Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA TATU
Aina ya sehemu ambazo walikuwa wanapita ndizo zilimpa taarifa kwamba alikuwa amewekwa kwenye chumba cha mbali sana na wenzake. Njiani alikuwa anakutana na vyumba vingine ambavyo vilikuwa wazi huku vikiwa kwenye hali mbaya sana ambayo kiuhalisia hakutakiwa binadamu yeyote yule kuishi ndani ya vyumba hivyo. Dakika tano zilitosha kabisa kuwafikisha sehemu ambayo walitokezea kwenye uwazi, uwazi huo ulikuwa ni tofauti kabisa na sehemu ambayo yeye alikuwa amepelekwa mara ya kwanza na hapo ndipo akagundua kwamba haikuwa usiku kama alivyokuwa akihisi yeye bali ilikuwa ni mapema tu wakati kunakucha huku upepo ukiwa unapiga kwa mbali.

Kwenye uwanja huo ambao ulikuwa mkubwa kiasi cha kutosha watu hata elfu moja lakini watu ambao walikuwa hapo kwa hesabu za haraka haraka walikuwa ni watu kama miamoja tu pekee na wote walikuwa ni wafungwa. Pembeni kabisa mwa uwanja huo kulikuwa na wanajeshi wengi mno, hapo ndipo alielewa kwamba sehemu hiyo ilikuwa inalindwa sana tofauti na mawazo yake yalivyokuwa mwanzo. Katikati ya uwanja huo kulikuwa na sehemu ambayo ilikuwa imevia kwa damu ambayo ilifikia hatua damu ikawa imeganda sehemu hiyo huku kwa mbele yake kidogo kukiwa na jukwaa ambalo lilijengwa kwa zege na katikati yake kulikuwa na vyuma viwili ambavyo viliunganishwa na mashine ya kunyongea watu katikati ya jukwaa hilo kukiwa na kamba ngumu sana. Hakuhitaji maelezo mengi kuweza kuelewa kwamba sehemu hiyo ilikuwa inatumika kwa ajili ya kufanyia mauaji na kunyongea wafungwa ambao walikuwa wanastahili au wanatakiwa kuipokea adhabu hiyo.

Akiwa amesimama pekeyake sehemu ambayo kila mfungwa aligeuka kumuangalia huku asimuone yule mzee ambaye alimuona kwa mara ya kwanza, alishangaa kuna mwanaume amebebwa mpera mpera na kufikishwa sehemu ile ambayo ilikuwa na damu nyingi. Mwanaume huyo alikuwa anaomba sana aweze kuonewa huruma lakini hiyo nafasi nani angempa wakati ulimwengu kwa wakati huo ulimkataa? Ilikuwa ni yeye na Mungu wake tu hakuwa na namna ya kuweza kufanya.

Lahaula! Baada ya kumwangalia kwa umakini, alimkumbuka vyema, alikuwa ni moja kati ya watu ambao walikuwepo kwenye chumba ambacho alihifadhiwa baada tu ya kufikishwa ndani ya gereza hilo. Ni mmoja kati ya wale ambao afya zao hazikuwa mbaya sana bado walikuwa kwenye ubora wao. Hakujua kwamba mwanaume huyo alikuwa amefanya kosa gani haswa mpaka kufikia hatua ya kwenda kuuawa lakini kitu pekee ambacho kilimchukua umakini zaidi ni kwa namna mwanaume huyo alivyokuwa anaomba aweze kupewa nafasi ya kuishi huku kwenye shingo yake akiwa amefungwa chuma ambapo alilazwa shingo yake kwenge gogo moja kubwa ambalo ndilo lilikuwa linatumika kutolea adhabu. Alisikia mburuzo wa shoka upande mwingine kutoka kwa mtu ambaye bila shaka alionekana kuwa amechoka sana hata kuibeba shoka yenyewe ambayo ilikuwa kwenye mkono wake ilikuwa ni shida.

Baada ya kugeukia upande huo, alishangaa tena kumuona mwanaume mwingine wa chumba kile kile ambacho yule aliyetakiwa kuuawa alikuwa anatokea lakini utofauti wao ni kwamba huyo aliyekuwa na shoka mkononi alikuwa ni miongoni mwa wale ambao walikuwa wamekondeana sana. Mwanaume huyo baada ya kufika pale hakuuliza mara mbili alilibeba shoka lake na kulishusha kwa taabu sana kwenye shingo ya mwenzake hali ambayo ilimfanya Remy ajikute anatoa sauti bila kutarajia;

"Noooooooooooooo" ilikuwa ni sauti kali sana ambayo ilimshtua kila mtu hata yule ambaye alimuua mwenzake alijikuta anaanza kulia huku akiwa anatetemeka hata shoka lenyewe liliweza kumponyoka kwenye mkono wake.

Sauti yake kali ndiyo iliwaibua baadhi ya watu na hapo ndipo aligundua kwamba gereza hilo halikuwa na watu kama mia tu ambao aliwaona pale bali wale walikuwa ni baadhi tu ya watu ambao walikuwa humo ndani. Wanaume wenye miili iliyoshiba kama watano walitokezea kwenye uchochoro mmoja ambao ulikuwa unatokezea kwenye huo uwanja huku wakawa wanamsogelea pale ambapo alikuwepo.

"We malaya, mtoto wa kiume unapiga piga makelele kama wasanii wa taarabu unahisi kuna mama yako wa kuanza kumdekea huku sio? Unatupigiaje makelele wanaume ambao tunaendelea na mambo yetu?" mwanaume huyo ambaye alikuwa na mbavu za kutosha aliongea huku akiwa anachomoa kisu chake na kumkimbilia mwanaume huyo ili amchome na kisu hicho ila lilitokea jambo la ajabu sana ambalo lilimfanya kila mtu sehemu hiyo abaki anashangaa;

mwanaume huyo hakuona upinzani wowote kutokana na jinsi mhusika alivyokuwa amefungwa minyororo mpaka shingoni hivyo aliurusha mkono wake wenye kisu kuelekea tumboni ambapo alikuwa na imani kwamba ungefika lakini wakati kisu hicho kinakaribia kufika Remy alijisogeza nyuma hatua ndogo sana kisha aliinyoosha mikono yake yote miwili ambayo iliunganishwa kwa pamoja na kuudaka mkono wa mwanaume huyo ambao aliubana na minyororo mpaka kisu kikamponyoka. Alipiga makelele wakati huo mkono uligeuzwa kwa nguvu na minyororo ambayo ilikuwa imemkaba akakosa balansi akajikuta anadondokea mwilini mwa mwanaume huyo. Licha ya kuwa mbavu ila alidondokea vibaya kwani Remy aliirushia minyororo yake upande wa mbele na kumkaba mwanaume huyo shingoni, alianza kufurukuta wakati huo wanajeshi walikuwa wanakimbilia hilo eneo kuweza kuwahi kumuokoa mwanaume huyo lakini wakati wanafika ndio wakati ambao shingo ya mwanaume huyo ilikuwa inavunjwa vibaya.

Wakati wanajeshi wanaanza kumpiga na virungu vya chuma alimwachia mwanaume huyo chini akiwa tayari ni marehemu. Mwanajeshi mmoja baada ya kumkagua mtu huyo alitoa taarifa kwamba amekufa tayari hali ambayo iliwafanya wamshambulie Remy kwa virungu na mabuti mengi sana kisha askari mmoja akasimama mbele ya wote na kutamka

"Yule pale ni muuaji wa kutisha sana hivyo kwa namna yoyote ile hamtakiwi kumsogelea wala kuchangamana naye maana kama mkifanya hivyo kitawakuta kama kilicho mkuta mwenzenu, kila mtu arudi kwenye chumba chake" ilikuwa ni amri ya kijeshi hivyo hakuna ambaye alikuwa anaweza kuhoji wala kuuliza jambo lolote lile wakatawanyika huku wanajeshi hao wakimchukua Remy na kuondoka naye tofauti na ilivyokuwa kwa watu wengine.

Lakini wakati mambo yote hayo yanatokea kuna mwanaume mmoja ambaye naye alikuwa ni mfungwa na alionekana kuwa mgeni kabisa ndani ya eneo hilo. Mwanaume huyo alikuwa makini sana kufuatilia kila jambo ambalo lilikuwa limefanyika pale huku akionekana kuweka zaidi umakini kwa Remy kisha naye akajichanganya kwa wafungwa wengine na kutoweka hiyo sehemu.

UKWELI WANGU WA SIKU.
Lilikuwa ndilo gazeti maarufu ndani ya nchi ya Tanzania ambalo lilipendwa sana na wananchi kwa sababu ya kutoa habari ambazo watu wengi hawakuwa wakizipata kirahisi. Ni gazeti ambalo hata mmiliki wake hakuwa anajulikana ila lilikuwa linaonekana tu sokoni na ndilo lilikuwa linaongoza kwa mauzo zaidi ndani ya nchi.

