Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 14



Baada ya hapo mashine ilijifunga na kuwaka taa nyekundu ndani ya mashine hiyo. "nakutakia usingizi mwema" iliongea ile computer na ghafla usingizi mzito ukanichukua.
*****.
"We David si unakwenda kwenye interview leo" baba alifungua mlango wa chumba changu na kunishtua, nilikurupuka kutoka kitandani na kuangalia saa yangu ya mezani. Iliniambia saa moja kamili asubuhi, na natakiwa niripoti white house saa moja na nusu kwaajili ya hiyo interview.Hapo nilikuwa na miaka ishirirni na ndio kwanza nilikuwa nimaliza chuo kikuu katika cozi ya IT. Niliingia chooni haraka na kujisafisha kisha nilirudi chumbani kwangu na kuvaa suti aliyoninunulia baba. Hata chai sikunnwa nilitoka nduki mpaka kwenye gari yangu na kuelekea ikulu.
Dakika ishirini na nane nilikuwa mapokezi na kuelekezwa sehemu nnayo takiwa kuwepo, nilipofika nilishangaa kuona msururu wa vijana wakisubiri na wengine walikuwa wakitoka katika chumba cha interview huku machozi yakiwatoka, hiyo ilikuwa ni dhahiri kuwa walikosa kazi hiyo. NIkiwa katika hali hiyo niliskia jina langu likiitwa. Niliitika na kuelekea mlangoni, mlango ulifunguliwa nikaingia. Alinihoji maswali ya kawaida kwanza kisha wakanisogezea computer na kunambia nihack system ya white house, nilitabasamu kidogo kwa sababu kuhack ndio kitu nnachokipenda katika maisha yangu. Wakaniekea saa mbele na kunambia nina dakika tano tu za kufanya hivo.


Saa ilipobonyezwa tu na mimi nikaanza maujuzi yangu, kila nilivojaribu nilifika pahali nikakwama lakini baadae nilishtuka kama kuna mtu mwengine pia anahack computer ninayo tumia. kwanza lazima nimzuie halafu ndio niendelea na kuhack. Nilipoangalia saa niligundua kuwa dakika mbili na nusu zishateketea, niliongeza kasi na kufanikiwa kumzuia anaehack compuetr niliopewa ndani ya sekunde arobaini tu. Hapo niliongeza kasi mara dufu huku nikitumia ufundi wa hali ya juu kufanya kazi hiyo ngumu, dakika nne na sekunde hamsini na sita ndio muda niliomaliza kuhack na kufanikiwa. Kisha nikiwapa computer yao. Hawakushangaa sana, mmoja aliondoka nayo na baada dakika kadhaa alirudi huku akionyesha uso wa simanzi, mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio na kijasho chembamba kikaanza kunitoka. "samahani umejitahid sana lakini hujafikia kiwango tulichokitaka" aliongea na kunionyesha mlango uliokua na alama ya kutokea. Kiunyonge niliiuka na kuelekea kwenye mlango huo, lakini nilipoufungua nilishangaa kuona hakuna hata mtu mmoja aliekuwa akisubiria kuingia kwenye chumba hicho. Lakini sikutilia maanani kwani mawazo yote yalikuwa mbali sana nikikumbuka jinsi nilivyokuwa natamani sana kulitumikia taifa langu.
Ghafla nikiwa katika dimbwi hilo la mawazo kengele zinazoashiria hatari zilianza kulia, na kwa mbali niliona kikundi cha watu kikija upande wangu wakiona kama kuna mtu wanamlinda. Na kila walivyosogea niligundua kuwa alikuwa ni raisi, nilianza kuetetemeka huku nikishangaa, waliponikaribia mmoaja wao alinivuta na kunambia "mlinde raisi" nilitaka kumwambia kuwa mimi sio mlinzi lakini nilichelewa kwani risasi zilianza kurindika na kunibakisha nisiwe na chaguo zaidi ya kumlinda raisi lakin Ukweli hata kukamata silaha nilikuwa sijui. .
 
15.



Mambo yalikuwa magumu sana kwangu maana nilikuwa sijui nifanye nini kumuokoa raisi, japo mkono nlikuwa nauweza kidogo lakini sikuwa na moyo wa kupambana na watu wenye silaha kali. Ila nilielewa kitu kimoja kama sasa maisha ya raisi yapo miokononi mwangu, basi nilimshika na kuanza kutmimia nae lakini ajabu nilipoangalia nyuma wlinzi wote walikuwa chini, na sasa nilikuwa nafuatwa mimi na raisi. Nilifika pahali nikajibanza na kumvizia anaekuja, kwa kasi ya ajabu nilichomoka na kumpiga kikumbo kilichomfanya aangushe silaha. Hapo sasa ilikuwa ni mkono kwa mkono, nilichezea ngumi kadhaa nilifanikwa kumpiga katika sehemu ambazoni pressure point na kumzidi lakini sikumuuwa. Wakati nageuka tu nilimuona mtu akiwa na bastola na amemlenga raisi bala kuchelewa nilimuwahi raisi na kukinga mgongo. Niliskia tu mlio wa risasi lakini sikujua nini kimeendelea.

Nilikuja kushtuka nipo katika chumba kidogo hivi, na nilipoangalia pembeni nilishangaa kuwaona wale walinzi wote ambao nilidhani wamekufa. Hapo nikajua bila shaka niko kuzimu, "hongera kijana umechagulia kujiunga na kikosi maalum cha siri cha kumtumikia raisi wa nchi hii". Aliongeamzee mmoja aliekua pembeni ya kitanda hicho. Kisha akanipa mkono kuashiria nikae, "kesho fika ikulu saa mbili asubuhi na chunga kila kilichoanyika kiwe siri kisitoke nje ya chumba hichi" aliniambia na kunionya "yoyote atakae kuuliza unafanya kazi gani,mwambie kuwa wewe ni mlinzi tu wa ikulu" aiendelea kuongea. Baada hapo alikuja mtu mwengine na kunambia nimfuate nami nikafanya hivo bila kuuliza, alinipeleka mpaka nje na kunambia tukutane kesho.

Nilienda kwenye gari yangu na kurudi zangu nyumbani, nilipofika tu baba aliniuliza kama nimefanikiwa nikamjibu ndio. Basi akanipa hongera na kunambia sasa maisha yangu yameanza hapo, baada maongezi mawili matatu nilielekea chumbani kwangu kwa ajili ya mapumziko. siku ya pili mapema niliamka na kujiandaa, nilifika sebleni na kumsalimia baba maana ndie mzazi pekee nlokuwa naishi nae, mamaangu alishatangulia mbeleza haki siku nyingi sana. Baada kunywa chai niliaga na kuondoka kuelekea ikulu, huko nilipewa maelekezo yoote na kuambiwa kuwa nijiandae na safari ya kuelekea mafunzoni. Jioni nilirudi nyumbani na kumueleza mzee, alifurahi sana na kunipa baraka zote. Siku ya safari ilifika, sikuwa peke yangu nlikuwa na wenzangu wanne ambao pia walipata nafasi hiyo..

Kwa muda wa miezi sita tulikuwa mafunzoni na kwa kweli mafunzo yalikuwa magmu sana kiasi kwamba kuna wakati nilijuta kukubali kazi hiyo. Wote watano tulipewa mafunzo ya sniper na kiukundi chetu kikapewa jina la "suicide squad" (kikosi cha mauaji). tulipikwa tukapikika mpaka tukaiva. Nikiwa nimebakiza mwezi mmoja tu kumaliza nikapokea habari mbaya sana, baba yangu alipata mshtuko wa ghafla nakupoteza maisha. Nililia lakini mwiso nikakumbuka msemo mmoja ambao mzee alipenda kuutumia "Maisha ni safari na wote tunapita, kama ilivyo hatuwezi kuchagua tuzaliwe na nani na siku gani ndio hivyo hivyo hatuwezi kuchagua tufe vipi na kwa muda upi". Maneno hayo yaliibadilisha hali yangu kunipa moyo wa chuma. Hatimae tulimaliza mazoezi na kutambuliwa rasmi na raisi wa nchi hiyo.
 
16.


