FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #161
Okay
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Okay
Sawa, nilihisi ulisha potezewa nikausahau kabisa.....Mkuu Sisi tunafuatilia
Ni rahisi sana ku pata attention ni kurekebisha tu approaching style yako. Mfano badala ya kutuma kwa wiki mara moja jaribu kufululiza hata kwa wiki mbili tu kutuma kila soku episode moja alafu utupe mrejesho ila hii ya mara moja moja kwa wiki inachosha Sema basi tuNadhani hauna wachangiaji huu uzi hivyo huwa nausahau mara kwa mara....
Huwa naukumbuka tu wa IDAIWE MAITI YANGU...
Leo nitajitahidi tusome angalau episodes hata 5 ✍️
Ushauri wako ni mzuri ila hiyo approach ambayo unaisema nimeifanya kwa muda mrefu sana na ndiyo nilianza nayo tangu siku ya kwanza naleta simulizi yangu ya kwanza kuiandika ambayo wengi husema ndiyo bora zaidi ULIMWENGU WA WATU WABAYA.....Ni rahisi sana ku pata attention ni kurekebisha tu approaching style yako. Mfano badala ya kutuma kwa wiki mara moja jaribu kufululiza hata kwa wiki mbili tu kutuma kila soku episode moja alafu utupe mrejesho ila hii ya mara moja moja kwa wiki inachosha Sema basi tu
Hapana mkuu hii simulizi kali sana. Tupo tunaifatilia, mimi huwa sipendi sana kutoa comment simulizi ikiwa haijaisha na mara nyingi huwa sisomi ambazo hazijafika mwisho ila bidii yako ya kuweka ndo ilinishawishi niusome uzi wako.Sawa, nilihisi ulisha potezewa nikausahau kabisa.....
Nimeukumbuka baada ya kuona notifications zake
Sawa kiongozi shukrani.Hapana mkuu hii simulizi kali sana. Tupo tunaifatilia, mimi huwa sipendi sana kutoa comment simulizi ikiwa haijaisha na mara nyingi huwa sisomi ambazo hazijafika mwisho ila bidii yako ya kuweka ndo ilinishawishi niusome uzi wako.
Baada ya kuona uko kimya sana uzalendo ukanishinda ikabidi tukuombe utukumbuke.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja sana.Sawa kiongozi shukrani.
Saa 4 naweka episodes 5 hapa.
Hakuna andiko lako linaweza potezewa mkuu maana yote ni 🔥🔥🔥. Tunafuatilia haswa kila sentensi na nuktaSawa, nilihisi ulisha potezewa nikausahau kabisa.....
Nimeukumbuka baada ya kuona notifications zake
ShukraniHakuna andiko lako linaweza potezewa mkuu maana yote ni [emoji91][emoji91][emoji91]. Tunafuatilia haswa kila sentensi na nukta
Kaka una nafas yako taar katik hii Kaz 🙌🙌 usituweke sana walau once per weekHADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 80
“Mara nyingi mtu akihitaji kumhoji mtu kinguvu hawezi kwenda naye kwenye mazingira ya nyumbani kwake, huwa wanatumia magodauni, majengo yaliyo telekezwa, viwanja ambavyo havifanyi kazi na majengo kama hayo hivyo tuhakikishe anapatikana haraka Saimon na ikiwezekana kama hakutakuwa na mazingira ya kumuokoa basi auawe” ilikuwa ni amri ambayo ilitakiwa kufanyiwa kazi mara moja wakati huo.
Ulifanyika msako mkali kila sehemu ya jiji mpaka ilipotimu majira ya saa kumi na moja asubuhi ndipo ulipatikana mwili wa Saimon, mwili ambao ulikuwa umechakaa isivyo kawaida akiwa amekufa. Madam Kate alipewa taarifa ambayo ilimlazimu kuweza kufika mwenyewe eneo la tukio kuweza kumshuhudia moja ya vijana wake ambao alikuwa akiwategemea kwani alimfanyia mengi makubwa isivyo kawaida. Alishangaa kwa aina ya kifo cha kikatili ambacho alikufa nacho, kichwa kilitobolewa vibaya, shingo yake ilikuwa inatisha kuitazama hata mara mbili, hapo ndipo aliikumbuka kauli ya mwanasheria Jack kwamba siku hiyo isingepita hivi hivi lazima mtu wake mmoja angeweza kupoteza maisha. Jambo hilo lilikuwa la kweli kabisa na mpaka Saimon kuuliwa maana yake mtu huyo alikipata ambacho alikuwa anakitaka kutoka kwake, kama alikipata alichokuwa anakitaka maana yake ni kwamba baadhi ya siri zake zilikuwa uchi hivyo hakuwa salama tena, lilikuwa jambo la hari kwake.
