Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Hatariiii
 
Ndiooooo
 
Hivi juma tano c leo? Singanoja, sema kitu, tusubiri au tuvute kete tu
 
AUTHOR : DR SINGANOJR
SPONSORED BY : MIND LINK ENTERTAIMENT.

SEHEMU YA 447
Zilipita dakika kama therathini hivi wakati waheshimiwahao wakiendelea na kikao , mlango wa ukumbi ulifunguliwa na akaingia msaidizi wa Raisi afahamikae kwa jina la Kabwe.
“Mheshimiwa tukio la kigaidi limekuwa neutralized na kikosi cha kundi la Yamata Sect”Aliongea Kabwe kuwafanya waheshimiwa kushangazwa na taarifa hio
“Yamata Sect ndio kundi gani?”
“Yamata Sect ni kundi la kihalifu kutoka Japani ambalo mwaka uliopita mkuu wa kundi hilo alikuwa ni Noriko Okawa , mpaka alipouliwa na Roma Ramoni nchini Japani na madaraka kuhamia kwake”Aliongea Mkurugezi wa kitengo cha usalama wa Taifa na kufanya chumba chote kuwa kimya na kumwangalia.
“Mkurugenzi kundi hili kama ni la Japani imewezekanaje wakahusika kwenye misheni hii?”
“Kwa taarifa tulizo kuwa nazo mpaka sasa kundi hili liliingia Tanzania wiki kadhaa zilizopita kama wafanyakazi wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kuunga vifaa vya simu kilichopo Kibaha, ujio wao Tanzania nadhani ni kwa ajili ya kuimarisha ulinzi wa Familia ya Roma dhidi ya Yan Buwen”Aliongea na wote walionekana kuelewa hata hivyo habari za Yan Buwen hazikuwa mpya.
“Mkurugezi taarifa ya ujio wa hawa Yamata Sect mbona haikufika ofisini kwangu?”
“Mheshimiwa taarifa ya ujio wao tuliweza kuipata siku ya jana baada ya muda mrefu wa uchunguzi”Alijibu Mkurugenzi.
“Kabwe kuna taarifa nyingine?”
“Ndio mheshimiwa, tumeweza pia kupata taarifa ya kikosi cha The Eagles kumkamata jasusi wa siri afahamikae kwajina la Aishapova wa familia ya Kyluchevsky wakati alipokuwa akijaribu kumteka Profesa Clark na wenzake wa tano ambao wanne wote wamekufa hapo hapo”Aliongea na kuwafanya wote kuangaliana.
“Mheshimiwa nadhani kama huyu Aishapova yupo hai tuombe The Eagles watupatie ili tuweze kumuhoji na kujua sababu nyingine ambayo imepelekea kuungana na kikosi cha Alshababu na kutaka kutushambulia”
“Naunga hoja pendekezo la Waziri wa ulinzi , tunaweza kupata majibu yote kwa kumuhoji huyu mwanamke , ili kujua ni mpango gani ambayo Klyuchevsky wanapanga zidi ya Tanzania”Aliongea Waziri mkuu , lakini muda huo huo Katibu wa Ikulu alionekana kuingia tena katika ukumbi hio na kuwafanya viongozi hao kumwangalia kujua kuna taarifa ipi nyingine.
“Mheshimiwa Balozi kutoka Urusi yupo kwenye Line kupitia Vidio call”Aliongea mwanamama huyo na mheshimiwa alimpa ishara ya kuunganishwa nae na ndani ya muda mfupi tu Tv iliokuwa imefungwa ukutani ndani ya ukumbi huo ilionyesha sura ya mheshimiwa Balozi Anneth Kimba.
“Mheshimiwa kikosi cha The Eagles kifahamikacho kwa jina la Expendable kimeanza kufanya mashambulizi zidi ya wanafamilia wa Klyuchevsky, Wizara ya mambo ya nje ya Urusi wametoa malalamiko yao na kutishia kuiwekea vikwazo nchi yetu kwa kukata biashara zote zinazofanyika kati ya Urusi na Afrika Mashariki kama hatutachukua hatua za kumzuia Roma”Aliongea mwanamama huyo mara baada ya kutanguliza salamu za awali na kuwafanya viongozi wote kushangaa
Hakuna alieamini kama Roma angeweza kuchumua mamuzi haraka ya namna hio ambayo ni kama yana athiri diplomasia ya taifa.
“Expendable! ? , ndio kikosi gani hicho?”Aliuliza Mheshimiwa Raisi huku akionekana kukunja ngumi kwa hasira.
“Kwa taarifa chache nilizokuwa nazo hapa mheshimiwa , Kikosi hiki ni cha kijeshi kutoka kundi la The Eagles ambacho pia kina muunganiko wa moja kwa moja na Profesa Clark , Miaka mitano iliopita Profesa Clark alitangaza kamwe tkutojihusisha kutengeneza siraha za aina yoyote za kibailojia lakini hata hivyo aliweza kutengeneza dawa ambayo inasaidia wanajeshi kupona haraka mara wanapopata majeraha lakini moja wapo ya athari ya dawa hio ilifanya miili ya wanajeshi kuwa na nguvu kubwa zisizo za kawaidaa , kutokana na matokeo hayo kikosi hicho kilitolewa katika mjumuisho wa jeshi la kawaida la The Eagles na kuingizwa katika kundi la Ninja lifahamikalo kwa jina la Zero Unity na kupatiwa jina la Expendable , idara nyingi za kijeshi zimewabatiza kikosi hicho kwa majina mengi ikiwamo jina lao maarufu la Assassin from Hell”Aliongea Mkurugenzi kutokea maelezo.
“Kama ni hivyo hili swala lina haribu uhusiano wetu na Urusi ukizingatia tunao ushirikiano mwingi wa kibiashara , Roma anaharibu uhusiano wa kidiplomasia wa hili taifa”Aliongea Raisi Senga kwa hasira.
“ Mheshimiwa nadhani tukiangalia swala hilo kwa mtazamo mwingine kuna faida , Nchi yetu haijawahi kuwa na ushirikiano mzuri sana na taifa la Urusi na sidhani kama washawahi kutuchukulia siriasi”Aliongea Mheshimiwa Waziri.
“Unamaanisha nini?”
“Ninachomaanisha kama serikali ya Urusi imeruhusu familia ya Klyuchevsky kutaka kutulipua na bomu la kibailojia kwa kupitia kikosi cha kigaidi cha Alshababu kuna ushirikiano gani hapo , wao ndio wametuchokoza kwa kuona sisi hatuna umuhimu na wanaweza kufanya wakavyo kwasababu wanajiona taifa kubwa , kama tunataka kuwa na ushirikiano imara na maaifa ya nje lazima kwanza sisi wenyewe tuwe imara kijeshi ili tuogopeke”
“Mheshimiwa Waziri una ujasiri wa hali ya juu sana , tunawezaje kuwa na jeshi kubwa kuzidi urusi ilihali hata siraha tunawategemea”
“Kama hatuna jeshi kubwa kuwazidi ndio watuchokoze , mimi namuunga mkono Roma kwa kuanza kuwashambulia , licha ya kwamba maamuzi yake yalikuwa ya haraka sana na yanaweza kutuathiri, hatuna haja ya kuogopa ili mradi Roma ataendelea kuwa upande wetu”Aliongea Waziri
“Mheshimiwa Waziri kwahio unachomaanisha ni kwamba tuache swala ili kama lilivyo licha ya athari ambazo zinaweza kutokea?”
“Mheshimiw anadhani anachoongea Waziri tunaweza kufikiria mara mbili pia, kwa taarifa za haraka haraka ambazo tulikuwa nazo ni kwamba mtoto wa Samweli Nguluma aliweza kuwekewa Kirusi kifahamikacho kwa jina la Tribute To Maria , kitendo hiki cha siraha hii ya kibailojia kuweza kuingizwa Tanzania bila sisi wenyewe kujua ni udhaifu mkubwa sana kwa taifa , kama swala hili halijaleta athari leo . vipi siku zijazo , lazima tuanzee kufikiria namna ya kujilinda kwa teknolojia zetu na sio kutegemea mabeberu, waliongiza kirusi hiki kwetu ni hawa warusi ambao tunawachukulia kama washirika wetu”
“Nadhani pia uchunguzi ufanyike ili kujua ni kwa namna gani Alshababu wameweza kusogelea mpaka wetu bila majirani zetu kufahamu”Aliongea Afande Tozo.
“Wizara ya ulinzi kwa kuhishirikiana na jeshi pamoja na idara ya usalama wa taifa mfanye uchunguzi ili uweze kufahamuni kwa namna gani kundi hili la Alshababu wakaweza kufanikiwa kuufikia mpaka wetu pasipo majiran zetu kutupa taarifa, kuhusu namna ya kumhoji Aishapova idara ya usalama wa taifa nawapa ruhusa ya kufanya majadiliano na kundi la The Eagles”Aliongea mheshimiwa na kisha palepale akampigia simu waziri wa mambo ya nje kufika ofisini kwake siku hio hio na kikao kikafungwa.
Muda huo huo wakati kikao hiko kikiendelea kilomita kadhaa kutoka ikulu , ndani ya hoteli ya Johari Rotana katika chumba cha Presidential Suite , alionekana Roma akiwa ameketi kwenye sofa huku chini yake kukiwa na mwili wa Maksim ambao unatobo kubwa upande wa kifuani , ilionyesha dhahiri Roma aliunyofoa moyo wa Maksim na kumuua hapo hapo.
Maksim alionekana amekufa kifo ambacho hata yeye menyewe hakukitarajia na kwa maiti yake ilivyokuona ikionekana ni kama alikuwa akishangaa kwanini anauliwa.
Muda huo Roma akiwa ameketi kwenye sofa , mlango wa chumba hicho ulifunguliwa na akaingia Adeline alievalia suruali na Jeans na kwa hali aliokutana nayo hapo ndani ilimfanya mwili wake kutetema.
