Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

Hakuna mkuu hii ni nzuri Sana ila haiwezi kuizidi Ile ni extraordinary
Mwandishi anazipatiaga simulizi za aina hii
Kwanza stering huwa ni mtu wa kazi, akili nyingi, mtu wa haki na Hana Cha kupoteza.

Upande WA pili pia Huwa na watu wa kazi chafu hasa na wanaojielewa.
 
GEREZA LA HAZWA, ni noma lakn Gavin Luca ni noma pia.. sema huwa anatokea na kupotea,

Na Yohane Mawenge ni noma sana, ujasusi anaujua.
(Hii ingekuwa ya picha mjongeo ingekuwa poa sana)
 
GEREZA LA HAZWA, ni noma lakn Gavin Luca ni noma pia.. sema huwa anatokea na kupotea,

Na Yohane Mawenge ni noma sana, ujasusi anaujua.
(Hii ingekuwa ya picha mjongeo ingekuwa poa sana)
Mfano sakata la Uganda kwenda kumuua gerezani MTU wao Ile sinema ilikuwa poa Sana aisee watu Wana akili Sana😆😆😆
 
Mfano sakata la Uganda kwenda kumuua gerezani MTU wao Ile sinema ilikuwa poa Sana aisee watu Wana akili Sana😆😆😆
Kwangu me simulizi yenye upande WA Majambazi😂 unaojielewa Huwa naikubali saana.
Wahuni ambao steering wa muvi kuwasimamisha lazima afanye kazi haswaa.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 86

“Unaweza ukanieleza kwamba ni sehemu gani ambayo haiko sawa kwake labda?”
“Amekuwa na maamuzi ya kitoto siku hizi, hayupo makini na kazi yake kabisa kiasi kwamba mambo yameanza kuwa hovyo. Taarifa zetu zinavuja kila mahali na hakuna hatua yoyote anapiga. Yanafanyika mauaji ya hovyo kila siku tena kwa uzembe mkubwa, anawaamini watu ambao hawatakiwi kuaminika lakini zaidi mpaka sasa bado hakuna hatua ya maana yoyote ile ambayo ameipiga kwa huyu kijana wake Edison. Naelewa kama mzazi huenda kuna jambo linamtatiza ila kiuhalisia alishakula kiapo hivyo alitakiwa mpaka sasa awe amemuua”
“Kiongozi hizi taarifa huwa unazipatia wapi? Maana unazipata taarifa ambazo zingine hata mimi nazikosa wakati nashinda na bosi muda mwingi”
“Napata taarifa za kila tukio ambalo linatokea, kuto kuonekana kwangu haina maana kwamba sijui yanayo endelea Yohani. Leo hii Saimon ametekwa na asubuhi huenda mtapokea taarifa za msiba wake kwa sababu ya yule binti Nicola ambaye alimuamini kwa sababu alidai anataka kulipa kisasi kwa kumuua Edison. Hivyo nilicho kuitia hapa ni kukupa msisitizo ukamwambie kwamba anatakiwa kulikamilisha jambo hili ndani ya masaa sabini na mawili, asafishe makosa yake yote na uzembe mkubwa ambao ameufanya atasamehewa ila kama hataweza kufanya hivyo basi anatakiwa kufa na mtu ambaye atatakiwa kumuua ni wewe hapo” Yohani alishangazwa na taarifa hiyo ambayo ilikuwa ni ya ghafla mno kwake na mbaya. Kulikuwa na uwezekano yeye ndiye akahitajika kumuua bosi wake ndani ya saa sabini na mbili (Saa 72) ambazo zilikuwa zinafuata kama mwanamama huyo angeshindwa kuyatekeleza majukumu yake hayo.
“Kiongozi kwan……”
“Fanya nilicho kuagiza na mfikishie ujumbe kwamba kama akiniona mimi nimekuja kwake basi hiyo ndiyo itakuwa siku yake ya mwisho kuuona mwanga na baada ya hapo kazi itabaki kwako kutekeleza yanayo hitajika halafu mkuu wa majeshi anatakiwa kufa siku ya kesho jioni hayupo pamoja na sisi tena na hiyo kazi ifanye kwa mkono wako” Yohani alizidi kuchanganyikiwa, alipewa jukumu lingine na Nikolai hakusubiri jibu alianza kuondoka kuelekea kwenye gari aina ya V8 nyeusi ambayo ilikuwa ikimsubiri huku ikiendelea kuunguruma.
“Sawa mkuu” aliitikia na kuinama kutoa heshima kwa binadamu huyo aliye mtengeneza ila aliamini kwamba alikuwa ni hatari zaidi yake yeye kwa sababu mara kadhaa aliwahi kuua vijana mbele yake hali iliyo mtisha mno na kuanza kumuogopa isivyo kawaida. Aliondoka kuelekea kwenye gari yake kichwani akiwa na mambo mapya ambayo alitakiwa kuyafanya hususani usiku wa kesho yake lakini pia kumfikishia taarifa bosi wake. Jambo lingine ambalo lilimshangaza ni baada ya kusikia kwamba Saimon alikuwa ametekwa usiku huo, kwanza hakuamini inawezekanaje Saimon kutekwa kirahisi kwani aliujua uwezo wake lakini pia hakuelewa kwamba mwalimu wake taarifa hizo yeye alikuwa anazipatia wapi kiasi kwamba alikuwa anakuwa mtu wa kwanza kabisa kuzipata nyepesi hizo. Na ni asubuhi hiyo hiyo ambayo ulipatikana mwili wa Saimon ukiwa umefanywa kitu hamna hivyo taarifa za Nikolai zilikuwa sahihi kwa asilimia miamoja.


