Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Simulizi ya Kijasusi: Bado Ninaishi

Nahitaji kusoma mpaka mwisho. Utaratibu upoje??????
Lipia 2000 kwenye namba yoyote hapa kisha nicheki WhatsApp

0621567672 (HALOPESA).....WhatsApp

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

FEBIANI BABUYA
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
"Na vijana ambao nilikuwa nahitaji uniletee umekuja nao?"
"Ndiyo mkuu, nimekuja na wanaume wa kazi haswa sita"

"Safi mimi na wewe tutapanga muda mzuri wa kuweza kuonana ila hakikisha kwanza kesho unakutana ana kwa ana na vijana wote wakujue ili ujue kampuni inaendaje kisha nitahitaji ripoti yako"
"Sawa bosi" simu ilikatwa raisi akiwa anatabasamu kwa sababu watu ambao alikuwa anawahitaji sana tayari walikuwa nchini, aliona ni muda mwafaka wa yeye kuanza kuyakamilisha mambo yake kwa ukubwa sana bila kujulikana.

Mwanaume huyo ambaye alikuwa amefika muda mfupi tu uliokuwa umepita, aliitoa simu yake na kuipiga kwa katibu mkuu kiongozi wa Tanzania usiku huo. Aliipokea simu hiyo kwa mara ya kwanza ikiwa ndani ya taifa la Tanzania maana alikuwa amezoea kuipokea ikiwa nje ya nchi.
"Bosi"

"Nipo Tanzania. Kesho waite vijana wote tutakuwa na kikao na mimi nitakuja moja kwa moja wote mnifahamu"
"Sawa bosi japo imekuwa ghafla sana"
"Kuwa ghafla sio shida, nataka uandae majibu kwamba ni kwanini mpaka sasa masuala madogo kama haya umeshindwa kuyaweka sawa mpaka nimelazimika kuja mwenyewe, halafu ulivyo na akili fupi huoni shida raisi wako kuchafuliwa huku unajua kabisa kwamba wewe ndo utakuwa mtu wa kwanza kunyooshewa kidole kitu ambacho kitaifanya kampuni yetu kuweza kuingia kwenye matatizo huku wewe ukinenepa tu na kubadilisha wanawake"

"Naomba unisamehe sana kiongozi, hili nitaliweka sawa nipe nafasi nyingine"
"Maisha hayakupi nafasi nyingi hivyo Gedfrey, maisha haya ni mafupi sana hivyo ukifanya makosa mengi inatakiwa ufundishwe namna sahihi ya kuitumia kila nafasi ambayo unakutana nayo"
"B....." kabla hajajibu simu hiyo ilikatwa, bosi wake ambaye alikuwa anaishia kuwasiliana naye kwenye simu tu alikuwa nchini, kwake ilikuwa ni habari mbaya sana kwa sababu kuna uzembe mkubwa mno ambao ulikuwa umefanyika na yeye ndiye ambaye alikuwa nyuma ya huo uzembe hivyo kukutana na kiongozi huyo moja kwa moja ilikuwa inamletea mazingira magumu sana hasa kwenye kumshawishi ili aweze kumuelewa.

Alihisi kuchanganyikiwa, akaanza kupiga simu kwa vijana wake wote watano ambao ndio walikuwa wanaufanya muunganiko wa kampuni hiyo uweze kuwa mkubwa, aliwapigia wanne na kuwapata taarifa za ujio wa mtu mkubwa zaidi kwenye kampuni wa juu yake, habari ambayo huenda iliwashtua sana wenzake lakini yeye ndiye alishtuka zaidi yao na taarifa zingine ambazo zilimpa sana wasiwasi ni baada ya kusikia kwamba mmoja ya wanaume hao watano hakuwa akipatikana. Ulimboka ndiye mtu ambaye alishindwa kumpata wakati huo ili kumpa taarifa hiyo ili keshoyake asije akakosekana kuwepo.

Kushindwa kumpata mwanaume huyo hewani ilikuwa sababu nzuri kabisa ya kumpigia Justin na kumtaka yeye na vijana wake wakamchukue mtu huyo kama sio kumpatia taarifa kuhusu kikao kikubwa ambacho kingefanyika kesho yake. Justin aliwachukua wanaume wanne jumla wakawa watano ili kuelekea Tabata sehemu ambako alikuwa anaishi mwanaume huyo Ulimboka.

Walitumia dakika arobaini kuweza kufika sehemu hiyo ila walicho kutana nacho kiliwashangaza sana kwani geti la kuingilia ndani lilikuwa wazi. Ndani ya uzio kulikuwa na mijengo minne mikubwa hivyo walianza kuzunguka kila jengo lakini walicho fanikiwa kukutana nacho ni miili ya watu ambayo ilikuwa imeuliwa kikatili sana kila sehemu. Walifanikiwa kuingia kwenye kila nyumba hawakufanikiwa kumkuta mtu wao zaidi ya familia yake mke na watoto wawili ambao walikuwa wamefungiwa chumbani tu. Justin alipiga simu kwa katibu mkuu kiongozi kumpa taarifa hiyo.

