Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 505
“Umepitia mengi sana katika siku hizi chache na ni makosa yangu kuwafanya wote kupitia maumivu makali na mateso , nakuahidi nitafanya kila kitu kuhakikisha kitu kama hiki hakitokei tena’Aliongea Roma akijitahidi kumfariji Mage.
“Alright … Kwahio tunafanya nini sasa hivi , tunarudi nyumbani?”Aliuliza Mage na kumfanya Roma kwanza ageukia mahema yaliokuwa hapo na kabla hajatoa jibu alijikuta akihisi nguvu ya ziada ikitoka kwenye moja wapo ya hema.
“Hii nguvu…”Roma alitaka kuongea na kisha akamgeukia Mage.
“Nifuate”Aliongea na kisha walienda kuingia kwenye hema ambalo lilikuwa katikati kabisa , ndio hema ambalo Roma aligundua linatoa msisimko wa nguvu ambayo haikuwa ya kawaida.
Mage alikuwa kwenye mshangao kwani hakujua kwanini Roma alionyesha kuwa na mchecheto , baada ya kuingia ndani ya hema hilo eneo la katikati kulikuwa na kreti kubwa la mbao ya Mwaloni(oakwood), lilikuwa ni kreti ambalo lina urefu wa makadirio ya zaidi ya mita moja upana na urefu wake na ndio pekee ambalo lilikuwa kubwa ndani ya hema hilo.
“Hubby unajaribu kuangalia nini kwenye hilo Kreti”Aliuliza Mage kwa shauku kwani namna ambavyo Roma analifungua ni kama kuna kitu alikuwa akifahamu kipo ndani yake.
“Kama hisia zangu zipo sahihi , hiki ndio kitu ambacho nilikuwa nikitafuta sana muda wote”Aliongea
“Huh..?”Mage alionekana kuchanganyikiwa
Na muda huo huo Roma alifanikisha kubanjua loki ya kreti hilo kwa mkono mmoja na kutoa karatasi ya juu na kufanya kilichomo ndani kuonekana.
Mbele yao kulionekana Cauldron ya shaba (Sufuria kubwa au jungu la shaba), kaika kuta za Cauldron kulikuwa na naksi za kisanifu za bamba ambazo zimechorwa kama mchoro na wembamba sana kama vile ni uzi wa hariri.
Cauldron ya Shaba ilionyesha kushinda jaribio la muda kwa namna ambavyo kutu yake haikuwa ya kiwango kikubwa , lilikuwa kama sufuria kubwa la chuma kigumu ambalo kwa kuangalia tu lilistaajabisha na heunda ungejiuliza matumizi yake ni yapi.
“Kwasababu wakati nafika hapa nilikuwa nimepoteza uwezo wangu ndio maana nilishindwa kugundua uwepo wake , kwa nje unaweza kuona ni lisufuria tu la chuma lakini linatoa nguvu isiokuwa ya kawaida”Aliongea Roma kumwelezesha Mage ambaye alikuwa akishangaa shangaa.
“Kama nitakuwa sahihi katika kuotea basi naamini hiki ndio kitu ambacho Rufi aliniambia nitafute , chombo ambacho kina uwezo wa kuhimili moto mweupe na wa njano”Aliongea Roma na kumfanya Mage kushangaa ,tokea ajifunze mbinu za kijini maneno kama hayo hayakumchanganya kabisa.
“Kwa maana hii naamini ndio maana tulitaka kufa , kumbe kuna kitu cha thamani kilikuwepo karibu yetu”Aliongea Mage.
“Hata wewe umegundua hilo?”
“Ndio na kama ulivyosema ni sahihi basi tunaweza kusema misheni yetu imetimia”
“Lakini sina uhakika wa asilimia mia moja kama ndio kitu chenyewe ambacyo Rufi alikuwa akizungumzia , inabidi athibitishe mara baada ya kupona, kwasasa nitatafuta watu waje kukibeba na kukipeleka makao makuu”
“Unamaanisha nini kusema makao makuu?”Aliuliza na kumfanya Roma kuanza kuelezea kuhusu visiwa vya wafu na mpaka anamaliza ndio sasa Mage alipoelewa ndio mahali ambapo ndoa yake na Edna ilifanyika na aliikuta akionyesha hali kidogo ya huzuni.
“Usiwe hivyo niliwaalika lakini mkaamua kutohudhuria na isitoshe kama siku mkitaka kwenda nitawapeleka”
“Kwanini tusiende nacho Tanzania?”
“Tungefanya hivyo lakini mtu alievaa maski alienishambulia na mtu mwingine mwenye nguvu sana alienisaidia wote bado taarifa zao hatuna , kama wameweza kuja Australia basi inamaanisha kwamba na nyumbani itakuwa ni hatari zaidi, kama tutakipoteza hiki basi itakuwa hasara kwa maumivu yote tuliopitia”Aliongea Roma na kumfanya sasa Mage kuelewa.
Baada ya kukagua baadhi ya vitu vingine na kuona havikuwa sana na maana kwao waliacha na Roma alifanya mawasiliano na Makedoni kutuma maveterans kuja kuchukua mzigo wake na vitu vyote ambavyo vipo hapo ,ma vinavyohusiana na serikali ya China virudishwe kwa wahusika na ambavyo havikuwahusu vikahifadhiwe visiwa vya wafu.
Sababu ambayo Roma hakutaka kumtaarifu Sauroni kuleta wanajeshi wa The Eagles ni kutokana na kwamba vitu vya hapo vilikuwa na thamani kubwa na asilimia kubwa ya wanajeshi wake hawakuwa na uelewa navyo , hivyo kwa kutumia watu wa Mossad wenye ujasiri ingekuwa rahisi zaidi na salama , kwani kwa haraka haraka mizigo yote hapo huenda thamani yake ni dola bilioni moja.
Kuhusu Cauldron alipanga kwanza ikahifadhiwe kwenye ngome yake katika visiwa vya wafu mpaka atakapo fanya maamuzi mengine.
Baada ya kufanya mawasiliano Roma moja kwa moja alimchukua Mage na kumrudhiisha mjini na akampandisha kwenye ndege kuelekea Tanzania na baada ya ndege kupaa yeye aliondoka Australia na akarudi tena London kwa ajili ya Rufi.
Roma baada ya kufika ndani ya hospitali ya St mary’s alipewa maelekezo ya wodi aliopo Rufi , alikuwa alishatolewa muda tu kwenye wodi ya uangalizi wa karibu na kupelekwa katika wodi ya VIP.
Roma mara baada ya kufungua mlango aliweza kumuona, na sasa alionekana kurudiwa na fahamu na hata ule urembo wake kumrudia.
“Hey .. usinyanyuke utaumiza majeraha yako , kwanini unahangaika kama unakutana na raisi”Aliongea Roma mara baada ya Rufi kujitahidi kuamka haraka kiuoga woga mara baada ya kumuona Roma.
“Nilisikia ulinileta ndani ya hii hospitali usiku manane , na ukamleta daktari bingwa namba moja duniani kunitibu , nataka nikushukuru..”Aliongea kwa wasiwasi kama vile Roma alikuwa mgeni kwake.
“Kuna kipi cha kunishukuru sasa , hilo ndio jambo ambalo nilipaswa kufanya”Aliongea Roma kwa sauti ya chini na kumfanya Rufi kugnudua mabadiliko ya sauti yake tofauti na alivyokuwa akimwongelesha siku kadhaa zilizopita , sauti hio ilikuwa ni ya kujali.
“Vipi uko sawa?”Aliuliza Rufi. na kumfanya Roma ashindwe kujibu swali hilo mara moja maana aliona yeye ndio ambaye alipaswa kuuliza , alijikuta hisia mchanganyiko ziki uvaa moyo wake.
Ijapokuwa Roma alimsaidia kupona kwake kwa kumleta ndani ya hospitali hio , lakini kile alichokifanya kwa ajili yake na Mage ni jambo la kijasiri ambalo mtu yoyote asingeweza kufanya , Rufi alijitolea kupigwa risasi ili kuruhusu wao wasiweze kushambuliwa.
“Kwahio nini kiliokea baada ya hapo?”Aliuliza baada ya kumuona Roma amepiga kimya.
Na Roma alishituka na kuanza kumwelezea namna ambavyo amefanikisha kupata Cauldroni iliotengenezwa kwa madini ya shaba na kumfanya kushangaa.
“Lakini haikupaswa kuwa ya shaba , kama kuna nguvu ndani yake basi nina uhakika ilitumika kutengenezea vidonge na makadirio yangu kama yatakuwa sahihi huenda ina mwonekano wa rangi ya shaba kwasababu kimeishi muda mrefu sana , nina uhakika hakukuwa na teknolojia kubwa yakutengeneza jungu kubwa la kijini namna hio kwa kutumia shaba kwani teknolojia ilikuwa bado ndogo”Aliongea.
Cauldron ni Artifact ambayo ilitegenezwa miaka mingi sana iliopita huenda ziaid ya miaka elfu mbili, sasa kwa ukubwa wake ilikuwa ngumu kuamini kwamba kuna watu duniani waliotengeneza Cauldron ya madini ya shaba kwa ukubwa huo , kwani teknolojia ya kipindi hiko ilikuwa ndogo mno.,
“Kwasasa usiwe na wasiwasi sana , ukishapona nitakupeleka ili ukaone na kuthibitisha”Aliongea Roma na mara baada ya kumaliza alichaneli nguvu ya andiko ya urejesho katika mwili wa Rufi ili kumrahisishia kumponyesha majeraha ya nje ya mshono wake.
“Kwasasa nipo sawa , nadhani ni muda wako sasa wa kurejea Tanzania , naamini familia yako itakuwa na wasiwasi kwani tuliondoka muda mrefu”Aliongea Rufi na maneno yake yalimfanya Roma kweli kukumbuka nyumbani ,alimkumbuka sana mke wake na mtoto wake lakini pia pamoja na mama yake mzazi.
Roma alifanya maamuzi ya haraka na kisha akamwambia Rufi kupumzika hapo hoospitalini angalau kwa wiki mbili na ndipo angerudi kumchukua na kumrudisha Tanzania.
Roma hakutumia ndege tena kurudi nyumbani na isitoshe hakujisumbua hata kubadilisha mavazi hivyo moja kwa moja aliondoka Uingereza kwa mavazi yale yale ambavyo yalikuwa yamechafuka na damu, slijiambia ataoga akishafika.
Tanzania ilikuwa ni asubuhi ya siku ya ijumaa wiki mbili tokea Roma kuondoka , ndani ya nyumba yake alionekana Edna ambaye alikuwa hajavaa chochoe miguuni licha ya kuonekana na mavazi ya kutokea akifukuzana na Lanlan huku akiwa ameshikilia sweta mkononi.
“Lanlan if you don’t come over mummy gonna be really mad, come on”
“Lanlan usipokuja hapa mama atakasirika , njoo haraka?”Aliongea Edna akimwangalia Lanlan ambaye amevalia sare za shule bila ya sweta , sasa Edna alikuwa akitaka kumvalisha sweta lakini Lanlan hataki.
“No! Lanlan hates that , no more clothes it’s warm”Aliongea kimaanisha kwamba anachukia sweta na hataki nguo nyingine kwani kuna joto.
Kwasababbu ilikuwa ni asubuhi Edna aliona Lanlan anapaswa kuvaa sweta , lakini upande wa Lanlan kutokana na mwili wake ulivyo hakuhitaji sweta.
“Lanlan acha kuwa mbishi na nisikilize mama yako kama unataka watoto wengine wakupende”
“Kama ni hivyo Lanlan haendi shule na nitasubiri mpaka baridi iishe”Aliongea na kumfanya Edna ashindwe kujua cha kufanya alikuwa akitamani kumfokea lakini hakutaka kumfanya anune asubuhi asubuhi kwani alikuwa akimlea kama yai.
“Edna mwache avae hivyo hivyo kama hataki hilo sweta”Aliongea Blandina ambaye alikuwa akitokea nje.
Wakati Roma anaondoka Blandina alikuwa nyumbani kwao na sasa kwasababu baba yake mzazi alishafariki asingeweza kukaa katika nyumba ya Tajiri Azizi, ukiachana na hela alizovuna akiwa mke wa raisi. lakini pia katika urithi alipokea asilimia nyingi sana za hisa ambazo mmiliki wake alikuwa baba yake katika makampuni ambayo yanaongozwa na tairi Azizi hivyo angeweza kuishi mahali popote pale , lakini alishindwa kufanya hvyo kwani angeenda kuwa mpweke , hivyo mahali sahihi ilikuwa ni nyumbani kwa mtoto wake Roma.
“Lakini mama muda huu ni asubuhi na kuna baridi , nina wasiwasi anaweza akashikwa na shida ya kifua”
“Mh..!, Edna haina haja ya kumchukulia Lanlan kama mtoto wa kawaida ili hali sio wa kawaida , hata asipovaa hilo sweta na hali ya hewa ya jiji hawezi kupatwa na shida yoyote”Aliongea na Edna aliona amsikilize mama mkwe.
Muda huo huo wakati wakiongea upande wa nje ndio Roma alikuwa akifika , akiwa na mavazi yake yaleyale yaliochafuka na kugandiana damu.
“Son, kwanini unaonekana hivyo?”Aliongea Blandina kwa mshangao mara baada ya Roma kuingia ndani, Edna na yeye baada ya kumuona Roma akiwa na madoa doa alijikuta akikunja sura.
“Hio ni damu kwenye shati lako?”Aliuliza lakini alijikuta akijawa na aibu mara baada ya kufanyiwa kitendo ambacho hakukitegemea , Roma alimsogelea bila ya kumjibu na kumkumbatia.
Alijikuta akitaka kutoa ukulele kutokana na harufu mchanganyiko iliokuwa ikimtoka Roma iliochanganyika na harufu ya msituni baharini na damu.
“Mwaah..!! babe wife nimerudi”Aliongea Roma bila aibu pasipo ya kujali mama yake yupo kwani haikuwa kumkumbatia tu bali mpaka kumpiga busu la shavuni.
“Ni vyema umerudi , lakini kwanini unataka kuniua kwa kunikosesha pumzi asubuhi asubuhi?”Aliuliza Edna huku akijiangalia mavazi yake ambayo tayari alikuwa na mpango wa kuyatumia siku hio.
“Hehe.. nimefurahi kuwaona wote ni wazima wa afya”Aliongea Roma huku akimsogelea Lanlan kumshika lakini alimkimbia.
“Chubby unamkimbiaje baba yako wakati ndio amerudi?”
“Bad daddy , My name is not chubby”Aliongea na kumfanya Roma kutamani kucheka , alidhania Lanlana alishazoea jina lake la utani kumbe bado.
Roma hakutaka kubakia hapo zaidi , baada ya kumsalimia na mama yake pamoja na Bi Wena na Qiang Xi alianza kupandisha juu lakini aliishai katikati na kugeuka nyuma.
“Wife unaonaje ukaja kunisugua mgongo?”
“Screw you!!’(Kwenda huko)Aliongea Edna kijeuri akionyesha hayupo tayari na kuwafanya wengine kuangaliana na kujiuliza kuna nini kinaendelea maana Edna bado alionyesha kutokuwa kwenye hali ya kawaida ya kufurahia mume kurudi.
“Blandina unafikiri nini kimemtokea?”Aliuliza Bi Wema kwa wasiwasi na kumfanya Blandina kuwaza kidogo.
“Nashindwa kufahamu, lakini kama kuna tatizo ambalo limewatokea wengine alioambatana nao nadhani asingeweza kurudi nyumbanni mapema , hisia zangu zinaniambia kuna kitu amefanya akiwa mbali na nyumbani”
Edna yeye hakujali, kwanza nguo zake muda huo ni kama zimechafuliwa na alitaka kutoka nazo , hivyo alipandisha juu kwa ajili ya kuzibadilisha na wakati akibadilisha mawazo ya kumpeleka Lanlan siku hio shule yalikatika na kujiambia bora ampigie simu mwalimu wake kumwombea ruhusa ili akae chini apate kusikiliza nini kimemtokea Roma mpaka akarudi na damu kwenye nguo zake.
Baada ya Roma kuoga vizuri na kubadili mavazi hatimae aliweza kushuka chini akiwa anasubiriwa na watu waliojawa na shauku kubwa ya kumsikiliza kile ambacho kimetokea na safari yake kwa ujumla imekuwaje.
Roma mara baada ya kuketi alianza kuelezea hatua moja moja namna ambavyo waliweza kufika msitu wa Arnhem , namna ambavyo walishambuliwa na mtu asiejulikana na kumpelekea kupoteza uwezo wake kwa muda na mpaka waliposhambuliwa na kundi la masenari wa kundi la Hydralisk mpaka kupelekea Rufi kupigwa risasi.
Ijapokuwa alionekana kueleezea kwa sauti ya kawaida kama mtu ambaye anachukulia kilichotokea kawaida , lakini kila mmoja alishangazwa na kadhia waliopitia.
Katika stori nzima kila mmoja aliweza kumkubali Rufi kwa namna ambavyo alijitahidi kujitolea kulinda wengine.
“Huyu msichana Rufi ni mwenye roho nzuri sana , kama sio yeye huenda wewe au Mage mngepatwa na matatiz”Aliongea Blandina kwa wasiwasi.
“Nakubaliana na wewe , hata mimi siku ya kwanza kumuona amefika hapa nyumbani nilishamuona ni msichana mzuri sana mwenye ujasiri”Aliongea Bi Wema huku akimwangalia Edna kwa tahadhari.
“Roma unaonaje akishapona umualike nyumbani ili angalau tuweze kupata nae chakula na kumfahamu zaidi , Edna unaonaje juu ya hilo?”
Edna hata yeye aliguswa na ujasiri wa Rufi lakini kwa namna ambavyo Blandina alionekana kumkubali ilimfanya kupata ukakasi kidogo.
Kitendo cha Rufi kujitolea kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya Roma na Mage haikuwa cha kawaida na kilimfanya Edna ashindwe kukataa pendekezo lililotolewa, hata hivyo angekataa isingekuwa na maana kwani alijua ukiburi wa Roma akiwa ameamua la kwake kichwani.
“Okey mama hakuna tatizo”Aliishia kujibu Edna na mpango ukawa ni Rufi kukaribishwa nyumbani kwa ajili ya kupata chakula na familia ya Roma.
Je Bi Wema ndio siku ya kumfahamu Rufi kama mtoto wake?