Mwisho niliitwa katika chumba fulani hivi na kupewa picha, ilikuwa na maelezo nyuma. Nilitakiwa kumuua huyo mtu kwenye picha, nilipewa sniper na risasi moja tu. Jaribio hilo ni la kufa au kupona maana nikimkosa atanishambulia mimi. Nilijiandaa na mapema siku ya pili nikapanda ndege kuelekea Moscow Russia, kama kawaida nilimfuatilia mpaka niliporidhika na taarifa nilizochuma ndio nikaamua kumtenda. Nilitafuta jengo moja refu jirani sehemu anayopenda kukaa usiku, niliiunnga mtambo na kuingiza risasi ile kisha nikaikoki na kuanza kumlenga, sikutka kupoteza muda nilfyatua risasi na iliopita sawa sawia katika paji la uso. Kisha haraka nikakunja sniper yangu na kusepa.
Nilirudi na kupokewa kwa shangwe na kuanzia siku hiyo ikawa ndio kazi yangu, kuuwa kwa sababu ya raisi. Ukweli niliingia katika mapenzi mazito na kazi hiyo, maana mwisho nilikuwa naona kuuwa kwangu ni kitu cha kawaida sana. Lakini tulivyo binaadamu tumeumbwa na moyo wenye kupenda, miaka mitatu ilipita na ndipo nilipokutana na mwanadada mmoja alieitwa Melinda. Nilitokea kumpenda sana, na nilimueleza hisia zangu juu yake. Mwanadada huyo mmarekani mwenye asili Yahudi, mrefu wa wastani, macho yenye kiini cha buluu kilichokoza na mcheshi kupita maelezo alinikubalia ombi langu na muda si mrefu tukafunga ndoa japo kuwa shirika langu walikubali shingo upande lakini ndio hivyo moyo ulishapenda.
Ndoa hiyo ndio ilionifanya nigundue kuwa kazi nnayofanya si nzuri hata kidogo lakini kuiacha ilikuwa siwezi kwa muda huo. Mke wangu alipo niuliza kazi nnayo fanya nilimdanganya na kumwambia kuwa nafanya kazi kama mtu computer tu. Na hakuwahi kuinyesha kama nlikuwa namdanganya, alikubali bila kpingamizi. Maisha yaliendelea kuwa mazuri na yenye fuaraha na amani tele ndani ya nyumba yangu, hatimae mwaka mmoja ulikata tukafanikiwa kupata mtoto wa kike, tulimwita Christina. Kwa kweli furaha yangu ilikuwa sio ya kitoto maana dah hata kueleza nashindwa, nikiwa katika furaha hiyo nilipigiwa simu kuwa raisi anataka kusafiri kuelekea Syria kwa ajili ya mazungumzo hivyo nikuwa nahitajika kwenye msafara huo.
.
Nilimueleza mke wangu, alikubali japo hakupendezwa na mimi kuondoka siku muhimu kama ile. Nilimbusu yeye pamoja na mwanangu na kuondoka kuelekea ikulu kwa ajili ya safari, kumbuka huu ni mwaka wa nne tokea niwe sniper. Muda wa safari ulifika tukapanda ndege na safari ikaanza, kilichonishangaza ni kwamba inakuaje masniper wote watano tumechukuliwa na hiyo sio utaratibu wa kawaida. Lakini hakuna alioongea, nakumbuka tulipewa kikombe cha chai kwa ajili ya kupasha tumbo, ila baada ya kunywa funda moja tu nilianza kuona mawenge na hatimae nikapoteza majira.
 
17.

Sikujua chochote kilichoendelea, nilikuja kushtuka nipo kwenye jengo moja refu sana huku nikiwa tayari jicho langu lipo kwenye daubini ya sniper yangu. Pembeni kulikuwa na simu ghafla ikaingia sms ikinambia kwa kuna watu wamevaa nguo sare na wapo wanne niwauwe wote. Bila kuchelewa niliwatafuta lakini kilichonishtua baada kuwaona ni watoto wadogo umri kati ya miaka kumi hadi kumi na tano. Sikuwahi kuuwa mtoto na kila nilivojaribu kujiizia akili yangu haikuwa tayari kukubaliana na mimi na bila kuchelewa niliafyatua risasi tano tena kwa kasi ya hali ya juu na kuwauwa wote lakini baada kufanya hilo machozi yalianza kunitoka.
Nilikunja kila kitu changu na kuondoka eneo hilo, maswali mengi yalinijia kichwani na kukosa majibu. Kilichonishtua zaidi nilikuwa hata sijui niko wapi lakini nilikuwa nikitembea tu mpaka kwenye gari na kuingia kisha nikaondoka zangu. Kwa kweli nilianza kuhisi kama naendeshwa sasa maana mambo yote hayo sijui yalikuwa yanatokea vipi. Nilifika kambini na kuwataarifu kuwa kazi imefanyika na kukamilika, lakini nilipotaka kuuliza imekuwaje nikauwa watoto mdomo ulikuwa mzito na hivyo kushindwa kuuliza. Tuliambiwa tukunje kila kitu safari ya kurudi nyumabni ilikuwa imewadia, kwa furaha nilokuwa nayo nilijianda huku lengo langu ni kuwa kuonana na mke wangu na mtoto wangu ambae amezaliwa siku chache zilizopita.

Jambo la kwanza baada kutua marekani niliaga na kuelekea nyumbanni, lakini nilishanga kuona mazingira yamebadilika sana kilichonifanya nishtuke sana. Niligonga mlango, mke wangu alifungua lakini hakuonesha furaha hata kidogo badala ya kunipa salamu alitandika kibao kizito shavuni jambo lilinishangaza sana. Kisha akaongea "sasa ndio nini kuniacha peke katika kipindi ambacho nilikuwa nakuhitaji zaidi", "sasa mi si nimeondoka juzi tu" nilimjibu kwa mshangao, "juzi gani inamaana hata hujui leo ni siku gani" aliniuliza kwa mshangao pia. Na kwa kweli nilikuwa sijui "tokea uondoke siku ile niliojifungua mpaka leo ni mwaka mzima umepita" aliongea na kunifanya nitoe macho kama mjusi aliebanwa na mlango..
Kwakweli nilihisi kuchanganyikiwa maana sikutegemea kama muda ambao nilikuwa nje ni mkubwa hivo. Lakini ni kweli hata mwanangu christina alikuwa tayari anaweza kukaa, hasira ilianza kunipanda na ile furaha yangu yote ya kukutana na familia yangu ilitoeka. Siku hiyo ilipita kwa mtindo wa kulazimisha tabasamu, siku ya pili kama kawaida nilienda kazini lakini nilikwenda kiugomvi ugomvi tu. Sikumpa hata mtu mmoja salamu wala kumuuliza hali na wote walioniongelesha niliwalia bati tu, wakubwa wangu waligundua kuwa mda wowote ule mtu atakaonizingua basi atakiona cha mtema kuni. Wakati nikiwa katika ofisi yangu alipita mtu mmoja na kuniangalia sana kisha akaondoka na alipofika mbele nilimsikia akimwambia mtu "jamaa kawa kama mbwa sasa maana akiambiwa uwa basi haulizi, anafanya tu" maneno yalinitia hasira na kujikuta nikiinuka na kumfata na nilipomkaribia nilimsalimia kwa ngumi mbili nzito za uso zilizomtia mawenge na kumtupa chini.
 
18




Niliendelea kumshushia kipondo, kwa mbali nikamsikia mtu akiniambia "acha" kwa ukali, nikshangaa kuona mwili wangu unatii amri hiyo. Kisha akanambia "Njoo" basi nami nikafanya hivo na nilipofika alipo akaniambia "kaa" nami nikakaa, yote hayo niliyafanya bili akili yangu kufanya maamuzi yoyote yale. Nilihisi kweli sasa nimekuwa mbwa maana siwezi kukataa amri yoyote ntakayopewa, nilitamani kulia lakini mbele za watu ingekuwa aibu. Hali hiyo ya kuendeshwa kama mbwa iliendelea kwa muda mrefu takriban miaka mitatu, kuna wakati nilitumiwa sms usiku nikiwa faragha na mke wangu. Nilijikuta naacha kila kitu na kuelekea kazini. Hali hiyo iliitia dosari familia yangu na furaha ilitoweka, siku moja mke wangu akaniambia kuwa anahitaji kwenda kuwaona wazazi wake Miami. Na kwa hali ilivokuwa ikiendelea ndani ya nyumba yangu nilihisi nisipomruhusu basi ndoa yangu ingevunjika, nilikubali na siku ya pili mapema akaondoka pamoja na mwanangu.
Ukweli niliwalaumu sana kitengo changu kwa kuniharibia maisha yangu, maana nilikuwa sina maamuzi tena juu ya maisha yangu. Siku zilipita, na wiki zikakata na hatimae mwezi bila kuiona familia yangu, niliomba ruhusa na kuelekea miami kwaajili ya kuungana na familia yangu. Nilikubaliwa nasiku ya pili mapema nilifunga safari ya kuelekea huko, nilifurahisi sana kuonana na mke wangu, wakwe zangu pamoja na mtotot wangu ambae alishkilia kusema "baba umeniletea pipi". Nilimkabidhi mfuko mzima wa pipi kutokana na uchovu wa safari nilitaka kupumzika, mke wangu akanipeleka kwenye nyumba nyingine. Aliniandalia maji na kuniogesha kisha akaniandalia chakula na pia alinilisha, kwa kweli nilishangaa sana alifanya yote hayo utadhani mtu aliekuwa anakaribia kuiga dunia. Kisha alinisindikiza kitandani na yeye akiwa pembeni yangu na bila kuchelewa tukajikuta tupo katika huba za dunia. Baada jambo hilo nilipata usingizi mzito sana uliojaa ndoto nzuri, nilikuja kushtuka asubuhi baada kusikia kelele za watu na kwa mbali kupitia dirisha langu nikawa naona moshi mzito sana. Nilivaa nguo haraka na kutoka nje ili kama kunahitajika msaada nitoe. .
Sikuamini kama ilokuwa inangua ni nyumba ya wazazi wa mke wangu, nilijikutanikienda mbio na kuingia ndani bila kujali kama ningeungua au laa. Nilichokutana nacho ndani ndo kilonifanya nikaishiwa nguvu, miili minne ilikuwa chini, na kwa haraka niliitambua yote kuwa ni ya wakwe zangu,mke wangu pamoja na mtoto wangu. Nilipoangalia vizuri niligundua kuwa bado mke wangu alikuwa hai, nilimfata nimbebe lakin akanishika mkono na kutaka kunambia kitu "CODE....." hakuwahi kumalizia alikata roho. Machozi ya lianza kunitoka na kujikuta napoteza fahamu."
Nilizinduka kutoka katika usingizi huo huku jasho likinitoka kama maji, "karibu tena duniani MR Allen James" niliiskia ile computer ikiongea, "ile ni ndoto au" niliuliza kwa mshangao. "hapana yale ni maisha yako kabla ya kuitwa Allen James, zote ni kumbukumbu za maisha yako ya nyuma". Nilishindwa kujizuia na kuanza kulia kama mtoto mdogo, lakini swali lilikuwa ni nani alieiteketeza familia yangu yote.
 
