Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA MOJA
"Mbona kama taarifa haijakamilika?"
"Ndiyo haipo kamili"
"Kivipi?"
"Kwa sababu kuna mkanganyiko mkubwa wa habari juu ya uhalisia wa maisha ya mtu huyu"
"Unamaanisha nini?"

"Kwanza jina ambalo analitumia linaonekana kuwa sio lake kwa sababu msaidizi wangu amefuatilia kwenye mahospitali yote lakini hakuna mtu ambaye amewahi kuzaliwa akawa na jina kama hili hivyo ni wazi ametengeneza jina ambalo sio lake"
"Sasa kwanini afanye hivyo?"
"Kwa sababu inaonekana kwamba kuna watu ambao yeye anawatafuta watakuwa ndani ya lile gereza la DOMINIC"
"Unataka kuniambia hata jela ambako alipelekwa mara ya kwanza ameua watu makusudi ili aende kwenye lile gereza?"
"Ndiyo mheshimiwa"
"Why?"
"Huenda hao watu ana historia nao kubwa kwenye maisha yake ndiyo maana ameamua kurisk kila kitu chake ili tu aende kule"
"Kwahiyo unataka kuniambia hata kukamatwa pia ulikuwa ni mpango wake?"

"Sina uhakika ila tunahisi hivyo mheshimiwa"
"Ohhhh shit!"
"Msaidizi wangu anatuma mtu kwenye lile gereza ili aanze kumchunguza taratibu kila ambacho anakifanya kule nadhani ndiyo itakuwa njia bora zaidi ya sisi kuanza kujua mambo ambayo anaonekana kutuficha na kwanini anatumia jina ambalo sio lake maana yake lazima kuna mambo magumu na mazito sana nyuma yake"

"Hizo taarifa nahitaji kuzipata haraka sana na ikiwezekana inatakiwa niende mimi mwenyewe kukutana na huyo mfungwa"
"Mheshimiwa huwezi kwenda kwenye gereza lile"
"Mimi ni raisi wa nchi, naenda sehemu yoyote ile ambayo naitaka mimi, sasa kwanini unahisi kwamba sitakiwi kwenda kule?"
"Nisamehe mheshimiwa"
"Sawa unaweza kwenda nataka nitulie mwenyewe kwanza kwa muda" raisi habari zile zilimshtua sana kuona mtu anajiingiza kwenye hatari kubwa namna ile ili afanikiwe kuingia gerezani tu? huenda kulikuwa na mambo magumu na mazito sana nyuma yake.
"Sawa mheshimiwa, uwe na usiku mwema" mwanamama huyo aliaga na kuanza kutoka humo ndani ila hakujibiwa maana ni kama raisi huyo alikuwa amezama kwenye mawazo lakini wakati anashika mlango ili aufungue na kutoka humo ndani aliitwa na mheshimiwa hivyo ikamlazimu kurudi tena kukaa chini ili kumsikiliza mkubwa wa nchi.

"Una kumbukumbu zozote zile juu ya DOMINIC SAWA SAWA?"
"Unamaanisha yule ambaye lile gereza liliitwa jina lake?"
“Huyo huyo”
"Ndiyo mheshimiwa, yule familia yake yote iliuawa akiwepo yeye mwenyewe hivyo hakuna ambacho kilibakia kuhusu yeye"
"Sawa, waweza kwenda" kauli za mheshimiwa hata mwanamama huyo zilimpa wasiwasi na mashaka sana maana tangu ampatie raisi huyo hizo taarifa alionekana kubadilika kabisa tofauti na alivyokuwa amemkuta mwanzo kabla ya kumpatia taarifa hizo ila hakuwa na namna zaidi ya kutoweka ndani ya ofisi hiyo.


GEREZANI
Ndani ya gereza, kutokana na hali ambayo alikuwa nayo Remy, waliogopa kwamba anaweza kufa bila msaada pekeyake hivyo walimchanganya kwenye selo ambayo ilikuwa na watu wengine watano. Watu hao walionekana kujikatia tamaa kabisa ya maisha kwani sura zao hazikuwa na nuru kabisa. Wanaume wawili walikuwa wamekondeana sana huku wakionekana wazi kwamba walikuwa wamekaa ndani ya gereza hilo kwa muda mrefu. Remy ambaye alikuwa kwenye maumivu makali alibaki anawashangaa watu hao maana walipauka mpaka wakawa wanatoka kwenye ubinadamu ukijumlisha na harufu kali ambayo ilikuwepo humo ndani basi ilimfanya kuona namna baadhi ya watu walivyokuwa wanayaishi maisha magumu.