Baada ya sekeseke la kukamatwa kwa mtu ambaye alidaiwa kuongoza moja kati ya magenge ya kihalifu, mtu ambaye hata picha yake haikuwa wazi kabisa kwa sababu hata picha ambazo serikali ilizitumia kutoa taarifa hizo zilikuwa zimewekewa vivuli ili kutoweka taharuki kwa wananchi, gazeti hilo halikuwa limetoa taarifa yoyote mpaka mtuhumiwa anahamishwa kutoka jela moja na kupelekewa ndani ya gereza la Dominic. Lakini siku ya pili yake tu tangu mtu huyo apelekwe ndani ya gereza hilo, gazeli la UKWELI WANGU WA SIKU lilitoa taarifa ambayo aliwashtua watu wengi sana hata viongozi wakubwa ndani ya nchi.

13 naweka kalamu pembeni.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA NNE
"KWELI ILIYO FICHWA"
Ndicho kilikuwa kichwa cha habari cha taarifa hiyo ambayo ilileta mkanganyiko mkubwa sana. Gazeti hilo lilitoa taarifa kwamba viongozi wengi wa kisiasa pamoja na vyombo vya usalama hawakuijua kazi yao na wengi walitakiwa kutoka kwenye nafasi zao kabla hawajachelewa kwani kuendelea kukaa sehemu hizo walikuwa wanaendelea kuibomoa nchi na muda mfupi ujao huenda hali ingekuja kuwa ya tofauti sana nje na matarajio yao yalivyokuwa.

Gazeti hilo lilieleza kwamba siku kadhaa nyuma kuna tukio lilitokea la kukamatwa kwa kiongozi mkubwa sana wa genge la kihalifu la SARAFU KUMI NA TANO na kuhukumiwa miaka sitini gerezani lakini walishindwa kujiuliza maswali kadhaa kuhusu uhalisia wa mtu huyo kwamba ni nani haswa na historia yake ni ipi mpaka akaishia hapo. Kushindwa kwao kujua hilo kulikuwa kunaenda kuleta matatizo makubwa sana kwenye nchi. Gazeti hilo lilielezea kwamba ili kukwepa mambo hayo ambayo huenda yangeenda kutokea siku za mbeleni basi watu hao walitakiwa kuichimbua historia ya miaka ishirini ambayo ilipita kuhusu mtu mmoja ambaye alikuwa anaitwa DOMINIC SAWASAWA na baada ya kupata majibu na uhalisia juu ya tajiri huyo ambaye alikuja kuuawa na mali zake zikataifishwa basi raisi wa nchi alitakiwa kujitokeza hadharani na kupiga magoti kisha aombe msamaha kwa wahusika ambao bado walikuwa wanaishi na hiyo ndiyo njia pekee ambayo ingewafanya baadhi ya watu wasife au kuokoa umwagaji damu ambao ulikuwa ni lazima tu utokee.

Gazeti hilo lilieleza kwa undani kwamba viongozi wengi walikuwa wanaujua ukweli huo na hata baadhi ya viongozi wa vyombo vya usalama ila waliamua kuufukia na kuamua kuulaghai umma. Watu hao waliamini kwamba historia ya mtu huyo tayari imekufa lakini haikuwa kweli kwa sababu mtu huyo kufa kwake ulikuwa ni mwanzo wa maisha mengine.

Gazeti hilo lilisisitiza sana kwamba watu wote ambao walikuwepo kwenye mpango huo hususani wanasiasa wakubwa na viongozi wa ulinzi na usalama walitakiwa kuziachia nafasi zao na kuomba msamaha hadharani huku raisi mwenyewe akitakiwa kupiga goti na kuomba msamaha maana licha ya familia hiyo kudaiwa kwamba yote ilifutwa duniani lakini ukweli ni kwamba mtoto wa Dominic Sawasawa alikuwa hai bado anaishi na kwa wakati huo alikuwa ni mtu mzima kabisa baada ya kupotea kwa kipindi kirefu sana cha zaidi ya miaka ishirini na sasa alikuwa amerudi rasmi.

Ilikuwa ni habari mbaya sana ambayo ilianza kusambaa kwenye vyombo vya habari hususani kwenye mitandao ya kijamii. Habari hiyo ulikuwa ni udhalilishaji mkubwa sana kwa mheshimiwa raisi wa nchi ya Tanzania na taasisi yake nyeti zaidi ya nchi ambayo ni Ikulu lakini pia ulikuwa ni udhalilishaji mkubwa kwa idara zote na taasisi zote za ulinzi na usalama pamoja na viongozi wote wa serikali kwa ujumla kwa sababu walionekana kwamba hawakuwa wakijua majukumu yao na walikuwa ni watu ambao walikuwa wanatetea mambo mabaya kuendelea kutokea nchini.

Kutokana na gazeti hilo kupendwa sana na wananchi ilipelekea habari hiyo kusambaa nchi nzima kwa muda mfupi hali ambayo ilianza kuzalisha minong'ono mingi miongoni mwa wananchi huku wengine wakidai kwamba huenda kuna uhuni mwingi sana ambao ulikuwa unafanywa na viongozi wakubwa serikalini na wananchi walikuwa wanaonewa tu usikute hata huyo mfungwa alionewa wala hakuwa anahusika kwa lolote lile.

Licha ya serikali kujaribu kwa siku nyingi sana kumtafuta mmiliki wa gazeti hilo bila jitihada hawakuona kama kulikuwa na haja naye sana maana huko nyuma gazeti hilo lilikuwa linasambaza habari zenye mkanganyiko lakini hazikuwa na utata mkubwa kiasi hicho. Ila kwa wakati huo lilivuka mipaka ya uhuru na ilikuwa lazima wahusika watafutwe haraka sana na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.


DOWNTOWN KARIAKOO.
Ndani ya chumba kikubwa ambacho kilikuwa kimesheheni mitambo mbali mbali, alikuwepo Robert na Hezironi. Wawili hao walikuwa wamekaa humo ndani kwa muda mrefu sana na ndio ambao walikuwa nyuma ya kila kitu kuhusu gazeti hilo ambalo mmiliki wake alikuwa ni Robert.

Mwanaume huyo alianzisha gazeti hilo siku tu ambayo alifanikiwa kuishi na kushindwa kumuokoa bosi wake pamoja na familia yake na Hezironi ndiye ambaye alikuwa anadili na mambo ya kuandaa habari zote ambazo zilikuwa zinatolewa na gazeti hilo.

Robert alifanya jambo hilo ikiwa ni kama kutaka kujipa uhakika wa lile jambo ambalo alikuwa analiwaza akilini mwake kuhusu Remy Claude. Aliwasisitizia watu wake kwamba alikuwa na imani kwamba huyo alikuwa ni mtoto wa bosi wake lakini kwenye nafsi yake bado hakuwa na uhakika sana juu ya jambo hilo na kwa kufanya hilo ungekuwa ni mwanzo wake mzuri wa kuwa na uhakika zaidi kwani taarifa ambayo waliitoa ilikuwa inaleta kelele nyingi sana kwenye vyombo vya habari na huenda kupitia hilo ukweli ungeanza kujulikana kisha hapo ndipo angeingia na na watu wake mtaani kuhakikisha wanalifanyia kazi jambo hilo, moyo wake ulikuwa unamuenda mbio akiwa anatamani kuhakikisha anampata kijana huyo na kukutana naye ana kwa ana jambo ambalo alijua kabisa kwamba lilikuwa nin hatari na hata kuwezekana kwake kulikuwa na asilimia ndogo.

"Kwa sasa tunatakiwa kuwa makini sana kwa sababu tutakuwa tunatafutwa na nchi nzima kuanzia watu wa usalama lakini hata jeshi la polisi na kama tukikamatwa basi hakuna mtu atakuja kujua kwamba tuliwahi kuwepo hapa duniani" Robert aliongea huku akiwa anafunua funua kurasa za mitandao ya kijamii kushuhudia namna gazeti lake lilivyokuwa limepata nafasi kubwa ya kuziteka nyoyo za watu.

"Bosi kwanini unafanya haya kwa kitu ambacho unaonekana hauna uhakika nacho? huoni kama utakuwa unaleta hatari kwa watu ambao hawana hatia? kwa sasa kuna watu wataanza kukamatwa na kuhojiwa kwa kuhisiwa, kuna vijana wanaweza kupoteza ajira na kuishia kufungwa lakini hayo yatapelekea watu baadhi kufa na huenda hata mtaani hali haitakuwa nzuri sana kwa sababu jambo hili limefanyika. Sasa kwanini umeamua iwe hivi?"