“Take care of this , I have some Business in Russia to attend to..”
“Shughulikia hali ya hapa ndani nina maswala yangu nchini Rusia naenda kuyafanyia kazi”Aliongea Roma na palepale akayeyuka na kumfanya Adeline kukosa utulivu.
********
Mji wa kihistoria wa Keswick ulijengwa katika kipindi cha utawala wa Malkia Victoria(Victorian era) kati ya miaka 1800 kwenda 1900 ndani ya nchi ya Uingereza
Juu kabisa ya kilele cha mlima mita kadhaa kutoka Ziwa la Keswick kuna ngome kubwa ya kizamani iliokuwa imesimama imara huku juu ikiwa na bendera ya taifa la UK, usanifu wa jengo hilo uliwakilisha zama za miaka ile iiliopita , lakini licha ya jengo hili kuonekana kama la Zamani kwa upande wa nje lakini ndani yake ni moja ya sehemu nzuri sana yenye kupendeza mno macho kutokana na kazi nyingi za kisanaa zilizotengenezwa na kupamba eneo lote la ndani kuanzia juu kwenye Ceilling mpaka chini kwenye sakafu.
Sasa ndani ya Ngome hii katika eneo la sebuleni alionekana mwanaume mweusi akiwa ameegamia kwenye sofa kivivu huku akiwa anapiga miayo na kugeukia saa iliokuwa ukutani.
Mwanaume huyu alionyesha huko atokako hakukuwa na amani kutokana na hata mavazi yake aliovaa yalikuwa yamejaa madoa mengi yenye damu lakini si hivyo tu juu ya meza kulikuwa na kiroba ambacho kilikuwa kikitoa maji maji kama ya damu.
Muda huo huo wakati mwanaume huyu akiendelelea kupiga miayo huku akiangalia juu kwenye Ceiling Board , mlango wa kuingilia eneo la sebuleni ulifunguliwa.
Alionekana mwanaume mzee wa miaka isiopungua kama sabini hivi , mzungu , alievalia suti ya rangi nyeusi pamoja na saa ya mfukoni mfano wa Henry graves ambayo ameivaa shingoni kwa kutumia Cheni.
Pembani yake alikuwa ameongozana na mwanamke mwenye nywele nyeupe , mzungu pia ambaye mara baada ya kuangalia mtu alieketi kwenye sofa nguo zake zilivyokuwa na madoa ya damu alijikuta akifumba mdomo.
Mwanaume yule mzee na yeye pia alionekana kwenye mshituko kwa kile kilichokuwa mbele yake , lakini alijikuta akuvaa ujasiri na kukohoa kidogo kusafisha koo.
“How rare for you to visit us , You Majesty Pluto , You Haven’t visited us Rothchilds in years”
“Imekuwa nadra sana kwako mfalme Pluto kututembelea haujawahi kututumebelea sisi Rothchild kwa zaidi ya miaka sasa”Aliongea yule mwanaume huku akijaribu kuweka tabasamu ili aonekane kuwa jasiri.
Naam mwanaume ambaye muda wote aliikuwa akipiga miayo , huku akiangalia saa ya ukutani hakuwa mwingine bali ni bwana Roma Ramoni , haikueleweka ni muda gani kafika hapo , lakini ilionekana kabisa ni zaidi ya masaa tokea alivyotoka Tanzania..
“Kwanini nahisi sauti yako ni ya kinafiki na haijafurahishwa na ujio wangu”Aliongea Roma
“Utakuwa unatania Mfalme Pluto ,Familia yetu ya Rothichild inakukaribisha muda wote”Aliongea kwa lugha ya kingereza akiwa amesimama karibu na Roma , lakini upande wa Roma hakuwa na furaha ya kuendeleza mazungumzo juu ya familia hii ambayo alikuwa akijua inajali pesa kuliko kitu chochote.
“Hebu angalia huo mfuko kwanza , ni zawadi yangu kwako”Aliongea Roma akimpa ishara yule mzee kuangalia Kiroba ambachokinavuja damu kwenye meza.
Yule mzee alijikuta akivuta pumzi na kuzishusha na kisha akampa ishara mwanamke aliekuja nae aite mabodigadi waliokuwa wakilinda nje na ndani ya dakika chache tu waliweza kuingia na kufungua mfuko ule , lakini walijikuta wakitoa macho kwa woga na kurudi nyuma.
Mfuko huo uliokuwa na ukubwa wa kiroba cha Safleti ulikuwa umejaa vichwa na damu ambayo ilikuwa ikitoa halufu isiopendeza kabisa kwenye pua za binadamu yoyote.
“Ware.. Warewolves!?”Aliongea yule mwanaume mara baada ya kuona vichwa vile havikuwa na mwonekano wa kawaida bali ni kama vya wanyama..
Roma hakujali mshutuko wao , alichokifanya ni kusimama na kisha alivua shati lililokuwa na madoa ya damu na kulitupia kwenye sofa na kisha akaendelea kufungua na mkanda wa suruali.
“Imenichukua masaa zaidi ya sita kuua wanafamilia wote wa Klyuchevsky , Hivi vichwa unavyoviona ndio vya wale wanafamilia wenye ushawishi ndani ya familia”Aliongea Roma na kumfanya yule mwanaume kutetemeka
“Mfalme Pluto kwanini umefanya hivi?”
“Nyie si ndio mlipanga kumuozesha Clark kwenda kwa familia ya Klyuchevsky , Sasa wanafamilia wote washapoteza maisha hivyo naamini ndoa hakuna tena”Aliongea Roma na kumfanya yule mzee kukosa nguvu na yule mwanamke kumshikilia kwa haraka sana asije akadondoka.
“Mfalme Pluto naamini unafahamu kwamba kuna makubaliano pamoja na wenzako ya kutoingilia maswala yanayohusu binadamu kabisa , athari za matokeo kwa hiki ulichofanya?”
“Naheshimu makubaliano yaliopo na ni kweli kabisa sipendezwi na maswala ya matafia mengine , lakini hichi kilichotokea ni kwasaabu watu wangu wa karibu wameguswa, Clark ni mwanamke ambaye siku zote alikuwa akiendelea na maisha yake bila kuathiri wengine , nitafumbia macho kwa matendo yenu yote maovu mnayofanya kwa ajili ya kujipatia pesa lakini sitovumilia kuona mambo yenu yanaingilia maswala yangu binafsi”
“Hahaha., Athari !... kwa nilichokifanya leo kama kuna mtu yoyote anataka kulipiza basi namsubiria kwa hamu zote , nitamuua kila mtu ambaye ataingilia mambo yangu , Maneno ya kisiasa hayana athari yoyote kwangu na siku zote nitarudia kusema mwenye nguvu ndio muongoza njia na dhaifu hufuatia .. Oh! tena nimekumbuka hawa watu jamii ya Wolverine imenichukua masaa sita tu kuwaua wote licha ya uwezo wao mkubwa wa mapambano unafikiri binadamu wa kawaida atachukua muda gani kushindana na mimi”Aliongea lakini muda huo huo aliingia mwanaume mwingine mwenye nywele nyeupe , hakuwa mwingine bali ni Edward na baada ya kukutana na hali hio alijikuta akianza kumwangalia Roma kwa wasiwasi na kisha akamgeukia yule mzee.
“Edward nakushauri uishawishi familia yako kuzingatia sana kile wanachokifanya kupata pesa zao , wewe unaweza kuwa rafiki yangu lakini ninao uwezo wa kuiangamiza familia yako bila ya kuangalia nyuma”
“Nilidhania maswala ya kuua kikatili ushayaacha , lakini nadhani nilikufikiria vibaya , Serikali ya Urusi mpaka sasa hivi wamechukua hatua kwa kitendo ulichokifanya na wanaogopa utaenda Bersek kumuua kiongozi wao”Aliongea Edward.
“Ngoja wafanye wanavyotaka ,ninaenda kuoga kwa muda huu fanya mpango uniandalie ndege nataka kurudi nyumbani”Aliongea Roma.
*******
Ni siku nyingine kabisa muda wa asubuhi ndani ya jiji la Dar , Edna alionekana kusimama kwenye Balconi huku macho yake yote yakiangalia baharini na akifurahia kijua cha asubuhi.
Alionekana kuwa na wasiwasi kwenye macho yake, hata hivyo yote hayo ni kutokana na Roma kuondoka siku ya jana asubuhi pasipo kurudi siku nzima mpaka muda huo , ijapokuwa Roma aliaga kwa kusema ataelekea Urusi lakini Edna bado alionekana na wasiwasi na yote hayo ni kutokuwepo kwa maelewano wakati Roma anaondoka mara baada ya kuongea kauli yake ya kutaka Clark aweze kuolewa na Maksim.
Muda huo huo wakati akiendelea kuangalia upande wa baharin geti la jumba lao lilifunguliwa na gari aina ya V8 nyeusi iliingia na kusimama na palepale alitoka mwanamke mnene kidogo ambaye alimfanya Edna atoke kwenye Balconi haraka haraka na kushuka mpaka chini kwa ajili ya kumpokea.
Alikuwa ni mdogo wake Blandina afahamikae kwa jina la Jestina au Mama Nusra , mke wa tajiri Azizi ndio aliefika hapo nyumbani muda huo wa asubuhi akiwa ameshikilia boksi.
Blandina ndio aliekuwa wa kwanza kumlaki mdogo wake na kupokea lile boksi na kuliweka kwenye meza.
“Edna yaani unashuka mwenyewe kunisalimia , nikajua na Roma angekuja”
“Hajarudi bado?”Alijibu Edna.
“Ooh!... nikajua asharudi tayari, tutaongea baadae kidogo akisharudi maana nimekuja kwa ajili yake”Aliongea na kumfanya Edna kuwaza kwanini Mama Nusra alikuwa na uhakika Roma angerudi siku hio.
