singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #2,841
SEHEMU YA 514.
Tarehe mbili ya mwezi wa sita ndio safari ya kwenda Korea ilianza rasmi, Edna ilikuwa mara yake ya kwanza kwenda Korea tofauti na Roma ambaye alishawahi kufika mara kadhaa, hivyo kwake alikuwa kama mwenyeweji.
Edna alikuwa na shauku ya kuona jiji la Seoul kwani ndio mahali ambapo tamthilia nyingi za kikorea zilikuwa zikiigiziwa na isitoshe kwa kipindi hiko alikuwa mpenzi kweli wa filamu hizo.
Upande wa Roma sio kwamba alikuwa na shauku kubwa ya kwenda Korea , kwake taifa kama hilo alilichukulia kama dogo kwenda na isitoshe hakuwa na koneksheni sana Korea tofauti na mataifa ya Amerika na Ulaya , lakini kwasababu alikuwa akienda kwa ajili ya Yezi hakujali sana kukaa muda mrefu kwenye ndege japo swala hilo kwake hakulipenda kwani alijiambia alikuwa na uwezo wa kupaa tu na kuibukia moja kwa moja Korea kuliko kupoteza muda , lakini kwasababu ya Edna aliona afuatishe hatua za kawaida za kibinadamu.
Jini la Seoul lilikuwa na joto la wastani , hakukuwa na baridi sana wala joto sana kwa mwezi huo, ki ufupi hali yake ya hewa ni ile ya kuzoeleka kwa wepesi.
Muda wa jioni ndio ambao waliweza kutua na ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Incheon.
Park Jonghyun ndio mtu ambaye alipewa jukumu la kuwapokea kiwanjani hapo na baada ya kuwaona wageni wake alijjikuta akifaurahi huku akipeana nao mikono ya salamu kwa ukarimu wa hali ya juu akiwakaribisha Korea.
“Yezi amewakumbuka sana , alitaka hata kuja hapa kuwapokea lakini yupo na ratiba ya masomo na mwalimu wake Vivian hivyo kashindwa kufika”Aliongea Park Jonghyun.
“Teacher Vivian ? is she a westerner?”aliuliza Edna akimaanisha je huyo mwalimu Vivian ni mzungu , kwani ni ngumu kwa Korea kukutana majina ya aina hio .
“She is not a westerner but a Tanzanian woman who is fluent in english and Korean my grandfather’s proffesor from states recommended his best student”Aliongea akimaanisha kwamba sio mmagharibu bali ni mwanamke wa kitanzania ambaye anajua kuongea lugha ya kikorea na kingereza na moja wapo ya Profesa kutoka Marekani ambaye ni rafiki yake na Park Juan ndio alimpendekeza Vivian kumfundisha Yezi.
“Kwanini mnabana sana na masomo wakati ana muda wa kutosha wa kwenda chuoni?”Aliuliza Roma kwa kikorea na Edna hakutaka kuingilia maongezi yao tena zaidi ya kugeukia dirisha kuangalia mandhari ya jiji hilo la kuvutia.
Seoul ulikuwa mji mkubwa wenye miundombin ya kuvutia , ilimfikirisha Edna na kujiambia jiji hilo lingekuwa Tanzania angejivunia sana.
Baada ya madakika kadhaa ya kuwa barabaranni hatimae waliweza kufika kwenye jumba la kifahari la Park Juan ambalo lilikuwa ndani ya wilaya maarufu ufahamikao kama Gangnam.
Lilikuwa jumba kubwa mno ambalo lilimfanya Edna kuona kweli Yezi amekuwa mtoto wa kishua sio kwa mandhari nzuri kama hio.
Kwa haraka haraka Roma aligundua kuna zaidi ya watu waliokuwa wakiwasubiria hapo ndani , kwani nje kulikuwa n magari mengi ya kifahari yaliokuwa yameegeshwa.
Kwanzia mlangongi mpaka ndani kulikuwa na wahudumu waliokuwa wamejipanga mstari wakiwainamishia vichwa kwa heshima , jambo ambalo lilimmfanya Edna kushanganzwa na utamaduni huo , lakini mara baada ya kukumbuka kwenye filamu za kikorea maisha yapo hivyo alituliza mshangao wake.
