Ndugu Mwandishi huu mwendelezo wa leo ni kama story nyingine tofauti na hii FEBIANI BABUYA
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nashukuru kwa kunisaidia, maana nilihisi Konyagi ninayokunywa ndio inanichanganya!Ndugu Mwandishi huu mwendelezo wa leo ni kama story nyingine tofauti na hii FEBIANI BABUYA
Shukrani kwa kunikumbusha, nilichanganya na simulizi mpya.Ndugu Mwandishi huu mwendelezo wa leo ni kama story nyingine tofauti na hii FEBIANI BABUYA
Big up FEBIANI BABUYAHADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 66
“Kwa sasa wewe hautakiwi kufanya jambo lolote wala kujionyesha kwamba kuna kitu unajua kwani wakifahamu hiyo basi wewe ni maiti inayo tembea”
“Ila kwa sasa mimi hawawezi kuniua”
“Kwanini?”
“Kwa sababu nina mzigo wao wa thamani kubwa”
“Mzigo upi?”
“Mzigo wa dhahabu wa Madam Kate”
“Madam Kate ndiye nani?”
“Nadhani ndiye kiongozi wa jambo hili ambalo linaendelea”
“Ni mtanzania?”
“Ndiyo”
“Maana yake sio bosi mwenyewe”
“Umejuaje hilo?”
“Kwa sababu mwanzilishi wa hili jambo sio mtanzania. Kama kweli una huo mzigo wao wa thamani kubwa kama unavyo dai basi hawawezi kuwa wanakuacha hivi hivi lazima kuna watu watakuwa wanakufuatilia kwa kila hatua ambayo unaipiga na siku ambayo watafanikiwa kujua sehemu ambayo mzigo wako upo basi watakutesa kisha kukuua” Nicola alibaki kama amechanganyikiwa, Edison alisogea kwenye kabati ambapo alitoa laptop na frash mfukoni. Alihitaji kujua yaliyokuwa kwenye ile frashi hasa yalikuwa ni yapi maana tangu aipate frash hiyo hakuwahi kuifanyia kazi wala kutazama yaliyokuwa humo ndani kiasi kwamba mpaka yaondoke na maisha ya Issa kule Jangwani.
Walicho kishuhudia humo ndani kilikuwa kinatisha, kulikuwa na mipango mikakati yote kuanzia taarifa za baba yake Edison, kuuawa kwake na makomando wenzake lakini mpaka taarifa za ndani za jamii hiyo. Baadhi ya majina ya memba wa hiyo jamii likiwemo jina la daktari Namaki Prasad bila kumsahau bosi ambaye alikuwa ni Zulpha Mazipa, jina hilo alilikumbuka vyema kabisa kwa sababu lilikuwa jina la mama yake mzazi, kupitia hilo alithibitisha kwamba mama yake alikuwa hai tena akiwa ndiye kiongozi wa umoja huo kwa taarifa ambazo zilikuwa zimeainishwa hapo ndani.
Wote walibaki wameduwaa kama watu ambao wanaulizana maswali ila hakukuwa na wa kuweza kuyajibu kwa wakati huo.
“Inawezekana Madam Kate ndiye…….!” Nicola alikatishwa na Edison
“Yeah nadhani ndiye mama yangu mzazi”
“Oohhh shiiit! Nadhani hii ni habari mbaya sana kwako”
“Yeaha haiwezi kuwa nzuri”
“Kwamba mama yako ndiye mhusika wa haya mambo yote ambayo yanafanyika?”
“Inaonekana hivyo”
“Unaweza ukamkumbuka kwa sura labda?”
“Hapana sidhani kwa sababu ilikuwa ni zamani mno”
“Kwahiyo unahisi utafanya nini?”
“Siku ambayo nitakutana naye ana kwa ana ndiyo siku ambayo nitajua kitu ambacho natakiwa kukifanya ila kwa sasa bado sijui. Najaribu kuwaza ni mama wa namna gani anaweza kuamua kumuacha mtoto wake kwa kumkimbia! Ni mama wa namna gani hajawahi hata kujihangaisha kumtafuta mtoto wake licha ya taarifa kibao kusambaa kila sehemu kuhusu uwepo wangu tena nikipewa kesi ambayo sikuhusika nayo? Nina maswali mengi ya kumuuliza”
“Kama yeye ndiye kiongozi maana yake yeye ndiye ambaye anapanga mipango yote ili wewe uweze kufa”
“Hilo ndilo jambo ambalo siwezi kuyapata majibu yake mpaka sasa mpaka siku ambayo mimi nitakutana naye”
“Mimi naweza kuwasiliana naye na kuna mtu mmoja tu peke ambaye anaweza kutusaidia sisi kukutana au kufanikiwa kuongea naye”
“Nani?”
