FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #201
🏃Jioni sio ndio hii lakini au bado haijafika?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
🏃Jioni sio ndio hii lakini au bado haijafika?
Jioni sio ndio hii lakini au bado haijafika?
[/QUOT
Fanya kweli mkuu.
Tatizo hakuna warembo wanaofuatilia hii simulizi tungewaomba wakuite😃😃maana mkiitwa na warembo mnakuja Kasi kama risasi
😁Tatizo hakuna warembo wanaofuatilia hii simulizi tungewaomba wakuite😃😃maana mkiitwa na warembo mnakuja Kasi kama risasi
😅😅😅Shida nini Mzee unaogopa mizinga😁
Huwa sina muda nao kabisa mkuu
Ubarikiwe mno kiongozi, wacha ninogeshe safari yangu sasa ya kurudi homeHADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 84
Joeli John, waweza kumuita Joh alipata begi la pesa, pesa ambazo hakuwahi kuwaza kuwa nazo kwenye maisha yake huku akiambiwa kwamba alikuwa anaweza kufanyia jambo lolote lile ambalo angelitaka yeye. Alijihisi kuchanganyikiwa lakini hakuwa na namna kwa sababu pesa zilikuwa zake na aliruhusiwa kuzitumia kwa namna atakayo yeye, baada ya mtu ambaye alimletea pesa kuweza kuondoka, yeye alikimbia kuelekea kwenye kituo cha daladala, alipanda daladala akiwa ndiye binadamu mwenye furaha zaidi duniani kwa siku hiyo.
Safari yake ilimpeleka mpaka SHOPPERS, huko alienda kufanya manunuzi ya nguo mpya na za gharama kubwa. Alifika eneo hilo ambalo lina maduka mengi makubwa ya vitu vitu vya gharama, kuingia hapo kununua bidhaa kama nguo unatakiwa uwe ni mtu ambaye una uhakika wa milo mitatu ndani ya jiji hili na hauwazii kodi mara kwa mara mama mwenye nyumba anapo ipiga simu yake kwenda kwako. Hata badhi ya wahudumu walibaki wanashangaa, mteja ni mfalme ndiyo lakini hali yake ilikuwa ya kushangaza ila hata wachache ambao walimhoji hususani wateja wenzake kuhusu hali yake alidai kwamba alikuwa kwenye machimbo ya madini ila alikuwa amerudi zake mjini sasa.
Alinunua mavazi ya gharama na kuhitaji kuonyeshwa zilipo sehemu za gharama za kwenda kufanyiwa usafi hususani kuogeshwa na warembo pamoja na kufanyia masaji kwenye mwili wake, pesa ilikuwepo yanini ajitese Joel? Ulikuwa ni muda wake wa kuyafaidi maisha bhana pesa zilimkubali ndani ya jioni moja tu pekee. Kijana huyo alibadilika mwonekano wake ndani ya saa moja tu, kama ungebahatika kuonana naye halafu ukaambiwa kwamba alitoka kwenye maisha ya kimaskini basi nafsi yako isingekubaliana na hiyo hali kwani ungekuwa moja ya watu ambao wangegoma kukubali.
Safari yake iliishia Serena hoteli, alichukua chumba cha bei kubwa huku akihitaji kutafutiwa mrembo mkali zaidi ndani ya eneo hilo ambaye alitakiwa kukaa naye usiku huo na kama angempenda basi angempa ofa nyingine ya kuendelea kuwa naye usiku uliokuwa unafuata. Hoteli hiyo ya nyota tano alikuwa akiiona tu kwenye runinga hususani wakati wafanya biashara wanafanya mikutano yao na wasanii wakubwa, yeye alikuwa anaziishi moja ya ndoto zake usiku huo. Aliletewa mwanamke mmoja mrembo haswa, alikuwa ni Mhabeshi yule, unaijua Ethiopia wewe? Mhabeshi ikawa halali yake kuyadhalilisha mashuka na yalikoma usiku ule, mwanaume yule alikuwa amepania kufanya mapenzi na mwanamke mrembo kama huyo na aliapa siku akimpata basi angenyooka na usiku huo aliyadhihirisha maneno yake mpaka mhabeshi hakutaka kumuacha mwanaume huyo kwa show ambayo alimpatia.
