Asali ya limao
Member
- Dec 27, 2018
- 57
- 104
- Thread starter
- #21
MAANDIKO NA NADHARIA MBALI MBALI ZINA SISITIZA KWAMBA KATIKA MAMBO YOTE NI VYEMA KUSEMA UKWELI, LAKINI KATIKA HAYO SIYO KILA WAKATI NA KATIKA KILA KITU YATUPASWA TUSEME UKWELI…………KWANI YANA MAANA GANI MANENO HAYA MANENO UNGANA NAMI SEHEMU YA KUMI NA NNE
"nasikia vanessa alikuwa ‘SHIMO LA TEWA’ leo anahojiwa vikali na malaika wa kifo pamoja na kile kimama cha nyumba nyeupe" alifungua maongezi hayo pande la mtu lilikuwa limeyaficha macho yake katika miwani na mkononi alikuwa ameshika kimiminika cha mvinyo wa bei mbaya brandi ya ‘Cabernet Sauvignon’
"unasema amehojiwa wapi na nani? mchongo si ulikuwa uishie polisi na vipi maelezo na askari wa kumhoji si tulikuwa tusha mpenyezea kamanda wa mkoa huku akiniahidi hakuna kitakacho haribika imekuwaje tena uniambie ameenda kuhojiwa sijui wapi Kobe acha kunichanganya"aliongea mzee wa makamo ambayo bado mwili wake ulikuwa timamu kwa ratiba ya mazoezi anayozingatia kila siku huku akiwa na sigara kubwa mdomoni
"eeennhh niliambiwa hivyo na yule mtu wetu aliyeko jikoni na alinieleza kuwa watu wetu walikuwa wanahojiwa vikali na watu wa idara ya kupambana na dawa za kulevya na uhamiaji, ila ni vanessa peke yake aliyepelekwa kuhojiwa na idara ya ujasusi tena alikuwa katika mahojiano makali na dada mmoja wana muita malaika wa kifo na mheshimiwa raisi" alisema yule jamaa mwenye jina la kiroboto huku akipiga mafundo mawili ya mvinyo ule ulioanza kumkolea.
"weeee kiroboto umeanza lini kuleta habari za magazeti ya udaku kwangu.....tanzania na kiidara chake cha ujasusi mbona wanafanya maigizo sana haya huyo malaika wa kifo unayemsemea amepata nini kwa mtu wetu"aliongea kwa dharau na majivuno konokono jamaa aliyekuwa amekaa kimya muda wote akiwa sikiliza.
"mpaka raisi anaondoka mle ndani mtu wetu alikuwa hajatapika maelezo yoyote kiufupi aliwakazia sana na hakusema chochote kutuhusu "
"safi sana nimeongea na mkuu na amesema ndani ya masaa matatu mtu wetu atakuwa anaiacha nchi kuelekea visiwa vya Havana-Cuba kupumzika ama jiji la Arusha liwe majivu, kikamshuka yule mmama na sasa ana haha kutafuta bomu lilipotegwa ila amehakikishiwa hata apewe mwezi mzima wa kulitafuta hatolipata na hata akina kapeto nimeambiwa watatoka lisaa limoja baada ya vanessa kuiacha ardhi ya tanzania.
"hahahah kazi nzuri sana nina imani hata chatu anafurahia sana kuwashika pabaya sana yule mama na vibaraka wake sasa baada ya hapo ndiyo ule mpango wa mapinduzi utafutata hahahahaha mimi nikiwa waziri wa fedha najua wewe kobe watakupeleka madini ushindwe tu kumiliki bastola ya dhahabu hahaaha watoto wazuri wote wa hapa mjini watali imba jina lako"watu hao watatu wenye majina ya uficho ya kiroboto,kobe na konokono walikuwa nchi ya jirani ya Rwanda huku wakibwia mvinyo huku wakipiga soga za hapa na pale
********
saa moja lililopita katika ofisi ya idara ya ujasusi, underground ilikuwa na watu watatu tu peke yake na mazingira yalikuwa ya ukimya wakati walinzi wa mheshimiwa raisi na chifu wakijua kuna kikao kinaendelea ofisini, chifu alikuwa amewasha kompyuta yake huku akifatilia kinachoendelea huko chini huku ajenti chiku akiwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia huko chini akiwa makini kufatlia nyendo za yule binti wakati anafanya mazungumzo na mheshimiwa raisi.
