwa anasimamia hilo eneo angejikuta anakula risasi bila kutarajia.

"Nina safari usiku huu, kesho nina mazungumzo marefu sana na wewe" aliongea kwa jazba huku akiwa anaitupa bastola chini na kutoka kwenye hicho chumba huku akiwa anaitoa simu yake mfukoni na kuitafuta namba ya mheshimiwa raisi ambaye alipokea simu baada ya muda mfupi sana.
"Mheshimiwa unanificha nini?"
"Hiyo ndiyo heshima ya kuongea na raisi wako?"

"Jambo ambalo nakuuliza linaushikilia usalama wa nchi. Umekuja hili eneo bila kunitaarifu halafu unaondoka wewe na watu wawili wanakufa nyuma, unataka niamini kwamba hili jambo ni bahati mbaya?"
"Kwahiyo unataka kuniambia mimi nimewaua watuhumiwa?"
"Hakuna sehemu nimesema umewaua ila nataka kujua kwanini wewe uje na wao wafe hasa baada ya wewe kuzungumza nao? Kuna mazungumzo gani ya siri ambayo umeyafanya na hawa watu mpaka waishie kwenye kufa huku mwingine akijiua mwenyewe?"

"Hiyo ni kazi yako wewe, ni uzembe wako mwenyewe watu wanauawa sehemu ambayo unaisimamia, unanikumbusha kwamba hauwezi kuifanya kazi yako?"
"Mimi siogopi wewe kunitoa kwenye hii nafasi ila nayahofia mambo ambayo hayaonekani kwa macho kumbuka kila jambo baya huwa lina mwanzo mzuri sana ila mwisho wake huwa mbaya na wa kutisha. Sitaki ije kufika siku naanza kukufikiria kwa ubaya mheshimiwa, kama unasema hakuna kitu chochote unacho kifahamu kuhusu hili sawa haina shida ila unajua kabisa kwamba ni suala la muda mfupi sana nitajua kila kitu na kuhusu kuja hapa haimaanishi kwa sababu wewe ni raisi basi ujifanyie kila unacho kitaka ulitakiwa kufuata utaratibu kwa kuheshimu sheria za nchi" Cleopatra aliikata simu hiyo kwa hasira sana hata hivyo alijitahidi kuongea kistaarabu kwa sababu mtu huyo ndiye alikuwa bosi wake ila vinginevyo mtu huyo hakutakiwa kabisa kupewa hiyo heshima kwa sababu alianza kumhisi vibaya sana.

Ilikuwa ni kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake kumkatia raisi simu kabla hawajamaliza makubaliano huenda ni jambo ambalo hata raisi mwenyewe lilimshangaza sana ila haikuwa sababu ya kuwarudisha hai ambao walikuwa tayari wamekufa. Mambo yalikuwa yanaanza kujiweka wazi, mafuta yalikuwa yanaanza kujitenga na maji na wakati huo huo alikuwa anahitajika kuweza kufika sehemu ambayo vijana wake wa Holy Trinity wapo ili aangalie hali zao maana alianza kuona kila dalili za kuwapoteza vijana wake kwenye suala la ujinga wa mtu fulani ambaye hakuwa anajali maisha ya watu wengine zaidi ya madaraka yake na tumbo lake tu.

39 BYE.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI
Safari ya mkuruenzi ilikuwa ni kuelekea sehemu ambayo ilikuwa kambi ya siri ya vijana wake watano ambao aliambiwa kwamba hali zao hazikuwa nzuri sana. Hakutaka kusindikizana na mlinzi yeyote yule usiku huo hivyo hata gari yake alikuwa anaiendesha mwenyewe kwani aliona kama ni moja ya njia ya kuweza kuzituliza hasira zake nyingi ambazo zilikuwa zimemkaba.

