FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #301
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 97
Safari yake ilikuwa ni kuelekea Kinondoni na alikuwa nyuma ya muda hivyo aliitoa gari yake kwa spidi kali mno, kama angekutana na kitu chochote hata kidogo tu barabarani basi angepata ajali moja mbaya ambayo isingeacha hata mfupa wake ukiwa salama. Alifikia kindondoni kwa muda mfupi kutokana na spidi yake, ilikuwa ng’ambo ya eneo kubwa ambalo huwa linatumika kama mnada na muda mwingine watu kufanyia kampeni za biashara zao au siasa ambalo lipo karibu na makao makuu ya OPEN UNIVERSITY ila yeye alikuwa kwa ng’ambo yake.
Kulikuwa kweupe, alikuwa anaonekana mtu mmoja mmoja wengi wakiwa ni wale ambao walitoka kwenye starehe. Watu walionekana kutopita pita kutokana na kwamba eneo hilo Tanesco walikuwa wamepita na umeme wao hivyo maeneo mengi yalikuwa na kiza. Alikunja kushoto kuifuata barabara nyingine ya lami ambayo alinyoosha nayo kwa dakika moja akaiacha gari yake na kubeba silaha zake ambazo zilikuwa kwenye buti yake ya gari. Alitembea kwa dakika moja nyingine akawa amelifikia jengo moja kubwa la kifahari, sehemu hiyo yalikuwa ni makazi ya siri ya mkurugenzi wa shirika la kijasusi la nchi na usalama wa taifa kwa ujumla.
Mwanamama huyo masaa kadhaa nyuma ndiye ambaye alisababisha Aaliyah kuuawa mbele yake lakini kabla mrembo huyo hajafa, alimuomba ahakikishe anamuua mama huyo kwa ajili yake huku akisisitiza kwamba mama huyo kama angeendelea kuishi basi huko mbeleni kungekuwa na matatizo zaidi ya hapo ambayo yalitokea. Mwanamama huyo alikuwa ni mtu wa siri kwa sababu kipindi hicho serikali haikuwa ikiwatangaza hadharani wakurugenzi wa eneo hilo nyeti la usalama kwa sababu za kiusalama hivyo ikapelekea kutokujulikana kabisa kwa watu.
Kutofahamika kwake kulimfanya kuwa na maisha ambayo sio ya ulinzi mkali kila sehemu ili kutoleta maswali mengi kwa watu, alikuwa na nyumba zake nyingi lakini hiyo ilikuwa ni sehemu yake ya siri ambayo mara nyingi alikuwa akiitumia kwa ajili ya kupumzika baada ya kukamilisha mambo yake na eneo hilo lilikuwa na ulinzi lakini walinzi hawakuwa wengi ili kutozua maswali kwa watu wa Kinondoni kwani kushinda na ulinzi mkali awapo maeneo hayo ingezua minong’ono ambayo huenda ingepelekea watu kuanza kumhisi ama kujua anacho kifanya na jambo hilo lingekuwa ni hatari kwa usalama wake na siri za nchi kwani yeye alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa na siri nyingi za taifa.
Kwenye mkono wake alikishika kisu ambacho alikuwa anakiangalia kisha anaukadiria ule ukuta kwa sababu ulikuwa mrefu kiasi, alihema mara moja akauparamia ukuta ule ambapo alichomeka kisu kile akakiacha kimeshika ukutani, alikitumia kama ngazi akakikanyaga na kurukia juu ya ukuta baada ya kugundua kwamba ukuta ule haukuwa na nyaya za umeme zaidi ya Vyuma vikali. Alichungulia ndani kwa sababu nyumba hiyo ilikuwa na umema kwa mbali aliona kuna watu wanaranda randa wakiwa na silaha, aligundua kabisa ni wanajeshi, aliishikiza miguu yake kwenye vile vyuma akainamia ule upande wa chini alipokuwa amekichomeka kisu chake kikali, alifanikiwa kukishika na kukichomoa.