SEHEMU YA 506.
SEOUL-REPUBLIC OF KOREA
Jumba la kifahari la wamiliki wa kampuni kubwa ya Starmoon , familia ya Park ilikuwa ni kielelezo tosha cha kuonyesha utajiri wao ndani ya eneo lote la Gangnam ndani ya jiji la Seoul nchini Korea kusini.
Familia ya Park ilikuwa ndio moja wapo ya familia ambazo zimefanya vizuri sana katika maswala ya uwekezaji katika bara la Asia lote , hususanni kwa mzee mwenyewe mmiliki.
CEO Park Juan alikuuwa shujaa ambaye mafanikio yake yanatazamwa kwa jicho la kipekee zaidi kwa mchango wake alioufanya katika ukuaji wa uchumi wa Korea kusini.
Lakini wahenga wanasema kifo hakimsubiri mtu na hili ndio jambo kubwa ambalo lilikuwa likienea kwa kasi ndani ya jamii za kitajiri(Chaebol) mara baada ya familia kuweka wazi juu ya Park Kuan mwenyekiti na raisi wa makampuni ya Starmoon kuwa na ugonjwa wa saratanni ya ini.
Tajiri akifariki au pale anapokumbwa na ugonjwa ambao utampelekea kifo ndani ya muda mchache wengi hawatozungumzia kifo wala ugonjwa na hilo ndio jambo ambalo lilikuwa likiendelea.
Habari kubwa ilikuwa ni nani ambaye anakwenda kurithi kampuni ya mabilioni ya tajiri huyo mara baada ya kufariki kwake , kwani kwa hali ambayo alikuwa nayo wengi waliamini asingechukua muda mrefu kuendelea kuishi.
Waandishi wa habari na watu ambao walikuwa wakipendelea sana kufatilia habari za kibiashara walikuwa wakitoa michanganuo yao na uchambuzi wa kila mwanafamilia na asilimia zake katika kurithi kampuni.
Katika majina ambayo yalikuwa yakizungumziwa yalijumuisha mtoto wa pili wa tajiri huyo aliefahamika kwa jina la Park Jiki , mtoto wake wa kike afahamikae kwa jina la Park Jiyeon na mtoto wake mwingine wa kumlea afahamikae kwa jina la Park Jonghyun.
Kitu ambacho kila mmoja hakuweza kufahamu wala kuotea ni pale Park Juani kuagiza mtu kwenda mpaka nchini Tanzania kwa ajili ya kumrudisha nyumbani mjukuu wake wa mtoto wake wa kwanza.
Wengi wao bara baada ya kupata habari hio waliona kuruhusiwa kwa mtoto ambaye amekaa sana nje ya taifa la Korea kurithi kampuni kubwa kama hio ni jambo ambalo haliwezekani na hata kama maamuzi kama hayo yatafanyika basi ni ya kijinga. lakini hata hivyo hakuna ambaye alikuwa akijua ni maamuzi gani ya mwisho mwisho ambayo Park Juan angefanya kuhusiana na mtu ambaye angefaa kumrithi, hivyo habari nyingi zilikuwa za makisio kutokana na uadifu wa kila mwanafamilia.
Unajua katika mataifa yalioendelea kuendesha kampuni sio swala la kuamka na kwenda kazini tu , hasa kwa kampunni kubwa kama Starmoon, swala la Park Juan kuwa mgonjwa lilikuwa jambo la kufatiliwa na wengi kwasababu kuu moja, kampuni ya Starmoon ni public company na ina raia wengi ambao wamewekeza hisa zao na ili siku zote waendelee kupata faida lazima wajue kila kitu kinachoendelea si ndani ya kampuni tu lakini mpaka ndani ya familia.
Wananchi wa mataifa yalioendelea kama Korea wengi wao elimu yao ni ya viwango vya juu na si ajabu kumkuta mwanamke wa miaka themanini akifuatilia maswala ya uchumi wa kampuni flani ndani ya taifa ili kuwekeza.
Sasa ndani ya jumba la kifahari la familia ya Park katika chumba kikubwa kilichokuwa floor ya tatu juu kabisa alionekana mwanamke wa kikorea mzuri wa wastani , kijana kiasi alievalia mavazi ya ukijakazi akiingia ndani ya chumba upande wa kushoto.
Kilikuwa ni chumba kikubwa mno ambacho kimepambwa kwa mapambo ya kileo yalioendana na mpangilio wa thamani za gharama kwanzia chini mpaka juu darini, kilikuwa mpaka na hadubini katikati ambayo hutumika kwa ajili ya kuangalia nyota.
Yule kijakazi mara baada ya kuingia alionyesha heshima kwa kuinamisha kichwa chake mbele ya kitanda kikubwa cha sita kwa sita ambacho kimewekwa eneo la katikati ya chumba na juu yake alionekana msichana aliejilaza kivivu kwenye kitanda.
Ni msichana alievalia mavazi ya kulalia yenye vidoti doti vya rangi ya pinki na nyekundu na kwa staili aliolala alionyesha kabisa hana mpango wa kuamka licha ya muda kuonyesha umeenda sana tokea kulivyokucha.
“Miss Yezi kifungua kinywa kipo tayari , tafadhari naomba uamke, kama utaendelea kulala utachelewa kwenda darasani”Aliongea kwa kikorea huku akichanganya na kingereza na Yezi aliekuwa amelala alimsikia vizuri tu lakini hakufumbua macho.
Kwa kipindi chote ambacho alikaa Korea alikuwa ashaanza kuelewa kikorea licha ya kwamba mdomo ulikuwa mzito kuzungumza.
Tokea alipofika Korea aliweza kutafutiwa mwalimu ambaye si tu alimfundisha kikorea lakini pia alimfundisha na lugha ya kingereza rasmi.
Yezi alikuwa akiandaliwa kwa aili ya kurithi kampuni kubwa ya Starmoon hivyo ilikuwa ni mantiki kuweza kuelewa vizuri kingereza na Kikorea, yale maisha yake aliozoea nchini Tanzania yalibadilika kwa kiwango kikubwa sana kwani kila akiamka alikuwa amepangiwa ratiba ya kufanya hiki na kile mpaka jua linapozama.
“Eunjung nimechoka naomba uniache nilale kidogo”Aliongea Yezi
“Young miss!!, Mwalimu Vivian ametoa taarifa kwamba jana hukumaliza ratiba yako yote ya mafunzo na kaniambia kama utaendelea kuwa hivi atampigia simu CEO na wewe mwenyewe unaelewa tokea urudi CEO afya yake imeimarika sana na hata siku ya jana amefanikisha kutembea mwenyewe umbali mrefu na hata daktari amesema kwasasa ugonjwa wake utategemea na hisia zake , hivyo kama atasikia taarifa za utoro wako na kulala muda wote naamini atakasirishwa sana na tabia yako”Aliongea mwanadada aliefahamika kwa jina la Eunjung na kauli yake ilimfanya Yezi kushikwa na hairia na kisha kujinyanyua kutoka kitandani.
Alionekana kupendeza zaidi na zaidi kuliko alivyokuwa Tanzania , ijapokuwa mwili wake ulionyesha dalili za kukonda lakini aliimarika katika mambo mengi.
“Nadhani kwasasa unajua kwanini nakuita muuaji mwenye tabasamu, kila siku unaniamsha kwa kunitafutia sababu ya kunifanya nijione ni mwenye hatia”
“Hapana Miss , sio hivyo , mimi ni kijakazi tu wa hapa na najitahidi kutimiza majukumu yangu , sikutaka tu kukuona ukiendelea kumsubirisha mwalimu wako Vivian nadhani unajua hasira zake za karibu”Baada ya kukumbuka ukali wa mwalimu wake alijikuta akianza kuharakisha mambo.
Wakati anarudishwa Korea kwa ajili ya kuonana na babu yake ambaye alikuwa na kinyongo nae kadri siku zilivyosogea hatimae sasa taratibu alianza kujiona kama mwanafamilia.
Na kwasababu hio familia ya Park ni kama familia za kitajiri nyingi ambazo zilikuwa na sheria kali, na kwa mtoto kama Yezi alipaswa kuzifuatisha, kwaYezi ilikuwa ni lazima zaidi ili kumfanya kuweza kufahamu zaidi tamaduni za kikorea , hivyo kwa maneno marahisi alikuwa na mengi ya kujifunza na ndio maana Park Juan alihakikisha Yezi anapata mwalimu mzuri
Na hapo ndipo alipokuja kuajiriwa mwalimu ambae ana Advanced Diploma ya lugha na fedha , ambaye ana uwezo wa kuzungumza lugha tatu , Kiswahili , Kingereza na kikorea., alikuwa ni mwalimu wa kike mpole mrembo sana aliefahamika kwa jina la Vivian.
Na kwa kile alichokifahamu Rufi ni kwamba mwalimu wake ni msomi kutoka chuo maarufu duniani cha Harvard na jambo la kushangaza zaidi kuhusu mwalimu wake ni kwamba alikuwa amezaliwa nchini Tanzania , akakulia nchini Tanzania na ndipo alipoenda masomoni Harvard na kupata ajira nchini Korea.
Mwalimu Vivian kutokana na tabia yake ya ukali na usiriasi ilimfanya kupata pointi za kutosha kutoka kwa babuu yake Yezi na kuona ni mtu sahihi ambaye anaweza akamfundisha Yezi.
Mwanzoni Yezi alionyesha kuwa na furaha mara baada ya kufahamiana na mwalimu Vivian kutokana na kwamba alikuwa mbongo lakini mara baada ya masomo kuanza ndipo alianza kumchoka kutokana na ukali wake linapokuja swala la kujifunza lugha na maswala ya uongozi wa biashara.
Baada ya kujisafisha kwa haraka ili kumuwahi mwalimu Vivian , alivaa nguo zake safi na kisha akavuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha akamfuana Eunjung kwenda chini.
Nyumba hio kubwa hakuna mtoto wa Park Juan anaeishi kwani wote walikuwa wakubwa na ni wenye familia zao , hivyo mwanafamilia pekee aliebaki ni Park Juan yeye mwenyewe pamoja na Yezi mara baada ya kurudi.
Wakati huo upande wa eneo la chini sebuleni alionekana mwanamke alievalia Blazer ya rangi nyeusi , ambaye ana nywele ndefu alizofunga nyuma na kibanio, hakuwa mkorea bali alikuwa mwafrika wa rangi nyeupe ambayo imefifia , huenda kutokana na hali ya hewa ya ubaridi ya jiji la Seoul kwa nyakati hizo.
Alikuwa amekaa kwa kujiamini sana akiwa amekunja nne na mkononi alikuwa ameshikilia jarida flani la maswala ya uchumi na siasa akipitia pitia.
Baada ya kusikia vishindo vya hatua kutoka juu , aliizungusha shingo yake na kugeuka na kisha akatoa tabasamu la kupendezesha sana uso wake uliojaa haiba ya upole , uzuri wa huyo mwanadada huenda angekuwepo tanzania angekuwa habari ya mjini na kilichombeba si tu kwamba alikuwa mzuri wa sura lakini pia alionekana kuwa na mapozi ya watu waliostaarabika.
“Yezi kwasababu umelala kwa muda mrefu leo , nitahakikisha masomo yetu ya leo tunayafidia na muda wako wa mapumziko”Aliongea kwa sauti yake tamu ambayo iliharibiwa na matamshi ya lugha ya kikorea.
“Mwalimu Vivian naomba tupunguze spidi , kwa staili hio nitachoka sana”Alilalamika Yezi.
“Sio kuchoka ila wewe ni mtoro na fanya haraka upate kifungua kinywa na kisha tuendelee na kujifunza kingereza kuanzia pale tulipoishia siku ya jana na baada ya hapo nitakupa zoezi la kufanya”Aliongea na Yezi ashamjua hivyo hakuitikia zaidi ya kukaa kwenye meza na kuangalia vyakula mbalimbali vilivyoandaliwa kwa ajili yake tu, hakuwa yule Yezi tena mkaanga chipsi au Yatima huyu alikuwa Yezi mwingine ambaye huenda Tanzania angebatizwa jina la mtoto wa kishua.
Yezi alikunywa kiasi cha supu akijua sio ya moto na alijikuta akiitema chini na kuichafua kwenye nguo zake na kuanza kujifuta na mkono.
“Usijifute na mkono tumia tishu”Alifoka Vivian.
“Kwanini unakula pasipo kujali ustaarabu, mpaka sasa unatakiwa kuelewa utakuwa na vikao vingi baada ya kupewa kampuni pamoja na kuhudhuria matukio mengi na watu wazito wazito hivyo kila unachokifanya lazima kionyeshe namna gani umestaarabika”Aliongea Vivian kwa kuelekeza.
Eujung hakuingilia, alikuwa kimya akimwangalia Yezi aliekuwa akihangaika kutafuta napkin na palepale alimpa ishara kijakazi mwingine aliesimama kwenye meza ili kumpatia Yezi tishue ajifute.
Yaani licha ya kwamba alikuwa akila mwenyewe lakini wadada warembo vijakazi wa nyumba hio walikuwa wamejipanga msururu wakimwangalia namna ambavyo alikuwa akila chakula, na huo ndio utaratibu wa familia nyingi za kitajiri ndani ya Korea , wakati wanafamilia wakipata chakula wafanyakazi hata kumi utakuta wamejipanga mstari wakiwaangalia wanakula ili ikitokea wanahitaji kitu waweze kuwahudumia kwa haraka.
“Mwalimu Viviani wote sisi tumezaliwa Bongo , haina haja ya kuwa mkali kiasi hicho , yale maisha ya uswahilini unaelewa wewe mwenyewe , halafu ukiendelea kukasirika sura yako inakunjamana na utapoteza urembo wako ohoo…”Aliongea kwa kiswahili kile kile cha kitanzania kabisa na kuwafanya wahudumu wasimwelewe ameongea nini lakini kwa Vivian alielewa kila kitu.
“Sio kama nakuwa mkali ila nakuelekeza namna ya kuwa mstaarabu , sitaki watu waanze kukuzungumzia vibaya kama moja ya watoto wa familia ya Park na kuanza kusema taifa langu vibaya na isitoshe walionipa kazi ya kukufunza wana mategemeo makubwa juu yangu”
“Sura ya kimalaika lakini roho ya kishetani”Aliongea Yezi chini chini ili Viviani asimsikie.
“Nasikia maneno yako ya kunilaani , halafu nikukumbushe mara nyingine usitumie lugha ya kiswahili mbele yangu , ni kingereza na kikorea ndio lugha unazopaswa kuzungumza ili ulimi wako uwe mlaini.
“Sawa nimekuelewa mwalimu, lakini naomba nikuulize swali?”
“Uliza?”
“Umekaa kwa muda gani Marekani?”Aliuliza Yezi.
“Mh.. nadhani kama miezi sita kwenda saba hivi”Aliongea.
“Miezi sita , Wow!! inaonekana una uwezo mkubwa, umeweza kujifunza kuongea kingereza fasaha ndani ya miezi sita na kupewa cheti cha heshima?”Aliongea na akamfanya Vivian kucheka kidogo na kisha akaongea.
“Wakati nilipokuwa Tanzania nilikuwa nikisomea mtandaoni na nilichukua kozi nyingi za lugha ya kingereza na Kikorea na Harvard nilienda kupata kutambulika kitaaluma tu”Aliongea.
“Lakini bado upo juu na hata kama utamuuliza babu kuhusu wewe ni dhahiri atakuwa na mawazo sawa na ya kwangu”Aliongea Yezi akijaribu kumpamba pamba mwalimu wake.
“Unafikiri unaweza kunifanya nipunguze ukali kwa kunipamba?”
“Ah,,! kwanza mwalimu Vivian nina maswali mengi juu yako na mpaka sasa nashangaa kwanini umeamua kuwa mwalimu , kwa mwonekano wako wa kirembo naamini kuna wanaume wengi mabachela ambao wangeweza kukuoa , kwanini unapoteza ujana wako kwa kuwa mwalimu wa mtoto mtukutu kama mimi?”
“Yezi malizia muda unasonga , unapaswa kuelewa mimi kuwepo hapa kukufundisha nipo field niliopewa na profesa wangu na nikikamilisha mafunzo yako kwa kupata uzoefu narudi Marekani kuendelea na masomo yangu ya Masters , kwahio usinipe wakati mgumu wa mimi pia kukamilisha kazi yangu”
“Masters?Mwalimu Vivian nakushauri usijifanye hivyo ni kupoteza muda kama mwanamke , wewe ni mrembo na ni rahisi kuolewa na mwanaume aliefanikiwa na ukayafurahia maisha yako”
“Wewe mtukutu mwenye maneno mengi , umekazania mwanaume mwanaume , mimi kwangu kwasasa nachagua masomo kuliko mwanaume”Aliongea huku akimzodoa.
“Acha kunifanyia hivyo mimi sio mtoto?”
“Katika macho yangu wewe ni mtoto tu”Aliongea na kumfanya Yezi kutoa ulimi wake nje akimchokoza mwalimuwa wake.
“Lakini bado mwalimu Vivian mimi sikuelewi, kwahio mpaka muda huu huna hata mpenzi kama hutaki ndoa?”
“Hakika sina mpenzi na sitafuti kuwa na mpenzi wala ndoa?”Aliongea Vivian huku akionyesha kukunja sura na kwa jinsi anavyoongea ni kama wale wanawake ambao wameumizwa kwenye mahusiano.
Unganisha doti imfahamu Vivian ni nani…
ITAENDELEA
Vivian = Najma, why kabadilisha jina, tutajua huko mbele[emoji3][emoji3][emoji3]
 
it's all about choices kwasababu maelezo yanajitosheleza mwenzako kalipia 2500 tu kusapoti juhudi huku akipata urahisi wa kupata mwendelezo huna haki ya kusema ni ujinga.
Endelea kusubiri mwendelezo hapa wanaotusapoti kwa kidogo wataendelea kufanya hivyo
Hao wanalalamika huko kwa group kuwa unazingua.

Wamekuamini wakajuinga na group ila unawaacha na arosto nyingi japo wamekulipa.

Ikiwa wewe sio mzinguaji hawawezi kukulalamikia ikiwa unawapa kitu mfululizo.

Nimeamua kutokuingia kwa group kwa sababu ya malalamiko yao hao waliolipia, ni heri nibaki na arosto hapa hapa, nikiona hawalalamiki basi na mie nitaingia kwa group 😂
 
Hao wanalalamika huko kwa group kuwa unazingua.

Wamekuamini wakajuinga na group ila unawaacha na arosto nyingi japo wamekulipa.

Ikiwa wewe sio mzinguaji hawawezi kukulalamikia ikiwa unawapa kitu mfululizo.

Nimeamua kutokuingia kwa group kwa sababu ya malalamiko yao hao waliolipia, ni heri nibaki na arosto hapa hapa, nikiona hawalalamiki basi na mie nitaingia kwa group [emoji23]
Mbongo kwenye Ubora wako
 
SEHEMU YA 507.