Aliishia Ubungo maji umbali wa kutosha kutoka lilipokuwa jengo la Tanesco kwa ng'ambo yake. Alifika kwenye geti moja na kuiweka kadi yake sehemu moja ambayo ilikuwa ni kama kioo kidogo cha kujiangalia geti likafunguka, aliingia na gari yake kisha geti hilo likawa limejifunga tena. Alipitiliza mpaka ndani ambako alikuta vijana hao wamepewa matibabu na madaktari ambao walikuwa wanamalizia kazi wakati huo na aliyekuwa salama alikuwa ni Suzane tu huku wengine wakiwa hawapo kwenye fahamu zao.

Mwanamama huyo alionyesha masikitiko makubwa sana kwa sababu hao hawakustahili kupatwa na jambo baya kama hilo kwenye maisha yake.
"Kuna yeyote ambaye unahisi kwamba tunaweza kumpoteza?"
"Lukas amepigwa risasi mbili kifuani, nina mashaka naye sana japo inaonekana mpigaji alijua anacho kifanya, amezipitisha maeneo ambayo siyo hatari sana ila siwezi kuthibitisha mpaka aamke na Luqman kichwa chake kimegongeshwa vibaya sana chini hivyo tunasubiri majibu sahihi kama atakuwa sawa tena"

"Ni yeye mwenyewe ndo amefanya hivi?"
"Ndiyo bosi ila nina maswali kadhaa kwako"
"Uliza"
"Kwanza kwanini huyu mtu hataki kutuua sisi, leo alikuwa na hiyo nafasi lakini hakuna alicho kifanya kwanini atuache hai na kuonekana kama sisi ndiyo tunalazimisha yeye kututendea haya?"

"Hiyo sababu siwezi kuijua labda huenda mna bahati tu lakini kusema mnalamishwa kumkamata sio kweli hiyo ni kazi ambayo nyie mlizaliwa kuifanya"
"Nimempiga risasi kwenye mbavu yake akiwa amejeruhiwa tayari lakini bado hakujibu licha ya kuwa na bastola kwenye mkono wake alicho niambia tu ni kwamba hana shida ya kutuumiza sisi na yupo tayari hata kama tunahitaji kumuua lakini kwanza tumuache aifanye kazi yake. Bosi kuna jambo ambalo labda tunatakiwa kulijua na unanificha?"
"Hapana Suzane"

"Sio kweli, tulikuwa hatua za mbali lakini nimesikia akiwa anaongea na wewe kwenye simu, je nalo hili utalikataa?" mwanamama huyo alisimama na kumwangalia sana binti huyo ambaye ni kama alianza kupoteza imani na bosi wake.
"Ashrafu nilikutana naye kabla hajaenda jela"
"Are you serious?" Suzane aliona ni kama hilo jambo haliwezi kuwa kweli ni kama bosi wake alikuwa anafanya ni masihara tu.
"Ndiyo Suzane"

"Unataka kuniambia huyu mtu mnafahamiana kabla?"
"Ndiyo"
"Why boss?"
"Kama ungekuwa sehemu niliyopo ungefanikiwa kuja kuelewa kwamba ni kwanini kuna mambo yanafanyika kinyume na utaratibu"
"Nataka kujua kwamba ni kwanini unatufanyia hivi? angalia vijana wa watu wanayatoa maisha yao kwa sababu wanakuamini, wapo tayari hata kufa kwa ajili yako sasa kwanini inaonekana kama unatuzunguka tena?" aliongea kwa uchungu mno kwa sababu ni kama bosi wao alikuwa anayachukulia maisha yao kawaida kawaida sana kitu ambacho kilimuuma mno.

