Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 390.

Kilichotokea kwa Edna kuamka mapema nje ya muda Roma alioukadilia ni kama kile kile kilichotokea Ufaransa, wakati Roma akipambana na Depney , sasa haikueleweka kwanini Edna kuathiriwa kidogo sana na nguvu zao miungu , kwani ufaransa aliemlaza kwenye usingizi alikuwa ni Apollo..

Edna aliamka ndani ya lisaa limoja tu , yaani wakati Roma alivyokuwa usingizini ndio muda ambao Edna aliamka na kuanza kuomboleza.

Edna tokea siku ambayo aliweza kujua siri ya mama yake , siri aliopata kupitia flash Disk aliopewa na raisi Kigombola , alikuwa akitegemea siku moja atakuja kugundua kitu ambacho kitakuja kumuumiza sana kihisia.

Ikumbukwe katika flash ambayo Raisi Senga alimpatia Edna , hakukuwa na maelezo mengi , alichokigundua Edna ni kwamba mama yake alikuwa na kisasi alichokuwa akikiendeleza, lakini pia akampa kazi hio ya kisasi yeye kuikamilisha , huku akiacha orodha ya kampuni ambazo hakukuwa na maelezo yoyote kwamba alichokuwa akitakiwa kufanya ni nini mpaka alipokuja kugundua uwepo wa ‘Deposit Box’ ndani ya Swiss In, ambapo ndani yake ilikuwa imebeba bahasha iliokuwa na taarifa ambayo ndio inamfanya kuwa kwenye hali ya huzuni na majonzi.

Raheli Adebayo katika stori yake ya kimaisha mara baada ya kujua ukweli kwamba mtoto wake Lorraine, pacha wake na Edna anaishi kwa jina la Agent 17, ndio kisasi chake kilianza rasmi , lakini kutokana na kwamba watu ambao walikuwa na mtoto wake kuwa wakubwa serikalini, aliamini pesa pekee ndio zitakazo muwezesha kutimiza azma yake, Azma ya kumrudisha mtoto wake huyo ili kutoendelea kujutia kosa alilolifanya miaka mingi nyuma , kosa la kukubali kumuachia Lorraine Kwenda kulelewa na Raisi Jeremy jambo ambalo lilipelekea kadhia ambayo mtoto wake amekutana nayo mpaka kubadilishwa jina , lakini bahati mbaya mpaka anakufa hakuwa ametimiza Azma yake.

Kwahio ni rahisi kusema kwamba Edna sasa anajua kifo cha mama yake ni cha kutengenezwa , lakini hafahamu kama kuna Zaidi ya kile anachokifahamu ambacho kilikuwa kikiendelea kwenye Maisha ya mama yake, anajua tu kwamba mama yake alikuwa mjamzito wa Watoto mapacha lakini hakuwa akielewa pacha mwenzake yupo wapi.

Edna alikaa kitandani akiwa peke yake huku machozi yakiwa yanamtiririka , kila akijaribu kuyafikiria maisha magumu ambayo mama yake alikuwa akiishi moyo wake ulimuuma na alijidharau mno kwa kutogundua kama mama yake alikuwa akipitia kipindi kigumu , yeye kama mtoto alijihisi alikuwa na haki ya kuwa karibu na mama yake lakini kutokana na ubize wa masomo akashindwa kujua kile kinachoendelea.

Baada ya kuwaza na kuwazua alijikuta akifuta machozi yake na kisha akachukua picha ya mama yake iliokuwa pembeni kwenye kijimeza na kisha akaishika kwa kuikodolea macho , lakini kadri alivyokuwa akiangalia alijikuta machozi yakizidi kumtoka kwa mara nyingine , mrembo Edna alionekana kuwa katika hali ya huzuni mno.

“Mom naomba unisamehe , sikuwepo karibu yako wakati ulipokuwa unapitia kipindi kigumu , I am so so….”Alijikuta akishindwa kuendelea na kuanza kulia kwa kwikwi awamu hii kwa takribani nusu saa nzima alizitumia kuomboleza , mpaka aliponyamaza mwenyewe.

“Nitautafuta ukweli wote na nitahakikisha nalipa kisasi kwa ajili yako mama yangu , ndio njia pekee ambayo naamini utanisamehe kwa kutokufahamu kama ulikuwa ukipitia magumu mengi”Aliwaza Edna huku hali yake ikirejea upya , ijapkuwa hakuonyesha furaha , lakini alionekana kuacha kulia na kuwa na sura iliojaa usiriasi.

Saa moja za jioni ndio alishuka kutoka chini huku akiwa ashaongea na halmashauri ya kichwa chake , alishajiambia kwenye akili yake kwamba vita ndio inaanza , vita ya kulipa wale waliohusika kumfanyia mama yake majaribio ya kisayansi mpaka kupelekea kifo chake , alikuwa ashafanya maamuzi tayari , maamuzi ambayo ili kuyakamilisha alitakiwa kuwa na nguvu na sio kukaa kitandani kuomboleza , alitakiwa kuwa jasiri ambaye muda wowote yupo tayari kukabiliana na maumivu ili kutimiza malengo yake.

Muda ambao alikuwa akishuka kutoka juu ndio muda ambao Afande Kweka alipiga simu kumwambia kwamba ataondoka na Lanlan Kwenda nae Iringa kwenye mashamba yake na Edna jibu alilotoa ni kwamba mpaka amshirikishe mume wake Roma kwanza ,lakini Afande Kweka alimwambia atampigia mwenyewe simu kumjulisha.

Roma alienda kukaa karibu na mke wake na kisha kumshika mkono , Blandina aliekuwa amesimama alijiua kuna kinachoendelea , lakini hakutaka kuingilia na alitembea mpaka jikoni kwa ajili ya kuandaa chakula.

Edna alimwangalia Roma alieshika mkono wake , huku akiwa na sura isio jaa furaha wala huzuni , ilikuwa ni sura yake ile ile ya kikauzi ambayo imezoeleka.

“Edna mke wangu , najua unapitia kipindi kigumu kwa sasa na sijui namna ya kurudisha furaha yako, jana nilikuambia nitakuwa bega kwa bega na wewe kwa nyakati zote za furaha na huzuni hilo ndio nilaloweza kukuahidi”Aliongea Roma na Edna alimwangalia Roma kwa dakika kama moja huku vitu vingi vikipita kwenye kichwa chake , haikueleweka alikuwa akifikiria nini lakini alionekana kuwa na hisia mchanganyiko , hisia za kumlaumu Roma kwanini alimficha juu ya Suzzane , kwanini alimficha mara baada ya kujua ukweli juu ya mama yake lakini wakati huo huo aliamini Roma alikuwa na sababu ya kumficha na huenda hata yeye angekuwa kwenye nafasi yake angeweza kufanya hivyo lakini wakati huo huo akiwa na hisia kwamba mambo yote yameanza kuwa hadharani kwasababu ya uwepo wa Roma kwenye Maisha yake.

Edna alijikuta akitoa machozi na kisha alimsogelea Roma na kumkumbatia na kuanza kulia kwa kwikwi , kitendo ambacho kiliwafanya Bi Wena na Blandina waliokuwa wakiandaa chakula kutoka kuangalia kuna nini kinaendelea.

“Roma kwanini Edna yuko hivi umemfanya nini?”Aliongea Blandina kwa wasiwasi huku akimsogelea Edna na kumshika mikono kwa namna ya upendo na Bi Wema na yeye alimsogelea na kukaa mbele yake , huku upande wa Yezi aliekuwa juu chumbani kwake pia akishuka chini aliona jambo hilo na kumsogelea dada yake wa hiari pia.

Wanafamilia wote walionekana kuwa na wasiwasi na Edna na walitaka majibu, kitendo cha Edna kuona kila mwanafamilia alikuwa na wasiwasi juu yake alijikuta akiinua macho yake na kumwangalia Roma kwa huzuni.

“Edna nisikilize kuna hisia mbaya zinaniambia kilichopo kwenye hii bahasha kinaweza kukutoa machozi, nataka uangalie ukiwa nyumbani na watu wote wanaokupenda wakiwa pembeni yako”Edna alijikuta akikumbuka maneno ya Roma na sasa anaelewa alikuwa akimaanisha nini.

Maisha yake yalikuwa yamebadilika sana , alikuwa na watu wengi waliokuwa wakimpenda tofauti na kipindi cha Maisha yake ya nyuma , sasa alikuwa na familia kubwa ambayo yote inamjali sana.

Edna ilibidi awaelezee kile alichogundua , stori yake iliwafanya kila mmoja kushangazwa na jambo hilo na kuhuzunika kwa wakati mmoja na wote walijikuta wakimfariji.

Roma alipendezwa sana na jambo hilo , swala la kuwa na familia iliokuwa inakujali kwa kila kitu , yalikuwa ni Maisha ya kipekee na alijua nini maana yakuwa na familia Maisha yake ya nyuma alikosa kujua radha halisi ya kuwa na familia na hapo yeye mwenyewe ni kama alikuwa katika hatua za kujifunza nini maana ya familia.

Wakati akiendelea kuwaangalia wanafamilia wake , simu yake iliokuwa kwenye mfuko ilianza kuita mfululizo aliitoa na kuangalia jina la mpigaji na alijikuta akishanga, kwani alikuwa ni rafiki yake Makedoni kutoka Mossad.

Roma alinyanyuka na kisha alipandisha juu kwa ajili ya kuongea na Makedoni , kwani aliamini ikitokea Makedoni akianza kumtafuta yeye basi kuna jambo kubwa ambalo limetokea.

“Your Majesty Pluto were you too bored after not killing anyone for two years , why did you destroy the American Fleet entirely” Ilisikika sauti ya kitetemeshi kutoka kwa Makedoni akimuuliza Roma kwamba amechoshwa na kutoua mtu kwa miaka miwili ndio maana akaharibu meli ya kivita ya Kimarekani.

Roma macho yalimtoka , hakuelewa Makedoni alikuwa akimaanisha nini , Meli ya Kimarekani , mtu yupo Tanzania kwanini aharibu Meli ya kivita ya kimarekani ,

“Makedon , What is this nonsense ? what did I do which even I am not privy to?”Aliuliza Roma kwamba ni ujinga gani Makedoni anaongea juu ya kufanya jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakuwa na uelewa nalo.

*******

Ni siku nyingine kabisa alionekana Raisi Jeremy akiwa ndani ya ofisi yake , huku mkononi akiwa ameshikilia picha ndogo , picha ambayo ambayo alikuwa akionekana yeye na mke wake Kizwe wakiwa kwenye pozi la tabasamu huku Kizwe akiwa amevalia gauni la harusi.

Raisi Jeremy picha hio alikuwa akiangalia tokea jana yake usiku alipompa maagizo Linda kwa ajili ya kuandaa mpango wa kumuua Kizwe , mheshimiwa huyu licha ya kufanya maamuzi ya kumuua Kizwe lakini haikumaanisha kwamba hakuwa akiumia ndani kwa ndani, ukweli alikuwa kwenye majonzi makubwa , Kizwe ni mwanamke ambaye alitoka nae mbali sana tokea kabla hata hajawa raisi wa nchi hio ya Rwanda , walipitia nyakati tofauti tofauti , za furaha na zile za huzuni..

Lakini licha ya histora yao, aliamini Kizwe hakuwa na mapenzi kwake tena na kumuweka hai karibu yake ni hatari zaidi, kitendo cha kuweza kuishi kwa kumuigizia kilimfanya hata yeye mwenyewe kumuogapa na kujiuliza ni mangapi Kizwe amemficha , ni mangapi ambayo amefanya pasipo yeye kujua, ndio alikuwa ni mke wake lakini alimuona kama vile amemfahamu juzi na sio miaka mingi iliopita..

Mheshimiwa Jeremy na mke wake Kizwe walibahatika kupata Watoto wawili pekee ,mmoja akiwa ni Desmond ambaye ndio aliekuwa wa kwanza na wa pili alikuwa ni msichana anaefahamika kwa jina la Kyler.

Kyler alikuwa ni marehemu baada ya kupata ajali kwenye mashindano ya magari nchini Marekani wakati alipokuwa masomoni , hivyo unaweza kusema ni Desmond pekee ambaye alibakia kwenye uzao wake ambaye anaweza kumfanya kama mrithi.