"Hezroni kwenye maisha yako umewahi kuhusika kwenye kifo cha mtu ambaye hana hatia na ukawa hauna cha kufanya?"
"Hapana"
"Huwezi kunielewa kijana wangu. Mimi nilishindwa kuisaidia familia ambayo niliapa kuilinda mbele ya macho yangu. Walikufa nikiwa nawaona wakati huo mimi ndiye nilikuwa mlinzi mkuu wa familia halafu leo nakuja kujua kwamba mtoto ambaye niliapa kuyatoa maisha yangu kwa ajili yake yupo hai. Unaweza ukakaa kwenye nafasi yangu labda ukaniambia kwamba ungefanya nini huku watu ambao walitakiwa kuifanya kazi hii wameamua kukaa kimya na mbali wakati mtu huyo wa maisha yake hapo zamani alikuwa ni msaada mkubwa sana kwa serikali? Siwezi kuacha jambo hili lipite au liende kirahisi kama wanavyotaka wao"

"Kumbuka wale wana mitambo mikubwa ya ulinzi kuliko sisi, nina wasiwasi kwamba ipo siku watakuja kutufahamu na kutukamata, baada ya hapo unahisi nini kitatokea? tunaweza kupoteza maisha kabla ya kufika hata nusu ya safari yetu ambayo tumeianza, nadhani moja kati ya makosa makubwa ambayo tumeyafanya ni hili, hili jambo ilitakiwa tulifanye kimya kimya na wangekuja kushtuka wakati wamesha chelewa ila kwa sasa ni kama umewaamsha usingizini hivyo watakuwa wanayafanya mambo yao kwa umakini sana"

14 nakaa pembeni.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA TANO
"Mimi nakuamini sana wewe kwenye habari ya mitandao, haitajalisha kwamba wana watu wa namna gani lakini hawawezi kutukamata kirahisi hivyo na sitaruhusu jambo hilo liweze kutokea wala kufanyika na kama siku wakija kufanikiwa kunikamata basi nitakuwa nimeikamilisha kazi ambayo naishi kwa ajili ya kuifanya maana nafsi yangu ni kama tayari ilishakufa kwa muda mrefu. Nilicho kifanya kina umuhimu mkubwa kuliko kama nisingekifanya kwa sababu kwa sasa hawatakuwa watu ambao watakuwa na amani bali wao ndio wataanza kuishi kwa papara sana na huenda watatafuta mtu wa kumtupia mzigo ili aonekane yeye ndiye mbaya na hapo ndipo sisi tutaanzia kazi yetu ya kunyooka nao.

Asili inaeleza kwamba mtu akiwa kwenye presha kubwa huwa anafanya makosa mengi tofauti na mtu akili yake ikiwa imetulia. Kwa sasa wale wapo kwenye presha hivyo hata maamuzi ambayo watayafanya mengi yatakuwa ya presha kubwa sasa hapo ndipo ambapo sisi tutautumia huo mwanya kuweza kudili na makosa ambayo wao watakuwa wanayafanya na makosa hayo ndilo tundu ambalo sisi tutakuwa tunalitumia kukamilisha hii kazi. Lengo la haya yote nahitaji kukutana naye ili niwe na uhakika wa asilimia miamoja kwamba ni yeye kweli"

"Yupo gerezani sasa unahisi utakutana naye vipi?"
"Hii ndiyo kazi ambayo ipo mbele yetu, sina uhakika wa namna ya kukutana naye kwa sababu ya sheria za lile gereza haliruhusu mtu yeyote wa nje kwenda kusalimia mfungwa, ukiingia kule unakuwa umeenda dunia nyingine kabisa hivyo nitatafuta namna nzuri ya kuweza kufika kule"
"Unataka kwenda gerezani?"
"Ndiyo"
"Bosi umeanza kuumwa ugonjwa wa akili sio? Unataka kwenda kule, hapana nahisi hauko sawa, ile ni sehemu ambayo ukiingia hauwezi kuja kutoka tena sasa kwanini unataka kufanya hivyo na unajua wote tunakutegemea?"

"Siku zote kwenye maisha wale ambao wanachagua njia ngumu zaidi kwenye kufanya mambo yao ndio ambao huwa pia wanapata mafanikio makubwa zaidi. Kwahiyo ni wewe unachagua, upite na njia rahisi huku mafanikio yako yakiwa kidogo au upite kwenye njia ngumu ambayo ukifanikiwa unakuwa umepiga hatua kubwa. Sina namna nahisi hii huenda ndiyo njia pekee ya kufanya hivyo"
"Unahisi utaingiaje kule?"

"Hapo ndipo ilipo kazi yako sasa, tafuta namna ya kuingilia ulinzi wa lile gereza. Huenda ni ngumu ila nina imani unaweza kulifanya hili jambo kwa ukubwa zaidi, hata kama ni gereza ambalo wanaishi maisha magumu lakini najua kwamba ni lazima kuna magari huwa yanaenda kwa ajili ya kutoa taka, kuna magari ya kwenda kupeleka chakula kule kikiisha, lazima huwa kuna shift za walinzi wa ile sehemu, lazima huwa kuna mafundi ambao huwa wanaenda ile sehemu hivyo kazi yako kubwa ni kuweza kujua hayo yote na ratiba yao nzima kisha turudi tena mezani kuweza kuelewa kwamba ni kitu gani tunaweza kukifanya na siku ambayo ulinzi hautakuwa mkubwa na kutakuwa na mwanya wa kuingia sehemu hiyo basi natakiwa kuingia haraka nadhani inaweza kuwa njia yangu rahisi zaidi kufika huko lakini jitahidi sana tuweze kuipata na ramani ya gereza lenyewe"

Hakuwa tayari kuweza kumsikiliza Hezroni mwanaume huyo, ilikuwa ni lazima kulifanya jambo hilo kwa nguvu zote. Hezroni alikosa cha kuongea kwa sababu alipewa maelezo ambayo binafsi alikuwa na wasiwasi nayo lakini aliyekuwa ameongea alikuwa ni bosi wake na asingekuwa na huo uwezo wa kuweza kumpinga kwa namna yoyote ile.
"Sawa nitaifanya hiyo kazi lakini hili halitakuwa ndani ya uwezo wangu pekee, timu nzima inatakuwa kuja hapa na kwenye hili nitasaidiana na Nicole kwa ajili ya ulinzi zaidi, hii kazi ya kudukua taarifa nyeti za namna hiyo ni ya hatari sana hivyo nitamhitaji sana"
"Ok, kesho watakuwepo wote hapa" mazungumzo yao yalikuwa yamefikia mwisho na kilicho takiwa kufuata wakati huo ilikuwa ni utekelezaji tu.





*****************
Kosa kubwa ambalo alilifanya Remy la kumuua mfungwa mwenzake lilimletea mabalaa mazito. Baada ya kutolewa ndani ya lile eneo alipelekwa sehemu moja ambayo ilikuwa na matenki makubwa ya maji ambayo yalikuwa yapo wazi, akiwa anasubiri kuona kitu ambacho kingemkuta hapo, alimuona mkuu wa gereza hilo akiwa anakuja na baadhi ya wanajeshi ambao hata sare zao zilikuwa ni tofauti na wenzao bila shaka walikuwa ni wakubwa kuliko wengi ambao aliokuwa amewaona ndani ya gereza hilo.

Baada ya kufika hapo alipokuwepo, mwanaume mmoja alimnasa kibao kikali cha sikioni mpaka sikio likawa linatoa sauti kama vitu vinagongana.
"Bwana mdogo unahisi hapa tupo kwa ajili ya kukupa burudani sisi sio? Au unahisi hapa ni huko mtaani ambako ulikuwa unawatumikisha watoto wadogo na wanawake kwa namna ulivyo muoga kwa wanaume wenzako? niamini mimi leo utakutana na jambo gumu kwenye maisha yako" ilikuwa ni sauti ya mkuu wa gereza ambaye alimsogelea na kumpiga ngumi kali ya tumbo akiwa amefura kwa hasira.

"Mteseni huyu mjinga mpaka amkumbuke bibi mzaa bibi yake ila msimuue kisha mtamhamishia kwa wanaume wenzake kule ila akae kwenye kile chumba kilicho salitiwa" aliongea kwa jazba na kutoweka ndani ya eneo hilo. Wanaume hao walimbeba na kumsogeza karibu na kwenye tenki moja la maji wakamkalisha kwenye kiti na kumfunga vizuri.

Hakuwa ameangalia ila baada ya muda aligundua kamba kiti hicho kilikuwa kimeunganishwa na nyaya za umeme. Mwanaume mmoja alichota maji ya kwenye tenki na kummwagia mwilini, alihisi mwili unaganda kwa namna maji hayo yalivyokuwa ya baridi. Akiwa kwenye taharuki hiyo kubwa wanaume hao walianza kumpiga shoti za mwili, mwanaume alitamani hata kulia lakini kutoa machozi kipuuzi haikuwa tamadunia yake hivyo aliishia kupiga makelele sana mpaka udenda ukawa unamtoka mdomoni.

Alijihisi kuchoka sana Remy ila watu hao hawakuwa na mpango naye kama sio kujifanya hawaoni ile hali ambayo alikuwa anaipitia. Baada ya kuyapokea hayo mateso kwa muda walimbeba na kumtupia kwenye tenki hilo ambalo maji yake yalikuwa ya baridi isivyokuwa kawaida. Alizama mpaka chini hali ambayo ilimfanya ahisi anaenda kufa kizembe kabisa hivyo alijikongoja japo hakuwa na nguvu mwilini mpaka akafanikiwa kusimama akiwa na minyororo yake mwilini bado.

Baada ya kusimama kwenye maji hayo, yalikuwa yanamfika shingoni sasa adhabu akawa ameielewa kwamba kama alitaka kuishi basi alitakiwa kusimama mpaka pale ambapo wangekuja kumtoa wenyewe kwani maji kumfika shingoni ina maana kwamba kama angeinama kidodo tu basi ni lazima angezama. Licha ya kulielewa somo vizuri lakini haikuwa sababu ya yeye kupona kwa baridi kali ambalo alikuwa analipata kwenye hayo maji ambapo alijihisi kwamba alikuwa anaenda kuganda.