"Kwa sababu Ashrafu amelelewa na mdogo wangu wa damu" maneno hayo yalimnyanyua Suzane akiwa anacheka kwa uchungu.
"Whaaaaat?"
"Yeah hivyo mimi namfahamu vizuri sana huyu bwana mdogo" Suzane alitikisa kichwa kukataa hilo jambo akiwa anazunguka na mkono wake anamnyooshea bosi wake.
"Kwahiyo muda wote huu ulikuwa unatuchora na kutuenjoy kwa kila jambo ambalo lilikuwa linaendelea sio bosi?"
"Hapana"

"Ukiwa na maana ipi labda ili nikuelewe"
"Sikutaka kuwa sababu ya moja kwa moja ya anguko la kijana huyu hivyo niliamua kuacha majukumu ya kazi ndiyo yaamue hatima yake ndiyo maana niliruhusu mmtafute kisheria kabisa lakini sio mimi kumkamatisha yeye moja kwa moja"
"Why?"
"Mdogo wangu asingenisamehe"
"Samahani wewe umesema una ndugu?"
"Yes"

"Lakini inajulikana kwamba wewe ni yatima"
"Kweli kabisa"
"Sasa huyo ndugu anatokea wapi tena?"
"Usiyaamini sana maandishi ya kwenye makaratasi ambayo kila mtu anaandika kile ambacho anaona kinamfurahisha yeye. Kama uliwahi kulisikia jina la Brigedia Mariana Amboni, basi huyo ndiye mdogo wangu aliye nifuata mimi na tupo wawili tu ambao tumesalia kwenye hii dunia"
"Kwahiyo mpaka sasa yupo hai?"
"Yeap"

"Bosi kipi kinaendelea mpaka unaonekana kuwa na siri nzito sana hizi moyoni mwako, ni jambo gani hasa ambalo limekufanya uamue kuuchagua upande huo wa kuishi na hizo siri moyoni?"
"Siku ukiwa mkubwa kama mimi au kuja kuwa na familia yako utakuja kunielewa Suzane na huenda wakati huo utakuwa umechelewa sana kuelewa maana za kuyafanya maamuzi magumu duniani hapa. Mdogo wangu mimi na yeye tangu tukiwa mabinti hatukuwahi kuelewana kabisa kwa sababu niliwahi kumzuia kuwa na mwanaume ampendae kitu ambacho kilifanya mwanaume huyo kuondoka kwa hasira sana na wakati anaondoka siku ambayo nilimpa onyo la kutomuona na mdogo wangu kwenye maisha yangu maana ningemuua, kwa bahati mbaya aligongwa na gari akawa amekufa. Jambo lile limefanya mdogo wangu anichukie sana kwenye maisha yangu licha ya kumpambania sana na kumtafutia nafasi kubwa jeshini lakini haikuwahi kuwa sababu ya yeye kunisamehe mimi hivyo akawa anaishi maisha yake kama hana ndugu mpaka akabadili hadi jina la ukoo na ndiyo sababu, ni ngumu sana mtu kuweza kujua kama mimi na yeye ni ndugu wa damu"

40 BYE.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
"Sioni kama hayo maelezo yanahusiana kwa namna yeyote na yeye kuwa mlezi wa Ashrafu"

"Miaka ishirini huko nyuma iliyopita kuna siku nilifanikiwa kwenda kwake bila taarifa majira ya usiku ndipo nilimkuta akiwa anambembeleza kijana wa miaka kama kumi na tano hivi na alipo niona tu alimficha kijana huyo chumbani kabla hata sijafanikiwa kumfahamu. Nilimshangaa sana kumuona na yule mtoto kwa sababu kwenye maisha yake hakuwahi kupenda watoto tangu siku aambiwe kwamba hakuwa na uwezo wa kuzaa hivyo akawa kama amewachukia watoto wote, kumuona na mtoto yule lilikuwa ni jambo la ajabu sana hivyo ikabidi nimkalishe chini aweze kunijibu maswali yangu"

"Maria huyu mtoto ni nani na umemtoa wapi?"
"Sio biashara yako kuweza kujua"
"Ni biashara yangu kwa sababu ni jukumu langu kuhakikisha usalama wa hii nchi na unalijua hilo, huyu mtoto anaweza kuwa anatafutwa kwao huko unasemaje kwamba hainihusu?"

