Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO
"Hapana ni ofa yangu tu kama raisi kukualika"
"Kauli yako ni amri sidhani kama kuna haja ya kuijadili mheshimiwa"
"Hapana hapa sikwambii kama amri bali ni ombi langu binafsi, nitakuwa na mazungumzo binafsi na wewe ambayo sio vyema tukayafanyia hapa Ikulu"

"Sawa mheshimiwa nitakuwa hapo bila shaka"
"Basi jioni ujiandae kuna watu watakuja kukuchukua"
"Sawa bosi" mwanamke huyo aliinuka kwa mikogo na kuanza kutoweka hapo na walinzi akiwa ananesa nesa na kuyafanya maungo yake kucheza cheza mheshimiwa raisi akiwa amekodolea macho vibaya kama aliambiwa yangedondoka.

Baada ya muda muda kidogo kupita Cleopatra Gambo na msaidizi wake Henry Mawenzi waliwasili nje ya gereza la Dominic. Walizuiwa kabisa kuingia ndani ya sehemu hiyo kwa sababu hawakuwa wakijulikana hali ambayo ilimlazimu mwanamama huyo kupiga simu yake kwa mkuu wa gereza hilo ambapo aliambiwa kwamba kuna ugeni kutoka serikalini hivyo alikuwa anahitajika haraka sana getini. Kauli hiyo ilimpa sana hofu Luka Gambino kutokana na tatizo ambalo lilikuwa limetokea asubuhi hiyo ndani ya hiyo sehemu hivyo aliwahi kwa kukimbia kuelekea lilipokuwa geti kubwa la gereza hilo.

Baada ya kufika eneo hilo, wanaume kadhaa ambao walikuwa na suti walikuwa wamesimama mbele ya mabosi wao na alipofika kiongozi wa gereza hilo walimuonyesha vitambulisho hapo akajua kwamba hao walikuwa ni watu wa usalama. Hakuwa na taarifa kabisa za mama huyo lakini kwa mazingira tu alijua huenda ni mtu mkubwa sana ndani ya idara hiyo japo hakufahamu kama ndiye mkurugenzi kwani uapisho wake ulikuwa ni siri kubwa mno. Hakuwa na namna zaidi ya kuwakaribisha watu hao ofisini kwake akiwa mwingi wa wasiwasi.

"Luka Gambino, nalikumbuka sana jina lako kwa sababu kuna kipindi liliwahi kuwa kwenye notes zangu za moja kati ya watu ambao nikitakiwa kuwapoteza kabisa kwenye uso wa ulimwengu huu" mama huyo aliongea akiwa anaikagua ofisi hiyo kisha akamgeukia mwanaume mtu mzima huyo.
"Kwanini umemuachia huyu bwana mdogo?"
"Sijamuachia bali ametoroka"
"Hilo ni jibu ambalo unaweza kumjibu hata raisi akija hapa?"
"Hapana"
"Unahisi utakuwa na kipi cha kumwambia?"
"Nitamtafuta mtu huyu"

"Utamtaftia wapi mtu ambaye hata haumfahamu zaidi ya taarifa zake chache ambazo nilizituma kwako?"
"Unisamehe sana mheshimiwa"
"Unahisi msamaha ndiyo huwa kitu cha mhimu ukifanya jambo la kijinga?"
"Hapana"
"Nipe jibu la kueleweka kwanini umemuachia huyu mtu aende?"
"Sijafanya hivyo kiongozi"

"Hili gereza lina ulinzi wa watu, lina ulinzi wa umeme, hakuna namna inawezekana mtu atoroke bila wewe kujua haiwezekani. Ukiacha hayo yote hili eneo lina kamera kila sehemu sasa inawezekana vipi haya yatokee? inamaanisha kuna kitu huwa mnakifanya kwenye kamera si ndio?"
"Sio hivyo mheshimiwa"
"Unaweza ukanionyesha hizo video za wiki nzima nione kilichokuwa kinaendelea hapa?"
"Zimefutwa zote"
"Na nani?"
"Bado nachunguza kiongozi"

"Luka Gambino. Nakujua sana, nalijua sana hilo jina kwa sababu ni asili ya familia moja ya kimafia huko New york city Marekani, ni miongoni mwa familia za kutisha sana ambazo zimewahi kutokea ndani ya jiji hilo. Naelewa kwanini ulijiita jina hilo kwa sababu hata wewe zamani ulikuwa unajishughulisha na hizo shughuli kitu kilicho kupelekea ukaamua kujipa jina la hivyo huku ukiamini kwamba kila kitu kilikuwa kipo chini ya mikono yako"

"Jina lako lilikuja kwangu mapema sana na ilitakiwa nikuue kipindi kile unajihusisha na hizo shughuli zako chafu lakini unajua kwanini mpaka leo upo hai? huenda hata hujui kama mimi ndiye niliamua kukuacha uendelee kuishi?"
"Sijajua kiongozi"
"Kwa sababu niliona kwamba licha ya uchafu uliokuwa nao tunaweza kukubadilisha kuwa mtu ambaye tunaweza kukutumia kwa ajili ya manufaa ya taifa hili. Nilimshawishi sana raisi wa kipindi kile kukupa nafasi nyingine ndipo ukaingizwa jeshini ambako ulikuja ukafanikiwa kuwa mpaka kanali baadae kwa kazi yako tukuka ambayo uliifanya ukiwa umeacha kabisa shughuli zote za ajabu ambazo ulikuwa unazifanya tangu mwanzo. Je una sababu yoyote nyingine ya msingi ya kunifanya mimi niendelee kukulinda mpaka sasa?"

"Luka ile ilikuwa ni nafasi ya dhahabu kwako, kwa madhara ambayo ulililetea taifa hili ulipaswa kufanya kazi kwa moyo mmoja haswa ili kulipa ile fadhila lakini kitu cha ajabu umekuja kufanya mambo ya hovyo zaidi na bado unataka nikuache baada ya kukupa nafasi kubwa ya kuwa mkuu wa gereza kubwa la kihistoria kama hili ukiwa unalipwa pesa nyingi na kila kitu unapewa?"

"Kiongozi nimefanya uzembe mkubwa sana, naomba nipe nafasi ya mwisho nitalirekebisha hili na sitoruhusu lije kutokea tena"
"Unataka nafasi nyingine wakati mtu ambaye tumemtafuta miaka zaidi ya kumi ametoweka? unajua tumepoteza makomando wangapi kufanikiwa kumkamata mtu yule mpuuzi mkubwa wewe? unajua ni vijana wangu wangapi wapelelezi wamepoteza maisha kwa ajili ya kumpata mtu yule? halafu kirahisi tu unakuja kuniambia habari zako za kipuuzi hapa!" mwanamama huyo aliongea kwa hasira sana akiwa anamtwisha kibao kikali sana mkuu wa gereza hilo na hakuwa na cha kufanya maisha yake yangeweza kubebwa muda wowote ule. Mzee huyo alipiga magoti kuomba nafasi nyingine kuweza kusahihisha makosa yake lakini hakuna mtu ambaye angemsikiliza kwa wakati huo.

"Mimi sina nafasi nyingine kwa ajili yako tena, huyo mtu wewe hapo hauna uwezo wa kufanya lolote ili kumkamata, kumtunza hapa ndipo uwezo wako ulipokuwa unaishia sasa kama hauwezi hata kumtunza unahisi utaweza kumkamata? unamjua kwanza mtu mwenyewe namna alivyo au unaropoka tu kwa sababu uliletewa akiwa kwenye minyororo tayari? nionyeshe aliko Bruno Josephat kisha utampigia simu mheshimiwa raisi wewe mwenyewe umpe hiyo taarifa kwa mdomo wako nafikiri baada ya hapa tunaondoka na wewe ili ukatupe maelezo ya kutosha kwanini unawaingiza watu humu ndani unapo jisikia wewe na kuwatoa unapo jisikia wewe. Kuanzia muda huu hii sehemu ipo chini ya usimamizi wetu mpaka tutakapo pata mtu sahihi" kauli yake haikuwa na majadiliano tena kwa sababu za kiusalama shirika lake lilitakiwa kusimamia gereza hilo mpaka ambapo angepatikana mtu sahihi baada ya kuwasiliana na mheshimiwa raisi pamoja na mkuu wa majeshi ambaye hakuwa na taarifa yoyote ile mpaka wakati huo.

25 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA
Luka Gambilo alipata mshtuko mkubwa sana, kwa sababu mpaka wakati huo alikuwa amepoteza kazi tayari na alitakiwa kuwapeleka alipokuwepo tajiri huyo haraka sana huku akiwa na maswali mengi sana kuhitaji kujua kwamba ni kivipi watu hao walizipata hizo taarifa juu ya uwepo wa mtu huyo ndani ya hiyo sehemu maana ilikuwa ni siri kubwa sana.

Safari yao ilienda kuishia kwenye chumba kimoja safi na kikubwa sana ambacho alikuwa anapatikana mwanaume huyo Bruno Josephat. Kilikuwa ni chumba ambacho kilikuwa tofauti sana na vyumba vingine, ungehisi kwamba yeye alikuwa anaishi ni nje ya gereza. Cleopatra alimwangalia sana mkuu wa gereza hilo wakati huo ndani ya chumba hicho ilikuwa inasikika sauti ya runinga ikiwa inapiga kelele bila shaka mhusika alikuwa anatazama runinga humo ndani. Geti la chumba hicho lilifunguliwa akiwa na wavaa suti wake ambao walibaki nje kisha yeye akaingia humo ndani na msaidizi wake akiwa ameongozana pamoja na mkuu wa gereza.

Bruno Josephat alishtuka baada ya ujio wa watu bila taarifa eneo hilo hivyo akawa amejiandaa kufoka lakini wakati anageuka kwa hasira kutaka kujua ni nani huyo ambaye alifika eneo hilo bila taarifa, alishtuka sana sura ambayo aliiona mbele yake, ilikuwa ni sura ambayo hakutegemea au huenda hakutamani kabisa kuonana nayo kwenye maisha yake kwa mara nyingine tena.
"Tajiri kama wewe kuja kujificha gerezani na kumlipa huyu mpuuzi pesa ili akufiche huku huenda kuna jambo gumu na kubwa sana ambalo limekupata na linatishia maisha yako Bruno. Kwanini mpaka leo bado unapenda kucheza michezo ya watoto hii?"

