Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 88

“Yuko wapi baba yangu?” aliuliza lakini hakuna ambaye alijihangaisha kuweza kumjibu.
“Nawauliza yuko wapi baba yangu?”
“Kuna kazi nahitaji uifanye kwa ajili yangu ndiyo maana upo hai mpaka sasa”
“Siwezi kuongea na wewe lolote mpaka nijue hali ya baba yangu”
“Baba yako amerudishwa nyumbani, kazi yake ilikuwa rahisi tu kukuleta wewe kwangu kisha nikamalizana naye baada ya wewe kufika. Kwa sasa familia yako itakuwa salama kwa muda mfupi tu kama utakubali kuifanya kazi hii basi mimi nitaiacha salama ila kama utagoma basi nitaua kila mtu kwenye familia yako nadhani unajua kabisa kwamba kwa sasa mimi sina cha kupoteza kwenye huu ulimwengu” Damasi alimeza mate kwa shida akiwa anahema kwa wasiwasi mwingi.
“Kazi gani hiyo?”
“Nahitaji unikutanishe na Yohani Mawenge pamoja na bosi wake au Yohani mwenyewe tu atatosha”
“Hilo ni jambo ambalo haliwezekani kwa sababu bosi sijawahi kupata nafasi ya kukutana naye hata Yohani anako kaa sikujui, huwa anatutafuta mara moja moja sana kukiwa na kazi maalumu ya kufanya”
“Mpaka huwa anawatafuta maana yake una namna ya kuweza kumfikia, nahitaji unikutanishe naye kwa namna yoyote ile kama hautaweza kufanya hivyo basi unajua kinacho enda kutokea”
“Na ukikutana nao una mapango gani?”
“Kinacho fuatia huko mbele wewe hakikuhusu, nimeingia makubaliano na baba yako kwamba ukikubali kufanya kazi yangu nitakuacha uishi na siri yako ya kudanganya kifo utabaki nayo mwenyewe ila kama ukigoma basi inatakiwa kurudi maiti nyumbani kwake”
“Nitaifanya ila naomba sana usiifanye chochote familia yangu”
“Natarajia baada ya hapa utakuwa mtu mwema, sitegemei kuja kukutafuta tena kwa sababu kama hii ambayo imetukutanisha leo” Damasi alitikisa kichwa chake. Edison alimfungulia mwanaume huyo na kumpa vidonge vya kutuliza maumivu kwani mwili wake bado ulikuwa na maumivu makali, alikunywa dawa hizo na kujinyoosha. Alimtoa mpaka nje na kumruhusu aweze kuondoka lakini jambo hilo Nicola hakufurahishwa nalo kabisa.
“Hili ni kosa kubwa unalifanya kumruhusu aweze kupafahamu tunapo ishi, huoni kama anaweza kurudi kwa mara nyingine tena hapa akiwa na mpango mwingine kichwani?”
“Atakuwa hayapendi maisha yake kwa sababu atakuwa amejichimbia kaburi ambalo nina uhakika kwa kilicho tokea hayupo tayari kufanya hivyo lakini kama akifanya hivyo pia atakuwa kanisaidia mimi kuwapata kirahisi watu hao hivyo waache waje” Edison alionekana kujiamini isivyokuwa kawaida hali iliyo anza kuleta mashaka kwa Nicola, wanadamu hawakutakiwa kuwekewa imani.

Aaliyah alikuwa ofisini kwake akiwa mwingi wa mawazo, ni asubuhi hiyo tu alikuwa ametoka kushuhudia mauaji ya makamu wa raisi namna yalivyokuwa, kichwa chake hakikuwa sawa. Edison alikuwa anaonekana wa kawaida machoni ila matukio yake yalikuwa ni ya kutisha isivyokuwa kawaida, alipiga hesabu zake zikagoma, yaani mtu anamuua makamu wa raisi halafu anataka sura yake ionekane? Kivipi? Hakuwa na jibu la moja kwa moja lakini alihisi kwamba mtu huyo huenda alijua hawawezi kutangaza hadharani kwamba yeye amehusika kwa sababu umma ulikuwa unajua kwamba amekufa ama watu hao kufanya hivyo wangekuwa wanaanza kutoboa siri zake mwenyewe.
Aliachana na hayo mawazo na kuingia kwenye chumba cha mikutano ambako wenzake watatu Jumapili Magawa, Davidi Mbatina na Ruben Magesa walikuwepo. Hatua zake za kinyonge ziliwapa ishara wenzake kwamba mambo hayakuwa sawa hata yeye alikuwa anawaangalia watu hao kwa macho ya mawenge makubwa kwa sababu hakuwa akiwaamini tena, alihisi watu hao walikuwa wanamzunguka na kula sahani moja na bosi wake na muda wowote bomu lilikuwa linamlipukia hivyo alitakiwa kwenda nao kwa akili hususani baada ya kugundua kwamba usiku wa jana alikuwa anafuatiliwa na Jumapili ambaye alikuwa amejikausha kama hakuna jambo ambalo lilikuwa limetokea kabisa.
“Jumapili unaweza ukaniambia uliishia wapi kwenye ile kazi ya kuifuatilia familia ya Damasi kujua kilicho tokea mpaka akadanganya kifo?”
“Ndiyo nilifuatilia kwa umakini lakini familia yake inaonekana kutojua lolote na kaburi lake lipo vile vile”
“Lakini kuna taarifa kwamba askari polisi ambaye alikuwa anaitwa Julius alifukua kaburi hilo na kwenda kufanya vipimo juu ya ukweli wa jambo hilo lakini usiku huo huo alikutwa amekufa huko ufukweni, una taarifa yoyote kuhusu hili labda?” walikuwa kama wanachorana sasa kila mtu hakuwa na uhakika na mwenzake.
“Hizo ni taarifa ngeni kabisa kwangu kwani mzee Kazimoto anasema kwamba askari huyo alienda huko tu kufuatilia jambo hilo lakini hakufanya hayo yote ya kufukua kaburi”
“Una uhakika?”
“Ndiyo kiongozi”
“Sawa, kuna taarifa mbili mbaya” wote walibaki wamemtumbulia macho kusubiri atoe taarifa hizo”
“Ya kwanza ni kifo ambacho kimefichwa ila ni kwamba bondia maarufu Wilson Ndamaru alikutwa amekufa ila inaonekana kuna watu wanajaribu kuhitaji kulificha jambo hili” wote walibaki wametulia bila hata kushtuka maana yake hiyo taarifa walikuwa nayo, alishangazwa na jambo hilo kwamba vijana wake wanapataje taarifa ambayo hata yeye hana? Alibaki ameduwaa tu akaishia kujicheka maana alionekana kama mjinga mbele yao.
“Kwahiyo mnajua hata ambao wapo nyuma ya hili?”
“Hapana”
“Mbona mna taarifa hizi na hakuna hata mmoja wenu ambaye amethubutu kuniambia?”
“Tulijua utakuwa nazo”
“Basi nina uhakika hata hizi habari zingine mtakuwa nazo haina haja ya kuwaambia” aliongea kwa hasira ila alijaribu kujizuia kwa sababu wenzake ni moja kwa moja walikuwa wanamtenga halafu kibaya alikuwa ndiye kiongozi. Angeweza kuwawajibisha kama angejua mkurugenzi yupo upande wake lakini alijua kabisa mkurugenzi hawezi kumuelewa ukzingatia kwa yale ambayo aliyasikia kwa kiongozi huyo kwenye simu.
Aliukunja mkono wake kwa hasira huku akiwa anauma meno yake lakini akiwa hajanongeza neno lolote aliingia kijana mmoja akiwa kwenye suti na kifaa cha mawasiliano kwenye sikio lake humo ndani.
“Team leader mkurugenzi anakuhitaji haraka ofisini” aliwaangalia wenzake kwa awamu, hakuongea kitu na kuelekea alikokuwa ameitwa na mkurugenzi wake. Aliingia ofisini na kumkuta mwanamama huyo akiwa anaangalia nje ya dirisha la kioo kizito cha shaba, aligeuka baada ya kugundua kwamba binti huyo alikuwa ameingia humo ndani.
“Umeishia wapi kwenye kesi ambayo nilikupatia?”
“Mwanasheria ameuawa, wananchi wamepaniki wanahitaji majibu ya sababu za kuuawa kwake lakini kwa bahati mbaya imeenda kutengenezwa stori ambayo siyo ya kweli ili kumchafua yeye na Edison bila sababu za msingi kwanini usinge subiri tufanye uchunguzi ndipo tutoe majibu bosi?” mwanamama huyo alimwangalia kwa jicho kali baada ya kutamka kauli hiyo, ni kama alikuwa anaingilia majukumu ya bosi wake na kumuona hajui anacho kifanya.
“Vipi unaona kwamba mimi sijui kuifanya kazi yangu?”