"Kwa sababu hana kwao huyo mtoto, mimi pekee ndilo tumaini ambalo limebakia kwenye maisha yake. Wamekufa wote" aliongea akiwa analia kwa uchungu sana, nikawa namshangaa kwa maana sikumuelewa, sikuwahi kumuona mdogo wangu anamlilia mwanadamu yeyote yule zaidi ya yule mpenzi wake ambaye alikufa.
"Nani amekufa?"
"Familia yake yote"
"Ni nani huyu mtoto?"

"Ashrafu Dominic Sawa sawa" jibu lake lilinifanya nikae chini kwanza, Dominic Sawa sawa alikuwa ni moja ya watu maarufu sana nchini kwa kipindi hicho kwa sababu alikuwa ni tajiri mkubwa na ni kweli siku kadhaa nyuma alikuwa ameuawa huku ikisemekana kwamba familia yake yote iliuliwa.
"Huyu mtoto ameponaje wakati inasemekana kwamba familia nzima ilikufa?"
"Hapana huyu aliishi kwa sababu nilienda kumuokoa mimi"
"Ulienda kumuokoa? Ulijuaje kwamba hilo litatokea?"
"Dominic aliniomba msaada"
"Ulikuwa unafahamiana na Dominic?"

"Ndiyo"
"Kivipi"
"Alikuwa mpenzi wangu"
"Maria!!!!!" majibu yake yalinishangaza sana, sikuwahi kujua kama mdogo wangu alikuwa hawala wa Dominic Sawa sawa.
"Alikuwa ni mpenzi wangu kwa muda mrefu sana, tulikutana nikiwa kwenye kazi naye akiwa kwenye biashara huko Mwanza na ndipo mahusiano yetu yalianza ghafla sana. Aliniweka wazi kwamba alikuwa ni mtu mwenye familia na aliipenda sana familia yake lakini kwangu halikuwa tatizo kubwa kwa sababu nilikuwa nimeamua kumpenda kwa namna yoyote ile nikakubali kuwa nae hivyo hivyo. Yule ndiye mwanaume pekee kabisa ambaye alikuja kunirejeshea furaha kwa mara nyingine tena kwenye maisha yangu."

"Siku ile ambayo aliuawa na familia yake alinipigia simu akiwa mwenye wasiwasi mkubwa sana, sauti pekee ambayo niliisikia kutoka kwake ni kwamba naomba uwasaidie wanangu. Nilimuuliza kama yuko wapi lakini sikupata jibu lingine hivyo nilichukua gari ya jeshi haraka sana na kuitraki simu yake ambayo ilinionyesha alikokuwepo. Kwa bahati mbaya sana wakati nafika pale nilikuwa nimechelewa kwani yeye alikuwa amekufa tayari ila niliona Ashrafu akiwa hai bado na kuna mtu alikuwa anataka kumpiga risasi hivyo nilimuwahi mwanaume yule na kumuua pale pale kisha nikaondoka na Ashrafu maana baada ya kuondoka tu niliona kuna watu wengine nyuma wakiwa wanafika lile eneo, sikutaka tena kuendelea kukaa pale zaidi nikaamua kuondoka na mtoto kwa sababu alikuwa hai hivyo nitamlea mimi kama mwanangu wa kumzaa"

"Maria kwanini hukuniambia kuhusu hili jambo?"
"Unataka kumuua mtoto? kwa sababu kama ni hivyo unatakiwa kuniua mimi kwanza"
"Maria umefanya jambo kubwa lakini ni la hatari sana kwa sababu maisha yako yanaweza kuwa hatarini muda wowote ule nadhani huyu mtoto itakuwa ni vizuri kama ukinikabidhi mimi niondoke naye"

"Hilo ni jambo ambalo haliwezekani Cleopatra na kuhusu maisha yangu tangu lini umeanza kujali mimi kuwa hai? Acha kunienjoi dada angu"
"Kumbuka wewe ni mdogo wangu wa damu na tupo wawili tu"
"Sijali kuhusu hilo. Kama kweli unanipenda mimi kama mdogo wako wa damu, kuna jambo naomba unisaidie na itakuwa shukrani yangu ya maisha kwako"
"Nakusikiliza"