"sina dakika nyingi za kukaa hapa andika majina unikabidhi karatasi" alisema mheshimiwa raisi huku akimkabidhi kalamu na karatasi huku akiwa makini
"mheshimiwa raisi hili jambo ni zito na linahusisha watu wakubwa sana na wengine wako katika serikali yako, nakwambia hivi siyo sababu ya mateso niliyoyapata ila ni kwasababu ya wema kiduchu ulionionesha na kiuhakika mtandao wa dawa za kulevya kwa nchi yetu unaongozwa na mtu mmoja ambaye hata mimi sijawahi kumtia machoni anaitwa ‘VANOSACA’ ila usishangae mtu huyu kuwa na jina hili kwani ukiligeuza unapata maana halisi ila ni mtu hatari na hapa ikulu ashakuja sana tu kiasi cha kutengeneza mtandao wake serikalini huku akiwa na kofia ya ufanyabiashara, biashara zake ni kama kivuli tu ukitaka kumpata angalia video footage za wafanyabiashara wanaoingia ikulu mimi sijawahi kumuona zaidiya kusikia jina la CASANOVA tu kama mkuu lakini mkimpata huyo atawapeleka kwenye mzizi mnaoutaka" alisema Vanesa
"umeniita hapa ili uje uniambie hayo maelezo machache tu ambayo hayajitoshelezi"
"la hasha mheshimiwa mimi wala siyo shemeji yake na makamu wa raisi"
"what.......unasemaje binti?"
"mimi siyo shemeji yake na makamu wa raisi bali wote watatu tulikuwa kwenye misheni, misheni hiyo ilianza kwa kukutana kigoma sijui wakaoana ilikuwa ni kuwapa giza machoni idara ya ujasusi ila mimi ni mzaliwa wa burundi na kwa upande wa mke wa makamu wa raisi, ni mzaliwa wa burundi ila makamu wako wa raisi anatoka nchi jirani ya congo" kulikuwa na kiyoyozi cha kutosha kwenye hilo gari lakini halikuzuia jasho jembamba kumtoka mheshimiwa raisi kwa nimaelezo aliyokuwa anayatoa yule binti ni mazito na watu wale walikuwa jikoni kabisa na kama ni nchi ilikuwa iko uchi bila nguo, kama jasusi mbobevu alijilaumu sana kuto kuyajua hayo tangu mwanzo lakini mwili wake uliingiwa na ubaridi baada ya kukumbuka mchakato mzima wa uchaguzi kwamba kuelekea kura za maoni ndani ya chama alifuatwa na mheshimiwa raisi mstaafu na kwa heshima akamuomba apambanie kiti na huyo bwana akiwa kama makamu wake.
"lakini hilo siyo kubwa sana kushinda hili, hivi unakumbuka oparesheni iliyorudisha maiti mbili za wanajeshi wenu ndiyo oparesheni ya mwisho mliyofanikisha kwa kiasi kikubwa kutuliza amani nchini Congo, kuna watu hawakupenda iwe hivo ndiyo maana mamluki ni wengi serikalini kwako kuliko wazalendo na kwa taarifa tu ninayokupa ni kwamba una siku chache sana za kuvuta pumzi kabla Chatu hajakumeza na ambacho hujui ni kwamba walifanikisha kuiba codes za kuendeshea mitambo ya nyuklia yanayodhalishwa kisiri siri katika maabara za kambi ya jeshi Mafinga na hata mlipuko wa kambi ile na kuibiwa silaha chache ilikuwa geresha tu kuficha kilichotokea nyuma ya pazia."
