Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hatimaye nimefika kwenye arosto sasa singano huna bayaSEHEMU YA 495.
Roma alishangazwa na kupatwa na huzuni ya taarifa hio ya kifo kwani siku hio hio ndio walipanga kwenda yeye Edna na Lanlan kumtembelea, kwao ilikuwa ni kama wamechelewa kwenda , lakini hata hivyo hakujilaumu sana kwa kutowahi kwenda kumuona.
Mzee Atanasi ni moja wapo ya wazee waliokula chumvi nyingi na alikuwa akikaribia kutimiza miaka mia moja na moja na kwa uzito wake ndani ya serikali ya Tanzania ni sahihi kuitwa babu wa taifa.
Ndio mwanajeshi pekee aliebaki ambaye alipigania uhuru wa Tanzania pamoja na Raisi Nyerere.
Roma hakuwa na haraka ya kwenda moja kwa moja msibani , alitaka kwanza kumaliza kilichomfikisha hapo na kisha ndio arudi nyumbani na kuelekea huko , ile safari yao ya kwenda kwa ajili ya kusalimia iligeuka na kuwa safari ya kwenda msibani.
Roma baada ya kukata simu kwa kumpa mama yake pole aliwageukia Diego na kuwapa taarifa hio ya msiba na Diego na Bram walimpatia pole.
Roma aligeukia kwa mara ya pili picha iliokuwa ikionekana kwenye skrini , picha ya mwanaume aliefahamika kwa jina la Bikindi , alikuwa ni baba mzazi wa Lekcha na Roma alimkumbuka kwasababu ni moja ya wanasayansi wa Zeros organisaiton aliowaua.
“Mfalme Pluto unamfahamu huyu mwanaume?”Aliuliza Diego na Roma alitingisha kichwa kuashiria anamjua.
“Mmefanikisha kuchunguza taarifa za Joseph Bikindi za hivi karibuni”
“Ndio mfalme Pluto kwa taarifa tulizoweza kupata kutoka Rwanda mpaka miezi michache iliopita alikuwa mkufunzi wa chuo kikuu cha taifa lakini kwa wiki kadhaa sasa ameripotiwa kutoonekana chuoni bila ya taarifa”.
“Endeleeni kumchunguza kwa ukaribu zaidi na sura yake iunganishe na mfumo wetu wa ‘facial recognition’ ili kama itatokea akiwepo Tanzania tuweze kutambua mara moja”Aliongea Roma huku akipata hisia huenda Lekcha alikuwa Tanzania kwa kutafuta namna ya kulipiza kisasi na kwa muda huo ambao Kizwe alionekana kutokuwa wa kawaida aliamini huenda wapo wote na wanajiandaa na mipango ya kulipiza kisasi , hakusahau na Denisi alikuwa hivyo hivyo tu ndio maana alihitaji kuchukua tahadhari mapema.
Jambo lingine ambalo lilimfanya kuwa na wasiwasi ni juu ya Athena ,tokea apewe cheo cha Hades hakuwahi kujionyesha kwake na alikuwa akijua ana mzunguka lakini hakuwa akijua sababu ni ipi ,lakini alijiambia maadamu yupo hai basi kuna siku tu wataonana na atathibitisha maswali yake yote.
“Vipi kuhusu uchunguzi wa Chriss mlikamilisha?”
“Mfalme Pluto taarifa za Chriss imekuwa ngumu sana kuzipata na mpaka sasa hatujapiga hatua lakini kuna jambo moja tu ambalo tulifanikiwa kupata”
“Mmepata nini?”Aliuliza Roma kwa shauku na Diego alitoka ndani ya chumba hiko na ndani ya muda mfupi aliweza kurudi na mfuko wa plastic ambao ndani yake ulionekana kuwa na mkufu uliofungwa na kishaufu cha madini ya almasi.
“Huu ni…”
“Ni mkufu ambao unaonyesha Chriss alikuwa mwanachama wa Freemason”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuchukua na kuangalia vizuri na kweli aliweza kugundua maana ya mchoro uliokuwa kwenye kishaufu(Pendant).
Ijapokuwa sasa ameweza kuanza kupata ukweli wa Chriss alikuwa akitokea jamii ya siri ya freemason lakini ilikuwa ngumu kwake kuweza kuamini kama watu wa jamii hio ya siri ndio walitaka kumuua mke wake na moja kwa moja alijua huenda majibu yapo kwenye mchoro.
Roma ilibidi kwanza amuelezee Diego na Bram kile ambacho alikuwa akitambua kuhusu Chriss.
“Mfalme Pluto hata sisi tunashindwa kuelewa kama Chriss alikuwa mwachama wa Ant- illuminat”
“Kwanini mnaamini hawezi kuwa mwanachama unajua taarifa zote za umoja huo?”
“Ndio mfalme Pluto najua taarifa zote zinazohusiana na umoja wa ant- illuminat na baadhi ya mipango yao ya mbeleni japo mpaka sasa hakuna uthibitisho kwani ni taarifa ambazo ni kama uzushi”
“Ni taarifa gani ambazo unafahamu?”
“Mfalme Pluto ushawahi kusikia kuhusu mpango TASAC?”
“Mpango TASAC!, si huu ulioanzishwa na serikali ya Urusi kuyafanya mataifa ya Afrika kutounga mkono wala kukataa vamizi anazozifanya Raisi wa Urusi nchini Ukraine?”
“Ndio mfalme Pluto lakini ni ngumu kusema mpango TASAC umeanzishwa na Urusi”
“Kwanini?”
“Taarifa za siri za daraja la tatu zinaonyesha mpango TASAC waanzilishi ni Ant- illuminat”Aliongea na kumfanya Roma kuguna ilikuwa habari mpya kwake na huenda angekuwa anafatilia sana maswala ya siasa angekuwa ashaijua , huenda ilikuwa sahihi kwa Christen kumwambia hayuko ‘flexible’ kama mtangulizi wake”
“Uzushi mwingine unaoenezwa kuhusu Ant-illuminat ni juu ya mataifa ya kiarabu kuwekeza zaidi katika mataifa yalioendelea ya kimagharibi katika nyanja ambazo zinagusa moja kwa moja hisia za watu mfano kwenye vilabu vya mpira na kadhalika”Aliongea Bram.
