SEHEMU YA 412.
Omari mara baada ya kuingia ndani ya ofisi ya Roma alishangazwa na uwepo wa mwanamke mrembo kama Amina, Omari kutokana na kutofatilia sana mambo mengi hakuwa akimjua Amina, kwa namna mrembo huyo alivyokuwa akimwangalia Roma alijua lazima kungekuwepo na mahusiano , hata hivyo alikuwa akisikia Habari za Roma kuwa na wanawake wengi , jambo ambalo lilimshangaza na kujiuliza yeye kafanikiwa vipi , kwani yeye mpaka muda huo alikuwa akihangaishana na Queen ambaye ni mjamzito na hakuwa akimtaka licha ya kwamba alikuwa akitaka kumuoa na mimba yake.
Roma wala hakujali Zaidi ya kutabasamu na Omari alichukulia hilo kama jibu.
“Hades ni mbinu gani unatumia kuwapata hawa warembo mbona mimi wananikataa”
“Umeanza lini kujilinganisha na mimi?”Aliuliza Roma na kumfanya Omari kucheka.
“Sitaki kujilinganisha na wewe , hata hivyo wewe ni mfalme Pluto ni haki kwako kupendwa na warembo sifa yako inakutangulia pasipo ya kutambulishwa”Aliongea Omari huku akiendelea kumwangalia Roma , ukweli alikuwa akimuona kuwa na mabadiliko makubwa tokea mara ya mwisho walivyoachana.
“Hades kabla hatujaendelea nataka uniambie imekuwaje sioni uwezo wako wa kijini tena , mara ya mwisho nilikuacha ukiwa katika levo ya mzunguko kamili , na kama nitasahihisha kauli yangu naweza kusema nilikusaidia kufikia levo ya mzunguko kamili?”
“Nishavuka hio levo na sasa nipo ya juu Zaidi, Levo ya kuipita Dhiki”Aliongea Roma na kumfanya Omari kushangaa na kusimama , akiwa kama haamini.
“Unadanganya, haiwezekani?”
“Hahaha,.. hata mimi najua haiwezekani , lakini ndio hivyo nipo levo ya kuipita Dhiki na huwezi kuniletea upinzani tena”Aliongea
“Kama ni kweli upo Levo ya kuipita Dhiki kwanini siwezi kuona uwezo wako wa kijini ndani yako na kugundua levo uliopo?”
“Hio ndio sababu kati yangu na nyie , mimi nilianza kujifunza mbinu za kijini za njia ndefu”
“Unamaanish ya Maandiko ya Urejesho?”Aliuliza kwa mshangao na Roma alitingisha kichwa na kumfanya Omari kuduwaa mno , alijiambia kama ni hivyo si atakuwa sawa na wale Grand Master waliopo kwenye vitabu vya historia huko ujinini, alijiambia kama ni kweli basi Roma hakuwa mtu wa kawaida kabisa na sio kwake tu lakini mpaka kwa viumbe wasioonokena.
“Nilikuja nyumbani kwako wiki kadhaa zilizopita , nadhani mkeo hajakuambia kama nilifika?”Aliongea Omari na Roma alimwambia hajui.
“Ndio niliweza kupata namba yako ya simu kupitia mkeo mrembo Edna”
“Edna ndio kakupa namba yangu? Hajaniambia kuhusu swala hilo”
“Ndio , kilichonileta nyumbani kwako ni kutaka kuhakiki kile kilichotokea kwa Meli ya kivita ya Marekani kulipuliwa , kwani jeshi letu lilipokea malalamiko kutoka taifa la Marekani walionyesha hofu yao juu ya ushirikiano wetu wa karibu na taifa la China”Aliongea na kumfanya Roma kumeza mare kidogo.
“Wewe unahisi ndio niliehusika na kushambuliwa kwa meli ya kimarekani ya kivita?”
