Simulizi ya Kijasusi: Kiguu Na Njia

Simulizi ya Kijasusi: Kiguu Na Njia

SEHEMU YA 95

anaandika hayo na jibu alilotoa akisema, “Sultani atapata amani. Itakuwa ni amani ya milele. Nitawaonyesha Wagogo, Wajerumani ni watu wa aina gani.”
Ndipo, kwa maelezo yake mwenyewe alipoanza kutekeleza mpango wa kuteketeza na kuiteka sehemu hiyo, “Nilisonga mbele dhidi ya kijiji cha mwanzo. Wagogo walijaribu kujilinda, lakini baada ya wengi wao kupigwa risasi walitimka ovyo kupitia lango la kusini. Kijiji kikawa mikononi mwetu.”
“Teka nyara kijijini humo, choma nyumba zote, vunjavunja kila kitu ambacho hakikuweza kuungua… walijitahidi kukimbiza mifugo yao lakini tuliweza kupora ng’ombe mia mbili au tatu, huku tukiwapiga wale waliokimbia. Bunduki yangu ilikuwa ya moto sana kutokana na kupiga risasi kila mara hata ikawa shida kuishika.”
“Asubuhi yake zilipokelewa ripoti za kuuawa zaidi ya watu hamsini. Makenge akaomba tena amani. Peters alijibu, “Mwambie kuwa sitaki amani naye. Wagogo ni waongo, lazima waangamizwe kabisa duniani. Lakini ikiwa Sultani atataka kuwa mtumwa wa Wajerumani hapo tena yeye na watu wake wataweza kuishi.” Baada ya maneno hayo aliomba na kupewa ushuru wa ng’ombe dume, kondoo, mbuzi, maziwa na asali. Kisha akaahidi kuwapelekea bendera ya Ujerumani.
Unyama huo wa Peters ulifanyika pia Mpwapwa na sehemu nyingine ambako Chifu mmoja aliyeitwa ‘Muniama,’ Chifu wa Kigogo wa Kogollo, aliwaua wapagazi wake wawili. Peters alihakikisha anamuua yeye na watu wake na kuteka silaha zake ikiwemo bunduki aina ya mauser.
Lakini utawala wa Wajerumani Dodoma ulikuwa na sura tofauti. Wakati wa ujenzi wa reli, june 2, 1910 ilipotolewa amri ya kuchukua eno fulani la ardhi kwa ajili ya kupisha



majengo ya serikali watu mbalimbali waliokuwa na majengo na mashamba katika eneo husika walilipwa fidia. Miongoni mwao ni bwana Ndogwe aliyelipwa fidia ya rupia 27. Bwana mwingine aliyeitwa masala alipokea rupia 15. Kweche na Kihale kila mmoja alilipwa rupia kumi.
“Wajerumani pia walianza mchakato wa kuhamisha makao makuu ya Tanganyika hapa Dodoma tangu wakati ule,” alieleza mzee huyo kwa sauti ya majigambo.
Aliutaja mwaka 1921 kuwa ulikuwa na mengi yaliyofanyika kwa ajili ya azma hiyo ambayo haikupata kuwa baada ya himaya ya Mjerumani kutimuliwa nchini.
Kwangu, maelezo hayo lilikuwa somo kubwa la kisheria. Somo ambalo si rahisi kulipata toka katika kumbukumbu za mtu mmoja. Hivyo, nilimtazama mzee huyo na kumuuliza, “Wewe ni mwalimu?”
Alicheka kabla hajasema, “Hapana. Mengine nimeyaona kwa macho yangu, mengine nimesimuliwa na baba na babu yangu. Yaliyobakia nayasoma katika vitabu. Nakuhakikishia mwanangu ipo siku na haiko mbali sana utukufu wa Idodomya utakumbukwa na mji utakuwa na kustawi kuliko unavyoona leo.

*​
*​
*
UmbaliwasafaritokaDodomahadiKondoa
haukutofautiana sana na ule wa Dar es Salaam hadi Morogoro. Hata hivyo, ilikuwa safari ndefu na ngumu zaidi. Barabara haikuaminika sana, katika sehemu nyingi ilitulazimu kupita kwa uangalifu mkubwa kutokana na makorongo yaliyotafuna nusu ya barabara na madaraja mabovu ya hapa na pale.



Toka Dodoma kuja Kondoa ilitulazimu kupita kwa uangalifu mkubwa kutokana na makorongo yaliyotafuna nusu ya barabara na madaraja mabovu ya hapa na pale.
Toka Dodoma hadi Kondoa ilitulazimu kubadili mwelekeo. Badala ya kuelekea Magharibi kama tulivyofanya toka Dar es Salaam sasa tulielekea Kaskazini. Tulipita vijiji mbalimbali ambavyo sikuweza kushika majina yake yote isipokuwa Melamela, Babaiyo Nafakwa. Hapo tukavuka Mto Mbu na kuingia kwa Mtoro, eneo lenye maajabu yake.
Kwa Mtoro lilikuwa eneo kame zaidi. Ardhi yake ilitawaliwa na mchanga mwingi. Ungeweza kumwona mtu aliye umbali wa kilometa hadi tatu bila kuhitaji darubini wala jitihada za ziada. Kwa mtazamo wa harakaharaka ungeweza kudhani kuwa eneo hilo lisingeweza kuwa na watu. Lakini watu walikuwepo. Nyumba moja mbili, aina ya tembe, zilionekana hapa na pale, wenyeji wake wakionekana kwa nadra sana. Na kila aliyetokea alionekana nusu mtupu kwa mavazi duni waliyovaa. Aidha, karibu kila mmoja alionekana kupauka kwa vumbi na jua kali. Hilo halikupata kunishangaza sana. Kwani sikuwa nimepata kuona dalili ya maji ya kisima wala bwawa katika umbali mrefu wa safari yetu. Hata kile kilichoitwa mto mara nyingi yalielekea kuwa makorongo tu, ambayo hupata maji kwa vipindi vifupi vya mvua kabla hayajakauka tena.
“Wanaishije watu upande huu wa dunia?” alihoji Mary Leakey akitazama huku na huko.
“Wanayo namna yao ya kuishi,” mumewe alijibu. Jibu ambalo lilithibitika pale tulipofika mahala na kukuta watu wawili wakichimba katika mkondo wa mto mmoja uliokauka
 
SEHEMU YA 96

ili kupata maji kwa matumizi yao na mifugo yao “Unaona?” Leakey alimwonyesha mkewe.
Tulisimamisha gari, nikashuka ili kuwauliza jambo. Ni hapo nilipokutana na mwujiza wangu wa kwanza katika eneo hilo. Watu hao, wakiwa weupe zaidi ya weupe wa kawaida kwa Mwafrika walisimama na kunitazama kwa mshangao. Kila dalili ikionyesha kuwa hawakuelewa lugha yangu.
“Nawasalimu, hamjambo?” Nilirudia tena. Nilipoona bado hawanielewi nilirudia salamu hizo kwa lugha ya Kigogo ‘mbukwenyi’ niliwaona wakitabasamu, dalili ya kuelewa. Kazi ilikuwa pale mmoja wao aliponijibu. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuisikia lugha kama ile. Kwanza nilihisi kuwa anaondoa kitu mdomoni mwake kwa ulimi pale alipobandika ulimi wake kwenye fizi na kutoa sauti mnato.
Aliporudia tena, na baadaye kupokewa na mwenzake kwa namna ileile ndipo nikabaini kuwa wanajaribu kuniambia kitu kwa lugha yao, ambayo nadhani haiyandikiki kwa herufi hizi za kizungu tunazotumia.
Wasandawe! Nikakumbuka. Kwa kiasi fulani nililinganisha lugha yao hiyo na ile ya Wamang’ati au Wandorobo ambao si Wabantu. Sikuwa na la kufanya zaidi ya kugeuka na kurejea kwenye gari, tukaendelea na safari.
Dalili za neema katika ardhi hiyo zilianza kujitokeza pale tulipofika mji wa Kondoa. Ulikuwa mji mdogo lakini watu wengi na pilikapilika nyingi kuliko nilivyotegemea. Kulikuwa na nyumba ya wageni, maduka mawili ya Waarabu na kituo kidogo cha afya. Hii ilikuwa nchi ya Warangi, ambao ni Wabantu zaidi. Aidha, wengi wao walizungumza Kiswahili



kwa ufasaha, lafudhi ya Kiarabu ikiwa imetamalaki katika matamshi yao. Dini ya Kiislam pia ilijikita zaidi, kwani hata kabla hatujatulia tulilakiwa na sauti ya ‘wahadhini’ ambao walikuwa wakiwakumbusha waumini kwenda msikitini kwa sala ya jioni.
Tulipata nyumba tukapumzika. Kesho yake pia tuliamua kupumzika. Leakey aliandaa ratiba ya pilikapilika zake za safari, mimi nilivinjari katika mitaa na vitongoji vya Kondoa. Fursa ambayo iliniwezesha kuona na kujua mengi juu ya mji huo. Kwa mfano niliweza kubaini kuwa kihistoria haukuwa mji mdogo kama unavyofikiriwa. Ulikuwa na sehemu yake, kubwa tu katika kurasa za kihistoria ya vita kuu zilizohusisha Tanganyika.
Kondoa ni mji mdogo lakini una mengi ya kusisimua. Kinyume na Dodoma, Kondoa ilikuwa na sehemu yake katika historia ya vita kuu. Pale wakazi wa eneo hilo walionja makali ya vita hivyo kuliko wale wa Dodoma, jambo lililofanya Wajerumani waiweke Kondoa katika hifadhi ya kumbukumbu zao za matukio muhimu ya vita ile.
Kiutamaduni Kondoa pia ina nafasi ya pekee. Wakati wakazi wa Dodoma wakisubiri maji kwa msimu Kondoa wao mizimu ya babu zao iliwazawadia maji ya kudumu yanayotoka hadi hivi leo.
Ntomoko ni jina la mlima wenye chemchem ya maji safi yanayotoka kwenye jiwe kubwa lililoko kwenye mlima huo. Mlima huo ni mkali na uhitaji ushujaa mkubwa kuupanda. Kuna maelezo kuwa jina hilo la Ntomoko, kama ilivyo ‘Idyodoma’ lilitokana na mapigano kati ya Warangi na Wamasai. Kwamba





Wamasai walikuwa wakivizia mara kwa mara na kuwaibia Warangi ng’ombe. Hali hiyo iliwachosha Warangi ambao waliishi juu zaidi ya kilima hicho. Hivyo siku moja walizingira kilima chote na kuanza kuwashambulia Wamasai kwa mikuki na mishale. Wamasai wakawa wakikimbia kwa kujirusha katika kichaka kilichokuwa na miti mingi bila kujua kuwa pale kulikuwa na chemchem. Kila aliyejirusha hapo alididimia na kufa. Warangi walipoona hali hiyo ndipo wakaliita eneo hilo ‘Ntomoko’ kwa maana ya mahala ambapo watu hutokomea.

Baadaye Wamasai walilifanya eneo hilo mahala pa tambiko kwa kuwakumbuka wahanga waliotokomea katika eneo hilo. Inadaiwa kuwa tambiko hilo liliambatana na kumpeleka ng’ombe aliye hai na kumfungia. Wanaporudi baadaye hukuta ng’ombe huyo kachinjwa na kuchunwa. Nusu ya nyama hiyo waliila nusu wakiiacha hapo kwa ajili ya mizimu.

Awali, kabla ya kuhusishwa na teknolojia ya kisasa katika chanzo hicho cha maji zilikuwepo taarifa nyingi za miujiza. Ilielezwa kuwa mtu aliyekwenda hapo ghafla bila kuhusisha wazee wafanye tambiko alijikuta akipakwa kinyesi cha binadamu bila kujua nani kampaka. Usiku zilisikika sauti za ngoma na watu wakicheza lakini hawakuonekana. Wakati mwingine unapokaribia maji, maji hayo yalibadilika rangi ghafla na kuwa kama maziwa au yaliyojaa tope. Mara nyingi saa za usiku wakazi walidai kuona mlima ukiwaka taa. Hali iliyopelekea wazee wa Kirangi kufanya tambiko hapo kwa kupeleka kondoo mweusi kila mwaka ili maji yasikauke.

