Simulizi ya Kijasusi: Giza la Wasaliti

Simulizi ya Kijasusi: Giza la Wasaliti

"Katika giza, kila kivuli kina hadithi, na kila hadithi ina siri ambayo inahitaji kulipwa kwa damu………..na shetani hutabasamu katika mipango, hufurahia katika utekelezaji ila hubadilika katika matokeo” bado hujanielewa
Ni miaka mitatu baada ya changamoto na mikiki mikiki taifa, viongozi na wapigania uchumi kuzimika na hali kuwa shwari huku chombo kikielea bila bughudha yoyote ndipo zinapokuja siku za hofu kuelekea uchaguzi mkuu wa wabunge,madiwani na raisi katika taifa hilo huku kukighubikwa na matukio ya mauaji, ujambazi, hujuma na utowekaji wa watu huku pazia la giza likificha wahusika, Chifu anafukuzwa kazi akiwa anaipenda ofisi yake, uongozi unakosa dira, tamaa inazidi utu, kifo kinabaki msaada namba moja kuliko maisha, sheria inabaki kwenye makaratasi na haki inakuwa jinai magerezani……….yote haya utayapata katika katika kitabu cha WATU WA GIZA……..DONT MISS IT
 

Attachments

  • IMG_0946.png
    IMG_0946.png
    928.4 KB · Views: 10
KIONJO
Alishusha pumzi ndefu na sekunde hiyo hiyoakazama kwenye tafakari huku kauli za bosi wake zikijirudiarudia akilini mwake na punde akagutushwa na mlio wa simundogo aina ya Motorola C113, akaipokea na kuiweka sikionihuku akipima utulivu wa upande wa pili
"je ne paux pas croire tu as ete si negligent au point de gâchertout le plan,et maintenant nous sommes exposés au grand jour.il ne reste plus que le monde nous brûle" Alifoka mtu yule aliyepiga simu na kumfanya mpokeaji kutetemeka kwa hofuhuku akichakata ni jibu lipi atatoa kuzima lawama na tuhuma nzito zilizopelekea mpango kuharibika kwa uzembe wa bwana huyu.
"J'ai déjà commencé à résoudre le problème et je te garantisqu'avant ce soir , tu recevras de bonnes nouvelles, madame"alijitutumua kujibu bwana yule kwa sauti ya unyenyekevu huku naye akitumia lugha ya kifaransa kujibu tuhuma zile huku akimhakikishia jua halitazama bila mwanamama huyo hajapata habari ya kumfurahisha.
"pour la négligence que tu as commise, tu as deux options maintenant:démissionner et mourir d'une mort doulureuse.J'attends ta réponse immediatement" alifoka mwanamama yule huku akitoa machaguo mawili kwa yule bwana kwamba kabla jua halijazama awe ametekeleza wazo la yeye kufa pasipo maumivu au asubiri na kukaidi kisha kufa kifo cha mateso, hakika ni machaguo yaliyofanya koo lake likauke kwa hofu.
"madame,donne-moi une autrechance ,c'etait juste un accident,cela ne se reproduira plus, fais-moiconfiance"alijitutumua tena huku akiomba nafasi ya pili ili asahihishe makosa yake.
"if you want second chance kill me, if not do as i say and remember my eyes are on each step you hit, take that on your head and dont try me Rest in Paradise Director......tititititi" simu ilikatwa na kumuacha mtu yule akivuja jasho la kutosha huku kiyoyozi kikiendelea kukifanya chumba kuwa cha baridi na hewa safi, mzee yule akazama katika tafakuri nzito huku akihesabu kila pumzi inayoingia na kutoka alijutia sana kujingiza katika mtandao huo na alichakata kila wazo linalopita kichwani mwake na mwisho akaivuta kompyuta mpakato yake na kuwahi nyumbani kwani mahali hapo hapakuwa salama, ilimchukua dakika kadhaa kufika kwake huku ofisini akiaga kuwa anakwenda hospitali na hajisikii vizuri huku msafara wake ukijipnga tayari kwa kuondoka.
"Mama Johnson leo hajaenda kazini?" Lilikuwa ni swali aliloulizwa mlinzi ambaye alijikuta akibabaika kujibu, kupitia taswira ya macho ya yule mlinzi ilionekana kuna kitu hakiko sawa alishuka na kupitiliza kwenye jumba lake moja kwa moja, jumba lilimlaki kwa ukimya akapitiliza mpaka chumbani nako hakukuta mtu zaidi ya kitanda kilichokuwa kimetandikwa vizuri.
"atakuwa wapi huyu mwanamke.....nina sekunde chache sana kabla hawa jaharibu mpango wangu" alichukua kompyuta yake na diski mweko kisha kwa haraka akaunganisha na intaneti na kuyatuma mafaili kadhaa kwenye barua pepe kisha akafuta kila kitu na kupiga magoti akikielekea kitanda na muda huo huo mwili ulimsisimka kwani kwa jasusi mbobevu kama huyo kunusa hatari inayokuja mbele yake ni sawa na pua kunusa manukato yenye harufu nzuri.
vishindo vya buti kama wavaazo wanajeshi kulimfanya afumbue macho huku masikio yake ya kihesabu kila hatua miguu inapokanyaga katika chumba kile kikubwa na kipana. Almanusura akimbie kwa alichokiona mbele yake koo likamkauka ghafla na kumfanya ahisi miguu haina nguvu kwani sura ya mwanamke mrembo na mpole ulikuwa mbele yake huku ukiwa katika hali ya ukatili, bwana yule akatizama picha iliyokuwa ukutani ikiwaonesha watu hao wakiwa na furaha na tabasamu la mahaba kisha akamtazama mwanamke aliyeko mbele yake.
"mama johnson unafanya nini na hao ni akina nani mkewangu?"aliuliza mkurugenzi wa idara ya ujasusi huku akiwatazama kwa zamu wanaume wanne ambao hakuwa akiwafahamu na alibaki akijiuliza wameingiaje ndani humo huku nje kuna ulinzi mkali wa vijana wa idara ya ujasusi ya nchini humo SNR.
************************************
KWA SHILINGI BUKU TU UNAIPATA HADI MWISHO USIUKOSE UHONDO WA SIMULIZI HII
 
