Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Nakushukuru sana Kaka Singanojr kwa usanifu wako wa riwaya hii.
nakutakia jioni njema.
Adios 390.
 
dah eti kupitia dhiki ndio mpo levo iyo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
404
Shukrani Kaka Singanojr.
adios
 
Duh! Hali ni zogolezagala shaghalabhaghala😎😎😎

413
Adios
Kaka Singanojr.
 
Jamaa anatamaa za kijinga sana
Ni muongo wa kutupwa
Katika hili amejiharibia sana
 
Kama vipi mngesaidia kutupia muendelezo kwa sisi tunaosoma JF angalau tusogee mbele manake tumeachwa !
 
Hatariii
 
M
 
Kiukweli hata mimi nlipata taabu kidg mwanzon lakn toka nmeelewa lengo/dhamira ya mwandishi, imenibd niwe tu mwelew Bila kuchukia Bila kinyongo
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI :SINGANOJR.
WATSAPP: 0687151346.

SEHEMU YA 605.
Baiju miguu yake katika vigoti ililelegea palepale mara baada ya kujua mwanamke ambaye hakuwa amemtambua ni Aoiline mkuu wake.
“Bwana wangu , sikujua kama upo hapa tafadhari naomba unisamehe”Aliongea kwa kutetemeka huku akiwa amemsujudia chini , hakuwa tena yule mwenye kiburi.
Aoiline aliachana na Roma na kisha alimsogelea Baiju kwa hatua hafifu huku uso wake ukiwa ni ule wa kichokozi , hakuonyesha kabisa kuwa na hasira.
“Baiju nimepewa ripoti kwamba unakusanya kiwango kikubwa cha mawe ya kiroho kupitia Madanguro , ukiichukulia faida kwa mimi kutokuwa makini na maswala hayo , inaonekana umeweza kuteka majini wanawake kwa tamaa zako”
“Bwana wangu wananisingizia tu , waliochini yangu ndio ambao wamefanya kosa hilo kwa kunipatia rushwa , nitahakikisha nina wahukumu vifo nikirudi”Aliongea Baiju huku akionekana kutengeneza kisingizio.
“Hata mimi naona , kwa hio unasema mimi ndio mkosaji hapa kwa kusingizia si ndio?”Aliongea huku kitingishcha kichwa chake kama mtu ambaye anajaribu kumwelewa.
Baiju alitaka kutingisha kichwa kujaribu kujitetea kwamba hakupaswa kumbebesha lawama zote lakini hakuweza kufanya chochote wala kukubali kama ana kosa na uso wake ulibadilika rangi na kuwa mwekundu kutokana na presha ambayo ilikuwa ikijiandaa kumkumba.
“Umekuwa na mimi kwa zaidi ya miaka mia mbili , nimekufanya uwe Bwana wa mji wangu wa Wingu Jeupe na ukapokea tani na tani za mawe ya kiroho kutoka katika maghala ya mji na watu wengi wakakuonea wivu lakini bado ukaamua kukusanya zaidi Mawe ya kiroho kupitiia Danguro , Ingekuwa ni sawa kama tu ungekuwa ukidanganya hao ambao walikuwa wakipenda kufanya kazi chini yako lakini ukathubutu kuteka wale ambao wanajaribu kupita katika mji wetu , hivi unadhani mimi siwezi kuishi bila wewe , unafikiri mimi ni mwepesi kudanganywa?”
Jasho la baridi lilimtoka Baiju na kuloanisha nguo zake na aliishia kutingisha kichwa chake akiwa amekiinamisha chini akishindwa hata kumwangalia Aoiline.
“Bwana wangu, Sikuwa nikifikiri sawa sawa , tafadhari naomba unisamehe kwa dhambi nilizoafanya kwa zaidi ya karne moja”
“Sawa”Aliongea huku akikusanya nguo za mkono wake na kutingisha kichwa.
“Itakuwa ni ukatili kama sitoweza kukupa nafasi , nitakusamehe kwa kuwateka wasichana wa kijini nyuma ya mgongo wangu”Aliongea na kumfanya Baiju kufurahiswa na maneno yake huku akitaka kuanza kusujudu kwa mara nyingine lakini Aoiline alimkatisha.
“Lakini hata hivyo napaswa kukuadhibu kwa jambo moja”
“Ah..!”Alitoa sauti huku sura yake akipeleka chini kwa mara nyingine akiwa kama amechanganyikiwa.
“Watu wako hususani Huji wameniteka siku ya leo na wakaniingiza kwenye kiroba ,… ningekuwa mrembo wa kukuingizia hela ndani ya Danguro leo kama sio Mr Roma kunisaidia”
Hio ilikuwa ni taarifa mbaya sana kwa Baiju na sasa aliweza kuelewa kwanini Aoiline alibadilisha mwonekanno wake , kila kitu kilikuwa ni mtego wa kumkamata na ufisadi wake.
Ingekuwa afadhari kama angekamata wanawake wengine lakini sasa alikuwa amemsaliti hata Bwana wake hakukuwa na sababu ya kuachwa hai.
Dakika hio alivyojaribu kuunganisha Dot katika akili yake , Baiju alijiambia hakukuwa na faida yoyote ya yeye kuomba kusamehewa au kujitetea na anapaswa kufanya kitu chochote kile ili kuweza kukimbia na kutoka katika hio miliki, alijiambia kama ataweza kufika katika Korongo la Joka , Mfalme wa Majoka lazima angemlinda kwani alikuwa ni jini mwenye uwezo mkubwa wa kimapambano katika levo ya nane.
Baada ya kupatwa na mawazo hayo hakutaka tena kuchelewa, palepale aliita kwa hisia ndege wake mweupe kwa ajili ya kumshambulia Aioline .
Ndege mweupe na yeye akasikia kuitwa na mkuu wake , na palepale lilitoa kilio kikubwa cha juu huku likipiga piga mabawa yake kumsogelea Aoiline moja kwa moja.
Aoline hakuonakana yule mpole tena kwani alibadilika na alikuwa na uso wa kikauzu usio kuwa wa kawaida na kwa Roma ni kama alikuwa akimuona Edna party two, ilikuwa ni kama vile hewa iliokuwa ikimzunguka imeganda.
“Wewe mjinga , unathubutu vipi kujaribu kunipinga mimi?”Aliongea kwa nguvu na palepale kulitokea mwanga kama nguzo mbili nyuma ya gauni lake na nguo moja ya mwanga ilimshikilia yule ndege kwa kumfunga funga.
Roma aliangalia kwa ukaribu zile nguzo zilizokaa kama kamba kamba na palepale ndipo alipogundua ni mikia na pale ndipo alipojihakikishia kweli huyo ni jini ambaye alikuwa akiitwa Mbweha wa mikia tisa.
Mikia yake ilikuwa ni mirefu mno na haikuwa ya kawaida , ilikuwa ni kama boriti au nguzo.
Yule ndege licha ya Roma kumuona mkubwa lakini mbele ya ile mikia alionekana kuwa mdogo mno kwani alikamatwa na akawa hafurukuti kabisa.
Ndege yule alianza kutapa tapa kama vile kuku ambaye anapoteza uhai na ndani ya dakika tu damu zilionekana kuruka juu , ilionekana alikuwa amekamuliwa kwa kiwango kikubwa kiasi cha viungo vyake kuharibika na hata manyonya yake yalianza kusambaa angani.
Sophia alishindwa kabisa kuangalia kitendo kile lakini kwa Roma alikuwa akiona kitu kile kama hasara kwani yule ndege alimpenda na kujiambia angalau kabla ya kutoka katika ulimwengu huo amwendeshe hata mara moja.
Wakati Aoiline akidili na ndege Baiju alikuwa ashakimbia kwa kupaa umbali mrefu kidogo , lakini bahati mbaya kwake ni kwamba mkia mwingine wa Aoiline ulikuwa ukimfukuzia na ulikuwa ukiongezeka urefu kadri alivyokuwa akikimbia kwenda mbali..
Roma ni jambo lingine ambalo lilimshangaza kwani hakuamini kama mkia huo ungekuwa na uwezo wa kuongezeka urefu na kusafiri umbali mrefu tena kwa haraka sana.
Ni kufumba na kufumbua tu Baiju alipigwa na mkia ule kwa nguvu mara baada ya kusogelewa na alijikuta akitema damu kutokana na kichapo.
“Rudi”
Ule mkia ulimviringa Baiju kufumba na kufumbua tu na kumvuta nyuma na kisha kumrudisha ardhini mbele ya Aoiline na dakika ileile ulipotea katika macho yao , ilikuwa ni kama vile haukuonekana kwani licha ya urefu wake ulirudi ndani ya mwili wa Aoiline kwa spidi kubwa mno.
Roma alijikuta akitengeneza sauti kupitia ulimi wake , Roma alikuwa akijua mwanamke huyo alikuwa na mikia tisa na ameonyesha mwili tu na kilichotokea sio cha kawaida.
Pengine siraha yake kubwa ni hio mikia na kama atapambana nae basi atakuwa ni moja ya washindani hatari ambao ashawahi kukutana nao kwani angekuwa na uwezo wa kujikinga na wakati huo huo akishambulia.