"Cleopatra! umejuaje kama mimi nipo huku?"
"Kwangu huwa ni suala la muda tu kuweza kupata taarifa za mtu yeyote kwenye nchi hii ambaye nikiamua na unalijua hilo, acha kuniuliza maswali ya kipumbavu sana namna hiyo"
"Unataka nini kwangu Cleopatra?"
"Kwanini umekuja kujificha huku? Ni kipi unakiogopa huko nje kwenye maisha yako?"
"Mimi ni mtuhumiwa kwani sitakiwi kufungwa?"

"Mhhhhh mtuhumiwa ndo unaishi maisha safi haya? kwa kosa lipi kwanza mpaka umefungwa ndani ya sehemu hii?"
"Hilo halikuhusu Cleopatra, kwamba wewe ndo unaamua yupi afungwe na nani asifungwe?"
"Mpaka nipo hapa basi ujue kabisa kwamba linanihusu tayari, na unatakiwa kuongea kwa heshima sana kwa sababu huyo mbwa wako ambaye huenda unapata kiburi kwamba anakulinda hivi tunavyo ongea ni mtuhumiwa tayari na tunaondoka naye"

"Sasa hilo mimi linanihusu nini?"
"Unaweza ukanieleza kila kitu ingali bado unayo nafasi ya kufanya hivyo kwa amani Bruno"
"Unanitisha mimi?"
"Sikutishi ila nakwambia ukweli, hili ni onyo"
"Jiangalie sana Cleopatra unaweza ukaja kuishia sehemu mbaya sana kwa sababu haujui ni wapi ambako unataka kujiingiza"

"Tumesoma darasa moja shule ya msingi huenda ndiyo sababu unahisi unanifahamu sana mimi Bruno. Nakupa nafasi nyingine tena kipi kimekufanya uingie ndani ya sehemu hii kuja kujificha? au unahisi kwamba unaweza kwenda popote na kwa muda wowote ule ambao unautaka wewe"
"Niache Cleopatra ondoka hapa kabla sijabadili maamuzi yangu na kukuweka kwenye orodha ya maadui zangu" mwanamama huyo alisimama na kucheka sana, alitoa ishara vijana watatu wa Bruno ambao walikuwa nje ya chumba hicho waletwe haraka sana na wavaa suti wake, vijana hao waliletwa mbele yake alitoa bastola na kuwamiminia wote risasi kiasi kwamba kila mtu alibaki anatetemeka humo ndani maana mwanamama huyo roho yake ilikuwa ni tofauti na alivyokuwa anaongea kwenye mdomo wake.

"Hivi Bruno unahisi labda mimi najali wewe ukifa au ukiwa hai? I don't give a f***k about you. Mtu yeyote ambaye anataka kucheza na amani ya taifa hili nipo tayari hata kuua kizazi chake chote lakini sio taifa kuharibika nikiwa bado hai labda niwe nimekufa. Nina maswali mengi sana kwako, nataka kujua kila kitu hususani kwanini Remy baada ya kukutana na wewe akawa amepotea ndani ya gereza? Nimekuuliza kistaarabu sana ambapo ningekusikiliza kwa amani na kuona kama upo kwenye matatizo ili kama naweza kukupa msaada nikusaidie lakini umekuwa jeuri na kunijibu kwa namna unavyotaka wewe, kwa sasa sina haja na majibu yako tena kwa sababu unaenda kuyatoa kwa lazima Bruno, hauna wazo ya kile ambacho kinaenda kukutokea" mwanamama huyo aliongea akiwa anacheka kwa hasira sana maana aliona mtu huyo anampotezea muda na kumletea dharau wakati yeye mwenyewe alikuwa na kazi nzito sana ya kuzifikisha taarifa hizo mbaya kwa raisi wa nchi.

Aliwapa ishara vijana wake waweze kumbeba mtu huyo pamoja na Luka Gambino hali ambayo ilimfanya Bruno kuanza kupiga makelele akigoma kuchukuliwa na watu hao ili wafanye mazungumzo lakini nafasi yake aliichezea mwenyewe kwa kutanguliza majivuno mbele badala ya uhalisia wa mambo ambavyo yalitakiwa kufanyika. Kelele zilipozidi alizimishwa kwa kupigwa na kitako cha bastola shingoni, hata mkuu wa gereza naye alizimishwa ili asijue kwamba ni wapi alikuwa anapelekwa. Walikuwa wanapita na watu hao wakiwa wamebebwa karibu na zilipokuwepo selo za wafungwa hali ambayo iliwafanya wafungwa hao kuanza kushangaa sana sababu ambazo zilipelekea kiongozi wa sehemu hiyo kukamatwa na watu ambao hata hawakuwa wakijulikana.

Baada ya kutokezea sehemu ambayo ilikuwa na uwanja mkubwa, msaidizi wa mkuu wa gereza alitoka anakimbia akiwa an bastola yake mkononi ili kwenda kuhoji kama mkuu wake alikuwa anapelekwa wapi lakini wakati mwanamama Cleopatra Gambo anamgeukia mtu huyo kwa sababu ya makelele yake alimpiga risasi ya kichwa habari yake ikawa imeishia hapo hapo.

"Hii sehemu kwa sasa itakuwa chini ya uangalizi wako mpaka mambo yatakapo tulia, baadae kidogo nakuongezea watu wengine huku nikifanya mawasiliano na mkuu wa majeshi ili tuone hili jambo tunaliweka vipi" alikuwa anampa maagizo msaidizi wake Henry Mawenzi ambaye alilipokea kwa mikono miwili jambo hilo kisha yeye akapotea na watu wake ambao alikuwa amewafuata huko.

Robert alirudi Downtown ambako alikuwa anasubiriwa kwa hamu kubwa na Hezroni ambaye alishangaa sana kwa sababu hakutegemea kama kiongozi wake huyo angerudi mapema sana namna hiyo maana aliondoka usiku wa manane na mchana huo akawa amerudi. Robert hakuongea jambo lolote lile zaidi ya kuipiga simu Arusha ambako aliwataka vijana wake wote waweze kufika ndani ya jiji la Dar es salaam haraka sana huku kila mmoja akitakiwa kuja kwa njia yake mwenyewe maana hakuwa na imani sana na usalama wao kwa sababu kutokewa na Justin kule Arusha aliamini kwamba walikuwa wanafuatiliwa kwa ukaribu sana.

"Mbona umerudi haraka sana namna hii?"
"Ametoroka gerezani"
26 inafika tamati.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
"Whaaaaat?"
"Yeah, hayupo tena kule wakati naingia asubuhi kuna mtu nilipishana nae akiwa na nguo za walinzi, nilihisi kama ni yeye na ni kweli nilikuwa sahihi sana kwa sababu baada ya kuingia tu ndani ndipo ikaja taarifa kwamba mtu huyo hayupo hivyo nikawa na uhakika moja kwa moja kwamba alikuwa ni yeye"
"Kwahiyo tunafanyaje?"
"Unatakiwa kuandaa makala nyingine kwa ajili ya kuichapisha leo usiku"
"Unataka tutoe taarifa juu ya kutoroka kwake? huoni kama tutamuingiza kwenye hatari kubwa?"

"Hapana, taarifa ikitolewa maana yake wataingizwa watu watu wengi sana mtaani na watu hao ndio watatusaidia sisi kuweza kujua yeye alipo"
"Bosi una uhakika na jambo hili?"
"Nina uhakika, usiku wenzetu wakifika tunaondoka hili eneo kwa sababu sina imani sana na usalama wake"
"Sawa bosi" Hezroni hakuwa na cha kupinga zaidi ya kutakiwa kufanya kile ambacho alikuwa ameagizwa kukitekeleza.


Muda ulikimbia sana. Mida ya jioni Anelia alikuwa amepata ugeni mpya nyumbani kwake wakati huo akiwa anasubiria kuweza kukutana na mheshimiwa raisi kama alivyokuwa ameahidiwa na kiongozi huyo mkubwa zaidi wa serikali. Mkurugenzi wa usalama wa taifa alikuwa amefika hapo kwake kwa ajili ya kufanya naye mazungumzo ya mhimu sana kwa sababu kwa wakati huo walikuwa wanaingia kwenye hatua ngumu sana.
“Bosi umenishtua sana na taarifa ya wakati ule”
“Kulikuwa hakuna namna zaidi ya kuweza kukupatia taarifa ili uiweke akili yako sawa kwa sababu kesho inatakiwa urudi tena kazini”
“Kivipi imewezekana mtu huyo kuweza kutoroka sehemu kama ile?”
“Hilo ni swali ambalo hata sisi bado hatuna majibu yake ila nimekuja na mkuu wa lile gereza baada ya kugundua kwamba kuna mambo anayafanya nyuma ya pazia ambayo tunatakiwa kuyashughulikia haraka sana kabla hayajatuletea matatizo huko mbeleni”

“Kwahiyo kwa sasa ni jambo gani ambalo mimi napaswa kulifanya?”
“Unajua tupo kwenye wakati mgumu sana kwa sababu ya mambo kadhaa ambayo yanaendelea, kwanza tunatakiwa kumpata mtu ambaye anamiliki gazeti ambalo liliitoa ile Makala ya kukamatwa kwa Remy, bila kulifanikisha jambo hilo hakuna kitu tutakuwa tumekifanya. Na kwa sasa ametoroka tena gerezani kuna uwezekano akaitumia tena nafasi hii kuweza kutusambazia habari mbaya sana tutazidi kupoteza imani kwa raia wetu”

“Lakini unahisi ni kwanini huyu mtu anafanya haya yote, je kuna jambo ambalo labda unalijua unajaribu kuniweka mbali nisilifahamu?”
“Unazungumzia habari ya mtu huyo na Domini Sawa sawa?”
“Ndiyo”
“Hapana ningekuwa nimekwambia, hakuna ninalo lijua kuhusu hayo mambo na ndiyo ambayo tunatakiwa kuyapigania kwa sasa ili tuweze kuyafahamu”
“Najiuliza sana bosi, haiwezekani tu mtu bila sababu ya msingi akaanza kuzusha hizi habari lazima kuna namna imewahi kufanyika na kuna watu wanaujua ukweli ila wanajaribu kuukwepesha”