“Jeshi letu limethibitisha hauhusiki na hata kilichonileta nyumbani ilikuwa ni kuthibitisha Alibi yako na tumeweza kutoa ushirikiano wa kutosha na Serikali ya kimarekani na swala limemalizwa juu juu , lakini hata hivyo halijafika mwisho”
“Unazungumzia kuhusu mtu aliegizia sura yangu?”Aliuliza Roma na Omari alitingisha kichwa.
“Nafasi yako katika ulinzi wa taifa ni ipi, ijapokuwa nakufahamu kama una mafunzo ya kijini , lakini sijakufahamu vizuri”
“Hahaha.. Hades inaonekana haupo siriasi , inamaana umeshindwa hata kutafuta kuhusu taarifa zangu?”
“Niliona hazina umuhimu , kwanza kwanini nizitafute kama wewe mwenyewe unaweza kuniambia , au yale maneno yako siku ile yalikuwa hewa , ukitaka tuwe marafiki lazima uniweke wazi nafasi yako hapa nchini , nione kama una faida au hauna faida”
“Na kama sina faida?”
“Ni bora niendeleze urafiki na warembo wangu”
“Hahaha… , naweza kukuelezea lakini vipi kuhusu wewe , unaweza kuniambia kila kitu”
“Kuna utofauti mkubwa kati yetu”Aliongea Roma na kumfanya Omari kuona kuna ukweli , hata hivyo hakuna siku ambayo aliamini angekuja kuongea na Hades ana kwa ana namna hio , ilikuwa bahati kwake mara baada ya kusikia Hades yupo Tanzania.
Ilibidi ili maongezi yaendelee Omari ajitambuliesha vizuri kwa Roma juu ya nafasi yake ndani ya serikali ya ulinzi ya Tanzania na mpaka anamaliza Roma aliweza kufahamu Omari alikuwa ni mtoto wa CDF wa majeshi ya Tanzania bwana Gambino Tozo na akiwa kama mtoto wa kwanza na wa mwisho wa kiume ndani ya familia hio lakini pia kilichomfurahisha ni kwamba Omari alikuwa akifanya kazi chini ya kitengo cha usalama wa taifa.
“Sio mbaya kuwa na urafiki wa mtoto wa mkuu wa majeshi , tokea nifike hapa nchini sijapata rafiki lakini bado nakuona hunifai maana umezidi ubahiri , inakuwaje mtoto wa CDF unaendesha kirikuu?”Aliuliza Roma kwa kebehi huku akijisahaulisha hata yeye alivyokuja Tanzani alikuwa akibeba mizigo.
“Mzee hanipi hela yoyote ya matumzi na ndio kwanza nimerudi Tanzania , kutembelea kirikuu ni kubana matumizi maana muda si mrefu nataka nioe”.
“Nielezee sasa kwanini ukataka kuonana na mimi?”Aliongea Roma akipotezea sababu za Omari zisizokuwa na mashiko.
“Kilichonileta ni kutaka kupata jibu kutoka kwako , nipo nafanya uchunguzi binafsi”
“Uchunguzi gani?”.
“Kuhusu Profesa Yan Buwen”Aliongea Omari na kumfanya Roma kushangaa kidogo
“Naona unaonekana kumfahammu ?, ndio ninaemfanyia uchunguzi binafsi kwa sasa na ndio kazi za aina mbili zilizonirudisha hapa Tanzania”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kidogo alikuwa akikumbuka kuhusu Yan Buwen kuhusika na kifo cha Profesa Shelukindo , lakini kitendo cha wanajeshi wake kutowaruhusu kuendelea kufanya uchunguzi Zaidi alikuwa na maana yake.
“Hades labda haufahamu hili , unadhani kwasababu gani nimeweza kujifunza mbinu za kijini na kufikia levo ya Nafsi na kuja uraiani?, Katika kanuni za Hongmeng binadamu yoyote aliebahatika kujifunza mbinu za kijini na kufikisha levo ya Nafsi haruhusiwi kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida”.
“Kwahio kutoka kwako Hongmeng ni kutokana na maagizo ya kumfuarilia Yan Buwen?”Aliongea Roma na kumfanya Omari kutabasamu.