Alifanikiwa kuyamaliza masaa sita na hapo ndipo akaja kutolewa akiwa kwenye hali mbaya sana mwanaume huyo. Alikuwa anahema kwa nguvu na kila alipohema alikuwa anatoa mvuke ambao ulikuwa wa baridi ungehisi kwamba alikuwa anaishi kwenye nchi zenye baridi kali sana.
"Wewe si kidume? Ngoja tukupeleke kwa wanaume wenzio ukawaletee huo utemi" aliongea mwanajeshi mmoja akiwa anamzoa na mwenzake kama mzoga kisha wakawa wanaelekea ndani ya vyumba vya gereza hilo ambapo walishuka ngazi kuelekea chini ambako kulionekana kuwa na vyumba vingine tofauti na vile vya mwanzo ambavyo vilikuwa juu. Hapo Remy aligundua kwamba kuna watu wengine walikuwa wanaishi chini kabisa ya gereza hilo.

15 niseme bye.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA SITA
Huko walikuwa wanaishi wanaume ambao miili yao ilikuwa na afya za kutosha, wanaume ambao hakuwa na uhakika kama walikuwa ni wafungwa ama walikuwa ni miongoni mwa wanajeshi maana hata uvaaji wao ulikuwa wa tofauti. Alitupwa mbele ya wanaume hao na kufunguliwa minyororo yote mwilini na kubakia huru kabisa lakini kwa bahati mbaya hakuwa na hizo nguvu za kufanya jambo lolote kwa sababu alikuwa amelegezwa sana.

"Amedai kwamba nyie wote ni wachumba tu mliopo humu ndani hivyo kwake ni kama dada zake tu" mwanajeshi mmoja ambaye ndiye alimfungulia mwanaume huyo minyororo aliongea kwa sauti yake nzito ambayo ilikuwa inakwaruza kwaruza huku akiwa anasogea pembeni na kuiwasha sigara yake.

Kauli hiyo ilikuwa mbaya kwa wanaume wa kazi sita ambao walikuwa eneo hilo. Mwanaume mmoja ambaye alikuwa amevaa kipensi kifupi tu akiwa peku na kifuani akiwa wazi alimsogelea Remy pale alipokuwa ametupwa, alimuinua kidevu chake na kumkadiria.
"Kwahiyo wewe ndiye kidume ambaye umeletwa hapa sio? unahisi bado upo kwenye magereza ya watoto wenzako huko ulikotoka? Acha kunitilia huruma hapa, simama utuonyeshe huo uwanaume wako vinginevyo tutakuvalisha dera hapa sasa hivi na ngonjera zako za taarabu hizo" aliongea maneno ya udhalilishaji sana kwa Remy, kauli ya yeye kufananishwa na mtoto wa kike ilikuwa imevuka mipaka hata kama ingekuwa ni dhihaka ya kuvumiliwa ila isingekuwa hiyo.

Yule mwanaume akiwa kwenye kibukta chake hicho alipishana na vidole ambavyo vingelitoboa koromeo lake, Remy alitaka kusimama lakini hakuwa na nguvu sawa sawa hivyo alipokea mguu ambao ulirushwa kama mtu anapiga mpira aina ya volley, alipata maumivu makali sana tumboni ukizingatia bado hakuwa amepona vyema majeraha yake ya visu na mapajani alikuwa ametolewa risasi kwa muda mfupi tu ambao ulikuwa umepita.

Nguvu ya mguu huo ilimpeleka mpaka ukutani ambako alijibamiza vibaya. Alijikongoja mpaka akasimama, alisogea hatua kadhaa lakini ilikuwa ni ngumu sana kufanya mijongeo hali ambayo ilimfanya aume meno kwa hasira kwa sababu alikuwa anaonekana kama miongoni mwa watu wadhaifu kwenye maisha yake. Mwanaume yule alimsogelea pale alipokuwepo akitaka kumkunja shingo yake lakini hilo hakufanikiwa, mkono wake ambao aliurusha kwa kuulegeza kwa sababu alijua mtu wake alishalegea ulikamatwa na kukunjwa kwa nguvu kisha alipokea ngumi ya mbavu ambayo ilimfanya ayumbe yumbe sana na kwenda kudondokea mbali akiwa anaguna.

Ilimuingia kisawa sawa ngumi ile kutokana na jinsi ilivyokuwa imerushwa kwa nguvu kubwa hata mrushaji mwenyewe alionekana kutumia nguvu nyingi hali iliyompelekea mpaka kupiga magoti huku damu zikimtoka tumboni na mdomoni. Kumpiga mwanaume yule ngumi ni kama alijichotea matatizo kwani alifuatwa na mwanaume mwingine ambaye alipo jaribu kutaka kupangua ngumi zake mwili ulimsaliti jumla hivyo akajikuata anapokea kipigo kitakatifu mno. Yule ambaye alipigwa alisimama akiwa anachechemea kwa maumivu ya ubavu wake mmoja, alikuwa na hasira sana hivyo alimsogelea Remy pale chini na kuanza kumshushia kipigo, alimpiga kwa hasira sana kiasi kwamba walihisi angemuua hivyo wale wanajeshi walilazimika kupiga risasi juu ambayo ilimshtua kila mmoja na kuwafanya wanaume wale kusogea nyuma na hapo ndipo wanajeshi hao walimchukua Remy akiwa kwenye hali mbaya maana hata miguu ilikuwa imetoneshwa akiwa anahema kwa nguvu mithili ya mtu asiye na pumzi anapokuwa amekimbia kwa umbali mrefu bila kupata mapumziko.

Alibebwa msobe msobe na baada ya kupitishwa kwenye kona kadhaa ambazo zingine hazikuwa na mwanga wa kutosha alienda kutupwa kwenye chumba kimoja ambapo baada ya kugusa tu malango ya chumba hicho aligundua kwamba kilikuwa na harufu mbaya sana ndani yake. Baada ya kutupwa humo na taa ziliwashwa huku akiwa anamuona mwanajeshi mmoja akiwa analifunga geti la nondo la chumba hicho.
"Huku ndiko utakuwa unaishi na wanaume wenzako na shukuru Mungu tunakufungia kama tungepaacha wazi hapa basi ni lazima wangekuua. Jihesabie kama ni mtu mwenye bahati sana" maneno ya kejeli aliyasikia vyema huku wanajeshi hao wakapotea hilo eneo.

Baada ya kubaki mwenyewe ndipo aligeuka ili kuweza kuona ile harufu ilikuwa inatokana na nini, alicho kishuhudia hakupata kukiamini mpaka alipo hakikisha kwamba akili yake imetulia ndipo aliweza kuamini jambo hilo ambalo alikuwa analiona mbele yake. Kwenye kona moja zilikuwa zimerundikwa maiti nyingi sana ambapo nyingi zilikuwa zimeanza kuoza kabisa na kutoa funza na hapo ndipo aligundua kwamba ni hizo ndizo ambazo zilikuwa zinaleta harufu kali sana ndani ya chumba hicho.

Huenda alikuwa anajua kabisa aina ya gereza ambalo anaenda halikuwa lelemama lakini hakufikiria kwamba kwenye taifa lake kulikuwa na unyama wa namna hiyo ambao ilifikia hatua maiti zikawa zinatupwa ndani ya chumba ili walio hai waje kuteseka, ilikuwa ni nje na ubinadamu wa kawaida na kama wananchi wangefanikiwa kulijua hilo huenda wangepoteza kabisa imani na serikali yao lakini hata hivyo hakuona umuhimu wa wananchi kujua kwa sababu alikuwa anajua kabisa kwamba wananchi wenyewe walikuwa ni waoga sana huku wakiwa ni mabingwa tu wa kutoa porojo midomoni kitu ambacho hakikuwa na msaada wowote ule kwa maendeleo ya taifa.

Hali ilikuwa ni mbaya kwenye chumba hicho huku hata mahali ambapo alirushiwa kukiwa na funza kadhaa ambao walikuwa wametambaa kutoka ile sehemu ambako kulikuwa na miili ambayo ilitupwa humo ndani. Hakuona kama angefanikiwa kupata hata usingizi ndani ya hicho chumba licha ya kuwa kwenye hali ngumu na mbaya ila hakuona mtu wa kumdekea hapo hivyo alitakiwa kukomaa yeye mwenyewe na moyo wake kwa vile hata huyo mtu wa kumdekea kwenye maisha yake hakuwa naye.
"Huu ni mwanzo ila hakuna anaye ujua mwisho na hapo ndipo hatari kubwa ilipo kwa hawa watu. Huenda wanahisi mimi mjinga sana ila unapo zidiwa akili na mjinga unakuwa na nafasi ndogo sana ya kuishi kwa sababu mjinga siku akiipata akili ambayo unahisi hana ndio unakuwa mwisho wako. Tafsiri fupi ni kwamba hawa ambao wanajihisi kuwa na akili hatima ya maisha yao ipo kwenye mikono yangu na nitawaua wote" mwanaume aliongea pekeyake akiwa anaziangalia maiti hizo ambazo zilikuwa zimeliwa vibaya ndani ya chumba hicho akiwa pekeyake.




