Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 91

“Kipi kilikufanya uamini kwamba ipo kweli?”
“Kwa sababu mwanasheria alinipa ukweli juu ya jambo hili lakini niliona pia inatumika nguvu kubwa kuzima kusambaa kwa taarifa zake, kama lingekuwa jambo lisilo kuwepo basi isingekutumika nguvu kubwa namna hiyo”
“Unajua mlengo wa kuanzishwa kwake?”
“Hapana mheshimiwa”
“Mimi ni miongoni mwa watu wa jamii hii tena watu ambao wanategemewa kuliko watu wengi” Bibie alibaki amehamaki, aliangalia kila upande kuona kama labda walinzi walikuwa wanakuja kumkamata lakini alishangaa kuona kila mlinzi yupo makini na kazi yake na hakuna ambaye alionekana kumlenga yeye. Kilicho mshangaza ni raisi kumfunulia mwenyewe kwa mdomo wake siri yake nzito namna hiyo, jambo hilo halikuwa salama kwake, kujua siri ya mtu namba moja nchini tena siri nzito kama hiyo ilimaanisha maisha yake hatarini kuanzia wakati huo. Alimeza mate jasho likianza kumtiririka usoni kwake, alijaribu kujikaza ila hali halisi ilikuwa inamkataa.
“Mheshimiwa samahani kama nitakosea kuuliza hili, sijajua kwanini unaniambia habari hii kwa sababu mimi ni mtu wa chini sana kwako ambaye sistahili hata kupata nafasi ya kukaa na wewe hapa muda huu!” raisi alitabasamu, aliiona hofu ambayo ilikuwa imemzonga binti huyo, alimsogezea kitambaa ili ajifute jasho na kumsikiliza. Aaliyah alikipokea kitambaa hicho mikono yake ikiwa inatetemeka kwa hofu na wasi ambao ulimzonga, alijifuta kisha akaambiwa anywe maji kutuliza presha.
“Nahitaji msaada wako”
“Mheshimiwa nahisi sijakuelewa vizuri unahitaji msaada wangu mimi hapa?”
“Ndiyo” alizidi kuduwaa, raisi alikuwa na nguvu kila kona, alikuwa anaweza kukutana na mtu yeyote ambaye anamtaka yeye kwa muda autakao, alikuwa na uwezo wa kufanya lolote kwenye nchi yake sasa kivipi ahitaji msaada kwa mtu wa kawaida kama yeye? Aliduwaa!
“Mimi nipo tayari kufanya lolote kwa ajili yako mheshimiwa, chochote kile nitafanya ukisema tu na nitafurahi kuwa sehemu ya watu ambao watafanya jambo kukupatia amani na furaha”
“Nahitaji kukutana na Edison na wewe najua ndiye mtu ambaye unaweza kunisaidia mimi nikalifanikisha hili” hakuamini alicho kisikia japo kilimpunguzia presha.
“Unakutana vipi na mtu ambaye amekufa mheshimiwa?”
“Mimi na wewe wote tunajua kwamba yupo hai bado na kwa uchunguzi wangu wewe ndiye mtu ambaye unaweza kuonana naye hivyo nahitaji kuongea naye tena kwa siri sana tukiwa wawili tu na jambo hili hatakiwi kulijua mtu yeyote yule” Aaliyah alihema kwa nguvu
“Naweza kujua sababu ya wewe kufanya hivyo mheshimiwa?”
“Ndiyo, nimechoka kuwatumikia watu hawa, nahitaji angalau niitumie nafasi hii kuweza kuisaidia nchi yangu na watu wangu. Nimefuatilia kwa umakini kuhusu Edison, ukweli ni kwamba najua kila ambacho kilimtokea na mimi nilikuwa miongoni mwa watu ambao walikuwa wanahitaji afe kwa namna yoyote ile lakini nafsi inanisuta kila nikikumbuka niliko toka, naona kabisa siasa imeniharibu kwa sasa hivyo nataka kuwa yule wa zamani. Aaliyah mimi nimehusika kuua watu wengi, kuzika siri nyingi na kuiba mali nyingi za taifa hili kwa maslahi ya hawa watu, kuna muda nilitamani kutofanya haya lakini nilishindwa kwa sababu ni watu wenye nguvu kubwa, wana watu karibia kila sehemu mhimu na wao ndio ambao waliniweka mimi hapa na hata maraisi wenzangu waliopita ambapo mmoja alihitaji kuwasaliti wakamuua madarakani na mwingine walikuja kumdunga sindano ya virusi” raisi alitulia na kaungalia pembeni kama kuna mlinzi alikuwa karibu kisha akaendelea
“Hili jambo nimetamani kulifanya kwa muda mrefu ila nisingeweza kufanya hivi kwa sababu kuna watu wanaripoti kila kinacho endelea humu ndani, wana mapandikizi kibao kiasi kwamba wakihitaji kuniua ni jambo la dakika moja tu kupiga simu hivyo nimeona hii ndiyo nafasi pekee ambayo naweza kuitumia hata kama nitakufa lakini sitaki kufia kwenye hatia ya kuendelea kuumiza watanzania. Wewe na Edison ndio watu ambao mnaweza kunisaidia hili kwa sasa hivyo nakuomba uhakikishe nakutana naye ni mhimu, ujio wake umenifanya nipate tumaini la mtu wa kunisaidia kutimiza hili” Aaliyah alikuwa makini kusikiliza, alisikiliza habari ambazo zilikuwa zinatisha mno tena zikitoka kwa mtu ambaye aliaminika kuwa na nguvu zaidi nchini.
“Mheshimiwa kuna watu wengine ambao nao wapo huko na unawafahamu?”
“Makamu wa raisi alikuwa huko ambaye nina uhakika ni Edison amemuaa, mkuu wa majeshi yupo huko hata bosi wako yupo huko ndiyo maana nimekuuliza kama una uhakika naye? Mtu yeyote ambaye wanamhitaji lazima ajiunge nayo kwa namna yoyote ile ndiyo maana unaona sehemu mhimu za usalama zote zipo chini yao hivyo wanaweza kufanya lolote na kwa muda wowote, mambo mengi huwa sifanyi mpaka nipate amri yao hivyo kwa sasa naomba uende umtafute Edison kisha utanipigia kwa namba ambayo utaikuta humo ndani, ni laini maalumu ambayo ina namna moja na simu hiyo inakubali kupiga kwenye hiyo namba moja tu, utapiga kuniambia mahali na muda” aliongea akiwa makini na kumsukumizia simu ndogo.
Aaliyaha aliipokea na kuitikia kwa kichwa, aliitiwa walinzi wa kumsindikiza mpaka ambapo angeona panamtosha kufika. Alitoa heshima kwa raisi wake kisha akatoka kuelekea kwenye gari kichwa chake kikiwa kinazidi kuwa na mambo mengi. Aliendeshwa na kuombwa aachwe mnazi mmoja. Alishuka kwenye gari na kukatiza mitaani akiviacha vichochoro kadhaa, alitembea mpaka kwenye hoteli moja ambayo ilikuwa ya ghorofa huku chini zikiendelea shughuli za kawaida ambapo watu wengi walikuwa wakiuza vifaa vya umeme na maofisi mengine ya vifaa. Aliingia ndani ya hoteli hiyo akalipia chumba na kuhitaji kutulia kwa sababu kazi ambayo alikuwa amepewa haikumtaka aingie kwenye mkono wa mtu yeyote na alijua kabisa karudi ofisini lazima angekamatwa na hata nyumbani kwake hapakuwa salama tena.
Tangu anatoka Ikulu kuna gari ilikuwa inawafuatilia kwa mbali ila hawakulishtukia jambo hilo. Baada ya kushushwa pale naye mwanaume ambaye alikuwa kwenye gari ya nyuma alisimama na kushuka akaanza kumfuatilia mwanamke huyo. Kwenye kichwa chake alivaa kofia hivyo ilikuwa ngumu kumtambua, alienda naye bampa to bampa mpaka pale alipo muona anaingia kwenye ile hoteli, alisubiri kama dakika tano zipite ndipo naye akaingia mle ndani jua likiwa kali nje maana ilikuwa ni alasiri kama kawaida ya Dar jua huwa halina huruma mchana na alasiri.
Baada ya kuingia ndani ya hoteli, alisogea mpaka mapokezi ambapo alidai kwamba mpenzi wake alitangulia ndani dakika kadhaa zilizo pita akiwa anamwelezea kwa mwonekano na mavazi aliyokuwa nayo. Dada wa mapokezi alikubali kumpokea mwanamke wa aina hiyo na alimhakikishia kwamba alikuwa amechukua chumba hivyo kama kuna uwezekano angeweza kumtaarifu ili ajue mpenzi wake yupo kama vipi amruhusu aende chumbani kwake lakini mwanaume huyo aligoma kwa kisingizio cha kwamba alikuwa anaenda dukani kwanza kununua vitu kisha angemfanyia surprise. Hakukaa tena baada ya kukamilisha kazi yake, alitoka nje ya hoteli hiyo na kuelekea kwenye gari yake.
Aliingia kwenye gari na kuisogeza karibu na hoteli ile sehemu ambayo alikuwa na uhakika wa kuona kila aliyekuwa anaingia na kutoka ndani ya ile hoteli. Aliivua kofia yake usoni, alikuwa Jumapili Magawa akiwa anaifanya kazi yake kama alivyo agizwa na mkubwa wake kuhakikisha anaijua kila hatua ya mwanamke huyo kwani waliamini kuna kitu wangekipata kwake na baada ya hapo walitakiwa kumuua kama wakijihakikishia kwamba hayupo nao. Je ni kweli ingekuwa rahisi namna hiyo? Muda ulitakiwa kuamua kuhusu jambo hilo.