Tulipoishia ni pale Yezi anamuuliza mwalimu wake kama hakutaka ndoa je mpenzi pia pia hakuwa nae?, sasa jambo la kukumbuka ni kwamba maongezi haya yalikuwa yakifanyika siku kadhaa zilizopita kabla hata Roma hajaanza kufikiria safari ya kwenda Australia ni siku kadhaa mara baada ya Yezi kumpigia simu Roma akiwa analia halafu akakata simu.

“Hakika sina mpenzi na sitafuti kuwa na mpenzi wala ndoa?”Aliongea Vivian huku akionyesha kukunja sura na kwa jinsi anavyoongea ni kama wale wanawake ambao wameumizwa kwenye mahusiano.

Jibu lake lilimfanya Yezi kuona kabisa Vivian hakuwa akidanganya , alionyesha kuwa siriasi alipojibu kwamba hakuwa akitafuta mpenzi wala mwanaume wa kumuoa na kwake elimu ndio kipaumbele kwa muda huo , licha ya kwamba ilionyesha umri wa Vivian ni mkubwa na alipaswa kuwa na mpenzi au mchumba wa kumuoa ukizingatia na uzuri wake.

“Lakini kwanini?, au uliumizwa na mahusiano yaliopita na ukapata maumivu makali baada ya kuchana na mweza wako?”Swali lile lilimfanya Vivian kuanza kubadilika uso wake na kujawa na nishati ilioashiria huzuni , alijikuta akivuta pumzi na kisha akazishusha na kumwangalia

“Yezi wewe ni mdogo sana kuelewa na sijisikii kuzungumzia haya maswala , malizia muda unaenda”

“Mwalimu Vivian haina haja ya kuona aibu na isitoshe hakuna hata mmoja hapa anaelewa kiswahili , C’mon Vivian , mapenzi yana maumivu, lakini naamini mwanaume ambaye amekuumiza ni kipofu kumuacha mwanamke mzuri kama wewe , nakushauri awamu hii msahau kabisa na tafuta mwanaume mwingine ambaye ni bora zaidi”Aliongea Yezi

“Una uhakika gani kama yeye ndio kaniacha?”Aliuliza Vivian huku awamu hii akiwa siriasi kidogo kana kwamba maneno ya Yezi yalimgusa sana.

“Mh.! Kwahio wewe unasema ndio ulimwacha , kama ni hivyo kwanini bado unaonekana mnyonge?”

“Kuna mambo ambayo watu wengine wanaweza wakakusamehe , lakini wewe mwenyewe huwezi kujisamehe”Aliongea Vivian

“Kwahiho unamaanisha kwamba ulifanya kitu kibaya na kwasababu hio unaogopa kumfanyia mtu

mwingine?”Aliuliza na kumfanya Vivian kushitushwa na swali lake na kushindwa kuliijibu kwani alibakia kimya.

“Kwahio kama umefanya makosa ndio nini, binadamu tunakosea muda wote , kama mtu ukiunguzwa na supu mdomoni mara baada ya kunywa kijiko kimoja huwezi kusema maisha yangu yote siwezi kunywa supu , kwanini ujutie maisha yako yote kwa kosa la mara moja?”Aliongea na kumfanya Vivian kushindwa kujibu na alionekana kama mtu ambaye alikuwa akifikiria.

“Actually naamini mwalimu Vivian hujawahi kusikia maisha yangu yalivyokuwa, wakati nilipokuwa shuleni nilikokuwa nalelewa niliishia kupigana na wanafunzi wenzangu na mara nyingi nilirudishwa hosteli na kupewa adhabu nyingi mpaka nikafikia kipindi nikatoroka kabisa na kwenda kuishi mtaani na kuanza maisha ya kiharamu ya kuuza madawa na kufanya mambo mengi ya ukibaka na nilikamatwa mara kibao , kila kipindi nilipokuwa nikipelekwa kituoni nilikutana na dada mmoja aliefahamika kwa jina la Afande Mage , aliishia kuniambia binadamu husamehewa madhambi yake yote ya nyuma kama ataamua kubadilika, kwanzia hapo ndio nikaachana na maisha haramu na kujiingiza kwenye maisha halali ili kurekebisha makosa yangu, lakini licha ya hivyo sikuwa na ujasiri kabisa mpaka nilipokutana na uncle mmoja hivi…”

“Uncle!!?”Aliuliza Vivian huku akionyesha kuchanganyikiwa kwani ni mara ya kwanza kusikia stori ya Yezi.

“Yeah!, kuna mtu mmoja ambaye alikuja kuwa muhimu sana kwangu , ijapokuwa mara nyingi amekaa kijanja janja na matendo yake sio mazuri lakini ni mtu mzuri sana , nilipomuibia waleti yake hakuonyesha kunikasirikia kama ilivyo kwa watu wengi na aliniacha mpaka nifike sehemu isio na watu ndio akaniambia nimrudishie kistaarabu kabisa , lakini sio hivyo tu ikatokea nikakutana nae tena na akanisaidia tena kupiga watu waliokuwa wakinitafuta.

Kuanzia siku hio niliweza kugundua kwamba makosa ya binadamu ni maisha yaliopita na yanapaswa kuchukuliwa kama funzo kwa kadri mtu unavyoweka juhudi ya kubadilika na kuanza kuaminiwa tena , hivyo usijutie kwa kile ulichokifanya kwani kila kitu kitakuwa sawa , wewe ni binadamu na kukosea ni sifa ya kibinadamu hivyo usijitese tena”Aliongea na kumfanya Vivian kukosa neno.

“Una uwezo mkubwa wa kuchanganua mambo na muda wote una matarajio chanya na haupo kama mimi , lakini juu ya yote nitajaribu”

“Mwalimu Vivian mpaka sasa naamini unampenda huyo mwanaume kama sio hivyo usingekuwa na mwonekano huo wakati tukizungumzia hili swala"Aliongea Yezi na kumfanya Vivian kuinamisha kichwa chini huku akitoa kicheko cha chini chini.

“Pff.. unanificha tena, haya sikuulizi mimi tena, ngoja nimalizie chakula changu”

Akiwa anamwangalia Yezi akiendelea kupata breakfast yake alijikuta sasa ni kama amepata nafasi ya kupumua licha ya kwamba akili yake ilijawa na mawazo lukuki.

Muda huo huo mwanaume alievalia suti ya bei mbaya iliomkaa vyema mwilini aliingia ndani ya nyumba hio akiwa anafuatiwa na wanaume wawili ambao wote walivalia suti na walionyesha kuwa walinzi wake .

“Za asubuhi mwenyekiti?”Alisalimia Eunjung kwa kikorea huku akinamisha kichwa chake chini na upande wa Vivian na yeye alisimama na kisha akampa heshima ya kuinama vilevile.Alikuwa ni Park Jonghyun.

Yezi alionyesha kukosa utulivu mara baada ya mwanaume huyo kuingia hapo ndani lakini hata hivyo alipaswa kumuita mwanaume binamu yake mkubwa.

“Binamu naona bado unapata kifungua kinywa , nadhani unapaswa kufanya haraka la sivyo utamfanya Miss Vivian kusubiri kila anapofika hapa”Aliongea Park jonghyun.

“Sawa Binamu najitahidi pia , vipi unaenda kazini leo au umekuja tu kumwangalia babu?”Aliuliza Yezi.

“Niliona itakuwa jambo zuri kumuona , lakini kwasasa naona yupo na afya nzuri kutokana na uwepo wako “Aliongea huku akijichekesha.

“Huna haja ya kujali uwepo wangu”Aliongea lakini Jonghyun hakuendelea kuongea nae zaidi ya kumgeukia Vivian.

“Miss Vivian naamini bado hujazoea vyakula vya kikorea, kama unaona tabu kupata vya kitanzania badi nitamwandaa mtu kwa ajili yako”Aliongea kwa kingereza huku akimwangalia Vivian ki’swaga’ zaidi.

“Una ukarimu wa juu sana , lakini kwangu nipo sawa , kama Yezi anafurahia chakula cha kikorea na mimi pia ni rahisi kukipenda”

“Okey vizuri sana kusikia hivyo , lakini pia nina jambo lingine la kukuambia ….”

“We’re having a conference banquet with our American partners tonight , many renowned academics would be invited as well , I’ll like to invite you to be my partner..”

“Tuna sherehe ya chakula usiku wa leo na

wafanyabiashara wenza kutoka Marekani, na wanataaluma maarufi wengi wataalikwa pia , ningependa kukualika kuwa kama mwenza wangu..”Aliongea akimaanisha kwamba Vivian amsindikize kama mtu wa pembenni kwenye sherehe hio ya usiku.

“Mr Park inashukuru umenialika lakini mimi sio mtu wa kupendelea sherehe”Alimkatisha.

“Oh..!! basi hakuna shida,…”Huku akinaamisha kichwa akiwa kama mtu aliekosa utulivu baada ya ombi lake kuchomolewa “nitaenda juu kumsalimia mzee”Aliongea alionekana kama mwanaume ambaye amekataliwa na mwanamke baada ya kutupia ndoano.

Jonghyun kabla hajazipandisha ngazi kuelekea juu aligeuka nyuma na kumwangalia Yezi akionekana kama mtu ambaye amekmbuka kitu.

“Binamu babu ameniambia hisa za kampuni ya Starmoon zitahamishwa kutoka kwake kwenda kwako baadae , kidani cha mwezi ambacho baba yako alikupatia unatakiwa kuwa nacho , wakati ukija kuwa sahihi kidani hiko cha mwezi kitaungana na kingine cha babu cha Kundinyota(constellation)”

“Si ndio kile ambacho niliachwa nacho wakati nipo mdogo?”

“Ndio hiko au kuna tatizo?”Aliuliza na kumfanya Yezi kujin’gata ng’ata..

“Ni kwamba kuna mtu nilimpatia ..”Aliongea na kumfanya Jonghyyun kuwa katika mshangao.

“Nani umempatia?”

“Ni ni….”

“Subiri..”Alimzuia kuongea na kisha akawapa ishara watu wote waliokuwepo hapo ndani kuondoka ili aongee nae , ilionekana kidani hiko kilikuwa cha umuhimu sana. “Ongea kwa sauti ya chini , hilo swala ni nyeti mno kuliko unavyofikiria?”Aliongea na kumfanya Yezi kukosa utulivu

“Kipindi cha nyuma ili kuonyesha shukrani yangu nilimpatia uncle Roma”Aliongea.

“Mr Roma Ramoni!!!?”

“Yeah!!”

Jonghyun alionyesha kushangaa sana lakini mshangao wake aliuficha na tabasamu ili kumtoa hofu Rufi.

“Usijali nitaongea na babu , lakini nikwambie kwamba hiko kishaufu ni hazina ya familia hivyo lazima tukichukue kwani hakiwezi kutolewa kama zawadi lakini kwasababu umempatia Mr Roma basi tutakichukua kwa heshima”Aliongea na kumfanya Yezi kuhisi kabisa Jonghyun ana mpango wa kumwalika Roma nchini Korea na kama jambo hilo lingeenda kutokea aliona ingekuwa vizuri kwani alikuwa amemmisi sana na kuna muda alikuwa akilia kwa kuona Roma amempotezea na ajabu ni kwamba licha ya kumisi Edna lakini kwa Roma ilikuwa tofauti ndio mtu pekee ambaye alihitaji kumuona tena.

Unafikiri Kishaufu hicho kwanini kinaonekana muhimu , zingaita maeneno niliowekea wino.

*****

Nchini Tanznia, baada ya Roma kumaliza stori yake , Edna hakutaka kuamini moja kwa moja , alikuwa na wasiwasi huenda Rufi alifanya mpango wa kupigwa risasi makusudi ili kumvuia Roma , hivyo baada ya kurudi kwenye chumba chake cha kujisomea alimpigia simu Mage akitaka amweleze habari zote zilizotokea Australia.

Na Baada ya Mage kuelezea kila kitu bila ya kuficha aliona kabisa haikuwa makusudi kwa Rufi kupigwa risasi na hata akashindwa kuuliza zaidi lakini licha ya hivyo alijihisi kutokuwa na furaha na kilichotokea na mambo yanaavyokwenda kuendelea , alijihisi kama mwanamke ambaye anaonewa.

Na kwa jinsi ambavyo Mage aliongea , Edna aliona kabisa Mage anamchukulia Rufi kama mke mwenza tu , lakini hata hivyo aliona ni mantiki.

Rufi alikuwa na mwili wa kawaida kabisa kama binadamu lakini alikubali kwenda na Roma Australia na baada ya kufika huko alijitahidi kwenda nao sambamba bila ya kuwachelewesha , kwani kulikuwa na utofauti kati ya Yezi na Mage , yeye Mage alikuwa tayari ashaingia kwenye levo ya nusu mzunguko hivyo mwili wake haukuwa wa kawaida , lakini kwa Rufi ilikuwa tofauti, kwa fikra nyepesi Edna aliona Rufi alifanya kila kitu kwa ajili ya Roma na Mage na hakukuwa na tone hata dogo la ubinafsi katika matendo yake.

Na kwa kufikiria hivyo aliona kabisa hakuna namna ambayo Roma anaweza kumpotezea tena Rufi , alijikuta akijihisi kama mtu ambaye amekosewa kwani kwa muda huo hata hisia zake alishindwa kuzielewa na hata machozi yalianza kujitengeneza kwenye mboni za macho yake , aliogopa mno kumuona Roma akiongeza mwanamke mwingine.

Wakati akiwa anafikiria kwa kina , alishtuliwa na sauti ya Bi Wema iliokuwa ikimwita.

“Miss njoo chini haraka kuna kitu tunapaswa kuzungumza”Aliongea Bi Wema













SEHEMU YA 508.

Edna aijifuta haraka machozi yake na kujiweka sawa ili asije kushtukiwa kama alikuwa akilia.

“Nakuja Bi wema”Aijibu na kisha akajiweka sawa na kutoka kwenye chumba hicho na kushuka moja kwa moja mpaka chini sebuleni.

“Edna binamu yake Yezi kutoka Korea Kusini ametupigia?”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kushangaa.

“Binamu yake Yezi? Unamaanisha Park Jonghyun , Yezi yupo salama?”Alionekana kuwa na wasiwasi.

“Yupo salama , nadhani unakumbuka mara ya mwisho alipiga na kuulizia kuhusu kishaufu cha mwezi ambacho Yezi aliachiwa na kukiacha?””Aliuliza na kumfanya Edna kutingisha kichwa kwamba anakumbuka.

“Kishaufu chenyewe ni hiki , nakumbuka sikukuonyesha , kwa maelezo ya Park Jonghyun anasema siku ya kutangazwa kwa Yezi kama mwanafamilia imesogezwa nyuma hivyo anatualika twende Korea kusini kuhudhuria na kukirudisha”Aliongea Roma ambaye mara baada ya kupokea simu kutoka Korea alipandisha juu kwenye chumba chake na kukichukua ili kumuonyesha mama yake aliekuwa na shauku ya kukiona.

“Mh..!! mbona cha kawaida sana , kwanini kinaonekana kama kitu cha thamani kwao?”Aliuliza Edna huku akikaa kwenye sofa.

“Ndio inaonekana kina thamani kwao , amesema tarehe saba yaani ya mwezi wa sita ndio tukio kubwa la familia hio litafanyika, hivyo kabla ya tarehe hio kiwe kisharudishwa kwa Yezi”Aliongea Edna na kumfanya kwanza kupiga mahesabu ya kwanzia tarehe ya leo kwenda siku hio na haraka haraka ilionekan zimebaki siku kama ishirini mpaka kutimia kwa tarehe tajwa.

“Familia nzima ametualika pamoja na Mama Issa lakiini hatuwezi kwenda wote , hivyo mnaonaje nyie wawili mkienda pamoja na isitoshe tokea mfanye harusi hamjaenda Honeymoon , mnaweza ichukulia safari hio kama muda wa mapumziko kwenu”Alishauri Blandina na Edna alimwangalia Roma kiabu aibu na Roma alimtingishia kichwa akubali.

“Sawa mama hakuna shida , hata hivyo ni siku nyingi tunazo za kujiandaa”Alijibu Edna na hivyo wote wakakubaliana kwambe siku ishirini zijazo safari ya kwenda Korea kusini ianze.

Upande wa Roma aliona sio tatizo , kwanza ndani ya muda huo angefanya mambo yake kwa uharaka , kwa mfano alishamuahidi Yezi kumfuata Uingereza ndani ya siku chache zijazo hivyo safari hio ya Korea haikuwa ikiingiliana na ratiba zake , alipanga ampeleke kwanza Rufi akaone Caulron aliopata ili aweze kuithibitisha kama ndio yenyewe.

Iapokuwa uwezo wake wa kijini(nguvu za mbingu na ardhi) kwa muda huo zilikuwa juu zaidi , lakini bado hakuwa akijiamini, alihitaji kuimarika zaidi na zaidi kwani aliamini bado kuna waliomzidi.

*******

Ni nchini Korea kusini katika chumba cha kujisomea cha Park Juan ndani ya jumba hilo la kifahari.

Vioo vya madirisha viliingiza mwanga wa jua kwa rangi iliofanya eneo la ndani kupendeza kwa kuendana na samani za bei zilizopapangwa kwa usanifu wa hali ya juu.

Park Juan mzee mwenye nywele zilizoanza kubadilika rangi na kuwa nyeupe alikuwa amekaa kwenye sofa kubwa la Leather akiwa amevalia sweta la shingo ndefu pamoja

na koti lililotengenezwa kwa manyoya , alikuwa mzee lakini hakutumia miwani kuangalia watu waliokuwepo ndani ya chumba hiko.

Mbele yake kulikuwa na watu wanne ambao walikuwa wamekaa kwenye masofa , wa kwanza kulia alikuwa amevalia suti iliomkaa vyema mwilini rangi nyeusi na tai ya bluu bahari akiwa na miwani yenye fremu zilizotengenezwa kwa madini ya dhahabu ni mwanaume ambaye alifahamika kama msaidizi wake wa karibu.

Mwingine alikuwa mwanaume alievalia shati pekee rangi ya samawati la kitambaa cha katani ambalo iliubana mwili wake vizuri na kuonyesha kifua kilichojengeka kimazoezi lakini licha ya kuwa na mwili uliotuna , lakini alionekana kutokuwa na hamasa yoyote ya kusikiliza kile kilichokuwa kikizungumziwa hapo ndani.

