Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
TayariJaman tukumbuke basi
Hapana uchovu na kutaitika huku sitaki mpate kiu na alosto ndo maanaMkuu ulikuwa unakimbizwaa 😂
Usiseme hivo maana ni mara ngapi nimekuwa nikitoa taarifa humu ndani lakini vile vile siyo kwamba muda wote nakuwa huru nimeishika simu kuwapostia humu toleo ila pale nnapopata nafasi basi nakuwa nafanya hivo hata mara mbili hivyo usinichoke mapema hiyo bado nakuhitaji sana kama hadhirahuyu mtunzi sahivi anazingua tu mwanzo alianza kwa kasi nzuri vipande vya kutosha ila baada ya kupata wafuasi ndo wanajifanya wana mambo mengi hadi ameanza kunata eti kipande kimoja tena kifupi na hadi tubembeleze na kulia lia ndo aturushie kimoja..
alisema kwakiswahili kilichonyooka huku ikifuatia na ngumi kavu mgongonimwa Richard huku akimsukuma atembee hilo likawa kosa kwani Sorge alijifanya amejikwaa ili kuvuta umakini wa mtu yule naye akahadaika na sekunde iliyofata mtu yule alijikuta akielea hewani huku silaha yake ikiwa mbali na yeye, mapigo kadhaa yalimfata huko huko ila aliyakwepa kwa wepesi kama unyoya kwa kujiviringisha kisha alitua kwa mguu mmoja huku mkono wake akiutanguliza chini ni hapo Sorge alihamaki baada ya kukutana na sura anayoifahamu sana kuanzia kambini walipokutana huku mtu huyo akiwa mkufunzi wake baadae akaja kusikia mtu huyo alifukuzwa kwa utovu wa nidhamu.
"ni wewe kanali sentonyo ndo umeibukia upande usioutakia mema nchi yetu" alisema hivo Sorge huku akiongeza umakini kwani mtu aliyekuwa mbele yake ni zaidi ya neno hatari.
"tulia wewe mtoto wa malay* unaongelea nini mimi nimechagua pesa uzalendo mnaolilia na yule bibi yenu mtauona kwa vitendo mkiwa mmebakiza sekunde thelathini mkiwa mnahesabu kila pumzi yenu ya mwisho."
"kumbe kuna watu wazima hovyo kiasi hiki kwanini hukutulia ustaafu ukalee wajukuu zako.....kwa heshima tu piga magoti na ujisalimishe" aliongea tena akimwangalia mzee yule kwenye giza lile lililokuwa linafukuzwa na mwanga hafifu wa taa ya umeme kutoka nyumba iliyokuwa mita kadhaa kutoka pale waliposimama mafahali wale waliokuwa wakiangaliana kwa uchu.
"hahahahha na wewe unaleta ngonjera kama yule marehemu uliyemuacha ndani nasikitika kwamba hutaiona maiti yake ila mtakutana huko huko kuzimu msimuliane ukatili wa vifo vyenu...muda wa kupiga stori umeisha wasalimie kuzimu" alimaliza huku akirusha makonde mazito yaliyochana upepo na kumfanya mkwepaji aone akizembea kweli utabiri utatimia, akarudi nyuma hatua kadhaa kupanga hesabu zake vizuri........alikosea!........alikosea! kwani sekunde zisizo pungua thelathini alijikuta akielea hewani huku akitoa yowe la hofu.
"leo nitakufundisha kwanini fisi miguu yake ya mbele ni mirefu kuliko ya nyuma we mtoto wa malay*" hapo kulifatiwa na mateke mazito yalichana upepo, Sorge aliinama na katika namna ya ufundi na akamchota mtama uliomtupa mtu yule na kisha kutulia mgongo kiasi cha kubweka kama mbwa koko, jitu lile punde liliibuka na bastola iliyokuwa limeisunda kwenye soksi yake ya mguu wa kushoto.