19
Nikiwa katika dimbwi hilo la mawazo nikaskia "na kuna ujumbe wa mwisho aliuwacha mke wako". Nilishuka kitandani na kuelekea kwenye meza ilioluwa na computer na punde ulifunguka ujumbe kwenye computer hiyo uliosema hivi.


"Mpendwa mume wangu najua utadhani nilikuwa nakasirika kwa jinsi ulivyobadilika, laa sikuwahi hata siku moja kufikiria hivo. Matatizo yote uliokumbana nayo chanzo ni mimi na timu yangu yenye wanasayansi ishirini, tulipewa tenda ya kutengeneza kemikali ambayo itamfanya mtu atii chochote atakachoambiwa bila kuuliza sikujua kama na wewe utakuwa ni mmoja wapo naomba unisamehe kwa hilo. Siku ile uliorudi kutoka safarini baada mwaka mzima kupita, niligundua kuwa huko sawa hivyo usiku nilikutilia dawa ya usingizi ili niweze kuchukuwa damu yako na kuipima nilichogundua kilinitisha sana hivyo niliandika ripoti na kuiwasilisha ikulu kwa lengo la kupewa kibali cha kuteneza dawa yake. Lakini raisi alikataa kuniruhusu kufanya hivyo kwa ajili ya maslahi yake mwenyewe, Kwa kweli niliumia sana na nikaamua kufanya kazi hio bia ruhusa. Pia nilichogundua kuwa ni kwamba hakukuwa na dawa yoyote inayoweza kuizimua kemikali hiyo hivyo nikaamua kutengeza tena kemikali kama hiyo ila hii ilikuwa tofauti kidogo kwa maana iliweza kumpa uwezo mtu uwezo wa kujenga hoja. Kwa muda wa miaka mitatu nimekuwa niifanyia uchunguzi wa kina kemikali hiyo nilioipa jina la CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X (C.O.D.E.X). Baada kuridhika na majibu hayo ndio niliamua kuja Miami ambapo ndipo zilipo maabara zangu. Lakini kuna mmoja kati ya wenzangu kwa tamaa ya fedha alivujisha siri hii kwa raisi hivyo amri ya kuuwawa wewe pamoaja na familia yako yote ikatolewa. Na ulivyoomba likizo tu wamekupa bila maswali hiyo ni kwa sababu walitaka wafanye tukio hilo liwe kama ajali ya moto. Siku uliofika tu usiku wakati umelela nilikuingiza maabara kwa siri na kukufanyia operesheni ndogo ya jicho la kushoto na kukuingiza kifaa kidogo ambacho kilikuwa na kemikali hiyo. Na niliiset computer ikiwa nitakufa basi, kemikali hiyo iachiwe kidogo ili kuzifuta kumbukumbu zako na uanze maisha mapya kama Allen James. Na kuhusu mtoto wetu usijali yuko hai na yupo na wazazi wangu Califonia. Ile miili mitatu ilikuwa ni ya kutengeneza tu ila mimi nimeona bora nife kwa sababu mimi pekee ndie ninae jua kitu gani nimekiongeza katika kemikali ile na kuifanya iweze kumpa mtu uwezo wa kuhoji tafauti na awali. WAKO MPENDWA MELINDA"
Nilijikuta nikitokwa na machozi baada kuisoma barua hiyo, huku nikijiuliza kwanini watake kuniuwa wakati nilifanya kila walichotaka. Au kwasababu mke wangu ametaka kunipa uhuru tu "nakuahidi Melinda muhanga wako hautoenda bure, lazima watalipa kwa kila walichotutendea, nitauwa mmoja badala ya mwengine mpaka niwamalize wote waliohusika na kifo chako na mateso yangu" nilijikuta nikiongea kwa hasira kisha nikaipiga meza ngumi na kuivunja. Mi mwenyewe nilishangaa kisha nikasema "pia asante kwa zawadi ulionipatia",
 
20
"sasa Mr David ingia store kwa ajili ya kuchukua silaha kisha utoke kabisa katika nyumba hii maana muda si mrefu italipuka, na pia fuata akili yako itakapokuelekeza" iliongea ile comuter na ghafala taa nyekundu zikaanza kuwaka, bila kuchelewa niliingia store na kukusanya kila kitu ambacho nilihisi kingenisaidia katika kazi yangu kisa nikatoka nje na kuelekea gereji na kuchukua gari aina ya Jeep, niliiwasha na kuondoka. Sikufika hata mbali niliskia mlipuko mkubwa na nilipangalia ile nyumba yote ilikuwa inatekeketea kwa moto. Nilitafuta nyumba nyingine hukohuko Miami na kuhifandhi silaha zangu kisha nikaelekea uwanja wa ndege na kukata tiket ya kueleke Califonia kwa ajili ya kumuona mwanangu.
Muda wa safari ulifika na ndege ikaondoka, safari nzima kwangu ilikuwa ya unyonge na hatimae ndege ilitua Califonia na kwa msaada wa kitabu nilichokicukua niliweza kufika kwa wakwe zangu lakini sikutaka wajue kama niko hai mpaka nitakapomaliza kazi yangu. Kwa mbali nilimuona binyi mdogo kati ya miaka nane na kumi, kwa kweli alikuwa kafanana na mama yake kama katolewa photocopy. Nilitamani kwenda kumkumbatia lakini haikuwezekana kabisa hivo nilimuangalia kwa mbali huku nikibubujikwa na machozi kisha nikajisemea "nisubiri mwanangu muda si mrefu tutaungana tena" kisha nikageuza na kurudi uwanja wa ndege na kurudi Miami. Nikiwa Miami nilianza kufuatilia nyenendo za kila aliehusika na yalionikuta, na kwa kweli kemikali iliyokuwemo kwenye mwiliwalngu ilinisaidia sana maana iliugeza ubongo wangu na kuwa unafanya kazi kama computer. Baada mwezi mmoja nilipata majina thalathini jina la aliekuwa raisi likiwemo, nilianza kujipanga sasa kwa ajili ya ukatili wa hali ya juu. Nilikusudia niwamalize wote ndani ya muda mfupi sana ili nikaungane na mwanangu pamoja na mke wangu mtarajiwa Tania. Niliondoka Miami siku ya pilia asubuhi na kuelekea mjia wa macasio yaani Las Vegas, huko kulikuwa na watu sita katika list yangu.
.
Nilifika nikakodi nyumba na kuanza mikakati yangu, usiku nilipumzika na asubuhi mapema nikatoka na kuelekea maabara anayofanya kazi yule mwanasayansi aliemuuza mke wangu wangu kwa rais. Nilivomuona tu hasira zikaanza kunipanda, nilitamani nimfate nikamkate vipandevipande halafu nimlee kwa wali mchana. Lakini nilijizuia, kwa vile niliiona gari yake nilisubiri aingiendani nikamuwekee ujumbe mdogo tu. Baada kungia ndani nilifanya hivo kisha nikakaa kwenye mgahawa pembeni, hakupita muda alitoka na kuingia kwenye gari yake huku akitabasamu. Nikajisemea

"laiti ungejua kama leo unakufa wala usingetabasamu", aliondoa gari kwa mwendi mdogo na mimi niliingia kwenye gari yangu na kumfata kwa yuma. Nilipohakikisha amefika mbali kiogo nilitoa simu yangu na kumpigia kwa simu ambayo nilimuekea kama zawadi kwenye gari yake, ilichukua muda kupokewa na alipoipokea alianza hivi

" vipi kuna tenda nyingine nini maana nyinyi kwa kuniwekea simu hamchoki",

"ndio dokta kuna tenda nyingine" nilimjibu.
 
21

"ok nambie nikufanyie kitu gani",

"unamjua David Robert Mccanoo" nilimuuliza,

"ndio si yule mpumbavu" alijibu huku akicheka.

"sasa tumepokea taarifa kuwa hakufa siku ile na hivi sasa yupo nyuma anakufatilia" niliongea hivo ili kumtia hofu, nilimuona akianza kuongeza mwendo.