Watatu miili yao ilikuwa bado imeshiba na walionekana waliingia gerezani humo muda sio mrefu sana maana wao hawakuwa wamefubaa kama wenzao. Wanaume hao walikuwa wamelala lakini baada ya mtu huyo kuletwa na kutupwa humo kama mzigo walishtuka kutokana kwanza na hali ambayo alikuwa nayo kwenye mwili wake. Alikuwa na kisu mwilini pamoja na nondo kwenye paja lake huku mapaja yake yakiwa yamebeba risasi ndani yake. Wakati wanaendelea kumshangaa mwanaume huyo ambaye naye kwa mbali alikuwa anayashangaa mazingira ya humo ndani walisikia sauti ya kejeli ambayo ilichanganyika na matusi kutoka kwa moja ya maaskari ambao walikuwa wamemleta sehemu hiyo Remy.

"Ole wenu hata mmoja wenu ajaribu kumsaidia kwa lolote huyo mbwa hapo tutanyooka naye" ilikuwa ni sauti ya mamlaka haswa ambayo walipaswa kuitii kwa nguvu zote kisha askari huyo akalifunga geti la chuma la chumba hicho kidogo ambacho walihifadhiwa jumla wanaume sita.

Chumba kilikuwa kidogo sana huku kikiwa kinafukuta joto ambalo lilifanya kila mmoja humo ndani kutoa jasho sana isipokuwa wale wawili ambao walikuwa wamefubaa sana, sura zao hazikuwa hata zinaonyesha kama walikuwa wanavuja jasho sana huenda kwa sababu walionekana kuwa wazoefu ndani ya hilo eneo ukilinganisha na wenzao.

Harufu kali ambayo ilikuwa inapatikana ndani ya chumba hicho ni kwa sababu ya uchafu na kinyesi ambacho kilikuwa kinapatikakana humo humo, yaani hicho chumba ndicho kilikuwa choo na sehemu ya kulala hivyo kufanya hali kuwa mbaya sana hususani kwa afya ya mwanadamu ambaye bado yupo hai. Mmoja kati ya wale wanaume ambao walikuwa wamefubaa alionekana kuchoka sana kiasi kwamba alikuwa kwenye hali mbaya kama sio kiafya basi ni kwa sababu ya kukosa lishe lakini hakuna ambaye alikuwa na muda naye kabisa maana kila mtu alitakiwa kujiwazia yeye kwanza kabla ya kumuwazia mwenzie.

Watu hao ni kama walikuwa wana maswali mengi kwa huyo mgeni ambaye alifanyiwa kitu kibaya lakini hakuna mtu hata mmoja ambaye alikuwa na muda naye. Kutokana na hali kuwa mbaya humo ndani Remy hakufanikiwa hata kupata japo lepe wala tone la usingizi hali ambayo ilimfanya usiku mzima ateseke na vitu vitatu. Kwanza yalikuwa ni maumivu makali ambayo yalikuwa kwenye mwili wake, pili harufu kali na mbaya ambayo alikuwa anaipata humo ndani japo hakufanikiwa kuona kila kitu kwani kulikuwa na mwanga mdogo tu wa taa ya nje ndio ambao ulimfanya kuona baadhi ya vitu ambavyo vilikuwa karibu yake usiku huo ila vingine hakufanikiwa kuvitia machoni kabisa. Lakini jambo la tatu lilikuwa ni joto kali ambalo alilipata sehemu kama hiyo halikumfanya kuwa na nafasi ya kupata usingizi hata kidogo hivyo mpaka asubuhi alikuwa yupo macho na ndipo alifanikiwa kuuona mwanga na mijongeo ya askari ambao wengi alikuja kugundua kwamba hawakuwa askari wa kawaida kama alivyokuwa anadhani mwanzo bali walikuwa ni wanajeshi kabisa na wengi walikuwa kwenye magwanda yao huku idadi ya askari ikiwa ndogo zaidi ya wanajeshi ambao walifurika kila sehemu.