UKURASA WA 88 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 89

“Sina maana hiyo, wewe ndiye ambaye umenifunza yote haya ambayo nayafanya lakini kwa kinacho endelea sasa tunavunja itifaki za kazi zetu, unawezaje kutoa amri itolewe taarifa ambayo hatuna uthibitisho nayo tena bila hata kunishirikisha?”
“Huujajibu swali langu Aaliyah, umeishia wapi kazi ambayo nilikupa?”
“Kuna ugumu wa kupata hizi taarifa kwa sababu ya stori za uongo zinazopikwa nashindwa kujua nianzie wapi na niishie wapi maana hata ushirikiano haunipi” mwamama Lionela Philson aligonga mkono wake kwenye meza kwa nguvu kwa hasira kali maana kijana wake alianza kumpanda kichwani.
“Nisikilize kwa umakini binti, kazi yangu kubwa ni kulinda amani ya taifa hili bila kujali nani atakufa au damu ya nani itamwagika kikubwa kama nchi itakuwa salama bila machafuko kwangu ni sawa. Leo unakuja hapa unaanza kuniimbia ngonjera zako kunifundisha kazi, sasa ni hivi watu wa Ikulu wamekuja hapa na kudai kwamba raisi anahitaji kukuona, utaripoti kila utakacho kiongea na raisi hapa baada ya hapo unasimamishwa kazi mpaka pale nitakapo jiridhisha na mienendo yako ya sasa” Lilikuwa ni onyo lakini pia ilikuwa ni amri ambayo asingeweza kuipinga, jambo hilo alilihisi hivyo lilikuwa ni suala la muda tu. Aliweka kitambulisho chake mezani kwa sababu mpaka wakati huo hakuwa na kazi, aligeuka ili kutoka humo ndani lakini alisimama baada ya kusikia sauti.
“Unajua kama makamu wa raisi amekufa?”
“Hapana sijui” mwanamama huyo hakuongea kitu zaidi ya kugeuza laptop yake ambayo ilikuwa na video fupi ikimuonyesha Aaliyah akiingia mle ndani ya mkuu wa majeshi lakini muda mfupi baadae akatoka pekeyake na kutoka na gari ya mkuu wa majeshi. Lionela alimsogelea binti yule kwa umakini na kutamka
“Hili jambo mpaka sasa wananchi hawajui na viongozi wengi hawajui, tunataka kulifukia kisha atengenezwe mtu mwenye mfanano na makamu wa raisi kwa sababu kama hili likitambulika kwa wananchi lazima kutakuwa na machafuko. Nina uhakika una husika katika hili Aaliyah na baada ya kutoka Ikulu nahitaji majibu ya sababu ya wewe kwenda kule, ulijuaje na una uhusiano gani na mkuu wa majeshi mpaka ndiye ndio muwe watu wa kwanza kujua kilicho tokea. Kama hauhusiki katika hili basi lazima unamjua ambaye amehusika kwa sababu kamera za nje ya eneo lile zinaonyesha wote walio ingia pale ni walinzi wa eneo lile sasa swali la kwamba mheshimiwa amekufa vipi wakati hakuna mgeni aliye ingia ninayahitaji majibu kutoka kwako na baada ya hapo nitakuwa na mazungumzo marefu sana na mkuu wa majeshi” Alimpiga piga begani Aaliyah na kumuacha aende kuonana na raisi kwanza kisha wao wangekaa chini vizuri.
Alimuacha aende kwa wakati huo kwa sababu alijua kwamba binti huyo alikuwa anaijua misingi hiyo ya kazi vyema na asingeweza kukimbia kwani kama angekimbia basi alikuwa anajiingiza kwenye hatia mweyewe. Kwenye mipango yake aliona binti huyo anaanza kuwa kikwazo na huko mbeleni huenda angemletea shida kubwa, zoezi la kwanza lilikuwa ni kumtoa kwenye kuitengo kwanza kwa sababu ingemzuia yeye kupata taarifa za kila siku lakini alihitaji kuutumia muda huo kumchunguza kwa undani ndipo afanye maamuzi. Baada ya Aaliyah kutoka alimuita Jumapili, kijana ambaye alikuwa anafanya naye kazi kwa ukaribu mkubwa kwa wakati huo.
“Aaliyah hatakuwepo tena kazini hivyo kuanzia sasa wewe ndiye kiongozi wa THE RIGHT HAND ila nahitaji umfuatilie kwa umakini Aaliyah kuanzia muda huu na hata baadae akitoka Ikulu basi hakikisha unajua anacho kifanya na anakokwenda maana najua hatarudi hapa kirahisi kwa saabbu anajua nitamuweka ndani. Kama kutakuwa na mazingira yoyote yale ya sitofahamu kuhusu yeye na ukajiridhisha juu ya hilo basi hakikisha unamuua na mwili wake usije kupatikana mahali popote pale” Hayo ndiyo maelezo ambayo yalihitimisha kwamba walikuwa wamamua kumfuta mazima binti huyo kwa kutaka kuwa tofauti na maslahi ya wakubwa wake, haustahili kuendelea kuivuta pumzi ya bure huyo kama kuna mazingira yangeleta walakini zaidi.