"Amechukuliwa"
"Na nani?"
"Hakuna mtu ambaye anaonekana, mke wake anasema alihisi kuna mtu alikuwa nyuma yake kisha hakuelewa kilicho tokea na alipokuja kuzinduka alikuwa yupo chumbani na watoto hakujua nini kilitokea huko nje. Walijaribu kupiga simu mtandao haukuwepo na walifungiwa nje hivyo wakawa hawana cha kufanya"

"Hakuna kamera ili uweze kujua kwamba ni nani alikuwa hapo?"
"Kamera zote zilizimwa, ni wazi mhusika alikuwa anajua alichokuwa anakifanya"
"Namtafuta kijana mmoja serikalini ambaye ni mdukuzi bora sana japo ni mtu wa siri, mumtafute mtoa gazeti la UKWELI WANGU WA SIKU na uhakikishe anapatikana, huyu ndiye atakuwa nyuma ya kila kitu"
"Nimekuelewa bosi nitahakikisha anaingia kwenye mkono wangu"

"Justin do it" aliongea kwa hasira akiwa anaikata simu, wanaume hao waliifungulia familia hiyo na kuondoka nayo hapo ndani huku katibu mkuu kiongozi akionekana wazi kuchanganyikiwa maana kesho yake kulikuwa na kikao kizito sana na alikuwa na mambo mengi ya kujibu lakini wakati huo huo tena akawa amefanya uzembe mwingine wa kupotea kwa mtu wao mmoja ambaye ni Ulimboka, hilo lilikuwa ni jambo jingine kabisa.

SAA MOJA NYUMA.
Ashrafu alikuwa na namba ya nyumba pamoja na sehemu ambayo alikuwa ameelekezwa na Benard Taradadi mmiliki wa benki za TUNAKUWEZESHA jinsi ya kumpata mtoto wa Bruno Josephat ambaye mpaka wakati huo hakuwa anajua kwamba tayari alishakufa kwa kuuawa na raisi ili kumlinda huyo binti yake.

Mwanaume usiku wa manane kabisa jiji likiwa limetulia ndio wakati ambao aliona ni sahihi kuweza kuifanya kazi yake. Nafsi ya huruma ilikuwa imemtoka kwenye moyo wake wakati huo maana aliona anapoteza muda tu kwa mambo ambayo alitakiwa kuyamaliza mapema sana.

Tabata kwa wala bata kama ambavyo huwa wanapaita ndipo alifanikiwa kupatembelea usiku huo akiwa taratibu kwenye gari yake ya Vx nyeusi tii. Mwendo wake haukuwa mkali sana kwa sababu hakutaka kuwashtua watu kabisa hususani wale ambao walikuwa wanakula bata kwenye sehemu za starehe. Aliishia Tabata Kimanga sehemu moja ambayo zilijitenga nyumba kadhaa ambazo zilikuwa zimejengwa kwa ubora mkubwa sana, bila shaka walijitenga watu ambao walikuwa na uwezo wa kumudu vyema milo yao bila wasiwasi.

Alishuka ndani ya gari yake akiwa amevaa nguo nyeusi ambazo zilikuwa zinamfunika kila sehemu mpaka kichwani, ni macho tu ndiyo yalikuwa yanaonekana. Alizunguka nyuma ya jengo la kwanza, akatembea kidogo akiwa makini sana kuangalia namba za nyumba na baada ya muda kidogo alikutana na nyumba ambayo alikuwa anaitaka akiwa anaiangalia kama mita hamsini mbele yake. Aliivuta simu mfukoni na kuibonyeza mara kadhaa ambapo kwenye ile nyumba umeme ulizima ghafla kisha ukawaka tena na wakati unawaka kwa mara ya pili kamera zote zilikuwa zinazima. Mwanaume alivaa gloves mikononi na kusogea getini ambapo aligonga geti kwa nguvu sana kisha akakimbilia upande wa pili ambapo alijivuta juu ya ukuta na kutua ndani nyuma ya jumba moja.

48 NAWEKA NUKTA.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA AROBAINI NA TISA
Mlinzi alisogea getini kwa kasi akiwa na silaha yake mkononi, ni wazi aliyegonga alimpa hasira sana kukosa ustaaarabu hivyo alifungua kwa hasira ili kumkomesha mtu huyo lakini baada ya kufungua hakuona mtu hivyo aliishia kusonya kwa hasira sana.
"Kuna nini huko David?" mwenzake ambaye hakuwa mbali naye alimuuliza akiwa amekaa kwenye kiti lakini aligeuka ili kumjibu kwa kichwa lakini wakati anageuka alishangaa hamuoni mwenzake kwenye kiti alipokuwa ameketi. Alisogea mbele ya kibanda kikubwa cha karibu na getini hapo alishangaa kutomuona kabisa aliyekuwa analinda naye, baada ya kuzunguka nyuma alikutana na damu nyingi sana kitu chenye ncha kali kikionyesha kupita kwenye shingo ya mwenzake. Alitaka kupiga kelele wakati anageuka ili kukimbila lakini bahati mbaya sana alijigonga kwenye mwili wa mwanaume mwenzake ambapo alipigwa buti la mguu wakati anataka kudondoka shingo yake ilitengeshewa kwenye goti na kuvunjwa kikatili mno habari yao ikaishia hapo.

Mwanaume alikutana na shoka ambalo walikuwa wanalitumia wanaume hao kulindia hapo, alilishika na kulitikisa kidogo akaona kwamba lingemfaa sana hivyo alilibeba. Baada ya kuzungukia upande wa pili aligundua kwamba mwanaume mmoja alikuwa anakuja kule alikokuwa hivyo alirusha shoka kwa nguvu likaenda kukita katikati ya kifua cha mwanaume huyo ila kwa bahati mbaya sana wakati anaanguka chini alikuwa ameachia risasi moja ambayo ilitoa mlio wakati inapoteza uelekeo na kuelekea angani.

Alisogea na kulichomoa shoka kisha akajibana ukutani, risasi hiyo iliwaamsha walinzi wengine kwa zile kelele hali ambayo iliwafanya wote wajitokeze hilo eneo wakiwa kumi na silaha zao. Mmoja ambaye alitangulia mbele alipigwa na shoka la shingo kwa sababu hakujua kama eneo hilo kulikuwa na mtu, shingo yake ilijitenga kutoka kwenye kichwa lakini wakati huo wanaume tisa walikuwa wamememzunguka Ashrafu wakiwa wamemuweka chini ya ulinzi. Hakuwa na namna zaidi ya kuiweka silaha yake chini kwani kama angefanya uzembe tu alikuwa anakufa.

