Simulizi ya Kijasusi: Giza la Wasaliti

Simulizi ya Kijasusi: Giza la Wasaliti

1 Yohana 1:9 - "Ikiwa tukikiri dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutuosha na uovu wote."…………. Usishangae kuanza na nukuu ya kitabu cha maandiko ungana nami tukashangae yaliyomo kwenye toleo hili litakalo kusisimua na kukuburudisha karibu tusomane……..
"mtu huyo tayari yuko mikononi mwetu na hivi tunavyoongea yuko 'SHIMO LA TEWA' anangojea huruma yako"alisema chifu kwa tabasamu
"nitakuwa ofisini kwako ndani ya dakika tatu kutoka sasa....titititi" Simu ilikatwa kuashiria ni muda wa yeye kuwa mazingira ya ofisini kwasababu ndani ya sekunde chache bosi wake atakuwa ofisini kwake
"kijana tuongozane" alisema chifu huku akimgusa bega ASP Richard na wakanza kuzitupa hatua ndefu ndefu kuelekea ofisini kwake,
********
"Chifu nipe ripoti za huko mitaani, wamefikia wapi vijana wa Arusha?" Aliuliza raisi huku akimtazama chifu katika macho yake.
"nkutoe wasiwasi mheshimiwa mpaka Sasa vijana wamefanikiwa kuyapata mabomu manne yaliyo kuwa yamepangwa kutegwa katika sehemu tofauti tofauti na hiviSasa wanawafanyia mahojiano ila mpaka Sasa wametajiwa Jina la Mohamed mahboob kwamba ndiyo ufunguo wa kumpata Mustapha Abd nur Ahmed mheshimiwa......" Alitoa maelekezo hayo Chifu na wakati huo huo simu ya ASP Richard ikaunguruma mfukoni mwake kiasi cha kufanya umakini wa watu wale wazito katika nchi kuhamia kwake naye bila ajizi alitoa na kuwaonesha mpigaji.
"pokea na weka loudspeaker chifu rekodi kila kitu" yalikuwa ni maagizo Mazito ya mheshimiwa raisi.
"jambo afande" alitoa salami hiyo ASP Richard kwa sauti ya unyenyekevu
"Sihitaji salamu yako ila nahitaji kujua umeanza lini kufanya kazi za utekaji na mauaji, hivi unaweza Kunambia ulifata nini? nyumbani kwa Askofu na umempeleka wapi mtumishi wa Mungu, kijana nilikuona wa maana Sana kumbe siyo kweli kabla hujaingia matatizoni niambie tu umempeleka wapi Askofu na ni Nani huyo aliyekupa amri ya kufanya hivyo Kisha jisalimishe kituo chochote cha polisi huenda hutaumia kama wakikusaka vijana wangu wa jeshi la polisi." Alifoka IGP huku akiporomosha msululu wa lawama.
"unataka kujua mahali alipo kinara wa dawa za kulevya kwenye taifa hili na Nani aliyenitum....." Alikatishwa
"nyamaza mpuuzi ni wapi ulichunguza na ukakuta Ana tuhuma za hivo Tena chunga kinywa chako kijana nijibu maswali yangu na ujisalimishe jambazi mkubwa wewe kuanzia Leo 'HUNA KAZI' na wewe ni mhalifu kama raia wengine waharifu nikukumbushe tu kuwa usisahau kwamba serikali ina mkono mrefu hivyo futa mawazo ya kutorokea nchi jirani kwani utadakwa kama kuku" aliendelea kutokwa na mapovu IGP
"usihangaike kumlaumu na kumtukana kijana wa watu nilaumu mimi, na askofu unayemsema yuko idarani kwangu anasubiri mahojiano na aliyemtuma kiukweli sistahili kumuongelea" aliongea chifu kwa ustaarabu
"kwahiyo Chifu umeanza kuwatumia vijana wangu kufanya kazi zako ili tu ulipake jeshi letu matope, Kila siku tunalaumiwa kwa mauaji na utekaji na lawama zinapanda kwetu sisi wa juu huku wewe na vijana wako mkila kuku kwa mrija, nataka nikwambie kama uliyemtuma ni wewe basi ameyakanyaga hahaha gereza litamhusuna nitasimamia kesi yake kwa kufuata sheria hadi ahukumiwe kunyongwa kwa kiherehere chake" aliongea IGP huku akichanganya na kicheko
"nilimtuma Mimi na gerezani ataenda Askofu na washirika wake tusishinde tukipiga soga, na nakujua vizuri mzee wangu tena vizuri tu kama mpokeaji wa posho kutoka kwa Hilo zungu la unga, hujiulizi ni kwanini nilivunja Ile timu ya kwanza ni kwasababu wengi wenu mlikuwa mnahujumu jitihada za kuhakikisha wahalifu wanavaa nguo za rangi ya machungwa, umesema kijana ajisalimishe kituo chochote cha polisi, Sasa mimi nakwambia ifikapo kesho saa mbili asubuhi uwe umeandika barua ya kujiuzulu vile vile uwe umejisalimisha kambi yoyote ya jeshi la wananchi na ntampa maelekezo jenerali usiku huu huu kuwa akupokee na akulete mwenyewe ofisini kwangu nadhani nikutakie usiku mwema na maamuzi yaliyo sahihi." aliongea mheshimiwa raisi huku upande wa pili ukiwa kimya na simu ikakatwa.
" mkuu hawa watu ni hatari sana wameweza kuwashika masikio hadi maafisa wa jeshi na wa idara ya ujasusi" aliongea ASP Richard huku akiwatazama Chifu na mheshimiwa raisi kwa tuo.
"unataka kusema mini? Richard" aliongea chifu kwa udadisi huku mheshimiwa raisi akijaribu kuchakata kauli hiyo
"niliwakuta meja tumbaku na ajenti Diana nyumbani kwa Askofu tena ilionesha walikuwa pale kwa lengo la kumlinda mtu huyo lakini hata nilipomuweka chini ya ulinzi bado walidiriki kunitolea bastola zao huku wakitoa maneno ya kashfa sana, bahati iliyoje hawajaujua upande wangu wa pili ambao hata shetani hukaa mbali kushuhudia matusi yangu, nikatieni tiketi ya ndege inayoelekea kigoma usiku huu maana nahitaji asubuhi ya kesho niwe bujumbura kuna watu wanahitaji kuvuta 'PUMZI YA KIFO' na tutamleta hapa yule mjinga aliyejifanya ni mzawa na kuwahadaa viongozi mpaka akapata nafasi" aliongea huku akiwa na munkari ya kazi na uchungu mkubwa.
"Chifu hawa ndiyo watu ninaofanya kazi nao......mpe kile anachokihitaji kwa wakati sahihi, Richard hakikisha unarudi ukiwa mzima na mwenzako, sihitaji kuipa mahakama gharama za kutafuta wakarimani sijui kuwasimamisha kizimbani ninachohitaji hawa watu wote waliokimbilia huko wazikwe kwa aibu, Chifu nitakuja asubuhi kuonana na askofu macho kwa macho ili nijue kama malaika wake ni wa nuru au giza" aliongeamheshimiwa raisi kwa msisitizo na kwanza kuondoka
**********
JOMO KENYATA INTERNATIONAL AIRPORT-KENYA
Saa 05:47 usiku.
"sikiliza tutakutana bujumbura kesho saa nne asubuhi ili tuanze kulinusa jiji hilo na undani wa kifo kutatanisha cha balozi"
"wala usijali mkuu kama tulivyopanga na ikawe hivo tukutane saa 4 asubuhi" haya yalikuwa mazungumzo baina ya watu wawili mmoja akiwa Kapteni Jumanne Saidi huku mwinginenakiwa ni Thobias Chumvinyingi, afisa wa idara ya ujasusi aliyehudumu katika ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini burundi ambaaye atakuwa mwenyeji wao kwani duru za kiusalama zinaonesha hata wale maafisa wa ubalozi nao pia waliuawa wote pasipo kupewa nafasi ya kukimbia kifo chao na sasa wawili hawa walikubaliana waingie kwa mtindo wa kutumia ndege na mwingine aingie jijini bujumbura kwa usafiri wa gari akitokea mpakani. hivyo walikubaliana kapteni Juma saidi atumie usafiriwa gari kupitia mipakani na huku Thobias Chumvinyingi akiunganisha na ndege mpaka uwanja wa ndege ulioko jijini bujumbura katika nchi ya burundi, wakaagna huku wakikumbushana muda wa miadi yao hapo kesho katika mgahawa wa 'belvedere restaurant' katika katikati ya mji wa Gatumba.
mungu alikuwa upande wao kwani mara baada tu ya Thobias Chumvinyingi kupaa na ndege ya kenyan's Airways naye kapteni Jumanne Saidi alikuwa amebahatisha usafiri uliowabeba watawa kuelekea jijini bujumbura kwa ajili ya shughuli nzimaya kueneza neno la Mungu katika maeneo kama hayo ambayo uhalifu umeshamiri kiasi cha kuonekana kana kwamba watu hao hawana hofu ya Mungu, kupeleka kwao huduma katika eneo hilo wakitokea Kenya watumishi hao wa bwana katika safari yao walijipamba kwa mavazi nadhifu kama ya kitawa huku muda wote wakiwa na biblia mkononi, haikuwa ngumu kwa kapteni Jumanne Saidi kupata mavazi na kukaa kama watumishi wale kwani kwa uzoefu wake katika kazi za kijasusi. kuigiza na kuendana na mazingira ndiyo ilikuwa nguzo muhimu katika kufanikisha kazi mbalimbali alizotumwa na mabosi wake, na kwa uhakika hata hili la kuwa kama mtumishi bado lilimpendezea kuliko hata mchungaji anayehubiri madhabauni kwani mbali na kuwa muumini wa dini ya kiislamu lakini kuna wakati anabadilika na kuwa joseph au paulo ili tu kuendana na mazingira, hapa alikamata biblia huku akiwa na miwani yake ya macho huku msalaba mkubwa ukining'inia shingoni kwake na muda wote alikuwa amefunua biblia akisoma na kutafakari maandiko kimya kimya kama walivyofanya watumishi wengine huku gari aina ya land cruiser kama zile watumiazo watalii iikizidi kuchanja mbuga kuiacha ardhi ya Kenya na vitongoji vyake na kuanza kuitafuta ardhi ya Tanzania kupitia mpaka wa silali na kisha kuunganisha mpaka jiji la mwanza huku wakiwa na uhakika wa kupitia mpaka wa manyovu kigoma kuingia katika ardhi ya Burundi
"nyie iko kwenda wapi usiku huu na muko binadamu wa ngapi?kwa gari?lete hizo bunduki muko nazo" ni maswali mfulululizo kutoka kwa askari wa kikenya kuelekea kwa dereva wa gari lile waliokuwa lindo katika mpaka wa Tanzania na Kenya
"sikiliza ofisaa humu hamuna bunduki mazee, hawa ni watumishi wa gospel na wako na biblia pekee, tunaingia tizii then tuvuke twende kwa nkurunzinza kuna watu wafaa waokolewe manzee"
"acha kushinda ukisema wenzio waokolewe na wewe ni mkola tu kama hao wa huko.....haya patiana kitu kidogo au tuingie tukisaka ID"
"woiii afisa hata ukitaka utafute ID mapassenger wangu wako na hizo passport manzee wewe tugongee hayo mamihuri sisi tulale mbele, na kitu kidogo na hiyo tumbo uko nayo labda 50 bob itakufaa"
"huyu kijana ako na madharau yaani 50 bob na familia nimeacha iko na njaa.....fanya hivi weka thao sita hapa kwa mfuko na niwagongee hiyo mihuri chap chap la si hivyo tukuwekelee bangi kwa carrier kijanaa machaguzi ni yako." alitokeza afisa mmoja wa uhamiaji na kupigilia msumari
"thao nne mazee niko nazo tugongee muhuri chaap si unajua tuko nje ya muda wasee" alilalamika dereva wa gari lile
"sa si udumbukize kwa mfuko wewe morio wa wapi, unakuwa mzito kama rangi ya silk" dereva yule akaweka elfu nne ya kikenya na kisha wote wakagongewa passport na kisha kuanza safari ya kuigusa ardhi ya Tanzani huku wakichanja mbuga kulitafuta jiji la mwanza na kwa mahesabu ya haraharaka itawachukua mpaka saa tatu asubuhi kulifikia jiji bujumbura.
*********
Ghrrr Ghrrrr............ simu ya ASP Richard iliita mna ni wakati alipoiwasha mara tu aliposhuka katika helkopta ya kukodi naalikuwa akishuka katika uwanja wa mpira wa miguu katrika shule ya sekondari ya kutwa iitwayo 'MANYOVU SECONDARY SCHOOL' na hapo akaitazama simu ile iliyotoa mwanga na juu ya kioo likisomeka jina la mdogo wake akaipokea na kuiweka sikioni
"kaka shikamoo...."