Mbele kabisa upande wa kulia alikuwa amekaa mwanamke ambaye kimakadirio umri wake ulikuwa kama miaka arobaini hivi kuendelea mwenye sura mchongoko ambayo iliashiria kupitia mateso ya plastic surgery mara kadhaa ili kumfanya kuwa mrembo , alikuwa amevalia

necklace(mkufu) kubwa ya Lulu huku akiwa ameyarembesha macho yake na kiasi kidogo cha Mascara..

Pembeni ya mwanamke alikuwepo mwanaume kijana wa umri wa kati ambaye alionekana kuwa mwenye kujiamini huenda kuliko kila mmoja aliekuwepo ndani ya chumba hiko, alikuwa ni Park jonghyun ambaye alikuwa amevalia suti ya rangi ya zambarau ya kifungo kimoja.

“Baba unaonekana vizuri kwasasa, yule daktari kutoka Marekani aliekuhudumia kweli anaishi ndani ya umaarufu wa jina lake”Aliongea yule mwanamke huku akijichekesha mbele ya baba yake ambaye ni Park Juan

“Haha.. shukrani zote ziende kwa mjukuu wangu Yezi, maneno yake ya faraja yamenifanya ni mkumbuke kaka yako sana, kajaaliwa maneneo ya busara kweli, siku ya kwanza alivyofika hapa nyumbani nilifikiri naota”Aliongea huku akitoa kicheko hafifu.

“Gosh..!! Baba licha ya kaka kufariki lakini amebakia kuwa mtoto wako pendwa kwenye moyo wako , licha ya kila mmoja kufanya juhudi za kuziba pengo lake, lakini hata hivyo naona huenda nafasi yake ishapata mrithi’

“Jiyeon , huwezi kumuongelea kaka yako hivyo , wewe ni watoto wangu na hakuna wa kwanza wala wa pili , kusema hivyo ni kama kumsimanga wakati ashatangulia mbele za haki , na hata hivyo alijitolea sana kwako wakati ukiwa mdogo na nimeona kumlipa kwa ukarimu wake kupitia mtoto wake”.

“Nakupata vizuri baba , hata hivyo kaka alikuwa na aibu na kamrithisha na mtoto wake na ndio maana Yezi ameshindwa kabisa kuniita shangazi”Aliongea Park Jiyeon huku akitoa kicheko cha kinafiki.

“Haha..kwahio hivyo ndio ilivyotokea , basi nitakuomba uwe unamwangalia mara kwa mara maendeleo yake na kumfanya ajisikie mwanafamilia”Aliongea na kisha akaanza kuangalia wengine waliokuwa hapo ndani mmoja mmoja.

“Sitaki kuwapotezea sana muda , hivyo nitaenda moja kwa moja kwenye swala ambalo limenifanya niwaite hapa”Aliongea na kuwafanya wale waliokuwa wamezika vichwa vyao chini kuviinua kumwangalia.

Kwenye nyakati kama hizo hakuna ambaye alitaka kuonyesha utomvu wa nidhamu kutokana na kwamba ndio kipindi ambacho baba na babu yao anakwenda kuchagua mrithi.

“Jonghyun kuhusu mwaliko wangu kwa familia ya Miss Edna nchini Tanzania , je tayari wameshapata taarifa?”Alimuuliza Park Jonghyun huku akimwangalia. “Nishalifanyia kazi tayari babu”Alijibu

“Kazi nzuri , nafahamu sina haja ya kuwa na wasiwasi kutokana na umakini wako , Kuhusiana na nafasi yako ndani ya kampuni kama mwenyekiti utendaji wako ni wenye kuonekana , lakini hata hivyo nimeamua kufanya maamuzi mengine , baada ya tarehe saba mwezi wa sita nimeona ni muda sahihi wa kukupa majukumu makubwa zaidi ya kufanyia kazi”Park jongHyun mara baada ya kusikia kauli hio alipata hamasa kubwa ya kutaka kusikiliza ni majukumu gani ambayo alikuwa akipangiwa na kumfanya Park Juan kucheka kidogo.

“Nimefanya maamuzi ya wewe kwenda Ujerumani ndani ya mwezi mmoja kwanzia sasa , ili ukawe CEO wa Starmoon katika ukanda wote wa bara la Ulaya”Muda ambao anakamilisha kauli yake lile tabasamu la hamasa la Park Jonghyun lilipotea palepale.

Kwenda kuwa CEO nje ya nchi halikuwa tatizo ukilinganisha na kwamba anakwenda kupanua zaidi biashara , lakini kama utafananisha fursa ambazo zipo ndani ya makao makuu ya kampuni hapo nchini na kwenda nje haikuwa na utofauti na kupelekwa uhamishoni, ngumi aliokunja chini ya meza ilionyesha dhahiri hakuwa amefurahishwa na maamuzi ambayo yametangazwa kwake.

Park jiyeon mara baada ya kusikia kauli hio ya baba yake alitabasamu kinafiki , kwake ilikuwa kama habari ya adui yake kushindwa, alikuwa ni moja wapo waliokuwa wakijua kwanini baba yake alikuwa akimpeleka Park Jonghyun nje ya nchi.

Starmoon ndani ya Korea yalikuwa ni makao makuu ya kampuni zote tanzu katika mataifa yote waliowekeza , hivyo kwenda kuwa CEO nje ya nchi halikuwa tatizo sana , tatizo ni kwamba atakaepewa majukumu ya kuongoza makao makuu angekuwa na maamuzi makubwa kuliko yeye na kutokana na hali ya mzee ilivyo ingekuwa ni bye bye kupata nafasi tena makao makuu , hivyo maisha yake yote yangekuwa ni nje ya nchi.

Kwa mtu hajakulia katika mfumo wa kifamilia za kitajiri hapo ndani angeona huenda kauli ya Park Juani ni kumpandisha cheo Park Jonghyun , lakini ukweli ni kwamba ilikuwa kauli ya kumuelewesha nafasi yake ndani ya familia..

Ikumbukwe kwamba Park Jonghyun yeye pekee ndio ambaye hakuwa mjukuu wa damu wa Park juan , alikuwa amelelewa na mzee huyo tu baada ya kutolewa katika kituo cha kulelea watoto yatima.

“Asante sana babu…”Aliijibu Park Jonghyun kwa sauti ya chini lakini Park cheon hakujali sana alifahamu kwamba hajaridhika lakini hilo halikuwa la kwake kufikiria.

“Haoming wewe umekuwa mwenyekiti msaidizi kwa muda mrefu sana , na kwasababu Jonghyun anaelekea Ujerumani hivyo nafasi yake utairithi na kuwa mwenyekiti kamili , nakupa nafasi hio ili uweze kumfundisha Yezi kazi wakati atakapokuwa CEO wa kampuni”

Kwasababu Haoming alikuwa tu ni mkwe ndani ya familia ya Park aliridhika na nafasi aliopewa kwani ilionyesha kwmaba alikuwa akitambulika kama mwanafamilia.

“Nitahakikisha siendi kinyume na matarajio yako mema baba”Aliongea Liu Haoming mume wa Park Jiyeon na kisha akasimama na kupiga magoti kabisa kuonyesha shukrani zake na kumfanya babu yake Yezi kuridhishwa na kisha akamgeukia Park Jiyeon.

“Jiyeon wewe utaendelea kubakia kwenye nafasi yako kama CFO(Chief financial oficer), sio hivyo tu lakini pia utamsaidia Haoming kama mwenyekiti msaidizi”Aliongea na Park Jiyeon kwa heshima alitingisha kichwa kukubali.

“Jonghyun na Haoming mnaweza kuondoka wewe Jiyeon utabaki kwani nina mazungumzo na wewe”Aliongea na wanaume hao wawili walisimama na kuondoka hapo ndani akabakia msaidizi wa Park juan ambaye alikuwa kama sanamu na jiyeon.

“Baba nilishafahamu una busara ya kujua mipango ya huyo mtoto mtukutu , umefanya la maana kumpeleka Ulaya”Aliongea Jiyeon mara baada ya kubaki peke yao.

“Jonghyun ni mtoto mwenye akili sana , aliweza kupanua biashara zetu wkakati akiwa CEO tawi la Marekani na ndio maana nikaona sio mbaya kama ataenda kufanya kazi Ulaya ili tuzidi kujipanua zaidi na zaidi

kibiashara”Aliongea na kumfanya Park Jiyeon kuingiwa na wivu kidogo lakini hata hivyo aliona bado hakuwa na haja ya kuwa na wasiwasi kwani adui yake angekuwa mbali na macho yake.

“Nimekwambia ubaki kwasababu kuna kitu nataka kukuonyesha”Aliongea Park Juan huku akimwonyeshea nyaraka iliokuwa juu ya meza.

Park Jieyeon kwa utaratibu sana aliichukua na kisha akafungua bahasha na kutoa kaatasi zenye maandishi.

Baada ya kuisoma alijikuta akipatwa na mshituko kiasi kwamba alishindwa hata kupumua vizuri na alitamanni ardhi ipasuke atumbukie kwa wasiwsi aliokuwa nao.

“Baba ni makosa yangu naomba unisamehe?”Alianza kupasha viganja mikono akiwa amepiga mgoti huku akionyesha kuomba msamaha na kumfanya Park Juan kukunja sura.

“Simama haraka , kwa umri wako huo kwanini unashindwa kuwa makini , kama ulikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo unapaswa pia kuwa na ujasiri wa kuwajibika kwa matokeo yanayokwenda

kutokea”Aliongea kwa kufoka kidogo na kumfanya Park jiyeon machozi kumtoka huku akiomba kusamehewa.

“Umevunja uaminifu wangu kwako mara baada ya kukufanya kuwa CFO(Chief financial officer) na kufanya ubadhilifu wa mabilioni ya hela kwa ajili ya kufanya plasic surgery na kuhonga ‘machawa’ ,, lakini sio hivyo tu ukapata mpaka ujasiri wa kuhonga watu wengi katika soko la mziki kwa ajili ya Yoonhee kupewa tuzo na kufanya mafanikio yake yote aliokuwa nayo kuwa udanganyifu”

“Sina mpango wa kukudabisha kwa makosa ulioyafanya na nilichokifanya ilikuwa ni kukusanya makosa yako yote moja baada ya jingine , na karatasi unayoshikiria hapo ni kopi tu na karatasi yenye kumbukumbuu ya makosa yako yote ipo chini ya timu ya siri ya mwanasheria Kim nadhani unaelewa nini namaanisha”

“Baba samahani naomba unisamehe , ni makosa yangu na nakuahidi hii ni mara ya mwisho na sitorudia tena na tena … lakini Yoonhee pia ni mjukuu wako , kwanini hutaki kumuonyeshea mapenzi japo kiasi tu kama unavyofanya kwa Yezi?”

“Inatosha…!!”Alifoka na kisha akaendelea kuongea akionyesha hasira.

“Mwanafamilia yoyote yule katika ukoo wangu hawezi kutumia njia ya mkato kufikia mafanikio yake , chochote kile wanachotaka lazima wakifanyie kazi kwa kuvuja jasho , namjali sana Yezi sio tu kwa utiifu wake na heshima lakini pia ni kwasababu ya deni analonidai , Yoonhee kaamua kuachana na biashara na kujiingiza katika maswala ya burudani na hilo sina tatizo kwani ni maisha aliochagua , lakini sifurahishwi na mafanikio yake yanayotokana na udanganyifu , familia yangu haiwezi kulea watu wa aina hio, matendo yako unayoyafanya yatapelekea familia yetu kupata sifa mbaya”

Park Jiyeon alionekana kukosa neno lingine la kujitetea nalo zaidi ya kumuomaba baba yake amsamehe.

“Ila usiwe na wasiwasi , kama utaamua kuirekebisha na kuanza kuweka juhudi katika njia za halali basi nitakuzawadia kwa kile unachostahili , hata hivyo wewe ndio mtoto wangu wa pekee uliebaki hivyo siwezi kukutendea vibaya, nadhani umenielewa?”

“Nimekuelewa baba, Haoming na mimi tutajitahidi sana kuhakikisha Yezi anafanya vizuri katika kujifunza namna ya kuongoza kampuni”Aliongea na kisha Park Juan alimpa ishara ya kwamba aondoke.

Alijikuta akivuta pumzi nyingi mara tu baada ya kutoka nje ya mlango wa chumba hicho cha baba yake kwani ilikuwa ni kama ametoka jera, lakini licha ya kufokewa alishia kulaani tu , ilionekana hakuwa na mpango wa kubadilika.

Park Juan alifanikisha kupata watoto wawili tu katika uzao wake , ambaye ni Park Joonchen baba yake Yezi na Park jiyeon mama mzazi wa Yoonhee msanii aliekuja Tanzania kipindi cha shindano la kizazi nyota.

Park Jonghyun yeye alilelewa tu kama mjukuu na Park Juan mara baada ya kutolewa katika kituo cha kulelea yatima.

Park Jiyeon baada ya kufika floor ya chini alimuona Park jonghyun ndio kwanza anaondoka na mwonekano wake wa huzuni ulibadilika na kupambwa na tabasamu lililojaa dhihaka.

“Jonghyun nisubiri ..”Aliongea na kumfanya asimamae na kumwangalia.

“Shangazi kuna kitu ambacho unapanga kuniambia?”

“Nina swali ndio la kukuuliza , nimesikia kuhusu familia ya Adebayo kutoka Tanzania kualikwa na baba je ni kwasababu ipi na kwa kubwa gani waliokuwa nao?”

“Babu alikuwa na mpango wa kutoa shukrani zake kwao kuokana na kuishi na Yezi vizuri , ni kwa nia nyema tu ndio maana wamealikwa”Aliongea

“Ni hivyo tu?”

“Ndio hivyo”

“Vizuri , endelea kufanya siri lakini usije ukasema sijakuonya baba anaweza akawa amebakiza siku chache duniani lakini akili yake inafanya kazi vizuri sana na kama unataka akugaie nyama yake hakikisha mikono yako ni misafi , niamini mimi usije ukafanya kosa kukanyaga mkia wake kwani ni simba alielala.”Aliongea kimafumbo.

“Niwie radhi kama kuna kitu hakijakuridhisha kuhusu mimi shangazi , lakini mpaka sasa sijaelewa unamaanisha nini , tokea nilipo lelewa nilikuwa nikipokea malezi bila ya kutengwa na kwasasa kilichobaki kwenye moyo wangu ni shukrani tu kwenda kwa babu kwa yale yote alionitendea”

“Acha kujifanyisha hujanielewa , nikukumbushe sisi wote tupo kwenye kivuli chake hivyo anajua kila kitu”Aliongea na kisha alimwangalia na tabasamu la dhihaka na kuanza kupigiza viatu vyake vya mchongoko kwenye tailizi na kutoka nje.

Upande wa Park Jonghyun aliishia kusimama akiwa ana mwangalia kwa tabasamu ambalo pia halikuwa likiashiria nia nzuri kabisa kwenye moyo wake.

“Jione uko juu yangu tu , mwezi mmoja tu ndio ninaohitaji kukamilisha kila kitu baada ya hapo utalia kilio kibaya sana”Aliwaza kwenye nafsi yake.

Unafikiri ni mpango gani anaandaa , au ndio kujitakia kifo.
 
SEHEMU YA 509.

Siku tatu zilipita haraka haraka tokea arudi kutoka Australia, katika siku hizo tatu Roma alikuwa karibu sana na Amina ambaye baba yake amerejea nchini akiwa mgonjwa bado lakini alikuwa mwenye nafuu.

Amina alionekana kuwa mwenye huzuni na kumlaumu baba yake kwa kutokumwambia hali halisi ya ugonjwa wake.

Mzee Kanani alikuwa amegundulika kuwa na saratani ya kongosho ambayo ipo hatua ya pili , ugonjwa ambao ulikuwa ni changamoo sana kwenye uponaji, sasa ilionekeana tokea afahamike kuwa na ugonjwa huo aliamua kukaa kimya na kutokumwambia mwanae Amina na baada ya kuona hana maisha marefu kutokana na kukosa matibabu nje ya nchi ndio akaamua kumwambia ukweli ili ajiandae kisaikolojia kabisa na kumwangaa kama mrithi wa mali zake.

Licha ya kwamba baba yake kuna mambo aliomfanyia ambayo hajaridhika nayo , lakini kwake ndio mzazi pekee ambaye alibaki nae duniani ndio maana alihuzunishwa mno, ilikuwa afadhali kwake uwepo wa Roma kidogo umemfanya kuweza kusharabu kwa haraka taarifa hio.

Roma baada ya wiki moja kupita alifanya maamuzi ya kurejea tena Uingereza kwa ajili ya kumchukua Yezi na kumpeleka visiwa vya wafu kuthibitisha Cauldron alioipata kule kwenye fukwe ya Arafura.

Aliwaaga wanafamilia wake kwamba siku hio angerudi na Yezi hivyo kuwa siku rasmi ya kuungana nae kwa chakula cha usiku na mama yake alifurahi kusikia hivyo.

Aliweza kufika ndani ya hospitali ya St Mary’s katika wodi aliolazwa yezi baada ya kufanya malipo ya matibabu akiamini muda huo atakuwa peke yake, lakini mara baada ya kuingia ndani alishangaa kumkuta Clark akiwa anapiga stori na Yezi.

“Ona sasa aliefika hapa kwa ajili ya kumchukua mpenzi wake , lakini anakosa muda wa kunitembelea na kunipa salamu tu”Aliongea Clark kwa namna ya kulalalma na kauli yake ya neno ‘mpenzi’ ilimfanya Rufi kuona aibu kwani haikuwa ya kweli licha ya kwamba alikuwa akimpenda kweli Roma.

“Naonaga sio jambo zuri kukusumbua na mambo yangu mengi muda wote ndio maana”

“Na mimi nashukuru sana kwa kutonisaidia kuniondolea upweke niliokuwa nao, yaani mtu anaweza afikirie huwa unaniepuka, kama usingenikuta hapa sidhanni kama ungepata nafasi hata ya kunitembelea”Aliongea lakini Roma aliona ni muda sahihi wa kubadilisha topiki , hata hivyo ni kweli asingeenda kumtembelea siku hio , mpango wake ulikuwa ni kumchukua Rufi na kurudi nae tu na kuonana kwao ndani ya hio hospiali ni bahati.

“Haya niambieni kwanza mnaongea nini, daktari na mgonjwa? Maana ni kama mmeshakuwa marafiki sasa”

“Tulikuwa utkiongelea kuhusu maswala vikokotoo na mambo mengine kama hayo ya kimahesabu , inaonyesha dokta Clark anapendelea sana topiki hizo ndio maana , sio tu kwamba ni daktari lakini pia yuko vizuri kwenye maarifa yanayohusiana na vikokotoo ambavyo husaidia katika maswala ya ki udukuzi”

“Upo sahihi , Clark ni jiniasi , maswala ya kidaktari yanaweza kuwa ndio taaluma yake kubwa lakini kila sehemu ameweka miguu”

“Kwanini kama unajisifia wewe mwenyewe na sio mimi?”Aliuliza Clark.

