Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #121
SEHEMU YA 95
anaandika hayo na jibu alilotoa akisema, “Sultani atapata amani. Itakuwa ni amani ya milele. Nitawaonyesha Wagogo, Wajerumani ni watu wa aina gani.”
Ndipo, kwa maelezo yake mwenyewe alipoanza kutekeleza mpango wa kuteketeza na kuiteka sehemu hiyo, “Nilisonga mbele dhidi ya kijiji cha mwanzo. Wagogo walijaribu kujilinda, lakini baada ya wengi wao kupigwa risasi walitimka ovyo kupitia lango la kusini. Kijiji kikawa mikononi mwetu.”
“Teka nyara kijijini humo, choma nyumba zote, vunjavunja kila kitu ambacho hakikuweza kuungua… walijitahidi kukimbiza mifugo yao lakini tuliweza kupora ng’ombe mia mbili au tatu, huku tukiwapiga wale waliokimbia. Bunduki yangu ilikuwa ya moto sana kutokana na kupiga risasi kila mara hata ikawa shida kuishika.”
“Asubuhi yake zilipokelewa ripoti za kuuawa zaidi ya watu hamsini. Makenge akaomba tena amani. Peters alijibu, “Mwambie kuwa sitaki amani naye. Wagogo ni waongo, lazima waangamizwe kabisa duniani. Lakini ikiwa Sultani atataka kuwa mtumwa wa Wajerumani hapo tena yeye na watu wake wataweza kuishi.” Baada ya maneno hayo aliomba na kupewa ushuru wa ng’ombe dume, kondoo, mbuzi, maziwa na asali. Kisha akaahidi kuwapelekea bendera ya Ujerumani.
Unyama huo wa Peters ulifanyika pia Mpwapwa na sehemu nyingine ambako Chifu mmoja aliyeitwa ‘Muniama,’ Chifu wa Kigogo wa Kogollo, aliwaua wapagazi wake wawili. Peters alihakikisha anamuua yeye na watu wake na kuteka silaha zake ikiwemo bunduki aina ya mauser.
Lakini utawala wa Wajerumani Dodoma ulikuwa na sura tofauti. Wakati wa ujenzi wa reli, june 2, 1910 ilipotolewa amri ya kuchukua eno fulani la ardhi kwa ajili ya kupisha
majengo ya serikali watu mbalimbali waliokuwa na majengo na mashamba katika eneo husika walilipwa fidia. Miongoni mwao ni bwana Ndogwe aliyelipwa fidia ya rupia 27. Bwana mwingine aliyeitwa masala alipokea rupia 15. Kweche na Kihale kila mmoja alilipwa rupia kumi.
“Wajerumani pia walianza mchakato wa kuhamisha makao makuu ya Tanganyika hapa Dodoma tangu wakati ule,” alieleza mzee huyo kwa sauti ya majigambo.
Aliutaja mwaka 1921 kuwa ulikuwa na mengi yaliyofanyika kwa ajili ya azma hiyo ambayo haikupata kuwa baada ya himaya ya Mjerumani kutimuliwa nchini.
Kwangu, maelezo hayo lilikuwa somo kubwa la kisheria. Somo ambalo si rahisi kulipata toka katika kumbukumbu za mtu mmoja. Hivyo, nilimtazama mzee huyo na kumuuliza, “Wewe ni mwalimu?”
Alicheka kabla hajasema, “Hapana. Mengine nimeyaona kwa macho yangu, mengine nimesimuliwa na baba na babu yangu. Yaliyobakia nayasoma katika vitabu. Nakuhakikishia mwanangu ipo siku na haiko mbali sana utukufu wa Idodomya utakumbukwa na mji utakuwa na kustawi kuliko unavyoona leo.
haukutofautiana sana na ule wa Dar es Salaam hadi Morogoro. Hata hivyo, ilikuwa safari ndefu na ngumu zaidi. Barabara haikuaminika sana, katika sehemu nyingi ilitulazimu kupita kwa uangalifu mkubwa kutokana na makorongo yaliyotafuna nusu ya barabara na madaraja mabovu ya hapa na pale.
