Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 514.

Tarehe mbili ya mwezi wa sita ndio safari ya kwenda Korea ilianza rasmi, Edna ilikuwa mara yake ya kwanza kwenda Korea tofauti na Roma ambaye alishawahi kufika mara kadhaa, hivyo kwake alikuwa kama mwenyeweji.

Edna alikuwa na shauku ya kuona jiji la Seoul kwani ndio mahali ambapo tamthilia nyingi za kikorea zilikuwa zikiigiziwa na isitoshe kwa kipindi hiko alikuwa mpenzi kweli wa filamu hizo.

Upande wa Roma sio kwamba alikuwa na shauku kubwa ya kwenda Korea , kwake taifa kama hilo alilichukulia kama dogo kwenda na isitoshe hakuwa na koneksheni sana Korea tofauti na mataifa ya Amerika na Ulaya , lakini kwasababu alikuwa akienda kwa ajili ya Yezi hakujali sana kukaa muda mrefu kwenye ndege japo swala hilo kwake hakulipenda kwani alijiambia alikuwa na uwezo wa kupaa tu na kuibukia moja kwa moja Korea kuliko kupoteza muda , lakini kwasababu ya Edna aliona afuatishe hatua za kawaida za kibinadamu.

Jini la Seoul lilikuwa na joto la wastani , hakukuwa na baridi sana wala joto sana kwa mwezi huo, ki ufupi hali yake ya hewa ni ile ya kuzoeleka kwa wepesi.

Muda wa jioni ndio ambao waliweza kutua na ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Incheon.

Park Jonghyun ndio mtu ambaye alipewa jukumu la kuwapokea kiwanjani hapo na baada ya kuwaona wageni wake alijjikuta akifaurahi huku akipeana nao mikono ya salamu kwa ukarimu wa hali ya juu akiwakaribisha Korea.

“Yezi amewakumbuka sana , alitaka hata kuja hapa kuwapokea lakini yupo na ratiba ya masomo na mwalimu wake Vivian hivyo kashindwa kufika”Aliongea Park Jonghyun.

“Teacher Vivian ? is she a westerner?”aliuliza Edna akimaanisha je huyo mwalimu Vivian ni mzungu , kwani ni ngumu kwa Korea kukutana majina ya aina hio .

“She is not a westerner but a Tanzanian woman who is fluent in english and Korean my grandfather’s proffesor from states recommended his best student”Aliongea akimaanisha kwamba sio mmagharibu bali ni mwanamke wa kitanzania ambaye anajua kuongea lugha ya kikorea na kingereza na moja wapo ya Profesa kutoka Marekani ambaye ni rafiki yake na Park Juan ndio alimpendekeza Vivian kumfundisha Yezi.

“Kwanini mnabana sana na masomo wakati ana muda wa kutosha wa kwenda chuoni?”Aliuliza Roma kwa kikorea na Edna hakutaka kuingilia maongezi yao tena zaidi ya kugeukia dirisha kuangalia mandhari ya jiji hilo la kuvutia.

Seoul ulikuwa mji mkubwa wenye miundombin ya kuvutia , ilimfikirisha Edna na kujiambia jiji hilo lingekuwa Tanzania angejivunia sana.

Baada ya madakika kadhaa ya kuwa barabaranni hatimae waliweza kufika kwenye jumba la kifahari la Park Juan ambalo lilikuwa ndani ya wilaya maarufu ufahamikao kama Gangnam.

Lilikuwa jumba kubwa mno ambalo lilimfanya Edna kuona kweli Yezi amekuwa mtoto wa kishua sio kwa mandhari nzuri kama hio.

Kwa haraka haraka Roma aligundua kuna zaidi ya watu waliokuwa wakiwasubiria hapo ndani , kwani nje kulikuwa n magari mengi ya kifahari yaliokuwa yameegeshwa.

Kwanzia mlangongi mpaka ndani kulikuwa na wahudumu waliokuwa wamejipanga mstari wakiwainamishia vichwa kwa heshima , jambo ambalo lilimmfanya Edna kushanganzwa na utamaduni huo , lakini mara baada ya kukumbuka kwenye filamu za kikorea maisha yapo hivyo alituliza mshangao wake.

Baada ya kuingia ndani kabisa ya eneo la sebuleni waliweza kukutana na watu wengi wa rangi nyeupe wakiwa wamesimama kwa ishara ya kuwakaribisha ni mtu mmoja pekee ambaye alikuwa amekaa huku akiwa ameshikilia fimbo ya kutembelea.

Alikuwa ni Park Juan na Roma na Edna waliweza kumtambua kwani alikuwa maarufu na isitoshe picha zake washawahi kuziona mara kibao.

Upande wa Roma mara baada ya kuwakagua watu wote waliokuwa hapo ndani mtu pekee aliemvutia ni bwana wa makamo ambaye alikuwa amekaa nyuma ya Sofa ambalo amekalia Park Juan , uso wake kwa namna ambavyo ulikuwa ukionekana ni kama mtu ambaye hakujali chochote ambacho kinaendelea hapo ndani na macho yake yote yalikuwa kwenye mkono wake wa kulia ambao alikuwa ameshikilia gololi atu akizichezesha kwa kuzisuguanisha.

Roma kwa haraka haraka aliweza kugundua mtu yule alikuwa ni hatari sana , licha ya kwamba hakuwa na nguvu za kijini kama yeye na hisia zake zilimwambia lazima atakuwa ni Bodigadi wa babu yake yezi yaani Park Juan.

Upande wa kulia alikuwa amesimama Park Jiyeon na Haoming na kwa ufupi aliokuwa nao Haoming alimfanya kuonekana mdogo mbele ya Park Jieyeon.

Msichana mwingine mrembo ambaye aliwashangaza Roma na Edna simwingine bali ni msanii Yoon Hee .

Kwa namna alivyojipamba ilimfanya kupendeza zaidi na kutokana na weupe wake lipsi zake nyekundu zilionekana vizuri zaidi , alikuwa amevalia kitop cha rangi nyeusi cha mkato wa V huku shingoni akiwa amejifunga scarf.

“Karibuni sana , naona mmeshangazwa kuniona hapa?”aliongea Yoon Hee kwa kingereza huku akimwangalia Roma kwa kebehi.

“YoonHee kuwa mtaratibu?”Alifoka Park Juan.

“Yes grandfather”Alijibu.

“Mr Roma na Miss Edna nice to meet you , mimi ni shangazi yake na Yezi nafahamika kwa jina la Park Jiyeon na huyu ni mume wangu anaitwa Haoming , Yoonhee ni mtoto wetu wa kike , asanteni kwa kumkarimu vizuri alipokuwa Tanzania”aliongea Park jiyeon huku akionyesha tabasamu.

Roma na Edna sasa waliweza kufahamu kumbe YoonHee na Yezi ni wajukuu wa Park juan.

Utofauti wao tu ni kwamba Yezi yeye alikuwa ni mtoto wa mtoto wa kwanza wa Park Juan na Yoonhe alikuwa ni mtoto wa Park Jieyeon , hivyo mwenye uzito zaidi katika familia alikuwa ni Yezi kwa tamadunni za Korea,

Roma alikumbuka kitu kipindi cha nyuma nchini Tanzania Yoonhee aliweza kugombana na Park Jonghyun na walionekana kama walikuwa wapenzi na palepale alijiuliza je hawakuwa ndugu?

Baada ya utambulisho mfupi Park Juani aliwaonyeshea ishara ya kuketi na ni muda huo huo ambao waliweza kusikia sauti wanayoifahamu ikiwaita.

“Bro Roma , Sister Edna”Alikuwa ni Yezi ambaye alitokea huku akikimbia kushuka ngazi kwa shangwe.

Walikuwa hawajamuona kwa kipindi kirefu na waliweza kumuona ameongezeka na kuwa mzuri zaidi , nywele zake zilionekana kuwa nyeusi zaidi tofauti na alivyokuwa Tanzania , ijapokuwa waligundua alikuwa amekonda kidogo lakini ilimfanya kupendeza zaidi na zaidi.

Roma alijiambia Rufi alikuwa akianza kuwa kama mkorea halisi sasa na kwa uzuri wake hakuhitaji kufanya hata upasuaji wa sura ili kuonekana mrembo kama ilivyotabia za wanawake wengi wa Korea.

“Kuwa makini usije ukadondoka”Aliongea Park Juan kwa sauti akimtahadharisha mjukuu wake na aliweza kuonyesha wasiwasi namna ambavyo Yezi anashuka kiasi kwamba Edna na Roma waligundua kuna mapenzi makubwa sana kati ya Yezi na babu yake.

Upande wa Yoonhee alijikuta akibetua mdomo kwa kejeli ni kama alimuona Yezi ni kituko , alionyesha waziwazi hakuwa akimpenda , lakini Yezi hata hakulitambua hilo kwani macho yake yote yalikuwa kwa Roma na Edna na alianza kumkumbatia Roma na kisha akahamia kwa Edna.

“Jamani siamini kama mmefika , nilitaka nije niwapokee lakini mwalimu wangu amenizuia , nimejikutaka hata nikipoteza mudi kwasababu hio”

“Ulikuwa ukosoma hadi muda huu?”aliuliza Edna na Yezi alijibu kwa kingereza ili kumfanya na babu yake asikie.

“Mwalimu Vivian ni mkali sana na babu hataki hata kunisaidia?”Aliongea na kumfanya Park Juan kucheka.

“Naweza kuruhusu ufanye kila unachotaka , lakini siwezi kukuona unacheza likija swala la masomo yako , maelfu ya watu wanaweza kupoteza ajira zao kama hutakuwa na elimu ya kutosha ya kuongoza kampuni”Aliongea Park Juan na kuwafanya watu waliokuwa hapo ndani kuona wivu ndani kwa ndani huku wakiweka tabasamu bandia katika nyuso zao.

Muda huo huo mwanamke mwingine mrembo alionekana akishuka kutoka juu kwa madaha kabisa , alikuwa amevalia gauni ambalo limeishia magotini pamoja na koti kwa juu alionekana kuwa mrembo mno na rangi yake ya kiafrika.

“Teacher Vivian you’ve worked hard , stay back and have dinner with us”Aliongea Park Jonghyun ambaye alikuwa akimwangalia Vivian kwa macho ya matamanio kweli.

“Najma…!!”Roma ndio aliekuwa wa kwanza kumtambua Najma, jina la Vivian lilikuwa jipya kwake na ukijumlisha na mavazi yake ya kisasa ndio kilichomfanya kutomfahamu kwa haraka na sio kwake tu hata kwa Edna vilevile na aliweza kumtambua mara baada ya kumsikia Roma anaita hilo jina.

Najma hata yeye alishangazwa na uwepo wa Roma na Edna hapo ndani na mshtuko wake uliwafanya kila mmoja kushangaa na kuamini lazima wanafahamiana.

Edna alijikuta maswali kibao yakiianza kupita kwenye kichwa chake , tokea siku ambayo aliweza kupata taarifa kutoka kwa Suzzane juu ya Najma kukatisha ufadhili wake wa masomo , sasa alishangaa Najma ambaye alikuwa akiitwa Vivian yupo nchini Korea lakini hakutaka kuumiza kichwa sana aliamini ana muda mzuri wa kuongea na Najma.

“Kwahio wewe ndio mwalimu Vivian?”Aliongea Edna huku akijitahidi kutabasamu , Najma alikuwa ni rafiki yake wa kwanza kukutana nae katika kituo cha kulelea watoto cha Son and daughter orphanage.

Roma alijikuta kumbukumbu zake zikimpeleka nyuma sana kipindi ambacho ndio kwa mara ya kwanza anafika nchini Tanzania , namna alivyoweza kukutana na Najma na kumpokea kwa ukarimu na kumpatia chumba katika nyumba yao na kupanga , alikumbuka vitu vingi namna mrembo huyo alivyotokea kumpenda na yeye kumpotezea.

Ijapokuwa Najma yule na huyu walikuwa mtu mmoja lakini Najma mpya alikuwa wa tofauti sana , huyu alionekana kama mwanamke aliekomaa kiakili mno na kuzidi kustaarabika.

Najma wa kipindi kile alikuwa akivaa Hijab lakini huyu alikuwa kichwa wazi huku nywele zake zikiwa ndefu zilizowekwa dawa ya kupendeza na ilikuwa ni kama ameachana na maswala ya dini.

“Mr Roma and Mrs Edna its been a long time”Aliongea kwa kingereza cheye rafudhi safi na kauli yake iliwashangaza mno Park jonghyun na wengine.
 
SEHEMU YA 515.

Baada ya eneo lote kuwa kimya babu yake Yezi alianzisha yeye mazungumzo

“Mwalimu Vivian , lazima leo upate chakula cha usiku kwani marafiki zako wapo hapa”Aliongea kwa lugha ya kikorea.

“Asante Sir”Alijibu , asingeweza kukataa mwaliko wa Parl Juan kwani angeonekana kama mtu ambaye anawakimbia Roma na Edna.

Upande wa Park Jonghyun alijikuta akikunja ndita baada ya kuona namna ambavyo Najma anamwangalia Roma, kwake aliona ni kama vile amefurahi sana na macho yake yalikuwa kama mtu ambaye amepata kuona kitu cha thamani alichopoteza muda mrefu

Hata Roma na Edna waliona Najma amefurahia kuwaoana na kumfanya Roma kumwonea huruma kwani kwa mwonekano wa Najma aliona kabisa hakuwa amemsahau , lakini Roma kwa namna yoyote alijiambia Najma alikuwa kwenye kundi sawa na Sophia , alijiambia ni wanawake ambao anapaswa kukaa nao mbali kwasababu ya Edna.

Yezi alimwangalia Roma na kisha akamwangalia Najma na kumfanya kujawa na shauku ya kutaka kujua maisha ya mwalimu wake yalivyokuwa nyuma.

Wote kwa pamoja walikusanyika katika meza ya dining na wafanyakazi waliandaa chakula kilichopikwa kwa ufundi wa hali ya juu , ilikuwa sio jambo la kushangaza kwa familia kubwa kama hio kuita wapishi wakubwa kuandaa chakula.

“Mr Roma kuna sababu mbili ambazo zimenifanya niwaalike kuja nchini kwetu , kwanza ningependa wewe na mkeo kuhudhuria sherehe za urithishaji wa kampuni ,pili tulitaka utuletee hadhina yetu ya familia , je umekuja nayo?”Aliongea Pak Juan.

Roma aliingiza mkono wake kwenye mfuko na kisha akatoa kidani kilichochongwa kwa mfano wa mwezi kikiwa kimeunganishwa na mkufu , kila alipokuwa akiangalia kidani hiko alishindwa kuelewa nini cha pekee.

“Ndio, hiki ndio chenyewe , hiki kidani nilimpa mwanangu wa kwanza , hatimae kimeweza kurejea nyumbani, Kim Jip nisaidie kukishikilia”aliongea huku akikichunguza na kisha akampatia mwanaume aliekuwa nyuma yake afahamikae kwa jina la Kim Jip , alikuwa ndio mlinzi wake na kwa jinsi Roma alivyomuona aligundua bwana huyo hakuwa na matamanio ya mtu mwingine hapo ndani zaidi ya bosi wake tu.

‘Babu unapaswa kunipa mimi kwasababu ushakipata tayari , ndio kitu pekee ambacho niliachiwa na wazazi wangu”Aliongea Yezi

“Usijali mjukuu wangu , nitakupa vyote viwili hiki na cha kwangu cha kundi la nyota baada ya sherehe ya kampuni, nitakupa kila kitu changu usijali …”Aliongea na kumfanya Yezi atabasamu kwa furaha , kwa jinsi Edna na Roma walivyomuona Yezi ni kwamba aliweza kuwa na uhusiano wa karibu sana na babu yake.

