Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #141
121.
Macho yakamtoka pima akiwa haamini kile anachokiona nyuma yake kinakuja pale mbele.
“Simeria?” Akaita kwa sauti ya chini Dokta Ice.
“Ndiye Simeria. Mkeo wa zamani, Ice.” Uzo akamwambia Dokta Ice wakati mwanamama aliyeitwa Simeria akisogea upande wake wa kushoto na kusimama. “Lakini sasa, si mkeo tena.” Akamgeukia Simeria, naye yule mwanamke akamgeukia na kupeana ndimi zao kwa sekunde kadhaa kitu kilichomfanya Dokta Ice kutaka ardhi ifunguke naye aingie, kisha ijifunge naye afie huko.
“Nini kimekubadilisha Simeria?” Akauliza kwa uchungu Dokta Ice.
“Hamna. Ni maisha tu! Nilitakiwa kuwa nawe ili yatimie haya. Umenifundisha folmura nyingi sana. Na sasa ni muda wangu kwenda nazo.” Akajibu Simeria.
“Kwa hiyo mapenzi yote yale, yalikuwa ni maigizo?” Akauliza tena na Uzo alikuwa kimya wala hakutaka kuingilia ule ugomvi.
“Heri yawe maigizo ya kutisha ama ya mapenzi, tunaweza kukumbwa na hisia za kweli. Lakini hayakuwa maigizo hayo, bali yalikuwa maigizo ya vichekesho. Yaani unaweza kufa, mtu asiamini kama umekufa kwa sababu ni ucheshi.” Akajibu Simeria na kumfanya Ice kusikitika. “Una swali lingine kabla hujafa?” Akauliza tena Simeria lakini Dokta Ice alikuwa kimya kainamisha kichwa chake asijue aulize nini. “Baby,” Simeria akamuita Uzo.
“Naam, honey.” Akaitika yule mwanaume mwenye umri kati ya miaka arobaini hadi arobaini na sita.
“Huyo ni wenu. Naomba nianze kazi yangu.” Akaongea yule mwanamama ambaye naye si haba. Licha ya kuwa na umri kati ya miaka thelathini na sita hadi arobaini, lakini alikuwa kama msichana wa kileo kutokana na mavazi pamoja na mikwatuo aliyokuwa anajikwatulia.
“Okay baby.” Uzo alimuitikia na kisha mwanamke yule akajipeleka na kukutanisha ndimi zao tena kwa mahaba makubwa hadi baadhi ya walinzi wakawa wanaona aibu kuwaangalia. Walipomaliza tendo hilo la aibu, Simeria akaanza kuelekea kule ilipo mitambo.
“Simeria.” Akaitwa na Dokta Ice. Mwanamke yule akageuka na kurudi tayari kwa kumsikiliza.
“Merice….” Akalitaja jina hilo kwa kigugumizi. Ni wazi alitaka kuuliza lakini hakutaka kupata majibu anayoyafikiria.
“Merice nini? Mbona humalizii sentensi?” Akauliza kwa ngebe Simeria.
“Merice, mtoto wetu. Naye yuko wapi?” Ikambidi amuulizie mwanaye pekee wa kike ambaye inasemekana alikufa kwenye ajali mbaya ya gari akiwa na mama yake, lakini mama yake kaonekana, je mwanaye?
Simeria akamsogelea Dokta Ice hadi wakakaribiana nyuso zao.
“Si mwanao tena.” Akaongea maneno hayo na kuchapa vidole vyake na kutoa sauti kama ya kuita kitu fulani kije. Ndipo mlango ukafunguliwa na akatokea mwanamke mmoja mrefu na mwenye nywele mwanana akiwa kavalia mavazi ya kijeshi. Dokta Ice akawa kakodoa macho yake asiamini kile anachokiona.
“Umemuharibu hata mwanao wa kumzaa Simeria?” Aliongea Dokta Ice baada ya kushuhudia uso wa Merice ambaye naye alikuwa katika muonekano wa kutocheka wala kutambua lolote kuhusu wazazi na watu wengine.