Kiongozi mmoja wa serikali aliamua kwenda Haubi,
 
SEHEMU YA 97

kilipo chanzo cha maji. Alipoona maji hayo yanavyotoka kwa wingi alitamka kuwa anadhani kama ungechimbwa mfereji mkubwa maji hayo yangeweza kuhudumia watu katika maeneo mengi zaidi ya Kondoa. Kwamba mara baada ya kauli yake hiyo maji yalibadilika ghafla na kuwa machafu. Wazee wakashauri kufanya tambiko. Baada ya tambiko maji yakarejea hali yake ya kawaida, ikiwa ishara kuwa mizimu iliafiki wazo lake. Miaka kadhaa baadaye mradi mkubwa wa kuchimba mfereji wa kufikisha maji hayo katika vijiji vipatavyo kumi na vinane vya Irangi nchini. Baadhi ya vijiji hivyo ni Busi, Mairinya, Kirere cha Ng’ombe, Goima, Chandama na vinginevyo. Watu wapatao 30,000 wakinufaika na huduma hiyo.
Siku mbili baadaye Leakey aliniarifu kuwa alikuwa tayari kwa kile alichonilezea kama ‘maandalizi’ ya kazi yake. Maandalizi yalikuwa magumu kuliko hata kazi yenyewe. Kwa msaada wa mzee mmoja wa Kirangi, Msii, ambaye alipewa ajira ya muda tulikuwa watu wa kusafiri katika maeneo mbalimbali ya Kondoa, safari nyingi zikihusisha kutembea kwa miguu katika mapori, majangwa, milima na mabonde ambayo Leakey aliyapendekeza kutokana na ramani yake. Mara kwa mara tulishinda porini, mara kadhaa tukilala huko huko ili tuweze kuamka alfajiri na kuendelea na kazi. Haukupita muda mrefu kabla mzee Msii hajatutoroka na kutoweka bila hata ya kuchukua ujira wake.
Safari hizo zilitufikisha Serya, Mondo, Goima, Sombwa, Mnenya na baadaye Kolo ambako kwa mara ya kwanza niliona Leakey akitoa tabasamu lake la kwanza. Ilikuwa baada ya kugundua mapango na majabali kadhaa yaliyokuwa na michoro



ya ajabuajabu. Michoro ambayo baada ya kuichunguza sana Leakey na mkewe waliniambia kuwa ilichorwa na watu wa kale.
“Leo ni siku ya kihistoria. Nina hakika makazi ya kale zaidi ya watu wa kale. Michoro hii inaweza kuwa na umri wa miaka isiyopungua elfu thelathini hadi leo,” alisema kwa furaha akiyumba huku na kule kama mtu aliyegundua machimbo ya dhahabu.
Mingi kati ya michoro hiyo ilikuwa ya wanyama hasa swala na nyati. Mingine ilikuwa ya watu waliokuwa katika mawindo, silaha zao mishale au mawe ikiwa mkononi tayari kuua mnyama. Vifaa walivyotumia kuchora ndivyo vilivyoniacha zaidi ya michoro yenyewe. Ilikuwa aina fulani ya rangi ambayo iliweza kuingia kwenye jiwe na kudumu kwa miaka mingi ikistahimili jua, mvua na misukosuko mingine tele ya kimaumbile.
Tulikaa katika eneo hilo kwa wiki mbili. Mary akiitumia kamera yake kupiga picha kila mchoro na kila kifaa walichokishuku kuwa ni cha kale. Tulifanya pia, kazi ya kuchimba hapa, kufukua pale. Kazi hiyo iliwezesha kukusanya vifaa vingi kama silaha, mawe ya kusagia, mabaki ya mifupa ya wanyama walioelekea kuuawa na binadamu na vitu vingine tele. Dalili ambazo zilizidi kuthibitisha hisia za Leakey na mkewe kuwa mtu wa kale zaidi ya duniani aliishi hapo au maeneo hayo.
Hisia ambazo zilithibitishwa na wenyeji pale alfajiri moja tuliposhangaa kuwaona wazee watatu, mmoja wa kike waliovaa kimila wakija katika eneo hilo na kuendea moja ya





jabali yenye michoro na kuanza tambiko la kimila. Waliimba na kucheza kabla ya kumwaga mchele na vyakula vingine kama zawadi kwa wahenga.

Baadaye tulibaini kuwa eneo hilo hutumiwa na wenyeji tangu enzi za mababu zao kwa ajili ya matambiko ya kuita mvua au kujiepusha na maafa mbalimbali kama mlipuko wa maradhi au vita. Kwamba ilikuwa nadra sana matambiko katika eneo hilo kutojibiwa kwa neema.

Eneo hilo lililojaa miamba, ardhi yake ikiwa nusu jangwa kama ilivyokuwa sehemu kubwa ya ardhi ya Dodoma iliashiria kuwepo kwa ardhi nzuri, yenye miti, majani na wanyama tele miaka mingi iliyopita.

“Mtu wa kale aliishi hapa,” Leakey alisisitiza akitazama huko na huko. “Naweza kusema kuwa aliishi hapa miaka milioni mbili iliyopita. Naamini uchunguzi wa kimaabara kwa baadhi ya vifaa hivi tulivyopata utathibitisha hivyo,” aliongeza.​

Nilimtazama kwa kumpongeza. Pia, nilijipongeza kwa kuwa sehemu ya mafanikio ya uvumbuzi huo.
 
SEHEMU YA 98

SURA YA KU5MI TANO


S
Bonde Ufa na Morani


ikumbuki niliishi na akina Leakey kwa muda gani. Hazikuwa siku wala miezi. Wala haukuwa mwaka. Niliishi nao kwa miaka, tukihangaika
pamoja katika mapori, miamba, mito, milima na mabonde mbalimbali ya Bonde la Ufa.
Tulichimba hapa, tulifukua pale, tuliokota hiki, tulitupa kile ilimradi mtu asiyejua tunachokifanya angeweza kutufananisha na genge la wendawazimu.
Haikuwa kazi nyepesi. Ilihitaji vifaa na watu wa kutosha. Mara kwa mara tulilazimika kutoa ajira za muda kwa watu ambao walitusaidia kwa shughuli hizo ngumu. Hali kadhalika, hatukuwa na kituo kimoja. Tulipiga kambi katika miji na vijiji mbalimbali vya Babati, Mbulu, Manyara na kwingineko. Kupokea na kusikiliza kwa makini simulizi za wazee na hata hadithi za mapokeo ilikuwa sehemu ya kazi yetu kwa ajili ya utafiti tuliokuwa tukiufanya.
Eneo la kazi nalo lilikuwa pana sana. Bonde la Ufa ni uwanja mrefu sana. Unakadiriwa kuwa na urefu wa kilomita 6,000 ukiwa umeambaa toka nchi ya Syria, Lebanon, Jordan, Israel, Kenya, Tanganyika hadi Msumbiji. Mto Jordan ambao hupeleka maji yake katika bahari mfu na Galilaya, milima ya



Virunga na Luenzori, maziwa kama Tanganyika, Nyanza na Magadi au Nakuru ya Kenya ni sehemu ya Bonde la Ufa. Baadhi ya milima kama Kilimanjaro, mlima Kenya na mengineyo inaaminika kuwa ilikuwa ikipata milipuko ya Volkano miaka ya nyuma. Mlima Oi Doinyo Lengai hadi sasa hupatwa na mlipuko huo wa volkano.
Katika Bonde hilo la Ufa ndimo lilimo eneo la Olduvai Gorge, wenyeji wakiliita ‘Oldupai.’ Likiwa katika uwanja wa Serengeti, ambao pia una wanyama wengi kuliko mahali popote pale duniani, lilikuwa na mito, milima na maziwa madogo kwa makubwa. Moja ya maziwa hayo likiwa Olduvai. Maumbile ya eneo yalionyesha dalili za kuwepo kwa jambo kubwa kama tetemeko kubwa la ardhi na jambo jingine kubwa zaidi ambalo lilitikisa dunia na kufanya ididimie katika Bonde hilo la Ufa huku maeneo mengine yakiwa yameathirika zaidi. Bonde la Olduvai. Pia liko katika maeneo hayo.
Zipo hisia kitaalamu kuwa eneo ilo lilikaliwa na watu, takribani miaka milioni mbili iliyopita. Dalili nyingi zilithibitisha hivyo. Ni humo ambalo Leakey aliendesha utafiti wake kwa muda mrefu na kuchimbua vitu mbalimbali ambavyo vilizidi kuashiria hilo.
Jitihada hizo zilizaa matunda siku ile alipogundua fuvu la kichwa cha mtu wa kale. Fuvu ambalo lilipopimwa kwa njia za kisasa zaidi lilibainika kuwa lilikuwa la mtu wa kale zaidi duniani. Kwa maneno mengine, mtu wa kale zaidi duniani aliaminika kuishi katika maeneo ya Tanganyika. Ugunduzi huo ulimpa Leakey sifa kubwa miongoni mwa wataalamu wa masuala ya mambo ya kale. Hali hiyo ilimsababisha awe mtu wa safari nyingi sana, katika nchi mbalimbali za dunia. Aliudhuria warsha na semina nyingi hapa na pale,



alikaribishwa katika vyuo vikuu mbalimbali kutoa miadhara, alitembelea majumba ya kumbukumbu za mambo ya kale huku na kule na kuendesha mikutano mingi ya kuchangia fedha ili zimwezeshe kuendelea na utafiti wake mrefu na mgumu.
Safari hizo zilinifanya niwe mtu wake wa karibu zaidi Tanganyika, mara kwa mara nibakie kuwa kiongozi na msimamizi wa shughuli zake. Nilikuwa na uwezo wa kuajiri na kufukuza. Nilihifadhi nyaraka na kumbukumbu za utafiti. Kwa kweli sikuwa tena mtu mdogo kama yule kondakta wa gari bovu kule Mbeya au Mnyampala wa mashamba ya katani kule Pangani.
Posho au mshahara wangu haukuwa mbaya, aidha matumizi hayakuwa mengi. Muda mwingi uliishia maporini ambako sikuhitaji kutumia fedha zozote. Hali iliniwezesha kufungua akaunti benki na kujiwekea akiba kidogo kidogo. Hiyo ni faida nyingine niliyoipata katika ajira yangu kwa akina Leakey.
Lakini faida kubwa ilikuwa elimu. Sikubahatika kupata elimu ya darasani. Ndoto ya kurudi shule zilikwishayoyoma tangu niliposahau madaftari yangu kule Pangani na kwenda Bagamoyo, baadaye Dar es Salaam hadi huku. Nilitafuta elimu vitabuni. Leakey na mkewe walikuwa watu wa vitabu. Walisoma kila kitu; toka historia, sayansi, jiografia hadi riwaya. Walisoma vitabu vya dini, majarida na makabrasha ya kila aina. Walipobaini kuwa mimi pia nilikuwa ‘mgonjwa’ wa vitabu waliniruhusu kusoma kitabu chochote nilichokitamani. Ingawa sikuwa na kiongozi wa kunielekeza kile ninachokisoma bado nilijifunza mengi na kupata ufahamu wa kutosha.
Lugha ya kiingereza ni jambo jingine ambalo nilinufaika nalo kwa kuwa nao. Mara kwa mara, walizungumza nami
 
SEHEMU YA 99

kwa lugha yao, hali iliyopelekea niondoe hali ya kutojiamini na kuwajibu bila kujali kama nakosea au la, kama ambavyo wao pia waliongea Kiswahili bila kujali kama wanapatia au la. Taratibu nikajikuta naimudu vizuri lugha yao. Hata pale nilipokutana na watu wengine, wawe wageni wasiojua kabisa Kiswahili, au wasomi wa vyuo mbalimbali, niliweza kuzungumza nao kwa ufasaha hata wakashindwa kuamini kuwa elimu yangu haikuvuka daraja la kati.
Habari ulikuwa ugonjwa wangu mwingine. Pamoja na ukweli kuwa muda mwingi niliutumia maporini, ambako redio nyingi hazikuweza kusikika na ilikuwa ndoto kuona magazeti, bado kila niliporejea mijini niliyafuta hata yale ya mwezi mmoja uliopita. Nilisoma habari, makala, matangazo, hadithi na mashairi. Gazeti jipya la Mwangaza lililoanzishwa Mei 10, 1951 na lile la kwetu la tangu 1943 likihaririwa na Chifu Thomas Mareale II (OBE) ni miongoni mwa magazeti ya Kiswahili ambayo pamoja na upatikanaji wake wa nadra bado yalininufaisha sana kuelewa mtazamo wa mtu mweusi katika nchi yake.
Habari ya Pangani kufanywa wilaya (Janua 7, 1938), samaki wa aina ya sangara kupandikizwa katika ziwa Nyanza, ambalo sasa liliitwa Victoria (1950), Laurian Rugambwa kuteuliwa kuwa askofu wa kwanza Mwafrika nchini Tanganyika (Desemba 13, 1951), kuanzishwa kwa Chama cha TAA kikidai haki za watu weusi (1949). Amri ya serikali kuitangaza rasmi Serengeti kuwa hifadhi ya taifa (April 20, 1948 na kadhalika).​
Vyombo hivyo vya habari viliniwezesha pia kufahamu kuwa sensa ya mwaka 1948 ilionyesha kuwa Tanganyika ilikuwa na idadi ya watu 7,744,600 kati yao 183,860 au



asilimia 2.4 pekee wakiishi mijini. Idaidi ambayo miaka tisa baadaye (1957) ilibadilika na kuwa watu 9,087,6000 nchi nzima, 364,070 au asilimia 4.0 wakiishi mijini.