"Naomba sana hili jambo ubaki nalo kwenye kifua chako, ulimwengu usije ukajua kuhusu huyu mtoto wala mtu yeyote yule, mimi nitamlea kwa siri sana na hakuna mtu atajua, nitampa kila kitu lakini pia nitamtengeneza kuwa mwanaume haswa ili hata huko baadae aje kujilinda mwenyewe kwenye huu ulimwengu usi na huruma"
"Unamaanisha unataka kumtengeneza ili aje kulipa kisasi?"
"Hilo ni juu yake yeye wala halinihusu mimi na kama akitaka hivyo siwezi kumzuia kulipa"

"Maria tafadhali usifanye hilo jambo, naweza kukuruhusu kumlea kwa siri kama unavyo hitaji wewe na hata msaada nitakupa lakini usimkuze kwa kumlisha hiyo sumu ni jambo ambalo linaweza kuja kuwa hatari sana kwa hapo baadae na tunaweza kuingia kwenye mgogoro ambao utakuja kunilazimu nimuue kwa mikono yangu"
"Cleopatra utalikubali ombi langu nililokuomba au utaendelea kunipatia risala hapa?"
"Naomba nimuone kwanza" aliitwa akiwa anatetemeka sana yule kijana, huruma ilinishika sana kwa sababu alipatwa na jambo baya sana akiwa bado ana umri mdogo.

"Unaitwa nani?"
"Remy Claude ndilo jina langu" nilishangaa sana na kumgeukia mdogo wangu lakini aliishia kutabasamu tu hapo nikagundua kwamba ni yeye ambaye alikuwa amembadilishia hilo jina.
"Nitailinda hii ahadi yangu mdogo wangu. Mlee kwa namna ambayo utaona kwamba inakupendeza wewe" ile kauli yangu baada ya miaka mingi sana kupita nilimuona mdogo wangu akinifurahia na kunikumbatia hivyo niliamua kuondoka na kumuachia yule mtoto amlee anavyotaka yeye" mkurugenzi aliitema siri ambayo aliishi nayo moyoni mwake kwa zaidi ya miaka ishirini, siri ambayo Suzane ilimtoa machozi sana kwa kuisikia historia fupi ya Ashrafu waweza kumuita Remy Claude.

"Kwa maana hiyo huyo ndugu yako ndiye aliye mtengeneza huyu mtu?"
"Yeah, kwa sababu mdogo wangu ana mafunzo ya kikomando na ni mtu ambaye alikuwa hatari sana kwenye mambo ya mapigano mpaka wenzake wakawa wanamuogopa sana, hivyo ni yeye mwenyewe kwa mkono wake aliye mtengeneza Ashrafu kama alivyokuwa ameniahidi"

41 BYE.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI
"Kama ni hivyo maana yake ni yeye pekee ambaye Ashrafu anaweza kumsikiliza?"
"Hilo ni jibu sahihi Ashrafu anamsikiliza yeye tu hapa duniani lakini mdogo wangu ndo hawezi kukusikiliza maana anampenda Ashrafu kuliko kitu chochote kile"
"Tunaweza kumtumia yeye bosi akatusaidia kwenye hili"
"Kwamba amsimamishe kufanya anacho kifanya?"
"Ndiyo tuingie makubaliano" mkurugenzi alicheka sana mpaka Suzane akabaki anamshangaa tu.

"Ana uchungu sana na watu ambao walimuua mpenzi wake halafu unataka ukamshawishi amsimamishe Ashrafu kuwatafuta hao watu? kama una huo uwezo mimi nakupa address ya namna ya kumpata kisha ukaongee naye mwenyewe ila hakikisha unaenda mwenyewe na kwa siri sana kwa sababu kama ukimpelekea watu mimi mwenyewe sitakusamehe" mkurugenzi aliandika address hiyo kwenye karatasi na kumpatia Suzane. Suzane alikuwa bado kama haamini maana walikuwa wapo ndani ya mchezo ambao bosi wake alikuwa anaujua sana lakini cha ajabu mchezo huo ulikuwa ni mgumu kwao kwa sababu ya kulinda amani ya mdogo wake. Alianza kutoka humo ndani lakini Suzane alimsimamisha bosi wake kwa mara nyingine.