Baada ya hapo alijigeuza na kujivutia tena juu, aliruka sarakasi akatua ndani akiwa anakizungusha kisu hicho kwa hasira kali. Alizunguka nyuma akamuona mwanaume mmoja akiwa anaangalia kila upande, alihisi kama aliona kivuli ila hakuwa na uhakika, alirudi nyuma kwa wasiwasi akiwa makini lakini kwenye kona ambayo alifikia ndipo alikuwepo Edison, alimdaka na kuzamisha kisu kwenye shingo yake kwa nyuma, aliichana vibaya na kumtupa mtu huyo hakuwa anafaa tena.
Alizungukia kwa mbele akawaona wanaume wawili wakiwa wanapiga stori, hawakuwa na bahati kuwa kwenye kazi kama hizo halafu wanaziachia. Alikirusha kile kisu ambacho kilitua kwenye paji la uso la mwanaume ambaye alikuwa upande wake wakati huo alikuwa anaenda kwa zigzaga kuelekea hilo eneo, mwanaume ambaye alimshuhudia mwenzake akipingwa kisu cha paji la uso alipigwa na butwaa lakini aligundua kwamba mvamiaji alikuwa nyuma yake, alihitaji kugeuka ila alitulia, kitu cha baridi kilikuwa shingoni kwake. Ni ule upanga ambao aliupenda ulikuwa kwenye mkono wake
“Bosi wako yuko wapi?” mwanaume huyo hakujibu bali alijaribu kutaka kufanya hila kuweza kukabiliana na mtu huyo, alionjwa kidogo shingo ikachanika ikamlazimu kuwa mpole.
“Yupo ndani ghorofa ya pili, kuna mlango mkubwa mwekundu hicho ndicho chumba chake”
“Funguo za huo mlango ziko wapi?”
“Anazo Batoni”
“Batoni ndo nani?”
“Mlinzi wetu mkuu wa hii nyumba”
“Yuko wapi?”
“Yupo ghorofa ya kwanza”
“Huwa anakaa hapo kwa masaa yote?”
“Ndiyo mpaka bosi aamke”
“Mpo wangapi humu ndani?”
“Walinzi tupo sita”
“Hao wawili wengine wako wapi?”
“Wapo sebule…..” hakumaliza sentensi yake alimaliziwa kwa risasi kutoka kwenye bastola ambayo ilikuwa imewekewa kiwambo cha kuzuia sauti.
Aligonga mlango wa kuingilia ndani kistaarabu, kwa ndani zilisikia hatua taratibu zikielekea mlangoni. Mlinzi wa ndani bila shaka alijua kwamba alikuwa ni mwenzake hivyo hakuona taabu kumfungulia, wakati amefungua alibaki ameduwaa akiwa anamkagua mtu huyo kuanzia juu mpaka chini, alikuwa tofauti kabisa ndipo alishtuka akihitaji kunyoosha bastola ambayo ilikuwa kwenye mkono wake. Ulikuwa muda wa mahesabu kwenye biashara, kichwa chake kilifumuliwa kwa risasi akadondoka chini kama gogo.
Kudondoka kwake ndilo kulimshtua mwenzake ambaye alikuwa ameketi kwenye sofa akiwa anasinzia, wote hao walikuwa ni maafisa usalama. Mwanaume yule kushtuka kwake lilikuwa somo jipya endapo angelipata nafasi ya kuweza kuishi kwa mara ya pili, angehitaji kulala hakutakiwa kuwepo kwenye hiyo kazi. Edison alikanyaga kwenye sofa likampa lifti kwa sarakasi ambapo alitua karibu na alipo mwanaume yule, kutua kwake pale kisu kikali kilizama kwenye koo lake akaongezwa risasi ya mdomoni habari yake ikaisha hapo, Edison akaitupa na bastola yenyewe kwa sababu risasi zilikuwa zimeisha hivyo haikuwa na kazi tena wakati huo.
Alitembea taratibu kwenye ngazi kupandish ghorofa ya kwanza mkononi akiivaa ile chuma ya mviringo huku mkono mmoja akiwa na upanga ambao alikuwa anaubana kwenye koti jepesi ambalo lilikuwa kwenye mwili wake. Aliona kama kivuli kinakuja kwa chini akainama, risasi ilipita juu yake ikaenda kukita kwenye ukuta na kuchimba chimba eneo hilo, aliurusha ule upanga ukakita kwenye ukuta kwa sababu mhusika aliukwepa. Bastola ilifungwa kwenye kiwambo chake ili ikitokea dharura walinzi hao waweze kuzuia makelele kumpata bosi wao.