“Na pia ndio kinara wa mapambano ya sarafu ya Dola ya kimarekani kutaka kuiangusha”Aliongezea Diego.
“Inaongekana mnapenda sana uzushi”
“Your Majesty if no Somke no Fire “Aliongea Diego akiingiza msemo ambayo unaoendana na ule wa kiswahili usemao yasemwayo yapo na kama hayapo yaja au penye moshi hapakosi moto.
Roma hakutaka kukaa sana hapo kwani kuna msiba ambao ulikuwa ukimuhusu na mpango wake ni kuunganisha kwanza msibani kujua kile kinachoendelea na kujua taratibu zinazofuatia, hivyo alitoa msisitizo wa usalama zaidi wa watu wake wa karibu kuzingatiwa hususani muda huo ambao alijua na Lekcha ni adui yake mpya alieingia kwenye orodha.
Akiwa garini alijaribu kuwasiliana na mke wake kumuulizia kama kapata taarifa na ilionyesha Edna alikuwa na taarifa na alikuwa akijiandaa kwa ajili ya kufika msibani pamoja na Bi Wema na Roma alimwambia angemkuta huko huko kwani anatangulia.
Baada ya kufika Masaki nyumbani kwa Tajiri Azizi aliweza kuona watu wengi waliokuwa wakiingia ndani ya nyumba hio na kutoka na pia kulikuwepo na baadhi ya waandishi wa habari.
Kwa haraka haraka Roma alishajua msiba huo ni wa kitaifa hivyo wageni wengi lazima wangefika kutoa salamu zao za pole.
Roma hakuingiza gari ndani ilibidi apaki pembeni kwa kuhofia ndani kusingekuwepo na nafasi na baada ya kuegesha aliingia moja kwa moja ndani na alikuta tayari maturubai yashasimamishwa pamoja na viti ambavyo vilikuwa vikipangwa.
Mtu wa kwanza kuonana nae alikuwa ni Kassimu mtoto mkubwa wa tajiri Azizi ambaye alikuwa akipokea wageni na alimkaribisha Roma na kumpeleka kuonana na mama yake pamoja na wanafamilia wengine.
Dakika chache mbele na Edna aliweza kufika na kutoa pole , msiba haukuwa na vilio sana zaidi ya sura za majonzi tu huenda ni kwasababu mzee huyo kaishi miaka mingi na muda wake umewadia hivyo alipaswa kutangulia mbele za haki .
Ratiba ya msiba ilikuwa ni siku inayofauta mwili kuagwa katika viwanja vya Karimjee na kisha safari ya kuelekea Kilosa kijijini ingeanza ili kumpumzisha Babu Atanasi.
Katika watu ambao walikuja kutoa salamu za pole ni Samweli Nguruma kiongozi wa kundi la ZoaZoa na ilikuwa ni kama amekuja kumtafuta Roma kuongea nae.
Roma alishawahi kuwasiliana na bwana huyo kwa kupitia simu ila hakuwahi kukutana nae ana kwa ana na siku hio ndio waliweza kufahamina kwa mara ya kwanza.
Samweli Nguruma baba yake na Benadetha alikuwa ni kama bosi mtu mwenye kitambi na kipara cha nywele na ilikuwa ngumu kuamini ndio ambaye alikuwa akijihusisha na biashara za magendo lakini hata hivyo Roma hakutaka kumtoa dosari ukizingatia hata Rose hakuwa na mwonekano wa kuongoza kundi la Tembo.
“Mr Roma unamwonaje mtoto wangu Benadetha?”Aliuliza Samweli Nguruma na kumfanya Roma kushangazwa na swali hilo.
Ilikuwa ni saa za mwisho mwisho za kuaga mwili ili safari ya kuelekea Morogoro ianze ndio maana Roma alishangaa.
“Kwanini unauliza hivyo mzee?”.
“Nataka kujua maoni yako, umefanya nae kazi kwa muda mrefu kidogo hivyo sio dhambi kutoa maoni yako unavyomuona na tabia yake kwa ujumla”Roma ijapokuwa muda huo aliona hakupaswa kujibu swali hilo kutokana na muda kutokuwa mzuri lakini aliona ni kheri kujibu kile anachokiona kwa Benadetha.
“Namuona kama msichana mzuri mwenye sheria zake na inaonyesha ashatambua mapema kama mwanamke anataka nini katika maisha yake”Alijibu Roma na kumfanya Samweli nguruma kutabasamu.
“Upo sahihi Benadetha ni binti mwenye msimamo na mara nyingi uwezo wake mkubwa wa kujielewa unanifanya hata mimi baba yake kumhofia”
“Hongera kwa malezi, kwa ninavyomuona atakuja kuwa na maisha yenye furaha sana mbeleni”
“Furaha ya mwanamke inakamilika pale akiridhika na kila kitu kunachomzunguka, asipo ridhika ataishia kutangatanga kukidhi haja ya moyo wake”Aliongea
“Ndio maana nikasema Benadetha atakuja kuwa na furaha kwasababu kama mwanamke ukishafahamu kwenye maisha unataka nini mapema ni rahisi pia kuridhika”
“Upo sahihi Mr Roma lakini ushawahi kujiuliza kwanini kipindi Benadetha alipopelekwa kituoni na mkeo nilitaka wewe ufanye kazi ya kumtoa?”
“Kwanini?””
“Nilijua tayari mkeo ashafahamu hisia za Benadetha kwako”Aliongea na kumfanya Roma ashangae.
“Mzee labda utakuwa haujamfahamu Benadetha vizuri , mimi na yeye hatuna ukaribu huo na hata kama Benadetha anipende mimi kama mwanaume siwezi kumpokea kwani tayari nina mke”Aliongea Roma bila ya wasiwasi.
“Haha.. Mr Roma nimekutana na vijana wengi ila ujasiri wako na kujiamini ni wa viwango”
“Na wewe pia ujasiri wako ni wa viwango kumnadi mtoto wako wa kike kwangu ilihali tayari nina mke sio jambo la kawaida kabisa kwa tamaduni za kiafrika”
“Upo sahihi imenichukua ujasiri kuongea na wewe kuhusu maswala ya binti yangu na nimetidhika pia kama huna nia ya kumfanya kuwa sehem ya wanawake wako”Aliongea na kumfanya Roma kumchanganya na kuona huenda habari za yeye kuwa na wanawake wengi zilikuwa zikifahamika kwa watu wengi.