Blandina alionekana kufurahi baada ya kutembelewa na mdogo wake , kwani tokea wahamie hapo Jestina hakuwahi kufika , ijapokiuwa waliishia ndani ya jiji moja lakini kila mtu alikuwa bize kiasi cha kutokutembeleana.
Nyumba ilichangamka kwani Soga zilionoga mpaka wakati wa kujipatia kifungua kinywa.
“Jestina umesema umekuja kwa ajili ya Roma , je una uhakika atarudi leo?”
“Asubuhi ya leo nilisikia kutoka kwa mume wangu angerudi leo ,lakini alionekana kuwa ni mwenye wasiwasi , hivyo hakuwa na uhakika sana”
“Kwanini awe na wasiwasi , kuna jambo ambalo Roma kafanya huko alipoenda?”Aliuliza Blandina.
“Kama kuna taarifa mbaya nsingekuja na furaha kama hivi , siku ya jana Roma alisaidia sana taifa , huenda isingekuwa yeye taifa lingekuwa kwenye matatizo sasa hivi”Aliongea na kuwafanya waangaliane akiwemo Bi Wema.
“Mhm! mbona unaongea kimafumbo mwenzetu , ni nini Roma kafanya kusaidia taifa?”
“Ni siri nilioweza kuijua kwenye kikao kilichofanyika jana nyumbani, ila ngoja niwaambie, kwa maelezo ya mume wangu ni kwamba jana kulikuwa na tishio la kigaidi mkoani Tanga na bahati nzuri magaidi waliweza kufikiwa mapema kabla ya kufanya shambulizi la siraha za kibailojia , lakini hata hivyo inasemekana wanajeshi waliotumwa walichelewa kwani Aslhababu wameweza kuachia bomu moja ambalo lilivamia kijiji cha Mabando wilayani Pangani, lakini hata hivyo hali imedhibitiwa na hakuna madhara kwani mpaka sasa wananchi wote wa kijiji hicho wanapatiwa chanjo ambayo iliwezekana kwa msaada wa Profesa Clark”Aliongea.
“Unamaanisha kirusi chenyewe ndio hicho kinachofahamika kwa jina la Tribute to Maria”
“Yes! kumbe mshapata hizo habari”
“Ndio jana Roma na Profesa Clark walikuwa wakizungumzia kuhusu hiko kirusi”
“Basi ndio hivyo , uzuri ni kwamba licha ya kirusi hiko kuboreshwa kwa kuweza kusambaa kwa njia ya hewa lakini udhaifu wake ni kwamba kinachukua siku tatu mpaka kuonyesha athari katika mwili hivyo Chanjo muda huu zinatolewa kwa wananchi wote wa kijiji cha Mabando na maeneo ya karibu na inatagemewa hadi kesho zoezi litakuwa limemalizika ,kama sio Roma na Profesa Clark huenda kuongetokea ugonjwa wa ajabu Tanzania”
Ndio siku ya jana licha ya kwamba taarifa zilionyesha Yamaa Sct kufanikiwa kuwadhibiti magaidi wa Alshababu lakini inasemekana kuna baadhi yao ambao walivuka mpaka na kuingia Tanzania na kurusha bomu hilo kwenye kijiji kilichokuwepo wilayani Pangani kifahamikacho kwa jina la Mabando, kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba walidhania ni mabomu ya machozi, lakini baada ya taarifa kutolewa kwenye ngazi ya serikali ndipo uchunguzi ulipobaini ni sehemu ya mashambulizi ya siraha za kibailojia ndani ya kijiji hicho na ndipo kulipotolewa rai kwa wananchhi wote kutosafiri nje ya kijiji mpaka waweze kupatiwa chanjo.
Ilikuwa rahisi kwa Profesa Clark kutengeneza chanjo kwani tayari alikwisha kutengeneza chanjo ambayo alipewa Mika.
“Tena nimekumbuka , nasikia kuna bwana mzungu ambaye anafahamika kwa jina la Maksim aliekuja kuwatembelea hapa pamoja na waziri wa Viwanda , sasa nasikia huyo ndio ambaye amejihhusisha na utengenezaji wa Virusi hivyo ambavyo inasemekana athari zake zinafanana kabisa na za Ebola, imekuwa bahati kwamba Profesa Clark yupo hapa nchini na amewasaidia wataalamu katika hospitali ya Muhimbuli kuandaa chanjo ya haraka na kwa maelezo ambayo nimeweza pia kusikia ni kwamba Maksim alitaka kumuoa Clark ili kuzuia asijetengeneza Chanjo tofauti na wao wenyewe”Aliongea kwa kirefu huku akijaribu kuelekeza sifa zote kwa Roma kwa kusema ndio sababu ya ujio Profesa Clark Tanzania na hata kusaidia taifa kuliokoa na janga la mlipuko wa kirusi kinachotokana na kimimnika cha Tribute To Maria.
Sasa maneno ya Jestina yalimfanya Edna kujihisi ni mwenye hatia kwa kauli yake aliomwambia Clark , alijiambia alikuwa mbinafsi kwa kumfikiria Clark vibaya kwa kushauri aweze kwenda kuolewa na Maksim, kumbe mwanaume yule hakuwa na nia ya dhati ya kumuoa bali alitaka kutumizia mipango yake.
Wakati huo wakati akiwaza, mngurumo wa gari kutoka nje ulisikika ikimaanisha kmaba kuna mtu ambaye alikuwa akifika ndani ya nyumba yao .
Blandina ndio aliekuwa wa kwanza kwenda kuangalia juu ya mgeni anaefika na aligeuka.
“Ni Roma karudi kweli”Kaongea Blandina kwa furaha.



SEHEMU YA 448
Roma aliweza kuchukua masaa kadhaa kuwa angani kwa ndege binafsi ambayo iliandaliwa na Edward.
Alishangaa mara baada ya kuona ndani kwake kulikuwa na ugeni , alisogea hadi sebuleni huku macho yake yote yakimwangalia Edna.
“Roma msalimie kwanza mama yako mdogo”Aliongea Blandina mara baada ya kuona Roma muda wote kamwangalia mke ,ilibidi asalimiane nae, ukweli hakuzoea kusalimia kwa kusema ‘Shikamoo’ kutokana na mazingira aliokulia hivyo alitumia lugha ya kingereza tu kusalimia.
“Babe mbona unaniangalia hivyo bila ya kuongea lolote ? Au ndio furaha ya kuniona nimerudi”Aliongea Roma akimchokoza Edna ambaye alikuwa akimwangalia Roma bila neno.
“Hamna tu nimefurahi umerudi”Alijibu Edna kwa sauti ndogo na kuwafanya Blandina na Mdogo wake kutabasamu.
“Roma nimekuja leo kwasababu babu yako kaniagiza nije nikualike angalau ukamuone , lakini pia anataka kukupa pongezi kwa msaada uliofanya siku ya jana , anataka kupitia msaada wako umshawishi Profesa Clark kuendelea kubakia nchini Tanzania ili kuweza angalau kusaidia wanasayansi wetu waweze kujitegemea katika tafiti mbalimbali ikiwemo za siraha”Aliongea
“Unamaanisha yule mzee Atanasi , bado tu na umri wake ananikumbuka?”
“Baba ni mzee lakini kumbukumbu zake zinafanya kazi vizuri tu na ni mtu wa kufatilia siasa kila siku na anatamanni kuona Tanzania ikipiga hatua kabla ya kifo hakijamchukua , mwenyewe anasema anataka akikutana na Nyerere awe na taarifa nzuri ya kumwambia”Aliongea na kuwafanya kucheka.,
“Kwannini wanataka Profesa kubakia Tanzania , waliweza kumruhusu Yan Buwen kuingia Tanzania mpaka kupatwa na ukichaa na sasa amekuwa tishio la usalama wa familia , Siwezi kumfanya Clakr kubakia hapa Tanzania kama hapendi ,kama wamemshawishi akakataa basi mimi sina sababu ya kuongea nae”Aliongea Roma.
Ndio Jestina aliagizwa hapo nyumbani ili aweze kumshawishi Roma kufika nyumbani kwa Mzee Atanasi kwa ajili ya mazungumzo , lakini kubwa zaidi ni kutaka Clark asaidie kutengeneza wanajeshi kama wa kikosi cha Expandable lakini pia kusaidia wanasayansi wa Tanzania kujiendeleza katika uundaji wa siraha kwa siri.
“Nimekuja tu kukupatia taarifa , hata hivyo kila taifa linampigania Profesa Clark kwa uwezo wake”
“Tanzania kama ilifeli kumshawishi Profesa Shelukindo kuwasaidia katika hilo , hawatoweza kwa Clark ni bora wakaacha kuota ndoto ya mchana na wafanye mpango wa kutuma vijana nje ya nchi kuweza kupata ujuzi”Aliongea Roma na Jestina hakutaka kutia neno , hata hivyo alionyesha kumhofia Roma kwani pia alipata taarifa ya namna alivyoweza kuua wanafamilia wote wa Klyuchevsky.
Baada ya Mama yake mdogo kuondoka akisindikizwa na Mama yake , Roma alimfuata Edna ambaye alikuwa ndani ya chumba chake cha kujisomea alitaka angalau kuongea nae , kwani aliona alikuwa amenuna bila ya kutokujua sababu..
“Vipi Edna kuna jambo lingine nimefanya ambalo limekukwaza?”
“Mh! Hapana najihisi hatia kwa kukukosea?”
“Kwanini , kuna kitu kimetokea, Wife niambie kama kuna mtu kakuchokoza, nitahakikisha halioni jua likizama”
“Sio hivyo, kwanini kila kitu kwako lazima utangulize neno kuua, ni jambo jepesi sana kwako?”
“Nilikuwa natolea mfano kama mtu atakuchokoza , ni mfano tu”
“Mfano! , hivi unafikiri nilishindwa kuona namna Mama Nusra alivokuwa na wasiwasi na wewe hata wa kukuangalia machoni?””Aliongea Edna.