UKURASA WA 91 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 92

SURA YA TISA
MADAM KATE
Kama alivyokuwa amedai kwenda Ikulu kwa ajili ya kuhitaji msaada kwa mara ya kwanza kwa raisi ndicho ambacho alikuwa anakifanya, kwa mara ya kwanza raisi alikuwa anakutana na mwanamama huyo na kumfahamu kwamba ndiye alikuwa nyuma ya kila kitu baada ya kupokea ugeni huo Ikulu na taarifa alipewa. Aliduwaa kushuhudia jambo hilo lakini hakuelewa shida ilikuwa nini hasa mpaka mwanamama huyo aweze kumfuata moja kwa moja wakati alikuwa na nafasi ya kuweza kumtafuta kwa njia ya simu.
“Najua umeshangazwa na kila kitu, kuanzia kuniona mimi hapa mtu ambaye hukunitarajia, zaidi mimi kuja binafsi hapa Ikulu. Hilo lisikupe shida kwa kiasi kikubwa kwani hata mimi siku ya kwanza nilishangazwa na ukweli kwamba hata raisi wa nchi yangu naye ni mmoja wetu”
“Unahitaji nini Cersie?”
“Nahitaji msaada wako”
“Kama wewe una nguvu kubwa kiasi hicho, ni kitu gani ambacho unakihitaji kwangu?”
“Nahitaji unisaidie kumtafuta Edison, tumia mamlako zako zote za ulinzi, kamera ambazo zipo ndani ya jiji hili kwa sababu nina uhakika kwamba yupo hapa hapa na kazi yako itakuwa rahisi tu kunipa taarifa mahali ambapo ataonekana basi hapo utakuwa umemaiza zoezi lako”
“Kwamba unanipa ni amri?”
“Nimeomba ni msaada wa kawaida sidhani kama utahitaji tufikie hatua ya kutumia nguvu mheshimiwa”
“Na nikisema hapana?”
“Unajua kabisa kitakacho fuata” raisi ndilo jambo ambalo alikuwa halitaki hilo kuweza kuendeshwa. Licha ya kushangazwa kumuona mwanamke huyo Ikulu lakini matakwa yake ndiyo yalimuacha hoi, alikuwa ameelewa kwamba mwanamama huyo alikuwa ni miongoni mwa wale viongozi wa ngazi za juu ndani ya umoja huo kuliko hata yeye hivyo alitakiwa kuwa makini kwenye mazungumzo naye, kufa lilikuwa jambo la muda mfupi hususani ukizingatia alijua kabisa kwamba Ikulu kulikuwa na mamluki kibao kuchunguza kila ambacho alikuwa anakifanya.
“Nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kuona nampata wapi kwa sababu mimi mwenyewe nina shida naye kwa kiasi kikubwa kwani uwepo wake unazidi kunipa wasiwasi mkubwa”
“Fanya hivyo utakuwa umefanya jambo la maana na kuna zawadi yako baada ya hilo kukamilika”
“Lakini nina swali binafsi kwako Cersie”
“Nakusikiliza”
“Kuna habari sio rasmi nilizisikia kwamba huyu kijana mama yake yupo hai. Je habari hizi ni kweli na kama yupo yupo wapi kipindi chote hiki mbona sijawahi kuambiwa hata kwa bahati mbaya?” maana ya raisi iliubadilisha uso wa Cersie Mhina kutoka kuwa na furaha mpaka kujawa gadhabu, yeye ndiye alikuwa mama mzazi wa huyo mtoto hata hivyo alijikaza na kucheka kinafiki.
“Fanya kazi ambayo ipo mezani Faraji mengine utayajua kwa muda wako” alinyanyuka na kuondoka moyo wake ukiwa unamuenda mbio, alihisi kila muda ulivyokuwa unazidi kwenda ndivyo siri hiyo ilivyokuwa ikiendelea kuwa wazi kwa kila mtu na jambo hilo lingemletea shida endapo lingewafikia wananchi ukizingatia alikuwa ametengeneza jina kubwa kila mahali na watu walimpenda kwa sababu ya kusaidia kwake jamii ila laiti kama wangefanikiwa kuijua hata sentensi moja ya uhalisia wa maisha ambayo alikuwa anayaishi na mambo yake basi wangehakikisha kwamba haendelei kuishi, alikuwa hatari kwa taifa.

Damasi alipewa kazi ya kufanya na Edison ili kuweza kuilinda familia yake, alikuwa kwenye mtihani mzito mithili ya mtu ambaye alitupwa na kuachwa mwenyewe kwenye bwawa lenye mamba wengi bila msaada. Alikuwa anawaza watu ambao alikuwa akifanya nao kazi hawakuwa watu wa masiara, kosa moja tu lilikuwa linayaondoa maisha yake tena angeshuhudia kwanza familia yake yote ikichinjwa mbele yake kisha ndipo yeye angefuatia kufa kwa maumivu makali. Lakini kwa bahati mbaya tena alitua kwenye mikono ya mtu ambaye alikuwa mkatili mno huku akimpa kazi hiyo na kumuacha huru kwamba kama angewaza kukimbia basi familia yake yote ingekufa kwa muda huo huo na yeye hakuna mahali angeenda angekamatwa tu.

Aliwaza kukimbia na familia yake ila hakuona namna kwa ukubwa wa familia yake asingeweza kuondoka na watu wote halafu wasijulikane kwamba walikimbia angalau angekuwa mwenyewe angepotea na kwenda mbali ambako hakuna mtu angejua aliwahi kuwepo duniani kama ulimwengu ulivyokuwa unaamini kwamba yeye ni mfu kwa miaka miwili kitu ambacho hakikuwa cha kweli. Alihema na kulazimisha tabasamu usoni kwake kwa sababu alitaka kucheza mchezo hatari ambao ungemfanya awe salama kutoka pande zote na ule upande ambao ungeshinda kwa baadae angebaki nao kisha angejua hatua za kuzifuata ila kwa wakati huo alitakiwa kuifanya hiyo kazi ambayo alipewa na Edison huko mbele angejua cha kufanya.
Eneo pekee ambalo aliamini kwamba angefanikiwa kufanikiwa kupata ambacho alikuwa anakihitaji ni MHINA PLAZA, Mida ya jioni alijongea mpaka eneo hilo na kupaki gari yake umbali fulani kutoka lilipo jengo lile ambalo lilikuwa na ofisi nyingi lakini karibia zote zilikuwa zinamilikiwa na mmiliki wa jengo hilo. Alikaa kwa muda mrefu eneo lile bila kukata tamaa mpaka usiku akiwa makini kuangalia watu waliokuwa wanaingia na kutoka, aliongeza umakini baada ya kuona mwanaume mmoja akiwa kwenye hood akiingia ndani ya eneo lile.