"huna sababu ya kuishi wewe nyau mweusi ulidhani nitakukubalia ushinde, kutwa ukinipasha mwili wangu joto risasi mbili zitafanya maiti yako isitizamike, kenge wewe haya tuma salamu kwa watu wawili kabla maiti yako haijawa chakula cha mamba wakali" alifoka mtu yule huku akiuma meno kwa hasira
"kwa watu waoga kama wewe unayebweka kama mbwa.............ya pili kwa wahujumu wote wa serikali yaTanzania na vibaraka wote kwani kiama chenu kimekaribia"
"kawasimulia huko kuwa hivi sasa mke wako ataenda kuwa mjane na wiki mbili zijazo atakuwa anani bembeleza kitandani FACUND................" ghafla umeme ukikatika mtaa ule na kutanda giza huku mlio wa cheche za transfoma iliyozima huku kukifatia na milio mitatu tofaui, Ndiyo kwani sauti ya kwanza ya mlio kama chafya ya mtoto iliendana sambamba na sauti ya miguno ya maumivu na yowe la mtu aliyekuwa ameshindwa kupiga hesabu zake vizuri na sauti ya tatu ni mlio mbaya wa risasi iliyochana upepo, kisha kukawa kimya, kuashiria kila mtu anamvizia adui yake, mbali na hayo yote bunduki ile iliyotoa mlio wa chafya ya mtoto ilizipiga chafya hizo mara tatu zikifutiwa na yowe la hofu lililoambana na kupaa hewani na kisha kutulia.
"kamanda tuondoke hapa tuko nje ya muda asubuhi inatakiwa itukute tumeshavuka ngara" sauti nzito yenye mamlaka ilikoroma huku kukifatiwa na watu wale kutoweka mahali pale, kapteni jumanne saidi pamoja na Sorge waliondoka eneo hilo.
SNR HQ-BURUNDI
Saa 8:25 usiku
simu inapigwa katika eneo la vyoo vya ofisi moja iliyo ndani yajengo la makao makuu ya idara ya ujasusi nchini Burundi.
"muda wowote kuanzia sasa ngoma inaweza kupasuka na nchi ikawa uchi kweupe ila kwa taarifa tu kuna maiti mbili kutoka kwa majirani zimegundulika jirani na ubalozi na kinachotia shaka ni yule mtu aliyekuwa akitafutwa na idara kwa siku nzima amekutwa akining'inia juu ya jengo huku maiti yake pia ikikutwa na matundu ya risasi acha hilo hili ndiyo litakustua, kanali mmoja kutoka huku naye alikuwa kwenye msitari wa kumlaki bwana mawinguni kwani naye alichezea mvua ya risasi na kisha mwili wake kutoweka na kisha kuibukia mochwari za hospitali ya taifa"
"whaaaaaat!!!,,,,,,,,,,nini kinachoendelea ina maana mkurugenzi halioni hili au ana mkono na ametia baraka kwenye hili?" aliuliza swali mtu aliyeonekana kama ana mamlka fulani
"siwezi kusema ndiyo au hapana kwa sababu kwa binadamu yote yanawezekana na sheria namba moja ni kuto kumuamini mtu yoyote ikiwa ni pamoja na mimi mwenyewe" alisema mpigaji
"fatilia kila kitu na walau nipe ripoti ya kilichojiri kesho asubuhi..........TITITI"simu ile ilikatwa huku ikiacha maelekezo ambayo yalibakisha saa chache kabla hayajatolewa ufafanuzi na mpigaji wa simu aliyekuwa ndani ya jengo la idara hiyo nyeti kisha mtu huyo akatoka ndani humo na kurudi katika kiti alichokuwa amekikalia huku akijikita kwenye kuchakata taarifa zitakazotolewa maelezo asubuhi kwa mkuu wake hakujua kuwa mita kadhaa kutoka katika ofisi yake kuna watu sita walikuwa wakiyasikiliza mazungumzo yale yaliowafanya wasisimke kiasi cha kuadhimia watu wale waliokuwa wamepigiana simu kutokuliona jua laa kesho hii ilimaanisha walikuwa wameshapewa hukumu ya kifo bila hata kupewa notisi
*******************
POSTA-DAR ES SALAAM
Saa 12:00 asubuhi
ilikuwa ni asubuhi nyingine iliyolifukuza giza na kuukaribisha mwanga kutamalaki, jogoo wakiwika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es salaam na kona zingine za nchi ya tanzania, muda huo huo ulizoeleka ya kwamba mtangazaji wa redio atawapitisha katika kurasa za magazeti.