“Babu hivyo vidani vina maana gani?”Aliuliza Yoonhe na kumfanya Park jiyeon kumgusa mtoto wake mgongoni akimwashilia kukaa kimya.

Wakati huo upande wa Najma alikuwa akimwangalia Roma kwa kumchunguza kwa sekunde na kisha alirudisha macho yake chini , alikuwa akifanya hivyo mara kwa mara huku mikono yake akiwa ameishikilia chini ya meza akionyesha namna ambavyo alikuwa na wasiwasi na kukosa utulivu.

“Mzee hebu sema , kuna watu wengine ambao tunawasubiri sijala chochote tokea mchana”Aliongea Roma mara baada ya kuona mabakuli yamefunikwa tu na hakuna ambaye anaanza.

Park Juan licha ya kwamba alikuwa mzee kweli lakini Roma kumwita Mzee kilimfanya mwonekano wake kuwa katika hali isioelezeka.

“Upo sahihi, nina tangazo nataka kutoa siku ya leo , hivyo nimearika wageni wengine waheshima kuungana na sisi”Alijibu.

Muda huo huo baada ya kumaliza kuongea, mlio wa ngurumo za magari ambayo yalikuwa yakiingia ndani ya nyumba hio ulisikika na kwa namna ambavyo yalisikika kwa nje ilionyesha kuna ugeni wa watu wengi waliokuwa wakifika.

Baada ya dakika, vijakazi waliwakaribiasha wageni hao , wa kwanza kuingia alikuwa ni mwanaume wa makamo, mkorea alievalia suti huku nywele zake akiwa amezichana kwenda nyuma , nyuma yake alikuwepo pia mwanaume mwingine mtanashati kijana , mkorea ambaye amevalia koti refu(trench coat) rangi ya ugoro , huku akiwa amevalia jeans huku akiwa na nywele zake zilizokuwa ndefu zikuwa zimerudishiwa nyuma, kwenye mikono yake alikuwa ameshikilia funguo ambazo Roma baada ya kuziangalia kwa haraka haraka aligundua zilikuwa ni za Ferrari , ilikuwa kama alivyotabiri kwani alisikia mngurumo mkubwa wa gari ukiingia na alijua lazima ni aina ya Sport car

Kulikuwa na mwanaume mwingine nyuma yao walioambatana nae, alikuwa amevalia suti nyeupe na alikuwa na nywele zake za rangi ya kijivu, miwani ya fremu ya dhahabu iliomfanya kuonekana zaidi kuwa mpole na mtu mtaratibu , lakini pia mkononi alikuwa ameshikilia briefcase(mkoba).

“Raisi Gong Gyechung naona umefika hapa na Gong Woo”Aliongea kwa kikoerea Park Jiyeon huku akioa tabasamu na kumfanya yule mwanaume alietangulia kucheka kidogo.

“Mjomba Park tusamehe kwa kuchelewa kwetu , tumetoka uwanja wa ndege kumpokea Dokta Lee Eunjeong ndio maana”Aliongea akimaanisha yule mwanaume ambaye amevalia suti nyeupe ndio ambaye alifahamika kwa jina la Dokta Lee Eunjoeng.

“Nimesikia habari zako raisi Park , nafahamika kwa jina la Lee Eunjeong,daktari bingwa wa upasuaji”Aliongea akijitambulisha yule mwanaume na kufanya watu waliokuwa hapo ndani kushangazwa na utambulisho wake , hawakuelewa kwaninni baba yake kaalika daktari bingwa wa upasuaji.

“Unajitahidi kujishusha sana Dokta, kila mmoja hapa naomba mumtambue Mkurugenzi na Dokta , Lee eujeong ambaye analiheshimisha taifa , sio tu kwamba ni mkurugenzi na mganga mkuu wa hospitali ya chuo ya Seoul lakini pia anafanya kazi kama mshauri katika idara ya upasuaji wa moyo pamoja na Ini nchini Marekani katika chuo cha Harvard”Aliongea Gong Gyehung.

Upande wa Edna alipotaka kusimama ili kumsalimia mara baada ya kusikia utambulisho wake Roma alimrudisha chini.

“Kuna haja gani ya kusimama na kumsalimia wakati humjui, mimi mwenyewe sijasimama”Aliongea Roma na kumfanya Edna aone Roma kaongea jambo la maana , hakuwa mahali hapo kwa ajili ya kazi hivyo akaamua kumsikiliza Roma.

“Mr Roma , Mrs Edna mnaweza msiwe mnawafahamu wati waliopo mbele yenu kwasababu mnatokea Tanzania , ukoo wa Gong ndio unaoongoza katika maswlaa ya Elimu ya chuo ndani ya taifa letu hususani upande wa maswala ya kitabibu , wanamiliki vyuo vingi na ni washirika hai wa karibu na baadhi ya mataifa makubwa kutoka Ulaya na Amerika ya kaskazini, Gong Gyechung ndio kiongozi wa ukoo na Gong Woo ni mtoto wake”Aliongea Park Juan na kuwafanya wale wanaume wawili kugeuza macho yao na kuwaangaliaRoma na Edna.

“Hawa ndio marafiki zetu kutoka Tanzania?”Aliuliza Gong Gyechung .

“Ngoja nikutambulishe kwako , huyu ni Miss Edna Adebayo raisi wa kampuni ya kimataifa ya Vexto na wa pembeni yake ni mume wake anaefahamika kwa jina la Roma Ramoni mtoto wa raisi wa taifa la Tanzania, Yezi ana deni kubwa kwao”Aliongea Park Jonghyun.

“Kampuni ya Vexto!? Unamaanisha kampuni ya kitanzania ambayo iliingia mkaba wa usambazaji wa malighafi mpya na kampuni ya Yamakuza kutoka Japan?”Aliongea Gong Woo huku akionyesha dharau kwa jinsi alivyokwa ameweka uso wake.

Upande wa Edna hakuwa akifahamu kikorea hivyo hakuelewa nini kilichokuwa kikiongelewa na alimwangalia Roma akiwa na uso kidogo uliochanganyikiwa na Roma ilibidi kumtafsiria palepale.

“Upo sahihi na hata koti ambalo umevaa limetokana na malighafi mpya ambazo kampuni yangu na Yamakuza i inasambaza na kudhalisha , asante kwa kuwa mteja mtiifu”Aliongea Edna kwa kingereza na kuwafanya wote waliokuwa hapo ndani kucheka.

Gong Woo ambaye alikuwa ashaanza kuonyesha dharau alitaka kuongea jambo lakini baba yake alimzuia.

Muda huo huo wakati wageni waliotangalulia wakikaa mlango ulifunguliwa tena , ilionekana kuna wageni wengine zaidi ambao walikuwa wakihudhuria.

Ilikuwa ni bahati kwmaba jumba hilo eneo la kulia chakula lilikwa kubwa hivyo isingekuwa tabu kufanya watu wengi kuweza kutosha kabisa.

Muda huo huo wanaume wawili wa kizungu warefu waliovalia buti za leather waliingia huku nyuma yao alikuwa ni mwanamke mrembo pia wa kizungu ambaye aliwashangaza kila mmoja aliekuwa hapo ndani.

Roma alijikuta hata yeye akishangaa kwani hakuwa akimtegemea Clark ndani ya nchi hio na hata kwa Clark hivyo hivyo alishangazwa kumuona Roma na Edna hapo ndani.

“Roma , Miss Edna why are guys here too?”Aliuliza akimaanisha kwamba na wao wanafanya nini hapo ndani pia.

“Mr Roma unafahamiana nae?”Aliuliza Park Juan na kufanya kila mmoja kumgeukia Roma , kila mmoja alikuwa ameguswa na urembo wa Clark ambaye ametokea ghafla.

“Ndio Clark ni rafiki yangu , na sikutegemea kama nitamuona hapa’Aliongea Roma .

Wakati walipokuwa London Clark hakumwambia Roma juu ya safari ya kuja Korea na waliachana akiwa anaelekea Marekani kwa ajili ya kufanya upasuaji

“Raisi Park huyu ni mwalimu wetu , tumemwalika kutoka Royal Academy of science , alitakiwa kuwepo hapa wiki moja kabla lakini kwasababu ya ubize wa kufanya upasuaji wa kawaida , alichelewa kufika”Aliongea mwanaume wa kuzungu ambaye aliingia na Clark na kufanya jopo lote kushangazwa kwani hakuna mabaye alitegemea kuona msichana mrembo wa umri mdogo kama huyo kuwa na wanafunzi wakubwa namna hio.

“Mr Park wanafunzi wangu , Vincent na Wallen wamenipa historia yako ya kimatibabu na nishaiangalia tayari , ninaweza kukufanyia upasuaji, nikishamaliza kufanya uchunguzi wa mwili wako na kufanya pia upembuzi”Aliongea

“Upasuaji?”Park Jieyeon ndio aliekuwa wa kwanza kushangazwa na maneno ya Clark.

“Upasuaji gani , au ni ugonjwa uliokuwa nao baba?”Aliuliza na hakuwa yeye tu ambaye alikuwa kwenye mshangao , kila mmoja alikuwa akijiuliza kwanini Park Juan anataka kufanyiwa upasuaji.

“Nadhani mmeshangazwa kwanini nimemuagiza Gong Gyechung na Doka Vincent kualika madaktari wabobezi, kwanza kabisa nilimfanya Dokta kutoa taarifa isiosahihi kuhusu afya yangu ili kumfanya mjukuu wangu Yezi kurudi nyumbani, ni kweli nina saratani ya ini , lakini haimaanishi kwaba siwezi kupona”

“Nilijua tu kuna kitu hakipo sawa katika taarifa yako , ulisema una saratani ambayo haiwezi kupona ilihali ndio imegundulika hivi karibuni na haileti maana kwa mtu mwenye hela kama wewe kushindwa kutibu tatizo la ini kwani machaguo ya kimatababu yapo mengi..”Aliongea Roma na kisha akafunua mabakuli na kuanza kujisevia msosi bila kujali macho yao, alikuwa akitimiza kauli maarufu isemwayo ‘jisikie upo nyumbani’/

“Ni watanzania wote wenye tabia kama yako , Mr Park hajanza kula wewe unapata wapi ujasiri wa kuanza?”Aliongea Gong Woo.

“Nina njaa ndio maana ninakula, inakuuma nini wakati hapa sio kwenu, mwenye nyumba katulia lakini wewe ni mwendo wa kiherehere, unanifanya nikufananishe na wale Enuch wa kwenye tamthilia zenu”Aliongea Roma na kumfanya Gong Woo kupandwa na ghadhabu.

“Hey Gong Woo haina haja ya kuwa hivyo kwa mgeni?”Aliongea Gong Gyechung akimtuliza na kisha akamgeukia Roma.

“Tafahdari naomba umsamehe mtoto wangu kwa tabia yake”Aliongea na kumfanya Park juan hata asijali mazungumzo yao na kumgeukia Dokta wa kizungu ambaye alikuwa na ndevu nyingi.

“Dokta Vincent asante kwa kusafiri umbali mrefu kwa ajili yangu?”

“Ndio jambo ambalo tunapaswa kufanya , umekuwa ukitufadhili kwenye projekti zetu nyingi na tunafanya kila namna kukulipa fadhila , lakini kwa bahati mbaya hatuna ujuzi wa hali ya juu ndio maana tukamualika mwalimu wetu”Aliongea huku akiweka sura ya ukarimu.

“Kama ni hivyo naomba uelezee kuhusu hali ya ugonjwa wangu”aliongea na kumfanya Dokta Vincent kutingisha kichwa na kuanza kuelezea hali ya Park Juan.

“Kutokana na utambuzi(diagnoss) wa shida yako naweza kusema ni ngumu kuondoa seli za ini ambazo zina chembe chembe za saratani , vipimo vya x ray vinaonyesha hepatic cirrhosis ambayo haitibiki , hivyo tunachpaswa kufanya ni kukubadilishia ini mapema iwezekanavyo na hakutakuwa na tatizo kama kila kitu kikienda sawa”

“Unamaanisha Liver Transplant , si utakuwa upasuaji mkubwa sana huo?”Aliuliza Park Jonghyun akionyesha wasiwasi wa maigizo kiasi kwamba hata Yezi aliliona hilo.

“Babu kama kuna uwezekano wa wewe kupona kabisa nashauri ufanya huo upasuaji”Aliongea Yezi.

“Usijali mjukuu wangu , hatuwezi kuharakisha mambo ndio maana nimewaita madaktari bingwa na wabobevu , ninachotaka ni wao kunihakikishia kama upasuaji unawezekana kuwa na asilimia mia za mafanikio”Aliongea na sasa wakaanza kuelewa juu ya mpango wake.

Vincent na Wallen walikuwa ni madaktari bingwa kutoka Calfornia ambao walikuwa wanahusika moja kwa moja na idara ya hepatolojia na ilionyesha Park juan alihitaji kuaminishwa na madaktari hao wakubwa mfanikio ndio akubali kufanyiwa upasuaji.

“Babe huyu mzee ni kama wewe tu , maisha yake ni ya kimitego mitego”Aliongea Roma kwa Kiswahili akimania Edna.

“Kaa kimya na endelea kula”Aliongea Edna na kumfanya Roma kuendelea kula chakula chake kwa adabu.

“Sir, Dokta Lee umaarufu wake katika upasuaji wa ini ni mkubwa mno na anafahamika ndani ya Marekani , lakini pia ni daktari mkubwa tu ndani ya taifa letu nadhani itakuwa vyema kama utamtegemea kukufanyia upasuaji , nadhani hata DoktaWallen na Vincent wana mawazo sawa na mimi”Aliongea Gong Gyechung.

“Ni kweli hata mimi nishawahi kumsikia Dokta Lee kutoka chuo cha Harvard nilipokluwa Calfornia , nimeona baadhi ya majarida yakimzungumzia kwa ubobevu wake , naomba nikupe hongera kwa ufanyaji mzuri wa tafiti zako Dokta Lee”Aliongea Dokta Vincent.

“Sifa zako ni nyingi kwangu , nimesikia kuhusu wewe pia , madaktari wawili ambao mnakesho inayong’aa.., nimesikia pia kuhusu Miss Clark lakini kwa bahati mbaya alifanikiwa kufundisha katika chuo cha john Hopkin pekee, Idara yetu ndani ya Havard itafutahishwa kama utakuja siku moja kufundisha wanafunzi wetu”

Ijapokua Clark alikuwa maarufu na mbobevu katika fani ya kitabibu lakini mara nyingi alifanya kazi zake akiwa ndani ya mataifa ya ulaya hususani UK, lakini watu wengi kutokana na umri aliokuwa nao hawakuamini uwezo wake na kumdharau , hususani katika vyo vya Duke, Columbia na Harvard.

Vyuo hivyo walikuwa na vigezo vikubwa pamoja na wanasayansi wenye umaarufu mkubwa hivyo haikuwa rahisi kuweza kuvutiwa na kila mmoja .

Na hata hivyo kama utafananisha chuo cha John Hopkin na Harvard katika maswala ya mafunzo ya tabibu basi Harvard lazima kishike namba moja ndio kifautie hiko.

Hivyo moja kwa moja Dokta Lee aliamini yeye ndio ambaye atafanikisha kumfanyia upasuaji tajiri Park kutokana na ukubwa wa jina lake , lakini pia ukubwa na ubora wa chuo ambacho alikuwa akitokea.