Hakufanikiwa kuiona sura yake lakini heshima ambayo alipewa na walinzi wa lile eneo ndiyo ilimpatia taarifa ya kujua kwamba ni yule mtu wake ambaye alikuwa akimhitaji hivyo akashuka kwenye gari yake na kuelekea lile eneo. Alikuwa akifahamika kwenye mamlaka za ulinzi wa eneo hilo hivyo kwake haikuwa shida kabisa kuweza kupita kwani alikuwa mmoja wao japo hakuwahi kabisa kumfahamu wala kukutana na bosi halisi wa hilo eneo. Alisogea mpaka kwenye lifti ambapo alipanda mpaka juu na kutokezea kwenye uwanja mpana wa ambao pembeni ulizungukwa na milango kadhaa na mbele yake palikuwa na sehemu ambayo ilitengenezwa kama sebule kubwa ikiwa na masofa ya gharama.
Alitembea taratibu akiwa makini kuangalia kila pembe, baada ya kutokezea kabisa kwenye sebule hiyo ndipo alishtuka baada ya kumkuta mtu ameketi kwenye pembe moja ya sofa kwa juu akiwa amempa mgongo. Alikuwa ni yule ambaye alimuona akiingia kwenye jengo hilo, kukutana naye ghafla kulimshtua kiasi hivyo akawa anafikiria cha kuongea
“Una muda gani tangu uanze kunifuatilia?” sauti nzito ilipenya kwenye masikio yake, ilikuwa ni ile sauti ambayo alikuwa anaitegemea, sauti ya Yohani Mawenge na ndiye huyo ambaye alikuwa amemlenga haswa kuweza kumpata.
“Unazungumza nini mkubwa, mimi nianze kukufuatilia wewe kwa sababu zipi?” aliongea akiwa anajichekesha ili kujiweka kwenye hali ya kawaida.
“Nimekuona kwenye kamera tangu unasogelea mlango wa kuingilia ndani, hatujawahi kuwa na makubaliano ya wewe kuja eneo hili bila taarifa, kuja kwako kienyeji inamaanisha kwamba kuna jambo ambalo unalifanya na kama jambo hilo lipo basi ungekuwa umelifanya hata mchana sasa inakuwaje umesubiri mpaka mimi nimefika hapa ndipo na wewe unakuja tena kwa kuvizia vizia?” sauti hiyo ndiyo ilimpa ishara kwamba mtu huyo alikuwa anamaanisha kile ambacho alikuwa anakiongea hivyo alipaswa kuwa makini na kauli zake na alimjua mwanaume huyo mbele yake, lilikuwa dubwana la kutisha lisilo na masiara.
“Hilo naweza kukiri kwamba upo sahihi kabisa, mimi nimekuja hapa kwa ajili yako na nimekaa kwa muda mrefu kukusubiri ila sio kwamba nakufuatilia” aliamua kufunguka kwa sababu kama asingetumia akili habari yake ilikuwa inaishia hapo, Yohani alikuwa kwenye wakati mgumu wa kumpata mtu wake ama kumuua bosi wake hivyo hakuwa na muda wa kupoteza.