"wewe binti wewe haya yote umeyapata wapi"
"samahani mama wakati niko kwenye hiki kikundi nilimvutia sana jenerali mstaafu kiasi cha kunifanya niwe mchepuko wake kwa siri sana na alipogundua mimi ni mwenzao hakuwa akifanya siri kuongea na simu za washirika wake mbele yangu na hapo ndipo kulipokuja kutokea mpango wa kukufedhehesha wewe ki madaraka kwa kukupiga matukio huku akishirikiana na mtu mmoja ambaye hakuwahi kumtaja ila anaonekana ana nguvu sana au alishawahi kuwa na nguvu kwenye nchi hii na huyo ndiyo anaemfadhiri huyu jamaa mwenye kitu kingine"
"kitu kingine???......"
"ndiyo.....huyu mtu mwenye nguvu anamfadhiri MUSTAPHA ABD NUR AHMED, ambaye nyie mnamchukulia kama gaidi ila ni zaidi ya gaidi anayetafutwa na serikali ya marekani kwa miongo miwili sasa na kutunzwa kwake katika lile gerezai likuwa ni siri na hata kuondoka kwake gerezani mle pia ilikuwa ni siri na kwa kiasi kikubwa kuna mikono ya watu wazito ilipita ndiyo maana hata kwenye data base yenu ya makampuni hakuna kampuni iliyosajiliwa kutoa huduma za uzibuaji wa mabomba na kama haipo ilipataje tenda ile je wizara na jeshi la magereza halijayatambua haya?" Aliuliza swali tena binti yule na kumuacha mheshimiwa mdomo wazi
"kuna mabomu wameniambia yatalipuka katika jiji hili hebu nisaidie katika hili binti yangu, hebu angalia ni watu wangapiwatapoteza maisha uhawahi kuwaza kama mlipuko huo utatokea ni watoto wangapi watapoteza ndoto zao na maisha yao kwa ujumla, ni mashabiki zako wangapi utawapoteza lifikirie hilo kisha uniambie ni wapi yalipo." Aliongea mheshimiwa raisi kwa sauti ya kusihi
"mimi sijui yalipo ninachokijua nadhani nimekueleza maamuzi ni yako japo sidhani kama itasaidia chatu amekasirika kupata hasara ya kiasi kikubwa cha pesa hivvo hata ukinipeleka bado mabomu yatalipuka na usipofanya hivyo bado atakutia hasara tu kama walivyo zikwapua zile trilioni tano kule katika mapori ya singida......kiufupi unatakiwa uwaze maili nyingi kuweza kuwapata wahusika ukiwa na ushahidi mzito bila hivyo nauona utawala wako ukidondoka na wewe ukizikwa kwa aibu"
"kwahiyo unataka kunambia jenerali mstaafu mzee Chukurubu thomas ndiyo yuko nyuma ya haya masuala" aliuliza mheshimiwa huku akikunja sura
"utakuwa sahihi kwa upande mmoja ila kwa upande mwingine kama uliniskiliza kwa umakini nilikwambia kwamba kuna mtu anawasiliana nae mara kwa mara na huyo ndiyo mkuu wake ambaye ana nguvu na ushawishi mkubwa kwa watumishi wa serikali na vile vile jamii na kama haitoshi fununu zilizopo nikwamba hata huyu mtu ana bosi wake ambaye sio jenerali mstaafu wala kibaraka mwingine anayemfahamu zaidi ya huyu mtu mwenye nguvu katika nchi hii, na kumfikia inabidi uwe umefanya kazi ya ziada sana kwani hata huyo mtu mwenye nguvu sidhani kama kuna mtumishi wako yoyote anaweza kumpata kirahisi labda kama utawapata watu wawili tu jenerali au yule aliyejifanya ni dada angu maana ndiye kiburudisho chake.” Alimaliza huyo binti huku akimuangalia mheshimiwa raisi kwa masikitiko
"nini unaongea wewe binti unataka kusema yule mke wa makamu alikuwa anamsaliti mmewe kwa huyo mtu.........na mbona habari hii haijaletwa mezani kwangu au chifu anatambua hili na akaamua kunyamaza nalo" alijiwazia kwa sauti mheshimiwa raisi.