*********
Tokea kumalizika kwa maziko ya Babu Atanasi siku zilienda haraka haraka mno na katika watu ambao walikuwa wako bize basi ni Roma ,kuna muda alijiambia uwepo wa Lanlan kidogo ulikuwa umesaidia sana kupunguza migogoro yake na Edna.
Kwani kitendo cha Lanlan kung’ang’ania kulala na mama yake ilimpa nafasi Roma ya kila usiku kutembelea wanawake wake kwa zamu na hilo pia lilisaidia sana kuyafatilia maendeleo yao.
Vidonge ambavyo aliweza kuvipata baada ya kuwaua watu wa hongmeng vilisaidia sana katika kumfanikisha Rose kupanda levo na Roma aliona kabisa muda si mrefu Rose angefanikisha kupata ufunuo wa nguvu ya mbingu na Ardhi jinsi ya kutumia elementi zote za dunia.
Katika mafunzo ya kijini kila mmoja alitofautiana na mwenzake katika kupata ufunuo wa namna ya kutengeneza maajabu kwa kutumia elementi za dunnia na hicho ndio ambacho kilimfanya Roma kupatwa na hamu kubwa ya kuwaona wakifikia levo ya kupata ufunuo.
Mage na yeye hakuwa mbali sana na ilionyesha juhudi zake zilionyesha manufaa kwani alianza kuelewa levo ya nusu mzunguko kikamilifu na Roma aliona kabisa muda si mrefu angeweza kuingia levo ya mzunguko na alijiambia kama atafanikisha mpango wake wa kutengeneza vidonge vyenye nguvu basi huenda ndani ya mwaka mmoja kila mmoja anaweza kuingia kwenye levo ya Nafsi na matumaini ya kuweza kupata mtoto yangekuwa juu.
Upande wa Amina msukumo wa ndani zaidi kujifunza mafunzo hayo ni kwa ajili ya kutunza urembo wake na kufanya tahajudi muda mrefu haikuwa kazi kubwa kwake, ,ijapokuwa maendeleo yake yalikuywa ya taratibu lakini alileta matumaini na hata hivyo Roma alifurahi kuona Amina alikuwa mzoefu wa mazoezi ya Yoga na hilo ndio lilirahisisha.
Neema Luwazo ndio ambaye alikuwa akijifunza kwa fujo sana na tamaa kubwa ya kufikia levo za juu na Roma aliona huenda ni kwasababau alikuwa akiukaribia utu uzima ndio maana alitaka kupanda levo kwa haraka ili asiendelee kuzeeka na kubakia na mwonekano wa ujana.
Lakini licha ya fujo alizokuwa nazo za kutaka kujifunza maendeleo yake yalikuwa ni ya taratibu mno kulinganisha na wengine wote kutokana na utu uzima wake kwani ilikuwa rahisi kwa vijana kujifunza na kupanda levo kwa haraka tofauti na watu wazima na Roma ilibidi achukue jukumu la kumtuliza.
“Roma nimeachia majukumu kabisa ya kampuni kwa Alhaji kwa ajili ya kujifunza”Aliongea Neema usiku Roma alipomtembelea.
“Umefanya vizuri lakini unatakiwa kwelewa mbinu hizi huwa zinaendana na utulivu wako wa akili ukiwa na tamaa ya kupanda levo kwa haraka utakosa utambuzi wa kunyaka kila viashiria vinavyokujia wakati wa kufanya Tahajudi na ndio maana nakushauri usichukulie sana hili swala siriasi lifanye kama ni moja wapo ya starehe, kama unavyokaa kwenye Jakuzi ukiwa umeshikilia glasi ya mvinyo ukiyafurahia mafanikio yako”Aliongea Roma nakumfanya Neema kutabasamu.
Na alfajiri Roma alijaribu kufanya nae mafunzo na sasa angalau aliona akili yake ilikuwa imetulia , ilionekana maneno yake ya jana usiku yalikuwa yamefanya kazi.
Upande wa Edna na Nasra maendeleo yao yalikuwa ya kinyonga lakini yalioleta mabadiliko kwenye miili yao.
Zamani Edna alikuwa akimhofia Lanlan kumrukia kutokana na uzito wake lakini kwa kipindi chote alichokuwa akichukua mazoezi alikuwa ameimarika na kumudu hata uzito wa Lanlan vizur.
*******
Ni baada ya wiki moja kupita hatimae Omari na Queen waliweza kufunga ndoa yao rasmi kwa tamaduni za dini ya kiislamu ambazo zilimtaka Queen kubadili dini jambo ambalo Mzee Alex hakupinga, hata hivyo ni Omari pekee ambaye alionyesha kumpenda mtoto wake kwa mapenzi ya dhati licha ya kwamba alikuwa mjamzito hivyo hata swala la Queen kubadili dini kuwekwa mezanni kwake hakuwa na kipingamizi.
Saa tano na nusu za usiku ndio muda ambao Roma na Edna walirudi kutoka kwenye sherehe ya harusi hio ya Omari na Queen na wakati Roma anaingiza gari ndani ya geti alishangazwa kuona nyumba bado inatoa mwanga wa taa kutokea sebuleni kwani kwa muda huo aliamini wanafamilia wote wangekuwa washalala.
Roma usiku huo akiwa njiani alikuwa akipanga kwenda kuburudika na mke wake Edna usiku kucha kwa kuamini muda huo Lanlan angekuwa tayari amekwisha kulala na Qiang Xi.
Lakini sasa ile wanaingia sebuleni lile tumaini lake lote lilipotea baada ya kumkuta Qiang Xi na Lanlan wakiwa wamekaa sebuleni na hata Edna mwenyewe alishangaa kuwakuta hapo kwani muda ulikuuwa umeenda.