"Ndiye wewe taarifa zilikuja kwamba umetoka jela bila shaka"
"Unanifahamu mimi?"
"Nakujua sana ndugu yangu labda kama kuna wengine ndio hawajukui ila sio mimi" aliongea mwanaume mmoja ambaye aliiwasha sigara na kumsogelea Ashrafu, aliuvuta moshi wa sigara na kumpulizia usoni akiwa anacheka.

"Una muda mchache sana wa kufurahi, bosi wako yuko wapi?"
"Unamtaka bosi? hauwezi kukutana naye mpaka niupime huo uwezo wako ambao unasifiwa sana kuwa nao" alijibu huyo mwanaume huku akiwa anachana tshirt ambayo ilikuwa kwenye mwili wake kuonyesha namna mwili wake ulivyokuwa umepasuka. Kusikia kwake sifa za huyo mtu hakutaka kuingia kwenye huo mkumbo mpaka aweze kuupima uwezo huo yeye mwenyewe moja kwa moja maana aliamini kwamba wanadamu wana tabia ya kuweza kuongeza chumvi sana.

"Hahaha hahaha hahaha nipeleke kwa bosi wako mtoto wa kike wewe, mimi sipiganagi na vijana ambao hawajui hata kama jinsia zao ni za kiume" Ashrafu aliongea makusudi ili kumpa hasira mwanaume huyo kwa sababu alijua akiwa na hasira atatumia mihemko kuweza kufanya maamuzi kitu ambacho kitampa nafasi ya kujitoa mikononi mwao ili ampate mtu wake.

"Muachieni" aliwapa amri wanaume ambao walikuwa wamemshikilia Ashrafu ili wapimane maana hakuweza kuyavumilia yale matusi yake. Ashrafu alimwangalia mwanaume huyo kwenye mwili wake na kugundua kwamba alikuwa na bastola kwenye kiuno chake huku yeye akiwa na kisu, alijua hivyo vinatakiwa kumsaidia haraka sana kuwamaliza watu hao kwa pamoja.

Mwanaume huyo alimpa Ashrafu ishara ya kumsogelea alipokuwepo lakini mwanaume alitishia kama anaenda ila alibaki amesimama, mwenzake alikubali kuingia kwenye huo mtego ambapo alimfuata mara ya pili na kumkosa na buti kali la shingo ambalo lilikita kwenye ukuta, Ashrafu alipigwa mtama na mguu mmoja ambao ulikuwa umebaki chini, alimanusura adondokee shingo ila mkono wake ulidunda chini kisha akadunda kwenye ukuta na kuja na kasi ya ajabu kama upepo ambapo alitua kwenye kifua cha yule mwanaume kwa goti moja kali na kabla ya mwanaume huyo hajatua chini alimshindilia kwa ngumi mbili za moto na kumfanya atoe damu mdomoni.

Wenzake walitaka kuingilia lakini aliwakataza kabisa na kuwapa onyo kiasi kwamba ambaye angeingilia ugomvi huo angekiona cha mtema kuni, wakawa hawana namna zaidi ya kuwa wapenzi watazamaji maana kiongozi wao alionekana kuwa na hasira sana. Wakati ananyanyuka Ashrafu alimzunguka nyuma kwa spidi kali sana na kumdaka shingo ambapo alimvutia kwake na kuichomoa bastola kiunoni ambayo aliitumia kuwaua wanaume sita akiwa amemuweka mwanaume huyo kama ngao yake.

Watatu walikuwa mbele yake wakiwa hai na bastola zao kwenye mikono lakini hawakuwa na uwezo wa kufanya lolote kwani kiongozi wao aliwekwa mbali. Ashrafu alianza kusogea pembeni mwa nyumba akiwa anamtumia mwanaume huyo ambaye alikuwa hoi kama ngao yake. Wakati anazama kwenye huo ukuta alirusha kisu chake ambapo kilitua kwenye shingo ya mmoja wakawa wamebaki wawili tu. Alipotea konani na wanaume hao wakati wanatokezea ili kumfuatilia walisukumiziwa mwili wa mwenzao na kuanguka chini.

Ni nafasi ya pekee ambayo aliitumia kujigeuza kwa sarakasi na kutua kwenye shingo ya mmoja kwa buti kali kisha akaichukua bastola ambayo alikuwa nayo kwenye mkono wake na kumpiga mmoja aliyekuwa amebakia kichwani sasa akawa amebakia yule kiongozi wao ambaye ndiye alihitaji kupigana naye.

Mwanaume alimfumua kwa risasi tano zote ambazo zilikuwa zimebakia kwenye bastola. Risasi zote ziliishia kwenye goti lake la kulia ambalo lilimpatia maumivu makali sana kisha Ashrafu akaliokota lile shoka ambalo alipenda kulitumia. Alimsogelea mwanaume huyo na kuukata mguu wake ule ambao aliupiga risasi bila huruma huku mwanaume huyo akiwa anabembeleza sana asiweze kuuawa.