"mama johnson hebu niwashie redio nisikilize kulikoni katika hii nchi iliyojaa mizengwe"
"hebu huko usinisumbue......hizo habari zitatulisha badalau amke ukatafute pesa kama wanaume wenzakokutwa unahangaika na mimi" alisema mwanamke yule huku akimgeuzia mgongo
"funga bakuli lako na niwashie redio kabla sijakutia tatuu hapo usoni uone faida ninayopata nkisikiliza uchambuzi wa kurasa za magazeti."
"haya......stesheni gani mume wangu"
"weka mawimbi Fm kama siku zote na harakisha ole wako niikute habari ishachambuliwa nusu utanitambua" alikoroma mwanaume yule
"hebu nawe usinitishe bwana habari habari hadi unanyima amani haya sasa sikiliza habari zako hizo......utadhani mjumbe wa nyumba kumi" aliongea mama yule huku akilifunga tenge lake vizuri tayari kwa safari ya jikoni ndani ya nyumba hiyo."
"hujui ulisemalo mke wangu" akiwa katika tafakuri fupi huku macho yake yakitua kwenye mgongo wa mkewe akakatishwa na habari iliyokuwa katika ukurasa wa mbele wa gazeti la
"GAZETI LA TAA YA JAMII KATIKA HABARI PICHA LINAANDIKA MAUAJI DAR ES SALAAM NA BUJUMBURA HAPATOSHI!!!" alisema kwa mbwembwe za kiandishi wa habari huku akiwaacha wasikilizaji kwa sekunde kama siyo dakika kadhaa wakitafakari ni kitu gani kinaendelea.
"inasemekana kuna fukuto linalo endelea kama siyo mapinduzi katika moja ya nchi ni kuvunja uhusiano wa kidiplomasia, wahusika katika suala hili vigogo wazito katika majiji haya wadaiwa kuhusika, jitahada za kumpata waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa afrika mashariki zagonga mwamba ,Habari kamili utaipata katika ukurasa wa pili...........gazeti la habari moto lenyewe limepambwa na habari picha ikimuonesha Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania akiwa kwenye mkutano na wakuu wa vyombo vya usalama huku kichwa cha habari kikikolezwa kwa wino mwekundu na maneno 'SAFARI HII WAMEYATIMBA!!! kina nani hao jipatie nakala yako katika ukurasa wa pili na wat atu upate kujua undani wa habari hii '"
"Kumbe kuna mambo yanaendelea chini chini na sisi tupo kama vipofu mme wangu" aliongea mke wa jamaa yule huku akiacha kufagia na kuganda kwa sekunde kadhaa huku akimuangalia mme wake
"mambo kama haya huwezi kuyatambua kwa sababu mitandao imewaziba macho na fikra zenu mmekuwa kama wenda wazimu kutwa kucha umbea mara huyu kalala na huyu sijui huyu kala kitimoto siku ya mfungo wa Ramadhani.......inasaidia nini katika kukujenga kiuchumi na fikra kama mpigania uchumi mke wangu" aliongea kwa msisitizo huku akionekana kukereka bwana yule
"sasa nimekuuliza vizuri unanijibu kwa kunifokea..........wewe umeamka na mimi si bure ngoja nikaoshe vyombo maana huchelewi kunipiga" aliongea. mwanamke yule huku akijifunga tenge lake huku akifata uelekeo wa jikoni ndani ya nyumba ile.
"wanawake wengine ni wapumbavu sana yeye anadhania kishinda mtandaoni ni sifa........unaweza kutembea kwa mwili wako unaonekana mzima wa afya kumbe ulishakufa kifikra na mawazo shenzi kabisa nijiendee kazini nikiendelea kukaa hapa nitamzaba vibao" alijisemea yule jamaa huku akiamka kitandani pale na dakika kadhaa mbele alikuwa ndani ya vazi nadhifu lililo chafuka vyeo mabegani, akakisogelea kioo kilichokuwa katikati ya kabati kubwa la nguo na taswira ya pande la mtu ikajichora na tabasamu likaonekana upande wa pili wa kioo hata hivo halikudumu sana kwani lilipotea baada ya sekunde zisizozidi kumi.baada ya simu yake kutoa mlio.
"usipite ofisini kwako nyoosha ikulu moja kwa moja na sihitaji maswali tititititi,,,,,,,,,,,,,"
*itaendelea
Ni bora kusafiri kwa matumaini kuliko kufika, tukutane toleo lijalo kwani kuna mengi utajiuliza ni nani mtu huyu anayeamshwa na taarifa za magazeti? Je ataweza kupambana na waasi wanaosemekana kuharibu amani? Tukutane toleo lijalo.Tcaho
Hizi ndiyo fikra za watu maskini. Umeona tunafaidi sana sio!!!!Inatosha...