“Qiang mbona mpaka muda huu Lanlan hajalala na asubuhi anatakiwa kuwahi kuamka”
“Madam nimejaribu kumfanya alale lakini hana usingizi na anasema anakusubiria”Aliongea Qiang Xi huku akionyesha hali ya uchomvu ilionekana alikuwa akijitahidi kuwa macho kwasababu ya Lanlan na alikuwa amechoka.
“Lanlan kwanini unashindwa kulala?”
“Mama sipati usingizi , Lanlan anataka kulala karibu na mama”Aliongea na kumfanya Roma akunje sura alijiambie kama watoto wake watakuja kuwa kama Lanlan basi maisha yake yangekuwa magumu sana.
Edna alimuonea huruma kuona alikosa usingizi na swala hilo lilikuwa likimsumbua kichwa namna ya kulitatua kuishia kujiuliza kama siku nyingine asingekuwepo na Lanlan angelala vipi.
Upande wa Roma alishajua kwanini Lanlan alikuwa akikosa usingizi , sababu ilikuwa ni kutokana na damu yake kuchemka kila wakati na kumfanya kukosa utulivu wa akili ndio maana alikuwa akikosa usingizi na njia pekee ambayo aliona huenda ingemsaidia Lanlan ni kumfundisha ya mbinu ya kimaandiko ya urejesho ili aweze kudhibiti uwezo wake lakini alimuona Lanlan ni mdogo na hata kama angejaribu kumfundisha kutamka maneno ya maandiko na kuyageuza kuwa nguvu ingekuwa ngumu kwake.
Hivyo suluhisho la muda mfupi ambalo aliona lingefaaa kwa muda huo ni Lanlan kuendelea kulala na Edna mpaka atakapogundua namna ya kumsaidia kupata usingizi bila ya uwepo wa Edna.
Roma mara baada ya kurudi kwenye chumba chake akijiandaa kwenda bafuni kujimwagia maji alale simu yake ilitoa mlio wa ishara ya mwaliko wa mtu kumpigia kwa njia ya Vidio Call.
Baada ya kuangalia inatoka kwa nani aligundua ni Sauron na alijikuta akiwa na shauku ya kumsikia maana ni kama mwezi unakaribia kuisha tokea ampatie Sauroni kazi ya kusambaza vijana kutafuta maeneo walioishi binadamu enzi za kale , maeneo ambayo yalifanikisha ukuaji wa mila na tamaduni za kijamii za mwanzo kabisa(Ancient Civilization) lakini baada ya muda maeneo hayo yakatelekezwa , aliamini upatikanaji wa maeneo hayo ingekuwa rahisi kwake kuweza kupata mimea anayojitaji itakayosaidia katika utengenezaji wa vidonge vya kijini.
SEHEMU YA 496.
Licha ya mwonekano wa kutisha kutokana na mtindo wake wa nywele nyingi alizokuwa nazo kwa upande wa Roma alikuwa ashamzoea na kumuona mtu wa kawaida lakini kwa mwingine huenda mwonekano wa Sauroni ungemkosesha amani hususani wakati anapokuwa siriasi.
Ilionekana muda huo Sauroni upande wa kwao kulikuwa ni mchana maana alionekana ndani ya ofisi huku kwenye meza yake kukiwa na mafaili mengi, huku yeye mwenyewe akiwa amevalia miwani ya kusomea.
Roma mara baada ya kupokea simu na kubadilishana salamu na Sautoni ilibidi amwambie aende moja kwa moja kwani alitaka kulala.
“Mfalme Pluto nishakutumia mafaili yanayohusiana na taarifa ulizo omba kupitia barua pepe yako , tumefanikisha kupata maeneo nane yanayofanana na sifa ulizotupatia”Aliongea Sauroni
“Asante sana Sautoni kwa juhudi zako zilizopelekea kufanikisha , vipi kuna changamoto yoyote uliweza kupata?”
“Sijapata changamoto kubwa mfalme Pluto lakini nina shauku ya kufahamu kwanini unahitaji taarifa za hayo maeneo kwani kwa uelewa wangu hayo maeneo sasa hivi hayakaliwi na binadamu na huenda hata uwepo wa hio mimea ni kwasababu hio na binadamu wa kawaida ambaye angesafiri kwenda kwenye hayo maeneo asingeweza kutoka hai”Aliongea na kumfanya Roma kucheka kidogo
“Maeneo ambayo watu waliishi na sasa hawaishi ndio ambayo ninayatafuta kwani naamini inaweza kufanikisha kupata kile ninachohitaji , najua una shauku lakini nitakuelezea siku nyingine kwasasa taarifa hii ulionitumia nitaipitia na kuanza na mikakati ya kuelekea huko”Aliongea Roma na Sauroni aikubali na kisha akakata mawasiliano
Roma alighairi kwanza kwenda kuoga na kuanza kupitia taarifa ambazo ametumiwa na Sauroni na ilionekana ziliandikwa vizuri ili kueleweka kwa urahisi, ni ‘Document’ ambayo ilikuwa na peji nane ambazo zilikuwa zikielezea maeneo husika ambayo yalikuwa yakikidhi vigezo.
Na mpaka anakuja kumaliza alikwisha kupata sehemu ambayo aliona inafaa kuanzia kutafuta mimea hio lakini kwakuwa hakuwa mzoefu sana alitaka kwanza kusikia maoni kutoka kwa Rufi na kwasababu muda huo ulikuwa ni usiku sana aliona angewasiliana nae asubuhi.
Siku iliofauta jambo la kwanza ilikuwa ni kuwasiliana na Rufi na akamtumia na faili la taarifa alizotumiwa na Sauroni na wote walijikuta wakiachana na baadhi ya maeneo yalio orodheshwa kwa sababu za aina moja, waliachana na eneo la Eveglades ambalo lipo kusini mwa Marekani , Msitu wa Panama , msitu wa Amazoni na maeneo mengine na wakaja kuchagua eneo lililofahamika kwa jina la Arnhem Land ambalo lipo kaskazini mwa bara na nchi ya Australia.
Arnhem Land ni eneo ambalo walichagua kutokana na historia yake kwani sio tu kwamba miaka ya hivi karibuni halikukalika lakini miaka mingi iliopita lilikaliwa na watu wa asili zaidi wa nchi ya Australia na ilikuwa ni eneo ambalo ni kama tamaduni nyingi zilizaliwa na hivyo ndio vigezo ambavyo Rufi alipendekeza.