Aaliyah Beka na CDF walikuwa barabarani usukani ukiwa umeshikiliwa na CDF mwenyewe, jambo ambalo lilitokea lilikuwa la ghafla hivyo alihitaji kulishuhudia yeye mwenyewe ndiyo maana alihitaji kwenda huko bila walinzi wake zaidi ya Aaliyah ambaye kwa wakati huo alikuwa kama patner wake kwenye kazi kwa sababua alikuwa na siri zake. Makamu wa raisi alikuwa akiishi Osterbay.
CDF alipishana na walinzi kadhaa karibu na maeneo hayo kwa sababu ni moja kati ya maeneo ambayo yalikuwa na ulinzi mkali, alishangaa kuona watu hao wanampa heshima tu huku wakiwa hawana habari. Akawa anajiuliza sasa iliwezekana vipi eneo hilo kuvamiwa wakati kulikuwa na walinzi na iliwezekana vipi wasiwe na taarifa juu ya jambo ambalo lilikuwa limefanyika hapo? Hakuwa na jibu. Alisimamisha gari karibu na geti la nyumbani kwa makamu wa raisi, akafungua geti hilo ambalo aligundua kwamba lilikuwa limeegeswa tu.
Lahaula! Alitaka kupiga kelele kwa kile ambacho kilikuwa ndani ya uzio huo. Damu ilikuwa imetapakaa vibaya mno, watu walikuwa wamechinjwa kama kuku hali iliyo mtisha akawa anajifuta jasho wakati uhalisia ni kwamba eneo hilo huwa halina joto kwa kuwa karib na habari, muda mwingi upepo huwa unapuliza safi kabisa. Aaliyah mwenyewe alibaki anashangaa akiwa anajiuliza ni binadamu gani alikuwa na roho ya kikatili namna hiyo mpaka kuyatenda hayo na mtu huyo alimkosea nini? Hakuwa na jibu.
Walitembea wakiipita miili hiyo ambayo haikuwa na uhai kuelekea ndani, kulikuwa na miili kadhaa pia. Walitafuta chumba ambacho kilikuwa kinatumika kuongozea kamera kwa sababu waliamini humo wangepata taarifa zote. Chumba hicho CDF alikuwa anakifahamu kwa sababu kiongozi huyo alikuwa rafiki yake wa karibu, alikifungua kwa kuvunja mlango na kutua ndani ndipo akarudisha nyuma ili aweze kuona kipi kilitokea humo ndani. Kamera hizo ziliinasa sura ya mwanaume mmoja akigonja nje ya geti hilo akiwa na mavazi kama ya walinzi waliokuwa humo ndani ila yeye vazi lake lilikuwa na nyota kadhaa kiasi cha kumfanya kuonekana kuwa na cheo kikubwa kuliko wao.
Baada ya kufungua mlango mlinzi alitoa heshima akiwa kwenye vazi la jeshi kwani alijua kabisa yule ni mkubwa wake hivyo akamruhusu kuingia kwa ajili ya kumfanyia ukaguzi kama sheria zilivyokuwa zinahitaji lakini wakati analisukuma lile geti ndipo shughuli ilianzia pale, mwanaume yule alikuwa na upanga kwenye ukwapa wake ambako aliubania, alikata shingo ya mlinzi yule vibaya. Hawakutegemea kupata uvamiizi huo hivyo wakati wanashtuka walikuwa wamechelewa, aliua walinzi kikatili kama hana roho ya ubinadamu uso wake ukiwa umefunikwa na kofia ya jeshi. CDF alielewa kwamba sababu ya mtu yule kufika hapo kirahisi ni hayo mavazi ambayo yalikuwa mwilini kwake, alionekana kuwa kiongozi wa ngazi ya juu jeshini ndiyo maana hakusumbuliwa na walinzi njiani wakati anaelekea kwenye nyumba hiyo lakini hakuwa na uhakika kama huyo alikuwa moja ya vijana wake.