Toka Dodoma kuja Kondoa ilitulazimu kupita kwa uangalifu mkubwa kutokana na makorongo yaliyotafuna nusu ya barabara na madaraja mabovu ya hapa na pale.
Toka Dodoma hadi Kondoa ilitulazimu kubadili mwelekeo. Badala ya kuelekea Magharibi kama tulivyofanya toka Dar es Salaam sasa tulielekea Kaskazini. Tulipita vijiji mbalimbali ambavyo sikuweza kushika majina yake yote isipokuwa Melamela, Babaiyo Nafakwa. Hapo tukavuka Mto Mbu na kuingia kwa Mtoro, eneo lenye maajabu yake.
Kwa Mtoro lilikuwa eneo kame zaidi. Ardhi yake ilitawaliwa na mchanga mwingi. Ungeweza kumwona mtu aliye umbali wa kilometa hadi tatu bila kuhitaji darubini wala jitihada za ziada. Kwa mtazamo wa harakaharaka ungeweza kudhani kuwa eneo hilo lisingeweza kuwa na watu. Lakini watu walikuwepo. Nyumba moja mbili, aina ya tembe, zilionekana hapa na pale, wenyeji wake wakionekana kwa nadra sana. Na kila aliyetokea alionekana nusu mtupu kwa mavazi duni waliyovaa. Aidha, karibu kila mmoja alionekana kupauka kwa vumbi na jua kali. Hilo halikupata kunishangaza sana. Kwani sikuwa nimepata kuona dalili ya maji ya kisima wala bwawa katika umbali mrefu wa safari yetu. Hata kile kilichoitwa mto mara nyingi yalielekea kuwa makorongo tu, ambayo hupata maji kwa vipindi vifupi vya mvua kabla hayajakauka tena.
“Wanaishije watu upande huu wa dunia?” alihoji Mary Leakey akitazama huku na huko.
“Wanayo namna yao ya kuishi,” mumewe alijibu. Jibu ambalo lilithibitika pale tulipofika mahala na kukuta watu wawili wakichimba katika mkondo wa mto mmoja uliokauka
anaandika hayo na jibu alilotoa akisema, “Sultani atapata amani. Itakuwa ni amani ya milele. Nitawaonyesha Wagogo, Wajerumani ni watu wa aina gani.”
Ndipo, kwa maelezo yake mwenyewe alipoanza kutekeleza mpango wa kuteketeza na kuiteka sehemu hiyo, “Nilisonga mbele dhidi ya kijiji cha mwanzo. Wagogo walijaribu kujilinda, lakini baada ya wengi wao kupigwa risasi walitimka ovyo kupitia lango la kusini. Kijiji kikawa mikononi mwetu.”
“Teka nyara kijijini humo, choma nyumba zote, vunjavunja kila kitu ambacho hakikuweza kuungua… walijitahidi kukimbiza mifugo yao lakini tuliweza kupora ng’ombe mia mbili au tatu, huku tukiwapiga wale waliokimbia. Bunduki yangu ilikuwa ya moto sana kutokana na kupiga risasi kila mara hata ikawa shida kuishika.”
“Asubuhi yake zilipokelewa ripoti za kuuawa zaidi ya watu hamsini. Makenge akaomba tena amani. Peters alijibu, “Mwambie kuwa sitaki amani naye. Wagogo ni waongo, lazima waangamizwe kabisa duniani. Lakini ikiwa Sultani atataka kuwa mtumwa wa Wajerumani hapo tena yeye na watu wake wataweza kuishi.” Baada ya maneno hayo aliomba na kupewa ushuru wa ng’ombe dume, kondoo, mbuzi, maziwa na asali. Kisha akaahidi kuwapelekea bendera ya Ujerumani.
Unyama huo wa Peters ulifanyika pia Mpwapwa na sehemu nyingine ambako Chifu mmoja aliyeitwa ‘Muniama,’ Chifu wa Kigogo wa Kogollo, aliwaua wapagazi wake wawili. Peters alihakikisha anamuua yeye na watu wake na kuteka silaha zake ikiwemo bunduki aina ya mauser.