Kumfanyia upasuaji mtu mkubwa kama tajiri Park halikuwa jambo dogo , kwa mtu yoyote ambaye angafanikisha, moja kwa moja angezidi kuwa maarufu zaidi na kutafutwa na madaktari wengi ndio maana alikuwa akitaka nafasi hio kwa udi na uvumba.

“Wakati nikiwa chuoni nilikuwa mvivu sana , na hata sikuhudhuria chuoni mara kwa mara nadhani ndio maana vyuo vikubwa nchini Marekani hawaamini katika uwezo wangu”

“Ndio maana nakushauri usikadirie kwa kiasi kikubwa uwezo wako kwasababu tu una umaarufu”Aliongea Dokta Lee akijaribu kumshauri Dokta Clark na palepale alitoa karatasi kwenye mkoba aliokuwa nao na kuzishikilia mkononi.

“Sir nimefanikiwa kupitia kumbukumbu za matibabu yako na sidhani kama kutakuwa na shida yoyote kuhusiana na ubadilishwaji wa ini lako”aliongea huku akijaribu pia kushikiria picha ya X-Ray.







SEHEMU YA 515.

Park Juan mara baada ya kusikia maneno chanya kutoka kwa Dokta Lee alionyesha kufurahi..

“Kama ndio hivyo mnaonaje tukiendelea kwanza kula wakati huo Dokta Lee akituelezea kwa ufasaha namna ambavyo upasuaji utafanyika, nimefarijika kuona unajiamini”

Aliongea na wengine wote walitingisha vichwa , kwanza walikuwa na njaa na hakuna aliekuwa na ujasiri kama wa Roma kuanza kula kabla ya kukaribishwa.

“Mafanikio ya kubadilishiwa ini siku zote yamekuwa yapo juu , baadhi ya vitu ambavyo vinachangia mafanikio hayo ni kulandana kwa ini linaolotolewa na linalowekwa(compatilibility of liver), Umri wa mgonjwa lakini pia hali ya ini la mgonjwa , hivyo tutahitaji kwanza kuweza kumpata mchangiaji wa ini linaloendana na wewe mapema iwezekanavyo, kuhusu umri wako na shida ya Liver Cirrhosis sio tatizo kubwa, mpango ni mimi kufungua tumbo lako na kisha kuanza kusafisha mishipa ya damu kwa haraka , nitakuwa makini na kuzuia damu kutovilia ndani kwa ndani na kufanya ini lako kubaribika na kisha nitaondoa uvimbe wote wa saratani na kuacha nafasi ya kutosha ya msihipa ya ya damu ya ini kuungana na ini jipya…”

Ijapokuwa watu wengine hawakuelewa kuhusu mpango wake lakini waliridhishwa na namna ambvyo alikuwa akijiamini.

Vincent na Walen walikuwa wakipatwa na wasiwasi juu ya mwalimu wao ambaye muda woe alikuwa bize na kutafuna nyama ya pweza kana kwamba kinachoongelewa hapo hakikuwa kikimuhusu. .

Walikuwa wakimkubali sana Clark, ijapokuwa Dokta Lee alikuwa daktari bingwa maarufu lakini hakuwa akimfikia Dokta Clark kwa namna yoyote ile, hivyo hali ya Clark kutoonyesha kukasirika au mwonekano wake kutotafsrika iliwafanya kuwa katika hali ya wasiwasi.

Upande wa Park Juan sio kwamba alikuwa tayari moja kwa moja amemruhusu Dokta Lee kumfanyia upasuaji , madhumuni yake ya kuitisha chakula hicho cha usiku ilikuwa ni kwa ajili ya kuangalia ni daktari gani angeweza kumwamini na kisha kumruhusu kumfannyia upasuaji.

“Kuhusu taarifa nyingine nitazielezea baada ya kupata ini?”Alimalizia Dokta Lee na kumfanya Park Juan kutingisha kichwa kwa kurishidhwa na maelezo yake.

“Wewe ni dokta Clark , je una maoni yoyote juu ya hali yangu ya kiafya?”Aliuliza.

Clark alikuwa bize kutafuna nyama ya pweza akiwa na mwonekano usioelezeka na baada ya kuulizwa swali hilo alijilamba midomo kwanza na kisha akajibu.

“Nadhani Dokta Lee amefanya kazi nzuri katika kutolea maelezo hali yako , upasuaji utaenda vizuri kama kila kkitu kitakuwa sawa , sina neno la kuongezea”

“Ni kutokana na uzoefu wangu kama daktari , upasuaji wa kubadilisha ini ni mgumu lakini ni mwepesi kwa wakati mmoja na kama tu utaweza kunichagua mimi kama daktari wako’Alijisifia Dokta Lee huku akimwangalia Park Juan.

Kila mmoja alionyesha kutoridhishwa na maneno ya Clark kwani , hawakutarajia kwamba atamsapoti dokta Lee katika upasuaji huo.

“Mwalimu kwanini umeshindwa kuongea chochote , hatuwezi kuwaachia wakafanya wao upasuaji’Aliongea dokta Vincent ambaye alionyesha kutoridhishwa.

“Dokta Lee anafanya haya yote kwa ajili ya kumsaidia mgonjwa na amefanya kazi nzuri kuandaa kila hatua ya matibabu , haya sio mashindano bali malengo ni kumsaidia mgonjwa , hatuwezi kuweka maslahi mbele”

Ijapokuwa bado hakurishidhwa na maneno ya mwalimu wake lakini aliishia kukubliana nae , ni kweli hakukuwa na haja ya kushindana kama mgonjwa angeweza kupona.

Chakula kiliendelea kulika , huku hali ikionekana kuwa tulivu , upande wa Roma alikuwa bize na chakula na hakuwa hata na ule ujasiri wa kumwangalia Najma aliekuwa mbele yake.

Upande wa Najma hakula chakula kingi zaidi ya muda wote kuongea na Yezi.

Upande wa Park Jongyun alijitahidi kumuonyeshea upendo Najma kwa kumsogezea bakuri la supu ya kuku iliochanganywa na mzizi wa Ginseng na Najma alichukuwa kidogo tu na kisha kumwambia ameshiba, ni kwamba hakutaka kile ambacho alikuwa akikifanya kwenye meza.

Upande wa kijana mtanashati, mkorea bwana Gong Woo , alikuwa akimwangalia Edna kwa wakati na kisha akamwangalia na Profesa Clark , ijapokuwa wawili hao wote kwake walionyesha kuwa tofauti , yaani Edna kuwa mwafrika na Clark kuwa mzungu lakini uzuri wao kwenye macho yake ulikuwa wa viwango na kushindwa kujua yupi anamzidi mwenzake.

“Mkurugenzi upasuaji wako utaenda vizuri kabisa chini ya dokta Lee, nadhani baada ya kupona tuanze sasa kuzungumzia swala la ndoa”Aliongea Gong Gyechung na kufanya kila mtu kushangazwa na kauli yake maana hakuna ambaye amemuelewa ni nani ambaye anakwenda kuolewa na kuoa.

“Ukoo wetu haujawafanyia mazuri kwa muda mrefu”Aliongea Park Juan huku akiweza uma chini.

“Tafadhati haina haja ya kuongea hivyo, nina furaha kwamba mjukuu wako ameweza kurudi nyumbani akiwa salama … nyie watu mnaweza msielewe uhusiano wetu , lakini baba yangu mzazi na Mkurugenzi hapa walikuwa ni makomredi kipindi cha vita na baada ya kutoka jeshini dada yangu alipaswa kuolewa na Park Joonchen mtoto wa mkurugezi lakini ndio hivyo akatokea kumpenda mwanamke wa kitanzania ,hivyo ndoa ikashindwa kufanyika na kuunganisha koo zetu, kwasababu mtoto wangu Gong Woo ashafikia umri halali wa kuoa na Yezi amerudi nyumbani tumeona kile ambacho hakikufanikiwa miaka mingi iliopita kifanyike sasa hivi , natumaini ombil langu litafanikiwa , tafadhari Mkurugenzi Park idhinisha hilo”Alichokuwa akimaanisha ni kwamba Yezi aolewe na Gong Woo.

“Siwezi kuolewa nae”AliongeaYezi huku akisimama kwa mshangao mara baada ya kusikia kauli hio.

“Yezi acha kuwa mtukutu , kaa chini “Aliongea Park juan.

“Babu kweli , unataka niolewe na yeye , anaonekana mtoto kabisa wa mama huyo ambaye hajui hata kujitaftia maisha na kila kitu kutegemea wazazi wake”Aliongea na kumfanya Gong Woo sura yake kujikunja kwa maneno ya Yezi.

“Nisikilize mimi”Alifoka babu yake na kumfanya Yezi kushangazwa na jambo hilo na kujikuta akikaa chini huku akiwa amekosa amani.

“Kwanini unapatwa na wasiwasi , wakati ndio kwanza ameongea na hakuna ambaye amethibitisha kama kweli unaolewa?”Aliongezea babu yake

“Park Yezi!, Gong Woo anaweza kuwa na hasira za haraka lakini ni mkarimu sana , ndio mtoto pekee mwenye tabia nzuri karibia koo zote za kitajiri ndani ya Korea , yuko vizuri pia katika maswala ya kibiashara hivyo naamini anaweza kuwa msaidizi mzuri kwako”Aliongea Gong Gyechung. lakini upande wa Yezi maneno yake yaliingiilia sikio la kulia na kutokea la kushoto kile ambacho alikuwa akiona kwenye filamu za Kikorea ni kama alikuwa akikiona laivu sasa kikimtokea, yaani mtoto wa tajiri kuolewa na familia nyingine ya kitajiri kwa ajili ya kibiashara bali si mapenzi.

“Binadmu yangu Gong , kwanini tusiongelee hili mara baada ya upasuaji , Yezi ndio kwanza amerudi na sitaki aniache kwa haraka namna hio”

“Oh , Bila shaka , nilikuwa nikitoa pendekezo tu baaada ya kuona wote tupo hapa”Aliongea kwa kujibarguza.

Baada ya chakula hiko kila mmoja aliondoka kasoro Yezi , Roma na Edna kwani walikuwa ni wageni wa heshima ndani ya familia hio , hivyo walipaswa kulala hapo hapo.

Lakini kabla ya Najma kiuondoka waliona ni muda mzuri wa kuongea nae.

Edna alijisikia huzuni mara baada ya kusikia sababu kwanini Najma alikuwa ameamua kufuta ufadhili wake , ilionekana bado alikuwa akijiona mwenye hatia kwa kosa alilolifanya kwa kuungana na Desmond pamoja na Elvice kipindi kile na kutaka kuivunjna ndoa ya Edna , lakini pia alijiona kama mzito kwa Edna kwani alikuwa amemsaidia kaka yake lakini pia na yeye pia alikuwa akimsaidia , msaada wa Edna ulimkosesha Njma amani kabisa , licha ya kwamba walikuwa kwenye makubaliano maalumu.

Kwa maelezo ya Najma ni kwamba alipendwa sana na mmoja wapo wa Profesa ndani ya chuo cha Harvard na ilifikia wakati mpaka akamwambia kuhusu namna ambavyo hana amani na makosa ambayo aliyafanya na Profesa huyo ndipo alipoamua kutafuta namna ya kumsaidia Najma ili kuondokana na hatia.

Alianza kumtafutia ufadhili wa masomo ndani ya chuo , lakini bado jambo hilo lilionekana gumu mno kutokana na kwamba hakukuwa na sababu ya msingi ambayo Najma angeeleza uongozi wa chuo na kumpatia ufadhili.

Profesa huyo alionekana kumpenda Najma kutokana na juhudi zake za kimasomo na kuwa mwanamke wa kiafrika ambaye alionyesha kujiamini na kuwa mkarimu sana na mwenye shauku ya maisha.

Sasa wakati Profesa huyu akijitahidi kuangalia namna ya kumsaidia Najma ndipo alipoweza kupata ombi kutoka kwa rafiki yake kutoka Korea kumtafutia mwalimu mzuri mwenye kufahamu kiswahili , kikoea na kingereza ambaye pia ana ufahamu kiasi katika maswala ya uongozi wa biashara.

Baada ya kupewa kazi hio moja kwa moja ndipo jina la Najma lilimjia akilini , iijapokuwa Najma bado hakua amehitimu , lakini alijiambia kama angeenda kufanya kazi Korea kwa muda , akiwa kama yupo field basi angeweza kutengeneza koneksheni ambayo ingemsaidia kupata ufadhili wa kimasomo kupitia tajiri huyo.

Kuhusu Najma kuitwa Vivian alisema ni jina ambalo Profesa huyo alikuwa akipenda kumwita kutokana na kwamba alikuwa akifanana sana na marehemu mtoto wake, alikuwa ni Profesa mweusi ndio maana huenda ilikuwa rahisi kuelewana na Najma.

Hayo ndio maelezo ya Najma yalivyokuwa na aliendelea kusema kwamba hana mpango kabisa wa kurudi Tanzania hata kama akija kuhitimu , kauli hio ilimfanya Edna kujawa na wasiwasi na kumuonea huruma kwa wakati mmoja.

“Najma usiseme hivyo , unapaswa kurudi nyumbani kusalimia unapopata muda , kaka yako bado anakuhitaji na ndio ndugu pekee uliekuwa nae , huwezi kumtupa kwa kuendelea kuishi nje ya nchi”

“Kaka nawasiliana nae na ameniambia ashaachana na kazi yake ya kubeba mizigo na sasa anafanya kazi ya miamala na ashaoa hivyo sidhani kama anahiaji uwepo wangu zaidi ya mke wake”

“Najma huwezi kuongea hivyo , nyumbani ni nyumbani tu”

“Lakini kila ninapofikia makosa yangu nashindwa kabisa kupata ujasiri wa kurudi , angalu nikiwa nje kama hivi nakuwa na amani”Aliongea na Roma na Edna walishindwa kumshauri chochoe kwani alikuwa ni kama ashaamua.

…………………..

“Wife kwanini unaniangalia hivyo, sidhani kama kuna kosa ambalo nimefanya leo , maana nimejithidi kuwa mtiifu, kwanini unaonekana kama una hasira na mimi?”Aliongea Roma na muda huo ni mara baada ya Najma kuondoka.

“Kwahio naonekana kama mtu mwenye hasira?”

“Kwanini upo hivyo sasa kama huna hasira?”

“Haukumsikia Najma , amesema hawezi kujisamehe kwa yale aliyoyafanya”

“Nimemsikia akisema hivyo , lakini sina cha kumsaidia”

“Acha kujifanyisha huelewi , anaogopa kurudi Tanzania kwasababu anaogopa kukuona kwani bado anakupenda wakati hawezi kukupata ndio maana kaamua kukaa huku mbali”

“Mke wangu naomba tusiendelee na hii mada , Najma bado ni mdogo na naamini kabisa anaweza kupata mwanamke bora zaidi yangu”

“Kwanza ni kipi ambacho kilikufanya usiwe nae kwenye mahusiano , au ni kwasababu ya kaka yake?”

“Haikuwa hivyo , nilikuwa na sababu zangu za msingi”Alijibu Roma na kumfanya Edna asikubaliana na majibu yake maana Najma alikuwa mrembo na aliishi nyumba moja na Roma kabla ya kukutana na yeye , sasa alijiuliza katika kipindi hiko kwanini Roma kashindwa kutoka kimapenzi na Najma kwani alionekana kupenda sana wanawake warembo.

******

Upande mwingine baada kama ya nusu saa hivi kupita , kaskazini mwa jiji la Seoul ndio mahali ambapo Najma alikuwa akiishi kwenye jengo la Apartment alipopangishiwa na familia ya Park.