“Forgive me Kizwe Mke wangu?”Aliongea Raisi Jeremy kwa huzuni na kisha ile picha ambayo ilikuwa kwenye mikono yake aliichana vipande vinne na kisha akatupia kwenye dastibin.

Muda huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Linda ambaye amevalia suti ya rangi nyeusi iliomkaa vyema mwilini pamoja na shati rangi ya ugoro ndani yake.

“Mheshimiwa hili ni faili la taarifa za mwanaume aliekuwa na Madam”Aliongea Linda na kisha akampatia raisi Jeremy lile faili na kuanza kulisoma na kadri alivyokuwa akiendelea kusoma alijikuta akishangaa.

“Hii taarifa ni sahihi?”

“Ni sahihi mheshimiwa hata ndugu zake wapo hapa nchini , jimbo la Mashariki”Aliongea na kumfanya Jeremy kufikiria kidogo na kisha akaliweka chini.

“Vipi kuhusu maagizo mengine niliokupatia”

“Kila kitu kipo tayari mheshimiwa, tutampa dawa ambayo itamfanya moyo wake kufeli , ni njia nzuri zaidi ambayo itafanya watu wasitilie mashaka kifo chake”Aliongea Linda kwa huzuni kidogo.

“Okey , nitaelekea State Area D , nikishamaliza mazungumzo ,mpango huo utafuatia”

“Mheshimiwa una uhakika na hili?”

“Linda nishafanya maamuzi tayari na hakuna wa kunizuia tena”Aliongea Raisi Jeremy na kisha alisimama kwa ajili ya kuondoka.

State Area D ni moja ya maeneo maarufu ndani ya Rwanda, eneo hili umaarufu wake ulitokana na kwamba yalikuwa makazi maalumu ya raisi Jeremy.

Sasa muda huo wa asubuhi ulinzi ndani ya hili eneo ulikuwa umeimarishwa mno tokea jana usiku , sabababu kubwa ya kuimarishwa kwa ulinzi ndani ya eneo hilo na makachero wa serikali ni kutokana na maagizo ya raisi mwenyewe mara baada ya Kizwe na Lelcha kufikishwa kwa siri sana nchini kwa ndege binafsi ya kijeshi.

Kwenye watu ambao walikuwa kwenye maswali mengi ni Lekcha tokea siku ya jana anapandishwa ndege mpaka kufikishwa nchini Rwanda kwake kila kitu ilikuwa ni mshangao , hakuwa akijua ni kipi kinaendelea na alishindwa kuuliza pia , kwani alitenganishwa na Kizwe.

Sasa baada ya kutolewa kwenye ndege na kuingizwa kwenye gari ya pamoja na walinzi ndio alipata nafasi ya kuongea na Kizwe.

“Hey nini kinaendelea , hawa watu walitotuleta hapa ni wakina nani?”Aliuliza Lekcha.

“Vipi una wasiwasi?”

“Wasiwasi , mimi niwe na wasiwasi nishakuwa kwenye hali hatarishi kuliko hata hii , kwanini niwe na wasiwasi, unafikiri kwanini nina mguu bandia , yote haya ni Maisha magumu niliopitia kama nilikuwa tayari kushindana na wanyama wakali kwanini niogope binadamu wachache wanaotaka kunidhuru?”

“Wanyama ni rahisi kuwafukuza kwa hila , lakini kuhusu binadamu ni Habari nyingine , binadamu ni kiumbe kisichotabilika na hatari Zaidi”Aliongea Kizwe na tabasamu la uchungu mno.

“Hey hupaswi kuwa na huzuni kiasi hiki kama vile familia yako yote imekufa , wewe ndio ulitendwa kwanini unaonekana kama mwenye kuogopa kama vile kuna mtu kakuwekea siraha kwenye kichwa chako?”Aliuliza Lekcha lakini kabla hajajibiwa gari ilisimama ndani ya eneo hilo la Area D na geti lilifunguliwa na kuingizwa ndani.

……..

Saa tano kamili za asubuhi ndio muda ambao raisi Jeremy aliweza kufika ndani ya eneo hili la Area D, safari yake ambayo ilikuwa ya kimya kimya akiwa ametangulizana na Linda pamoja na walinzi wachache.

Baada ya kufika tu aliongozwa na wanajeshi wawili waliokuwa wana siraha za moto kuzunguka upande wa nyuma na kuingia kwenye moja ya jengo kati ya matatu yaliokuwa ndani ya eneo hilo la makazi maalumu ya raisi Jeremy.

Baada ya kuingia ndani ya chumba aliweza kukutana na sura mbili , ya kwanza ikiwa ni ya mke wake Kizwe na ya pili ilikuwa ni ya Lekcha , wote wakiwa wameketi kwenye masofa wakiwa chini ya ulinzi mkali.

“Nafikiri unanichukia kwa staili niliokurudisha nchini Rwanda?”Aliuliza Raisi Jeremy bila salamu mara baada ya kumwangalia Kizwe kwa dakika kadhaa.

“Kitendo cha kuja mpaka hapa kwa ajili ya kukutana na mimi licha ya yote , nadhani napaswa kushukuru”Aliongea Kizwe. Na kumfanya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Kwanini uliamua kumchokoza Roma?”Aliuliza kwa kifaransa awamu hii.

“Hindsitght is real bitch , you know that ? You might as well say that I shouldn’t have taken action against that little bitch”

“Nyuma ya pazia ndio kuna mbwa halisi na ndio alietoa maagizo na unafahamu hilo? , unaweza pia kusema sikupaswa kuchukua hatua kwa mbwa huyo mdogo”Aliongea kwa namna ya kimafumbo hapo alikuwa akimlenga Edna na alijibu kwa Kingereza.

“Kaa kimya , kwanini unamwita kwa jina la kukera namna hio , unapaswa kufahamu sasa ni mtoto wangu na pia ni mdogo wake Desmond”Aliongea kwa hasira.

“Mtoto wako.. hahaha… hio mimi inanihusu nini? , Edna ni matokeo ya usaliti wako ulionifanyia , kama sio Afande Athumani babu yake kumlinda ningekuwa nishamuua mpaka wakati huu”Aliongea kwa hasira.

“Sijakuleta hata kwa ajili ya ngonjera zako?”Aliongea Raisi Jeremy

“Uko sahihi kabisa , kama nisiposema ninachotaka nani anajua kama naweza kutopata nafasi tena?”

“Ni bora kama ungeendelea kuniigizia kwa Maisha yako yote na kufanya mambo yako kwa umakini, sisi ni wanandoa lakini kudanganyana ingekuwa bora Zaidi kuliko kilichokutokea kama mke wa raisi, Kizwe nilitamani sana siku utakayogundua juu ya Edna ndio mwanzo wetu mpya na kuzika yaliopita , lakini kwa hili linaloendelea najikuta sina chaguo lingine”Aliongea huku uso wake ukibadilika.

“Unaogopa Jeremy ninaweza kukufanyia jambo baya Zaidi kwa kuweza kukuigizia miaka mingi , unaogopa naweza pia kukutoa kwenye nafasi yak kutokana na nguvu yangu ndani ya taifa hili , hivyo unahisi mimi kuwa hai ni hatari Zaidi kwako”

“Unaweza kuwa sahihi , umepotea siku chache tu lakini mabaraza yote yanataka kujua taarifa zako na serikali kwasasa haiko na utulivu , hata kama nikikuua sasa hivi maswali mengi yataibuka”Aliongea Jeremy.

“Kwahio unataka kunifanya nini?”

“Nina mtu tayari ashaandaa sindano ya kimiminika , ambayo itakuwa na uwezo wa kukufanya kama mgonjwa ambaye moyo wake umefeli , nitaelezea uma baada ya kifo chako kama mke wa raisi lakini mwanaharakati wa taifa hili kwamba baada ya kuwa nje ya nchi ulipatwa na tatizo ambalo lilipelekea tatizo la moyo na kutokuonekana kwako hadharani kwa siku hizi chache ni kutokana na kwamba ulikuwa chini ya uangalizi wa madaktari wakijaribu kuokoa afya yako , lakini mwisho wa siku hakuna kilichowezekana kwani hali yako ilikuwa kwenye hatua ya mwisho kabisa”Aliongea Jeremy bila ya kuwa na huzuni kabisa , alionekana ashavunja ndoa yake na kizwe moyoni mwake pekee na hakuna chochote ambacho anajutia.

Kizwe alijikuta akishangazwa kabisa na maneno ya mume wake yakimtoka bila wasiwasi kabisa.

“Sikuweza hata siku moja kufikiria kama itakuja siku mume wangu ndio anaagiza kifo changu , maneno yanakutoka kana kwamba hatukuwahi kupendana hapo kabla , hakika wewe ni raisi wa taifa hili ambaye unapambana kwa maendeleo makubwa Zaidi , Hahahaha… haha,, mbinu yako Jeremy ni nzuri sana na haiwezi kabisa kuacha maswali kama kweli nitakufa kwa shida ya moyo ni mbinu nzuri sana umefikiria”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kufumba macho kwa hisia na kisha akayafumbua.

“Dawa utakayopewa itakuletea maumivu katika mchakato mzima wa kuathiri moyo wako , nilitamani kufanya kifo chako kisiwe cha maumivu lakini hakuna mbinu mbadala Zaidi ya hii , Kizwe nakuhakikishia baada ya kifo chako mwanao Desmond atarithi kila kitu changu nakuahidi”Aliongea

“Hakika utamrithisha kila kitu , sio kwasababu unampenda bali ni kwasababu hauna mbadala hahahaha.., kuna muda nishawahi kufikiria kama Edna angekuwa mwanaume agekuwa na nafasi sawa na Desmond? , kinachoniumiza siku zote kila nilivyojitahidi kujitoa kwa ajili ya Desmond lakini hukukubali msaada wangu na kunipenda kama mkeo bali mawazo yako yalikuwa kwa mpuuzi Raheli na mtoto wake muda wote”Alifoka lakini Jeremy alishindwa kumjibu alimwacha aongee kwani ndio siku yake ya mwisho ya uhai hata hivyo.

“Kwasababu nitakufa muda wowote naomba nikuambie siri ambayo niliificha kwa miaka mingi , ili kukuonysha ni kwa kiasi gani wewe ni mbumbumbu “

“Siri gani?”

“Miaka iliopita sio kweli kwamba Raheli alikufa kwa kansa ya damu iliompelekea moyo wake kufeli”

“Unataka kumaanisha nini?”Aliongea Jeremy kwa wasiwasi.

“Namaanisha kama unavyofikiria , najua hakuwahi kufikiria lakini daktari Hubery aliekuwa akimhudumia Raheli alikuwa chini yangu na vipimo vyake vya kimatibabu vilivyotolewa hospitalini vyote vilikuwa ni feki, hakuna ugonjwa uliomuua bali nilimuua mimi kwa mikono yangu”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kuanza kutetemeka kwa hasira.

“Wewe mwanamke ni shetani wa aina gani , hivi unajua ni kwa kiasi ganri Raheli alikuwa akikujali , ni kweli nilikuwa na uhusiano nae lakini hakutaka uhusiano wake na mimi kukuathiri hata kidogo , ndio maana akaamua kuolewa na mwanaume asiekuwa na mapenzi nae , aliishi bila ya kunitafuta na siku zote mimi ndio niliekuwa nikimsumbua ,kwanini hukujali yote hayo na alikuwa rafiki yako?”Aliongea kwa hasira mno , huku macho yake yakiwa mekundu.

“Niite shetani na majina mengine ,lakini siku zote nilikuwa mwenye kupta ninachokitaka”Aliongea bila ya hatia.

“Sawa ulichokifanya kishakwisha kufanyika , ni wakati wa kulipwa kwa makosa yako , jitafakari kwa matendo yako yote kabla ya sumu ya kifo haijaletwa kwako na kuchomwa”Aliongea na kisha alimwangalia Lekcha.

“Kwasababu huyu bwana wako ndio aliekuokoa lakini pia ameweza kusikiliza kila kitu, tulichoongea hapa angalau safari yako haitakuwa ya kinyonge mnaweza kuendelza mapenzi yenu mbele ya safari huko kuzimu”Aliongea na kisha akaondoka kwenye chumba hicho na kuwaacha marehemu watarajiwa.