* * *​
Alfajiri moja nilipata mtihani wangu wa kwanza wa kiutamaduni nikiwa kama mkuu wa kambi ya Leakey. Tulikuwa tumepiga kambi katika maeneo ambayo hayakuwa mbali sana na ziwa Manyara. Akina Leakey walikuwa nje ya nchi kwa miezi kadhaa. Usiku huo mzima ngoma za Wamasai ambazo wenyeji zaidi yangu walizitambua kama ‘Omorata’ ambayo huchezwa majira ya tohara, miezi hiyo ya julai zilitumbuizwa. Niliamshwa toka usingizini kwa kelele za mtu aliyekuwa akilia nje ya hema langu kwa sauti huku akiita kwa nguvu, “Nisaidie. Baba nisaidie…” nilipotoka nilikuta msichana mdogomdogo akiwa hapo nje, kapiga magoti, akilia na kutetemeka kwa hofu. Alikuwa msichana wa Kimasai. Alipambwa kwa shanga kwenye kichwa chake chenye nywele fupi, shanga nyingine tele shingoni, masikioni, mikononi na miguuni. Alivaa vazi la buluu, lililomfunika hadi miguuni. Hakuwa na viatu. Nadhani msichana huyu alitegemea zaidi kumwona mtu mweupe akitoka humo ndani badala ya mweusi kama mimi, kwani niliona dalii za kukata tamaa katika macho yake. Hata hivyo aliendelea kupiga magoti huku akisema “Nisaidie baba…​
naomba unisaidie.”
“Kuna nini?” niliuliza.
“Na… niko naogopa…” alisema kwa Kiswahili chake cha​

shida.

“Unaogopa nini?”
“Naogopa. Naogopa sana. Kufa …”



“Kufa!”
“Ndiyo… kufa. Ndito mmoja kafa jana. Damu… damu nyingi. Naogopa,” aliendelea kusema huku mara kwa mara akigeuka nyuma alikotokea kwa dalili za hofu.
Ndipo nikaelewa. Msichana huyu alikuwa akikimbia tohara, jambo ambalo wasichana wote wa Kimasai, kabla ya kuolewa, hutakiwa kufanyiwa. Kwa maana hiyo msichana huyu alikuwa Ndito. Alikuwa hajafikia hadhi ya kuitwa kokoo. Yeyoo au Shangiki ambazo ni hadhi maalumu za wanawake wa kimasai waliopitia hatua mbalimbali za kimila na kimaisha.
“Wewe unatoka wapi?” nilimuuliza.
“Enkang,” alinijibu, akiwa na maana ya boma lao. Mimi nilitaka kujua kama anatokea Kenya au
Tanganyika. Nikamuulia hivyo. “Hapana.”
“Hapana? Hutoki Kenya?” “Ndiyo.”
“Kwa hiyo wewe n Mtanganyika?” “Hapana.”
Nikashangaa. “Kwa hiyo wewe ni raia wa nchi gani?” “Siye ni Wamasai,” alinijibu.
Ilinibidi nicheke kidogo. Alinikumbusha tabia ya Wamasai ya kujiona kuwa wao ni raia wa nchi hizo mbili. Tabia hiyo ilijengeka katika fikra zao kutokana na kukulia katika utamaduni wa kuahama hama wakifuata malisho ya mifugo yao bila kujali kama wameruka mpaka au la.
“Nisaidie… wanakuja…” alisema akiinuka na kukimbia ndani ya hema langu. Nilipotanabahi, nilikuta hema zima limezingirwa na vijana wa Kimasai wapatao ishirini, wakiwa na ngao zao mikononi, mkuki mkono wa pili. Walikuwa tayari
 
SEHEMU YA 100

kwa lolote. Tayari kwa vita, tayari kwa mauaji.
“Iko naficha yeye wapi?” mmoja wao aliniuliza. Nikamtazama. Alikuwa ‘Layoni’. Mwenyewe akiwa bado hajatahiriwa, hajaua simba wala kuoa lakini hawaogopi isipokuwa wakati wao bado.
Walikiri kuwa nikweli msichana mmoja alifariki usiku huo katika kufanyiwa tohara. Lakini walilielezea tukio hilo kuwa la bahati mbaya tu, ambalo hutokea kwa nadra sana. Wakasisitiza msichana huyo kufanyiwa tohara ili aweze kuwa mtu mzima, abebe majukumu ya kifamilia.
“Ataolewaje bila emorata? Atapataje watoto na familia? Ndito lazima apitie mila zote alizopitia mama na bibi yake,” mmoja wao alisisitiza.
“Lakini huyo hataki,” nilijaribu kutetea.
“Siyo suala la kutaka au kutokutaka. Ni suala la ukoo. Akikataa atatengwa na jamii nzima. Atafukuzwa kila anakokwenda. Hataolewa milele. Huoni kama hilo pigo kubwa kwake kuliko kifo?” alinihoji kijana huyo wa Kimasai.
Kama wenzake alivaa nguo nyekundu. Nywele zake ndefu zilizosukwa vizuri kurudi nyuma zilipambwa kwa rangi au udongo mwekundu. Mikononi na miguuni alivaa bangili za shanga ambazo zilifanya kila hatua aliyopiga wakati tukizungumza itoe mlio ambao nadhani huchangia kumchanganya hata simba kwa wale waliopata kupambana nao.
Wamasai ni watu wanaothamini utamaduni wao kwa kiwango kilekile wanachotamani ng’ombe wao. Ujenzi wa maboma yao, ambayo nilipata kuyatembelea mara kwa mara unathibitisha hilo. Vijiji vinavyoitwa ‘Enkang’ hujengwa kwa mduara, ng’ombe wao wakilala katikati ya duara hilo ili



kuwaepusha na wanyama wakali pamoja na wezi wa mifugo. Vijiji huwa havidumu sana kwani mara malisho ya mifugo yao yanapoonyesha dalili za kupungua, au kifo kinapotokea katika eneo hilo huondoka mara moja na kuhamia sehemu nyingine. Maamuzi mengi ya Wamasai hufanywa na ‘Laibon,’ ambaye ni kiongozi na pia kuhani wao kwa mungu wao, wanayemwita ‘Enkai’. Kutoboa masikio pili aweze kuvaa bangili, kung’oa watoto meno ya mbele ili aweze kulishwa uji wakati akiumwa na kuhakikisha mtoto wa kiume anapotahiriwa hapigi kelele za kuogopa maumivu ni baadhi ya mila za Kimasai ambazo zimedumu miaka nenda rudi. Lugha yao ‘maa’ pia wanaithamini sana kiasi kwamba kuwa hawafanyi jitihada za​
haja za kujua lugha za watu wengine.
Tofauti na makabila mengi nchini, kazi za ujenzi wa nyumba zao hufanywa zaidi na wanawake wakati wanaume wakijihusisha na ulinzi wa makazi na mifugo.
Kwa Wamasai tohara ni tukio la aina yake. Ndilo ambalo humtoa msichana au mvulana katika hadhi moja kwenda ya pili. Hivyo, tukio hilo huambatana na mbwembwe nyingi, zikiwemo ngoma maalumu ambazo huchezwa miezi ya Julai na kufuatiwa na tukio lenyewe ambalo hufanyika alfajiri, kabla jua halijachomoza. Tukio hufanyiwa karibu na zizi, moto mkubwa huwashwa na ng’ombe mmoja kuchomwa mkuki shingoni. Damu ya ng’ombe huyo hukingwa na kuhifadhiwa katika kibuyu maalumu kiitwacho ‘Eng’oti’. Damu hiyo huchanganywa na maziwa na watahiriwa wote kunyweshwa kabla ya tohara.
Kilimo ni moja ya mambo ambayo hayawavutii sana Wamasai. Chakula chao kikuu ni nyama ama kupika ama ya kuchoma. Nyama za kupika zina maadili yake. Huchanganywa



na dawa mbalimbali. Kwa mfano dawa ya ‘Okiritaraswa’ humfanya mtu awe na hasira sana. Dawa nyingine ni ‘Orumukatani’ ambayo nayo hupikwa na humpa mtumiaji nguvu. Mara nyingi watumiaji wa dawa hizi ni wale walio tayari kwenda vitani au kupambana na simba. Dawa ya tatu, ‘Orokirotiti’ humfanya mtumiaji kuwa na hamu ya kula pamoja na kuwa mchangamfu. Nyingine ni dawa za kuondoa mafuta mwilini, kujikinga na maumivu ya misuli na kujenga mwili.
Hawa ndio Wamasai. Watu wanaojipenda na kujithamini. Watu wanaoupenda na kuuthamini utamaduni wao kiasi kwamba ujio wa wageni mbalimbali nchini, toka makabila yaliyoingia toka kila upande wa nchi, Waarabu waliotoka mbali na ujanja wao, Wazungu na hila zao na wengine hawakupata kuwatikisa Wamasai na imani zao. Watu wa aina hiyo ambao walikuwa tayari kwa lolote, ikiwa pamoja na kutoa uhai wao, ili kulinda hadhi yao, mimi ni nani hata nibadili imani yao katika muda wa saa moja? Niliwaza nikiingia ndani ya hema kwa dhamira ya kumtoa dada yao.
Nilimkuta akibubujikwa na machozi huku akitetemkea mwili mzima. “Tafadhali, usiwaruhusu wanichukue. Naogopa… Nitakufa!” alinisihi akipiga magoti miguuni mwangu.
Nilipatwa na huruma. Nikahisi machozi yakinilengalenga hasa pale nilipomtazama usoni na kuona alivyonitumbulia macho ya huzuni kama mfamaji aliyekata tamaa, anayetegemea msaada wangu pekee.
Huko nje Morani walisikiliza wakianza kupiga kelele. Nadhani walihisi kuwepo kwa jambo linaloendelea humo ndani. Mara wakaanza kuimba nyimbo zao zinazoashiria vita huku wakirukaruka kulizingira hema langu. Ghafla mmoja mmoja akaingia ndani ya hema, mkuki wake ukiwa umetangulia.



Mwingine akafuatia, sime mkononi. Walimwendea ndito moja kwa moja na kuanza kumvuta nje. Msichana akazidi kulia akinitazama kwa macho yake yaliyoloa machozi.
Sikufikria mara mbili. Nilichupa na kuichukua bunduki
ya Dakta Leakey na kuilekeza kwao huku nikifoka, “Mwacheni!”​
Hawakuamini macho yao. Walinitazama kwa mshangao na hasira kali.
“Tokeni!” Nilifoka tena.
Yule mwenye sime alipandwa na hasira. Akamwachia msichana na kunifuata huku akichomoa sime yake. Lakini mwenzake alimshika na kumnong’oneza jambo.
Nadhani alikuwa hajasahau maafa ya risasi kwa miili yao. Pengine alikumbuka tukio la kinyama la mamia ya watu wao waliouawa na Stanley walipopambana naye kwa mikuki na sime zao. Mwezie alimsikiliza. Kama kondoo, waligeuka na kutoka nje ambako waliwashawishi wenzao kuondoka. Lakini haikuwa kabla ya kunitupia jicho kali, la kisasi, ambalo hadi leo sijapata kulisahau katika njozi zangu za usiku na mchana. Mara walipoondoka, nilimrudia msichana yule na kumtaka yeye pia aondoke. “Nenda zako, wakirudi hapa​
hawatafikiria mara mbili,” nilimhimiza.
Aliinuka, akanitupia jicho la shukrani kisha kwa sauti ndogo alisema, “Umesaidia mimi sana. Ahsante Laibon.”
Laibon! Heshima aliyonipa haikuwa ya kawaida. Nilimtazama akigeuka na kuondoka taratibu. Nje ya hema alitazama huko na huko kabla ya kuondoka akielekea upande wa pili wa walikoelekea wabaya wake.
Wasaidizi wangu walinifuata baadaye, mmoja akinipongeza wa pili yule anayejua Kimasai akinipa pole.
“Pole ya nini?” Nilimwuliza.