Kwa spidi yake hio na nguvu zake za kijini aliona kabisa hata yeye hakuwa akimuweza kimapambano kabisa, na hakutaka kujiona yeye ni mkubwa zaidi hivyo alikubali Aoiline alikuwa ni levo ya juu kuliko yeye.
Baiju alijikuta amepauka mno kwa woga , alikuwa tyari amekwisha kujikatia tamaa katika kukimbia na aliishia kusujudu kadri awezavyo na kujaribu kuomba kuhurumiwa , lakini licha ya kujitetea huko kulifanya tabasamu la kikatili la Aoiline kuzidi kutisha.
“Bwana nimetenda dhambi zidi yako , unaweza kuondoa nguvu zangu zote za kijini na kunigeuza kuwa mnyama lakini tafadhari naomba usinie , naomba unisamehe”
“Siku zote nilikuwa mpole sana kwa viongozi kama nyie , kwanini nikuondolee nguvu zako za kijini ?,Baiju je utanisaidia jambo moja?”
“I’m willing to redeem myself!”Aliongea
“Great”
Kufumba na kufumbua Aoline alikuwa nyuma ya Baiju na kuishika shingo yake na palepale mkandamizo wa hali ya juu ulianza kumtoka.
“Sophia kuwa makini”
Aliongea Roma na palepale alimsogelea Sophia na kumzingira na nguvu ya kijini kwani tayari ashajua ni nini kinachokwenda kutokea .
Aoiline alikuwa akipanga kumkandamiza na nguvu yake ili kuweza kutawala uwezo wake hivyo kutokana na mkandamizio mkubwa ambao alikuwa akijaribu kutoa Aoiline ilikuwa ngumu kwa Sophia kuweza kuhimili na angetema damu kwani mara nyingi inakuwa kama vile ni mlipoko wa bomu.
Ilikuwa ni kama vile mwanamke huyo mrembo amegeuka na kuwa mungu wa huo ulimwengu kwani macho yake yalikuwa yamebadilika kabisa na kile kiini cheusi kilikuwa kimempotea kwenye macho na jicho likabakia jeupe kama vile ni barafu.
Dakika ileile Aoiline alifumbua mdomo wake na meno yake yaliongezeka urefu kama Vampire na kuyapelekea katika shingo ya Baiju na kumng’ata.
Baiju sura yake mwanzo ilikuwa imepinda kutokana na mkandamizo mkubwa lakini mara baada ya kung’atwa mwili wake ulibonyea palepale .
Sophia aliekuwa nyuma ya Roma hakuweza kupata ujasiri wa kuangalia kile kinachotokea kwani iliogopesha , upande wa Roma alikuwa katika bumbuwazi kwa kile kinachotokea
Alijiambia swala la kunyonya damu ni la kawaida kwani kilichofanyika ni kujaribu kunyonya nguvu za lile jini lakini hakutegemea mwanamke mrembo kama huyo ndio ambaye anafanya kitendo hicho.
Kile kitendo huenda angekuwa ni binadamu wa kawaida ambaye anaangalia angepoteza fahamu palepale , Sophia kwa kiasi hakuwa wa kawaida kwani alikuwa ashaishi na Roma na kuzoea baadhi ya mambo ya ajabu ya namna hio.
Dakika chache tu mwili wa Baiju ulibadilika na Akawa Kunguru mkubwa ambaye ameoza huku mifupa yake ikianza kuonekana na Aoiline alimsukumia mbali maiti ile ya Kunguru na kuanza kuilamba midomo yake kwa damu zilizokuwa pembeni, alikuwa ni kama vile analamba asali kwa jinsi alivyonekana kufurahia.
Baada ya mkandamizo wa hewa kuondoka ndio aligeuza macho yake kwa Roma huku akiachia mkandamizo wa kawaida kama vile alikuwa akijaribu kumuogopesha Roma.
“Mr Roma huna haja ya kuniangalia hivyo na kuniona kama mchawi mnyonya damu , nimefanya hivi kwa zaidi ya miaka elfu moja , hatima yake ilikuwa ni kifo hata hivyo , kwanini nisimtumie kama kirutubisho , Au naongea uongo?”
Roma alikuwa akianza kuwa na wasiwasi juu yake , hata kama alionekana kuwa mrembo wa kuita lakini matendo yake na uwezo wake wa kijini ulimpa mashaka makubwa na kushindwa kuijua nia yake halisi juu yao.
“Nadhani tunapaswa kuendelea na safari yetu maana ushamaliza maswala yako”Aliongea Roma na kisha akamwangaliaSophia akimwambia waanze safari ya kuondoka hapo haraka iwezekanayvyo.
Sophia hakuwa na shida na alikubali kuondoka , yule Aoiline ambaye alitaka kuwa nae karibu hakumtaka tena maana alikuwa akitisha.
Aoiline palepale alitoa tabasamu la kifedhuli na kufumba na kufumbua alikuwa mbele ya Roma na kuwazuia wasiondoke.
“Mr Roma tupo karibu na jumba langu la kimalkia kwanini msiende kupunzima kwa muda”
“Hakuna shida sana juu ya hilo , safari yetu ni kuelekea kando ya ziwa la Mbingu”Aliongea Roma huku akijaribu kutafuta upenyo wa kumpita.
“Hata kama nimekudanganya kuhusu ubini wangu , lakini sikuwa nikidanganya kuhusu mambo mengine , kuna zaidi ya wiki tatu mpaka kwa mnara kufunguka , kwenda huko ni kupoteza muda wako tu”
“Mimi naweza kutokuwa na akili kama wewe lakini siwezi kuwa kichaa kabisa na kuanza kupigana na mtu kama wewe ambaye umeishi maisha marefu , lazima una nia nyingine hivyo acha kuzunguka zunguka”Aliongea Roma mpaka hapo alijua mwanamke huyo hakuwa na nia ya kuwaruhusu waondoke kirahisi.
“Mr Roma sisi majini tunaweza kufikiria pia na sio wanafiki kama binadamu , mosi nimekuja huku kwasababu nimesikia taarifa kutoka kwa watu wangu ndio maana nimekuja kujionea mwenyewekama ni kweli Baiju alikuwa akitenda mambo ya kifisadi, kitu kingine pia waliniambia kwamba kuna binadamu wageni ambao wameweza kufika katika ulimwengu wetu , Watu watatu ambao ulipigana nao katika msitu wamekuongelea vibaya sana lakini sikuwachukulia siriasi na sina nia ya kuwalipizia kisasi kwa uliowafanyia”
“Lakini bado siamini mtu kama wewe unaweza tu kunialika kwako kwa ajili ya kupumzika”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu.
“Nimeongea vya kutosha je tunaongozana au hatuongozani”
“Hatuongozani”Aliongea Roma kwa sauti huku akitingisha kichwa chake kukataa kusisitizia msimamo wake.
Aoiline alitoa pumzi ya kukatishwa tamaa huku akimwangalia Roma kwa masikito.
“Kama hutaki kuongozana na mimi basi sina budi kukulazimisha”Baada ya kuongea hivyo msisimko aliokuwa ukitoa ulibadilika kabisa na macho yake hayakuwa mazuri tena kwani yalibadilika na kuwa ya chuki.
Roma alishindwa kuelewa chuki yake inatokana na nini , aliajiambia kwanini kumbadilikia namna hio ndani ya dakika tu wakati hajamchokoza.
Roma palepale alimsukumia mbali Sophia ili tu asije akapata madhara na baada ya kumuona ameenda mbali zaidi aliita nguvu zake za kijini ili kuweza kuhimiri mkandamizio uliokuwa ukitolewa na Aoiline.
Dakika hio hio Aoiline muonekano wake wa kirembo ulikuwa umebadilika na kuwa kama vile ni jitu kubwa la kutawala , macho yake yalikuwa ni kama yale ya kutaka mtu yoyote anaemuona kumsujudia.
Roma hakutaka kumruuhusu msichana kama huyo kuendelea kumkandamiza , hakutaka tena kulinda nguvu yake ya kijini isipotee na alimsogelea Aoiline kwa nguvu zake zote.
Mpira wa moto wa bluu ulionekana katika mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto ulitegneneza maji ya kiroho ya kuosha uovu.
Aoiline alitoa tabasamu la kejeli kama vile alikuwa akidharau kile anachotaka kufanya.
Awamu hio hakutoa mikia yake bali nguo yake ilianza kutengeneza kamba kama Ribbon kutoka kwenye nguo yake ya hariri akidhamiria kupigana na hio .
Roma hakutaka kujali mbinu yake ambayo anataka kutumia na dhamira yake ilikuwa ni kutaka kumchapa na maji ya kiroho akiamini hata tone lake linaweza kumletea madhara.
Lakini nguo yake ile haikuwa nguo kama nguo kwani ilikuwa ikidhalisha kiwango kikubwa cha nishaiti isiokuwa ya kawaida na kadri ilivyokuwa ikipepea kuelekea upande wa Roma ni kama ilikuwa ikimzuia asimfikie.
Roma alijikuta akishangazwa na uwezo wake , aliweza kujua mtu anaepambana nae ndio yupo katika levo ya juu kabisa ya daraja la tisa la mafunzo ya kijini ya kuita pepo.
