Simulizi ya Kijasusi: Giza la Wasaliti

Simulizi ya Kijasusi: Giza la Wasaliti

"Watu hujifunza kutoka kwa makosa yao, lakini wengine hujifunza kutoka kwa makosa ya wengine………na Siri nyingi za gizani zinazofichwa ila zinapoanza kufichuliwa, kila mtu anakuwa na hatia.” Eeeeebbhna eeennhh kwani ina maana gani hii nukuu hebu tufunue pazia tuone kulikoni?
Endelea……..
"ila jeshi la polisi chini ya huyu mzee lilikuwa limepwaya Sana rushwa na dawa za kulevya zilikuwa kweupe, utekaji ndiyo usiseme ukija kwenye suala la utekaji ndiyo kabisa kikubwa tumuombee apumzike aendako huenda Mungu amesaidia kumuondoa." Aliongea kijana mmoja aliyeonekana kuwa makini kupitia Vichwa vingine vya magazeti.
"eebhana eeeennnhhh kumbe Kuna mauaji mengine nyumbani kwa Askofu wa kabisa la JEHOVAH AMESHINDA na yeye mwenyewe Askofu hajulikani alipo, nini kinaendelea" alizungumza yule kijana Tena.
*******
Haya yakiendelea nchini Tanzania, Burundi Hali ilikuwa hivyo hivyo huku magazeti Yakipambwa na picha ya bastola na pasi ya kusafiria ya Thobias Chumvinyingi huku kukipambwa na maneno ya kifaransa kuwa huyu ndiyo muuaji wa.mfanyakazi wa hoteli ya Roca Golf na anatafutwa na vyombo vya ulinzi na usalama, hasa idara ya ujasusi nchini humo SNR, huku akikolezwa kwa maandishi ya mtu hatari na jasusi kutoka Tanzania huku kukitolewa tahadhari kwa maeneo ya mkusanyiko wa watu wengi huku donge nono la dola 25000 zikiahidiwa kutolewa kwa atakaye fanikishwa kukamatwa kwake, hayo yote aliyaona kapteni Jumanne baada ya kuazima gazeti, safari haikuwa ndefu sana hatimaye daladala waliyokuwa wameipanda iliwasili kwenye mji wa Gatumba, mara baada ya kushuka hakutaka kuonekana kama mgeni haraka alisogelea maegesho ya Taxi na kumfata mzee mmoja aliyekuwa akisubiri abiria kwani hisia zake zilimtuma hivo.
"kijana wangu hujambo, tunaelekea wapi" alianzisha mazungumzo mzee yule huku akilitia moto gari lake moto kuingia barabarani
"sijambo msee, nipeleke belvedere tafadhari nkapate kifungua kinywa" aliongea kapteni Jumanne, rafudhi yake ilimfanya ageuze kioo cha katikati ili kumuona vizuri sura ya abiria wake akatabasamu.
"kwa mara ya kwanza tangu nianze kazi hii sikuwahi kupata abiria anayetoka katika taifa la kenya.......japo mama angu ni mtu wa huko na bahati mbaya alifariki tungali watoto wadogo na hatukufanikiwa kufika huko hata angalau tuwajue ndugu zetu wengine, ila kusikia sauti nimefarijika sana naitwa cliff sibomana" alimaliza na kutaja jina lake huku tabasamu lake likiwa lile lile, muda huo walikuwa wakiyapita majengo kadhaa ya jiji lile huku wakisindikizwa na mziki wa mahadhi ya hip hop kutoka kwa mwanamziki Tupac Shakur na kibao chake cha 'My block' kilichomfanya kapteni Jumanne atabasamu na kukumbuka maisha yake mtaani hasa pale kwenye mstari wa mwisho wa 'verse' ya pili " i close my eyes and picture home for my block"
"msee mbona ka iko wewe hufananii na hii mughizi"alisema hivo kapteni jumanne huku akitupa na swaga ili aendelee kuvuna pointi tatu kwa mzee huyo
"hahaha vijana tatizo mnahisi sisi hatupendezwi na mahadhi haya na nyie ndiyo mna haki ya kusikiliza, usisahau hata mimi nilikuwa kijana kama ulivyo, tena mimi huenda nilikuwa zaidiyako pengine, burundi hii nimeizunguka nikila bata kweli kweli, nilitaka kufika nairobi maana naskia ni jiji la raha na gharama afrika mashariki hii.....ila sikufanikiwa kwa sababu nilipata msala mzito ulinimaliza kila kitu nimedondokea huku kusogeza siku" alisema mzee yule kwa bashasha huku akimaliza kwa sauti ya masikitiko.
"pole sana mzee japo sijui kilichokupata ila inaonekana hakikuwa chema ila naamini kina kuhuzunisha kila ukikikumbuka" alisema kapteni jumanne kwa udadisi
"ni stori ndefu kijana wangu ila kiufupi nilifungwa jela kwa kosa lisilo langu na huwezi amini waliofanya hilo kosa walikuja kutoa ushahidi dhidi yangu na walinikandamiza kweli kweli nilibaki nikipigwa na butwaa kwenye kizimba mwisho wa siku nikaiona milango ya gereza na mimi kumezwa humo kwa muda wa miaka kumi na tano......maadam upo jiji hili siku moja ntakusimulia labda nkuachie anuani yangu kijana, alafu tushafika mg hahawa ndiyo huo hapo mbele." akampa kikadi kilichoonesha anuani ya mzee yule dereva taxi, na muda huo alikuwa ashafika katika mgahawa huo, wakaagana na kapteni Jumanne akisogelea moja ya Meza na muda uliofata alikuwa ameshaketi na mhudumu alikuwa mbele yake kupokea oda ya chakula kutoka kwa mteja huku akitumia lugha ya kifaransa ambayo ilijibiwa vizuri na kapteni Jumanne.
"karibu chakula kaka mzuri" aliuliza yule Dada kwa lugha Ile Ileya kifaransa huku akitabasamu.
"Asante Dada mzuri" alisema huku Akitabasamu huku sekunde ya pili akikivuta kijiko na kwanza kuishambulia supu Ile ya kuku na maandazi matatu yaliyokuwa kwenye sahani ndani ya dakika kumi alikuwa mbele ya Meza ya malipo.
"Samahani naweza kufanya malipo kwa kadi" aliuliza kapteniJumanne.
"bila shaka mashine ni hiyo hapo" kauli Ile ilikuwa kama taa yakijani kwa kapteni Jumanne, naye hakusita kuchanja kadi yake aliyokuwa ameisunda katika mahali ambapo palikuwa Salama zaidi hasa ukizingatia alitambua madhara ya safari za usiku, baada ya kupata kifungua kinywa Sasa mwili wake ulikuwa umeanza kurudisha utimamu wake kitu kilichobakia ilikuwa nikuondoa uchovu na kukutana na Thobias Chumvinyingi, alielewa kichwa chake kisha kuwa dili na kukutana maeneo ya watu itakuwa ngumu
"atakuwa wapi huyu mtu" alijiwazia kapteni Jumanne alichekecha akili kwa sababu hakuwa na Ramani ya wapi pa kuanzia. Suluhisho aliona akapumzike kwanza Kisha aanze kaziya kumtafuta mwenyeji wake
******
TSS HQ- DAR ES SALAAM
Saa 2:30 asubuhi
Ni asubuhi nyingine, ofisi hii ilikuwa na pilika pilika huku wanausalama katika ofisi hii walikuwa bize kiasi kwamba hakuna ambaye alikuwa amesimama bila kazi hata chifu mwenyewe ambaye ndiyo bosi wao alikuwa bize akitazama taarifa za mtu aliyefikishwa alfajili ya siku hiyo, faili hili lilikuwa na rangi nyekundu na yenye maandishi meusi yenye nyota tatu katikati, huku yakikolezwa na maandishi meusi 'TOP SECRET', Punde simu ya mezani ilitoa mlio kumaanisha kulikuwa na simu inaingia, akanyanyua mkono wa simu Ile na kuiweka sikioni huku umakini wake ukiendelea kutazama taarifa zilizomo ndani ya faili lile.
"samahani Chifu, kuna wageni wako wanahitaji kukuona" ilisikika sauti nyonyoro wa katibu muhtasi wake Mwanamama Caroline chakachaka.
"waambie waje saa 7 za mchana Sasa hivi Nina kazi na usisahau mheshimiwa raisi atakuwa hapa muda wowote" aliongea chifu huku akionekana kukereka.
"ni jenerali yuko na wale watu wa siku Ile" alisema Tena yule mwanamama mweupe wa rangi, macho makubwa, nywele kazitengeneza mtindo wa fidofido huku akibeba umbo la kuvutia ambalo kwa umri wake wa miaka 45 ni Nadra sana kumkuta nalo mwanamke wa umri wake, midomo mipana iliyowatoa udenda wavnaume kibao ila ndiyo hivo hawakuwa na namna ya kukubaliana na ukweli kwamba kujisogeza kwake ni kukisogelea kifo kwani mwanamke yule ni mke wa ndoa wa Chifu, miiko ya kazi ilikuwa pale pale na miaka yote aliyofanya kazi kama katibu muhtasi wa mkurugenzi wa idara ya ujasusi hakuwahi kuleta mazoea au majivuno kisa tu bosi ni mmewe.
"ooooohh waruhusu na waambie waingie tafadhari, Tena wamefika wakati muafaka" japo alikuwa kazini Ila kibinadamu roho yake ilisononeka kufoka Tena kwa mtu mzima kama yule, alimezea na alijua wapi ataenda kuomba msamaha na muda huohuo aliingia jenerali akiwa katika vazi lake nadhifu huku kofia yake ikipambwa na nyota nne, huku nyuma yake akifuatiwa na mtu aliyevaa suti nadhifu ya rangi ya bluu bahari kwa umbile alikuwa mwanamke ila tembea yake ilimsadifu ni mtu wa Aina gani hakuwa mwingine Bali ni Chausiku Deusi huku nyuma yake pande la mtu lilikuwa katika gwanda za jeshi, naam alikuwa katika gwanda zilizomtambulisha kama komandoo wajeshi la wananchi huku bawa la ndege katika kifua chake upande wa kulia lilisadifu kuwa mtu huyu amefuzu mafunzo ya juu katika medani za kijeshi, kofia ya zambarau na vyeo mabegani vilimsadifu kuwa yeye ni Nani? katika jeshi, kwa Hakika asubuhi hii alipendeza kiasi cha kumfanya chifu atabasamu, kwani hakutarajia kama angeshangazwa kiasi hiko, baada ya kufunga mlango wote walikakamaa na kutoa heshima mbele ya chifu mpaka jenerali na yote ni kwa sababu Chifu ni bosi wao wote.
"karibuni mketi.....niseme tu ugeni went umenipa faraja na niseme tu mmefika wakati sahihi" aliongea chifu huku akiwataza wote kwa umakini
"jenerali tangu mwanzo nilikueleza hii kazi ni ngumu na hapa nilikuwa napitia taarifa za huyu akofu wa kanisa la 'JEHOVAH AMESHINDA', aiseee taarifa zake zimenisisimua Sana yaani hapa nilikuwa nawaza vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinakwama wapi mpaka kufumba macho na watu hawa kuifanya hii nchi kama ghetto Lao la kufanyia uchafu wao, Katika taarifa zilizomo humo ndani…….jenerali, watu wangu walioko idara ya uhamiaji wameweka rekodi Sawa kwamba Jamaa siyo raia wa nchi hii"
"whaaaaat!!!! Hebu chifu tuwekane Sawa kwenye Hilo" aliongea jenerali kwa kupigwa na butwaa ila pia katika namna ya kutafuta ufafanuzi.
"ni kweli kabisa Jamaa siyo raia wa nchi hii japo alivihadaa vyombo vya ulinzi na usala ila Jamaa ni mzaliwa halisi wa nchi ya............Ghrrrr Ghrrrrr......aaaahhh sorry ni simu yamheshimiwa raisi" aliongea chifu huku akipokea simu Ile iliyotoa maelekezo kuwa dakika chache kutoka pale angekuwaofisini kwa chifu na haikusubiri kujibiwa.