“Una uwezo mkubwa sana Hades wa kuelewa mambo, labda kwa kitu ambacho haukifahamu ndani ya taifa la China , kuna mgogoro kati ya Serikali pamoja na Hongmeng”
“Unataka kumaanisha nini?”
“Hongmeng hawaungwi mkono kwa asilimia mia moja na familia zote kubwa ndani ya China na wanatafuta mbinu kuondoa Koneksheni iliopo na Serikali kujitegemea kwa asilimia mia moja”Aliongea Omari na kumfanya Roma kuguna.
“Hilo nililitegemea , licha ya kwamba sina sana uelewa na jamii hizi za Hongmeng , lakini hili linahusiana vipi na Yan Buwen?”
“Kwasasa siwezi kujibu hili swali mpaka uchunguzi ukamilike lakini Afande Yang kutoka China ambaye ni mkuu wa majeshi ya Ardhini ni moja ya familia ambayo haikubaliani na jamii za siri kuingilia maswala ya kiserikali na wasiwasi wa Hongmeng ni Afande Yang kushirikiana na Athena”Aliongea Omari na kumfanya Roma kushangaa, ijapokuwa mwenyewe alikuwa akiijua nguvu ya Athena ndani ya dunia kwa kufahamika kama The Doni lakini hakuwahi kuwaza sana ushwishi wa Athena ndani ya serikali ya China.
“Unamaanisha kuna uwezekano wa Afande Yang kushirikiana na Athena? , hili ni jipya kwangu na sijawahi kulifikiria hapo kabla, lakini hata hivyo kwanini liwe na muingiliano na Yan Buwen?”
“Yan Buwen ni mwanasayansi na mbinu pekee ambazo Familia yote ya ukoo wa Yang unachoamini ni katika sayansi , wanaamini sayansi inaweza kuwaweka kwenye nafasi ambayo Hongmeng haiwezi kuingilia maswala ya serikali , mathalani katika jeshi ndio maana inawapa wasiwasi Hongmeng na kuona Athena anaweza katumia udhaifu wa mgogoro uliopo kupindua ushawishi wao katika ulimwengu wa kawaida , mathalani ndani ya serikali ya China , nguvu ambayo waliweza kuidumisha kwa miaka mingi”Aliongea na kumfanya Roma kuona huenda hilo likawezekana.
“Wewe uko upande upi?”
“Nimeweza kupata nafasi ya kuishi katika ulimwengu wa kawaida licha ya kuwa na levo ya Nafsi ya mafunzo ya kijini kutokana na kuahidi nitafanya uchunguzi ya kile kinachoendelea na kazi niliopewa ni kumfuatilia Yan Buwen , kuhusu Hongmeng kuendelea na utawala wao wa siri ndani ya Serikali ya China , hili ni jambo ambalo halina athari yoyote kwangu hata hivyo mimi ni mtanzania”Aliongea.
“Mtanzania ambaye ni shushu wa Hongmeng naweza kusema hivyo”
“Unaweza kuniita hivyo, mwanzoni nilivyoanza kujifunza mbinu za kijini niliwaza jambo moja tu , kuponyesha jicho langu na mwanamke ninaempenda kuniona wa kawaida na kunipenda , lakini mara baada ya kupanda levo na kufikia ya Nafsi na kutimiza haja zangu uhitaji wa kuwa na mwanamke wa ndoto yangu ulirudi upya lakini sheria zinanibana, hivyo naamini mimi na wewe hatuna utofauti sana , naamini upo tayari kufanya lolote kwa jina la Mapenzi”
“Unachoongea ni sahihi ninaweza kufanya chochote kama mtu wangu yoyote wa karibu kama ataguswa , hata kama ni kupindua miliki zote za kijini”Aliongea Roma na kumfanya Omari kucheka sana.
“Inaonekana sisi tunafanana sana Roma?”