Joeli alijiona mjinga mno alipo jitazama kwenye kioo, alikumbuka ni jana yake tu jioni alitaka kujiua kwa sababu ya mwanamke! Tena mwanamke wa kawaida tu huenda ni ugumu wake wa maisha ndio ambao ulimfanya amuone mrembo. Alijicheka na kujitia kibao, yaani Joeli mimi ndiye nilikuwa nalia, mimi ndiye nilitaka kujiua kwa sababu ya mwanamke wa Tandale tena kwa Tumbo? Aaaah fala mimi. Alijiongelesha wakati huo alikuwa akimwangalia mhabeshi kitandani, alipewa show nzito mpaka akapitiwa na usingizi. Mwanamke huyo alilala kihasara kiasi kwamba hata mwili wake ulikuwa umejiachia wazi kabisa hivyo akawa anaona kila kitu, ulikuwa ni uumbaji bora zaidi wa kiumbe kinacho itwa mwanamke kuwahi kuuona kwa macho yake. Mhabeshi alikuwa mrembo mpaka alihisi mama yake alifanya sifa kumzaa mwanamke huyo, aliivua nguo yake ya ndani na kurudi tena kitandani kuweza kuufurahia ulimwengu wa uumbaji.
Joeli maisha yalikaa upande wake, alikula starehe kama amechanganyikiwa. Baada ya wiki moja alirudi Tandale akiwa na gari kali, alikuwa amevaa mavazi ya gharama kali mno ili kwenda kuwanyoosha wanazi wake. Baada ya kufika mtaani alikuwa gumzo Joeli, kila mtu alidai kumfahamu yeye na kuwa rafiki yake, kila mtu alihitaji ukaribu na kijana huyo lakini hakuwa na hizo shobo, heshima ilitakiwa kufuata mkondo wake. Tena hakurudi mwenyewe, alirudi na wale watunisha misuli wa gym ili asisumbuliwe na wapenda kushobokea watu. Taarifa ile ilimfikia Tina aliyekuwa mkewe, mwanamke huyo kusikia habari hiyo alitoka anakimbia kiasi kwamba hata nguo zilikuwa zinamdondoka kumuwahi Joh wake ambaye aliambiwa kwamba kawa tajiri ghafla.
Wanawake na pesa tena? Ni kama Messi na mpira wake, mwanamke huyo hakukumbuka kwamba siku kadhaa nyumba alimdhalilisha Joeli mbele ya wanaume wawili waliokuwa wakifanya naye mapenzi kwa fujo tena mbele yake, eti siku hiyo alikuwa akimkimbilia mmewe, hahaaha wanawake wanawake! Mwanamke huyo licha ya kufika hapo na kushuhudia maajabu ya dunia, Joh mfanya vibarua alikuwa akilindwa lakini aliishia kuwa kama Mussa. Mussa aliambiwa kwamba utaiona nchi ya ahadi ila hautafanikiwa kuingia, hata Tina hakufanikiwa kumgusa mwanaume huyo ambaye alikuwa na ghadhabu naye kubwa, jambo hilo alilihifadhi kwenye moyo wake kama kiporo.
Licha ya Tina kulia na kugala gala akijifanya kujutia kitendo chake, Joeli hakuwa na muda na mwanamke huyo baradhuli. Aligawa pesa kwa baadhi ya watu mtaani hapo kisha akatoweka na watu wake akimuacha mwanamke huyo anaushangaza mtaa akijilalamisha kwamba alikuwa akimpenda mno mumewe na hakuwa tayari kumuacha, watu wakabaki wanamshangaa kwa sababu kila siku Joh alikuwa akisalitiwa eti kawa na pesa ndipo kampenda ghafla? Alidhalilika mtaani hapo binti huyo.
Joel alijisahau mno, alikula bata mpaka mji ukamshangaa lakini alisahau kwamba alipewa mwezi mmoja tu pekee. Huenda ni utamu wa yale maisha mapya ndio ulimfanya asikumbuke kwamba muda wake ulikuwa unakaribia kufika hivyo akawa anaendelea kuponda raha mpaka siku moja ambayo alipokea ugeni, ugeni ambao haukuwa mgeni kwake. Alikuwa baharini kwenye boti na warembo kumi akiponda raha ndipo ambapo alishangaa boti hiyo inageuzwa uelekeo na kuelekea ndani zaidi ya bahari jambo lililomfanya kumfuata nahodha amwambie sababu ya kwenda kinyume na yeye ambaye ndiye alikuwa anamlipa lakini nahodha huyo alimwambia kwamba muda wake ulikuwa umeisha hivyo kuna mtu alihitaji kuonana naye.