Kutokana na mkandamizio wake kuwa mkubwa Roma alijikuta akiamini huenda hata Athena akashindwa kabisa kudili nae.
Kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao mpizani wake Roma alianza kupoteza pambano mapema kabla hata hajaanza kushambulia kwani alishindwa hata kubadilisha nguvu zake kuleta faida katika kushambulia.
Aoiline hakuonyesha kutumia nguvu yoyote alikuwa ni kama vile anacheza na zile kamba za nguo zake za hariri na alianza kuzifanya zipeperuke hewani na zilikuwa zikitoa nguvu kubwa mno .
Roma palepale aliweza kufikiria huenda mbinu yake haikuwa ikitegemea muundo au nguvu bali alikuwa akitegemea akili yake na ufahamu . mpaka hapo alijua kwamba ulimwengu huo wenyewe ulikuwa kikwazo kwake hivyo hakuwa na namna ya kumshinda.



SEHEMU YA 606.
“Mr Roma huu ni ushauri wangu kwako , nifuate mwenyewe kwa hiari yako au endelea kuwa kiburi na nikufunge na kuondoka na wewe”Aliongea Aoiline.
“Sina jinsi tena”Aliongea Roma katika nafsi yake , katika maisha yake hakupenda kushindwa kirahisi.
Palepale Cauldron iliweza kutokeza na kuanza kutoa moshi kiasi cha kusababisha anga kubadilika huku msisimko wa ajabu kuzingira eneo lote la msitu unaowazunguka na kufanya hata baadhi ya ndege kukimbia.
“Pumbavu kabisa , kwanini una tumia Cauldron?”
Aoiline alikuwa ashaishi muda mrefu sana , muda mfupi alikuwa akijaribu kumuita ‘Mr Roma’ kama kumchokoza lakini mara baada ya kuona dhana hio ya hatari hakutaka tena kumchukulia mwepesi.
“Bado tu unataka kupigana licha ya kuonyesha kufahamu hiki ni nini?”Roma alitumia kiasi kikubwa cha nguvu ya kijini akijiandaa kwa ajili ya kukipa nafasi kumshambulia Aoiline , lakini Aoiline alianza kutoa cheko la hali ya juu.
“Najua hilo ni tanuru la maafa na ni sehemu ya Dhana za kijini ambazo zijashawahi kuwepo lakini licha ya nguvu yake kubwa huwezi kukitumia katika nguvu yake yote kutokana na levo yako kuwa chini , ndio kwanza umeipita Dhiki unadhani unaweza kunishambulia kwa uwezo wako huo , fuata ushauri wangu kama mkubwa kwako usikitumie maana roho ya mnyama iliopo ndani yake itaishia kutawala mwili wako , Roho yake iliopo ndani haiwezi kufa na hata wale miungu hawana uwezo wa kuihimili , kwa haraka haraka naamini Roho ya mnyama hio imekuchagua lakini kama utaendeelea kukitumia ukiwa na nguvu ndogo utaishia kuwa shushu, utakuwa sio binadamu tena na wakati huo ukifikia utakuwa umechelewa kwani huwezi kurudi kuwa wewe tena”Roma alikuwa katika mshangao licha ya kwamba hakuonyesha katika uso wake, alijiuliza je ni kweli chungu hicho kinaweza kumtawala , maneno ya Aoiline yalimfanya moja kwa moja kuwa na moyo mzito.
Aoiline palepale zile kamba za hariri yake zilipotea na kisha akamsogelea Roma kwa mapozi.
“Huwezi kunishinda hata kidogo , Sijawahi kukutana na mshindani wa ukweli katika ulimwengu huu , ijapokuwa uwezo wangu sio wote kutokana na mazingira lakini gepu letu ni kubwa sana , nimekuacha mbali na sina haja ya kutumia uwezo wangu wote kukushinda ni kidogo tu”Roma alijikuta akikunja ngumi yake kwa hasira baada ya kusikia maneno yale.
“Ndio unavyoona , sio mbaya najua nafasi yangu ni ndogo kukushinda lakini sijawahi kujisalimisha kirahisi hivyo”Mwisho wa sentensi yake palepale alikielekeza Chungu chake uelekeo wa Aoiline
Aoilinepalepale alijikuta akikunja macho yake lakini kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana ni kama hakuwa na mpango wa kukikwepa.
“Mjinga sana wewe”
Ghalfa tu mikia mitano iliweza kutokea nyuma yake na kwenda kukishikilia kile chungu , nguvu yake ya mvutano ilitaka kuimeza ile mikia lakini nguvu kubwa ya kijinni aliokuwanayo Aoiline iliweza kushinda na kile chungu kilirushwa kwa nguvu kuelekea hewani kama mpira huku yale macho ya mnyama ambayo mara nyingi huonekana ndani ya chungu kile yalipotea.
Kutokana na Roma kutumia nguvu nyingi kukitawala kile chungu na wakati huo huo Aoiline na yeye kutumia uwezo wake kukidhibiti maumivu aliyapokea yeye, ilikuwa ni kama viungo vyake vya ndani vinapasuka na aliishia kutema damu.
Kitendo hicho kilimuonyesha kwamba Aoiline uwezo wake ulikuwa ni mkubwa sana kuliko isivyokuwa kawaida kwani chungu chake ambacho aliamini kilikuwa na nguvu kiliweza kudhibitiwa kwa sekunde tu bila kuonyesha ukinzani wowote.
Sophia aliekuwa akishuhudia kitendo hicho alijikuta akijawa na wasiwasi mno hasa mara baada ya kumuona Roma akitema damu na alishindwa kujizuia na kumsogelea.
“Bro vipi hali yako?”Aliongea Sophia kwa upole na Roma alijikuta akikosa nguvu na kumuegamia Sophia.
Ijapokuwa alitaka kumwambia kwamba atakuwa sawa lakini alikosa nguvu kabisa hata ya kunyanyua mdomo na aliishia kutingisha kichwa chake tu.
Uwezo wake wa kujiponyesha ulikuwa ni wa taratibu mno kutokana kuwa na nguvu kidogo ya kijini na palepale chungu kile kilipotea.
“Nilikuonya mwenyewe , kwa nguvu zako za kijini Cauldron inaweza kuwa na nguvu kwa majini pepo wa kawaida lakini kwangu hapana”
Alimwangalia Sophia ambaye alikuwa na sura iliopauka na kisha palepale hakuonyesha kutaka kupoteza muda na alirusha kamba zake za hariri na kuwafunga funga.
“Nyie wote wawili tunaondoka pamoja kuelekea Palace”
Roma alitaka kumsukuma Sophia asifungwe na zile kamba lakini hakuweza kabisa na waliishia kuburuzwa wote kama mateka.
Roma hakuwahi kukata tamaa mara baada ya kuingia katika ulimwengu huo uliojjtenga lakini alijihisi kukata tamaa mara baada ya kumuona Aoiline akipaa bila tatizo kwa spidi kubwa na umbali mrefu kirahisi kabisa licha ya kwamba alikuwa akipambana na yeye.
Aoiline alisema kwamba mazingira yalikuwa yakizuia kutumia nguvu zake ,sasa alijiuliza kama ni hivyo uwezo wake ulikuwa ikifikia wapi kama tu ataweza kutoka katika ulimwengu wa kawaida.
Roma hakuona shida kupoteza pambano lakini alimuonea huruma Sophia kutokana na ukiburi wake na mbaya zaidi asingeweza kurudisha nguvu zake ambazo zilikuwa zimepotea na hata kama ikitokea asingeweza kuwa na uwezo wa kumshinda Aoiline.
Alijikuta akikumbuka ule usemi kwamba haijalishi una nguvu kiasi gani lakini kumbuka kuna mwenzako ana nguvu kuliko wewe , ni sawa na kusema haijalishi una akili kiasi gani lakini kumbuka kuna mwingine ana akili kuliko wewe , au unaweza kusema haijalishi unajiona bora kiasi gani lakini kumbuka kuna aliebora zaidi yako hivyo kuna mazingira inapaswa kujishusha na kuukubali ukweli lakini yeye alienda kinyume na sheria hio.
Licha ya kwamba kuna misemo mingi ya kihenga lakini siku zote haifanyi kazi katika kila mazingira , anaweza akawa ameonyesha kiburi lakini dhamira yake ilikuwa ni kutaka kujaribu ndio maana hakuona aibu kushindwa ni vile tu nafsi yake ilikuwa ikijutia kumuingiza aliekuwa nae matatizoni.
Baada kupaa kuelekea mashariki kwa muda mfupi majengo yalianza kujionyesha mbele yao kwa chini.
Yalikuwa ya kitamaduni lakini makubwa na ya kuvutia , mchanganyiko huo wa kitamaduni wa makabila mbalimbali ya watu wa nje ya dunia iliwafanya kujihisi kama vile dunia ya kale imeunganiska sehemu moja, yaani waarabu , wachina , wakorea wazungu pamoja na makablila mengineyo ambayo yalikuwa yakiwakilishwa na sanifu zao za kimajengo.