“Hapo kwenye kufanana usiniingize kuna mambo unayafanya mimi siwezi kuyafanya , kwanza mimi sio mbahiri , ninavyokuona huna aibu mimi mwenzio nina aibu , nina wanawake wengi na wewe unaonekana unahaingaika kwa mwanamke mmoja…”Aliongea Roma na kumchekesha sana Omari.
“Haina haja ya kuendelea sijamaanisha tunafanana kwa asilimia mia , ila kuna vitu vinatufanya tufanane”Aliongea
“Niambie kwanza kwanini ukaamua kunielezea maswala ya Hongmeng ?”
“Kwasababu wewe ndio unajua Zaidi kuhusu kanuni za Anga lakini pia Afande Yang alionekana kutembelea Tanzania hivi karibuni , kwa taarifa nilizonazo jambo hili nimeamua kulifanya kimya na hata kuacha kuhusisha familia yangu, swali langu kwako ni je kuna namna unavyohisia mtu alieigiza kuwa wewe?”
“Nina maadui wengi na jambo la kufurahisha maadui zangu hawajawahi kukaa chini na kutulia ni wenye kusubiria nafasi ili kunichokoza , mtu ambaye ameigiza kuwa mimi sina haja ya kumtafuta ,mpango wake ulikuwa ni kunichokoza na naamini bado hajatimiza malengo yake na atarudi tena , kuhusu yeye kufanana na mimi hilo halinipi shida sana”Aliongea na kumfanya Omari kukuna kichwa.
Omari na Roma waliongea kwa muda mrefu mpaka ilipofikia muda wa chakula cha mchana Omari aliondoka.
********
Muda wa jioni Roma aliweza kuendesha gari aina ya Rolly Royce mpaka kwenye kampuni ya Vexto kwa ajili ya kumchukua Edna kuelekea kwenye kusanyiko la marafiki wa chuo,, kwasababu alikuwa washawasiliana ni ndani ya dakika mbili tu Edna alievaa akapendeza alitokea eneo la maegesho ya gari na kumfanya hata Roma mwenyewe kushangaa kidogo , ijapokuwa aliamini Edna asingevaa mavazi aliotoka nayo nyumbani lakini hakutarajia angeweza kupendeza kwa kiasi hicho.
Roma alimfungulia mke wake mlango huku akiwa amepambwa na tabasamu na kwa upande wa Edna alionekana kuridhika na namna ambavyo Roma amevaa na kuweka sawa nywele zake , ilionekana Roma siku hio kabla ya kurudi nyumbani alienda saluni.
Ni ndani ya dakika chache tu Roma aliweza kuingiza gari kwenye lango la hoteli ya Hyatt Kilimanjaro iliokuwa pembezoni mwa bahari , mwanga wa hoteli hio usiku ulifanya eneo lote kupendeza.
Baada ya wote kushuka kwenye gari Roma hakuwa na haja ya kulipeleka maegeshoni bali alimpatia mtu wa kazi hio ufunguo na kisha alimsogelea mke wake mrembo Edna na kisha kumpa ishara ya kushikilia mkono wake.
Edna hakusita sana kwani haikuwa mara ya kwanza kufanya hivyo,
This is far as you go , Don’t test your luck”Aliongea Edna akimpa onyo Roma kwamba asijaribu kupeleka mkono wake sehemu zingine za mwili, Edna alionekana kuwa siriasi mara baada ya Roma kumvuruga,
“I am your to command”Alijibu Roma huku akitabasamu lakini kabla hawajaanza kupiga hatua kuelekea ndani iliingia gari nyingine eneo hilo na Kwenda kusimama mbele yao.
Ilikuwa gari zuri kweli ya kifahari kampuni ya BMW Sport Car ambayo ni machache sana kuyaona Tanzania.
Baada ya gari hio kusimama alishuka mwanaume mmoja wa kizungu kijana alievalia suti nyeusi kampuni ya ‘Armani ‘ huku akiwa na miwani nzuri ya macho ilionakshiwa na madini ya dhahabu , alikuwa amependeza haswa kwa mwonekano wake na ilimfanya kuonekana wa kuvutia mno, kitendo cha mwanaume yule kushuka kilimfanya Edna kumsogelea Roma karibu zaidi kuliko isivyokuwa kawaida.