“Hehe.. upo sahihi ni kwamba najivunia kuwa na koneksheni na mtu mzito kama wewe”Aliongea na kumfanya clark kucheka kidogo.

“Nimekuja kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya Rufi , nimemfanyia upasuaji mimi mwenyewe hivyo inamfanya kuwa mgonjwa wangu , mpaka sasa niseme afya yake imeimarika kabisa na ndani ya siku mbili zijazo anakwenda kuwa sawa kabisa , naamini yote haya yamewezekana kutokana na mbinu zako”Aliongea na Roma alitingisha kchwa.

“Upo saihihi , ili mradi anakuwa sawa haijalishi namna ambavyo anapona, lakini mbona unaonekana kama unajiandaa kusafiri?”

“Upo sahihi nasafiri kwenda Marekani, nimepigiwa simu na moja wapo ya wanafunzi wangu juu ya upasuaji wenye changamoto , hivyo akaniomba nihudhhurie nikamsaidie kumwona mgonjwa na nitoe mawazo yangu”

“Nina uhakika hawakuiti tu bure bure , itakuwa wanakulipa pesa nyingi ndio maana upo tayari kusafiri umbali mrefu hivyo?”

“Kwanza kabisa napenda changamoto zinazohusiana na taaluma yangu ili kupata uzoefu zaidi , pili wananilipa ndio ,tena kiwango kizuri ambacho kinanifanya kupata hela ya kuwekeza kwenye tafiti ninazoendeleza , hivyo unaweza kusema ni shinda ni shinde.”Aliongea na kisha palepale alionekana hakutaka kukaa zaidi kwani aliaga na kuondoka.

“Roma kwanini hujamchukua Clark kama mpenzi wako , mimi mwenywe kama mwanamke nimeona anavutia zaidi

, ana akili nyingi , anajiamini , lakini pia uwepo wake tu ni burudani tosha bila kusahau urembo wake, kwanini umejizuia kwake?”Aliuliza Rufi mara baada ya Clark kutoka.

“Ndio , najua pia mimi ni mdhaifu sana mbele ya wanawake warembo lakini kwa Clark ni tofauti , nimekutana na Clark miaka kumi iliopita na alikuwa ni mtoto kabisa hivyo unaweza kusema nilimwangalia wakati akiwa anakua , hivyo haraka haraka unaweza kusema alikuwa mdogo wangu ,kwangu mimi nataka apate mtu sahihi zaidi wa kuwa nae,.. halafu huu sio muda wa kuanza kujadiliana kwani nataka kurudi nyumbani mapema , amka hapo nimekuja kukuchukua ili ukachunguze Caulron kama ni yenyewe na baada ya hapo nikupeleke nyumbani kwani mama yangu na wengine wanasubiria ujio wako ili waweze kutoa shukrani zao kwa kuyaokoa maisha yangu”

“Tulia kidogo basi , nataka kuwaaga manesi wote walionihudumia , nadhani unamfahamu mwanafunzi wa Profesor Clark afahamikae kwa jina la Grace? Alikuwa akinijali sana tokea ulivoondoka hivyo siwezi kuondoka bila kumuaga”

“Nilijua jambo kama hili ushalifanya mapema kabla sijaja hapa”

“Mhmh… unalalamika nini sasa wakati ulikuwa kimya wkati Clark akiwa hapa, mimi bado ni mgonjwa unatakiwa kulifahamu hilo”

“Nisingeweza kulalamika mbele ya dakari wako , lakini ratiba zako ndio zinanifanya nilalaamike ilihali tayari nishakupatia taarifa ninakuja kuchukua leo”

“Kwahio ilikuwa sawa kwako kupoteza muda kwa kuanza kuongea na Clark hapa kupoteza muda , lakini mimi nikitaka kwenda kuaga unaona napoteza muda , wanaume mnasikitisha sana”Aliongea huku akijiweka kwa kuvaa nguo ambazo aliletewa na Clark.

“Basi fanya haraka, isitoshe Clark ni rafiki yangu , na sio kama nilikua nakulalamikia , ila nipo hivyo kwa vipenzi wangu wote, Babe Rufi usikasirike”Aliongea Roma akilegezza sauti na kumfanya Rufi ngozi yake kuwa nyekundu kutokana na kauli ya kuitwa Babe.

“Eww..!! eti Babe Rufi.. huoni aibu?”Aliongea na kisha akandoka ndani ya chumba hiko haraka haraka, alijisikia vizuri sana kuona ameunganishwa akatika kundi la wapenzi na kujawa na mategemeo zaidi ya kile kinachomsubiria katika maisha ya mbeleni.

Katika maisha yake yote hakuna siku ambayo ilitokea akajihisi utamu ndani ya moyo wake kama hivyo.

Baada ya dakika chache za kuawaaga manesi na kuwashukuru kwa huduma za kikarimu

walizomwonyeshea , hatimae walichukuana na Roma na kisha kuondoka kwani Roma alikuwa ashafanya tayari malipo yote yaliohitajika.

Ndani ya dakika chache tu waliweza kutua visiwa vya wafu katika ngome ya Roma, hakushangazwa na namna walivyosafiri kutokana na kwamba alishazoea sana wakati akiwa katika miliki za kijini , kilichomshangaza ni mazingira ya visiwa hivyo na Roma ilibidi kwanza amuelezee kwa ufupi mara baada ya kuingia ndani , lakini Yezi licha ya kupagawa na maelezo hayo hakushangaa sana , kwani hata yeye mwenyewe ametokewa kwenye mazingira ambayo yapo kiajabu ajabu kiasi cha kumfanya mtu yoyote asiamini akimwelezea.

Baada ya nusu saa kuongea hatimae waliwenda moja kwa moja mpaka vyumba vya chini ya ardhi , sehemu ambako Roma alihifadhi mimea waliokusanya kule Australia pamoja na Cauldorn.

“Ulikuwa unaongelea hiki Cauldron?”Aliuliza Rufi mara baada ya kuona kifaa ambacho sufuria sio sufuria wala chungu sio chungu kutokana na namna kilivyotengenezwa.

“Unaonaje , nguvu yake isiokuwa ya kawaida inayotoka , ninaweza kuinasa kwa urahisi sana , naamini kama utaipanga katika Dhana za kijini basi hii inaweza kuwa daraja la kati au la juu”aliongea Roma na kumfanya Rufi kuchuchumaa na kuanza kukikagua.

“Hiki ni Cauldron ndio , lakini mwonekano wake sijawahi kuuona wala kuusikia katika miliki za kijini lakini pia hata mchoro wake haueleweki , kama nitakifananisha labda kinafanana na Taotie , lakini hata hivyo Taotie katika nyaraka inaonyesha tofauti sana na hiki , kama sio

Taotie basi sijui dhana hii ya kijini ilitokea kwenye miliki ambazo hazihusiani na China”

“Jaribu kwanza kuchunguza madini yake , huenda ikawa rahisi kutambua?”Alishauri Roma na kumfanya Rufi aanze kupangusa kutu na kusogelea kwa ukaribu zaidi na alijikuta akitoa mshangao.

“This is ethereal hyacinth gold”Aliongea Rufi kwa mshangao akimaanisha kwamba chungu hiko kimetengenezwa kwa madini ya dhahabu aina ya hyacinth.

Hyacinth ni aina ya dhahabu ambayo rangi yake ni kama imetoka kuwa njano na kuwa shaba , ni dhababu ambayo imechanganyika na madini mengine ili kuifanya iwe na ugumu wa kiwango cha juu.

“Hyacinth Gold, mbona unaonekana kama vile ni madini ambayo ni adimu , wakati kama kumbukumbu zangu ziko sawa Urusi wanayo aina hio ya dhahabu?”Aliongea Roma.

“Hapo si ndio mwisho wa ufahamu wako, sasa kuhusu aina hii ya madini , yanaitwa ethereal hyacinth gold kwasababu maalumu (ethereal ni sawa na kitu adimu kisichokuwa cha kawaida).

“Katika ngano za miliki ya kijini inasemekana wanyama wakubwa wa enzi hizo wanapokufa maiti zao pamoja na mifupa hugeuka kuwa madini haya baada ya miaka elfu kumi , ni ngano ambazo zipo kwa muda mrefu na zimesambaa mpaka katika baadhi ya mila katika ulimwengu wa kawaida,, sasa kuhusu aina hii ya dhahabu mara nyingi ni adimu sana kuiona , na dhahabu zote za rangi ya shaba unazoona nni kutokana na mchanganyiko wa madini mengine , kwenye maisha yangu nimeshuhudia kisahani kimoja tu tena ujinini kilichotengenezwa na madini haya katika hali safi na asilia , sasa hebu jiulize wewe una Chungu kikubwa kama hichi kilichotengenezwa kwa madini hayo adimu , unafikiri miliki yoyote ya kijini ikifahamu watakuacha salama?, lazima mtaingia kwenye vita”

“Kwahhio unachomaanisha ni kwamba kutengeneza vidonge kwenye hiki chungu , vitakuwa vya viwango si ndio?”

“Upo sahihi , lakini sijawahi kusikia Cauldron ambayo imetengenezwa kwa dhahabu hii adimu lakini naamini kabisa ni nguvu sana kuyeyuka na moto wa rangi nyeupe(pure fire)

Moto mweupe unaozungumziwa ni tofauti sana na ule wa gesi wa nyumbani kwani ule una mchanganyiko kidogo na rangi ya bluu , moto mweupe ni mweupe kabisa ambao ni msafri usiokuwa na moshi hata kidogo na mara nyingi moto huu ni ngumu sana kutenganishwa , ijapokuwa moto wa bluu unaweza kuwa na joto kali mpaka kufikia nyuzi 1600 lakini unakosa sifa ya ‘pure’ hivyo katika miliki za kijini wanaamini moto mweupe ndio ungamanisho na nafsi zao na ndio ambao upo kiroho zaidi.

“Kama maneno yako ni sahihi na kina uwezo wa kuhimili moto mweupe je kimetengenezwaje?”Aliuliza Roma.

“Kwanza kabisa hii ndio mara yangu ya kwanza kuona Cauldron ya namna hii ila nina uhakika sio kwamba hakiwezi kuyeyuka kama tutaweka kisayansi zadi, lakini ukija kiroho ni ngumu sana kukiyeyusha kwani kina maungamano ya nafsi kali za enzi na enzi tena za wanyama wakubwa ambao ni hatari”Roma alionekana kuelewa kiduchu lakini kwasababu alimuona Rufi kukosa maelezo sahihi ya kuelezea jungu hilo aliona asiulize zaidi kwani muda unapotea.

“Unaonaje ukanisaidia kupangilia mimea ambayo tuliipata kimakundi , nataka kesho nirudi kujaribu kutengeneza vidonge nione kama naweza fanikisha, nyumbani watakuwa wanasubiri ujio wako hivyo lazima tuondoke mapema”

“Kwahio ulikuwa ukimaanisha kwamba leo hii ndio napaswa kujumuika na familia yako katika chakula?”Aliuliza na Roma alitingisha kichwa. “Kwanini tusivute vute siku , bado najihisi sipo tayari kwenda kuonana nao”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kwa muda.

“Kama ni hivyo basi , hakuna shida, nitawapigia simu ili kuwaeleza nadhani wataelewa”

Rufi alikuwa akihofia kwani mpaka muda huo alijua kabisa hataenda nyumbani kwa Roma kama Rufi wa mwanzo ,bali mahusiano yake na Roma yamepiga hatua hivyo bado alikosa ujasiri hasa mbele ya Edna.

Baada ya kukubaliana Roma ilibidi kwanza afanye mawasiliano nchini Tanzania kuwaeleza kwamba hatoweza kurudi kwa muda wa siku mbili kwani kuna kazi anaifanya na kwasababu hakuwa akiomba ruhusa baada ya kujielezea hakuhitaji ruhusa kutoka kwa mke wake, kwani baada ya Edna kuitikia kwa neno ‘okay’ bila nyama nyama alikata simu.

Rufi alimwaga mimea yoe waliotafuta katika nyika ya Arnhem na kuanza kuipanga kutokana na aina ya vidonge ambavyo wanatarajjia kutengeneza na ndani ya masaa mawili walikuwa wametenganisha mimea katika makundi matatu , yaani mimea ambayo ingetegneneza vidonge vya daraja la kwanza , la pili na la tatu.

Daraja lwa kwanza vilikuwa ni vile ambavyo mara nyingi mtu anapotumia humuingizia nguvu ya ajabu ambayo hufanya akili yake kuwa tulivu mno kama vile mtu ambaye ametumia madawa ya kulevya kwa kusudi la kuona picha flani la kufikirisha , vilikuwa vinasaidia sana mtu kukusanya nishati ya mazingira.

Kundi la pili ni vya kumsaidia mtu kumbusti uwezo wake ili kuweza kupata ufunuo wa mbingu na matumizi ya elementi za dunia kwa kupitia tahajudi na kundi la tatu sasa hivi ndio ambavyo Roma alipaswa kutumia yeye , ni vidonge ambavo vinasaidia mtu kuvuka levo kwa haraka.

Baada ya makusanyo hayo ya mimea , hatua iliofuata kwanza ni Roma kuanza kujua namna ya kutumia

Cauldron hiyo ya madini ya dhahabu rangi ya shaba.

Katika utengenezaji wa vidonge katika miliki za kijini ni kubadilisha mmea katika mfumo wa majani kwenda kiroho zaidi , hivyo Roma angepaswa kwanza kudhibiti Cauldron kwa kubalansi joto la moto mweupe na kisha mimea hile ndio aitupie kwenye jungu hilo.

Haikuwa chungu cha kawaida na ndio maana hata mbinu zake za utengenezaji wake wa vidonge haukuwa wa kawaida, kwani Roma alipaswa kudhibiti joto lake na kutupia ile mimea na baada ya hapo vidonge vingejitengeneza vyenyewe na kubakia chini kama chembechembe ambazo angekusanya na kufanya ziwe kidonge.

Sasa Roma alikikalisha chimi kile chungu na baada ya hapo Rufi akasogea pembeni na yeye akakaa chini kama vile anafanya Tahajudi na hatua ya kwanza alikusanya nguvu za kimaandiko na kuzituma kwenye kile chungu ili kuunganisha akili yake na kile chungu cha kichawi.

Baada ya hapo angeruhusu nguvu zake za kijini katika kiwango chote cha juu cha levo ya kuipita dhiki na kisha angeanza kudhibiti sasa moto kwa kubalansi nguvu ya kijini iliokuwa kwenye kibofu , moyo na figo.

Sasa Roma baada ya kufuata hatua zote hizo na kuanza kufanya kazi ghafla tu kilianza kutoa moto ndani yake kwa kuanza na wa rangi ya njano na bluu na baada ya Roma kuweza kusafisha na kubakiza moto wa mweupe kile chungu kilielekea hewani kwa namna ya ajabu mno huku kikianza kufoka kwa sauti zizizokuwa za kawaida , lakini muda huohuo Roma alihisi ni kama mwili wake unaingiliwa na nguvu ya ajabu mno ambayo palepale iliteka akili yake na akawa hajitambui tena, ni kama vile yupo ndotoni kwenye ulimwengu usiokuwa wa kawaida huku yeye mwenyewe akiwa kama mnyama anaefanana kama vile ni Dragon , ambalo linatema moto wa rangi nyeupe.

Roma alijitahidi kudhibiti akili yake kwa kuurudisha ufahamu wake , lakini kadri alivyokuwa akijitahidi alishindwa kabisa na katika ndoto aliona ndio kwanza yeye akiwa katika umbo la mnyama wa kutisha akikasirika zaidi na zaidi na kupaa angani huku akikausha kila kiumbe anachoona chini yake.
 
SEHEMU YA 510.

Hakikuwa chungu cha kawaida kabisa na huenda Roma asingekuwa na uwezo mkubwa wa nguvu ya kimaandiko basi akili yake ingekamatwa kabisa na akageuuka kuwa binadamu mwenye nafsi ya mnyama.

Kwa haraka haraka kama ingetokea mtu ambaye mafunzo yake ya kijini yalikuwa kwenye levo ya Nafsi huenda ufahamu wake ngetekwa kabisa , lakini Roma kwasababu nguvu yake ilikuwa kubwa kuliko Jungu hilo basi aliweza kufanikisha kurudi kwenye hali yake ya kawaida baada ya baada ya nafsi yake kushinda.

Roma mara baada ya kushinda pambano la nafsi palepale kile chungu kiilipotea kwenye hewa na ndio wakati ambao alifumbua macho.

“Rufii…!!”Roma alimwita Rufi baada ya kumkosa mbele yake huku akihofia huenda kitu kibaya kimempata kutokana na yeye mwenyewe fahamu zake kutekwa kwa muda , lakini mara baada ya kugeka nyuma alimwona Rufi ambaye alikuwa amejificha kwenye kona akiwa amepauka kwa woga.

“Ooh ..Asante Mungu uko sawa”Aliongea Roma huku akivuta pumzi na kuzishusha kwa ahueni.

“Umeona nini na chungu kiko wapi?”Aliuliza kwa shauku na Rufi alijikuta akimeza mate mengi na kujirudisha katika hali ya kawaida kwani alionekana kuwa katika hali ya mshangao na mshituko.

“That… cauldron ..i’m afraid isn’t an ethereal hyacinth gold”Aliongea akimaanisha kwamba jungu hilo la kijini sio kama alivyofikiria kuwa ni la madini ya dhahabu yanayokaribia rangi ya shaba.

“Unamaanisha nini?’Aliuliza Roma akiwa kwenye mshangao wa kuchanganyikiwa.

“Baada ya chungu kukutana na pure fire ndio kilijidhihirisha na kunifanya nitambue sio kama nilivyofikiria , nahisi ni zaidi ya chungu cha dhahabu , kama fikra zangu zinaweza kuwa sahihi basi kinaweza kuendana na immortal item aina ya dhana ambazo ni adimu sana katika miliki ya kijini.”Aliongea na kumshangaza Roima.

Immortal item?”Aliuliza Roma huku hisia zake zikimwambia huenda ikawa Dhana ya kijini ya thamanni kubwa.

“Umejuaje ni immortal item?”.