Baada ya kuingia ndani kabisa ya eneo la sebuleni waliweza kukutana na watu wengi wa rangi nyeupe wakiwa wamesimama kwa ishara ya kuwakaribisha ni mtu mmoja pekee ambaye alikuwa amekaa huku akiwa ameshikilia fimbo ya kutembelea.
Alikuwa ni Park Juan na Roma na Edna waliweza kumtambua kwani alikuwa maarufu na isitoshe picha zake washawahi kuziona mara kibao.
Upande wa Roma mara baada ya kuwakagua watu wote waliokuwa hapo ndani mtu pekee aliemvutia ni bwana wa makamo ambaye alikuwa amekaa nyuma ya Sofa ambalo amekalia Park Juan , uso wake kwa namna ambavyo ulikuwa ukionekana ni kama mtu ambaye hakujali chochote ambacho kinaendelea hapo ndani na macho yake yote yalikuwa kwenye mkono wake wa kulia ambao alikuwa ameshikilia gololi atu akizichezesha kwa kuzisuguanisha.
Roma kwa haraka haraka aliweza kugundua mtu yule alikuwa ni hatari sana , licha ya kwamba hakuwa na nguvu za kijini kama yeye na hisia zake zilimwambia lazima atakuwa ni Bodigadi wa babu yake yezi yaani Park Juan.
Upande wa kulia alikuwa amesimama Park Jiyeon na Haoming na kwa ufupi aliokuwa nao Haoming alimfanya kuonekana mdogo mbele ya Park Jieyeon.
Msichana mwingine mrembo ambaye aliwashangaza Roma na Edna simwingine bali ni msanii Yoon Hee .
Kwa namna alivyojipamba ilimfanya kupendeza zaidi na kutokana na weupe wake lipsi zake nyekundu zilionekana vizuri zaidi , alikuwa amevalia kitop cha rangi nyeusi cha mkato wa V huku shingoni akiwa amejifunga scarf.
“Karibuni sana , naona mmeshangazwa kuniona hapa?”aliongea Yoon Hee kwa kingereza huku akimwangalia Roma kwa kebehi.
“YoonHee kuwa mtaratibu?”Alifoka Park Juan.
“Yes grandfather”Alijibu.
“Mr Roma na Miss Edna nice to meet you , mimi ni shangazi yake na Yezi nafahamika kwa jina la Park Jiyeon na huyu ni mume wangu anaitwa Haoming , Yoonhee ni mtoto wetu wa kike , asanteni kwa kumkarimu vizuri alipokuwa Tanzania”aliongea Park jiyeon huku akionyesha tabasamu.
Roma na Edna sasa waliweza kufahamu kumbe YoonHee na Yezi ni wajukuu wa Park juan.
Utofauti wao tu ni kwamba Yezi yeye alikuwa ni mtoto wa mtoto wa kwanza wa Park Juan na Yoonhe alikuwa ni mtoto wa Park Jieyeon , hivyo mwenye uzito zaidi katika familia alikuwa ni Yezi kwa tamadunni za Korea,
Roma alikumbuka kitu kipindi cha nyuma nchini Tanzania Yoonhee aliweza kugombana na Park Jonghyun na walionekana kama walikuwa wapenzi na palepale alijiuliza je hawakuwa ndugu?
Baada ya utambulisho mfupi Park Juani aliwaonyeshea ishara ya kuketi na ni muda huo huo ambao waliweza kusikia sauti wanayoifahamu ikiwaita.
“Bro Roma , Sister Edna”Alikuwa ni Yezi ambaye alitokea huku akikimbia kushuka ngazi kwa shangwe.
Walikuwa hawajamuona kwa kipindi kirefu na waliweza kumuona ameongezeka na kuwa mzuri zaidi , nywele zake zilionekana kuwa nyeusi zaidi tofauti na alivyokuwa Tanzania , ijapokuwa waligundua alikuwa amekonda kidogo lakini ilimfanya kupendeza zaidi na zaidi.
Roma alijiambia Rufi alikuwa akianza kuwa kama mkorea halisi sasa na kwa uzuri wake hakuhitaji kufanya hata upasuaji wa sura ili kuonekana mrembo kama ilivyotabia za wanawake wengi wa Korea.