"marhaba dogo....bado hujalala tu mpaka hivi sasa au uko lindoni, kama uko lindoni si unajua hutakiwi kuongea ongea na simu utatengeneza mashaka kwa wenzio, haya sema nakusikiliza shida ni mini?" aliongea kwa sauti ya utulivu ASP Richard na muda huu alikuwa ndani ya gari aina ya range rover lililokuwa halina namba za usajili huku likiwa na chasis namba pekee huku maelekezo yakisomeka kwamba lilikuwa likisafirishwa kuelekea jijini bujumbura na hivyo walitumia mwamvuli wa udereva ili aweze kuingia jijini humo bila maadui kustuka,
"salama tu kaka sema siko lindo bali niko nyumbani hapa sasa kuna habari zimekuja kwenye grupu letu kwamba unatafutwa kwa mauaji na utekaji.......ni ya kweli hayo au figisu figisu za ofisini kwa sababu ninavyokujua huwezi kufanya hivyo" aliongea mdogo wake ASP Richard huku akipima utulivu waupande wa pili.
"hahahaha dogo watu hubadilika hivyo usimzoee mtu kwa sura ya upole na uaminifu wake kwako, sisi binadamu ni viumbe tulioumbwa na kupewa akili ambayo humfanya mtu kubdilika mara tu anapohisi anaipata amani ya nafsi, ni kweli hata mimi nimeliona hilo Tangazo ila nkutoe wasiwasi kwamba hizo ni propaganda tu, kingine hata wakikuuliza chochote kuhusu mimi elezea vile unanivyonijua bila kuacha neno maana najua watakusumbua sana kwa sasa, cha muhimu kabisa kuwa naamani na usiwe na papara kiasi cha kufanya uingie matatizoni nadhani umenielewa dogo" aliongea kwa msisitizo na punde baada ya kumaliza maongezi aliikata simu ile na kukitafuna kipande cha laini ile ya simu na kukitupa katika choo cha jirani na shule ile na kisha kurudi kwenye gari mara moja na hapo alikutana na karatasi nyeupe na hata alipoifunua alikutana na ramani na kuanza kuisoma ramani vizuri na kuinakili kichwanina kisha kukichana chana kipande cha ramani ile na kukitafuna kisha kukitema mara alipofika jirani na ofisi za mpaka wa Tanzania na Burundi,
Baada ya kumaliza taratibu zote sasa alikuwa ameikamata ardhi ya burundi huku akilitafuta jiji la bujumbura ambapo kwa taarifa za awali zinasema mwenzie kapteni Jumanne Saidi ameshatangulia na shirika la ndege la kenya na kwa muda huo huenda ameshaanza kunusa hiki na kile kitakachowafanya kuwafikia wahusika wa shambulio na mauaji ya balozi pamoja na wafanyakazi wote wa ubalozi wa Tanzania nchini Burundi, aliamua kutumia njia hiyo ya mpaka kwasababu kila jasusi kutoka idarani anapotua uwanjani basi taarifa zake huwafikia watu wenye nia ovu na kusababisha usiku huo huo mtu yule kutoliona jua la kesho hali hii iliwafanya majasusi kutoka idara ya TSS kushtuka na kutumia mbinu tofauti na hiyo ilikumpumbaza adui. hivyo alijua ni wapi atakapo patana na mwenzie bila kujua yeye ndiye atawahi kufika kuliko mwenzie anayelitafta jiji la mwanza kupitia gari iliyobeba watumishi.
***********
AL NOOR MOSQUE-ARUSHA
Saa 6:35 usiku
katika nyumba moja iliyo jirani kabisa na msikiti wa 'AL NOOR' inapata ugeni huku mwenyeji akiwa ni mjumbe wa nyumba kumi bwana said kiberiti aliyeambatana na watu wawili mmoja mwanaume na mwingine mwanamke mrembo asiyeonekana kuwa na madhara yoyote zaidi ya kuleta raha kwa mwanaume yoyote atakaye bahatika kuufaidi mwili wake teketeke
"ustaadh Othman samahani bwana kuna ugeni wako na wana maongezi kidogo na wewe" alisema mjumbe yule kwa sauti ya ustaarabu
"wageni gani usiku huu sie tushalala bhana tunashindwa kufaidi matunda ya ndoa kwa raha bila kubugughiwa kwanini usiwaambie waje kesho, wametoka wapi kwanza wageni hao mzee kiberiti"
*****itaendelea
Eneo la Msikiti limepata ugeni ni wageni gani hao??? Wana shida gani na ustadh aliyekuwa akikila chakula cha usiku muda huo je ni wa kina nani hawa? Ungana nami katika toleo lijalo tupate kuwajua wageni hawa na ustaadh othman kwa undani. Tchao
 
“JIFUNZE KUTOKANA NA MAJUTO YAKO, LAKINI USIRUHUSU YAWE KIKWAZO KWAKO”…………..NA NDIYO NJIA YA MAISHA KWANINI MANENO HAYA KETI NA NISOME KATIKA TOLEO HILI.
"nadhani hivo sivyo tunavyo wa karimu wageni wetu hata dini yetu haisemi hivyo unavyofanya bwana ustaadh othman, ungekuja uwasikilize bhana hata kwa dakika kadhaa" alisisitiza mjumbe yule huku akiwa na shauku ya kujua kilichowaleta wageni wale usiku ule uliokuwa umeanza kuwa na giza zito.
"haya nakuja ila ni kwasababu ya heshima yako mzee kiberiti" alisema bwana yule aliyejulikana kama ustaadh huku purukushani za hapa na pale zikionekana kufanyika ndani humo huku wageni wale wakiangaliana na kisha kusogea jirani na mlango kitu kilicho mvuta na mjumbe yule kusogea mlangoni pale dakika zilikuwa zimeyoyoma kiasi cha kufikia saa 7 kasoro ya usiku na punde kitasa cha mlango kilizungushwa kumaanisha muda wowote kuanzia pale mwenyeji angetoka nje.
"haya mzee kiberiti nimetoka kama ulivyosema, eeeennnhh wageni mna shida gani usiku huu mnene" aliongea huku akipiga miayo huku akionekana bado ana wenge la usingizi huku akiwatizama wote watatu kwa tuo.
"nadhani wange jielezea wenyewe kwa maana wenyewe ndiyo wana shida na wewe" alisisitiza tena mjumbe
"aaahhh labda tusipoteze muda wenu wazee wetu, ni kweli tuna shida na ustadh Othman na sisi wote hapa ni maafisa wa jeshi la polisi na vitambulisho vyetu hivi hapa na mimi cheo changu ni mrakibu mwandamizi wa jeshi la polisi na mwenzangu ni mkaguzi wa jeshi la polisi hivyo tunakuhitaji kituo cha kati kwaajili ya mahojiano kuhusu tuhuma fullani ambazo kwa sasa hatuta ziweka wazi kwasababu za kiupelelezi" aliongea kwasauti kavu huku uso wake muda wote ukiwa wa baridi usio na masikhara hata kidogo.
"mahojiano.....maafisa wa polisi, kituo cha kati mmmmhhh mnanipa wakati mgumu ila kwa vile nimeona vitambulisho ila bado haitoshi mimi kuwaamini maana siku hizi Kuna utekaji au nakosea mjumbe, maadamu mmeshajua kwangu basi kesho wakati wa mwanga ukiwa mweupe Kabila alafu isitoshe mimi ni ustaadh hapa nafahamika na sijafanya kosa lolote kiasi niogope kuambatana nanyi nasita hivi Sasa kwa sababu ni Giza na kiufupi karibia Askari wengi wa pale nawafahamu ila sure zenu ni ngeni na zinanipa walakini"
"ni kweli ulisemalo ustaadh Othman, Hali inatisha kidogo ila ndugu zetu wanaonekana waungwana na huenda wamekusikia na kukuelewa au waungwana mnasemaje" alikandamizia mjumbe kauli aliyoisema ustaadh Othman.
"kazi zetu hazituruhusu kumpa mtu nafasi ya kuharibu upelelezi, hizo ngonjera sijui za nini. Sisi hatufanyi kazi kwa kubahatisha na tunajitoa usiku na mchana macho hayafumbi kuhakikisha nyinyi na familia zenu zinakuwa salama, leo unakuja kuzungumza nini unadhani mpaka tunkuja kwakwo tulikuwa tunabahatisha, kwanini hujiulizi mtaa mzima huu wa Sakina hatujaenda kokote zaidi ya hapa, siku nyingine mzee ujifunze kunyamaza watu wanapokuwa kazini, ustaadh othman geuka unipe mikono yako ni amri na siyo ombi" aliongea chiku kwa msisitizo na sauti iliyojaa utemi. ilitokea tukio la ghafla sana kwani chiku alihisi kama upepo umechanwa na kitu mara baada ya kuinama naye bila ajizi aliwahi kuuchota ule mguu uliokuwa chini kiasi cha mpigwaji kutoa yowe la hofu huku akiwa hajatua vizuri alikutana na teke la mbavu lililomfanya abweke kama mbwa aliyepigwa jiwe huku akiachia tusi kavu la nguoni kitu kilichomuacha mdomo wazi mjumbe.
"mnataka vita nyie makafiri acha niwape vita mtakayowasimulia mababu zenu huko mtakapofika" alisema ustadh othman huku akikunja ngumi kwa mtindo wa karate.
"anatupotezea muda acha mimi nimalizane naye wewe nenda na mjumbe ndani mkatafte cha kutusaidia kwenye upelelezi wetu" aliongea luteni kanali Charz huku akimpa maelekezo Chiku na wakati anamaliza alipishana na kisu kikali kilichorushwa kwa ustadi wa hali ya juu kitu kilichomfanya mjumbe kukimbilia ndani kwa hofu, huku nje wanaume waliendelea kuoneshana nani alikimbia darasa la sanaa ya mapigano, ustadh alirusha makonde yaliyochana upepo kwani hakutambua anayeepigana naye ni mtu wa levo gani,
"mbona unapigana kama mwoga wewe ni askari kweli au mgambo" aliongea ustaadh huku akihema sana, kitu kilichomfanya luteni kanali charz kumsikitikia tu kwani hakuwa na pumzi ya kuhimili mapigano.
"wewe bado sana, unatafuta kuumia kabla hujaumia mpaka ujute kuja duniani, leo nitakufundisha somo kwanini mwanamke akienda chooni kutoa haja ndogo anachuchumaa na mwanaume akienda haja hiyo hiyo ndogo anasimama" alisema hivo huku akimfata kwa mtindo wa judo huku akichanganya na mitindo ya eagle claw kung fu kujilinda na kushambulia huku akitumia ‘simple combination’ kumdhibiti ustaadh Othman ambaye mpaka muda huo hakuwa na meno matatu ya mbele kwa ngumi kavu zilizoupasua mdomo wake, mpambano uliendelea huku ustadh Othman akiwa kama mbogo aliyejeruhiwa na Mshale wa jangili alimfata kwa mapigo ya 'tiger fist' lakini alikuwa akipishana na upepo huku akiambulia maumivu ya kwenyembavu kila ngumi kavu ilipokita kwenye mbavu zake lilikuwa pambano la kimya kimya huku mazingira yakiwapa faida kwani usiku huo hakukuwa na Rabsha Rabsha za watu kufika eneo Hilo hasa ukizingatia kesho yake kulikuwa na tamasha kubwa na asilimia kubwa ya wakazi walikuwa majumbani mwao, ustadh alipoona mambo yanazidi kuwa magumu alitoa kisu kwa lengo la kupambana ila alichokutana nacho mbele yake, Koo lilimkauka kwa hofu na mapigo kwenda kasi kwani alikuwa akitazamana na mdomo wa bastola Aina ya BUL-M5 na muda huo huo kilinda usalama kikaondolewa kumaanisha risasi imepanda kwenye chemba tayari kutumwa kulipokusudiwa
"baaaasi......nimeku...bali imetosha mkuu usiniue.......usiniue mkuu" alisalimu amri huku akikubali uwezo wa luteni kanali charz kwani ndani ya dakika kumi sura yake ilipendeza kwa uvimbe huku maumivu makali ya kizisumbua mbavu zake, hapohapo alizungushwa mikono yake bila kipingamizi na kuvishwa pingu huku akiwa kapiga magoti.
"kweli watu ni wengi ila binadamu ni wachache na umdhaniaye ndiye kumbe siye....dah kumbe tunaswali na kuishi na watu wenye roho ngumu kiasi hili siyo wewe ustaadh Othman kila unaposimama kwenye mimbali unazungumzia 'Amani' na'mshikamano, kumbe nyuma ya pazia unapanga machafuko, ustaadh Othman wewe ni wa kumiliki SMG yenye risasi thelathini.....aaahhhaaa kumbe ndiyo maana ulimtanguliza mkeo na watoto Tanga ukisingizia wanaenda kusalimia kwa wakwe zako.'"