“Kwa sasa tunatakiwa kwanza kuizingatia kazi ambayo ipo mbele yetu, nahitaji kuanzia kesho uingie mtaani mwenyewe kwa sababu naamini unaweza kuifanya hii kazi kwa weledi mkubwa sana. Fuatilia kila hatua kuweza kujua kwamba mtu huyu yuko wapi, kumbuka wewe ndiye umeishi naye hivyo unamjua angalau kidogo alivyo na ni matumaini yangu utatusaidi sana katika hili”
“Kama ukifanikiwa kumpata atakapokuwepo basi utoe taarifa mapema sana ili upatiwe msaada wa haraka kabla haujaingia kwenye hatari maana kwa sasa ni wazi hata wewe akikuona anaweza akakufanyia jambo baya sana”
“Nimekuelewa kiongozi, kesho naianza hiyo kazi”
“Kuna kitu unataka kuniuliza Anelia?”
“Kwanini?”
“Uso wako unaongea”

“Hivi ni kweli haujui lolote kwamba ni kwanini baba yangu na mama yangu waliuawa? Haujui kwamba huenda ni nani alihusika na jambo hili labda?”
“Kwanini unataka sana kujua kuhusu haya mambo ambayo yalishapita Anelia?”
“Kwa sababu ile ni familia yangu na wale walikuwa ni wazazi wangu, kuondoka kwao kumenifanya niwe mpweke mpaka leo naishi kwa shida na taabu ya maumivu makali sana moyoni”

“Najua kila kitu Anelia ila huu sio wakati wake wa wewe kujua hayo mambo. Najua unaweza ukanifikiria vibaya sana kwa kulijua hili na kushindwa kukuambia mapema ila haya yote yalikuwa ni kwa ajili ya kukulinda wewe hapo”
“Kuniweka mbali na ukweli juu ya familia yangu ndiko kunilinda mimi? Kwanini unifanyie mimi jambo kama hili? Why?”
“Kwa sababu kama ungeujua ukweli ungekuwa umeshakufa muda mrefu sana, sikuwa tayari kukupoteza na wewe?”

“Haukuwa tayari kunipoteza na mimi? Unamaanisha nini kusema hivyo?”
“Anelia, ifanye kazi ambayo ipo mbele yako na ukiimaliza nakuahidi mimi mwenyewe nitakwambia kila kitu kuhusu familia yako ila kwa sasa siwezi” mwanamama huyo aliongea kama vile anatania ila alikuwa anamaanisha sana, kwa wakati huo Anelia alitakiwa kuwa makini tu na kazi ambayo ilikuwa mbele yake na sio kupatiwa taarifa ambazo ni wazi kiongozi wake alijua kabisa kwamba mrembo huyo hakuwa tayari kuzipokea kwani moyo wake bado haukuandaliwa kwa ajili ya taarifa za kutisha sana kama hizo.

Anelia alishangaa sana kuhusu bosi wake, alionekana kumjua sana zaidi hata ya yeye alivyokuwa anamjua. Maswali yalikuwa ni mengi sana kwake asielewe kwamba ni jambo lipi ambalo lilikuwa linaendelea kwenye maisha yake. Akiwa anaendelea kujiuliza maswali mengi sana hapo alipokuwepo, simu yake ya mkononi ilikuwa inaita na baada ya kuipokea ilikuwa ni taarifa kwamba alitakiwa kujiandaa na kuwaelekeza watu hao alipokuwepo kwani muda wa kwenda kukutana na mheshimiwa ulikuwa unakaribia kufika hivyo alipaswa kuwa tayari.


Usiku wakati raisi anajiandaa kwenda kufanya mazungunzo yake ya siri na Anelia Baton, alipokea simu kutoka kwa mkurugenzi wa usalama wa taifa.
“Hello mheshimiwa”
“Nakusikiliza”
“Naomba tuonane nina taarifa za mhimu sana za kukupatia” raisi huyo kabla ya kujibu aliiangalia kwanza saa yake kisha akaguna maana ulikuwa ni muda wa kwenda kukutana na mrembo Anelia Baton

“Njoo kesho asubuhi ofisini, kwa sasa nina majukumu binafsi”
27 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
“Ni taarifa za mhimu sana ambazo hazitakiwi kulala kabisa”
“Nakupa dakika kumi na tano uwe ofisini hapa”
“Sioni kama ni vizuri tukiongelea ofisini mheshimiwa, kama itakupendeza tukutane nje ya Ikulu”
“Ok. Tukutane Kawe” alitaja eneo hilo kwa sababu halikuwa mbali sana na kule ambako alikuwa anaelekea yeye.

Ndani ya nusu saa tu alikuwa amefika hiyo sehemu ambapo walinzi walishuka kwenye gari na mkurugenzi ambaye naye alikuwa na vijana wake alisogea na kuingia kwenye gari hiyo ambayo alikuwepo raisi.
“Vipi kusumbuana na usiku huu na nimekwambia kuna ratiba zangu binafsi ambazo natakiwa kuzikamilisha. Kuna jambo gani haswa unataka kuniambia”
“Remy ametoroka gerezani”

“Whaaat the f**k”
“Ametoroka asubuhi ya leo”
“Hilo ni jambo ambalo haliwezekani”
“Nimeenda mwenyewe kuhakikisha nimegundua hilo lakini kuna mambo ambayo yanaendelea kule ndiyo yamepelekea jambo hilo litokee”
“Yapi?”

“Bruno Josephat alikuwa kule gerezani”
“Nadhani unanitani sio”
“Hapana mheshimiwa huo ndio uhalisia”
“Bruno anatafuta nini kule na alifungwa kwa ruhusa ya nani?”
“Mkuu wa gereza”
“Luka Gambino?”
“Ndiyo mkuu”
“Hahahah hahahaah hhahaha mpuuzi mkubwa huyu, sababu gani imemfanya afanye hayo yote?”
“Inaonekana kwamba amelipwa pesa nyingi sana”
“Sababu ni ipi hasa mpaka Bruno alipie pesa nyingi kwenda kufungwa?”
“Inaonekana kuna uhusiano mkubwa sana kuwepo kwake kule na Remy kutoroka”
“How?”

“Kabla ya wewe kwenda gerezani kuongea na Remy alikuwa amekutana na Bruno hivyo kuna makubaliano inadaiwa kwamba wameingia na Bruno ndiye amamesaidia Remy kutoroka kule”
“Hizi taarifa wewe umezipatia wapi?”
“Henry alihisi hili jambo mapema nikampa ruhusa ya kulifuatilia hilo hivyo akawa amemuingiza kijana wake mmoja kule gerezani ambaye ndiye amatuletea majibu na taarifa za kutoroka kwa mtu huyo”
“Umefanya maamuzi yapi?”
“Mpaka sasa gereza lipo kwenye usimamizi wangu, Luka Gambino na Bruno wapo kwenye mkono wangu kwa ajili ya mahojiano sema sikuona kama ni ustaarabu kulikamilisha hili bila ruhusa yako”

“Ametoroka gerezani mtu ambaye zimefanyika jitihada kubwa kumpata, mtu ambaye ameua watu wengi sana na kutupotezea pesa nyingi sana halafu kiwepesi tu hawa wajinga wanamtorosha gerezani? Wahoji kwa namna yoyote ile mpaka waseme ukweli wote ambao wanaukumbatia, kesho mimi nitakuja kwa ajili ya kuipata ripoti kwako ila hakikisha hawafi kwa sababu na mimi nitakuwa na mazungumzo nao binafsi hasa Bruno huyu namhitaji sana”
“Sawa bosi”

“Na kuhusu Remy kuna taarifa gani’’
“Muda huu naenda kwenye kikao na vijana wangu, usiku huu huu wanaanza kazi ya kumtafuta”
“Apatikane haraka sana namhitaji, halafu hakuna taarifa zozote zile kuhusiana na hawa wapumbavu ambao wameniharibia sana jina langu kwa hilo gazeti lao la kipumbavu”
“Yote kesho nitakupa majibu kiongozi”
“Nawahitaji hawa watu, unatakiwa kuelewa kile nakwambia kwenye kinywa hiki usiku huu kwamba namaanisha sana”

“Sawa bosi” maelezo yake yalikuwa yametosha hivyo alishuka lakini mheshimiwa raisi alibaki ametulia kwanza maana kila muda ulivyokuwa unazidi kwenda mambo yalikuwa yanazidi kuwa mengi sana. Aliitoa simu yake na kuipiga mahali;
“Kesho nakuhitaji uwepo Tanzania mapema sana” ilikuwa ni amri kisha akaikata simu hiyo na kuamuru vijana wake wamuwahishe kwenda kukutana na mlimbwende Anelia Baton.


Ilikuwa ni mara ya kwanza kabisa kwenye maisha yake Anelia kuingia sehemu ya kifahari sana kama hiyo, jumba la kifahari la mheshimiwa raisi lilikuwa limepambwa kwa vito vya thamani ambavyo hakuwa na imani kama kuna mahali alipata kuviona, alishangaa jinsi viongozi hao wakubwa wa taita walivyokuwa wanaliingiza taifa kwenye hasara kubwa sana namna hiyo ya kutumia vitu vya gharama huku watoto wakiwa hawana hata viti vya kukalia kwa ajili ya masomo yao.