Siku ya pili ilikuwa ya mawazo mengi kwa Yohani Mawenge, mwanaume huyu ilikuwa ni mara chache kumkuta kwenye hali ya mawazo lakini alichokuwa ameambiwa na mwalimu wake kilimtisha. Alipewa chaguo gumu la kuweza kumwangamiza bosi wake Madam Kate kama angeshindwa kukamilisha kazi ambayo aliachiwa, alikuwa anawaza namna sahihi ya kuweza kumfikishia ujumbe huo bosi wake lakini hakufanikiwa kujua ni kwa jinsi gani angemwambia na akamuelewa kwani alikuwa anamheshimu mno mwanamama huyo kwa sababu muda mrefu alikuwa anamtunza vyema na kumpa kila kitu.
Alikuwa anawaza huku cigar zikiwa zinateketea kwa fujo huku kitandani kwake kukiwa na wanawake wawili warembo mno ambao walikuwa uchi. Aliangalia saa yake ya mkononi, muda ulikuwa umeenda ila aliichukua simu yake na kuitafuta namba ya bosi wake, alipiga mara moja ikapokelewa.
“Bosi samahani upo nyumbani kwenye nyumba ya Kigamboni?”
“Ndiyo kuna nini?”
“Ni jambo la dharura, gumu na mhimu kwa upande wako naomba tuonane saivi”
“Asubuhi unakuja huku kuna ulazima gani wa kuonana saivi?”
“Naomba iwe hivyo, nina uhakika walinzi waliopo wanatosha, tukutane kwenye daraja la Tanzanite” hakujibiwa simu ikawa imekatwa, ukimya wa bosi wake aligundua kwamba alikuwa amekubali kukutana naye hivyo alivaa haraka warembo wake wakiwa wamelala kwa kulaliana lakini hakujali, alitoka ndani na kuondoka.
Alifika darajani hapo na kutulia huku akivuta moshi kwa mbwembwe, mji ulikuwa kimya kwa sababu ulikuwa ni usiku wa manane. Jiji la Dar lilikuwa linavutia mno majira ya usiku likisindikizwa na upepo mkali wa bahari, alisubiri kwa nusu saa ndipo alipo ona msafara wa gari tano ukiwa unaingia hapo alipokuwepo, walishuka wanaume kadhaa na kukagua eneo la tukio ndipo bosi akashuka kwenye gari na kumsogelea Yohani pale alipokuwepo Yohani.
“Kuna tatizo gani mpaka unanisumbua usiku huu”
“Kuna taarifa mbaya kutoka ngazi za juu”
“Kivipi hiyo taarifa ipitie kwako?”
“Mr Nikolai Gibson anadai kwamba alikupigia simu lakini hakukupata hewani hivyo akaniita mimi kunipa maagizo”
“Yapi?”
“Ilikuwa ni siku ya jana nilipo onana naye nilihisi huenda anatania ila leo amesisitiza tena kwa kutuma barua ambayo nimeikuta mlangoni nahisi alijua kwamba sijakwambia. Wakubwa wanadai kwamba tumekuwa na uzembe mkubwa kwenye majukumu ya kazi siku hiizi kiasi kwamba siri zinasambaa kirahisi na mambo ya hovyo yanatokea ambayo yanazalisha minong’ono hivyo linaweza kuwa suala la muda kabla kila kitu hakijaanza kuharibika”
“Nenda kwenye pointi ya msingi”
“Ni kwamba tumepewa masaa sabini na mawili ya kumpata Edison na kumuua, kama tukishindwa kufanya hivyo basi mimi na wewe tunatakiwa kufa kwa sababu kuishi kwake huyu mtu imekuwa tatizo kwa upande wao” mwanaume huyo kwanza alidanganya kwa kujihusisha yeye kwenye jambo hilo kwa sababu yeye ndiye alitakiwa kumuua mama huyo kama mambo yangeharibika. Madam Kate alihema kwa shida akionekana naye kusombwa na dimbwi la mawazo akahitaji kijana wake huyo amuwashie sigara kwanza kukiweka kichwa chake sawa.
“Wametoa muda gani?”
“Masaa sabini na mawili”
“Ambayo ilikuwa ni jana?”
“Ndiyo”
“Kwahiyo mpaka sasa bado masaa mangapi?”
“Arobaini na manane”
“Umefanya ujinga kushindwa kuniambia mapema kuhusu hili. Wanajua kwamba ule mzigo ulipotea?”
“Sina hakika kwa sababu hakuliongelea kabisa hilo”
“Kitu cha kwanza tuupate mzigo na kuupata mzigo Nicola anatakiwa kupatikana kwa gharama yoyote kwa sababu anaonekana ameshashtuka ndiyo maana amepotea na baada ya hapo ndipo Edison anatakiwa kupatikana kabla ya huo muda ambao umetajwa”
“Sawa bosi, hilo naenda kulifanyia kazi mapema kuanzia asubuhi”
“Unaanzia wapi?”