"Taratibu mzee usiamshe waliolala ukatuharibia kaziyetu......hayo uliyoyaona chukulia kama hujawahi kuyaona wala kusikia sahau kuhusu haya madakika tuliyokuwa chukulia kama ulikuwa unayaota ndotoni na utakapo hitajika mbele ya safari usisite kutoa ushirikiano, narudia Tena yabaki kifuani kwako na ukithubutu kuropoka sidhani kama utai ona siku inayofatia" ilisikika sauti ya msisitizo kutoka kwa mwanamke yule huku akimlenga mjumbe.
"Kuna dondoo zozote umepata" aliuliza luteni kanali Charz huku akitazama kwa makini nyendo za Ustaadh Othman
"tuondoke tutazungumza tukifika" alizungumza Chiku hukuakianza kupiga hatua kuelekea kwenye gari, Mara baada ya kuingia aliigeuza gari Ile uelekeo wa barabarani na punde waliingia watu wawili mmoja akiwa mtuhumiwa na mwingine akiwa amekamata bastola yake vizuri waliingia na gari ikakanyagwa mafuta mengi huku Hali ile ikimuacha mjumbe katika bumbuwazi naye akaondoka kuelekea kwake.
"tunampeleka shimoni akatapike ukweli au huyu anapelekwa kuzimu" aliongea chiku akiwa nyuma ya usukani huku wakiwa kwenye kinjia cha kuingia barabarani
"yeye ndiye mwenye machaguzi......eti ustaadh tuambie yukowapi Mohamed Mahboob muda huu"aliongea kwa sauti ya utulivu luteni kanali Charz
"Mohamed Mahboob.......mmmhh Mimi simjui huyo mtu na sijawahi kusikia Jina Hilo masikioni Mwangu" alisema ustaadh huku akiwa ameinamisha kichwa
"ni jibu zuri Sana ila Lina gharama ndani yake, tuelekee monduli tukamfanyie mahojiano huko mpigie jenerali mwambie tunaelekea huko atuandalie mazingira wezeshi" aliongea luteni kanali Charz huku akipitisha kitambaa kilichougawa mdomo wa ustaadh kwani alielewa watu wa namna hiyo hawachelewi kujikatisha Maisha kwa njia ya kutafuna vidonge vya sumu wawapo hatarini au kwa kujing'ata ulimi, gari iligeuzwa kuitafuta njia ya monduli kutokea mitaa ya sakina
**********
ROCA GOLF HOTEL-BUJUMBURA
saa 7:15 usiku
hii ndiyo hoteli aliyoamua apumzike bwana Thobias Chumvinyingi afisa wa idara ya ujasusi ya Tanzania, tayari kuungana na kapteni Jumanne Saidi kwa kazi moja tu ya kuwapelekea wale wote wanaohusika na mipango ya kuhujumu taifa ambalo waasisi wake walilipa garama ya maumivu na jasho kuwamwagika ili tu taifa kuungana na kulinda amani bila kujal iitikadi za dini wala kabila, sasa walikuwa na kibali cha kuwapeleka kuzimu wale wote waliohusika na shambulio la ubalozi sambamba na vifo vya maafisa waandamizi bila kumsahau balozi nchini humo bwana CHACHA SAMWEL, ambaye mbali na kuwa balozi pia alikuwa mkurugenzi wa idara ya ujasusi mstaafu, hiyo ilikuwa dharau kubwa sana kutoka kwa watu walioonekana kuwa tishio kwa usalama wa taifa, alilaza mgongo wake huku akitazama juu mawazo yakiwa kwenye kazi nzito ya kufa au kupona kwani hawajui nguvu aliyo nayo mara akasikia mlango unagongwa alistuka na akili yake kurejesha utimamu kwani alishajua watu aliowawaza walikuwa wameamua kujitokeza tena katika usiku huo mzito bila kusubiri jua lichomoze, mara hii alikuwa katika mavazi yake mwilini na kama haitoshi akarusha swali ili kujua jinsia ya mgongaji.
"nani anasumbua usingizi wangu" aliongea kwa sauti iliyojaauchovu na kukereka.
"Room service" ilijibu sauti nyororo na muda huo kadi yakufungulia mlango ikatiwa mahali pake na mlango ukafunguka, ndipo ikaonekana na sura ya mwanadada maji ya kunde ikiwa na tabasamu mwanana sicho hicho tu kilicho mpendezesha kiasi cha kufanya aonekane mrembo ila ni umbo lililobeba kiuno chembamba kama nyigu na miguu iliyoshiba nyama nyama kiasi cha kuweza kuhimili mzigo ulioshuka chini kidogo ya mgongo kichwani alikuwa amepuguza nywele kwa mtindo wa 'low cut' na macho yake ya duara na makubwa yalitosha kuwatoa udenda wanaume wakware kwa kutamani kuugusa hata kwa sekunde thelathini, lakini mbali na vyote mwanaume aliyekuwa amesimama huku bastola yake aina ya colt 45 ikiwa kiunoni mwake tayari kwa kucheka na wavamizi. alistaajabu kuona mikono ya binti imebeba kinywaji kikali na cha bei mbaya brand ya Jack Daniel huku kukiwa na glasi tatu kwenye trei iliyoshikiliwa na mikono ya mwanadada yule na hapo akajikuta ameropoka
"vya nani hivi Binti"
"vya kwako........kwani wewe si umepiga simu kutaka huduma na umesema chumba chako ni namba 103 ghorofa ya tatu au siyo hili" naye alitupa swali na kumfanya bwana Thobias Chumvinyingi kugeuka na kutazama kibao kidogo cha mlango kilichoandikwa kwa maandishi meusi yaliyona namba ya chumba husika moyo wake ukapiga paaah!, huku akitafakari ni muda upi ameshika simu, akavunja tena ukimya
" ni sahihi namba ya chumba ndiyo hiyo ila hili la simu hapana mimi simu sijapiga kwakweli utakuwa umekosea chumba sababu mimi niko peke yangu na sijaagiza hiyo pombe kali na glasi tatu, alafu umesahau nimechukua chumba dakika kumi na tano zilizopita na sijafanya mawasiliano kuwa nahitaji chochote, hata kama hoteli yenu ni wakarimu kiasi hiko lakini ulitakiwa kuniletea glasi mbili ya kwangu na yako tukausogeza usiku ila nimestuka kuona glasi tatu huyu mtu wa tatu yuko wapi?"
"hahahaha huyu wa tatu ni rafiki yangu na anatoka sasa hivi zamu ni yule wa mapokezi na ndiyo atanisindikiza nyumbani" aliongea mwanadada yule huku safari hii akichanua mdomo wake huku akiendelea kumsulubisha mwenyeji wake kihisia ila tatizo ni kwamba amegoma kukubaliana na hoja za mwanadada huyo
"hapana kwa sasa nimechoka niache nipumzike kesho tutazungumza mrembo asante kwa ukarimu wako" alisema huku akigeuka kurudi ndani, sekunde hiyo hiyo akakutana na ngumi kavu aliyopigwa karibu na sikio ilimfanya kuhisi nyuki wanalilia sikioni mwake na kama haitoshi alijikuta akipokea ngumi nyingine ya mbavu iliyomfanya abweke kama mbwa aliyepigwa na mwiko huku akijikunja kusikilizia maumivu akataka kukimbia kwani aliona hali inaanza kuwa ngumu na jitu lililoko ndani halina uungwana akalihadaa kama anata kakurusha ngumi kisha akakimbilia mlango ile kuufungua alikutana na teke la kifua lililopigwa kiustadi na mwanadada yule mrembo lililomrudisha ndani na kudakwa hewani huku akishushiwa ngumi tatu nzito za kifua na kumfanya atokwe jasho huku akitamani kutoa machozi mbele ya mwanaume mwenzake ila akajikaza alivyojipapasa kwa siri aligundua bastola yake imedondoka sehemu.
"siku nyingine unapopewa ofa na mwanamke mrembo unatakiwa utekeleze usiulize maswali mengi unamchosha simama ukae tuzungumze au hujampenda rafiki yangu" liliongea jitu lile lililokuwa jeusi na lenye misuli iliyovimba kama mizizi ya mihigo kwa rafudhi ya kirundi iliyofanania na Ile ya watu wanaotoka mkoa wa kigoma, hakuwa na jinsi alijizoa zoa pale chini huku akitafuta upenyo wa kuchomoka mbele ya watu wale kwani aliona maji yamefika shingoni alijikuta Hana ujanja baada yakuguswa na kitu chenye asili ya chuma na chenye ubaridi nakuoneshwa Ishara ya kuketi ambayo aliitekeleza na alitii kana kwamba ni kama mtoto wa chekechea aliyepewa uji wa maziwa shuleni na mpishi huku sharti ni kuupokea uji na kuketi hapohapo na muda huo mwanadada yule alikuwa akikagua nyaraka alizozikuta mezani na upande mwingine Thobias alijilaumu kuwa mzembe ila akagundua uchovu ndiyo tatizo alikuja kugutushwa na sauti ya yule mwanadada iliyokuwa nyororo nalaini
"Thobias Chumvinyingi hili siyo jina la kirundi na hata rafudhi siyo ya huku wewe ni mtanzania na uko burundi kwa siku nne, tuambie umekuja bujumbura kufanya nini? aliuliza mwanadada yule huku akisoma kilichoandikwa kwenye pasi ya kusafiria nakumkazia macho muulizwaji
"mimi ni mfanyabiashara na kesho tutakuwa na mkutano katika hoteli ya Lake Tanganyika hapa hapa katikati ya jiji hili" aliongea huku akimkazia macho mwanadada yule
"muongo mfanyabiashara gani unaingia na silaha zenye usajiliwa nchini kwenu....mkaka mzuri kama kuwa muongo haipendezi" aliongea kwa madaha mwanadada yule huku akiigeuza geuza silaha ile
"kweli nakwambia mimi ni mfanyabiashara na niko hapa kwaajili ya mkutano" alivyomaliza sentensi yake kibao kilishuka kwenye mgongo wake kiasi cha kumfanya ahisi kichefu chefu kama siyo kutapika, ndipo alipojikuta akihusudu mpango wa kapteni jumanne Saidi wa kutumia usafiri wa gari na alikiri kuwa mtandao ule umesheeni watu wengi tena wana nguvu.
"unapoongea na mwanamke mrembo kama huyu yafaa uwe mkweli na muwazi unasikia komredi" lilikoroma lile jitu ambalo sura yake haikuonesha Mara ya mwisho kutabasamu ilikuwa lini huku upara uking'aa kwa mafuta aliyoyapaka, bado tabasamu la mwanadada yule halikwenda likizo na hapo alivunja ukimya.
"mkaka mzuri umechagua njia ya maumivu.......kunywa kidogo hiyo pombe iliyoko kwenye glasi nadhani itakupunguzia maumivu" alisema Tena yule Dada huku safari hii akionesha na mwanya Kabisa.
"Mimi ni mlokole situmiagi vilevi.....ingekuwa juisi saw..." alikatishwa na kibao kikavu alichopigwa shingoni kilichomfanya aanze kuona nyota nyota
"wewe una kichwa kigumu Sana kuelewa si ndiyo na hii ni Mara ya mwisho kukwambia ukirudia ntakutawanisha hichi kichwa.