Alijua hali hiyo haikuwa njema hivyo wakati bwana yule anarusha risasi alitembea kwenye vyumba ambavyo vilijengwa pembezoni mwa ngazi zile ili kutengeneza balansi nzuri wakati mtu anashuka na kupanda. Alitua karibu na alipo mwanaume yule aliyekuwa na sura ngumu na nyeusi isivyo kawaida, bwana yule alijivuta akiachia risai nyingine ambayo ilitoboa koti la Edison ila haikumpata kwenye mwili wake.
Alirusha mkono wake ambao ulikuwa na ile chuma, bwana yule aliipangua ila alirudi nyuma kwa maumivu kwani mkono wake ulikutanishwa na chuma na sio mkono. Alitaka kuinyanyua tena ile bastola yake ila wakati huo hakupewa nafasi nyingine, baada ya kukutanishwa na chuma cha kichwa kisha akaguswa mbele ya mguu wake ambapo aliyumba akakutana na buti la uso, hakukumbuka hata bastola aliko irushia. Alirudi akiwa na jaziba akiwa anairusha mikono yake yote miwili kwa pamoja, aliizungusha ngumi kwa umaridadi mkubwa ikamkosa Edison na kukita ukutani ambapo mkono huo ulidakwa na kuvutiwa pembeni ukashushwa kwa nguvu.
Mkono ulishushiwa lile eneo ambalo upanga ulikuwepo, hivyo kiganja cha mkono kiliachana na mkono wenyewe, bwana yule aliangalia wakati anaona kiganja chake kinaachiwa chini akaanza kulia. Haikutakiwa kelele, aliinama akihema baada ya kugundua kwamba kisu kilizama katikati ya kifua chake, kilishusha chini kukipasua kifua hicho mithili ya kuku wa sikukuu ambavyo huwa anapasuliwa na mtu mwenye uchu mkali kwa kuipania sikukuu hiyo.
UKURASA WA 97 unafika mwisho.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 97
Safari yake ilikuwa ni kuelekea Kinondoni na alikuwa nyuma ya muda hivyo aliitoa gari yake kwa spidi kali mno, kama angekutana na kitu chochote hata kidogo tu barabarani basi angepata ajali moja mbaya ambayo isingeacha hata mfupa wake ukiwa salama. Alifikia kindondoni kwa muda mfupi kutokana na spidi yake, ilikuwa ng’ambo ya eneo kubwa ambalo huwa linatumika kama mnada na muda mwingine watu kufanyia kampeni za biashara zao au siasa ambalo lipo karibu na makao makuu ya OPEN UNIVERSITY ila yeye alikuwa kwa ng’ambo yake.
Kulikuwa kweupe, alikuwa anaonekana mtu mmoja mmoja wengi wakiwa ni wale ambao walitoka kwenye starehe. Watu walionekana kutopita pita kutokana na kwamba eneo hilo Tanesco walikuwa wamepita na umeme wao hivyo maeneo mengi yalikuwa na kiza. Alikunja kushoto kuifuata barabara nyingine ya lami ambayo alinyoosha nayo kwa dakika moja akaiacha gari yake na kubeba silaha zake ambazo zilikuwa kwenye buti yake ya gari. Alitembea kwa dakika moja nyingine akawa amelifikia jengo moja kubwa la kifahari, sehemu hiyo yalikuwa ni makazi ya siri ya mkurugenzi wa shirika la kijasusi la nchi na usalama wa taifa kwa ujumla.
Mwanamama huyo masaa kadhaa nyuma ndiye ambaye alisababisha Aaliyah kuuawa mbele yake lakini kabla mrembo huyo hajafa, alimuomba ahakikishe anamuua mama huyo kwa ajili yake huku akisisitiza kwamba mama huyo kama angeendelea kuishi basi huko mbeleni kungekuwa na matatizo zaidi ya hapo ambayo yalitokea. Mwanamama huyo alikuwa ni mtu wa siri kwa sababu kipindi hicho serikali haikuwa ikiwatangaza hadharani wakurugenzi wa eneo hilo nyeti la usalama kwa sababu za kiusalama hivyo ikapelekea kutokujulikana kabisa kwa watu.