MWISHO WA SEASON 13

Unafikiri ni nani alieharibu meli ya kivita ya Marekani , je ni Hades kama alivyosema Makedoni.

Yan Buwen na teknolojia yake ya Growth acceleration kama ni kutengeneza Clone ya Roma basi atahitaji angalau miezi minne , swali je amefanikiwa nje ya miezi minne.

Je kifo cha Kizwe ndio mwanzo wa Jeremy kumtangaza Edna kama mtoto wake , unafikiria Desmond atakuwa na hali gani akijua baba yake ndio aliemuua mama yake.

Yajayo yanafurahisha sanaaaaaa…..

OYA ACHA UBAHILI BWANA NI BUKU TATU TU KUJIUNGA GRUPU TUPO SEHEMU YA 460 , NICHEKI NAMBA 0687151346 ONLY WATSAPP

SEE YOU SOON
Nakushukuru sana Kaka Singanojr kwa usanifu wako wa riwaya hii.
nakutakia jioni njema.
Adios 390.
 
Na mkilipia Mnaachwa njia panda maana sisi tunaolipia kule whatsapp tunagombana naye kila siku, stori haijaisha na mwendolezo ni wa kusuasua jamaa hakosi sababu na akitoa ahadi hatekelezi kamwe.
So ukitoa buku 6 utapata vipande kadhaa then ukitufikia tulipo unaungana nasi kwenye kuipita dhiki.
dah eti kupitia dhiki ndio mpo levo iyo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
SEHEMU YA 404.

Robert alijikuta akiwa kwenye mshangao na sio kwake tu na wafanyakazi aliokuwa akiwafokea pia walijikuta kuchanganyikiwa.

“Pumbavu kabisa , inaonekana tumapata tatizo lingine la kushughurikia kwanza, tunapaswa kuondoka”Aliongea akiwapa ishara wamfuate.

Walitoka na moja kwa moja walienda mpaka floor ya chini Zaidi , sehemu ambayo ndio kuna udhibiti wa mitambo yote ya idara hio.

Eneo hilo na la juu lilikuwa na utofauti mkubwa sana , chini yake pia kulikuwa na eneo kubwa sana ambalo limejengwa kwa teknolojia kubwa , huku Gajeti na skrini mbalimbali pamoja na taratikishi zikiwa zimezungukwa na wafanyakazi Zaidi ya mia moja wakifanya kazi yao , eneo hilo ndio moyo wa idara hio kwa taarifa zote.

Lakini licha ya mkusanyiko ya wabobevu wa komputa wakizicharanga batani , lakini kulionekana hakuna mafanikio ya aina yoyote kabisa na mbaya Zaidi sasa ni kwamba mdukuzi aliehusika alifanya skrini zote kuonyesha muvi moja maarufu kwenye skrini zote.

“What the hell do you think you are paid for ?How can the HQ be hacked by just anyone , Our national intel is at stake”Alianza kufokea wafanyakazi wake kwa hasira

Robert Mueller kilichomfanya kukalia kiti cha ukamishina kwa muda mrefu ni kutokana na umahili wake katika kuzuia mambo ya udukuzi lakini pia kuwa mkamilifu katika kila misheni inayoibuliwa na idara hio.

Lakini mambo yanayomtokea siku hio , yalikuwa ni kama yanahatarisha nafasi yake , kwanza kabisa alikiuka maagizo ya wakuu wake na Kwenda kumshambulia Hades na pili makao makuu yamedukuliwa ilikuwa ni kibao cha uso kwake kwa aliefanya hivyo.

“Sir kaa kwa kutulia kabisa , mtu ambae amedukua anaonyesha kutokuwa na shida na taarifa zetu , bali amedukua mfupo wa mawasiliano wa Frequency , inaonyesa kuna kitu anataka kuonyesha laivu”Aliongea mmoja wapo

“Tayari mdudu ashaingia kwenye mitambo yetu halafu unaniambia huo upuuzi , unajua inamaanisha nini kama kuna mtu ndani ya dunia anaweza kutudukua?”Aliuliza kwa hasira.

“Sir”Aliita msichana mmoja mwenye nywele nyeupe kichwahi na kumfanya Robert amuangalie.

“Nadhani nimefanikiwa kujua mdukuzi wetu ni nani?’’

“Nini ?Ni nani?”

“Inaonekana ni Mossad kutoka Israel “Aliongea na kumfanya Robert kuwa katika mshangao , alijiuliza kwanini Israel wachukue hatua ya kudukua taarifa zao.

Lakini kabla wote hawajafahamu ni ipi nia ya wayahudi kuwadukua , ghafla muvi ilibadilika kwenye skrini na kuwafanya wote kushangaa.

“Oooh!... Taratibu mpenzi unaniumiza wewe mtoto”

“Una genye la kufa mtu mbwa wewe kama vile Nguruwe”

“Ni kwasababu yako wewe mpuuzi mambo yako si haba .. Aissii”

Kwenye skrini hizo kilionekana chumba cha sebule kikiwa na mwanga mkali wa taa unaomulika , huku mwanamke mmoja anaekaribia kuuaga ujana akiwa amekunjwa vizuri na mvulana wa makadirio ya miaka ishirini.

Kitendo kilichokuwa kikifanyika kilikuwa ni cha aibu mno mbaya Zaidi wafanyaikazi wote waliokuwa wakiangalia muvi hio walikuwa wakiwafahamu watu wanaoonekana kwenye hizo skrini.

Na walijikuta wote kwa pamoja wakimwangalia Robert ambaye alikuwa kwenye mshituko wa kutoamini kile kinachoendelea .

Miaka mitatu nyuma mara baada ya Robert kutalikiana na mke wake alijikuja kupata mwanamke mrembo sana mwanamitindo na kumuoa , Wakati huo Robert alikuwa tayari anaishi na mtoto wake wa kiume wa miaka kumi na saba katika nyumba yake aliempata na mke wake wa kwanza.

Hivyo watu waliokuwa wakionekana ni mke wake pamoja na mtoto wake wa miaka ishirini wakifanya ufilauni , kwa haraka haraka mpaka kufika kwa video hio ndani ya makao makuu inaonyesha kwamba ni skendo kubwa sana kama ingetoka hadharani na ingemaanisha kumdidimiza kabisa Robert katika fani yake na kumuondolea vyeo vyote, ijapokuwa ni mwana na mama wa kambo haikumaanisha kwamba wanakosa uhusiano wa kindugu wa kuhalalisha matendo yao.

“Unaonaje umahiri wangu … vipi mimi na mzee yupi ni noma?”Aliongea lile toto lisilokuwa na aibu.

“Jamani mpenzi wangu , kuna haja gani ya kumtaja huyo mwanaume , tokea niolewe nae hajawahi kuwa kama mwanaume kwa Zaidi ya mwaka , nahisi kujuta hata kufunga nae ndoa”

“Huh.. sio mbaya lakini, huoni yote haya ni kama yamepangwa tuseme asingekuoa unafikiri tungekuwa na hii burudani”

Wafanyakazi wenzake walijikuta wakijitahidi kutumia nguvu zao zote kuzuia vicheko maana mazungumzo hayo hayakuwa ya kawaida hata kidogo.

“Natoa agizo ya kupasuliwa kwa Monitor zote , pasueni”Aliongea Robert kwa hasira

“Boss punguza hasira , hatuwezi kuruhusu adui yetu kuzidi kushinda tukipasua”

“Screw off”Aliongea kwa hasira na kusogelea kijisturi na kukinyanyua na kuanza kukipigiza kwenye skrini.

“Bang!”

“Mzuieni asiendelee, hasira zake hazina faida ni hasara”Aliongea mmoja wapo mwenye cheo na palepale wanajeshi walimsogelea na kumshika kwa nguvu kumzuia

“Niachieni nyie wapuuzi kama hamtaki niwafukuze kazi , mimi ni Robert Mueller Boss wenu”Aliongea lakini alishikiliwa vyema pasipo ya kuachiliwa.

“Sir hutakiwi kuwa hivi kwa muda huu , wote tunajua Mossad ndio wamemua kutushambulia , lazima tujue sababu ni nini?”Alishauri mmoja akijaribu kumtuliza Robert.

“Hapana sio kweli ninachokiona , nimemkuza mwenye yule mtoto kwanini kaamua kufanya vile”Aliongea kwa huzuni huku akitamani kulia , kwa hali alioina hakuna mwanaume ambaye anaweza kuvumilia , lakini sio hivyo ni bora mwanaume angekuwa ni wa nje lakini mtoto wake ,ilikuwa ni ibu kubwa sana kwake.

Wakati wakiendelea kumtuliza boss wao Alarm ilianza kutoa mlio kama vile jengo limeshika moto na mitambo kuanza kubipu kwa rangi nyekundu

“Nini kinaendeea?”

“Nadhani tupo chini ya mashambbulizi”Aliongea mmoja wao kwa wasiwasi na wanajeshi wote walijiandaa kwa ajili ya kujilinda , lakini kabla hata hawajazifikia siraha zao ulisikika kama mtikisiko.

“BANG”

Ukuta wa jengo wa juu ulionekana kubomoka na kuacha eneo lote kuwa vumbi na kushikwa na woga usiokuwa wa kawaida , lakni wakati bado wakijiuliza ni nini kinaendelea mwanaume mmoja mwenye Ngozi nyeusi alitokezea mara baada ya vumbi kutulia.

“Pluto!!”

Walijikuta wote wakiwa kwenye mshangao baada ya kugundua mtu aliebomoa ukuta na kufosi kuingia alikuwa ni Pluto mwenyewe , walijiuliza imekuwaje akawa hajaumia popote.

Walishangaa hivyo kutokana na kwamba kuna misheni iliokuwa ikiendelea , misheni ya kumkamata baada ya kusikia hana nguvu zozote baada ya kupigana na Poseidon.

Roma mara baada ya kuangalia skrini za humo ndani alijikuta akiridhishwa na alijiambia vijana wa Mekedoni chini ya Mossad hakika wanaijua kazi yao , hakutegemea wangeweza kufanya vizuri namna hio lakini hakujua pia Mossad watakuwa na aina hio ya Vidio kwenye mafaili yao.

Hata hivyo hakushangaa sana , kwani imekuwa tabia ya idara nyingi za kijasusi kuwashikia viongozi udhaifu wao, Kiongozi unaweza kujikuta unafanya mambo yanayochafua taswira yako ukajua hufuatiliwi , lakini kumbe watu muda wote wapo macho na sio kwa kiongozi tu mpaka kwa familia, hivyo ukishakuwa na madaraka ni kama upo gerezani kwni lazima uhakikishe familia yako inafanya mambo katika mstari wa maadili ndio uwasimamie wengine.

Sasa Roma siku zote alikuwa akichukia sana uchokozi , ijapokuwa siku zote alikuwa na visasi na kundi la Dhoruba Nyekundu lakini aliamua kupotezea , kitendo cha Robert kutuma watu kumchokoza aliamini ni uchokozi wa hali ya juu ambao adhabu yake ni kifo bila rufaa.

FBI walikuwa washirika wakubwa wa Dhoruba nyekundu , ijapokuwa mpaka sasa inashindwa kueleweka makao makuu ya Dhoruba nyekundu yako wapi , lakini inasemekeana kila nchi kubwa duniani wana ofisi zao za siri sana na mara nyingi hushirikiana na mamlaka husika kutekeleza mambo yao na hio ndio sababu ya kufanya mambo yao Kwenda rahisi , kwa mfano kwa Marekani walikuwa na kambi ambayo kiongozi wao mkuu ni moja ya viongozi wa FBI ambaye ni Robert Mueller.

Roma alilifahamu hilo muda mrefu tu ndio baada hata haikumpa shida kugundua mchawi wake ni Robert Mueller.

“Naomba mnisahemue kwa kuchelewa kwangu , najua wote mlikuwa mkinitafuta na kujiuliza nimetowekea wapi , nilikuwa nyumbani nikipata chakula kabla ya kuja hapa”Aliongea Roma bila ya wasiwasi utadhani kuna aliemuuliza.

“Wewe shetani , kwanini ukaamua kufanya kitendo cha namna hii cha kunidhalilisha?”