“Karibu sana malkia, umeipendezesha sana hii nyumba leo” mzee huyo aliongea akiwa anafurahia sana ujio wa mrembo huyo.
“Asante sana mheshimiwa, nimefurahi sana kuweza kupata mwaliko wako ndani ya sehemu nzuri na salama sana kama hii”
“Unajua kuwa raisi ni moja kati ya kazi ngumu sana ambazo watu wengi hawazijui, akili yako inabidi iwe inafanya kazi kwa masaa ishirini na manne kwa sababu maamuzi yako yanakuwa yamebeba hatima ya maisha ya watu wengi sana, ukikosea kidogo tu unawaumiza wengi hivyo kuna muda inakuwa ni vyema ukiwa na sehemu iliyo tulia kama hii kwa ajili ya kutuliza akili”

“Unalo liongea ni sahihi kabisa mheshimiwa lakini sijaelewa lengo hasa la sisi kuweza kukutana hapa”
“Hahaha hahaha Anelia mbona unaniuliza swali la kitoto sana, au unahisi kwamba naweza kukuumiza?”
“Sina maana hiyo mheshimiwa, sio rahisi sana mtu wa kawaida kama mimi kukaribishwa kwa heshima kubwa sana namna hii tena na raisi huenda kuna jambo ambalo labda natakiwa kulifanya na mimi silijui”

“Unapenda kuishi hivyo mpaka siku unakufa Anelia?”
“Hapana mheshimiwa”
“Kweli kwa mwanamke mrembo kama wewe sio vizuri sana kila siku ukawa unapishana na risasi mitaani huko, unatakiwa kupata muda wa kuuweka vyema urembo wako”
“Unamaanisha nini mheshimiwa?”

28 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA
“Unamaanisha nini mheshimiwa?”
“Mimi sio mzuri sana kwa wanawake kwa sababu muda mwingi nakuwa natingwa sana na majukumu ya taifa lakini pia majukumu yangu binafsi ila naweza kuikiri nafsi yangu kwamba kwenye maisha yangu sijawahi kukutana na mwanamke mrembo kama wewe. Kukuona tu kwa mara ya kwanza nilitamani sana kama tungepata nafasi ya kujuana kwa mengi zaidi ndiyo maana nilihitaji tuweze kukutana tukiwa wenyewe ili tuweze kuzungumza kwa mapana yake”

“Mheshimiwa unamaanisha unanipenda?” Anelia aliona mzee huyo amemuelewa sana sema alikuwa anauzunguka mbuyu tu hivyo akaamua kumrahisishia ili asihangaike sana. Mheshimiwa aliguna kwanza na kuiweka glasi yake ya wine pembeni akiwa amemkazia mboni zake mrembo Anelia.

“Ni jambo zuri kama umejionea hilo jambo mwenyewe. Sikutaka kukuharakisha ili unifikirie vibaya na kuhisi kwamba nayatumia madaraka yangu kukupata hapana ndiyo maana nilitumia nafasi nzuri sana ya kukutana mimi na wewe ili tuweke makubaliano”

“Kwangu ni jambo la bahati sana kuweza kupendwa na mkubwa wa taifa lakini nahisi kama jambo hili haliwezekani kwa sababu kuu mbili mheshimiwa. Kwanza bosi wangu akijua kuhusu hili linaweza kuniletea matatizo makubwa sana lakini sababu ya pili wewe tayari una mke’’ mheshimiwa alijiweka sawa baada ya kauli hizo. Mara ya kwanza alikatishwa tamaa baada ya mwanamke huyo kudai kamba haiwezekani lakini baada ya kugundua kwamba sababu zenyewe zilikuwa ni za kitoto aliona kabisa ushindi ukiwa kwenye meza yake hivyo ilikuwa ni yeye mwenyewe kumalizia pasi tu.

“Kwanza bosi wako hawezi kujua kuhusu hili kwa sababu itakuwa ni baina yangu mimi na wewe na jambo hili litakuwa linafanyika kwa siri sana. Pili mimi na mke wangu tuna migogoro mikubwa sana kiasi kwamba hata haki yangu ya ndoa siiipati hivyo nikimaliza tu miaka yangu ya kukaa madarakani tunapeana talaka, hilo ni jambo ambalo haupaswi kulitilia shaka kabisa” alijipambanua sana mheshimiwa ili kuushinda moyo wa mtoto wa kike.

“Mheshimiwa….” kabla hajamaliza kuongea mzee huyo alipiga goti lake na kumuomba kwamba hakuwa anamtaka kuwa mwanamke wake kwa sababu ya madaraka yake hapana bali moyo wake ulimpenda mwanamke huyo. Alikuwa anawaza mambo mengi sana Anelia kama huyo mzee ni kweli alimpenda au ni tamaa za ngono tu zilimpanda kutokana na ubora wa umbo lake na urembo wa kutupwa ambao alikuwa nao? Jibu alikuwa nalo mhusika ambaye alikuwa amepiga goti wakati huo akiwa natia huruma ili aweze kupatiwa nafasi hiyo.

“Hii ni nafasi yangu kuweza kutimiza kila ninalo lihitaji kwenye taifa hili kwa kumtumia raisi, kama akiwa upande wangu basi natakiwa kumpatia penzi ambalo litamfanya kila wakati aanze kuniwaza mimi tu ili awe ananisikiliza mimi kwa kila kitu. Remy nitakutafuta kwa gharama yoyote ile” Anelia aliona ndiyo njia sahihi kwake akiwa anawaza hayo kwenye akili yake hivyo alimuinua mheshimiwa raisi kutoka pale alipokuwepo wakaangukia kwenye sofa kuanza kubadilishana juisi ya asili ambayo ilikuwa kwenye midomo yao.

Hali hiyo wawili hao iliwasahaulisha kwa muda kuhusu hii dunia ambayo sisi wengine wote tunaishi, wakaenda mbali sana kwenye huba ambalo huwa linawapa ugonjwa wa moyo wale ambao wanajifanya ni magwiji sana kwenye uwanja wa mapenzi.

Anelia aliamua kuanza kuutumia urembo wake ili kuweza kutimiza yale ambayo alikuwa nayo, moyo wake ukiwa una mengi sana ya kuyajua na kuyafanya huku kasi kubwa ya kuweza kulipa kisasi kwenye moyo wake ikiwa inamuwaka moto. Penzi lilizalisha safari mpya ya maisha yake kwa kuwa hawala rasmi wa mheshimiwa raisi wa Tanzania Tobias Maalimu.






SENTINEL NEXUS INTELLIGENCE AGENCY HEADQUARTERS.
Yalikokuwepo makao makuu ya usalama wa taifa, HOLY TRINITY walikuwa wameitwa na kiongozi wao Cleopatra Gambo, kulikuwa na kikao maalumu kuhusu upatikanaji wa mtu ambaye alikuwa amepotea na kuweza kuwapata watu ambao walikuwa wanasambaza taarifa mbaya sana kwenye magazeti kumharibia raisi.

"Nimewaiteni hapa leo kuna kazi ya dharura na kubwa sana ambayo imejitokeza kwa mara nyingine tena. Remy amefanikiwa kutoroka gerezani na mpaka sasa hatujui kwamba yuko wapi au amepanga kufanya nini baada ya kutoka huko hivyo anatakiwa kupatikana haraka sana"
"Bosi inawezekana vipi mtu huyo aweze kutoroka gerezani?"
"Kuna mchezo ulikuwa unachezeka pale ndio ambao umemsaidia kuweza kutoka huko"
"Tunaweza kuanza na huyo mkuu wa gereza? kwa maelezo yako maana yake ni wazi atakuwa anajua ni wapi alipo mtu huyo"

"Huyo tunaye na sio mhimu sana, Buno Josephat ndiye anaweza kuwa anajua mengi sana kwa sababu kabla ya Remy kutoroka walikuwa na mazungumzo ya siri sana"
"Unatupatia ruhusa ya kumhoji huyo mtu mkuu?"
"Suzane ndiye atakaye mhoji na mimi nikiwepo, nyie wengine mtakuwa watazamaji tu. Suzane hakikisha anaongea ila asije akafa, huyu tunamhitaji sana akiwa yupo hai bado" mama huyo alitoa maelekezo ambayo yalilishangaza sana kundi hilo liliokuwa na watu watano ambao waliongozwa na mwanamke. Kundi hilo lilikuwa ni kundi la hatari na la kutegemewa sana na mwanamama huyo ndiyo maana alikuwa anawatumia kwenye zile kazi ambazo aliona moja kwa moja kwamba vijana wake wengine wasingeweza kuzifanya.

Waliongoza kwa pamoja mpaka ndani ya chumba ambacho alikuwa amehifadhiwa tajiri huyo, alipewa nafasi ya kuweza kuongea kwa amani wakiwa gerezani akaleta kiburi, aliahidiwa kwamba angeongea kwa lazima. Mwanaume mmoja ambaye alijulikana kama Kai alimuwekea bosi wao kiti kwa mbali kidogo akiwa anaangaliana na mtu huyo huko Suzane akiwa anafungua box lake la kazi. Bruno hakuwahi kuiona kabisa sura hiyo kwenye maisha yake yote na wakati huo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kabisa kumuona Suzane mwanamke ambaye hakuonyesha hata dalili ya tabasamu licha ya uzuri aliokuwa nao.

Alitoa kisu kikali sana, misumari mikubwa pamoja na nyundo kisha bastola nayo akaiweka pembeni. alimsogelea mwanaume huyo akiwa anamkadiria sana, aliishia kusikitika baada ya kuona alikuwa mlaini sana kwenye mwili wake. Alimtandika kibao kikali sana kwenye shavu lake, alihisi kama shavu linataka kuchanika hali ambayo ilimfanya kufumba macho nadhani hakuelewa kwamba hilo lilikuwa ni kosa zaidi kwani wakati anayafumbua macho yake baada ya kupokea maumivu makali sana ya goti aligundua kwamba msumari uligongelewa kwenye goti lake.

Alikuwa kama amezinduka kutoka kuzimu kwa sababu alipiga makelele sana ila hayo makelele yake hayakuhitajika humo ndani, kuzidisha kwake kuyapiga kulifanya Suzane azamishe kisu kikali kwenye paja la mwanaume huyo kisha akamuwekea alama ya kidole mdomoni
"Shiiiiiiiii!" bosi alikuwa karibu hivyo hakutakiwa kupiga makelele yake kwa maana yalikuwa yanamuumiza mwanamama Cleopatra Gambo. Kisu kilichomolewa kwa nguvu sana yeye akiwa anahema kwa taabu.