"huna haja ya kuongeza mwendo bwana mkubwa kwa sababu hivi sasa unaongea na David".

"natumai mungu atakulaza mahali panapostahiki" nilongea kisha nikakata simu na hapohapo gari yake ikalipuka na huo ndio ukawa mwisho wake. Watu wengi walikusanyika katika ajali hiyo mimi nilipita na kueleke nyumba niliokodi, niliinfia ndani na kuipiga yake mstari mwekundu nikiimanisha kuwa kazi yake imekwisha.


Usiku nilitoka na kuelekea katika Casino, kama kawaida huwa siendi pahali kama hakuna kitu nnachohitaji. Niliingia ndani kuanza kuangaza huku na kule na hatimae nikamuona mlengwa mmoja, nilisogea mpaka katika eza aliokaa na kukaa meza ya pembeni yake. Kwa sababu nilijua nimtu wa madawa hivo nilitoa kipakti kidogo chenye unga mwupe mezani, alipokiona tu alinipa ishara nimafate bila kuchelewa aliinuka na mimi nikamfata. Alielekea chooni na kwa furaha kubwa nikmfata, nilipofika nilimkuta akinisubiri, nilimpa kile kijipakti nae alikipokea kwa shange na kuchana kisha akalamba ule unga kidogo, "kiasi gani" alinuliza, " nilimuangalia kisha nikamjibu "bei yake ni maisha yako" hapohapo akaaza kutoka damu maskioni,puani,mdomoni na kuanza kukakamaa. nilitoka chooni na kutoka nje kabisa ya casino na kuenda zangu nyumbani kupimzika nikiwa nimebakiza watu wanne tu katika orodha waliokuwepo Las Vegas.
Asubuhi ilifika na bila kuchelewa nilitoka kuelekea kukamilisha kazi yangu maana nilitaka siku hiyo hiyo nisafiri kuelekea Moscow Russia. Na kwa bahati nzuri nilwafumania watatu wakiwa pamoja, katika mgahawa fulani hivi, nilikwenda kukaa pembeni yao na kuagiza kifungua kinywa huku nikiwaangalia kwa makini wanavyofurahia chai yao ya mwisho. Walimaliza na kuinuka kisha wakaondoka, bila kuchelewa niliinuka na kuanza kuwafata mpaka walipoicha njia kubwa na kupita vichochoroni. Kwa vile nyuma sikuwa peke yangu hawakunishtukia, walitokea barabara nyingine kubwa na kuza kwenye kundi la watu na hapo nikaona muda muafaka wakutekeleza mauji ya kisayansi. Kwa mweno wa haraka nilikatiza kati yao na kuwachoma vishindano vidogo nyuma kweye shingo zao. Vishindano hivyo vilikuwa na sumu kali sana inayosababisha mwili kupoteza mawasilia na akili kukosa damu safi, vinauwa kwa sekunde thalathini tu. Ghafla wote walianguka chini na kuanza kupaparika kama samaki waliotolewa majini, nilitabasamu na kabla askari hawajafika katika eneo hilo nilitoweka kama vumbi..
Nilirudi katika nyumba niliokodi na kupanga kila kitu changu kwaajili ya safai ya Moscow, baada kuridhika na kila kitu niliekea uwanja wa ndege na kukata tiket ya usiku kuelekea Moscow. Nilirudi na kuchukua sniper kisha nikaelekea mahala ambapo ningemkuta mtu huyo. Nilifka eneo hilo na kumsaka, kwa mbali nilimuona akitoka katika jengo moja hivi. Nilitafuta gorofa la karibu na kuipanga sniper yangu. Lakini hii ilikuwa tafauti na zile za kawaida, hii ilikuwa ikiendesha kwa computer, baada kumaliza kazi hiyo nilitoa simu yangu na kuiconnect na GPS ya sniper hiyo kisha nikashuka chini na kuelekea alipokwa amesimama. Nilimpa salamu na kumuomba tuongee kidogo, alikubali na tukasogea pembeni.
 
22.

"unajua Mr Hudson upo katika hatari" nilimwambia huku nikijifanya nina wasiwasi, "we nani" aliuliza kwa sintofahamu. "kweli umeenisahau mr" nilimuuliza huku nikimakzia macho, aliniangalia kwa makini kisha akshtuka kidogo na kusema "haiwezekani, wewe ulishakufa siku nyingi" alongea kwa kitete. "vipi kwani unasema nimekufa mbona niko mbele yako" niliongea huku nikisogea pembeni na kumuweka usawa wa sniper ambalo nilikuwa nalicontrol kwa kutumia siku yanugu ambayo nilikuwa nimeshika mkononi na nilipoitazama ilinambia "target locked" kisha nikabonyeza kitufe cha kupiga simu na hapohapo ukaskika mlio wa bunduk, Mr Hudson alianguka vhini huku akiwa na tundu la risasi katika paji la uso kisha nikabonyeza kitufe cha kukata na ghafla sehemu iliokuwepo sniper uliskika mlipuko mkubwa. Kisha nikaungana na watu waliokuwa akikimbia hovyo na kutokomea.

nilirudi katika nyumba niliopanga na kuchukua mabegi yangu, nilirudisha funguo na kuaga kisha nikaondoka. Nilifika uwanja wa ndege na kupanda, hatukukaa sanaa ndege iliacha ardhi na kuwa angani kueleke Russia. Moyoni nilikuwa na furaha sana na pia nilikuwa na majonzi makubwa juu ya mke wangu, usingizi ulinichukua na kulala fofofofooooo. Nilishtushwa na mtingisiko uliotokana na ndege niliopanda kwenda chini kwa kasi sana, nilishtuka baada kusikia kelele za watu wakisali kwa lugha wanazozojua wao wenyewe. Mimi sikuwa mgeni kwenye matukio hayo kwa sababua si mara ya kwanza kupata majanga ya ndege. Kwa mbali nilimsikia rubani akisema tutulie kwenye siti zetu, ndege inatua kwenye maji. Bila kujishauri niliukaza mkanda wangu na kuinama kama maelekezo yanavyosema wakati wa dharura kama hiyo unatakiwa kuegemeza kifua chako kwenye magoti ili kuepuka mgandamizo na mara ndege iligota kwa nguvu juu ya maji na kwa umakini marubani wa ndege hiyo waliweza kuituliza isibiringitie na hatimae tuligota ufukweni. Mlango ulifyetuka na wote tukaabiwa tutoke haraka na bila kuchelewa watu walianza kukimbilia mlangoni, mimi nilitenbea taratibu mpaka nilipofika na kuruka kwa msaada kifaa maalum cha dharura niliteleza mpaka chini.
Hata tulikuwa hatujui tuko wapi maana sehemu ndege ilionguka ilikuwa ni kisiwa tu, baadhi ya abiria walipata majeraha makubwa na kwa wakati huo walikuwa wakipewa huduma ya kwanza. Mimi binafsi sikuumia sana zaidi ya michubuko midogo midogo tu, wakati nikiendelea kutafakari wapi tulipo niliskia kelele kutoka kwenye ndege. Kulikuwa na mtu akiomba msaada ilibidi nisikilize kwa makini sana ili kujua sauti hiyo ilikuwa ikitokea upande gani. Ghafla nilijuta nikitimka tu bila kutarajia kueleleka kwenye ndege, niliparamia lile dude la kuteleza kwa kasi ya ajabu sana japo kuna wakati niliteleza lakini sikukata tamaa. Niliingia ndani ya ndege moja kwa moja na kugundua kuwa sauti ilikuwa inatokea chumba cha rubani, kwa haraka niliusigelea mlango na kuupiga push mara kadha kabla ya kufunguka.
 
23.