"nijibu haya maswali na tutakuacha uendelee na starehe ya usingizi......bujumbura umefata nini? na mmetumwa wangapi katika jiji hili? Je wenzako wamefikia wapi?" Yalikuwa ni maswali matatu Mazito yaliyoulizwa na sura ambayo dakika kadhaa ilipambwa na tabasamu na hapo ndipo thobias chumvinyingi aliamini kuwa watu walioko mbele yake ni zaidi ya alivyokuwa anawafikiria na kabla hajajibu swali simu Aina ya iPhone ilipata uhai na kupelekea mwanadada yule kusimamana kusogea pembeni ijapokuwa alikuwa matatizoni ila akilini alikiri kuwa mwanadada yule alibarikiwa na Muumbaji wake hasa mzigo aliorundikiwa nyuma chini ya mgongo, kusimama kwa yule Dada Sasa kulimpa nafasi ya kuweza kutazama pazia lililoziba kioo cha chmba kile na kuweza kutazama uwazi
unaofanya upepo kulitunisha pazia lile na hapo ndipo alipoona hiyo ndiyo nafasi pekee ya kuwatoka watu wale wenye kuonekana ni wauaji wabobevu, alijikuta akiguna tu nakumfanya Dada yule kugeuka huku akiwa amepambwa na tabasamu la kikatili, kengele ya hatari ikalia kichwani mwake na kama nyani alijigeuza kama tairi na kukipiga kikumbo kioo cha dirisha huku mvua ya risasi ikimkosa kosa na alijikuta ametuajuu ya gari na mgongo wake kupata maumivu kiasi cha kutoa tusi la nguoni na sekunde Ile Ile mvua ya risasi iliendelea kumfata na kama mweu alichanganya miguu na kupoteleamitaani
"shit.....amekutorokaje huyu bwege, umekuwa mzembe Sana Bosco unadhani wakuu watatuelewa vipi"
***itaendelea
Uhondo ndiyo kama umeanza kuja na kiu yenu ya simulizi imeanza kukolea swali la kujiuliza Je? Atapona katika mdomo wa simba wenye njaa kali? Ustaadhi wanampeleka wapi? Vipi kuhusu Askofu nini kitamtokea mara tu atakapokutana na mheshimiwa raisi? Ungana nami toleo lijalo
NB: kesho simulizi hii inaweza ikachelewa kupandisha kwa sababu zilizoko nje ya uwezo wangu
 
TUwe wa pole alisema leo itachelewa kidogo ni vyema tutulie hatujui anaemergency gan
 
“WAKATI MWINGINE UKWELI NI MBAYA ZAIDI KULIKO UWONGO” NUKUU NZITO YENYE KUBEBA UJUMBE MZITO KWA WAHUSIKA KWA SABABU SIRI ZA ZAMANI ZINAWEZA KUKUANGUKIA KAMA MVUA……..FUATANA NAMI UPATE KUJUA UNDANI WA NUKUU HII
NB:SIMULIZI HII NI YA KUTUNGA NA WALA HAIHUSIANI NA MATENDO NA WAHUSIKA KATIKA IDARA NA TAASISI TAJWA ILA NI KAZI YA FASIHI YENYE LENGO LA KUBURUDISHA NA KUELIMISHA JAMII HASA LINAPOKUJA SUALA LA UHALIFU,UZALENDO NA MSHIKAMANO KATIKA TAIFA LETU BILA KUSAHAU MCHANGO NA UPENDO WA MAHUMAA KATIKA VYOMBO VYETU………..TUFUATANE PAMOJA KWENYE GIZA HILI KUTAFUTA MWANGA WA KUWAMULIKA WASALITI.
TUSONGE SASA………..
"shit.....amekutorokaje huyu bwege, umekuwa mzembe Sana Bosco unadhani wakuu watatuelewa vipi" alilalama Sana yule mwanadada huku Akionekana kuishiwa pozi kwani ndege wao amewatoka wakati na muda ambalo walishapewa amri yakummaliza mtu yule.
"sikiliza haja nitoroka yule tumbili Bali katutoroka na tembea yako ndiyo ilimpa nafasi.....nimeshtukia tu amekwisha ruka na kujigeuza kama nyani vile, nimekuja kumuona vizuri Mara alipopita na dirisha nikiri tu huyu ni mtu hatari na ili kuyafanya Maisha yake yawe mafupi mtaani tumtengenezee kesi atafutwe na polisi muda huo na sisi tuna mtafuta huku tukitengeneza vuguvugu dogo la chuki dhidi ya nchi yake na ninavyojua tu watamkana hivyo itakuwa nafasi kwetu kumfyeka na maiti yake haito onekana Tena mahali popote unaonaje huo mpango Diane." Lilisema lile jitu huku likisikiliza wazo la mwenzake.
"fanya hivo na tupotee maeneo haya hakikisha huachi nyayo zetu humu" aliongea mwanadada yule huku akipiga funda Zito la pombe Ile kali huku akiendelea kuikagua pasi ya kusafiria huku muda mwingi akiitazama Ile picha.
"nitakupata na nitakufanya ulie huku ukiita mizimu ya kwenu ikusaidie ila hawataweza ntakuua kikatili mpaka shetani akatae kukupokea huko kuzimu ashangae aina ya kifo chako" alijiwazia Diane huku akipiga funda la mwisho na kuitia glasi Ile kwenye mkoba wake Kisha wakaanza kufuta kila sehemu waliyogusa walipomaliza wakafanya kama. walivyopanga na kupotea hayo mazingira.
NGOSOKI POLICE POST@ TADMOR-ARUSHA
saa 7:55 usiku
"wakuu huyu naye vipi" aliuliza Askari aliyekuwa chumba cha mashtaka
"tuna mazungumzo naye kidogo......kiufupi naitwa SSP tumaini kaoneka natoka makao makuu na mwenzangu naye anatoka ofisiya mkurugenzi wa makosa ya jinai na vile vile ni mkaguzi wa jeshi la polisi Dada Saida Thomas na vitambulisho vyetu ni hivi, sijajua kama taarifa za ujio wetu mnazo?" Aliongea kwa sauti kavu na iliyohitaji Majibu kutoka kwa afande yule aliyeonekana ndiye kiongozi wa zamu kituoni pale. Wote waliokuwa kituoni pale walikakamaa huku na kupiga saluti
"tunazo afande na mazingira tulisha yaandaa kwa maelekezo ya afande OC, tuongozane" alisema afande yule huku wakimkokota ustaadh Othman na upande mwingine walimuonea huruma kwani huko ndani atakutana na sura ambazo wao kucheza na kuupa maumivu MakalI mwili wa mwanadamu ndiyo kazi Yao jumlisha na hawa ambalo hawawajui HaKIka waliona huyu mtuhumiwa kayakanyaga🙆🏾‍♂️😂😂😂, aliingizwa kwenye chumba chenye taa Aina ya bulb watts 100 huku kukiwa na sura za kazi tatu na wote walikakamaa na kupiga saluti, bareti za damu ya mzee zilisadifu kuwa wale siyo Askari wa jeshi la polisi Bali makomandoo kutoka jeshi la wananchi wenye vyeo vya koplo, huku mmoja akiwa luteni usu na kiongozi wa wale wawili, kitendo cha kumfikisha alipokelewa na sekunde tano zilitosha kumuacha mtupu luteni kanali Charz alisimama mlangoni huku akiwatazama vijana wanavyomtoa wenge ustaadh Othman kwa kummwagia maji ya baridi yaliyokuwa yamewekwa barafu, baada ya zoezi Hilo wakampandisha kwenye chuma kilichokaa mfano wa goli la mpira kichwa kilikuwa chini huku mikono ikipitishwa katikati ya miguu na Kisha kufungwa kila mkono pingu yake zikiunganishwa na bomba miguu ilifungwa na kamba ngumu huku ikining'inia upande mwingine kukatia kwenye mkunjo wa goti hadi kwenye visigino.
"kwa majina naitwa ulimwengu, nadhani umeshawahi kusikia ule msemo wa wahenga kwamba 'asiyefunzwa na ***** atafunzwa na ulimwengu' Sasa ulimwengu mwenyewe ndiye mimi, ntakufunza Kadri ya majibu yako na nitakuwa mwema Sana ukijibu kwa ufasaha sijui unaitwa Nani mwenzangu. Aliongea kwa sauti ya zege komandoo yule mwenye cheo cha ukoplo huku akijinasibu kwa kujiita'ulimwengu’ na Sasa alikuwa anaenda kumfunza mkaidi aliyeshindwa kufata malezi ya mama yake
" ustaadh Othman omary Kamanda" alijibu kwa haraka huku akiogopa shuluba kutoka kwa pande lile la mtu.
"vyema ukienda hivi wala hutoona Rabsha ya Aina yoyote.......unaweza kutuambia kesho mmepanga kulipua mabomu mangapi? Alimkazia macho huku mikono na miguuyake ikiwa tayari kucheza na viungo vya mtuhumiwa yule endapo angejitia kiburi au nunda.
"mbona mnanichanganya Janani wale wananiuliza alipo Mohamed Mahboob nyie mnaniuliza mabomu Sasa mimi mnaniweka njia pand...." Alikatishwa na Kofi Zito lililopigwa kifuani mwake kiasi cha kujuta kutoa jibu lile.
"niueni tu mimi sijui chochote zaidi ya kufundisha watoto madrasa msikitini basi" alilalama ustaadh Othman ila jicho kali aliloangaliwa na Chiku lilimnyong'onyeza kabisa. Akajua mziki anaocheza biti yake ni ya kwaya na yeye anacheza kwa miondoko ya mahadhi ya muziki wa reggae.
"kufa hufi ila Leo utamuona malaika wa kifo kwa macho yako" aliongea luteni kanali Charz akiwa ameegemea mlango kiupande huku mikono akiwa ameikunja kifuani akiwaangalia vijana wake aliowaacha kozi wanapambania bawa la ndege huku yeye akiwa mkufunzi wao miaka kadhaa iliyopita Sasa amekutana nao wakati yuko kwenye majukumu mazito aliyokabidhiwa na raia namba moja huku akikimbizana na muda.
"Huyu atatuharibia sifa kwa mkuu" alijiwazia luteni usu yule akachukua spoku ya baiskeli, muda huo mtu yule alikuwa analegezwa na yule komandoo mwingine aliyekuwa kimya muda wote na Sasa mikononi mwake alikuwa ameshika kipande cha nondo na kuzigonga sehemu za maungio ya mifupa muda huo huo chiku akaudaka uume wa ustaadh na kwanza kuuchua huku luteni usu yule akiipaka mafuta spoku ile ya baskeli.
"mnataka kunifanyaje kuweni na ubinadamu mimi sijui Majibu ya vitu mnavyoniuliza na hata hayo mabomu mimi sijui yanafanana aje zaidi ya kuona kwenye muvi za wazungu" ustaadh Othman mwenye rafudhi ya watu wa Tanga alilalamika huku akitia huruma usoni kilisikika kibao kikavu kilichotua shavuni mwa ustaadh Othman kilimfanya atake kupiga yowe kama siyo kuzimia kwani maumivu yake hayakuwa na mfano kutoka kwa komandoo aliyejulikana kama ulimwengu, Hali iliyomfurahisha Sana Luteni kanali Charz aliona jinsi mtu wao anavyopata shuruba ya maana.
"ustaadh Othman unakumbuka kauli yangu Kule nyumbani kwako kwamba 'unatafuta kuumia kabla hujaumia' Sasa hapa ndipo utaumia na utapapenda penyewe hahaha......nipe mahali alipo Mohamed mahboob na wenzako wengine na mlipo yatega mabomu hayo"
"kamanda. Mimi mnanionea sijui cho......" Hakusubiri amalizie Chiku alimpiga ngumi kavu ya kifua iliyomfanya atumbue macho huku uume wake ukiwa umesimama baada ya kuchezewa na mikono ya chiku, hapo Sasa alistaajabu luteni usu yule akija mbele na kuukata uume wake,
"unataka kunifanya nini eeennhhh.....kamanda nisamehe......" Alitulizwa na ngumi nzito iliyotua kwenye mbavu yake ya kulia na kumfanya atoe mlio kama wa nguruwe aliyepigwa na jiwe tumboni
"Tulia mpuuzi wewe nikusafishe bomba la mkojo wewe si nunda tutakusulubu mpaka ujibu kwa ufasaha" aliongea akiwa anauingiza waya ule wa tairi la baskeli katika kitundu cha mkojo, ustaadh Othman alipiga kelele nyingi Sana kiasi cha Koo lake kuanza kumsaliti, alihisi maumivu makali Sana muda huo huo alipigwa kibao shavuni kiasi cha kuhisi amepigwa na jiwe wakati akitafakari ni ngumi au jiwe alisikia kitu kama mbao imepitishwa kiulalo katikati ya mdomo wake huku akipe waonyo la kuto kukidondosha.
"ukikidondosha hiko ki mbao hakikisha huoneshi kutokuwepo kwake labda tu unataka kutoa majibu" ilikuwa ni kauli tata Sana kumaanisha hawataki kelele na ikitokea kimedondoka pia hawakuhitaji sauti yake isipokuwa kwa Nia moja tu ya kutoa majibu, muda huo huo ilishuka nondo ya kwenye unyayo kiasicha kuhisi damu yote iko utosini na inataka kupitia hapo, Hakika maumivu yalikuwa makali Sana kiasi cha kumfanya avute hewa kwa shida nafuu aliyoona ni kukiachilia kile ki mbao na muda huo huo ikashuka nondo nyingine kwenye goti akajikuta ametoa ukulele na alipoona wote wana muangalia kwa uchu akaamua kuzima friji lake lisigandishe.
"aaaaaaahhhh nasema......nasema msinipige Jamani mtaniua nasema yote mtakayo hitaji" aliomba huku akitoa machozi huku na jasho likimtililika kwa kasi, jicho lilishabadilika kuwa jekundu na mwili wake ulionekana kuchoka.
"mleteni Mezani.....atujibu maswali yetu muda unakimbia na Arusha mpaka kunakucha tunataka kuikabidhi Salama.
"hiiiiiii sijawahi kumuona gaidi mdhaifu kama wewe unakaza mdomoni huku chini unasimamisha hivi watoto wetu wanapona kweli huko madrasa....." Aliongea chiku huku ukitazama jinsi ustaadh Othman anavyoshushwa, Kisha kuketishwa kwenye kiti huku akitazamwa mbele yake na macho makali ya luteni kanaliCharz.