UKURASA WA 89 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 90

“Najua kama hawa watu wameanza kutujua basi lazima kuna mtu atakuwa anatufuatilia kuanzia ofisini hivyo kwa sasa wewe hata kwa bahati mbaya hautakiwi kugusa ofisini kwa namna yoyote ile kwa sababu wanaweza wakapata kujua unapo ishi, mimi nitashinda pale kuona kila mtu ambaye atakuwa anaingia na kutoka na kama ikifika mpaka usiku bila chochote basi kuna watu nitakutana nao nina imani mpaka kesho asubuhi nitakuwa na majibu juu ya hilo”
“Sitegemei kuona kuna kosa lolote unalifanya Yohani kumbuka wewe ndiyo kama mkono wangu wa kulia”
“Nakuahidi bosi”
“Unajua kama Edison amemuua makamu wa raisi?”
“Ndiyo, alikuwa ni mmoja wa wale watu watano ambao nilikuwa nafanya nao kazi kwa ukaribu. Kama amefanikiwa kumfahamu yule basi hata mimi kuna asilimia nyingi anajua kila kitu kunihusu ukiongezea na kumkamata Saimon, mpaka sasa sipo salama huenda anategea ufike muda mwafaka aweze kufanya tukio ambalo hatujalitarajia”
“Kuna umuhimu ukaongea na raisi anaweza kurahisisha jambo hili”
“Nina huo mpango nitaenda Ikulu kuongea naye nadhani kwa mara ya kwanza nitakwenda kukiri mbele yake kwamba nahitaji msaada wake juu ya hili tutumie vyombo vya usalama kudukua kamera zote ndani ya jiji ili tuweze kumpata mtu huyu kirahisi”
“Hilo litachangia kurahisisha kazi yangu pia kwa sababu wale wanaweza kunipa taarifa ambazo zitafanya nimpate kirahisi”
“Usiniangushe Yohani” aliitikia kwa kichwa na kutoa heshima wakati mama huyo anaondoka na kuingia kwenye gari. Yohani alibaki pale pale akiwa anawaza mengi juu ya jambo hilo lilivyokuwa na uzito wa namna yake, alikuwa amefanya kazi nyingi za hatari, alikutana na watu wa kutisha wa kila aina lakini ilikiwa ni mara ya kwanza kwake kukutana na mtu ambaye alifanikiwa kumsumbua kichwa namna hiyo kama ambavyo alikuwa akiwafanyia Edison. Aliunganisha matukio kuanzia kwa yule mwanasheria mpaka kuigiza kwake maisha ya kujifanya ni mshika kalamu kumbe ni pandikizi, alijua kabisa kuzidiwa akili na mwanasheria yule ndiyo sehemu kubwa ambayo walifeli. Yule mtu alitakiwa kuuawa mapema hayo yote yasingefika ambako walikuwa wamefikia wakati huo, alitupa Cigar yake kwenye maji akaingia kwenye gari yake aina ya Land Rover ya gharama akapotea kwenda kuianza kazi mahususi ya jasho na damu kuhakikisha Edison anapatikana pamoja na Nicola ambaye alikuwa ameuficha mzigo wao wa bei ghali na kushindwa kwake kufanya jambo hilo kungemfanya kuwa na chaguo la kumuua bosi wake ambapo wakubwa waliamini kwamba mwanamama huyo alikuwa hataki kumuua Edison kwa wakati huo kwa sababu alikuwa ni mama yake mzazi.



IKULU
Palikuwa panavutia, ni sehemu ambayo ni ndoto ya wengi kuweza kuwepo ama hata kupata mwaliko tu kuwepo eneo hilo. Aaliyah siku hiyo alikuwa miongoni mwa watu wenye bahati ya kuweza kuwepo Ikulu tena akiwa amepewa mwaliko wake na mheshimiwa raisi, alikuwa amefika muda mrefu lakini alisubirishwa mno kukutana na mtu huyo na baada ya masaa kadhaa alichukuliwa na walinzi kupelekwa alipokuwepo raisi.