Niliingia na kuwakuta marubani watatu wakiwa tayari washaaga dunia na mmoja alionekana ni mweny maumivu makali sana, nilitumia nguvu zangu zote kumtoa katika kiti na kufanikiwa. Baada ya hapo nilimsaidia kwa kumshika begani na kutoka nae nje kisha tukateleza mpaka chini, watu walimpokea na haraka akaanza kupatiwa huduma ya kwanza.
Kwa vile ndege ilianguaka usiku, tulisubiri mpaka asubuhi ili kujua tuko wapi. Kulipambazuka bila kupata hata lepe la i usingizi maana mipango yote nilihisis huenda ikaharibika. Kwa msaada wa black box ambayo inapitikana kwenye ndege tuliona meli na helicopter zikija kwa ajili ya uokozi. Baada ya kutua tu jambo la kwanza nilimbebba rubani ambae hali yake ilikuwa mbaya sana na kumpeleka kwenya helicopter na hiyo pia iliniaptia njia ya rahisi kuingia keny helicopter hiyo na punde ikaruka. Ilielekea moja kwa moja mpaka hospitali ya Saint Petersburg, alishushwa na kuwahishwa chumba cha wagonjwa mahututi huku mimi nikipelekwa kwa ajili ya kupata matibabu madogomadogo. Ukweli sikutaka kukaa hapo hospitali maana nilikuwa na haraka sana, niliwaambia mimi ni mzima na nina uhakika ndugu zangu watakuwa wananisubiria Moscow. Walinielewa na kwa msaada wa helicopter nilipelekwa mpaka uwanja wa ndege na kupandishwa ndege ya mmuda ule kuelekea Mjini Moscow. Masaa machache baadae tulituwa Moscow na moja kwa moja nikaelekea hoteli na kuchukua chumba, nilioga na kubadili nguo kisha nikapumzika. Jioni nilitoka kama kawaida kuelekea mawindoni..
Nilipita duka la silaha na kununua silaha ambazo zingetosha kukimu haja zangu ikiwemo shot gun pamoja na AK47 na sniper pamoja na bastola ndogo mbili. Kisha niliondoka hapo na kuelekea internate cafe, niliwasachi watu nnao wataaka nikagundua kuwa wapo wawili tu. NIlirudi hotelini na kujipanga vizuri kwaajili ya kazi siku ya pili, nilila mapema usiku huo. Mapema siku ya pilia asubuhi nilielekea ubalozi wa marekani uliokuwepo Moscow kwa sababu mmoja alikuwa anafanya kazi hapo. niliziweka silaha zangu sehemu nzuri na kuingia ndani, nilimtafuta pande zote lakini sikumuona. Baada kugundua hayupo nilitoka nje kwaajili ya kujipanga upya, bahati alikuwa ndio kwanza anashuka gari bila kuchelewa nilielekea upande alipo na kumpiga kikumbo kisha nikamuomba samahni. Alikubali na kuelekea zake ndani, lakini kikumbo kilie hakikuwa cha bure. Katika simu yangu kuna programa inayoniruhusu kuiconnect na simu nyingine pindi zinapo gongana tu. Na kwa vilie alikuwa anaongea na simu wakati tunagongana, simu yake ilianguka na kwa kasi ya ajabu niliitoa simu yangu na kuikutanisha na yake hapo ikawa tayari nishaivamia sim yake.
Nilielekea sehemu nilioficha silaha zangu na kuzichukua kisha nikapanda katika gorofa lililokaribu na ubalozi huo.
 
24.

Nilipofika juu nilianza kuipanga sniper yangu na kama kawaida huwa naweka risasi moja tu katika mtutu huo, kisha nikaangalia simu yangu nikagundua sehemu alipo basi na mimi nikabadilisha upande na kuelekea kule ambapo ntampta vizuri kabisa. Baada kuridhika na nafasi niliokaa nilianza kumlenga kwa kutumia darubini ya sniper mpaka pale nilipohakikisha yupo katika kumi na nane zangu. Nilifyatua risasi na kukisambaratisha kichwa huku nikitabasamu kwa kazi nzuri.
Nilirudi hoteli niliopanga na kupumzika huku nikitafakari jinsi ya kummaliza aliebakia, usingizi ulinichukua na ndoto zangu zilikuwa ni za kumwaga damu tu. Asubuhi nilirauka mapema na kupata kifungua kinywa na kutoka kuelekea kwenye kazi ilionipeleka nchini humo. Najua mtajiuliza pesa napata wapi lakini ukweli ni kwamba kutokana na asili ya kazi yangu mimi nina uraia wa nchi nyingi sana takriban nchi zote za zinazounda bara Europe.


Nina uraia wa England, France, Italy, spain na nyingine nyingi tu, na pia nina account nyingi tu ambazo zinapesa za kuniendesha kwa muda wa miaka zaidi ya thalathini mbele kwa sababu kila kazi nilipewa nililipwa mpunga mrefu sana kiasi kwamba hata kama ningesema niache kazi ile basi nigeweza kuishi kwa muda mrefu bila kupata tatizo la pesa. Basi nilianzakuzunguka huku na huko kutafuta kitu ambacho kitanipa muelekeo nianze wapi katika kumsaka huyo mpuuzi. Baada kuzunguka muda mrefu bila mafanikio yeyote yale hatimae nilikutana na gazeti lilisoma kuwa bado the BERGS ni tatizo uturuki, habari hyo ilinivutia na kulinunua gazeti lile. Habari ya ndani katika gazeti hilo imesema kuwa

"bado kikundi cha THE BERGS kinachoongozwa na Louise Millano ni tatizo kwa nchi ya urusi, wamefanya uhalifu katika kampuni kubwa ya vifaa vya umeme na magari" niliishia hapo kusoma maana mtu niliekuwa namtafuta ndie mkuu wa kikundi hicho cha majambzi. Na moja kati ya sera za kikundi hicho ni kwamba ukimapiga mmoja wanakuwinda na hawapumziki mpaka wahakikishe na wewe umekufa.

Akili ilinichemka huku nikiwaza ni mbinu gani nitumie ili kumfikia na kutenda nnachotaka kutenda. Nilianza kufwatilia nyendi zao kwa uakribu zaidi na mwisho nikafikia maamuzi ya kujiunga nao ili niweze kutekeleza kazi yangu. Basi niliendelea kuwafatilia chini kwa chini na siku moja nilikuwa nje ya bank moja hivi, ghafla ilisimama gari moja hivi aina mercedes banz nyeusi na kushuka watu watatu na kuingia bank. Baada dakika kama mbili hivi walitoka na kuingia kwenye gari yao na kuondoka kwa kasi ya ajabu bila kuchelewa niliingia kwenye gari yangu na kuanza kuwafata kwa nyuma. Loooo hawakufika mbali wakagongwa pembeni na gari ya askari, walitoka kwenye gari huku wakimimina risasi na kuwaua maaskari waliokuwepo kwnye gari ile.
 
25.
Bila kuchlelewa nilipita mbele yao na kusimamisha gari na kuwaambia waingie kisha nikaondoa gari kwa kasi huku nikifwata na gari kadhaa za polisi. Lakini kutokana na ufundi wangu mkubwa katika usukani nilifanikiwa kuwatoroka polisi na kufika sehemu salama kisha nikasimama na kuwaambia washuke niondoke. Basi hapo hapo mmoja akatoa bastola na kuniekea kichwani kisha akanambia niendeshe gari, sikubisha kwa sababu hicho ndio nilichokitaka na mimi ndio niliowapigia polisi simu na kuwapa maelekezo njia waliopita. Basi bila kuuliza huku nikionyesha kutetemeka niliondoa gari huku nikifata maelekezo wallionipa mpaka tukafika katika jengo moja kubwa hivi. Hapo walinambia nisimame na nishuke kwenye gari, bila kuhoji nilifanya hivyo. Mmoja wao alinishika na kunivuta akielekea ndani, sikuonesha ugumu wowote ule. Tuliingia ndani huku wakiongea kwa sauti ya chini chini, nilipigwa na bumbuwazi baada kuingia ndani na kuona umati wa watu ambao ni wanachama wa kikundi hicho. Kwa mbali nilimuona mtu aliekaa kwenye kiti na kwa haraka sana niligundua kuwa ni Mr Louise Millano. .
Alikuja mpaka walipo wale wawili pamoja na mie, walimkabidhi pesa walizoiba na kila mmoja akapewa bunda moja nono la pesa. Aliniangalia sana na kuwauliza wale wawili "huyu ni nani na inakuwaje yuko hapa" kwa hasira. "ah bosi huyu ametusaidia baada gari yetu kugongwa na polisi" mmoja aliongea kwa kigugumizi, aliangalia tena kisha akaniuliza "kijana unaitwa nani", "naitwa Hilarove Gregovic" nilidanganya jina langu. "IMekuaje ukatoa msaaada wakati unaju kabisa kama ungekamatwa ungehukumiwa kifo" aliendelea kunuliza, "ah mi nimechoka kuishi maisha ya kudhalilika". "kivipi"alihoji tena "mimi ni dereva wa taxi tu hapa Moscow lakini nimechoka kuishi maisha ya utumwa na leo wakati nasubiria abiria ndio nikaona gari ikigongwa na polisi ndipo nilipowaona hawa wakitoka na kuanza kuwashambulia polisi, nikaona bora niwasaidie kwa sababu hata wao ni kama mimi wanatafuta riziki japo njia yao ni ngumu, ukweli nilishindwa kuvumilia kuona vijana wenzangu wadogo wakiingia mikononi mwa polisi hivyo nikawapa msaada kwa kuwatorosha pale" nilijibu kwa kujiamini sana. Basi alianza kupiga makofi na wengine wakafuata, kisha aliwatuliza na kuongea "karibu kwenye kikosi, karibu THE BERGS". Nilifurahi sana na kujisemea moyoni laiti kama angejua anakikaribisha kifo wala asingenipongeza, maana alikuwa anamkaribisha izraieli katika maisha yake.

Kuanzia siku hiyo nilianza kufanya nao kazi na kwa muda mfupi nilijizolea mapenzi ya kutosha kutoka kwa bosi wangu ambae pia ni adui yangu mkubwa. Hayo yote yamewezekana kutokana na kuwa mimi nilikuwa si mgeni kwenye mchezo huo. Kuna mara moja tulipewa mchongo wa kwenda kuiba mabilioni ya mapesa katika bank moja hivi, hapo nilitaka kuonyesha uwezo wangu katika kuendesha gari. Niliomba kitengo cha kutoroka na pesa hizo nae akanikabidhi kwa roho safi, mapema siku iliofuata tulitoka kambini na kuelekea kwenye bank hio. Mimi nilibaki nje nikisubiri mzigo uletewe na mara walitoka na mifuko kadhaa mikononi huku wakiongozwa na Mr louise Millano. Waliingiza mifuko ya pesa kwenye gari yangu na Mr Louise aliingia siti ya mbele na kunambia niondoe gari.
 