Akiwa anaangalia mazingira ya nje, aliona wanajeshi wakija pale na kupitisha vibakuli vya supu ambayo haikujulikana ilikuwa ya nini maana ndani yake hakukuwa na nyama hata moja zaidi ya mchuzi tu, vilikuwa vibakuli vitano vya wale wafungwa watano ambao Remy aliwakuta mle ndani. Kila mtu alikikimbilia kibakuli kimoja kana kwamba walihofia aliye vileta asije kuvitoa tena kama wangechelewa kuvipokea. Hiyo ilikuwa ishara mbaya sana kwa Remy na kugundua kwamba watu hao hilo eneo walikuwa wakiteseka kwa njaa kali isivyokuwa kawaida ndiyo maana kwao chakula walikuwa wanakipa thamani ya hali ya juu tofauti na watu wa maisha ya nje walivyokuwa wanaishi kwa kuchagua vyakula huku wengine hata vile vyakula vya thamani wakivitupa jalalani, hiyo hali ilimpa moja kati ya masomo bora sana ya kuweza kuthamini kitu ambacho unakuwa unacho hata kama ni kidogo kwa wakati huo.

11 sina la ziada.

Febiani Babuya.
Shukrani kiongozi
 
Makini sana, vipi documents 72 part 2 Bado haijatoka?
DOCUMENT NUMBER 72/ NYARAKA NAMBA 72 ndiyo part 2 mkuu. Mpangilio uko hivi

1. ULIMWENGU WA WATU WABAYA. Part one
2. NYARAKA NAMBA 72. Part 2.

Kwa sasa inayo subiriwa ni THE CONCLUSION (CHAPTER 3) ambayo ndiyo itakuwa mwisho wa hizo collection. Jina lake ni👇
3. KALAMU ILIYO-TUMWA KUNIUA....... Hii ndiyo ambayo itamkutanisha baba mtu na mtoto wake. Yaani Calvin Jackson wa kwenye ULIMWENGU WA WATU WABAYA pamoja na mwanae Calvinjr ambaye tumemsoma kwenye DOCUMENT NUMBER 72.

Kukujibu swali lako ni kwamba bado haijatoka.
 
DOCUMENT NUMBER 72/ NYARAKA NAMBA 72 ndiyo part 2 mkuu. Mpangilio uko hivi

1. ULIMWENGU WA WATU WABAYA. Part one
2. NYARAKA NAMBA 72. Part 2.

Kwa sasa inayo subiriwa ni THE CONCLUSION (CHAPTER 3) ambayo ndiyo itakuwa mwisho wa hizo collection. Jina lake ni👇
3. KALAMU ILIYO-TUMWA KUNIUA....... Hii ndiyo ambayo itamkutanisha baba mtu na mtoto wake. Yaani Calvin Jackson wa kwenye ULIMWENGU WA WATU WABAYA pamoja na mwanae Calvinjr ambaye tumemsoma kwenye DOCUMENT NUMBER 72.

Kukujibu swali lako ni kwamba bado haijatoka.
Nikuelewa kaka mkubwa
 
Hii story vipi ,mbona kimya sana au majukumu yamekubana?
 
Hello fellas,

Hope wote mko poa kabisa, binafsi niwape pole kwa kusubiri kwa muda wa siku kadhaa ambazo nilikuwa nimepotea.

Kiafya sikuwa sawa hivyo pia niliamua kuwa mbali kidogo na mitandao kuipa akili utulivu na kwa ajili ya usalama wa macho pia. Nilikuwa available WhatsApp tu napo kwa baadhi ya masaa maana mitandao mingi nilikuwa nafungua kucheki notifications tu na kutoka.

Mungu ni mwema sana, nimerudi na leo tutaendelea pale tulipo ishia.

Simulizi ina episodes 100 incase kuna mtu alikuwa anahitaji kujua hivyo bado episodes 89 mpaka kuja kufika kwisho.

Good morning.
 
Ni wakati [emoji355]
FB_IMG_1713700409446.jpg
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Akiwa ndani ya minyororo yake, waliingia wanajeshi wawili ambao walimbeba asijue wanampeleka wapi. Safari iliishia kwenye uwazi mpana ambao ulikuwa nyuma ya jengo moja kubwa na pembeni yake kulikuwa na kuta nzito. Alifungwa kwenye chuma kimoja kama mtu ambaye anatakiwa kusulubiwa kisha wanaume hao kila mmoja akawa amesogea pembeni na kutafuta sehemu ya kuweza kusimama wakiwa na bunduki zao mwilini.

Ndani ya muda mfupi Luka Gambino, mkuu wa gereza alikuwa anaingia eneo hilo akiwa na watu wake kadhaa na gwanda lake ambalo lilikuwa na nyota kadhaa za kumpa wadhifa awapo sehemu yoyote ile. Mwanaume huyo mtu mzima haswa alimsogelea Remy ambaye mdomo wake ulikuwa umepauka kwa kukosa maji kwa muda mrefu na hakuna ambaye alikuwa anajali.

