SEHEMU YA 20
SURA YA TATU
Jiji la Dar es Salaam si dogo. Ni kubwa tosha. Na lina wingi wa watu, watu mbalimbali. Kadhalika, kila mmoja akiwa na shughuli mbali na mwingine. Wakati wengine wakilima, wengine huvua, wakati wengine wakinadi wenginne hufua, na kadhalika.
Hivyo, usiku ule ambao Joram Kiango aliketi katika moja ya baa za Buguruni akimtazama yule msichana mzuri, mtu mwingine alikuwa kajifungia katika chumba chake cha kuchorea; akikamilisha picha yake mpya. Huyu alikuwa Silivano Rashidi, mchoraji ambaye sifa zake zilikwishatapakaa Afrika Mashariki nzima na kupenya hadi ughaibuni. Picha zake zilikuwa nzuri za kuvutia. Kila mtu alitaka awe na moja ya picha hizo katika nyumba yake, lakini si kila mtu aliyeweza kuzinunua kwa ajili ya ukubwa wa bei zake. Hivyo, wateja wake wengi walikuwa matajiri na watalii ambao walikuwa tayari kutoa pesa zozote.
Pamoja na umaarufu wake ni watu wachache sana waliomjua Silivano kwa sura. Hata baadhi ya watu walioishi Buguruni, jirani zake, hawakumfahamu kwa sura zaidi ya kusoma habari zake magazetini. Na waliomwona wakielekea kushindwa kuamini kama kweli huyu ndiye Silivano aliyeweza kuchora picha ainaaina.
Walimwona kama mfupi mno, mkimya mno na asiyejua kitu. Baadhiwalidiriki kumwambia hivyo. Yeye aliwajibu kwa tabasamu akisema, “Ubora wa mtu umo kichwani tu.”
Hata hivyo, waliendelea kushangaa wakidai kwenye miti hakuna wajenzi, kwani ingawa Silivano alikuwa tajiri lakini hakujua namna ya kuutumia utajiri wake