Alitoa amri mwili huo ukazikwe porini huku kichwa chake kikiwa cha moto akiwaza jambo ambalo alitakiwa kulifanya kwa wakati huo. Hakujua kijana huyo alikuwa anamzidi wapi akili kwani kwenye maisha yake yote hakuwahi kukutana na mtu wa namna hiyo na watu wake walianza kupungua mmoja mmoja. Hofu ilimzidia alipo ikumbuka kauli nyingine ya Jack kwamba angejisikiaje siku ambayo angeuliwa kwenye mikono ya mtoto wake wa kumzaa? Alihisi kuna kitu kinamkaba shingoni hali ambayo ilimpelekea yeye kutoka hapo kwa hasira.
Aaliyah asubuhi sana kabla jua halijaroka alikuwa barabarani kuelekea Upanga. Safari yake ilikuwa ni kuelekea ilipokuwepo ofisi ya mkuu wa majeshi. Sababu kubwa ambayo ilimfanya aelekee huko ni baada ya kuyasikia yale mazungumzo kwenye simu kati ya bosi wake pamoja na mheshimiwa huyo ambaye alikuwa analalamika kutohusishwa kwenye masuala ya mhimu ya nchi. Alihisi kama raisi na mkurugenzi huyo walikuwa wanamsaliti kwa sababu alijua wana mahusiano ya kimapenzi yanayo waweka karibu kila wakati.
Akiwa ndani ya gari mawazo yalikuwa mengi, akiwa ndani ya gari ni taarifa nyingi zilikuwa zinakatiza kwenye kichwa chake akiwa anaziwazia kwa mengi. Mambo ambayo alikuwa anayaona yalikuwa yameanza kumtisha na kumpa hofu, hakujiona salama hata kwa watu wake hivyo aliona njia sahihi ni kuutumia kila udhaifu ambao aliona mbele yake. CDF alionekana kabisa kwamba alikuwa pamoja na watu hao lakini ugomvi wao wa muda mfupi yeye alihitaji kuutumia kwa manufaa yake binafsi.
Alifika kwenye ofisi hizo ambapo alikaguliwa, hakuwekewa vizuizi kwa sababu taarifa za kufika kwake hapo zilikuwa zimefika hata kabla hajawasili hivyo aliruhusiwa moja kwa moja kwenda kumuona kiongozi huyo wa juu kabisa kwenye jeshi.
“Aliyah nimeshtuka kupokea simu yako, wewe ni miongoni mwa watu wachache ambao wanaendesha vikosi vya siri na vyenye nguvu zaidi ndani ya taifa hili, unaweza ukaniambia ni sababu ipi imekuleta hapa kiasi kwamba umenisisitiza nisimwambie bosi wako kwamba tunaonana” mheshimiwa aliongea akiwa anasogeza kikombe kimoja cha kahawa kwa mrembo huyo ambayo ililetwa na katibu wake. Aaliyah aliipokea na kupiga funda moja akakirudisha kikombe mezani kwa sababu hakuwa hapo kwa ajili ya kuifurahia kahawa.
“Mimi najua kwamba wewe ni miongoni mwao ila nipo hapa kwa ajili ya kukupa nafasi ya pekee ambayo itakulinda hata kama kuna mambo yatatokea”
“Nisikilize Aaliyah, nakuheshimu sio kwa sababu upo karibu na mkurugenzi wako bali kwa sababu ya kazi yako tukuka ambayo wachache tunaojua uwepo wenu tunaitambua, nina muda mchache wa kukusikiliza hivyo fupisha maelezo yako nenda kwenye shida iliyokuleta hapa na asubuhi yote hii”
“Najua kwamba wewe ni miongoni mwa wanafamilia wa jamii ya siri ya LUNATIC SOCIETY” Mheshimiwa alikuwa mtulivu, hakuwa mtu wa papara kwa sababu papara haikuwa ikifaa maeneo kama hayo.
“Unaongelea kuhusu nini bibie?”