Upande mwingine wa mlango ulifunguliwa na akatokea mwanamke mwingine wa kizungu pia alievalia Earings kubwa na gauni lake la maua mua ambalo linavikamba vilivyoshikilia mabegani ambalo lilifanya umbo lake kuonekana vyema , ijapokuwa hakuwa na mwili mkubwa lakini alionekana kupendeza sana.
“Edna Long time no see”Aliongea yule mwanaume kwa kingereza akimaanisha kwamba hawajaonana muda mrefu na Edna alimwangalia mwanaume huyo aliekuwa mbele yake na kisha macho yake yakageukia upande wa mwanaumke mrembo alieambatana nae.
“Not Long enough”Alijibu Edna akisema sio kitambo sana.
“Glad to see you’re still the same old stone -Cold Edna”
“Nimefurahi kukuona ukiwa Edna yule yule kauzu”Aliongea yule mwanamke huku akishika shika nywele zake kwa mapozi , lakini Edna hakujali kuendelea kuongea nao Zaidi ya kumpa ishara ya Roma kuendelea na safari yao kuingia ndani ya hoteli hio
Jambo hilo lilimfanya Roma kushangaa kwani Edna alionekana kutokuwa na muda wa kuwatambulisha watu hao kwake, wanaume wale walifuatishana na Edna na Roma kiupande upande.
“Edna kwanini usinitambulishe mume wako , nimesikia kutoka kwa Richie umeolewa , sikushawishika mwanzoni lakini nadhani ni kweli”Aliongea na kumfanya Edna kusimama na kisha kumwangalia yule mwanaume.
“You think you are only ones who can get married?”
“Mnafikiri nyie ndio mnaweza kufunga ndoa tu?”
“Edna nafikiri sio alichokimaanisha , wote hakuna alietarajia mwanamke kauzu wa chuo kama wewe unaweza kupata mwanaume hivi karibuni na kufunga ndoa, kama marafiki zao tunazo kila sababu za kujua maendeleo yako”Aliongea yule bidada wa kizungu na kisha akamgeukia Roma.
“Naamini huyu ndio mume wako Edna, Mr Roma kwa jina naitwa Hanson nilikuwa chuo kimoja na mkeo , huyu hapa ni mke wangu anafahamika kwa jina la Cindy hata yeye alikuwa darasa moja na kozi moja na Edna”Aliongea bwana Hanson lakini Edna alionekana hakutaka Roma aongee nao licha ya kutojua imekuwaje Hansoni kuweza kufahamu jina mume wake.
“Kwasababu mnafahamina wote , mnaonaje tukiingia sasa ndani?”Aliuliza Edna na akampa ishara Roma ya kufuatishana nae Kwenda ndani pasipo kuwajali.
Baada ya kuwaona wameingia ndani Cindy alimwangalia Hansoni usoni na kisha akatoa tabasamu la kejeli.
“Babe you miss that woman , don’t you?”
“Babe unammisi yule mwanamke si ndio?”
“She is even prettier than she was back in college , A beuty that has only grown , how can I not miss that?”
“Amekuwa mrembo kuliko alivyokuwa chuo , kwa uzuri ule uliongezeka kwanini nisimkumbuke?”
“Hanson huoni kwamba unavyomsifia mbele yangu nitapata wivu?”
“Hahaha,, kipindi kile aliponikataa kule chuoni , sikuweza kumzingatia tena , Mwanamke yoyote ambaye anauwezo wa kunikataa mimi no matter her beuty is nothing but a pitfull insect”Aliongea huku akitoa tabasamu la kejeli la kuonyesha kutojali.
“Edna nini kinaendelea mbona unaonekana kuwakwepa?”Aliuliza Roma wakati wakiingia kwenyeLift.