“Kamishina tuliza wenge ijapokuwa hatukubaliani mahusiano ya kimapenzi kati ya mtoto na mzazi , lakini hata hivyo una mke mzuri sana naweza kusema isingekuwa siku zangu chache za kukaa hapa Marekani , huenda ningeenda kumtembelea , siamini kama atanikataa”

“Kaa kimya mbwa wewe unaongea ujinga gani , mpigeni risasi”Aliamrisha lakini hakuna ambaye alikuwa na ujasiri wa kufanya kama alichoongea.

Mtu aingie ndani y makao makuu ya FBI bila wasiwsi tena kwa namna ya kuvunja ukuta ambao umejengwa kwa vyuma vizito na zege kisha kuingia kwenye vyumba vya ardhi kama ni kwake halafu siraha za risasi ziweze kumdhuru , ilikuwa kichekesho ndio maana walitulia.

Robert baada ya kuona hakuna mwajaeshi anae chukua hatua alijikuta akijituliza kidogo na kumwangalia Roma.

“Naona haukupoteza uwezo wako?’

“Imekuuma?”

“Kivipi .. kwanini iniume Generali Prandell najua hakuwa na sababu ya kutudanganya lakini nina uhakika kwa masikio yangu mawili nilimsikia akisema hauna nguvu zozote na umekuwa kama binadamu wa kawaida , lakini kwanini..”

“Unaniuliza mimi tena , hilo ni swali ambalo unatakiwa kujiuliza wewe mwenyewe , najua ni kweli kasema hivyo lakini je nilikuambia nimepoteza uwezo wangu?”Aliongea Roma.

“Kama ni hivyo naamni Seidel na Stark , pamoja na wanajeshi tuliotuma hakuna hata mfupa uliobakia dunani?”

“Mh sioni mwanajeshi yoyote wa Dhoruba nyekundu hapa , wewe ndio kiongozi wao kwa hapa nchni, unaonaje ukiwakusanya na wote mkawepo sina haraka , lakini itakuwa shangwe kwangu wakiwa wote baada nina hamu ya kuwamaliza wote niwe na amani”

“Nyie wengine mbona mpo mpo tu kizembe hammnichulii hatua wakati jengo lenu limeingiliwa?”Aliuliza Roma akiwangaangalia.

“Mtukufu mfalme Pluto tunaomba ukarimu wako kuliacha hili lipite , kwa mtu mwenye heshima yako na hadhi ya juu huruma na ukarimu ni vitu ulivyojaaliwa ,kwasababu watu walioagizwa kukuua wamekufa unaonaje ukituacha sisi hai”Aliongea Robert kinafiki mara baada ya kujituliza.

“Unaongea nini wewe , yaani umeagiza mimi niuliwe lakini nikajiokoa nakuja hapa kulipa kisasi unakata nisamehe , dunia haiendi hivyo unafiikiri nimekuja hapa kwa ajili ya kufanya utani au kujionyesha kwenu nina uwezo wangu”

“Mfalme Pluto nadhani unaelewa hapa ndio makao makuu ya usalama wa taifa na kama utafanya jambo lolote baya ni kama kutangaza vita na serikali yetu ya Marekani , naamni uwezo wa hisia zako ni mzuri na utafanya maamuzi yalioyabusara Zaidi”Aliongea mmoja wao lakini maneno yake hayakumfanya Roma kuona woga.

“BANG !BANG!”

Aliharibu takribani tarakishi kumi kwa kuzilipua na uchawi wake kama onyo la kutoletewa vitisho vya serikali ya Marekanni na upuuzi mwingine.Moto na cheche tu ndio zilijaza eneo lote na kuwafanya watu wote kunywea huku wadada wakiogopa Zaidi.

“Nikisikia tena mambo ya kidiplomasia kama majibu yenu nitahakikisha hakuna mtu atakaetoka hapa na uhai”Aliongea Roma na kuwafanya kunywea mno na Robert alielianzisha alijikuta akikosa cha kuongea na hasira zake juu ya Pluto ziliongezeka maradufu.

“Sir ilikuwa ni kosa letu kukuchokoza hivyo naamini swali la kukuuliza sio kukuomba utache hai bali ni kukuuliza unataka nini kutoka kwetu , Vipi tunaweza kusahihisha na kufanya hali itulie? , kama unataka kuwaua wanajeshi wote wa Dhoruba Nyekundu naogopa kusema kwamba ni swala ambalo lipo nje ya uwezo wetu na hata hivyo Dhoruba Nyekundu haishikiliwi na taifa la Kimarekani pekee, mpaka sasa tunajua Maisha yetu yapo mikononi mwako , lakini pia miungu mingine imekubaliana na serikali zote kuishi kwa kuheshimu sheria za binadamu bila kuleta machafuko , hivyo nikuombe usiendelee na hili na tutafanya kila linalowezekana kukufidia”Aliongea mwanajeshi mwingine wa Kiafrika na kumfanya Roma kuvutiwa nae.

“Unaitwa nani?”

“Mario Balotelli Sir”Alijibu

“Wewe ndio umezielewa hisia zangu ni kweli kabisa mpaka sasa mnaishi kwasababu nimemua , kama ningetaka ningebomoa jengo hili na mkafia ndani na hakuna mtu angeweza kunigusa “

“Ndio nafahamu hilo ndio maana nimechkua nafasi hii kuongea ile nisije kosa haki ya kuongea kabla kufa”

“Okey maneno yako yamenivutia , nitakupa nafasi ya kuwaokoa wenzako”

Aliongea Roma na kisha alisogelea siraha na kuikoki kisha akampatia Mario Baloteli.

“Kwasababu shida yangu ni boss wenu , nataka umpige risasi wewe mwenyewe na ukifanikisha hilo kila mtu hapa atatoka akiwa na uhai wake”Aliongea Roma na kuwafanya wengine wote kutoa macho ya mshangao.

“Mfalme Pluto unamaanisha nini juu ya hli?

“Namaanisha muue , jambo rahisi tu”Aliongea Roma na kumfanya Baloteli kumwangalia bosi wake na kuanza kusita sita kufanya kama alichoelekezwa.

“Narudia tena , una chaguzi mbili tu za kuachia risassi kumuua boss wako na kukoa kila mmoja hapa ndani , pili usimuue boss wako na mimi kwa niaba ya uaminifu wenu kwa boss wenu , nitahakikisha mnamsindikiza kuzimu” baada ya wote kuona Roma yupo siriasis waliangalina.

“Wewe mpuuzi kama haupo tayari kumuua nipe mimi hio siraha”Aliongea mmoja wapo na wote walianza kuunga mkono , hakuna ambaye alitaka kufa wakati nafasi ya kuwa hai ipo.

“Jiangalie ulivyomsaliti , unakwenda kweli kutotii maagizo ya wakuu wako na kuniua , je unajua ni kipi kitakukutana ukifanya hivyo, Baloteli hebu nisikilize , kwanini umuogope huyu mpuuzi na yupo kwenye makao yetu makuu na pia sio kwamba yeye ndio mungu pekee kati ya miungu yote, kama ataharibu na ktua ni hakika miungu mingine itaanza kumuwinda”

“BANG!”

Kabla hata hajamaliza sentensi yake Baloteli hakuta kuleta ujinga alivuta triga na palepale risasi ikampata Robert kwenye kifua , Robert alidondoka taratibu kama mtu ambaye hakuwa akiamini moja ya vijana wake aliokuwa akiwaongoza ameamua kumuua kifo kilimnyemelea kwa mafadhaiko.

“Sisi sio watumwa wako , bali tulikuwa wafanyakazi wenzako wewe mjinga”Aliongea Baloteli mara baada ya kuhakikisha Robert kadondoka chini na kuzungukwa na dimbwi la damu.

Roma alijikuta akipiga makofi kwa kuridhika , mpaka hapo alijiambia hana kesi kwani aliemuua sio yeye bali ni Baloteli.

“Hongera umefanikiwa kuwaokoa wenzako , kama itatokea siku ukaja kuwa Kamishina wa FBI usije ukafanya kosa kama hili tena”Aliongea a kumfanya Baloteli kuwa katika mshangao maana hata siku moja hakuwahi kufikiria kama anaweza kuwa Kamishina wa FBI, kwani siku zote waliopatiwa cheo hiko ni watu weupe.

Roma aliwapotezea kwa jinsi walivyokuwa wanashangaana , huku wengine wakimshukuru Baloteli kwa kuwaokoa , yeye alipita na kuiinamia mwili wa Robert na kuanza kumpapasa mfukoni na ndani ya dakika chache to aliweza kutoka na saa ya rangi ya Dhahabu na Copper.

Walimwangalia kwa mshangao na wachache walijiua saa alioshikilia Roma ni moja ya vitu ambavyo vilikuwa vikipendwa sana na Robert.

“Msiniangalie kwa macho yenu hayo , mnafikiri namuibia huyu mpuuzi, kasababisha nimepoteza gari ya watu mpaka sasa hivyo najaribu kujilipa fidia , ijapokuwa saa hii haiwezi kutosha kwa thaman ya ghari ila inaweza kupunguza hasara”Aliongea na akaendelea kumsachi na kukuta hakuwa na kitu kingine Zaidi ya pakiti ya sigara na kujikua akimpiga Teke na kujiambia kweli hakukuwa na mtu hapo na bora hajajitia mikosi kumuaa ,alijiuliza inakuwaje mkuu wa FBI kutokuwa na kitu cha thamani. ,

Roma mara baada ya kuridhika aliwageuka na kuwaangalia wafanyakazi wote waliojipanga msururu, mara nyingi idadi yao ni tofuati na nyakati za mchana kwani jengo hilo lingekuwa na wafanya kazi wengi .

“Nimeridhika sasa na kisasi changu sitaki swala hili lijirudie tena , kwasasa eneo hili sio salama kwa ninyi kuendelea na kazi , kwa niaba ya serikali yenu Marekani nawapa ruhusa ya Kwenda kupumzika majumbani kwenu, ambao mmeolewa mkatoe haki ya ndoa na ambao mmeoa mkatimize haki ya ndoa, ninyi warembo ambao hamjaolewa ni muhimu pia kupata usingizi wa kutosha sura zenu zisikunjamane na mkakosa soko , kwenu pia washikaji kulala mapema kunaongeza nguvu za kiume na mvuto”Aliwapa ushauri wa kiafya akijikuta ni mwenye kujali na kisha bila kujali mwonekano wao aliondoka na ile wanachungulia kwenye Korido , tayari alishapotea

Dakika chache mbele Roma alikuja kutua nje ya bustani ya jumba la Christen ndani ya Loss Angeles .

Christen alionekana tayari alisharudi na sasa alionekana juu ya balkoni akiwa ameshikilia mvinyo wake akiruhusu upepeo wa baharini kumpuliza , alimwona Roma alivyoibukia na kujikuta akitabasamu kwa kejeli.

Alikuwa na kila taarifa ya kile kilichotokea ndani ya jiji hilo, kitendo cha Roma kuwaangamiza wanajeshi wote pamoja na kundi la ninja kutokaTakamagahara.

Roma mara baada ya kugundua uwepo wa Christen juu ya Balkoni akiwa na kigauni chake kinachopeperushwa na upepo , mwili wake ulimsimka , kwani alikuwa akiona kila kitu ndani ya nguo za kigauni chepesi cha mrembo huyo na kugundua hana nguo ndani yake aliamini Christen alikuwa bado hajamkatia tamaa na alikuwa akiendelea na mitego yake.

“Siwezi kuendelea kukaa Hapana na huyu mwanamke , kesho narudi Bongo”Aliwaza Roma huku akianza kupiga hatua kuingia ndani ya jumba hilo.
404
Shukrani Kaka Singanojr.
adios
 
Duh! Hali ni zogolezagala shaghalabhaghala😎😎😎

413
Adios
Kaka Singanojr.
 
Na mkilipia Mnaachwa njia panda maana sisi tunaolipia kule whatsapp tunagombana naye kila siku, stori haijaisha na mwendolezo ni wa kusuasua jamaa hakosi sababu na akitoa ahadi hatekelezi kamwe.
So ukitoa buku 6 utapata vipande kadhaa then ukitufikia tulipo unaungana nasi kwenye kuipita dhiki.
Jamaa anatamaa za kijinga sana
Ni muongo wa kutupwa
Katika hili amejiharibia sana
 
Na mkilipia Mnaachwa njia panda maana sisi tunaolipia kule whatsapp tunagombana naye kila siku, stori haijaisha na mwendolezo ni wa kusuasua jamaa hakosi sababu na akitoa ahadi hatekelezi kamwe.
So ukitoa buku 6 utapata vipande kadhaa then ukitufikia tulipo unaungana nasi kwenye kuipita dhiki.
Kama vipi mngesaidia kutupia muendelezo kwa sisi tunaosoma JF angalau tusogee mbele manake tumeachwa !
 