26.

Kwa kasi ya ajabu niliondoka huku nyuma nikifatwa na wenzangu,na haukupita muda polisi walikuwa nyuma yetu wakitufukuza. Nilimgeukia Mr Louise na kumambia afunge mkanda maana sasa itakuwa pata shika nguo kuchanika. Alifanya hivo na hapo sasa nikakanyaga mafuta na kuanza kuzungushana na maskari lakini nia yangu ilikuwa ni kupotezana na wengine ili nikamalize kazi yangu. Mara kadhaa nilishuhudia gari za wenzangu zikipata ajali, lakini niliendelea kusepa zangu huku askari wakiona kutokata tamaa. Nilindelea kucheza na usukani kwa uzoefu wa hali ya juu huku nikijitahidi kuwakwepa askari pamoja na kukwepa miba wanayo weka njiani. Nilizungushana na polisi kwa muda wa dakika thalathini na nilipohakikisha nimepotezana na wenzangu wote ndipo nikaamua kuwatoroka askari, na Kwa sababu nilizijua njia za vichochoroni nyingi haikuwa shida sana. Nilifika katika jengo moja na kuingia ndani kisha nikasimama, "hapa ni wapi" aliuliza Mr Louise. "tulia bosi subiri joto la polisi liishe halafu tutaondoka" nilimjibu huku nikimuangalia kwa makini usoni. "kama unata maji angalia siti ya nyuma" nilongea na kushuka, na kwa kweli baada mshike mshike ule lazima uhisi kiu. Basi aligeuka nyuma na kuchukua chupa ya maji na kunywa, kisha alishuka kwenye gari na kuanza kuelekea nipokuwa nimesimama. Hatua ya kwanza, ya pili , ya tatu akaanguka chini na kupoteza fahamu..
Alikuja kuzinduka baada kumwagia maji ya baridi usoni, "we ni nani na yuko wapi Hilarove" hilo ndio swali la kwanza alilouliza, nilicheka kidogo na kuongea " Jina langu ni David Robert Mccanoon au ukipenda pia unaweza kuniita Hilarove". Alishtuka baada kusikia kauli ile, najua utajiuliza kwanini kanisahahau lakini baada kuamua kujiunga nao nilianza kufuga ndevu nyingi na nywele ili kuficha sura yangu halisi. Jasho lilianza kumtoka huku akioneka akijibizana na akili yake kuhusu jambo fulani, nilitoa bastola ndogo na kuifunga kiwambo cha kuzui sauti kisha nikamwambia "ukifika huko kwa mungu nisalimie na wenzako saba kisha waambie wasijali kwani waliobaki wote wataungana nanyi muda si mrefu. Nilipomaliza nilimtandika risasi kadhaa za kifua mpaka nilipohakikisha hapumui tena, ndipo nikambeba na kumuingiza kwenye gari iliokuwa na pesa. Nilikamata usukani na kuondoka mpak karibu na kitu cha polisi kisha nikapiga simu na kuwapa taarifa juu ya gari hilo. Mimi mdogomdogo nikasepa na kwasababu nilishaanyowa nywele hakuna alienijua. Huyo ndo mimi bwana mzee wa kumwaga damu na kuuwa ndio starehe yangu.
Nilirudi hotelini na kupimzika, usiku uliingia na taarifa iliopamba moto ni kuuwa kwa kiongozi wa kikundi hatari cha THE BERGS. Serekali ilitoa sana shukrani za dhati kwa aliemuuwa mtu huyo, nilitabasamu kidogo kisha nikatoa simu yangu ambayo ni satellite phone. Nikisema hivi namaanisha kuwa simu hiyo ni aina ya simu ambayo haiwezi kugundulika kwa kutrack. Niliandika ujumbe mdogo wa maneno uliambatana na ramani kisha nikautuma makao makuu ya jeshi la polisi la urusi.
 
27.

Baada hapo nilala usingizi mwanana kabisa , nilikuja kushtuka asubuhi baada simu yangu muita, nilipoiangalia niligundua aliekuwa anapiga ni Tania kipenzi cha roho yangu na asali wa moyo wangu. Niliipokea kwa tabasamu kisha tukaongea machache, baada ya kumaliza mazungumzo niliingia chooni na kujimwagia maji. Nilimaliza nikajiandaa na kutoka, nilirudisha funguo mapokezi na kuaga kisha nikatoka hotelini hapo na kuingia katika mgahawa wa karibu na kupata chai nzuri ya asubuhi.




Nilimaliza na kuchukua taxi na kuelekea uwanja wa ndege, nilikata ticket ya kuelekea mjini Hong kong kwa ajili ya kufa kama nilivyofanya urusi na kwengineko ambako nimepita. Ndege ilitua mjini Hongkong, nilishuka na kuelekea nje ya uwanja huo. Nikavhukua taxi mpaka hotelini na kuchukuwa chumba, kitu cha kwanzo baada kuingia chumbani humo niliwasha tv na kuangulia BBC. Habari iliokuwa imepamba moto ni ya kukamatwa kwa kikosi kizima cha BERGS, na serekali ilikuwa ikitoa shukrani kwa msamaria mwema alietoa ramani ya kufika katika kambi yao lakini kilichonishtua ni baada kuona taarifa ikisema kuwa bado mmoja hajakamatwa na anaitwa Hilarove Gregovic na picha iliowekwa ni ile nlokuwa na madevu. Sikuitilia maanani japo ilinishtua, niliingia chooni na kujisafisha then nikavaa nguo nzuri na kutoka kuelekea katika harkati zangu za kawaida. Kupitia msaada wa google nilifanikiwa kuwapata watu niliokuwa na haja nao, lakini kilichimiweka njia panda ni kwamba watu hao takriban ishirini kati ya ishirini na mbili wameuwawa. Sasa walibakia wawili tu nilamuwa kuwasaka kwa udi na uvumba ili niwafikie mimi mwanzo, nilifanikiwa kupata anuani ya mmoja wao na bila kupoteza muda nilianza safari ya kuelekea kwake. Nilipofika nilijitanbulisha kama mwandishi wa kujitegemea na nlikuwa nahitaji kuongea nae mawili matatu. Alikubali bila kipingamizi, tuliingia ofisini kwake kwa ajili mahojiano hayo.
Nilimuuliza kuhusu kuuwawa kwa wenzake, alichonijibu kilinifanya nikae vizuri ili nisikose kitu. Japo tulikubaliana nisiirekodi kitu lakini ukweli ni kwamba katika shati langu kulikuwa na kamera ndogo mithili ya kifungo na wala hakikuwa tofauti na vifungo vingine katika shati hilo. "Najua hata mimi mua wangu wa kufa ushakaribia sina budi kukwambia ukweli kuhusu mauaji ya wenzangu ishirini, ukweli ni kwamba miaka takribani kumi iliopita tulishiriki kitendo kibaya sana kwa kumtumia kijana aliekuwa ni agent wa siri wa marekani na sniper mzuri sana. Kwa sababu ya tamaa zetu tulimfanya auwe watoto zaidi ya mia moja ili kuzitia matatizoni nchi mbili amabazo kwa muda mrefu zimekuwa na ugomvi lakini mwishoni walitaka kumaliza ugomvi wao kwa kukaa na kuzimaliza tafauti zao. Lakini sisi kama mataifa makubwa tulijua kabisa ikiwa watakubaliana kuishi kwa amani kati yao basi tungekosa sehemu za kuuza silaha na kuiba rasilimali nyingi sana ambazo tilikuwa tukizifaidi kipindi chote cha mapigano yao ambayo pia chanzo kilikuwa ni amtaifa mkubwa. Basi tulitowa tenda kwa madaktari bingwa ili watengeze kemikali ambayo ingeweza kumfanya mtu aweze kutii bila kuuliza maswali yeyote yale, na tulifanikiwa.
 
28.