"Mguu ulikuwa unatisha sana huo kuutazama ukawa unanipa kichefu chefu, sasa unaweza ukaniambia mwanasheria Ulimboka yuko wapi na binti wa Bruno Josephat amehifadhiwa wapi?"
"Mimi sijui" kauli yake ilifuatiwa na kukatwa mguu mwingine wa pili
"Unanipoteza muda wangu"
"Bosi yupo nyumba ya mwishoni kabisa kule na huyo binti amewekwa nyumba ya pili kutoka mwishoni kwenye chumba namba 7" alijibu akiwa analia maana damu nyingi sana ilikuwa inamtoka bila kusahau maumivu ambayo aliyapitia. Mwanaume alisimama na kukichomoa kisu chake na shoka ila baada ya kupiga hatua kadhaa aligeuka na kukirusha kisu kwa vidole vyake viwili ambapo kilienda kukita kwenye moyo wa mwanaume huyo akaruka ruka kidogo na kutulia kimya hapo chini.

Alisogea mpaka kwenye nyumba ambayo alidaiwa kuwepo ULIMBOKA, alifika mlangoni na kuukanyaga mlango huo kwa nguvu akaingia nao ndani. Alisikia kelele za hofu kubwa sana kutoka kwa mwanamke ambaye ni wazi alitokea kwenye friji kuchukua kinywaji maana mkononi alikuwa na juisi, kwa bahati mbaya sana mwanamke huyo alikuwa amempa mgongo hivyo wakati anageuka ili kumuona mtu huyo ambaye aliingia na mlango alipigwa ngumi ya shingo akapoteza fahamu.

49 INAFIKA MWISHO.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI
"Sto...." ni sauti ambayo ilitokea nyuma ya mgongo wa Ashrafu kumtaka atulie kama alivyo lakini mtu huyo kaufanikiwa kuikamilisha kauli yake hiyo baada ya Ashrafu kugeuka na shoka ambalo lilitenganisha bega la mwanaume huyo akashuka chini akiwa anakufa huku anajiona.

Ashrafu alipishana na risasi wakati anageuka hali ambayo ilimfanya kurusha shoka lake kuelekea juu kwenye ngazi. Risazi hizo ambazo zilirushwa na mtu ambaye alikuwa amekosa umakini mkubwa zilitoka kwa baba mwenye nyumba mwenyewe Ulimboka ambaye ndiye alimjia hapo lakini shoka ambalo alilirusha kifundo chake kilimgonga mzee huyo kwenye paji lake la uso hali ambayo ilimfanya kudondokea chini kabisa kwenye ngazi akawa ametulia kimya. Ashrafu alimsogelea na kumgusa puani akagundua kwamba alikuwa amepoteza fahamu. Alimbeba mkewe na kumpeleka kwenye chumba ambacho alikutana na watoto wakiwa wanatetemeka sana bila shaka ni ile milio ya risasi waliyokuwa wameisikia. Aliwaangalia sana watoto hao na kumtua mama yao kisha akuufunga mlango na kurudi chini.

Alimbeba mzee huyo begani na kusogea nyumba ya pili yake ambapo alitumia shoka kuvunja mlango huo. Alikuwa makini sana kuangalia namba lakini alishangaa kuna sehemu namba zimeishia 5 na aliambiwa chumba namba7. Wakati anayanyanyua macho yake aligundua kwamba kwenye kona moja kulikuwa na ngazi za kushuka chini hivyo alishuka nazo mpaka alipo kutana na chumba namba 7 ambacho kilikuwa kimefungwa kwa nje. Alifungua na ndani yake alikutana na mwanamke mzuri sana ambaye baada ya kumuona mwanaume huyo alianza kupiga makelele kwamba asije akambaka wala kumuua, Ashrafu alimsogelea na kumgusa na vidole vyake shingoni akawa kimya, alimbeba na kutoka naye humo ndani huku akiwa amembeba Ulimboka pia upande mmoja. Aliwafikisha kwenye gari na kutoweka nao na wakati anaondoka ulipita muda mchache sana ndipo Justin na vijana wake waliingia eneo hilo na kukuta mauaji ya kutisha na mhusika alikuwa tayari ametoweka hivyo nao waliamua kuondoka maa hilo eneo huenda kwa muda mchache tu ambao ulikuwa unafuata vyombo vya usalama vingeanza kujazana hapo.

Ulipita muda mchache sana tangu Justin na vijana wake waweze kuondoka, mkurugenzi wa usalama wa taifa alifika hapo kama alivyokuwa amepewa taarifa na Suzane akiwa na wanaume waliokuwa kwenye suti zao na gari mbili lakini baada ya kufika hapo walikuwa wamechelewa sana kwani wahusika hawakuwepo walikuwa wamemaliza kazi yao na kuondoka.

Walianza kufanya uchunguzi wao na ndani ya nusu saa tu Suzane naye alikuwa anaingia hilo eneo akiwa anapaki gari na kukimbilia ndani ila hata yeye alikuwa nyuma ya muda sana.
"Inawezekanaje mtu anaua wanadamu wenzake kikatili sana namna hii?" Mkurugenzi alikuwa anauliza huku akiwa anaukagua mwili wa mwaname ambaye alikuwa amekatwa miguu yake yote na kuchomwa kisu kwenye moyo wake.

"Ndiyo maana huyu mtu hatakiwi kukamatwa tena bali anatakiwa kuuawa" alijibiwa na sauti ambayo ilimfanya asimame na kugeuka nyuma. Suzane alikuwa ameingia ndani ya hilo eneo lakini kabla hajajibiwa alikuja mwanaume mmoja akiwa na bastola mkononi.
"Colt paterson Revolver, ni bastola adimu sana duniani hizi ndiyo tumeiokota hapa ambayo tunahisi kwamba mvamiaji ndiye ameidondosha. Kwa taarifa za kwenye mfumo wetu ni kwamba bastola kama hii iliwahi kufanya mauaji miaka zaidi ya ishirini iliyopita. Ni bastola ambazo wamewahi kupewa watu wachache sana hususani wale ambao walikuwa na vyeo vikubwa jeshini na ambao walitumwa kufanya oparesheni maalumu ngumu ili wasifahamike pindi wakizitumia maana ni ngumu kuujua utambulisho wake" mwanaume huyo alitoa maelezo ambayo yalimfanya Suzane amwangalie sana bosi wake maana alikuwa ameguswa mahali pake.