Baada ya kuingia kwenye jengo moja refu ambalo lilikuwa mlimani waliweza kuona madini ya Nephriti yaliokuwa yamening’inizwa katika korido kuingia ndani kabisa ya jengo la kimalkia, ilikuwa ni kama vile ni yale majumba makubwa ya kifalme lakini ambalo limejengwa kwa mahadhi ya kisanifu tofauti tofauti .
Juu kabisa ya mlango wa kuingilia kulikuwa na ubao juu(Lintel) uliokuwa na maandishi makubwa ya kingereza na lugha isiokuwa ikieleweka , ‘Jade Fox Palace’, ni maandishi ya kubandika na hata kwa mjinga ungejua ni madini ya dhahabu yaliotumika.
Baada ya kuingia kwenye Baraza kubwa ambalo sakafu yake hiakueleweka imejengwa na madini gani kutokana na mtelezo wake palepale Aoiline aimtenganisha Sophia na Roma wakiwa wamefungwa katika staili moja lakini tofauti ni kwamba Sophia alikuwa amepoteza fahamu.
Roma akiwa amesimama katika eneo moja akiwa amefungwa na kamba za hariri palepale sehemu ambayo alikuwa amesimama ilianza kutengeneza duara kwa kuonyesha michirizi ya madini ya dhahabu na ilikuwa ni kufumba na kufumbua Roma alitumbukia ndani na kwenda kutua chini ya Gereza la Ardhini.
Roma alitaka kutoka haraka kabla shimo halijajifunga lakini alizuiwa na mwanga mkali wa dhahabu uliokuwa kama kioo.
“Wewe mtukutu hilo gereza limetengenezwa kwa madini yalitoka katika bahari Isio na mwisho , chuma chake kukuzunguka ni kile cha miaka mingi iliopita na kazi yake kubwa ni kunyonya nguvu za kijini na huu mwanga wa njano uliokuwa juu yako hauwezi hata kidogo kuupita , elewa ushauri wangu , kubali kuwa mfungwa wangu ili usipoteze nguvu zako”
Roma alijikuta akijaribu kupiga ngumi kuta za chumba na alijikuta akiona hakuna namna ya kuweza kutoboa .
“Pumbavu zako kabisa wewe Aoiline , kama unataka kulipiza kisasi cha watu wkao kwanini ipigane na mimi mpaka nife kuliko kunifungia”
Roma alikuwa na hasira alikuwa na hamu sana ya kutoka katika ulimwengu huo kuirudia familia yake , angewezaje kufikia mnara kama ndio hivyo ni mfungwa.
“Nini .. haha!, huwezi hata kushindana na mimi lakini bado unafikiria kwenda kwenye Mnara , mimi mwenyewe licha ya uwezo wangu nina asilimia hamsini tu za kupona mapigo tisini na tisa ya radi, nakushauri uache ndoto zako”
Baada ya kusema hivyo alitembea kuelekea kwenye Majilisi (Chamber au chumba) akiwa amemfunga Sophia vilevile akimburuza akiwa katika hali ya kupoteza fahamu.
Majini waliokuwa ni wahudumu na vijakazi wake walikuwa tayari wamekwisha kujipanga muda mrefu tokea anaingia na Roma .
Baada ya kuingia kwenye Majilisi wahudumu wa ngazi ya juu waliiinamisha vichwa vyao chini kwa heshima, hakuna jini ambao halikuwa na mwonekano tofauti na binadamu.
“Mchukueni na muingizeni kwenye Majilisi ya kushoto , mhudumieni vizuri lakini asiruhusiwe kutoka bila rushusa yangu , mnanielewa?”
“Ndio Bwana wetu”
Wahudumu wale hawakutaka kuuliza mtu huyo ni nani na anatokea wapi zaidi ya kutii maagizo.
Baada ya vijakazi wale kuondoka alitembea na kwenda kukaa kwenye kiti chake kilichotengenezwa kwa madini ya Dhahabu tupu huku pembeni yake kulikuwa na aina ya madini ambayo hayakuwa yakielezekza , ni kama vile ni vinundu vya Akmasi huku ndani yake kukiwa na madini mengine ambayo yalikuwa yakipumua kwa kubadilika badilika rangi.
Alifumba macho yake kwa kuvuta pumzi nyingi huku masikio yake yaliokuwa na uwezo wa kusikia mitetmeo yaliweza kunasa sauti za Roma kushindana na kuta za gereza chini ya ardhi lakini alionyesha kutojali ni kama alikuwa na uhakika asingeweza kutoka.
“God why did you send in onother headless man when I’ve almost forgotten about him?”
“Mungu kwanini ukaamua kutuma mwanaume mwingine kichaa ilihali yule nakaribia kumsahau”
Aliongea mrembo huyo akiwa anaangalia eneo la juu ambalo lilikuwa kama na kioo kinachopitisha mwanga kutoka juu angani na macho yake yalionyesha chuki na huzuni.
Kauli yake ilikuwa ikitafsirika kama vile kuna mtu aliempoteza na sasa anakaribia kumsahau lakini anamuuliza Mungu kwanini kamleta mwingine kichaa..
*******
Kulikuwa na baridi sio ya mchezo ndani ya Iringa kwasababu ilikuwa kipindi cha vuli lakini licha ya hivyo Edna hakuonekana kuathirika kwasababu alikuwa ni tofauti tokea aanze kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Ilikuwa ni muda wa jioni ndani ya jiji la Iringa, Edna alikuwa amesimama nje ya geti katika shule ya watoto maarufu iliokuwepo karibu na chuo akimsubiria mtoto wake kutoka nje ya geti kama wazazi wangine walivyokuwa wakisubiria.
Wiki mbili zilikuwa zimekwisha kupita tokea kupotea kwa Roma na hakukuwa na habari zozote za kumuhusu.
Familia ya Afande Kweka haikutaka kumruhusu Edna kurudi Dar es salaam na kujifungia akiwa mwenyewe, hivyo wakamshauri Lanlan kuandikishwa shule ya muda ndani ya jiji hilo aendelee na masomo.
Lanlan alikuwa na akili hivyo aliweza kuendana kwa haraka na mazingira ya shule mpya na hakuonyesha malalamiko yote na alipenda michezo iliokuwa ikifanyika shuleni kwao.
Ukweli ni kwamba ukoo huo wa Roma ulikuwa na utajiri mkubwa sana kutokana na kuwa na vitega uchumi vingi na haikuwa hivyo tu hata yeye mwenyewe alikuwa na hela na ingekuwa rahisi kwa Lanlan kutafutiwa mwalimu ili kufundishwa akiwa nyumbani lakini Afande Kweka hakutaka Lanlan akikaa ndani tu aliamini kuchanganyika kwa Lanlan na wenzake kutampatia msingi mzuri wa kijamii.
Edna alikuwa akielewa dhamira yao ni nini hivyo hakutaka kukataa na kuruhusu Lanlan kuanza shule lakini ukweli ndani kwa ndani mrembo huyo alikuwa na huzuni, wakati wengine wakiwa na tabasamu na tumaini yeye muda wote alikuwa akiwaza yu wapi mume wake.
Ni wiki mbili sasa hakuwa akilala usingizi mzuri na alikuwa akisumbuliwa na ndoto nyingi na alishindwa kabisa kuvuta taswira ya kila wazo baya linalomjia , maswali haya ndio yalikuwa yakikitawala kichwa cheke , vipi kama Roma asiporudi milele? , Vipi kuhusu yeye atafanya nini?.
Wanawake wa Roma kutoka Dar walikuwa wakimsumbua kwa kumpigia kutokana na kushindwa kufanya mawasiliano na Roma na Edna hakuthubutu kuwaambia ukweli kama amepotea , aliishia kudanganya kwa kuwaambia kwamba Roma yupo katika sehemu ya kujitenga akiwa kwenye mafunzo makali sana ya kimapigano.
Hakuna alieweza kushuku maneno yake , pengine ni kwasababu walikuwa wakimuamini au matamannio yao zidi ya mwanaume huyo yalikuwa makubwa kuliko wasiwasi wao.
“Mommy!!”
Sauti ya kitoto iliweza kumtoa katika hali yake ya kimawazo na Edna alionyesha tabasamu huku akichanua mikono yake kumpoktea Lanlan kwa kumbatio.
Lanlan alikuwa amevalia koti la Track suit la bluu pamoja na suruali yake kwani siku hio ilikuwa ni ya michezo shuleni
Akiwa na Lanlan mikononi mwake alitembea nae kuelekea kwenye gari huku akimuuliza maswali kama siku zote.
“Lanlan what did you learn today?”
“Leo Lanlan amecheza michezo mbalimbali ya kukimbizana na nilimshinda hadi mwalimu”Aliongea na kumfanya Edna kushindwa kuvumilia kauli yake na kutoa kicheko , Binti yake ndio mtu pekee ambaye alikuwa akimchekesha kama hivyo katika kipindi hicho cha mawazo
“Darling , you have to be easy on your teacher nextime or else it would be hard for the teacher to teach other children”Aliongea na kumfanya Lanlan kutingisha kichwa chake kukubali ushauri wa mama.
“Mama tunaenda kula sasa hivi?”