Baada ya hapo tuliwarubuni vijana watano ambao tulitaka kuwafanya kama majaribio ya kemikali hiyo ambayo haikuwahi kutumika katika mwili wa binaadamu. Tulikwenda nao mpaka karibu na nchi moja kati ya zile mbili na kufanya majaribio lakini matokeo yalikuwa mabaya kati ya wale watano mmoja tu ndie aliepona na kemikali ile ikafanya kazi yake, nakumbuka yule kijana aliitwa David Robert Mccanoon na ndie alietumika kufanya mauaji yale ya kinyama huku akijifanya ni mwananjeshi wa nchi zile kwa nyakati mbili tafauti." mpaka hapo mapigo ya moyo yalianza kunienda mbio na kijasho chembamba kilianza kunitoka japo chumba hicho kilikuwa na ac.
"nikiongea hivyo namaanisha kuwa kuna baadhi ya wakati alivaa kama askari wa nchi moja na kuuwa watoto wa nchi jirani na wakati mwengine alivaa kama asakari wa nchi waliouwawa watoto na kuuwa wale wa nchi nyingine. Kazi iliendelea kuwa hiyo mpka tulipohakikisha ugomvi umeanza upya ndipo tuliamua kurudi kila mtu nchini kwake. Miaka mingi imepita mpaka havi karibuni kukatokea mtafaruku kati yetu na hapo ndipo mauwaji yalipoanza na anaetoa amri hizo ni....." kabla hajamaliza alidondoka chini huku kukiwa na tobo kubwa la risasi iliopenya sawa sawia usoni katila paji la uso. Kwa upigaji ule ilikuwa niwazi kabisa muuaji ni mzoefu nabila kupoteza muda nilichomoka kutoka kweny kiti nikaruka kupitia dirishani na kuanza kukimbia upande uliotoka risasi na kwa mbali niliweza kumuona mtu akiwa katika mavazi meusi.
Moja kwa moja nilijua ndio mwenyewe na kuanza kumuungia, kutokana na kemikali niliokuwa nayo mwilini ilinisaidia na kunipa uwezo mkubwa wa kukimbia bila kuchi mapema. Nilipomkaribia nilimchota mtamaa na kumfanya aanguke kama mzigo, nilimshindilia ngumi za kutosha baada ya kufika huku nkimhoji nani aliemtuma kufanya kazi hiyo. Hakujibu chiochote zaidi ya kuniangalia tu usoni, nikaona isiwe tabu nilimgonga kweny mshipa wa fahamu na kumkata network kisha nikaondoka nae. Nilikwenda nae hadi sehemu moja ya siri na kumuseka hapo kisha nikaelekea hotelini kuchukua zana zangu za mateso. Nilifika sehemu niliomuacha na kujianda vizuri maana lazima ukweli niupate hata kama kwa kutoa tone mojamoja la damu katika mwili wake. Nilimgusa tena sehemu ileile na ghafla akazinduka "kijana naomba unieleze kishkaji tu nani aliekutuma, mimi sina haja ya kukuuwa" niliongea uku nikivaa gloves, "hahahahahahaha" alicheka kwa nguvu "hivi we unajua kama unadili na muuaji wa kimataifa" aliongea kwa kujiamini. Nilimwangalia kisha nikaachia tabasamu zito "dah nilikuwa sijui lakini na wewe unajua unaongea na mtu ambae dunia nzima inamtafuta", alishtuka kidogo "muda wa kujigamba umekwisha,sasa utasema au nikufanye useme" niliendelea kuongoea lakini wakati huu nilivaa sura ya kikatili "kama unaweza nifanye niseme" alijibu kwa kejeli..
Nilifungua begi yangu ndogo na kutoa nguo iliozungusha kisha nikaitandaza kwenye meza, alivoona vitu vilivyokuwa ndani alianza kucheka "ndio utanifanya niseme kwa kutumia sindano". "ndio na utasema tu" nilimjibu kiulaini kisha nikatoa koleo ndogo, nilimsogelea na kumbana kucha kwa koleo "nambie umetumwa na nani".
 
29.

Akanitemea mate usoni, bila kuchelewa niliivuta kucha ya kidole gumba na kuinyofoa, alipiga kelele za maumivu lakini wala sikushtuka.Nilisogea mkono mwengine na kuibana kucha ya kidole gumba cha mkono huo kisha nikamuuliza tena, muda huu alinitukana basi nikarudia tena zoezi lile nikaing'oa kucha ile kisha nikarudisha koleo kwenye ile nguo na kucgukua kisu kidogo cha kufanyia operesheni na kumsogelea. "bado tu hutaki kusema" nilimuuliza tena, "nimeshakwambia kuwa utaambulia patupu hapa" alijibu jabo kwa tabu. "ulishawahi kumuona mnyama akichunwa ngozi, basi na mimi ntakuchuna ngozi tena bila ganzi" nilongea nikiwaserios kabisa. Nilimshika mkono wa kulia na kuanza na kwa kutumia kisu kile kidogo, nlikiingiza katika ngozi na kuanza kazi ya kuibandua ngozi kutoka katika mwili. Alipiga kelele mpaka lakini wala hazikunshtua "nitasem,nitasema nakuomba acha kufanya hivyo" aliongea kwa kwikwi. "ah sasa ungesema mapema yasingekukuta haya yote" niliongea huku nikirudisha kile kisu. "ok ongea sasa" nilivuta kiti na kukaa, huku nikimuangalia usoni maana nilielewa katika hali ile akiongea uongo tu nitajua.
"mimi ni mwanajeshi wa U.S.A na niwasiri kutoka katika kitengo cha CIA , nimepewa kazi hii ya kuwaua wote waliohusika katika Project code x na alienipa kazi hii ni raisi mstaafu" alimaliza, "sasa ungesema mapema yote haya yasingekukuta" nilongea huku nikiinuka na kuelekea kwenye ile nguo na kutoa pini mbili ndogo. "hivi vipini vitakusaidia kupunguza maumivu, lakini vitakupa usingizi kwanza na utakaposhtuka nenda kamwambia aliekutuma kuwa David Robert Mccanoon anakuja" aliposkia jina langu alishtuka bila kumruhusu kuhoji zaidi nilimchoma vile visindano na hapo hapo usingizi ukamchukua.Na kwa sababu sikuwa na nia ya kumuua basi nilimpatia huduma ya kwanza na kumueka GPS tracker katika sehemu ambayo nilijua haitoshtukiwa,kisha nilimfngua kamba. Bila kuchelewa nkasepa zangu. Nilirudi hotelini na kupanga kila kit changu kwaajili ya kumafatilia kila atakapo kwenda. Masaa mawili baadae GPS tracker iliwaka kwenye simu yangu na hapo hapo nikatoka na kuelekea kwenye gari yangu. Bila kuchelewa niliiwasha na kuanza kuelekea kule iliponionyesha simu yangu, niliendelea kufwatilia mpaka nilipofika nje ya nyumba alioingua yule kijana. NIliipaki gari pembeni na kusubiria atoke, masaa mawili baadae alitoka na kuingia kwenye gari yake na kuondoka na mimi bila kuchelewa nilimfata. Alielekea uwanja wa ndege, "hapa leo mpaka kieleweka,utakapoelekea mi ntakua nyuma yako kasoro kaburini tu" nilijisemea moyoni na mwisho nikajifanyia utani.
Alishuka na kuingia ndani ya uwanja huo, nilisubiri mpaka kashapita mlangoni na mimi nikashuka kweya gari na kuchukua begi langu kisha nikavaa kapelo na kuilekea ndani ya uwanja wa ndege. Kwa msaada wa kile kifaa nilichomuekea niliweza kugundua yuko wapi, nilishtuka baada kuona tiket aliokata ni ya kuelekea nchi za Africa.
 
30.

Na mimi nilikwenda kukata tiket na kwa sababu tulipishana kwa karibu niliona kuwa amekata tiket ya kuelekea nchi moja miongoni mwanchi zilizojaa amani duniani japo ilikuwa na maisha duni. Nchi hiyo ni inajulikana kwa jina la Tanzania. Machale yalianza kunicheza kwa nilivyosoma Tanzania ni miongonimwa nchi zenye vito vingi sana yakiwemo madini yaliobeba jina la nchi hiyo maarufu kama tanzanite na pia kunapatikana madini hatari aina Uranium yanayotumika kutengeneza mabomu ya nyuklia. Basi muda ulifika tukapanda ndege na safari ikaanza, safari yote sikupata usingizi kwani niliwaza itakuwaje ikiwa nchi kama ile ikiingia matatizoni na amani walioilinda kwa miaka mingi ikitoweka itakuwaje, maana ni wazi kama yule mshenzi atakuwa Tanzania basi ni lazima atakuwa anataka kufany mchezo mchafu. "kweli katika maisha yangu sijafanya hata moja zuri lakini nitahakikisha nchi ya watu haingii matatizoni kwa sabau ya tamaa za huyu fisi" nilijisemea moyoni huku mwili ukinitetemeka kwa hasira.
Ndege ilikanyaga ardhi ya Tanzania na abiria wote waliokuwa wakishuka hapo wakashuka, nilitoka huku nimevaa kapelo yangu hivyo kunifnya nisitambulike. Nilimfata mpaka nje ya uwanja huo huo wa DIA, aliingia kwenye gari na kuondoka mimi nilichukua taxi na kumwambia awafuate lakini kwa umbali kidogo. Safari ilikuwa ndefu kutokana na foleni kubwa iliokuepo katika jiji maarufu la Daressalaam, walifika sehemu ya kuvuka na kulikuwa boti ndogo za mwendo kasi mbili zikiwasubiri. Nilishuka na kumlipa derva pesa yake kisha taratibu nikasogea maeneo ya ambayo niliamini ndio mlango wa kuingilia katika pantoni. Mbele ya watanzania waliokuwa katika eneo hilo nilikuwa kama mtalii na hata mimi nilitaka iwe hivyo na mara kadhaa niliwahoji vijana ambao nillikuwa nao karibu kuhusu utamaduni wa nchi yao na kwa hali gani wanapambana na maisha ya kupigwa na jua tokea wanapoamka mpaka wanapokwenda kuupitisha usiku. Kwa kweli nilishangazwa na baadhi ya majibu ya baadhi yao, na nilistaajabu sana inakuaje mtu anaweza kuishi na kiwango kidogo cha fedha chini ya dola moja ya kimarekani. Katika ongea ongea yangu nilikutana na kijana mmoja ambae alinifurahishwa kwa uchangamfu wake. Alionekana ni msomi kidogo maana hata kujibu kwake maswali alikuwa akijibu vizuri sana. Tuliongea mengi mpaka pantoni lilipofika upande wa pili ambapo kwa jina paliitwa kigamboni. Nilimuomba anitafutie nyumba nitakayokaa kwa muda wote nitakaokuwa nchini humu, hakuwa nyuma tulihangaika kwa pamoja mpaka tukapata nyumba. Yeye alinisaidia katika kuwasiliana maana kiswahili nilikuwa sikijui hata kidogo. Nilimlipa kiasi kadha cha fedha na kumwambia kuwa makutano yetu mimi na yeye yawe ni siri..
 