"Unaweza kunipa sababu ambayo ilikufanya uwaue askari wa polisi na wafungwa wenzio?" mheshimiwa swali lake halikujibiwa kitu ambacho kwake aliona kama ni dharau. Alitoa ishara kwa kijana mmoja ambaye alikuwa umbali kadhaa kisha akajiweka pembeni. Lile eneo ambalo Remy alifungwa alishtuka baada ya kuhisi kama mwili wake unaelekea kuganda hapo ndipo aligundua kwamba juu kulikuwa na bomba kubwa la maji ambalo lilifunguliwa. Maji hayo yalikuwa ya baridi isivyokuwa kawaida mpaka alianza kutetemeka ndani ya sekunde thelathini tu tangu lifunguliwe bomba hilo kisha likafungwa akiwa anaweweseka pale alipokuwepo.

"Hakuna mtu ambaye anatakiwa kukaa kimya pale ambapo mimi nakuwa namuuliza jambo, inakuwa ni hatari kwa upande wake kwa sababu huwa nahesabia kama nimekosewa heshima na mfungwa kama wewe kunikosea heshima ni jambo moja ambalo linanifanya nijisikie vibaya sana kitu ambacho kinakufanya uwe kwenye hali mbaya. Nadhani kwenye chumba ambacho umelala leo umewaona wenzako wawili kwa jinsi maisha yalivyo wanyoosha. Wale nao mara ya kwanza walikuwa wabishi na walijifanya wagumu kama wewe hapo ila kilicho wakuta walianza kupiga magoti na kuomba niwasamehe au niwaue kila siku ya Mungu ila kwa bahati mbaya kati ya machaguo yao mawili yote hakuna hata moja ambalo niliwahi kulitekeleza, walijutia sana mpaka leo adabu huwa zimekaa mahali pake, sasa naona na wewe unataka kuishia kuwa kama wale kitu ambacho mimi nitakutimizia bila shaka" mkuu wa gereza alikuwa anaongea kwa majivuno na hasira ambazo zilijionyesha kwa sauti yake na jinsi ndita zilivyokuwa zimejichora kwenye paji lake la uso lakini mtu ambaye alikuwa anamuongelesha hakuonekana kumsikiliza kabisa kwa yale yote ambayo alikuwa anayatoa kwenye kinywa chake.

Remy akiwa kwenye hali ya kukatisha tamaa alishangazwa na kitu kimoja ambacho kiliifanya akili yake isiwepo hapo ambapo alikuwa anaongeleshwa na mkuu wa gereza hilo. Ni baada ya kumuona mtu mmoja ambaye naye alionekana kuwa mfungwa lakini yeye ni kama alikuwa anaishi tofauti na watu wengine maana alinawiri sana na hata nguo zake zilikuwa safi ukilinganisha na wafungwa wengine. Alikuwa ni mtu mzima wa makamo ambaye aliongozana na watu watatu huku wanajeshi wawili wakiwa karibu yake mmoja mbele na mwingine nyuma yake wakiwa na silaha.

Mtu huyo alisimama kuangalia kule ambako Remy alikuwa anaipata adhabu yake macho yao yakawa yamegongana. Ni kama kila mmoja alikuwa anamuwazia mwenzake vitu ambavyo ni yeye mwenyewe na akili yake zilikuwa zinajua, mtu huyo alisimama na kumwangalia sana kijana huyo ambaye alikuwa anasulubiwa asubuhi ya mapema kabisa hapo nafsi zao zikawa zinaongea taratibu.

Mwanaume aliuma meno yake kwa hasira sana akiwa anaiangala kwa mbali sura ambayo ilikuwa kwa mbali nayo ikiwa inamtathmini. Mmoja alionekana kumjua mwenzake lakini mmoja hakuonekana kuwa na taarifa yoyote juu ya uwepo wala kuonekana kumfahamu mwenzake kwenye maisha ya huu ulimwengu. Nafsi yake ilikuwa inaongea mengi sana huku akiwa anajiongelesha yeye mwenyewe pasipo kutoa sauti yoyote ile wala mtu yeyote yule kumsikia. Wakati mkuu wa gereza akiwa anaendelea kufoka mwenyewe mwanaume alikuwa mbali sana na hata nafsi yake haikuwa hapo kwa wakati huo hali ambayo ilipelekea kuchomolewa visu na ndondo ambavyo vilikuwa mwilini mwake bila kujua huku akiwa hasikiii lolote lile.