NIMEJIKUTA HATA MIMI NIKITAMANI KUJUA HUYU JAMAA NI RAIA WA WAPI? JE HII SIMU ILIYOINGIA HIVI SASA ITALETA TATIZO JIPYA AU INA KITU GANI?? TUKUTANE TENA TOLEO LIJALO.Tchao
 
"Katika ulimwengu wa ujasusi, ukweli ni silaha yenye nguvu, lakini baadhi ya majasusi wanajua kuwa kukaa kimya kunaweza kuwa na matokeo makubwa zaidi kuliko kusema uwongo." Kwani nukuu hii ina maana gani nisome ugundue ambacho hujui tangu umeanza kuisoma simulizi hii
Tuendelee…………
"ni kweli kabisa Jamaa siyo raia wa nchi hii japo alivihadaavyombo vya ulinzi na usala ila Jamaa ni mzaliwa halisi wa nchiya............Ghrrrr Ghrrrrr......aaaahhh sorry ni simu yamheshimiwa raisi" aliongea chifu huku akipokea simu Ile iliyotoa maelekezo kuwa dakika chache kutoka pale angekuwa ofisini kwa chifu na haikusubiri kujibiwa.
"Janani nimepokea simu kutoka kwa mheshimiwa raisi kuwa atakuwa hapa " aliongea tena chifu huku jenarali bado akiwa na duku duku lake moyoni juu ya kula jambo Zito Chifu kumuacha njiani ....alishindwa kuonesha kuchukia kwa sababu huo ungekuwa utovu wa nidhamu hivyo alimezea tu na Hali ya ukimya kutawala mle ndani, dakika mbili peke ziliwatosha kusikia heka heka huko nje na punde mlango ulifunguliwa na mheshimiwa raisi akiingia huku akiwa katika suti yake ya pande mbili ya rangi nyeusi huku ikiwa imempendeza na wote walisimama na kumpa heshima huku Chifu akimpisha mheshimiwa raisi kwenye kiti chake, Kisha wote wakaketi.....mheshimiwa raisi akalitazama lile faili akalipitia kwa muda wa sekunde sitini na kuliweka pembeni huku akichukua faili jingine lenye rangi Sawa na Ile na kukutana na sura ya mtu hakuwa mwingine Bali Mohamed mahboob hakukuwa na taarifa nyingi Sana ilaalivutiwa na maandishi yaliyokolezwa kwa wino mwekundu'UFUNGUO WA KUTOKOMEZA UGAIDI NCHINI' maandishi Yale yalimsisimua kiasi cha kumtazama chifu huku macho Yao yakiongea lugha ya kijasusi kwani wote walikuwa watu wa Aina moja.
"chifu unasubiri nini kupata maelezo ya kujaza kurasa kwenye faili hili" aliuliza mheshimiwa raisi
"nilikuwa nikifata kile tulichoongea Jana usiku mheshimiwa" aliongea chifu kwa sauti yenye unyenyekevu mkubwa, na hapo macho yake akayahamisha kwa jenerali
"jenerali natambua nilikupa hii oparesheni ila utajiuliza kwanini maelekezo mengi Nampa Chifu.......ni kwasababu ofisi yako siyo Salama, ndiyo siyo Salama kwasababu imepoteza nyaraka muhimu Sana ambayo mwanzo ililindwa kwa gharama kubwa ila imepotea kizembe Sana, natambua uliambiwa faili jeusi lilikuwa likishughulika na mambo yanayowahusu luteni kanali Charz na wenzake huko DRC ila siyo kweli, ulipigwa changa la macho, japokuwa wewe ni jasusi ila ulishindwa kuunda doti kupata mstari, Faili Jeusi lilihusu maabara ya siri ya kutengeneza mabomu kupitia uchimbwaji wa madini ya yureniamu na mwanzo kabisa ilianza kama uzalishwaji wa nishati ya umeme, lakini baadae iligundulika jeshi kupitia jenerali mstaafu wanazalisha mabomu hayo hatari ulimwenguni na huwezi kuamini, daktari aliyekuwa akiyazalisha ilikuja kugundulika ni gaidi wa kimataifa anayesakwa na marekani na alijificha kwenye kichaka cha udaktari tulimkamata na kumfungia gereza la ukonga.....na huo ndiyo mwanzo wa jenerali mstaafu kumuandikia barua raisi mstaafu kuomba kujiuzulu na Hilo lilifanyika kwa uharaka ila wakati unakabidhiwa ofisi kuna nyaraka ulifichwa na hukupaswa kuzijua kiufupi zilistaafishwa machoni mwa watu kama wewe" aliongea mheshimiwa raisi huku akimkazia macho jenerali ambaye alikuwa akichakata kwa umakini kula sentensi katika kauli Ile ya mheshimiwa raisi.
"hivyo kuna mengi utayajua kupitia huyu.......na Imani atatapika nyongo waliyoifunga na nati ngumu za mjerumani Charz na Chiku it is your time to show him how devil you are, asiache hata neno moja kinywani kwake" aliongea raisi huku akinyanyuka na wao wakaamka kuelekea alipowekwa Mohamed mahboob.
"walimkuta amesimamishwa katika chumba kimoja na chapchap luteni kanali charz alichukua kisu na kukivuta kiti kilichokuwa kimetengenezwa kwa muundo wa kama wa mfuko wa chumvi chumvi kwenye sehemu ya kukalia na Kisha kuikata kwamtindo wa duara Kisha alimfata Mohamed mahboob na kuzirarua nguo zake zote Kisha kumuacha kama alivyozaliwa, ngumi moja kavu ya tumbo ilitosha kumfanya ajipinde huku akigugumia maumivu na wakati huo huo alibebwa n akukalishwa kwenye kiti kile huku mikono ikikazwa kwa nyuma, akavuliwa kigunia cheusi na hapo alikutana na sura zilizomchakaza huko babati manyara.
"heeeeeh ni nyie Tena" alitahamaki kwani watu waliokuwa mbele yake sura zao hazikuonesha mzaha hata kidogo na alijuayuko pale kwa sababu gani? Mahojiano.........
"mnajisumbua tu Arusha asubuhi ya Leo kutakuwa na vilio nakila kona kutakuwa na maturubai hahahaha" alitoa kicheko huku akiwatizama badala yake usoni mwa mwanaume yule mwenye gwanda la jeshi na mwanamke yule mwenye suti alikutana na tabasamu, siyo tabasamu la furaha Bali tabasamu la uchu la kufanya unyama......looh Koo lilimkauka ghafla.
"sikiliza bwana mdogo hapa hatujaja kutazama onesho la vichekesho labda kama hujui, Ashraf,hussein,Mansoor,Seif, ustaadh Othman omary na wewe hapo tamari mmeingia mikononi mwa serikali na mabomu yote tumeshayapata na jiji liko Salama kabisa bwana Mohamed" aliongea chiku huku akimzunguka.
"Sasa kama jiji lenu lipo Salama mimi mnaniuliza nini kingine nipelekeni mahakamani Sasa" aliongea Mohamed kwakupayuka huku hasira ikiwa imemkaba kooni, alitulizwa na kibao cha mgongo kilichomfanya ajikunje kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa.
"siku nyingine ukiwa unaongea na watu kirafiki usipayuke kamauko mnadani......alafu wewe ni mwanaume simamia kauli yakona sauti uliyoanza nayo, muda wa kupayuka ukifika utapayuka mpaka sauti iishe, tumeelewana ndugu" aliongea chiku huku akimsogelea usoni.
"nataka kujua yuko wapi SAIDI CHAKUPEWA na MUSTAPHA ABD NUR AHMED na aliyewafadhili kufanya ugaidi Arusha" alitupa swali Chiku huku akimtazama usoni Mohamed Mehboob
"hahahaha kalale na baba ako Malaya wewe alafu umuulize hivyo atakujibu" aliongea kwa jeuri Kisha akamtemea mate katika kifungo suti na kurudia kicheko, luteni kanali Charz alimpa Ishara ya kumuacha Kisha akasogea karibu na ilipo Meza, na kwanza kuvua bareti, Kisha akatoa kitambaa kilichobeba wadhifa wake jeshini na kuvua gwanda la juu na kubaki na Tsheti(jungle green), na kumgeukia mtu yule aliyeko kwenye kiti.
"wakati Nikiwa mafunzoni katika nchi ya Japan nilivutiwa Sana na mchezo wao wa ki mapigano unaitwa 'SUMO' nadhani ulishausikia hata kuuona kwenye televisheni bwana Mohamed......kilichonivutia siyo vile wanavyo angushana kama wacheza mieleka hapana, kilichonivutia ni vile wanavyolinda sehemu zao za Siri kwa kuzibana na kuzificha isitokee hata bahati mbaya zikaguswa wakati wa mchezo huo, wewe ni mwanaume kama mimi hivi unatambua ni kwanini korodani hujificha kipindi chote wakati wa ukuaji hadi wakati wa balehe ndiyo huning'inia katikati ya miguu yako; hahaha pengine ni kwasababu ya uzito wake na nguvu,ila nikwambie tu korodani ni sehemu muhimu Sana kwenye mwili wa mwanaume yoyote kama wewe Sasa nisingependa kumaliza kizazi chako kwa kuzisumbua, nahitaji unijibu kile ulichoulizwa chap kwa haraka" aliongea luteni kanali charz huku akimtazama.
"sibabaishwi na hizo hadithi zako za magazeti ya udaku wewe fanya unalofanya mm sijui chochote" alipayuka mtu yule nahapo hapo alishangaa mkaa wa moto umemwagwa chini ya kiti na muda huo uume na korodani za Mohamed zilikuwa zikipashwa joto na sekunde iliyofata alijikuta akibweka kama mbwa kwani alipigwa na kitu kama mpira mgumu uliofungwakamba na ulizipiga korodani zote na kuzifanya zisambaze maumivu makali Sana yasiyovumilika.
"ongeza moto hapo chini nataka tuzibanike kabisa ili asilete kizazi kibaya katika nchi hii....nataka baada ya hapa ashuhudie mkewe na watoto wake mapacha wakifa mbele yake ili ajue nini maana ya Maisha.......huwezi ukajisifu kupeleka kilio kwa watu huku na wewe una Familia msiba utaanza kwake kabla ya saa nne ya asubuhi" alikoroma luteni kanali Charz huku Chiku akiongeza na kuukoka moto kiasi cha kwanza kuwaka, jasho na yowe la hofu vilimtoka Mohamed kiasi cha kuifanya rangi yake nyeupe kwanza kubadilika kuwa nyekundu.
"hahahaha Sina Familia mimi......mnajidanganya tu kwa kuwapata watu ambao siyo sahihi hehehehe" alisema kwa kebehi bwana Mohamed
"Vipi kuhusu shehe wa mkoa wa Arusha bwana Jafari tambisa....naye siyo mtu sahihi" aliuliza Chiku huku akimkazia macho.
"sikiliza bwana Mohamed tumesha ambiwa wewe siyo raia wanchi hii, ndugu yako aliyejificha kwa Jina la mtu ambaye amefariki miaka thelathini iliyopita, ndiyo mkaona yeye atumie huku wewe ukitumia Jina la mtu ambaye kwenye taarifa za watu katika taifa hili hazipo na mtu anayeitwa Mohamed mahboob inavyoonesha hakuna mtu anayeitwa hivyo na pia mahojiano makali aliyofanyiwa amekiri kuwa kaka yako wa damu na wote ni raia wa Kenya, mliingia Tanzania mkitokea Mombasa kupitia mpaka wa horohoro mkajipenyeza Tanga na Sasa mkajiwekea makazi Arusha na kaka yako kupitia watu wenu wanaowafadhili akafanywa kuwa shehe wa mkoa ili mtimize mipango."
"Sasa kama amewaambia yeye si mngemuuliza hayo maswali mnakuja kujisumbua kuniuliza mimi ikiwa Sina majibu" alilalama Tena Mohamed mahboob kwa maumivu makali.
"mpaka tunakuja kwako ujue hatubahatishi ngoja uone madhara ya kukaa kimya" alimpiga Tena ule mpira safari hii alibwekaTena kama mbwa na muda huo huo akawekewa Kimbao mdomoni huku akipewa onyo la kuto kukidondosha labda tu kama anataka kujibu maswali, waliangalia kamera na muda huo aliletwa shehe wa mkoa bwana Jafari Tambisa akiwa amechokakwa kipigo Ile amekaa tu Chiku akamshindilia risasi ya paja na kumimina spirit chupa nzima Alicia Sana kiasi kwamba alizimia kwa maumivu makali aliyokuwa anayasikia, kilio kile kilimfanya Mohamed aumie Sana ila hakutaka kuonesha Hilo ila alikwisha Chelewa kwani macho yaliyo makini kutazama nyendo zake yaliuona msisimko wake ' kweli damu ni nzito kuliko maji'
"mmwagie maji ya baridi huyu anajidai kuzimia wakati mzima tu.....hatuna faida na mtu anayejifanya ni shehe kumbe gaidi" aliongea chiku na muda huo huo luteni kanali Charz alichota maji ya baridi na kumumwagia usoni, kitu kilichomfanya aziduke.