“Roma niambie huko ulipotoka umeua tena?”Aliuliza Edna na kufanya Roma kushindwa kujibu , hata hivyo hakujua kama Edna angefahamu kwamba amefyeka familia nzima ya Maksim , Roma alishawahi kumuahidi Edna kwamba asingeua watu hovvyo hivyo alichokifanya ni kama alienda kinyume na ahadi yake.
“Edna nisamehe , nilichokifanya sikudhania kingekufanya kukasirika lakini nilikuwa na sababu ya kufanya hivyo”
“Yote hayo ni kwasababu ya Clark tu ndio maana unavunja ahadi tuliowekeana, Sitaki uombe msamaha tena , hata hivyo haujanifanyia kosa lolote”Alongea Edna huku sura yake ikijikunja na kuonyesha alikuwa na hasira.
Roma ilibidi ajaribu kumsogelea akitaka kumgusa Edna , lakini hata hivyo aliogopa kwamba angekasirika zaidi, kwa jinsi Roma alivyokuwa akimhofia Edna ni kama sio Mfalme Pluto aliekwenda kuchinja familia nzima ya Wolverine , Edna alikuwa udhaifu wake mkubwa,
“Edna mpenzi wangu…”
“Sitaki uniite hivyo , sistahili kuwa mke wako, ulimwengu wako na wangu ni tofauti , Kwako wewe kuua ni sawa sawa na kupumua , pesa na madaraka kwako wewe unaamini ni kwa wale wanaoweza kuwaua wengine , unaweza kuua watu zaidi ya kumi bila hata ya kuonyesha hatia lakini mimi kushuhudia kifo cha mtu mmoja tu kunaweza kunifanya usiku nisilale vizuri wiki nzima “
“Maadui zako wewe sio binadamu wa kawaida na huenda wananiona sistahili hata kuitwa mkeo , Siwezi kukusaidia kwenye lolote na sina ninachokijua zaidi ya kugombana na wewe kuhusu wanawake wako wengine , I have nothing left to offer , My dignity , my pride and my beliefs are just a piece of fragile paper in front of you , halafu bado nakuona kama mtu wa thamani sana kwangu , naonekana kama mwanamke kichaa , Eh,..”Aliongea huku akianza kutoa machozi na kumfanya Roma kushangaa ,ijapokuwa haikuwa mmara ya kwanza kuuona Edna akiongea hivyo lakini ni mara yake ya kwanza kumuona Edna akionyesha hali ya kutojiamini mbele yake kwa namna ya kujishuku.
“Muda mwingine nahisi wapenzi wako wanafuraha kuliko hata ilivyokwangu mimi ambaye ni mkeo , Hawana sababu ya kujihisi kutokuwa wa thamani kwako ili uwapende, hawana haja ya kuwaza utawatembelea au utarudi nyumbani mapema kama ilivyo kwangu , labda ningekuwa sio mkeo na kuwa kama wao ningekuwa na furaha na mimi”
“Edna usiongee hivyo..”Roma alishindwa kusikiliza na kutoa kauli ya kinyonge.
“Roma naamini yatakuwa maamuzi sahihi kumfanya Clark kuendelea kuwa karibu yako , ndio yeye pekee ambaye ana akili nyingi za kukusaidia hivyo ni wa thamani kwako , ni mrembo na kubwa zaidi anatoka kwenye familia kubwa ya kifalme , Anakupenda mno kiasi kwamba yupo tayari hata kuolewa na shetani kwa ajili yako , hawezi kuota usiku kucha kwaasababu tu eti umeua mtu, wala kuogopeshwa na wanawake wengine , kwasababu hakuna hata mmoja ambaye anaweza kufikia levo zake”
“Edna unaongea nini wewe?”Aliongea Roma huku hasira zikianza kumpanda.
Edna usiku mzima alishinda kuanza kujifananisha na wapenzi wa Roma katika vitu vingi na katika kufikiria alijua hakuna cha ziada ambacho anampatia Roma , hakuwa akimpa kitumbua kama wenzake walivyokuwa wakifanya , hakuwa na akili nyingi kama Clark kwamba angemsaidia kwenye mambo mengi, yaani Edna alijiona kwamba hana chochote cha kumsaidia Roma kwani kama ni hela Roma anazo , kitendo hicho kilimfanya ajione hana thamani kubwa kwenye maisha ya Roma kama ilivyo kwa Clark na hilo ndio swala ambalo lilimkasirisha na kumuona Clark kama tishio kwake , ilikuwa ni maya yake ya kwanza kuanza kujilinganisha na mwanamkie mwingine kwanzia uzuri na vitu vingine.
“Edna nishakuambia wewe kwangu ni wa kipekee na bila wewe nisingekuwa na maisha ya aina hii , kwanini uanze kujihisi hauna thamani kwangu”Aliongea Roma.
“Mimi sijui , labda kwasababu nashindwa kujielewa mimi mwenyewe , naomba unisamehe kama nimekukwaza ninaenda kazini”Aliongea na kisha alitoka kwenye chumba hicho cha kusomea na kuingia kwenye chumba chake na kumuacha Roma ambaye hakujua cha kufanya kumpoza Edna, alijua wanawake hisia zao hubadilika badilika kutokana na mazingira lakini hakutegemea jambo hilo kwa Edna kwani siku zote alimchukulia kama mwanamke anaejiamini kwa kila sekta , lakini mwisho wa siku alijiona yeye ndio mjinga , wanawake wote wanafanana kwa kila kitu likija swala la hisia , Edna alikuwa akilalamika kwa kumchukulia Clark kama mshindani wake.
Roma mara baada ya Edna kuondoka kihasira hasira aliweza kupokea simu kutoka kwa Amina ambako angalau aliweza kupunguza stress zake zote zilizosababishwa na mke wake.
Siku yake iliisha vizuri kwani waliweza kuzurura mchana wote hata walipokuwa eneo la Mlimanni, Roma aliweza kumuona Rufi akiwa pamoja na Mika lakini Rufi yeye hakuweza kumuona Roma.
Muda ambao Roma alirudi nyumbani, mke wake alikuwa asharudi tayari , Roma alikuwa akiwaza siku nzima namna ya kumbebembeleza Edna na kurudi kwenye hali yake ya kawaida na katika kufikiria kwake aliona ni heri siku hio wakienda kupata chakula nje na nyumbani.
Na ndio ambacho Roma alifanya, alivyofika aliwapa taarifa Bi Wema na mama yake kwamba hawatokula chakula cha usiku kwani wnatoka Out na Blandina hakua na kipingamizi kwanza alifurahi kuona mwanae anaweka juhudi kumfurahisha mke wake.
Haikueleweka Roma alimwambia nini Edna huko walikotoka lakini Edna alirudi akiwa na furaha mno , huku kila alipokuwa akimwangalia Roma usoni kwa jicho la huba alikuwa akitabasamu bila sababu..
Kule kukasirika kwa Edna kulikuwa kumeisha kote na hata aliporudi na Chumbani ilimchukua kidogo tu kujilaza kitandani na kupotelea usingizini.
Roma baada ya kuona Edna kalala alirudi kwenye chumba chake kwa ajili ya kubadili mavazi baada ya kuoga , lakini ile anamaliza tu , simu yake ilianza kuita mfululizo na alipoangalia jina la mtu anaempigia aligundua ni Neema Luwazo.
“Hivi wewe mwanaume kwanini huna huruma?”Sauti ya malalamishi ilisikika mara baada tu ya Roma kupokea simu.
“Darling mbona unaongea ukiwa na jaziba hivyo , Donyi kakukasirisha nini?”Aliongea Roma.
“Unao uwezo wa kumtoa out Amina siku nzima lakini pia kubebana na mkeo kule ufukweni lakini umeshindwa hata kunijulia tu hali , hebu niambie ni lini ushawahi kunitoa Out hata mara moja , unanichulia mwepesi kwasababu muda wote nipo kimya , unafikiri nashindwa kuja kukutembea kila siku hapo nyumbani kwako ili nimkasirishe mkeo?” Roma alijikuta akikosa usemi , aliamini huenda Neema Luwazo alimuona akiwa ufukweni na Edna akiwa amembeba mgongoni kimahaba , maana hivyo ndicho walichofanya baada ya kupata chakula cha usiku kwenye mgahawa.
“Neema usiwe na hasira , unajua mwenyewe muda mwingi nakuwa na mambo mengi kichwani lakini pia niliogopa kuja kwako kwa kuhofia uwepo wa mtoto wako Donyi”
“Acha kutafuta sababu zisizokuwa na maana , kama ungekuwa unaogopa sana uwepo wa Donyi kwenye maisha yangu usingenisogelea kabisa . Hata hivyo namshukuru Mugnu sio kwamba nakutegemea kunihudumia , hivyo naomba usije ukanitafuta tena , mimi na wewe basi”Aliongea Neema kwa hasira na kisha akakata simu.
Roma alijikuta akitabasamu kwa uchungu , hata hivyo alijua tu Neema Luwazo aliongea hivyo kwasababu ana hasira na wivu, ilionyesha mwanamke hata awe na kila kitu lakini kwa mwanaume ataishia kuwa dhaifu tu.
Roma alivaa na hakujiuliza mara mbili mbili , kwasababu alijua Edna ashalala muda huo , ilimbidi kwenda nyumbani kwa Neema Luwazo muda huo huo kupitia Balkoni akajaribu kutulizza gubu lake.
Na kweli ile anafika nje ya Balkoni kwenye chumba ambacho kilikuwa cha Neema Luwazo aliona taa bado ipo wazi na kumfanya atabasamu kifedhuli, Roma aliona kabisa maneno ya Neema Luwazo ni mtego tu , kwanza kilichomchekesha hata mlango wa kutokea kwenye Balkoni haukuwa umegufungwa kwa ndani.
Roma baada ya kuingia alimkuta Neema akiwa amejilaza kitandani pasipo kujifunika shuka na nguo za kulalia nyepesi ambazo zilichora umbo lake.