UKURASA WA 92 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 93

“Kipi kinakufanya uhitaji kuonana na mimi?”
“Kukusaidia kumtafuta Edison” mwanaume huyo aligeuka baada ya kusikia hayo maneno.
“Unajua ninakoweza kumpata?”
“Hapana ila nipe masaa kumi nitakuwa nimejua eneo ambalo yupo hilo naweza kukuahidi” aliamua kudanganya ili kununua muda, alijua kabisa kwamba mpaka ufike wakati huo basi angekuwa amepata majibu sahihi juu ya nini anatakiwa kukifanya. Yohani alimsogelea kijana huyo na kumwangalia kwa umakini kwenye macho yake ili kuweza kuyapima yale maneno yake kama alikuwa anamaanisha kile ambacho alikuwa anakisema.
“Hakikisha tu hautapoteza muda wangu kwa sababu unajua kabisa kwamba nitakuua”
“Nakuelewa kiongozi” Damasi alimkumbatia Yohani kwa bega moja kama ishara ya kumhakikishia alichokuwa amemwambia, wakati anafanya hivyo kwenye mkono wake alikuwa na kifaa kidogo cha mawasiliano ambacho alikibandika nyuma ya hood akakiacha on, kilikuwa ni kidogo mno kiasi kwamba ilihitajika umakini mkubwa mtu kuweza kugundua na kama asingekuwa makini basi angehisi kwamba ni mapambo ya hiyo hood ambayo aliivaa.
Damasi alikuwa amekamilisha zoezi lake kwa sababu alijua kifaa hicho kingempeleka mpaka kule ambako Yohani angeenda hivyo kulikuwa na mambo mawili na moja wapo lingewezekana, kupajua nyumbani kwa Yohani au nyumbani kwa bosi wake kama angeenda kabla ya kubadili hood hiyo na kama mojawapo kati ya hayo lingewezekana angekuwa amekamilisha ile kazi yake aliyokuwa amepewa na Edison.
Alizitupa hatua zake haraka haraka ili kuweza kutoweka lile eneo haraka lakini bahati haikuwa kwake, aliitwa kwa sauti kali ambayo ilimfanya asimame, akazisikia hatua zikija kwa nyuma, zilikuwa hatua za sauti ya buti ambalo lilikuwa kwenye mguu wa Yohani. Mwanaume huyo alikuwa anageukia upande wa ukutani ambako kulikuwa na kioo kikubwa, kioo hicho kiliaksi kitu kwenye hood yake ndipo akagundua kwamba alikuwa na kifaa. Baada ya kukichomoa pale karibu na mgongo akawaza alikipatia wapi hicho? Hakukuwa na mtu mwingine ambaye angefanya hivyo zaidi ya Damasi ambaye ni sekunde kadhaa tu alitoka kumkumbatia tena akiwa amekuja kwenye mazingira ya kutatanisha hivyo alijua kabisa kwamba ni huyo ndiye ambaye alikuwa amefanya jambo hilo.
Damasi alijua kabisa kwamba jitu hilo lilikuwa limemshtukia, maisha yake yalikuwa hatarini na njia pekee ilikuwa ni kutoweka. Alitaka kukimbia, muda wa kufanya maamuzi ulimponza japo bado hakuwa na imani kama angefanikiwa kuwakwepa walinzi wote njiani, kipindi anajiandaa kutoweka Yohani alidunda pembezoni mwa ukuta na kusimama mbele yake hivyo asingeweza kwenda popote.
“Nilijua tu kuna sababu ya wewe kuja hapa, sasa tusipoteze muda unaweza kuniambia ni nani amekutuma uje kwangu na lengo lake ni lipi hasa?” licha ya kuulizwa alikausha, alichomoa bastola kwenye kiuno chake, alihitaji kumnyooshea Yohani, kasi yake ilikuwa ndogo mkono wake ulikutana na mguu uliokomaa ile bastola ikandokoa ukutani, lile teke lilizungushwa likatua kwenye kifua chake likambeba mpaka kumrudisha karibu na yale masoma. Alisimama kwa sarakasi safi na kusimama kama mwanzo, alijigusa kifuani ili kujiweka sawa akaupanga mkono, silaha yake ilikuwa mbali namna pekee ya kuishi ilikuwa ni kuitegemea mikono yake.
Alitembea kwa haraka kisha akasita, alitanguliza mikono yake chini akazungusha miguu yake kwa nguvu kwenye tairizi kuelekea alipokuwepo Yohani, miguu yake ilitua kwenye mbavu za Yohani ambaye hakutikisika, ni kama alikuwa anapiga jiwe. Aliitua miguu yake chini ili aweze kujikunjua kwa mara nyingine, wakati ananyanyua uso wake alikutana na ngumi ambayo ilikuwa imelenga mdomo, aliipisha kidogo ikatua kwenye paji lake la uso ambalo lilichanika hapo hapo na kuanza kutoa damu nyingi.
Ngumi ilikuwa nzito ikamyumbisha nyuma, alicheza cheza mtu wake alimfikia, Yohani alikuwa anachagua sehemu za kupiga, alimsubiri kijana huyo arushe mkono wake kwa hasira ili kuliiza ndipo alipo udaka na kuuvunja. Damasi alitoa kilio kwani alishtukizwa na hakujiandaa kwa hilo, kilio chake kiliongezeba baada ya Yohani kujibetua akaruka sarakasi ya mbele ambayo ilitua kwenye goti la Damasi. Goti lilivunjika kama kuna kuni zilikuwa zinavunjwa, Damasi alikuwa anauvuta mguu wake huku mkono akiwa ameushikilia.
Alichotwa ule mguu ambao ulikuwa sawa akabaki anaambaa ambaa kama ule mpira wa kutengwa, si unakumbuka alichokuwa anakifanya Ronaldinho kwenye penalti eeh? Yohani aligeuka na buti la nyuma ambalo lilitua kwenye uso wa Damasi, alipoteza meno matatu kwa mkupuo huku mdomo ukichanika. Alitua juu ya kioo akadondokea chini, Yohani aliichomoa bastola kiunoni na kumsogelea Damasi pale chini, hakumuuliza jambo lolote zaidi ya kummiminia risasi tatu kwenye ule mguu ambao ulikuwa salama, ulimletea maumivu ambayo yalimfanya alie kama mtoto mdogo.
“Nani amekutuma uje hapa?”
“Familia yangu haihusiki tafadhali” alitanguliza neno familia kwa sababu alijua watu hao ndicho kituo ambacho kingefuata ili kumpa somo, tayari alionekana msaliti na ule mpango wake ulifeli.
“Edison”
“Whaaaat?”
“Ndiyo, anakutafuta sana hivyo alihitaji kujua ulipo ama bosi wako”
“Kwahiyo wewe mpuuzi umekubali kutuuza sisi kwa ajili ya huyu mjinga ambaye tunamtafuta? Unajua kabisa alipo halafu unakuja hapa kujifanya unataka kunisaidia kumtafuta? Damasi nilikupa nafasi kubwa, nikakupa kila kitu, nilikufanya ukawa na maisha mazuri ya kila namna na kukupa uwezo wa kufanya jambo lolote halafu leo unatusaliti?”
“Naomba uiache familia yangu nipo tayari kukuonyesha anako patikana”
“Unajua kabisa madhara ya kufanya jambo kama hili na bado umefanya. Hauna chaguo nahitaji unipeleke huko aliko muda huu tena ninaenda mimi na wewe tu sitaki kijana yeyote aongozane na mimi ila nimemfunze huyu mtu namna hii dunia ilivyo mbaya” aliongea akiwa anasogea kwenye meza ambapo chini yake kulikuwa na kitufe, aliobonyeza alamu ikawa inapiga humo ndani ambapo ndani ya dakika moja kulikuwa na walinzi wa kutosha eneo hilo.
“Mbebeni huyu mumuweke kwenye gari yangu halafu sitaki mtu yeyote anifuate muda huu na hakikisheni mnasafisha hapa ofisi ibaki safi” wote waliinama kutoa heshima kwake, vijana wawili walimbeba Damasi akiwa anagugumia kwa sauti ya kilio, hali yake haikuwa njema, huo mwili haikuw ana muda tangu upokee kizito kikali kutoka kwa Edison halafu muda huo tena alikutana na mtu ambaye alihisi kwamba alikutana na shetani. Alitoka ndani ya ofisi hiyo na kuingia kwenye gari ambamo Damasi alifungwa kwenye siti za nyuma, alivuta muda mpaka ulipofika muda ambao aliutaka ili ampeleke huko aliko Edisoni, alikuwa na usongo na mtu huyo, alikuwa akimtamani kwa kipindi kirefu na siku hiyo aliamini kwamba alikuwa anaenda kuumaliza ule usongo wake. Edison angeyajutia maisha yake ambayo yalimbakisha hai mpaka wakati huo.

Aaliyah alichomoka hotelini mida ya usiku, baada ya kufika mapokezi alishangaa kupewa taarifa kwamba kuna mtu alikuja kumuulizia hapo, akashtuka. Alishtuka kwa sababu hakuna mtu ambaye alikuwa anajua juu ya uwepo wake hapo ama kuwa na miadi naye ya kumfanya ajue yeye alipo. Alimuomba mwanadada huyo ambaye alionekana kufanya kazi siku nzima kuonyesha video za mtu huyo kupitia video zao za marejeo kwenye CCTV lakini aligoma kwa sababu haikuwa misingi ya kazi yao kwani angekuwa anatoa siri za mteja mwingine, video zingetumika kama kungekuwa na utata wa usalama au tatizo kubwa la dharura likitokea.
Alitamani kumfahamisha kwamba yeye ni mtu wa usalama lakini akaumbuka kwamba ile baji ambayo ilikuwa ikimtambulisha alisha ikabidhi kwa bosi wake hivyo hapo hakuna kitu ambacho kingemuaminisha. Aliishia kutukana tu na kutoka humo ndani kwa sababu wakati huo alikuwa anaenda kukutana an mkuu wa majeshi ili waende sehemu ambayo walitakiwa kufanyia mkutano kati ya mkuu wa majeshi na Edison kama alivyokuwa ameomba lakini ni usiku huo huo ambao mkuu wa majeshi alitakiwa kufa kwa namna yoyote ile yakiwa maelekezo kutoka kwa Madam Kate kwenda kwa kijana wake wa kutegemewa Yohani Mawenge.