Mwanaume huyo baada ya kusababisha mauaji hayo, aliinua uso wake wakati anaelekea ndani, alikuwa anainagalia ni kamera tena makusudi kabisa, akaivua na ile kofia ili sura yake iweze kuonekana vyema kabisa. Ilikuwa sura ya Edison ndiye ambaye alikuwa anafanya unyama huo, Aaliyah alichoka kiasi kwamba alishindwa kuhimili kusimama akajikuta ameketi kwenye kiti, hakuamini kabisa kama mtu huyo ndiye ambaye alikuwa amefanya unyama huo. Mkuu wa majeshi alimwangalia Aaliyah kwa jicho la maswali mengi lakini hawakuwa na majibu hivyo ikawalazimu kupanda mpaka ghorofa ya tatu ambako ndiko waliukuta mwili wa makamu wa raisi ukiwa umelala chini. CDF alichungulia chini upande wa nyuma ya jumba hilo akauona mwili wa mtu, alikuwa ni mlinzi mkuu wa makamu wa raisi bila shaka alitupwa huko na kuuawa wakati ambao alikuwa anaendelea kuongea naye.
Ndani ya nyumba hiyo kwenye ngazi ilipangana miili ya walinzi ambao walikuwa wameuawa, CDF alisogea pale ulipokuwepo mwili wa rafiki yake ili kuangalia namna alivyo uawa, aliyafumba macho yake baada ya kugundua kwamba koromeo lilitobolewa vibaya kwa vidole na ulimi wake ulikatwa ukadondokea pembeni.
“Ndo huyu mtu umedai kwamba unataka nifanye naye kazi?” CDF alimuuliza Aaliyah kwa hasira
“Ndo huyo”
“Hapana siwezi”
“Kama upo tayari yakukute kama yaliyo mkuta makamu wa raisi ni sawa”
“Unaanza kunitisha?”
“Nakwambia ukweli”
“Binti unatakiwa kutambua kwamba mimi ndiye mkuu wa majeshi yote ya taifa hili, nina kila aina ya watu kwenye mkono wangu na huyu mpuuzi kwa hili nakuhakikishia nitamuua kwa mkono wangu”
“Mimi na wewe wote tunajua kwamba makamu wa raisi ana ulinzi mkali kuliko hata wewe hapo. Wewe kuwa na watu hatari haimaanishi kwamba watakuwa wanashinda na wewe muda wowote ule na kumbuka hapa mtu ambaye tunamzungumzia ndiye komando bora zaidi kuwahi kuzalishwa ndani ya taifa hili. Analijua jeshi huenda kuliko hata wewe kwa sababu wewe uliteuliwa kuwa hapo ila yeye ameyaishi zaidi maisha ya huko kuliko wewe hivyo wakati unamzungumzia usizungumze kama unaenda kushindana na askari polisi wa mtaani ambaye unaweza ukamtuma hata mwanajeshi mmoja akamuua. Nimewahi kushuhudia vifo vingi ila sio kifo cha namna hii, mtu ambaye hana shida naye hawezi kumuua kikatili hivi kwahiyo lazima kuna mambo nyuma ya pazia ambayo aliwahi kumfanyia” CDF alisikitika kwa sababu aliambiwa ukweli, angeweza kumtafuta mtu huyo lakini yeye alihitaji nafasi moja tu kuweza kuyatoa maisha yake.