Kutofahamika kwake kulimfanya kuwa na maisha ambayo sio ya ulinzi mkali kila sehemu ili kutoleta maswali mengi kwa watu, alikuwa na nyumba zake nyingi lakini hiyo ilikuwa ni sehemu yake ya siri ambayo mara nyingi alikuwa akiitumia kwa ajili ya kupumzika baada ya kukamilisha mambo yake na eneo hilo lilikuwa na ulinzi lakini walinzi hawakuwa wengi ili kutozua maswali kwa watu wa Kinondoni kwani kushinda na ulinzi mkali awapo maeneo hayo ingezua minong’ono ambayo huenda ingepelekea watu kuanza kumhisi ama kujua anacho kifanya na jambo hilo lingekuwa ni hatari kwa usalama wake na siri za nchi kwani yeye alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa na siri nyingi za taifa.
Kwenye mkono wake alikishika kisu ambacho alikuwa anakiangalia kisha anaukadiria ule ukuta kwa sababu ulikuwa mrefu kiasi, alihema mara moja akauparamia ukuta ule ambapo alichomeka kisu kile akakiacha kimeshika ukutani, alikitumia kama ngazi akakikanyaga na kurukia juu ya ukuta baada ya kugundua kwamba ukuta ule haukuwa na nyaya za umeme zaidi ya Vyuma vikali. Alichungulia ndani kwa sababu nyumba hiyo ilikuwa na umema kwa mbali aliona kuna watu wanaranda randa wakiwa na silaha, aligundua kabisa ni wanajeshi, aliishikiza miguu yake kwenye vile vyuma akainamia ule upande wa chini alipokuwa amekichomeka kisu chake kikali, alifanikiwa kukishika na kukichomoa.
Baada ya hapo alijigeuza na kujivutia tena juu, aliruka sarakasi akatua ndani akiwa anakizungusha kisu hicho kwa hasira kali. Alizunguka nyuma akamuona mwanaume mmoja akiwa anaangalia kila upande, alihisi kama aliona kivuli ila hakuwa na uhakika, alirudi nyuma kwa wasiwasi akiwa makini lakini kwenye kona ambayo alifikia ndipo alikuwepo Edison, alimdaka na kuzamisha kisu kwenye shingo yake kwa nyuma, aliichana vibaya na kumtupa mtu huyo hakuwa anafaa tena.
Alizungukia kwa mbele akawaona wanaume wawili wakiwa wanapiga stori, hawakuwa na bahati kuwa kwenye kazi kama hizo halafu wanaziachia. Alikirusha kile kisu ambacho kilitua kwenye paji la uso la mwanaume ambaye alikuwa upande wake wakati huo alikuwa anaenda kwa zigzaga kuelekea hilo eneo, mwanaume ambaye alimshuhudia mwenzake akipingwa kisu cha paji la uso alipigwa na butwaa lakini aligundua kwamba mvamiaji alikuwa nyuma yake, alihitaji kugeuka ila alitulia, kitu cha baridi kilikuwa shingoni kwake. Ni ule upanga ambao aliupenda ulikuwa kwenye mkono wake
“Bosi wako yuko wapi?” mwanaume huyo hakujibu bali alijaribu kutaka kufanya hila kuweza kukabiliana na mtu huyo, alionjwa kidogo shingo ikachanika ikamlazimu kuwa mpole.
“Yupo ndani ghorofa ya pili, kuna mlango mkubwa mwekundu hicho ndicho chumba chake”
“Funguo za huo mlango ziko wapi?”
“Anazo Batoni”
“Batoni ndo nani?”
“Mlinzi wetu mkuu wa hii nyumba”
“Yuko wapi?”
“Yupo ghorofa ya kwanza”
“Huwa anakaa hapo kwa masaa yote?”
“Ndiyo mpaka bosi aamke”
“Mpo wangapi humu ndani?”
“Walinzi tupo sita”
“Hao wawili wengine wako wapi?”
“Wapo sebule…..” hakumaliza sentensi yake alimaliziwa kwa risasi kutoka kwenye bastola ambayo ilikuwa imewekewa kiwambo cha kuzuia sauti.