“Mwenyewe sifahamu lakini ninachoelewa ni kwamba Dhana ya aina ya immortal zina upekee wake , maarifa ya kijini yanaeleza kwamba ni dhana ambazo zimeunganishwa na nafsi au roho za wanyama wakubwa ambao walitokea enzi kubwa za kale na kwasababu hio kama utataka kukiyeyusha, lazima kwanza uvunje nguvu yake ya kiroho ilioshikiria nafsi za mnyama huyo na kadri mnyama anavyokuwa nkubwa zaidi ndio nguvu yake huwa kubwa zaidi”

Immortal item ni dhana za kijini za kale sana ambazo inasemekana maisha yake ni marefu, ni vifaa ambavyo vinadumu pasipo ya kupotea au kuharibika kwa muda mrefu sana , sasa vifaa hivi vimetengenezwa na madini lakini madini ambayo yameungamanishwa na roho za wanyama(Beast) wakubwa waliowahi kutokea duniani mfano wa mnyama kama Dragoni.

Maelezo ya Rufi yalikuwa yakiendana kabisa na kile Roma ambacho alikishuhudia kwenye ndoto , aliona mnyama mkubwa ambaye alishindwa kumtambua , mnyama ambaye alitaka kuivaa roho yake na kuutawala mwili wake.

“Kuna jambo lingine pia , Dhana kama hizo huwa zinatabia ya kuchagua nani anaweza kumiliki hivyo sio watu wote ambao wanauwezo wa kuvimiliki na kuviendesha na pale kinapopata mmiliki basi kitakuwa kama mtumwa kwako na kufanyia kazi maagizo yote kadri ambavyo mmiliki atakavyoendelea kuishi”

“Inaonekana nimebahatisha kitu cha thamani kweli?”Aliongea Roma huku akitabasamu.

“Ndio umebahatisha, aina hio ya Cauldron naweza kusema huwezi kuikuta kabisa katika miliki za kijini na cauldron ambazo unaweza kukuta haziwezi kuwa na nguvu kama ilionyesha hapa , jambo moja la kuzingatia ambalo linaweza kuwa la faida kwako ni kwamba hii dhana ikishakuchagua basi moja kwa moja inaungana na roho yako , hivyo kadri unavyopanda levo na yenyewe inapanda levo vilevile na kuwa kali zaidi na kama fikra zangu zipo sahihi kupotea kwake ni uhakika wa kwamba kishaungana na nafsi yako na muda wowote unaweza kukiita na kikafanyia kazi maagizo yako”Aliongea Rufi na kumfanya Roma kujawa na msisimko zaidi.

Cauldron haikuwa dhana ya kawaida kabisa, licha ya kwamba mwanzoni Roma alitafuta kwa ajili ya kutengenezea vidonge lakini kazi yake haikuwa kutengenezea vidonge tu , ni Jungu ambalo linatumika kumeza nafsi dhaifu.

Hivyo kwa lugha nyepesi ni siraha ya hatari sana kwa majini ambao wapo kwenye levo ilio chini ya Roma au waliopo kwenye levo sawa na yeye ambao hawana kinga , kama watakutana na mdomo wa Jungu hilo basi ni hakika watamezwa.

Sifa yake nyingine ni kwamba mdomo wake upo kama shimo jeusi(black hole) , yaani shimo ambalo linavuta kila kitu kilichopo karibu yake na kumeza palepale , ilikuwa ni makosa kufananisha chungu hicho na vyungu vya kawaida kwani chenyewe ni roho ya mnyama hatari ambaye yupo katika mfumo wa Chungu, hivyo Roma mara baada ya kukiingizia moto mweupe ni kama amefanya kukiwasha(activate) na kubadilika kutoka kuwa chungu na kuwa Jungu sasa la ajabu.

“Naamini nikikutana tena na yule bwana mwenye maski lazima atanitambua , nitamfanya roho yake kumezwa na chungu changu”Aliongea Roma huku aking’ata meno kwa hasira , alionekana kama mtu ambaye alitamani wakati akiwa anapambana na mtu yule awe na hiko chungu.

Roma palepale alijaribisha kukiita kwa kunuia tu na kikatokezea tena hewani kikifuka moto wa rangi nyeupe(pure fire), Rufi aliishia kushangazwa na jambo lile licha ya kwamba ni mara ya pili kuona , lakini bado hakuwa amezoea kabisa.

“Babe Rufi nikipatie jina gani hiki chungu changu?”Aliuliza Roma.

“Unaweza kukipatia jina lolote unalotaka , hata hivyo sio kwamba kina ufahamu kwani roho iliofungamana nacho ni ya mnyama”

“Unaonaje nikikiita , Jungu akili, bingwa na kiboko ya majini?”Aliuliza Roma huku akicheka kifedhuli.

“Acha kuongea pumba na tuanze kazi ya kujaribu kutengeneza vidonge”Aliongea Rufi huku akikaa chini kiwasiwasi maana Jungu hilo kwa namna linavyotoa msisimko na sauti kama ya mnyama ilimuogopesha.

Kwa mara ya kwanza Roma alifanikisha kutengeneza vidonge tena havikuwa vidonge vya kawaida , bali vilikuwa ni vidonge vyenye ubora wa hali ya ju, kiasi kwamba aliona haitofaaa kuviita vidonge vya Poya , hivyo akaamua kuvipatia jina ambalo aliona linafaa katika kichwa chake , ili kuendana na ubora wake.

Alitumia mimea yote walioweza kukusanya ndani ya bara la Australia mpaka ikaisha , lakini licha ya hivyo Roma bado hakuridhika kabisa na alijiambia ni kheri akaenda tena kutafuta mimea mingine ili kuendeleza kazi.

Alikuwa na mpango kumalizana kabisa na utengenezaji wa vidonge kabla ya safari yake ya kuelekea Korea haijaanza rasmi.

Roma alishauriana na Rufi kwenda kutafuta tena mimea katika maeneo mengine ambayo hawajaenda na Rufi kwasababu alikuwa akitaka kuwa karibu zaidi na Roma alikubali mara moja na safari yao ikaanza , na mpango wa kwanza ilikuwa ni kwenda msitu wa Amazoni , wakiwa na uhakika ndani ya msitu huo wangefanikisha kupata kile wanachokitafuta.

Roma hakuwa na wasiwasi tena kuhusu kushambuliwa kutokana na kwamba kujiamini kwake kuliongezeka mara dufu mara baada ya kupata Chungu cha ajabu ambacho kilikuwa na nguvu ya kumsaidia kupambana na maadui zake.

Kutokana na msitu kuwa mkubwa mno na kutopatikana kwa haraka mimea waliokuwa wakihitaji iliwachukua siku zaidi ya nne ndani ya msitu huo.

Roma hakuwa na wasiwasi , kwani alishampigia simu mama yake kwamba anaelekea Amazoni hivyo angechelewa kurudi nyumbani.

*********

Ni alhamisi mchana nchini Tanzania katika makao makuu ya kampunni ya Vexto kulikuwa na kikao cha watendaji wa juu wa makampuni ya Vexto , kikao ambacho kilikuwa kikiongozwa na Edna mwenyewe.

Ndani ya ukumbi huo wa mikutano kulikuwa na kimya cha muda mrefu huku wanaume na wanawake waliovalia suti wakimwangalia CEO ambaye alikuwa ameshikilia karatasi na kuzisoma, ilikuwa ni kama kuna maamuzi ambayo wanasubiria kuyasikia kutoka kwake.

Kila mmoja alimwangalia Edna kwa mawazo tofauti , hususani namna mwanadada huyu mwenye umri mdogo jinsi ambavyo amefanikisha kuipaisha kampuni ya Vexto.

Kwa wale wamama ambao tayari wana watoto wa kike wenye umri wa Edna walitamani angalau watoto kufikia nusu ya uwezo wa Edna.

Nasra na Dorisi pia walikuwa ni moja wapo ya wafanyakazi waliohudhuria katika kikao hiko kama viongozi wa juu wa kampuni na walikuwa wamekaa upande wa kulia na kushoto karibu na alipo Edna na wote walikuwa wakimwangalia kutoa mawazo yake mara baada ya presentation(uwasilishaji iliotolewa na mkuu wa idara ya Quality Assurance.

“CEO is there anything you are dissatisfied about?”Nasra aliamua kuvunja ukimya mara baada ya kumuona Edna hatoi mawazo yake ilihali kila mmoja alikuwa akimsubiria yeye.

Ukweli ni kwamba katika wiki yote hivyo Nasra alimuona kabisa Edna hakuwa yule ambaye amemzoea , alionekana kama mwanamke ambaye alikuwa na mawazo.

“Nothing much , I am aware that the profit of this project are viable , but it involves venturing ino uncharted territory…..”

“Naelewa kwamba faida ya mradi huu inawezekana lakini ni swala la kujitosa katika eneo ambalo halitambuliki….., kwasasa umakini wetu tumeulekezea kwenye mradi wa Adani na pia katika maswala ya fasheni , huu mradi unahusisha uwekezaji mkubwa kwanzia matayarisho yake mpaka kukamilika, hivyo kwa maoni yangu nadhani tuendelee kuangalia kwanza namna hali ilivyo kuliko kuingia moja kwa moja , haya ni mawazo yangu tu hivyo nitaacha kila mmoja atoe mchangao wake ili kufikia makubalino…”Aliongea na kisha akapumua kidogo.

“I hereby annaounce to those who are in favour of our collaboration with the Hanson enterprise and BMW group for this project please raise your hands”

“Natakangaza kwa wale ambao wanaunga mkono ushirikiano na kampuni ya Hanson na BMW GROUP kwenye hii projekti wanyooshe mikono”

Hakuna ambaye alinyoosha mkono kwani tayari Edna ashatoa mawazo yake , hivyo hawakutaka kumpinga wazi licha ya kwamba ushirikiano wa kibiashaa na kampuni ya BMW ukanda wa Afrika mashariki ungekuwa na faida kubwa na sio hivyo tu ungeipaisha Vexto zaidi kibiashara , lakini licha ya hivyo hawakutaka kupiga kula ya ndio walikuwa washaelewa kwanini Edna alianguliza kutoa mawazo yake na kisha akaanzisha upigaji kura , katika siku za nyuma Edna sio mtu wa kukosa maamuzi, kama mradi ungekuwa na faida kwake basi angeukubali moja kwa moja ama kukataa na hakuna wa kupinga mawazo yake , lakini siku hio ilikuwa tofauti.

Nasra alijikuta akiangaliana na Dorisi na kutafsiri kitu kuhusu Edna na walijua huenda Edna maamuzi yake yameathiriwa na maswala yake binafsi.

Walikuwa wakifahamu Hanson na Edna walikuwa na ukaribu ambao ulianzia chuoni lakini hawakuwa wakifahamu kama Roma alikuwa akielewana vibaya na Mzungu Hanson.

Upande wa Edna ni kweli dili lilikuwa nono, lakini aliamini kama angekubaliana nalo basi asingeweza kuzuia ukaribu kati yake na Hanson, hivyo ili kuepusha mgogoro na mume wake , aliona bora apotezee tu dili hilo.

Baada ya Edna kuona hakuna ambaye alikuwa akipingana na mawazo yake , hatimae alihitimisha kikao na kila mmoja akaondoka, hivyo rasmi ikawa imejulikana kwamba ombi la biashara kati ya kampuni ya Vexto na kampuni ya BMW limekufa rasmi.

“Edna nimeona ulivyokuwa kwenye kikao na hisia zangu zimeniambia sio maswala ya kibiashara yaliokufanya ufanya maamuzi ya aina hii?”Aliongea Nasra bala baada ya kumfuata Edna ofisini kwake.

Edna baada ya kuulizwa hivyo alijua kabisa hana sababu ya msingi , hivyo hakuwa na haja ya kumficha Nasra.

“Nadhani unajua kwanini nimefanya maamuzi haya”Aliongea kwa sauti ya chini na kumfanya Nasra kucheka.

“Naona umemkumbuka sana mumeo , lakini sio kwamba ni mara yake ya kwanza kusafiri , sikudhania kwamba mahusiano yako yanaweza yakaingilia utendaji wako wa kazi.. , sio kwa Edna ninaemfahamu mimi, kipinid cha nyuma licha ya kwamba ulikuwa kwenye majonzi ya kufiwa na mama mzazi , lakini bado uliweza kuongoza kampuni vizuri na kuipitisha katika kipindi cha mpito , lakini sasa hivi ni Roma ambaye amesafiri na Rufi peke yao imekufanya uathirike namna hii kweli!”Aliongea Nasra na kumfanya Edna kukosa jibu.

Ulikuwa ukweli mtupu kitendo cha Roma kuwa nje ya nchi akiwa na Rufi lilimfanya kukosa utulivu wa akili mno , alihisi wivu wa kiwango cha juu kiasi cha kumfanya utendaji wake wa kazi kupungua.

Yule Edna ambaye muda wote alikuwa akijali biashara ru alikuwa ni kama amepotea kwenye macho ya Nasra , dili la kibiashara ambalo liliwekwa mezani na Hanson hakuna mtu yoyote ambaye ni mpenda faida akalikataa , kwa Edna hata yeye alijiambia kama mtu ambaye anakwenda kufanya kazi asingekuwa Hanson basi angelikubali na biashara ikaendelea.

“Inaonekana mwanamke mfanyabishara makini tuliekuwa tukimfahamu kwasasa amekuwa mke kweli anaefikiria nyumba yake muda wote”

“Nasra naomba uache”Aliongea Edna ambaye hakutegemea Nasra kuongea hivyo kuhusiana na namna mpya ya maisha yake.

“Sawa nitaacha , najua una mawazo yako mengine lakini kwasasa unaonaje tukienda mpaka chini nje upande wa pili angalau kupata keki , najua huna mpango wa kusubiria chakula cha usiku moja kwa moja kama mimi”Aliongea na kumfanya Edna akubali , alikuwa akipenda sana kula keki hivyo mara baada ya kutajiwa na Nasra hamu ilimvaa hapo hapo na aliona inafaa kuongozana kwani wangenunua keki moja na kushirikiana kula.

“Nisubiri niweke vizuri vitu vyangu halafu tuondoke”

*********

Upande mwingine , nyumbani kwa Roma alionekana Blandina mama yake Roma akiwa ameketi kwenye masofa huku mkononi akiwa ameshikilia kalenda ya familia, baada ya kuangalia tarehe aligundua siku ya kesho ilikuwa ni sikukuu ya Eid kama mwezi ungeandama , lakini pia siku hio hio ya kesho katika kalenda ya kifamilia ilionyesha ni siku ya kumbukumbu ya tarehe kifo cha bibi yake Edna.

Tokea Marium bibi yake Edna kufariki ulianzishwa utaratibu wa kifamilia wa wa kuzuru kaburi lake na hata wanafamilia walikuwa wakifanya kazi nusu siku au kutokwenda kabisa kazini..

Baada ya Blandina kuona tarehe hio alifikiria jambo na kisha akamgeukia Bi Wema ambaye alikuwa akimfundisha Qiang Xi kuongea kiswahili.

“Wema nadhani kesho itakuwa jambo zuri kama nitamsindikiza Edna kwenda kutembelea kaburi la mama yake , lakini pia sio mbaya kama tutaungana na waislamu kusheherekea sikukuu ya Eid , hivyo naona ni vizuri kama nitaenda sokoni kabisa kwa ajili ya kununua mahitaji, najua Roma anaweza asirudi leo usiku kama ilivyopangwa lakini kesho lazima atarudi , hivyo ni vizuri kujiandaa mapema”Aliongea na kumfanya Bi Wema kufurahishwa na namna ambavyo Blandina alikuwa makini kwenye mambo madogo ya kifamilia, alikuwa ashasahau kama siku ya kesho ndio ambayo Edna alipaswa kutembelea kaburi la Bibi yake pamoja na mama yake.

“Nadhani sio mbaya kama tutamkumbusha Edna kwa njia ya simu”

“Anaweza kuwa bize muda huu , haina haja ya kumsumba kwa kumpigia kuna mzigo wangu nitaufuata posta hivyo nitampitia ofisini kwake ili angalau nione na mazingira anayofanyia kazi”Aliongea Blandina na kumfanya Bi Wema kutabasamu na kuona ni wazo zuri.

************

Edna na Nasra waliweza kufika ndani ya mgahawa uliokuwa upande wa pili wa jengo hilo la kampuni na kisha wakachukua keki moja na juisi ya matunda na kwenda kukaa upande wa dirishani kabisa upande wa barabara.

Nasra alionekana na yeye kupenda keki zenye sukari kama Edna tu na wakati akiwa kipande cha pili Edna alikuwa cha kwanza

“Hakika malkia uko ligi tofauti na sisi masuria, hata kwenye ulaji wa keki?”Aliongea Nasra akimtania Edna kutokana na kula keki kipole sana lakini kauli yake ilimfanya Edna kushangaa kwani ni kama hakuitegemea

“Nasra huoni kuongea hivyo si vizuri?”

“Kwanini sio vizuri?”

“Unajua kwa muda mrefu nilikuwa najiuliza maswali , kwa mfano kwa mwanamke kama Rose kutokana na namna alivyolelewa ni sawa tu kuwa na mwanaume bila ya kutegemea kuolewa na asione shida , lakini kwa wewe. Mage Dorisi na wengine mngechagua maisha mengine mazuri zaidi , kuliko kuwa katika mahusiano yasio na malengo, najua naweza kuonekana labda ni mkatili lakini angalau napaswa kuwa mkweli , siamini kama kuna kitu kikubwa ambacho mnaweza kukipata kwenye mahusiano haya mnayo endelea nayo”Aliongea Edna na kumfanya Nasra furaha yake kupotea na alishika glasi yake na kunywa kidogo juisi kwa kutumia mrija.

“Edna ni kwamba unanionea huruma au unaniona kama mwanamke niliepotea?”

“Sijamaanisha hivyo , siku zote nimekuwa mwenye kuamini maamuzi yako na tumefahamiana kwa muda mrefu sana, na nilichokuuliza ni swali nililokuwa nalo kwa muda mrefu sana”

“Kwa swali hili naaweza kusema ndani ya moyo wako unatuchukia na kumchukia Roma pia , si ndio?”

“Vipi kuhusu wewe , nadhani lazima ufikirie hivyo kwani mwanaume unaempenda ndio huyo huyo ambaye amenioa mimi , haijatokea siku ukanichukia kwa sababu hio?”Aliuliza Edna.

“Nadhani sasa nimepata majibu kwanini wiki hii yote ulionekana kukosa utulivu , wasiwasi wako upo kwa Rufi ,unaogopa Roma anaweza kuleta mwanamke mwingine kama mpenzi wake.