Wapeleke wasap ukavute mkwanja...
Mjini shule.......
Sasa mimi na wewe nani masikini?Hizi ndiyo fikra za watu maskini. Umeona tunafaidi sana sio!!!!
Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
Uko sahihi kabisa mkuuSasa mimi na wewe nani masikini?
Mimi ninauwezo wa kumungisha buku buku kila kipande apate za kujisogeza
Wewe tajiri huna hata buku, umuunge mshikaji anajipinda kuleta burudani ?
kwani ww una uhakika gani kama mtunzi ana njaa ya hela hizo bukubuku unazojitapa unazo..tuliza kijambio ww na vp kama mtunzi yupo vizuri kiuchumi amejitosha sasa ww nani umpangie hobby zake kwenye maisha yake.?Sasa mimi na wewe nani masikini?
Mimi ninauwezo wa kumungisha buku buku kila kipande apate za kujisogeza
Wewe tajiri huna hata buku, umuunge mshikaji anajipinda kuleta burudani ?
Mkuu weka mawasiliano yako iwe rahisi kukupata...ili tuweze kupata huduma“Mazingira si kitu kinachotokea nje yetu; ni sehemu yetu. Hatupaswi kufikiria juu ya kuokoa dunia tu, bali kutafuta njia ya kuishi kwa usawa na dunia."
Sadhguru
TUENDELEE TULIPOISHIA……………….
sauti nzito na yenye mamlaka ilikoroma
"mmmhhhh kuna nini.........siku ngumu imeanza asubuhi yote hii Mungu nitangulie" akapitisha sekunde kadhaa akiwa kwenye tafakuri nzito na kisha akajongea hadi mlangoni na kutokomea nje na hapo alimkuta dereva wake na mlinzi wake wakimsubiri, walipomuona walikakamaa na kutoa salamu ya heshima kwa kupiga saluti akaitikia na kuingia kwenye siti ya katikati tayari kwa safari ya kwenda ikulu geti lilifunguliwa na mtu yule aliyeonekana kuwa afisa wa ngazi za juu wa jeshi la polisi, wakati hayo yakiendelea meza mbalimbali za kuuzia magazeti zilikuwa zimezungukwa na watu huku mijadala mbali mbali ikiwa ni ile iliyoibuliwa na habari zilizokuwa kwenye vichwa vya habari katika ukurasa wa mbele wa magazeti pendwa mawili.
"Muda mwingine serikali inajifanya ni pumbavu ili kuwapumbaza wa pumbavu wanaofikiria wanai pumbaza yenyewe" aliongea mzee mmoja kiasi cha kuwafanya watu wote kugeuka
"kwanini unasema hivyo mzee wangu ikiwa nchi yetu kwa sasa inaghubikwa na matukio ya kutisha na kila taarifa zinapotoka hazina majibu kamili mara leo hivi kesho unasikia mara IGP ameuawa haiingii akilini hata kidogo mtu kama yule ajiue kwa kipi ulinzi anao tena wa kutosha hii inanifanya niamini kuna kitu hakipo sawa nchini" alihoji kijana mmoja huku akimtazama mzee yule akiwa ametengeneza hoja zake.
"kho kho kho sikiliza kijana umeanza vizuri ila umemaliza vibaya iko hivi usiwe na pupa na papara kuamini kila kinachopenya kwenye ngome za masikio yako na siyo wewe peke yako hata nyie wengine" alisema hivo huku akiwatupia macho watu wale kwa zamu nao waliishia kucheka tu na wengine wakimdhihaki kuwa mzee yule ameikimbia familia yake huko kijijini na amekuja kusumbua watu mjini.