"bila ndugu yako kusema ukweli utakufa ukiteseka nadhani unaelewa maana yake" aliongea Chiku huku luteni kanali Charz akimsogelea na kumtandika vibao viwili vikavu vya kumtoa wenge vilivyomfanya atoe machozi.
"unalia nini wewe 'CHUI ULIYEJIFICHA KWENYE NGOZI YA CHUI' gaidi mkubwa kama wewe unalia na hapa sijakugusa." Kauli hiyo ilimsisimua Tena bwana Mohamed mahboob, kikavutwa kiti kingine na hapo Mohamed alijua nini kinafatia, Koo lilimkauka na punde akamuona ndugu yake akiwa mtupu huku akimtazama huku macho yao yakiongeakuwa hawana namna ila Mohamed akajipa subira sekunde iliyofata alisikia kilio cha ndugu yake huku kikifuatiwa na tusi kubwa la nguoni lililokuwa kama kipooza maumivu.
"mdogo wangu mudi waambie tu.....naumia ndugu yako, mkeo tangu wamemchukua sijapumzika mateso" alilalama mtu mzimayule wa urefu futi Sita pointi mbili, mweupe wa rangi na mwili mnene kiasi huku ukiwa na kitambi, umri wa miaka arobaini na saba ila Alilia kama mtoto mdogo, mkaa ukavutwa na kuhamishiwa pale Chini ilisikika kilio tena kilichomfanya friji la Mohamed kuacha kugandisha na badala yake kikaanza kupasha
"nasema......nasema muacheni kaka yangu hajui kitu" alilalama tena Mohamed na wakati huo mheshimiwa raisi alikuwa akiusubiri kwa hamu akampa Ishara chifu ya kamera zote kuzimwa na badala yake waingie huko kwenye mahojiano.
"well well done vijana, mmefanya kazi nzuri Sana, Sasa ni zamuya hawa magaidi kuniambia washirika wao.........heeeeeh kumbe na wewe shehe wa mkoa siyo raia wangu, Sasa ndugu zangu mniskilize kwa makini tutatumia karatasi kumaliza hili tumeelewana, kwanza kwa mlipofikia sauti zenu zinakata sitasikia vizuri nipeni maandishi ya vitu mlivyoombwa na jingine hili nahitaji mniambie ni wapi mnapokalia vikao vyenu na Nani mwenyekiti wake hivyo tu" aliongea raisi na kutoa Ishara na chifu akatoa karatasi nyeupe na kalamu katika mfuko wa Kaunda suti aliyovaa Kisha kumkabidhi mheshimiwa.
"Mohamed katika shughuli zako za biashara unapenda kutumia mkono gani kupigia hesabu na kusaini mikataba"
"Waa..kulia" alibabaika kwa maana mtu aliyopo mbele yake nimtu mzito katika nchi hii na alikuwa mbele yake macho kwa macho na siyo kwenye televisheni alipozoea kumuona na kusikiliza sauti yake katika kipaza sauti, mheshimiwa raisi alitoa Ishara na punde mkono wa Mohamed ulikuwa huru isipokuwa mkono wake wa kushoto na mguu uliunganishwa na Meza Ile ya chuma akasogezewa karatasi nne huku akipewa onyo kali la kutokuacha hata nukta kwani silaha mbili zilikuwa zimeinuliwa na kuelekezwa kwenye kichwa cha shehe Jafari Tambisa huku macho makini ya Chifu ikizisoma fikra na nyendo za Mohamed, saa ya ukutani ilikuwa ikipiga ule mlio wa 'Tik Tak!' Ikizihesabu sekunde.
*****
MSASANI -DAR ES SALAAM
saa 3:10 asubuhi.
Katika nyumba moja ya kifahari, Simu inaita na kupokelewa na pande la mtu Lililojaa mwili kutokana na kuifata kikamilifu ratiba ya mazoezi, huku kiunoni likiwa limejifunga taulo jeusi.
"Heshima kwako mkuu" lilisema jitu lile kwa unyenyekevu
"una Habari zozote kuhusiana na mpango wetu ule wa kwanza?"
"mpaka naenda kulala kila kitu kilikuwa Sawa.......ila Leo sijapata chochote"
"chukulubu are you serious? With this huh unataarifa kuwa kila kitu kimeanza kuharibika do? you know wameanza kusogelea hadi ngomeni anytime wanaenda kutuweka uchi kweupe, you sleeping too much, mkuu kakasirika kupita maelezo kwamba why tunazidiwa akili na yule mwanamke" ilikoroma
"mkuu Sasa hivi sipati taarifa za uhakika ni kwamba kaamua kutokumuamini mtu yoyote isipokuwa Chief, na kinachoendelea ni kwamba kuna watu hatari Sana wametumwa kutuliza mtumbwi tuliyokuwa tunautoboa na kiukweli wameanza kufanikiwa nikutoe wasi wasi Leo Arusha itamfanya Chai aone ni kahawa don't worry mkuu atakuwa wa mwisho kuuona mtumbwi ukizama kwenye kina kirefu Kisha tutampa mimba atakayoenda kuzalia kuzimu" lilisema lile pande la mtu
"hebu amka katika huo usingizi, watu wote wameshadakwa na wapo katika mahojiano makali ambayo huenda yakawatapisha nyongo mbona umetoka kwenye ule utimamu niliyokufanya wewe ukawa jenerali, umepoteza umakini kiasi kwamba unashindwa kupata taarifa kutoka kwa watu wako Kule monduli kwamba ustaadh alikuwa kisongo akisulubiwa na vijana uliowapa recommendation ya kwenda urusi hivi unatambu......" Alikatishwa
"unataka kusema 'watoto wa nyati' wamerudi mjini?" Alisema jenerali mstaafu huku akiweka uso wa umakini kwani taarifa anazozipata kutoka kwa mtu huyo ambaye inaonesha ni mzito
"Haukuwa katika nafasi ya kuniuliza maswali, ila kwakuwa mambo ni hivi inabidi nikueleze kinagaubaga, hivi unatambua Mohamed na Familia yake wamefichwa idarani, hivi unatambua ya kwamba Malaya wako wa kigoma ndiyo katufikisha hapa, hivi unatambua huko Burundi tayari kuna nyoka kaingia chumbani na umeme umekatika?
"inabidi yule Malaya asiione sikukuu ya nane nane maana tumemchekea Sana Sasa Anaanza kutushika sharubu iwe kwa sumu au risasi Jerry anatakiwa alimalize hili suala haraka iwezekanavyo" aliongea kwa hasira.
"be smart ex-general, hivi unatambua kinachoendelea ni kwamba mudi na ndugu yake wanakula kibano kikali na alfajiriya Leo ilitoka order kutoka kwa chifu kwenda kwa mkurugenzi wa ulinzi wa raisi kwamba kuanzia siku hii raisi atalindwa na kikosi chake alichokiunda na kibaya zaidi ni watu wakatili Sana mkuu amesema, ni watu nane, wanaume watano huku wanawake wakiwa watatu, hiyo siyo shida, shida ni kwamba wanawake wawili ni maninja na wanaume watatu wana taaluma hiyo hiyo ya uninja ambayo ilipigwa marufuku duniani kote kitu ambacho kimemstua Sana mkuu, kiasi cha kumuona ni kikwazo katika hili." Aliongea kwa msisitizo mtu yule huku sauti yakeikiwa ya utulivu.
"unanichanganya mkuu kwa sababu haya mambo yamefanyika usiku mzito"
itaendelea******
Hata mimi nimechanganyikiwa ni kwanini mambo haya yamefanyika usiku mzito, je ni nini chachu ya haya mambo? Tukutane toleo lijalo Tchao
 
“Msela yake noma ila kwenye noma msela hakai” Fortunatus Buyobe.
Endelea…….
"bado huja changanyikiwa hivi unatambua IGP hatuko naye duniani Toka alfajiri ya leo stop using Cognac too much you lose....... focus,umekuwa mzembe kiasi cha mkuu, kuwa pilipili kila sauti yake inapopenya kwenye ngome za masikio yangu, sikiliza mtu aliyeingia ngomeni amejiacha uchi kweupe kwani amejitambulisha yeye ni Nani hili ni kama tusi kwa idara kuwatuma wanafunzi, japo kayeyuka kama barafu ila ameshaliingizia taifa lake uhasama na ngome, na kingine cha kusikitisha ni kwamba Askofu amefichwa idarani, Hilo la kufichwa siyo suala, ngoma imeanza kuwa nzito kwa wamarekani kuingilia mchezo huku wakiwa hawana mzaha wanawataka watu wawili ambao ni Karata muhimu Sana"
"akina Nani Hao mkuu?" Aliuliza Tena jenerali
"hivi wewe bado umelala si ndiyo ni hivi wa marekani wakija kwako kwa sura ya mbuzi ni either ugaidi au madawa ya kulevya, unakumbuka wakati nikiwa pale kwenye kiti nilimpambania Sana asichukuliwe Sasa kipindi hili huyu mama na ujasusi ni Pete na kidole hivyo wakimpata Mohamed anawapa ila hivi Sasa anawapatia Askofu kitu ambacho hata mkuu kinamnyima usingizi, wakati ambao Jerry alitakiwa kufanya kazi ndiyo tunazidiwa akili, mkuu ameuhusudu uwezo wa huyu mama kwakuwa na akili nyingi Sana kiasi cha kupendekeza Jina lake kwa ajili ya kwenda Cuba na Kisha marekani kabla ya kurejea na kuteuliwa kuwa mkurugenzi msaidizi huku mmewe akimrithi mikoba ya mkuu" alitoa maelezo yule bwana wa upande wa pili
"unanisisimua kwa hizi taarifa mkuu"
"hivi unataarifa kwamba luteni kanali Charz yuko mjini na amepewa fagio kusafisha kila utando wa but but ulioanza kujishikiza na unajua Alivyo na kisasi na wewe"
"whaaaat.....mbona taarifa zinasema hayuko kazini na ni kutoka kwa mtu wa uhakika ofisini kwa jenerali"
"wameshapiga hatua kutufikia nikikueleza hawa watu wawili, Chifu na huyu mwanamke ni kama tui la nazi na maziwa hufanana kwa rangi, hutoniamini ila nikueleze tu ukweli meja Tumbaku na Diana wamekutana na vitu vya ajabu, mwanajeshi mwenye gwanda la polisi ndiyo huyo aliyempeleka askofu shimoni Tena kikatili Sana, naomba kina Jerry wahakikishe huyu mtu na luteni kanali Charz wamezikwa kabla ya jumapili.......mengine tutaambizana kwenye kikao
"saw......titititi" Simu ilikatwa ikimuacha yule Jamaa kwenye msongo wa mawazo hata mwanamke aliyekuwa amelala kitandani hakukumbuka uwepo wake amekuja kustuka mikonolaini ikimpapasa huku akipulizwa na upepo mgongoni uliomfanya mwili wake usisimke.
"Hey Sabina siko kwenye hiyo Hali nzuri, kuna kazi nzito mbele" alisema jenerali huku akitazama mbele
"ni nani huyo anayefanya nishindwe kuburudika na mpenziwangu nikaumwage ubongo wake kwa risasi yangu moja tu na jongoo wako asilale tena" alitoa sauti ya madeko huku akiwa ana Maanisha anachokisema huku hisia zikiwa juu.
"unataka kumjua anayeisumbua akili yangu na hata nikikutuma unaweza kuitumbukiza risasi kwenye kichwa chake?"
"asilimia zote mpenzi.....mtoto wangu hajakohoa siku nyingi Sana" alijigamba Tena yule Binti ambaye alikuwa tayari kufanya chochote kwa Jina la mapenzi na hisia zake kwa mtu huyo ambaye ndiye chanzo cha yeye kwenda kozi mbali mbali kiasi cha kufikia hatua ya ukomandoo Hakika ilitisha na kikubwa zaidi alisifika kwa ulengaji wa shabaha, alikuwa moto wa kuotea mbali Binti huyu wa kikurya, jibu lile lilimfanya jenerali ajifikirie Mara mbili huku akimhurumia Binti huyo maana kazi iliyoko mbele kifo kilikuwa karibu na macho.