"mheshimiwa wewe ni mwepesi sana au kusahau habari nilizokupa zimekuchanganya ni hivi tangu wameanza kuishi kwa kujiita mume na mke makamu wako hajawahi kushiriki tendo la ndoa na huyo unayemjua ni mke wake kwasababu huyu makamu wako wa raisi alikuwa hana nguvu ya kusimamisha uume wake baada ya kuchomwa sindano iliyokuwa na dawa kali kiasi cha kuuwa mshipa mkuu wenye kazi ya kupeleka damu kwenyeuume wake na walimuahidi kwamba watampa dawa ili arudie hali yake ya uanaume kamili endapo kama kazi ya kukuangusha ikikamilika ila alifanya kosa moja la mwaka ambalo litamtesa maisha yake yote kwani kiukweli hakuna dawa ya kufanyahivyo na hata wale.watoto walikuwa siyo wake bali ya huyo mtu ndiyo maana huoni hata mmoja akimfanana hata kwa sikio lakini pia bado kuna jambo moja zito huja lifahamu na hilo ndilo linawapa kiburi mpaka kukufanya ukose maamuzi sahihi ni kwamba wanataka kushambulia nchi jirani ya kenya kwa ajili ya kuibua taaruki ili nchi isitawalike huku ukionekana umeshindwa kuongoza na kile ambacho hujui hata huyu spika wa bunge ni mtu wao na wamepanga kumtumia yule mbunge wa kule mkoa wa kusini kupeleka hoja katika hati ya dharura ya kutokuwa na imani na raisi na robo tatu ya wabunge watanunuliwa na watapiga kura ya ndiyo kisha wanakutoa madarakani na baadaya hapo utabaki huna ulinzi utauwawa na baada ya hapo utazikwa kwa aibu badala ya heshima." jasho liliendeleakumwagika japo kuwa kiyoyozi cha gari ile aina ya GMC kikiwa kinaendelea kuweka ubaridi na hewa safi.
***********************************
WALE WOTE WANAOTUFUNDISHA MAANA YA UBINADAMU KUMBE SIYO WANADAMU WENZETU…………. Kumi na nne inaisha hapo tukutane kumi na tano tuone hili jahazi litafika au litazama katikati ya kina cha bahari Tchao
"nasikia vanessa alikuwa ‘SHIMO LA TEWA’ leo anahojiwa vikali na malaika wa kifo pamoja na kile kimama cha nyumba nyeupe" alifungua maongezi hayo pande la mtu lilikuwa limeyaficha macho yake katika miwani na mkononi alikuwa ameshika kimiminika cha mvinyo wa bei mbaya brandi ya ‘Cabernet Sauvignon’
"unasema amehojiwa wapi na nani? mchongo si ulikuwa uishie polisi na vipi maelezo na askari wa kumhoji si tulikuwa tusha mpenyezea kamanda wa mkoa huku akiniahidi hakuna kitakacho haribika imekuwaje tena uniambie ameenda kuhojiwa sijui wapi Kobe acha kunichanganya"aliongea mzee wa makamo ambayo bado mwili wake ulikuwa timamu kwa ratiba ya mazoezi anayozingatia kila siku huku akiwa na sigara kubwa mdomoni
"eeennhh niliambiwa hivyo na yule mtu wetu aliyeko jikoni na alinieleza kuwa watu wetu walikuwa wanahojiwa vikali na watu wa idara ya kupambana na dawa za kulevya na uhamiaji, ila ni vanessa peke yake aliyepelekwa kuhojiwa na idara ya ujasusi tena alikuwa katika mahojiano makali na dada mmoja wana muita malaika wa kifo na mheshimiwa raisi" alisema yule jamaa mwenye jina la kiroboto huku akipiga mafundo mawili ya mvinyo ule ulioanza kumkolea.