“Ni wako huyu Uzo.” Simeria badala ya kuongea na Dokta Ice, akamruhusu Uzo, yule mwanaume wake mwingine afanye anachoweza kumfanya Dokta Ice. Naye Uzo bila haya, wakati Simeria anaondoka eneo lile, akampiga kofi kwenye makalio yake na mwanamke yule alitabasamu kana kwamba kile ni kitendo cha kawaida sana.
“Watakuua tu siku moja Simeria. Kama ulivyoniua mimi.” Dokta Ice aliongea lakini Simeria hakujibu lolote bali kupotea kabisa eneo lile.
“Turudi kwenye biashara yetu Dokta.” Aliongea Uzo huku anaanza kusogea mbele ya Dokta Ice.
“Sina biashara na wewe Uzo.” Akajibu mapigo Dokta Ice.
“Unayo. Na tambua hata kama huwezi kuongea sasa, tutakufanya utapike yote. Nadhani unalitambua hilo vema sana.” Uzo alibwabwaja. “Nachotaka kujua, ni huyu mwanajeshi uliyemtorosha, anaubora gani na ulitumia folmura ipi?” Akauliza.
“Hahahaaaa.” Dokta Ice akacheka kwa sauti kabla ya kutulia na kumuangalia Uzo. “Unamuogopa sana eeh! Ni hatari sana huyo, mara mia na hawa niliyowatengeneza.” Akaongea kwa furaha Dokta Ice.
“Sijakuuliza uhatari wake. Nimekuuliza kitu kingine kabisa.”
“Unajua sheria za udaktari, huruhusiwi kutoa siri za ugonjwa au mbinu za kutibu ugonjwa. Nipo hapa kama daktari. Kwa hilo hutopata.” Akajibu Ice.
“Okay. Na kuna risasi ulikuwa unazitumia kule kwako….” Uzo ni kama alikuwa kasahau kitu. Akakatisha yale maneno. “Na nilitaka kusahau, ni mkeo ndiye alituambia nyumba yako ya siri.” Akaongea maneno hayo baada ya kujishtukia.
“Si mke wangu. Ni malaya wetu.” Akaongea Dokta Ice na kumfanya Uzo acheke.
“Leo ni malaya?” Akauliza kwa mshangao.
“Kama unaweza kumpiga matako na akacheka tu, unadhani yupo salama akilini huyo?” Maneno hayo yakamfunga mdomo Uzo.
“Hayakuhusu.” Mwishowe akaongea. “Nachotaka sasa ni kujibu nachokuuliza.” Akaongea kwa ukali zaidi.
“Oooh! Umekuwa mbogo pia? Napenda ukiwa na hasira kuliko ukijidai mwema.” Akaongea huku katabasamu Dokta Ice. “Hata hivyo, hutaambulia lolote.” Akaongeza na kumfanya Uzo amfate pale kwenye kiti na kumchapa ngumi moja ya nguvu.
“Nahitaji majibu. Na siyo porojo zako.” Akaongea Uzo kwa hasira.
“Uzo rafiki yangu. Umesahau kuwa tulisomea wote upelelezi? Umesahau yale mateso yote tuliyoshiriki kwa pamoja ili tuseme kambi yetu iko wapi? Hivi tulisema kweli?” Akamuuliza lakini hakumpa nafasi ya kujibu. “Nadhani unaelewa unachokifanya ni kujisumbua tu kwani sitosema lolote.” Akamaliza.
“Ipo njia ya kusema.” Uzo alipoongea hayo, akafanya ishara ya mkono wake na Dokta mmoja alifungua mlango ule aliotokea Simeria na aliingia eneo lile akiwa kabeba sahani iliyofunikwa kwa bakuli la bati.
Akaenda hadi kwa Uzo na kuifunua sahani na hapo ikaonekana sindano ambayo muhimili wake uliundwa kwa chuma na ulikuwa na muonekano kama wa bastola. “Pinnacle.” Akaongea Uzo akiwa kakamata ile sindano huku anaingalia. “Nadhani jina la sindano hii uliipa wewe kwa sababu ya maumivu yake na ulevyaji wake. Ni muda wa wewe kuelewa maana ya pinnacle.”