"nahitaji Chifu asilione Jua la kesho......huyo ndiyo anayesumbua kichwa changu" aliongea jenerali kwa msisitizo
"whaaaat.......Chifu huyu huyu hapana ni rahisi kumfikia raisi ila ni ngumu kumfikia Chifu kwanza anaogopwa na kula mtu hadi jenerali na kingine nilichokisoma ni kwamba Ana ulinzi unaonekana na usionekana kama raisi ila yeye naskia analindwa na watu wakatili Sana kwakweli mkuu peke yangu sitaweza" aliongea kwa masikitiko Sabina huku akiwa anachekecha akili
"umeanza kuwa muoga.....umesahau nguvu tuliyonayo mipango utaipata baadae kwenye kikao" alisema jenerali huku akimalizia kuitupa suruali yake mwilini.
********
BUNGENI-DODOMA
Saa 3:30 asubuhi
Bunge lilikuwa limezizima tangu ujio wa mpambe wa raisi bungeni hapo na kikao hicho kuongozwa na naibu spika na kuitisha hoja ya kutokuwa na Imani na makamu wa raisi toka kwa waziri wa ulinzi aliyeiwasilisha huku akitaja tuhuma mbalimbali ikiwemo Ile ya uraia na kutuhumiwa kuhusika na kuihujumu nchi vile vile ubalozi ulioko burundi ambazo zilitosha kumuondoa makamu wa raisi kwenye kiti kile ila ilihitajika matakwa ya Katiba kupitia Ibara ya 50(g) ,Hakika haikuwa kazi ndogo, watanzania walikaa wakisikiliza kwa makini na mwisho Bunge liliridhia kwa kauli moja kumuondoa makamu wa raisi na punde tu baada ya kiti kuwa wazi, mpambewa raisi akiwa na bahasha yenye Jina lililopendekezwa na raisi na naibu spika alipopewa bahasha Ile Mara moja aliichana na kuwatangazia wabunge pendekezo la mheshimiwa raisi pamoja na kutaja Jina.
"ndugu zangu wabunge, kama ilivyo wapendeza na kutumia demokrasia katika kupiga kura iliyoleta maamuzi haya Sasa niwasomee Jina la mtu ambaye atamsaidia mheshimiwa raisi katika muda aliyo bakiza kabla ya kuelekea uchaguzi mkuu, Jina lilipendekezwa na mheshimiwa raisi ni la mheshimiwa 'MASELE MAJIMENGI' waziri wa ofisi ya raisi kazi maalum" Bunge lililipuka kwa shangwe na nderemo na bila kupoteza muda spika aliitisha hoja ya kupiga kura nayo ilifanyika kwa weledi mkubwa na punde waziri wa Katina na sheria aliwasilisha hoja mbili za upitishwaji wa mabadiliko ya sheria mbili huku mabadiliko yakiwa yamelenga kuongezwa makali ya adhabu ambapo wabunge walikubaliana kuwa adhabu ya kukutwa na hatia ya kusafirisha au kuuza dawa za kulevya iwe kunyongwa hadi kufa huku nyingine ni Ile iliyohusu ugaidi nayo ikitiwa makali ya kunyongwa hadi kufa kama ukijihusisha kwa njia yoyote iwe kufadhili au kula njama kufanya hivyo au kutenda kabisa ugaidi.
Watanzania wengi walizipokea sheria zile kwa shangwe huku wahusika wakishikwa na hofu na mbaya zaidi sheria zilielekezwa wazi kuwa utekelezaji wake utafanywa mubashara kwenye televisheni ya taifa, yote hiyo ni kulinusuru taifa.
********
TSS-HQ/IKULU-DAR ES SALAAM
Saa moja lililopita.
Mheshimiwa raisi alikuwa akipitia maelezo nukta kwa nukta baada ya kujiridhisha kuwa kilichoandikwa mle kilikuwa sahihina hapo bila kuchelewa alisema waongozane ikulu kuna kitu anataka wakione, walipofika ikulu Chiku na Luteni kanali Charz walishangazwa na mabadiliko waliyoyakuta tangu wanaingia geti la kwanza mpaka la mwisho Harika ulinzi uliimarishwa kuliko kawaida, waliingia ofisini kwa raisi huku watu wale nane wakijipanga mlangoni.
"nimepitia haya maelezo na nimeridhishwa na kile kilichoandikwa na yule gaidi ni kwamba kuna msululu wa viongozi wakubwa tu wa serikali za ndani na nje ya nchi lakini Hao ni kama mawakala ila mabosi wao wapo na mmoja wapo ni jenerali mstaafu mzee Chukulubu, nashindwa kumkamata kwasababu bado sijapata ushahidi wa moja kwa moja kuhusu uhusika wake ila watu tuliowapitisha kwenye tanuru wamemnyooshea kidole yeye, na kama tulivyokubaliana nanyi kuwa hii ibaki kuwa 'classified information' tunamuashia full kuanzia hivi Sasa na mnarudi kazini Leo mpaka usiku nataka kujua ni hatua ipi mmepiga." Aliongea raisi kwa msisitizo na muda huo macho yake yalitua kwa Chifu.
"kuna nini kinachoendelea mpaka unawatuma wanafunzi kwenye misheni hatari kama Ile au uliunda Tena kikosi chako kingine, kwa hili siwezi kumlaumu jenerali kwa sababu aliyetupaka matope ulimwenguni ni kijana wako, imekuwaje Thobias Chumvinyingi akafika Bujumbura." Aliuliza raisi huku akihitaji ufafanuzi na muda wote chifu alikuwa akitabasamu tu
"unajua mheshimiwa ukifahamu kanuni za mchezo kamwe huwezi kucheza Vijaya maana kisa moja litakugharimu, ni kweli kabisa Thobias Chumvinyingi katupaka matope ila tambua Burundi hivi Sasa ni Sawa na mtego wa panya, Kila mgeni kutoka Tanzania anachunguzwa Vikali kuliko kawaida, na ndicho kilichomkuta kijana yule nikutoe wasiwasi bado hakijaharibika kitu, wakati idara Yao inaongeza nguvu kumtafuta na sisi tunaongeza nguvu kutafuta ukweli, na kuna fununu kwamba aliyekuwa makamu wako naye yuko huko huko Bujumbura nafikiri adui yetu mkubwa atakuwa na ngome huko" aliongea Chifu huku akivuta glasi ya maji na kumimina kilichomo kinywani mpaka ikabaki nyeupe, akatengeneza Koo lake na kuendelea.
"unapokuwa mchezaji mzuri Sana wa michezo basi usisahau kuwa michezo hiyo hiyo inaweza kukucheza na wewe"
"una maana gani Chifu" aliuliza raisi kwa udadisi
"kilichotokea usiku mzito wa Jana kimetupa picha halisi kuwa kuna watu wazito katika nchi Ile hawataki ukweli ujulikane ndiyo maana gazeti Lao limetoka asubuhi na mapsma Sana kabla hata uchunguzi haujafanywa na Hali hiyo hiyo imejirudia kwenye gazeti letu moja hapa nchini kuhusu Habari ya IGP, kuwashikilia watu wao na kuharibu mpango wao wa kwanza kunaweza kuwafanya wachukue maamuzi mabovu na nafikiri aliyeko nyuma ya hili huenda anataka kitu kutoka kwenye nchi hii ni wenda anataka hiko kiti, Amani itoweke au analipiza kisasi, Katika watu wote tuliowahoji wanadai lengo kubwa ni kukuondoa wewe, kuhusu jenerali mstaafu yeye anaonekana mfadhili lakini katika akaunti zake zinaonekana pesa za kawaida ila hizi za ufadhili anazitoa wapi.......ana akaunti za Siri? No anatakatisha fedha? Mmmhhh Hilo Lina usahihi wa asilimia chache Sana ila taarifa aliyonipa jenerali wakati tunakuja ni kuwa mtu wetu aliyewatoroka Chiku na Charz amekutwa na noti kwenye waleti yake huku namba kwenye noti hizo zikifanana na zile zilizoibiwa Kule kwenye mapori ya singida, anakiri kuwa fedha hizo alivuta kibunda kimoja kwa ajili ya kujikimu na kufanya starehe, wenzake hawakugundua Hilo na ameeleza bayana ya kuwa baada ya mzigo kufika waliamriwa kugeuka na kuondoka huku mke wa makamu wa raisi atakayeondolewa na Bunge muda mchache ujao akiondoka na magunia yaliyojaa pesa kupitia ndege uliyomtuma nayo makamu wa raisi aliye asi akahudhurie mkutano huko Addis Ababa,Ethiopia" maelezo yaChifu yalimsisimua kila mtu mle ndani
"kwanini tusizizuie zisije kuingia kwenye mzunguko huko siku za usoni" alisema Chiku huku akimtazama Chifu
"ndiyo Maana nkasema ukijua ni muda gani usukume kete yako ya ushindi utamuacha adui akiwa Hana cha kusukuma, ukijua wakati na udhaifu wa adui yako Hakika hakuna vita utapoteza,mfanye adui yako akuone mnyonge alafu kwa vile Ushamsoma na kujua udhaifu wake mmalize na usishangilie ushindi huo kama unajua kuna nyayo zake ameziacha sehemu zifute na hizo, unadhani ni jambo la kawaida balozi kumalizwa kwa mtindo ule ambao sisi tuliopita kwa waalimu tofauti kwenye Sanaa ya uuaji tunasema ule haukuwa mshituko wa moyo tunasubiri vijana watupe ripoti." Aliongea Tena chifu huku akimtazama Chifu na kuweka vidole kidevuni.
"vyema......Sasa ni hivi kwa mujibu wa maelezo ya Mohamed Leo Wana kikao Chao cha Siri katika ukumbi wao wa Siri huko Sinza mori, Chiku unajua nini cha kufanya nataka kujua ni watu gani Hao ambao ni 'CHUI WENYE NGOZI YA KONDOO', Kisha utanipa majibu ikiwezekana Leo hii, luteni kanali Charz maelekezo yanasema mtu wetu yuko Tanga anajiandaa kuzamia kenya kupitia mapango ya amboni, hii ni intel ya uhakika kwani nilimtega yule mtu hapa hivyo utapigwa kampani na rafiki zetu hawa, mfadhili wao mkuu kama alivyosema chifu anaonekana kama ni jenerali ila kuna mtu ana jina la uficho 'Chatu' ila huyo siyo muhimu sana kama tukimjua mkuu wao, hivyo vijana mnajua ninicha kufanya, chifu na jenerali mnajua nini cha kufanya adui asitupotee machoni kwetu baada ya taarifa hiyo fupi niwatakie majukumu mema" alisema raisi
*****itaendelea
Kama mkuu wao siyo jenerali mstaafu atakuwa nani??? Unataka kumjua mkuu wa hujuma hizi tukutane toleo lijalo.Tchao
 
“Binadamu ni kiumbe anayeishi katika ulimwengu wa mabadiliko, akijifunza kupitia uzoefu, na kuunda uhusiano wa kijamii ambao huathiri maamuzi yake na desturi za jamii. Katika harakati zake za kutafuta maarifa na kuelewa ulimwengu, anajikuta katika mizozo na changamoto za kimaadili ambazo zinahitajika kutatuliwa kwa busara na ujasiri."…………unaweza usiielewe nukuu hii leo ila utaielewa siku moja tu tuendele……
MUTAMBU-BURUNDI
Saa 5:30 asubihi
Ni muda ambao ASP Richard alikuwa akipata kifungua kinywapamoja na Thobias Chumvinyingi huku wakijiuliza atakuwa wapi kapteni Jumanne, huku wakikabidhiana majukumu kuwa wakati Thobias akipekua nyaraka mbalimbali basi ASP Richard aelekee jijini Bujumbura kwa ajili ya kukusanya taarifa kuhusuu balozi pamoja na kuisogelea nyumba ya balozi kuona kama atapata chochote cha kuwafikisha kwenye ukweli, hasa ukizingatia afisa wa mwisho kuondolewa alikuwa ni balozi mwenyewe kabla ya maafisa wengine kuondolewa duniani kila walipoikanyaga ardhi hiyo, alishuka mpaka kwenye maegesho na Kisha kuchagua gari Aina ya 'Lexus GX' na kuitia moto kulitafuta jiji la Bujumbura na kwa fikra zake zilitakiwa kuanzia nyumbani kwa balozi alifika na kulipaki gari Hilo mitaa Mia tatu kutoka pale huku akilipaki karibu na mgahawa mmoja wapo na Kisha kutembea kwa hatua za kawaida huku akiyasoma mazingira Yale na kuyaweka katika kumbukumbu zake tayari kwa kazi ya usiku, aliporidhika aliondoka eneo lile huku akiwa makini kutazama vioo vya pembeni Hali ilikuwa shwari mpaka aliporejea Tena nyumbani pale kwa yule afisa mwandamizi wa ubalozi.