SEHEMU YA 556.
Damu zililikuwa zikitoka kwenye majeraha yake na alikuwa na michubuko kutokana na kudondoshwa chini, jambo ambalo lilimfanya iwe ngumu kusogea.
Ijapokuwa Roma alikuwa ashageuka na kumwangalia lakini hakufanya chochote zaidi ya kumwangalia tu.
“Huwezi kuendelea kuishi hapa tena”Aliongea Roma mara baada ya kimya kifupi.
“Mmh..!”
Jumba lote lililokuwa likionekana kuwa zuri kwa nje lilishaharibiwa na hata kama angetafuta mafundi kurekebisha ingechukua muda.
“Usisogee ngoja nikusaidie kupona”Aliongea Roma na kisha akamnyooshea mkono ili kumsaidia kusimama lakini Roma mikono yake ilikuwa ikimtetemeka na kumfanya Edna amwangalie usoni na kugundua hakuwa na hasira bali alionekana kuwa na wasiwasi.
“Nini tatizo?Kwanini mkono wako unatetemeka?”Aliuliza Edna huku akimwangalia Roma kwa wasiwasi lakini upande wa Roma aliangalia pembenni huku akificha macho yake ambayo yashaanza kuwa mekundu kama mtu anaetaka kutoa machozi.
Lakini kitendo kile Edna aliweza kukiona na alipatwa na mshutuko halafu akaingiwa na wasiwasi zaidi.
“Bado tupo kwenye hatari , nini kinaendelea?”Aliuliza Edna.
“Hatari gani? Kidogo tu ungekufa”Aliongea Roma huku sauti yake ikiwa tofauti na ile iliozoleka , sauti kama ya mtu ambaye amekosa ujasiri na kumfanya Edna kushangaa na hapo hapo kujua kilichomjaa Roma ni hisia za woga.
Alikuwa akijaribu kuficha lakini alikuwa na woga ambao umemvaa na Edna alfikia hatua ya kujiuliza ni hofu gani aliokuwa nayo mpaka akawa hivyo kwani ni mara yake ya kwanza kuwa hivyo.
“Je unajua ungekuwa maiti iliokauka kama ningechelewa kidogo tu , kwanini haya yanatokea , kwanini inaonekana kama nashindwa kukulinda wakati bado nipo hai?”
“Je mimi sina maana tena , nilishashuhudia kifo chake yule mwanamke akiwa na mtoto wangu tumboni miaka mitatu iliopita , sina ujasiri kama nitaweza kuvumilia kama ikitokea mara nyingine , Edna nakuomba usije ukafa mbele yangu hata kama ni mwisho wetu naomba nife mimi kwanza tafadhari”
“Na…”Alitaka kuongea neno lakini Roma alimkatisha.
“Usiongee chochote ..”Baada ya kuongea vile mkononi mwake ilionekana ile bangiri .
“Najua unanioona kama vile mimi ni mbinfasi m, niawezaje kukuambia haya ikiwa mimi ndio mwenye makosa , sio kwamba nakulazimisha kunisamehe na pia sina ujasiri wa kusema siwezi kukasirisha tena lakini tafadhari vaa hii bangiri ili angalau niweze kujisikia vizuri , ni kwa ajili ya usalama wako”
Edna alimwangalia kwa upole na aliishia kuchukua bila ukinzani ile bangiri katika mikono yake na kisha akaivaa.
Muda huo huo waliweza kusikia magari yakiingia hapo ndani kwa kufuatana , wale wachawi kutoka Scotland wa kundi la siraha kwenye jiwe inaonekana wamekuja kwa kuchelewa.
Tukio zima lilitokea kwa takribani dakika ishirini na Roma yeye aliwahi kufika kutokana na kwamba ameteleport lakini kwa watu hao walifanya kuendesha magari yao ndio maana iliwachukua muda kufika.
Mwanamke wa kizungu aliefahamika kwa jina la Lola alitoka nje ya gari na alijikuta akipigwa na butwaa mara baada ya kuona miili ya watu waliokufa ikiwa imesambaa.
Muda huo Roma aliweza kutoa ule Mshipi wa Kichawi na kuushikiria mkononi na Lola na watu wake walijikutua wakiungaa mara baada ya kuuona lakini kilichowashangaza zaidi ni kukuta alieushikilia ni Roma.
“Damn it we came too late This divil has killed everyone”Aliongea Prince akimaanisha kwama wamekuja kwa kuchelewa na Shetani Roma ameua kila mtu.
“Funga domo lako Prince , hujakoma tu”Alifoka yule mwanamke aliewafuata ambaye jina lake ni Lola.
“ Hali ni mbaya , kwanini hakuna maiti yoyote ya kundi la wanywa damu hapa?”Aliuliza mmoja wao kwa lugha ya kingereza.
Roma hakujali mshangao wao zaidi ya kuchunguza mshipi ule wa kichawi uliokuwa kwenye mikono yake huku pembeni yake akiwepo Edna.
“Sijui nani ameuweka hapa kwenye hii nyumba , lakini hii Dhana ni feki”Aliongea na wale wachawi wa kuzngu hakuna ambaye aliongea lolote wala kusogea kutokana na kuogopa uwezo wake.
Roma aliwaangalia kwa macho ya dharau na kisha aliutupa ule mkanda hewani na palepale aliita moto wa kijini wa rangi ya njano na aliiunguza , lakini kutokana na ule mkanda kuwa na nguvu ya ziada ya kichawi ulivyokutana na nguvu ya Roma ulilipuka kama bomu na palepale ukageuka na kuwa majivu.
Wale wachawi wa Siraha kwenye Jiwe walijikuta wakipatwa na mshutko kwani hawakugetemea kitendo hicho.
“Okey , Sijui nani kaanzisha huu uzushi lakini nyie wote safari yenu ya kuja Tanzania haikuwa ya maana , Rada za jeshi kitengo cha wachawi zimewashawanasa , nadhani mnapaswa kurudi nchini kwenu Scotland , nani anaweza kujua, huenda kuna chochote kinachoweza kutokea nyumbani kwenu na ukawa huu ni mtego”
Mwanamke wa kizungu aliefahamika kwa jina la Lola alitingisha kichwa kumuelewa Roma na kisha akainamisha kichwa chake mbele yake kwa ishara ya heshima.
“Mfalme Pluto asante kwa kututaarifu tuondoka Tanzania mapema iwezekanavyo”Baada ya kuongea hivyo Lola aliwapa ishara wachawi wenzake na waliingia kwenye gari na kuondoka katika eneo hilo.
Tunafanya nini kuhusu hizi maiti , au tuwapigie simu polisi?”Aliuliza Edna mara baada ya kuponyeshwa majeraha yake.
“Usiwe na wasiwasi , Jeshi kitengo cha wachawi watadili na hili , turudi nyumbani”Aliongea Roma.
Ndio polisi wa kawaida wasingeweza kudili na hali ya namna hio kutokana na kwamba hawakuwa na kitengo chochote cha kudili na uchawi pamoja na nguvu za ziada , hivyo maswala yote ya giza ndani ya taifa yalishughulikuwa na wanajeshi maalumu ambao walienda nchini China kufundishwa kupambana na uchawi na ndio kikaja kuwepo kwa mara ya kwanza katika jeshi la Tanzania.
Kwa mfano nchini Scotland jeshi lao lilikuwa likishirikiana kwa karibu zaidi na SIS(Sword in the Stone) kupambana na nguvu za ziada ambazo zinahatarisha usalama wa nchi.
Roma hakujali mavazi ya Edna ya kulalia , alimbeba juu juu kama mtoto na kisha akapotea nae kurudi nyumbani.
Roma mara baada ya kufika nyumbani akiwa na Edna aliweza kumpigia simu Bi Wema na kumtaarifu kwamba Edna amerudi na taarifa hio ilimfurashisha Bi Wema na kuahidi kufika kesho kuendelea na majukumu yake .
Upande wa Rufi mara baada ya kusikia Edna karudi alijikuta akipatwa na huzuni kwani angekosa muda wa kukaa na mama yake.
Bi Wema aliichukulia siriasi kazi yake na isitoshe mshahara wake ulikuwa ukiingia kwa mwezi hivyo alipaswa kuzingatia wajibu wake na ndio maana Rufi alikuwa na huzuni kwani mama yake hushinda huko na hurudi kila ifikapo jioni.
Edna yeye mara baada ya kufikishwa nyumbani moja kwa moja aliingia mpaka ndani ya chumba cha Roma na kuoga , ijapokuwa walikuwa wamekosana lakini baada ya tukio Edna moyo wake ulishasahau kila kitu na sasa alitaka angalau kuanza upya ndio maana alimsubiria chumbani walale wote.
Sasa Edna alikaa zaidi ya nusu saa kumsubiri Roma aingie chumbani walale lakini hakuingia na ilimfanya Edna kuwa na wasiwasi na kutoka kwenda kumwangalia na alishangazwa mara baada ya kumkuta akiwa ameketi kwenye Sofa bila ya kufanya chochote akiwa kama mtu mwenye mawazo.
Aliweza kumuona mwanaume huyo kuwa katika hali ya usiriasi mno , hali ambayo hakuwa ameizoea na kumfanya kuwa na wasiwasi kwenye moyo wake.
“Huna usingizi?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kugeuza shingo yake kumwangalia.
“Tangulia kulala kwanza , kuna kitu nafikiria hivyo nahitaji utulivu kidogo”Aliongea Roma kwa sauti kavu.
“Bado una hasira na mimi?Najua nina hasira za haraka..”Aliongea kwa sauti ya chini kama vile ni mwenye kujutia kitendo cha kuondoka hapo nyumbani mpaka kuingia kwenye matatizo na kumfanya Roma kukumbuka yalitokea kwenye maisha yake ya nyuma.
“Usiwaze sana , ni swala ambao halihusiani na wewe, ni mimi mwenyewe”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutingisha kichwa licha ya kutoridhishwa na jibu lake na akarudi juu kulala na ndani ya dakika chache alipitiwa na usingizi.
Siku iliofuata Bi Wema saa kumi na mbili alishafika kwa ajili ya kuandaa kifungua kinywa na kufanya usafi na wakati akiwa bize ndio aliweza kumupona Edna akishuka kuja chini.
“Edna hatimae umerudi, nimeona taarifa ya habari leo asubuhi inayohusiana na nyumba ulionunua kushika moto na kuteketea , bora hata ulitoka mapema kabla ya janga hilo halijakukuta , siku nyingine usiwe mwepesi wa kuondoka baada ya kutokea migogoro sawa”Aliongea Bi Wema na Edna alijikuta akishangaa mara baada ya kusikia jumba lake lote kushika moto lakini ndio muda ambao alikumbuka kuhusu Roma kumwambia jeshi kitengo cha wachawi lingefuta aina yote ya ushahidi.
Hakujali zaidi kwamba amepoteza mabilionni ya pesa kununua nyumba hio wala kuomba fidia , alijiambia angetumia kiwanja hicho kujenga nyumba nyingine kwani ni eneo ambalo ni zuri zaidi.
Baada ya kusalimiana na Bi Wema alijikuta akianza kuangaza kichwa chake kulia na kushoto kumtafuta Roma , maana wakati alivyoamka aligundua hakupandisha kuja kulala.
“Bi Wema hujamuona Roma?”
“Sijamuona , nikajua bado amelala”
Alijibu Bi Wema na kumfanya Roma kushindwa kuzuia hisia zake kujisikia vibaya kidogo ijapokuwa Roma alimwambia hajakasirika kwa chochote lakini moyo wake ulikuwa mzito kuamini maneno yake na aliona bado Roma alikuwa amekasirika.
Kikawaida Roma asingetoka asubuhi bila ya kuaga na muda kama huo wanegejiandaa pamoja kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.
“Kwanini usimpigie simu na kumuuliza , huenda kuna jambo baya limetokea?”Alishauri Bi Wema na Edna aliinua simu yake na kutafuta namba yake kwa ajili ya kumpigia lakini alisita.
“Tusahau tu , pengine yupo bize sasa hivi , siwezi kumuongoza na kumzuia kufanya baadhi ya vitu muda wote”Aliongea huku akilazmisha tabasamu.
“Upo sahihi , huna haja ya kuwazia yupo wapi na kujisikia vibaya , isitoshe ndio kwanza mmepatana”
“Mmmh.. sawa Bi Wema, kesho nitaenda kumchukua Lanlan, naomba chakula kisiwe na mafuta sana, nimeambiwa anakula tu nyama huko aliko na sitaki aendelee hivyo kwani atakuwa bonge”