"nadhani Sasa upo tayari kunipa majina ya washiriki wenzio na wapi mlipoweka mabomu na ni kwanini Ramani ya jiji imekutwa kwako Tena Kuna sehemu umeziwekea x na kwanini unamiliki silaha ya kivita kinyume na sheria na uniambie ni Nani aliyefadhili kulipuliwa kwa kiwanda cha maziwa na ni wapi alipo Mohamed Mahboob, ukiona hayo mengine ni ngumu kuniambia hili la mwisho niambie haraka sana" alisema kwa utulivu luteni kanali Charz.
"Mimi kusema ukweli ni mwalimu wa madrasa na ustaadh na nimekuwa msikitini pale kwa muda mref......." Alikatishwa kwa kugongeshwa kwenye Meza Ile ngumu ya mbao kiasi cha kutoa yowe la hofu.
"hivi wewe unahisi tunataniana si ndiyo unaniletea mambo ya hadithi za sungura na fisi.....luteni chomelea
"naam mkuu hebu mrudishe pale nitasema naye mimi mwenyewe nataka amuone malaika wa kifo kwa macho yake kenge huyu" aliongea Chiku akiwa kakunja ndita urembo wote pembeni.
"Hapana tusifike huko nasema........mabomu yako Sita manne tumeyaweka mjini na Mawili tumeyatawanya nje ya mji ilikusiwe na wakuingia wala wa kutoka, LA kwanza tulipangakuliweka pale uwanja wa mpira, jingine lilitakiwa kuwekwajengo la Samsung ila limebadilishwa na limeshategwa KIA ila sijui ni nyumba gani, moja limetegwa part gallery, jingine limetegwa stendi , jingine muda huu linaenda kutegwa Soweto jirani na ukumbi wa mikutano wa kimataifa (AICC) na moja limeshategwa Monduli na Mohamed mwenyewe, washiriki waku yatega walikuwa Sita mimi kazi yangu ilikuwa ni kuwahifadhi na kuhakikisha zoezi linaenda vizuri baada ya kukaimishwa na Mohamed.
"Hao wategaji ni akina Nani na wametoka wapi? Na Nani mfadhili wa hili jambo" aliuliza Chiku ili kupata uhakika wa taarifa ili kupima uongo na ukweli"
"Mkuu wetu ni Mohamed Mahboob ambaye ni mfanyabiashara jijini hapa na mkoa jirani wa kilimanjaro, mwingine ni mimi ambaye ninasimamia shughuli zote hapa jijini na kwingineko, wa tatu ni Shaban chakupewa huyu ni mwanajeshi wa zamani kikosi' cha mizinga na mwalimu wetu wa mafunzo, wengine ni vijana kutoka tanga na waliletwa na Mohamed mwenyewe.
"hawana majina" aliulizwa na yule koplo aliyemtazama kwa usongo
"nawajua wawili tu ambalo ni ndugu na walilala nyumbani kwangu kwa vile nilikuwa nime shamtanguliza mke wangu na watoto kwa wakwe zangu kwa kisingizio cha watoto kusalimia babu na bibi Yao, hawa vijana wawili wanaitwa Mansoor huyu ni mkubwa na mdogo anaitwa Seif, basi nilipokuwa stendi nilitumia kupeleleza ni wapi ni mahali pazuri pa kutegea bomundipo nilipoona kwenye vibanda vya kuuza sigara na pombe kali ndiyo sahihi kwa maana ule milio wa bomu kuhesabu hawatausikia kwa sababu watakuwa wamelewa au kusizi na lengo kubwa ni kuleta taharuki. :..nisaidieni maji ya kunywa" koplo mmoja alichota maji yaliyokuwa kwenye pipa na kumpatia, yalikuwa Yana chumvi ila aliyafakamia kama ni ya mvua vile.
"tuendelee nadhani maji yamekutosha. "alitia unoko luteni usu yule huku Akitamani aruhusiwe hata amtie makonde hata matatu hivyo Akawa anasubiri itokee hiyo nafasi.
"niambie ni wapi anapatikana Saidi chakupewa"
"hahaha huyu mtu hakuna anayejua makazi yake na inasemekana ni mlinzi wa Siri wa Mohamed na huenda atakuwa ameshaungana naye na kwa muda uliosalia sidhani kama mtayapata yote......hahaha Kuna baadhi ya sehemu arusha kutakuwa na misiba ya kutisha hahaha" alicheka kicheko kilichokuwa na kebehi ndani yake huku mapengo yake matatu ya meno aliyodondosha ya kionekana wazi.
"mabomu manne Kati ya Sita uliyosema tuko nayo na watuhumiwa Saba uliowataja watano ikiwemo wewe tunawashikilia mmoja amefariki hivyo utambue umebakiza swali moja ili ukaungane na wenzio au mwenzio hapo aliona wametoa bastola zao na kuzikoki tayari kwa kumsafirisha mtu akaungane na Ibrahim na yakobo mawinguni aliongea luteni kanali Charz huku uso wake kuwa mbali na mzaha.
"ni wapi alipo Mohamed mahboob kwa Sasa" aliuliza huku akiminya minya viganja vyake vilivyotoa sauti ya kunyooka kwa mfupa
"Mohamed mpaka saa nne alikuwa babati na alinambia atakuwa kwenye nyumba yake ya kulala wageni na kesho alisema ataunganisha kwenda kukutana na mtu handeni Tanga ni hicho tu najua mengine yote anajua Mohamed"
"Mohamed Anayo Familia arusha hii?" aliuliza Tena kwa udadisi luteni kanali huku akimkazia macho.
"aaaahhh hap.....eeennnhhh ndiyo" aliongea kwa kigugumizi ila alivyoona wamemuweka Kati ilibidi akubali.
"wanaishi wapi hao watu?" Aliuliza Chiku
"wanaishi nyumbani kwa Shehe wa mkoa huu" ni jibulililo waacha midomo wazi na Sasa walikuwa katika hitimisho la maongezi Yale
"hiyo nyumba ya wageni inaitwaje?" Aliuliza luteni usu yule mwenye usongo
"MOMA'S lodge" alijibu haraka huku akimtazama Chiku kwaku geuza shingo.
"picha ya huyu mtu naipataje?" Aliuliza komandoo yule mwenye cheo cha luteni usu aliyejulikana kwa Jina moja la chomelea
"hajawahi kupiga picha na hapendi picha ila ninaweza kuwatajia Alivio Maana nilikutana naye safari mbili Mara moja msikitini na Mara moja kwenye kikao cha mwisho hivyo Haiba yake haijanipotea kichwani" aliongea ustaadh Othman kwa utulivu.
"Sawa Asante kwa ushirikiano wako, luteni chomelea huyu na wale watatu walioko Usa River na vielelezo vyao viko vinne, mwili wa mmoja uko hospital ya mount marry jenerali amesema awakute mmewapa chumba kila mtu chake, pale Monduli hakikisheni hawaonani na mtu zaidi yenu na hata uingiaji wenu usifahamike na watu zaidi ya saba Tena wenye utambulisho wa bawa kama nyinyi, kuhusu getini ameshaweka mazingira Sawa na mkifika Usa fanyeni juu chini hiyo Familia nayo iwe Monduli na huyu shehe atatuongoza, vingine siyo Leo na saa mbili asubuhi ya kesho iwakute ofisini kwa jenerali yeye atawapeleka sehemu mkamtoe mtu mapepo ya uharibifu" aliongea kwa sauti ya mamlaka luteni kanali Charz.na kuondoka eneo Hilo huku wakimkabidhi ustaadh Othman kwa makomandoo wale waliomfunga kamba ngumu miguuni na pingu mikononi huku mmoja akimuweka begani kwani mtu wao alikuwa hajiwezi kutembea, wakaaga kituoni hapo tayari kwa safari ya babati usiku huo wa kazi ya Kimnyakua Mohamed mahboob na Shaban chakupewa kama ikiwezekana kama yupo na bosi wao huyo, akatoa taarifa kwa mkuu wa kikosi cha kutegua mabomu kilichopo hapo hapo Monduli kwa ajili ya kutafuta na kutegua mabomu yaliyosalia, na Mara baada yakuwasiliana waliondoka na hata walipofika maeneo ya mzani wa makuyuni walipishana na gari tatu za jeshi zikiwa na wanajeshi Sita Sita bila kusahau uwepo wa mbwa Aina ya Germany shepherd, zikielekea jijini kitu kilichowafanya wajisikie Amani na morali ya kufanya kazi ya babati.
itaendelea*
BABATI INAPATA UGENI SIYO WA HERI BALI WA KUONDOKA NA MTU AMBAYE WANAMUITA UFUNGUO, UNATAKA KUFAHAMU KILICHOJILI TUSOMANE TOLEO LIJALO Tchao
 
“NIKIANGALIA NYUMA YANGU NAONA WINGU ZITO LA GIZA ILA NIKITAZAMA MBELE YANGU NAONA MWANGAZA WA MATUMAINI”……….TUFUATANE ILI TULIKIMBIE GIZA HILI
MUTAMBU-BURUNDI
Saa 8:47usiku
Ni mji ulioko nje ya jiji la Bujumbura kilomita 33.0 Sawa na mwendo wa dakika 45 kwa saa kwa wale waliokuwa na usafiri wa magari, ni mji uliokuwa kimya Sana kiasi kumaanisha wakazi wake wametopea katika usingizi mzito, muda huu alishuka bwana Thobias Chumvinyingi katikati ya mji huu na kutelekeza gari aliloliiba katika nyumba moja iliyokuwa haIkiliwi na mtu katika pori dogo katika mpaka wa kuingia jijini Bujumbura na mji wa Rumonge, Kisha akafungua tenki la mafuta na kuwasha kiberiti cha gesi ambacho kilikuwa kwenye mfuko wa suruali yake ya dengirizi kwani ukiondoa kadi ya Benki aliyoisunda mfuko wa nyuma nyaraka nyingine ikiwemo pasi ya kusafiria ilisahaulika mikononi mwa watu wale waliomvamia usiku alistuka Sana alipojisachi na kukumbuka simu ameisahau juu ya Meza ndogo iliyo jirani na kitanda alichokuwa amelalia katika chumba cha hoteli Ile, baada ya kuiwasha moto gari Ile Aina ya Toyota Mark II aliyoiiba katika moja ya maegesho bubu ya jiji lile la Bujumbura ambayo mlinzi wake alikuwa amelala usingizi wa pono.
Sasa lilikuwa likiteketea kuficha ushahidi wa yeye kuwepo katika mji huo alizipiga hatua ndefu ndefu na Sasa alikuwa Almanza kuziona taa za mji ule lengo lake ilikuwa ni kufika katika nyumba ya siri ya moja ya maafisa waandamizi wa ubalozini hapo aliyekuwa anahusika na jukumu la ulinzi wa ubalozini pale, ilibaki umbali wa mite Mia moja kabla hajaifikia nyumba Ile aliamua kuuvaa uhusika wake kama afisa usalama na jasusi, akazunguka mtaa wa nyuma na kuangalia mazingira yaliompokea kwa utulivu akausogelea ukuta ule na kuukwea na kujivuta hadi juu ambalo alichungulia ndani na kupokelewa na mazingira yalioonekana kutokupewa matunzo kwa muda mrefu. Akajivuta na kutua kama unyoya wa kuku bila kutoa sauti akaanza kunyata kwa kuambaa na ukuta Giza lilimpa faida na lilipozoea macho yake ilikuwa kama aonavyo mchana sekunde ya kwanza ilipita akiwa amebana pale pale, sekunde ya pili alikuwa anacheza na kitasa cha mlango wa kutoka nje kupitia upande ule wa nyuma, akafanikiwa kuingia na kukutana kiza totoro, alipiga hatua ya kwanza kuifata korido akafanikiwa na sekunde iliyofata alitaka kuifata swichi ili kuwasha taa alifanikiwa kuifikia kitendo cha mwanga kujitokeza alipigwa na butwaa kukutana na mdomo wa bastola Aina ya Taurus PT-109 iliwa imefungwa kiwambo, alijikuta anatetemeka na Koo kumkauka, alijilaumu kwa kila kosa analolifanya linamgharimu, alijiona ni binadamu mwenye mkosi kuliko wote,
"wewe ni Nani? na unafanya nini hapa na Nani amekutuma Kuja usiku huu hapa?" sauti nzito na kavu ilivunja ukimya kwa Kiswahili kilichonyooka , hii ilimpa ahueni kidogo kukutana na mtanzania mwenzake
"Mimi ni Thobias Chumvinyingi ni afisa wa ubalozi huu uliolipuliwa na nilikuja hapa kutafta hifadhi" sentensi hiyo ilichakatwa kwa sekunde kadhaa Kisha kikafuatia kitendo cha kustaajabisha kwani mtu yule aliirudisha silaha kiunoni Kisha akamhadaa kwa kumpa mkono ambalo thobias bila kujua akajuani Ishara ya Amani naye akaupeleka sekunde Ile ulidakwa na mikono imara na kuvuta kwa nguvu Kisha akapigwa kichwa kwenye mwamba wa pua kitu kilichomfanya apige yowe la hofu, kabla maumivu hayajapoa alipokea makonde Mawili ya mbavu yaliyomfanya aangaike kuvuta pumzi huku akisikilizia maumivu.