“Umekuja kufanya nini hapa , si nimekuambia mimi na wewe basi”Aliongea lakini Roma macho yake ya kifisi yaliendelea kuchunguza umbile la mrembo Neema.
“Unaniangaliaje hivyo , wakati una mke mrembo wa kuvutia umemuacha nyumbani?”
“Acha hizo basi nishafikta tayari haina haja ya kujifanyisha kama mtoto mdogo, vipi Donyi keshalala?”
“Kashalala huyo muda mrefu tu , Vipi upo hapa kwa ajili ya mchezo au kuna kingine kimekuleta , kwanini unaniambia najifanyisha kama mtoto?”
“Kwa muda huu unafikiri nini kimenileta zaidi ya mchezo , hatuwezi kwenda kutemba sasa hivi ni usiku “Aliongea Roma na kumsogelea karibu na kuanza kumnusa nusa kama mbwa.
“Wewe usiniharakishe nipo na hasira bado?”
“Tunaweza kuendelea ukiwa na hasira , hakuna kinachoharibika “Aliongea Roma huku akipeleka Mkono kwenye sehemu ambazo ndio mashteni ya Neema yanalala.
“Argh..”
Walifukunyuana usiku mzima kiasi kwamba Roma usiku huo alisahau kabisa kurudi nyumbani na ile anashituka ilikuwa saa tatu asubuhi, alijikuta akijikasirikia kwa kupitiwa na usingizi muda mrefu , lakini alijua ashachelewa na upande wa Neema hakujali hata kumuamsha zaidi ya kuandaa kifungua kinywa.
“Donyi yuko wapi?”
“Kafuatwa na mpenzi wake asubuhi na wameondoka?”Aliongea Neema na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Mpezi wake , sijawahi kusikia Donyi akiwa na mpenzi”
“Kassimu mtoto wa Tajiri Azizi ndio mpenzi wake mwanzoni Donyi alionekana kutompenda , lakini sasa hivi kakolea na leo asubuhi wamechukuana wanaenda Ngorongoro”AliongeaNeema na Roma hakuingizia swali na kuendelea kunywa chai huku wakibadilisha stori nyingine.
Neema kila alipokuwa akimwangalia Roma aliishia kutabasamu , ilionekana alikuwa na kumbukumbu ya kile kilichotokea usiku ndio maana muda wote alionyesha hali kama ndio kwanza anafahamiana na Roma.
Neema Luwazo hakuwa na haja ya kufanya kazi sana kama ilivyokuwa Edna , kwanza walikuwa wakitofautiana namna wanavyofanya biashara , Neema alipenda watu wenye uwezo kumsaidia kufanya kazi zake , huku yeye akidili na baadhi ya maamuzi tu ya kampuni hususani upande wa bodi ya wakurugenzi.
Alikuwa tofauti na Edna ambaye alipenda kufanya kila kitu yeye na kusimamia wafanyakazi wake kwa kila wanachofanya na hata likija swala la ki uwekezaji Edna alikuwa ni mwanamke anae take risk kila fursa inapojitokeza.
Wakati wakiendelea kunywa chai simu ya Roma ilianza kuita mfululizo na alipoangalia jina ni la Edna mke wake na moyo ulienda mbio na kumfanya apokee palepale.
“Sijui upo kwa mwanamke gani muda huu na sitaki hata kujua , lakini kwanini haupo kwenye kikao saa tano hii , Kama hutaki kuendelea kuongoza kampuni ni bora unieleze nitafute mtu mwingine, Acha kunikasirisha Roma”
“Kikao gani , mbona sijui kama kuna kikao?”
“Uko siriasi kweli, Hujapata kusikia kuna kikao cha viongozi wa juu wa kampuni za habari na burudani na wizara?”
“Ndio mara yangu ya kwanza kusikia kuhusu kikao hicho?”
“Kama ni hivyo kwanini umemuajiri Tanya kama Secretary wako.Kwanini hajakuambia swala muhimu kama hilo?”Aliongea Edna huku sauti yake ikioneysha kukasirika.
“Hajaniambia , ni kweli jana sikufika kazini lakini sikujua kuhusu kikao”
“Sawa naomba uwahi ukutane na hawa wageni muhimu wakufahamu”Aliongea Edna na kukata simu na kumfanya Roma kuvuta pumzi
 
SEHEMU YA 449.
Roma mara baada ya simu kukatwa ilibidi kwanza awasiliane na Tanya kujua nini kinaendelea kwani hakuwa hata na taarifa.
“Master ni yapi maagizo yako?”Aliongea Tanya mara baada ya kupokea simu , lakini sauti ya Tanya Roma hakuwa akiizoea kabisa.
“Tanya Boss Edna kasema kuna kikao nimekosa leo , nini kinaendelea ?”
“Ni project ilioandaliwa makao makuu , inayohusisha Semina kwa wafanyakazi wote wa kampuni yetu pamoja na Wizara ya Habari na utamaduni,lakini pia kuna kikao ambacho kilijumuisha wawekezaji kutoka nje ya nchi ambao wanapanga kufanya kazi na sisi , Semina na watu wa Wizara imekwisha isha lakini kikao na wageni kutoka nje ya nchi bado hakijaanza”Aliongea Tanya kwa lugha ya kingereza.
“Sasa kwanini hujanipatia taarifa?”
“Nisamehe sana Master ,nilidhania utakuwa bize ndio maana sikuthubutu kukusumbua”Aliongea huku sauti yake ikiwa na uoga , lakini Roma aliishia kumlaumu Noriko Okawa kwani alimfunza Tanya kuishi kama mtumwa kwa watu ndio maana muda wote ametawaliwa na hofu.
Roma alikata simu na kisha aliagana na Neema Luwazo ambaye ilionekana pia alikuwa akijua kuhusu Semina hio , Roma aliondoka haraka na kurudi nyumbani na kupiga suti ya Tuxedo haraka haraka baada ya kuoga , alipuliza unyunyu alionunuliwa na Edna na kisha akaingia kwenye gai yake ya Lexus ambayo hata namba hakuhangaika kuzibadilisha.
Dakika kadhaa mbele aliwasili ndani ya Posta nje ya jengo la makao makuu ya kampuni na aliweza kushuhudia watu wengi wakitoka kwenye jengo hilo kwa makundi makundi na alihisi amechelewa.
Alitoa simu yake na kisha akatafuta namba ya mke wake na kupiga , lakini iliita kidogo tu na kisha ikakatwa hapo hapo, alijikuta akitabasamu kwa uchungu na kisha akatafuta namba ya Recho na kupiga.
“Nikusaidie nini Roma?”Sauti kutoka kwa Recho ilisikika upande wa pili.
“Acha kujifanyisha hebu niambie Edna yupo wapi?”
“Recho kata simu , tuna shughuli nyingi za kukamilisha leo”Sauti upande wa pili ya Edna ilisikika.
“Roma kuna wageni wameakuja kwa ajili ya kikao na Directors wote wa kampuni , inabidi uje kwenye ukumbi wa mkutano siti yako ilikuwa wazi tokea asubuhi”Aliongea Recho haraka haraka .
Roma sasa alielewa wapi anatakiwa kwenda , hivyo alitoka kwenye gari na kuanza kupiga hatua kuingia ndani ya jengo hilo , wafanyakazi siku hizi walikuwa wakimpa heshima yake kutokana na kujua kwamba alikuwa mume wa bosi na sio hivyo tu alikuwa mtoto wa Raisi.
Dakika chache mbele Roma aliweza kuingia ndani ya ukumbi wa mikutano katika ghorofa ya kumi na nane ya jengo hilo linalomilikiwa na mke wake , ambalo ndio makao makuu ya Vexto.
Ndani ya jengo hili katika chumba cha mikutano kulikuwa na meza ndeefu ambayo imejaa watu waliovalia suti , huku mbele yao kukiwa na maiki , makaratasi pamoja na chupa za maji ya uhai ,ilikuwa ni kama kikao cha raisi na mawaziri wake.Edna alikuwa mwisho kabisa wa meza huku akiwa ametulia na sura iliojaaa usiriasi akidhihirisha nini maana ya kuwa bosi.
Muda huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Roma ambaye alimfanya Edna aliekuwa akiangalia karatasi ziliokuwa kwenye meza yake kumwangalia mpaka alipoenda kukaa kwenye siti yake.
Upande wa Roma hakujali sana sura zilizokuwa zikimwangalia , kwanza alikuwa akijiamini , ni hivyo tu hakuwa akizoea ukauzu wa mke wake.
Edna alikuwa na hasira na Roma kwani usiku wa jana tu mambo yao yaliikuwa mazuri mno na alikuwa na huba nae la kiwango cha juu , lakini asubuhi mara baada ya kwenda kwenye chumba chake na kukuta kitanda kimetandikwa na hakikuwa na dalili ya kulaliwa usiku mzima, alijikuta akitoa matusi ya ndani kwa ndani na kumsuta Roma kwa kumlaani.
Kilichomkasirisha zaidi ni mwanaume huyu kushikiliwa na mchepuko kiasi kwamba amesahau hata kuwahi kazini kwenye kikao muhimu.
Roma mara baada ya kukaa aliweka suti yake vizuri na kujiweka sawa na kuanza kuangalia watu wote waliohudhuria hapo ndani na alishangazwa na uwepo wa wazungu , ukimtoa Richie kuna mmoja ambaye hakumpenda kabisa.
Alikuwa ni mwanaume alievalia suti ya rangi ya bluu kampuni ya Armani na tai nyembamba ambayo ilitoa ‘Vibe’ yenye kuelezea uanaume wake hivyo kuwa wa hadhi ya juu , hakuwa mwingine bali ni Hanson mwanaume ambaye siku kadhaa zilizopita aliweza kukutana nae kwenye kusanyiko la wanadarasa wa Edna , mpaka Roma kumzidi kete kwa kuonyesha uthamani wa Henry Graves.