"umepata nini katika nyaraka hizi" alisema ASP Richard huku akimtazama kwa udadisi
"hebu ona hizi karatasi hapa, zilikuwa ni majibu ya kuwa maafisa kumi na Sita walikuwa wamekufa kifo cha Aina moja, lakini vile vile hata balozi yeye alikufa kifo hicho hicho na siku hiyo hiyo tofauti ya dakika kumi na tano ndiyo balozi aliuwawa hapo ripoti inasema ni mshtuko wa Moyo ila kuna kitu kipo nyuma yapazia, tazama hizi picha za hii miili ni kwamba kuna jeraha dogo Sana upande wa shingo ambalo kwa macho ya kawaida huwezi kuona, ukitazama picha ya pili na ya tatu pia Hali ni Ile ile komredi" alitoa maelezo Thobias chumvinyingi.
"kapteni jumanne atakuwa wapi, mpaka sasa hivi na hata simu haipatikani na hana uenyeji huku" alijiwazia Thobias chumvinyingi.
*******
PEMBA- ZANZIBAR
katika jengo moja la kifahari na lenye ulinzi mkali, anaonekana mzee mmoja ambaye bado mwili wake unaonesha una nguvu, kaunda suti nyeusi, mweupe wa rangi lakini vile vile sura isiyo tabirika, mbele yake kulikuwa na chupa ya pombe ya be imbaya brandi ya 'BOWMORE ISLAY' ndiyo ni pombe ya gharama huku ikiwa na karne kadhaa sokoni tangu itengenezwe mnano mwaka wa 1772 huko islay, scotland. mtu yule aliendelea kuigida pombe ile huku akichakata mambo kadhaa yaliyokuwa yakipita kichwani kwake, akachukua simu yake ya setelite na kuiwasha kisha kuipiga sehemu ilichukuwa sekunde mbili kuita kabla haija pokelewa na upande wa pili.
"yes boss"
"hii line iko Salama" iliuliza sauti nzito yenye kuchakata kila linalopita kichwani
"ndiyo master, haina shida yoyote nasubiri maelekezo yako" ilisema sauti ile kwa unyenyekevu
"huyo nyoka aliyeingia kwenye ngome, Giza hili lisiishe hajamfuata balozi" alisema yule mtu mzito kwa sauti ya utulivu ila yenye msisitizo.
"this time no mistake boss, somebody is going to meet his creature, nkutoe wasiwasi vijana wako field nikuhakikishieakitokeza hata kucha safari yake itakuwa imeishia hapo" alijigamba yule mtu wa upande wa pili.
"mambo yameanza kwenda kombo, ila hayo ya situtoe kwenye reli ila kuna watu lazima waondoke na wa kwanza kufutika ni Chifu sijui atafutikaje ni jukumu lenu na siwafundishi jinsi ya kufanya kazi ila ninachowapa mimi ni tahadhari tu kwamba katika hatua zenu Angalia kila mguu unaonyanyua na kuutua hakikisha unaufikisha Salama, kingine yule mgumba asilione Jua la hapo Burundi hapo kesho kwani Hana Tena msaada na anawindwa na Tanzania kama sarafu ya mjerumani, maelekezo mengine utayapata kwenye kikao cha jioni na hayo yatekelezwe haraka iwezekanavyo ni vyema kumuwahi adui kabla hajakuwahi" ilikoroma Tena ile sauti
"Sawa mast.......tititi" Simu ilikatwa huku ikimuacha yule mtu wa upande wa pili katika tafakuri nzito Sana na moja ya sababu ya tafakuri ile ni kuhusu kutekeleza mauaji ya Chifu wa idara ya ujasusi kilikuwa ni kitu kigumu Sana alichokiwaza Jamaa huyu aliyeko nje ya Burundi kwa ajili ya kazi mbili Kisha aungane na wenzie watano huku yeye akiwa kama kiongozi wao.
********
KINGSTON-JAMAICA
SIKU NNE ZILIZOPITA.
"mkuu Hali ni mbaya nchini Tanzania mpaka tunavyoongea hivi"
"una maanisha kiuchumi ama vingine" aliuliza kwa sauti iliyotulia na ya Chini na yenye udadisi.
"La hasha, nchi iko matatizoni na aliyekuwa mke wako pia muda wowote anaweza kuzikwa na ndoto zake za kuifikisha mbali hiyo nchi" iliongea sauti ya mtu mwingine aliyeonekana kama mlinzi wake mkuu.
"hahahaha hakuna anayeweza kumgusa yule mwanamke, unadhani alichaguliwa kuwa msaidizi wangu kwakuwa tulikuwa tunajifunika Shuka moja?, 'BIG NO' ni kwasababu she is more intelligent and is actually a half machine if not machine as well 180 IQ, she has an extraordinary and conciseness decisions, military tricks and everything you know in espionage tactics, Boris haya yote yanayotokea anaweza kuyarekebisha for just few days and I got some Intel the same same as you said, but kitu hawata weza kamwe kufanya ni kuugusa unywele wake achilia mwili ulionipatia watoto watatu and you knew it, how much I love that woman, hata kama tumetengana ila kuna mawasiliano makubwa baina yetu hivyo Hao watu wasije kujaribu kufanya uthubutu wa kumsogelea, mpigie chifu hivi Sasa." Yalikuwa ni maelezo yaliyotoka katika kinywa cha mwanaume aliyeonekana mkakamavu japo umri wake ulikuwa wa miaka 55 ila alionekana kama ana miaka 45 na kuendelea, mkononi bado alikuwa na glasi iliyo na kimiminika brandi ya'Scotch' na muda huo huo alipewa simu na kwanza kuzungumza.
"Chifu Habari za Sasa hivi?" Aliaanza mzee huyo
"ni njema ni Nani yuko kwenye line na una shida gani?" Iliuliza sauti ya utulivu ila yenye kudadisi jambo
"The killer" Mara hii tu unasahau watu" alipigwa na butwaa Mara baada ya kuitwa Code name aliyokuwa akiitwa na watu wachache Sana Tena wazito idarani, Sasa kilichokuwa kinamsumbua huyo atakuwa Nani
"kimya chako kinamaanisha bado hujanijua Sawa sawa ngoja niende kwenye jambo la msingi na uliweke akilini kwako kuanzia Leo, MWEWE KUANZIA LEO ASIPAE NJIA MOJA NA VIFARANGA ANAOONGOZANA NAO WENGI WAMESHAKUWA KUNGURU, NI MUDA WA GORILLAS KUINGIA KAZINI KUMLINDA MWEWE, ALAFU KINGINE SUTI ZOTE WA NYUMBA NYEUPE ZITOLEWE ZILETWE ZILE ZILIZOKUWA KIWANDANI MBWENI NA KULE KISIWANI KISHA ZIWEKWE NYUMBA NYEUPE NA HATA ZILE ZA KAKI NA BAKABAKA ZITOLEWE LETA ZILE ZA KIGAMBONI NA MOROGORO ALAFU SAFARI YA MWEWE ANGANI ZIFUTWE KUANZIA LEO NA AWE ANAENDA WAZIRI MKUU,nadhani tume elewana na la muhimu zaidi ikitokea mwewe ameng'atwa hata na mbu basi na wewe usiwe unavuta hii hewa ya bure" iliunguruma sauti ile
"kwanini unaniamrisha na unajua kabisa sipokei amri yoyote isipokuwa ya mheshimiwa raisi pekee, na hata Hao vijana unaosema wako mbweni ama kisiwani kwanini hawawezi kuwa kunguru na Huoni kwa Mara moja hivo kutazua taharuki na mpasuko wa ndani ya serikali" aliuliza chifu huku akijinasua kwenye mtego ule kwa ku 'act professional ' na kuweza kuchota dondoo moja mbili kutoka kwa yule bwana aliyeonekana kuwana Siri nyingi ambazo nyingine hata hazijui ila anazipata kwa mtu ambaye hajajua kama yuko ndani ya mfumo au lah.
"wewe tekeleza nilichokwambia na mengine utayakuta kwenye email ya mke wako 'MAMA JUNIOR' na fikiria ile sentensi ya mwisho una mke mzuri Sana kama alivyo wangu kosa lako moja litamfanya wanaume wenye uchu wammendee" iliongea sauti ile ile ya utulivu
"unasemaje wewe mpumbavu unayejifanya kunijua siku nyingine, ukithubutu kuongelea Familia yangu jihesabu ni maiti na nadhani huna hoja yoyote kwa mchana huu na utakuwa umemtafuta mtu asiye sahihi na taarifa uliompa siyo sahihi kwake"
itaendelea
Je? Ni nani huyu aliyepewa amei ya kumuondoa Chifu na Mgumba wa Burundi ni nani? Ni aliyetoa amri ya kuuwawa kwa chifu tukutane toleo lijalo.Tchao
 
Wakati mgumu, rafiki ni mali,Marafiki ni kama nyota; si kila mmoja ni angavu. Wengine wanakuja na kuondoka, lakini wale wanaokufanya ujisikie vibaya ni vigumu kuwaona kwa mwanga wa ukweli………unataka kufahamu Sogea karibu na nisome
alifoka chifu kwa sauti ndogo huku akiwa amesimama ofisini kwake akakunjua pazia na kulakiwa na mandhari nzuri ya bahari ya hindi upande wa ukuta wa upande kulia wa ofisi ile.
"hahaha ngoja nikwambie Chifu, sikuwahi kumuogopa mtu ndiyo maana nchi haikuwahi kuingia majaribuni kama hivi Sasa, ila kwa ujeuri wako naona kama vile unaji fupishia muda wa kukaa kwenye hicho kitu, mmekamata watu ambao nasema ni vibaraka hivyo usilale usingizi ukajua ushindi unakaribia, utakuwa kiongozi wa ujasusi katika idara mjinga haijawahi kutokea tangu kuundwa kwa idara hiyo laiti ukielewa ni gharama kiasi gani nchi imetumia kukusomesha usingenifokea, sisi ndiyo watu unatakiwa kutushukuru kukuonesha maana ya 'Jicho la sindano', hata raisi wangu hajawahi kunifokea Leo unanifokea kisa hasira za kifamilia unapuuza mambo ya kitaifa labda kama ulikuwa hujui vijana wako uliowatuma Burundi waambie wasihangaike Sana kuzurura huku na huko kutafuta chanzo cha kifo cha balozi bali wamtafute bwana mmoja anaishi RUMONGE, jirani na Kota za kituo cha polisi, nyumba namba 37, wakiulizwa kwanini wako pale waseme 'JOHNY WALKER'.........Kisha huyo bwana atawapa faili lililo na maelekezo na ujumbe huu ufanyiwe kazi Mara moja kabla Jua hili halijalikimbia giza"sauti ile iliendelea kuunguruma kwa kutoa maelekezo mengine.
"Whaaaaat, you can't be serious comrade" alisema Chifu huku akilengwa na chozi la furaha Mara tu aliposikia Jina Hilo kwanini yeye ndiyo aliyempachika Jina hilo mtu huyo kwani alikuwa akipendelea kinywaji cha 'blue labled' Brandi ya 'Johnny walker' hivyo Jina Hilo waliitana wakiwa wawili akalinganisha maelezo aliyoambiwa kabla ya mfarakano na ile sentensi kwamba 'mkeo ni mzuri kana alivyo wangu na hapo picha ya mheshimiwa raisi ikapita kichwani na hapo hapo akapigia mstari jibu kuwa ni mtu aliyempisha kiti anachokikalia hakuwa mwingine Bali alikuwani Balozi Calistus Daniel Chacha, aliyesadikika kuuwawa siku chache zilizopita baada ya ubalozi kulipuliwa na maafisa wake wore kufa vifo vya kutatanisha ila vyenye uwino Sawa.kama balozi alikufa huyu ni Nani?