“Kama niliitengeneza mimi, basi najua jinsi ya kuihimili.” Akajibu Dokta Ice na kabla Uzo hajasogea pale alipokuwa kakalishwa, Dokta Ice akarusha teke lake na kumpiga sehemu za siri Uzo na kwa taharuki ya hatari, akajirusha kwa nyuma huku kiti bado kikiwa mgongoni kwake, akadondokea mgongo na kukifanya kiti kile kivunjike na wakati huo karibu yake kulikuwa kuna mwanamaabara mmoja aliyepigwa mtama wa kushtukiza jambo lililofanya adondoke na kumpa nafasi Dokta Ice asimame naye huku kamkaba.
“Mkileta papara tu! Navunja shingo ya huyu mbwa wenu.” Akawachimba mkwara na wakati huo wanajeshi wawili, mmoja aliyekuja na Dokta Ice na mwingine Merice, mtoto wake wa kumzaa, wote walikuwa wamemuoneshea bastola.
“Msifanye lolote.” Aliongea Uzo kuwaelekeza wale wanajeshi lakini kitendo cha kushtukiza sana
“Kama niliitengeneza mimi, basi najua jinsi ya kuihimili.” Akajibu Dokta Ice na kabla Uzo hajasogea pale alipokuwa kakalishwa, Dokta Ice akarusha teke lake na kumpiga sehemu za siri Uzo na kwa taharuki ya hatari, akajirusha kwa nyuma huku kiti bado kikiwa mgongoni kwake, akadondokea mgongo na kukifanya kiti kile kivunjike na wakati huo karib yake kulikuwa kuna mwanamaabara mmoja aliyepigwa mtama wa kushtukiza jambo lililofanya adondoke na kumpa nafasi Dokta Ice asimame naye huku kamkaba.
Macho yakamtoka pima akiwa haamini kile anachokiona nyuma yake kinakuja pale mbele.
“Simeria?” Akaita kwa sauti ya chini Dokta Ice.
“Ndiye Simeria. Mkeo wa zamani, Ice.” Uzo akamwambia Dokta Ice wakati mwanamama aliyeitwa Simeria akisogea upande wake wa kushoto na kusimama. “Lakini sasa, si mkeo tena.” Akamgeukia Simeria, naye yule mwanamke akamgeukia na kupeana ndimi zao kwa sekunde kadhaa kitu kilichomfanya Dokta Ice kutaka ardhi ifunguke naye aingie, kisha ijifunge naye afie huko.
“Nini kimekubadilisha Simeria?” Akauliza kwa uchungu Dokta Ice.
“Hamna. Ni maisha tu! Nilitakiwa kuwa nawe ili yatimie haya. Umenifundisha folmura nyingi sana. Na sasa ni muda wangu kwenda nazo.” Akajibu Simeria.
“Kwa hiyo mapenzi yote yale, yalikuwa ni maigizo?” Akauliza tena na Uzo alikuwa kimya wala hakutaka kuingilia ule ugomvi.
“Heri yawe maigizo ya kutisha ama ya mapenzi, tunaweza kukumbwa na hisia za kweli. Lakini hayakuwa maigizo hayo, bali yalikuwa maigizo ya vichekesho. Yaani unaweza kufa, mtu asiamini kama umekufa kwa sababu ni ucheshi.” Akajibu Simeria na kumfanya Ice kusikitika. “Una swali lingine kabla hujafa?” Akauliza tena Simeria lakini Dokta Ice alikuwa kimya kainamisha kichwa chake asijue aulize nini. “Baby,” Simeria akamuita Uzo.
“Naam, honey.” Akaitika yule mwanaume mwenye umri kati ya miaka arobaini hadi arobaini na sita.