“Sawa hata mimi nimemkumbuka sana , Kaa kwanza upate kifungua kinywa kabla ya kwenda kazini”Aliongea na Edna aliketi na wakati anataka kupeleka kikombe mdomoni alijikuta akisita na kuanza kuandamwa na mawazo ya kujiuliza wapi alipo Roma , kwani hakuzoea kukaa mezani kama hivyo akiwa peke yake.
******
Upande mwingine nchini Rwanda alionekana Raisi Jeremy akiwa ameketi katika makazi yake ya mapumziko maarufu kama State Area D.
Raisi Jeremy alikuwa ameketi eneo la nje pembeni ya bwawa la kuvulia samaki huku pembeni yake kulikwa na mabwana wawili ambao walijitambulisha walikuwa wakitokea katika jamii ya kijini ya Panas.
Raisi Jeremy tokea anuse harufu ya hatari kutoka kwa aliekuwa mke wake Kizwe aliongeza ulinzi unaomzunguka.
Haikueleweka moja kwa moja alikuwa na uhusiano gani na jamii hio ya Panas lakini mwanaume aliefahamika kwa jina la Geni pamoja na Nix wote walikuwa ni walinzi wake, watu ambao walikuwa na uwezo wa kijini katika levo ya Nafsi.
Ijapokuwa Linda alikuwa na uwezo mkubwa wa kumlinda lakini hakumuamini sana kama alivyokuwa akiamini watu kutoka jamii ya Panas.
Kwanza hakueleweka raisi huyu ilikuwaje mpaka akawa na mahusiano ya karibu na jamii hio ambayo ilikuwa ikiogopwa sana katika ulimwngu wa wavuna nishati ya mbingu na ardhi.
“Huku duniani kuna hali mbaya sana ya kutuwezesha kuvuna nishati za mbingu na Ardhi, kuna vitu vingi vya kutamanisha ambavyo ni vya kupita na asilimia kubwa vinaharibu nguvu ya moyo”Aliongea jini kutoka Panasi aliefahamika kwa jina la Geni.
“Mkuu Geni kuvuna nishati ya mbingu na ardhi tafsiri yake kimafanikio ni kuweza kuendana na mazingira , haina haja ya kukazana sana”
“Haha.. ni kweli , ndio maana umekuwa raisi , upo sahihi kabisa”
“Haijalishi kama tutaendelea kuvuna nishati za mbingu hapa lakini Jeremy vipi kuhusu binti yako na yule mtoto wa familia ya Kweka , kama wataachana utakosa ushawishi mkubwa na taifa la Tanzania na mipango yetu kufeli”Aliongea bwana aliefahamika kwa jina la Nix.
“Msiwe na wasiwasi kabisa naendelea kuwafatilia kwa siri , ukweli ni kwamba Roma na binti yangu wameoana kwa zaidi ya mwaka sasa, lakini kwa hali ninayoona hawezi kumuacha Edna kwani matendo yake yanaeleza kila kitu , ugomvi wao wa hivi karibuni umenipa faida ya kuonana nae , lazima atajisikia vizuri nilienda kumuona”
“Kama ni hivyo basi ni vyema kusikia , yule mtoto sio mwepesi kabisa na hatujui ni mbinu gani ameweza kutumia katika mafunzo yake ya kijini , inashangaza kuona hata wanawake wake wameweza kufikia katika levo zile, kama utafanikisha kumfanya binti yako kukutambua kama baba moja kwa moja taifa la Tanzania litakuwa la wakwe zako , nadhani ikifikia hatua hio ujitahidi kujenga ukaribu na yule kijana kwani itatusaidia zaidi katika ukamilishaji wa mpango wetu hapa duniani”Aliongea Geisha na Raisi Jeremy alitingisha kichwa kuelewa.
********
Siku ilienda haraka haraka kwa mrembo Edna , huenda ni kutokana na hamu yake ya kurudi nyumbani mapema.
Edna mara baada ya kutoka kwenye lift moja kw amoja alipita eneo la mapokezi huku baadhi ya wafanyakazi wakimpa heshima yake kila alipopishana nao na Edna aliwarudishia kukubali salamu yake na kisha aliwapita akiwa na uso wa nusu kujali nusu kutojali..
Kipindi cha nyuma Edna angepanda Lift ambayo ingempeleka moja kwa moja mpaka eneo la maegesho ya magari lakini siku za hivi karibuni alikuwa akipitia eneo la mapokezi na kisha ndio aelekee kwenye maegesho ya magari.
Utaratibu huo ulitokana na uwezo wake wa akili kuimarika zaidi, kipindi cha nyuma hakupenda hata kukutana na wafanyakazi njiani lakini kipindi hicho mara baada ya kujua nini maana ya familia alipenda kupitia eneo la mapokezi ili angalau kusalimiana na wafanyakazi hata kwa kupungiana mikono tu.
Edna mwenyewe alikubali kabisa ile tabia yake ya kujitenga tenga mbali na watu ilikuwa ishaanza kubadilika mara baada ya kuoana na Roma.
Angalau kwa kipindi hicho wafanyakazi hawakuzidi kumuogopa na walipata ujasiri wa kumsalimia , lakini zamani hakuna ambaye alitamani kabisa hata kwenda ofisini kwake kutokana na kuhofia ukauzu wake.
Licha ya hivyo Edna hakujua tabia yake mpya ni nzuri au mbaya kama bosi wa kampuni lakini angalau kuona wafanyakazi wakimsalimia kwa tabasamu na matamanio kulimfanya kujihisi hisia za aina mbili , hisia za kufurahi na kutoridhika kwa wakati mmoja.
Uwezo wake uliomfikisha kuwa na pesa nyingi , umaarufu na kuwa msomi ilikuwa ni msingi mkubwa sana kwake kama mwanamke , alijihisi kujiamini na kujiona ni mwanamke ambaye amejitosheleza , wanawake wengine walitegmeea sana wanaume wao kuwasapoti kimaisha lakini yeye alijitegemea katika kila kitu.
Moja ya hisia kubwa ambayo ilimfanya kujisikia vizuri na kujiona kama mwanamke mwenye mafanikio ni pale alipoona wafanyakazi wengi walikuwa wakiendesha maisha yao kwa furaha kupitia kipato wanachopata kwa kufanya kazi katika kampuni yake, kutokana na kuajili watu wengi ilimpa nguvu hata pale anapopatwa na changamoto binafsi kuendelea kufanya kazi bila kuathirika.
Baada ya kuingia kwenye gari yake aliitoa katika jengo hilo na moja kwa moja aliingia katika barabara kuu na kukanyaga pedeli ya kuongezea spidi na kuzidi kuendesha kuingia katikati zaidi ya jiji, lakini licha ya kuwa makini na barabara akili yake ilikuwa ikimuwazia Roma tu , akiwa na shauku ya kujua kama tayari amekwisha kurudi nyumbani.
Siku nzima ya leo alitamani sana angalau kumpigia simu na kumuuliza ni wapi alipo , lakini alihofia kufanya hivyo kwa kudhania kwamba simu yake inaweza isipokelewe au isipatikane.
Kitendo cha kuwa na wasiwasi , hofu pamoja na huzuni vilimfanya kutoweza kuzuia hisia za mawazo yake, hisia alizokuwa nazo wiki iliopita wakati akiiishi mwenyewe baada ya kutoka nyumbani hakuwa nazo , pengine huenda aliamini Roma atakuja tu kwake na kumbembeleza ndio maana hakuwa na hofu .
Lakini wakati huo ambao Roma aliondoka bila kumuaga alihofia huenda mwanaume huyo amemkatia tamaa ndio maana akaondoka.
Alihisi maisha yake yamebadilika kwa viwango vkubwa sana , kwa mfano miaka kadhaa iliopita kitu ambacho alikuwa akifikiria muda wote akirudi ni namna ya kupandisha mauzo katika kampuni yake,yaani muda wote ilikuwa ni kampuni na hakudhania kama maisha yake yangeweza kubadilika na muda huo kuwazia familia.
Hakuweza hata kufahamu ameweza vipi kufika nyumbani , lakini alijishtukia ameendesha umbali mrefu mpaka kufika nje ya geti
Kwa namna ambavyo alikuwa mzuri ukijumlisha na mafanikio yake pengine huenda kama angeolewa na mwanaume wa kawaida angemnyenyekea sana , lakini mrembo Edna bahati mbaya mwanaume ambaye moyo wake umependa ndio huyo mwenye wanawake kibao na tena haonyeshi kujali kabisa.
Kwa mtu wa nje huenda angeuliza mwanamke mrembo kama Edna kampendea nini mwanaume kicheche kama Roma. Lakini mwisho wa siku mwenye kujiuliza maswali angekosa majibu sahihi na pengine angeweza kupata maswali zaidi kama angekutana na Rose , Rufi , Amina , Najma , Mage ,Dorisi na wengineo.
Edna mara baada ya kuingia ndani moja kwa moja alichungulia chumbani kwa Roma na kukagua mazingira haraka haraka na hakuona dalili ya mtu na alijikuta huzuni ikimwandama , alienda na chumbani kwake kuangalia lakini hakukuwa na dalili na mwisho kabisa aliamua kushuka mpaka chini akiwa bado hajabadilisha mavazi aliotoka nayo kazini.
Baada ya kufika sebuleni alikuwa kama vile ni mgeni amefika sasa anatafuta wenyeji..
Bi Wema aliekuwa akishuka kutoka juu alishangazwa na mwonekano wa Edna na kujiuliza ni kitu gani anatafuta.
“Miss , umerudi saaa ngapi , kwanini unaonekana kama kuna kitu unatafuta?”Aliuliza Bi Wema kwa upole na Edna mara baada ya kumwangalia Bi Wema kwa dakika kadhaa alijikuta akikosa ujasiri na machozi yalianza kumtoka palepale na kuanza kulia kwa kwikwi huku akiwa ameegemeza kchwa chake katika kifua cha Bi Wema.
“Edna mwanangu una tatizo gani , kuna mtu yoyote kakuchokoza,nini kimekupata , kwanini unalia?”Aliuliza Bi Wema ambaye alikuwa kwenye mshituko na wasiwasi.
“Bi Wema, Roma hanitaki tena ..”Aliongea huku akifuta machozi na kumfanya Bi Wema kukosa neno la kusema kwani aliishia kushangaa ,
“Bado ana hasira na mimi , nadhani ananiona nina kiburi na simsikilizi hivyo kaamua kunipotezea ..”Aliongea huku akiendelea kulia kwa kwikwi
“Miss hakuna jambo kama hilo”Aijaribu kufariji Bi Wema.
“Lipo Bi Wema, angalia sasa tokea asubuhi haonekani , anaoneana hataki kuoniona tena ,, na ameenda kujificha..”
“Unamaanisha nini haonekani , si ndio amerudi sasa hivi tu”Aliongea Bi Wema huku akiwa ni mwenye mshangao na kauli yake ilimfanya Edna kuacha kulia na kumwangalia Bi Wema kama vile amemsikia vibaya.
“Amerudi!!”
“Ndio , na huo mfuko umejaa nguo zake chafu na sijui hata ametokea wapi maana zimejaa matope , ni kama vile alilala porini”Aliongea Bi Wema na kisha alifungua ule mfuko mweusi wa plastic na kumuonyesha Edna.
Baada ya kuangalia na kuona kweli ni nguo za Roma zilizochafuka alijikuta palepale kuanza kushikwa na aibu mbele ya Bi Wema.
“Mr atakuwa anaoga sasa hivi , usiwe na wasiwasi”Aliongea Bi Wema huku akimgusa mabega yake.
Edna alijikuta akiangalia sakafu bila kuinua uso wake , alitamani ardhi itengeneze shimo na atumbukie kutokana na aibu aliokuwa nayo mbele ya Bi Wema , alianza kujilaumu kwanini hakuthibitisha kwanza.
Likija swala la mahusiano akili ya mwanamke haifanyi kazi kisawa sawa na Edna aliweza kuamini siku hio , mwanzoni alikuwa akipinga lakini mara baada ya kuwa katika hali hio aliamini moja kwa moja na kile kilichokuwa kikisemwa.
“Basi Bi Wema… nadhani napaswa kwenda juu”Aliongea Edna kiaibu na hakutaka kusubiri jibu kutoka kwa Bi Wema kwani aliona aibu kumwangalia usoni na palepale alikimbia nduki kupandisha ngazi na kumfanya Bi Wema awe na wasiwasi kwani aliogopa anaweza kuteleza na kudondoka.