Sasa nje ya barabaa iliokuwa ikielekea katika jengo hilo alionekana mrembo Najma akiwa anatembea kinyonge sana huku akionyesha kuwa na mawazo kwani hata kichwa chake alikuwa amekinamisha chini.

Mrembo Najma alikuwa na mawazo mengi sana kiasi kwamba hata machozi yalianza kumtoka , alihisi kabisa ashaachana na Roma baada ya kukaa nje ya nchi , lakini siku hio mara baada ya kumuona tena alijua kabisa hakuwa amemuacha kwani alihisi moyo wake kuwa vilevile katika hali ya kumuhitaji.

Kwake Roma alikuwa mwanaume aliempenda siku ya kwanza tu kumuona mwaka mmoja uliopita na kwanzia hapo mapenzi yake kwake yalikuwa ya viwango mno.

Najma baada ya kumuona Roma alijihisi kupata matamanio ya kumkumbatia Roma , lakini alishindwa kufanya hivyo kwasababu ya Edna.

Licha ya kwamba ni kweli Edna alimsaidia katika mengi lakini moyo wake hakuacha kuuma na alijikuta kadti anavyoendelea kuishi na kukosa hitajio la moyo wake alianza kumchukia Edna kwa kumchukua mwanaume ambaye alimpenda wa kwanza , mwanaume ambaye alikuwa ndio wa kwanza kumuona na hio ndio sababu ambayo ilimfanya hata kutopendezwa na fadhila zake , kwani msaada wa Edna alianza kuutafsiri kama hela ambazo zinatumika kuziba hisia zake jambo ambalo halikuwa likiwezekana.

Wakati Najma akitembea taratibu kwa mwanga wa taa za njiani usiku huo , ghafla ilionekana gari ikisimama kando yake kwa spidi na palepale mlango wa gari ile ulifunguliwa na wanaume watatu wenye miili ya kujazia na kisha wakamkamata Najma kwa nguvu huku wakimwekea kitambaa puani.

Najma alijitahidi kujitetea lakini hakufua dafu na aliishia kulegea na kisha akaingizwa kwenye gari hio na kisha ikaondolewa kwa spidi , kilikuwa ni kitendo kilchofanyika haraka sana kiasi kwamba kutokana na eneo hilo kutokuwa na watu wengi , hakuna ambaye alishitukia namna Najma alivyotekwa kirahisi.

ITAENDELEA NAMBA YA SIMU WATSAPP 0687151346
 
SEHEMU YA 517.

Park Juan alikuwa ameketi kwenye Sofa ndani ya chumba chake cha kujisomea huku akifuatilia maendeleo ya Yezi katika masomo yake , kwa kumuuliza baadhi ya maswali ambayo alipaswa kujibu.

Licha ya kwamba Park juan hakusoma sana , lakini kutokana na uzoefu wa muda mrefu alikuwa akijua mambo mengi zaidi ya msomi wa kawaida, hivyo alikuwa akijaribu kuuliza baadhi ya maswali muhimu zaidi ambayo yalikuwa yakiendana na maswala ya kibaishara.

Alikuwa akielezea baadhi ya mambo lakini aligundua akili ya Yezi ni kama haipo hapo tofauti na siku nyingine.

“Yezi unafikiria nini? , ni adimu kwangu kuwa na nguvu ya kukuuliza maswali na kukufundisha”

“Babu sitaki kuolewa na yule mwanaume wa kukera”Aliongea Yezi na kumfanya Park Juan kushangaa kidogo lakini aliishia kucheka.

“Bado unafikiria kuhusu hilo ? kwanini niruhusu uolewe nae wakati najua sio mtu mzuri kwako?”

“Kwahio hutokubali niolewe nae si ndio?”

“Bila shaka ..”Aliongea na kisha akamshika mkono.

“Babu yako nakupenda sana hivyo siwezi kukuruhusu uoelewe na mwanaume mtukutu kama yeye , lakini hata hivyo familia ya Gong ndio moja wapo ya koo ambazo zinaushawishi mkubwa , babu yake alikuwa rafiki yangu wa karibu na kama si hivyo nisingeweza kabisa hata kukutana nao , hivyo usiwe na wasiwasi kwani nishasema kuhusu swala hilo tutazungumzia baada ya upasuaji wangu kwenda vizuri”

“Nilijua tu babu huwezi kuniangusha”Aliongea na kumfanya Park Juan kushika mashavu ya Yezi na kuyatingisha huku akitoa tabasamu.

“Walijua mimi ni mzee hivyo naweza kuwa mjinga mpaka kumwalika Dokta Lee eujeong , ni kweli nahitaji daktari bingwa na mwenye ujuzi lakini wamenidharau sana kwa kuona nitaruhusu wanidai fadhila , tutalipa gharama zote za matibabu ili waache kuota ndoto ya kukupata wewe mjukuu wangu”Aliongea.

“Ndio!, Wanataka niolewe na mtoto wao ili waweze kuchukua mali zetu kirahisi , wana nia ovu sana”

“Unaonekana kuwa na akili sana mjukuu wangu na nimefurahi kwamba umeweza kurudi kwenye maisha yangu , usijali kabisa nitahakikisha nakutafutia mtu ambaye ana tabia njema , uwezo na utanashati ili kuwa mume wako’”

“Babu kuhusu mwanaume nitamtafuta mwenye , huu ni ulimwengu wa kisasa kwanini unichagulie mume?”

“Kwanini nisikuchagulie? , au kuna mtu ambaye unampenda , usinidanganye kwani nimeishi miaka mingi kujua kile unachofikiria”Aliuliza na kumfanya Yezi kutingisha kichwa kwa haraka.

“Hapana babu sina mtu ninae mpenda na usifikirie sana kuhusu hilo”

“Yezi mapenzi sio kama mchezo haijalishi kama ni masikini , an asura mbaya au hana akili ili mradi uwe unampenda, kikubwa awe na tabia nzuri lakini pia asiwe na makando kando , lakini pia huwezi kumpenda mwanamme mwenye mke au Casanova”

Casanova ni mwanaume mwenye wake wengi au wapenzi wengi , unaweza kumuita Roma Casanova hivyo babu yake Yezi alimaanisha kwamba asingeruhusu Yezi kuoelewa na Casanova.

“Babu usiongee hivyo siwezi kupenda mwanaume wa hivyo mimi”Alijibu Yezi huku akionyesha aibu.

“Nakuamini mjukuu wangu , baba yako kuondoka nyumbani mpaka kifo kumkuta ni majuto ambayo sitaki yajirudie kwako, hata hivyo naamini mama yako hakuwa mbaya pia, hivyo mtu yoyote ambaye anafaa utakaempenda nitakusapoti”Aliongea na kumfanya Yezi kutabasamu kwa furaha.

******

Gari ambalo lililomteka Najma lilisonga kwa spidi kuelekea katikati ya jiji ambalo lilikuwa na mataa mengi.

Nyuma kabisa ya gari kulikuwa na mwanamke alievalia koti la Leather huku akiwa ameshikilia glasi ambayo alikuwa akizungusha zungusha kuchezesha mvinyo uliokuwa ndani yake.

Alikuwa ni Yoon Yeonhee ambaye alikuwa ndani ya familia ya Park kwa ajili ya chakula cha usiku , haikueleweka alipanga saa ngapi na kukamilisha tukio la kumteka Najma.

Alimwangalia Najma kwa macho ya dharau sana huku akimchunguza kwanzia juu mpaka chini kuona ni kipi cha ziada anacho ambacho yeye hana mpaka akatokea kupendwa na Park Jonhyun.

“Hana uzuri wowote kuliko mimi , lakini pia ni mweusi , nashangaa kwanini Park Jonghyun akapenda mwanamke kama huyu , lazima atakuwa na uchawi wa kiafrika huyu mwanamke lakini bado naona pia kuna kitu kinaendelea kati yake na yule mwafrika mwenzake”Aiongea kwa Dharau..

Yonhee alikuwa na hisia kali sana , alikwa ashajua nini kinaendelea kati ya Najma na Roma kwa kuangalia tu.

Mwanaume aliekuwa amemshikilia Najma alionekana kuongea na simu na kisha akamgeukia Najma.

“Miss , Bar tayari iko tayari”aliongea

“Vizuri sana, mpe taarifa Roma Ramoni na taarifa iwe nzuri”aliongea na kumfanya yule mkorea kutoa tabasamu la maudhi huku akishikilia simu yake vizuri.

Baada ya Yoonhee kuongea hivyo alitoa simu yake tena huku akiendelea kumwangalia Najma kwa macho yasiokuwa na nia njema na kisha akatafuta jina la Park jonghyun kwenye simu yake na kisha akapiga , ilichukua dakika kadhaa mpaka simu kupokelewa.

“Unataka nini ..” mtu upande wa pili aliongea akionyesha kabisa hakupendezwa kupigiwa simu na huyo mwanamke na jambo hilo lilimfanya Yoon Hee kuona wivu.

“Kwahio huwezi kuongea na mimi vizuri licha ya kwamba nimekupigia mimi?”

“Acha porojo na elezea shida yako , nipo na kazi nyingi”

“Haha… unafanya kazi , kazi gani unafanya wakati mnufaika ni binamu yangu Yezi?”

“Twitwii..!!”Simu ilikatwa palepale na kumfanya Yoonhee kupandwa na jazba na kuipigiza simu yake kwenye kioo cha gari.

“Fine…. Si unajifanyisha kunichukia, basi nitahakikisha naharibu maisha ya huyu kapuku wako mweusi, tuone kama uaendelea kunichukia na kumpenda”Aliongea kwa hasira.

******

Upande wa chumba cha wageni katika jumba la familia ya Park katika floor ya pili alionekana Roma ambaye alikuwa akimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake aliekuwa akijifanyisha kuwa bize.

Edna muda huo alikuwa amekaa kiandani huku akiwa ameshikilia tablet ambayo inampa nafasi ya kufanya kazi kwa kutumia software maalumu, alikuwa amevalia tayari nguo za kulalia za kitambaa cha pamba,upande wa Roma yeye alikuwa na buka lake tu pasipo ya kuwa nguo nyigine.

“Mpenzi tumekuja Korea kwa ajili ya mapumziko yetu , unapanga kufanya kazi usiku kucha?”Aliongea Roma lakini Edna hakutoa jibu zaidi ya kuendelea kukodolea macho skrini ya tarakishi yake , ilionyesha kama vile hakuwa amemsikia Roma.

Roma alikosa kabisa uvumilivu na mpaka hapo aliona Edna anamjaribu , hivyo alitoka kitandani na kisha akambeba juu juu kwa kumshitua na kumtupia katikati ya kitanda.

“Ah! Unafanya nini?”Aliongea akijaribu kujitetea lakini Roma hakumjali zaidi ya kupanda huko huko katikati ya kitanda na kisha akashika vidole vya miguu ya Edna na kuanza kuvisugua kwa mkono na kumfanya Edna kuhisi mtekenyo wa ajabu kiasi kwamba alikosa uvumilivu.

“Unastahili hiki ninachokufanyia kwa kushindwa kuwa mtiifu kwa mume , nishasema hapa tupo Honemoon na matendo yetu yanatakiwa kuwa ya ki ‘HaniMuni muni’ halafu wewe unachojali ni kazi , unanifanya nijione nina kasoro kama mume wako”

“Huna aibu wewe mwanaume ..”Aliongea na kumfanya Roma asimjali na kuanza kumtekenya kwa kuchezesha mkono kwenye nyayo zake za miguu.

“Ah.. unanitekenya bwana … acha jamani.. hahaha.. Hubby niachie …haha..mamaa.. sifanyi kazi tena naahidi , hahaha..”Edna alicheka na kuomba kwa wakati mmoja kutokana na namna ambavyo alikuwa akiadhibiwa kwa kutekenywa.

Alijikunja kunja kushindwa kuvumilia na kufanya gauni lake la kulalia kuacha mwili wake wazi mbele ya Rom na hata ile Tablet aliokuwa ameshikilia ilidondoka chini kwenye kapeti.

“Hii ndio adhabu yako kwa kujifanya jeuri”Aliongea Roma na kwa jinsi ambavyo Edna amekaa mtupu mbele yake alijikuta mwanaselele akivimba na hakutaka kuchelewa , alimpandia Edna kwajuu na kisha akafungua kamba ya gauni lake la kulalia na kutupa kule.

Hisia nazo hazikuwa mbali kwani hawakufanya muda mrefu kidogo , hivyo Roma hakutaka kupoteza nafasi hata moja kwa nyakati zote ambazo angekaa Korea.

Mkono wake ulisafiri mpaka ndani ya pichu ya Edna na kisha akaaanza kusugua na kidole kimoja cha kati na kumfanya Edna pumzi kuanza kumuishia kwa msisimko wa ajabu aliokuwa akisikia, ni kama alikuwa akipigwa na shoti kuanzia kwenye kitumbua na umeme kusafiri kwenda mpaka kwenye ubongo na hatimae kwenye macho na kumfanya kuanza kutoa machozi, Roma aliendeleza mapambano mpaka alipoona Edna yupo tayari kumpokea hivyo alivua haraka haraka bukta lake na kutupia kule na kisha akamuweka vizuri.

“Ring!!Ring!”

Ni simu ya chumba karibu na kitanda ndio iliokuwa ikitoa mlio , Park Juan alikuwa ameweka kila chumba simu.

Roma alijikuta akipandwa na hasira na kujiuliza ni nani ambaye alikuwa akimharibia fursa yake muda huo.

Edna kifua chake kilikuwa kikipanda na kushuka na aligeuza uso wake pembeni mara baada ya Roma kuondoka na kwenda kupokea simu.

Baada ya upepo kupuliza kuingia ndani alihisi ubaridi wa hali ya juu katikati ya mapaja yake kutokana na kupandwa na hisia za kiwango vha juu , alijikuta akibana miguu kwa wasiwasi.

Roma alijitahidi kupunguza hasira zake , alikuwa na mpango wa kukata simu hio lakini alijikuta akisikiliza mara baada ya kusikia kitu.

‘Mr Roma Teacher Vivian is with us now and if you don’t want her to be turned into a vegetable you’d beter come here..”Roma aliweza kusikia sauti ya kingereza yenye rafudhi mbovu ikiongea.

Roma alijikuta mikono yake ikimtetemeka wakati alipokuwa akikata simu hio.

Alitoa tabasamu la uchungu mara baada ya kuona Edna kafumba macho yake huku aking’ata lipsi zake kwa wasiwasi, ilionyesha alikuwa akimsubiria Roma , lakini aliona bado alikuwa akichelewa na kumfanya afumbue macho yake na kumwangalia na kushangazwa kuona Roma alikuwa akivaa nguo.

“Wewe., hutaki kufanya tena?”Aliuliza kwa wasiwasi huku akiwa na mshituko na kumfanya Roma kushindwa kutoa jibu.

Edna alijikuta akikaa kitako huku akimwangalia Roma na kulaani ndani kwa ndani huku akijilaumu yeye mwenyewe kwa kutegemea mambo makubwa zaidi.

“Mbona unaonekana kuwa na hasira hivyo , nini tatizo?”Aliuliza na kumfanya Roma asione sababu ya kudanganya.

“Kuna mtu kamteka Najma , hivyo natoka kwenda kuangalia kama ni kweli , unaweza kupumzika kwanza au kunisubiria lakini sina uhakika nitachukua muda gani?”

“Nini! Kuna mtu kamteka najma?”

“Sina uhakika lakini ndio nilivyoambiwa kwenye simu , hivyo ninaenda kuangalia kama ni kweli , usijali hakuna kitu kibaya ambacho kiinaweza kutokea”

“Wasiwasi wangu sio kwako kwani nakuamini lakini kwa Najma ambaye hana namna ya kujjilinda”

“Edna hujakasirika nakuacha mwenyewe?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi.