“Anaitwa Saimon, ni kijana wake mtiifu na wa karibu kwake japo nahisi amesha anza kunishtukia na sidhani kama ananiamini tena baada ya kumuuliza baadhi ya maswali”
“Kwani wewe huyu Madam Kate haumfahamu kwa sura?”
“Hapana, wakati nafanya naye mawasiliano sura yake ilikuwa imezibwa”
“Maana yake kama anaziba sura yake basi kwenye maisha ya kawaida atakuwa ana jina lingine ambalo analitumia mbali na hilo la Madam Kate pamoja na jina lake la kuzaliwa la Zulpha Mazipa, lazima kuna jina lingine ambalo analitumia na hilo ndilo jina ambalo nalihitaji”
“Saimon ndiye mtu pekee ambaye atatusaidia kwa hilo”
“Basi wewe unatakiwa kurudi na kuendelea na maisha kama ya mwanzo kwani kama ukipotea kwa sasa lazima watakuwa na mashaka na wewe. Kwa sasa nataka kukutana na yule binti mpelelezi Aaliyah, baada ya hapo utanipeleka kwa huyo Saimon”
“Sawa, kuwa makini Edison” alitamka kinyonge Nicola, ni kama alijihisi amani na salama kuwa karibu na mtu huyo lakini muda haukuwa sahihi. Mambo ambayo waliyaona kwenye frash hiyo yalikuwa na maelezo ya mipango mingi ambayo ilikuwa imechukua maisha ya watu wengi mno lakini kulikuwa na majina ambayo mengine hawakuwahi kuyasikia popote lakini yake machache ambayo walikuwa wameyapata nayo walitakiwa kuyafanyia kazi kubwa ili kuweza kuwapata wahusika wake ambao ndio walikuwa wamiliki wa majina hayo hususani mama yake mzazi ambaye ndiye alidaiwa kuwa kiongozi wa jamii hiyo ya siri na huenda ndiyo sababu kubwa ambayo iliwafanya watu hao kuitafuta hiyo frash kwa nguvu kubwa kwa sababu ya uwepo wa jina la bosi wao ndani ya taarifa zilizokuwa ndani.
Aliamshwa na maji ya baridi kali, alishtuka kwani ubaridi wake haukuwa wa kuvumilika kirahisi hali ambayo ilimfanya ajihisi alitundikwa ndani ya friji ambayo haikuwahi kuzimwa kwa mwaka mzima. Kushtuka kwake kulipokelewa na taa zenye mwanga mkali, ilimlazimu kuyafumba macho yake kisha akayafumbua kwa mara nyingine macho yakiwa yanaona nyota nyingi mbele yake. Baada ya muda wa dakika tano macho yake yalirudisha uangavu wake, hapo ndipo akagundua kwamba alikuwa ametekwa na watu ambao hakuwafahamu na hiyo haikuwa shida kwake kwa sababu alikuwa ni mtu mwenye soko kubwa kwenye utafutwaji wake.
Kumbukumbu zake zilimpa fahamu ya kumrudisha nyuma kujua kilichokuwa kimetokea, ndipo alikumbuka jambo ambalo lilitokea kipindi ambacho walikuwa wamefika pale Morocco baada ya kutoka kufanya mazungumzo na raisi wa nchi akiwa anasafirishwa kwenda mahali ambako binafsi hakuwa akijua kwamba ni wapi. Eneo lile alilikumbuka kwa usahihi kutokana na tukio la kutisha ambalo lilitokea pale kisha yeye akabebwa na watu wasio julikana na baadae akachomwa sindano tatu kwenye mwili wake zilizo mfanya akazima na wakati anarejesha fahamu zake ndipo alijikuta akiwa ndani ya eneo hilo. Alitoa tabasamu hafifu kwa sababu hakuwa na matumaini yotote ya maisha yake tena na hilo alikuwa analitambua vizuri kwamba ana muda mchache wa kuendelea kuivuta pumzi ya dunia, hali hiyo haikumsumbua hata kidogo alijiandaa maisha yake yote kuikabili.
Chumba ambacho alikuwepo kilikuwa kikubwa, kilizungukwa na walinzi wenye silaha kali kila kona huku mwanaume mmoja mbavu ambaye alikuwa kifua wazi ndiye ambaye alikuwa anashughulika naye kwenye suala zima la kuhakikisha anaamka na kuwa macho kwa kumpatia dozi ya hayo maji ya baridi kali. Alikisa kichwa chake kukiweka vyema kwani alijua hapo asingepata nafasi ya kulala kwa mara nyingine tena. Lango la chumba hicho lilifunguliwa ndipo aligundua kwamba kulikuwa kumekucha tayari hususani baada ya kufanikiwa kuuona mwanga wa jua kwa mbali kutokana na nafasi finyu ambayo ilikuwepo wakati lango lile linafunguliwa.
UKURASA WA 66 unafika mwisho.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app