Eneo la bustani ambayo ilipandwa kwa ustadi mkubwa ndiko ambako mheshimiwa alikuwepo, alikuwa kwenye hema moja ambayo lilitengenezwa kwa ufundi ili kufanya jua liwe mbali naye, eneo hilo lilikuwa na upepo mtamu huku kwenye meza ya mninga kukiwa na chupa kadhaa za wine. Faraj Asani, raisi wa Tanzania alikuwa amejiinamia kwenye meza hiyo bila shaka alikuwa amemezwa na mawazo ambayo yalimpeleka mbali, alikuwa anawaza mambo mengi kwenye kichwa chake mpaka pale aliposhtuka baada ya kusikia hatua za watu zikija upande wake.
Eneo hilo lilikuwa na ulinzi mkali lakini alikuwa na wasiwasi kwa sababu alijua kuna mamluki wengi walikuwa wamependwa humo.
“Imekuwa ni heshima kubwa kwangu kuweza kuitwa na wewe hapa mheshimiwa, nashukuru kwa nafasi hii adhimu ambayo nimeipata kwako”
“Hii ni sehemu ambayo wengi huwa wanaitamani mno wengine wakiwa tayari kutoa hata maisha ya maelfu ya watu ili wafanikiwe kuingia hapa ila ukifika hapa mambo yanaweza kuwa tofauti na vile ulivyokuwa unayaona ama kusimuliwa na watu wengine. Unaweza kuketi ili unipe kampani ya kupata kinywaji hapa” mheshimiwa alimpa ishara binti huyo kuketi huku yeye akiwa anamimina wine kwa mikono yake mwenyewe jambo ambalo hata Aaliyah lilimshangaza.
“Asante sana mheshimiwa”
“Una miaka mingapi kwa sasa”
“Thelathini”
“Oooh una familia labda?”
“Hapana”
“Ni kwa sababu ya kazi yako eeh?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Nafurahi kuona umejitoa kwa ajili ya taifa lako, kuna muda nchi haiwalipi watu kama wewe kwa namna wanayo stahili kwa sababu inaonekana unatimiza ni wajibu wako. Kwenye maisha haya familia ndicho kitu bora zaidi hivyo ukiona mtu ameamua kutokuwa na familia kwa ajili ya jambo fulani anastahili kupewa pongezi kwa hilo ni hatua kubwa”
“Asante sana mheshimiwa kwa kulitambua hilo, heshima yako ina maana kubwa kwangu”
“Unamwamini bosi wako?” ni swali ambalo lilimshtua na kumshangaza, alihisi lilikuwa ni swali la mtego kwake kwa sababu huyo bosi wake ambaye alikuwa anazungumziwa ni mkurugenzi wake ambaye kimsingi anateuliwa na raisi na hata shirika hilo lilikuwa lipo chini ya raisi kwa sababu ndiye kiongozi wa juu zaidi. Alituliza akili ili asije kujichanganya kwani kwenye kazi yao kupimwa namna hiyo ni jambo la kawaida na ukitoa jibu la hovyo inaweza kuwa hatari kwako kwa kuhisiwa kwamba huenda unaihujumu nchi.
“Ndiyo mheshimiwa, namuamini zaidi ya nafsi yangu” raisi alisikitika akinyanyua bilauri la wine la kuligida mara moja kisha akalitua chini, Aaliyah naye pia alifanya hivyo hivyo.
“Maisha haya ya wanadamu, haupaswi kukiamini kiumbe ambacho kilinyonya kwa mwanamke haijalishi kitakuaminisha vipi. Najua wewe hapo una mafunzo ya kutosha kwamba jambo la kuliamini zaidi ni hisia zako wewe haijalishi umeaminishwa nini hivyo kusema unamuamini kuliko hata wewe mwenyewe sio kweli ila nakuelewa kwa sababu unajaribu kumtetea bosi wako na kumpa heshima kwa kadri ambavyo unapata hiyo nafasi” Raisi alipiga kwenye mshono kiasi kwamba alishindwa hata aongeze nini bibie akabaki ameinama tu. Mpaka wakati huo alijua kwamba hata raisi ni wale wale na kujichanganya kwake hata kidogo hapo alikuwa anafia humo humo Ikulu na mwili wake usingekuja kuonekana maisha yote ambayo yangekuwepo hapa duniani, aliuinua uso kwa ujasiri na kumuangalia mheshimiwa raisi.
“Namuamini kwa sababu ni kiongozi shupavu na najifunza kutoka kwake” hakujali kauli hiyo aliitoa simu yake na kuonyesha nembo moja ya ndege aina ya Tai katikati kukiwa na herufi kubwa mbili “LS”
“Unajua maana ya hizi herufi?” Aaliyah bado alikuwa anaogopa kufunguka kwa kuhisi bado alikuwa kwenye mtego, aliamua kujilipua.
“Ndiyo”
“Maana yake ni nini?”
“LUNATIC SOCIETY, jamii ya siri ambayo inadaiwa kuanzishwa na memba wa zamani wa KGB lakini tuliamriwa kuachana na kuifuatilia baada ya jina lake kuingia kwenye rada za shirika letu kwa kudaiwa kwamba ni nadharia ambazo sio za kweli (CONSPIRACY THEORY) hivyo tutapoteza bajeti bure tu kufuatilia jambo ambalo halipo”
“Safi sana, na wewe uliamini kwamba ni kweli jamii hiyo haipo?”
“Hapana”

UKURASA WA 90 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 90

“Najua kama hawa watu wameanza kutujua basi lazima kuna mtu atakuwa anatufuatilia kuanzia ofisini hivyo kwa sasa wewe hata kwa bahati mbaya hautakiwi kugusa ofisini kwa namna yoyote ile kwa sababu wanaweza wakapata kujua unapo ishi, mimi nitashinda pale kuona kila mtu ambaye atakuwa anaingia na kutoka na kama ikifika mpaka usiku bila chochote basi kuna watu nitakutana nao nina imani mpaka kesho asubuhi nitakuwa na majibu juu ya hilo”
“Sitegemei kuona kuna kosa lolote unalifanya Yohani kumbuka wewe ndiyo kama mkono wangu wa kulia”
“Nakuahidi bosi”
“Unajua kama Edison amemuua makamu wa raisi?”
“Ndiyo, alikuwa ni mmoja wa wale watu watano ambao nilikuwa nafanya nao kazi kwa ukaribu. Kama amefanikiwa kumfahamu yule basi hata mimi kuna asilimia nyingi anajua kila kitu kunihusu ukiongezea na kumkamata Saimon, mpaka sasa sipo salama huenda anategea ufike muda mwafaka aweze kufanya tukio ambalo hatujalitarajia”
“Kuna umuhimu ukaongea na raisi anaweza kurahisisha jambo hili”
“Nina huo mpango nitaenda Ikulu kuongea naye nadhani kwa mara ya kwanza nitakwenda kukiri mbele yake kwamba nahitaji msaada wake juu ya hili tutumie vyombo vya usalama kudukua kamera zote ndani ya jiji ili tuweze kumpata mtu huyu kirahisi”
“Hilo litachangia kurahisisha kazi yangu pia kwa sababu wale wanaweza kunipa taarifa ambazo zitafanya nimpate kirahisi”
“Usiniangushe Yohani” aliitikia kwa kichwa na kutoa heshima wakati mama huyo anaondoka na kuingia kwenye gari. Yohani alibaki pale pale akiwa anawaza mengi juu ya jambo hilo lilivyokuwa na uzito wa namna yake, alikuwa amefanya kazi nyingi za hatari, alikutana na watu wa kutisha wa kila aina lakini ilikiwa ni mara ya kwanza kwake kukutana na mtu ambaye alifanikiwa kumsumbua kichwa namna hiyo kama ambavyo alikuwa akiwafanyia Edison. Aliunganisha matukio kuanzia kwa yule mwanasheria mpaka kuigiza kwake maisha ya kujifanya ni mshika kalamu kumbe ni pandikizi, alijua kabisa kuzidiwa akili na mwanasheria yule ndiyo sehemu kubwa ambayo walifeli. Yule mtu alitakiwa kuuawa mapema hayo yote yasingefika ambako walikuwa wamefikia wakati huo, alitupa Cigar yake kwenye maji akaingia kwenye gari yake aina ya Land Rover ya gharama akapotea kwenda kuianza kazi mahususi ya jasho na damu kuhakikisha Edison anapatikana pamoja na Nicola ambaye alikuwa ameuficha mzigo wao wa bei ghali na kushindwa kwake kufanya jambo hilo kungemfanya kuwa na chaguo la kumuua bosi wake ambapo wakubwa waliamini kwamba mwanamama huyo alikuwa hataki kumuua Edison kwa wakati huo kwa sababu alikuwa ni mama yake mzazi.