31.
Baada ya hapo tuliagana na yeye akaondoka zake, niliingia ndani na kujiweka sawa kabla kuanza kazi ya kuwasaka maadui zangu. Kutokana na joto kali nilioga na kuvaa nguo nyepesi kama hali ya hewa ya nchi hio inavotaka. Nilipomaliza nilitoa computer yangu na kuiunga na internate kupitia satellite ya CIA na kwasababu nilikuwa hacker mzuri nilifanikiwa kuifunga kabisa ili wasijue nani aliehaki satellite yao. kisha nilitoa simu yangu na kuiconnect na computer yangu, nikaanza kutumia elimu yangu mpaka nikajua walipowweka kambi yao. Nilifanikiwa kuhack system yao nakuchunguza kila kitu kunaziz njia mpaka kila mtu aliehusika na kambi hiyo. Baada ya kuridhikka na taarifa nlokuwa nilizozipata,niliamua kupumzika ili siku ya pili niangalie uwezekano wa kupata silaha nzito kwaajili ya kazi hiyo. Huku nikisindikizwa na kiyoyozi usingizi ulinichukua ghafla tu, nilikua kushtuka baada kupiagwa na miale ya jua usoni. Kwa kujikongoja niliamka na kuelekea chooni kwaa ajili ya kujisafisha, dakika kumi baadae nilitoka na kubadili nguo kisha nikavaa ndevu za bandi pamoja nasharubu ambazo zilinibadilisha na knifanya kama mkoloni. Bila kuchelewa nilitoka na kuelekea katika maeneo kambi hiyo ilipo, nilijifanya nazunguka tu huku nikiangaza sehemu mbali mbali. Nilijua kabisa itakua shida kupenya katika kambi hasa ukiziningatia katika nchi ile kupata silaha itakuwa ngumu. Lakini ilikuwa ni lazima nipenye tu kwa gharama yoyote ile, niliumiza sana kichwa nikifikiria njia ambayo nitaingia bila kuonekana.


Katika kufikiria sana nikagundua ipo njia ila ni lazika nipate gwanda za mmoja kati ya wanajeshi wanaolinda kambi ile. Nilisubiri hadi usiku ulipoingia nikavaa nguo nyeusi na kufunika uso wangu kama ninja kisha nikatoka kimykimy bila hata kushtukiwa. Nilijibanza pahali kwa umakiniwa hali ya juu sana ili ikitokea akapita mwaajeshi yeyote yule basi atakuwa mali yangu. Baasa kama nusu saa hivi alipita mmoja akiwa anaongozana na mwanamke na nilipowatazama vizuri niligundua kuwa alikuwa amelewa tilalila. Hiyo ndio ilikuwa nafasi pekee nilinza kumfatilia kwa taratibu na kwa umakini wa hali yajuu sana. Nilipofika sehemu nikaona muda wa kuchukua gwanda zangu umefika, nilimvamia kwa nguvu na kumgonga shingoni kitendo kilicomfanya apoteze fahamu kabisa, na yule mwanamke nimminya kwenye sehemu ambayo nilijua akiamka hatokumbuka chochote kilichotokea usiku ule. Baada hapo nilimbeba na kurudi nae nyumbani kwangu, nilimuingiza katika chumba kimoja na kumfungia humo lakini kabla ya kutoka humo nilichukua finger print zake na kwenda nazo kuzifanyia uchunguzi, hiyo ilikuwa ni kwaajili ya kusoma tabia zake. Na kwa utaalamu wangu nilitengeza kifaa kidogo ambacho nilikiweka shingoni kwa ajili ya kuiga sauti yake. Nilirudi yena kule ndani na kumpiga picha kisha nikaitia kwenye computer, nilifanya nnavo jua mwenyewe na kuchukua kifaa ambacho nilikuwa nacho muda mrefu, kifaa hicho kilikuwa maalum kwa kubadlisha sura. Nilikivaa nyuma ya sikio na kukiactivate, papo hapo sura yangu ilibadilika na kuwa kama ya yule mwanajeshi. Niliporidhika na maandalizi hayo nilisubiri mpka asubuhi nakavaa gwanda za yule mwanajeshi na kuelekea kambini.
 
32.


Nilipofika getini nilionesha kitambulisho changu na kuruhusiwa kupita,nilitabasamu kama ishara ya kushukuru na kwa vile nilizisoma tabia zake zote hivo kwa msaada wa kifaa maalumu nilliweza kuzivaa tabia hizo jambo ambalo lilinifanya niwe kama yeye tu kwa kila kitu. Nilielekea mpaka kwanye chumbaa alichokuwa anakaa na kuvua gwanda zile kisha nikavaa nyingine. Nikiwa chumbani humo aliingia mwanajeshi mwengine na kuongea "sergnt Jones unaitwa na bosi", bila kuchelewa nilitoka na kuelekea ofisini nikakuta kikao cha dharura, nilisalimia na kuungana nao na aliekuwa anaongwa hakuwa mwengine bali ni raisi mstaafu "hapa mambo mawili makubwa, la kwanza ni kwamba tumetumia mbinu zote kutaka kuanzisha vurugu lakini inaonekana kama ilivyosifa ya watu hawa kuwa vurugu kwao ni mwiko lakini la pili ambalo huenda likawa kikwazo kikubwa ni kwamba yule kijana tulimtuma Hongkong ameleta salamu kuwa David Robert Mccanoon yuko hai na kama hivo nikweli basi nilazima atakuja tu huku. Na shughuli ya huyu mpuuzi si ndogo maana kuuwa kwake ni jambo dogo sana na wala halimuumizi kichwa. Ili kuepuka yote haya sasa inabidi tuje na mbinu mpya ili tufanya kazi mapema na kila mtu arudi kwao. Mbinu yenyewe ni kwamba, tufanye matukio ya kigaidi kisha lawama tuzipeleka kwa kikundi maarufu cha kigaidi cha Al-shabaab". "una maanisha nini bosi" niliuliza kwa kujiamini, aliniangalia kisha akatabasamu na kuongea "ninachomaanisha ni kuwa, tutatega mabomu na kuripuwa na target ya kwanza ni mji huu wa Daresalaam. huu ni mji wa kibiashara na umejaa watu wa aina mbalimbali hivyo na ikisadikika kuwa ni kitendo cha kigaidi basi watalii wataanza kurudishwa katika nchi zao kisha tufanya tena hivo katika visiwa vya Zanzibar, Arusha, Dodoma pamoja na morogoro. Matukio haya yatasababisha nchi kuingia machafuko na hapo ndio tutakapoingia sisi kwaajili ya kuwapa msaada na masharti tutakayowapa ni kutuurusu kuchimba madini ya Tanzanite pamoja na Uranium" alimaliza kuongea wote tukapiga makofi, "kazi itaanza lini" aliuliza mmoja kati ya watu waliokuepo katika kikao hicho. "mabomu yatawasili mwishoni mwa wiki hii na punde yatakapofika basi kazi itaanza, kwa heri amani ya Tanznia kwa heri furaha" aliongea maneno hayo watu wote wakayarudia nikiwemo na mimi na kikao kiliishia hapo..
Nilirudi chumbani kule nikiwa na mawazo kibao maana nilijua nikifanya mchezo kweli watafanikiwa mipango yao hivyo nilitakiwa kuisambaratisha kambi hiyo ndani ya siku tatu kwa sababu ndizo zilizokuwa zimebaki mpaka kuwasili kwa mabomu hayo ya kuangamiza amani ya nchi ile. Maongezi yote niliyarikodi bila mtu kujua, usiku ulifika na kama kawaida yake sergent Jones huwa anatoka kwenda kunya kidogo na kulala na wanawake wa kiswahili. Basi na mimi nilitoka na kuelekea nyumbani kwangu, niliingia katika kile chumba nilichomuweka na kumkuta akiwa macho. "habari yako pacha wangu" nilimtania "we nani" aliuliza kwa hasira, "mimi ni kifo chako" nilimjibu na kutabasamu kisha nikatoka ndani ya chumba hicho.
 
Back
Top Bottom