29 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI
"Huwa sipendi sana kuongea ongea hususani vitu ambavyo havina umuhimu kwangu na kwenye maisha yangu kwa ujumla. Unaweza ukayajibu maswali haraka sana kabla hatujafika mbali ili kila mtu akapumzike" kwa mara ya kwanza aliisikia sauti ya Suzane mwanamke huyo akiwa anamzunguka hapo alipokuwa amekalishwa.

Hakuwa na cha kujibu Bruno, alikunja ndita zake kwa gadhabu sana huku akiwa anamwangalia mwanamama Cleopatra Gambo kwa hasira sana.
"Nitakuua msh......" alikatwa sikio kwa nguvu mno baada ya kujaribu kumtukana bosi wa idara hiyo. Alilia sana lakini ni kama alikutana na malaika mtoa roho kwani mwanamke huyo alikuwa na roho mbaya sana, aliichomoa bastola alipokuwa ameiweka kisha alipiga risasi mbili kwenye kiganja cha vidole vya mguu wa kulia, nguvu ya risasi hizo zilitoboa kiganja hicho na kwenda kuchimbua chini ya sakafu huku akibaki analia sana mr Bruno hali iliyo mpelekea mpaka kujikojolea.
"Nasema, nasema"

"Una dakika tano tu za kujielezea kabla sijaondoka na mguu wako mmoja" Suzane aliongea kwa nguvu na kusogea pembeni ili mtu huyo aweze kumuona bosi wa idara hiyo na kuweza kumjibu maswali yake.
"Mimi nilienda kwenye lile gereza kwa sababu natakiwa kuuawa kama nikionekana nje"
"Kwanini?"
"Wamemteka binti yangu"

"Nani?"
"Kama nikimtaja mwanangu atakufa"
"Mhhhh nina imani utamtaja kwa kutaka au kwa lazima. Nambie kwanza kuna mpango gani kati ya wewe na Remy?"
"Nimemsaidia kutoroka ili akamsaidie mwanangu"

"Kwahiyo kutoroka kwake ni kwa sababu tu ya kuhitaji akamsaidie mwanao?"
"Ndiyo ndiyo"
"Wapi?"
"Aliko sijui ila kuna mtu mmoja ambaye ndiye mwenye taarifa zote juu ya mwanangu aliko"
"Anaitwa nani huyo?"

"Benard Taradadi"
"Unamaanisha huyu mmiliki wa benki za TUNAKUWEZESHA?"
"Ndiyo"
"Mna ugomvi gani hadi ahusike na kupotea kwa mwanao?"

"Yule ndiye anaweza kuwapeleka kwa mtu ambaye ndiye mhusika mwenyewe wa haya mambo"
"Kwanini umtumie Remy? je mnafahamiana kabla?"
"Sijawahi kufahamiana naye kabla ya kukutana naye lakini baada ya kufika kule gerezani ujasiri wake na jinsi alivyo muua mwanajeshi mmoja akiwa kwenye minyororo yake alinivutia sana baada ya kumtazama mara kadhaa tu kwenye macho yangu"

"Hiyo ni sababu dhaifu sana kama ungekuwa unalitaka hilo kuna watu wengi sana ambao ungewatumia kwa sababu wewe ni mtu mwenye pesa nyingi sana bruno"

"Sababu kubwa ya kumtumia yeye ni kwa sababu hajulikani kwa hao watu hivyo wasingehisi kama ni mimi nimemtuma, kama ningemtuma mtu mwingine lazima wangejua kwamba ni mimi nipo nyuma ya mchezo hivyo ningempoteza mwanangu kirahisi sana"

"Umejiuliza labda kwamba ni kwa sababu gani amekubali kazi yako kirahisi tu?"
"Nilimuahidi kuwa huru na kumlipa pesa nyingi sana kama mwanangu angefanikiwa kurejea salama"
"Unahisi Remy ana shida ya pesa kwenye maisha yake Bruno?"

"Kama sio pesa basi itakuwa ni kwa sababu ya kumuweka huru ndiyo maana alikubaliana na mimi" mwanamama huyo aliishia kusikitika sana
"Bruno wewe ni moja kati ya watu wapumbavu sana, inawezekanaje mtu ambaye amejipeleka mwenyewe jela akafurahia wewe kumuweka huru?"
"Unamaanisha nini kusema kwamba alijikamatisha mwenyewe?"

"Kuhusu hili tumepata uhakika tukiwa tumechelewa sana hivyo tulikuwa kwenye mpango wa kuweza kumkamata mtu huyo tumlete huku aje ahojiwe kiundani ila wakati tupo kwenye hiyo mipango ndipo tumepata taarifa kwamba ametoroka na ni baada ya kuzungumza na wewe. Jibu rahisi ni kweli umekiri mwenyewe kwamba umemsaidia kutoroka lakini uhalisia ni kwamba haya yote alijua kwamba yatatokea hivyo lengo la kuja kule gerezani lilikuwa ni kukutana na wewe"

"Hapana, akutane na mimi kivipi na sina tatizo nae lolote?"

"Huyu mtu alifungwa jela baada ya kuhukumiwa miaka sitini lakini huko jela aliua askari na wafungwa wenzake kitu ambacho kilimfanya kuwa hatari sana kwa eneo lile hivyo akawa amehamishwa kuja huko ulikokuwa. Haya yote alikuwa ameyapigia mahesabu muda mrefu sana ndiyo maana moja kwa moja alijua wewe hapo unatafuta mtu wa kumtafuta binti yako na lazima ungetamani kumtumia yeye. Hivyo umeingia kwenye mtego wake moja kwa moja"

"Why?" Bruno alibaki ameduwaa asijue ni kitu gani kilikuwa kinazungumzwa.
"Hatuna uhakika ila mtu huyu anawatafuta wewe na wenzako ili awaue wote"
"Hahaha hahaha hahaha sasa anitafute kuniua mimi kwa sababu ipi labda?" aliamini watu hao walikuwa wanamuingiza ni kwenye mtego wa panya ili anase kwenye kumi na nane zao hivyo aliona kwamba wanaongea vitu vya kijinga tu. Akiwa kwenye kicheko chake cha maumivu maana alikuwa anavuja damu, Cleopatra Gambo alimrushia gazeti ambalo lilikuwa na taarifa ya kumtaka raisi akapige magoti na kuiomba msamaha familia ya Dominic Sawa sawa kwa kosa ambalo lilifanyika miaka ishirini iliyopita. Bruno Josephat alishtuka mno baada ya kuiona taarifa hiyo kwenye gazeti, hilo jina halikuwa geni kwake aliyageuza macho yake na kumwangalia mkurugenzi huyo ambaye naye alikuwa amemkazia macho.

30 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA
"Je kuna jambo lolote ambalo unalijua kwenye hiyo miaka ambayo imezungumziwa hapo na hilo jina?" Bruno alicheka tu akiwa bado haamini
"Huyo mtu niliwahi kumfahamu kwa sababu alikuwa ni mtu tajiri sana hapo zamani lakini sielewi jina lake linatafuta nini hapa kwa sababu hakuna ninacho kijua kuhusu yeye"
"Una uhakika na unacho kisema?"
"Ndiyo" mwanamama huyo hakuongea lolote zaidi ya kuitoa picha ambayo ilikuwa kwenye mfuko wake wa koti na kuirushia karibu na alipokuwa Bruno. Kwenye picha hiyo alikuwa ni yeye pamoja na mtu mwingine.

"Hiyo ni picha yako wewe na Dominic Sawa sawa na mlionekana kuwa karibu sana, leo unaniambia vipi kwamba hukumfahamu kwa undani mtu ambaye ulikuwa karibu naye kwenye biashara? Bruno sipo kupoteza muda na wewe hapa, unaweza ukachagua kuniambia ukweli nikusaidie kwa sababu ni lazima watakuua au ukatae kuniambie ukweli nikulazimishe kuusema ukweli kisha nikuue mwenyewe. Kama nilivyo kwambia hakuna anayejali kuhusu wewe ukifa au ukiwa hai, hakuna mtu anapata hasara yoyote ile" alikamatwa mbavuni haswa, alitakiwa kusema kila ambacho alikuwa anakifahamu kuhusu mambo hayo vinginevyo ilikuwa inakula kwake.

"Unataka kuniambia kwamba yule bwana mdogo ni, ni......." alikuwa anababaika sana hivyo mkurugenzi akalazimika kumsaidia kumalizia sentensi yake.
"Mtoto wa damu wa Dominic Sawa sawa. Hatuna uhakika na hilo bado ila kwa matukio ambayo tunajaribu kuyalinganisha ni wazi kwamba ni mtoto wake wa damu"
"No, haiwezekani"
"Kwanini isiwezekane?"
"Familia yake yote ilikufa mtoto wake akiwa na miaka kumi na tano tu"
"Uliuona mwili wake?"
"Hapana"
"Una uhakika gani kwamba sio yeye? kwa sababu hata jina lake ni la uongo na historia yake ni ya kufoji"
"Kuhusu jina ni kweli hakuwa akiitwa Remy, mtoto wa Dominic Sawa sawa alikuwa anaitwaaa......" alivuta maneno yake akiwa analikumbuka jina la huyo kijana hatimaye lilikuja kwenye kichwa chake.

"Ashrafu. Yes, Ashrafu ndilo lilikuwa jina lake mtoto wa Dominic Sawa sawa"
“Una uhakika?"
"Ndiyo, hilo ndilo lilikuwa jina la mtoto wake wa kiume, na alikuwa na watoto wawili tu" wote humo ndani walibaki wanaangaliana, ikamlazimu Suzane kufungua taarifa za mtu huyo na kulisoma jina la kundi lake ambalo lilikuwa linajulikana kama SARAFU KUMI NA TANO zilizo potea. Akamgeukia Bruno ili kumuuliza.

"Huyu mtu familia yake ilikuwa na jumla ya watu wangapi?" Bruno alimwangalia sana mwanamke huyo kwa sababu muda mfupi ambao ulikuwa umepita ndiye alikuwa ametoka kumpatia maumivu makali sana ila hakuwa na namna zaidi ya kumjibu maana angemletea matatizo zaidi.
"Kumi na tano"

"Oooooh shit! ni yeye mwenyewe" Suzane aliongea kwa sauti kubwa sana akiwa anaangalia kwa umakini taarifa hizo. Ikabidi wote wamgeukie Kai akaamua kuuliza.
"Umepataje uhakika?"