IKULU
Palikuwa panavutia, ni sehemu ambayo ni ndoto ya wengi kuweza kuwepo ama hata kupata mwaliko tu kuwepo eneo hilo. Aaliyah siku hiyo alikuwa miongoni mwa watu wenye bahati ya kuweza kuwepo Ikulu tena akiwa amepewa mwaliko wake na mheshimiwa raisi, alikuwa amefika muda mrefu lakini alisubirishwa mno kukutana na mtu huyo na baada ya masaa kadhaa alichukuliwa na walinzi kupelekwa alipokuwepo raisi.

Eneo la bustani ambayo ilipandwa kwa ustadi mkubwa ndiko ambako mheshimiwa alikuwepo, alikuwa kwenye hema moja ambayo lilitengenezwa kwa ufundi ili kufanya jua liwe mbali naye, eneo hilo lilikuwa na upepo mtamu huku kwenye meza ya mninga kukiwa na chupa kadhaa za wine. Faraj Asani, raisi wa Tanzania alikuwa amejiinamia kwenye meza hiyo bila shaka alikuwa amemezwa na mawazo ambayo yalimpeleka mbali, alikuwa anawaza mambo mengi kwenye kichwa chake mpaka pale aliposhtuka baada ya kusikia hatua za watu zikija upande wake.
Eneo hilo lilikuwa na ulinzi mkali lakini alikuwa na wasiwasi kwa sababu alijua kuna mamluki wengi walikuwa wamependwa humo.
“Imekuwa ni heshima kubwa kwangu kuweza kuitwa na wewe hapa mheshimiwa, nashukuru kwa nafasi hii adhimu ambayo nimeipata kwako”
“Hii ni sehemu ambayo wengi huwa wanaitamani mno wengine wakiwa tayari kutoa hata maisha ya maelfu ya watu ili wafanikiwe kuingia hapa ila ukifika hapa mambo yanaweza kuwa tofauti na vile ulivyokuwa unayaona ama kusimuliwa na watu wengine. Unaweza kuketi ili unipe kampani ya kupata kinywaji hapa” mheshimiwa alimpa ishara binti huyo kuketi huku yeye akiwa anamimina wine kwa mikono yake mwenyewe jambo ambalo hata Aaliyah lilimshangaza.
“Asante sana mheshimiwa”
“Una miaka mingapi kwa sasa”
“Thelathini”
“Oooh una familia labda?”
“Hapana”
“Ni kwa sababu ya kazi yako eeh?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Nafurahi kuona umejitoa kwa ajili ya taifa lako, kuna muda nchi haiwalipi watu kama wewe kwa namna wanayo stahili kwa sababu inaonekana unatimiza ni wajibu wako. Kwenye maisha haya familia ndicho kitu bora zaidi hivyo ukiona mtu ameamua kutokuwa na familia kwa ajili ya jambo fulani anastahili kupewa pongezi kwa hilo ni hatua kubwa”
“Asante sana mheshimiwa kwa kulitambua hilo, heshima yako ina maana kubwa kwangu”
“Unamwamini bosi wako?” ni swali ambalo lilimshtua na kumshangaza, alihisi lilikuwa ni swali la mtego kwake kwa sababu huyo bosi wake ambaye alikuwa anazungumziwa ni mkurugenzi wake ambaye kimsingi anateuliwa na raisi na hata shirika hilo lilikuwa lipo chini ya raisi kwa sababu ndiye kiongozi wa juu zaidi. Alituliza akili ili asije kujichanganya kwani kwenye kazi yao kupimwa namna hiyo ni jambo la kawaida na ukitoa jibu la hovyo inaweza kuwa hatari kwako kwa kuhisiwa kwamba huenda unaihujumu nchi.
“Ndiyo mheshimiwa, namuamini zaidi ya nafsi yangu” raisi alisikitika akinyanyua bilauri la wine la kuligida mara moja kisha akalitua chini, Aaliyah naye pia alifanya hivyo hivyo.
“Maisha haya ya wanadamu, haupaswi kukiamini kiumbe ambacho kilinyonya kwa mwanamke haijalishi kitakuaminisha vipi. Najua wewe hapo una mafunzo ya kutosha kwamba jambo la kuliamini zaidi ni hisia zako wewe haijalishi umeaminishwa nini hivyo kusema unamuamini kuliko hata wewe mwenyewe sio kweli ila nakuelewa kwa sababu unajaribu kumtetea bosi wako na kumpa heshima kwa kadri ambavyo unapata hiyo nafasi” Raisi alipiga kwenye mshono kiasi kwamba alishindwa hata aongeze nini bibie akabaki ameinama tu. Mpaka wakati huo alijua kwamba hata raisi ni wale wale na kujichanganya kwake hata kidogo hapo alikuwa anafia humo humo Ikulu na mwili wake usingekuja kuonekana maisha yote ambayo yangekuwepo hapa duniani, aliuinua uso kwa ujasiri na kumuangalia mheshimiwa raisi.
“Namuamini kwa sababu ni kiongozi shupavu na najifunza kutoka kwake” hakujali kauli hiyo aliitoa simu yake na kuonyesha nembo moja ya ndege aina ya Tai katikati kukiwa na herufi kubwa mbili “LS”
“Unajua maana ya hizi herufi?” Aaliyah bado alikuwa anaogopa kufunguka kwa kuhisi bado alikuwa kwenye mtego, aliamua kujilipua.
“Ndiyo”
“Maana yake ni nini?”
“LUNATIC SOCIETY, jamii ya siri ambayo inadaiwa kuanzishwa na memba wa zamani wa KGB lakini tuliamriwa kuachana na kuifuatilia baada ya jina lake kuingia kwenye rada za shirika letu kwa kudaiwa kwamba ni nadharia ambazo sio za kweli (CONSPIRACY THEORY) hivyo tutapoteza bajeti bure tu kufuatilia jambo ambalo halipo”
“Safi sana, na wewe uliamini kwamba ni kweli jamii hiyo haipo?”
“Hapana”