“Hujui? Unadhani Mmasai ni mtu wa kuvumilia kitendo ulichokifanya? Kwao umedhalilisha kabila zima. Lazima watataka kulipa kisasi. Kama si leo kesho, kama si kesho keshokutwa au hata mwakani,” alinifafanulia.
Kwa kuamini kuwa Wamasai wasingependa kucheza na risasi, hasa baada ya kuona bunduki mikononi mwangu, niliipuuza hofu yake. “Enzi zile zimepita ndugu yangu. Sasa wanajua bunduki, wanajua utawala wa sheria,” nilimweleza.
Hakuonekana kuafikiana na fikra zangu, ingawa hakutia neno jingine. Niliamini hivyo jioni hiyo aliponitaka ruhusa ya kwenda nyumbani kwake kuitazama familia yake. Hakukuwa na kazi nyingi. Hivyo nilimruhusu. Msaidizi wa pili alitoweka bila kuaga. Bila shaka kwa hofu ileile.
Usiku huo nilijikuta peke yangu katika kambi, katikati
ya uwanda mpana wenye jangwa na majani hafifu.
Sina budi kukiri kuwa kwa kiasi fulani nilishikwa na hofu. Nilikusanya magogo na kuwasha moto nje ye hema langu kwa dhamira ya kutishia wanyama wakali waliozowea kutembelea makambi yetu hasa nyakati za usiku. Ulipofika wakati wa kulala niliweka bunduki yangu kando ya kitanda na kujilaza chali na huku nikijiambia kuwa nisingeruhusu usingizi unichukue.
Usingizi ulinichukua. Tena ule wa pono.
Nadhani nililala kwa masaa manne au matano kabla ya kuzinduka ghafla kwa hisia ambazo sikufahamu zilitokana na nini. Nilihisi kuwepo kwa mtu au kitu cha ziada hemani humo. Nikafumba macho na kutazama kwa makini huku mkono wangu ukiwa tayari kuichukua bunduki yangu.


Je nini kilifuata?
Huyo mtu ni nani?

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 101

Usingizi ulinichukua. Tena ule wa pono.
Nadhani nililala kwa masaa manne au matano kabla ya kuzinduka ghafla kwa hisia ambazo sikufahamu zilitokana na nini. Nilihisi kuwepo kwa mtu au kitu cha ziada hemani humo. Nikafumba macho na kutazama kwa makini huku mkono wangu ukiwa tayari kuichukua bunduki yangu.
Kweli kulikuwa na kitu. Hapana, mtu! Kwa nuru ndogo iliyotokana na moto uliokuwa ukiendelea kuwaka pale nje,
niliweza kuona kiwiliwili cha binadamu kikipenya kimyakimya, kama mzimu, kunifuata kitandani. Niliinuka mara moja na kusimama huku nikianza kuinua bunduki yangu
“Shhhh! Hapana kelele,” ilinong’ona sauti ya mtu huyo. Ilikuwa sauti ya kike! Sauti ya yule msichana aliyetoka hemani humu asubuhi hii.
“Kuna ni…” Nilijaribu kumuuliza. Lakini kwa mara nyingine alinizuia kuzungumza, safari hii kwa kuniziba mdomo kwa kiganja chake cha mkono wenye baridi.. Kitendo kilichofuatiwa na sauti yake ya mnong’ono vilevile ikisema, “Haraka… Ondoka. Wanakuja kukuua.”
“Nani?” Nilinong’ona kama yeye.
“Morani. Wanakuja…” Hata kabla hajamaliza kunifafanulia. Nilisikia hatua za watu wanaotembea kulifuata hema. Nilipochungulia nje, niliona viwiliwili vya miili ya watu wapatao ishirini, silaha mkononi, wakitembea kulifata hema langu.
“Kimbia!” Alisema akinisukuma kutoka nje. “Wewe?”
“Acha mimi… nitakufa… peke yangu. Wewe hapana.” alinong’ona.
Sikuafikiana naye. Nilimshika na kumvuta mkono kutoka naye nje, huku tukiwa tumeinama. Nje ya hema tulinyata taratibu kuelekea upande wa pili, kulikokuwa na vichaka na miti miwili mitatu.
Hata kabla hatujafikia vificho hivyo, Morani walikwishafika kwenye hema na kulizingira. Walipita huko na huko wakikagua hema baada ya hema. Walipobaini kuwa mahema yote hayakuwa na watu, waliutumia moto niliouwasha mwenyewe kuteketeza mahema yote. Walifanya



hivyo huku wakiimba nyimbo za kivita au za ushindi, wengine wakirukaruka juu kama waliopagawa.
Bila ya msichana yule kunishikilia, ningeweza kurudi waliko ili kupambana nao. Moto, ambao niliushuhudia ukiteketeza mahema hayo, kwangu ulikuwa pia ukiteketeza ndoto na matumaini yangu ya maisha.
Achilia mbali vitabu na nyaraka zangu binafsi, nyaraka zote za Dakta Leakey na mkewe, baadhi ya vifaa vyake katika shughuli zake za utafiti na kumbukumbu mbalimbali za muhimu zilizotafunwa na moto huo. Kama mchezo wa kuigiza. Ilikuwa dhahiri kuwa nisingeweza kuwa naye, kwani nisingeweza kumweleza chochote ambacho angekielewa.
Nadhani nilitokwa na machozi kama mtoto. Nadhani miguu yangu iliishiwa nguvu, kwani nilijikuta nimeketi chini huku mikono ya msichana huyo mdogo ikiwa imenikumbatia kwa namna ya kunifariji. Yeye pia alikuwa akilia. Bila shaka akijiona chanzo cha mkasa huu mzito katika maisha yangu.
Nilimtazama, mara nikajikuta nikimuonea huruma badala ya kujionea huruma mimi mwenyewe. Nilimwona katika nuru tofauti. Si kama msichana aliyekimbia tohara bali shetani au malaika aliyetumwa kuvuruga maisha na matarajio yangu kama ilivyokuwa ada katika maisha yangu. Nikainuka na kisha kumwinua.
Aliinuka kwa taabu. “Twende!” Nilimwambia.
“Wapi?” Alinong’ona kwa sauti yenye kwikwi .
Wapi! Nilijiuliza vilevile. Ndio kwanza ikanipambazukia kuwa toka muda huo sikuwa na mahala pa kwenda. Nilikuwa nimerudi nilipoanzia; Mtu wa kutangatanga kama ndege asiye na makao maalum.





Niende wapi? Nilijiuliza tena. Ningeweza kwenda polisi kutoa taarifa ili Morani wale watafutwe na kuadhibiwa, lakini hilo lisingesaidia. Ni vigumu sana kuwapata Morani katika uwanda huo mpana. Kesho wanaweza kutorokea Arusha, kesho kutwa wakawa Kenya. Zaidi ya hayo sikuona vipi adhabu hiyo ingeweza kunisaidia. Kamwe isingerudisha chochote kati ya yote yaliyoteketea.

Nilimvuta taratibu kuelekea nje ya eneo hilo. Tulitembea taratibu, tukikurupusha wanyama hapa na pale hadi tulipofikia mti mmoja mkubwa. Msichana yule alininong’oneza jambo akielekeza kidole chake kwenye mti ule. “Unasemaje?” Nilimhoji.

“Jana nashinda juu ya mti ule. Nalala juu yake hadi nasikia ngoma ya vita. Nakuja ita wewe,” alisema

Nilimwelewa, nikawa nimepata jibu la swali lililokuwa likinisumbua, la kutaka kufahamu alijuaje kuwa ndugu zake walikusudia kunidhuru. Ukiwa juu ya mti huo mkubwa, unaweza kuona hadi mbali. Na ukiwa msikivu, unayezifahamu mila zako, hutashindwa kujua ngoma inayopigwa kwa mbali inaashiria nini.

Alinishauri tulale juu ya mti ule.

Nikaafiki.

Tulipata tawi kubwa, lililofanya tuketi bila hofu kubwa ya kuanguka. Kwa ajili ya baridi kali, usiku huo, pengine na hofu ya uzito wa matukio, binti huyo aliniegemea kifuani, usingizi ukamchukua. Joto lake na uwepo wake ulinifariji. Lakini sikuweza kupata usingizi. Jogoo wa kwanza alipoanza kuwika, nilimuamsha taratibu. Aliamka kiasi akishikwa na aibu kwa jinsi alivyonikumbatia. Mimi sikuwa huko. Akili zangu zilikuwa mbali maili nyingi nje ya eneo hilo.
 
SEHEMU YA 102

“Nadhani nianze safari ya kuondoka.” Nilimwambia.
“Wewe nakwenda wapi?” aliniuliza akifikicha macho
yake kutoa usingizi.
“Sijui ninakokwenda lakini sihitaji kukaa hapa.
Nitakwenda popote.”
Alinitazama kwa makini kabla hajatamka taratibu, “Nakwenda na wewe.”
“Unakwedna na mimi! Wapi?”
“Sijui. Popote nakwenda wewe mimi nakwenda,” alisema.
“Mimi sijui nakwenda wapi.” Nilimwambia.
“Hata mimi yenyewe sijui. Nabaki hapa itaniua. Wewe nasaidia mimi. Hapana acha iniue.”
Niliishiwa nguvu. Nikaduwaa
Jogoo wa pili walianza kuwika. Sikutaka alfajiri inikute hapo. Nikashuka kwenye mti na kuanza safari. Msichana wa Kimasai alishuka na kunifuata.

16
Ben R. Mtobwa











SURA YA KUMI SITA

Na Wangu Hadi


K
una fasihi simulizi nyingi nchini ambazo zamani nilidhani zilikusudiwa kumsisimua msikilizaji wake peke yake. Nyingi kati ya hizo ziliwalenga
watoto. Baadhi zilikuwa hadithi za kusisimua au kutisha sana kiasi cha kuwatoa machozi wasikilizaji wake, wengine zikiwakosesha usingizi.
Moja ya hadithi hizi ni zile za kubeba ‘mzigo’ ambao mhusika alishindwa kuutua kwa urahisi, kwa mfano, kuna ile inayosimulia kijana ambaye alikuwa akitembea porini peke yake. Kwamba alifika mahala penye mto ambao alitakiwa kuuvuka. Kando ya mto huo alikuta msichana mdogo, mzuri sana aliyetaka kuvuka vilevile lakini alikuwa akiogopa mkondo mkali wa mto huo. Hivyo alipomwona kijana huyo msichana aliangua kilio akimsihi amsaidie kuvuka. Kwa huruma zake, kijana alikubali. Akambeba binti huyo mgongoni na kuogelea naye hadi upande wa pili ambako alijaribu kumtua. Lakini msichana huyo alikataa. Alipotanabahi kijana huyo alibaini kuwa alibeba kikongwe ambacho kilimng’ang’ania mgongoni usiku na mchana hadi mvulana akakosa nguvu.
Nyingine inayofanana na hiyo, ni ile ya mvulana mwingine aliyekuwa akivuka mto vilevile. Yeye alielezewa





kukuta kikongwe kikilia kando ya mto huo kikiomba msaada wa kuvushwa. Kilikuwa kibibi kichafu kinachonuka na kutoa tongotongo na kamasi muda wote. Mhusika alikihurumia. Akakitia mgongoni na kukivusha. Kinyume na mhusika wa kwanza, huyu mara tu alipokitua, alibaini kuwa kikongwe kile kilikuwa msichana mrembo sana, mwenye uwezo wa kimalaika. Walipendana, wakaoana. Maisha ya mvulana huyo yakiwa yamebadilika toka kwenye ufukara na kuwa tajiri na mtu maarufu sana nchini kwao.