"Nipatie nitaishughulikia mwenyewe kisha kaendelee na uchunguzi"
"Sawa bosi" mwanaume huyo aliikabidhi na kuondoka hapo kwa sababu kazi yake kubwa alikuwa ameikamilisha tayari.
"Bosi utaendelea kumlinda mdogo wako mpaka lini kama mtu mwenyewe hataki kulindwa? Hivi unahisi ikijulikana kwamba hiyo bastola aliwahi kuitumia yeye nini kitatokea?" Suzane aliongea akiwa anamsogelea bosi wake.

"Kama sijakuelewa vibaya, hicho ni kitisho kwangu Suzane?"
"Hapana mimi sina huo uwezo wa kuanza kukutisha wewe ila ninacho kwambia ni uhalisia, kumbuka wewe ni bosi wetu ambaye tunakusikiliza wewe na jambo la kwanza ambalo unatakiwa kulijali ni kuutanguliza kwanza usalama wa raia kabla ya jambo lolote lile hata kama ni familia lakini wewe umeruhusu mapenzi kwa mdogo wako yafanye uharibu kazi" mwanamama huyo alicheka kwa nguvu sana.

"Mara ya kwanza sikuwa sahihi Suzane nilihisi wewe ni binti makini sana ila nilipoteza muda wangu kukupa hizo sifa kwa sababu haustahili. Hivi unajua upumbavu ambao umeufanya na madhara yake ambayo yanaenda kutokea?" Cleopatra Gambo alimsogelea mrembo huyo ambaye ni kama alianza kuvimba kichwa akawa anaisahau mipaka yake. Kauli hiyo haikuwa mara ya kwanza anaisikia hata wakati yupo nyumbani kwa mdogo wake na bosi wake alipewa hiyo kauli;

"Nina uhakika asilimia tisini mpaka sasa kwamba ulikuwa unafuatiliwa na kama ulikuwa unafuatiliwa maana yake ni kwamba tayari wamepajua nyumbani kwa mdogo wangu na hawa watu ambao binafsi siwajui ambao watakuwa nyuma ya huu mpango watakuwa wanaunganisha doti. Hilo litapelekea wao kumteka mdogo wangu ili kuweza kumpata mwanae kirahisi, baada ya hapo unajua mambo gani yanaenda kutokea? Umeileta vita ambayo hata mimi sina imani kama kuna mtu anaweza kuja kuizima kwa sababu ya upumbavu wa mihemko yako ya kijinga badala ya kutumia akili. Hivi kwenda na haya mambo taratibu ulikuwa unaniona kama mimi sina akili sio? Ukajiona wewe ndiye umekuwa bosi wangu na unaweza ukafanya kile ambacho unakitaka wewe kwa majivuno ambayo uliyaingiza ndani yako. Nakuapia kama kuna jambo baya litamkuta mdogo wangu Suzane, nitakuua kwa mkono wangu wewe na wenzako wote kwa sababu nimeanza kuwa na hisia kwamba hata huko unakokuwa nao huwa unawalisha ujinga hivyo wanakusikiliza"

"Kuna kitu kimoja ambacho wanadamu wengi sana huwa mnaingia kwenye huo mtego ambao baadae huwa unawaletea madhara makubwa sana. Wengi mnaamini kwamba kuwa na nguvu za madaraka au kipesa basi wewe ndiye unakuwa mfalme wa kila kitu ila sio kweli binti, akili nyingi na mipango isiyo fahamika ndizo silaha za hatari zaidi hapa duniani maana unaweza ukawa na madaraka na pesa na bado ukatawaliwa na watu ambao hawatumii mihemko kufanya maamuzi bali wanakaa chini kuandaa mipango mikali ya maisha. Ulitakiwa umjue kwanza Ashrafu yupo vipi kabla ya kuingia kwenye maisha yake, huyo kijana ni mtu mbaya sana hususani unapo hitaji kuyagusa maisha ya mdogo wangu, wanaenda kufa watu wengi sana ambao hawana hata hatia kwa sababu ya ujinga wako. Sikutaka kumshughulikia mapema Ashrafu kwa sababu nachunguza kwa undani sana inaonekana kuna kundi la watu wengine ambao hawajulikani lipo nyuma yake kwahiyo nao walitakiwa kupatikana ila kwa sasa umeharibu kila kitu. Lolote litakalo tokea Suzane mimi nitakula sahani moja na wewe" Cleopatra alitema nyongo kali sana na kutoweka hilo eneo haraka na baadhi ya walinzi wake huku wengine wakibaki wanafanya uchunguzi kabla polisi hawajafika.

Suzane alinyong'onyea kama sio yeye, alikuwa anahisi yeye ndiye ana akili nyingi sana kufanya vitu kwa mihemko kumbe alikuwa bonge la mjinga. Alishangaa sana baada ya mkurugenzi huyo kumhakikishia kwamba kwa asilimia nyingi ni lazima alikuwa anafuatiliwa kwa sababu alikuwa na uzoefu na hizo kazi kwa miaka mingi sana huku yeye moyoni akihisi kabisa kwamba hakuona kama kulikuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa anamfuatilia sehemu yoyote ile.

50 NAWEKA KALAMU PEMBENI.
 
Lipia 2000 kwenye namba yoyote hapa kisha nicheki WhatsApp

0621567672 (HALOPESA).....WhatsApp

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

FEBIANI BABUYA
hata mm naitaka nakutumia hio 2000 lakini sina whatssap..unaweza kunitumia facebook inbox.?
 
hata mm naitaka nakutumia hio 2000 lakini sina whatssap..unaweza kunitumia facebook inbox.?
Ndiyo inawezekana vizuri tu.