UKURASA WA 90 unafika mwisho.
Daaaaah 🔥🔥🔥
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA KWANZA

SURA YA 1.
MIMI NI NANI?

MZIZIMA
Mvua zilizokuwa zimeambatana na upepo mkali zilikuwa zikiendelea kulisumbua jiji la bandari ya Salama, jiji la kale ambalo watu wa zamani walilijua kama mzizima. Mvua hizo ziliwafanya Tanesco wapate kisingizio kizuri kabisa cha kuweza kuukata umeme ambao ulikuwa unaimulika mitaa mbali mbali na kuonyesha umaridadi wake.

Kwenye chumba kimoja maeneo ya Kigogo Mwisho alionekana ndani mwanaume mmoja, kuonekana kwake kulidhihirisha wasiwasi na hofu ambayo ilikuwa imeugubika uso wake na simanzi ikauzidisha upole wa ile sura yake ambayo haikuwa ikionekana vyema huenda kwa sababu ya kukosekana kwa mwanga. Uso wake ulitoa taarifa ya kwamba maisha yake hayakuwa salama ndiyo maana alikuwa hana amani wala kuwa na utulivu wa kutosha, alikuwa ameketi kwenye mkeka ambao ulikuwa umetandikwa chini kwenye chumba kidogo cha hovyo ambacho kiligubikwa na joto kali kwa kukosa nyenzo mhimu za kupambana na joto. Sanjari na hilo udogo wa chumba nao ulichangia kwa kiasi kikubwa.
Mwanaume yule alijizoa kutoka kwenye ule mkeka na kusimama, alijisogeza kwenye dirisha dogo ambalo lilifunikwa kwa tambala kuu kuu lilolokuwa chafu, alifunua kidogo pazia hilo ili kujua kama nje kulikuwa na chochote lakini hakufanikiwa kuona jambo lolote lile zaidi ya radi ambazo zilikuwa inamulika kila wakati kwenye kiza totoro kilicho lifanya jiji hilo kuwa na utulivu ambao sio kawaida yake. Alirudi tena kwenye mkeka wake akiwa anatweta kwa jasho kutokana na joto kali huku akiwa anajifuta jasho hilo kwa kutumia shati lake ambalo lilikuwa mwilini.

Akiwa anaendelea kuhema kwa hesabu maalumu ambazo alizijua yeye na nafsi yake, alihisi kama kuna kitu kinamtekenya kwenye mfuko wake wa suruali, hapo ndipo akakumbuka kwamba kwenye mfuko huo alikuwa amehifadhi kisimu kidogo ambacho alikuwa amekifunga funga kutokana na uchakavu ambao kilikuwa nao. Aliipokea haraka simu hiyo ambayo namba yake haikuwa na jina na kuiweka kwenye sikio lake.
“Ondoka haraka kwenye hilo eneo, una dakika kumi na tano tu za kuyaokoa maisha yako, vinginevyo unakufa” sauti ya upande wa pili iliongea kwa msisitizo kisha simu ikakatwa. Alibaki kwenye mshangao mithili ya mtoto ambaye alikuwa ametelekezwa na mama yake mzazi huku akiamini kwamba alikuwa na usalama wa kutosha kwa sababu mama yake alikuwa karibu.

Alijizoa kivivu huku moyo wake ukiwa unamuenda mbio, alisogea kwenye ule mkeka na kuukunja upande wa juu ambapo eneo hilo kulikuwa na udongo ambao ulijazwa, aliufukua haraka haraka na kukitoa kimfuko cha plastiki. Alikifungua na ndani yake kulikuwa na pesa za kigeni maarufu kama dola huku pembeni yake kukiwa na bastola moja pamoja na kisu kimoja. Alizoa pesa haraka haraka na kuzitupia kwenye mfuko wake, bastola akaipachika kwenye kiuno chake huku kisu akikishika mkononi.
Alipafukia kama alivyokuwa amepakuta mwanzo na kuurudishia ule mkeka kwa mara nyingine tena kisha akanyanyuka na kuanza kutoka nje. Baada ya kufika mlangoni alikuwa amepoteza dakika tatu tayari, aliufungua mlango taratibu kisha akaangaza kila upande ili kuona kama angefanikiwa kuona kile ambacho alikuwa ameambiwa kinaenda kutokea lakini hali ilikuwa shwari kabisa hivyo akajitosa kwenye maji ya mvua na kuanza kutembea haraka haraka ili kuelekea kilipokuwepo kituo cha magari.
Alikunja kona ya kwanza akiwa anapishana na sauti ya kudondoka kwa maji, akakutana na uwazi ambao ulikuwa na mita kama kumi na tano, sehemu ambayo ilimshtua kidogo kwa sababu moyo wake ulimuenda mbio isivyokuwa kawaida. Alitembea haraka haraka ili aweze kulivuka eneo hilo salama huku kwenye mkono wake kisu akiwa amekishikilia vyema, ila hakupiga hatua hata kumi akahisi kabisa kulikuwa na harufu ya mtu ndani ya eneo hilo hali ambayo ilimfanya kupunguza mwendo na kumfanya aanze kutembea taratibu.