Awali sikupata kufikiria uzito wa falsafa iliyokuwemo katika simulizi hizo. Sasa nikiwa na matukio yale, nilizichukulia kwa uzito unaostahili. Tatizo ni kutokujua nilikuwa katika nafasi ipi kati ya wahusika wale wawili.

Hayo yalipita akilini mwangu baada ya kumtazama kwa mara nyingine yuleyule msichana wa Kimasai aliyeniganda kama kupe. Jitihada zangu zote za kumwacha ashike hamsini zake nami nishike zangu hazikupata kuzaa matunda. Nilijaribu kumtelekeza hapa na pale lakini machozi yalimtoka na macho yake yenye huruma aliyonikazia yalinipokonya ujasiri. Hali iliyopelekea nijikute nikipanda naye lori la kwanza lililopita barabarani alfajiri hiyo

“Mnakwenda wapi?” Dereva aliniuliza.

Sikuwa na pa kwenda. Nilichohitaji ni kuondoka eneo hilo kuelekea popote. Sikuwa tayari kuwaona wale vijana wa Kimasai tena. Kwani kama wasingeniua mimi ningewaua wao au mmoja wao.

Pia sikuwa tayari kutazamana na akina Leakey macho kwa macho, iwapo wangerejea ghafla kutokana na hasara niliyowatia.

“Wapi?” Dereva alihimiza.
 
SEHEMU YA 103

“Kwani nyie mnakwenda wapi?”
“Singida, kupitia Babati,” Sikuhitaji kumjibu. Niliparamia gari lake. Msichana alifanya hivyohivyo. Tukaondoka. Tulipumzika kwa muda. Nilitumia mapumziko hayo kumvuta kando na kumtaka abakie hapo na kuwatafuta ndugu zake wengine. Alikataa katakata kwa maelezo kuwa toka alipokataa tohara tayari amekataa ndugu wote hivyo hana mahala pa kwenda.
“Kwan nini usikubali kupata tohara?” Nilimhoji. “Naogopa.” Lilikuwa jibu lake.
“Unaogopa?”
“Kufa. Mwenzangu alikufa jusi tu.” Alisisitiza.
“Lakini mimi sina pa kukupeleka. Mwenyewe sijui nitakwenda wapi, nitalala wapi. Huoni kuwa unanipa mzigo juu ya mzigo?” Nilijaribu kumshawishi. Badala ya kunielewa aliangua kilio. Kwa mara nyingine ushujaa ulinitoka, ubinadamu ukachukua mkondo wake.
Kwa bahati nzuri nilikuwa na tabia ya kutembea na akiba yangu yote ya fedha mfukoni, isipokuwa zile zilizokuwa benki peke yake. Hivyo, mkasa huo ulinikuta nikiwa na vijisenti ambavyo vingeweza kuniweka hai kwa wiki mbili tatu kabla ya kuanza kutaabika kwa njaa. Nilitumia sehemu ya senti hizo kulipia nauli na kula chakula cha mchana kabla ya kuanza tena safari ya Singinda.
Mzee mmoja tuliyekuwa naye safarini humo. Nadhani alisoma sura yangu iliyojaa mashaka na ule uso wa Kimasai uliolowa machozi. Aliniuliza kulikoni. Nilihitaji sana ushauri hivyo sikusita kumsimulia kila kitu, toka mwanzo hadi mwisho wa mkasa. Kwa mshangao wangu nilimwona akiangua kicheko baada ya kunipa pole.



“Sioni kama kuna jambo la kuchekesha hapo,” nilimwambia kwa sauti ndogo iliyoficha hasira zangu dhidi ya kitendo chake hicho.
Mzee alinishika bega kabla ya kuninong’oneza ili msichana yule asisikie. “Nacheka kwa kuwa unasumbuliwa na jambo dogo sana,” alinieleza.
Sikumwelewa. “Dogo kivipi? Mtoto wa watu hana pa kwenda kwa sababu ya uzembe wangu. Mimi mwenyewe sina pa kwenda kwa sababu ya uzembe uleule. Unaliita jambo dogo?” nilimwuliza.
“Dogo sana.” Alisema. “Nitakusaidia mara tutakapofika Singida. Naitwa Kingu. Halfan Kingu. Kwa hilo ondoa wasiwasi mwanangu.”
Nilishusha pumzi. Kwa muda nilisahau matatizo yangu na kuifurahia safari kwa kuyaruhusu macho yangu kuburudishwa na mandhari mbalimbali za mazingira kando mwa barabara hiyo. Mbuga pana zilizojaa ndege na wanyama ainaaina zilitulaki, majabali yaliyosimama katika maumbile ya kusisimua yalitushangaza, majangwa yasiyo na msitu wala nyasi nayo yalikuwa sehemu ya mazingira hayo.
Tulifika Singida jioni sana. Wakati huo tayari roho yangu ikiimba tenzi na mashahiri juu ya Singida niliyoifahamu kupitia simulizi za kihistoria na maandishi ya vitabuni.
Kwa mfano, nilipata kusoma juu ya reli iliyojengwa enzi za vita kuu inayounganisha mji huo na reli ya kati kupitia Manyoni. Leo nilikuwa nimepata fursa ya kuiona kwa macho yangu mwenyewe reli hiyo.
Singida, nchi ya mwanamke pekee shujaa katika historia ya mapambano ya Watanganyika dhidi ya ujio wa wakoloni. Mwanamke huyu Leti Kidanka, kati ya mwaka 1903





hadi 1907 aliongoza majeshi ya Wanyaturu kupambana na yale ya Wajerumani hata wakaelekea kusalimu amri. Kama isingekuwa kwa ajili ya silaha zao kali na nyingi Wajerumani wale wasingefanikiwa kumkamata, wakamchinja na kuondoka na kichwa chake kama walivyofanya kwa Mkwawa.

Niliweza kuyaona majengo ya kale, boma la kilimatinde walilojenga Wajerumani hao kati ya mwaka 1880 na 1890 na lile la mkoloni lililojengwa 1900 hadi 1911. Boma ambalo lilikuwa makao makuu, ofisi, gereza, makazi ya maafisa wao na eneo la kunyongea watu. Nilishangaa kuona mti uliokuwa ukitumika kunyongea watu toka enzi zile ukiwa hai hadi leo.

Mzee Kingu ambaye tulifuatana naye katika safari hiyo ya mjini baada ya kuhusika kwenye gari alitabasamu kila aliponiona nikivutiwa na hiki au kile.

“Laiti ungefika Iramba,” alisema na kuongeza “Kuna vivutio tele ambavyo kwa udadisi wako vingekusisimua sana. Kuna mapango kama yale ya Kondoa Irangi na majabali yaliyoumbwa kwa namna ya binadamu,” alisema.

“Unaifahamu Sodoma na Gomora?” Aliniuliza ghafla. “Naam. Imesimuliwa katika Biblia na Koran,” nilimjibu. “Unafahamu chochote juu ya mwanamke aliyegeuka

mwamba wa chumvi baada ya kugeuka nyuma kuutazama mji wa Sodoma ukiteketea kinyume cha maelekezo waliyopewa?”

Hili pia nililifahamu, “Mke wa Lutu sio?”

Mzee Kingu alitikisa kichwa kuafikiana nami. “Kwa taarifa yako sanamu ya mwanamke yule aliyeganda na kugeuka nguzo ya chumvi iko huku kwetu. Ukienda Iramba, uingie maporini utaikuta. Na chumvi inapatikana hadi leo kama ilivyoandikwa,” aliongeza.

“Wewe ulipata kuiona?” Nilimuuliza.
 
SEHEMU YA 104

“Sijapata lakini wazazi wangu walinihakikishia. Wao walikuwa wakienda huko katika safari zao za uwindaji.”
Sikuweza kumkubalia wala kumkatalia. Tulikuwa tukitembea mjini. Yeye mbele, mimi kati, msichana wa Kimasai nyuma. Ilikuwa safari iliyobuniwa na mzee huyo kwa maelekezo kuwa ni ya kunisaidia. Hata hivyo, alikuwa hajaniambia tunakwenda wapi.
Vivutio vya mji wa Singida havikuwa na mwisho. Maziwa yaliyojikita katikati ya mji, Singidani na Kindai ni miongoni mwa mambo ambayo yasingekosa kumvutia mgeni yeyote. Sehemu fulani tuliwaona wavuzi wakitafuta riziki zao katika maziwa hayo, huku ndege kama bata maji na yangeyange nao wakijishughulisha na yao.
Safari yetu iliishia mbele ya jengo moja lililokuwa na maandishi yaliyosomeka EVANGELICAL LUTHERAN AUGUSTANA SYNOD. Kingu aliniambia kuwa hiki kilikuwa kitengo cha kanisa ambacho kilijishughulisha na kusomesha watoto yatima na wale wasiojiweza. Aliniambia kuwa wasingesita kumpokea msichana huyo na kumlea, hasa baada ya kuonyesha msimamo wake wa kupingana na mila potofu za jamii yake.
Nilimweleza hivyo msichana yule. Nilishukuru kuona akiipokea habari hiyo kwa utulivu. Tulikaribishwa ndani. Mtumishi aliyetupokea hakushangazwa na maelezo yetu hata kidogo. Alimshika msichana yule mkono kwa dalili zote za upendo kabla ya kumwuliza umri wake.
Hakujua ana miaka mingapi. Kwa kukadiria kwangu hakuzidi miaka kumi na miwili. Mchungaji wao hakuwepo. Hivyo alitutaka mimi na Kingu kuondoka kwa maelezo kuwa msichana huyo alikuwa katika mikono salama.



Tuliinuka. Nilishangaa kuona msichana huyo naye akiinuka na kunifuata. Nilimtazama kwa macho makali yenye maswali mia moja na moja. Hata hivyo, nilipumua pale nilipomuona akitabasamu na kisha kusema kwa kiswahili chake kibovu, “Taka kushukuru. Yenyewe imeokoa maisha yangu.”
Alinikumbatia. Machozi yakimlengalenga machoni.
Kitendo chake kiligusa ile sehemu laini katika moyo wangu. Mie pia nilihisi machozi yakinilengalenga. “Hapana ni wewe uliyeokoa maisha yangu,” nilimwambia. Ulikuwa ukweli toka katikati ya moyo wangu.
“Hapana kweli… mimi haribu maisha yako,” alijitetea.
Sikutaka kuendelea na mjadala huo. Hivyo nilijikwanyua taratibu toka katika mikono yake na kuanza kuondoka, huku nikijitahidi kuyaepuka macho yake.
Hutaki kujua hata jina langu? Nilihisi swali hili katika macho yake. Nikajikuta nikitokwa na swali hilo.
“Mimi naitwa Nashifa,” alisema.
“Vizuri sana Nashifa. Mimi naitwa Petro. Petro Kionambali,”

* * *
Kuutua ‘mzigo’ ilikuwa mwisho wa tatizo moja. Tatizo la pili, langu binafsi lilikuwa palepale. Sikujua usiku huo na siku zinazofuata ningekitua wapi kichwa changu wakati nikianza upya kufikiria hatma ya maisha yangu, baada ya miaka kadhaa ya kuzungukwa na akina Leakey katika Bonde la Ufa na miji au vijiji vya jirani.
Nadhani kwa mara nyingine Kingu aliweza kuusoma moyo wangu. Ni pale nilipomsikia akianza kujinadi ghafa





kwamba anatoka katika ukoo unaoheshimika na usio na njaa. “Wanyaturu wote wananifahamu. Natoka katika ukoo wa Machifu. Huyu unayemsikia Chifu Said Gwao mdogo wangu upande wa baba. Kwangu utalala, utakula bila wasiwasi wowote.”

Nikashtuka. “Hayo yametokea wapi tena?” nilimwuliza.

“Naona unasumbua kichwa chako kufikiri leo utalala wapi,” alinijibu. “Hilo achana nalo kabisa mwanangu. Fikiria mengine.”

Nilimtumbulia macho ya mshangao uliochanganyika na aibu. “Nisingependa kukusumbua zaidi. Tayari umenisaidia sana. Kunipatia makazi ya yule msichana lilikuwa tatizo langu kubwa. Mengine sioni kama yatanisumbua,” nilimweleza.