Hanson mara baada ya kukutanisha macho na Roma aliachia tabasamu la furaha.
“Director Roma hatimae ameweza kufika , nilikuwa nikitaka kusema ni jambo gani la kuhuzunisha nisingeonana na wewe kwa mara nyingine”Aliongea na kufanya wale watu ambao hawakuwa wamemfahamu Roma sasa kumfahamu kwamba ndio Director wa kampuni ya Vexto Media.
“Mr Hanson is here as a representative for BMW’s African Division which Explain his attendance today”
“Mr Hanson yupo hapa kama mwakilishi wa kampuni ya BMW upande wa Afrika , Swala linaloelezea kuhudhuria kwake siku ya leo”Aliongea Edna baada ya kuona Roma anamwangalia kwa wasiwasi.
“Oh! Naona , Lakini kumbukumbu zangu zinaniambia kabisa sijawahi kukutana nae kwenye maisha yangu yote , inashangaza sana yeye kunifahamu”Aliongea Roma na kumfanya Hanson kukunja sura alijua ?Roma anamkejeli.
“Mr Roma utakuwa unatania , lakini hata hivyo sijali kujitambulisha kwako kwa mara nyigine , Mara ya mwisho tulikutana kwenye mkusanyiko wa wahitimu wa chuo cha Oxford wiki kadhaa zilizopita ukiwa na boss Edna”Aliongea .
“Okey Okey nimekumbuka nisamehe bwana Hanson , nimependa mtindo wako wa nywele , kwa maisha yangu nilitamani sana kuwa na nywele ndefu za kizungu lakini inanisikitisha kuzaliwa na nywele fupi kama zangu pamoja na hii sura”Aliongea akimtania Hanson maana tofauti na siku kadhaa walizokutana leo alikuwa amepunguza nywele na zikawa fupi mno.
“Kuna joto sana siku hizi ndio maana ufupi wa nywele ni sahihi kwangu , Oh Yeah , tena Director wewe ni mume wa CEO Edna , mahusiano yenu mazuri yamekuwa ni jambo la kuvutia watu wengi sana lakini hata hivyo President Edna anaaminika kwa kujali umakini likija swala la kazi”Aliongea Hanson na kumtupia dongo Roma kwa kuchelewa kwake hata watu walishangaaa pia inakuwaje Edna anesifika kwa uchapa kazi akawa na mume wa aina hio , hawakujali sana cheo cha kuwa mtoto wa Raisi kwani ni jina tu tofauti na pesa.
Edna baada ya kuona mazungumzo hayo yangeenda vibaya alianzisha kikao palepale baada ya kusafisha koo.
Kikao kiliendelea kwa zaidi ya msaa kadhaa mpaka mchana yote jambo ambalo lilimchosha mno Roma , kwani aliishia kusinzia bila ya kuelewa chochote kinachoendelea , ilikuwa afadhali kwake kwani Tanya aliweza kufika mapema na kuchukua kumbukumbu ya kikao chote.
Baada ya kikao kumalizika ilikuwa ni saa tisa za mchana na Roma baada ya kumuona mke wake anaelekea ofisini alifuata nyuma.
Edna baada ya kuingia ofisini kwake alichukua mfuko mkubwa uliokuwa juu ya meza yake na kuingia kwenye chumba cha mapumziko.
Wakati Roma akiwa anapangilia mistari yake kwa ajili ya kumlegeza , Edna alitoka akiwa kwenye mavazi tofauti na yale ya mwanzo na kumfanya Roma kubung’aa , kwani alikuwa amependeza haswa.
Kiuno chembamba kilichochangamshwa na lishepu lililojipangilia upande wa chini ilimfanya Roma damu kumcheka, Edna alimwangalia Roma kwa jinsi macho yake yalivyokuwa ya kifisi na kutoa kicheko cha chini chini ilionekana hata hasira zake zilikuwa za maigizo tu.
“Vipi nimependeza?”Aliuliza Edna huku akijigeuza geuza mbele ya Roma aliekaa kwenye sofa na Roma alitingisha kichwa mara mbili nakumfanya Edna kukunja sura.
“Ndio unamaanisha nini kwa kutingisha kichwa?”
“Mwanaume Gentlemen akitingisha kichwa mara moja inamaanisha kwamba umependeza sana , lakini akitingisha kichwa mara mbili ni kwamba umependeza zaidi ya neno lenyewe mimi nimetingisha mara mbili”Aliongea Roma na kumfanya Edna kupumua kwa afadhali yote hayo ilikuwa ni kutaka kujua kama gauni lake limempendezesha.
“Usiku wa leo tumealikwa katika hafla ya ugawaji wa Tuzo za sanaa zilizoandaliwa na serikali , kutakuwepo wasanii mbalimbali wakubwa na nimepewa heshima ya kutoa Tuzo kwa moja wapo wa wasanii ndio maana lazima nivae nipendeze kuiwakilisha kampuni yangu ya mitindo, linaonekana kidogo kunibana kwenye kiuno lakini muda wa kutafuta gauni lingine sina hata hivyo ilinitumia muda mrefu kuweza kuchagua hili gauni….”Aliongea lakini palepale alijikuta akiwa hewani kwenye mikono mikakamavu ya Roma akiwa amembeba juu juu.,Roma alimpiga mabusu rasha rasha huku akimzungusha.
“Unafanya nini , utaharibu gauni langu bwana?”
“Darling nadhani unapaswa kutafuta gauni lingine , nina wasiwasi na hao masuperstars watakaokuwepo, wanaweza kukomezea mate. Na mimi nitaona wivu”
“Wewe sibadilishi hivi hivi ndio fasheni , kwanza linaniacha wazi kwenye mabega tu, hili ndio linaendana na Red Carpet”Aliongea na kisha alijitoa kwenye mikono ya Roma.
“Sio mbaya umependeza sana mke wangu , lazima nikusindikize ili watakaojaribu kusema ni warembo kuzidi wewe ninawanyofoa makoromeo yao”
“Yaani , huwezi kuongea vizuri mpaka uweke vitisho”
“Natania mke wangu , Oh.. tena babe vipi hauna hasira na mimi tena si ndio?”Aliuliza na kumfanya Edna atingishe kichwa kukubali.
“Sio jambo jipya hata hivyo na najua utafanya tena na tena , inabidi tu nikuzoee hivyo hivyo , nashindwa kujizuia na kuwa na hasira lakini ni kwa muda mfupi tu , hata hivyo umeweza kumuona Hanson kwenye kikao lakini hujaniuliza chochote hivyo naona unaniamini”
“Wifey mimi nakuamini ila yule mpuuzi akikusumbua nitahakikisha na mnyonga”
“Wewe..”Edna aling’ata meno yake kwa hasira na kugeuka na kumfanya Roma kucheka.
“Wifey ukweli licha ya kwsamba hatujaoana kwa muda mrefu lakini ndoa yetu imepitia mambo mengi ambayo wengine wanaweza kuyazungumzia ,Baadhi ya mambo ambayo yanaweza kuwa mlima kwa wengine kwetu ni vijimlima vidogo vidogo vya kupanda na kushuka , nimefurahi hatuna ugomvi”
“Usijifanyishe hapo na maneno yako , bado hata sijaanza kukuhoji vozuri , Haya uniambie jana usiku umelala wapi?”Aliuliza lakini Roma alianza kufikiria namna ya kujibu.
“Arrgh .. Edna unaharibu viatu vyangu bwana?”Roma alilalamika mara baada ya kukanyagwa na kiatu cha kisigino kwenye viatu vyake vyeusi.
“Kwahio viatu vyako vinathamanni kuliko miguu ?”
“Ulifikiria ukinikanyaga hivyo nitahisi maumivu?”Aliongea
“Subiri uone”Aliongea na kukanyaga kwa nguvu mpaka alipohakikisha ameridhika .
“Inakutosha hio kwa leo ukirudia nitakupa adhabu kali mpaka ukome kutoroka usiku”Aliongea na kisha akaondoka na kurudi kwenye chumba cha kubadili.
*********
Naam ilikuwa ni usiku wa tukio lililopewa jina la Tuzo ya Taifa , Saa moja na nusu ndio muda ambayo Roma na Edna waliweza kufika ndani ya eneo la Mlimani City kwa ajili ya kutii mwaliko wa tuzo hizo.
Roma alikuwa amependeza na suti yake ya Brown Luis Vuiton akiwa na mke wake mrembo pembeni tajiri Edna Adebayo, Kamera ziliwamulika wakati wa kupita kwenye Red Carpet na Edna hakuacha kutabasamu.
Edna alikuwa ameanza kubadilika kidogo katika msimamo wake .zamani alikuwa akigopa sana umaarufu ndio maana hata licha ya kuwa tajiri surayake haikuonekana sana mitandaoni na sio watu wengi waliokuwa wakimjua , hata akaunti kwenye mitandao ya kijamii hana.
Watu waliokuwa wakifika walikuwa wengi , lakini pia siku hio ilikuwa ikiangaziwa na wasanii wengi mno kutokana na uwepo pia wa msanii wa kimataiafa kutoka Ireland.
Baada tu ya Edna na Roma kupita kwenye Red Carpet, Roma aliweza kumuona Recho akiwa ndani ya ukumbi akiongea na mwanamke mmoja mrembo wa Kizungu , lakini hata hivyo hawakumsogelea moja kwa moja kwani walisogelewa na watu mbalimbali na kusalimiana nao , wakiwemo wasanii wakubwa ambao pia walijipendekeza kwa Edna na Roma ili kuweza kupata ufadhili wa nyimbo zao , lakini pia kupewa ‘Airtime’ kwenye Chaneli Tv ya Vexto.
Baada ya kusalimiana na watu kadhaa wakiwemo wafanyabiashara , Recho alimsogelea Edna akiwa na yule mzungu.