“Nadhani umetoka kuelezea ubora wa kazi ambayo huwa naifanya hivyo unajua kabisa kwamba nina taarifa za watu wengi kwenye taifa hili hata zako pia kwa sababu ni kazi yangu kuhakikisha nalilinda taifa kwa namna yoyote ile”
“Unataka kuniambia ulikuwa unanipeleleza mimi? Unaijua adhabu yake binti?”
“Sipo hapa kubishana na wewe, naijua nguvu yako, najua unaweza ukafanya lolote kukamilisha na kulinda mambo yako ya nyuma ya pazia lakini unatakiwa kuijua nafasi yangu mimi ni nani pia na hujui nyuma yangu kuna watu gani hivyo ukifanya jambo lolote la hovyo umma wote utajua wewe ni nani na unajishughulisha na nini nje ya kazi yako”
“Unataka nini?”
“Mimi nataka kufanya kazi na wewe”
“Umechanganyikiwa?”
“Mimi sijalewa ni asubuhi saivi. Jana ulikuwa unaongea na bosi wangu na nilimsikia vizuri mkipishana kwenye kauli hususani akionekana kukuficha taarifa nyingi za mhimu ambazo zinaweza kukusaidia wewe na jeshi lako. Mimi nataka nikusaidie wewe kukupa kila taarifa ambayo utaitaka”
“Halafu mimi natakiwa kukupa nini?”
“Ufanye kazi na mimi”
“Kivipi?”
“Kuna mpango wa kuiondosha hii jamii ya siri, najua nyuma yake kuna watu wenye nguvu ila wewe ukiwa upande wetu nina uhakika tutalikamilisha hili”
“Hahaah hahaha hahah nina uhakika haujui hata unacho kiongea”
“Kama makubaliano hayawezi kufikiwa basi naenda ila kitakacho kutokea usije ukanilaumu, kumbuka tu kwamba nina siri zako nyingi” Aaliyah alianza kutoka baada ya kuona mheshimiwa hamsikilizi.
“Subiri” alimuita kimamlaka na kumsogelea mpaka pale alipokuwepo.
“Mimi sikupenda kujiunga na hawa watu ila nafanya haya kwa sababu ya familia yangu, kama nikienda kinyume nao basi familia yangu inakufa”
“Hilo nalijua ndiyo maana nipo hapa”
“Kazi unafanya na nani?”
“Edison”
“Umekosea, huyu alitekwa baada ya kutoka Ikulu”
“Hajatekwa, yupo huru”
“Unataka kuniambia Jack hakuwa yeye?”
“Ile ni kama copy yake tu sio yeye”
“Plani yako ni ipi?”
“Nitakupa taarifa zote kwa sasa nilitaka tu nijue kama tupo upande mmoja kwa sababu hata bosi wangu amenisaliti simuamini tena” Kabla CDF hajatoa jibu lake kwenye hilo simu yake ya mezani ilianza kuita kwa fujo, simu hiyo iliyakatisha maongezi yao. Alisogea na kuipokea
“Hello!”
“Mheshimiwa, kuna tatizo kubwa” ilikuwa sauti ya upande wa pili kutoka kwa mtu ambaye alikuwa anahema na kuongea kwa sauti ya chini.
“Nani wewe?”
“Jaiwelo”
“Kuna tatizo gani?”
“Bosi ameuawa”
“Niambie kwamba unanitania”
“Huu ndio ukweli, ni mimi tu ambaye nimefanikiwa kutoka hai japo nipo kwenye hali mbaya na muda wowote naweza kupoteza maisha. Mtu ambaye amefanya hilo ni niiii!” mwanaume huyo hakumalizia maongezi yake zaidi ilisikika sauti moja kali ya kilio kukawa kimya, simu ilikuwa imekatwa.
“Jaiwelo, Jaiwelo ongea na mimi uko wapi na nini kimetokea?” sura na hali ya mkuu wa majeshi ilikuwa imebadilika kabisa. Alibaki anaongea mwenyewe mpaka akaibamiza simu hiyo na kuipasua. Alionekana kuchanganyikiwa hali iliyo anza kumpa mashaka hata Aaliyah, lilionekana ni jambo kubwa lilitokea.
“Hapana hapana, hii sio kweli” aliongea tena kwa kufoka akiwa anazunguka kila sehemu, jasho lilikuwa linamtoka kwa mbali usoni.
“Kimetokea nini?”
UKURASA WA 80 unafika mwisho.
Once per week au once per day?Kaka una nafas yako taar katik hii Kaz 🙌🙌 usituweke sana walau once per week
Respect mkuuSalute mwandishi