“Huwezi kulala nje. Huwezi kutupa pesa katika vyumba vya wageni kwa ajili ya kulala tu. Utakuwa mgeni wangu. Leo, kesho na keshokutwa. Utakaa hadi hapo utakapoamua vinginevyo.”

Sauti yake iliashiria kufunga mjadala. Akiwa mtu mwenye umri mkubwa, bila shaka zaidi ya baba yangu, ingawa hakumpata babu, nililazimika kumsikiliza. Tukaongozana kuelekea kwake. Yeye mbele mimi nyuma.

Mzee Kingu alikuwa akiishi nje kidogo ya mji. Kauli yake kuwa hakuwa mtu mwenye njaa ilidhihirika mara tulipofika nyumbani kwake. Kwa kweli haikuwa nyumba bali majumba. Alikuwa na kijiji! Nyumba kama nane hivi, zikiwa katikati ya shamba la ekari zipatazo tano au zaidi, za matama na alizeti. Tatu zilikuwa nyumba za wake zake, nne za wanawe na moja niliyoambiwa kuwa ilikuwa maalumu kwa ajili ya wageni. Pembeni alikuwa na zizi kubwa la mifugo. Milio ya ng’ombe na mbuzi ilisikika.
 
SEHEMU YA 105

Tofauti na alivyokuwa safarini, mcheshi na mzungumzaji sana, hapa nyumbani alikuwa mtu mwingine kabisa. Tulifika yapata saa mbili za usiku. Mji huo ulikuwa umechangamka kwa kelele za watoto, sauti za redio na pilikapilika za akina mama. Hali ambayo ilibadilika mara mzee alipotia mguu katika himaya hiyo. Wajukuu walipunguza kelele, kila mmoja akirejea kwa mama yake. Watoto walimfuata na kumsalimu, lakini katika hali ambayo haikuwa tofauti sana na salamu za askari na afande wake. Walibadilishana maneno mawili matatu, ya juujuu, kabla ya watoto hao kuteleza kila mtu akienda anakokufahamu. Hali haikuwa tofauti sana na wake zake wadogo. Ni mke mkubwa pekee ambaye baada ya kumsalimu aliketi na kumwuliza habari za safari. Hata hivyo, baada ya dakika moja tu yeye pia alijikuta hana cha kuzungumza. Aliketi pale kwa utulivu kama anayesubiri amri, ambazo zilianza kumiminika mara moja.
“Huyu ni mgeni wangu. Chumba chake kimeandaliwa?” “Wale ng’ombe wawili wagonjwa wamepatiwa dawa?” “Nina mashaka kama mmekumbuka kurekebisha lile
ghala linalovuja…”
Mkewe ambaye tayari alikuwa mama wa makamo alijibu kila swali kwa ufupi na umakini mkubwa kama mwanafunzi kwa mwalimu wake.
Muda mfupi baadaye chakula kililetwa. Hakikuwa chakula cha watu wawili wala watatu. Ulikuwa mlo ambao watu sita wangeweza kula na kusaza. Ulikuwepo mguu wa mbuzi wa kuchoma, kuku wawili waliopikwa, sinia kubwa la wali na bakuli la matunda. Wakati mimi niliishia kula mapaja mawili ya kuku na wali kidogo mzee Kingu aliteketeza robo tatu ya chakula kile. Alikula nusu ya matunda na kushushia kwa birika zima la maji.



“Endelea kula.” Alinihimiza “Mimi nimechoka. Unajua utu uzima tena! Watakuonyesha sehemu ya kulala,” alisema akiondoka bila kusubiri shukrani zangu.
Mie pia uchovu ulikuwa umenishika. Hivyo, mara alipoondoka nilinawa mikono, nikamshukuru bi mkubwa ambaye muda wote alikuwa pale. Kisha niliomba nielekezwe yalipo malazi yangu. Mvulana mmoja alinipeleka kwenye nyumba ya wageni. kiasi ilijitenga na nyumba nyingine na hivyo kutoa uhuru wa kutosha kwa wageni. Taa ya chemli ilikuwa ikiwaka chumbani, kando ya kitanda kilichotandikwa kwa blanketi na shuka mbili safi. Mara tu kijana huyo alipotoka nilivua nguo zangu na nikafunga mlango na kisha kujibwaga kitandani.
Mkesha wa siku hiyo, uchovu wa safari ya miguu na gari pamoja na purukushani za siku nzima vilifanya usingizi unichukue mara tu nilipokitua kichwa changu juu ya mto. Ulikuwa usingizi wa pono. Nililala hadi saa tisa au kumi za alfajiri nilipoamshwa na kitu fulani. Sikufahamu ni kitu gani lakini hisia zilifanya nishuku jambo. Sina tabia ya kukoroma, bado niliamini kuwa nilijisikia kama nakoroma usingizini. Nilitulia kimya nikijaribu kufikiri kitu gani kiliniamsha. Sikuelewa. Wakati usingizi ukianza tena kunichukua hisia zilezile za kukoroma zilinireja. Hapa, hazikuwa hisia. Ilikuwa sauti halisi ya kukoroma tena ikitoka chini ya kitanda.
Nilishuka toka kitandani, nikapandisha mwanga wa taa na kuchungulia uvunguni. Nilishangaa kuona kitu kama tochi mbili zikinimulika toka chumbani humo. Tukio ambalo lilifuatiwa na mguno mzito kama ule wa mbwa anayehisi kuhatarishiwa uhai wake.
“Fisi!”



Niliropoka baada ya kutazama vizuri. Fisi mkubwa kabisa alikuwa amelala uvunguni humo, chini ya kitanda changu! Nilitetemeka. Nikaruka kuendea nguo zangu ambazo nilivaa harakaharaka na kutoka mbio.
Mbio ambazo ziliishia mbele ya nyumba ambamo nilimuona mzee Kingu akiingia kulala. Kabla hata sijagonga niliona mlango ukifunguliwa, mzee akiwa amevaa kikoi, kifua wazi. Alitoka. “Kuna nini?” alihoji kwa sauti kali kidogo.
“Fisi yuko chumbani kwangu.” Nilimjibu.
Mzee akaangua kicheko. “Hilo tu?” alinihoji baadaye. “Yule pale hana neno. Zaidi anakulinda kama anavyoulinda mji huu.”
Sikumwelewa. “Hana madhara! Kwa hiyo nikalale na

fisi?”

Mzee alicheka tena. Kisha akasema, “Kumbe wewe bado

mtoto mdogo sana sio? Unadhani himaya hii utailinda vipi bila kuwa na vitu kama vile? Yule amefugwa. Anatii amri zangu zote na hafanyi jambo lolote bila maagizo yangu. Isitoshe ni mtumishi mzuri anayebeba mzigo na hata kunibeba mimi mwenyewe katika safari zangu za usiku.”
Nilizidi kuchanganyikiwa. Nazungumza na binadamu au shetani? Anazungumzia kufuga fisi kama kufuga mbwa!
“Binadamu anawezaje kumfuga mnyama kama yule?” nilimwuliza bila kutarajia.
Na bila kutarajia vilevile alinijibu. “Ujuzi tu mdogo wangu. Nyie mnaita uchawi lakini ni ujuzi. Ukipata jino la fisi unaweza kumfuga fisi. Ukipata la mamba unaweza kummiliki mamba. Vivo hivyo kwa simba, chui na hata nyoka. Watu wanawafuga binadamu wenzao washindwe kumfuga mnyama?” alisema. Sasa nilikuwa na hakika kuwa sizungumzi na binadamu
 
SEHEMU YA 106

wa kawaida. Sikuona kama nilihitaji kuendelea kumsikiliza. Alizisoma hisia zangu. “Nenda kalale,”akaniamuru.
Nikageuka kuondoka. Mara akaniita tena, “Kijana,” alisema. “Kitu kimoja kinanisumbua. Umekula nini wewe?”
“Nimekula nini? Una maana gani?” sikumwelewa.
Maana wenzako wote hulala na fisi wangu hata kwa
mwezi bila kumwona wala kumsikia. Wewe umetafuna nini?”
Sikumjibu. Niliondoka. Wala sikurudi kwenye banda lake la kuchangia na fisi. Nilipitiliza kuifuata njia iliyonifikisha katika mji huo. Nilitembea taratibu hadi mjini. Alfajiri ilinikuta nikipitapita katika mitaa ya mji huo. Jua lilipochomoza lilinikuta nimeketi kando ya ziwa Singidani nikitazama pilikapilika za wavuvi.
Sikuwa na wazo jingine zaidi ya kutafuta gari litakalonipeleka kokote kwenye usalama. Sikuwa tena na hamu ya kuendelea kuivinjari Singida.
Niliuliza mahala wanapopandia magari ya kwenda mikoani, nikaonyeshwa. Sikusita kulipia nauli ya kwenda Kilimanjaro na kuianza safari mara moja.

17
Ben R. Mtobwa











SURA YA KUMI NA SABA

Kilimanjaro, Paa la


N
ilikuwa nimesikia mengi ju ya Kilimanjaro, mlima mrefu kuliko wote barani Afrika. Hali kadhalika, nilisoma mengi na kutazama picha nyingi
zilizoonyesha mlima huo. Lakini katika yote hayo niliyosikia au kuona kwenye picha hakukuwepo lolote lililoniacha nisiweze kupigwa na butwaa huku nikiwa siyaamini macho yangu pale nilipoutia machoni mlima huu. Kwa kweli, ni mlima ambao lazima uuone, kusimuliwa pekee kulikuwa hakutoshi.
Ilikuwa ndio kwanza nashuka toka katika basi lililonileta mjini hapo, macho yangu yalipopokelewa na utukufu ule. Ujio wangu Kilimanjaro ukiwa umefanyika bila matarajio baada ya yale mapokezi ya kutisha niliyoyapata Singida. Mapokezi ya kulazwa chumba kimoja na fisi.
Ni mawazo hayo yaliyofanya Singida kama nuksi nyingine iliyokuwa ikinisubiri. Hali iliyopelekea baada ya siku mbili tatu za kuzurula mjini hapo nipande basi lililonileta Kilimanjaro, kwa matarajio ya kupata kazi au biashara yoyote ambayo ingeniwezesha kupata chochote ili nitimize azma yangu ya kurudi nyumbani. Azma ambayo umuhimu wake uliongezeka siku baada ya siku.
Mlima ulisimama pale kwa kiburi na fahari zote. Ulikuwa​



peke yake, ukiwa umechomoza hadi juu ya mawingu, kiasi cha kujionyesha vizuri popote uliposimama katika eneo la miji kama Moshi, arusha na vitongoji vyake. Ukiwa umepambwa kwa theluthi iliyokuwa ikimeremeta kileleni, Kilimanjaro ulisimama pale, peke yake, kama mfalme aliyevalia taji lake ambaye hakuwa na mpinzani. Hapana, alionekana zaidi kama malkia mwenye majivuno, aliyevalia mapambo yake yote, ambaye hakupenda kujichanganya na watu wengine. Sijui ningeukodolea macho kwa muda gani mlima huo kama nisingehisi kushikwa bega huku sauti ya mtu mmoja ikisema, “Angalia, yasije yakakukuta yaliyomkuta Rebmen kwa kuushangaa mlima huo.”
Nikazinduka. Nikayaondoa macho yangu toka kileleni na kumtazama msemaji. Alikuwa mpita njia tu, mvulana aliyevaa mavazi ya shule, mfuko wa madaftari yake ukiwa kwapani. Alikuwa akitabasamu.
“Rebmen gani?” nilimuuliza.
“John Rebmen. Yule Mjerumani aliyekuwa Mzungu wa kwanza kuutia machoni mlima huu,” alifafanua.
Nikalikumbuka jina hilo. Nikakumbuka pia tarehe na mwaka ambao Rebmen aliuona mlima huo kwa mara ya kwanza. Ilikuwa Mei 11, 1848.
“Rebmen alifanya nini?” niliuliza.
“Hukumbuki?” mwanafunzi huyo alinihoji. “Hukumbuki yaliyompata? Hukumbuki kuwa aliibiwa mfuko wake uliokuwa na fedha zake, nyaraka zake na kumbukumbu zote za safari yake? Ulivyokuwa umeduwaa pale wewe pia ungeweza kuporwa huo mfuko wako bila kujijua”
Nikacheka. Nilikumbuka kusoma tukio hilo kwenye kitabu cha mwandishi mmoja. Nadhani alikuwa Rebmen
 