"nyie ndiyo wasaliti tunaowatafuta na Leo utanieleza kila kitu kilichotokea mshenzi wewe nilijua mtakuja huku" alifoka Tena yule mtu kwa gadhabu kama nyati aliyejeruhiwa
"nisikilize ndugu yangu mimi nimefika jijini hapa massa mawili na......" Akataka kufunguka ila akajikatiza na kukumbuka sheria namba moja ya ujasusi kuwa haitakiwi kumuamini mtu yoyote yule hata kivuli chake kwani kinaweza kukukimbia akiwa kwenye matatizo, lakini alishtukia amepigwa Kofi Zito lililomfanya ahisi kichefu chefu na kuona rangi rangi machoni mwake.
"mbona unanipiga Tena ndugu yangu" alilalama mwanaume yule aliyeona ameyakanyaga, akamtazama mtu yule mikononi mwake na kuona Pete inayofanana na Ile aliyomuona nayo Kapteni Jumanne Saidi.
"Leo Utanitajia wasaliti wote Simama juu nyani wewe" alifoka Tena mtu yule na hapo akatoa bastola kiunoni mwake nakuinyoosha usawa wa kichwa cha Thobias huku akimsachi mifukoni katika namna iliyompatia maumivu kila kiganja cha mtu yule kilipopita kwa namna ya kumsachi, alihusudu kuwa yule mtu alikuwa hatari kuliko wale aliowakimbia
"haya nambie watu unao shirikiana nao kulihujumu taifa" alibaki njia panda kujibu kwani bado hakujua yule mtu yuko upande gani, ila alijipa matumaini kwa rafudhi ya mtu yule ambaye hakuiona sura yake vizuri kwani ilifunikwa kwa kofia na barakoa nyeusi ikibakiza macho tu yaliyotoa taswira ya unyama ulioko ndani ya mtu huyu, Kuona hivo ilibidi aulize kitu kuona kama ni mmoja wa mtu aliyeko upande wao.
"siku ya jumamosi kule chuoni Zanzibar maafisa wote watarajiwa walitakiwa kula pilau la kachumbari lililochanganywa na nyama ya Bata mzinga na siku ya kuapishwa tulikula kiapo cha kuwa waaminifu na wazalendo na kulinda Siri za nchi ikiwa ni pamoja kufichua, kutafuta na kuchakata taarifa zinazohatarisha usalama wa nchi iwe ndani au nje ya nchi na kumtii raia namba moja wa nchi yetu" alijaribu kutia kidole kwenye maji kuona kama ni saizi ya miguu yake kuyavuka.
"Hilo ni jambo dogo Sana, hivi hutambui wapo watu wanakula kiapo na bado Kuna wasaliti na umesahau sheria ya kwanza uliyoambiwa siku ya kwanza uliyokuwa mafunzoni, hiyo Mimi naitekeleza kama sheria zingine za nchi na Mungu, tusipotezeane muda kwa hadithi nyepesi wenzako wake wapi? Safari hii alibwata huku akiikandamiza kabisa bastola Ile kichwani.
"wasalimie kuzim....." Alikatishwa na Jina lililotajwa kwa sauti ndogo
"ukikutana na Kapteni Jumanne Saidi mwambie Hali ni mbaya Sana jijini Bujumbura" aliongea kwa kukata Tamaa na sekunde Ile Ile alishangaa bastola imeshushwa chini
"umemfahamu vipi Kapteni jumanne Saidi" hakuwa na huyana zaidi ya kujitambulisha na kumsimulia tangu alivyoanza naye safari jijini Dar es salaam na kuachania katika uwanja wa ndegewa Jomo Kenyata.
"ndugu ni heri kusafiri ukiwa na matumaini kuliko kufika" aliongea hivyo ASP Richard huku Akivua barakoa na kofia, akamsimulia jinsi alivyoutumia usafiri wa gari huku Mara kadhaa akikutana na vizuizi hivyo alifanikiwa kupita kwani nyaraka zake zilionesha akielekea rumonge kupeleka gari hiyo kwa tajiri mmoja hivyo kuepuka kushtukiwa na watu wabaya miongoni mwa Askari waliokuwa kwenye vizuizi.
"tangu umeingia jiji la Bujumbura Kuna kitu gani umegundua" alitupa swali Hilo kuelekea kwa thobias chumvinyingi
"tangu nimefika roho yangu imewindwa na nimeishia kuponea chupuchupu tu" alisema thobias chumvinyingi kwa masikitiko.
BABATI-MANYARA
Saa 9:03 usiku.
wakati watanzania wengine wakiwa wamelala, kuna watu katikavyombo vya ulinzi na usalama walikuwa macho na sasa walikuwa wana muuwinda mtu ambaye ana hatarisha usalama wa nchi na yuko mita kadhaa kutoka wao walipo katika nyumba yake ya kulala wageni.taarifa za uwepo wa mtu huyu zilithibitishwa baada ya kunaswa sura yake na kamera za siri zilizopachikwa na idara ya ujasusi lengo kuu hasa ni kuiweka nchi katika hali ya ushwari kila siku ieandayo kwa mungu, taarifa walizozipata kutoka Arusha ya kuwa wamefanikiwa kuyapata mabomu yale ambayo yalitakiwa Yazuie kesho yake watu kutoka na kuingia ili Yale mengine yakitarajia kuwazika asubuhi Ile wakazi wa jiji lile ule muda punde tu baada ya tamasha kuanza ilikuwa ni kazi iliyotukuka ya The chameleone hasa ukizingatia hakukuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutafuta mtu ambaye atafanya kazi bila kuwa mamluki, neno uaminifu likiwa limepotea kwa watu wa juu kabisa wa vyombo vya ulinzi na usalama kama jenerali wa jeshi, chifu wa idara yaujasusi na hata raisi mwenyewe hakutambui yupi yupo upande wake yupi ni mamluki, sasa walipeana ishara waanze kuingia katika uzio wa nyumba ile ya kulala wageni ulinzi ulikuwa wa kawaida, lakini wakaghairi na kuamua kutumia njia ya kawaida huku silaha zao kiunoni zilikuwa ziko tayari kukohoa na kuondoka na pumzi ya mtu.
" kaka Habari" alimsalimia luteni kanali Charz, mlinzi wa getini
"sogeeni hatua kumi alafu mjieleze nyie ni akina nani na mnataka nini" ulikuwa ni mkwara wa mlinzi aliyekuwa getini.
"tunataka chumba tukapumzike mimi na mume wangu" aliongeakwa sauti nyororo huku akimlalia kifuani luteni charz kitu kilichomfanya mwili kumsisimka kwani joto mwanana la chiku lilitaka kuamsha hisia zake za tangu miaka kadhaa ya ujana wake......akamezea kwani alikuwa na kazi mbele yake ambayo ilitakiwa kukamilishwa kabla ya alfajiri.
"watu wengine bhana mtu unakutana naye barabarani huko humjui umeshajipachika cheo cha mke haya bhana mna bahati Sana kimebakia kimoja tu tatizo sijajua kama mna pesa ya kukichukua" alibwabwaja Tena yule mlinzi huku safari hii akitikisa kiberiti huku akimtazama luteni kanali Charz.
"kwani ni bei gani hiyo ambayo siwezi kuilipa Kisha nikaufurahia usiku na mrembo kama huyu" alizungumza kwaj euri ya pesa luteni kanali Charz
"kimebakia cha laki mbili bosi teeth teeeh" alirudia tena mlinziyule huku akijichekesha kinafiki.
"Sawa tunalipa wapi hapa au mapokezi" aliuliza Tena luteni kanali Charz.
"mapokezi mkuu, Tena ngoja tuongozane ili nikawaoneshe" walifika mapokezi na kumkuta Binti wa makamo akiwa amejiegesha huku akipambana na kero za mbu na baridi
"mamaaaaa......kumbe ni wewe nilidhani nyoka au limdudu " wote waliishia kucheka huku Binti yule akijiweka sawa
"wewe mrembo acha uwoga hehehehe si nikuoe tu nikufundishe ujasiri" alisema mlinzi huku mate ya uchu yakimdondoka baadaya kuona paja la kinyaturu lililokuwa jeupe, kupanda kwa sketi ndiyo kulimnyanyasa kihisia.
"koma mshenzi wewe nakupeleka wapi mtu sura kama unanizomea....hebu acha ujinga wako mimi niwahudumie watu wakajivinjari.....umewaambia kimebakia kimoja na bei yake" aliongea yule Dada huku akiwa amekasirika kutaniwa na mlinziyule ambaye kwa ni ushahidi Tosha kuwa sura yake ilikuwa inatumika kutishia watoto katika mtaa anaokaa ambapo huwenda mtoto amegoma kula, kuoga na hata kulala wakilisikia Jina la Majuto basi hutekeleza kile alichokuwa anagomea kukifanyia utekelezaji.
"upo na mkurugenzi husikii ananukia pesa" alichombeza kipambe mlinzi yule.
"mwaka huu utautafuta uchawa na usipate nyani wewe....achaneni na huyo kaka unaweza kulipia tu, huyo anawalia unit zenu za usingizi Hana lolote ona jisura lake" alibwata Tena yule Dada huku akimnanga mlinzi yule ajulikanaye kama Majuto
"Sina cash ila si hata kwa kadi nalipia?" Alimuuliza Dada yule huku akimtazama machine.
"bila shaka kaka angu mashine hiyo hapo" aliongea yule Dada huku akiweka machine ya kuchanjia kadi. Alipomaliza utaratibu wa malipo ukaja utaratibu wa kusaini ambapo chiku alilivuta daftari lile na Kisha kuandika Jina la JACOB FRANK akaandika taratibu taarifa nyingine huku muda huo luteni kanali Charz akijifanya kumbusu Chiku huku jicho lake kama LA mwewe liki ya peruzi Yale majina ya wageni wa siku hiyo kwa umakini mkubwa, ndiyo aliamua kutumia njia Ile kuwazuga mlinzi na Dada yule wa mapokezi waliofikiri watu wale walikuwa wanajifanya wanapendana Sana takribani dakika tatu zilitosha kupata kile walichokitafuta,Naam kwa namna Mohamed mahboob alivyojifanya kuwahadaa wanausala kwa kujifanya raia mwema hata akiwa hotelini kwake kwa kuandika Jina kama mgeni ndivyo alivyowasogeza karibu na bahati nzuri ni kwamba chumba Chao kilikuwa kwenye mstari wa vymba vilivyokuwa ghorofa ya tatu, jumbo lililo wastaajabishani kutoliona Jina la Shaban Chakupewa, wakati taarifa zinasema ndiye mlinzi wake wa mwisho waliishia kutabasamu na kuanza kuzipanda ngazi kwa pupa, wakakipita chumba kile kilicholaliwa na windo lao, mlango wa pili kutoka kile ndiyo kilikuwa chumba Chao.
"walipoingia ndani ya chumba kile kipana chenye kitanda cha Sita kwa Sita, jokofu dogo lililokuwa na chupa ya mvinyo Brandi ya pearly Bay, juu kulikuwa na feni yenye mapanga boi marefu huku chini kukiwa na zulia jekundu, chumba kilitamanisha kwani kilipambwa kwa mapazia mazito ya rangi ya pinki iliyochanyikana na weupe kwenye baadhi ya michoro katika mapazia Yale, Hakika chumba kiliendana na bei waliyotoa kiufupi hawakupigwa kama wasemavyo vijana wa mjini. Chiku alizima taa punde tu baada ya kufunga mlango, shiiiiiiii ni ishara ambayo luteni kanali charz aliielewa kwani haraka alitoa simu yake na kuiweka upande wa kamera ili kutafuta kamera za Siri kama zimetegwa hotelini humu huku Chiku akitoa combo kinachotambua uwepo wa vinasa sauti, zoezi Lao lilidumu ndani ya dakika tano kwa weledi wa Hali ya juu kuhofia kuharibu mpango, Naam ukafatia muda wa maigizo.
"aaaaaaissshhh mume wangu taratibu baba" ilisikika sauti ya mwanamke kwenye hoteli Ile ya MOMA'S
"hapo hapo mme wangu.....nakojoa nakojoaaa baba sikuachi nimesema sikuachi" alilalama mwanamke kwa sauti huku kelele za kitanda zikiwa nyingi kiasi cha kuwa kero kwa wateja wengine kiasi cha kupiga simu mapokezi kuwasaidia kuondosha kero hiyo mmoja wao akiwa Mohamed mahboob mwenyewe, Dada wa mapokezi alifika na kugonga lahaula! Chumba alichokipiga hodi aligundua ni kile cha wateja waliokichukua dakika kumi na tano zilizopita.