UKURASA WA 93 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 94

Alitoka kwenye hiyo hoteli akiwa amejifunika kofia, akatembea kidogo na kwenda kuchukua boda boda, wakati yote hayo yanafanyika kuwa watu walikuwa wanamfuatilia kwa umakini mkubwa wakiwa ndani ya gari bila yeye kujua huenda ni kwa sababu hata wao walikuwa na mafunzo makini kama yake ila kama angekuwa mtu wa kawaida basi huenda angemshtukia muda mrefu tu. Piki piki ilimshushia kwenye daraja ya Mfugale ambapo alikuwa anasubiriwa na gari ambayo bila shaka ndani alikuwepo mkuu wa majeshi japo siku hiyo alikuwa amevaa nguo tofauti na gari lilikuwa ni tofauti kiasi kwamba mtu kumshtukia kwamba ni yeye alipaswa kuwa makini isivyo kawaida.
Aliingia kwenye gari safari ikaanza ya kuelekea Mwembe Yanga. Walitembea kwa muda mpaka wapipofika sehemu ambayo ilikuwa na uwazi na mbele yake kulikuwa na jengo kubwa ambalo lilionekana ni muda mrefu lilikuwepo bila kutumika ndipo location ilipokuwa inasoma. Walishuka kwenye gari lakini wakati wanafanya zoezi hilo CDF alishtuka, ni kama kuna jambo alilihisi japo hakuwa na uhakika nalo. Aligeuka kuangalia nyuma hali ambayo ilimpa shaka hata Aaliyah Beka hivyo naye akalazimika kugeuka lakini hakuona kitu zaidi ya gari moja ambayo ilikuwa umepakiwa pembezoni mwa fremu moja.
“Nahisi tunafuatiliwa” CDF aliongea kama akiwa anamaanisha kwa sababu kwa kumbukumbu zake ni kwamba hakuna gari ambayo waliikuta kwenye ile fremu wakati wanapita.
“Punguza wasiwasi hili eneo lipo salama, hakuna mtu hata mmoja anajua kwamba tupo huku mheshimiwa” aliamua kumezea ili asionekane mwoga ila aliuwa na wasiwasi na hisia zake aliziamini.
Walitembea mpaka ndani ya jengo hilo ambalo lilikuwa refu na kubwa kiasi, baada ya kuingia ndani waliona kuna mtu amekaa kwa mbali kwenye kiti. Walisogea karibu zaidi na ndipo walimuona Edison akiwa ameketi kiti kimoja huku kiti kimoja kikiwa pembezoni, kwenye paja lake alikuwa ameuweka ule upanga ambao aliiupata kwa Saimon akaupenda kwani ulikuwa unrahisisha kazi yake, kwenye kiti cha pembeni aliiweka bastola moja, kisu kikali na chuma kimoja ambacho mara nyingi kilikuwa kikitumika kwenye mapigano hususani pale ambapo mpiganaji asingekuwa anahiaji kuumiza mkono wake basi angevaa chuma hicho cha mviringo kwenye kiganja chake.
CDF hakuwa akimuamini mtu huyo kwa sababu aliyo yashuhudia kwa makamu ya raisi yalimpa onyo kwamba anakutana na kichaa ambaye akili yake aliijua mwenyewe. Jengo hilo halikuwa na umeme ila kwa sababu lilikuwa na madirisha mapana kutokana na ukubwa wake, ilikuwa rahisi kwa umeme wa maeneo ya jirani kuweza kupenya humo ndani na kufanya kuwe na uwezo wa watu kuonana na kufanya mazungumzo bila tatizo kama ingebidi.
“Nina dakika ishirini tu za kuwepo eneo hili. Mheshimiwa CDF unaweza ukanipa sababu kwamba ni kwanini vifo vya watu hawa wakubwa serikalini vinafichwa?”
“Unaongea na mimi kama unaongea na mtu wa kawaida mtaani?”
“Kumbuka mimi sifanyi kazi chini yako CDF hivyo usitegemee kwamba mimi naweza kukunyenyekea wewe. Hapa unapo ongea na mimi kisahau cheo chako, ongea kama binadamu wa kawaida tu ila ukitoka hapa unaweza kuendelea na hizo amri zako kwa vijana wako”
“Kwa sababu jambo hili halitakiwi kufika kwa wananchi itakuwa ni hatari”
“Kwanini?”
“Wakubwa wanahofia kwamba kama ikijulikana hawa viongozi wakubwa wamekufa basi wananchi wanaweza kuacha kuiamini kabisa serikali hivyo kila anayekufa kwa sasa itawekwa siri na kama ikija kujulikana basi uwe umepita muda mrefu ambao utahakikisha usalama wao kwanza”
“Hao wakubwa unao wazungumzia ni akina nani?”
“Unajua kila kitu Edison kuhusu jamii hii ya siri”
“Kama wewe ni mmoja wao kwanini unahitaji kuongea na mimi?”
“Nahitaji kutoweka huko”
“Kwa sababu zipi?”
“Hawa watu wana nguvu kubwa, wanaiendesha Ikulu, wapo kila sehemu hata walinzi wangu ni miongoni mwao ndiyo maana ninapokuja kwenye mambo yangu binafsi kama haya sipendi kutembea nao”
“Bado haujanipa sababu ya msingi ya wewe kuja kuniona”
“Naomba unisaidie niweze kuondokana na hali hii niliyo nayo kwa sababu wataniua”
“Bado sijakuelewa, kwamba unahitaji mimi nikulinde wewe?”
“Ndiyo na mimi nitakusaidia. Nimeamua kufanya hili kwa sababu nimechoka kuua, nimeua idadi ya watu ambao hawahesabiki lakini kingine ni kwamba naonekana kama kibaraka tu nisiye na maana yoyote ile. Ukuu wa majeshi ni miongoni mwa vyeo vikubwa nchini kiusalama ila naonekana kama afisa wa polisi wa kawaida tu, wanaweza wakafanya lolote wanalo litaka na chochote na kwa muda wowote ule. Kinacho nisikitisha hata vijana wangu wanatumika kunipeleleza mimi, nahitaji tuunganishe nguvu tuweze kulimaliza jambo hili” Edison alimwangalia Aaliyah ambaye alionyesha alama ya kukubali wakati huo aliushika upanga wake kwa usahihi baada ya kuhisi jambo lisilo la kawaida, alitikisa kichwa chake.
“Mmefanya kosa moja la kipuuzi, mnafuatiliwaje bila kujua?” hapo wote wakashangaa, walikuwa wamechelewa. Huenda kama Aaliyah angemsikiliza CDF basi wasingeweza kufikia hali kama hilo ila mshale wa muda haukuwa upande wao. Waliingia wanaume watatu wakiwa na silaha zao mkononi, walikuwa ni vijana wa Aaliyah yaani Jumapili, David na Ruben.
David na Ruben walikuwa wameshika silaha zao kwa umakini mkubwa huku Jumapili akiwa anapiga makofi ya shangwe akiwa anacheka.
“Aaaliyah Aaliyah Team Leader, nilijua tu kuna kitu hakipo sawa kuhusu wewe, mara ya kwanza wakati bosi ananipa kazi ya kukufuatilia nilijua kuna kitu hakipo sawa. Kipo wapi Aaliyah leo wewe unashirikiana kwa siri na mkuu wa majesh….” Jumapili alishtuka alicho kiona kwani alihisi huenda Aaliyah alikuwa na ajenda ya siri na mkuu wa majeshi tu pekee lakini alicho kiona mbele yake kilimtisha, alikuwa ni yule mwanaume ambaye walikuwa wakipanga mipango mikali ya kuweza kumkamata kwa gharama yoyote. Sasa ilikuwaje Aaliyah akawa karibu na mtu huyo? Alitaharuki huku akiwa anamwangalia binti huyo ambaye mkono wake ulikuwa kiunoni akiipigia hesabu bastola yake lakini alionyeshwa alama ya kukataliwa na Jumapili, hakutakiwa kufanya hicho alicho kikusudia, haukuwa muda sahihi kwa sababu Jumapili alikuwa na msala wa kuwa makini na Edison, aiwahi kuona mauaji yake, hakikuwa kiumbe cha kawaida ni kwamba kosa moja tu lilikuwa linatosha kuondoka na maisha yako.
Ule muda ambao Jumapili aliutumia kumshangaa Aaliyah kukutana na Edison alifeli kuupigia hesabu kwa sababu alikumbushwa na kitu ambacho kiling’aa kwenye macho yake kupitia ule mwanga wa nje hapo akagundua kwamba kuna kitu kinakuja. Aliruka na kuchana msamba hewani, alipishana na upanga ambao ulikuwa ukate sehemu zake za siri. Kuuruka kwake ilikuwa ni hatari kwa Ruben Magesa ambaye alikuwa nyuma yale ambapo upanga ule ulikita kwenye upaja wake kiasi kwamba ulizama mpaka ukatokezea nyuma.
Hakutegemea kukutana na kadhia hiyo hivyo alipiga yowe, ilipelekea kushindwa kuimudu silaha yake akaanza kuzimwaga risasi hovyo. Jumapili alitua kwa goti chini akiwa ameinama baada ya kuruka hivyo risasi hazikuwa na madhara kwake, mkuu wa majeshi naye alilala chini baada ya kusikia tu lile yote hivyo mtu pekee ambaye alikuwa kihasara hasara ni Aaliyah ambaye kwa bahati mbaya risasi zilitua kwenye kifua chake. Lile mbilinge mbilinge la risasi lilimpa nafasi Edison kujizoa akiwa amechomoa kisu kingine kisha alitembea kwa mikono kama paka mpaka vumbi lilisambaaa humo ndani kwa namna alivyokuwa anatembea na hiyo mikono yake akiburuza mabuti yale mawili kuelekea pale alipokuwepo Jumapili.
Jambo lile lilimshangaza kwa sababu ilikuwa ni kama anaangalia tamthiliya ya kutisha, lijirusha mbeni akakoshwa na mguu, Edison alizunguka kuelekea kwa David Mbatina ambaye hakuwa anaelewa ashambulie wapi wakati huo maana kiongozi wake hakumpa amri yoyote ile. Alishangazwa na lile vumbi la ghafla ambapo ndani ya muda mfupi alishangazwa kumuona Jumapili akirukia pembeni ndipo alishangaa Edison akiwa anamjia yeye kwa kasi, alielekezea silaha yake huko, kwa bahati mbaya wakati anaachia risasi Edison alikuwa ameinama chini na kumfikia, alichomeka kile kisu kwenye goti la David na kulipasua kisha akapitiliza mpaka upande wa pili kwa kujiburuza katikati ya miguu yake.