"Inaonekana kabisa kwamba Dominic Sawa sawa alionewa sasa ilikuwaje lile gereza likaitwa jina lake?" Mama huyo aligeuka na kumwangalia sana huyo binti.
"Ni kazi yako kutafuta ukweli wa mambo magumu kama hayo, nimekupa address ni kazi yako sio yangu hata mimi huenda sijui" alimalizia jibu lake na kuishia akimuacha kwenye mshangao tu akiwa anaishangaa dunia ilivyokuwa inaenda kwa kasi sana.

Ashrafu wakati anatoka kupambana na Holy Trinity hali yake ilikuwa mbaya sana ila hakutaka kuwa mnyonge kwa sababu alitakiwa kutoweka eneo hilo haraka kabla hajaingia kwenye mikono ya watu hao ambao aliamini kwamba msaada wa kwenda kuwaokoa ungefika mapema tu. Aliingia kwenye gari yake akiwa ana kizunguzungu lakini haikuwa sababu ya yeye kusimama hilo eneo, aliiwasha gari na kuondoka akiwa anaitafuta njia ya kuelekea Tegeta ambapo baada ya kufika hapo alikunja barabara ya kuelekea Mbezi Mwisho akiwa kwenye mwendo mkali sana. Baada ya kufika Madale hali yake ilizidi kuwa mbaya sana akawa haoni kabisa mbele, aliipiga simu yake mahali ila baada ya upande wa pili kupokelewa hakuwa na uwezo wa kuongea tena wala kuona mbele, gari yake ilipinduka na kwenda kujibamiza vibaya sana kwenye mti.

Nusu saa tuu tangu litokee tukio hilo, kuna gari nyingine ya kifahari ilifika hilo eneo ikiwa na watu wawili ambao walikuwa ndani ya mavazi meusi mwanaume na mwanamke. Baada ya kushuka kwenye gari yao aina ya VX walikimbilia kwenye eneo lilipokuwa gari ambalo alikuwa nalo Ashrafu aina ya Cadilac Escalade na kumkuta akiwa ameinamia kwenye usukani. Walimbeba na kumuingiza kwenye Vx huku mwanamke akiwa anampa maelekezo yule mwanaume kuweza kuichukua ile gari ambayo Ashrafu alipata nayo ajali akiwa anamsisitiza kutoacha alama yoyote eneo hilo kisha yeye akatoweka na Ashrafu.

Asubuhi kulikuwa kumekucha mapema sana, Ashrafu alikuwa anakurupuka kutoka kwenye usingizi wa kifo, alishangaa baada ya kujikuta akiwa amefunikwa kwenye shuka, aliruka chini ghafla ili kujua yupo wapi, alishusha puzmi baada ya kugundua kwamba alikuwa nyumbani kwake. Alikuwa amebadilishiwa nguo kwenye mwili wake na kuvalishwa traki nyeusi na vesti nyeupe ila nguo ya ndani hakubadilishiwa aliishia kutabasamu tu.

Dakika chache zilizo fuatia aliingia mwanamke mrembo sana akiwa na sinia lenye supu, mwanaume huyo alimeza mate sana baada ya kuiona hiyo supu maana alionekana kuwa na njaa isivyokuwa kawaida.
"Ni wewe ulinibadilisha nguo zangu?"
"Hahahah unaogopa kwamba nilikuchungulia"
"Oooooh shiiit, nilishakukataza kufanya hivi ujue"
"Sikuwa na namna kwa sababu Reus alikuwa amebaki kuhakikisha haachi alama ile sehemu ambayo ulipata ajali"
"Mama anajua kuhusu hili?"
"Hapana, sijamwambia chochote"
"Safi sana"