“Huyo ni wenu. Naomba nianze kazi yangu.” Akaongea yule mwanamama ambaye naye si haba. Licha ya kuwa na umri kati ya miaka thelathini na sita hadi arobaini, lakini alikuwa kama msichana wa kileo kutokana na mavazi pamoja na mikwatuo aliyokuwa anajikwatulia.
“Okay baby.” Uzo alimuitikia na kisha mwanamke yule akajipeleka na kukutanisha ndimi zao tena kwa mahaba makubwa hadi baadhi ya walinzi wakawa wanaona aibu kuwaangalia. Walipomaliza tendo hilo la aibu, Simeria akaanza kuelekea kule ilipo mitambo.
“Simeria.” Akaitwa na Dokta Ice. Mwanamke yule akageuka na kurudi tayari kwa kumsikiliza.
“Merice….” Akalitaja jina hilo kwa kigugumizi. Ni wazi alitaka kuuliza lakini hakutaka kupata majibu anayoyafikiria.
“Merice nini? Mbona humalizii sentensi?” Akauliza kwa ngebe Simeria.
“Merice, mtoto wetu. Naye yuko wapi?” Ikambidi amuulizie mwanaye pekee wa kike ambaye inasemekana alikufa kwenye ajali mbaya ya gari akiwa na mama yake, lakini mama yake kaonekana, je mwanaye?
Simeria akamsogelea Dokta Ice hadi wakakaribiana nyuso zao.
“Si mwanao tena.” Akaongea maneno hayo na kuchapa vidole vyake na kutoa sauti kama ya kuita kitu fulani kije. Ndipo mlango ukafunguliwa na akatokea mwanamke mmoja mrefu na mwenye nywele mwanana akiwa kavalia mavazi ya kijeshi. Dokta Ice akawa kakodoa macho yake asiamini kile anachokiona.
“Umemuharibu hata mwanao wa kumzaa Simeria?” Aliongea Dokta Ice baada ya kushuhudia uso wa Merice ambaye naye alikuwa katika muonekano wa kutocheka wala kutambua lolote kuhusu wazazi na watu wengine.
“Ni wako huyu Uzo.” Simeria badala ya kuongea na Dokta Ice, akamruhusu Uzo, yule mwanaume wake mwingine afanye anachoweza kumfanya Dokta Ice. Naye Uzo bila haya, wakati Simeria anaondoka eneo lile, akampiga kofi kwenye makalio yake na mwanamke yule alitabasamu kana kwamba kile ni kitendo cha kawaida sana.
“Watakuua tu siku moja Simeria. Kama ulivyoniua mimi.” Dokta Ice aliongea lakini Simeria hakujibu lolote bali kupotea kabisa eneo lile.
“Turudi kwenye biashara yetu Dokta.” Aliongea Uzo huku anaanza kusogea mbele ya Dokta Ice.
“Sina biashara na wewe Uzo.” Akajibu mapigo Dokta Ice.
“Unayo. Na tambua hata kama huwezi kuongea sasa, tutakufanya utapike yote. Nadhani unalitambua hilo vema sana.” Uzo alibwabwaja. “Nachotaka kujua, ni huyu mwanajeshi uliyemtorosha, anaubora gani na ulitumia folmura ipi?” Akauliza.
“Hahahaaaa.” Dokta Ice akacheka kwa sauti kabla ya kutulia na kumuangalia Uzo. “Unamuogopa sana eeh! Ni hatari sana huyo, mara mia na hawa niliyowatengeneza.” Akaongea kwa furaha Dokta Ice.
“Sijakuuliza uhatari wake. Nimekuuliza kitu kingine kabisa.”
“Unajua sheria za udaktari, huruhusiwi kutoa siri za ugonjwa au mbinu za kutibu ugonjwa. Nipo hapa kama daktari. Kwa hilo hutopata.” Akajibu Ice.
“Okay. Na kuna risasi ulikuwa unazitumia kule kwako….” Uzo ni kama alikuwa kasahau kitu. Akakatisha yale maneno. “Na nilitaka kusahau, ni mkeo ndiye alituambia nyumba yako ya siri.” Akaongea maneno hayo baada ya kujishtukia.