**********
Taarifa ambayo ilikuwa imechapishwa kwenye gazeti ilikuwa imefika kwa mkubwa wa nchi. Raisi alichukia sana kuweza kupokea taarifa kama hiyo kwa sababu kwa kiasi kikubwa ni kama alikuwa anakosewa heshima. Gazeti hilo kumtaka mheshimiwa akampigie magoti mwananchi wa kawaida kuliidhalilisha ofisi yake na Ikulu kwa ujumla hivyo alihitaji mtu ambaye alikuwa nyuma ya huo mpango atafutwe haraka.

Taarifa hiyo mheshimiwa ilimkutia ndani ya ofisi yake akiwa ameketi, katibu wake alimletea gazeti la siku hiyo ambalo moja kwa moja lilikuwa linamhusu yeye na mfumo wake mzima wa uendeshaji nchi. Baada ya kuipokea taarifa hiyo aliitoa simu yake ya mfukoni na kumpigia mkurugenzi wa usalama wa taifa.
"Una jibu lolote la kunipa juu ya maswali yangu?"
"Hapana mheshimiwa"
"Njoo ofisini haraka sana"
"Sawa bosi" aliongea kwa ukali baada ya kiongozi huyo mkuu wa usalama wa taifa kuipokea simu yake na baada ya kukamilisha mazungumzo hayo raisi aliikata simu na kuibamiza kwenye meza akiwa amekunja ndita.

16 inafika mwisho.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA SABA
Wakati mheshimiwa akiwa kwenye hasira kali na mawazo mengi, kwenye ofisi yake aliingia katibu mkuu kiongozi
"Umeona kinacho endelea?" ndilo lilikuwa swali la kwanza la raisi kwa mtu huyo.
"Ndiyo mheshimiwa"
"Kuna lolote umelifanya?"
"Hapana, imekuwa ni ghafla sana hili jambo limetokea bosi, nadhani sio muda sahihi wa kulaumu mtu yeyote kwa sababu inaonekana ambaye anayafanya haya anajua anacho kifanya hivyo kwa sasa utulivu wa akili ndicho kitu cha mhimu zaidi ambacho kinahitajika miongoni mwetu"

"Unataka kusemaje labda?"
"Kwanza inatakiwa tujue lengo la huyu mtu kufanya haya ni lipi? kwa sababu tunaweza tukaanza kuhukumu mtu fulani lakini inaweza kuwa hata ni nchi nyingine kabisa inahitaji kutuchanganya sisi na wananchi wetu kitu ambacho kama tukikiruhusu kiweze kufanyika itakuwa ni hatari sana kwa sababu wakati huu tunatakiwa kuwa wamoja"
"Kwahiyo pointi yako unataka kuniambia kwamba hili gazeti linatumika na watu wa nje?"
"Sina maana hiyo mheshimiwa ila najaribu tu kuchambua kwamba huenda kuna sababu zaidi ya moja ya sisi kujua lengo la hiki kitu ni kipi. Kama atakuwa mzawa basi jambo litakuwa siriasi sana na kama atakuwa mtu wa nje basi huenda ni mtu anahitaji kutuchonganisha wenyewe ili watimize kile ambacho wanakitaka wao"

"Ni dharau kubwa sana mimi kuambiwa kwamba natakiwa kupiga magoti mbele ya halaiki kumuomba msamaha raia wa kawaida ambaye hata simjui ni nani? hii nchi nimejaza viongozi kibao wa ulinzi na usalama ambao mpaka sasa hata sijui wanafanya kazi gani. Nahitaji kila mmoja aingie mtaani na ndani ya masaa ishirini na manne tu nahitaji kumfahamu huyu mtu ni nani na aletwe hapa kwangu aje kujielezea akiwa amepiga magoti yeye"

"Bosi"
"Sitaki ushauri wao tena Godfrey"
"Sawa lakini umeyabeba kwa uzito yale maneno ambayo yameandikwa kwenye lile gazeti?"
"Unamaanisha nini?"
"Kuhusu Dominic Sawa sawa na familia yake" mheshimiwa aliyainua macho yake na kumwangalia katibu huyo kwa umakini sana kisha akataka kukifungua kinywa chake lakini kabla hajafanya hayo mkurugenzi wa usalama wa taifa alikuwa anaingia hapo akiwa na miwani yake usoni lakini baada ya kufika hapo aliivua. Alitoa heshima lakini haikuitikiwa zaidi raisi alimtoa katibu kwa mara nyingine tena, alihitaji kubaki na mkurugenzi pekeyake kwani alionekana kuwa na mazungumzo naye nyeti sana.

"Cleopatra hivi mimi ni nani?"
"Raisi wa jamhuri ya muungano"
"Yaani namaanisha neno raisi lina maana gani kwako?"
"Wewe ndiye kiongozi wa taifa na wewe ndiye namba moja wa taifa"
"Unahisi ni rahisi sana kufika hapa nilipo?"
"Hapana bosi, kama ingekuwa ni rahisi basi kila mtu angekuwa hapo. Mpaka kukuita wewe tunu ya taifa maana yake sio rahisi sana kufika kwenye hiyo nafasi"
"Sasa inatokeaje kwenye taifa ambalo mimi ndiye naamua kipi kiweze kufanyika anatokea mtu mmoja asiye julikana na kunitaka mimi nikapige magoti kuomba msamaha mbele ya raia wangu?"

"Mkuu hili jambo tunalifanyia kazi haraka sana na nitazitumia media zote kubwa kuweza kuifuta kashfa hii na kutengeneza kashfa ambazo zitamfanya aliye itengeneza kauli hii kuonekana yeye ndiye mbaya wakati tunamtafuta"
"Linaweza kuwa ni jambo zuri sana lakini je unahisi litakuwa limefuta doa kwenye moyo wangu? unahisi hii nchi kila mtu ni mjinga sana kwamba hataamini haya maneno? Kuna watu wataamini kwamba kilicho zungumzwa ni kweli na mimi nahusika kwenye hili kitu ambacho kitanichafulia sana jina kwenye uchaguzi unaokuja na unalielewa hilo Cleopatra"

"Nalielewa bosi"
"Safi, nakupa masaa ishirini na manne nahitaji huyu mtu awe amepatikana haraka sana na aletwe kwangu"
"Sawa bosi, lakini naweza kukuuliza kitu?"
"Nakusikiliza"
"Kwani kuna namna yoyote ile ambayo inaweza kukufanya wewe ukahusika na hili tukio la familia ya Dominic moja kwa moja?"
"Whaaaaat?"
"Nimeuliza hivyo kwa sababu ni ngumu sana mtu moja kwa moja kuhusisha tukio hilo na wewe kwenda kupiga magoti mbele ya wananchi hivyo natamani kufahamu kama kuna uhusiano wowote ule wa wewe na hilo tukio ili tusije kufanya kosa la aina yoyote ile kwenye kile hatua ambayo tunaipiga" raisi huyo alikuwa na jazba sana lakini hakuona kama inaweza kuwa njia bora zaidi ya kuweza kutatua tatizo hilo bali alitakiwa kutulia na kuwa mpole ili kuona namna sahihi ya kuweza kulimaliza.

"No, sina uhusiano wowote na familia hiyo kwa sababu miaka ambayo inatajwa hapo nilikuwa busy sana kuipambania siasa na maisha yangu ya kwenye siasa hivyo nisingeweza kufanya jambo la kipuuzi ambazo lingeyachafua maisha yangu ya kwenye siasa. Kazi yangu kubwa ni kuwalinda raia lakini huyu mtu alicho kifanya ni kunikosea heshima kubwa sana mimi na ofisi yangu hivyo namhitaji akiwa mzima"
"Sawa bosi"

"Halafu andaa msafara na utoe taarifa, usiku naenda ndani ya gereza la Dominic kukutana na huyo mfungwa ambaye ametajwa kwenye hilo gazeti"
"Bosi!!!!"
"Vipi unahisi sitakiwi kukutana naye?"
"Sina maana hiyo kwa sababu unaweza kwenda popote pale unapo pataka lakini hili ni jambo la hatari sana kukutana na huyu mfungwa halafu mapema sana namna hii. Ni mtu hatari sana na hana muda mrefu tangu aweze kufungwa hivyo kukutana naye inaweza kuleta picha mbaya sana kama hata kwa bahati mbaya tu hizi habari zikavuja kwa watu au waandishi wa habari"

"Ndiyo maana nimekupa wewe kazi ya kuandaa huu msafara kwa sababu sitegemei makosa kama hayo kuweza kufanyika. Nataka nikutane naye huyu bwana mdogo huenda kuna jambo anahitaji kulizungumza na amekosa mtu wa kuweza kumsikiliza hivyo mimi nitakuwa kwenye hiyo nafasi. Fanya niliyo kuagiza na nahitaji ufanye kazi niliyokupa haraka sana na kwa weledi mkubwa nimpate huyo mpuuzi"
"Sawa bosi"

17 inafika mwisho.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA NANE
"Halafu kabla hujaondoka, nikitoka huko nataka kukutana na huyo binti ambaye alifanikisha kukamatwa kwa kijana huyo"
"Sawa bosi, nitafanya hivyo" mkurugenzi wa usalama wa taifa alibaki ameduwaa sana na kushindwa kabisa kumuelewa kiongozi wake kwani alikuwa anafanya vitu kwa mihemko mikubwa sana na hakuhitaji kufuata wala kusikiliza ushauri wa mtu mwingine yeyote yule hivyo alitoka kinyonge sana lakini wakati anaotoka alikutana na katibu mkuu kiongozi akiwa anamsubiri.