"Kundi lake linaitwa SARAFU KUMI NA TANO mwisho akiwa amelifuta neno ZILIZO POTEA halafu familia yake ilikuwa na watu kumi na tano kwa ujumla ambao inadaiwa kwamba walipotea sasa huoni kama kuna kitu anajaribu kukimaanisha hapa" hilo sasa lilianza kumuingia kila mtu kichwani kuhusu uhalisia wa jambo hilo.

"Kuna watu wana akili sana hapa duniani. Maana yake alikuwa anamaanisha kwamba anazitafuta roho kumi na tano za ndugu zake ambazo zilipotea ikiwepo na ya kwake pia ambapo ilijulikana kwamba imepotea ndiyo maana ya hizo sarafu kumi na tano. Sarafu ni shilingi yenye thamani kwenye maisha ya mwanadamu kwa sasa maana yake kama ikipotea huenda mtu atakuwa amepoteza tumaini la kuishi tena hivyo maana yake ni kwamba yeye alishapoteza hilo tumaini ndiyo maana anazitafuta. Anacho jaribu kumaanisha hapo ni kwamba anawatafuta wahusika walio ziondoa hizo nafsi za ndugu zake hao kumi na tano. Ni lugha ya mafumbo sana ambayo inamhitaji mtu mwenye akili za ziada sana kuweza kuifumbua" Venance alielezea akiwa anamsifia mtu huyo kwa akili kubwa ambayo alikuwa nayo, ilikuwa ni ngumu sana kuweza kuling'amua jambo hilo kwa uharaka zaidi ndiyo maana walikuwa wengi hapo kwa kusaidiana mawazo hatimaye walifanikiwa kumjua Remy Claude uhalisia wake ulikuwa ni upi.

"Kama gerezani alikuwa amekufuata ni wewe maana yake ni kwamba wewe unahusika kupotea kwa familia yake na wewe tayari ameshakufahamu ila wengine hawajui hivyo alijua kupitia wewe angefanikiwa kuwapata wenzako kwa kumtumia binti yako." Suzane aliongea akiwa anamwangalia Bruno huku anacheka, mzee huyo aliishiwa nguvu kwa sababu kama ni hivyo mwanae alikuwa kwenye hatari kubwa sana kuliko hata mwanzo, kumuelekeza adui yake jinsi ya kumpata mwanae lilikuwa ni jambo la kipuuzi sana kuwahi kulifanya kwenye maisha yake.

"Bruno nataka kujua ni kipi kilitokea hiyo miaka ishirini, ni nani na nani mlihusika kwenye kuiteketeza familia ya Dominic Sawa sawa na kwanini?" mkurugenzi wa usalama wakati huo alikuwa amesimama na kumsogelea mwanaume huyo, ukweli ulikuwa unawekwa wazi taratibu nadhani alianza kuamini kauli maarufu sana inayo sema dunia haina siri hata siku moja huwa ni suala la muda tu.

"Nakuahidi nipo tayari kukwambia kila kitu na kukupa taarifa zote za juu ya nani anahusika na nani alikuwa nyuma ya hili na kila kilicho tokea. Nitakwambia sababu za mimi kwenda gerezani mwenyewe na kwanini rafiki yangu amemteka binti yangu kiasi kwamba nikionekana mtaani mwanangu anauawa ila kabla ya kufanya haya yote naomba msaidie kwanza binti yangu aishi. Naomba muwahi kwa Benard Taradadi kabla mtu huyo hajamfikia maana najua atamlazimisha kumfanya atoe maelezo mwanangu alipo. Nakuomba sana nipo tayari kufanya jambo lolote lile ambalo unalitaka ila nataka nimuone mwanangu kwanza please!" mzee huyo alikuwa amejiweka kwenye mdomo wa mamba mwenyewe huku akiwa anajihisi ndiye mchanga karata bora wa mji kumbe wenzake walikuwa wanamuona boya tu.

Alikuwa tayari kutoa kila taarifa ambayo watu hao wanaihitaji kutoka kwake lakini alihitaji kwanza wamsaidie kumpata binti yake kabla ya Remy mwanaume ambaye alionekana kuwa mbele ya muda sana kwenye upande wa matumizi ya akili kuliko mtu yeyote yule. Mkurugenzi alikuwa na mambo mengi sana ya kuhitaji kumhoji mtu huyo, yaani ndo kwanza walikuwa wanaanza lakini aliomba kwanza binti yake aweze kusaidiwa, watu hao walitakiwa kumuwahi Remy ili waifanye kazi kwa niaba yake maana tayari siri ilikuwa kweupe kabisa.

"Kwa sababu umekubali kufanya ninacho kitaka, nitamsaidia mwanao ila kwa sharti moja tu" mwanamama huyo aliongea huku akiwa anamwinamia mwanaume huyo.
"Raisi akija kukuona usimwambie jambo lolote lile wala kumpa taarifa kwamba tumeweka makubaliano mimi na wewe. kama ukijaribu kunifanyia uhuni Bruno, naapa kwa jina la mama yangu mzazi nitamfanyia mwanao kitu kibaya sana kisha utafuata wewe hapo" aliitikia kwa kichwa akiwa anatia huruma sana. Hakuwa na namna zaidi ya kuwapa address ya mahali anako patikana mmiliki wa benki za TUNAKUWEZESHA ili akawape ramani kwamba ni wapi alipokuwepo mtoto wake wa kike.

31 naweka nukta.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI
Walitoka ndani ya chumba hicho na kumuacha mwanaume huyo pekeyake ili wajue nini cha kukifanya maana walikuwa na muda mchache sana wa kuweza kuikamilisha kazi hiyo.
"Nilijua tu huyu binadamu ana uwezo mkubwa sana ila kuna michezo anaicheza ndiyo maana alijikamatisha kirahisi sana, ila kama nikikutana naye siku ya leo, naenda kuufanya ukatili ambao hata nafsi yangu itaujutia kwenye maisha yangu yote" Kai aliongea kwa jazba sana maana mtu huyo alionekana kucheza sana na akili zao.
"Kai usije ukafanya kosa lolote lile huyu mtu tunamhitaji akiwa mzima kabisa" mkurugenzi aligongelea msumari ili wasije wakafanya makosa.
"Yes, boss" waliitikia kwa pamoja na kuhitaji kutoka ndani humo kwa sababu walikuwa wanatakiwa kwenda muda huo ila bosi wao aliwaita.
"Hii kazi ikikamilika jambo moja la msingi ni kujua maisha ya huyu mtu kwa miaka yote ambayo alipotea. Tujue alikuwa wapi, alikuwa anafanya nini? Kwa sababu saivi tushajua sababu ya yeye kuyafanya haya yote lakini jambo la msingi hii siri inatakiwa kubaki kwenye vifua vyetu nisije nikaisikia sehemu yoyote ile maana sitawasamehe kamwe"
"Sawa maam"

The Holy Tninity walikuwa wanaingia rasmi kumuwahi mwanaume kabla hajampata binti wa Bruno Josephat ambaye wao walimjua kama Remy Claude lakini mpaka wakati huo taarifa ambayo ilikuwepo ni kwamba jina lake halikuwa hilo bali alikuwa anaitwa Ashrafu Dominic Sawa sawa. Kazi ilikuwa ipo kwenye mikono yao, je watawahi kweli, watampata mwanaume huyo na kama wakikutana naye nini kitatokea? Wao ndio walitakiwa kuleta majibu ya hayo maswali.

Usiku huo wakati Holy Trinity wanawapewa kazi ya kwenda kumchukua Benard Taradadi ili awaonyeshe alipo binti wa Bruno Josephat kuna mtu alionekana mitaa ya Kunduchi akiwa na gari kwenye mwendo mkali sana. Gari aliiacha barabarani na kuchepuka mtaani kwa mguu sehumu ambayo walikuwa wanaishi watu wenye ukwasi kidogo wa pesa, hawakuwa na maisha ya Tandale kwa tumbo, uhakika wa kuishi wanavyotaka walikuwa nao.

Mbele ya jengo moja ndipo palikuwa nyumbani kwa Benard Taradadi ambaye ndiye alitakiwa kumpatia ramani nzima ya wapi alitakiwa kwenda ili kumpata mwanamke ambaye alikuwa anamhitaji. Alisimama kwa mbali na kuiangalia kwa umakini sana sehemu hiyo ambayo ilionekana kuwa na ulinzi wa kutosha, alinyata mpaka ulipokuwa ukuta wa jengo hilo, alirudi nyuma kidogo na kugusa ukuta ambapo alijivuta mara mbili tu na kutua juu.

Ilibakia kidogo tu aguse nyaya ya umeme lakini aliwahi kurukia ndani ambapo alitua kwa mguu mmoja huku mkuu mmoja akiwa ameuweka chini kwa goti. Wakati anaruka alipita kwenye mgongo wa mwanaume mmoja ambaye walipishana kidogo sana akiwa anatembea na silaha yake. mwanaume huyo aligeuka haraka sana baada ya kuhisi kama kuna kivuli kilimpitia nyuma yake, hakuona mtu yeyote yule lakini mwanga wa taa ulikuwa umezuiwa kwa chini hivyo akaamua kuinama ndipo aliona kuna mtu chini yake anamwangalia. Aliielekezea silaha yake kwa mtu huyo ili ampige risasi ila alikuwa amechelewa sana kushtuka, Remy alisimama kwa kasi na kuidaka silaha hiyo kwa mkono wa kushoto huku mkono wa kulia akimtwisha nayo mlinzi huyo ngumi iliyo shiba ambayo ilipelekea kukakamaa hapo hapo bila kuongea alipo muachia ilikuwa maiti ya muda mrefu sana.