Nipigie kwa namba yoyote hapo au nitumie sms nitakupa maelekezo yote.
 
Ndiyo inawezekana vizuri tu.

Nipigie kwa namba yoyote hapo au nitumie sms nitakupa maelekezo yote.
sioni haja ya kupigiana simu ww niambie hapa kule facebook unatumia jina gani nikutumie sms inbox nikutumie hiyo 2000 kwa m pesa kisha unitumie inbox hii story hadi mwisho 100 kama uliyosema hapa tumalizane hivyo
 
sioni haja ya kupigiana simu ww niambie hapa kule facebook unatumia jina gani nikutumie sms inbox nikutumie hiyo 2000 kwa m pesa kisha unitumie inbox hii story hadi mwisho 100 kama uliyosema hapa tumalizane hivyo
Unamuogopa mshkaji mbona unatia shaka kutoa namba?
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA
Kwa maelezo aliyopewa ni kwamba alienda kurina asali mchana wa jua kali akiwa hana hata moto halafu kawachokoza nyuki. Ni maamuzi ya hovyo ambayo aliyafanya bila kutuliza kichwa au kuomba ushauri kwa sababu tu alipewa jina la mahali alipokuwepo brigedia mstaafu Mariana Amboni. Alitakiwa kusali sana mambo yasiende tofauti kwa sababu kama ingeshindikana basi yeye na wenzake walitakiwa kufutwa kabisa duniani isijulikane kama waliwahi kuwepo kabisa. Suzane alikuwa emeyabananga kwa kutumia mihemko badala ya akili ambazo mjini ndio msingi mkubwa wa maisha.

Mkurugenzi wa shirika la kijasusi la nchi ya Tanzania, Cleopatra Gambo baada ya kutoka Tabata na kumpa makavu bibie Suzane kwa ujinga aliokuwa ameufanya alikuwa anaongoza njia kuelekea yalipokuwa makao makuu ya jeshi la nchi na lengo lake kufika huko lilikuwa ni kukutana na CDF kwa sababu alikuwa na mazungumzo naye ya mhimu sana maana nchi haikuonekana kuwa sawa kama ilivyokuwa zamani.

Ofisi hizo za makao makuu ya jeshi zilikuwa Lugalo, msafara wake wa gari mbili ulikuwa kwenye mwendo mkali sana. Alipita Ubungo pakiwa kimya mno hivyo walipitiliza mpaka Mwenge ambapo waliikunja njia ya kushoto kuelekea sehemu yalipo makao makuu ya jeshi. Walifika ndani ya eneo hilo lakini walikutana na kizuizi kizito sana cha wanajeshi ambao walikuwa langoni hapo.

Mama huyo alishuka na kutembea taratibu akiwa kwenye viatu vyake virefu kuelekea getini.
"Upigie simu uongozi wako waambie nahitaji kukutana na CDF"
"Nani wewe ambaye unataka kukutana na kiongozi mkuu kama unaenda kununua nyanya sokoni?"
"Mwambie mkuu wa usalama wa nchi ana mazungumzo ya mhimu sana na wewe" licha ya maelezo hayo lakini mwanajeshi ambaye alikuwa anajibishana naye hakuonekana kumuelewa hivyo akataka kumsukuma mama huyo arudi nyuma. Alifanya kosa la maisha, huyo mama hakuwa akiguswa na binadamu yeyote kipuuzi sana namna hiyo. Mwanajeshi huyo alivutwa mkono ambao ulikuwa unaelekea kuigusa suti ya mwanamama huyo kwa nguvu na kuzungushwa, ulivunjwa vibaya sana lakini haikuwa nafasi ya kuachiwa, mwanaume mmoja mwenye suti alimchota mtama mkali saa kisha mwingine alijigeuza kwa sarakasi na kuitua miguu yake kwenye kifua cha mwanajeshi huyo ambaye alienda kujibamiza ukutani na kutulia kimya. Wenzake walisogea wakiwa wanawaweka chini ya ulinzi wanaume hao na mwanamama huyo ambapo nao walizitoa bastola wakiwa mbele yake.

"Bwana mdogo amefanya kosa kubwa sana kutaka kunigusa kwenye nguo yangu, nitahesabia hili halijatokea lakini kama likija kutokea kwa mara nyingine tena basi hakuna kati yenu hata mmoja ambaye ataishi" aliongea kwa jazba sana mama huyo akiwa anaitoa simu yake na kumpigia CDF yeye mwenyewe moja kwa moja ambapo iliita ndani ya muda mchache sana na kupokelewa.
"CDF nina mazungumzo ya mhimu sana na wewe nipo getini hapa kwa sasa"
"Whaaat?"

"Waambie vijana wako waniruhusu niingie ama kama hautaki nambie niondoke" mwanamama huyo hakutaka kubembeleza sana baada ya kuongea hivyo aliikata simu na muda mchache sana mmoja wa wale wanajeshi aliipokea simu na kufungua geti akiwa kwenye mashaka makubwa sana. Waliingia kwenye magari na kuzama ndani ya kambi hiyo usiku huo.

"Naomba uwasamehe sana vijana wangu kama hawajakuonyesha heshima nadhani ni kwa sababu hawakufahamu"
"Shida sio kunifahamu mimi Gabriel tatizo ni kwamba hawatakiwi kuwa na majivuno kiasi hicho ni hatari sana kwa sababu wanafanya jeshi lionekane sehemu ya kutisha sana husuani kwa wananchi. Wape elimu vijana wako waache ujivuni watakuja kuishia pabaya sana"
"Hilo nitalishuguulikia mwenyewe, nambie ni kipi kimekufanya uweze kufika hapa usiku wote huu bila hata taarifa?"