SEHEMU YA 557.
Bi Wema mara baada ya kusikia mlango ukifungwa kwa juu alijikuta akivuta pumzi na kuzishusha na akachukua mfuko wake na kutembea mpaka chumba maalumu cha kufulia na kuziingiza kwenye mashine ya kufulia.
Baada ya kumaliza na kazi hio ndogo alitoka kimya kimya kurudi sebuleni na kusogelea shelfu maalumu ya kuwekea picha.
Bi Wema aliinua picha iliokuwa kwenye fremu , ilikuwa ni picha ambayo Edna aikuwa mdogo akiwa amebebwa na Bibi yake , pembeni alikuwepo Mama yake Edna aitwae Raheli , Bi Wema pamoja na Mzee Adebayo ambaye yeye pekee alionekana ni mwenye kununa kutokana na kukosa furaha.
“Madam kabla hujaondoka katika huu ulimwengu uliniambia niendelee kumlea Edna mpaka atakapokuwa mkubwa , niliamini akishaolewa atakuwa tayari mkubwa na mwenye kujitegemea lakini mpaka sasa bado namuona ni kama mtoto .. bado ni mwenye kulia lia kama alivyokuwa mdogo..”Aliongea Bi Wema huku akiweka tabasamu ambalo lilishiria huzuni.
Upande mwingine ndani ya chumba chake Edna alikuwa akitembea kutoka dirishani hadi mlangoni na kisha anarudi tena dirishani , muonekano wake ulikuwa ni kama wa msichana ambaye hajavunja ungo ambaye yupo katika hali ya aibu.
Kutokana na kioja alichofanya hakupata ujasiri hata wa kurudi tena sebuleni na kuonana na Bi Wema tena , yeye mwenyewe hakumbuki ni lini aliweza kulia kitoto namna hio bila sababu ya msngi.
Edna alijikuta akiwa na aibu na alitamani arudishe muda nyuma na iwe ni wakati ambao ndio anatoka kwenye gari na kuingia ndani , lakini uwezo huo hakuwa nao ziadi ya kuzidi kuficha sura yake na mikono.“Haya yote yananitokea kwasababu ya huyu mpuuzi Roma”Alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira huku akimlaani Roma lakini muda huo huo mlango wa chumba chake uligongwa.
Edna alijua lazima atakuwa ni Bi Wema hivyo alivuta pumzi nyigi na kujituliza na kujiambia Edna tulia na hili litapita na kisha akasogelea mlango na kwenda kuufungua.
Lakini mara baada ya kufngua mlango alikutana na uso wa Roma , ambaye amekwisha kumaliza kuoga na muda huo alikuwa amevalia tisheti.
Edna alijikuta akianza kumkagua mwanaume huyo kwanzia kichwani mpaka miguunni na kumfanya Roma acheke namna ambavyo anakaguliwa.
“My Dear Edna , kwanini uko hivyo , mbona kama ulikuwa ukilia , kwanini macho yako ni mekundu hivyo?”
“Sikuwa nikilia , niliingiwa na mchanga machoni wakati nikitoka kwenye gari”Alitafuta sababu yoyote ya kudanganya lakini tukio alilolifanya bado lilimfanya kukosa kujiamini.
“Kuna kitu unataka?”Alijitutumua na kuuliza huku akiwa na hisia mchanganyiko.
“Ndio kuna kitu nataka , nimemuambia Bi Wema akimaliza arudi tu nyumbani maana ninakutoa Dinner , kwasababu Lanlan anarudi kesho nadhani sio mbaya kutumia muda huu peke yetu”
Edna alijikuta akishangaa , alikumbuka kabisa alionekana kwenye mawazo jana usiku , kwanin ameweza kurejea katika hali yake ya kawaida ghafla tu na sasa anataka kwenda nae kupata chakula cha usiku.
Ijapokuwa sio jambo la kushangaza mume na mke kutoka kwa ajili ya chakula cha usiku lakini ‘timing’ haikukaa vizuri.
“Kuna chochote unataka kuongea?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kubadilika na kutabasamu kidogo.
“Sina.. usifikirie sana ..”
“Tatizo mwonekano wako unaonyesha kama kuna kitu unanificha”Alongea akionyesha kutoridhika.
“Tutaongea tukiwa njiani , hatuwezi kuendelea kusimama hapa , muda unaenda”
Ukweli ni kwamba Edna alikuwa akikumbuka siku ile ambayo Roma alimpeleka katika lile jengo la hoteli na kutaka waachane, kutokana na kile kilichotokea jana yake alijuwa tu kuna jambo ambalo Roma anataka kumwambia , huenda mwanaume huyo ameshafanya maamuzi ya kuachana nae na anataka kwenda kuongea nae katika sehemu tulivu ili waachane kistaarabu.
Kitendo chake cha kukosa kujiamini na kujishutikia kilimfanya kujishangaa hata yeye mwenyewe lakini Roma alijitahidi kuonekana wa kawaida.
“Darling , usifikirie sana nishafanya booking , tondoke”Aliongea Roma huku akionyesha wasiwasi kwani ni kama Edna anataka kukataa.
Edna aliamua kuvuta pumzi na kuzishusha na kujiambia atakubaliana na kila maamuzi yake na isitoshe ndoa hailazimishwi, yaani alikuwa ashasahau kama siku zilizopita yeye ndio alietaka kuvunja ndoa tena kwa jeuri kabisa.
Lakini haikushangaza kwani ni mwanamke, na ni tabia ya kawaida kwa mwanamke likija swala la hisia kuwa mbinafsi.
“Sawa , lakini je ni mbali , napaswa kuvaa vizuri zaidi?”Aliuliza Edna kinyonge.
“Sio mbali tutafika mapema tu , tayari unaonekana mrembo na inatosha”Aliongea Roma akiwa ni mwenye tabasamu na kumfanya Edna aone huenda anavyowaza ni tofauti.
Baada ya Edna kujiweka sawa kidogo waliweza kutoka pamoja na baada ya kufika eneo la nje Edna alitaka kuelekea kwenye maegesho ya magari lakini Roma alimvuta kwake.
“Hatutotumia gari , kwasababbu hatuwezi fika kwa gari”
“Kwanini?”Aliuliza akiwa katika mshangao.
“Kwasababu tunaenda nje ya nchi kwa ajili ya chakula cha usiku”Aliongea huku akimkonyeza na Edna alieshangaa kabla hata hajatoa neno alijikuta akibebwa juu juu kama mtoto.
“Hey! , unafanya nini , wapi tunaenda?”Aliongea huku akishikilia vizuri shingo yake akiogopa kudondoka.
“Utajua tukishafika nishikilie vizuri , nitapunguza spidi lakini bado nitakuwa na haraka ukidondoka angani halitakuwa jambo zuri”Baada ya kumaliza kuongea maneno yale palepale walipotea kijini.
Ilikua mara yake ya kwanza kusafiri umbali mrefu kwa njia ya kijini , aliweza kuona nyota na mwezi kwa urahisi kabisa , ijapokuwa upepo upepo ulikuwa mkali lakini kwasababu ya kujikinga na ngao ya kichawi hawakuathirika..
Baada ya kugeuza macho yake na kuangalia chini alijikuta akishikwa na mshangao , kwani ni kama vile yupo katika sayari nyingine kabisa kutokana na mataa yaliokuwa yakionekana chini yake , na kadri alivyokuwa akishuka chini ndio ambavyo alivutiwa na mandhari.
“Hapa ni wapi??”Aliuliza Edna , hisia zake zilimwambia kabisa hapo ni wapi lakini kutoana na mshangao wake hakutaka kuamini.
“Hapa ni Dubai”Aliongea Roma na kumfanya Edna kukosa neno , ni kweli sehemu ilikuwa ni Dubai kutokana na kwamba haikuwa mara yake ya kwanza kufika , lakini hakuamini kama wametumia dakika chache kutoka Tanzania kuja Dubai tena kwa ajili ya chakula cha usiku.
“Tupo hapa kwa ajili ya chakula lakini nina surprise nyingine”Aliongea Roma.
Muda huo licha ya kwamba jiji la Dubai lilikuwa limechangamka kutokana na kuwa jiji la kibiashara , lakini eneo ambalo walikuwepo halikuwa na watu wengi kwani ni eneo ambalo limejitenga na mjini.
Mbele yao kulikuwa na jumba kubwa ambalo limejengwa kwa mtindo wa tamaduni za kiarabu, lilikuwa ni jumba la kifahari ambalo limezungukwa na bustani nzuri sana na Edna licha ya kwamba ametembelea mahoteli mengi ya kisasa na kuishi , lakini jumba binafsi kama hilo la kitajiri hakuwahi kutembelea , sio kama hakuwa na uwezo huo lakini kutokana na miasha yake kutojihusisha na kupenda ‘bata’ , huenda ndio maana sehemu nzuri kama hio ilikuwa ni ya kipekee kwake.
“Unajaribu kufanya nini?”Aliuliza Edna lakini Roma hakumjibu zaidi ya kumshikilia mkono na kusogelea jumba ambalo liko mbele yao , jumba ambalo limezingirwa na miti midogo midogo ya kupendeza.
Baada ya kukaribia na kupokelewa na miti maalumu ya maua Roma alisimama na kumfanya Edna kushangaa na kumuuliza kama ndio washafika lakini Roma alimpa jibu tofauti.
“Miss Edna please close your eyes and wait for me to count untill three then open them , alright?”Aliongea Roma kwa lugha ya kingereza akiwambia kwamba afumbe macho yake na amruhusu kuhesabu mpaka tatu ndio ayafumbue.
Edna alikuwa ni mwenye maswali mengi , lakini alishia kuyafumba ili kujua nini kinakwenda kutokea.
“Moja .. mbili..tatu”Baada ya kusema tatu alifumbua macho yake na kuangalia lakini alijikuta akiwa katika hali ya mshangao mara baada ya kuona kitu kilicho mbele yake na kuishia kuziba mdomo, ukiachana na namna ambavyo sehemu hio imepambwa na miti midogo midogo iliofungwa taa za rangi na kupendeza , lakini neno One year down , a lifetime to Go, Celebrating our marriage -HAPPY ONE YEAR MARRIAGE ANNIVERSALLY lilimfanya kumbukumbu zake kurudi nyuma.
Alijkuta palepale akikumbuka siku hio ndio siku ambayo alifunga nae ndoa ya Bomani na Roma.
Alishangaa maana hakuwa akikumbuka chochote kabisa siku hio. Alijiuliza inamaana kupotea kwake siku nzima alikuja kuandaa kitu kama hicho?
Edna moyo wake uliliainika kwa kitendo hicho , alimdhania vibaya Roma kama anaenda kumuacha kumbe alikuwa akiandaa surprise kwa ajili yake.
TUTAENDELEA KITAMBO KIDOGO.
Hatariii
 