“Unaongea nini wewe ni kweli sipendi uwe na mwanamke mwingine , lakini haimaanishi kwamba nina roho mbaya kiasi cha kupotezea ilihali wapo kwenye haari , Najma anajitahidi kuzuia hisia zake kwa ajili yetu , anafanya yote kwa ajili yetu kwanini niruhusu kuona kuna mtu anajaribu kumchokoza?”Aliongea Edna huku akionyesa wasiwasi hata zile ‘genye’ zilikata.

“Usikasirike ..nilikuwa nikijaribu kuuliza tu?”aliongea Roma huku akiona aibu kutokana na swali lake la kipuuzi , alikuwa akimwona Edna kama mtu mwenye moyo wa baridi likija swala la wanawake wengine ndio maana aliona angekasirika kama angetoka kwenda kumuokoa Najma.

“Acha kuchelewa , nenda haraka”Aliongea na kumfanya Roma asipoteze muda tena na kuondoka hilo eneo kupitia dirishani.

Ijapokuwa kwa nje eneo hilo lilikuwa na ulinzi mkali lakini hakuna mtu ambaye anaweza kudhania kama ametoka , kwani kwake ilikuwa ni swala la kupotea tu.

Roma mara baada ya kutokezea kwenye barabara alipanda Taksi(Cab) na kumpa maagizo dereva kumwendesha kuelekea kwenye Bar aliotajiwa kufika.

Ilimchukua dakika chache tu kuweza kufika kwenye mtaa mmoja wenye barabara nyembaba na gari ile ikasimama na kulia kwake ndio bar ambayo alitajiwa na mtu ambaye alisema amemteka Najma.

Roma alitembea moja kwa moja mpaka kwenye mlango na kusimamishwa na mwanaume alievalia suti ya rangi nyeusi na kwa haraka haraka Roma aligundua hilo eneo usiku huo halikuwa na watu wengi.

“From Tanzania?”Aliongea yule bwana kwa rafudhi mbovu ya kingreza na kumfanya Roma kutingisha kichwa kukubali na palepale walimpisha akaingia

Ilikuwa sio bar bali ni Club kabisa na ilikuwa na eneo kubwa sana ndani na alijiambia mtu ambaye alimteka Najma atakuwa na uwezo wa pesa , baada ya kuingia kulia na kushoto aliona wanaume ambao walisimama huku wakimwangalia.

Kupitia mwanga hafifu Roma aliweza kuona viti ambavyo vilikuwa tupu pamoja na meza ambazo juu yake zilikua na chupa zilizokuwa tupu na glasi huku nyingine zikiwa zimedondoka mpaka chini.

Baada ya kutembea kwenda mbele kwenye Bar aliweza kuona mwanamke wa kikorea ambaye aliweza kumtambua , alikuwa ni Yoon Hee ambaye alikuwa ameshikilia sigara akivuta huku mkononi akiwa na glasi ya mvinyo.

Tokea Roma anaingia hapo mwanamke huyu alikuwa akimwangalia kwa kumchunguza kana kwamba kuna kitu ambacho hakuwa ameridhishwa nacho.

“Miss Yoon yeon Hee nadhani una kinyongo kikubwa na mimi”Aliongea Roma mara baada ya kumfikia na kukaa pembeni yake.

Yoohee alimwangalia Roma kwa tabasamu la dharau kama vile kilichokuwa mbele yake ni kituko

“Bila shaka , sijakuita tu hapa kwa ajili ya kupata kinywaji?”Aliongea na kisha akamnyooshea glasi ya Whiskey kumpatia Roma .

“Mbona unasita au unadhania nimeiweka sumu , wewe ni mgeni wa babu yangu hivyo lazima niwe makini”Aliongea kinafiki na kumfanya Roma kuchukua ile glass yenye kimiiminika cha njano na kisha akashusha yote huku akikunja ndita kutokana na radha yake kuwa chungu.

Baada ya Yoonhee kuona Roma ashainywa alitoa tabasamu la kejeli mno.

“Najua matamanio yako ni kumuona Vivian lakini je unaweza kusikiliza stori yangu kwanza?”Aliuliza na Roma muda huo alishafahamu ni wapi Najma alipo kwa kutumia uwezo wake.

“Ofcourse it’s my pleasure”Aliongea Roma huku akitabasamu na kumfanya Yoonhee kumwangalia kwa kumkagua.

“Mpaka sasa nashangaa kwanini wanawake wanakupenda ilihali hauna mwonekano wa kitanashati kam wanaume wengi wa rangi nyeusi”Aliongea Yoonhee

“Wanaume sio kama wanawake , mwonekano una faida kwa wale wanaokuangalia tu lakini katika mapenzi mambo ni tofauti, wanaangalia kitu kingine kabisa”Aliongea Roma na kumfanya Yoonhee kutingisha kichwa kukubaliana nae.

“Kwasisi wanawake ni tofauti , kama tutaona mwanaume tunaempenda akimpenda mwanamke mwigine itatufanya tujishtukie “

“Mwanamke kama wewe Star na mrembo bado kuna mwanaume anaekukataa?”

“Ndio , na mwanaume huyo ni Park Jonghyun”

“Park Jonghyun!!”Aliongea Roma huku akionyesha mshangao japo alikuwa akitaraji jambo hilo kuwepo.

“Nadhani unashangaa kwanini naweza kuwa mpenzi wa Jonghyun wakati ni binadamu yangu , ngoja nikuambie ukweli, Park jonghyun sio mtoto wa damu wa familia ya Park bali alilelewa na babu yangu na alimfanya akue kwa malezi anayostahili kama mtoto wa kitajiri na kupewa elimu kubwa na baada ya kumaliza babu alimpa nafasi katika kampuni na aliweza kuonyesha uwezo mkubwa sana , kama utaniambia kati ya Yezi na Park Jonghyun nani anastahili kuongoza makampuni ya Starmoon basi nitakwambia Park Jonghyun ni bora zaidi kuliko Yezi.”Aliongea na kumfanya Roma kuendelea kumsikiliza.

“Nilifikiri alinipenda ndio maana akataka tuwe wapenzi licha ya mama yangu hakufurahishwa na jambo hilo lakini mimi niliamua kumpotezea mama na kuendelea na mahusiano yetu , ijapokuwa hatukuwahi kutangaza uhusiano weu hadharani lakini nilikuwa nikitegemea siku zijazo tungwewza kuwa mume na mke , sikujali kusengenywa na watu kwa jambo hilo ili mradi alikuwa akinipenda lakini ,,, Jonghyn alikuwa ni muongo mkubwa , alinipotezea mazima mara baada ya kugundua sikuwa na kidani cha mwezi na mimi sikuwa nikijua ni siri gani iliopo nyuma ya kidani hiko”Aliongea huku akiwa na hasira na hata kukaribia kuvunja glasi ambayo ameshikilia mkononi.

“Kwanini alifikiria unacho hiko kidani , si ni hadhina tu ya familia kuna kingine zaidi?”Aliuliza Roma.

“Kidani cha mwezi na kidani kingine cha kundi la nyota ni kweli ni hadhina ya familia na ambaye ni mrithi wa kuongoza ukoo ndio anajua maana yake halisi ni nini na siri iliopo nyuma yake , lakini Park jonghyun hakuwa akijua kama kuna mtu mwingine alikuwa akijua hilo , kupitia taarifa alizopata mtu anaemiliki kidani hiko ndio mrithi wa mali za familia , alidhania kwamba baba yake Yezi asingekuwa nacho kwani alimsaliti babu na kwenda kuoa mwanamke wa kiafrika hivyo moja kwa moja akamiini mimi ndio nitakuwa nacho , lakini ambacho hakuelewa ni kwamba licha ya babu mtoto wake wa kwanza wa kiume kumsaliti lakini bado alikuwa na mapenzi nae makubwa na kumpatia hadhina hio ya familia ambayo na yeye alikuja kumpatia mwanamke wake wa kiafrika na baada ya hapo mwanamke huyo akampatia Yezi”Aliognea.

“Umeniambia mambo mengi ambayo yananifanya nijawe na shauku ya kutaka kujua maana halisi ya hiko kidani ambacho ni hadhina ya familia yenu na kwanini inahitajika kupitia hiko tu Yezi anatakuwa kuridhi kampuni”

“Nataka pia mimi mwenyewe kufahamu siri yake , lakini sina ninachoelewa vinginvevyo ningekuambia “Aliongea huku akitabasa,u kwa uchungu .

“Mbona huna wasiwasi , hao wote unaowaona ni watu wangu na nikiwapa maagizo tu wanaweza kukudhuru”

“”Kwanini niogope , mke wangu hata hivyo atanishuku kama nitaendelea kubakia hapa kwa muda mrefu”

“Haha… Ni wanaume wote wa Kitanzania waoga kama wewe? Nashindwa kuelewa ni kipi wanawake wamekipenda kwa mwanaume muoga kama wewe , Vivian hampendi Park jonghyun kwasababu yako japo ni jambo zuri kwani linamfanya Park Jonghyun kuteseka , na isingekuwa hivyo ningekuachia uondoke hapa kwa amani”

“Unamaanisha nini?”

“Haujisikii kichwa kuuma wala kizungu zungu ?”

“Sijisikii chochote zaidi ya joto tu”Aliongea Roma

“Joto? Huo ni mwanzo tu ,,, hutopata hata hilo joto tena ,..”Aliongea huku akianza kucheka kwa kejeli.

“Umeniwekea sumu kwenye kinywaji?”Aliuliza Roma na Yoonhee alimjibu kwa kutumia ishara za vidole akimwambia pigia mstari.

Na palepale aliwapa ishara mabodigadi yake kufungua mlango uliokuwa kulia , ni mlango ambao huenda hutumiwa na wafanyakazi wa eneo hilo .

Na baada ya mlango ule kufunguliwa taa ziliwaka na kumfanya Roma sasa kumuona Najma ambaye amezingirwa na wanaume , midomo yake ilikuwa imeingiziwa matambala huku yeye akiwa amefungwa kwenye kiti na alijikuta akimwangalia Roma kwa wasiwasi kama mtu ambaye hakutegemea kama anaweza kufika hapo kwa ajili ya kumuokoa.

Najma alijikuta akikumbuka mara ya mwisho Roma alivyomwokoa kule jijijni Dar es salaam mara baada ya kutekwa na Karim.

“Nilikwambia kweye simu atakuwa salama mpaka utakapofika , lakini sasa umefika na hata sijui ni kipi niwafanye”Aliongea YoonHee.

Roma alisimama kutoka kwenye kiti taratibu na kuanza kuetembea uelekeo wa chumba alipo Najma akimsogelea Yoonhee ambaye alikuwa amesogea upande huo pia akimshika Najma kidevu kwa kejeli.

‘Unataka nini?”Aliuliza Roma na kumfanya Yoonhee kumwangalia .

“Mapigo ya moyo hayakuendi mbio?, Saivi kichwa chako lazima kitakuwa kinaanza kuchanganyikiwa kwa matamanio ya kukutana na mwanamke?”

“Kwahio unanitaka? , sijali kukutana na mwanamke mrembo lakini siwezi kuchafua kiungo changu kwa mwanamke mchafu kama wewe”

“Unasemaje? Unapata wapi ujasiri wakuongea na mimi hivyo wakati hujui hata ni kitu gani nilikuwekea kwenye kinywaji”?

“Yeah , nimekumbuka hujanielezea kuhusu hilo”

“Inaonekana sio wapenzi mpaka sasa kutokana na hali za mahusiano yenu , hivyo nimewawekea kitu ambacho kitawaongezea ujasiri , hakikisha humuonei huruma huyu malaya”Aliongea Yoonhee akimaanisha kwamba ameweka kitu kwenye kinywaji ambacho kitamfanya Roma kuwa na matamanio ya kufanya mapenzi , hivyo alimtaka afanye na Najma mbele yao.

Najma palepale alitolewa kwenye chumba kile na wale wanaume waliojazia miili yao huku akimwangalia Roma kwa macho yaliokuwa yamejaa machozi.

‘Hakika unafurahisha sana, bado dawa ipo?”Aliulizia.

“Unaijua?”Aliulizia Roma.

“Kwanini nisijue, ni dawa ya kuongeza hamu ya mapenzi inayotokana na Red spider(buibui rangi nyekundu),Nilishawahi kuwapatia watu wengi , hivyo nirahisi kwangu kuifahamu”Aliendelea kuongea Roma.

“Lakini kwanini unaone…”

“Kwanini ninaonekana sawa , si ndio unavyotaka kuongea?”

“Haiwezekani , unajaribu kuvumilia athari zake , hakuna mtu ambaye anaweza kuihimili , mishipa ya damu yako itapasukka kama utaendelea kuhimili athari zake”

Roma alichukua kijisturi kidogo kilichokuwa karibu yake na kisha akarusha kwenye kioo cha mlango wa upande wa kushoro karibu nae eneo la steji.

“Clang!!”

Kioo kile kilipasuka palepale vipande vipande na kilio cha mtu kilisikika upande wa mlango wa kioo ambao alipasua , alikuwa ni mwanamke(Strippers) ambaye mkononi ameshikilia Kamera kubwa ya lensi

“Naona mpango wako ulikuwa ni kunichukua vidio nikifanya vitu vya kipuuzi mbele yako si ndio?nadhani hunifahamu hata mimi ni mtaalamu wa hayo mambo”

Yoonhee alishangazwa na jambo hilo nakujiuliza Roma alifamu vipi kuna Stripper(Exotic dancer) alieshikilia kamera kwenye kile chumba , mpango wake ulikuwa rahisi sana , alitaka kwanza awachukue Video ya utupu Roma na Najma kwa ajili ya kuwatishia nayo.

Angeweza kumuumiza Park Jonghyun kutumia picha hizo na kukomesha hisia zake na mawazo ya kuendelea kumtaka Vivian na wakati huo huo angecheza na akili ya Yezi kwa kupitia picha hizo na kumfanya asikubali urithi kwani aliamini Yezi alikuwa akimchukulia Roma kama ndugu yake hivyo asingekubali adhalilike.

Lakini mpaka muda huo aliona mambo hayakuwa yakienda kama ambavyo alikuwa amepanga na kuanza kujiuliza mwanaume aliekuwa mbele yake ni nani.

Mabodigadi wake mpaka hapo walikuwa washaona hatari na walikuwa wakisogelea taratibu kwa ajili ya kumshambulia Roma

Upande wa Roma hakuwa na muda wa kupoteza na Yoonhee zaidi na isitoshe alishamweleza kile ambacho alitaka kusikia kuhusu kidani na mahusiano yake na Park Jonghyun , hivyo alimsogelea Najma.

“Mzuieni na mumkamate”Aliamrisha Yoonhee baada ya kukumbuka alikuwa na watu ambao anaweza kuwaagiza anavyotaka , mabodigadi waliokuwa na miili mikubwa walimkimbilia Roma kwa ajili ya kuanza kupigana nae , lakini Roma hakuona haja hata ya kutumia uwezo wake kwani alitaka kutumia njia za kiinadamu kudili nao

Roma aliinua mkono wake na kabla bodigadi wa kwanza hajamfikia tayari alishaachia ngumi ya ujazo wa kilo hamsini na kumpiga nayo eneo la tumboni na kumfanya arudishwe nyuma kama furushi,kwasababu Bodigadi yule hakutegemea swala hilo alijikuta akikosa kukwepa kungumi yake na kwenda kuvaa meza na kufanya mlio wa kuvunjika kwa meza pamoja na chupa kusikika ndani ya hilo eneo.