"weeee kiroboto umeanza lini kuleta habari za magazeti ya udaku kwangu.....tanzania na kiidara chake cha ujasusi mbona wanafanya maigizo sana haya huyo malaika wa kifo unayemsemea amepata nini kwa mtu wetu"aliongea kwa dharau na majivuno konokono jamaa aliyekuwa amekaa kimya muda wote akiwa sikiliza.
"mpaka raisi anaondoka mle ndani mtu wetu alikuwa hajatapika maelezo yoyote kiufupi aliwakazia sana na hakusema chochote kutuhusu "
"safi sana nimeongea na mkuu na amesema ndani ya masaa matatu mtu wetu atakuwa anaiacha nchi kuelekea visiwa vya Havana-Cuba kupumzika ama jiji la Arusha liwe majivu, kikamshuka yule mmama na sasa ana haha kutafuta bomu lilipotegwa ila amehakikishiwa hata apewe mwezi mzima wa kulitafuta hatolipata na hata akina kapeto nimeambiwa watatoka lisaa limoja baada ya vanessa kuiacha ardhi ya tanzania.
"hahahah kazi nzuri sana nina imani hata chatu anafurahia sana kuwashika pabaya sana yule mama na vibaraka wake sasa baada ya hapo ndiyo ule mpango wa mapinduzi utafutata hahahahaha mimi nikiwa waziri wa fedha najua wewe kobe watakupeleka madini ushindwe tu kumiliki bastola ya dhahabu hahaaha watoto wazuri wote wa hapa mjini watali imba jina lako"watu hao watatu wenye majina ya uficho ya kiroboto,kobe na konokono walikuwa nchi ya jirani ya Rwanda huku wakibwia mvinyo huku wakipiga soga za hapa na pale
********
saa moja lililopita katika ofisi ya idara ya ujasusi, underground ilikuwa na watu watatu tu peke yake na mazingira yalikuwa ya ukimya wakati walinzi wa mheshimiwa raisi na chifu wakijua kuna kikao kinaendelea ofisini, chifu alikuwa amewasha kompyuta yake huku akifatilia kinachoendelea huko chini huku ajenti chiku akiwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia huko chini akiwa makini kufatlia nyendo za yule binti wakati anafanya mazungumzo na mheshimiwa raisi.
"sina dakika nyingi za kukaa hapa andika majina unikabidhi karatasi" alisema mheshimiwa raisi huku akimkabidhi kalamu na karatasi huku akiwa makini
"mheshimiwa raisi hili jambo ni zito na linahusisha watu wakubwa sana na wengine wako katika serikali yako, nakwambia hivi siyo sababu ya mateso niliyoyapata ila ni kwasababu ya wema kiduchu ulionionesha na kiuhakika mtandao wa dawa za kulevya kwa nchi yetu unaongozwa na mtu mmoja ambaye hata mimi sijawahi kumtia machoni anaitwa ‘VANOSACA’ ila usishangae mtu huyu kuwa na jina hili kwani ukiligeuza unapata maana halisi ila ni mtu hatari na hapa ikulu ashakuja sana tu kiasi cha kutengeneza mtandao wake serikalini huku akiwa na kofia ya ufanyabiashara, biashara zake ni kama kivuli tu ukitaka kumpata angalia video footage za wafanyabiashara wanaoingia ikulu mimi sijawahi kumuona zaidiya kusikia jina la CASANOVA tu kama mkuu lakini mkimpata huyo atawapeleka kwenye mzizi mnaoutaka" alisema Vanesa
"umeniita hapa ili uje uniambie hayo maelezo machache tu ambayo hayajitoshelezi"
"la hasha mheshimiwa mimi wala siyo shemeji yake na makamu wa raisi"
"what.......unasemaje binti?"