"Cleopatra kuna kitu gani hasa ambacho kinaendelea kati yako na mheshimiwa?"
"Hamna kitu, ananihitaji nimtafutie huyu mtu ambaye amemchafua haraka sana ndilo jambo ambalo linaniumiza kichwa kwa sasa"
"Acha kunidanganya Cleopatra, jambo la kumtafuta mtu haliwezi kukuumiza akili wewe kwa sababu ni kazi ndogo sana kwako hiyo na wote tunalijua hilo, kuna mchezo gani unaucheza hapa?"
"Nilicho kwambia ndio uhalisia wenyewe"
"Unajua kabisa Ikulu ikianguka mtu wa kwanza kuulizwa nitakuwa mimi hapa kisha utafuatia wewe hapo hivyo acha kuniletea usela kwenye majukumu ya kulibeba taifa hasa kwenye wakati kama huu ambao unaona kabisa tunaweza kuingia kwenye mpasuko mkubwa kama huu Cleopatra"

"Kuna mambo nadhani unapaswa kumuuliza mwenyewe kwa sababu wewe ndiye mtu wake wa karibu ila ni kwamba anahitaji kwenda kumuona mfungwa huyo gerezani"
"Unamaanisha Remy Claude?"
"Ndiyo"
"Kwanini?"
"Hata mimi sijui" mwanamama huyo baada ya kumaliza maelezo mafupi aliondoka eneo hilo na kumuacha katibu mkuu kiongozi akiwa anawaza na kushangaa mambo yalivyokuwa yanakwenda halafu yeye ni kama alikuwa anawekwa nje ya box hivi.

ANELIA BATON
Mrembo ambaye alikuwa ni mpelelezi wa kutegemewa sana ndani ya usalama wa taifa wa nchi ya Tanzania alikuwa ametoka makao makuu tayari na kwa wakati huo alikuwa nyumbani kwake pembezoni mwa bahari. Maisha yake ya kuwa mpweke sana huenda ndiyo yalimfanya azame kwenye penzi kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake japo hakuwa uhakika sana na moyo wake.

Alikuwa ameifanikisha kazi kubwa sana ambayo ilikuwa imempa mpaka nafasi ya kukutana na raisi wa Tanzania lakini kwenye moyo wake hakuwa na furaha wala amani juu ya jambo hilo ambalo lilitokea, kuna sehemu ambapo alikuwa anahisi kwamba hakuwa sawa kwa kile kitu ambacho kilifanyika. Alikuwa na mawazo mazito sana akiwa ndani kwake kwenye balcony akiendelea kupata upepo wa bahari huku kwenye mkono wake akiwa na glasi ya wine. Kukutana na mwanaume ambaye alikuwa gerezani kwa wakati huo kwake kilikuwa ni kitu bora zaidi kuwahi kutokea kwenye maisha yake yote tangu azaliwe.
"Huenda nimefanya kosa kubwa kumpoteza mwanaume kama yule kwenye maisha yangu, lakini ningefanya nini wakati ndiyo kazi yangu ambayo nimeifanya tangu nikiwa binti mpaka sasa nakuwa mtu mzima? sidhani kama napaswa kujilaumu sana juu ya jambo hili lakini sikupaswa kumfanyia hivi, alikuwa bora sana kwangu" alitamka huku akiwa anaitoa simu kwenye mfuko na kuitazama picha ya mwanaume huyo akiwa kwenye tabasamu la kuvutia sana.

"I love you Remy" alitamka kwa msisitizo sana lakini wakati huo anamaliza kuongea tu alipokea taarifa ambayo ilitoka kwenye gazeti la siku hiyo ndipo alikumbuka kwamba ni muda kidogo hakushughulika na mitandao ya kijamii hivyo ikamlazimu kuifungua simu yake ili kuweza kuliona tukio hilo kwa ukaribu zaidi maana kichwa chake kilikuwa kinatisha na kumfanya msomaji atamani kugusa kile ambacho kilikuwa ndani yake.

Ile habari kutoka kwenye lile gazeti ilimshtua sana kwa sababu ilikuwa ni habari mpya kwake. Hakuelewa kwanini kwenye gazeti hilo ilitolewa onyo na kauli ya kuyachunguza maisha ya familia ya Dominic Sawa sawa, akiwa kwenye hiyo taharuki na kuanza kuhisi kwamba labda hakuwa akimjua vizuri huyo mwanaume ambaye dakika chache tu zilizokuwa zimepita alitoka kukiri jinsi alivyokuwa anampenda, simu yake ya mkononi ilikuwa inaita na mpigaji wa simu hiyo alikuwa bosi wake.
"Hello bosi"
"Anelia safari ya kuelekea nje ya nchi haitakuwepo tena, kwa sasa baada ya kuonana na mheshimiwa raisi nahitaji urudi tena kazini japo kwa sasa unatakiwa kuifanya kazi kwa siri kubwa pasipo kujulikana na mtu yeyote yule kwamba upo kazini"
"Kwanini nirudi kazini ghafla hivi?"
"Kwa sababu inaonekana huyu mtu historia yake ni ya uongo na hata kukamatwa kwake ni yeye mwenyewe alijikamatisha ili kutekeleza yale ambayo ameyakusudia"
"Kivipi bosi?"
"Hayo mengine tutayaongea vizuri tukikutana lakini kwa sasa jiandae na kazi"
"Kwanini mimi wakati kuna watu wengi ambao wanaweza kuifanya bila hata uwepo wangu?"
"Kwa sababu nakuamini sana, hakuna kazi ambayo nimewahi kukupa ukaiharibu" mwanamke huyo alibaki kwenye mshangao asielewe ni kitu gani kilikuwa kinaendelea kwenye dunia hivyo alibaki amekaa kimya tu asikumbuke kwamba alikuwa anaongea na bosi wake kwenye simu.
"Anelia umenisikia?" alikurupushwa na sauti ya bosi wake
"Ndiyo bosi nimekuelewa" kisha simu ikakatwa ghafla sana.

Anelia alibaki anaushangaa ulimwengu na walimwengu wake kwa sababu kwake hiyo ilikuwa ni habari mbaya sana kwa maana ndiye alikuwa amesaidia kwa kiasi kikubwa ukamatwaji wa mwanaume huyo sasa inakuwaje tena inonekane kwamba historia ya mtu huyo ilikuwa ni ya uongo? alibaki ameduwaa na kuanza kucheka kwa uchungu mkali sana kwenye moyo wake, kama jambo ambalo lilikuwa linasemwa lilikuwa ni la kweli basi alikuwa amefanya kazi ya bure tu kama kazi ya kanisa tu hakunaga malipo wala zawadi ya kuonekana kwa macho zaidi ya kubaki na imani tu moyoni kwamba utabarikiwa.

Mambo makuu ambayo yalimuumiza sana kuhusu jambo hilo yalikuwa ni mawili. Kwanza kama historia ya mtu huyo ilikuwa ni ya uongo maana yake mtu huyo alimjua yeye mapema sana na ujio wake kwenye maisha yake hivyo kifuniko chake cha udaktari Remy alikuwa anakijua muda mrefu sana tangu anaingia kwake hivyo ni yeye ndiye alikuwa anasaidia kutimiza kazi ya mwanaume huku akiamini kwamba yeye anamuingiza kwenye mtego, tafsiri yake ni kwamba tayari tangu muda mrefu Remy alikuwa anajua kwamba Anelia Baton ni mpelelezi ambaye alitumwa kwake kuweza kuikamilisha kazi ya kulipoteza genge lake na yeye mwenyewe kummaliza. Lakini jambo la pili ambalo kwake alihisi ni kama mkuki unauchoma moyo wake, kama mtu huyo alikuwa anaujua uhalisia wake maana yake ni kwamba hata yeye hakuwahi kupendwa kabisa na mwanaume huyo hivyo alikuwa anamuigizia. Hilo ndilo lilikuwa wazo baya zaidi kumjia kwenye akili yake kwa sababu licha ya kazi yeye alimpenda kweli huyo mwanaume na alikuwa akiombea kama naye angempenda kwa kiwango kile kile ambacho alimpenda yeye, sasa kama yeye hakuwa anapendwa ina maana hakukuwa na maana yoyote ile ya yeye kumuwazia mtu huyo kwa sababu mpaka wakati huo alikuwa ni adui yake mkubwa tayari.