"Bosi kwanini unafanya mambo ya hatari sana namna hii huoni kama utapoteza maisha yako kizembe sana?"
"Ariana najua unanijali sana na kujali afya yangu ila kwa sasa hatua niliyofikia siyawazii tena maisha yangu zaidi ya kufanya kile ambacho kipo mbele yangu"
"Unanipa wasiwasi sana, kuna muda unafika naogopa sana unapokuwa unaondoka mwenyewe tena bila hata kuaga, nina wasiwasi kwamba ipo siku hautarudi tena" mrembo huyo aliongea kinyonge sana akiwa amejikunyata, mwanaume alimsogelea na kumkumbatia.
"Kumbuka hata siku moja sijawahi kuitelekeza ahadi yangu hivyo utaniona kila unapo hitaji kuniona, hata haupendezi ukiwa umenuna hivyo" kidogo maneno hayo yalimfanya acheke sana na vishimo vikawa vimejichora kwenye mashavu yake.

Ariana Japhet ndilo lilikuwa jina lake, alikuwa ni mwanamke msomi mwenye taaluma ya udaktari na IT, kwa mara ya kwanza Ashrafu alikutana na mwanamke huyo baada ya kuumia sana mama yake alimleta mwanamke huyo ili amtibu kwa siri maana hakutakiwa kujulikana kwa mtu yeyote yule na ndipo ukaribu wao ulipo anzia. Baadae mwanamke huyo alikuja kuijua historia ya mtu huyo akakubali kuacha kazi yake na kuamua kumsaidia Ashrafu kwenye kazi ngumu ambayo ilikuwa mbele yake, ilikuwa ni kwa msaada mkubwa sana wa mama yake Ashrafu ambaye alikuwa ni mdogo wa damu kabisa wa mkurugenzi Cleopatra Gambo kwa sababu mwanaume huyo alikuwa mpweke sana kwenye maisha yake. Huyo ndiye alikuwa daktari wake binafsi lakini pia alikuwa ni hacker wa hatari sana kwenye suala la mitandao hivyo alikuwa anazifanya kazi nyingi sana hususani za kuuficha uhalisia wa mwanaume huyo kwenye mitandao ili zisije kuwa wazi kwa watu. Ashrafu alikuwa akimheshimu sana mrembo huyo na kuwa tayari kufanya lolote kwa ajili yake lakini ilikuwa ni tofauti sana na mwanamke huyo kwake.

Kwenye moyo wake ilizaliwa hadithi moja nzuri sana ya kufikirika ya mapenzi ambayo alikuwa anahitaji mwanaume huyo aweze kuikamilisha lakini hali haikuwa kama alivyokuwa anataka, alikuwa anaogopa kumwambia kwa sababu alikuwa anamheshimu kama bosi wake ila macho yake yalikuwa yakiongea kila kitu kila amtazamapo Ashrafu machoni. Huenda mwanaume huyo aliwahi kulijua hilo jambo akaamua kujifanya haoni au alikuwa hajui kweli kama mwanamke huyo alikuwa akimpenda sana.

Mahesabu madogo tu kwake kama mama yake mlezi angetaka yeye apate tu msaidizi basi angemletea hata mwanaume ila kumuweka karibu na mwanamke mrembo kama huyo Ashrafu alitakiwa kujiongeza mwenyewe lakini mwanaume huyo roho yake haikuonekana kabisa kuwa kwenye mapenzi kwa mwanamke huyo. Mwanaume alimwachia mrembo Ariana na kusogea mezani kisha akaanza kupata chakula lakini mwanamke huyo kila alipokuwa anamwangalia Ashrafu, moyo ulizidi kumuuma sana, nafsi ilikuwa inamsuta mno zile hisia ambazo alikuwa anazificha kwa muda mrefu kwenye maisha yake zilianza kumuumbua taratibu chozi likawa linamshuka kwenye macho yake mwanaume akiwa amempa mgongo anapata supu ya nguvu.

42 INAFIKA MWISHO.
 
Back
Top Bottom