“Madam , huyu ni mtoto wa kike wa msanii maarufu kutoka Ireland Marehemu Ms Doleres aliekuwa katika kundi la Cranberries , She and other artist are currentlly on their world tour stop in Tanzania , She insistend an Audience with you” Aliongea Recho , alikuwa vizuri mno kwenye lugha ya kingereza huenda nio credit iliomfanya kuwa Sekretari wa Edna.
Kabla Edna hajatoa jibu kuna mwanamke mrembo mmoja aliekuja kwa namna ya kupaniki na kuwasogelea.
“Oh My God! Nessa!”Aliongea kwa mshituko lakini alijiuzuia.
“Sorry! Let me introduce my self , I’m Dina and it’s pleasure to meet with you”Aliongea kwa kujitambulisha kwa jina la Dina.
Dina ni moja ya wasanii maarufu ndani ya Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla , ni moja ya wasanii wa kike wa Tanzania wanaosifika kwa kuwa na sauti nzuri , mwenyewe anajiita kwa jina la Malkia wa Afrika.
Ni kawaida sana kwa msanii kama Dina kushangazwa na uwepo wa Nessa msanii maarufu kutoka Ireland ambaye pia alikubalika sana ndani ya taifa lake kwa kumrithi mama yake marehemu Ms Doleres ambaye alikuwa chini ya Band Maarufu sana enzi za miaka ya tisini ifahamikayo kwa jina la Cranberries.
“Nice to meet you , it’s my first visit to Tanzania so do forgive me , I aren’t so familiar with a lot of peaple here”Aliongea Nessa akimaanisha kwamba ni mara yake ya kwanza kutembelea Tanzania , hivyo hafahamu watu wengi, kauli ile ilimnyong’onyesha kidogo Dina.
Edna ilibidi achukue jukumu la kumtambbulisha Dina kwa Nessa , Edna ijapokuwa hakuwa mpenzi sana wa mziki wa Rock , lakini Ms Doleres aliweza kumfahamu sana hususani na tukio la msanii huo kukutwa amejizamisha kwenye maji ya Swimming Pool ndani ya Hoteli usiku kwa kile kilichodaiwa ni Depression(Sonono)
Upande wa Roma alikunja sura kiasi , alikuwa akimjua vizuri Ms Doleres , lakini mtoto wake kuja Tanzania na kutaka kuongea na mke wake kulimfanya kidogo kuhisi huenda kuna zaidi ya hilo. .
Baada ya watu kutulia hatimae ugawaji wa tuzo uliozaminiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni ya Vexto ulianza rasmi..
“Nilikuona ukiwa huna furaha wakati wa kusalimiana na Nessa , nini tatizo?”Aliuliza Edna mara baada ya kukaa.
“Hakuna tatizo , ni kwamba tu nina mashaka?”
“Mh! Mashaka gani tena?”
“Siwezi kusema , ila kama ningetaja jina la baba yake huenda angeondoka mara moja hapa nchini”Aliongea Roma
“Baba yake!, unamaanisha nini , kwanini aogope kutajwa jina la baba yake?”
“Babe kuna mambo ambayo hayapaswi kabisa kuzungumziwa na yabakie kua siri , Kuna vitu viovu sana vinafanyika ambavyo vina haribu Dunia”Aliongea na Edna alivuta mdomo.
“Unajifanyisha mjuaji , Haya baba endelea kubakia na siri zako”Aliongea Edna na muda huo ukumbi ulibakia kimya na hio ni mara baada ya Nessa kupewa nafasi ya kutumbuiza siku hio kama mgeni wa Heshima.
Ijapokuwa alikuwa na vibao vyake maarufu vinavyotamba duniani , lakini usiku huo alitaka kuimba wimbo wa Dreams ulioimbwa na Band aliokuwepo mama yake ya Cranberries, haikueleweka kwanini alichagua wimbo huo , lakini inasemekeana kila nchi aliopita alikuwa akiimba huo wimbo huenda ilikuwa ni kumuenzi mama yake.
Nessa ijapokuwa hakuwa akimfikia mama yake katika uimbaji , lakini alikuwa na sauti nzuri mno , kwanzia mwanzo wa wimbo huo wa kistaarabu mpaka mwisho aliweza kuteka hisia za watu na sauti yake , lakini kubwa zaidi aliimba kwa hisia mno,Ile anamaliza kila mmoja alisimama na kupiga makofi ya kumshangilia.
“Ana sauti nzuri sana?”Aliongea Edna.
“Hawezi kumzidi Sophia”Alijibu Roma
“Unaongea kama vile ni ndugu yako , kama kweli unaamini Sophia anafanya vizuri kwanini unashindwa hata kutumia muda wako kuwasiliana nae”
“Ah! Ni ndugu yangu ndio kupitia wewe , halafu Daudi alinipa habari kwamba angerudi hivi karibuni Tanzania”
“Atarudi kuzindua albamu yake ya kwanza, yupo Nigeria kwa ajili ya Shooting , sasa hivi hayupo huru kama mwanzo kwani ashakuwa superstar”Aliongea
Baada ya ratiba za mwanzo kumalizika hatimae Ugawaji wa tuzo ulianza mara moja na Edna aliweza kumpatia Tuzo msanii bora wa kike wa mwaka, tunzo ambayo ilienda kwa Dina Queen of Africa..
Baada ya taratibu za tuzo kuisha hatimae Dina ndio aliepewa nafasi ya kutumbuiza kwa ajili ya kufunga tukio hilo , ikiwa imetimu saa sita kwenda saba usiku kutokana na mlolongo wa ratiba yenyewe.
Neema Luwazo pia alikuwepo kwenye mashindano hayo , akiwa amepatiwa pia nafasi ya kumpatia Tunzo msanii chipukizi wa kiume wa mwaka.
Ni muda ambao watu walianza kutawanyika Edna na Nessa walikuwa na maongezi ambayo Nessa alitaka yafanyike usiku huo huo kwani hatochukua muda mrefu.
Sasa mazungumzo hayo yalitakiwa yafanyikie kwenye moja wapo ya mgahawa uliokuwepo eneo hilo hilo la Mlimani , mgahawa ambao mpaka muda huo ulikuwa wazi , Edna ndio aliekuwa wa kwanza kufika ndani ya mgahawa huo akiwa ametangulizana na Roma.
Na kazi ya Nessa kuletwa hapo kwenye mgahawa alipewa Recho,kutoka ulipo ukumbi na huu mgahawa ni umbali mfupi sana kiasi kwamba watu waliokuwa wakitoka kwenye ukumbi wanaonekana.
“Bosi , Bosi….!!”Recho alikuja mbio mbio huku akihema na kumfanya Edna amwangalie Recho kwa namna ya mshangao.
“Kuna nini mbona uko hivyo na mgeni yupo wapi?”
“Kuna mtu kafa…”Aliongea huku akishika moyo wake , akishindwa kupumua vizuri , kauli ile ilimfanya Roma kumwangalia Recho kwa maswali.
“Unamaanisha nini , hebu punguza presha na utueleze nini kinaendelea”
“Dinaaa… Dina kafariki Madam..:”Aliongea huku machozi yakianza kumtoka , muda huo huo kelele za watu kutoka ukumbini zilisikika na kuwafanya Roma na Edna kuchukuana kurudi kwenye ukumbi.
Lakni ni ndani ya muda mchache sana polisi na wenyewe waliweza kufika.
Kwa maelezo ya Recho ni kwamba wakati anarudi kwa ajili ya kumchukua Nessa , alimkuta akiongea na baadhi ya wasanii hivyo alisubiri , lakini haja ndogo ilionekana kumbana sana , hivyo alitumia muda huo kuingia vyoo vya wanawake kwa ajili ya kujisaidia, lakini kitendo tu cha kufungua mlango wa choo kimoja wapo ndipo alipotahamaki kumuona msanii marufu anaefahamika kwa jina la Dina akiwa chini kwenye dimbwi la damu chini ya sink la choo cha kukalia.
Ni tukio la kutisha kutokea katika siku kama hio m ukizingatia kwamba mtu aliepatwa na kifo hicho ni msanii maarufu sana Tanzania.



SEHEMU YA 450.
Dina ni moja ya wasanii wenye umri mkubwa ndani ya taifa la Tanzania , lakini licha ya kuwa na miaka mingi uzuri wake ulikuwa ukifubaa kwa kiwango kidogo mno mpaka muda mwingine mashabiki wake kuhoji mwanamke huyo alikuwa akitumia chakula gani mpaka kuzidi kudumisha uzuri wake na kuonekana kijana zaidi.
Licha ya hivyo alikuwa akipendwa sana na watu kutokana na staili yake ya uimbaji , ashawahi kufanya Kolabo na wasanii wakubwa wa Nigeria akiwemo Tems, Davido na Burna Boy.
Kifo chake cha ghafla hivyo mara baada tu ya kutumbuiza kwa kufunga tukio la usiku wa Tuzo za Taifa , kiliibua maswali na joto kali.
Polisi waliweza kufika haraka haraka na kuweza kupima nini kimeweza kutokea , kwa maelezo ya awali Polisi wameweza kuelezea kwamba sababu ya kifo ni Dina kukatwa na kisu eneo la shingoni kwenye mshipa mkubwa wa kupeleka damu kwenye ubongo , hivyo kumsababishia kupoteza damu nyingi.
Roma aliekuwa karibu na eneo la tukio alijikuta akiguna, aliweza kupiga mahesabu kuanzia muda ambao waliweza kumuacha Dina akiimba stejini mpaka kumaliza ,lakini muda ambayo ameweza kwenda maliwatoni na kukutwa na tukio hilo , aliona kuna vitu haviingiii akilini kwa mlinganisho wa muda.
Polisi walitoa mwili wa Msaniii na Afande Mage aliweza kutangazia pia waandishi kuthibittisha kifo hicho na kuahidi uchunguzi ungefanyika kwa weledi mkubwa ili kubaini nani kahusika na kifo cha Dina ili sheria ichukue mkondo wake.