“Kuwa makini usije ukadondoka”Aliongea Park Juan kwa sauti akimtahadharisha mjukuu wake na aliweza kuonyesha wasiwasi namna ambavyo Yezi anashuka kiasi kwamba Edna na Roma waligundua kuna mapenzi makubwa sana kati ya Yezi na babu yake.
Upande wa Yoonhee alijikuta akibetua mdomo kwa kejeli ni kama alimuona Yezi ni kituko , alionyesha waziwazi hakuwa akimpenda , lakini Yezi hata hakulitambua hilo kwani macho yake yote yalikuwa kwa Roma na Edna na alianza kumkumbatia Roma na kisha akahamia kwa Edna.
“Jamani siamini kama mmefika , nilitaka nije niwapokee lakini mwalimu wangu amenizuia , nimejikutaka hata nikipoteza mudi kwasababu hio”
“Ulikuwa ukosoma hadi muda huu?”aliuliza Edna na Yezi alijibu kwa kingereza ili kumfanya na babu yake asikie.
“Mwalimu Vivian ni mkali sana na babu hataki hata kunisaidia?”Aliongea na kumfanya Park Juan kucheka.
“Naweza kuruhusu ufanye kila unachotaka , lakini siwezi kukuona unacheza likija swala la masomo yako , maelfu ya watu wanaweza kupoteza ajira zao kama hutakuwa na elimu ya kutosha ya kuongoza kampuni”Aliongea Park Juan na kuwafanya watu waliokuwa hapo ndani kuona wivu ndani kwa ndani huku wakiweka tabasamu bandia katika nyuso zao.
Muda huo huo mwanamke mwingine mrembo alionekana akishuka kutoka juu kwa madaha kabisa , alikuwa amevalia gauni ambalo limeishia magotini pamoja na koti kwa juu alionekana kuwa mrembo mno na rangi yake ya kiafrika.
“Teacher Vivian you’ve worked hard , stay back and have dinner with us”Aliongea Park Jonghyun ambaye alikuwa akimwangalia Vivian kwa macho ya matamanio kweli.
“Najma…!!”Roma ndio aliekuwa wa kwanza kumtambua Najma, jina la Vivian lilikuwa jipya kwake na ukijumlisha na mavazi yake ya kisasa ndio kilichomfanya kutomfahamu kwa haraka na sio kwake tu hata kwa Edna vilevile na aliweza kumtambua mara baada ya kumsikia Roma anaita hilo jina.
Najma hata yeye alishangazwa na uwepo wa Roma na Edna hapo ndani na mshtuko wake uliwafanya kila mmoja kushangaa na kuamini lazima wanafahamiana.
Edna alijikuta maswali kibao yakiianza kupita kwenye kichwa chake , tokea siku ambayo aliweza kupata taarifa kutoka kwa Suzzane juu ya Najma kukatisha ufadhili wake wa masomo , sasa alishangaa Najma ambaye alikuwa akiitwa Vivian yupo nchini Korea lakini hakutaka kuumiza kichwa sana aliamini ana muda mzuri wa kuongea na Najma.
“Kwahio wewe ndio mwalimu Vivian?”Aliongea Edna huku akijitahidi kutabasamu , Najma alikuwa ni rafiki yake wa kwanza kukutana nae katika kituo cha kulelea watoto cha Son and daughter orphanage.
Roma alijikuta kumbukumbu zake zikimpeleka nyuma sana kipindi ambacho ndio kwa mara ya kwanza anafika nchini Tanzania , namna alivyoweza kukutana na Najma na kumpokea kwa ukarimu na kumpatia chumba katika nyumba yao na kupanga , alikumbuka vitu vingi namna mrembo huyo alivyotokea kumpenda na yeye kumpotezea.
Ijapokuwa Najma yule na huyu walikuwa mtu mmoja lakini Najma mpya alikuwa wa tofauti sana , huyu alionekana kama mwanamke aliekomaa kiakili mno na kuzidi kustaarabika.
Najma wa kipindi kile alikuwa akivaa Hijab lakini huyu alikuwa kichwa wazi huku nywele zake zikiwa ndefu zilizowekwa dawa ya kupendeza na ilikuwa ni kama ameachana na maswala ya dini.
“Mr Roma and Mrs Edna its been a long time”Aliongea kwa kingereza cheye rafudhi safi na kauli yake iliwashangaza mno Park jonghyun na wengine.