Aligonga mlango wa kuingilia ndani kistaarabu, kwa ndani zilisikia hatua taratibu zikielekea mlangoni. Mlinzi wa ndani bila shaka alijua kwamba alikuwa ni mwenzake hivyo hakuona taabu kumfungulia, wakati amefungua alibaki ameduwaa akiwa anamkagua mtu huyo kuanzia juu mpaka chini, alikuwa tofauti kabisa ndipo alishtuka akihitaji kunyoosha bastola ambayo ilikuwa kwenye mkono wake. Ulikuwa muda wa mahesabu kwenye biashara, kichwa chake kilifumuliwa kwa risasi akadondoka chini kama gogo.
Kudondoka kwake ndilo kulimshtua mwenzake ambaye alikuwa ameketi kwenye sofa akiwa anasinzia, wote hao walikuwa ni maafisa usalama. Mwanaume yule kushtuka kwake lilikuwa somo jipya endapo angelipata nafasi ya kuweza kuishi kwa mara ya pili, angehitaji kulala hakutakiwa kuwepo kwenye hiyo kazi. Edison alikanyaga kwenye sofa likampa lifti kwa sarakasi ambapo alitua karibu na alipo mwanaume yule, kutua kwake pale kisu kikali kilizama kwenye koo lake akaongezwa risasi ya mdomoni habari yake ikaisha hapo, Edison akaitupa na bastola yenyewe kwa sababu risasi zilikuwa zimeisha hivyo haikuwa na kazi tena wakati huo.
Alitembea taratibu kwenye ngazi kupandish ghorofa ya kwanza mkononi akiivaa ile chuma ya mviringo huku mkono mmoja akiwa na upanga ambao alikuwa anaubana kwenye koti jepesi ambalo lilikuwa kwenye mwili wake. Aliona kama kivuli kinakuja kwa chini akainama, risasi ilipita juu yake ikaenda kukita kwenye ukuta na kuchimba chimba eneo hilo, aliurusha ule upanga ukakita kwenye ukuta kwa sababu mhusika aliukwepa. Bastola ilifungwa kwenye kiwambo chake ili ikitokea dharura walinzi hao waweze kuzuia makelele kumpata bosi wao.
Alijua hali hiyo haikuwa njema hivyo wakati bwana yule anarusha risasi alitembea kwenye vyumba ambavyo vilijengwa pembezoni mwa ngazi zile ili kutengeneza balansi nzuri wakati mtu anashuka na kupanda. Alitua karibu na alipo mwanaume yule aliyekuwa na sura ngumu na nyeusi isivyo kawaida, bwana yule alijivuta akiachia risai nyingine ambayo ilitoboa koti la Edison ila haikumpata kwenye mwili wake.
Alirusha mkono wake ambao ulikuwa na ile chuma, bwana yule aliipangua ila alirudi nyuma kwa maumivu kwani mkono wake ulikutanishwa na chuma na sio mkono. Alitaka kuinyanyua tena ile bastola yake ila wakati huo hakupewa nafasi nyingine, baada ya kukutanishwa na chuma cha kichwa kisha akaguswa mbele ya mguu wake ambapo aliyumba akakutana na buti la uso, hakukumbuka hata bastola aliko irushia. Alirudi akiwa na jaziba akiwa anairusha mikono yake yote miwili kwa pamoja, aliizungusha ngumi kwa umaridadi mkubwa ikamkosa Edison na kukita ukutani ambapo mkono huo ulidakwa na kuvutiwa pembeni ukashushwa kwa nguvu.
Mkono ulishushiwa lile eneo ambalo upanga ulikuwepo, hivyo kiganja cha mkono kiliachana na mkono wenyewe, bwana yule aliangalia wakati anaona kiganja chake kinaachiwa chini akaanza kulia. Haikutakiwa kelele, aliinama akihema baada ya kugundua kwamba kisu kilizama katikati ya kifua chake, kilishusha chini kukipasua kifua hicho mithili ya kuku wa sikukuu ambavyo huwa anapasuliwa na mtu mwenye uchu mkali kwa kuipania sikukuu hiyo.
UKURASA WA 97 unafika mwisho.