SEHEMU YA 107

mwenyewe aliyeandika. Kwamba akiwa Kilimanjaro, maeneo ya kibosh, aliibiwa mfuko wake uliokuwa na fedha zake zote na nyaraka zake zote muhimu. Siku hizi watani wa Wachaga, hasa Wapare, hulitumia tukio hilo kuwadhihaki Wachaga kuwa kwa ajili ya tukio lile Rebmen aliyekuwa mmisionari aliwalaani hata wakawa watu wa kupenda na kuabudu sana pesa kuliko utu. ‘Mchaga mzuri ni aliyekufa tu,’ ni moja ya kauli zinazoendana na utani huo.
Ingawa sikumbuki kama kweli Rebmen aliibiwa wakati akiushangaa mlima lakini bado nisingeweza kumlaumu. Kwa mtu kama yeye, aliyetoka mbali sana na ambaye hakupata kusikia wala kuona picha ya mlima huo kama mimi, kuduwaa kiasi cha kuibiwa begi lake kamwe lisingekuwa jambo la ajabu. Kitendo cha ardhi kuchomoza hadi meta 5894 juu usawa wa bahari, huku ukiwa umesimama peke yako siyo jambo la kawaida. Aidha, ile theluji kileleni na historia ya milipuko ya volkano katika vilele vyake vitatu vya Kibo, Mawenzi na Shira ni sababu nyingine za kihistoria ambazo zitamfanya mtazamaji aukodolee macho hata kuweza kuporwa begi lake.
Hata hivyo, kauli ya mtoto yule wa shule ilinifanya nianze tena kutembea mitaani, begi mkononi, macho yakiwa hayakomi kurudi kwenye kilele cha mlima mara kwa mara.
Mji huu wa Moshi, ulio mbali kwa kilomita 580 toka Dar es Salaam na 76 toka Arusha, uko kilomita 890 toka usawa wa bahari. Hesabu ya watu wa mwaka 1948 ilionyesha kuwa mkoa mzima wa Kilimanjaro ulikuwa na idadi ya watu wapatao 267,700.
Hiyo ilikuwa sehemu ya akiba yangu ya kumbukumbu juu ya Kilimanjaro. Sehemu nyingine ilikuwa juu mkazi mkuu wa mkoa huo, Mchaga. Wakati watu wengi walifahamu



kuwa Wachaga ni kabila moja, linaloongea lugha moja, mimi nilikuwa na taarifa tofauti. Wakiishi kusini mwa mlima Kilimanjaro Wachaga ni mkusanyiko wa makabila mbalimbali, wanaozungumza lugha mbalimbali wakiwa wametoka katika maeneo mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Watu hawa, ambao kwa bahati wote ni wabantu, baadhi yao wanafananishwa na Wakamba wa Kenya kwa siha na lafudhi. Wengine wanafaninishwa na wataveta na hata watu wa Niger na Kongo. Wataalamu wanahisi watu hawa walivutwa na hali ya hewa, mbali na utajiri wa misitu kwenye mteremko wa mlima tangu karne ya kumi na saba. Hali iliyowawezesha kuwa wakulima wakubwa wa mibuni kama zao la biashara na migomba kwa ajili ya chakula.
Miongoni mwa makabila yanayounda Wachaga ni pamoja na Warombo, Wamachame, Wavunjo na Wamarangu. Inaaminika kuwa katika zama zile za kuhamia Kilimanjaro makabila haya, ambayo yalikuwa na falme tofauti kama zilivyo lugha na tamaduni zao walipigana vita mara kwa mara. Kabila jingine maarufu Kilimanjaro, Wapare, lilitumia fursa hiyo kwa manufaa yao kiuchumi. Inaaminika Wapare walikuwa wafua vyuma mashuhuri ambao koo mbalimbali za Wachaga ziliwategemea kuundiwa silaha mbalimbali kama mikuki mishale na mapanga kwa minajili ya kujipatia ushindi dhidi ya koo nyingine.
Nilijikumbusha hayo wakati nikitembea taratibu toka kituoni hapo nikifuata barabara ambayo sikuifahamu, wala sikuwa na haraka ya kuifahamu. Nilikuwa nimejikumbusha nguo zangu za kazi, kaptula na shati la kaki murua ya Marekani, viatu vizito vya dhoruba na soksi nyeusi. Nywele zangu, kama kawaida, zilikuwa fupi zilizochongwa vizuri. Nadhani



nilionekana mrefu kuliko watu wengi eneo hilo. Nadhani pia ngozi yangu ya maji ya kunde, usafi wa mwili wangu na utulivu wangu wakati nikivuta hatua moja baada ya nyingine kutoka kituoni hapo ni miongoni mwa vitu vilivyovutia macho ya wapita njia dhidi yangu. Niliona nikitazamwatazamwa kuliko kawaida, baadhi ya watu walinong’onezana huku vidole vikielekezwa kwangu.
Halafu likatokea jambo ambalo halikupata kutembelea fikra zangu. Kundi kubwa la kinamama liliibuka toka mahala fulani kituoni hapo na kunifuata mbio. Waliponifikia walianza kuimba huku wakipiga makofi na vigelegele.
Babaaa baba huyoo…. Babaa baba huyo…. Baba…
Sikuelewa. Nilisimama na kugeuka huku na huko nikitazama nani anapokelewa na kushangiliwa kiasi hicho.
Hakuwa mwingine zaidi yangu. Walikuwa tayari wamenizingira, mfuko wangu ukapokonywa na mama mmoja kuamua kuubebea yeye. Waliendelea kuimba.
“Karibu sana baba,” mmoja wao alisema huku akinikumbatia.
Nilizidi kuchanganyikiwa. Ama wana wazimu ama mimi napata wazimu! Niliwaza nikijaribu kujibabadua toka katika mikono ya mama huyo.
“Vipi… kuna nini?” nilijaribu kuuliza. Sikusikika. Kelele zilikuwa nyingi. Yule aliyenikumbatia kwanza aliwageukia wenzake na kuwaambia, “Mnaona? Niliwaambia ni mtu mwenye haya sana.” Akawageukia vijana wa kiume waliokuwa kando na kuwauliza, “Mbona hamchangamki? Mpokeeni kishujaa shujaa wetu.”
Kauli hiyo ilifuatiwa na vijana hao wa kiume kunivamia,
 
SEHEMU YA 108

wawili kati yao wakaniinua na kunibeba juu wakiniongoza njia kunipeleka walikokujua. Katika maongezi yao nilisikia mmoja akisemea, “Nilidhani Nyerere ni jitu kubwa, linalotisha na kuwatetemesha wakoloni. Kumbe ni mtu wa kawaida…”
Ndipo nikaeleka. Walikuwa wamenifananisha na Nyerere!
Wakati huo vuguvugu la kudai uhuru likiwa linazidi kupamba moto majina ya akina Julius Nyerere, Oscara Kambona, Bibi Titi Mohamed na wengineo yalikuwa yametawala sana katika vyombo vya habari. Nyerere, ambaye wakati huo alikuwa mwalimu wa shule moja ya sekondari kule Tabora alifahamika zaidi kutokana na maandishi yake katika vyombo vya habari hasa magazeti akiwa msomi aliyefika hadi Makerere, Uganda. Nyerere aliwaandaa Watanganyika kujitawala. Alisema na alisikika sana.
Sikupata kufikiria kama ingetokea siku mimi, Kiguu na Njia nikapokelewa kwa heshima kiasi hicho. Hivyo, lazima nikiri kuwa kwa kiasi fulani nilifurahia nafasi hiyo ya kubebwa. Lakini pia, kwa ajili ya kelele na imani yao kuwa nina haya nilijua wasingeamini chochote ambacho ningewaambia. Nikaamua kutulia tuli juu ya mabega yao nikicheka kimoyomoyo.
Msafara huo uliishia katika nyumba moja ya wageni, mtaa wa tatu kutoka katika kituo hicho. Nilipelekwa moja kwa moja katika chumba maalum kilichoandaliwa kwa ajili ‘yangu’. Kilikuwa na bafu na choo chumbani humo. Mfuko wangu wa safari tayari uliwekwa juu ya meza, salama salimini. Yule mama aliyejipa uenyeji zaidi yangu alisema, “Baba, oga upumzike kidogo. Bibi Titi alifika jana. Nitamwarifu juu ya ujio wako, pengine mtapenda kuteta kidogo kabla ya kuanza safari ya Machame. Chifu Abdieli Shangai atakuwa tayari



amewasubiri.”
“Lakini mimi sio Nyerere,” nilimwonya. “Naitwa…” hakusubiri hata nitaje jina langu. Badala yake aliangua kicheko, akipuuza alichokichukulia kama mzaha wangu. Akatoka huku akiufunga mlango nyuma yake.
Sikuwa na jinsi. Nikaoga. Nikapaka mafuta na kuvuta zile nguo zangu za safari. Nikavaa suruali na shati safi. Nikatia tai na koti juu. Nilifanya hayo kwa uangalifu mkubwa bila kuchafua bafu wala kuvuruga kitanda ili mweye chumba chake halisi atakapotokea akikute kikiwa kisafi.
Wakati nikijiandaa kutoka, nikiwa na dhati ya kuwahakikishia kuwa mimi sikuwa Nyerere, mlango uligongwa nikaufungua. Bibi Titi Mohamed alikuwa pale. Sikuhitaji kutambulishwa. Alikuwa mwanamke mfupi, mnene, mwenye macho maangavu.
“Julius, umeruka kwa ndege? Nilidhani ungefika hapa jioni,” alisema kwa sauti yenye mamlaka. Sauti hiyo ilififia ghafla aliponitazama usoni na kubaini kuwa mimi sikuwa Julius Nyerere waliyekuwa wakimtegemea.
“Nimejitahidi sana kuwaambia mimi sio Nyerere, hawakukubali,” nilijitetea. “Ni kama nimetekwa nyara na kuletwa hapa,” niliongeza.
Bibi Titi aliangua kicheko. Aligeuka kuwatazama wenyeji wetu waliosimama nyuma yake kunisubiri. Kicheko chake kilizungumza kila kitu. Akageuka tena kunitazama, “Pole sana bwana. Ni kweli umefanana sana na mwalimu. Kwa mtu asiyemfahamu vizuri kuwafananisha si ajabu.”
Sikumjibu. Sikuwa na la kujibu zaidi ya kutabasamu.
“Ulikuwa ufikie wapi?” aliniuliza.
“Nilikuwa natafuta mahali pa kupanga.”



“Basi unaweza kulala hapa,” aliniambia. “Malaika wako amekwishakukuongoza hadi chumbani humu, huna sababu ya kupingana naye. Pumzika, baadaye tutakaa tuzungumze. Si ajabu mola kakuleta mikononi mwetu kwa sababu maalum.”
Sikuwa na sababu ya kukataa.