Roma hakuishia kwa mmoja tu aliwapiga wote kipigo kitakatifu na kuwalegeza , hakuwa na mpango wa kuwaua kwani alikuwa na sababu tatu , ya kwanza alikuwa bado anawahitaji, ya pili hakutaka kuanza kudidili na maiti na ya tatu na ya mwisho aliona hawakupaswa kufa kwani walikuwa wakifanya kazi kwa maagizo tu ya Yoonhee.

“Miss kimbia , ana nguvu nyingi na hatumuwezi”Bodigadi mmoja ambaye alionekana kuwa kiongozi alimshtuia Yoonhee,Roma mara baada y\ kusikia sauti ya yule mwanaume aliitambua.

“Wewe ndio ulinipigia simu si ndio?”Aliongea Roma huku akicheka na Roma palepale alimuona Yoonhee akitaka kukimbia na alimzuia.

“Unataka kukimbia?”

“Mlindeni Boss”Waliongea wale mabodigadi baada ya kuona Roma anataka kumdhuru bosi wake.
 
SEHEMU YA 518.

Kila kitu kililimgeukia Yoonhee ni hakika kwamba kutokumfahamu Roma ndio kulimfanya kuchukua maamuzi ya kijinga ambayo yanamgharimu.

Roma hakuwa na mpango wa kumuonea huruma , hivyo alichokifanya kwanza ni kumvunja shingo bodigadi mmoja mbele yake na baada ya hapo wale wengine wote walionyesha kumuogopa Roma mno , kwani alionekana kama mnyama.

Roma mara baada ya kuona wameshaingiwa na hofu alitabasamu kifedhuli na kuona sasa mpaka hapo wapo tayari kufanya kila agizo ambalo angetoa.

Roma alimpa ishara yule kiongozi wa mabodgadi na kumwambia alete dawa ya kuongea hamu ya tendo pamoja na vifaa vyote vya kuchukulia Vidio.

Najma ambaye ashafunguliwa alionyesha kuwa na wasiwasi mno na hakutaka kubakia hapo ndani.

“Roma kwanini tusiondoke tu hili eneo?”

“Siwezi kuondoka kabla sijalipiza kisasi , unaweza kutangulia kama unataka na isitoshe napenda sana hii michezo”Aliongea Roma na palepale alianza kutoa maeekezo kwa lugha kikorea.

“Zidisheni Dozi na weka kwenye hio glasi na kisha mnywesheni bosi wenu kwa nguvu , halafu wewe hapo rekodi kila kitu , nataka Vidio yenye ubunifu wa viwango”Aliongea Roma kwa amri na wale mabodigadi kutokana na kumuogopa Roma walifanya walichoambiwa na kuchukua glasi na wakajaza mvinyo na kisha wakazidisha Dozi ya Red spider na kutingisha vizuri huku mwezake akirekodi , Roma alihakikisha haonekani kwenye hio Vidio.

Baada ya hatua ya kwanza kumalizika Yoonhee alishikiliwa kwa nguvu na kisha akanyweshwa kile kinywaji chote huku akipiga makelele lakini Roma hakujali.

Baada ya kuona hatua ya pili imeenda sawa ikiwa imerekodiwa wale mabodigadi wawili walikunywa pia kinywaji cha Red spider ili kuwaongezea hamu ya tendo na Roma akatulia kwa sekunde na alivyoona macho yao yashaanza kubadilika rangi na kuwa kama wanyama hakuhitaji kuongea sana.

Wa kwanza alimvaia Yoonhee na kumvua nguo kisha kuanza nae na upande wa Yoonhee na yeye ile dawa ilimkolea vizuri mno na alianza kutoa ushirikiano.

Kifupi Roma alikuwa akirekodi filamu ya ngono ndani ya taifa ambalo sio la kwake , tena mwanamke ambaye alikuwa akirekodiwa ndio star wa taifa na ndugu yake Yezi huku kosa lake ni kumgusa Najma.

Najma uvumilivu ulimshinda na kuishia kuangalia pembeni kwani hakuweza kuhimili kuona kile kinachoendelea , lakini kwa Roma hakujali kabisa.

Kila kitu kilienda vizuri mno , kwani kama ni miguno ya kimahaba aliweza kuisikia na kilichomfurahisha zaidi ni wale wanaume kufanya kazi inayoridhisha , ilikuwa ni kama vile walikuwa wakimtanani kwa muda mrefu Yoonhee.

Ijapokuwa Najma alijua Roma hakuwa mtu wa kawaida kutokana na kwamba haikuwa mara yake ya kwanza kuona mambo ya ajabu anayofanya , lakini aliona kadri anavyozidi kumjua ndio anaona kabisa ni tofauti na vile ambavyo anamfikiria.

Kuna kitu kilibadilika kwenye moyo wake mara baada ya kuona tukio hilo la kikarili likifanyika mbele yake.

Roma baada ya kuona ashamaliza kazi , alichomoa memori yake na kuweka mfukoni .

Mara nyingi dawa ya Red spider inadumu kwa muda mfupi sana na ikitokea mtu akifikia kitonga basi athari yake hupungua kabisa na Roma alikuwa akielewa kuhusu hilo kwani ndio dawa maarufu iliokuwa ikitumika kwa watu ambao wanacheza filamu za ngono.

Yoonhee baada ya kuchezewa na kufika mshindo mara kibao , sasa dawa ilianza kuisha na kruudi katika hali ya kawaida na kuanza sasa kuona alivyokuwa , mwili wake wote ulijaa alama za michubuko huku manyonyo yake yakiwa yamekamuliwa mno .

Alishindwa hata kulia na alijiambia yote hayo yasingemtokea kama tu asingemteka Najma.

Alishindwa kuelewa nini kingetokea baada ya hapo na jambo pekee ambao alikuwa akiwaza kwenye kichwa chake ni kujiua tu , lakini bado alionekana kukosa ujasiri wa kufanya hivyo.

“Nafikiri mpaka sasa utakuwa na tabia nzuri , kama utanichokoza basi nakuhakikishia nilichorekodi kitasambaa dunia nzima”Aliongea Roma na baada ya kumaliza alitoka eneo hilo kwa furaha huku akipiga mluzi.

Yoonhee aliishia kumwangalia namna Roma anavyoondoka na alishindwa hata kipata ujasiri wa kuongea neno hata moja.

Najma ambaye hakutegemea mabadiliko hayo , alijikuta akimkimbilia Roma kumfuata.

Muda ulikuwa umeenda hvyo watu wengi walionekana tayari kwenda kulala kwani mtaa ulikuwa mtupu na ubaridi ulikuwa mkali mno kwa wale ambao hawajazoea hali hio.

“Roma asante kwa kuja kuniokoa ..”Aliongea Najma kwa kiswahili.

“Haina haja ya kunishukuru , najua kwa kilichotokea leo unaniogopa na unanona kama mnyama ninaependa kutesa watu , ulichokiona leo ni kawaida sana kwenye maisha yangu”Aliongea.

“Haiwezekani… Roma najua umenifanya vile makusudi mbele yangu , wewe ni mtu mzuri sana na najua hilo, umenisaidia mara nyingi sana na sio mimi tu hata kaka yangu pia, huwezi kuwa vile nni mazingira tu yamekulazimisha”

“Najma hebu fikiria kwa akili zako sio hisia , umeona nilichomfanyia Yoonhee , tena nilikuwa na mpango wa kumuanza mimi kabla ya kuruhusu wale wengine kuendelea , hata hivyo alionyesha kuwa mrembo mwenye mvuto”Aliongea Roma

“Unadanganya Roma haupo hivyo”

“Kwahio unaona nadanganya , wewe hunijui vizuri , unaweza kumuuliza hata Edna , yeye mwenyewe ashazoea kuniona nikivunja watu shingo , unaniona mtu mzuri kwasababu sijawahi kukuonyesha upande wangu mwingine wote , ulichokiona mara ya mwisho kule Dar ni cha mtoto na hiki cha leo ni cha mtoto pia , mimi ni katili zaidi ya unavyofikiria , fumbua macho yako Najma siwezi kukufanya kuwa mpenzi wangu kwani wewe ni wa kawaida sana kumvumilia mwanaume kama mimi , unajuaje naweza hata saivi kuhitaji mwili wako nikuonje maana umezidi kuwa mrembo na unavutia”Aliongea Roma huku akionyesha sura iliojaa ufedhuli.

Najma alijikuta akishindwa kuamini , ni kama mtu ambaye yupo mbele yake ni mwingine kabisa , maneno yake yaliuvunja vunja moyo wake vipande vipande ,

Mrembo Najma aliishia kutoa machozi mengi sana huku akishindwa hata kuendelea kutembea na kuchuchumaa chini kuanza kulia na kujiuliza kwanini ni yeye tu siku zote anaelilia mapenzi, kwanini sio wengine yeye anakasoro gani , kwanini Roma ana wanawake wengi na yeye pekee tu ndio anamkatalia.

“Kwannini unalia sasa? , sijakufanya chochote na zaidi ya yote nimekusaidia kukuokoa , nifuate kama hutaki kutembea wa mguu , maana muda huu ni ngumu kupata taksi”

“Roma kama hunipendi kwanini kila siku unaniokoa , kwaninni kila siku unatokea pale ninapokuwa katika hali ya hatari?”

“Acha hizo bwana dada yangu mpendwa , hata kama siwezi kuwa mpenzi wako lakini bado wewe ni rafiki yangu , walinipigia simu ndio maana nimekuja , usifikirie sana juu ya hilo”

Najma alizidi kuumizwa na kila neno ambalo anatamka Roma , aliona yalikuwa maamuzi sahihi ya kukaa mbali na nchi yake ili kumsahau , lakini wakati huo aliona huenda hayakuwa maamuzi sahihi kumkimbia Roma huenda ingekuwa rahisi kumsahau akiwa ana muona kuliko kumsahau akiwa hamuoni.

Muda ule ule bahati ilikuwa kwao ilitokea Taksi kumshusha mtu katika maeneo hayo na Roma aliisimamisha na kumwambia Najma aingie na aende nyumbani kwake , kwani yeye anataka kurudi kwa mke wake.

Najma aliekuwa na huzuni aliingia ndani huku akiwa haamini , na kujiona ni mwanamke mwenye gundu sana kwenye maisha yake , alikuwa na uzuri kumzidi Nasra rafiki yake , lakini bado Roma hakuwa akimtaka yeye lakini rafiki yake alikuwa akimtaka.

Roma alijikuta akiangalia gari hio ikipotea kwenye macho yake na alijihisi moyo wake kuuma kutokana na maneno makali aliomwambia Najma.

Siku zote alimchukulia Najma kama mwanawake mpole sana huenda katika wanawake aliokutana nao ni Najma ambaye alikuwa mpole zaidi ya wote , na alijua namna ambavyo Najma alipambana kwa ajili yake tokea siku ya kwanza aliyofika jijini Dar.

Roma sio kwamba hakuwa akimpenda Najma na huenda kama sio rafikki yake Juma kipindi kile na yeye pia mwenyewe kujizuia basi Najma angekuwa ndio mwanamke wa kwanza kuwa nae katika mahusiano mara baada ya kurudi Tanzania.

Lakini alishindwa kujielewa zaidi, huenda ni kwasababu ya kumjali sana ndio maana aliona uzito wa kumjumuisha kwenye kundi la wanawake wake , huenda alitaka kuona Najma akipata mwanaume bora zaidi kuliko yeye.

Roma baada ya kufikiria kwa muda mfupi , aliamua kurudi kwenye jumba la Park na kugonga mlango na walinzi walionyesha mshangao mara baada ya kumuona alikuwa nje , hawakuelewa ni muda gani aliweza kutoka hapo ndani.

Lakini licha ya hivyo waliishia kumruhusu tu huku wakiwa na wasiwasi.
 
SEHEMU YA 519.

Roma kabla ya kwenda moja kwa moja mpaka ndani alirudi tena nje , kuna kitu ambacho alisahau ndio maana akaona akakifanyie kazi, wale walinzi walimshangaa lakini kwasababu alikuwa mgeni hakuletewa shida.

Dakika chache mbele alirudi tena huku akiwa ameshikilia mfuko mzito na kupita nao kuongoza njia moja kwa moja mpaka ndani.

Edna hakuwa amelala bado , baada a kuingia kwenye chumba chao alimkuta akiangalia Runinga kipindi cha Variety show.

“Vipi kuhusu Najma yupo salama?”Aliuliza Edna mara baada ya kumuona Roma.

“Mbona unaonekana kama huna wasiwasi , yupo sawa ameenda anakoishi”Aliongea Roma na kumfanya Edna macho yake kuangalia kile ambacho Roma alishikilia.

“Kwenye huo mfuko umebeba nini?”

“Ni keki za kutengenezwa kwa mchanganyiko wa mayai na mchele”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutabasamu , alikuwa akijihisi njaa kutokana na kwamba hakula chakula akashiba kutokana na ule ugeni na hilo ndio ambalo Roma alikuwa amelisahau ndio maana akatoka nje na kwenda kununua kwa ajili yake.

“Nimeleta kwa ajili yangu kwanini wewe ndio unaonekana kinara wa kula, keki kama hizi zinanenepesha?”Aliongea Rom na Edna alishindwa kujibu kwani alikuwa akitafuna.

“Nilikuwa nikihofia kula sana kipindi cha nyuma , lakini sasa hivi nafanya mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na aardhi sina wasiwasi”Aliongea Edna na Roma hakushangazwa, alitegemea kadri wakatavyokuwa wanapanda levo ndio watajua kwanini alikuwa akipendelea kula sana.

Edna baada ya kumaliza kula alishika tumbo lake huku akiteuka kwa nguvu na kumfanya Roma kumwangalia kwa mshangao.

“Dear una miaka ishirini na tano sasa kwanini unafanya hivyo kama shangazi wa miaka arobaini?”

“Nani kasema kuteuka ni kwa watu wazima tu , tupo sisi tu hapa na siwezi kufanya hivyo huko nje kwenye watu wengi”Aliongea huku akionyesha kutokuwa na wasiwasi.

“Ndio maana wahenga wanasema ndoa ni kaburi la mapenzi , wanawake mnabadilika baada ya muda mfupi wa ndoa , huenda ndio maana wanaume wanafanya usaliri”Aliongea Roma na kumfanya Edna kukasirika na kumshika Roma mashavu na kuyaminya kwa nguvu.

“Unapata wapi uthubutu wa kusema hivyo , utaacha kwenda kwa wanawake wako kama nitaacha kuteuka mbele yako?”

“Nilikuwa nakutania mke wangu … babe unateuka vizuri sana na kaharufu pia ni kazuri”Aliongea Roma kumpamba.

“Acha kunipamba , unafikiri nimeshindwa kukuona jinsi sura yako ilivyokuwa wakati ukiingia hapa , vipi kuna kitu kilichotokea baina yako na Najma?, maana sikudhania kama unaweza kukumbuka hata kununua chakula”

“Ah!..nilileta chakula kwasababu nilikuwa na njaa na nikajua na wewe pia utakuwa na njaa kwani ulikula kiabu aibu”

“Wewe niambie tu ,mimi nakujua vizuri kama kweli hakuna kitu kilichotokea kati yako na yeye , ungetaka tuendelee kufanya kile tulichokuwa tukifanya , unaonekana kuwa na mawazo ndio maana unaonekana kuwa mkimya na kukosa kuchangamka”Aliongea Edna na kumfanya Roma amwambie tu kile kilichotokea.

“Akili yangu inaniambia umefanya vizuri lakini moyo wangu unasikitika juu ya Najma , usiku wa leo ataishia kulia tu”

“Kwahio unaniambia nimkubalie?”