Eneo ambalo lilikaliwa na watu wa asili na kuzaa tamaduni na mila ndio ambalo lingekuwa na mkusanyiko wa nguvu nyingi za kiroho ambazo zingefanikisha upatikanani wa malighafi za Alchemy.
Roma alikuwa akielewa Australia ilikuwa kusini mwa ncha ya dunia na kwa mwezi huo wa nne kwenda wa tano ni kipindi cha Vuli na kama angevuta muda vuta muda basi mwezi wa sita ingekuwa ni hatari zaidi kwenda kwani ingekuwa ni kipindi cha baridi kali na kwasababu hakuwa akienda mwenyewe alitakiwa pia kuzingatia hali ya kiafnya ya Rufi na ndio maana aijiambia ni kheti kuharakisha kufanya safari na kwenda kutafuta hio mimea na kuanza harakati zingine.
Rufi alikuwa ashakubali kuongozana nae kwani hakuwa na shughuli ya maana ya kufanya Tanzania na maisha yake yalikuwa ya upweke sana na aliona ingekuwa kama utalii kwake kusafiri mpaka Australia.
Tatizo ambalo Roma aliona ni changamoto ambayo alipaswa kuitatua ni kwa mke wake , alijua akimuaga kwamba anaelekea Australia na Rufi angemuwekea ngumu lakini hata hivyo aliona lazima akubaliane na matakwa yake kwani anachokifanya sio kwa faida yake mwenyewe bali ni kwa faida ya wote.
Usiku baada ya Roma kupata chakula aliona ndio wakati muafaka wa kumweleza Edna mpango wake wa kusafiri na Rufi na Roma alimsubiria kwanza Edna amalize kumwandaa Lanlan kwa ajili ya kulala na ndio aongee nae.
Roma mara baada ya kukaa chini na kumuelezea anachopanga mwanzoni hakushangazwa na taarifa hio lakini Roma alipokuja kusema anataka kwenda na Rufi alihisi hatari.
Tokea aanze kuwa na ukaribu zaidi na mume wake alikuwa mwangalifu mno hakutaka Roma aongeze mwanamke kabisa na ndio maana hakutaka mazoea kati ya Rufi na Roma kuongezeka kwani mwisho wake usingekuwa wa kheti kwake.
“Najua unaweza kuona sio sawa mimi kwenda na Rufi lakini hili ni swala ambalo napaswa kulifanya na hata hivyo Arnhem sio sehemu ambayo ipo kiburudani ni kama gereza na kila kitu ni msitu hivyo kwenda na Rufi kule ni kama nampeleka kuzimu, hivyo mke wangu usiwe na wasiwasi na toa ruhusa yako niweze kuondoka nae”Aliongea Roma kwa unyenyekevu baada ya kuona mabadiliko yake.
Edna alifikiria na alionekana kama mtu ambaye amechanganyikiwa, moyo wake siku hizo za karibuni ulikuwa tofauti na zamani, alikuwa tayari kuona Roma akiendelea na wanawake wale wale aliokuwa nao na asione wivu lakini kumuona mwaamke mwingine mpya kwake ilimuuma na kumuogopesha kwa wakati mmoja na hata yeye mwenyewe alijishangaa na hata Roma alivyoweka wazo hilo akili yake ilimwambia na yeye aungane nae ili aweze kumlinda vizuri , lakini alifikiria uwepo wa Lanlan aliona asingeweza kuongozana na Roma na kumuacha peke yake.
Wazo moja tu ambalo lilimjia katika akili yake na kuona ndio njia mbadala ni kumteua mtu mwingine wa kuongozana nae kwenda huko na ingekuwa rahisi kuzuia mahusiano kuibuka zaidi na zaidi
“Nimekubali unaweza kwenda nae lakini lazima uende na mtu mwingine pia”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.
“Mtu mwingine kwenda nae sio tatizo kwangu , nani unaona anafaaa kunisindikiza?”
“Mage”Aliomngea akiwa ni mwenye sura iliojaa usirias na kumfanya Roma moyo wake kupiga kite , alikuwa na mahusiano na Mage lakini alikuwa akiyafanya siri Edna asifahamu.
“Unashangaa nini Mage ndio mtu pekee ambaye unaweza kwenda nae ningewaruhusu mwingine lakini kwa walivyokuwa wadhaifu kwako wasingeweza kukuzuia kufanya jambo la kishenzi?”Aliongea na kumfanya Roma kukuna kichwa.
Roma alikuwa na mahusiano na Mage lakini hakuwahi luyaweka wazi na ndio maana alikuwa kwenye mshangao bara baada ya Edna kutaja mtu wa kuongozana nae kwenda Australia kuwa Mage, hali hio ilimfanya kuvhanganyikiwa yeye mwenyewe kwa kuona Edna alikuwa akifahamu siri yake halafu alikaa kimya.
"Mbona uko hivyo au Mage hafai ?"
"Sio kwamba hafai lakini kuna ulazima wa kutangulizana na mwanamke?"
"Ndio nataka utangulizane na mwanamke tena mwanamke huyo akiwa Mage ndio mtu pekee ambaye anaweza kukuzuia usifanye ujinga na Rufi na ndio sharti langu"Aliongea
"Edna ulifahamu lini?"
"Kuhusu nini?"
"Mimi na Mage tuna mahusiano" Aliongea Roma kwa ujasiri lakini kwa hofu ndani yake na swali lake lilimfanya Edna kucheka kidogo kwa uchungu.
"Hilo swali muulize Mage mwenyewe atakuwa na majibu" Aliomgea Edna na kisha hakutaka mazungumzo zaidi na kuondoka kwenye chumba hiko cha kujisomea na kumuacha Roma bado akiwa kwenye sintofahamu.
Ni kweli alikuwa na mahusiano na Mage lakini siku zote alikosa ujasiri wa kumuweka wazi Edna , lakini alishangaa Edna kutambua juu ya hilo bado lakimi aka kaa kimya bila ya kuzungumza.