Alitembea taratibu baada ya kuificha maiti hiyo ukutani, mbele yake aliwaona wanaume wawili wakiwa wanateta kwa sauti ya chini sana, mwanaume alirusha kisu kwa nguvu sana ambacho kilizama kwenye shingo ya mmoja na mwenzake wakati anashangaa kujua kilicho tokea mwanaume aliruka sarakasi za haraka haraka sana alikuja kusimama karibu na mwanaume huyo kisha akamgusa bega lake, alipogeuka vidole viwili vilizama kwenye koromeo na kumtoboa vibaya sana habari yake ikawa imeishia hapo. Alikichomoa kisu chake na kukifuta damu kisha akawa anasonga mbele kuelekea ulipokuwa mlango wa ndani.

Ule mchakacho wa kuwaua watu wale ambao aliwaua uliwaleta wanaume watano ambao walianza kurusha risasi kuelekea kule alipokuwepo, alishtuka baada ya risasi moja kumbaraza kwenye bega lake ikamlazimu kurukia pembeni hukua akiwa anaikoki bastola yake ambayo aliitoa kila alipo achia risasi moja ilikuwa inaenda na maisha ya mtu mpaka alipo bakia mmoja ambaye alimpiga risasi ya goti na kumfanya mwanaume huyo kuachia silaha yake akiwa anagugumia kwa maumivu makali sana.

Ujio wa Remy pale alipokuwepo ulimfanya kuanza kutambaa kuweza kuiwahi bastola yake lakini kabla ya kuifikia aklikanyagwa mguu, alihitaji kupiga kelele kwa maumivu makali ambayo aliyapata ila alipigwa buti kali sana la mdomo ambalo lilimnyanyua na kwenda kujibamiza kiuno chake vibaya ukutani, hakupewa hata nafasi ya kupumua, mwanaume huyo alikuwa amemfikia na kuchuchumaa sehemu ambayo alikuwa ameuegamia ule ukuta wake.
"Bosi wako yuko wapi?"
"Kwani wewe nani?"

"Haina umuhimu wa kunifahamu, nina muda mchache sana wa kuweza kukaa hapa, bosi wako yuko wapi?"
"Yupo ndani"
"Kuna watu wangapi ambao wanamlinda huko ndani?"
"Wawili" baada ya maelezo yake mwanaume alimuwekea bastola mdomoni na kuiachia risasi akawa amepoteza maisha hapo hapo.

Alinyanyuka na kuangalia saa yake ya mkononi, alianza kujongea taratibu kuelekea mlangoni ambapo aligonga na kuiweka bastola yake kiunoni. Kwa ndani zilisikika hatua za mtu zikiwa zinakuja mlangoni, mlango huo ulifunguliwa mtu wa ndani akawa anachungulia kwa nje ambapo alivutwa kwa nguvu na kupigwa kiganja lakini alikikwepa na kuruka juu ambapo aligeuka na sarakasi kali sana lakini alimkosa Remy wakati anatua mguu wake chini alibebwa na mtama ambao ulimfanya abaki anaelea elea hewani. Baada ya hapo alipokea goti na kukanyangwa vibaya sana kichwa kikajipigiza kwenye kuta za mlango kikiwa kinapasuka vibaya. kelele hizo zilimfikia mwenzake ambaye alikuwa ndani hivyo akawa anaita kwa nguvu.

"Hey Marcus" sauti yake haikujibiwa hivyo akaitoa bastola yake na kusogea mlangoni, alishtuka kuona mwili wa mwenzake ukiwa pale chini hivyo alitoka kwa tahadhari mno lakini kuja kwake ni kama alikuwa anasubiriwa kwa sababu wakati anaukaribia mlango huo Remy alipita na mlango ambapo alimzoa mwanaume huyo mpaka sebuleni kwenye masofa.

Alinyanyuka kwa spidi akiwa anageuka na bastola yake ambapo aliachia risasi ambayo iliishia kwenye skrini kubwa ya ukutani, alifanikiwa kumkutanisha Remy na mguu wake ambapo aliyumba. Benard mwenyewe aliamshwa na makelele hayo hivyo akawa atoka na bastola mkononi akiwa amevaa taulo tu pekee, lakini wakati anashuka ngazi kuelekea hapo chini Remy alimuona akiwa anaandaa kuachia risasi.

Wakati huo mlinzi alikuwa anamkimbilia Remy pale alipokuwa, alicho kifanya alimsubiri mlinzi huyo amsogelee alipo kisha akalipiga sofa kwa nguvu sana ambapo lilimvaa mlinzi huyo na kumpotezeshea balansi hivyo aligongana nalo akaruka juu ambapo Remy alimrukia na kumdaka kisha akainyonga shingo yake na wakati huo Benard Taradadi alikuwa anaachia risasi hivyo Remy alimtumia mwanaume huyo kama ngao yake ambapo risasi ziliishia kwenye kifua cha mlinzi huyo.

32 INAFIKA MWISHO.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
Benard alibaki anapiga risasi tu ambazo zilikuwa zimesha isha kutokana na hofu kubwa ambayo alikuwa nayo, akiwa anaendelea na zoezi lake, aliona kisu kinakuja kwenye paja lake akarudi nyuma ngazi moja kikaishia kwenye goti ambapo kilipasua mfupa na kujichomeka hapo. Alipata maumivu makali sana ambayo bila shaka hakuyatarajia, akiwa analalamika na kutukana kwa mtu huyo asiye mjua kumharibia siku yake aliona kivuli kinakuja upande wake baada ya mwanaume huyo kudunda kwenye sofa kisha akatua kwenye ngazi za kupandishia kwenye chumba chake. Kivuli ulikuwa ni mguu ambao ulikuwa unashuka pale mguu wake ulipokuwepo hivyo alijivuta kwa nguvu buti la Remy likawa limetua kwenye ngazi moja ambayo ilimeguka, mguu huo kama ungetua kwenye goti lake basi lingevunjika mithili ya nyama ambazo zilikuwa zimepondwa bondwa buchani.
"Ni nani wewe na kwanini unanifanyia mimi haya?"
"Usinipotezee muda mtoto wa Bruno Josephat yuko wapi?"
"Whaaaat?" mtu huyo alishtuka kama ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwenye maisha yake kuweza kulisikia hilo jina. Remy alitoa bastola yake ambayo haikuwa imetumika, aliachia risasi mbili ambapo moja alilenga kwenye bega la mtu huyo na nyingine aliipenyeza palipokuwa na kisu.

"Sina muda wa kuanza kuimba ngonjera na wewe"
"Wewe ni nani?"
"Unakumbuka mlicho kifanya miaka ishirini iliyopita kwa Dominic Sawa sawa?"
"Unataka kuniambia wewe ni?"
"Nipe taarifa nakoweza kumpata mtoto wa Bruno Josephat haraka sana"
"Mimi sina uwezo wa kuzipata hizo taarifa moja kwa moja lakini kuna mtu ambaye anaweza kukufikisha na kukupa taarifa zote ambazo wewe unazihitaji" Remy alishangaa sana kwa sababu alijua ni moja kwa moja mtu huyo angempa maelezo ya jumla ambayo yangemrahisishia kazi yake ikawa fupi zaidi.
"Unamaanisha nini?"
"Hata mimi viongozi siwajui huwa napewa amri tu kuweza kutekeleza majukumu ambayo napewa"
"Huyo mtu ni nani?"
"Binafsi simjui jina wala sura ila nina mawasiliano yake, huyu ndiye mtu ambaye huwa ananipa maelekezo ya nini natakiwa kukifanya na kukitekeleza kisha na mimi natoa maagizo kwa watu wengine"

"Unafanyaje kazi na mtu ambaye humjui?"
"Kwa sababu ni sehemu ambayo napata malipo makubwa zaidi hata ya miaka yangu yote ambayo ningefanya kazi kwenye taifa hili" alimtajia namba hizo ambazo alidai ndizo zilikuwa za mtu huyo ambaye alitakia kumpa maelekezo yote na mahali ambapo angempatia.
"Wewe sio mwanae na Dominic Sawa sawa, familia nzima ilikufa" alitamka akiwa bado haamini kile ambacho alikuwa anakihisi, Remy alimsogelea mtu huyo na kumtamkia
"MIMI BADO NINAISHI" kisha alimmiminia risasi kwenye kichwa, akakichomoa kisu chake na kutoka humo ndani.

Wakati anatoka, alikuwa amemaliza kazi hivyo hakuwa na wasiwasi kabisa, alikuwa anaziweka silaha zake vizuri ila baada ya kutoka tu mlangoni alisikia kitu ambacho kilimshtua sana, ni jina ambalo aliitwa na mtu ambaye hakuwa amemuona bado kwamba alikuwa wapi.

"Ashrafu" ni sauti nzito ya kiume iliita hilo jina kwa sauti kali sana, ilimlazimu kuuinua uso wake, hilo ni jina ambalo hakuna mwanadamu alikuwa hai alikuwa analifahamu kama ni lake, sasa alishangaa sana mwanadamu mwenye nafsi ya kawaida kulifahamu hilo jina, hata yeye ni habari ambayo ilionekana kumchanganya sana Ashrafu na ndilo lilikuwa jina lake halisi kabisa la kuzaliwa huku dunia ikimjua kama Remy Claude.

Aliuinua uso wake kumwangalia ni nani aliyekuwa anamuita kibabe huyo. Holy Trinity walikuwa wamefika ndani ya hilo eneo wakati mwanaume huyo ndo anatoka baada ya kumaliza kazi ambayo ilikuwa imempeleka ndani ya eneo hilo. Kai ndiye ambaye alilitamka jina hilo kwa msisitizo sana na alikuwa na usongo mkubwa sana na mwanaume huyo ambaye kwa mara ya kwanza wao ndio walifanikisha kukamatwa kwake mpaka akafungwa.

Sura hizo hazikuwa ngeni kabisa kwake mwanaume, aliwahi kukutana nao wakamzidi na kumfikisha kwenye mikono ya sheria ila kuitwa jina lake lilikuwa ni kosa kwa sababu kila anaye lijua jina hilo alikuwa anatakiwa kuuawa haraka sana iwezekanavyo lakini je alikuwa anaweza kuwaua wapelelezi wa hatari sana namna hiyo tena wakiwa kikosi kizima cha watu watano? Ashrafu majibu alikuwa nayo kwenye akili yake na kwenye mikono yake mwenyewe.