UKURASA WA 86 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 87

“Unahisi kwamba makamu wa raisi aliwahi kumfanyia jambo lolote lile?”
“Huyu ni mkubwa mwenzako, mimi ndiye natakiwa kukuuliza swali hili wewe na sio wewe kuniuliza mimi hapa” Aaliyah alikuwa anamgusa kwenye mshono ndipo wakakumbuka kuhusu familia.
“Kama angewaua lazima tungeikuta miili yao hapa”
“Hawezi kuua familia ambayo haihusiki hivyo lazima kuna mahali amewafungia ndani ya nyumba humu humu” Aaliya alitoa maoni yake kwa uzoefu wake kwenye hizo kazi.
“Wewe nenda, kachukue ule ushahidi wa video za marejeo uondoke nazo mimi nawasiliana na raisi kumpa taarifa nitawaambia video hizo mhusika ameondoka nazo hivyo hatujazipata ila hakikisha nakutana na huyo bwana mdogo kwa gharama yoyote ile nina mazungumzo naye ya mhimu na maswali mengi kwake. Afanye hivyo kabla mambo hayajawa mabaya zaidi kwani kumuua kiongozi mkubwa kama huyu inaenda kuwa tatizo kubwa huko mbeleni na wanajeshi watasambazwa kila kona pamoja na polisi kumsaka” Aaliyah aliitikia kwa kichwa wakati ambao CDF aliutumia kumpa taarifa raisi ambayo baada ya kupokea taarifa hiyo alichanganyikiwa ndipo akaamua kwenda kwenye bwawa la kuogelea kutuliza akili yake kabla ya kuja kuitwa ili akakutane na Christopher Nyemo.
Aaliyah aliingia kwenye gari ya CDF ambayo ndiyo alitakiwa kuondoka nayo kwa sababu hakutakiwa kukutwa hilo eneo, alikuwa anahema kwa kasi ambayo ilikuwa ni ishara ya wasiwasi. Hakuamini kama mwanaume yule alikuwa mkatili kiasi kile huenda ni kwa sababu hakuwahi kubahatika kumshuhudia akiwa anafanya mauaji kama ambayo aliyafanya hapo, mwili wake ulikuwa ukisisimka vibaya kila alipokuwa anakumbuka kila mwili ambao aliuona. Aliitoa simu yake na kumtafuta mwanaume huyo ambaye aliahidi kumtafuta lakini hakuwa amemtafuta mpaka wakati huo ili na bahati tu alimpatia namba yake binafsi.
Simu iliendelea kuita yeye akiwa anaitoa gari kwa kasi kuelekea njia ya Masaki ambapo alikunja kushoto kwake baada ya hatua kadhaa kuitafuta njia ya Macho Msasani ili aje kutokezea Namanga kisha aingie Moroko aishie alikokuwa anaelekea. Simu iliita mara ya kwanza mpaka ikakata, ikaita mara ya pili ikakata, mara ya tatu ndipo ilipokelewa. Nyuma yake ilisikika sauti nzito ya kiume, alikuwa na uhakika kwamba alikuwa ni Edison.
“Nakusikiliza”
“Kwanini umefanya haya?”
“Mhhhhh nadhani sio biashara yako kujua natakiwa kufanya nini na nini sitakiwi kufanya”
“Jambo ambalo umelifanya ni hatari mno kulivyo unavyo fikiria wewe na hapa kama sio CDF lazima wangeipata sura yako yule ndiye mtu peke ambaye amekubali kufanya kazi na sisi”
“Sisi?”
‘Mimi na wewe kwa sasa tunafanya kazi moja, CDF nimeongea naye, alikuwa mmoja wao lakini amechoka anahitaji kulitumikia taifa lake hivyo amekubali kuwa upande wetu na anahitaji sana kuonana na wewe kwa sababu ana mazungumzo binafsi ya kuongea na wewe”
“Naona umeanza kujichukulia maamuzi yako bibie, nani alikwambia namhitaji mkuu wa majeshi?”
“Edison nisikilize kwa umakini sura yako imeonekana huoni kama ni jambo ambalo litahatarisha maisha yako?”
“Sura imeonekana kwa sababu nilitaka ajue kwamba ni mimi ndiye nimefanya mauaji yale kumuua yule mpuuzi, kwahiyo wewe kuiharibu umeua mipango yangu unatakiwa kuijua mipaka yako sio kuanza kuingilia majukumu ambayo hayakuhusu ukihisi unanifanyia hisani” Aaliyah alibaki anashangaa asiamini kile ambacho alikuwa anakisikia kwenye masikio yake.