"Nchi inaelekea pabaya sana hivyo nipo hapa kuhitaji msaada wako"
"Mhhhh haijawahi kutokea kwenye maisha yako ukahitaji msaada kwa mtu yeyote yule"
"Maisha yanabadilika sana ndiyo maana nipo hapa"
"Ni msaada upi huo ambao unahisi kwamba mimi naweza kukusaidia wewe?"
"Nataka nimchunguze raisi lakini nah......"
"Ebu subiri kwanza. Unamaanisha unataka kuanza kumpeleleza raisi wa nchi?"
"Yeah"
"Nadhani utakuwa haujamaanisha kile ambacho unakisema"
"Mpaka nafika usiku huu eneo hili basi ujue kwamba ninacho kiongea nina uhakika nacho"

"Cleopatra nadhani unashindwa kuelewa mipaka ya kazi ambayo unaifanya, unafikia hatua ya kutaka kumpeleleza bosi wako ambaye amekuweka hapo?"
"Na vipi kama mawazo yangu yapo sahihi juu ya kile ambacho nakiwaza na nahitaji kukifanyia kazi?"
"Kwahiyo unataka mimi nikulinde?"
"Hapana"
"Sasa unataka nini? nenda kwenye pointi ya msingi"
"Nahitaji makomando"

"Hahaha hahah hahah Cleopatra unajua kabisa kwamba hilo jambo haliwezekani hata kama ungekuja na nani hapa" mwanamama huyo hakuongea bali alirusha gazeti na picha kwenye meza kubwa ambayo ilikuwa mbele yao.
"Nadhani umepata taarifa juu ya mtu ambaye alitoa taarifa za kufungwa kwa Remy Claude ambaye nilimkamata mwenyewe lakini kijana wako kule gerezani nadhani unajua alicho kifanya mpaka akasababisha mtu huyu kutoroka na wewe ukaridhia kabisa kwamba gereza liwe chini ya shirika letu kwa muda ili kupisha uchunguzi. Unajua ni mambo gani ambayo hukuambiwa Gabriel?"

"Angalia hizo picha hapo, ni picha ya Bruno Josephat na moja ni picha ya kijana wako Luka Gambino ambaye mimi mwenyewe ndiye niliwahi kukushauri sana kwamba apewe nafasi nyingine na ikawa hivyo. Ila mpaka wakati huu ninavyo ongea na wewe hawa watu wote wawili wamekufa"
"Whaaaaat?"

"Yeah hawa wote ni marehemu na ndiyo maana nimekuja kuomba msaada kwako"
"Yaani bado sijakuelewa wamekufaje kufaje?"
"Baada ya kugundua kwamba kijana wako anawaingiza baadhi ya watu wanao mlipa kule kwa manufaa yake tulimkamata pamoja na Bruno ambaye tuligundua kwamba baada ya yeye kukutana na Remy ndipo mwanaume huyo alifanikiwa kutoroka huko kwa maana hiyo bruno ndiye alimsaidia kufanya hivyo"

51 inafika mwisho.

Febiani Babuya.
 
HADITHI: BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI
"Bruno baada ya kumbana sana alikubali hilo na kudai kwamba ni kweli yeye alimsaidia mtu huyo kutoka ili akamuokoe binti yake bila kujua kwamba kijana huyo alifanya hayo yote ili kuwapata watu ambao alikuwa anawatafuta kwenye maisha yake na Bruno ndiye alikuwa njia yake ya pekee kuwafikia"

"Ngoja kwanza, umesema alikuwa anawatafuta watu wake kwani huyo ni nani na kwanini awatafute watu hao na ni akina nani?" Cleopatra Gambo alichukua faili kwenye begi lake na kulirushia mezani.
"Taarifa zote zipo humo nikitoka hapa nadhani utapata muda wa kuzipitia mwenyewe sina muda wa kuanza kukusimulia tukio moja moja kwa kinywa changu. Naweza kuendelea?" CDF aliitikia kwa kichwa.

"Bruno alikiri na kudai kwamba alikuwa tayari kunipatia taarifa zote za siri ambazo zilikuwa nyuma yao na watu wote ambao walikuwa kwenye mzunguko wao lakini alihitaji kwanza mtoto wake awe salama"
"Unataka kuniambia hata wewe alikupa kazi ya kumsaidia mwanae wakati alimtuma mtu wa kwanza?"
"Ni baada ya kugundua kwamba mtu aliye mtuma ndiye alikuwa hatari zaidi kwake hivyo akaniomba niwahi kumsaidia mwanae"
"Na raisi ameingiaje sasa kwenye huo mzozo?"

"Nilikuwa na maswali mengi sana kwamba ni kwanini raisi ahusishwe na kukamatwa kwa huyo kijana huku mwandishi akimtaka akapige magoti kwa kuomba msamaha hadharani kwa kudaiwa kwamba alikuwa mmoja ya watu ambao walikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na kuuliwa kwa mfanya biashara Dominic Sawa sawa kwa zaidi ya miaka ishirini iliyokwisha kupita;"

"Baadae ndipo nikaanza kuunganisha doti baada ya Bruno kunipa maelezo kidogo na kuhitaji nimsaidie mwanae hivyo nilimuacha makao makuu na kuondoka lakini muda mfupi baadae raisi alienda kumuona Bruno kisha akamuona na Luka Gambino. Baada ya muda mfupi tu tangu yeye aondoke Bruno amekutwa amekufa kwa kumeza kidonge chenye sumu huku Luka Gambino akiuliwa na kijana wangu mmoja ambaye wakati nimeanza kumhoji naye alijing'ata na kumeza sumu kisha akawa amekufa. Nadhani mpaka hapo ulishajua kwamba ni kwanini nahitaji kumpeleleza mheshimiwa raisi"