“Jua bado linawaka na tayari unawaza chakula”
“Mama Lanlan ana njaa”Aliongeana kumfanya Edna kumfinya shavu na kisha kumuingiza ndani ya gari lao la kifahari.
Mwanamke ambaye alikuwa akimwendesha Edna alikuwa ni mjeshi tena Komandoo na alipewa kazi hio maalumu kumuendesha Edna lakini kwa wakati mmoja kumpa ulinzi na mara baada tu ya kuingia ndani ya gari aliliendesha.
Wakati gari yao inaingia barabara kuu ikirudi nyuma kutokea mjini kuelekea nyumbani kwa Afande Kweka ambako ni nyuma kabla hujafika Iringa waliweza kusikia ving’ora vya gari ya kipolisi nyuma yao.
Mjeshi yule alionekana kushangaa mara baada ya kuona kuna polisi wanaomuashiria kusimamisha gari.
“Ma’ am nadhani napaswa kusimamisha”Aliongea na Edna alimpa ishara kwa kutingisha kichwa kukubali bila kufikiria mara mbili mbili.
Baada ya gari yao kusimama pembeni ya barabara walitoka polisi waliokuwa wamevalia mavazi ya kitrafiki na kuwasogelea na mmoja wao aligonga kioo na kuashiria kufungua mlango na dereva kushuka.
“Afisa nadhani sijakiuka sheria zozote za barabara”Aliongea Mjeshi mara baada ya kutoka nje ya gari.
Polisi mmoja ambaye alikuwa na chunusi nyingi usoni alimsogelea yule mjeshi na kwa spidi kubwa aliishikilia shingo yake , kilikuwa kitendo cha kushtukiza, pengine mjeda yule hakutagemea angeshambuliwa ndio maana ilikuwa rahisi kwake kupokea pigo lile kabla bata hajaweza kujitetea, ni mlio wa mifupa tu ulioweza kusikika na palepale alilegea na kudondoka chini.
Edna palepale alishituka na kugundua watu hao hawakuwa polisi kama alivyodhani , ilionekana ni majambazi ambao hawakuwa na nia nzuri kwao
“Mommy they’re bad guys!!”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kuguna.
Polisi yule mwingine hakupoteza muda kwani palele kupitia mlango wa mbele alirusha bomu la moshi kuelekea ndani ya gari na Edna alishindwa kuwa mwepesi na alijishtukia tu tayari mapafu yake yakiweza kuvuta ule moshi.
 
SEHEMU YA 607.
Gesi ile haikuwa na harufu hata kidogo wakati ikiwa inaingia kwenye mapafu yake na ilimfanya Edna kuanza kuona kizungu zungu , ijapokuwa alikuwa mwishoni mwa levo ya nusu mzunguko lakini haikusaidia kuweza kutokuathirika.
Upande wa Lanlan moshi ule haukuwa na athari kwake na palepale le alifanya maamuzi ya kufungua mlango haraka haraka kwa spidi zote na kumsogelea yule mwanaume mwenye chunusi kwa spidi kubwa akitanguliza miguu kama mpira vile.
Wale watu walishangazwa na namna ambavyo Lanlan alishindwa kuathirika na gesi ile ya kuulegeza mwili, baada ya kuona kitoto hicho kinamsogelea kwa ajili ya kumpiga alikuwa ni mwepesi sana kwani alisogea pembeni na Lanlan akapita na wakati huo huo akikamata mguu wake.
Edna aliweza kuona kila kitu lakini mwili wake haukuweza kufanya chochote hata kusogea na mara baada ya kuona namna ambavyo mmoja wapo amekwepa pigo la Lanlan kirahisi aliweza kuhisi kabisa huenda walikuwa na nguvu za ziada hata wao
Lanlan baada ya kuona kashikiliwa mguu alitumia kichwa kushambulia lakini yule mtu alimshika kwa wepesi zaidi.
“Pumbavu huu ni ukichaa , kana nguvu za kijini tena za kutosha tu , Bro mzimishe haraka”Aliongea yule mwingine.
“Gotcha”
Yule bwana mwenye chunusi alimshikilia Lanlan vizuri bila hata ya kupinda pinda na kwa ustadi wa hali ya juu kama mcheza Kungu Fu alimgusa Lanlan katika eneo muhimu la shingo na palepale akapoteza fahamu.
“Pumbavu kabisa huyu mtoto ni hatari kuliko hata mama yake , ni ,kheri tumefanikiwa na mpango wetu haujabuma”Aliongea yule bwana mwenye chunusi huku akijaribbu kuangalia mazingia kama kuna watu wanaowaangalia , lakini eneo ambalo walilichagua lilionekana kuwa kimya mno kwani hawakuonekana na dakika walizotumia zilikuwa chache mno , ilikuwa ni kama vile wamezuia magari kutopita kwani haikuwa kawaida kwa kutokuonekana hata pikipiki ikipita katika hilo eneo.
“Bro wewe mbebe huyo mwanamke na mimi nitambeba huyu mtoto , nina uhakika kuna kifaa cha GPS kwenye gari lao hivyo tunapaswa kuliacha”Aliongea
Bwana yule alikubaliana na wazo la mwenzake na kisha alitingisha kichwa katika mlango wa gari na kujaribu kama vile anamsiadia Edna kushuka na baada tu ya kumtoa alimbeba juu juu na kisha wakamuingiza kwenye gari lao la kipolisi na yule mwingine pia aliingia , muda huo Edna bado alikuwa akipambana na usingizi na alijaribu kusukuma sukuma lakini hakuwa na uwezo wowote na dakika chache mbele alisinzia…
*****
Upande wa nyumbani kwa Afande Kweka , Mzee Camillius mwenyewe alikuwa amekaa kwenye kiti chake cha kivivu huku akinywa chai ya moto akiangalia bustani yake ya Karoti.
Ilikuwa ndio tabia yake mara nyingi kama hayupo kwenye mifugo basi yupo kwenye bustani yake akikodolea mimea kama vile kuna kitu cha kufurahisha anachokiona na hakuwa akijali upepo na baridi kwani alikuwa na mavazi mazito lakini pia afya yake haikuwa mgogoro.
Dakika hio hio aliweza kusogelewa na mlinzi wa nyumba hio kwa spidi huku akiita sauti yake kwa wasiwasi.
“Marshall , Madam Edna na Lanlan gari yao imeonekana imesimama kando ya barabara na tumejaribu kuwapigia hawapatikani na Luteni Mlowe kakutwa kafariki ndani ya gari”Aliongea kwa wasiwasi na kufanya uso wa Afande Camillius kubadilika palepale kutoka katika hali yake ya amani.
“Vipi kuhusu kifaa cha GPS?”
“Signal zimepotea ni kama zimeingiliwa , Watekaji wanaonekana kuwa wabobezi”
“Kama ni hivyo hatuna muda wa kupoteza , si Afande Tobwe yupo Iringa bado , jaribu kuwasiliana nae na afanye muunganiko wa kimaagizo na mawasiliano na RCO polisi kuzuia magari kutoka nje ya Iringa, sikiliza maagizo yake na usiruhusu mtu yoyote kujua hili “Aliongea na mlinzi yule alitoa saluti na kisha alikimbia kuondoka.
Afande Kweka alisimama huku akiwa na uso usioelezeka na alionekana kama alikuwa akiongea mwenyewe huku sura yake yote ikiangalia bustani.
“Nadhani tayari siri zishavuja na maadui zako wanaitumia kama nafasi , kama hutorudi mapema nitashindwa kuhimili zaidi”Aliongea mwenyewe.
******
Jua lilikuwa tayari limekwisha kuzama na Mwezi kuchukua ufalme wake wa kuiangaza dunia , katika eneo ambalo lilikuwa kama bandari kavu kutokana na uwepo wa Makontena mengi yaliochakaa huku yakiwa yamepandiwa na uozo pamoja na miti kuota juu yake kulikuwa na ghala.
Eneo hilo lilikuwa limezungukwa na ukuta mkubwa , ni rahisi kusema ni ghala ambalo halikuwa likitumika na hata kama lilikuwa likitumika sio kwa shughuli ambazo zilikusudiwa tokea kujengwa kwake.
Ndani ya jumba bovu la mabati kama kiwanda lilikuwa limefungwa lote kwa nje huku ndani likuwa na tundu moja tu kama chanzo cha hewa safi.
Zilipita dakika chache tu eneo lote la ndani taa ziliwashwa huku mlango ukifunguliwa na hatimae walionekana Edna na Lanlan wakiwa wamefungwa katika viti wakiwa karibu karibu.
Watu waliokuwa wameingia hapo moja wapo walikuwa ni wachina na waafrika na walikuwa kama kumi na mbili hivi na walikuwa na miili iliojengeka kimazoezi.
Edna aliekuwa amefungwa katika kiti ile dawa aliowekewa ya usingizi ilikuwa imemuishia makali sasa alikuwa na fahamu zake , kwa kuangalia tu kundi la watu hao alijua kabisa ni ngumu kuweza kutoka kwani ni wengi mno.
Edna katika hali kama hio hakujali usalama wake , utashi wa mwanamke mwenye mtoto ulimvaa na kitu pekee alichokuwa akiwaza ni Lanlan kuwa salama.