"usijiumize kichwa fikiria nje ya box na utaelewa ni kwanini wakati wa mazishi ilitoka 'Order' kwamba jeneza lisifunuliwe kwa kisingizio cha mwili kuharibika hata wewe hukuuona mwili wa balozi ni kwasababu ofisi zenu kwa Sasa Zina manluki wengi, na hata hili ni mimi na wewe pamoja na aliyekuwa mke wangu ndiyo wanajua kinachoendelea kunihusu na mimi ndiye niliyepiga simu Langley marekani kwa mkurugenzi wao na wao walikuwa na Intel za kutosha kuhusu utorokaji wa gaidi'MUSTAPHA' je mmeshawahi kumhoji mkuu gani wa magereza au hata waziri wa wizara hiyo, nilifanya hivyo ilikukuombea usaidizi wa kuwapata wahusika wakuu na siyo vibaraka, lile faili la watakaofanya hiyo kazi nililituma mimi hivyo uelewe unachokifurahia hivi Sasa. Nami nimetia mkono, ndiyo utambue Hilo na kuliweka kichwani na ni Siri ya watu watatu na ni kutokana na uaminifu wako kwasababu ukifungua kinywa chako basi hutaamka huyo huyo uliyemwambia anaweza akawa malaika wako wa kifo hivyo hesabu kama vile hatujaongea chochote na wewe na mimi ni marehemu niliyekwisha zikwa, Cha mwisho mheshimiwa raisi mstaafu awashiwe taa kali pamoja na vyanzo vyake ili kuona Ngozi yake halisi ijapokuwa kuna watu wawili wenye nguvu nyuma yake ukimuondoa jenerali mstaafu nkutakie utekelezaji mwema wa hayo niliyokueleza"
"mmmmmhhh....titititi" Simu ilikatwa na ilileta msisimko kwa Chifu, na maelezo aliyopewa alijikuta akitabasamu kwani sekunde zilizopita alikuwa katika bumbuwazi ila sekunde iliyofata Sasa alielewa aliyekuwa anazungumza naye, kumbe raisi anajua kinachoendelea alafu yupo kimya.
MUTAMBU-BURUNDI.
SAA 9: 30 alasiri
Mambo yalikuwa yamepamba moto huku wana usalama kutoka idara ya usalama nchini humo SNR walimwagwa kila kona ya Burundi kunusa na kujua maficho ya Thobias Chumvinyingi mwenye siku moja jijini humo ila tayari amezua taharuki kiasi cha kufanya ageuke dili nchini humo kwa kichwa chake kuwekwa rehani kwa shilingi za kitanzania takribani millioni Sita, ni mwananchi gani angeweza kuziacha dola 2500 zikapita hivi kwa kumuona mtu huyo na kukataa kutoa taarifa.
"itabidi jioni ya Leo inikute Rumonge, kuna Jamaa nitakutana naye wewe unatakiwa kujificha hapa hapa na usitoe mguu wako humu ndani tafadhari maana utaharibu kila kitu na wewe hujapewa hili jukumu " aliongea kwa msisitizo Sana ASP Richard mwenye codename ya 'Sorge'
"haina tatizo komredi nitakuwa hapa" alijibu Thobias Chumvinyingi.
"nasema hivyo kwa sababu muda wowote kapteni Jumanne anaweza kufika hapa au nikakutana naye Kisha tukafika hapa wacha nijinyooshe kidogo" alisema Richard huku akiingia chumbani mezani aliacha simu yake ndogo na muda huo huo Thobias akaitwaa na kuandika ujumbe uliokwenda mahali na bila kuchelewa akaufuta ujumbe na kutulia kama vile hakuna kilichotokea.
******
SNR HQ-BURUNDI
saa 10:05 jioni
Ndani ya idara ya ujasusi ya Burundi kila mtu alikuwa bize huku wakipishana kwenye korido za jengo lile kubwa, miongoni mwa watu ambao hawakuwa na pilika pilika ni NDIKUMANA KALOZA huyu alijikita kwenye kutafakari maamuzi atakayochukua yatakuwa na athari zipi kwake yeye, wakuu wake na mtu aliyemtumia meseji na Mara baada ya kuisoma nakujua ni mtu gani aliyemtumia meseji alitabasamu.
"utanisamehe Rafiki yangu Thobias ni lazima Leo ukamatwe" alijisemea kimoyo moyo na kuinuka Kisha akaenda kwenye ofisi ya mkuu wake kwakuwa alisema analo jambo la msingi basi hawakusita kumruhusu na hapo alikutana na ofisi Pana iliyopakwa rangi ya kijivu huku mkuu wa idara hiyo akiwa amekaa kwenye kiti kilichokuwa upande wa kusini mwa ofisi ile huku mbele yake kukiwa na makablasha pamoja na kompyuta, chumba kilipambwa kwa hewa nzuri na mapazia mazito yaliyokipa hadhi chumba kile, alibisha hodi na kufunguliwa huku akikaribishwa na Sura ya pande la mtu jeusi na lililopanda hewani huku likiwa jitu la miraba minne na sura yake muda wote ilisadifu kazi, naam huyu hakuwa mwingine Bali 'JEAN PIERRE NDIYESHIMANA' brigedia wa jeshi Lao aliyeteuliwa kwenye nafasi ya kuongoza idara hiyo miaka miwili iliyopita na raisi 'CLAUDE AURRIE NYANYEMANA' akakaribishwa kwenye kiti na bila kuchelewa alitoa maelezo ya kile alichokitilia shaka na Kisha akatoa na ule ujumbe ulioandikwakwa lugha ya kimafumbo 'ROYAL PALACE HOTEL, 19:30Hrs, ROOM No.45, ujumbe ule ulimsisimua Sana kiongozi yule na muda huo huo akanyanyua simu akatoa maelekezo Kisha akamshukuru kijana yule kwa kutoa taarifa ile na hapo hapo akavuta simu.
"saa 12 juu ya alama, royal palace hotel mzigo uchukuliwe kama ulivyo ukiwa mzito basi upunguzwe na ufutike kabisa kwasasa tuangalie mawasiliano yanatoka eneo lipi......titititiii"
*itaendelea
Kosa moja linafanywa na mtu ambaye hajapewa jukumu na tayari simu zishapigwa kwa watu wenye kuijua kazi, Bado dhambi ya yuda inaishi na watu karne kwa karne. Je mzigo utachukuliwa kama ulivyo au utapunguzwa? Ilikuwa makusudi au bahati mbaya? Usikose toleo lijalo. Tchao
 
"Hakuna kitu kinachoitwa 'mauaji' au 'kifo' katika biashara ya ujasusi, kuna 'kutoweka tu na Mara moja ni bahati. Mara mbili ni tukio. Mara tatu ni kitendo cha adui"
IAN FLEMING,former secret service MI5(RIP), kwanini nimeanza na nukuu hii ya jasusi wa zamani wa uingereza aio bahati mbaya sogea tusomane
Endelea…………,,,,
Simu ile ilikatwa bila kusubiri majibu huku mtu yule akitazama saa ya ukutani iliyokuwa upande wa mbele wa ukuta uliokuwa ukitazamana na pahali alipoketi na kushusha pumzi ndefu.
*******
PEMBA-ZANZIBAR
Saa 11:45 jioni
Simu ya mtu mmoja mzito inaita huku akiwa bize akifanya mazoezi ya viungo huku akiwa kazungukwa na watu wenye miraba minne na wakiwa makini muda wote.
"hellow boss....how is it in the castle"alianza mtu yule huku akisitisha kuinua mkono uliokuwa na chuma chenye sahani za kilo kumi na tano kila upande
"crystal fine master, but there is one thing you guys still letting me down and remember that I can't allow my downfall while you people still breathing, It took me a million of dollars to build this organization, and you know exactly how many years we take to creates plans and execute them in a perfect manner, what is happening now? How dare are you my guys allow somebody to land on my Castle and cause f*cking damages and you still sitting on your mansion, giving directions and drinking Cognac, where is my people Bishop,Vanessa and recently MUSTAPHA is the target and just remember last night you told me to sit and waiting for news, whats happened 'MASTER' why did the bombs you proud of didn't blast? and still remaining sillence without taking any measures, are you serious to work with me?"
"sorry madame I think we have to reform our plan and show them how superior we are, from now I promise nothing wrong is gonna happen please"
"you think huuh?..........promise what Gentleman? Your mistake on your zone are going to expose to the whole world about our dark side, remember that and take to the head that before i get exposed, your head will be a sweet soup for my big boys(dogs), you have to do the following nightmare, first task kill that Chief Spy, then the General and lastly that bitch, that is the first part then you will see the phase two of our plan do i make myself clear?
"i got you my ladyship and like i said pri.......tititi" Simu ilikatwa huku ikimuacha mtu yule akitweta kwa jasho jembamba linalomtiririka maneno aliyoambiwa na upande wa pili Hakika yalimuogopesha na kuna muda alijikuta akijuta kuingia katika kundi lile ambalo hata hakujua kwanini liliongozwa na mwanamke na siyo mwanaume, na mwisho kabisa alijikuta akisadiki kuwa mwanamke yule ni katili kuliko hata yeye Hilo lilimtisha na kibaya zaidi kuna amri ya kuwaondoa watu ambao ki uhakika hakuwa na chaguo zaidi ya kufanya hivo
"ooopps! kuna kazi nzito ambayo sidhani kama itakamilika Salama bila damu zetu kumezwa na ardhi, kuna kazi ambayo mtaifahamu massa machache inayotakiwa kufanywa kwa weledi wa Hali ya juu ila tambueni tu ni kazi ya damu na jasho" alisema mtu yule na hakuna aliyejibu kwani walielewa uzito wa maneno ya bosi wao na hili lilisadifu msemo wa waswahili usemao' kiboko akikwambia mamba anaumwa wewe huna budi kumuamini
********************************
Kila tabasamu lijitokezapo kwenye uso wa mwanadamu, Lina maana ndani yake, Mbali kuwa tabasamu karibia Mara zote hulenga kufikisha jambo kukubaliana na kitu Fulani, ila tabasamu Hilo Hilo huwakilisha furaha na saa zingine majuto ya kitu Fulani, ndiyo na usishangae tabasamu la Majuto ni lile linalojengwa na aibu, ndiyo Maana likaitwa kwa lugha iliyonyooka kwamba ni 'Tabasamu la aibu' na hili lilimtoka Askofu wa kanisa la ‘jehovah ameshinda’ akiwa anatazamana na mheshimiwa raisi huku muda mchache ujao atachukuliwa na maafisa wa usalama kutoka idara ya ujasusi ya nchi ya marekani CIA kwa ajili ya mahojiano ya kina juu ya tuhuma nzito za uingizaji wa dawa za kulevya vile vile silaha huku akihusishwana tuhuma za unyanyasaji wa kingono wa watoto wanne wa umri wa miaka 16 na 17 huko new York walipokwenda kutoa semina katika shule moja jijini humo, Hakika alionesha aibu huku taswira ya gereza ikijengeka kichwani.
"mheshimiwa raisi ni heri mnishitaki huku huku usiniache tafadhari, Mimi ni raia wako na maamuzi ya kunibakisha na nikahukumiwa na mahakama za huku unao na sheria inakuruhusu" aliongea Askofu kwa sauti ndogo
"Leo mnakumbuka sheria.......hahaha sikiliza askofu sheria hiyo hiyo inaniruhusu kuwaruhusu kukuchukua naamini unalijua Hilo, ila the Good news ni kwamba utakwea pipa kwenda marekani my dear Askofu wa Giza" alisema mheshimiwa raisi akiwa ana mtazama huku akipandisha mabega.
"Nakupa ofa ya kukutajia kama ukinibakisha huku" alisema huku safari hii uso wake ukichanua tabasamu la 'Chomoa na hii'
"si unatambua Fika kuwa serikali yangu haiingii makubaliano na gaidi kama wewe" alisema Tena raisi huku akiweka vidole vyake mezani huku akimtazama Askofu kwa ukaribu kiasi cha kuzisikia pumzi zake zinavyopishana katika matundu ya pua na mdomo wake.
"ila unajua kabisa itakuchukua siku nyingi kumpata na pengine usimpate, Mimi ndiyo ufunguo hivyo unaweza kuutupa au kuuacha ukufungulie kufuli"
"hahahaha ndiyo maana umeweza kuwa na wafuasi wengi kwasababu ya sumu ya ulimi wako, Sasa nkwambie hivi ukitoka huko kwa wa marekani utarudi hapa mpaka uniambie kila unachofahamu kuhusu Tanzania Askofu wala Sina haraka na wewe."
"hahahaha siyo kirahisi hivyo kama walivyomuua mme wakowa zamani, alikuwa kimbele mbele Sana kiasi cha kupata taarifa na kuziweka kwenye lile faili alilolipa Jina uchwara 'Faili Jeusi' alikosea Sana kuwashika watu wasio shikwa na mikono milaini kama yake ona Sasa amekuacha mjane ila ni kwasababu hata wewe huna siku nyingi" alijigamba Askofu huku mh.raisi akiachia tabasamu la kinafiki huku akitamani kucheka kicheko kilichoishia machoni tu kabla ya kufikia kinywa.