Tarehe mbili ya mwezi wa sita ndio safari ya kwenda Korea ilianza rasmi, Edna ilikuwa mara yake ya kwanza kwenda Korea tofauti na Roma ambaye alishawahi kufika mara kadhaa, hivyo kwake alikuwa kama mwenyeweji.
Edna alikuwa na shauku ya kuona jiji la Seoul kwani ndio mahali ambapo tamthilia nyingi za kikorea zilikuwa zikiigiziwa na isitoshe kwa kipindi hiko alikuwa mpenzi kweli wa filamu hizo.
Upande wa Roma sio kwamba alikuwa na shauku kubwa ya kwenda Korea , kwake taifa kama hilo alilichukulia kama dogo kwenda na isitoshe hakuwa na koneksheni sana Korea tofauti na mataifa ya Amerika na Ulaya , lakini kwasababu alikuwa akienda kwa ajili ya Yezi hakujali sana kukaa muda mrefu kwenye ndege japo swala hilo kwake hakulipenda kwani alijiambia alikuwa na uwezo wa kupaa tu na kuibukia moja kwa moja Korea kuliko kupoteza muda , lakini kwasababu ya Edna aliona afuatishe hatua za kawaida za kibinadamu.
Jini la Seoul lilikuwa na joto la wastani , hakukuwa na baridi sana wala joto sana kwa mwezi huo, ki ufupi hali yake ya hewa ni ile ya kuzoeleka kwa wepesi.
Muda wa jioni ndio ambao waliweza kutua na ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Incheon.
Park Jonghyun ndio mtu ambaye alipewa jukumu la kuwapokea kiwanjani hapo na baada ya kuwaona wageni wake alijjikuta akifaurahi huku akipeana nao mikono ya salamu kwa ukarimu wa hali ya juu akiwakaribisha Korea.
“Yezi amewakumbuka sana , alitaka hata kuja hapa kuwapokea lakini yupo na ratiba ya masomo na mwalimu wake Vivian hivyo kashindwa kufika”Aliongea Park Jonghyun.
“Teacher Vivian ? is she a westerner?”aliuliza Edna akimaanisha je huyo mwalimu Vivian ni mzungu , kwani ni ngumu kwa Korea kukutana majina ya aina hio .
“She is not a westerner but a Tanzanian woman who is fluent in english and Korean my grandfather’s proffesor from states recommended his best student”Aliongea akimaanisha kwamba sio mmagharibu bali ni mwanamke wa kitanzania ambaye anajua kuongea lugha ya kikorea na kingereza na moja wapo ya Profesa kutoka Marekani ambaye ni rafiki yake na Park Juan ndio alimpendekeza Vivian kumfundisha Yezi.
“Kwanini mnabana sana na masomo wakati ana muda wa kutosha wa kwenda chuoni?”Aliuliza Roma kwa kikorea na Edna hakutaka kuingilia maongezi yao tena zaidi ya kugeukia dirisha kuangalia mandhari ya jiji hilo la kuvutia.
Seoul ulikuwa mji mkubwa wenye miundombin ya kuvutia , ilimfikirisha Edna na kujiambia jiji hilo lingekuwa Tanzania angejivunia sana.
Baada ya madakika kadhaa ya kuwa barabaranni hatimae waliweza kufika kwenye jumba la kifahari la Park Juan ambalo lilikuwa ndani ya wilaya maarufu ufahamikao kama Gangnam.
Lilikuwa jumba kubwa mno ambalo lilimfanya Edna kuona kweli Yezi amekuwa mtoto wa kishua sio kwa mandhari nzuri kama hio.
Kwa haraka haraka Roma aligundua kuna zaidi ya watu waliokuwa wakiwasubiria hapo ndani , kwani nje kulikuwa n magari mengi ya kifahari yaliokuwa yameegeshwa.
Kwanzia mlangongi mpaka ndani kulikuwa na wahudumu waliokuwa wamejipanga mstari wakiwainamishia vichwa kwa heshima , jambo ambalo lilimmfanya Edna kushanganzwa na utamaduni huo , lakini mara baada ya kukumbuka kwenye filamu za kikorea maisha yapo hivyo alituliza mshangao wake.