POSTA DAR ES SALAAM
Kikao kizito kilikuwa kinaendelea ndani ya ofisi moja kubwa sana ndani ya Posta. Kwenye ghorofa ndefu mno iliyokuwa ipo karibu na maeneo ya bandarini, ukumbi wa mikutano ambao ulikuwa wa kisasa ulikuwa umesheni watu watano ambao walikuwa wameketi huko kwa ajili ya kuyajadili yale ambayo yalikuwa sahihi kwao. Saa saba usiku ndio wakati ambao kikao hicho kilikuwa kinaendeshwa.

WE ARE BROTHER'Z TECH COMPANY
Jengo hilo lilikuwa ni jengo la teknolojia ambalo lilikuwa linamilikiwa na watu hao ambao walikuwa wanajiita brother’z. Wanaume hao watano wote walikuwa wamezificha sura zao kwa mask huku zikiwa zinasikika sauti zao tu pekee.
"Tunaanzaje kikao bila bosi kuwepo?"
"Amenipa maagizo yake tayari hivyo hawezi kufika hapa kwa leo kwa sababu ya majukumu ambayo yapo mbele yake"

"Kwanini hatoi taarifa? Au yeye anajiamulia tu kufanya kile ambacho kinampendeza?"
"Namba yake ya simu nadhani unayo, kama unahisi hayo maswali unayataka majibu yake unaweza ukampigia kumuuliza mwenyewe"

"Hatuna haja ya kuweza kupishana maneno kwa sababu sisi wote ni wamoja, cha mhimu hapa ni kuweza kujua namna ya kulitatua tatizo lililopo mbele yetu. Hili jambo ambalo limevujishwa kuhusu historia ya maisha ya Dominic Sawa sawa tusipokuwa makini linaweza kutuvua nguo wote hivyo tunatakiwa kulishughulikia haraka sana"

"Kwani vijana bado hawajampata mtu huyo?"

33 inafika mwisho.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA THELATHINI NA NNE
"Ni ngumu sana kwa sababu hata yeye anaonekana kujua kile ambacho anakifanya ila ni mtu ambaye anatakiwa kupatikana mapema kabla hili jambo halijafika mbali kwa sababu tutaishia pabaya sana"
"Hilo swala naona ni dogo sana, watafutwe vijana makini kama hawapo basi waagizwe vijana kutoka nje waje kuifanya kazi hiyo. Sijajua kwanini mnapoteza muda sana kiasi hiki"

"Unavyo ongea kiwepesi utadhani unaenda ni kumnywesha mtoto uji, wengine huwa mnakuwa mabingwa wa kuongea tu ila ukipewa hiyo kazi utaitekeleza kirahisi kama unavyosema? Usichukulie kirahisi sana mtu kujiamini mpaka kumtaka raisi wa nchi akapige magoti hadharani kumuomba msamaha, ni lazima ametumia muda mrefu sana kuweza kujipanga na anacho kifanya anakijua hivyo tukifanya mambo kwa mihemko inaweza ikala kwetu"

"Kwahiyo unataka tufanyaje labda?"
"Cha kwanza tunatakiwa kujua uhusiano uliopo kati ya huyu mtu ambaye alitoa hii taarifa pamoja na yule bwana mdogo ambaye yupo jela"
"Unahisi kwamba kuna mahusiano yoyote yale?"

"Inawezekana maana sababu ya haya yote inaonekana ilianzia baada ya yeye kukamatwa na sijui kwamba ni kwanini stori yake inahusishwa na Dominic"
"Tuwe makini sana kwenye hii kesi ya Dominic, hii kesi haitakiwi kuwa hai wala kurudi tena kwenye midomo ya watu kwa sababu itatumaliza wote. Kwa mtu yeyote yule ambaye atahitaji kuiweka kwenye mdomo wake basi tutakiwa kumuwahisha haraka sana sehemu ambayo anatakiwa kwenda kujifunza namna ya kuutumia mdomo wake vizuri"

"Kwamba inawezekana stori ya miaka ishirini irudi leo kirahisi tu hivi? huenda tuna msaliti miongoni mwetu"
"Bruno yuko wapi?"
"Nasikia alipotea ila kuna taarifa zinadai yupo gerezani"

"Whaaaat?"
"Inadaiwa hivyo ila kwa sababu tulimuweka nje ya mambo yetu kwa sasa nasikia amejificha gerezani"
"Amejificha kwa sababu zipi?"
"Bado haijulikani"
"Inatakiwa waandaliwe watu waanze kulifuatilia hili jambo na familia yake kujua ni kipi ambacho kinaendelea. Haya yote huenda yana uhusiano wa moja kwa moja na yanayo tokea na kama kuna jambo lolote likigundulika basi anatakiwa kuuawa haraka sana kwa sababu kinaweza kuwa kirusi ambacho kitatutesa sana hapo baadae"

"Sawa kiongozi nafikiri hilo litafanyiwa kazi haraka sana" wanaume hao walikuwa na mazungumzo mafupi kidogo juu ya usalama wao. Mazungumzo yalikuwa yameisha hivyo walihihitaji kutoweka humo ndani lakini kwa bahati mbaya sana kabla hawajafanya maamuzi ya kuweza kutoka eneo hilo, aliingia mlinzi akiwa anakimbia wakati huo ilikuwa imetimu saa nane usiku tayari.

Wote waligeuka kumuangalia kujua sababu ambayo ilimleta wakati huo, alimfuata yule ambaye alikuwa anaongoza kikao hicho ambaye alionekana kuwa mkubwa kuliko wenzake wote na kumnong'oneza kisha akampa simu ili aweze kujionea kilichokuwa kinaendelea.

Kwenye hiyo simu ilikuwa ni habari iliyokuwa inaeleza kuhusu kutoroka kwa Remy Claude gerezani, habari hiyo hata wao ilikuwa ngeni kwao. Wenzake walikuwa wanamuangalia kujua ni nini kilikuwa kinaendelea lakini alicho kifanya ni kuwapa ishara ya kufungua simu zao ili wapate kujionea wao wenyewe.

"F**K, huyu ni mtu mmoja au ni mtu mwingine"
"Lazima ni mtu mmoja ila kaamua kutumia njia tofauti tu za kuweza kuiwasilisha taarifa yake"
"Inawezekanaje mtu kutoroka ndani ya lile gereza au anacheza na akili zetu?"
"Huyu mtu kwa sasa amejipatia umaarufu sana hivyo ni ngumu sana kutoa habari ya uongo, ni lazima habari hizi zitakuwa na ukweli kwa asilimia nyingi na hili jambo kama kalizungumzia basi litakuwepo"

"Huyu aliye toroka ni nani hasa ambaye nilisikia alikuwa anamiliki magenge ya kihalifu?"
"Bado hatuna taarifa zake maana hakuwa mtu ambaye anatuhusu ila kwa sasa nadhani kuna umuhimu mkubwa sana wa kumchunguza na kumfahamu kwa undani tujue ana uhusiano gani na maisha ya Dominic"

"Miaka ishirini imepita tangu Dominic afe, sasa huu mkanganyiko unakuja vipi kutokea wakati huu? kwamba huenda kuna uhusiano baina ya huyu mtu na Dominic?"
"Hilo ni swali ambalo hakuna mtu anaweza kukujibu kwa sasa mpaka tupate uhakika kwanza, ngoja nimpigie mkuu wa lile gereza ili atupatie taarifa zilizo kamili juu ya mtu huyu na kama ni kweli ametoweka huko gerezani" aliitoa simu yake na kuitafuta namba ambayo alihitaji kuipigia wakati huo, alipiga namba hiyo lakini haikuwa ikipatikana kabisa, aliipiga tena ikawa ni vile vile haipatikani.

Kidogo ilianza kumpa wasiwasi maana haikuwa kawaida namba hiyo kupiga halafu isipatikane.
"Kutakuwa kuna jambo la hatari ambalo sio zuri sana kwetu, huyu mtu haijawahi kutokea hata siku moja akakosekana hewani, hii ni ishara mbaya"
"Mpigie bosi ili tujue tunafanyaje"
"Mhhhhhh huwa anachukia sana kupigiwa simu usiku wa manane kama huu"

"Hakuna namna hili jambo tunavyo endelea kulichukulia kirahisi ndivyo madhara yake yanazidi kuwa makubwa" mwanaume huyo hakuwa na maneno tena zaidi ya kuinyanyua simu yake ambayo ilikuwa mezani na kumpigia huyo ambaye walikuwa wanamuita bosi wao. Simu hiyo iliita kwa muda mfupi sana ikawa imepokelewa upande wa pili.
"Samahani kwa kukusumbua na usiku huu bosi, kuna tatizo limetokea ambapo mtu ambaye bila shaka ni mmoja ila leo hajatumia gazeti amechapisha taarifa juu ya Remy kutoroka gerezani hivyo tunasubiri amri yako utuambie nini cha kukifanya"
"Sawa bosi" maelezo yalikuwa ni mafupi mno kisha simu ikakatwa.
"Amesema kwa leo tukalale kisha akituhitaji atatuita, kesho hili jambo anaanza kulishughulikia mwenyewe" wote waliangaliana tu kisha kila mtu akanyanyuka kimya kimya na kutoweka eneo hilo.

Penzi la raisi na Anelia Baton lilikuwa ni tamu kiasi kwamba waliutumia muda mrefu sana wakiwa kitandani pamoja kujiburudisha. Raha walizopeana ziliwafanya wachoke sana hivyo wote walipitiwa na usingizi mkali mno. Usiku wa manane sana mheshimiwa aliamka na kwenda kuoga kisha akavaa nguo safi na kusogea pale kitandani ambapo Anelia alikuwa uchi kama alivyo zaliwa, alimwangalia mwanamke huyo hususani sehemu zake za siri akiwa anatabasamu maana alimfaidi sana kisha akatoka humo ndani na kuondoka kabisa hilo eneo.

34 inafika mwisho.
 
Back
Top Bottom