"mimi siyo shemeji yake na makamu wa raisi bali wote watatu tulikuwa kwenye misheni, misheni hiyo ilianza kwa kukutana kigoma sijui wakaoana ilikuwa ni kuwapa giza machoni idara ya ujasusi ila mimi ni mzaliwa wa burundi na kwa upande wa mke wa makamu wa raisi, ni mzaliwa wa burundi ila makamu wako wa raisi anatoka nchi jirani ya congo" kulikuwa na kiyoyozi cha kutosha kwenye hilo gari lakini halikuzuia jasho jembamba kumtoka mheshimiwa raisi kwa nimaelezo aliyokuwa anayatoa yule binti ni mazito na watu wale walikuwa jikoni kabisa na kama ni nchi ilikuwa iko uchi bila nguo, kama jasusi mbobevu alijilaumu sana kuto kuyajua hayo tangu mwanzo lakini mwili wake uliingiwa na ubaridi baada ya kukumbuka mchakato mzima wa uchaguzi kwamba kuelekea kura za maoni ndani ya chama alifuatwa na mheshimiwa raisi mstaafu na kwa heshima akamuomba apambanie kiti na huyo bwana akiwa kama makamu wake.
"lakini hilo siyo kubwa sana kushinda hili, hivi unakumbuka oparesheni iliyorudisha maiti mbili za wanajeshi wenu ndiyo oparesheni ya mwisho mliyofanikisha kwa kiasi kikubwa kutuliza amani nchini Congo, kuna watu hawakupenda iwe hivo ndiyo maana mamluki ni wengi serikalini kwako kuliko wazalendo na kwa taarifa tu ninayokupa ni kwamba una siku chache sana za kuvuta pumzi kabla Chatu hajakumeza na ambacho hujui ni kwamba walifanikisha kuiba codes za kuendeshea mitambo ya nyuklia yanayodhalishwa kisiri siri katika maabara za kambi ya jeshi Mafinga na hata mlipuko wa kambi ile na kuibiwa silaha chache ilikuwa geresha tu kuficha kilichotokea nyuma ya pazia."
"wewe binti wewe haya yote umeyapata wapi"
"samahani mama wakati niko kwenye hiki kikundi nilimvutia sana jenerali mstaafu kiasi cha kunifanya niwe mchepuko wake kwa siri sana na alipogundua mimi ni mwenzao hakuwa akifanya siri kuongea na simu za washirika wake mbele yangu na hapo ndipo kulipokuja kutokea mpango wa kukufedhehesha wewe ki madaraka kwa kukupiga matukio huku akishirikiana na mtu mmoja ambaye hakuwahi kumtaja ila anaonekana ana nguvu sana au alishawahi kuwa na nguvu kwenye nchi hii na huyo ndiyo anaemfadhiri huyu jamaa mwenye kitu kingine"
"kitu kingine???......"
"ndiyo.....huyu mtu mwenye nguvu anamfadhiri MUSTAPHA ABD NUR AHMED, ambaye nyie mnamchukulia kama gaidi ila ni zaidi ya gaidi anayetafutwa na serikali ya marekani kwa miongo miwili sasa na kutunzwa kwake katika lile gerezai likuwa ni siri na hata kuondoka kwake gerezani mle pia ilikuwa ni siri na kwa kiasi kikubwa kuna mikono ya watu wazito ilipita ndiyo maana hata kwenye data base yenu ya makampuni hakuna kampuni iliyosajiliwa kutoa huduma za uzibuaji wa mabomba na kama haipo ilipataje tenda ile je wizara na jeshi la magereza halijayatambua haya?" Aliuliza swali tena binti yule na kumuacha mheshimiwa mdomo wazi
"kuna mabomu wameniambia yatalipuka katika jiji hili hebu nisaidie katika hili binti yangu, hebu angalia ni watu wangapiwatapoteza maisha uhawahi kuwaza kama mlipuko huo utatokea ni watoto wangapi watapoteza ndoto zao na maisha yao kwa ujumla, ni mashabiki zako wangapi utawapoteza lifikirie hilo kisha uniambie ni wapi yalipo." Aliongea mheshimiwa raisi kwa sauti ya kusihi