Boti hiyo ilifika mahali ambako kulikuwa na meli ilipaki hapo, wanawake wale walirudishwa kuendelea na mambo yao huku yeye akiingia ndani ya meli hiyo ambayo bila shaka ilikuwa imepaki kusubiri tarehe yake ya kuondoka. Ndani ya meli hiyo alikutana na yule mwanaume ambaye ndiye alimletea lile begi la pesa, alishtuka na hapo ndipo akagundua kwamba siku zake zilikuwa zimeisha kama ambavyo aliahidiwa. Alishangaa mtu huyo kumpata kirahisi lakini mwanaume huyo alimahkikishia kwamba mtu anapokuwa anazipata pesa kwa mara ya kwanza hususani kwenye mazingira ambayo hata yeye mwenyewe hakuyatarajia basi lazima atataka kutamba kwamba hivyo hata ukihitaji kumtafuta hautumii nguvu kwani anakuwa maarufu ghafla lakini mbali na hilo alimhakikishia kwamba alikuwa akimfuatilia kila hatua ambayo alikuwa anaipiga.
Ndipo alipo mkalisha chini na kumpa mpango mzima wa lengo kubwa la kukutana naye, aliahidiwa maisha safi lakini pia alikuwa anaruhusiwa kutojiunga nao kama akiweza kulipa zile pesa ambazo alizitumia kula starehe kwa ule mwezi mzima. Angeitoa wapi tena pesa ya kulipa Joh! Kukubali ndiyo ikawa njia sahihi kwake, hata hivyo bila kupewa sharti hilo bado alikuwa tayari kujiunga na watu hao kwa sababu ni njia pekee ambayo ingemuweka mbali na umaskini.
Alijiunga na chuo cha siri ambacho kilikuwa chini ya mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Nikolai Gibson. THE FUTURE PROJECT, ndio ambao ulikuwa mpango rasmi wa kutekelezaji wa kuwafua vijana hao kwenye chuo hicho akiamini kwamba vijana hao ulikuwa ni mpango wa baadae wa jamii yao ya siri. Walitengenezwa vijana wengi shupavu huko ambapo waliokuwa wanaiva walikuwa wanafanyiwa majaribio kwa kupewa kazi za kuua kisha wanasajiliwa moja kwa moja na kuanza kupata malipo makubwa ambayo yaliwafanya waipende kazi yao na kuwa waaminifu lakini kulikuwa na sheria kali mno kiasi kwamba ambaye alikuwa anaenda kinyume na sheria hizo alikuwa anakufa na mkosaji aliwekwa wazi ili wengine wajifunze kwake.
Joeli John ndilo lilikuja kuwa zao bora zaidi kwenye mpango huo kwa sababu yeye alifundishwa moja kwa moja na Nikolai tena kwa mkono wake mwenyewe, alimtengeneza kwa misingi mikali mwanaume huyo ambaye alikuja kuwa binadamu hatari kwa sababu alikuwa anaifanya kazi kwa uchungu hususani kila alipokuwa anakumbuka maisha ambayo alikuwa ametokea. Miaka mitatu na nusu ilimfanya kuwa jabari la kutisha ambalo kila mwenzake ambaye alikuwa anye kwenye mafunzo hayo aliaanza kuliogopa. Joeli alitengenezwa akaiava haswa zaidi ya matarajio ya mwalimu wake na ndipo akapewa jina na utambulisho mwingine wa Yohani Mawenge ili asije kujulikana kwa mtu yeyote yule.
UKURASA WA 84 unafika mwisho.
Mpaka sasa Moja ya vitu ambavyo sijaona faida yake kwenye maisha yangu ni Mapenzi.....😅😅😅Shida nini Mzee unaogopa mizinga
Shukrani, uwe na safari njema mkuu.Ubarikiwe mno kiongozi, wacha ninogeshe safari yangu sasa ya kurudi home
😄😄😄Hongera mkuuMpaka sasa Moja ya vitu ambavyo sijaona faida yake kwenye maisha yangu ni Mapenzi.....
Ni upotezaji wa muda na pesa tu.
🤝🤝🤝Ungetutumia hata picha ya Yohane mawenge namkubali sana!! Na ticha wake Gib
Hahaha mwamba anaupiga mwingi sana mkuu.Ungetutumia hata picha ya Yohane mawenge namkubali sana!! Na ticha wake Gib
Yohan Mawenge atakapokutana na EdisonHahaha mwamba anaupiga mwingi sana mkuu.
Mwamba kabisa 🔥