Lanlan mwenyewe alikuwa macho huku akiwa na hasira nyingi na kwa nguvu zake alijaribu kufurukuta katika kiti alichokaliswa lakini bwana mwenye chunusi alikuwa amemshikilia vizuri sana , kitendo cha kuweza kushindwa kufanya chochote aliishia kutoa machozi tu ya hasira.
Lanlan katika hali kama hio akili yake iliweza kufikiria kauli ya baba yake akimlazimisha kufanya juhudi za kujimarisha katika mafunzo yake ya kuweza ku’master’ nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo, ni kama mtoto huyo mdogo ndio anajua sababu ya kuhimizwa na baba yake ilikuwa nini.
“Nyie watu ni wakina nani , hivi mnajua matokeo ya hiki mnachokifanya?”
“Bila shaka tunaelewa , wewe ni Madam kutoka ukoo wenye nguvu ndani ya taifa hili , mkwe wa Raisi Wa Jamhuri Ya Muunganno Wa Tanzania”
“Kama mnalijua hilo kwanini mnathubutu kufanya hivi?”
“Kwanini tusiweze kuthubutu , Mlengwa wetu ni moja wapo ya mwanafamilia ndani ya ukoo wa Kweka mathalanni mtu wa karibu zaidi na bwana Roma Ramoni , wewe ndio mke wake hivyo inakufanya uwe target yetu ya kwanza”
“Hamumuogopi mume wangu?”Aliuliza Edna akijaribu kujituliza.
“Madam Edna, kubali ushauri wetu na uache kuuliza maswali na kujifanyisha , tuna taarifa zote Roma Ramoni amepotea kwa zaidi ya wiki mbili sasa , hii taarifa bado haijafahamika na watu wengi na sisi tumeisikia kutoka katika chanzo cha kuaminika hivyo acha kujaribu kutufanya wajinga”
“Kama ni hivyo basi mtakuwa na sababu ya kumchukia mume wangu”
“Nitakuwa muwazi na wewe , Sisi tulishawahi kufanya kazi chini ya Kamanda Razaq kama Special Forces, tuna deni kubwa kwa Kamanda Razaq na ukoo wake wote , Roma ni shetani kabisa yule m amemuua Kamanda bila wasiwasi kwasababu tu eti ana nguvu kubwa na sapoti kubwa kutoka katika familia yake , Tupo hapa kwa ajili ya kulipiza kisasi cha Kamanda wetu”
Edna alijikuta akitoa macho na kutoa kicheko hafifu huku akiwaangalia.
“Mnajiita wanajeshi mliokuwa chini ya Kamanda Razaq , kama ni hivyo kwanini hamjatuua mpaka sasa , kwanini nyie watu mkajifanya kuwa polisi na mkatuteka?”Aliongea na kumfanya yule kiongozi wao mwenye chunusi kuwaza kidogo.
“Kama nilivyotegemea ,Mwanamke giniasi mfanyabiasara ndani ya taifa Tanzania , bado una akili kama kawaida yako licha ya kuachana na maswala ya biashara , upo sahihi tupo hapa na dhamira nyingine”Aliongea na kumfanya Edna kuhisi kitu , ni kama ashajua ni kitu gani ambacho wanataka kutoka kwake.
“Madam usijivunie bado , kutokuwaua kwetu hakumaanishi hatuna mbinu nzuri ya kimbadala kwa ajili ya kulipiza kisasi chetu , Mabraza wetu hapa wa kichina wapo katika levo za juu za mzunguko kamili katika mafunzo ya kijini lakini licha ya mipango yetu na kuwapata hawa bado ni wachache sana kuweza kupigana na ukoo wa mumeo, Roma Ramoni anajifanya kijogoo kwasababu tu ana mbinu za hali ya juu za kuvuna nishati kwa maelezo tulioyapata , kwa kumwangalia tu binti yako tunaona kitu kisicho kawaida kutoka kwake”
“Mnazunguka zunguka kwasababu hamna ujasiri wa kutuua … mpo hapa kwa ajili ya hila zenu za kuweza kupata mbinu ya mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , mpo hapa kwa mgongo wa kujifanya eti tunataka kulipiza kisasi cha Kamanda Razaq”
Bwana mwenye chunusi ambaye ni kiongizi mwili wake ulikakamaa kutokana na maneno ya Edna.
“Nendeni mkamuambie raisi Jeremy anapaswa kuacha kutumia hila zake kwangu , mimi bado ni sehemu ya ukoo wa familia ya Kweka hata kama mume wangu bado hajarudi “
“Jeremy? Hahaha.. nadhani ni kama uvumi unvyosambaa ikisemekana raisi Jeremy wa Rwanda ndio baba yako mzazi , kwanini unafikiri anaweza kufanya kitendo kama hiki kwenu nyie”
“Kwanini asiweze ,bila koneksheni nyie watu msingeweza kuwa na ujasiri wa kufanya yote haya .. hii ni Tanzania”Aliongea.
“Unachoongea hakina mashiko , nina sentensi moja tu ya kukuambia , mnatupatia mbinu hio au hamtupatii?”Aliuliza akiwa na macho makali akimwangalia Edna.
Muda huo Edna alichokuwa akijaribu kufanya ni kuvuta muda ili angalau iwe rahisi kwa watu kugundua wapo hapo
“Mnapoteza muda wenu kwani sijui chochote kuhusu nguvu za mume wangu na mbinu zake”
“Haha acha kupoteza muda au unadhani kuna mtu ambaye anaweza kuja hapa na kukusaida , ngoja tu niwe mkweli kwako hatumuogopi mtu yoyote atakae fika hapa ilimradi tu sio Roma”Aliongea kwa kejeli na kumfanya Edna kung’ata lips zake.
“Madam unaweza usielewe kitu kimoja , sababu ambayo inakufanya mpaka muda huu uendelee kuishi mbele ya macho ya watu wenye husda ni kwasababu tu umeolewa na mtu ambaye anaogopwa na kila mtu , sio kwasababu tu eti wewe ni mtoto wa nje ya ndoa wa raisi Jeremy wala sio kwasababu ni raisi wa mkampuni mkubwa kama Vexto pamoja na utajiri wako, Sasa hivi huna lolote kwetu kwani mumeo amepotea na huenda akawa amekufa huko alipo na hujui tu, hivi unafikiri tunaweza kukuogopa kuto kuukuua?”Aliongea bwana mmoja ambaye ndio aliehusika katika kumteka na meneno yake yalikwa mwiba katika moyo wa Edna.
“Hawezi kufa , Roma ni mzima”
“Nani anajali hilo . uzuri ni kwamba hayupo hata kama anaishi”
Macho yake palepale yalichanua na kuanza kumwangalia Edna na urembo wake usiovumilika na alishndwa hata kujizuia na kujiambia angalau hata kwa mara moja aguse ngozi yake ya uso na palepale alipeleka mkono huku akitetemeka tetekemeka, ni kama hakuwa akiamini anagusa shavu la mrembo Edna tajiri.
“Bad guy , don’t you dare touch mommy I’ll kill you”
“Mtu mbaya usije kuthubutu kumgusa mama , nitakuua”Lanlan aliongea huku akijaribu kufurukuka lakini bwana mmoja alimsogelea na kumlisha tambara mdomoni na kumwambia kaa kimya , hawakuweza kuvumilia kutishiwa maisha yao na mtoto mdogo kama Lanlan, hakuweza kusogea kwasababu wale watu walikuwa wamefunga kwa kulenga Meridian za mwili wake li kumzuia mtitiroko wa nishati katika mwili wake.
Lanllan aliishia kutoa machozi huku akitingicha kichwa akijaribu kutoa tambara mdomini
“Msimuumize binti yangu, ni mtoto tu hana kosa”Aliongea Edna.
Edna alijawa na hofu kubwa mara baada ya mkono wa ule mwanaume ukimsogelea kumshika , hisia kali za ukinzani kutoka kwake ziliamsha bangiri iliokuwa kwenye mikono yake na palepale ulisikika mlio wa ‘Chiii…’ kama vile ngendere anaenyongwa huku eneo lote likijaa mwanga wa kijani na wimbi lake lilikuwa na nguvu kiasi kwamba liliweza kuwapush yule mwanaume mwenye chunusi na yule mwingine, lakini kutokana na uimara wao hawakuweza kuumia.
“Shit , hicho ni nini?”Waliongea huku wakitoa macho na kundi lote lilirudi nyuma huku wakiangalia mwanga uliomzingira Edna kwa mshangao na wasiwasi wa juu.
Ule mwanga haukuwashambulia wao tu bali uliunguza mpaka zile kamba ambazo zilikuwa zimemfunga Edna na akawa huru.
Ile bangiri ni kama ilikuwa na akili kwani iliweza kumlinda Edna tu kwa kutoa mwanga ambao ulikuwa ukimzingira yeye na mtoto wake , hakika ilikuwa Dhana ya kijini kutokana na maajabu yake.
Wale majambazi hawakuelewa nini kilichopo kwenye ile bangiri , kuna hisia ziliwaambia ni siraha ya kijini lakini hawakuelewa kwanini ilikuwa na nguvu namna ile na waliogopa hata kumsogelea Edna.