Alimshuhudia mtu yule akiwa anaondoka ndani ya lile eneo ambalo alionekana kuishi tofauti na watu wengine walivyokuwa wakiishi pale. Alikuja kushtuka baada ya kupigwa na rungu la chuma sehemu ambayo kilichomolewa kisu, aliguna kwa maumivu makali hatimaye akawa amepoteza fahamu hapo hapo.

"Mkuu mtu huyu anatakiwa kupatiwa matibabu vinginevyo anaweza kufa hapa ikawa kesi nyingine kwa wakubwa, huyu kwa hali hii hawezi kumaliza hizo siku mbili ambazo ndizo ulisema atatakiwa kutibiwa. Mpaka kufikia wakati huo atakuwa amekufa huyu" msaidizi wake baada ya kufika hapo alimpa tahadhari kiongozi wake kwani mtu huyo waliambiwa kwamba walitakiwa kuhakikisha kwamba anakuwa hai vinginevyo wangesababisha madhara makubwa sana maana walipewa taarifa mapema kwamba hakutakiwa kufa.

Hakuwa na namna baada ya kuona ushauri huo ulikuwa bora, alitoa amri aitwe daktari wa gereza na mtu huyo aweze kupatiwa matibabu haraka maana sumu ya zile risasi ambazo zilikuwa mwilini mwake ilikuwa inaendelea kusambaa na kumlegeza sana ukijumlisha na mateso makali ambayo aliyapitia, yalimfanya kuwa kwenye hali mbaya ambayo huenda hata wao hawakuitarajia mwanzo.

Baada ya masaa kumi na saba kupita ndipo Remy alipokurupuka kutoka usingizini tangu apoteze fahamu. Alifumbua macho yake ndipo akagundua kwamba ulikuwa ni usiku wa manane kwa sababu hakuna ambacho alikuwa anaona zaidi ya kiza kinene ambacho hakikumpatia nafasi ya kuweza kuona kitu chochote ambacho kilikuwa mbele yake. Alihisi kitu tofauti kwa sababu hata kama ungekuwa ni usiku basi angeona taa za nje hususani za kwenye chumba ambacho alifikishwa kwa mara ya kwanza huku akiwa anasikia kelele za mikoromo za wanaume ambao aliwakuta ndani ya kile chumba lakini ukimya ambao ulitawala eneo hilo ndio ulimpatia taarifa kwamba hakuwa kwenye kile chumba bali alikuwa eneo lingine tofauti kabisa na kule kwa mwanzo.

Kumbu kumbu zake zilirejea vyema kichwani mwake mpaka wakati anapoteza fahamu na baada ya hapo hakuelewa kilichokuwa kimeendelea zaidi ya kuikumbuka sura ya mwanaume yule ambaye alimuona akiwa anapita karibu na lile eneo ambalo yeye alikuwa anapatiwa adhabu. Akiwa amezama kwenye dimbwi zito la mawazo, masikio yake yaliwashwa kwa sauti kali ya filimbi ambayo bila shaka ilikuwa mbali kidogo na hapo alipokuwepo ndipo akagundua kwamba huenda alikuwa amehifadhiwa kwenye vyumba vya mbali sana.

Baada ya dakika mbili kupita, alisikia sauti za buti za viatu zikiwa zinajongea kuelekea kule alipokuwa na baada ya kukaribia sana alipokuwepo kukawa kimya tena na hapo ndipo alishuhudia taa zikiwa zinawaka karibu na sehemu hiyo ambayo kilikuwepo chumba alichokuwa amehifadhiwa. Kitu cha kwanza kabisa alijiangalia kwenye mwili wake na kugundua kwamba alikuwa ametibiwa kwa sababu sehemu hizo zilikuwa na bandeji na mishono lakini bado minyororo na cheni nzito zilikuwa kwenye mwili wake. Hapo ndipo alipata nafasi ya kuweza kuyainua macho yake ili kumtazama mtu ambaye alikuwa amefika hapo, alishuhudia mtu mwenye mwili mkubwa sana akiwa kwenye kombati safi ya jeshi.

Mwanaume huyo alifungua geti hilo la chuma na kumpa ishara Remy ya kunyanyuka na kutangulia mbele yake kwenye njia ambayo ilikuwa na taa nyingi, hakutakiwa kuuliza kuhusu jambo lolote lile bali taa ndizo ulikuwa mwongozo wake wa pekee kuelekea sehemu ambayo alitakiwa kufika.

12 naweka nukta.

Febiani Babuya.
 
Back
Top Bottom