"kaka.......kaka fungua" aliongea Dada wa mapokezi
"Nani wewe unayesumbua starehe za watu......aaahhh kuharibiana tu utamu" muda huo alijifanya anavaa suruali, lakini ukweli ni kwamba hakuwa ametoa chochote aliulegeza mkanda na kifungo cha suruali yake Kisha akaiachia wakati anashuka kitandani Kisha kuidaka kabla haijafika chini na sekunde iliyofata alikuwa mlangoni huku akiweka sura ya kuonekana kana Kwanba kachukizwa na kitu.
"Kuna shida gani wewe Dada unagonga gonga Milango au mmepanga mimi nisiifaidi hela yangu si ndiyo? Aliongea kwa sauti ya kukoroma huku akikunja sura.
"kaka wateja wanalalamika mnawapigia kelele na wao wamepumzika"aliongea yule Binti kwa unyenyekevu.
"kwani Mimi nimewazuia wanawake wao wasipige kelele kama kuna anayechukia aje humu aone kinachofanya apige kelele hehehe"alimalizia kwa kicheko huku akimwangalia yule Dada
"kaka kuwa mstaarabu basi heshimu basi usingizi wa majirani zako" alilalama Tena yule Dada huku akionekana kuanza kuchukia.
"Sema basi na wewe kama unataka tuumalize usiku tukiwa mrembo acha pang'ang'a nyingi eeeennh" alisema hivo huku akiupeleka mkono wake kwenye shavu la yule mhudumu.
"Tena unikome usichukulie kila mtu ni Malaya ohooooo....tutaharibiana Sasa hivi ngojea uone, ms*nge wewe nisubiri hapo nkuletee hela yako alipayuka yule Dada huku akianza kupiga hatua mapokezi kana kwamba amesahau kitu, alivyoishia kwenye ngazi alijitokeza Mohamed kutoka chumbani kwake huku akiwa na bastola kiunoni, akamkuta yule bwana amesimama pale.
"nimekuja kuona hicho kinachopigisha kelele kama ulivyosema bwana mkubwa" aliongea Mohamed akiwa umeuweka uso wakazi, Hakika luteni kanali Charz aliuhusudu uwezo wa the chameleone katika kucheza na kompyuta pamoja na uchoraji wa picha kwani picha waliyotumia ilifanana na mtu aliyesimama mbele Yao, kitu kilichowastaajabisha ni umbile dogo la mtu yule katika picha lakini Sasa lilikuwa mbele ya luteni kanali Charz
"hahahaha dunia Ina mambo kweli nilijua atakuja mkeo ili sinema inoge......umekuja wewe hebu Rudi kamlete mkeo wewe utazame kama filamu hahaha" alisema hivyo kebehi kwa lengola kumpandisha hasira adui yake ili aingie kichwa kichwa.
"kafiri mkubwa wewe ingia ndani nkufundishe adabu unapoongea na wanaume wenzio mzungu wa reli wewe" alifoka huku akifunua Shati na kumuonesha bastola na muda huo huo alimsukuma luteni charz kurudi ndani, alipoingia yeye aliurudishia mlango na kuufunga kabisa ila alivyogeuka alistaajabu kukutana na midomo miwili ya bastola Zilizofungwa viwambo vya kuzia sauti vikimtazama, alitamani ardhi ipasuke aungie alijilaumu kuingia kwenye mtego ule kiwepesi namna Ile
"tupa silaha yako chini na piga magoti weka mikono kichwani" iliongea kitemi sauti ya mwanadada chiku huku Mohamed akiwa Hana namna zaidi ya kutii amri hakuamini kama angekamatwa kama kuku Tena akiwa kwenye nyumbaxaliyojenga mwenyewe, alipigwa take la mgongo na kudondokea kifua huku akipiga yowe la hofu.
"Tulia wewe mshenzi....nkakufunze kuongea na wanaume kwakuwa wewe umeshindwa kunifunza kuongea na wanaume" aliongea luteni kanali Charz huku akimsimamisha na sekunde iliyofata mlango ulipigwa take huku luteni kanali Charz akimpiga kikumbo Mohamed mahbobo na wote walidondoka chini, kuhama Kwao ni kama kulisaidia kwani mvua ya risasi ilichimba pale chini huku mpigaji akiwa amekusudia kuwamaliza wote huku yeye akiingia kwa mtindo wa kuzunguka kama tairi na hata yeye alikoswa na risasi zilizotumwa kwa lengo la kumuondoa shabani chakupewa kutoka kwenye bastola aliyoishika kikamilifu Chiku, muda huo mohamed akapigwa kabali huku akiwekwea bastola kichwani.
"mwambie mwenzio ajisalimishe au nikumwage ubongo" kuna kitu Luteni kanali Charz alijifunza kutoka kwa mohamed.......hofu ya kifo! alijikuta anatabasamu kwani alikwishaujua udhaifu wa mateka wake.
"shebby weka silaha chini......watanimaliza shusha silaha tumesha wahiwa" alipayuka mohamed huku kijasho chembamba kikimtoka wakati huo huo alijitokeza shaban chakupewa akiwa amenyanyua mikono na kuitupa silaha chini wakati chiku anajiandaa kumdhibiti alijitokeza yule mdada wa mapokezi akiwa na mlinzi wa getini na hapo hapo ikawa nafasi ya pekee kwa shaban kutoroka ndani mle, alifanikiwa kipita mlangoni ila akiwa na maumivu makali kwani risasi mbili zilizotumwa pamoja zilimuingia katika mfupa wa bega lake la kushoto, pamoja na maumivu ila alizikwea ngazi kwa uharaka na kupotea eneo lile.
********
"SIMBA WENYE NJAA KALI WALIVAMIA BOMA LA MTEMI NA KUONDOKA NA MTEMI NA MIMI NIMEPATA MAJERAHA NARUDI SAITI KWA AJILI YA KUJIAGUA ILA HAWA WATU NI HATARI SANA MKUU TUSIPOANGALIA WATAIFIKIA MBONI YA JICHO"
itaendelea******
JE NINI KITAJIRI KATIKA TOLEO LIJALO? Usikae mbali na simulizi hii……….MCHANA MWEMA
 
"Katika kivuli cha hekalu, hufichwa mbinu za giza. Wanaovaa mavazi matakatifu mara nyingine ni viongozi wa dhambi, wakijificha nyuma ya imani ili kuendesha mipango yao ya kishetani."……..mmmmhhhh maneno mazito sana haya sina cha kuongeza tusonge nayo
Endelea…………
Ujumbe ulitumwa kwenda kwa mhusika hakusubiri majibu aliivunja laini na simu ile aliidondosha katika bomba la shimo lililojengwa kwaajili ya kuhifadhia maji taka katika kijiji cha Endasaki kilichopo wilaya ya Hanang mkoani manyara kwa usafiri wa pikipiki aliona kurudi Arusha asingetoboa hivyo aliamua kutokomea kijijini humo ili kusikilizia upepo unavyoenda.
Bila kujua ujumbe ule ulisomeka katika kompyuta fulani katika kitengo nyeti na cha siri katika idara ya ujasusi, ndiyo ujumbe ulisomeka katika kompyuta ya 'The chameleone' ambayo aliunganisha mawasiliano ya namba zote zilizokuwa zinawasiliana na mohamed mahboob kusomeka kwake, alipofatilia kuhusu namba ile iliyotumiwa ujumbe hakukuwa na taarifa zozote kumhusu mtumiaji yule na hata pahali ilipo pia ilimwambia inapatikana BOSTON marekani kitu ambacho hakukubaliana nacho.
"CHIFU SAMAHANI KWA USUMBUFU WA SASA HIVI ILA NILIHITAJI UTUME MACHO NA PUA ZIWEZE KUONA NA KUNUSA HARUFU ZA GAIDI MMOJA ALIYEKIMBILIA WILAYA JIRANI" alituma ujumbe huo 'The chameleone' kwani aliunganisha maelezo aliyopewa na Chiku chenye hakika kuna ka harufu kakuufikia ukweli walianza kukanusa na sasa walikuwa na mtu ambaye atawasaidia kumfikia gaidi la kimataifa Mustapha Abd Nur Ahmed, baada ya kutuma taarifa ile akasogea kwenye kochi lililokuwa ofisini mle na kupumzisha mwili na akili tayari kwa kazi ya kesho ambayo hakujua kama itakuwa ngumu zaidi ya siku inayoisha huku ikimuacha katika uchovu wa usingizi
NGOZI-BURUNDI
Saa 10:34 usiku
Gari walilokuwa wamepanda watumishi wa mungu, lilikuwa likichanja mbuga huku likiwa limebakiza mwendo wa kilometa 124 sawa na mwendo wa saa moja na dakika zake hadi kuufikia mji wa bujumbura, watumishi wote walikuwa wamelala isipokuwa Kapteni Jumanne saidi ambaye tangu wamevuka mteremko mkali uitwao K9 na kuingia kabanga kisha kobero na kuingia nchi ya burundi akili na mwili wake vilikuwa timamu kuliko siku zote, ni kweli alichokiwaza ndicho kwani walipokaribia mji wa Muramvya ambao umepakana na mbuga ya taifa ya wanyama iitwayo kibira, dereva alitahamaki kukutana na mawe makubwa yamepangwa barabarani kabla hajachekecha akili aliona watu wanne wakitoka porini huku wakiwa na mapanga na visu mkononi, muda huo huo katika vioo vya pembeni aliona piki piki mbili zikija huku zikiwa na watu wawili huku waliokuwa nyuma wakiwa wameinua bunduki ainaya Riffle huku wakipiga kelele nyingi, kengele ya hatari ililia kichwani mwa Kapteni Jumanne Saidi na kujiandaa kwa chochote kwa sababu aliona usalama ni mdogo katika yale mazingira hivyo akajipa utulivu na punde wavamizi wale wakalifikia gari lao.
"dereva fungua milango tufanye kazi yetu" iliongea sauti nzzito na mbaya kwa rafudhi ya kirundi hakuwa na namna zaidi ya kufungua milango kwani mdomo wa bunduki ile ulikuwa ukimtazama kwa uchu wa kuondoka na pumzi yake
"mnatoka wapi na munaenda wapi" yalikuwa ni maswali kutoka kwa jitu lile lile lililokuwa na kovu baya upande wa juu kidogo wa jicho lake la kushoto huku likiwa na urefu wa inchi 6.7, na kifua kilichotuna mfano wa sokwe., mbali na hivyo mabuti makubwa kama ya kijeshi yalifumgwa vizuri miguuni kwake huku rangi ya ngozi yake na giza vikiwa kama vinataka kufanana kwani alikuwa ni mweusi wa rangi kiasi kwamba wenzie walipenda kumtania 'RANGI YA BUTI' ndiyo, hawakuwa mbali na ukweli kwani weusi wake ulitosha kabisa kumrahisishia kufanya kazi za gizani bila kustukiwa na mtu na macho yake yalikuwa mekundu kwa kuchanganya vilevi vikali pamoja na sigara kubwa(bangi), vinavyomfanya kuwa katili awapo katika mazingira kama hayo.
"aiseeeeee hibonimana njoo uone huku ndani, leo nimekutana na wanafunzi wa yesu wakiwa wote njoo tuangalie petro ni yupi na yuda ni yupi hahahahaha" aliongea kwa kejeli jamaa mmoja aliyeingia na kusimama mlangoni huku akimulika kwa tochi yenye mwanga mkali alioishika mkono wa kushoto na panga refu lenye kumeremeta kwa makali hata likiwa gizani.
"hebu washuke tuwatunzie pesa kwani huko wanapoenda hakuhitajiki pesa, si ulisikia yule mchungaji wa lile kanisa la jeshi la wokovu akisema mchungaji yoyote haitaji pesa kwenda mbinguni, Sasa na sisi tuna wimbo wetu na leo mtauimba hahaha" alisema hivo yule Jamaa aliyetambulika kama hibomana.
"kichana hebu kuwa na hofu ya Mungu hata kidogo kutusimamisha hapa hiyo ni kazi ya shetani na sisi tupo tayari tuombee wewe na mubadilike na muwe watu wema" aliongea mtumishi mmoja aliyeonekana kuwa na umri mkubwa.