Wanahabari waliweza kunakiri habari hio kwa munkari ya hali ya juu mnohuku picha nyingi zikipigwa.
“Shuhuda wa kwanza kuona mwili wa Dina alikuwa ni Recho , hivyo alitakiwa kwenda kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa maelezo , Recho alionekana kuwa na wasiwasi mno , lakini Edna alimtoa hofu kwamba kila kitu kitakuwa sawa aende tu na isitoshe Mage ndio anaeongoza kesi hio.
Wageni waliondoka kwa mshituko mkubwa, huku habari zikisambaa mtandaoni kwa moto wa kifuu , hakuna ambaye ameweza kuamini kama Dina kweli ameweza kufariki mara tu baada ya kumaliza kuimba, ilikuwa ni habari ya kushangaza lakini ya kusikitisha kwa wakati mmoja.
“Edna nitahakikisha Recho anahojiwa ndani ya muda mfupi na kurudi nyumbani mapema”Aliongea Mage.
“Sawa Mage, Recho anaonekana kwenye mshituko mkubwa ni kheri kama hatolala kituoni”
“Usijali baada ya kuchukua maelezo yake na kuruhusiwa nitakutaarifu”AliongeaMage na kumwangalia Roma kwa dakika na kisha aliondoka eneo hilo kwa kupanda Difenda.
Edna alijikuta akivuta pumzi , hata hamu ya kubakia eneo hilo imemwishia, Roma aliona hali aliokuwa nayo mke wake hivyo alimchukua na kumuondoa kwenye eneo hilo na kuanza safari ya kurudi nyumbani.
Dakika chache tu mara baada ya kuingia ndani , simu ya Edna ilianza kuita mfululizo na baada ya kuona jina ni la Mage alipokea haraka haraka.
“Edna nimeona nikupe taarifa usiku huu”
“Nini kimetokea?”
“Tumeweza kupata kisu eneo la tukio ambacho kimeweza kumkata Dina eneo la shingoni na kukuta alama za vidole na tulivyojaribu kuziingiza kwenye mfumo imeonekana ni za Recho”Aliongea na kumfanya Edna kutoa macho.
“Unamaanisha Recho ndio amehusika kumkata Dina na kisu?”
“Inaonekana hivyo , pia hata mkanda wa CCTV zinaoneyesha baada ya Dina kingia chumba cha maliwatoni na Recho pia aliingia na hakuna mtu mwingine alieingia tunashindwa kuthibitisha muhusika kwani hakuna Camera ndani ya vyoo”Aliongea Mage na kumfanya Edna kujikongoja na kukaa kwenye sofa.
Roma alichukua simu haraka haraka kutoka kwenye mikono ya Edna na kuongea na Mage.
“Mage ninaweza kuona mwili wa Marehemu?”
“Ndio , umehifadhiwa hospitali ya Lugalo , ninaweza kuongea na baba na ukapita kuuona ndio naelekea huko sasa hivi”Aliongea na Roma alikata simu mara moja.
“Edna usiwe na wasiwasi naamini Recho hawezi kuhusika katika hili , mpigie simu mwanasheria ili aweze kumuwekea Recho Zamana wakati uchunguzi ukiendelea”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa.
Ilikuwa usiku lakini Roma alijiambia lazima afanye uchunguzi muda huo huo , hata hivyo tokea mwanzo kulikuwa na kitu kinamtekenya mara baada ya kumuona Nessa mtoto wa marehemu Dolores kutoka Ireland.
Dakika chache tu zilimtosha kuweza kufika Lugalo na kukutana na Mage , ambaye alimuongoza moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha Forensic, sehemu mwili ulipohifadhiwa kwa muda kabla ya kuingizwa Mochwari.
Roma baada ya kuingia kwenye chumba hicho chenye ubaridi kiasi , aliweza kushuhudia mwili wa Dina ukiwa umelezwa juu ya meza kubwa ya bati ukiwa umefunikwa na shuka nyeupe kwa juu.
Mage alijikuta akiwa na wasiwasi mno na kujiambia kweli mtu akishakufa ndio basi tena , ni ngumu kuamini msanii aliekuwa akipendwa na watu wengi ndani ya Tanzania ndio huyo alielazwa peke yake kwenye chumba cha baridi.
Roma aliweza kuufunua mwili wote na kutoa shuka ambalo limemfunika , huku Mage akisogea taratibu kwa wasiwasi , ijapokuwa alikuwa Polisi lakini kukagua maiti haikuwa fani yake, kwani madaktari wa kipolisi walibobea kwenye upande wa ‘Forensic investigation’ ndio waliokuwa wakihusika na uchunguzi.
“Kwa uchunguzi wa mwanzo uliofanywa na madaktari wamesema kifo chake kimesababishwa na kupoteza damu baada ya kukatwa kwa nguvu eneo la Shingoni kwenye mshipa mkubwa wa damu , vipi unaamini kuna uwezekano wa sababu nyingine ambayo imesababisha kifo chake?”Aliuliza Mage kwa sauti ya chini.
“Hapana , kilichomuua ni kweli ni kukatwa na kisu , lakini naamini kuna uwezekano wa sababu nyingine pia”Aliongea Roma huku akisogea upande wa miguuni na kuanza kugusa mwili huo kwa namna ya kupapasa.
“Kwani lazima umguse hivyo , huwezi kuangalia tu”Aliongea Mage huku akivuta pumzi nyingi na kumfanya Roma kucheka .
“Mage hata kama nina genye kiasi gani siwezi kufanya maiti , ninachofanya hapa ni kuangalia kama kuna kidonda kingine tofauti na cha shingoni”Aliongea Roma.
“Kidonda kingine?, Kwanini kiwe kwenye maeneo kama hayo?”
“Swali zuri , kwasababu hakuna mtu ambaye anaweza kutegemea kidonda kuwepo kwenye hili eneo, Nilitaka kwanza wataalamu wafanye kazi yao na mimi nifanye kazi yangu kutokana na eneo nililotaka kuchunguza kuwa ‘sensitive’,mtu angeweza kuona labda naidhalilisha maiti”Aliongea Roma huku akichanua miguu ya Maiti na kusogeza macho karibu zaidi , maiti yote ilikuwa imevuliwa nguo hivyo ilikuwa kwake rahisi kuchunguza.
Mage bado alikuwa na wasiwasi na alichokuwa akifanya Roma , lakini aliamua kutulia kuendelea kuangalia mwisho wake.
Roma baada ya kuchanua miguu na kuangalia katikati karibu kabisa na sehemu za siri, alimpa ishara Mage kusogea na kuangalia na Mage alijikuta akiziba mdomo kwa mshituko.
Kulikuwa na matundu mawili ambayo yalionyesha kutoa damu ya wastani, yalikuwa madogo kiasi kwamba ilikua ngumu kwa mtu kuyaona hususani kwenye eneo lenyewe.
“Haya ni…”Afande Mage alionekana kukosa neno
“Wew unaonaje?”Aliuliza Roma
“Inaonekana kama ameng’atwa na nyoka , lakini haya matundu ni makubwa kidogo hivyo ni ngumu kusema ni nyoka..”Aliongea Mage kwa mshituko.
“Acha ujinga haya ni meno ya Vampire , Wanajiita wenyewe kwa jina la kingereza Blood Race”
“Unasema..!!”Mage ilikuwa mara yake ya kwanza kusikia kuhusu Vampires na Roma aliongea hivyo kwa kumdhania Mage ni Magdalena , kwani kuna siku moja Roma alimpatia Magdalena maelezo ya kutosha.
“Naona upo kwenye mshituko na unaweza usiamini ninachokuambia , ila nishawahi kukutana na Vampire miaka kadhaa iliopita”Aliongea lakini Mage alishindwa kuamini , alishawahi kusikia kuhusu Vampiea hata kuona muvi za aina hio , lakini haikuwahi kumuingia akilini kwamba hadhithi hizo ni za kweli.
“Kama kweli unasema ni Vampire kwanini wameng’ata eneo la huko na sio shingoni?”
“Vampire kunyonya damu eneo la shingoni ni uzushi mkubwa sana ambao walieneza wao wenyewe kupitia hadithi na baadhi ya Muvi hio yote ni kuficha namna wanavyoweza kumfyonza binadamu ili wasigundulike uhusika wao na tabia zao, Wenyewe wanaamini damu inatofautiana utamu kutokana na eneo katika mwili , Eneo la shingoni wanapenda pia lakini ni sehemu ambayo ipo wazi sana nadhani hata wewe umeona madaktari hapa wamethibitisha Dina amekufa kwa kukatwa na kisu wakati sababu ni nyingine kabisa , hii ndio mbinu yao”Aliongea. Roma na kuendelea.
“Mishipa yote ya damu maeneo ya mapajani mpaka sehemu za siri ndio sehemu wanazopenda sana , damu inayotoka hapo ni tamu sana , pili ni yenye kujitosheleza, lakini kingine kinachowafanya kupenda ni harufu ya Homoni za kike katika eneo hilo”Aliongea
“Aaah… inatia kinyaa”Aliongea Mage na Roma aliuweka mwili vizuri na kuufunika vna kisha alimwambia Mage waondoke hapo akaanze msako wa kutafuta Vampire halisi ambalo limehusika na kifo cha msannii Dina.
Unafikiri nani kahusika na ni raia gani ambaye ni Vampire
END OF SEASON 15 ,
SEE YOU 0687151346 watsapp nicheki by SINGANOJR - SPONSORED BY MIND LINK ENETERTAINMENT
 
Ndiooooo
 
Shusha Nondo nasema shusha vitu mkuu Hades SinganoJr,aka Roma Roman. Tunakufuatilia...hii weekend isipite hivihivi mambo yanazidi kuwa bambam.
 
Huu mji wq Iznik wa Uturuku niliona kwenye filamu ya The OTHOMAN Azam tv Kama sehemu mojawapo ambayo OTHMAN anapataka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…