“Hanson alikuwa ni rafiki yake Richie na mwanadarasa mwenzake kipindi ambacho nilikuwa nikisomea Masters , Cindy yeye tulikuwa darasa moja”
“Sio mbaya , Hanson sasa hivi anajihusiaha na nini?”
“Hanson ni moja ya familia kubwa sana ndani ya Norway na wanamiliki makampuni yanayojihusisha na maswala ya mabenki sio maarufu sana kwani mabenki yao yapo ndani ya bara la ulaya pekee , baada ya kumaliza masomo niliweza kufahamu familia yao pia wanamiliki baadhi ya viwanda vikubwa vya utengenezaji wa magari makubwa lakini pia ni moja ya wamiliki wa hisa kwenye kampuni ya Fyatt ya kiitaliano, kuhusu Cindy yeye ni Mwafrika kutoka South Afrika lakini familia yao yote Maisha yao yapo Uingereza, Mama yake anafanya kazi kwenye shirika la kimataifa la IMF”Aliongea Edna kwa kirefu
“Mh ndio maana wamekuja kwenye gari kali , inaonekana ni wazito huko duniani”Aliongea Roma.
“Upo sahihi labda tu ni kwasababu sijakutambulisha vizuri kwa Richie lakini hata yeye usimchukulie wa kawaida kwasababu ameamua kuja kufanya kzi kwenye kampuni yangu, Richie hakuwa akisomea kama mwanamitindo Oxford , yeye alikuwa akichukua maswala ya Banking and Finance na maswala ya mitindo ni kama fani tu anayopenda nje ya taaluma yake , wakati napendekeza aje kunisaidia Tanzania alikuwa amepata ofa ya Kwenda kufanya kazi ndani ya kampuni ya Kimarekani ya JP Morgan lakini Richie hakupenda kazi za kukalishwa chini , hata hivyo ukiachana kuwa marafiki zangu lakini pia alikuwa akipenda mazingira ya Tanzania ndio maana alikubali nilipopendekeza aje kunisaidia , ni rafiki mkubwa sana wa Hanson”.
“Hehe .. Babe kwa maelezo yako nadhani sisi tunaweza kuwa masikini kati ya wageni wote wa Richie?”Aliongea Roma kwa utani, lakini Edna alionekana kutopenda lakini alipotezea.
“Unachoongea ni sahihi , ijapokuwa nimeweza kuipaisha Vexto kimataifa lakini watu kama Hanson siwezi kujilinganisha nao , utajiri wa familia zao hakuanza juzi ni watu waliojikita kibiashara tokea zamani”
“Wakati ndio naanza masomo yangu nchini Uingereza bibi alinilazimisha kujihushisha na maswala yote yaliokuwa yakijumuisha familia za kitajiri zilizokuwa ndani ya chuo , hio yote ilikuwa ni kunifanya kupata ‘Exposre’ lakini pia kutegneneza koneksheni” Wakati Edna anamaliza kuongea lift ilifunguka juu kabisa na kuingia kwenye korido ambayo walichukua moja kwa moja mpaka eneo husika , mara baada tu ya kuingia kulikuwepo na watu wengi kidogo kuliko Roma alivyotarajia akiwemo Richie ambaye alikuwa na mke wake.
Ingekuwa Roma anafuatilia mambo mtandaoni angegundua uwepo wa meli ya kifahari iliokuwa ikitangazwa kutia nanga kwa kuleta matajiri kutarii ndani ya maeneo ya Dar es salaam na Zanzibar , wengi wao waliluwa ni hao waliokuwepo hapo ndani.
“Oh! !My beloved Edna you’re finally here So this is your husband Mr Roma I suppose ?”
“Oh Mpendwa wangu Edna , hatimae umefika , nadhani huyu ndio mume wako Mr Roma nadhani?”Walilakiwa na mwadada mwingine wa kizungu aliekuwa na macho ya bluu na lipsi zilizokuwa nyekundu mno kwa kupakwa marangi.