18 inafika mwisho.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA TISA
Anelia alisogea sehemu ambayo ilikuwa na picha kubwa akiwa yeye na mwanaume huyo akiwa anashusha chozi kwa mbali, ni wazi hisia za mapenzi zilishindikana kabisa kuzuilika ndani ya moyo wake na alihisi kusalitiwa pakubwa sana kama hayo ambayo yalikuwa yanaongelewa hapo yalikuwa ni ya kweli. Aliishika fremu ya picha hiyo kisha akaibamiza chini kwa hasira ambapo ilipasuka, baada ya hapo aliichukia picha ambayo ilikuwa ndani yake na kuanza kuichoma akionekana wazi kuwa na jazba sana kwa namna moto ulivyokuwa unamuwaka kwenye moyo wake.
"Why unifanyie hivi Remy?" alijisahau kabisa kwamba hata yeye dhamira yake ilikuwa ni kuyateketeza kabisa maisha ya mtu huyo lakini ilipokuja upande wake alihisi kuonewa sana na moyo wake ulimuuma mno isivyo kawaida.

Alijifuta machozi yake taratibu na kufungua droo moja kubwa ambayo ilikuwa chumbani kwake baada ya kuingia huko, kwenye droo hiyo kulikuwa na picha moja ambayo ilikuwa ya wazazi wake. Picha hiyo ilimtoa chozi kwa mara nyingine tena baada ya kuwaona wazazi wake ambao lilikuwa tumaini lake la pekee kabisa kwenye maisha yake ila kwa bahati mbaya Mungu aliwapenda zaidi kuliko yeye alivyo wahitaji.
"Nitaenda wapi kwenye dunia hii wazazi wangu, nani atanipa upendo wa dhati ambao mimi niliutegemea kwenye moyo wangu? Niliye tarajia kwamba huenda hata alikuwa ananifikiria kwenye moyo wangu leo hii ndiye mtu ambaye anaonekana kuwa kinyume kabisa na mimi. Nitamwamini nani? Nani atanipenda mimi?" yalikuwa ni maswali ambayo hayakuwa na uwezo wa kijibiwa kwani alikuwa anaongea na picha ambayo haiwezi kutoa maneno au kuongea jambo lolote lile hivyo akabaki anaumia ndani kwa ndani lakini maumivu hayo yalimkumbusha maisha ya zamani sana.

"Hahahaha binti yangu wewe ndiye fahari yangu mimi, kila ninacho kifanya ni kwa ajili yako mwanangu hivyo unatakiwa kusoma kwa bidii sana ili utakapo kua nikukabidhi mali zangu zote wewe ndiye uweze kuziendesha" Tajiri mkubwa wa madini na mwanaume ambaye alikuwa anamiliki migodi mingi sana ya madini huko Geita alikuwa anamwambia mwanae maneno mazuri sana ambayo yalimfanya binti yake awe na fahari kubwa sana ya kuwa na baba kama huyo.
"Eeeeeh mwache mwanangu asome kwanza, ukimzoesha hizo pesa mapema utamkosa shauri yako" mama yake aliingilia kwa utani huku wakiwa wanacheka sana lakini wakati huo walisikia mtu akiwa anagonga mlango nyumbani kwa tajiri huyo.

Baada ya kufungua mlango huo aliingia kijana wake wa kazi ambaye alitoa taarifa ambazo hazikuonekana kuwa njema sana kwake kwani mzee huyo alionekana kabisa kuchanganyikiwa hivyo ikamlazimu kumuita mkewe pembeni ili waweze kulizungumza jambo hilo. Baada ya muda mrefu kidogo baba yake na mama yake walirudi pale alipokuwepo binti yao ambaye wakati huo bado hakuwa mtu mzima alikuwa binti mdogo tu.
"Mwanangu moyo wa mzazi yeyote yule upo kwa mwanae na hivyo ndivyo ilivyo hata kwetu sisi hapa, kila ambacho unaona tunakifanya ni kwa ajili ya maisha yako ya baadae hivyo kwa sasa tunaondoka mimi na mama yako tunakuacha na dada wa kazi ila mapema sana sisi tutarudi na kuungana na wewe kwa mara nyingine tena. Kitu ambacho unatakiwa kukikumbuka siku zote ni kwamba; wewe ni binti jasiri sana, binti mrembo sana na unaweza kufanya kila kitu kwenye dunia hii. Hili liweke kwenye moyo wako ndiyo maana ukazaliwa wa kike kwenye familia yangu, nikirudi nitakuletea zawadi kubwa sana ya maisha mwanangu, baba anakupenda sana" yalikuwa maneno mazito sana kutoka kwa baba kwenda kwa mtoto ambayo yalikuwa kama ya kuaga moja kwa moja lakini ilikuwa ni ngumu sana kumuelewa mzee Baton.

Baada ya kumaliza maneno hayo alimkumbatia mwanae, mkewe hakuwa na la kuongea alikuwa anatoa machozi tu kisha naye akamkumbatia mwanae huku akilia na baada ya hapo wakawa wameondoka humo ndani na kutoweka kabisa. Tangu ule wakati ambao walimuaga Anelia ambaye ndiye alikuwa binti yao wa pekee kwenye ile familia basi wazazi wake hawakurudi tena kama walivyokuwa wameahidi bali ilirudi miili yao tu pekee ikiwa ni maiti.

Lile ni jambo la kutisha zaidi kuwahi kumtokea mrembo Anelia kwenye maisha yake, umri wake haukuwa tayari kumfanya apambane na harakati za majiji makubwa kwenye ulimwengu huu ambao ulijaa dhulma kila mahali tena akiwa pekeyake lakini dunia ilimchagulia aina ya maisha ambayo bila kupenda alitakiwa kuyakubali na kuweza kuyapokea kwa namna moja ama nyingine. Alifanikiwa kuiona miili ya wazazi wake, hakuweza kuhimili ile hali, alizimia pale pale na baada ya hapo alikuja kuzinduka baada ya siku mbili mbele ambapo alikuta wazazi wake tayari walikuwa wamepumzishwa kwenye nyumba zao za milele hivyo akabahatika kuona makaburi tu wala hakushiriki mazishi.

Alibaki na sonona kubwa kwenye maisha yake, bado hakuwa tayari kuzikabili changamoto za maisha ya dunia akiwa mdogo vile ila upande wa shilingi ulikuwa mbaya sana kwa upande wake. Akiwa anaendelea kumlaumu Mungu kwa kumuacha pekeyake kwenye ulimwengu huu unaotisha sana ndio wakati ambao aliongezewa pigo lingine baada ya makampuni kuanza kujitokeza na kudai kwamba mali ambazo alikuwa nazo baba yake zilikuwa ni za mikopo hali ambayo ilipelekea kila mtu kuanza kuchota alicho kiweza. Kwenye mchakato wa watu hao alifanikiwa kumuona mwanaume mmoja tu ambaye alikuja kuibeba mpaka nyumba ambayo yeye alikuwa anaishi na wazazi wake na baada ya pale hakuwahi kumuona tena mtu huyo hata siku moja. Aliwachukia sana wanadamu na kutamani kujiua kwa sababu hakuona umuhimu wowote wa yeye kuendelea kuishi tena maisha yenye mateso makubwa sana ya namna hiyo.

Wakati dunia nzima imempa mgongo, hakuelewa ilitokeaje au kama ulikuwa ni mpango wa Mungu ila ndiyo wakati ambao mwanamama Cleopatra Gambo alijitokeza kwenye maisha yake na kumpa mkono mpya wa tumaini la kuanza kuyapigania maisha mapya ili aweze kuichora ramani mpya. Hakuelewa kama aendelee kumlaumu Mungu kwa kumpa adhabu kali ya kubaki mkiwa au amshukuru kwa kumletea mtu kipindi ambacho dunia nzima ilikuwa imemkataa.

Mwanamama huyo kwa mara ya kwanza kabisa kwake alikuja kama mpita njia tu ambaye alikuja kumsaidia lakini baadae alikuja kugundua kwamba mwanamama huyo hakujitokeza kwake kwa bahati mbaya hasa baada ya kuingizwa na kutambulishwa rasmi ndani ya shirika la usalama wa nchi na kuwa mpelelezi ambaye alikuja kulisaidia taifa kukamilisha majukumu mengi sana ndani na nje ya nchi.

Tangu awapoteze wazazi wake, moyo wake ulikuwa umekufa ganzi kabisa kuhusu imani kubwa ya kuwapenda wanadamu, alifanya kazi nyingi sana ambazo kuna muda zilimlazimu kuutumia mwili wake ili kuzikamilisha na hakuwahi kujutia kuhusu hilo kwani alikuwa anakamilisha ni majukumu ya nchi lakini kwenye moyo wake hakuwahi kujua wala kuelewa nini maana ya mapenzi kwa sababu yeye alijua kwamba mwili wake ulikuwa kwa ajili ya kazi maalumu tu basi. Lakini kukutana na Remy kwenye maisha yake kulimletea tafsiri mpya kwenye moyo wake ya namna ya kuyachukulia na kuyaangalia mapenzi kwa jicho la tatu. Huyo ndiye mwanaume ambaye yeye alikuja kuzama kwake akiwa anayatimiza majukumu ya taifa huku akiwa na utaalamu wa udaktari ambao aliusomea kuwa kama kifuniko cha kazi yake ya kipelelezi, mwanaume huyo ndiye alikuja kuufungua moyo wake kuelewa kila herufi kwenye neno mapenzi ila ndiye huyo huyo ambaye alikuwa amemuingiza mjini na kuhisi amedhulumiwa moyo wake akianza kuyakumbuka machungu hata ya kuwapoteza wazazi wake, Anelia alijikuta anazalisha sumu mbaya sana na kisasi kikali sana kwenye moyo wake juu ya huyo mtu.