UKURASA WA 94 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 95

Goti lilimkosesha balansi David, alitoa sauti na kutaka kugeuka kwa kujilazimisha, hakupewa hiyo nafasi. Edison baada ya kumpita mwanaume huyo alisimama na kugeuka na ngumi ambayo ilitua kwenye uti wa mgongo, ilisikika tu ile sauti ya “Mhhhh” kutoka kwa David. Aliinamishwa na kupigizwa mgongo wake tena kwenye goti, mifupa ilisikika ikiwa inavunyika, kilichomolewa kile kisu cha kwenye koti kilichotumika kuzichoma sehemu za mwili wake kama nyama ilikuwa inacharangwa.
Lile tukio lilifanyika sio zaidi ya sekunde kumi, Jumapili alikuwa bado ameduwaa kushuhudia tukio la ajabu kama lile, alichomoa bastola lake na kuachia risasi nyingi kwenda kwa Edison, bahati mbaya ilikuwa upande wake. Zile risasi ziliishia kwenye mwili wa David ambao Edison aliutumia kama ngao kwake na baada ya kuona jumapili hana risasi alimrushia mwili wa mwenzake ambao alitumia nguvu kubwa kuupangua akajikuta anaingia mkenge wa kukutana na ngumi ambazo zilimbeba mpaka ukutani, ukuta ulikuwa ni wa zege, alijigusa kwenye kisogo chake aligundua kwamba alikuwa anatokwa na damu, alipasuka.
Mkononi Edison alikuwa na kile kisu ambacho kilikuwa kinamwaga damu, Jumapili aliupanga mkono wake akiwa anameza mate kwa shida, silaha yake ilimuishia risasi na mwenzake mmoja alikuwa anapambana kuchomoa upanga kwenye mguu wake silaha akiwa ameitupa mbali na mwenzake mmoja alikuwa amekufa tayari jambo ambalo lilichukua sekunde kadhaa tu hata dakika haikukamilika. Aliichezesha miguu yake na kuunyosha mmoja ambao ulikutana na hewa, aliruka teke la kuzunguka nalo Edison alilikwepa hapo akaamua kuutumia mkono wake wa kulia ambao aliurusha kwa nguvu kiasi kwamba kama ungekita sehemu yoyote ya mwili wa Edison angejuta kuzaliwa.
Mkono ulipata maumivu ambayo hakuwahi kuyatarahia kwenye maisha yake, aliurudisha ukiwa unatetemeka, baada ya kuuangalia aligundua kwamba ulikuwa unavuja damu. Alipigwa na butwaa baada ya kugundua kwamba wakati anaurusha ulikutanishwa na kile kisu ambacho kilizama na kuchomolewa, alirudi nyuma na kuanza kutafuta njia ya kuweza kukimbia, hakujali tena kama kulikuwa na mwenzake ambaye alikuwa hai. Alikatishwa tamaa na sauti ya mlio wa risasi ambao bila shaka ulitoka kwa CDF kwenda kwa mwenzake ambaye alionekana kufanikiwa kuuchomoa ule upanga na kufanikiwa kuifuata ile silaha yake ila kabla hajafanikisha hilo ndipo CDF aliibeba ile bastola ambayo Edison aliiacha kwenye kiti akamshambulia nayo mtu huyo.
Sasa alikuwa pekeyake, zile sifa zilikuwa zinamtokea puani. Alijawa na hofu jasho likawa linamtoka kila sehemu ya mwili wake, alitishiwa kama anafuatwa akajaa kwenye mfuno kwa kurusha ngumi ya mkono wa kushoto, Edison hakumkopesha naye aliipeleka ngumi yake zikakutana katikati, Jumapili alibaki anatetemeka kwa sababu mkono wake haukuwa ukifaa, mifupa ilitokezea pembeni. Alibaki anatoa machozi kama mtoto mdogo mpaka pale alipopiga goti baada ya kisu kuzama kwenye bega lake, kisu hicho kilizungushwa mpaka nyama ya ndani nyeupe ikawa inaonekana.
“Kwahiyo bosi wenu amewatuma mje kumuua mwenzenu”
“Ndiyo ndiyo” alijibu kwa lazima kwa sababu kisu kilizidi kuzungushwa
“Kwa sababu gani?”
“Alionekana kuanza kumfuatilia kiongozi hivyo akajua huyu ni msaliti kwake, alitaka tumfuatilie na baada ya hapo tumuue” Alikichomoa na kukizamisha mdomoni mwa Jumapili akiwa anaendelea kutoa kelele. Kilizama mpaka kikatokezea nyuma ya kichwa chake, alipo kichomoa mwanaume huyo alibaki anahangaika hapo, zilikuwa ni sekunde kadhaa tu kabla roho yake haijaacha mwili.
Alikimbia kwenda kule alikokuwepo Aaliyah, binti huyo alikuwa anatapika damu kwenye mdomo wake, Edison alimbeba kwenye paja lake binti huyo ambaye alionekana kuwa na mambo kadhaa ya kumwambia kabla hajakata kauli.
“Nimekutana na raisi na ameniomba nikwambie ukutane naye, ni mtu ambaye naye ni miongoni wa jamii ya LS, alitamani kutoka kwa muda mrefu lakini alishindwa kwa sababu hakuwahi kupata mtu yeyote yule, kutokea kwako kumemfanya apate hiyo nguvu na yupo tayari hata kufa ila anataka kukusaidia kuimaliza jamii hii. Nakutegemea wewe, najua utalimaliza hili ila tafadhali kwa ajili ya damu yangu kamsikilize na ukubali kufanya naye kazi, ni mtu wa mhimu na anamaanisha anacho kiongea” aliongea maneno mazito akiwa anaendelea kutapika damu nyingi.
“Kwenye mfuko wangu kuna simu ambayo amenipa, simu hii ina namba moja tu pekee ambayo amehitaji niipige mara moja ukikubali kumwelekeza eneo ambalo natakiwa kukutana naye pamoja na wewe hivyo ukiwa tayari kuna namba utaikuta humo utapiga kumwelekeza. Lakini nina ombi la mwisho, nahitaji pia umuue mkurugenzi wa shirika letu la IBA kwa sababu yule kuendelea kuwa hai kazi yako inaweza kuwa bure Edison” alihema kwa nguvu akayafumba macho yake kisha akayafumbua kwa taabu sawa akiwa anaongea sauti ya chini ambayo ilimlazimu Edison kuinama ili amskikie vizuri.
“Kuna jambo ambalo nilitamani kukwambia ila nilikosa nafasi, sitaki nife ukiwa haujajua Edison. I LOVE YOU” Aliongea akiwa anatabasamu kwa mbali kisha mikono ikalegea akawa anayapoteza maisha yake. Tukio hilo lilimpa uchungu na kumfanya amkumbuke mkewe Patricia Leonard kiasi kwamba alijikuta chozi linamshuka taaratibu. Alivua shati yake akabakia na vest tu akamlaza mwanamke huyo kwenye shati hiyo na kuitoa simu yake mfukoni kwa uchungu kuipiga kwa Damasi.
Alikuwa anahitaji kupata taarifa za alipokuwa amefikia kwani alipatwa na hasira kiasi kwamba alihitaji amfuate mtu huyo usiku huo huo lakini simu hiyo ikawa haipatikani kitu ambacho kilikuwa nyuma ya makubaliano yao. Jambo hilo lilimshtua na kuhisi kuna kitu hakikuwa sawa, aliitafuta namba ya Nicola ambaye alimuacha nyumbani ili kujua kama yupo salama, alipiga simu hiyo ikaita mara moja tu kisha haikupatikana tena, akajua kwamba kumuacha Nicola nyumbani ni kosa kubwa ambalo angelijutia baadae kwa sababu hata Nicola alimtahadharisha mapema kwamba kumuachia Damasi kirahisi akiwa amepajua nyumbani kwao ilikuwa ni hatari ila alikuwa mbishi, sasa ubishi wake ulikuwa unaenda kumtokea puani, hakuwa tayari kumpoteza mtu mwingine usiku huo.
“Asante kwa kuyaokoa maisha yangu usiku huu, kumuua yule kijana ambaye alitaka kunishambulia kwa risasi ni zaidi ya asante kwangu. Kwa sasa nenda nyumbani siku ya kesho nitakutafuta nije kukupa mipango yote tunapo takiwa kuanzia na kuishia” alimpiga piga CDF kwenye bega kama ishara ya kumkubalia alichokuwa anakihitaji akatoka kwenye hilo jengo akiwa anakimbia, alikuwa anamuwahi nyonga mkalia ini wake. Kumbuka tu kwamba ni usiku huo huo ambao Damasi alikamatwa na Yohani Mawenge akafanywa kitu mbaya na mwanaume huyo akamtaka ampeleke alipo Edison kwani alikuwa na msongo naye vibaya mno.
Edison mwenyewe ndiye huyo alikuwa mwembe Yanga nyumbani akiwa amebaki Nicola pakeyake, unahisi ingekuwaje Yohani kumkuta Nicola? Alifanikiwa kupambana na hilo dubwana? Edison aliwahi kufika eneo la tukio kumsaidia mpenzi wake mpya huyo? Maskini Nicola!