Kwa maelezo ya Zenzhei Bangiri ile haikuweza kuonyesha uwezo wake wote , hivyo nguvu yake ilikuwa ikiendana na levo ya Edna katika mafunzo ya kijini , sasa haikueleweka kama Edna akifikia katika levo ya Nafsi nguvu yake itakuwaje.
Wale wachina ijapokuwa na wao walikuwa katika levo ya mzunguko kamili ilimaanisha kwamba walikuwa ni wakawaida tu na hawajapata ufunuo bado wa kutumia elementi za dunia katika kufanya mashambulizi, hivyo faida pekee waliokuwa nayo ni nguvu za miili yao , lakini katika mazingira hayo hawana uwezo wa kumsogelea Edna kwani wangeunguzwa na ule mwanga.
“Ma afande hatupaswi kuwa na hofu kwa ajili ya hichi , msisahau na sisi tuna siraha pia”
Yule bwana mwenye chunusi aliongea na palepala alichomoa bastora maarufu kama Desert Eagle na kumnyooshea Edna huku akitoa tabasamu la kejeli , wale wengine wote nao pia walitoa siraha zao zinazofanana , ule mdomo mweusi wa bastora na tundu lake ulimwambia ikitapika itamuua palepale
“Madam Edna mumeo ndio kakuachia hio siraha kwa ajili yako , Aisee nakiri ni kinga nzuri”Aliongea Jambazi mwingine mwenye kovu kwenye uso.
“Mimi shauku yangu ni kutaka kujua kama ina uwezo wa kuzuia na risasi au kama inaweza kuwalinda wote wawili kwa wakati mmoja”Aliongea na palepale alibadilisha uelekeo wa siraha yake na kumlenga Lanlan.
“Hapana”
Edna alitoa ukulele na kisha akampakua Lanlan na kumkumbatia huku akiwapa watu wale mgongo, alikuwa yupo tayari kufa yeye ila Lanlan apone.
“Madam Edna unapaswa kujua sisi kuvuta triga na kuruhusu risasi ni kitu chepesi sana na tulichosomea , hata kwa angle niliokuwepo nina shabaha ya kuweza kumchapa risasi mtoto wako hio miguu yake inayoonekana au bega , unadhani bado hio bangiri yako inaweza kumlinda ,,, vipi kama isipofanikiwa kuwalinda na risasi?”
Maneno yae yalimfanya Edna kutetemeaka na kupauka kwa wakati mmoja
Jamaa yule alionekana bingwa wa kutumia maneno vizuri sana na alimfanya Edna kujiuliza je kama bangiri hio haina uwezo wa kuzuia risasi nini kitamtokea na isitoshe ndio mara ya kwanza kupatwa na tatizo kama hilo.
Edna alijiuliza maswali mengi na aliishia kuona kwamba hawezi kuchukua Risk kwa usalama wa binti yake na katika mazingira kama hayo anapaswa kufanya maamuzi.
“Mama usilie, Lanlan haogopi kitu”Edna alishindwa kujua kama muda huo alikuwa akilia.
Lanlan bado hakuwa na uwezo wa kufanya chochote mwili wake ulilegea licha ya kufunguliwa , wale wachina walikuwa wajanja sana ni kama haikuwa mara yao ya kwanza kuteka mtu ambaye ana uwezo wa kijini kwani mtiririko wa nishati katika mwili wa Lanlan ulikuwa mdogo.
Edna alijiambia hana thamani kabisa , katika mazingira ya hatari kama hayo hata binti yake tu hawezi kumlinda , yeye ni mama wa namna gani.
“Madam Edna tuna mwisho wa uvumilivu wetu , hatuwezi kukushambulia kama upo tayari kuvua hio bangiri , kama utakataa basi tutafanya majaribio kuona kama ina uwezo wa kukinga na risasi na mimi shabaha yangu ni binti yako tu”
“Nitaivua”
Aliongea Edna kwa kufoka , kila anaposikia kauli yoyote ya mtoto wake kutaka kudhulika aliogopa sana , huenda ndio udhaifu wake mkubwa.
Edna kwa mikono iliokuwa ikimtetemeka alimuweka Lanlan chini na kisha akaivua ile bangiri na kuikweka chini kweney sakafu na palepale ule mwanga uliokuwa ukimlinda ulipotea kama vile ilikuwa ndoto.
Yule bwana mwenye chunusi mara baada ya mwanga ule kupotea alimsogelea Edna na kisha akamsukumia kwenye kiti na kisha akamuwekea bastora kwenye paji la uso wake
Edna alijua uwezo wake wa kijini ni mdogo sana , hivyo akileta ukinzani atakaepata madhara ni Lanlan hivyo aliamua kutulia
“Kacha kacha”Risasi zilipandishwa kwenye chemba ya mlipuko katika bastora ile ya yule bwana mwenye chunusi.
“Nimewaza kwa haraka haraka , kama kweli wewe madam huwezi kutuambia kuhusu mbinu ya kimafunzo ya kijini basi mtoto wako ataweza kutuelezea … mtoto huyo wa Roma tayari ana nguvu za kijinni ndani yake tena kwa umri huu mdogo ninaamini uwezo wake ni mkubwa kukuzidi …. Chubby girl tuambie mbinu ya kimafunzo ambayo baba yako amekupatia”
“Your are a bad guy , daddy will come and kill all of you”Aliongea Lanlan huku akiwa na hasira nyingi na kwa jinsi alivyokuwa akiwangaalia kwa hasira ni Roma mtupu.
“Hehee upo kama baba yako tu , tayari mkali ktika umri huo “Aliongea huku akipiga piga mashavu ya Lanlan .
“Ngoja nikuambie kitu Chubby , mama yako atakufa kama hautasema sawa”Aliongea na kumfanya Lanlan kumwangalia mama yake na machozi kuanza kumtoka , lipsi zake zilikuwa zikicheza cheza.
“Mimi sijui kitu..”
Edna alikuwa kwenye maumivu makali ya moyo lakini alipatwa na ahueni kumuona Lanlan anakumbuka maagizo ya baba yake , aliamua kumtingishia na yeye kichwa kumwambia kwamba asiongee.
“You are all badguys .. I don’t want mommy to die..”Aliongea na Lanlan pale pale aliangau kilio cha kwikwi.
“Usilie sasa mtoto mzuri, nitamuua tu mama yako”Aliongea na palepale sura ya bwana mwenye chunusi ilibadilika na kisha akamwangalia Edna na kufanya kilio cha Lanlan kukoma palepale kwa mshituko.
Kwa namna ambavyo Edna alikuwa akiangaliwa na mchezo wanaofanyiwa na hao majambazi maumivu yake yalikuwa ya juu mno ilikuwa ni kama vile moyo wake una charangwa na visu.
Alijiambia ingekuwa ngumu sana kwa maisha ya Lanlan kama ataweza kushuhudia kifo chake katika umri huo mdogo.









SEHEMU YA 506.
“Little girl , nitakupa nafasi ya mwisho , niambie mbinu yako ya mafunzo au nitamlipua mama yako..”Aliongea huku akiisogezea karibu kabisa bastora yake na uso wa Edna.
Edna asingeweza kupona kama siraha hio itamlipua kwasababu mwili wake haukuwa na nguvu kama za Roma
Lanlan alikuwa ni mtoto lakini alikuwa akielewa kama bunduki ile itakohoa basi mama yake anakufa palepale na hakutaka kufanya chochote na palepale alionyesha kufanya maamuzi yake.
“Lanlan usiongee , hawawezi kuniua , usi..”
“Boom!!!”
Sauti ya mlipuko wa risasi ilimzuia kutoendelea kuongea na bwana mwenye chunusi alionekana alilenga juu kwenye bati na kisha palepale ikiwa inafuka moshi aliigeuzia kwa Edna tena.
“Madam acha kujifanya mjuaji , hii bastora ina risasi za kutosha”
Lanlan aliogopeshwa mno na mlipuko wa bunduki na alitetemeka huku akiendelea kulia kwa kwikwi.
“Little girl ,, kama hutotuambia mapema ,,, mama yako atakufa mbele yako ukisikia mlipuko kwa mara ya pili”Aliongea lakini Edna aling’ata meno yake kwa hasira na kumwangalia Lanlan.
“Lanlan usije kuwaambia , ukifanya hivyo sitokupenda tena na nitakuacha”Lanlan aliekuwa akitaka kuongea palepale alifumba mdomo wake kwa woga mara baada ya kusikia maneno ya mama yake
“Mimi sijui”
Alijibu tena huku akiwa na wasiwasi mkubwa wa kitoto , alikuwa akitia huruma kwani sura yake ya kitoto ilibadilika na kuwa nyekundu huku akiishia kumwangalia mama yake kwa hali ya wasiwasi , aliogopa kuachwa na mama yake tena kwa mara ya pili na kuishi maisha magumu.