Roma alijiuliza Edna alifahamu lini maana kama ingekuwa ni siku hio basi huenda angemnunia siku nzima lakini ajabu walikuwa sawa na hata siki yao iliisha bila shida.
Ila kitendo sasa cha Edna kuondoka wakiwa hawajamaliza mazungumzo alijua lazima angekuwa na hasira na yeye kutokumuambia ukweli lakini hata hivyi asingejuwa namna ya kujitetea kama hajui ni lini ameweza kujua ukweli.
Roma hapohapo aliona majibu ayapate kuroka kwa Mage mwenyewe , muda ulikuwa umeenda lakini alijua lazima Mage atakuwa macho na kweli baada ya simu yake kuita muda mfupi ilipokelewa haraka.
"Babe Mage mbona kama ulikuwa ukisubiria simu yangu"
"Mh ..! Roma vipi kuhusu Edna"
"Edna ana nini?"
"Mama leo kaharibu kila kitu"
"Kaharibu nini??"
"Sijui kaongea nini na Mkeo ila kamwambia kuhusu sisi baada ya Magdalena kakataa mchumba anaetaka kumuoa...."
Kwa maelezo ya Mage ni kwamba mtoto wa waziri wa sayansi na teknolojia afahamikae kwa jina la Jumbe alifika nyumbani kwa Mage na kuweka nia yake wazi ya kutaka kumuoa Magdalena jambo ambalo lilipokelewa kwa mikono miwili na Mama T.
Mwanamama huyu alikuwa ashachoshwa kuona watoto wake wa kike wakikosa ndoa ilihali wakina mama ambao ni marafiki zake watoto wao walikuwa wakiolewa na kuoa kwa sherehe kubwa na yeye kuishia kutoa michango pekee.
Na kilichompa shida zaidi ni kila mara alipofikiria Mage hawezi kuolewa tena kwa kuamua kuwa mchepuko wa Roma jambo ambalo hata mume wake alilibariki hivyo tumaini lake kubwa ilikuwa ni kwa Magdalena.
Alielewa watu wakiona Mage hajaolewa wangemnyooshea vidole na kumsema lakini kwasababu ilikuwa ni kwa ajili ya furaha yake hakutaka kumzuia lakini jambo hilo hilo hakutaka kuona likitokea kwa Magdakena pia na ndio maana Jumbe alupoweka nia yake wazi ya kutaka kumuoa mtoto wake alipokea taarifa hio kwa mikono miwili.
Lakini sasa kilichomshangaza ni baada ya Magdakena kukataa akisema hawezi kuolewa na Jumbe kauli ambayo ilimfanya kuhisi uchizi.
"Magdalena kama humtaki Jumbe inamaana tayari una mchumba kama ni hivyo mlete tumuone na nikiridhika nae nitakuruhusu uolewe nae" Aliongea Mama na kumfanya Mage aliekuwa amekaa upamde wa kushoto kushindwa kuongea chochote na kumuonea huruma dada yake kwani alikuwa akijua kike kilichokuwa kikiendelea kwenye moyo wake.
"Mama sina mchumba ila sipo tayari kuolewa na Jumbe" Alijibu Magdalena na kumfanya Mama T kushindwa hata kuelewa watoto wake wamekumbwa na nini , kwenye maisha ykje alijitahidi kuwalea kimaadili na kutegemea waje kuolewa na kuwa na furaha kakini imegeuka kuwa tofauti .
"Mume wangu mbona huongei chochote jamani hawa watoto wanataka kunitia uchizi?"
Afande Tobwe alikosa cha kusema kabisa kwani alikuwa ashajua muda mrefu sababu ya Magdalena kukataa ndoa na Jumbe , alikumbuka vizuri siku ya Roma alipokuwa akipambana na Yan Buwen namna ambavyo Magdalena alitaka kumuokoa Roma kwa kujitoa Muhanga yeye mwenyewe uhai wake.
Kwanzia kipindi hiko alikuwa akishindwa kujua tatizo la Magdakena linaisha vipi , kwenye maisha yake licha ya kuwa mwanajeshi likija swala ka familia yake alikuwa akizingatia zaidi watoro wake waje kuishi na furaha na ndio maana hata Mage alipo onyesha kuwa na mapenzi na Roma hakusita kumruhusu licha ya kujua Roma ana mke tayari na mwanae angekwenda kuwa mchepuko tu, lakini swala la Magdalena ilikuwa ngumu kumruhusu kuwa na mahusiano na Roma na wakati huo na pacha wake akiwa na mahusiano na Roma.
Jambo hilo kama angeruhusu jamii isingemuelewa na sio hivyo ru hata dini yake ilimzuia kuruhusu kitu kama hiko.
"Magdalena kama huna mahusiano, Jumbe anakufaa usikatae , najua kwa zama za sasa wazazi hawapaswi kuwachaguliwa watoto wao wachumba lakii siku zote mzazi anamuombea mtoro wake kuwa na furaha hivyo kuelewa ni kipi bora kwako , Jumbe anakupenda hivyo hata kama humpendi utajifunza"Aliongea Afande Tobwe kwa usiriasi na kisha akaamka na kuondokaneneo hilo la sebuleni.
Huku nyuma akiacha sura ya Magdalena kuwa katika hali isioelezeka , alitarajia baba yake kumuunga mkono lakini akaishia kumkandamiza kwa.kusimama upande wa mama yake.
Wakati wa mchana Edna alipofika dukani kwa ajili ya kutafuatilia mwenendo wa mauzo ya mavazi alioingiza sokoni kupitia kampuni yake kwa kutumia malighafi mpya ndio alipokutana na Mama T.
Walikuwa hawajaonana muda mrefu tokea Edna asafiri kwa ajili ya harusi yake hivyo waliongea sana huku Mama T akitaka kuona Edna alipendezaje na katika mwendelezo wa stori ndipo Mama T alipojikuta akiropoka kuhusu mtoto wake Mage kuwa na mahusiano na Roma.
Mwanzoni Edna alihisi kuna kitu kinaendelea kati ya Mage na mume wake lakini alikosa ushahidi wa wazi wa kuthibitisha kile anachowazia.