"hahaha ni Nani huyo anayeota ndoto za mchana, anasema Mungu na Yesu na sisi ndiyo tumeshikilia Maisha yake, mzee unatakiwa ujiombee nafsi yako huku Burundi hakuna Mungu, Mungu ni sisi tuliopo hapa ndiyo tunaamua uishi au ukacheze na yakobo ukiimba Mungu na yesu." Lilisema jitu jingine ambalo lilikuwa na msitu wa nywele ambazo haijulikani ni lini liliziosha, sura yake iliyoongea neno ukatili, kifua kipana kilichoshiba mazoezi na pua kubwa kama la kiboko huku ikionekana yeye ndiyo anavuta hewa nyingi kuliko wengine.
"imeandikwa atakaye iokoa nafsi yake ataiangamiza na atakaye iangamiza nafsi yake ataiponya" ilikuwa ni sentence iliyotoka kwa kapteni Jumanne Saidi muumini wa dini ya kiislamu lakini alifahamu vyema maandiko ya kiislamu kwenye korani takatifu vile vile biblia watumiayo wa kristo, kingine kilichostaajabisha ni kwamba yule mtu hakuwa mtumishi kama wao ila walikutana naye kwenye gari Mara baada ya kuombwa Sana watumishi wale na dereva wa gari lile na Kisha kuruhusiwa kusafiri nae huku akiomba nguo kama zao ambazo alipewa na mmoja watumishi wale aliyekuwa na asili yakizungu, Mali na Hilo hawakuamini kama mtu yule alikuwa na ujasiri wa kuongea mbele ya majambazi Yale yaliyokuwa yanaonesha ukatili, punde aliingia kijana mmoja ambaye ukimkadiria kuwa na miaka kumi na tano au Sita, mwembamba mrefu, mwili mkakamavu na uso uliokomaa kwa shuruba.
"naskia harufu ya pesa kutoka kwa watu hawa, shukeni wote chini na mpige magoti" aliongea kwa sauti nzito na yenye kukwaruza.kitu kilichotekelezwa na punde walishuhudia mabegi Yao yakisachiwa, walijawa na wasiwasi watumishi wale isipokuwa yeye ambaye hakuwa na begi alikuwa yeye kama yeye kwani hata silaha maelekezo ya chifu yalimuingia vyema kwamba atazikuta huko huko kitu ambacho alikubaliana nacho kwa asilimia zote kwani ni hatari kutembea na silaha. Wakaamrishwa kutoa kila walichonacho na kuamrishwa kuimba wote kwa pamoja huku wakiweka pesa na vitu vya thamani.
"mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe.....mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe" waliimba huku wakihakikisha wameshatoa kila walichokuwa nacho.
"kama Kuna mtu kabakisha chochote atamponza mmoja wenu" liliongea jitu jingine lililokuwa na kipara ambalo lilikuwa na sura kama linataka kucheka na mwili mwembamba ila imara akiwa na kisu kikubwa.
"wewe mzee simama juu nini hiko kimetuna hapo usawa wa tumbo?" Aliuliza yule huku akimkazia macho yule mzee mtumishi aliyejulikana kama James Kyoko.
"Sina kitu ni tumbo langu tu kijana wala usiwe na wasiwasi" alisema mzee Kyoko huku akijitahidi kuficha hofu yake, ndiyo ilikuwa hofu kwasababu kwa sababu wakati wanashuka aliweka pesa kidogo kwenye tumbo lake.na kujifunika kwa kanzu Ile, tukio ambalo lilionwa na yule mwingine akamezea kusubiri muda ufike, na ndiyo ulikuwa wakati wake.
"ndiyeshimana hebu mkague huyu mtu tuone kama ni tumbo la sadaka au Kuna vitu alitakiwa kuvitoa anavyo" lilisema jitu lenye nywele wakati huo kiongozi wao yule akiwa anatazama kila hatua, punde jitu lililojulikana kama Ndiyeshimana liliibukana pesa zilizokuwa katika note za dola Mia Mia ambazo zilikuwa noti kumi na tatu.
"hahahaha mzee wewe si ulisema utaniombea nibadilike na Nina shetani......hahaha hata sisi tunajua maandiko dogo mwambie lile andiko letu kuhusu mtu msema uongo" lilisema lile jitu lenye Jina la Rangi ya buti
"kimelaaniwa kinywa cha mtu kinenacho uongo.....uongo ni dhambi na mshahara wa dhambi ni mauti" aliongea kwa ujasiri yule dogo huku akiwa na uso wa mbuzi huku akimtazama kwa jicho baya mchungaji yule.
"nadhani umesikia kile walichokisoma na huyo bwana mdogo siyo andiko rasmi ila nadhani maneno hayo yako kwenye biblia yenu......kama hayapo mzee wangu sema hapa wote tusikie tujue kwamba pastor 'JOSEPH' alitudanganya jumapili hahahahaa" lilichombeza lile jitu lenye jina la hibomana,mzee hakuwa na la kujibu zaidi ya kutetemeka kwani kilichosemwa ni sahihi kabisa, kisha ikafatia ishara ambayo kapteni Jumanne Saidi alielewa maana yake ila alijipa utulivu kwani watu wale walikuwa wamesha washika pabaya. ikafuatia milio miwili ya risasi ambayo iliuondoa uhai wa yule mzee mtumishi aitwaye kyoko huku wenzie wakimtazama kwa namna ya masikitiko
" hahahaha sijawahi ona watumishi wa mungu wenye tamaa kama huyo kwani angetupa hiko kipesa angepungukiwa nini, wewe dereva wale majirani zenu Tizii si wanasemaga'Tamaa mbele Mauti nyuma' Kalani tumemuonea sisi si tume rahisisha kazi ya Mungu na wewe dereva kwanini unaendesha watu wenye tamaa" aliongea kwa kebehi huku akitema kohozi zito na kulitupa kwenye mwili wa mtumishi James kyoko na muda huo huo akamtazama dereva na kuachia tabasamu, Ndiyo ni tabasamu la kifo na sekunde iliyofata jitu lenye manywele lilishindilia kisu lilichokuwa nacho mkononi na kukizamisha katikati ya mgongo huku mpini ukibaki nje na dereva yule kupiga yowe la hofu huku akipanua mdomo kuitafuta pumzi kwa pupa huku macho yake akiyatumbua ilichukua sekunde kadhaa mtu yule kukaa kimya.
"hahahaha hahahaha mna kilometa 50 mpaka kufika Bujumbura sijui mtalisukuma gari hahahaha" alicheka Sana na muda huo huo walisikia mlio wa risasi mbili zikilitoboa tairi zote za mbele na kuziacha zikiwa 'flat' yani hazina upepo.
"mnaweza kwenda tuwatakie safari njema.....karibuni Burundi hehehehe" alisema yule dogo kwa kebehi na nyodo na wakati anapita karibu na kapteni Jumanne Saidi alimpiga kibao kitu kilichofanya wenzake wacheke Sana huku wakitokomea kwenye mapori Yale.
"watumishi walivuta pumzi nyingi kwani hawakuamini kama wangeachwa na hapo ndipo akili ya kuangalia upande wao wa nyuma ikawaijia katika fikra zao huku maiti mbili zikiwa zime tambarajika chini huku zote zikiwa kwenye dimbwi la damu, wakashauriana wakati wengine wanashughulika kuchimba Mashimo kwa ajili ya kuiziika miili Ile wengine wanahangaika kutafuta suluhisho la matairi ya gari lile kwani kulishaanza kupambazuka, kazi ya kuyaweka matairi alipewa kapteni humane Saidi ambaye aliifanya kwa haraka Sana na Kisha kuwasaidia wenzie kwani alikuwa anawahi miadi na mwenzake aliyekwisha kutangulia kwani hakujua maswahibu yaliyomkuta. Vote vilifanyika kwa uharaka mkubwa na gari kupigwa moto dakika kumi na tano mbele walikuwa wakilichungulia maghorofa ya jiji la Bujumbura, kilometa moja kabla ya kuingia jijini walikutana na kizuizi cha Askari wa jeshi waliokuwa nadhifu kwenye mavazi Yao nadhifu ya mabaka mabaka na bareti nyekundu huku silaha Aina ya SMG zikiwa zimekamatwa vema na mikono Yao imara, wakapewa Ishara yakusimama na kuweka gari pembeni
Askari wawili wakalizunguka gari huku wakionekana kuwa kwenye msako wa kitu au vitu Fulani kwani walikuwa making kuliko kawaida na Hilo alilisoma kapteni humane Saidi, na fikrazake kumtongoza kuwa huenda Kuna jambo kwenye nchi hii iko rehani isiyoisha milio ya risasi kila kukicha.
"Habari yako komredi" alisalimia kapteni Jumanne aliyekuwa nyuma ya usukani huku akitumia rafudhi ya kikenya.
"Nani komredi wako........mko wangapi kwenye hiki kiberiti?" Aliongea kwa udadisi na sauti kali
"kwa gari tuko watu nane kiongozi" alisema kwa unyenyekevu na rafudhi Ile Ile ya kikenya, yule Askari alichungulia katika namna ya kuwahesabu
"mnatoka wapi na mnaenda wapi?" Maswali mawili yaliyoulizwa kitemi yaliwasogeza wale Askari, jeshi waliokuwa wamesimama wakaanza kusogea huku wakijigawa mmoja akipita kulia mwingine kushoto.
"tunatoka Kenya kaunti ya Machakos tunaelekea Bujumbura kwenye mkutano wa injili, wenzetu wameshatangulia na tu mebakia sisi kiongozi" aliendelea kuongea kistaarabu kapteni humane.
"tuone passport isije mkawa mmepita kimagendo" baada yaAmari yule kusema hivo walitoa passport kula mtu na Askari wale waliwakagua kikamilifu.
"mbona hawana Mizigo hawa watu" alisikika Askari mmojaaliyekuwa anafanya ukaguzi huku swali lilimlenga aliyekuwa amekaa nyuma ya usukani.
"mizigo ilikuwepo kiongozi ila tatizo tumeporwa hapo nyuma......Muramvya na wakora" aliongea Tena kwa ujasirika pteni humane.
"mnaporwa vipi wakati mko wanawaume wengi......anyway karibuni Burundi hahahahaha"alisema kiongozi yule hukuakimaliza na kicheko cha dhihaka huku akionekana kutokuwa najuno moja la upande wa juu kushoto kiasi cha kufanya lionekanekama pengo, gari ikapigwa Gia tamari kulilaki jiji la Bujumbura na dakika tano mbele walikuwa katika hoteli ya Lake Tanganyika aliegesha gari katika maegesho huku wa tumishiwale wakimshukuru kwa msaada mkubwa aliyowapa.
"kijana ningependa tuonane keshokutwa kama utakuwepo hapa Bujumbura" alisema yule mtumishi mwenye asili ya kizungu. Bila kuchelewa alitafuta usafiri utakao mfikisha katika mgahawawa Belvedere uliopo mji wa Gatumba, alipata usafiri wadala dala ambao ungemfikisha katika ule mji dakika kadhaa Hali ya utulivu ilimpokea na hapo ilikwisha timia muda wa saa 12 za asubuhi.
*******
Asubuhi hii ilikucha kwa matukio makubwa, huku Vishwa vyaHabari vya magazeti vya Tanzania vikiwa vimepambwa na Habari moto moto kuwahusu watu wanaofanya kazi vyombovya ulinzi na usalama. Ndiyo Habari iliyokuwa kwenye kichwakilichokolezwa kwa maandishi meusi kilisomeka 'UTATA WA KIFO CHA IGP NINI KIMEJIFICHA NYUMA YA PAZIA?' nikichwa cha Habari kilichofanya gazeti la 'HOMA YA JIJI' Habari hii iliwavutaa watanzania na kuhoji undani wa taarifa hii.
"Kila siku matukio tu, hii nchi inaenda wapi kama IGP anakufakifo cha utata na analindwa na ulinzi wa kutosha je sisitunaolindwa na mbwa tuko Salama kweli? Aloongea mzee mmoja huku akiangalia maelezo ya mwandishi ambayehakuweka Jina lake bayana na kuishia kuandika Jina la mwandishi wetu.
"hakuna jipya watakuwa wamezurumiana tu hawa, au kayakanyaga serikali imeamua kumnyamazisha" aliongeamwananchi mwingine
"ila jeshi la polisi chini ya huyu mzee lilikuwa limepwaya Sana rushwa na dawa za kulevya zilikuwa kweupe, utekaji ndiyousiseme ukija kwenye suala la utekaji ndiyo kabisa kikubwatumuombee apumzike aendako huenda Mungu amesaidiakumuondoa." Aliongea kijana mmoja aliyeonekana kuwamaking kupitia Vichwa vingine vya magazeti.
"eebhana eeeennnhhh kumbe Kuna mauaji mengine nyumbani kwa Askofu wa kabisa la JEHOVAH AMESHINDA na yeyemwenyewe Askofu hajulikani alipo, nini kinaendelea" alizungumza yule kijana Tena.
**itaendelea
Je? Ni nani huyu aliyenza kumjadiki habari hizi asiwe ba uhusiano wao yote utayabata katika toleo lijalo
 
Back
Top Bottom