“Pumbavu kabisa … “Aliongea yule bwana mwenye chunusi na palepale alimsogelea Lanlan kwa ajili ya kumpiga kibao
Alikuwa akijua nguvu zake hivyo hakutaka kumlembesha na kutumia nguvu zake zote
Lanlan kwasababu nguvu zake zilikuwa zimezuliwa hakuweza kujizuia na bonge la bao lilimpata na kumtoa aliposimama na kwenda kujipigza kwenye ukuta puu.
“Hapana..!!!”
Edna alijikuta akitoa ukulele huku akiwa kama anataka kuzimia kwa maumivu .
“Ni mtoto bado , kwanini umemua kumpiga hivyo”Aliongea huku akihisi ni kama kuna mtu anaejaribbu kuwasha moto kwenye moyo wake
Ijapokuwa Lanlan alikuwa ni mwenye uwezo mkubwa lakini kibao kile ni kama maumivu yamemuingia yeye, kilio chake cha kuomba msaada kilijaza eneo lote.
“Huogopi kufa tu , Madam Edna wewe ni mbishi aisee , siwezi kujizuia tena . nimesikia binti yako ni wa kuasili hivyo hana damu ya Roma kama ni hivyo nadhani hutolaumu sisi kumpa mateso mpaka kifo kimkute mbele yako , isitoshe maisha yako yana thamani kubwa kuliko ya kwake”Baada ya kuongea hivyo alimsogelea Lanlan alipolala na kisha aliinua buti lake la kijeshi na kumbutua Lanlan na alikuwa na nguvu mno kwani Lanlan aliamba ambaa kama mpira na kwenda kutua kwenye mguu wa mwanajeshi mwingine na bwana mwingine mara baada ya kuona Lanlan kamfikia alitoa tabasamu la kifedhuli na yeye kujiandaa kuachia pigo lake.
Edna alishindwa kuvumilia na kusimama akiaka kujaribu kuwazuia lakini kwa bahati mbaya kadri alivyokuwa akijitahidi hakuweza hata kumfikia na aliishia kurudishwa kwenye kiti kwa nguvu na mikono ya majambazi wawili.
“Angalia kwa makini , haya ndio matokeo ya wewe kuuziba mdomo wako , mtoto wako anakwenda kufa kifo kibaya sana”
Jamaa yule mwingine mara baada ya kusema na yeye alimbutua tena Lanlan tumboni .
Lanlan masikini alijikuta akijipigiza kwa mara nyingine kwenye ukuta , hakutoa kilioa na aliishia kujikunyata tu kwa maumivu.
Edna alitoa kilioa mpaka koo linamkaukia na aliishia kuangalia tu namna ambavyo mtoto wake alikuwa akisurubiwa
“Pumbavu asiee hichi kitoto kina maajabu yake, bado tu kipo hai”
“Inawezekana akawa ni mtoto wa yule mwanaharamu kweli na hatuambiwi , mwili wake sio wa kawaida kabisa”
“Ni kajibonge na ukipiga kama vile ni mpira , hebu nijaribu na teke langu nione kama atavumilia”Aliongea bwana mwingine.
“Toto zuri , una bahati mbaya sana Roma Ramoni kuwa baba yako , unastahili hiki”Aliongea na pale walianza kumshambulia kwa mateke kwa zamu na kila pigo ni kama maumivu alikuwa akiyasikia Edna.
“Acheni .. acheni ,,, msipige tena binti yangu”
Machozi yaliishia kumtoka na kuloanisha mashavu yake , alikuwa kwenye maombolezo ya hali ya juu kiasi cha kushindwa kupumua ni kama kilio chake analalamika kwa Roma kuondoka na kuwaacha wenyewe.
Kila kitu ndani hapo kilianza kupotea katika macho yake , macho yake yalianza kuingiwa na ukungu huku mapigo yake ya moyo yakianza kudunda kwa kasi sana kiasi kwamba kama upo karibu yake ungeweza kusikia.
Mshipa wa damu maarufu kama ‘Jagular Vein’ na wenyewe ulianza kucheza cheza na akili yake ni kama ilihama katika mazingira hayo na kuingia katika ulimwengu uliojitenga.
Muda ule Lanlan alikuwa amechafuka na aliishia kukaa kwa kunyoosha miguu huku akimwangalia mama yake kwa huruma na aliishia kutema damu nyingi katika mdomo wake na kuchafua nguo zake.
Bwana mwenye chunusi alikuwa na roho ya kinyama kwani bila huruma alimsogelea Lanlan na kumlaza chali na kupeleka buti lake la kijeshi na kuweka mguu juu ya tumbo lake.
“Unaonaje Madam ,,, binti yako atakufa kweli kama huto…”
Aliijikuta akishidwa kuendelea na sentensi yake mara baada ya kuona kuna kitu ambacho hakikuwa sawa kuhusu Edna.
Kichwa chake kiliangalia sakafu na muonekano wake haukuonekana zaidi ya kivuli pekee .
Sio kwake tu kwa kila mtu aliekuwa hapo ndani alishituka , kwani waliweza kuhisi ubaridi zaidi ya kawaida huku hali ya hewa ikibadilika .
Wale watu waliokuwa wamemshikilia Edna wenyewe walianza kutetemeka kutokana na baridi kali iliokuwa ikisambaa katia miili yao , majambazi yote kimya wakiangalia nini kinataka kutokea.
Dakika chache tu ghafla eneo lote lilijaa mkandamizo wa hewa ambao uliwafanya kutetemeka na kukosa pumzi kwa wakati mmoja , ilikuwa ni kama vile kuna moshi uliokuwa ukiingia kutoka nje kutokana na jengo hilo kuungua.
Hatimae Edna aliinua uso wake na kuwaangalia , uso wake ulikuwa ni wa kirembo sana lakini kwa wakati mmoja macho yake yalikuwa tofauti, ni kama vile hakuwa mtu kamili kwani kiini cha macho ni kama kilikuwa kinafifia.
Edna aliwaangalia watu wale kwa dharau kubwa huku akionyesha nia dhahiri ya kimauaji , ni muonekano ambao licha ya wote hapo ndani kuwa wanajeshi msisimko wake uliwatisha.
“Mnastahili kufaa…”Sauti ambayo ni kama vile sio ya kwake ilisikika.
“Acha kutuogopesha, wewe ni..”
Kabla hata hajamaliza sentensi yake Edna palepale alichukua hatua , mikono yake ilijikunja katika angle isiokuwa ya kawaida na wale watu wawili waliokuwa wakimshikilia walijikuta wakipokea mapigo matakatifu makali sana katika matumbo yao na kiatu cha skuna.
Licha ya kwamba walikuwa na mazoezi lakini maumivu yake hayakuweza kuwa ya kuvumilika.
Ilitokea ndani ya sekunde tu kwani walianza kuvunywa mikono yao na ndio wakaunganishiwa na teke.
Edna hakuishia pale tu alikuwa fasta sana kama upepo kwani palepale aliweza kubeba bastora zao na spidi ya kukokiwa na risasi kuruhusiwa ilikuwa ni kubwa mno kiasi kwamba wale wachina waliokuwa kulia kwake walishindwa kuchukua hatua kwani palepale vichwa vyao vilifumuka baada ya kulengwa na shabaha isiokuwa ya kawaida.
Dakika ambayo wale wengine akili zao za kushambulia zinawarudia walikuwa wamechelewa kwani aliteleza kama jini na kumdhibiti mtu mwingine kwa kumvunja shingo na kumbeba juu juu na kurushia waliokuwa mbele yake ambao walikuwa wakielekeza bastora kuelekea kwake , ilikuwa ni staili ya kuwachanganya na palepale kwa spidi alishafikia na mmoja alikula mtama wa sarakasi huku mwingine akivunjwa shingo kwa staili ya kikatili mno.
Bahati mbaya sana kuna jamaa sijui kwanini kamua kuja na upanga, pengine ni sifa kwani hakuonekana kuweza kulitumia katika hilo eneo kwani ile anashtuka ashatenguliwa mkono na panga kuchukulia na koromeo lishakatwa ni matendo matatu yaliofanyika ndani ya sekunde tatu.
Ndani ya dakika chache walibakia wanne tu ambaye ni Bwana mwenye chunusi na mwenzake mwenye sare za kipolisi na wawili wengine na wawili wale wote kwa pamoja walimsogelea na ile wanamkaribia waliweza kuhisi upepo tu ukiwapita na mmoja alishika koromoe huku mmoja akishika upanga uliongia mgongoni na kutokezea kifuani eneo la moyo na kabla hata hajapata nafasi ya kujua upanga umemchomaje alikula teke la mgongo na upanga ukachomoka kwa nguvu na akadondokea mbali kama furushi huku damu kama bomba la maji ikiruka na kwa spidi kubwa Edna alishamfikia bwana mwenye chunusi na polisi mwenzake na palepale ni kama wamesogelewa na Israeli mtoa roho.
Staili ambayo alikuwa akitumia kupambana ilikuwa sio ile ya kubahatisha , ilikuwa ni kama ya ninja ambaye amefundishwa kuua tokea akiwa mdogo , ilikuwa ni ya kiasili kabisa kama mtu anazaliwa nayo.

ITAENDELEA
 
[emoji2923][emoji373][emoji2923][emoji373][emoji1635][emoji512]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…