UKURASA WA 95 unafika mwisho.
 
SIKU ZA MWISHO ✅ (GIZA LA MALAIKA)- THE DARKNESS OF AN ANGEL.....

Hii ni simulizi mpya ambayo inatoka tarehe 11 mwezi huu wa 3.....

Ni sehemu ya tatu na ya mwisho ya mwendelezo wa IDAIWE MAITI YANGU na SAFARI YA GAVIN LUCA (THE ODYSSEY OF GAVIN LUCA)....

Humu utajua hatima ya familia ya GAVIN LUCA na mwanae wa pekee LIONELA na hatima ya zile nguvu zao.

Kwenye SAFARI YA GAVIN LUCA uliona JABARI akionekana msaliti, hivyo kama unataka kujua sababu nyuma yake kwamba kwanini alimsaliti mkewe wa ndoa? Basi hii ndiyo sehemu sahihi ya kupata majibu yako.

JABARI alituacha wote mdomo wazi baada ya kumuoa LIONELA kisha akaanza kuua familia ya LIONELA Lakini mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Kenya (NIS) alikuwa na ajenda gani hatari kwa Tanzania na familia ya GAVIN LUCA? Jumuika nami ili uweze kupata majibu sahihi ✍️

Hili ni andiko langu la kwanza kwa mwaka huu tangu uanze hivyo tarajia kukutana na mambo mazito ndani yake.

Kwa wale ambao huwa wanapenda kuwa wa kwanza kusoma unaweza kuweka order yako mapema au kunitafuta mapema ili inavyotoka uwe wa kwanza kuweza kuisoma ✍️

Bux the storyteller

FEBIANI BABUYA ✅
 

Attachments

  • FB_IMG_1741158106381.jpg
    FB_IMG_1741158106381.jpg
    137.9 KB · Views: 2
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 96

NYUMBANI KWA EDISON
Edison bado alikuwa anaishi paipokuwa nyumbani kwa JACK THE LAWYER, alijua sehemu hiyo ilikuwa salama kwa sababu mhusika alikuwa amekufa hivyo kwake ikawa salama zaidi kuigeuza sehemu hiyo kuwa makazi yake rasmi. Usiku huo ambao aliondoka kwa ajili ya kwenda kuonana na CDF alimuacha Nicola pekeyake, kuna namna alikuwa anamjali binti huyo kiasi kwamba hakupenda kutembea naye kwenye maeneo ya hatari ukizingatia Jack alimwelekeza mapema kwamba alitakiwa kumlinda kwa namna na gharama yoyote ambayo ingekuja mbele yake hivyo alihakikisha analitimiza hilo.
Lakini ni usiku huo huo ambao aliamini kwamba Nicola alikuwa kwenye hatari kubwa kitu ambacho kilikuwa cha kweli kabisa. Damasi akiwa kwenye hali mbaya ya maumivu makali akiendelea kuvuja damu, alimleta Yohani mpaka kwenye eneo hilo ambapo alipaki gari yake nje ya hilo jengo. Aliangalia kila kona kama kulikuwa na mtu wa karibu, muda ulikuwa umekwenda hivyo aliihisi amani mbele yake, alirudi nyuma kidogo akadunda kwenye tairi ya gari akafanikiwa kuudaka ukuta wa juu kabisa. Alijivuta kwa nguvu na kusimama hao juu akiwa amepishana kidogo na nyanya za umeme ambazo zilipitishwa juu ya hilo geti.