“Si mke wangu. Ni malaya wetu.” Akaongea Dokta Ice na kumfanya Uzo acheke.
“Leo ni malaya?” Akauliza kwa mshangao.
“Kama unaweza kumpiga matako na akacheka tu, unadhani yupo salama akilini huyo?” Maneno hayo yakamfunga mdomo Uzo.
“Hayakuhusu.” Mwishowe akaongea. “Nachotaka sasa ni kujibu nachokuuliza.” Akaongea kwa ukali zaidi.
“Oooh! Umekuwa mbogo pia? Napenda ukiwa na hasira kuliko ukijidai mwema.” Akaongea huku katabasamu Dokta Ice. “Hata hivyo, hutaambulia lolote.” Akaongeza na kumfanya Uzo amfate pale kwenye kiti na kumchapa ngumi moja ya nguvu.
“Nahitaji majibu. Na siyo porojo zako.” Akaongea Uzo kwa hasira.
“Uzo rafiki yangu. Umesahau kuwa tulisomea wote upelelezi? Umesahau yale mateso yote tuliyoshiriki kwa pamoja ili tuseme kambi yetu iko wapi? Hivi tulisema kweli?” Akamuuliza lakini hakumpa nafasi ya kujibu. “Nadhani unaelewa unachokifanya ni kujisumbua tu kwani sitosema lolote.” Akamaliza.
“Ipo njia ya kusema.” Uzo alipoongea hayo, akafanya ishara ya mkono wake na Dokta mmoja alifungua mlango ule aliotokea Simeria na aliingia eneo lile akiwa kabeba sahani iliyofunikwa kwa bakuli la bati.
Akaenda hadi kwa Uzo na kuifunua sahani na hapo ikaonekana sindano ambayo muhimili wake uliundwa kwa chuma na ulikuwa na muonekano kama wa bastola. “Pinnacle.” Akaongea Uzo akiwa kakamata ile sindano huku anaingalia. “Nadhani jina la sindano hii uliipa wewe kwa sababu ya maumivu yake na ulevyaji wake. Ni muda wa wewe kuelewa maana ya pinnacle.”
“Kama niliitengeneza mimi, basi najua jinsi ya kuihimili.” Akajibu Dokta Ice na kabla Uzo hajasogea pale alipokuwa kakalishwa, Dokta Ice akarusha teke lake na kumpiga sehemu za siri Uzo na kwa taharuki ya hatari, akajirusha kwa nyuma huku kiti bado kikiwa mgongoni kwake, akadondokea mgongo na kukifanya kiti kile kivunjike na wakati huo karibu yake kulikuwa kuna mwanamaabara mmoja aliyepigwa mtama wa kushtukiza jambo lililofanya adondoke na kumpa nafasi Dokta Ice asimame naye huku kamkaba.
“Mkileta papara tu! Navunja shingo ya huyu mbwa wenu.” Akawachimba mkwara na wakati huo wanajeshi wawili, mmoja aliyekuja na Dokta Ice na mwingine Merice, mtoto wake wa kumzaa, wote walikuwa wamemuoneshea bastola.
“Msifanye lolote.” Aliongea Uzo kuwaelekeza wale wanajeshi lakini kitendo cha kushtukiza sana
“Kama niliitengeneza mimi, basi najua jinsi ya kuihimili.” Akajibu Dokta Ice na kabla Uzo hajasogea pale alipokuwa kakalishwa, Dokta Ice akarusha teke lake na kumpiga sehemu za siri Uzo na kwa taharuki ya hatari, akajirusha kwa nyuma huku kiti bado kikiwa mgongoni kwake, akadondokea mgongo na kukifanya kiti kile kivunjike na wakati huo karib yake kulikuwa kuna mwanamaabara mmoja aliyepigwa mtama wa kushtukiza jambo lililofanya adondoke na kumpa nafasi Dokta Ice asimame naye huku kamkaba.