"mimi sijui yalipo ninachokijua nadhani nimekueleza maamuzi ni yako japo sidhani kama itasaidia chatu amekasirika kupata hasara ya kiasi kikubwa cha pesa hivvo hata ukinipeleka bado mabomu yatalipuka na usipofanya hivyo bado atakutia hasara tu kama walivyo zikwapua zile trilioni tano kule katika mapori ya singida......kiufupi unatakiwa uwaze maili nyingi kuweza kuwapata wahusika ukiwa na ushahidi mzito bila hivyo nauona utawala wako ukidondoka na wewe ukizikwa kwa aibu"
"kwahiyo unataka kunambia jenerali mstaafu mzee Chukurubu thomas ndiyo yuko nyuma ya haya masuala" aliuliza mheshimiwa huku akikunja sura
"utakuwa sahihi kwa upande mmoja ila kwa upande mwingine kama uliniskiliza kwa umakini nilikwambia kwamba kuna mtu anawasiliana nae mara kwa mara na huyo ndiyo mkuu wake ambaye ana nguvu na ushawishi mkubwa kwa watumishi wa serikali na vile vile jamii na kama haitoshi fununu zilizopo nikwamba hata huyu mtu ana bosi wake ambaye sio jenerali mstaafu wala kibaraka mwingine anayemfahamu zaidi ya huyu mtu mwenye nguvu katika nchi hii, na kumfikia inabidi uwe umefanya kazi ya ziada sana kwani hata huyo mtu mwenye nguvu sidhani kama kuna mtumishi wako yoyote anaweza kumpata kirahisi labda kama utawapata watu wawili tu jenerali au yule aliyejifanya ni dada angu maana ndiye kiburudisho chake.” Alimaliza huyo binti huku akimuangalia mheshimiwa raisi kwa masikitiko
"nini unaongea wewe binti unataka kusema yule mke wa makamu alikuwa anamsaliti mmewe kwa huyo mtu.........na mbona habari hii haijaletwa mezani kwangu au chifu anatambua hili na akaamua kunyamaza nalo" alijiwazia kwa sauti mheshimiwa raisi.
"mheshimiwa wewe ni mwepesi sana au kusahau habari nilizokupa zimekuchanganya ni hivi tangu wameanza kuishi kwa kujiita mume na mke makamu wako hajawahi kushiriki tendo la ndoa na huyo unayemjua ni mke wake kwasababu huyu makamu wako wa raisi alikuwa hana nguvu ya kusimamisha uume wake baada ya kuchomwa sindano iliyokuwa na dawa kali kiasi cha kuuwa mshipa mkuu wenye kazi ya kupeleka damu kwenyeuume wake na walimuahidi kwamba watampa dawa ili arudie hali yake ya uanaume kamili endapo kama kazi ya kukuangusha ikikamilika ila alifanya kosa moja la mwaka ambalo litamtesa maisha yake yote kwani kiukweli hakuna dawa ya kufanyahivyo na hata wale.watoto walikuwa siyo wake bali ya huyo mtu ndiyo maana huoni hata mmoja akimfanana hata kwa sikio lakini pia bado kuna jambo moja zito huja lifahamu na hilo ndilo linawapa kiburi mpaka kukufanya ukose maamuzi sahihi ni kwamba wanataka kushambulia nchi jirani ya kenya kwa ajili ya kuibua taaruki ili nchi isitawalike huku ukionekana umeshindwa kuongoza na kile ambacho hujui hata huyu spika wa bunge ni mtu wao na wamepanga kumtumia yule mbunge wa kule mkoa wa kusini kupeleka hoja katika hati ya dharura ya kutokuwa na imani na raisi na robo tatu ya wabunge watanunuliwa na watapiga kura ya ndiyo kisha wanakutoa madarakani na baadaya hapo utabaki huna ulinzi utauwawa na baada ya hapo utazikwa kwa aibu badala ya heshima." jasho liliendeleakumwagika japo kuwa kiyoyozi cha gari ile aina ya GMC kikiwa kinaendelea kuweka ubaridi na hewa safi.
***********************************
WALE WOTE WANAOTUFUNDISHA MAANA YA UBINADAMU KUMBE SIYO WANADAMU WENZETU…………. Kumi na nne inaisha hapo tukutane kumi na tano tuone hili jahazi litafika au litazama katikati ya kina cha bahari Tchao