Lakini utawala wa Wajerumani Dodoma ulikuwa na sura tofauti. Wakati wa ujenzi wa reli, june 2, 1910 ilipotolewa amri ya kuchukua eno fulani la ardhi kwa ajili ya kupisha
majengo ya serikali watu mbalimbali waliokuwa na majengo na mashamba katika eneo husika walilipwa fidia. Miongoni mwao ni bwana Ndogwe aliyelipwa fidia ya rupia 27. Bwana mwingine aliyeitwa masala alipokea rupia 15. Kweche na Kihale kila mmoja alilipwa rupia kumi.
“Wajerumani pia walianza mchakato wa kuhamisha makao makuu ya Tanganyika hapa Dodoma tangu wakati ule,” alieleza mzee huyo kwa sauti ya majigambo.
Aliutaja mwaka 1921 kuwa ulikuwa na mengi yaliyofanyika kwa ajili ya azma hiyo ambayo haikupata kuwa baada ya himaya ya Mjerumani kutimuliwa nchini.
Kwangu, maelezo hayo lilikuwa somo kubwa la kisheria. Somo ambalo si rahisi kulipata toka katika kumbukumbu za mtu mmoja. Hivyo, nilimtazama mzee huyo na kumuuliza, “Wewe ni mwalimu?”
Alicheka kabla hajasema, “Hapana. Mengine nimeyaona kwa macho yangu, mengine nimesimuliwa na baba na babu yangu. Yaliyobakia nayasoma katika vitabu. Nakuhakikishia mwanangu ipo siku na haiko mbali sana utukufu wa Idodomya utakumbukwa na mji utakuwa na kustawi kuliko unavyoona leo.
* | * | * | ||||
| Umbali | wa | safari | toka | Dodoma | hadi | Kondoa |
Toka Dodoma kuja Kondoa ilitulazimu kupita kwa uangalifu mkubwa kutokana na makorongo yaliyotafuna nusu ya barabara na madaraja mabovu ya hapa na pale.
Toka Dodoma hadi Kondoa ilitulazimu kubadili mwelekeo. Badala ya kuelekea Magharibi kama tulivyofanya toka Dar es Salaam sasa tulielekea Kaskazini. Tulipita vijiji mbalimbali ambavyo sikuweza kushika majina yake yote isipokuwa Melamela, Babaiyo Nafakwa. Hapo tukavuka Mto Mbu na kuingia kwa Mtoro, eneo lenye maajabu yake.
Kwa Mtoro lilikuwa eneo kame zaidi. Ardhi yake ilitawaliwa na mchanga mwingi. Ungeweza kumwona mtu aliye umbali wa kilometa hadi tatu bila kuhitaji darubini wala jitihada za ziada. Kwa mtazamo wa harakaharaka ungeweza kudhani kuwa eneo hilo lisingeweza kuwa na watu. Lakini watu walikuwepo. Nyumba moja mbili, aina ya tembe, zilionekana hapa na pale, wenyeji wake wakionekana kwa nadra sana. Na kila aliyetokea alionekana nusu mtupu kwa mavazi duni waliyovaa. Aidha, karibu kila mmoja alionekana kupauka kwa vumbi na jua kali. Hilo halikupata kunishangaza sana. Kwani sikuwa nimepata kuona dalili ya maji ya kisima wala bwawa katika umbali mrefu wa safari yetu. Hata kile kilichoitwa mto mara nyingi yalielekea kuwa makorongo tu, ambayo hupata maji kwa vipindi vifupi vya mvua kabla hayajakauka tena.
“Wanaishije watu upande huu wa dunia?” alihoji Mary Leakey akitazama huku na huko.
“Wanayo namna yao ya kuishi,” mumewe alijibu. Jibu ambalo lilithibitika pale tulipofika mahala na kukuta watu wawili wakichimba katika mkondo wa mto mmoja uliokauka