"hongereni kwa Hilo na niwapongeze ila usijali mtakutana nao siku moja mkiwa mnaisogelea kamba........hahaha usishtuke na nimeona Jina lako liliweza kuhusika kwenye kufadhili ugaidi na unajua asubuhi ya Leo nimefanya nini, just wait nkuelezeyafuatayo adhabu ya sheria mbili zilizo rekebishwa Jana na Leo nimezisaini na zinaanza kutumika ukikutwa na hatia dawa za kulevya ni kamba, ugaidi ni kamba upo hapo baba Askofu Sasa utachagua mwenyewe Tanzania au Marekani, hakusubiri alisimama na kuuelekea mlango.
"EX SPY MASTER" iliongea sauti nzito ila yenye utulivu wakutomtilia shaka apokeaye hiyo taarifa.
"anahusiana nini na wewe baba wa maovu ndani na nje ya nchihii" alisema raisi huku akiwa amegeuka mgongo tu huku kiwiliwili kingine kikiwa kimeelekea mbele
"unaweza kuwa mjuvi wa vitu ila kuna vingine hutajua kwa maana wamekuzidi akili ndiyo maana walipewa jukumu la kukaa na Siri za nchi kwa takribani siku 365 au na 1/4, siyo kwamba Enzi zako hukuwa ukizijua la hasha ila kuna nyingi huzijui na hata marehemu mmeo alikuficha mengi tu kwa sababu ni Siri ya watu wachache, ndiyo maana mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu raisi Bendera alimteua kuwa balozi kwenye nchi ya kawaida akijua atakuwa naye sambamba hivyo undumilakuwili wake ndiyo ulioleta haya yote na nkuhakikishie tu una siku chache Sana za kuishi huku mimi nikiwa uraiani nikidunda"
"kitu usichokijua ni kwamba unaowategemea wote watatiwa nguvuni siyo muda mrefu ili kila mmoja alipwe malipo kulingana na kazi mliyoifanya na najua Leo wenzio wana kikao ila nkwambie tu baada ya hapo mtakutana nao mahakamani"
"acha kujidanganya kuwa unajua kila hatua unayosema tunapiga ila nina uhakika ipo siku utatusujudia na kutuomba tukuachie uhai wako huku ukitoa ahadi kedekede ila ndiyo siku utakayopata ujauzito na umri wako huo.....hahahahaha" Alicheka kwa dharau huku alitoa maneno ya kebehi,
"unatakiwa uelewe muda wa kuongea na wewe bado na usichokijua ni kwamba mkurugenzi wa CIA anakusubiri kwa hamu na hata nikitaka Leo hii hii natoa amri wakaendeleee na wewe,wewe si unajifanya kidomo domo haya kawaambie methali zako wa marekani" alisema mheshimiwa raisi huku akibenua mdomo kwa kebehi.
*********
CLUB 662-DAR ES SALAAM
Saa 3:40 usiku.
Muda huu katika klabu hii ya usiku kulikuwa kumechangamka kiasi cha kufanya watu kusahau shida zao kwa muda, eneo lilijawa na watu wa kila tabaka huku wengi wao wakiwa jinsia ya kike huku wakiwa katika mavazi ambayo yata kutoa pesa zako mfukoni ili mradi tu aketi pembeni yako, siku hiyo walijaa wakina wadada wanajiuza miili yao waliokuwa wamevaa nusu uchi miongoni mwao alikuwa ni Chiku alikuwa kapendeza katika vazi lake fupi kiasi cha kuwafanya wanaume kutokwa na udenda, Mbali na wadada poa wengine kujikita kwenye biashara ila Chiku tu ndiyo alikuwa na lengo zaidi ya Hilo, ndipo jicho lake liliponasa kwenye umbo la mtu, Jitu la miraba minne, mweusi na mrefu kupanda hewani, huku likiwa limenyoa nywele mtindo wa kipara na kuwa kama Monk, hakuwa mwingine Bali ni aliyekuwa mlinzi mkuu wa raisi bwana Jerry Elius dambaya, alijiuliza kuwepo kwa bwana huyu maeneo Yale au ni mmoja wao alijiwazia huku akihisi mkono wa mtu kumshika bega.
"uhali gani kipenzi.......ninaweza kukaa hapa na kuyafaidi Manukato yako kwa kuzishibisha pua yangu kwa harufu nzuri" alisema Jamaa mmoja aliyekuwa kavaa suti huku kichwani akiwa na kofia kama zile za machifu katika muvi za kinaijeria huku uso wake ukiwa na ndevu nyingi kama raisi wa Iran Ebrahim Raisi
"hujaacha tu maigizo yako charz" alisema Chiku huku akirembua jicho lake kubwa na la duara huku papi za midomo yake zikigombania Uganda wa juu wa ulimi, Harika ilipendeza huku ikitaka kuwavuta watu walioketi karibu na Meza yao.
"naachaje wakati mimi mwenyewe bonge la dili natafutwa ila nimeona umepatwa na mshangao kumuona namba moja hapa ila mimi nimeona la zaidi, nilikuwa maeneo haya mapema Sana hivi unajua ila nimemuona mwewe aliyebadilika rangi kuwa kunguru Hakika ni kweli tulikuwa tunazunguka na gizani tukiwa tumewasha mishumaa kumbe kuna watu wanaipuliza."
"hahahaha huishiwi vituko wewe mzee ninunulie basi shoti ya'Yamazuka' nimeimisi Sana bhana" aliongea kwa madaha huku akizungusha jicho lake kwa hila upande wa mashariki ilipo'counter' ya vinywaji
"huja achaga tu kutumia 'Japanese whisky' any way tusogee kaunta mrembo au umesha wahiwa na vibopa niko hapa mimi kama mimi" alisema Chiku kwa sauti nyororo akasimama huku akijiweka Sawa kisketi kifupi kilichoya acha mapaja yake manono yaliyokazwa na misuli yakiwa nje nje, ki'clop top' kilichokiacha kitovu chake nje huku cheni ya rangi ya Shaba ikionekana kwa mbali ikicheza kiunoni mwake kila anapotua mguu kwenye ardhi, mtikisiko ulioshuka mpaka kwenye makalio yake makubwa kiasi na kichwani lilipita wigi lililomfanya kuonekana kama Pacha wa mchezaji tenisi. mwenye rekodi zake duniani 'SERENA WILLIAMS' miwani ya urembo aliyoivaa hakufanania na Jina la uficho alilopewa 'Angel of death kwa urembo aliokuwa nao Hakika luteni kanali Charz alijikuta akidata kwa muda huku mapigo ya moyo yakienda kasi na kujikuta akiropoka.
"Damn your so sexy babygirl" jambo lililomfanya Chiku kutabasamu tu huku akivuta kiti na muda huo jicho lake lilichezeshwa huku na huko kuyasoma mazingira akaketi na kutoa Tena tabasamu lililomzuzua mhudumu wa kiume aliyekuwa pale.
"one shot of YAMAZAKI please' hakujibiwa zaidi ya vitendo kuendelea.
"45k cute" alijibu huku akiisogeza glasi ile jirani na mteja wake na mteja hakusita zaidi ya kuigida yote na kushusha glasi chini huku akisikilizia Radha chungu ya pombe ile iliyo tengenezwaJapan karne kadhaa huko nyuma.
"nyingine bill on me" ilisema sauti nzito na yenye kuonesha kuelemewa na kilevi, Chiku alitabasamu tu huku akijiweka Sawa kwa kujibinua zaidi kwenye kiti kile na kwanza kukinyonga kiuno chake kuendana na mdundo uliochujwa katika spika za club ile huku kibao kilichokuwa kwenye kompyuta ya Dj kikiwa kile cha Shakira alichomshirikisha Wyclef Jean 'hips don't lie' ndiyo ni amsha amsha katika klabu hii ilikuwa ni ya kutosha kiasi ni watu walioko mle ndani siyo walala hoi Bali ni magabachori wenye pesa zao chafu, waliendeleza soga mbili tatu huku wakiongeza utimamu kila dakika huku ghafla umeme ukakatika kwa muda wa dakika tano na Kisha taa zikapata uhai na kufanya ukumbi ulipukwe kwa shangwe huku mziki ukirejea kwa mdundo mkali huku kibao kilichokuwa kikikita ngome za masikio ya watu kikiwa cha Tupac Shakur 'Do for love' lakini ni watu wawili waliojua maana ya lile jambo ukiondoa wahusika wenyewe ya kwamba muda wa kikao ushaanza hivyo walijiambia wajipe muda kwa kujiagizia chupa nne nne za pombe brandi ya 'Guinness' huku wakigonga 'cheers' glasi zao.
"wajumbe wote mmefika?" Aliuliza katibu wa kikao ili kuweka adidi za rejea sawa
"ndiyo ukiondoa mateka hakuna ambaye hajafika alisema jenerali mstaafu Chukulubu huku akiielekea skrini inayoonesha kivuli tu.
" Master nadhani tuanze tu na maadam umesema una agenda nadhani ikikupendeza tunaweza kufanya kikao kwa maana mazingira ni Salama kabisa na vijana wengine wanaimarisha ulinzi kiufupi tuko Salama kiasi kwamba hata nzi hawezi kusogea kutega sikio.
"hahaha Bendera nakwambiaga siku zote wakati unaohisi uko Salama ndiyo wakati unaotakiwa uchunge Sana, kilicho mkuta Askofu na kitakachoenda kumkuta Askofu ni pigo kwetu na ni mwiba unaochoma kiasi kwamba unaweza kutuathiri kwenye biashara zetu ikiwezekana uhuru au uhai wetu, na kikwazo kikubwa ni idara ya ujasusi yenye Vichwa viwili kwa Sasa nadhani mnatambua kuwa mpaka Sasa Arusha wanavuta hewa ya baridi na kufurahia kwenye mabaa na starehe kedekede zinaendelea, hakuna asiyejua hii idara imekuwa kikwazo katika mipango yetu, kiufupi tunawindwa kama swala porini, hivyo basi mkuu ameadhimia nasi tumuwinde anayetuwinda na ninatoa maagizo kama ifuatavyo haijalishi umeyapokeaje, kuna kazi kubwa nne kwa Sasa moja ni ya kumtoa uhai Jenerali wa jeshi, kazi ya pili ni kumtoa uhai Chifu na kazi ya tatu ni kumpokonya uhai yule Malaya Kisha kazi ya mwisho ni kusuka upya umoja wetu kazi hizo zinatakiwa kwanza Mara moja Chukulubu simamia Hilo zoezi."
itaendelea**
⚠️No comment⚠️ hadi nimeogopa tukutane toleo lijalo tuone kama mkeka utatick au uta buma.Tchao
 
“Wanaotufundisha kuhusu ubinadamu, mara zote siyo binanamu” TUENDELE NA TUTAKUJA KUONA YAKE HUKO MBELE TUENDELEE…….

Kikao kilitawala na ukimya Mara baada ya kivuli kuondoka Kisha ikafatia na kukohoa kwamtu kama kurekebisha Kool.
"mmmmhh mkuu hapo tumekuwa kama ngedere kuvamia samba la pilipili kwasababu kwa Sasa ni rahisi Sana kumfikia jenerali kuliko Chifu anayelindwa na viumbe hatari Sana kuliko hatari yenyewe kuna tetesi kuwa wamekula kiapo kwa hiari yao wenyewe kumlinda mpaka pumzi yao ya mwisho ni watu ambao aliwatengeneza mwenyewe Tena wengine ni kutoka jeshini naaliwaweka akiba na ilikuwa Siri ya watu wachache Sana, nkiangalia Kati yetu sioni wa kusimama nao hata kwa sekunde kumi bila mwili wake kuwa kama dekio kwa kuchani wa chanwana hisia zangu zinaniambia mtu huyo yuko eneo hili naameshatuona baadhi yetu na huenda tukaingia kwenye rada za Chifu muda wowote kuanzia Sasa" alisema Jerry
"oops ni mshenzi gani ambaye hajitakii mema mpaka afike hapa haiwezekani Nina timu ya ulinzi wa kuonekana na kutoonekananikutoe wasiwasi muda mwingine hisia hudanganya" alisemameja tumbaku.
"hahaha meja Mara hii tu umeshasahau mbinu za kimeda nikwamba usiwahi kudharau hisia zako na kosa moja litagharimu dimbwi la damu kwa mtu wako wa karibu au wewe, India hiyosentensi yako kama kamanda na ujiongoze vizuri Mara nyingine" alikoroma Jerry huku akimtazama kwa macho yakumakinika meja Tumbaku.