******
Upande mwingine nchini Rwanda mheshimiwa Jeremy alikuwa akizunguka zunguka kwenye ofisi yake huku na huko akionyesha kama mtu mwenye hasira nyingi na hio yote ni mara baada ya kupata taarifa ambazo zilithibitisha Kizwe ndio ambaye alimtorosha Desmond hospitalini wiki kadhaa zilizopita.
Raisi Jeremy mara baada ya kumtoa Desmond Tanzania moja kwa moja alimsafirisha mpaka India kwa ajili ya matibabu , hakuwa akiamini maneno ya daktari wa Tanzania kwamba mtoto wake hawezi kupona kiungo chake cha uzazi na ndio maana alikuwa radhi kufanya lolote kwa ajili ya mtoto wake huyo na isitoshe ndio ambaye alikuwa ni mrithi wake akitaratjia siku za usoni kumwachia nchi aiendeshe , lakini akajiuliza kama Demsond hatokuwa na uanaume wake je angeweza kuendesha nchi kisawasawa na jibu lilikuwa hapana.
Upande wa Desmond mara baada ya kushituka katika kupoteza fahamu na kujua hakuwa na uwezo tena wa kumfanya chochote mwanamke wakiwa kitandani alilia sana na kuomboleza na maumivu yake yalikuwa ni zaidi ya siku aliopokea taarifa za kifo cha mama yake.
Mpaka muda huo alijiona hakuwa ni wa thamani tena kama mwanaume na ndio maana alijawa na huzuni isiokuwa ya kifani huku lawama zote akimwangushia baba yake mzazi ,kwani aliamini kama sio matendo yake basi huenda asingepatwa na kadhia hio.
Ilikuwa ni adhabu kubwa mno ambayo Roma alikuwa amemfanyia , ilikuwa ni zaidi ya kifo kwake na hakujiona wa thamani kabisa.
Hata pale raisi Jeremy alipomtembelea katika wodi aliolazwa hakutaka kumuona kabisa na alitangaza waziwazi kwamba anamchukia na hali ilio iliamsha sana huzuni kwa Raisi Jeremy ,hakujua ni kwa namna gani angemsaidia mtoto wake kupona kwani alishakuwa tayari Eunuch ,kwa mtazamo wake hata kama angetaka kulipiza kisasi kwa Roma asingeweza na pia ingekuwa laana kwake kushindana na mkwe wake.
Kuna muda aliona huenda matendo yake ndio yaliokuwa yakimfikisha katika hali kama hio, alikuwa na mafanikio katika uongozi wake lakini likija swala la familia alikuwa amefeli pakubwa na alijiona kama mtu ambaye hakuwa na bahati.
Madaktari wa kihindi walijitahidi kufanya juhudi za kila namna ili kumponyesha Desmond tatizo lake lakini majibu hayakuwa na tofauti sana na yale ambayo yalitolewa Tanzania.
Kwa ufupi ni kwamba mtoto wake hakuwa mwanaume mwenye makali tena , taarifa ambayo ilikuwa mbaya sana na kuishia kumlaani Roma kwa kumfanyia hivyo mtoto wake.
Wakati akiendelea kutafakari namna gani ya kumsaidia Desmond akiwa nchini India kwa siri, ndipo alipopokea taarifa za Desmond kutoweka hospitalini kwa hali isiokuwa ya kueleweka jambo ambalo lilimshangaza mno na sio kwake tu hata vitengo vya ulinzi vya hospitali vilishangazwa na jambo hilo kwani hakukuwa na Kamera yoyote ilionasa tukio la Desmond kutoroshwa na kitu kingine zaidi ni kwamba CCTV Kamera zote zilikuwa zikifanya kazi.
Kwa maelezo hayo mafupi alioyapata Raisi Jeremy alijua moja kwa moja Kizwe atakuwa anahusika katika hilo.
Tokea siku ambayo aliweza kupata taarifa za Kizwe kuwa hai kutoka kwa Linda ilimshangaza sana Raisi Jeremy kwani ilikuwa ni taarifa ambayo kwake ni kama anaambiwa mfu kafufuka , alishuhudia yeye mwenyewe kifo cha mke wake na kumuona akizikwa inakuwaje akawa hai.
Linda hata yeye mwenyewe alishindwa kuamini kama Kizwe alikuwa hai , aliweza kupata kuigundua sura ya Kizwe siku kadhaa wakiwa wanafanya uchunguzi ndani ya chuo cha taifa cha Rwanda mara baada ya Lekcha kupotea na walipoangalia kamera za Chuo ndio walipoweza kuona sura ya mwanamke anaefanana na Kizwe kabisa akiwa katika ujana.
Tena inasemekana wakati Kizwe anaondoka na Lekcha katika chuo hicho Kizwe aliangalia Kamera ya ulinzi na kisha akatabasamu kifedhuli na kutamka maneno kwa namna ya kuonyesha ishara za midomo yake, alifanya hivyo kama mtu ambaye aliamini kabisa Footage za sura yake zingemfikia Jeremy.
Katika rekodi hio ya camera Kizwe alikuwa akionyesha ishara kama ya kumtahadharisha Jeremy kwa kumwambia kwamba anarudi kulipiza kisasi.
Baada ya taarifa ya mwanamke anaefanana na Kizwe kumfikia raisi Jeremy kwanza kabisa hakuamini na aliweza kupitia hatua zote tano za mshituko ili kujibu hali ya taarifa hio na baada ya masaa mengi ya kufikiria ndio uamuzi wa kufukuliwa kaburi(exhumation) la Kizwe kwa siri sana ufanyike nyakati za usiku kazi ambayo iliongozwa na Linda.
Na ilichukua siku tatu kwa mchakato wote kumalizika na mara baada ya raisi Jeremy kuwekewa majibu mezani alijikuta akipagawa , mwili ambao ulifukiwa haukuwa wa mke wake Kizwe kwani vinasaba vilithibtisha hilo.
Sio kwake tu ambaye alishangazwa na hilo lakini hata Linda pia alishangaa na kutaka kuthibitisha hilo na hapo ndipo walipoanza kuwasiliana na wanasayansi na vitengo vya serikali nyingine ili kuweza kuthibitisha uwezekano wa mtu aliefariki kufufuka na katika majibu mengi ambayo walipokea moja wapo ni kesi ya siri sana iliomtokea raisi mstaafu wa China lakini kesi hio hio ikajirudia nchini Tanzania baada ya mwili mtoto wa tajiri wa makampuni ya Maya kuonekana akiwa hai mara baada ya kifo chake kuthibitishwa.