“Ulitaka sura yako ionekane? Why?”
“Nataka wajue nini maana ya hofu, nahitaji wajue kwamba ninakuja kwa sababu sina haja ya kujificha tena, wanajua kama aliyekufa sio mimi. Hofu itawafanya watambue walicho kifanya na kuanza kufanya mambo kwa mihemko na wakati wanakuja kukumbuka kutumia akili muda wao utakuwa umeisha”
“Kwanini umemuua makamu wa raisi tena kwa ukatili namna ile mpaka ukaukata ulimi wake?”
“Kwa sababu ule ulimi ndio mara ya mwisho ulitoa kauli ya mke wangu na mwanangu kuuawa. Ni binadamu ambaye sikuwa najua kwamba anahusika na hili mpaka siku ya jana ambapo nilibahika kukutana na mwanaume mmoja ambaye alinipa ukweli niliokuwa naukosa hivyo yule mpuuzi alistahili hili kwa kuhusika na mauaji ya mke wangu na mwanangu ambaye hakuwa amezaliwa bado. Nitakutumia muda na mahali wa kukutana na huyo CDF tena umlete wewe hilo eneo nitakuwa na dakika tano tu za kumsikiliza” simu ilikatwa.
Simu hiyo ilimkutia Edison akiwa ndani ya chumba pekeyake, chumba ambacho kilijaa picha za watu wake wa mhimu kuanzia baba yake mzazi, wale makomando wenzake tisa, Edward Pande mwanaume ambaye alikatisha ndoto zake zote ili kumlea yeye na kumlinda. Pembezoni pia kulikuw a na picha kubwa ya JACK THE LAWYER akiwa ndani ya mahamaka kwenye tabasamu la kusisimua lakini pia picha kubwa zaidi ya zote ilikuwa ni picha ya mkewe Patricia Leonard aliye uawa akiwa na mimba tumboni mwake.
Chini kabisa ya ukuta kulikuwa na picha ya Zulpha Mazipa, mtaani walimjua kama Cersie Mhina lakini ndani ya biashara haramu alifahamika kama Madam Kate. Kwenye picha hiyo alikuwa ameweka alama kubwa ya X kwa rangi nyekundu ikiwa na maana ya kuhesabia kama mwanamke huyo alikuwa ni mfu kwenye maisha yake ila alikuwa anahitaji kukutana naye. Jana yake alifanikiwa kwenda ndani ya karakana ya utengenezaji wa treni maeneo ya Tazara majira ya usiku. Alikutana na Kanaan yule mwanaume ambaye alielekezwa kwamba kama kutakuwa na maelezo ya ziada yalikuwa yanahitajika basi alitakiwa kumtafuta mwanaume huyo ambaye ndiye alimfunulia ukweli wa makamu huyo wa raisi aliyekuwa mwema machoni pa watu kiasi kwamba hata kwenye zile listi za watu wabaya hakuwepo.
Makamu wa raisi alikuwa moja kati ya sehemu mhimu kabisa ya jamii ya LUNATIC SOCIETY na ndiye ambaye alisimamia zoezi zima la kuuawa kwa mkewe. Kanaan alimwelezea kwa undani kuhusu mtu huyo na baadhi ya taarifa ambazo hakuwa nazo Edison kwa sababu kijana huyo aliwahi kufanya kazi kwa ukaribu na Edward Pande ndiyo maana alihakikisha anampatia taarifa hizo nyeti ambazo hakuzilazia damu, haraka alizifanyia maamuzi na kwenda kumuua kiongozi huyo mkubwa wa serikali.
Juu ya meza ndogo ambayo ilikuwa ndani ya chumba hicho uliwekwa upanga ambao bado ulikuwa unavuja damu kwa mbali, ndio ambao aliutumia kwenye ile nyumba akiwa ameupata kutoka kwa Saimon wakati wamemvamia kwenye parking kule na aliipenda mno silaha hiyo kwa sababu ilimfanya kumpitia mtu mara moja tu anamaliza biashara.
“Ni muda wa kukutana na wewe mama” aliongea kwa sauti kali akiuchukua upanga na kuukita kwenye kichwa cha mama yake kwenye ile picha. Zulpha Mazipa alitakiwa kufa kwa namna yoyote ile hata kama alimzaa na kumnyonyesha, uwepo wake duniani ulikuwa na hasara kubwa kwa watu wengi kuliko faida zake.