Uyu kashazingua fatilieni za FEBIAN BABUYA
Huyu kajazwa upepo wenzake mwanzoni uwa wanaziachia hadi mwisho ili mtu ajue uandishi wake uko vzur umaliziaj wa stry zake ukoje je mashabiki wameelewa kazi zake kwa ukubwa gan sas stry yenyewe moja wamemjaza upepo auze aya ajiuzie sas kuna waandshi wabora sana
 
Huyu kajazwa upepo wenzake mwanzoni uwa wanaziachia hadi mwisho ili mtu ajue uandishi wake uko vzur umaliziaj wa stry zake ukoje je mashabiki wameelewa kazi zake kwa ukubwa gan sas stry yenyewe moja wamemjaza upepo auze aya ajiuzie sas kuna waandshi wabora sana
Mcheki FEBIAN BABUYA ana story kali
 
Apo umefeli sana mwandishi walio kujaza upepo na wewe ukajaa wamekupoteza, hakuna anaye jua ubora wako wa simulizi me binafsi hii ndyo ya kwanza na haijafika popote ingetakiwa ifike angarau mwisho watu wajue ubora wako upoje kwenye utunzi au uwandishi ili ata zinazo kuja ukisema waje kumalizia wasap au inbox watu wanajua una kitu cha huwakika wangalie wenzio Kama sungano jr, Fabian babuya jifunze kwa wenzio walio kutangulia na cyo wa wapuuzi wachache wanao jikuta wanajua sana na wanajiweza, ujifikirie kijana
 
Apo umefeli sana mwandishi walio kujaza upepo na wewe ukajaa wamekupoteza, hakuna anaye jua ubora wako wa simulizi me binafsi hii ndyo ya kwanza na haijafika popote ingetakiwa ifike angarau mwisho watu wajue ubora wako upoje kwenye utunzi au uwandishi ili ata zinazo kuja ukisema waje kumalizia wasap au inbox watu wanajua una kitu cha huwakika wangalie wenzio Kama sungano jr, Fabian babuya jifunze kwa wenzio walio kutangulia na cyo wa wapuuzi wachache wanao jikuta wanajua sana na wanajiweza, ujifikirie kijana
Anadhan mafanikio mepesi yanakuja tu soko gumu angallia eddy msulwa angalia emanuel kway wameanzaje na wako wap sahv kuteka fikra za watu si jambo jepesi tulianza kumuelewa jini likampitia shwaa
 
Back
Top Bottom