“Usije kuthubutu ”Aliongea huku akimfinya sikio na kumfanya Roma amuombe amuachie na Edna alimwachia huku akijona ni mshindi.

Edna alionekana kuanza kubadilika ule ugumu mbele ya Roma ulianza kupotea na sasa alikuwa akijiachia anavyotaka kwa mazingira kama hayo ambayo wapo wenyewe.

“Ila Yoomhee ni shetani , napatwa na wasiwasi kuna uwezekano kuna kitu atapanga zidi ya Yezi”Aliongea Edna.

“Najua hata mimi mpango wao ni kutaka kungilia urithi wa Yezi ili wachukue kampuni ya Starmoon lakini kwasasa wanapanga mipango yao kwa siri ili isije kufahamika mapema na kuharibu , tumekuja hapa kwa ajili ya sherehe ya Yezi kutambulishwa kama mrithi lakini hatuwezi kuondoka baada ya tarehe yenyewe , tutakaa kwa muda kidogo ili kuona ni mipango gani wanayo”

“Nadhani pia kama upasuaji utafanikiwa , Babu yake atakuwa na afya nzuri ya kuweza kumlinda”Aliongezea na Edna.

Waliendelea kupiga soga karibia usiku mzima mpaka pale Edna alipokuja kupotelea usingizi kwenye kifua cha Roma.

Roma alipatwa na hisia nzuri mara baada ya kuona Edna kasinzia kwenye mikono yake , ni maisha ambayo alitamani kuwa nayo na aliona ni kama yanaanza kutimia , lakini aligundua bado sana kuweza kuwa na maisha ya amani ya kiasi hicho , kwani bado maadui zake hakuwa amewamaliza na mambo mengi yalikuwa yakimsubiria.

Asubuhi kulivyo kucha , vijakazi wa nyumba hio waliwaamsha kwa ajili ya kushuka chini kupata kifungua kinywa .

Ijapokuwa Roma alikuwa na mpango wa kuanza kufatilia nani ana mpango wa kumzuru Yezi lakini safari yao ya kuja hapo ilikuwa ni kama Honeymoon(fungate) kwani tokea waowane hawajawahi kufanya safari ambayo si ya kikazi kwa Edna.

Roma baada ya kumaliza kuoga na kutoka alimkuta Edna ashavaa tayari na kilichomshangaza ni pale alipomuona akiwa amevalia miwani ya jua , ilimfanya azidi kupendeza na hakutaka kuongezea neno.

Kwasababu hali ya hewa ya Korea kuwa ya ubaridi licha ya kipindi hicho kwa wenyejji kutafsri kama kipindi cha joto , lakini Edna yeye alivaa sweta na suruali ya Jeans iliomfanya kuonyesha umbo lake vizuri, usiku wa jana walipanga kwenda kutembea siku inayofatia ndio maana walivaa kimtoko zaidi.

Baada ya kushuka mpaka chini walimkuta Yezi akiwa ameketi kwenye meza ya chakula akiwa na mwalimu wake Najma.

Najma baada ya kukaribiwa na wanandoa hao alitingisha kichwa kwa ishara ya kuwasalimia huku akilazimisha tabasamu , akiwa na macho ambayo yalionyesha kuvimba ikiwa ni dhahiri kabisa alilia usiku kucha..

“Sister Edna naona mpo tayari kwa ajili ya kutoka , babu amenitakaza kuwasindikiza , nimechukia”Aliongea kwa kulalamika.

“Unamuda wa kutosha wa kucheza siku zijazo , lakini kwasasa lazima ujifunze namna ya kuongoza biashara na uache utoro”Aliongea Edna huku akimfinya mashavuni.

“Bora hata kama ningeendelea kubaki Tanzania , hapa panachosha mno kwani sina hata rafiki”

“Unataka rafiki wa nini? , si uoane na yule kijana wa jana,mtakuwa marafiki na mtaitana kila majina ya kimahaba’Alitania Roma na kumfanya Yezi amkate jicho.

Najma hakuongea chochote , muda wote alikuwa bize kupata kifungua kinywa chake kimya kimya na haikueleweka alikuwa akiwaza nini.

Ijapokuwa Roma na Edna walijua sababu lakini walijifanyisha kutojua chochote na kuendeleza stori.

Chakula cha kikotea kilimshangaza Edna na kilikuwa vilevile kama alivyokuwa akuoa kwenye tamthilia , supu ya kuku iliopikwa ulikuwa imewekwa mizizi ya kila aina , kwenye meza hakukukosekana Kimchi.

Kimchi ni chakula cha kitamaduni ndani ya nchi hio na walikichukulia siriasi kiasi kwamba asilimia kubwa za familia wana mafreezer makubwa kwa ajili ya kuhifadhi kisiharibike.

Baada ya kuhitimisha kifungua kinywa walitoka nnje na dereva aliepewa kazi ya kuwaendesha Roma alimkataa.

“Tunatembea?”Aliuliza Edna mara baada ya kutoka nje ya geti la nyumba hio.

“Ushawahi kusikia kuhusu Subway?”Aliuliza Roma na kumfanya Edna kushangaa alikuwa ashawahi kusikia kuhusu hiko kitu kwenye tamthilia zao, ilikuwa ni usafiri wa treni.

“Kwahio unataka tupande treni?”

“Ndio njia rahisi ya kuona maeneo mengi kwa jiji kubwa kama hili , na gharama yake sio kubwa ni Won elfu mbili tu na inaongezeka kadri ya mbali wa safari yako, itaokolea muda mwingi”

Won elfu mbili hela ya Korea ni sawa na elfu tatu mia tano za kitanzania

“Mh , kwanini unajua hayo yote?”Aliuliza Edna.

“Kwasababu mimi ndio mume wako…..”AliongeaRoma huku akijipiga kifuani.

“Kwenda huko”

Waliongea kwa kutaniana mpaka wakafaikia kituo cha treni(Subway ) na kisha baada ya kupata tiketi zao waliingia , yalikuwa maisha ambayo Edna hakuyazoea na ulikuwa uzoefu mzuri kwake.

“Babe , hivi unajua kwamba watu wa Japani wakiwa kwenye treni muda wote huangalia simu zao , wakati huo watu wa Hongkong wakiingia kwenye treni wanasoma vitabu na magazeti , Watu Taiwani wao huongea mfululizo kama chiriku wakiwa kwenye treni, lakini wakorea ndio ambao ni wastaarabu hawaongei na mara nyingi huchukulia muda huo kama fursa ya kutafakari kuhusu maisha yao”Aliongea Roma na kumfanya Edna kuamini maneno yake, ndani ya treni hilo la umeme hakukuwa na maongezi zaidi ya watu kuwaangalia kwa kuwashangaa.

Mpango wa Roma wa kwanza ni kwenda Namsangol Hanok ,hivyo baada ya kufika kituo cha treni cha Chungmuro walishuka na kuanza kutembea kwa mguu kuelekea uelekeo wa mashariki kutoka kituoni.

Kijiji cha Namsangol ndio sehemu maarufu ya kitamaduni zaidi ndani ya Korea na ndio mahali ambapo muvi nyingi za kihistoria huigiziwa hapo, ijapokuwa ilikuwa sehemu ya urithi wa kihistoria lakini pia ni sehemu muhimu sana kwa tamaduni za kikotea kitaifa.

Maandishi ya herufi za kizamani, Hanja yalikuwa kila pande ndani ya eneo hilo na Edna sasa aliweza kushuhudia kile alichokuwa akikiona kwenye muvi laivu, kilikuwa ni kijiji kikubwa ambacho kilikuwa na nyumba za kiamaduni za watu wa kawaida na wale ambao walikuwa ni wa familia za kifalme.

Baada ya kuyafurahisha macho Edna aliomba kupelekwa kwenye chuo kikubwa cha wanawake hapo Korea kifahamikacho kwa jina la Ehwa na karibu na chuo hiko ndio sehemu ambapo waliweza kupata chakula cha mchana.

Edna kabla hajaanza safari alikuwa ashatafuta maeneo ya kutembea atapokuwa nchini Korea na ndio maana alikuwa na mzuka wa kutembea kila mahali ambapo alipanga kufika na Roma aliridhishwa kuona Edna alikuwa na furaha , alimuona sasa huyu ni Edna ambaye anayafurahia maisha na sio yule ambaye anajifungia ofisini tu muda wote na akisafiri ni kwa ajili ya kazi.

Baada ya kutembea katika mitaa ya chuo cha wanawake cha Ehwa , Roma alimchukua Edna na kumpeleka kwenye soko moja kama la feri pale Dar lifahamikalo kwa jina la Noryangjin, ni soko ambalo lilikuwa likiingiza asilimia sitini ya vitoeo vyote vinavvovuliwa baharini.

Edna alishangazwa na ukubwa wa soko , lakini pia namna aina nyingi ya samaki na viumbe vingi wa baharini na walidhurula katika maeneo hayo mpaka muda ambao walirudi nyumbani.

Siku ya pili yake Edna alikumbuka mahali ambapo Bi Wema na Blandina walimwambia atembelee na apige picha , ilikuwa ni Sauna na Edna mara baada ya kufika ndani ya eneo hilo alijikuta akishangaa vitu vingi na kilichomshangaza ni nyuzi joto ya mvuke katika vyumba tofauti tofuti, kulikuwa na vyumba karibia sitini ambavyo vilikuwa na mvuke wa nyuzi joto tofauti tofauti.

Kwa Edna huenda ndio safari yake ya kwanza kutoka nje ya Tanzania ambayo hakuwa na mawazo ya kazi, walifanya vitu vingi kama kuendesha boti mwendokasi katika eneo maaarufu la Hangang na kuangalia makundi ya ndege pia katika fukwe na usiku walienda kunywa Soju ndani ya Pocha(Bar).

Siku zilienda kwa kasi sana tofauti na walivyotegemea na siku ya tarehe saba ndio waliweza kuonana kwa mara nyingine na Babu yake Yezi, ijapokuwa waliishi katika jumba moja lakini walioonana nae siku mmoja tu ile ya ukaribisho.

****

Ilikuwa ni sherehe ya kumtambulisha Yezi katika jamii za kitajiri(Chaebol) ndani ya Korea na kwa baadhi ya marafiki wa famiilia, lakini pia kwa Park juan alipanga siku hio kuwaeleza wafanya kazi wake juu ya mpango wake wa kufanyiwa upasuaj ili kuwatoa hofu.

Sherehe hio ilifanyika katika moja wapo ya hoteli ya nyota tano ambayo ilikuwa ikimilikiwa na kampuni yao.

Ukumbi mzima uliokuwa umepambika vizuri na kupendeza ulikuwa umejazwa na sura nyingi za weupe wa kikorea na watu ambao walikuwa ni weusi walikuwa wachache sana huenda hawakuwepo kabisa , ijapokuwa hakukuwa na ubaguzi wa rangi wa viwango ndani ya Korea , lakini Edna na Roma hawakuweza kuongea na watu zaidi ya kukaa sehem moja wakifurahia Champagne.

Upande wa Park Juan yeye alikuwa amekea katikati ya ukumbi hio akiwa na jukumu la kupokea wageni na watu waliokuwa pembeni yake ni Gong Gyechung pamoja na dokta Lee Eujeong.

Kutokana na watu walivyokuwa wengi wanaomsalimia , ilionyesha asingeweza kupata muda wa kuwakumbuka Roma na Edna ambao walikuwa nyuma kabisa kwenye kona.

Muda huo huo Clark alievalia gauni la rangi nyeusi alisogea mpaka kwenye meza ya Roma na kisha akaketi, alikuwa amependeza si mchezo na Roma alimuona tokea muda mrefu namna ambavyo wakorea walivyokuwa wakimzonga kutaka kuongea nae.

“Bora ningevaa kama Edna,wanaume wa kikorea ni wakorofi sana , najitahidi kuwaongelesaha kwa Kikorea lakini wao wamekadhana kuniongelesha kwa kingereza”Aliongea kwa kulalamika.

“Achana nao , sio dhambi muda mwingine kuwa mkorofi”Aliongea Roma

“Hapana siwezi , mimi ni msichana wa tofauti ukumbuke”Aliongea huku akicheka na kumfanya Roma kupotezea malalamiko yake.

‘Nani ambaye anakwenda kumfanyia upasuaji Park Juan au ni Dokta Lee?”

“Yule mzee naona kama haamini uwezo wangu labda kwasababu naonekana mdogo , familia ya Gong inampigia sana debe Dokta Lee na ni kweli kwamba amejiandaa vyema kuliko mimi , hivyo sikujisumbua kabisa tokea ile siku , siko obsessed kufanya upasuaji kihivyo na sioni maana ya kushindana , hata kuja kwangu hapa ni kwa ajili ya wanafunzi wangu”Aliongea na kumfanya Roma kushanga.

“Kwahio siku zote ulikuwa ukifanya nini?”

“I went to a village near Seoul and learned how to make the most authentic Kimchi”Aliongea akimaanisha kwamba alienda kwenye kijiji cha karibu na Seoul kujifunza namna ya kutengeneza Kimchi ya viwango.

Edna na Roma walishangazwa na kutamani kucheka na kujiuliza yote hayo anafanya kwa ajili ya nini.

“Lakini si ulisema kwamba ukoo wa Park umekupa ofa ya malipo makubwa kwa ajili ya upasuaji , kwanini sasa ukaongeza kiasi kwa ajili ya upasuji hiuo, ndio maana Lee Eujeong akaaminika”

“Bei niliotaja ilikuwa sahihi , kwa upasuaji wa kubadilisha ini mara nyingi hugharimu kiasi cha Dola za kimarekani milioni moja na nina uhakika Dokta Lee atafanya upasuaji bure kwa ajili ya familia ya Gong”

“Na wewe umemtajia ngapi gharama?”Aliuliza Roma na Clark aliinua vidole viwili na kuwaonyesha.

“Dolla milioni mbili?”Waliuliza wote kwa pamoja na Clark alitingisha kichwa kukataa.

“Milioni mbili ni kidogo sana na kwa gharama hio sipaswi hata kumfanyia uchunguzi hata ulimi wake, namaanisha paundi milioni ishirini”Aliongea na kumfanya Roma kushindwa hata kupumua kwani Clark alikuwa akimaanisha mabilioni zaidi ya arobaini ya kitanzania.

“Clark kwanini ni ghali hivyo?”Aliuliza Edna.

“Mara nyingi gharama inategemeana na mtu, unaweza kukuta kuna mgonjwa anafanyiwa upasuaji huo huo na akalipia kiasi kidogo sana ambacho hata milioni hakifiki , lakini kwa mtu kama Park Juan hicho kiasi ni haki kabisa ,mtu mwenye utajiri wa mabilioni ya hela paundi milioni ishirini ni kama hela ya mboga kwake na isitoshe anataka upasuaji kuwa na mafanikio ya asilimia mia moja”

“Ndio maana hajakuchagua , unataja vipi bei kubwa hivyo kwa ajili ya upasuaji tu?”Aliongea Roma.

“Hayo sio juu yangu sasa , nimekuja hapa kwa ajili ya kulipwa kiasi hiko cha pesa na isitoshe kesi yake ni ngumu kutokana na umri wake”Aliongea Clark huku akichukua kinywaji , alionekana kujiamini kwa bai ambayo ametaja.

Inawezekana kuna madaktari wengi ambao wangefanya kwa bei ya chini lakini kwa Dokta Clark yeye alikuwa akiuza jina na hiko ndio ambacho kilikuwa kikimlipa zaidi, kutaja bei kubwa sio kumfuja Park juan bali ni kudumisha uthamani wake.