Taarifa zilikusanywa kwa kutumia idara za kitelijensia na zilipomfikia Raisi Jeremy ndipo alipotambua sasa jina la mwanasayansi Yan Buwen ambaye alikuwa amepewa hifadhi ya kufanya majaribio yake nchini Tanzania.
Intellijensia ya Rwanda iliweka kila kitu wazi na kweli Yan Buwen wakati wa maombolezo ya kifo cha Firsr lady alionekana kuingia nchini Rwanda , muunganiko huo wa matukio ndio ulikamilisha uchunguzi wa kuamini Kizwe alikuwa hai bado na aliehusika kumrudisha hai ni Yan Buwen.
Na Raisi Jeremy alijiona mjinga kwa kuona alizidiwa akili na mke wake na hata kitendo cha Lekcha kumbakisha hai ulikuwa pia ni mpango uliosukwa , hatari aliweza kuiona mbele yake na kuanza kumuogopa Mwanamke aliekuwa ni mke wake na hata ulinzi wake aliongeza maradufu huku akihakikisha Desmond mtoto wake hafahamu ukweli wowote kuhusu hilo.
Asichokijua raisi Jeremy ni kwamba Desmond ndio moja wapo ya watu walioshuhudia mama yake mzazi akifufuliwa na Yan Buwen na hata nyakati za maombolezo ya taifa alikuwa akijifanyisha tu kuwa na huzuni.
Baada ya kifo cha raisi Kigombola pamoja na Yan Buwen Raisi Jeremy alipata unafuu na safari yake ya kuhudhuria maziko ya raisi Kigombola ilikuwa na sababu ya ziada ambayo ni kuona uwezekano wowote ambao ungemkutanisha na mke wake.
Siku ambayo Fredi aliandaa Party ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa na Edna na Roma kualikwa ndio siku ambayo pia hata yeye mwenyewe aliweza kupokea ujumbe kutoka kwa Kizwe akimwambia afike Maple speed Resort kama anataka kuonana nae.
Lakini Kizwe hakuwa na mpango wa kuonana na Jeremy bali aliandaa mpango wa kumfanya Jeremy kushuhudia Kaka akimbaka mdogo wake kwa macho yake lakini kwa bahati mbaya mpango wake huo ukaja kufeli mara baada ya bangili aliovalishwa Edna kuingilia kati na matokeo yake ni Desmond kuharibiwa uanaume wake.
Sasa zikawa zimepita siku kadhaa tokea Desmond apotee nchini India huku akiamini moja kwa moja muhusika ni Kizwe ambaye amebadilika na kuwa wa tofauti sana , sio tu kwamba alikuwa amefufuka lakini pia akarudi ujana.
Asubuhi hio aliokuwa akizunguka katika ofisi yake ni mara baada ya Kizwe kumthibitishia Jeremy kwamba yupo na Desmond na ajiandae kuachia uongozi wa nchi , kauli ya Kizwe kwake ilikuwa kama ya vitisho na ndio maana alikuwa na hasira na kuzunguka huku na huko huku akikosa namna ya kumshughulikia mwanamke huyo ambaye muda huo hakumuona kama mke wake tena bali alimuona kama shetani.
Mbaya zaidi aliogopa kwa kuamini na Desmond atakuwa amejazwa ujinga na mama yake kwa wakati huo .
Ilikuwa kama laana kwake kwa baba wa familia kushindana na familia yake na jambo hilo lilimkosesha amani kabisa.
ITAENDELEA.
Bange lako hua unavutia wapi manake bange la chooni hua linarandua vibaya mno..Huwezi amini nimekutana Edna jamani bonge la pisi Kali alikuwa posta offisini kwake jamani mtoto mzuri
Jamaa anazingua mnooo katutelekeza mpaka kwenye group lake kule na tumelipia ana keraAsante chief kwaiyo hapa tusubirie baada ya miezi mingapi tena kwa muendelezo..
Kwa nini ulimlipa cash pasipo kuhakiki kama ni mzinguaji?Jamaa anazingua mnooo katutelekeza mpaka kwenye group lake kule na tumelipia ana kera
hapo umenena mzee, hata mimi uwa napenda kununua story ikiwa imekamilika. nalipa, unanipa mzigo tunamalizana. kuna jamaa mmoja alikuwa anauza story, nikajua imeikamilika! nikalipia; si nikashangaa katuma hadithi nusu. nikamuuliza, mzee mbona unatuma mzigo nusu?! akajibu, bado naandika. aliniboa mpaka leo. kwanza sipendi arosto, sasa nalipia na arosto juu, ni ujinga.Kwa nini ulimlipa cash pasipo kuhakiki kama ni mzinguaji?
Waandishi wote wa story nusu nusu huku wakikusanya hela ktk group huwa ni wezi tu.
Nikushauri tu uwe unalipia story iliyokamilika hapo utakuwa hujaibiwa.
Ni ujinga kabisa kulipia kitu ambacho hakijakamilika.sasa nalipia na arosto juu, ni ujinga.
Mkuu hata sioni msingi wa malalamishi yako maana kama ulifuata maelekezo niliotoa kule na umelipia kwanini ukose mwendelezo huku wengine wanaupataJamaa anazingua mnooo katutelekeza mpaka kwenye group lake kule na tumelipia ana kera
it's all about choices kwasababu maelezo yanajitosheleza mwenzako kalipia 2500 tu kusapoti juhudi huku akipata urahisi wa kupata mwendelezo huna haki ya kusema ni ujinga.Ni ujinga kabisa kulipia kitu ambacho hakijakamilika.
Labda kama Una magroup tofaut tofaut Ile nilipo mm unatuma mwendelezo kwa kujisikia mnooo na umefunga comment unadhani tutakwambiajeMkuu hata sioni msingi wa malalamishi yako maana kama ulifuata maelekezo niliotoa kule na umelipia kwanini ukose mwendelezo huku wengine wanaupata