"Cleopatra naona kabisa unajiingiza kwenye jambo baya sana, hiyo sio sababu pekee ya kufanya ufike mbali sana kiasi hicho hususani kwenye jambo ambalo hauna uhakika nalo kabisa kama hilo. Vipi kama raisi akijua? ujue mimi sitakuwa upande wako wala sitakuwa na namna ya kukusaidia kwa wakati huo utakuwa ni msalaba wako wewe. Kumchunguza raisi ni jambo la hatari mno kwa sababu hujui ni nani yupo upande wako na nani hayupo upande wako Cleopatra"

"Kama kuna jambo litanitokea basi nitakufa na tai yangu shingoni na mazungumzo haya chukulia kama hayajawahi kufanyika wala hii siku haijawahi kutokea na mimi na wewe hatujawahi kukutana kufanya haya mazungumzo ila nahitaji unipe huo msaada" Cleopatra alimuweka kwenye mazingira magumu sana CDF kuweza kufanya maamuzi kwani alikuwa anachezea karata mbaya sana ya Jokey wakati yeye alikuwa na karata za kawaida kwenye mkono wake.

"Cleopatra unajua baadae mimi mwenyewe naweza kukuua kama ikibidi?"
"Hilo naliambua kama itafikia hiyo hatua basi hakikisha unaniwahi kabla sijakufikia kwa sababu nitaiteketeza hii sehemu ila sipo tayari kuona nchi inazama halafu kiongozi wa nafasi yangu nisifanye jambo lolote"

"Fanya maamuzi yaliyo sahihi ili baadae tusije tukaingia kwenye mtego wa kuanza kuuana wenyewe kwa sababu mimi siwezi kuusaliti upande wa raisi na unalijua hilo"
"Sijali kuhusu hilo nataka kuilinda amani ya nchi yangu kwanza hayo mengine yatafuatia baadae"
"Kabla sijakupatia hawa watu unaweza ukaniambia kwamba wanaenda kufanya kazi dhidi ya mtu gani na ni kwanini?"

"Nataka wamtafute Remy popote alipo kwa gharama yoyote ile ili afungwe sehemu ambayo hatakuja kutoka kwenye maisha yake yote" jibu la mkurugenzi lilimshtua CDF ambaye akimsogelea karibu na sikio lake akiongea taratibu.
"Una wapelelezi bora sana na wenye uwezo mkubwa mno na wote tunalijua hili, sasa sababu ya kuwatumia makomando maana yake kuna mtu unataka asijue kwamba wewe ndiye umehusika moja kwa moja sio? Hahaha Cleopatra unataka kuniuzia msala kwa raisi au ni nani haswa ambaye hautaki aje kujua kama ni wewe ulikuwa nyuma ya hili?" Gabriel alikuwa amemshtukia kiongozi huyo juu ya huo mchezo ambao alikuwa anataka kuucheza. lengo kubwa la kuwatumia makomando lilikuwa kwamba hata siku mambo yakienda vibaya basi atakuwa nje ya msala kwani watu hao hawapo chini yake hivyo ingekuwa rahisi hata kuwakana mbele ya safari.

"Sio raisi ila ni mtu mhimu sana kwenye maisha yangu"
"Unataka kuniambia una ndugu yako ambaye yupo hai?"
"Huenda ila sina uhakika"
"Sasa kwanini hautaki ajue kwamba unahusika katika hili?"
"Ni mtu ambaye nilikula naye kiapo cha maisha juu ya hili jambo hivyo sitahitaji kabisa aje kujua kwamba mimi nimehusika na huu mpango. Nataka nimkamate huyu bwana mdogo na kumpeleka sehemu ambayo hata huyo mtu ambaye nimekula naye kiapo haji kujua kwamba imewahi kuwepo hapa duniani hivyo hatajua kama ni mimi nilihusika katika hili jambo kwani itaonekana ni makomando ndio ambao wanahusika na mimi sihusiki nao"

"Inaonekana kama unataka kunitengenezea ubaya na watu ambao siwajui Cleopatra"
"Ni mtu ambaye hana hata uwezo wa kuja kukuuliza juu ya jambo hili mpaka anakufa na hautakiwi kabisa kumfahamu pia"

"Who is she/he"
"Gabriel Adamson kama unanisaidia nisaidie kama hautaki nambie kwa sababu huyo mtu siwezi kukutajia jina lake wala utambulisho wake labda niwe nimekufa kwanza" CDF alimwangalia sana mwanamke huyo huku akiwa anasikitika sana.

"Nakupa makomando saba kwa sababu ya maelezo yako kwamba huyo mtu ni hatari sana. Hawa ni watu wa siri sana ndani ya jeshi na hawajulikani sana, kikosi chao kinaitwa NIGHTFALL ASSASSINS (NA). Mara nyingi huwa wanafanya kazi za mauaji hususani kwa wale watu ambao wanaonekana kulinyima amani taifa hili na ni miongoni mwa vikosi vya siri sana ambavyo vinategemewa na jeshi kwa sababu ni watu wenye mafunzo ya hali ya juu sana hivyo nakupa hawa vijana ila hakikisha unanirudishia kikosi changu baada ya hii kazi na sitataka kusikia habari zingine kwa sababu tutageukana sisi wenyewe" mwanamama huyo alimpa mkono CDF na kutamka.

52 inafika mwisho
 
2000 tu kumalizia mpaka mwisho 100.

0621567672 (HALOPESA).....WhatsApp

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

FEBIANI BABUYA
 
Back
Top Bottom