Baada ya kuingia ndani kabisa ya eneo la sebuleni waliweza kukutana na watu wengi wa rangi nyeupe wakiwa wamesimama kwa ishara ya kuwakaribisha ni mtu mmoja pekee ambaye alikuwa amekaa huku akiwa ameshikilia fimbo ya kutembelea.
Alikuwa ni Park Juan na Roma na Edna waliweza kumtambua kwani alikuwa maarufu na isitoshe picha zake washawahi kuziona mara kibao.
Upande wa Roma mara baada ya kuwakagua watu wote waliokuwa hapo ndani mtu pekee aliemvutia ni bwana wa makamo ambaye alikuwa amekaa nyuma ya Sofa ambalo amekalia Park Juan , uso wake kwa namna ambavyo ulikuwa ukionekana ni kama mtu ambaye hakujali chochote ambacho kinaendelea hapo ndani na macho yake yote yalikuwa kwenye mkono wake wa kulia ambao alikuwa ameshikilia gololi atu akizichezesha kwa kuzisuguanisha.
Roma kwa haraka haraka aliweza kugundua mtu yule alikuwa ni hatari sana , licha ya kwamba hakuwa na nguvu za kijini kama yeye na hisia zake zilimwambia lazima atakuwa ni Bodigadi wa babu yake yezi yaani Park Juan.
Upande wa kulia alikuwa amesimama Park Jiyeon na Haoming na kwa ufupi aliokuwa nao Haoming alimfanya kuonekana mdogo mbele ya Park Jieyeon.
Msichana mwingine mrembo ambaye aliwashangaza Roma na Edna simwingine bali ni msanii Yoon Hee .
Kwa namna alivyojipamba ilimfanya kupendeza zaidi na kutokana na weupe wake lipsi zake nyekundu zilionekana vizuri zaidi , alikuwa amevalia kitop cha rangi nyeusi cha mkato wa V huku shingoni akiwa amejifunga scarf.
“Karibuni sana , naona mmeshangazwa kuniona hapa?”aliongea Yoon Hee kwa kingereza huku akimwangalia Roma kwa kebehi.
“YoonHee kuwa mtaratibu?”Alifoka Park Juan.
“Yes grandfather”Alijibu.
“Mr Roma na Miss Edna nice to meet you , mimi ni shangazi yake na Yezi nafahamika kwa jina la Park Jiyeon na huyu ni mume wangu anaitwa Haoming , Yoonhee ni mtoto wetu wa kike , asanteni kwa kumkarimu vizuri alipokuwa Tanzania”aliongea Park jiyeon huku akionyesha tabasamu.
Roma na Edna sasa waliweza kufahamu kumbe YoonHee na Yezi ni wajukuu wa Park juan.
Utofauti wao tu ni kwamba Yezi yeye alikuwa ni mtoto wa mtoto wa kwanza wa Park Juan na Yoonhe alikuwa ni mtoto wa Park Jieyeon , hivyo mwenye uzito zaidi katika familia alikuwa ni Yezi kwa tamadunni za Korea,
Roma alikumbuka kitu kipindi cha nyuma nchini Tanzania Yoonhee aliweza kugombana na Park Jonghyun na walionekana kama walikuwa wapenzi na palepale alijiuliza je hawakuwa ndugu?
Baada ya utambulisho mfupi Park Juani aliwaonyeshea ishara ya kuketi na ni muda huo huo ambao waliweza kusikia sauti wanayoifahamu ikiwaita.
“Bro Roma , Sister Edna”Alikuwa ni Yezi ambaye alitokea huku akikimbia kushuka ngazi kwa shangwe.
Walikuwa hawajamuona kwa kipindi kirefu na waliweza kumuona ameongezeka na kuwa mzuri zaidi , nywele zake zilionekana kuwa nyeusi zaidi tofauti na alivyokuwa Tanzania , ijapokuwa waligundua alikuwa amekonda kidogo lakini ilimfanya kupendeza zaidi na zaidi.
Roma alijiambia Rufi alikuwa akianza kuwa kama mkorea halisi sasa na kwa uzuri wake hakuhitaji kufanya hata upasuaji wa sura ili kuonekana mrembo kama ilivyotabia za wanawake wengi wa Korea.