"Remy nitakuua kwa mkono wangu mwenyewe" mrembo huyo aliongea taratibu ila kwa msisitizo sana ila kwa kumaanisha akiwa anajiangalia mbele ya kioo akiuma meno taratibu. Alivua pajama lake na kubaki uchi kabisa, aligeuka na kuiangalia kila pande ya mwili wake jinsi ilivyo umbika, alimshangaa sana Remy na kumuona ni miongoni mwa wanaume wasio na akili au wale fungu la kukosa kwa kushindwa kuelewa thamani ya kuufaidi mwili mzuri namna hiyo. Aliichukua bastola na kupiga risasi moja kwenye kioo ambacho kilikuwa mbele yake huku akitamka tena;

19 inafika tamati.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA ISHIRINI
"Nahisi hata wazazi wangu hawakufa kifo cha kawaida, huenda kuna mambo nafichwa hapa hivyo nitamuuliza bosi kwa mara nyingine na kama asiponipa jibu la kueleweka basi kwenye hii kesi ya Remy ndio utakuwa mwanzo wangu wa kuchunguza kilicho tokea. Huu unakuwa mwanzo wangu mpya wa maisha mapya kabisa" alitamka kwa hasira sana akiwa anahitaji kuchunguza hata kifo cha wazazi wake maana machungu aliyo yapitia wakati huo alihisi kabisa kuna mkono wa mtu ulihusika moja kwa moja kwenye hilo. Mapenzi yalikuwa yanaleta kizaa zaa kipya mjini.

GEREZANI
Ulipita muda mrefu sana Remy akiwa kwenye kile chumba ambacho alikuwepo mpaka akawa amepitiwa na usingizi licha ya harufu mbaya ambayo ilikuwa mle ndani. Alikuwa na njaa kali sana kwa sababu ni muda mrefu ulipita bila kugusa chochote kile.

Alishtuka baada ya kumwagiwa maji ya baridi ndipo akakurupuka akiwa na uchovu wa hali ya juu sana. Wanaume wawili walimbeba na kuondoka naye ambapo walimpeleka kwenye chumba kingine ambacho kilikuwa ni kisafi sana tofauti na alichokuwa ametoka na kile ambacho alifikia mara ya kwanza.

Baada ya kufika ndani ya chumba hicho, alikutana na chakula ambacho kilikuwa kipo safi na wakati huo ilikuwa ni majira ya kuelekea jioni pembeni kukiwa na maji ya baridi. Hakuuliza wala kujiuliza mara mbili, kwanza aliyafakamia maji sana maana alikuwa na kiu mpaka midomo ilikuwa imekauka, baada ya kuyapata maji alianza kukishughulikia chakula huku nje wanaume wale wawili wakiwa wanaulinda mlango wake. Baada ya kumaliza kula mwanaume mmoja alitoa vyombo na kuondoka navyo akawa amebakia mmoja ambaye alikuwa amemnyooshea silaha.

Zilisikika hatua za watu zikiwa zinakuja sehemu hiyo hivyo akawa anatamani kujua kwamba ni nani ambaye alikuwa anakuja eneo hilo. Mbele ya nondo za chumba alicho kuwepo aliona sura ya mtu ambaye alimuona kwa mara ya kwanza humo gerezani wakati akiwa anateswa nje. Mtu huyo umri ulikuwa umeenda sana lakini alikuwa amenawiri isivyo kawaida kwa sababu ya maisha safi ambayo alionekana kuwa nayo japo haikuweleweka ni sababu ipi ambayo ilimfanya kuwepo sehemu kama hiyo wakati alionekana kuwa na nguvu sana ndani ya sehemu hiyo na angeweza hata kutoka kama angehitaji.

Wote walikuwa wanaangaliana kwa muda mpaka pale mzee huyo alipo amua kuingia ndani ya chumba hicho akiwataka watu ambao alikuwa amekuja nao ambao nao walikuwa na nguo za kifungwa kubaki nje kisha akawataka wote na mlinzi wasogee mbali kwani alikuwa na mazungumzo nyeti sana na mwanaume huyo ndani ya hicho chumba.
"Maisha ya mtaani ni tofauti sana na sehemu kama hii, sehemu ambayo mwanadamu huthaminiki tena, huku wewe ni sawa na mbwa tu hivyo ukiwa unaleta kiburi sana kwa hawa mabwana hawana hasara kukufanyia unyama wowote ule wala kukupoteza kwa sababu hakuna mtu atahoji wala kuuliza kuhusu wewe kufa au kuwa hai hivyo badala ya kuwaletea kiburi nadhani ungeamua kuishi nao kama wanavyo hitaji tu japo unaweza ukakaa kwa muda mfupi sana hapa ndani kama tutakuwa na mazungumzo mazuri mimi na wewe" mzee huyo aliongea akiwa anakaa mbele ya mwanaume huyo ili wafanya mazungumzo kwa kuonana ana kwa ana.

"Wewe ni nani hasa mpaka unajali mimi kufa au kuishi kwa shida sana ndani ya eneo kama hili?"
"Usiwe na haraka utanifahamu na utajua kwamba ni kwanini nakuhitaji uwe mzima kwa sababu naweza kuwa na matumizi na wewe makubwa sana"
"Nenda kwenye pointi ya msingi, unahitaji nini kwangu?"

"Nimefuatilia faili lako nimevutiwa sana na utendaji wako wa kazi na kwa jinsi unavyo ifanya kazi yako, lakini jambo kubwa zaidi ambalo limenivutia sana kwako ni ujasiri wako ambapo haupo tayari kutumikishwa na mtu yeyote yule na nilikuwa namtafuta sana mtu wa aina yako nahitaji tufanye kazi"
"Ndo tumeonana leo na unahisi unanijua?"

"Yeah, kuna namna watu wa aina yetu macho yetu tu huwa yanazungumza lugha moja hivyo ilikuwa ni rahisi tu kutambua kwamba mimi na wewe tunaweza kufanya kazi kwa pamoja na ikawa kazi kubwa na nzuri pia"
"Mimi sio mtu wa hivyo na wala hakuna kazi yoyote ile ya hatari ambayo naweza kuifanya kwenye maisha yangu"

"Umejuaje kama kazi ni ya hatari?"
"Ingekuwa ni rahisi ungekuwa umeshapata watu wa kuifanya, acha kunifanya mimi ni mtoto mzee"
"Ila hata malipo yake ni makubwa sana"
"Unahisi kwamba nafanya kazi kwa sababu ya malipo?"

"Hautapata pesa tu bali kuna zawadi kubwa sana ambayo inawez ikakufanya upate nafasi ya kuishi kwa mara ya pili"
"Kwamba hicho ni kitisho cha kutaka kuniua?"
"Mimi na wewe hatuna ugomvi wowote ule hivyo sio mimi wa kukuua ila hawa watu ambao wamekuweka hapa, wewe upo hai kwa muda mfupi tu kwa sababu huenda kuna vitu ambavyo wanavihitaji kutoka kwako lakini kiuhalisia ni kwamba wakimalizana na wewe hawawezi kukuacha hai lazima wakuue"
"Kazi yako ni ipi?"

"Hapo sasa tunaongea kiume. Nina binti yangu ametekwa nahitaji ukamkomboe"
"Whaaaaaat?"
"Ukifanikisha hili nakuahidi kukupa pesa yoyote ile ambayo utaihitaji wewe lakini pia wakati unaenda kuifanya kazi hiyo mimi ndiye nahusika kukutoa wewe hapa gerezani na nakuahidi baada ya hapo hautarudi tena hapa. Nitakufutia utambulisho wako wote na unaweza kwenda taifa lolote lile ukaanza maisha yako mapya ambayo hakuna mtu yeyote atajua kwamba uliwahi kuwa hai"

"Mwanao ametekwa na nani?"
"Maelekezo yote utapewa lakini aliye mteka ni mtu ambaye alikuwa ni rafiki yangu hapo zamani"
"Kwanini amteke mtoto wako?"
"Ni stori ndefu sana na ndiyo maana nimeishia kwenye hili gereza. Nikiwa nje nafuatiliwa kila hatua ninayo ikanyaga na kama nikiteleza kidogo tu nikafanya jambo la kijinga basi nampoteza mwanangu kwa sababu watamuua"

"Ndiyo sababu umeogopa kuwatumia watu wako kwa sababu unajua wanafahamika itakuwa ni rahisi kujulikana ukampoteza mwanao?"
"Ndiyo, hii ndiyo sababu kubwa ambayo imenifanya nitafute mtu wa nje ambaye hakuna anaye kufahamu. Hata hapa gerezani nahisi kuna watu wananifuatilia hivyo wanajua nakutana na nani na nafanya nini ila kwa sababu nakula sahani moja na viongozi wa hapa kuna vitu naweza kuvifanya bila kujulikana"

20 inafika mwisho.

Febiani Babuya.
 
Ukitaka kumalizia episodes 80 zilizo bakia kwa mkupuo ni 3000 tu.

WhatsApp 0621567672
 
Back
Top Bottom