Aligeuka kuangalia nyuma yake, hakuona kitu zaidi ya anga ambalo lilikuwa linamcheka hivyo akahitaji kuendelea na safari yake tena lakini nafsi iligoma kabisa, moyo wake ulikuwa mzito na hakuwa mtu wa kuupuuzia huo mlango wake wa sita ambao ulikuwa wa hisia. Alishuka chini kama anajilaza kifudi fudi lakini hakufika chini kwa sababu ule mkono wenye kisu ndio ambao ulitangulizwa kisu ndicho kikafika chini na hata baada ya kufika pale chini kwa mkono wake hakuzubaa, alijigeuza kwa sarakasi kwa kuuviringisha mwili wake hali ambayo ilimfanya atue pembeni.

Mahesabu yake yalikuwa sahihi kwa sababu wakati anashuka pale chini, juu yake kilipitishwa kisu kutoka kwenye mikono ambayo ilionekana kuwa na nguvu kubwa na lengo la mtu huyo halikuonekana kuwa kumzimisha tu bali alikuwa anahitaji kuondoka na nafsi yake moja kwa moja. Hata baada ya kutua pale chini hakuzubaa kwa sababu alijua huenda akampa adui nafasi nzuri ya kuweza kufanikisha jambo lake kitu ambacho hakutaka kiweze kutokea kwake yeye ndiyo maana alijiviringisha kwa sarakasi na kutua pembeni. Kujiviringisha kwake kulimfanya kulikwepa buti zito la ngozi ambalo lilikuwa limeshushwa na mwanaume ambaye alionyesha kuwa na uhasama naye mkubwa mithili ya mtu ambaye alimuibia mkewe, buti hilo kama lingefanikiwa kutua kwenye mgongo wake basi asingefanikiwa kutembea tena kwenye maisha yake yote.

Kiza kinene kilimfanya mwanaume huyo ashindwe kumtambua mwanaume ambaye alikuwa amekuja mbele yake ila mwanga wa radi ulimumulika mtu huyo ambaye bila shaka alikuwa ni mweusi usoni akiwa kwenye ghadhabu isiyo pimika. Aliukunjua mkono wake ambao ulikuwa na kisu kwa sababu alijua kwamba anatakiwa kufa wakati huo asipo yatetea maisha yake, hakupata muda wa kutosha wa kupiga tathmini juu ya uwezekano kama alikuwa anamfahamu mwanaume huyo kwa sababu alikuwa anamjia kwa kasi pale alipokuwepo huku mabuti yake yakiwa yanapiga piga kwa nguvu kwenye maji ambayo yalikuwa yametuama chini.
Miguu yenye nguvu miwili ilikuwa inakuja kwenye uso wake, kama bahati tu, tope lililokuwa chini lilimsaidia kuteleza kidogo na kurudi nyuma hali ambayo iliifanya miguu hiyo kumkosa na badala yake akarushiwa maji machafu usoni ambayo yalimuingia kwenye macho. Mtetemo wa ardhi aliusikia vyema baada ya ile miguu ambayo ilimkosa kutua chini na kukita kwa nguvu. Aliyafumbua macho yake haraka ili kujilinda, alichelewa kwenye mahesabu, ngumi ilizama kifuani na kumfanya ahisi kama kuna mtu alimpasua na shoka.

Ngumi hiyo ilimburuza mpaka karibu na ukuta mmoja wa nyumba ambapo hakuruhusu kuufikia bali mguu wake ndio ulitumika kama ngao baada ya kuurusha na kukita kwenye ukuta wa nyumba hiyo ambao ulitingishika kwa nguvu na kutulia. Alitaka kujipanga vyema alihisi kuna kitu kinawaka kinakuja pale alipo, alifanikiwa kukikwepa kisu ambacho kilikuwa na makali ya kutosha, kilimbaraza kidogo kwenye bega lake na kumpatia maumivu lakini hakulizingatia hilo kwanza badala yake alikuwa anaangalia namna ya kumkabili mwanaume huyo ambaye bado alikuwa anakuja mithili ya mtu ambaye anachajiwa huku kisu chake kikizama kwenye ukuta wa nyumba hiyo ya tofali.

Alifanikiwa kuziona ngumi mbili zilizokuwa zimeulenga uso wake, alijisogeza pembeni na kumpa mtu huyo nafasi ya kumpatia goti la ubavu kisha akiwa anasikilizia maumivu mwanaume yule alikichomoa kile kisu na kukizamisha kwenye mbavu za mwanaume huyo hali iliyomfanya kutoa sauti kali ya mguno wa maumivu. Sasa alikuwa anajiona anakufa kizembe bila hata kumjua mtu ambaye alikuwa anamvamia hapo alikuwa nani.
Alisogea hatua mbili nyuma macho yake yakiwa makini kwenye kile kiza huku ubavu wake ukiendelea kuitoa damu taratibu ambayo ilikuwa inatoka kwa fujo mpaka wakati huo, yule mwamba ambaye alikuwa anaelekea kupata ushindi, baada ya kukichomoa kisu chake alikuwa anasogea kwa hatua chache ambazo zilimpa uhakika wa ushindi. Kusogea kwake mvamiaji naye alihisi kama kuna kitu hakipo sawa, mbele yake mtu aliyekuwa anamuwinda ni kama ghafla tu hakumuona na radi ilipo piga aliona mtu huyo akitokea pembeni yake ambapo alifanikiwa kuipangua ngumi yake moja lakini mkono ambao ulikuwa na kisu ulizama kwenye kifua chake.

Ndiyo kwanza tunaufungua ukurasa wa kwanza kabisa wa simulizi hii ya kusisimua. Ungana nami mpaka mwisho tuweze kuugusa wino huu bora mno.

NAFSI ZILIZO TELEKEZWA.
Hapa sihami
 
🔥
 

Attachments

  • Screenshot_20250225-152534.png
    Screenshot_20250225-152534.png
    1.5 MB · Views: 2
Back
Top Bottom