“Kuwa makini usije ukadondoka”Aliongea Park Juan kwa sauti akimtahadharisha mjukuu wake na aliweza kuonyesha wasiwasi namna ambavyo Yezi anashuka kiasi kwamba Edna na Roma waligundua kuna mapenzi makubwa sana kati ya Yezi na babu yake.
Upande wa Yoonhee alijikuta akibetua mdomo kwa kejeli ni kama alimuona Yezi ni kituko , alionyesha waziwazi hakuwa akimpenda , lakini Yezi hata hakulitambua hilo kwani macho yake yote yalikuwa kwa Roma na Edna na alianza kumkumbatia Roma na kisha akahamia kwa Edna.
“Jamani siamini kama mmefika , nilitaka nije niwapokee lakini mwalimu wangu amenizuia , nimejikutaka hata nikipoteza mudi kwasababu hio”
“Ulikuwa ukosoma hadi muda huu?”aliuliza Edna na Yezi alijibu kwa kingereza ili kumfanya na babu yake asikie.
“Mwalimu Vivian ni mkali sana na babu hataki hata kunisaidia?”Aliongea na kumfanya Park Juan kucheka.
“Naweza kuruhusu ufanye kila unachotaka , lakini siwezi kukuona unacheza likija swala la masomo yako , maelfu ya watu wanaweza kupoteza ajira zao kama hutakuwa na elimu ya kutosha ya kuongoza kampuni”Aliongea Park Juan na kuwafanya watu waliokuwa hapo ndani kuona wivu ndani kwa ndani huku wakiweka tabasamu bandia katika nyuso zao.
Muda huo huo mwanamke mwingine mrembo alionekana akishuka kutoka juu kwa madaha kabisa , alikuwa amevalia gauni ambalo limeishia magotini pamoja na koti kwa juu alionekana kuwa mrembo mno na rangi yake ya kiafrika.
“Teacher Vivian you’ve worked hard , stay back and have dinner with us”Aliongea Park Jonghyun ambaye alikuwa akimwangalia Vivian kwa macho ya matamanio kweli.
“Najma…!!”Roma ndio aliekuwa wa kwanza kumtambua Najma, jina la Vivian lilikuwa jipya kwake na ukijumlisha na mavazi yake ya kisasa ndio kilichomfanya kutomfahamu kwa haraka na sio kwake tu hata kwa Edna vilevile na aliweza kumtambua mara baada ya kumsikia Roma anaita hilo jina.
Najma hata yeye alishangazwa na uwepo wa Roma na Edna hapo ndani na mshtuko wake uliwafanya kila mmoja kushangaa na kuamini lazima wanafahamiana.
Edna alijikuta maswali kibao yakiianza kupita kwenye kichwa chake , tokea siku ambayo aliweza kupata taarifa kutoka kwa Suzzane juu ya Najma kukatisha ufadhili wake wa masomo , sasa alishangaa Najma ambaye alikuwa akiitwa Vivian yupo nchini Korea lakini hakutaka kuumiza kichwa sana aliamini ana muda mzuri wa kuongea na Najma.
“Kwahio wewe ndio mwalimu Vivian?”Aliongea Edna huku akijitahidi kutabasamu , Najma alikuwa ni rafiki yake wa kwanza kukutana nae katika kituo cha kulelea watoto cha Son and daughter orphanage.
Roma alijikuta kumbukumbu zake zikimpeleka nyuma sana kipindi ambacho ndio kwa mara ya kwanza anafika nchini Tanzania , namna alivyoweza kukutana na Najma na kumpokea kwa ukarimu na kumpatia chumba katika nyumba yao na kupanga , alikumbuka vitu vingi namna mrembo huyo alivyotokea kumpenda na yeye kumpotezea.
Ijapokuwa Najma yule na huyu walikuwa mtu mmoja lakini Najma mpya alikuwa wa tofauti sana , huyu alionekana kama mwanamke aliekomaa kiakili mno na kuzidi kustaarabika.
Najma wa kipindi kile alikuwa akivaa Hijab lakini huyu alikuwa kichwa wazi huku nywele zake zikiwa ndefu zilizowekwa dawa ya kupendeza na ilikuwa ni kama ameachana na maswala ya dini.
“Mr Roma and Mrs Edna its been a long time”Aliongea kwa kingereza cheye rafudhi safi na kauli yake iliwashangaza mno Park jonghyun na wengine.