Alihesabu mara mbili akanirusha kwa sarakasi mpaka ndani ambapo alitua kama paka bila kutoa kishindo. Alitazama buti lake, liliungua sehemu ndogo ambayo iligusa kwenye zile nyaya hivyo hata yeye angefanya ujinga basi angepata athari ya kukutana na adha ya umeme. Ndani kulikuwa kumetulia, mazingira yake yalikuwa safi ishara ya kwamba mtu ambaye alikuwa anaishi ndani ya eneo hilo alikuwa ana uhakika wa kula vizuri, maisha ya mawazo ya pesa hayakuwa sehemu yake.
Ndani ya sehemu ambayo alijiridhisha kwamba ilikuwa ni sebule aliona kuna mwanga, maana yake mwenyeji wake lazima alikuwa hapo sebuleni, alitabasamu kwa hasira akiwa anasogelea ule mlango ambao ulikuwa mbele yake. Bila kupoteza muda aliukita ule mlango na buti zito akaingia nao ndani, mwenyeji ni kama hakutarajia kuweza kukutana na hali kama hiyo hata hivyo hakuwa mzembe, alikirusha kisu ambacho kilikuwa kwenye mkono wake, Yohani alikikwepa kwa kuinamia pembeni kikaenda kukita kwenye ukuta na kudondoka chini.
Mbele yake alikuwa amesimama Nicola akiwa kwenye kipensi kifupi na kicloptop kilicho mchora vyema umbo lake. Mezani kulikuwa na matunda hivyo bila shaka ilikuwa ni ishara kwamba alikuwa akikitumia kile kisu chake kuweza kukatia yale matunda ambayo alikuwa akiyashughulikia pale mezani.
“Sikutegemea kukutana na wewe mazingira kama haya tena ukiwa umestarehe namna hii ukisubiri kuliwa baada ya kutufanyia usaliti. Binti ni mpuuzi wewe”
“Damasi kakuleta hapa sio?”
“Hakuwa na chaguo lingine nadhani hata wewe umewahi kusikia simulizi zangu kadhaa na ndicho ambacho kitakukuta hata wewe. Tufupishe maelezo bwana ako yuko wapi?”
“Ningekuwa mimi ndo wewe ningeondoka asije akanipata sehemu yoyote ile hapa duniani kuendelea kukaa kwako na kujileta hili eneo unajipunguzia nafasi ya kuendelea kuwa hai”
“Kwa maneno hayo ina maana hayupo. Kwahiyo nitapata vitu viwili kutoka kwako, mzigo wetu lakini pia huyo bwana ako najua atakutafuta tu kwa namna yoyote ile hivyo atalazimika kuja ninapo hitaji mimi ukiwa mkononi mwangu, zoezi langu linaenda kuwa rahisi kwa kuua ndege wawili kwa wakati mmoja” Yohani hakuwa mtu wa utani, maneno aliyo yaongea alikuwa anamaanisha mno, hawakuwa mbali kwa walipokuwa wamesimama. Kujiachia kwake Nicola kulimfanya asiwe na silaha yoyote ya maana ukiacha hicho kisu ambacho kiliishia kukita ukutani, maana yake alitakiwa kuyatetea maisha yake kwa mikono yake miwili.
Aliisukuma meza ambayo ilikuwa mbele yake kuelekea kwa YohanI, meza hiyo ilizunguka kwa kuviringika kwani ilisukumwa kwa nguvu. Nicola alikuwa anakuja tena akiwa peku mguuni kwake, meza hiyo ilipasuliwa kwa mguu Nicola akawa amefika, alirusha mguu wake ukakita kwenye shingo ya Yohani ambaye aliyumba mpaka ukutani ambapo aliutumia mguu wake kumpa balansi. Nicola alizunguka kwa mahesabu yaliyo enda sawa, mguu wake ukakita kwenye uso wa Yohani kwa mara nyingine, aliishia kuyumbisha uso wake na kurudi kusimama kama mwanzo.
Ngumi ambayo ilikuwa inakuja aliiona, alibonyea kwa nyuma kidogo ikaishia kumpapasa kwenye nguvu yake, alijivuta kusogea mbele kwa nguvu ambapo alimkita Nocola na kiganja cha shingo, alipata maumivu makali kwa kuyumba yumba kurudi nyuma, jitu hilo halikuwa na huruma kabisa. Yohani alikanyaga kwenye sofa lililo msaidia kudunda, alitua kwenye bega la Nocola ambaye alifanikiwa kuudaka mguu mmoja mwingine ulimkita kwenye kifua akadondokea kwenye kabati ambalo alilipasua.
Alisimama ghafla akiwa anarusha moja ya kioo ambacho kilipasuka, kioo kile kilikuja kwa spidi Yohani akapishana nacho baada ya kufanikiwa kukikwepa, alikidaka kwa mkono wake, kilimchana ila hakujali wakati huo alikuwa amesha anza kujongea kuelekea alipokuwepo Nicola. Nicola alikuwa anafanya kazi ya kukwepa tu kwa sababu alianza kuzidiwa nguvu na Yohani, alikutana na kiwiko cha mkono wa kulia aliyumbia kushoto ambako Yohani alitumia nafasi hiyo kile kioo kukizungushia nyuma akakidaka na mkono wake wa kushoto kisha akakizamisha kwenye mbavu ya mwanamke huyo.
Maumivu aliyasikilizia vizuri, alipiga kelele za maumivu, Aliongezwa ngumi yenye kilo kadhaa hilo eneo akadondokea ukutani. Mwanaume huyo hakuwa na roho ya kibinadamu kabisa, licha ya Nicola kuwa hai pale chini bado alimfuta na kumuongeza buti la uso lililo mzoa mpaka ukutani ambako alijibamiza vibaya mpaka akapoteza fahamu. Yohani aliangalia kwa umakini sebule hiyo, akawa anazitupa taratibu hatua zake kuelekea zilipo ngazi za kuelekea juu ila alisita baada ya kusikia kelele za kishindo nje. Alimbeba Nicola na kutoka naye nje ambapo mara hii alifungua geti na kutoka nje ambako alimkuta Damasi akipambana kuweza kutoka ndani ya gari ile ili aweze kulikimbia dubwana hilo.
Harakati zake zilimsaidia kufanikiwa kutua chini ya gari ila hakuwa na uwezo wa kwenda popote kwa sababu miguu haikuwa ikifanya kazi kabisa, mguu mmoja ulikuwa umevunjwa na mwingine ulikuwa umepigwa risasi za kutosha. Alimrushia Nicola kwenye buti kisha akamrejea Damasi ambaye hali yake ilikuwa mbaya kiasi kwamba hata kujivuta alikuwa anashindwa, alimbeba mwanaume yule mgongoni akaangalia kila sehemu ndupo aligundua kwamba juu ya geti kulikuwa na vyumba vikali ambavyo vilitokezea. Alisogea akamrushia Damasi kwa juu sana kicha akalishikilia lile geti kuelekea ule uelekeo ambao alimrushia Damasi, alifikia kwenye hivyo vyuma ambavyo vilimtoboa toboa mgongo wake, alimuacha akiwa anahangaika hapo akawasha gari akatoweka Joel John waweza kumuita Joh au Yohani Mawenge.

Dakika kumi baadae ndio muda ambao Edison alikuwa anaingia ndani ya hilo eneo, gari yake ilikuwa kwenye mwendokasi lakini hakujali, alishika breki ghafla hata kabla ya gari kusimama vizuri aliruka kukimbilia ndani. Alisita baada ya kulikaribia geti kubwa ambalo lilikuwa mbele yake, kwa sababu chini palitapakaa damu, mwili wake ulimsisimka huku akizidisha hofu ndani ya moyo wake ndipo akaamua kuyainua macho yake juu.
Alikuwa anaomba isije kuwa ni Nicola ndiye alifanyiwa vile, aliona mtu ametundikwa mithili ya mtu ambaye alikuwa amebanikwa akisubiri moto ukolee. Alikuwa ni Damasi ndiye ambaye aliuawa kikatili juu ya geti hilo. Alihema kwa nguvu na kukimbilia ndani, hakukuwa na dalili za uwepo wa mtu zaidi ya mlango kuvunjika lakini pia vitu kuvurugwa ndani, alijua kabisa Nicola alikuwa ametekwa tayari. Alisogea kwenye chumba cha kuongozea kamera kuona matukio ambayo yalitokea hapo, aliangalia kwa umakini akaishia kusikitika tu kwa sababu jambo hilo ulikuwa ni uzembe wake kumruhusu Damasi kuondoka kirahisi hapo, mara mia angemtoa akiwa amemfumba macho ili asione kwamba alikuwa wapi.

Aliitoa ile maiti kwa sababu watu wangeiona ingekuwa kesi nyingine hiyo kwa mapolisi, alisafisha kila kitu na kuangalia saa yake ya mkononi, ilikuwa inasoma saa nane. Aliitoa ile simu ambayo aliichukua kwa Aaliyah, alipiga ile namba ambayo ilidaiwa kuwa ya raisi, iliita mara moja tu na kupokelewa.
“Tukutane kituo cha mwendokasi gerezani saa kumi kasoro, sitaki kumkuta mlinzi yeyote pale nadhani patafaa kwa ajili ya mazungumzo ya mimi na wewe” hakusubiri jibu upande wa pili aliikata hiyo simu na kuipasua chini. Alitoka akalifunga geti kisha akaingia kwenye gari yake na kutoka hapo kwa kasi kama kuna ugomvi ambao aliuingia na watu kadhaa na alihitaji kuwawahi.

UKURASA WA 96 unafika mwisho.
 
Back
Top Bottom