Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 111
kuona dalili za udenda zikielekea kudondoka toka mdomoni mwake. Sikuwa na hakika kama niliona vizuri.
“Itabidi tuzungumze kama wanaume baadaye,” aliniambia. “Unatarajia kuondoka lini?”
“Sina haraka,” nilimjibu. “Nitapenda kufika Arusha pia
kabla ya kurejea maporini,” niliongeza.
“Nitakupeleka.” Alidakia. “Mimi ni mwenyeji Arusha kuliko hapa Moshi. Hutohitaji kulala au kula hotelini.”
Mchaga aliangua kicheko cha dhihaka, kicheko kilichofuatiwa na “Ndugu yangu umekwisha. Mpare ajitolee kukupeleka Arusha, akupe malazi na chakula! Kuna jambo hapo,” alisema.
“Atakwisha yeye,” nilijibu, “Maana siye Wamanyema tuna historia ya kula watu. Nitamla mzimamzima kabla yeye hajanila,” kauli ambayo iliniangusha kicheko kirefu.
“Lakini Wapare unawajua vizuri? Wana maradhi yasiyo na dawa ya uchoyo. Wewe na yeye mtakufa njaa hata kabla hujafikiria kumla, huku mkiwa na fedha mfukoni,” aliongeza na hivyo kuongeza kicheko. Sikujua mengi juu ya Wapare zaidi ya ukweli kuwa ni kabila jingine kubwa la Kilimanjaro, wanaishi katika miteremko ya milima ambayo ni sehemu ya mlima Kilimanjaro, na kwamba wao pia wamegawanyika katika sehemu kuu mbili, Wapare wanaozungumza Kingweno, wanaoishi kaskazini na Wachasu waishio Usangi, Kusini. Lugha zao zina aina fulani ya kulandana na zile za Wataveta na Asu wa Kenya.
Enzi za kale Wapare walisifika kwa uganga wa mvua na uhunzi. Uhakika kuwa kabila hili ni la kale ni pale nilipowahi kuona kitabu kitakatifu cha Biblia iliyoandikwa kwa lugha ya Kipare, kilichochapishwa mwaka 1910. Pamoja na ujio huo
wa dini za kisasa Wapare waliendelea na tiba mbalimbali za asili kama maziwa ya Konda badala ya mama kumtibu mtoto mwenye wintu, maradhi ya sangasi yaliyoharibu vinywa vya watoto, majani yaliyoitwa more yaliyotibu ‘Kirumu,’ ‘kiruti’ au ‘kinyoka’, maradhi ya macho kwa watoto wadogo.
Historia ya dini za kigeni Upareni inaanza na mmisheni Jakob Janssen Dannholz, Mjerumani wa madhehebu ya kiluteri ambaye mwaka 1908 alianzisha ‘kazi ya bwana’ huko Mbaga, Upare ya kusini. Aliishi hapo hadi mwaka 1907 alipokamatwa na kuchukuliwa na Waingereza kama mfungwa wa kivita hadi katika kambi yao ya Misri ambako alifariki mwaka mmoja baadaye. Alifariki na umri wa miaka arobaini lakini kazi aliyoianzisha iliishi, ikakua na inaendelea kukua hadi leo.
Kinyume na makabila mengi nchini, wanawake wa Kipare walikuwa mstari wa mbele, pengine kuliko wanaume zao, katika harakati za kupigania uhuru na haki zao. Kumbukumbu zangu toka vitabuni zilinikumbusha mwaka 1946, kule Usangi, pale maelfu ya akina mama walipoibuka na kuanzisha vurumai kubwa wakipinga kulipa kodi. Tukio hilo liliibuka pale Chifu mmoja alipotembelewa na mkuu wa wilaya kwa ajili ya majadiliano. Umati wa wanawake wapatao mia tano waliizingira nyumba hiyo kutaka ufafanuzi juu ya utaratibu wa kodi ambao hawakuafikiana nao. Mkuu huyo alipojaribu kuondoka bila kuwapa ufafanuzi walipandwa na hasira, walianzisha nyimbo huku wengine wakiipiga mawe nyumba hiyo ya Chifu. Tukio hilo lilifuatiwa na maelfu ya wanawake kujiunga katika vuguvugu hilo ambalo lilitikisa serikali ya mkoloni.
Kama Wachaga, Wapare pia walikuwa katika mstari wa
mbele katika kuiunga mkono TAA na baadaye TANU katika mapambano ya kudai kujitawala. Hali hiyo inachukuliwa kuwa ilisaidia kuondoka wazo la kuibuka kwa chama cha kikabila ambacho kingeweza kuwa chini ya ‘PARE UNISI’ ambayo ilikuwa na nguvu nyingi kutokana na mchango wa kiuchumi iliyotokana na kilimo cha mibuni, katani na chai.
“Unasemaje?”
Mpare alinizindua. Nikamtazama.
“Naona uko mbali sana,” aliongeza. “Nilikuuliza unadhani tuondoke lini kwenda Arusha?”
“Nilikuambia sina haraka, kwani hatuonani tena baada ya leo?” nikamuuliza.
“Tutaonana. Bila shaka yoyote.”
Mara akina mama walikwenda stendi kumpokea mwalimu wakaanza kurudi, mmoja baada ya mwingine. Hawakuwa na furaha kama ile waliyoonyesha wakati wakinipokea mimi. Hatukuchelewa kuelewa sababu.
Mwalimu Nyerere hakutokea.
Mchaga aliyekuwa kimya muda mwingi, akishughulikia kinywaji chake alitabasamu kidogo akinitazama. Kisha akasema, “Maadam Nyerere hakuja, na wewe umefanana naye, tutaendelea kukuita Nyerere. Unasemaje?”