"ndiyo tatizo la kizazi hiki chenye papara na ujuaji mwingi ila hakijui chochote ndiyo maana leo hii kuna matangazo ya kuongeza nguvu za kiume kuliko kizazi chochote kile..........iko hivi uongo una tabia ya kupanda ndege na kulifikia eneo la tukio tofauti na ukweli unao panda baiskeli na hakika huchelewa kufika ila unapofika tukioni uongo huona aibu na kutoweka kila kitu hubaki kweupe kama jua la saa tisa kila kitu kitakuwa wazi na hii ndiyo imani na hasira ya serikali hii" hakusubiri maswali katika mjadala ule alipotea eneo lile na mjadala ukazuka tena kuhusu mzee yule mwenye maneno mazito na ya kusisimua huku wengine wakimshuku ni afisa usalama wa taifa huku wengine wakikanusha huku wakijiapiza kumfahamu mzee huyo kama mshona viatu mtaa wa nyuma na aliitelekeza familia yake huko mbalizi mbeya na kukimbilia mjini.wengine wakaenda mbali kuwa huenda ni mchawi na ndiye anayewasumbua usiku wasilale kwa amani.
Wakati hao wakiendelea na mjadala huo mzee yule alikuwa akinunua salio na kisha kupiga simu sehemu ikaita kwa dakika kadhaa na kukatwa kisha ukaingia ujumbe.
"MAKUMBUSHO SAA 4 ASUBUHI, KAUNDA SUTI, ID UTAIKUTA GETINI JINA LAKO 012 titititi" simu ikakatwa na kumuachia tabasamu mzee huyo, halikuwa tabasamu la mahaba au tabasamu la furaha bali tabasamu la kikatili.
"mwandishi hakukosea kusema wameya kanyaga nawaonea huruma wale wote waliochagua maumivu ya majuto watakufa wakijutia kutochagua maumivu ya nidhamu napenda ninachokiona" alijiwazia mzee yule
BUJUMBURA-BURUNDI
Saa 1:25 asubuhi
Kama yalivyo andika magazeti ya nchini Tanzania,ndivyo ilivyokuwa nchini humo huko magazeti kama all Africa na The Africans ilikuwa kama vichwa vyake vimehaririwa na mwandishi mmoja kwani maudhui ni yale yale huku magazeti yakipambwa na picha za maiti mbili jirani na ulipo ubalozi wa nchi ya Tanzania nchini burundi lakini pia kukiwa na picha ndogo ya mkuu wa jeshi la polisi nchini humo huku maswali yakiwa lukuki vichwani mwa wananchi lakini pia viongozi waandamizi katika nchini hiyo kwani ni wiki kadhaa tangu yatokee mauaji na kulipuliwa jengo hilo huku ikisemekana balozi pia ameuwawa, leo tena wanaamshwa na habari hiyo nzito ya kuuwawa kwa watu wale huku mmoja akionekana ni yule aliyekuwa akitafutwa kwa donge nono asubuhi, huku mwingine akisemekana ni mtanzania mwanajeshi mwenye cheo cha luteni usu huku akionekana ni mtu aliyefuzu mafunzo na mbinu za kimedani.
SNR HQ-BUJUMBURA
Saa 3:45
"Good Morning Mr President........." aliongea kwa unyenyekevu mtu yule aliyeonekana kama bosi katika ofisi ile
"what is going on..........i appointed you not to just sit and wait for cosmetics reports, my country is in chaos and nothing is ongoing, ask yourself Director how many times i tell you to act smart and you still repeat those mother Where We Dare To Talk Openly mistakes" aliunguruma mheshimiwa raisi
"sorry boss but preliminary investigation shows that Tanzanian try to.........." alikatishwa asiendelee kuongea na mtu yule aliyeonekana ni bosi wake na raisi wa nchi hiyo
"listen carefully you son of b*tch, now i prove that your the most incompetent Director of intelligence in this country, let me tell you one thing if lift your *ss up there and i will drag it down here and just remember one thing you have 12 hours to come with answers or select any prison that you will be comfortable Mr.Director titititi"
"Ooops....." alishusha pumzi ndefu huku jasho likimmwagika.
***********************
NIPENDE KUTOA SHUKRANI TOKA MWANZO WA SIMULIZI HII HADI HIVI SASA ILIPOFIKIA NA NICHUKUE FURSA HII KUSEMA YA KWAMBA KWA TSHS 1000 UTAWEZA KUPATA VIPANDE VILIVYOBAKIA VYA SIMULIZI HII.
TUKUTANE PM KWA ATAKAYEHITAJI
Tchao.
Nicheki kwa whatsaap simu namba 0746099255Mkuu weka mawasiliano yako iwe rahisi kukupata...ili tuweze kupata huduma