“Hubby kwanini usitumie ile mbinu yako kumponyesha na ukapata hela?”Aliuliza Edna

“Mimi sio Mungu , naweza kumponyesha mtu majeraha ya nje , lakini kwa ugonjwa wa kansa siwezi kuutibu kabisa , shida yake hahitaji nafasi ya makosa kabisa na isitoshe mimi sio daktari na sijuo chochote kuhusu Physiology ya mwili , chukulia mfano kama gari , ninaweza kuliosha gari kubadili oil ya injini au kuziba pancha lakini kama tatizo lake ni la ndani zaidi na ni kubwa siwezi kulitegeneza kwani mimi sio injini hivyo lazima nitamtafuka Makenikia atengeneze , hivyo hivyo kwa mgonjwa kabla ya kumtibia itanihiraji kujua kila kitu kinachomsumbua vile vya moja kwa moja na visivyo vya moja kwa moja ,sasa hio ndio kazi ya daktari”Aliongea Roma kumwelewesha Edna.

Muda uleule wakati anageuza shingo yake nyuma aliweza kumjona Park Jonghyun ambaye ameongozana na Najma

Park Jonghyun alikuwa amevalia suti ya rangi nyeupe na alikuwa amependezwa sana kutokana na mwonekano wake wa urefu.

Upande wa Najma yeye alikuwa amevalia gauni la rangi ya pingi huku likiwa na Ribbon(mkanda mfano wa utepe) ya njano iliozunguka kiuno chake, kutokana na kubana kwa gauni alilovaa pamoja na mkanda wa kiunoni ilimfanya umbo lake kujionyesha vizuri snaa na akazidi kuvutia.

Walikuwa wameshikana mikono , waliingia hapo ndani kam wachumba na watu baada ya kuwaona waliwasogelea mmoja mmoja na kusalimiana nao , huku Najma akionekena kutingisha kichwa na aliekuwa akitawala maongezi alikuwa ni Park Jonghyun.

Roma na Edna walijikuta wakiangaliana , huku wakionyesha mshangao pamoja na wasiwasi kutokana na mwonekano wa Najma , namna ambavyo alikuwa akiweka tabasamu na kufurahi.

“Najma kwanini kaba…”Edna alijikuta akishindwa kumalizia sentensi yake kutokana na mabadiliko hayo ya ghafla ya Najma.

Upande wa Roma macho yake yote alikuwa ameyakodoa upande wa Najma na Najma na yeye licha ya kwamba alikuwa akijaribu kuongea na watu wanaomzunguka , lakini kuna muda alikuwa akiangalia upande wa Roma , alikuwa kama mtu ambaye alikuwa akihakikisha kwamba Roma anamuona kile anachokifanya.

Roma wasiwasi palepale ulimvaa , aliona huenda kuna kitu kibaya kinaweza kumtokea na hata kile kinachoendelea ni namna ya Najma kufanya makusudi mbele yake.

Roma alianza kukosa uvumilivu na kutaka kusimama kusogea upande wao , lakini Edna alimshika kumzuia.

“Unataka kufanya nini?”

“Siwezi kumwangalia akiyaharibu maisha yake”

“Kwahio kipi utafanya wakati mtu kafanya maamzui yeye mwenyewe , au unapanga kumuua Park Jonghyun , wewe ni nani mpaka uingilie maisha yao, na kama utafanya hiko unachodhamiria ni kama unamwambia Najma kwamba ulikuwa ukidanganya kuhusu maneno yako”Aliongea Edna.
 
SEHEMU YA 520.

Roma aliguswa na maneno ya Edna , ni kweli kabisa yeye ndio aliemwambia Najma kukaa nae mbali , hivyo alikuwa na haki ipi ya kuingilia maisha yake na kumpangia mtu wa kutoka nae kimapenzi..

“Najua una wasiwasi kwasababbu unamjali , unaonaje kama mimi nikiongea na Najma baada ya hapa , najua atakasirika sana kama wewe ukiingilia maisha yake”Alishauri Edna.

Roma aliona alichokiongea mke wake kinaleta maana zaidi kuliko kile alichokuwa akipanga yeye , hivyo alitingisha kichwa kukubali na kisha akakaa.

“Basi hili nitakuachia ulifanyie kazi wewe , sitaki kuona maisha yake yakiharibika kwasababu ya kunikomoa mimi”Aliongea na kumfanya Edna kutingisha kichwa kukubaliana nae, hata hivyo Edna bado alimchukulia Najma kama rafiki yake na ndio maana alitaka kuongea nae na kumshauri , alijua kabisa Jonhyun hakuwa mtu sahihi kwake na mara nyingi watu wa ngozi nyeupe kama hao wanatawaliwa na ule ubaguzi wa rangi hivyo Najma angeishia kutumika tu na kuachwa , lakini pia kuna dalili ambazo Roma na Edna wanaziona si nzuri kwa Jonghyun, ni kama walikuwa wakimhesabia siku za uhai wake.

Baada ya muda mfupi hatimae sherehe ilianza rasmi na Park Juan alitoa kwanza salamu kwa kila mmoja na kufungua sherehe hio na kisha akamwita Yezi mbele

Uzuri wa Yezi uliwaaacha hoi wanaume wengi ndani ya hilo eneo , ijapokuwa Yoonhee alikuwa na uzuri wa ajabu lakini ilionyesha kadri Yezi anavyozidi kuwa mkubwa ndio uzuri wake huongezeka zaidi.

Baada ya Park Juan kumtambulisha rasmi Yezi kama mjukuu wake ,Yezi alipewa nafasi ya kusalimiana na kila mmoja huku akijitahidi kuweka tabasamu la urafiki , alionyesha kujiamini na ilionekana mafunzo aliokuw akipewa ameyaelewa vizuri.

Park Juna alifurahishwa kuona watu wengi wamempokea Yezi kwasifa kedekede na aliona alikuwa amekamilisha jambo kubwa kwenye maisha yake , ya kurmrudisha mjukuuu wake huyo nyumbani.

Wana ukoo wote wa Park walikuwepo kasoro mtu mmoja tu , ambaye ni Yoon Hee , ijapokuwa wanaukoo hao hawakupendezwa na uwepo wa Yezi , lakini walijitahidi kuonyesha sura za furaha na kumpenda mbele ya kila mtu.

Dakika nyingine mbele Park Juan alienda mpaka kwenye jukwaa na kisha akaomba utulivu wa kila mmoja , ilionyesha kuna kitu ambacho alikuwa akitaka kuongea.

“Leo licha ya kwamba ni sherehe ya kumkaribisha nyumbani mjukuu wangu lakini ningependa kuchukua nafasi hii kutoa tangazo , Namtangaza Yezi mjukuu wangu kuwa mrithi wangu , atakuwa ndio mrithi halali wa ukoo wote na Kampuni ya Starmoon , asanteni”Aliongea na kisha akainama kamaishara ya heshima mbele ya wageni wake.

Lakini sasa palepale hali ilibadilika kwani ile anainama alienda mzima mzima na kudondoka chini na palepale akapoteza fahamu na kufanya kundi lote kupiga makelele.

Kati ya wote waliokuwa kwenye wasiwasi mkubwa ni Yeiz ambaye alitoa kilio na kukimbilia alipodondoka baba yake na kuanza kuita jina lake mara nyingi lakini hakukuwa na urejesho kwani Park Juan alikuwa tayari amekwisha kupoteza fahamu.

“Ita Ambulance haraka”Park Jieyon aliongea kwa kupaniki, upande wa Park Jonghyun alisogea haraka mpaka kwenye steji huku akiita jina la babu yake akionyesha wasiwasi lakini kwenye moyo wake akiwa na furaha.

Miuda huo huo mabodigadi walimzingira Park Juan ili watu wasisogelee , Roma na Edna wenyewe walikuwa wamesimama na upande wa Clark palepale alishikilia gauni lake na kukimbia kuelekea mbele.

Gong Gyechung alimpa ishara Dokta Lee kuangalia hali ya mgonjwa na palepale alikimbia kuelekea mbele na akawapa maelekezo mabodigadi kukaa mbali na mgonjwa kwani yeye ni daktari, alikuwa ndio aliekuwa wa kwanza kufika kabla ya Clark na alitumia vidole viwili kumpima mgonjwa kuona kama bado anapumbua.

“Msipaniki , bado anapumbua ninawahakikishia nitayaokoa maisha yake baada ya kupelekwa hospitalini”Aliongea Dokta Lee.

“Dokta Lee ni nini lakini kilichompata babu yangu?”Aliuliza Park Jonghyun.

“Sina uhakika bado , lakini naweza kushuku ni kutokana na uvimbe uliopo kwenye ini lake , tunaweza kuthibisha baada ya kumfanyia vipimo”

Clark ambaye ndio kwanza anafika kwenye steji alisukuma a watu kumpisha ili kumuona mgonjwa na baada ya kumfikia alichuchumaa na kuweka mkono wake kwenye kifua cha Park Juan na hakuna ambaye alimzuia kwani walikuwa wakijua ni daktari.

“Dokta Clark kuna kitu umeweza kupata?”Aliuliza Park Jiyeon.

“Hali yake ni ngumu kwasasa kutokana na makadirio yangu”Aliongea

“Dokta Clark acha kuwaogopesha , daktari hawezi kutoa majibu kabla ya kupitia vipimo”Aliongea Dokta Lee lakini Clark hakumjali na alisimama na kisha akaondoka kwenye steji huku wageni wakianza minong’ono ya chini chini.

Sherehe yote ilifika mwisho mara baada ya king’ora cha gari la kubebea wagonjwa kufika na Park Juan alichukuliwa kwa haraka na kupelekwa hospitalini.

Yezi alikuwa akilia na kumfanya Edna na Roma kuingiwa na wasiwasi na ilibidi wafanye maamzi ya kuelekea huko huko hospitalini .

Hospirali aliopelekwa Park juan ilikuwa ni Seol universtiy hospital , moja ya hospitali kubwa ndani ya Korea ambayo wamiliki wakuu wa hisa ni familia ya Gong

Baada ya kupewa matibabu ya dharula , hatimae Park Juan aliweza kurejewa na fahamu na kulazwa katika wodi ya ICU.

Karika chumba kidogo ndani ya hospitali hio familia ya Park pamoja na ya Gong walikuwa na kikao wakijadiliana hali ya Park Juan na watu ambao wangehusika na matibabu yake mpaka pale atakapokuwa amepona kabisa.

Clark na wanafunzi wake walikuwepo , lakini pia Dokta lee na timu yake ya madaktari walikuwepo , lakini pia Edna na Roma pia walihudhuria..

Upande wa wanafunzi wa Profesa Clark mara baada ya kuangalia picha za CT Scan walijikuta walikaa kimya huku wakioneysha wasiwasi kwenye nyuso zao.

“Dokta lee nini kimemtokea babu yangu? Kama hili halihusiani na tatizo lake la ini , nini kingine kimempata?”Aliuliza Park Jonghyun.

“Miaka mitatu iliopita raisi Park aliweza kufanyiwa upasuaji wa BATISTA , nadhani unakumbuka huo upasuaji?”Aliongea Dokta le.

“Upajuaji wa BATISTA , unamaanisha ule wa moyo?”Aliuliza Park Jiyeon.

“Upo sahihi na hili ambalo limetokea leo linahusiana na shida yake ya moyo”Aliongea lakini kati ya watu ambao hawakuwa wamelewa ni Yezi.

“Dokta ,nini maana ya upasuaji wa BATISTA?”Aliuliza Yezi.

“BATISTA ni aina ya upasuaji wa moyo ambao umegunduliwa na Profesa Batista ndio maana ukapewa jina hilo , ni mchakato wa kuondoa sehemu ya Ventrikali(Ventricular) ili kupunguza ukubwa wa moyo , ni upasuaji unaochanganya sana , lakini pia ni upasuaji muhimu kwa mgonjwa ambaye ana shida ya moyo lakini hawezi kupata moyo mwingine kwa ajili ya kubadilishiwa”Alijibu Dokta Lee.

“Upo sahihi , babu ni kweli alifanyiwa upasuaji wa BATISTA lakini yule daktari wa kimarekani alituhakikishai kwamba upasuaji ulienda vizuri na umefanikiwa”Aliongea Park Jonghyun.

“Umefanikiwa ndio lakini kilichomtokea babu yako sio kwasababu upasuaji ulifeli , moyo wake umedhorota sana kutokana na hali hio , hivyo licha ya kwamba alifanyiwa upasuaji wa BATISTA haikumaanisha kwamba moyo wake umepona kwa asilimia zote ,, kuna sabababu nyingi husianishi ambazo huchangia moyo kutorudi kwenye hali yake ya kawaida na kwasababu hio mzunguko wake wa damu mara nyingi unaathirika na ndio maana akadondoka leo”Aliongea Dokta Clark kwa kirefu na kumfanya kila mmoja kuwa katika hali ya kuchanganyikiwa lakini kwa wanafunzi wake walivutiwa sana na maelezo yake.

“Uchambuzi wako ni wenye kueleweka , je unajua namna ya kumfanyia matibabu?”Aliuliza Dokta Lee.

“Dokta Lee nadhani kila kitu kipo wazi , je ni matibabu gani yanamfaa mgonjwa ambaye moyo wake unaonyesha dalili za kufeli, jibu ni kwamba unapaswa kubadilishiwa(heart tranplan)”Aliongea na kumfanya Dokta Lee kuona ameuliza swali la kijinga kama daktari.,

“Doctor , please hear a layman out , I don’t think your treatment make sense , I might not be a doctor but according to what I know President Park Juan’s body will not be able to withstand two major surgeries for an organ transplant”

“Dokta tafadhari naomba unisikilize mimi mtu wa kawaida, sidhani kama mbinu yako ya kimatibabu inaingia akilini , naweza nisiwe daktari lakini kwa kile ninachojua mwili wa raisi Park hauwezi kuhimili upasuaji mkubwa wa ana mbili wa kubadilisha ogani”Aliongea Gong Gyechung na kufanya watu wote wamwangalie Clark kutaka majibu yake.

Kuna episode tano mbele za hapo Korea tu , sio kama nairefusha kama watu mnavotoa maoni ila mpango wa Athena unaanzia kukamilika ndani ya hio nchi.

Unafikiri atapona , Vipi Najma atakubali kushauriwa na Edna.

TUTAENDELEA 0687151346 watsapp and telegram only
 
SEHEMU YA 520.

Roma aliguswa na maneno ya Edna , ni kweli kabisa yeye ndio aliemwambia Najma kukaa nae mbali , hivyo alikuwa na haki ipi ya kuingilia maisha yake na kumpangia mtu wa kutoka nae kimapenzi..

“Najua una wasiwasi kwasababbu unamjali , unaonaje kama mimi nikiongea na Najma baada ya hapa , najua atakasirika sana kama wewe ukiingilia maisha yake”Alishauri Edna.

Roma aliona alichokiongea mke wake kinaleta maana zaidi kuliko kile alichokuwa akipanga yeye , hivyo alitingisha kichwa kukubali na kisha akakaa.

“Basi hili nitakuachia ulifanyie kazi wewe , sitaki kuona maisha yake yakiharibika kwasababu ya kunikomoa mimi”Aliongea na kumfanya Edna kutingisha kichwa kukubaliana nae, hata hivyo Edna bado alimchukulia Najma kama rafiki yake na ndio maana alitaka kuongea nae na kumshauri , alijua kabisa Jonhyun hakuwa mtu sahihi kwake na mara nyingi watu wa ngozi nyeupe kama hao wanatawaliwa na ule ubaguzi wa rangi hivyo Najma angeishia kutumika tu
 
Back
Top Bottom