Sikumbuki kama nilimjibu.
kuona dalili za udenda zikielekea kudondoka toka mdomoni mwake. Sikuwa na hakika kama niliona vizuri.
“Itabidi tuzungumze kama wanaume baadaye,” aliniambia. “Unatarajia kuondoka lini?”
“Sina haraka,” nilimjibu. “Nitapenda kufika Arusha pia
kabla ya kurejea maporini,” niliongeza.
“Nitakupeleka.” Alidakia. “Mimi ni mwenyeji Arusha kuliko hapa Moshi. Hutohitaji kulala au kula hotelini.”
Mchaga aliangua kicheko cha dhihaka, kicheko kilichofuatiwa na “Ndugu yangu umekwisha. Mpare ajitolee kukupeleka Arusha, akupe malazi na chakula! Kuna jambo hapo,” alisema.
“Atakwisha yeye,” nilijibu, “Maana siye Wamanyema tuna historia ya kula watu. Nitamla mzimamzima kabla yeye hajanila,” kauli ambayo iliniangusha kicheko kirefu.
“Lakini Wapare unawajua vizuri? Wana maradhi yasiyo na dawa ya uchoyo. Wewe na yeye mtakufa njaa hata kabla hujafikiria kumla, huku mkiwa na fedha mfukoni,” aliongeza na hivyo kuongeza kicheko. Sikujua mengi juu ya Wapare zaidi ya ukweli kuwa ni kabila jingine kubwa la Kilimanjaro, wanaishi katika miteremko ya milima ambayo ni sehemu ya mlima Kilimanjaro, na kwamba wao pia wamegawanyika katika sehemu kuu mbili, Wapare wanaozungumza Kingweno, wanaoishi kaskazini na Wachasu waishio Usangi, Kusini. Lugha zao zina aina fulani ya kulandana na zile za Wataveta na Asu wa Kenya.
Enzi za kale Wapare walisifika kwa uganga wa mvua na uhunzi. Uhakika kuwa kabila hili ni la kale ni pale nilipowahi kuona kitabu kitakatifu cha Biblia iliyoandikwa kwa lugha ya Kipare, kilichochapishwa mwaka 1910. Pamoja na ujio huo
wa dini za kisasa Wapare waliendelea na tiba mbalimbali za asili kama maziwa ya Konda badala ya mama kumtibu mtoto mwenye wintu, maradhi ya sangasi yaliyoharibu vinywa vya watoto, majani yaliyoitwa more yaliyotibu ‘Kirumu,’ ‘kiruti’ au ‘kinyoka’, maradhi ya macho kwa watoto wadogo.
Historia ya dini za kigeni Upareni inaanza na mmisheni Jakob Janssen Dannholz, Mjerumani wa madhehebu ya kiluteri ambaye mwaka 1908 alianzisha ‘kazi ya bwana’ huko Mbaga, Upare ya kusini. Aliishi hapo hadi mwaka 1907 alipokamatwa na kuchukuliwa na Waingereza kama mfungwa wa kivita hadi katika kambi yao ya Misri ambako alifariki mwaka mmoja baadaye. Alifariki na umri wa miaka arobaini lakini kazi aliyoianzisha iliishi, ikakua na inaendelea kukua hadi leo.
Kinyume na makabila mengi nchini, wanawake wa Kipare walikuwa mstari wa mbele, pengine kuliko wanaume zao, katika harakati za kupigania uhuru na haki zao. Kumbukumbu zangu toka vitabuni zilinikumbusha mwaka 1946, kule Usangi, pale maelfu ya akina mama walipoibuka na kuanzisha vurumai kubwa wakipinga kulipa kodi. Tukio hilo liliibuka pale Chifu mmoja alipotembelewa na mkuu wa wilaya kwa ajili ya majadiliano. Umati wa wanawake wapatao mia tano waliizingira nyumba hiyo kutaka ufafanuzi juu ya utaratibu wa kodi ambao hawakuafikiana nao. Mkuu huyo alipojaribu kuondoka bila kuwapa ufafanuzi walipandwa na hasira, walianzisha nyimbo huku wengine wakiipiga mawe nyumba hiyo ya Chifu. Tukio hilo lilifuatiwa na maelfu ya wanawake kujiunga katika vuguvugu hilo ambalo lilitikisa serikali ya mkoloni.
Kama Wachaga, Wapare pia walikuwa katika mstari wa
mbele katika kuiunga mkono TAA na baadaye TANU katika mapambano ya kudai kujitawala. Hali hiyo inachukuliwa kuwa ilisaidia kuondoka wazo la kuibuka kwa chama cha kikabila ambacho kingeweza kuwa chini ya ‘PARE UNISI’ ambayo ilikuwa na nguvu nyingi kutokana na mchango wa kiuchumi iliyotokana na kilimo cha mibuni, katani na chai.
“Unasemaje?”
Mpare alinizindua. Nikamtazama.
“Naona uko mbali sana,” aliongeza. “Nilikuuliza unadhani tuondoke lini kwenda Arusha?”
“Nilikuambia sina haraka, kwani hatuonani tena baada ya leo?” nikamuuliza.
“Tutaonana. Bila shaka yoyote.”
Mara akina mama walikwenda stendi kumpokea mwalimu wakaanza kurudi, mmoja baada ya mwingine. Hawakuwa na furaha kama ile waliyoonyesha wakati wakinipokea mimi. Hatukuchelewa kuelewa sababu.
Mwalimu Nyerere hakutokea.
Mchaga aliyekuwa kimya muda mwingi, akishughulikia kinywaji chake alitabasamu kidogo akinitazama. Kisha akasema, “Maadam Nyerere hakuja, na wewe umefanana naye, tutaendelea kukuita Nyerere. Unasemaje?”
Sikumbuki kama nilimjibu.