“Hapana sio kwamba nina hofu , anaweza akafanya kile anacho taka na sio kwamba nina uwezo wa kzmzuia”

“Unadanganya , unaonyesha kabisa umechukia”Alikandamiza zaidi Nasra

“Hata kama nimechukia unahisi nitafanyaje , vipi kuhusu wewe huna hofu kwa yeye kuongeza wanawake wengine zaidi , au ni kwasababu sio mume wako , unafikiri hayo ni mapenzi kuona sawa tu akiongeza michepuko kadri anavyojisikia?”Aliongea Edna huku sauti yake ikionekana kama ya kulalamika , ni kama alikuwa akimlaumu Nasra kuwa na mahusiano na Roma na wanawake wengine.

“Edna umebadilika sana , sijawahi kudhania unaweza kutia huruma kiasi hiki”Aliongea Nasra huku akionyesha kama hasira zinaanza kujitengeneza.

“Nataka unipe jibu la swali langu?”

“Unajua nini , nilikuwa nikikuonea wivu sana wewe ni mrembo kuliko mimi na hata kipindi ambacho mume wako alikuwa na wanawake wengi nje hukuonyesha ishara yoyote ya kuathirika kwasababu uliamini kila kitu kipo chini ya kiganja cha mikono yako , unajua nini kipindi chote hiko kwangu wewe ulikuwa kama mwanga, namaanisha kila saa nilipofikiria namna ulivyo ilinifanya niyachukie maisha yangu , nilijua siku zote nitakuwa wa pili na sio kwangu tu hata kwa Rose na wengine wote hakuna ambaye anaweza kukutoa katika nafasi yako”

“Edna hivi unadhani naendelea kubakia kwenye hii kampuni kwasababu nina deni la kulipa kwa yale ambayo mama yako alinifanyia? Hapana , naijua thamani yangu na huenda mpaka sasa ningeshaondoka kwenye kampuni na kwenda kwenye kampni nyingine kufanya kazi au kuanzisha ya kwangu , nimekaa ndani ya kampuni ya Vexto kwasababbu yako sio mtu mwingine , ulinihakikishia kwamba Vexto ndio sehemu ambayo natakiwa kuwepo , hata kama inaleta kashkashi na uhusiano wangu na Roma lakini licha ya yote niliona hapa ndio sehemu ambayo napaswa kubakia ili kukupa sapoti”Ijapokuwa alikuwa akiongea kwa sauti ndogo lakini alionyesha kuongea kwa hisia na usiriasi wa hali ya juu.

“Edna ambaye namwangalia kwasasa naona kama ni mgeni mbele ya macho yangu ,Edna ambaye anaogopesha kwa ukauzu wake , mwenye kujiamini na mwenye maamuzi naona kama hayupo tena , ninachokiona kwasasa ni Edna ambaye muda wote anajishtukia na mke ambaye anajichukia yeye mwenyewe”Aliongea na kisha akasimama na kuchukua pochi yake.

“Edna nimekuja kugundua jinsi ulivyokuwa mjinga , hauna taarifa zote za wapi unaelekea na bado hujajua maana halisi ya maisha, hujaishi wala hujakaa kuyafurahia maisha kwasababu bado huelewi maana ya maisha nini , acha kulaumu kwa kutoridhika kwako , kujishtukia kwako sio kosa letu wala sio kosa la Roma bali ni wewe mwenyewe.

Mahusiano sio kama kitabu kwamba ukisoma utaelewa , bali unatakiwa kuruhusu hisia zako ili kuyahisi yalivyo.

Kwa upande wangu kuwa na mwanaume ambaye ananipenda na kuwa tayari kukutana na mimi muda wowote inanitosha kabisa , mwanaume ambaye yupo tayari kuingia katika hatari kwa ajili kutafuta madawa ambayo yatanisaidia kuendelea kuwa kijana milele hio ni tosha kabisa na siwezi kuomba kitu kingine na kitu pekee ambacho naweza kumlipa ni uaminifu wangu kwake, nitamfanya atambue kwamba ninafuraha sana kuwa nae katika mahusiano.

Edna nisikilize kuna kipindi katika maisha yangu nilijali sana cheo cha mume na mke lakini kwasasa najua ni nini kinanifanya niwe na furaha na hilo ndio swala linalonifanya nijihisi kuridhika.

Kama unahitaji mwanaume ambaye muda wote atakidhi haja zako na kuendeleza hadhi yako basi naweza kusema itafikia kipindi Roma atakuja kutambua wewe kuwa mke wake yalikuwa makosa”Baada ya mchepuko kumaliza ngonjera zake alisimama na kisha akaondoka ndani ya eneo hilo.

Edna hata keki ambayo siku zote alikuwa akiipenda aliona haikuwa nzuri tena, juisi ya Strawberry hakuitamani tena , hamu yake ya kula ilikuwa imeyeyuka kabisa na sasa kilichobaki ni woga , hasira pamoja na wasiwasi wa kutokuwa salama kama mwanamke.

Muda huo huo wakati akiwa amezama kwenye mawazo ya kutafakari maneno ya Nasra, alihisi kivuli cha mtu kusimama mbele yake.
 
SEHEMU YA 511.

Edna aliweza kumtambua mtu ambaye amesimama mbele yake baada ya kuinua shingo yake.

“Hanson , nini tatizo?”Aliuliza Edna kwa kutumia lugha ya kingereza.

Mgeni aliekuwa amesimama mbele yake alikuwa ni Hanson akiwa amevalia suti yake ya rangi nyeusi , alikuwa amesimama huku akimwangalia Edna kama mtu ambaye amekosa neno la kuongea na baada ya Edna kumuuliza nini tatizo alisogea zaidi mpaka kwenye kiti cha wazi ambacho alikaa Nasra.

“Mind if I sit?”Aliuliza akimwambia kwamba je hatojali kama atakaa.

“Unaweza kukaa bila shaka lakini mimi naondoka”Aliongea Edna huku akisimama , kauli yake ilionyesha kabisa hakuwa hata na mudi ya kuongea na Hanson.

“Subiri”Aliongea na kumzuia

“Edna tunapaswa kuongea”

“Kuhusu nini??”

“Kwanini umeamua kukataa pendekezo zuri la kiiashara nililowakilisha kwako , ulikuwa ni mpango ambao umekamilika na unajielezea kuhusu namna kampuni ingenufaika na sio pesa tu lakini pia ushawishi wa kampuni yako kwa makampuni mengine ungeimarika , BMW sio kampuni ndogo”Aliongea lakini Edna alionyesha kutopendezwa na mazungumzo hayo.

“Maamjuzi tayari yamekwisha kufanyika na hata hivyo ni kampuni yangu na sitaki mtu anielekeze namna ya kuiendesha”Aliongea na kumfanya Hanson kushangazwa na kauli yake , lakini bado hakukata tamaa.

“Edna listen to me, give the proposal more thougth , there shouldn’t me any reason for you to reject it”

Edna alimwangalia Hanson namna ambavyo alikuwa akibembeleza kwa kutia huruma, hata hivyo alikuwa ni mtu ambaye alifahamina nae kwa muda mrefu lakini licha ya kwamba hakutaka kuwa na ukaribu nae bado aliheshimu ule urafiki uliokuwepo mwanzo.

“Okey nitakupa dakika tano tu ya kunielezea tena mpango wako wote na kama utashindwa kunishawishi ndani ya dakika hizo chache , basi maamuzi yangu yatabakia kuwa yaleyale”

Dakika chache zilizopita alifanya maamuzi kwasababu ya Roma , lakini muda huo kuna kitu kilimwambiwa kwamba alifanya makosa ndio maana alitaka kumsikiliza tena Hanson.

Edna ilibidi kukaa tena chini na kumfanya mzungu Hanson kuanza kukusanya mawazo yake ili kumshawishi Edna kukubaliana na mpango wake.

Wakati huo Blandina alikuwa amekwisha kufika ofisini kwa Edna na aliambiwa na Recho kwamba Edna katoka hayupo ofisini.

Blandina mara baada ya kupewa taarifa hio hakutaka kukaa sana hapo , hata hivyo alifika kwa ‘excuse’ ya kutaka kuona ofisi ya Edna, kwani tokea arudi nchini hakuwhi hata kutia mguu katika kampuni.

Lakini mara baada ya kupatia taarifa kwamba Edna katoka alijihisi mnyonge lakini hakulaumu kwani aliamini Edna ni mtu bize sana ukizingaia na ukubwa wa kampuni yenyewe, kwanza mara baada ya kufika ndani ya jengo hilo na kupewa taarifa kwamba lote lipo chini ya kampuni alishangaa mno maana ni jengo refu na kubwa.

Wakati akikunja kulia ili aelekee mtaa wa posta mpya mara aligeuza macho yake kuangalia upande wa mgahawa uliokuwa kulia kwake na kwasababu alikuwa akisubiria taa ya kijani iwake kuruhusu apite hivyo alipata muda wa kuangalia mazingira na muda uleule aliweza kuiona sura ya Edna ndani ya mgahawa huo na alijikuta akitabasamu na kuanza kutafuta nafasi ya kupaki gari ili amfuate.

Baada ya taa ya kijani kuwaka alisogeza gari lake kwenda mbele na kuliegesha mbele ya mgahawa wa vyakula vya kichina na kisha akashuka kuanza kurudi nyuma kwenye mgahawa.

Lakini sasa kilichomfanya kusimama ni mara baada ya kugundua Edna hakuwa peke yake bali mbele yake alikuwepo mwauame wa kizungu ambaye amevaia suti.

Pale pale alijihisi kuingiwa na mawazo ya kijasusi mara baada ya kuona keki mezani ambayo imeliwa nusu huku wote wakiwa wanajuisi, ilikuwa ni nadra sana kumuona mwanamke na mwanaume ambao hawana mahusiano kula keki pamoja hususani kwa wakati kama huo ambao muda mchache tu Edna anapaswa kurudi nyumbani.

Sasa swala hilo kidogo lilimshitua mama mkwe kwani mwanaume ambaye alikuwa akiongea na Edna alikuwa mzungu mtanashati mno halafu alionekana kuendana na Edna ki umri.

Kutokana na uzoefu wa kuwajua wanawake wengi wanavyoshobokea watu weupe , alihisi huenda kuna mahusiano yanaendelea.

Kiasilia ni kwamba Blandina alikuwa amejawa na mawazo hasi , kwani aliamini ni ngumu sana kwa mambo ya kibiashara kuongelewa mbali na ofisi tena wakati huo wa maongezi keki kuhusika kabisa tena na juisi.

Alianza kujishauri arudi kwenye gari yake kuondoka hilo eneo au amfuate Edna ili kujua nini kinaendelea , kama mama mzazi alikuwa akihofia siku zote ndoa ya mtoto wake , kutokana na uwepo wa wanawake wengi hivyo kudhania siku moja Edna anaweza kumkatia tamaa mtoto wake, kwani hata siku hizo zote wakati Roma akiwa amesafiri aliweza kumuona Edna kutokuwa na furaha.

Alijikuta akighairi na kuona huenda hakuna mahusiano bali ni maongezi ya kibishara tu , hivyo aliona ni bora kurudi , lakini alijikuta akigeuza tena uso wake mara baada ya kumuona yule mwanaume akimshika mkono Edna.

Upande wa mgahawani licha ya Hanson kujielezea vizuri Edna alishindwa kabisa kushawishika .

Upande wa Hanson alijua kabisa pendekezo la kibiashara halikuwa na tatizo kabisa , bali tatizo alikuwa yeye mwenyewe kutokana na kutoelewana vizuri na Roma.

Edna hakuona haja ya kuendelea kubakia hapo , hivyo baada ya kukataa kwa mara ya pili alisimama ili kuondoka , lakini Hanson mzungu kutokana na ile hali ya kubembeleza alijikuta anamshika Edna mkono kumsihi akubaliane nae.

Kitendo kile hata Edna mwenyewe hakuwa amekitarajia , kwani hata kipindi ambacho walikuwa chuoni licha ya kwamba walifahamiana na Hanson kumtongoza yeye mara kwa mara lakini haijawahi kutokea kwa Hanson hata kumshika mkono wake.

“Edna najua maamuzi yako yote pia yamezingatia mume wako , lakini nakuahidi kma utakubaliana na hili dili basi baada ya makubaliano nitaacha kila kitu chini ya wasaidizi wangu na nitarudi Norway .

“Achia kwanza mkono wangu”Aliongea Edna huku akijaribu kujitoa kwake , lakini Hanson alionekana kuushikilia vyema, sasa haikuweleweka kwanini mtu kama Hanson ambaye familia yake ilikuwa ni matajiri kuwa ‘obsessed’ na kampuni anayoongoza Edna kwani kulikuwa na makampuni makubwa tu ambayo angeweza kufanya nayo biashara.

“Edna tumefahamiana kwa muda mrefu na hii ndio mara yangu ya kwanza kumuomba mtu kitu kwa kubembeleza”

“Hanson I said let go of my hand”

“Give me a reason first”Aliongea Hanson huku awamu hii akiwa ni mwenye kuonyesha hasira.

“Hanson for the last time”Alionya Edna akimwambia kwamba kwa mara ya mwisho aachie mkono wake, alikuwa na hasira mno , huenda Edna hajawahi kuonekana hivyo na hata Hanson mwenyewe alijikuta akiachia mkono wake.

“Kwanini unakataa hili dili Edna?”

“Kuna kampuni nyingi ndani ya Tanzania ambazo zinahali nzuri ya kiuchumi kwanini usoombe ushirika nazo , ukweli unang’ang’ania kampuni yangu kwasababu zako binafsi , huenda ni kwasababu ya familia Roma anayotokea , hivyo jibu langu ni kwamba biashara zangu sitaki zihusiwe na maswala ya mume wangu”

“Edna acha kunisingizia mambo ambayo sijafikiria”Aliongea awamu hii na kumsogelea Edna kutaka kumshika tena , lakini Edna alionekana kukosa uvumilivu kwani alijihisi ni kama anadhalilishiwa na baadhi ya watu waliokuwa ndani ya hilo eneo waliowaona kama wapenzi ambao wanagombana.

Kitendo cha Hanson kutaka kumshika Edna lilikuwa ni kosa kwani akili ya Edna ilikuwa kwenye utahadhari wa kujilinda , hivyo wakati akiwa anainua mkono wake ili kumsukuma asimsogelee, haukuinuka mkono tu, kwani Hanson alikutana na wimbi la upepo la ajabu ambalo lilimsukuma palepale na kudondoka chini na kuvaa meza iliokuwa nyuma yake.

Hanson alishangazwa na kitendo kile , kwani hakuelewa kwa namna gani kimetokea kwani alijikuta tu akisukumwa na nguvu ya ajabu ,ilikuwa afadhali kwake kwani eneo hilo halikuwa na watu wengi kwa muda huo kwani wangeshangaa kuona kupigwa na mwanamke.

Edna hakuwa na sababu ya kuendelea kubakia licha ya kwamba hata yeye mwenyewe hakujua ni kwa namna gani ameweza kuziita nguvu za kijjini na kumsukuma Hanson , lakini hakutaka kujali , hata hivyo mambo kama hayo yalitokea kipindi cha nyuma akiwa kwenye hatari ya kutaka kubakwa na Desmond ambaye ni kaka yake.

Mita kadhaa kutoka katika makutano ya barabara ambayo yanatengeneza T alionekana Blandina akiwa kwenye gari yake akiwa ametulia akisubiria taa za za trafiki kumruhusu kuendelea na safari , muda huo alikuwa ameshikilia simu yake huku akipangusa kuangalia picha alizofanikisha kumpiga Edna na mwanaume wa kizungu.

Wakati alipoona mwanaume yule akimshika mkono , alijihisi kuwa na wasiwasi pamoja na woga kwamba Edna huenda akawa na mwanamke nje ya ndioa , hivyo kama binadamu pepo la kupiga picha lilimvaa palepale na ndio maana akatoa simu yake na kufanya kazi hio.

Adeline aliekuwa mita kadhaa na mgahawa aliishia kushangazwa tu na kitendo kile , lakini kwasababu alikuwa akimfahamu Blandina ni mama wa mfalme Pluto hivyo asingeweza kuchukua hatua yoyote , lakini ingekuwa ni mtu mwingine basi palepale angeenda kumpokonya mtu huyo simu.

Wakati akiwa kwenye mawazo namna ya kudili na picha hizo , alijikuta akshtuliwa na honi ya gari lililokuwa nyuma yake na kumfanya aziweke chini na kuendesha kusonga mbele huku akifikiria uamuzi wa kumuonyesha Roma picha hizo ili amkanye yeye mwenyewe .

Baada ya masaa kadhaa aliweza kufika nyumbani na kupokelewa na Lanlan ambaye alisharudi kutoka shuleni na alikuwa nje akicheza na mbwa wake akiwa na Qiang xi.

Lanlan mara baada ya kumuona bibi yake alimkimbilia na kumrukia kwa furaha na kumfanya Blandina kutabasamu a hata ile hali ya kimawazo kupungua kidogo lakini hata hivyo kukosa kwake furaha kulikuwa wazi kiasi cha kumfanya Qiang Xi kuhoji.

“Are you okay , you don’t look so good”Aliongea Qiang Xi na kumfanya Blandina kutabasamu kivivu.

“I am fine I guess my age is catching up on me”Aliongea akimaanisha kwamba labda ni kwasababu ya umri wake kuanza kumuathiri.

“Kwa umri wako bado sana”Aliongea Qiang Xi akijaribu kumpoza bibi yake Lanlan na Blandina aliishia kutingisha kichwa tu huku akimwelekeza baadhi ya vitu vingine ameacha kwenye buti la gari avichukue huku yeye akiingia ndani.

Muda huo huo wakati Blandina akipatwa na hamu ya kujaribu kumpigia Roma simu ili kujua kama anaweza kurudi nyumbani siku hio mlango wa kuingilia ndani ulifunguliwa na Roma.

“Wifey , Mama , Chubi nimerudi..”Roma alionekana kuwa na furaha kweli ni kama huko alikotoka kuna kitu amepata kwani aliingia na makelele ya kuita kila mmoja.

Wa kwanza kuamka alikuwa ni Lanlan ambaye alifyatuka kama mshale huku akitanguliza ngumi mbele na Roma hakumkwepa na kumuacha amfikie na kisha akamdaka.

“Bad dady, Bad dady ,I saidi never call me chubby”

“Baba mbaya , baba mbya , nimesema usiniite kibonge”Aliongea Lanlan na kumfanya Roma kutoa cheko.

“Kwahio kukuita Chuby ndio unanipokea baba yako kwa kipigo , ukiendelea hivi nitakumeza mzima mzima”Alitania huku akimshika pua yake na kuiminya na Lanlan aliishia kujinasua kutoka kwa Roma na kukimbia.