* * *​
Kwa mujibu wa maelezo niliyoyapata baadaye, vuguvugu la wagombea uhuru nchini, chama cha TANU ambacho kilikuwa kimeanzishwa kutokana na TAA kulikuwa na matatizo katika kanda hiyo ya mashariki, hasa Kilimanjaro. Kwa mujibu wa maelezo hayo, matatizo hayo hayakuhusiana na chama kukubalika au kutokukubalika eneo hilo bali yalitokana na mvutano ndani ya Wachaga wenyewe.
Baada ya ule mvutano na mapigano ya makabila mbalimbali yanayounda Uchaga ulifika wakati pamoja na kukubaliana kuwa kitu kimoja. Uamuzi huo ulifuatiliwa na kumteua Mangi mkuu kama msimamizi na msemaji rasmi wa masuala ya Wachaga. Mangi mkuu huyu aliyekuwa na makao yake huko Marangu aliwekwa juu ya viongozi wengine wote wa kikabila.
Hata hivyo, ule mzimu wa chuki na kutokutamaniana miongoni mwao, ingawa ulizikwa, bado haukufa. Ni kama ulizikwa hai. Ujio wa Mjerumani, ambaye alifuata nyayo za mpelelezi wao Rebmen, ulifanyika Kilimanjaro iwe chaguo lao la awali, wakati machifu wengine wakisita kuwapokea. Mangi Sina wa Kibisho, miaka ya 1890 akiwa amejizatiti kiuchumi kwa kilimo na ufugaji, alikuwa pia ameimarisha jeshi lake ambalo lilikuwa kero kubwa kwa utawala wa wajerumani. Awali ya hapo Wajerumani hao, chini ya uongozi wa Karl
 
SEHEMU YA 109

Peters, waliendesha utawala wa kinyama na ukatili mkubwa Kilimanjaro, hali iliyopelekea April 25, 1897 gavana huyo katili afukuzwe kazi na serikali yake.
Lakini miaka mitatu baadaye, Machi 2, 1890 Wajerumani hao waliwanyonga hadharani, mjini Moshi, viongozi tisa wa kikabila. Viongozi mashuhuri kati ya waliopoteza maisha siku hiyo wakiwa Mollelia wa Kibosho, Ngalami na Meli wa Moshi. Madai ya Wajerumani kwa kitendo hicho yakiwa kwamba viongozi hao walikuwa wakiwavurugia jitihada za uongozi wao Kilimanjaro.
Hivyo, mkataba ambao Mangi Rindi wa Chaga aliingia na Mjerumani miaka mitano kabla ya kitendo hicho cha kikatili, na kuufanya mji wa Moshi kuwa kituo kikubwa cha biashara ya ndovu na watumwa kati yake na Zanzibar, lilikuwa pigo jingine katika jitihada za kuifanya Kilimanjaro kuwa na sauti moja.
Ujio wa vuguvugu la kupigania uhuru kukawa kama msumari wa mwisho kwenye jeneza la jitihada hizo. Wakati huo tayari yakiwepo malumbano makubwa ya iwapo kulikuwa na uhalali na haja ya Mangi mkuu kuendelea kutoka katika ukoo na kabila moja na cheo hicho kiende kwa kupokezana au la. Mangi mkuu, wakati huo Chifu, Thomas Mareale na kambi yake walishikilia msimamo wao. Kwa upande mwingine, machifu kama Abdiel Shangali walilipinga hilo kwa vitendo. Wasomi wengi wakiwa nyuma yake, Shangali alitumia fursa hiyo ya mparanganyiko kuunga mkono TANU na kuwekeza kimsimamo mikononi mwa mkewe Solomon Eliofoo, aliyekuwa ametokea masomoni Uingereza na Marekani na kurudi na kuazishwa tawi la TANU Machame.



Lilikuwa tatizo zito kwa Chifu Mareale. Jitihada zake za kuwekeza kwa Petro Njau hazikuzaa matunda yaliyotarajiwa, hali iliyopelekea uhusiano wake na TANU ulegelege. Ingawa yeye binafsi aliwasiliana sana na Nyerere na wakati fulani kumtaka aje Kilimanjaro kuzungumza na Machifu wote bado alionekana kama mtu aliyekuwa njia panda. Hali ambayo baadaye ilishusha umaarufu wake, lakini hadhi yake na nafasi yake katika historia kamwe haikupata kufutika.
Kwa upande mwingine, Kilimanjaro haikuwa na njaa sana ya uhuru kama zilivyokuwa sehemu nyingine za Tanganyika. Kiuchumi alikuwa mbali zaidi. Kilimo cha mibuni kilikuwa kimeanzishwa katika eneo hilo tangu mwaka 1919 na kushika kasi 1930 na kuendelea. Hali hiyo iliambatana na kuanzishwa kwa vyama vya ushirika, ikiwa nchi ya Kwanza Afrika kuwa na mfumo huo. Hali ya hewa na ujio wa mapema wa wakoloni katika maeneo hayo pia ilikuwa neema nyingine kwao. Walipata shule nyingi na bora zaidi mapema.
Huduma za matibabu, barabara na maji pia walizijua
kabla ya maeneo mengi ya nchi kufikiriwa.
Hivyo, inaweza kueleweka pale ‘Mshumbue’ Mangi mkuu Thomas Lenana Mlanga Mareale II aliponukuliwa akishuku kuwa Nyerere ‘alikuwa akinikwepa,’ na kwamba alimsahau katika harakati za uhuru. Hata hivyo, Mangi mkuu huyu aliendesha harakati mbalimbali za kisiasa ndani na nje, ikiwa pamoja na kumlipa wakili ambaye alimtetea Kenyatta wa Kenya hadi akaachiwa toka kifungoni wakati akituhumiwa kujihusisha na Mau Mau.
“Hivyo, ni sehemu fupi ya historia ya uchagani kaka yangu,” Bibi Titi Mohamed alisema baada ya maelezo hayo ambayo niliyaunganisha na kujaribu kuyaweka katika mtiririko





mmoja baada ya huyu kusema hili, huyu lile nikijumuisha na yale yaliyokuwa katika kumbukumbu zangu.

Tulikuwa katika ukumbi wa hoteli hiyo. Watu wapatao wanane, wakiwemo wanawake watano, Bibi Titi na wawili wengine kati ya wale walionipokea pale kituo cha mabasi. Nilionekana kama muujiza. Nadhani hata kama angekuwa Nyerere mwenyewe hangepata idadi kubwa ya watu waliokuwa wakiingia na kutoka kwa nia ya kumwona ‘mtu aliyefanana na Nyerere’. Wingi wa watu hao wakiwa kina mama ambao walicheka na kujicheka sana kwa kosa la kunichanganya na kijana huyo aliyekuwa akitajwatajwa sana. Nadhani kwa namna fulani walidhibitiwa, kwani baadaye tuliketi na kuingia katika maongezi marefu, yaliyoongozwa zaidi na Bibi Titi, mwanamama msemaji sana, mwingi wa vichekesho huku akiwa pia msikilizaji mzuri.

“Wachaga wana historia tofauti na sehemu nyingi za nchi,” Bibi Titi aliongeza. “Sisi watu wa Pwani tuna historia inayotofautiana kwa kiasi kikubwa na wao. Nadhani wageni wengi waliotembelea makwetu toka enzi za enzi waliacha athari nyingi miongoni mwetu zaidi ya Uchagani ambako ni mbali kutokea Pwani.”

“Nadhani,” niliunga mkono. “Maana toka Waarabu, Wareno, Wajerumani na baadaye Waingereza wenyeji wao wa awali ni nyie tu.”

“Bibi Titi alitabasamu. “Tuyaache hayo,” alisema. “Hebu na wewe tuambie yako tukusikie. Ilikuwaje ukafananishwa na bwana Julius?” alinihoji.

“Kwa kweli sijui. Simjui Julius wala sijapata kumtia machoni labda imetokea tu tukafanana maana duniani wawili wawili,” nilimjibu.
 
SEHEMU YA 110

“Huna udugu naye?” “Hata kidogo.” “Wewe ni Mzanaki?” “Wala.”
“Kumbe nini basi.”
“Mie Muha. Natokea kigoma.”
Hufanani na Waha. Utakuwa Mmanyema.” Bibi Titi alidai. “Lakini hilo halina haja kwa sasa,” aliongeza. “Kama hutajali, tuambie wewe ni nani, unatokea wapi na unaelekea wapi.”
Nikawatajia jina langu. Nilitaja pia kazi niliyowahi kufanya ambayo sasa sikuwa nayo. Walivutiwa na taarifa ya safari za hapa na pale katika miji na vijiji mbalimbali vya Bonde la Ufa pamoja na mbuga za wanyama.
“Hujapata kufikiria kujiunga na harakati za kupigania uhuru?” Bibi Titi aliuliza. Akaongeza, “Maana wewe unaonekana ni mtu wa watu. Halafu, unatembea sana. Lakini la muhimu zaidi ni kwamba tungependa kupata mtu wa kwenda kuhamasisha harakati hizi huko kwenu. Ndiyo kuna watu tayari, lakini hawatoshi. Kumg’oa mkoloni siyo mchezo. Inahitajika kila silaha na kila askari.”
Wazo hilo halikupata kunitembelea akilini. Sikuwa na hakika kama mimi ni mtu wa kupanda jukwaani, mbele ya kadamnasi na kuanza kujinadi kuwa mimi ni bora zaidi ya wengine, au kumnadi mtu mwingine kwamba anafaa kuliko mwingine. Kwa ujumla sikupata kuwa na ndoto ya kuwa mwanasiasa maishani mwangu.
Bibi Titi alisoma hayo katika macho yangu. Akatabasamu. “Ni jambo linalohitaji kulifikiria.” Alinena. “Harakati zetu bado ni changa. Hakuna fedha za kulipa mtu wala kulipwa. Kwa



ujumla tunajitolea. Tunachopigania ni uhuru. Ukipatikana kila mtu atakula matunda ya uhuru.”
Alisita, akaitazama saa yake. “Nadhani basi alilopanda Mwalimu linakaribia kufika. Nisingependa akina mama wakampokee mtu mwingine wa watu na watu. Naenda mwenyewe kumpokea. Atafikia hoteli hiihii. Nitakukutanisha naye, pamoja na Kambona, ili uzungumze nao. Nadhani utakuwa tayari umefanya uamuzi.”
Akainuka na kuondoka, alifuatana na wale kina mama wengine na wanaume wawili.
Nilibakia na watu wawili mmoja alikuwa mtu mfupi, mweupe, ambaye kama si kwa ajili ya mvi mbili tatu kichwani ungeweza kumfikiria kuwa ni mtoto mdogo, ingawa umri wake ulizidi wangu kwa mbali sana. Hakuonekana kuwa Mchaga. Na hakuchelewa kunithibitishia hilo pale alipozungumza na mara moja nikabaini lafudhi yake kuwa ya Kipare zaidi.
“Nikweli miminiMpare,”alijibu swalilangu.“Nimeungana hawa watani wangu wajanjawajanja, katika harakati hizi za kupigania uhuru. Tatizo ni hapo utakapopatikana huo uhuru. Mchaga atapenda kuuteka nyara uwe wake, maana Mchanga mzuri ni yule aliyekufa tu.” Alisema akimtazama Mchaga.
Yule Mchaga akacheka. Yeye pia alinizidi umri. Alikuwa amevaa suti ya kijivu, tai shingoni na alishikilia mkoba wa nyaraka mkononi. Uso wake uliojaza ulipambwa na miwani. Hali iliyompa sura ya usomi.
“Achana na wajukuu wetu hao,” aliniambia. “Hao wameshindikana kabisa. Mpare anapata kesi ya kuku, ama kwa kuiba au kuibiwa. Atauza hata ng’ombe ili ashinde kesi hiyo. Kuna mtu hapo?”
Mie pia nililazimika kucheka.


soda.

Waliagiza vinywaji. Wao walikunywa bia mimi nilikunywa

“Bia?” alihoji mmojawao. “Sinywi.”
“Kwa nini? Unaumwa?”
“Hapana. Sijawahi kunywa toka nizaliwe.” Walinitazama kwa mshangao kana kwamba

nimewaambia jambo la ajabu kuliko yote waliyopata kuyasikia. “Kwa umri huo?” Yule Mchaga aliuliza, “Huo ni umri wa

kunywa vitu vya kiutu uzima.” Aliongeza.

“Tatizo ni kwamba sijapata kuitamani wala kuifiria.

Halafu bei yake kubwa mara tatu kuliko soda.” Nilijitetea. “Acha ubahili wa Kipare,” Mchaga alisema akicheka.

Mpare alicheka pia. Lakini alihamisha maongezi na kunitaka nimsimulie juu ya safari zangu za maporini. “Huko ulikokwenda kuna wanyama?”

“Wengi tu.” Nilimjibu “Unaweza kukutana na kundi la nyati wengi kama Ng’ombe wanaofugwa, kundi la twiga utadhani wako kwenye maonyesho na pundamilia kana kwamba wana sherehe.”

“Tembo?”

“Wengi kupita kiasi” “Vifaru?”

“Wengi tu.”

“Umepata kuwaona kwa macho yako?” “Mara nyingi tu.” Nilimjibu.

Mchaga alijaribu kuingilia kati, lakini Mpare alimkatisha kwa maswali yake juu ya wanyama na maeneo tuliyotembelea. Nilipomtajia kuyafahamu kwangu vyema maeneo ya Manyara, Ngorongoro na Tarangire alionekana kuvutiwa zaidi. Nilihisi
 
Back
Top Bottom