"heeey guys hold on hapa siyo mahala pake kuna taarifa ambazo siyo njema kidogo kwa upande wetu huko Burundi, Adui yetuanatutunishia misuli kiasi cha mkuu kutupa saa 72 kazi iweimeisha ikiwezekana ichukue saa 24, Jerry utaongoza kikosikazi, Cha kuzingatia zaidi ni umakini" aliongea mkurugenzi waulinzi wa raisi
"nadhani tumeelewana kwa kile kilichosemwa tuendeleekupeana Habari ili tuweze kulifikisha juu kwa taarifa stahiki, niwatakie utekelezaji mwema wa majukumu yenu" alisema raisimstaafu Saidi Bendera huku kikiwa ni mwanzo wa utekelezajiwa majukumu kama mwanzo tu umeme ulikata ila safari hiikitendo hicho kiliwakuta luteni kanali Charz na Chiku kwenyegari Aina ya Mercedes-Benz huku wakiigiza kupigana mabusuhuku macho yao yakiwa yanazunguka kama jicho la kinyongana hapo macho yao yalimuona meja tumbaku lakini vile vilemkurugenzi wa ulinzi wa raisi aliyewapita kwa kasi kuliwahigari lake huku akiwa na walinzi kadhaa huku wengi waowakiwa ni maofisa wakuu kutoka vyombo vya ulinzi nausalama. Baada ya dakika kadhaa shughuli zilirudi kamamwanzo kitu kilichomfanya Chiku kukanyaga mafuta nakuondoka eneo Hilo.
"tunaelekea wapi mrembo? Mmmmhhh I think kwa meja kunamengi tutayajua" alisema luteni kanali Charz
"heeeeeh wewe mwanaume na nguo hii huko kinondoni sinitabakwa na wahuni tu" alisema chiku huku akitabasamu.
"huyo muhuni atakayekusogelea itakuwa ndiyo siku yake yamwisho kusikia sauti za binadamu hahaha ila Leo umejuakunichokonoa hisia zangu" aliongea Charz na kuendeleakuangua kicheko tu kilichomfanya atazamwe kwa jicho pembena kutabasamu.
"tupite home nkabadilishe bhana hiki kisketi hakifai kwa kazi" alisema Chiku huku akipinda Barabara ya Haile selasie hukuwakizivuka hosteli za chuo cha muhimbili na kutokezea maeneoya coco beach wakazidi kusonga mbele mpaka katika nyumbamoja nzuri na ya kisasa.
"watoto wa ushuani bhana......" Alisema Charz huku akitazamahuku na huko kuangalia usalama
"alafu ushaanza utani wako.......mimi sipendi bhana" alisemaChiku huku akiweka sauti ya madeko.
"twende ndani basi au mimi ndiyo safari yangu imeishia hapa" alisema Charz huku akijiandaa kucheka.
"yaani kama bss, ndiyo nisubiri hapa Sawa daddy" alisemaChiku akimpiga busy shavuni na kushuka auntie kwake.
***********
BUJUMBURA-BURUNDI
Masaa mawili yaliyopita.
Wakati akiwa amepitiwa na usingizi alipata kuona katika njozipicha la kutisha huku likitawaliwa na madimbwi ya damu kilaalipokukanyaga huku magwanda na bareti za wanajeshiyakionekana kuelea kwenye madimbwi ya damu hakika ilitishaila alipigwa na butwaa kwa kile alichokiona mbele zake risasimbili kutoka kwa mtu aliyekatika umbile la kike lilimsh tuakutoka usingizini na kutweta huku mwili ukivuja jasho la kutosha, hii ilikuwa Issara mbaya kuwa adui alikuwa mite kadhaa kutoka pale na chap kwa haraka akajiweka Sawa nakutoka kilichomshangaza ni kutokumuona Thobias sebureni pale huku runinga ikiendelea kutoa matangazo ya kilekina and’s choendelea katika nchi zilizoko pande kuu nne za dunia, vile vile alijishauri akamuangalie vyumbani, nyumba ile ikiwana vyumba Sita vitatu kwa ajili ya malazi,kimoja kilitumikakama sebure iliyokuwa Pana kiasi, jiko pamoja na cha mazoezipia palikuwa na korido iliyovigawa vyumba.
"Thobi Thobi upo wapi komredi" aliita Richard hukuakiusogelea mlango wa kutokea nje na alijikuta akisimamakwani alipigwa na butwaa baada ya kumuona mwenzie yukobize kuzikagua gari zilizokuwa ndani mle kwa kuzifuta futavumbi.
"kumbe uko huku ndugu yangu una miadi na mtoto mzuri nini?" Alichombeza Richard.
"hahaha hapana Rich nakusafishia wewe uliye na miadi na toto la Kirundi hakikisha unaiwakilisha nchi vema" alisema Thobias huku akiachia tabasamu bila kujua yuko dakika za tisini nakilichobaki ni kipenga cha malaika mtoa roho kuikatisha pumziyake. Akaingia ndani na kujianda Kisha akatoka na kumkutaThobi amemaliza kazi yake na kumkabidhi ufunguo wa gari Aina ya Ford Ranger akaitekenya na ikaita.
"nafikiri tutaonana baada ya masaa kadhaa ndugu" alisemaRichard huku akiliacha geti la nyumba ile na kutokomeamitaani, aliikamata Barabara ya Rumonge kwani ndikoalipokuwa akienda kilomita chache kutoka Mutambu hukuakiwa na maelekezo ya kumtafuta mtu waliyeambiwa, maelekezo yalijirudia kichwani na punde mji wa Rumongeulimlaki kwa Majengo na mpangilio mzuri wa jiji Mithili ya ilewa Catalunya huko Hispania.dakika kadhaa zilimuwezeshakufika katika eneo alipo mlengwa aliyetakiwa kukutana nayealishuka kwenye gari mara baada ya kuipaki mite Mia tatu kutoka nyumba ile alishuka huku akiigusa mahali alipoiwekabastola yake Aina ya Mark 11 akashusha pumzi na kuanzakusogea kwenye nyumba ile aliipita kutokana na mazingira yaukimya akatulia juu ya mti uliokuwa na matawi makubwasehemu hiyo iliyokuwa kama maficho yake ya muda kwa ajili yakulipekua eneo Hilo kwa lengo la kung'amua wakazi wa eneoHilo ni watu wa aina gani. Hazikupita hata dakika tanoaliwashuhudia watu walioshuka kwenye gari aina land cruiser hardtop huku wakiruka na kutua katika mitindo iliyopendeza nakuwafanya waonekane wao ni watu wa Aina gani katika medanialijipa utulivu na kuendelea kuona sinema ile ya bure, Katina urukaji wao alipata king'smua kwamba wote watatu walikuwajinsia ya kiume akashikwa na kigugumizi, ndiyo alishikwa nakigugumizi cha kushuka mtini kwani hakujua ni watu wangapiwamesalia kwenye gari ukiondoa dereva aliyezima gari lile, napunde alisikia sauti ya kike kwenye gari sauti ambayo haikuwangeni masikioni mwake na kwanza kuvuta kumbukumbu niwapi aliisikia bado alijipa utulivu huku kukionekana kuwa namalumbano
"Bosco usiniletee ujinga umemkosa vipi ikiwa kila kitu kikokwenye maelekezo....Simu inasoma location iko wapi?"
"Rumonge mita chache kutoka nyumba mliopo na minarainasoma hivo na tamari tuko njiani Kuja kuwasaidia" Alilalamamtu wa upande wa pili kwenye simu ile
"Rumonge near our target mmmhhh Sawa ngoja niwawekeSawa watu wangu" alisema huku akishuka kwenye gari na ndipotaswira ya umbo la wastani la mwanamke likashuka huku likiwalimeshikwa na suruali ya jinsi ya tangu nyeusi na Raba nyeupebrandi ya Adidas huku kabashingo ikiwa imemkaa vyema hukubastola yake ikiwa imewekwa vizuri kiunoni.Katinamazungumzo yote yaliyonaswa na Asp Richard ni kugunduakuwa kuna mtu wanamtafuta kupitia mawasiliano ya simu nakibaya zaidi sehemu zote walimkosa na Sasa wanmtafuta kupitiasimu ya mkononi na kama aliyepigwa na ubaridi mailing alijikuta akiganda baada ya simu yake kutetema mfukoni, kumaanisha ilipata ujumbe.
"KOMREDI MBONA UMENIWEKA ALAFU HUJANITAARIFU KAMA UMEPATWA NA DHARURA, BADO NAKUSUBIRI ENEO LA MIADI" ujumbe ulisomekahuku namba ya mawasiliano iliyotumika kutuma ujumbe mfupiikiwa na 'codes' namba za Burundi, alichoka na ndipo alipokatashauri ya kuipiga simu ile iliyoita bila kupokelewa,ajabu hii! Hilo likawa kosa la pili la kiufundi kwani mnara ya simuulisoma mpaka mawimbi Yale yanapotokea, kama aliyechezwana machale akayahama maficho Yale na bahati ilikuwa kwakekwani simu ile ilidondoka kwenye jiwe lililokuwa sentimitachache kutoka lilipo shina la mti ule na katika Hali yakushangaza simu ile ikapata uhai, ndiyo ilitetema pale Chini huku mpigaji akiwa ni wa namba ile ile, hisia zikamtumahuenda alikuwa ni Kapteni jumanne lakini zilikutana napingamizi kali kutoka katika fikra kwamba hakuna anayejuayuko hapo nchini Burundi zaidi ya watu watatu, raisi Grolia, Chifu na Thobias Chumvinyingi na pia akapingana na hoja yakuwa na miadi na mtu yoyote nchini humo isipokuwa kujuakilichopo kwenye nyumba ile akaitazama saa yake na kugunduaashapoteza takribani dakika tano akatazama kushoto kwake nakuliona pipa la takataka lililokuwa pembeni ya nyumba ileiliyokuwa na kiza totoro kwa kutokuwashwa taa, akaitupa simuile mle ndani Mara baada ya kufuta kilochomo na kuondoka nabetri tu ya simu ile, akatembea hatua kadhaa kama anazifataKota za polisi wa Burundi Kisha akavuka Barabara na kuivutabarakoa yake akiwa amebakiza mita chache kuifikia ile nyumbaalipata kuona miale ya mwanga na hakujishauri Mara mbilialiweka maficho yake kwenye uchochoro wa nyumba ya pili kutoka ile walioingia watu wale na alipotupa jicho upande wabarabarani alimuona dereva akiwa anavuta sigara yake hukuakitazama muda kwenye saa yake na sekunde hiyo hiyo masikioyake yalinasa muungurumo wa chombo cha moto, uliokuwaukiongezeka na Kisha kupotelea kwenye moja ya nyumba mitaMia moja toka alipoweka maficho yake. Akajipa utulivu wasekunde kadhaa na Mshale wa dakika ulivyohamia nuktanyingine ya saa ulimkuta yuko upande wa Barbara na kwatahadhari aliingia kwenye siti ya mbele pembeni ya dereva nakumgusisha shingoni na kisu Kigali.
"Tulia hivyo hivyo komredi, nyie ni kina Nani na mnatafta ninikwenye ile nyumba" aliuliza Asp Richard kwa sauti kavu isiyona utani.
"watu mnavuta bangi ya kutoka wapi, wewe Huoni nimevaanin..." Alitulizwa na Kiwiko cha taya kilichomfanya agune kamaamefika mshindo kwenye tendo la ndoa
"ninapokuuliza swali sihitaji uniletee siasa nyau wewe"
"kijana unatafuta kifo.....ni heri upotee nchi hii kablahujaimbiwa parapanda" alisema huku akifanya hila ya kuivutabastola yake iliyokuwa kiunoni ila wepesi wa mikono yake badoulikuwa hatua moja nyuma ya Asp kwani muda ule ule kisu kilekilizamishwa shingoni na kusababisha damu nyingi kuchafuakioo cha mbele, alikoroma kwa sekunde kadhaa Kisha akakataroho hapo hapo akiwa amekaa, kwa makadirio yake alibakizadakika 5 kutoka kwenye zile alizopigia ili watu wale waliopigasimu kuwasili eneo Hilo, bila kutoa sauti alinyata na kuupitauzio wa nyumba ile huku akisikia watu wakimsulubu mtu
"mbona mmenigeuka dakika za mwishoni ndugu zangu, hatawewe Diane ni wa kunifanya hivi mbali na kuishi muda woteulimwengu ukitambua mimi na wewe ni mke na mme hayandiyo malipo, Mbali na kujifunika Shula moja Leo unan..."
 
huyu mtunzi sahivi anazingua tu mwanzo alianza kwa kasi nzuri vipande vya kutosha ila baada ya kupata wafuasi ndo wanajifanya wana mambo mengi hadi ameanza kunata eti kipande kimoja tena kifupi na hadi tubembeleze na kulia lia ndo aturushie kimoja..
 
Back
Top Bottom