Alishtuka na kukuta akiwa amefungwa kwenye kiti kwa kutumia nyanya ngumu za umeme. Alijitikisa kwa jazba lakini hakufanikiwa kuchomoka, akaishia kusonya, Ndani kulikuwa na kiza kikali kiasi kwamba hakuwa anaona kile ambacho kilikuwa kinaendelea hapo alipokuwepo. Alijaribu bahati yake kwa mara nyingine kuweza kutunisha misuli yake ili aweze kujitoa hapo ila mwili wake uliishia kwa maumivu makali akaamua kuwa mpole.
Alihisi kuna hatua za watu wawili zikiwa zinakuja upande wa chumba hicho, alikuwa makini kutaka kujua kwamba hatua hizo zilikuwa zinatokea wapi kuelekea hapo alipokuwepo. Taa zenye mwanga mkali ziliwaka ghafla na kumuumiza macho yake ambayo aliyafumba ghafla, baada ya dakika kama mbili aliyafumbua tena ndipo alifanikiwa kuwaona watu hao mbele yake. Edison na Nicola walikuwa wamependezana mno kuwa karibu, aliwakumbuka vyema hao ndio ambao walikuwa wamemteka na mara ya mwisho alizimia bila kuelewa kile ambacho kilikuwa kimeendelea.

UKURASA WA 87 unafika mwisho.
 
Back
Top Bottom