“Acha kumuogopesha mtoto hivyo , nadhani licha ya kuwahi lakini hufahamu kesho kuna nini?”

“Tena nilikuwa na mpango wa kurudi kesho , lakini simu yangu ilinikumusha ratiba ya kesho ndio maana nikarudi mapema , nimemsindikiza Rufi mpaka anapoishi atakuja kesho kwa ajili ya kujumuika na sisi”Aliongea Roma na Blandina alitingisha kichwa chake kwa kukubali.

“Roma nifuate mpaka sebule ya juu kuna kitu nataka kuongea na wewe”Aliongea huku yeye mwenyewe akitangulia na kumfanya Roma kushangaa kwani haikuwa kawaida kwa mama yake kutaka kuongea nae ghafla tu mara baada ya kurudi lakini aliishia kupandisha juu.

“Roma hivi humuoni Edna kama ana tatizo hivi karibuni?”Aliuliza Blandina mara baada ya Roma kuingia.

“Unamaanisha nini mama , sijakuwepo hapa kwa zaidi ya siku kumi nitajuaje kama kuna tatizo linaendelea?”

“Ni kwamba… je unafahamu Edna anakutana na watu wasioeleweka nje ya ofisi?”Aliongea na kumfanya Roma kucheka.

“Mama hilo najuaje , Edna anaenda kazini kila siku na anakutana na watu wengi ambao ni wateja wake wakubwa , je ni kuhusiana na hilo?”

“Kwanini usiongeze umakini wako katika watu wanaomzunguka?”Aliongea na kumfanya Roma sasa kuelewa mama yake anajaribu kumaanisha nini.

“Mama niambie kama kuna chochote ulichoona au kusikia usizunguke zunguke”Aliongea na palepale Blandina alitoa simu yake na kwenda upande wa picha na kisha akamwonyesha Roma.

“Hanson..!!”Aliongea Roma mara baada ya kuona ile picha.

“Unamfahamu huyu mzungu , jina lake ni Hanson si ndio?”

“Mama..!!”Roma aliita huku akionekana kama mwenye huzuni ya ghafla.

“Umetoa wapi hizi picha?”

Blandina ilibidi haraka haraka aelezee kila kitu alichoona kwa macho yake baada ya kwenda ofisini kwa Edna na kuwambiwa ametoka na kisha kumkuta katika mgahawa akiwa na mwanaume mzungu wakiwa wanakula keki .

“Baada ya kuzipiga nilikosa ujasiri wa kuziangalia tena , nilitaka kumfuata na kumuuliza nini kinaendelea lakini niliona nina hasira kali na naweza kumshuku kwa jambo ambalo sio la kweli ndio maana nikajizuia na kuona ninahitaji maelezo ya kutosha zaidi”Aliongea na kumfanya Roma kupumua akimwagalia mama yake na kisha alimrudishia simu yake.

“Hapa tatizo sio Edna bali ni huyu Hanson , ni watu wanaofahamiana tokea walipokuwa chuoni na Edna alinielezea kila kitu na hata mimi mwenyewe nishawahi kumshuku mara moja lakini kwa maelezo yake ilinifanya nimwamini . akirudi kutoka kazini unaweza kumuuliza tu na atakwambia ukweli kwani sioni kama kunaweza kuwa na tatizo kubwa”

“Ah.. kwahio unamaanisha alikwua ni mwanafunzi mwenzake , basi nadhani hakuna tatizo kwasababu unamfahamu, nilikuwa na wasiwasi kwani tabia za wanawake wa siku hizi hazieleweki na hawakawii kubadilika”

“Mama tangu lingi ukawa na imani kidogo kiasi hicho kuhusu mimi , siwezi kuruhusu mtu kama Hanson kuyaingilia maisha yangu na isitoshe Edna kwa ninavyomjua mimi sio rahisi kutokea kuanzisha mahisiano na mwanaume yoyote, yupo makini na anajielewa sana na kwa hapa naamini lazima huyu Hansin kalazimisha kushika mkono wake”

“Okey nimekuelewa , labda ni mawazo yangu potofu tu , naamini upo sahihi kuliko mimi , hata hivyo pia nilitamani kuisikia ninachohisi sio cha kweli, najua pia namna ulivyo na wanawake wengi huko nje , lakini wewe ni mtoto wangu siwezi kuruhusu kuona mwanamke anakosa uaminifu kwako”Aliongea na kumfanya Roma kuona wasiwasi wa mama yake lakini alijitahidi kumtoa hofu kwani yeye ndio ambaye anamjua Edna vizuri kuliko mtu mwingine.

Baada ya kukaa kwa muda mrefu kidogo hatimae saa kumi na mbili za jioni Edna alirudi akiwa amechelewa kidogo kuliko isivyokuwa kawaida.

Baada ya kuingia ndani na kumuona Roma aliingiwa na hisia mchanganyiko za kufurahi kumuona amerudi akiwa salama na nyingine za wasiwasi akifikiria huenda kuna kitu kimetokea kati yake na Rufi.

Roma mara baada ya kusalimiana nae na kumwelezea safari yake ilivyoenda Edna aliachia tabasamu, lakini Roma alionyesha kidogo kutokuwa sawa kimawazo kutokana na wasiwasi wa Edna na ilimfanya kuanza kukumbuka picha alioonyeshwa na mama yake na kuhisi moyo wake kushituka.

“Umepitia magumu mengi , ngoja nikabadili nije nisaidie kuandaa chakula ule ushibe”Aliongea Edna na alipandisha kwenda juu.

Baada ya dakika chache aliweza kurudi chini akiwa tayari kwenye mavazi ya nyumbani na kabla hajaelekea jikoni Roma alimzuia.

‘Wifey nimekuletea zawadi”Aliongea Roma na palepale alitoa mkono wake alioficha nyuma na kumuonyesha.

Muda huo na Blandina alikuwepo eneo la sebuleni akiangalia wana ndoa hao, ijapokuwa Roma alionekana kumwamini Edna lakini yeye bado hakumamini.

Lilikuwa jiwe la kung’aa sana kama vile ni Tanzanite , lakini lenyewe rangi yake ilikuwa ni ya Zambarau

“Oh! My how pretty”Qiang Xi aliekuwa aktokea jikoni aliweza kuona kitu hiko kinachong’aa na kushindwa kujizuia , kipindi hicho alikuwa akielewa ligha ya kiswahili licha ya kwamba ulimi ulikuwa mzito kuongea.

“Ni jiwe linalofahamika kwa jina la Amethisto(amethyst rock) nililitoa katika moja wapo ya migodi ya kuchimbia madini katika mpaka wa Brazil, linaweza kutokuwa na thamani kubwa lakini lina faida kubwa , nilifikiria kukaa kwako mbele ya tarakishi muda mrefu litakuondolea uchomvu na kama utaliweka karibu linaweza kufyonza pia miale hatarishi ya mwanga wa kompyuta”Aliongea Roma na kisha alimwinamia sikioni kuongea kwa namna a kunong’oneza.

“Baada ya kuliona nililificha ili Rufi asilione , kwani angelihitaji wakati mimi nilitaka nipate kitu cha kukupa zawadi wewe mke wangu kipenzi”Aliongea na kumfanya Edna kujisikia vizuri lakini bado hakutaka kumchangamkia kwani bado alikuwa na hasira kwa yeye kwenda mbali huko akiwa na Rufi peke yao.

“Ni zawadi nzuri , asante nimeipenda”Aliongea kivivu na kupokea kisha akaweka kwenye meza na kwenda jikoni moja kwa moja.

Sasa namna ambavyo alipokea ile zawadi ilimfanya mama mkwe kubetua mdomo kwani aliona kabisa Edna kuna kitu cha siri anaficha lakini kwasababu Roma alionekana kumwamini aliona akae kimya kwanza mpaka atakapopata muda sahihi.

……………..

“Edna leo nilikuja kazini kwako , niliona nikutembelee nione ofisi yako lakini pia kukuelezea kuhusu siku ya kesho kukusindikiza kwenda kuzuru kaburi la mama yako”Alivunja ukimya Blandina wakati wakiwa mezani na kumfanya Edna kushangaa.

“Ulikuja ofisini?mbona sikuambiwa “Aliongea huku akionyesha mshangao lakini kwa wakati mmoja akijisikia vizuri kwamba mama mkwe alikuwa akikumbuka siku muhimu kama hio.

“Nadhani sekretari wako alisahau”

“Ungenipigia simu tu mama , sikuwa hata mbali , nilikuwa upande wa pili mgahawani”Aliongea na kumfanya Blandina kuona huo ndio wakati sahihi wa kuingizia lile swala ili kuona kama Edna angeongea ukweli.

“Oh.. ulikuwa mgahawani , mbona ulichelewa kula chakula cha mchana , ulikuwa peke yako?”Aliuliza na kumfanya Roma ambaye alikuwa akishindana kula na Lanlan kupunguza spidi baada ya kusikia kauli ya mama yake ili asikilize majibu.

“Sikuwa peke yangu nilikuwa na Nasra , alitaka kula keki hivyo nikamsindikiza”

“Ulikuwa na Nasra tu ? hakukuwa na mtu mwingine?”Aliongea na kumfanya Roma kuona mama yake anavuka mipaka.

“Mama acha kumuuliza maswali kama vile unamhoji , ashakuambia alikuwa na Nasra , Si ndio Edna?”Aliongea Roma na kumfanya Edna alazimishe tabasamu lakini mikono yake ilianza kuloa jasho, ni kweli alikuwa amekutana na Hanson ambaye alikuwa akimbembeleza lakini aliofia akiweka swala hilo wazi Roma anaweza kukasirika na kupatwa na mauwazo ya kimauaji na isitoshe sio kwamba alikuwa kwenye mgahawa kwa ajili ya Hanson bali yeye ndio aliemkuta hapo.

“Mama kwanini unauliza hivyo , nilikuwa na Nasra kama nilivyokujibu , tulikuwa sisi pekee na hakukuwana mtu mwingine..”Aliongea Edna bila kuonyesha wasiwasi lakini jibu lake ni kama lilibadilisha mwonekano wa Blandina na hata Edna alionekana kuona hilo.

“Mama nini kinaendelea?”

“Siwezi kusema kama ulikuwa na Nasra kwani niliona mtu mwingine tofauti”Aliongea na kisha alitoa simu yake na kutafuta picha aliopiga na kumpatia Edna.

Maongezi hayo yalifanya wanaokula kukosa utulivu na kushindwa kujua nini kinachoendelea na hata Bi Wema aliona Blandina angeanzisha maongezi hayo baada ya chakula.

Baada ya Edna kuona picha hio sasa aliweza kujua nini Mama mkwe alichokuwa akiongelea , hali ile ilimfanya Roma kumwangalia Edna kama vile mtu anaehitaji majibu.

“Toa majibu”Aliongea na akamfanya Edna kuvuta pumzi na sura yake kuanza kupauka kwa wasiwasi.

“Mama .. ulikuwa ukinifatilia kwa nyuma?”Aliuliza Edna huku sauti yake ikibadilika na akaanza kuonyesha hasira kiasi kwamba hata Lanlan ambaye alikuwa akila aliacha na kumwangalia mama yake kwa hofu.

“Miss punguza hasira , hili ni swala ambalo linaweza kuzungumzika na likaisha”Alishauri Bi Wema lakini Edna alikuwa na hasira kali mno kiasi kwamba machozi yalianza kumtoka palepale kwani ni kama alikosewa.

“Mama unanishuku?”

“Nilikuchukulia kama mwanamke mwaminifu katika wote , lakini kwanini ulishindwa kuongea ukweli?”

“Nilikuwa na sababu zangu na kama hiko unachomaanisha ni kweli , kwanini mimi siruhusiwi?”Aliongea kihasira.

“Unafikiri ni sahihi?”Aliongea na kumfanya Edna kutingisha kichwa chake kwa masikitiko.

“Sijawahi kudhania kama unaweza kunifikiria hivyo?”

“Unavyomfanyia Roma ndio inanifanya nikufikirie vibaya , hivu unajua nilipomuonyesha Roma hizi picha alisemaje? Alianza kukutetea huku akisema kwamba utaongea ukweli hivyo nikuulize , alijaribu hata kunishawishi nikuamini, lakini unapata ujasiri wapi kutudanganya”Aliongea na kumfanya Edna kwa hasira kumgeukia Roma.

“Oh,, naona ulikuwa ukinitetea, umeona hizo picha na ukadhania mimi ni mwanamke muhuni ndio maana ukaona unyamaze bila kuniambia , nadhani sasa naelewa ulitaka mama aje anifokee yeye na kuanza kunihoji kwasababu ya woga wako?”Roma hata yeye alikuwa amejikatia tamaa na kuona huenda kuna kilichoendelea , lakini alikasirishwa na namna Edna anavyomlaumu.

“Edna kwahio unahisi labda nimemtumia mama kukuhoji si ndio?”

“Kama sio hivyo ni nini?”

“Jaribu tena kuongea kauli yako uone”

“Kwahio unahisi nitaogopa , unachukiza sana”

“Yaani nimekuamini na moyo wangu wote halafu unaniambia nachukiza?”Aliongea Roma huku awamu hii akipandisha sauti.

Blandina kwa mabadiliko hayo aliona kabisa amefanya makosa kwani ni kama amcwasha moto ambao yeye mwenyewe hawezi kuuzima , muda uleule alimpa ishara Qiang Xi kumtoa Lanlan hapo na kumpeleka juu ili kumuepushia kuona wazazi wake wakigombana.

“Naona kwako ni sahihi kuniona kama mwanamke ambae sijielewi , okey sawa”Aliongea Edna kwa hasira na kisha alisimama, hakujali tena kile alichovaa bali alichukua ufunguo wa gari yake kwenye meza na kutoka nje kwa kukimbia.

Roma alikuwa na hasira kiasi kwamba alishindwa kujua ni maamuzi gani ayachkue zaidi ya kukunja ngumi chini ya meza.

“Roma amka umfuate , hakikisha unamchimba mpaka aseme ukweli”Aliongea Blandina na kumfanya Roma apumue kwanguvu na kisha akasimama na kutoka nje.

Edna kabla hajawasha gari tayari Roma alishamfikia na kumshika mkono wake asifanye anachotaka kufanya.

“Unataka kufanya nini?”Alikoroma.

“Achia mkono wangu nakuambia”Aliongea Edna kwa jazba.

“Kwahio ndio unakimbia?”

“Nikimbie niende wapi , wakati kuna watu wako umewaweka kunifatilia kwa kila ninachofanya”

“Edna unaongea upuuzi gani , mama alikuona kwa bahati mbaya na sio kwamba nilimpa kazi ya kukufatilia”

“Oh.. kwahio ndio ilikuwa hivyo”Aliongea na kumfanya Roma kuzunguka kama kichaa na kisha kuinama tena kuchumngulia Edna aliekuwa ndani kwenye gari.

“Edna una nini wewe leo , kama kweli mama kakosea basi elezea ukweli wote , waambie hujakutana na Hanson na hamkushikana mikono , hata kama mama alishindwa kujizuia na kuishia kukupiga picha lakini haimfanyi kuwa mkosaji na kama ungeeleza ukweli asingepaniki”Aliongea Roma kwa sauti kiasi kwamba ilisambaa eneo lote.

“Kwanini unashindwa kufikiria nje ya mstari na kuruhusu hisia zako zichukue nafasi, kama sio tabia yako ya kutaka kumuua Hanson kisa tu kaja ofisini kwangu unafikiri ningeficha ukwel?i, kwanini kila kitu unataka kunibebesha lawama , wewe ulikuwa wapi muda wote , unao ujasiri wa kulala nje ya nyumba , unao ujasiri wa kutembea na mwanamke mwingine kuizunguka dunia lakini mara baada ya kurudi nyumbani ni kuanza kunisingizia mambo ambayo sijafanya”

“Kwahio unafikiri safari zangu za nje ya nchi ni kwa ajili ya kula bata na mwanamke si ndio? , nimetoka kwenda huko huku nikihatarisha maisha yangu kwa sababu yako kukutengenezea vidonge ambavyo vitakufanya kuwa na urembo wako huu bila kuzeeka..

Kama uwezo wangu usipokuwa mkubwa unadhani nitaweza kuwalinda , unafikiri nitaweza kulinda kila mmoja ndani ya familia , vipi kuhusu Lanlan nitamlinda vipi nikiwa dhaifu?.

Kuondoka kwangu na Rufi hakuepukiki kwani yeye anao ufahamu mkubwa kuhusu nguvu za mbinu na ardhi , hivyo hivyo lilikuwa swala la lazima ili anielekeze vile vitu ambavyo sina uelewa navyo , mtoto wa watu hakuwa hata na uwezo wowote wa kujilinda lakini hakujali chochote zaidi ya kunisaidia , kwanini unamfikiria vibaya?”

“Kwahio unachomaanisha hapa umeenda kuhangaika huko kwa ajili yangu na Lanlan si ndio , wanawake wako wengine hawahusiki katika hilo si ndio unachomaanisha? Ndio najua upo sahihi kuhusu Rufi kwani anakusaidia, na sio mimi tu Mage na weingine wote ni wanawake wenye msaada kwako na hata kuanza kufikiria labda sikutoshelezi na ni kosa umefanya kunifanya mkeo si ndio?”

“Edna sijawahi fikiria hivyo?”

“Lakini ndio ninachokiona?”Aliongea ilionyesha dhahiri alikuwa akichanganya na kauli za Nasra za mchana.

“Kwanini umekosa kuniamini , kama unaona labda nina mahusiano na Hanson na kama inakuuma kwanini usimuue tu, si upo vizuri kwenye kuua wewe ?”

“Kwahio unanipandishia si ndio?”

“Mimi sijali , nadhani utaacha kuwa na wasiwasi na kunisingizia mambo ya kipuuzi kama atakuwa mfu”Aliongea na kumfanya Roma akose neno , ukweli asingemuua Hanson licha ya kuona kama tishio kwenye mahusianno yake, lakini aliona ni kupotezaa muda na kuongeza tu idadi ya watu aliowaua.

“Achia mlango wa gari yangu”Aliongea Edna kibabe na kumfanyaRoma ashindwe kushindana nae tena na kuishia kuwa mpole.

Na Edna bila ya kumjali tena alizungusha ufunguo na kuliwasha gari na palepale mlango wa geti ulijifungua wenyewe na akatoka nje kwa spidi isiokuwa ya kawaida.

ITAENDELEA JUMAPILI
0687151346-WATSAPP
 
Back
Top Bottom