M
Na mkilipia Mnaachwa njia panda maana sisi tunaolipia kule whatsapp tunagombana naye kila siku, stori haijaisha na mwendolezo ni wa kusuasua jamaa hakosi sababu na akitoa ahadi hatekelezi kamwe.
So ukitoa buku 6 utapata vipande kadhaa then ukitufikia tulipo unaungana nasi kwenye kuipita dhikimh kama I hvyo mbna hatari sasa
 
Na mkilipia Mnaachwa njia panda maana sisi tunaolipia kule whatsapp tunagombana naye kila siku, stori haijaisha na mwendolezo ni wa kusuasua jamaa hakosi sababu na akitoa ahadi hatekelezi kamwe.
So ukitoa buku 6 utapata vipande kadhaa then ukitufikia tulipo unaungana nasi kwenye kuipita dhiki.
Kiukweli hata mimi nlipata taabu kidg mwanzon lakn toka nmeelewa lengo/dhamira ya mwandishi, imenibd niwe tu mwelew Bila kuchukia Bila kinyongo
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI :SINGANOJR.
WATSAPP: 0687151346.

SEHEMU YA 605.
Baiju miguu yake katika vigoti ililelegea palepale mara baada ya kujua mwanamke ambaye hakuwa amemtambua ni Aoiline mkuu wake.
“Bwana wangu , sikujua kama upo hapa tafadhari naomba unisamehe”Aliongea kwa kutetemeka huku akiwa amemsujudia chini , hakuwa tena yule mwenye kiburi.
Aoiline aliachana na Roma na kisha alimsogelea Baiju kwa hatua hafifu huku uso wake ukiwa ni ule wa kichokozi , hakuonyesha kabisa kuwa na hasira.
“Baiju nimepewa ripoti kwamba unakusanya kiwango kikubwa cha mawe ya kiroho kupitia Madanguro , ukiichukulia faida kwa mimi kutokuwa makini na maswala hayo , inaonekana umeweza kuteka majini wanawake kwa tamaa zako”
“Bwana wangu wananisingizia tu , waliochini yangu ndio ambao wamefanya kosa hilo kwa kunipatia rushwa , nitahakikisha nina wahukumu vifo nikirudi”Aliongea Baiju huku akionekana kutengeneza kisingizio.
“Hata mimi naona , kwa hio unasema mimi ndio mkosaji hapa kwa kusingizia si ndio?”Aliongea huku kitingishcha kichwa chake kama mtu ambaye anajaribu kumwelewa.
Baiju alitaka kutingisha kichwa kujaribu kujitetea kwamba hakupaswa kumbebesha lawama zote lakini hakuweza kufanya chochote wala kukubali kama ana kosa na uso wake ulibadilika rangi na kuwa mwekundu kutokana na presha ambayo ilikuwa ikijiandaa kumkumba.
“Umekuwa na mimi kwa zaidi ya miaka mia mbili , nimekufanya uwe Bwana wa mji wangu wa Wingu Jeupe na ukapokea tani na tani za mawe ya kiroho kutoka katika maghala ya mji na watu wengi wakakuonea wivu lakini bado ukaamua kukusanya zaidi Mawe ya kiroho kupitiia Danguro , Ingekuwa ni sawa kama tu ungekuwa ukidanganya hao ambao walikuwa wakipenda kufanya kazi chini yako lakini ukathubutu kuteka wale ambao wanajaribu kupita katika mji wetu , hivi unadhani mimi siwezi kuishi bila wewe , unafikiri mimi ni mwepesi kudanganywa?”
Jasho la baridi lilimtoka Baiju na kuloanisha nguo zake na aliishia kutingisha kichwa chake akiwa amekiinamisha chini akishindwa hata kumwangalia Aoiline.
“Bwana wangu, Sikuwa nikifikiri sawa sawa , tafadhari naomba unisamehe kwa dhambi nilizoafanya kwa zaidi ya karne moja”
“Sawa”Aliongea huku akikusanya nguo za mkono wake na kutingisha kichwa.
“Itakuwa ni ukatili kama sitoweza kukupa nafasi , nitakusamehe kwa kuwateka wasichana wa kijini nyuma ya mgongo wangu”Aliongea na kumfanya Baiju kufurahiswa na maneno yake huku akitaka kuanza kusujudu kwa mara nyingine lakini Aoiline alimkatisha.
“Lakini hata hivyo napaswa kukuadhibu kwa jambo moja”
“Ah..!”Alitoa sauti huku sura yake akipeleka chini kwa mara nyingine akiwa kama amechanganyikiwa.
“Watu wako hususani Huji wameniteka siku ya leo na wakaniingiza kwenye kiroba ,… ningekuwa mrembo wa kukuingizia hela ndani ya Danguro leo kama sio Mr Roma kunisaidia”
Hio ilikuwa ni taarifa mbaya sana kwa Baiju na sasa aliweza kuelewa kwanini Aoiline alibadilisha mwonekanno wake , kila kitu kilikuwa ni mtego wa kumkamata na ufisadi wake.
Ingekuwa afadhari kama angekamata wanawake wengine lakini sasa alikuwa amemsaliti hata Bwana wake hakukuwa na sababu ya kuachwa hai.
Dakika hio alivyojaribu kuunganisha Dot katika akili yake , Baiju alijiambia hakukuwa na faida yoyote ya yeye kuomba kusamehewa au kujitetea na anapaswa kufanya kitu chochote kile ili kuweza kukimbia na kutoka katika hio miliki, alijiambia kama ataweza kufika katika Korongo la Joka , Mfalme wa Majoka lazima angemlinda kwani alikuwa ni jini mwenye uwezo mkubwa wa kimapambano katika levo ya nane.
Baada ya kupatwa na mawazo hayo hakutaka tena kuchelewa, palepale aliita kwa hisia ndege wake mweupe kwa ajili ya kumshambulia Aioline .
Ndege mweupe na yeye akasikia kuitwa na mkuu wake , na palepale lilitoa kilio kikubwa cha juu huku likipiga piga mabawa yake kumsogelea Aoiline moja kwa moja.
Aoline hakuonakana yule mpole tena kwani alibadilika na alikuwa na uso wa kikauzu usio kuwa wa kawaida na kwa Roma ni kama alikuwa akimuona Edna party two, ilikuwa ni kama vile hewa iliokuwa ikimzunguka imeganda.
“Wewe mjinga , unathubutu vipi kujaribu kunipinga mimi?”Aliongea kwa nguvu na palepale kulitokea mwanga kama nguzo mbili nyuma ya gauni lake na nguo moja ya mwanga ilimshikilia yule ndege kwa kumfunga funga.
Roma aliangalia kwa ukaribu zile nguzo zilizokaa kama kamba kamba na palepale ndipo alipogundua ni mikia na pale ndipo alipojihakikishia kweli huyo ni jini ambaye alikuwa akiitwa Mbweha wa mikia tisa.
Mikia yake ilikuwa ni mirefu mno na haikuwa ya kawaida , ilikuwa ni kama boriti au nguzo.
Yule ndege licha ya Roma kumuona mkubwa lakini mbele ya ile mikia alionekana kuwa mdogo mno kwani alikamatwa na akawa hafurukuti kabisa.
Ndege yule alianza kutapa tapa kama vile kuku ambaye anapoteza uhai na ndani ya dakika tu damu zilionekana kuruka juu , ilionekana alikuwa amekamuliwa kwa kiwango kikubwa kiasi cha viungo vyake kuharibika na hata manyonya yake yalianza kusambaa angani.
Sophia alishindwa kabisa kuangalia kitendo kile lakini kwa Roma alikuwa akiona kitu kile kama hasara kwani yule ndege alimpenda na kujiambia angalau kabla ya kutoka katika ulimwengu huo amwendeshe hata mara moja.
Wakati Aoiline akidili na ndege Baiju alikuwa ashakimbia kwa kupaa umbali mrefu kidogo , lakini bahati mbaya kwake ni kwamba mkia mwingine wa Aoiline ulikuwa ukimfukuzia na ulikuwa ukiongezeka urefu kadri alivyokuwa akikimbia kwenda mbali..
Roma ni jambo lingine ambalo lilimshangaza kwani hakuamini kama mkia huo ungekuwa na uwezo wa kuongezeka urefu na kusafiri umbali mrefu tena kwa haraka sana.
Ni kufumba na kufumbua tu Baiju alipigwa na mkia ule kwa nguvu mara baada ya kusogelewa na alijikuta akitema damu kutokana na kichapo.
“Rudi”
Ule mkia ulimviringa Baiju kufumba na kufumbua tu na kumvuta nyuma na kisha kumrudisha ardhini mbele ya Aoiline na dakika ileile ulipotea katika macho yao , ilikuwa ni kama vile haukuonekana kwani licha ya urefu wake ulirudi ndani ya mwili wa Aoiline kwa spidi kubwa mno.
Roma alijikuta akitengeneza sauti kupitia ulimi wake , Roma alikuwa akijua mwanamke huyo alikuwa na mikia tisa na ameonyesha mwili tu na kilichotokea sio cha kawaida.
Pengine siraha yake kubwa ni hio mikia na kama atapambana nae basi atakuwa ni moja ya washindani hatari ambao ashawahi kukutana nao kwani angekuwa na uwezo wa kujikinga na wakati huo huo akishambulia.
Kwa spidi yake hio na nguvu zake za kijini aliona kabisa hata yeye hakuwa akimuweza kimapambano kabisa, na hakutaka kujiona yeye ni mkubwa zaidi hivyo alikubali Aoiline alikuwa ni levo ya juu kuliko yeye.
Baiju alijikuta amepauka mno kwa woga , alikuwa tyari amekwisha kujikatia tamaa katika kukimbia na aliishia kusujudu kadri awezavyo na kujaribu kuomba kuhurumiwa , lakini licha ya kujitetea huko kulifanya tabasamu la kikatili la Aoiline kuzidi kutisha.
“Bwana nimetenda dhambi zidi yako , unaweza kuondoa nguvu zangu zote za kijini na kunigeuza kuwa mnyama lakini tafadhari naomba usinie , naomba unisamehe”
“Siku zote nilikuwa mpole sana kwa viongozi kama nyie , kwanini nikuondolee nguvu zako za kijini ?,Baiju je utanisaidia jambo moja?”
“I’m willing to redeem myself!”Aliongea
“Great”
Kufumba na kufumbua Aoline alikuwa nyuma ya Baiju na kuishika shingo yake na palepale mkandamizo wa hali ya juu ulianza kumtoka.
“Sophia kuwa makini”
Aliongea Roma na palepale alimsogelea Sophia na kumzingira na nguvu ya kijini kwani tayari ashajua ni nini kinachokwenda kutokea .
Aoiline alikuwa akipanga kumkandamiza na nguvu yake ili kuweza kutawala uwezo wake hivyo kutokana na mkandamizio mkubwa ambao alikuwa akijaribu kutoa Aoiline ilikuwa ngumu kwa Sophia kuweza kuhimili na angetema damu kwani mara nyingi inakuwa kama vile ni mlipoko wa bomu.
Ilikuwa ni kama vile mwanamke huyo mrembo amegeuka na kuwa mungu wa huo ulimwengu kwani macho yake yalikuwa yamebadilika kabisa na kile kiini cheusi kilikuwa kimempotea kwenye macho na jicho likabakia jeupe kama vile ni barafu.
Dakika ileile Aoiline alifumbua mdomo wake na meno yake yaliongezeka urefu kama Vampire na kuyapelekea katika shingo ya Baiju na kumng’ata.
Baiju sura yake mwanzo ilikuwa imepinda kutokana na mkandamizo mkubwa lakini mara baada ya kung’atwa mwili wake ulibonyea palepale .
Sophia aliekuwa nyuma ya Roma hakuweza kupata ujasiri wa kuangalia kile kinachotokea kwani iliogopesha , upande wa Roma alikuwa katika bumbuwazi kwa kile kinachotokea
Alijiambia swala la kunyonya damu ni la kawaida kwani kilichofanyika ni kujaribu kunyonya nguvu za lile jini lakini hakutegemea mwanamke mrembo kama huyo ndio ambaye anafanya kitendo hicho.
Kile kitendo huenda angekuwa ni binadamu wa kawaida ambaye anaangalia angepoteza fahamu palepale , Sophia kwa kiasi hakuwa wa kawaida kwani alikuwa ashaishi na Roma na kuzoea baadhi ya mambo ya ajabu ya namna hio.
Dakika chache tu mwili wa Baiju ulibadilika na Akawa Kunguru mkubwa ambaye ameoza huku mifupa yake ikianza kuonekana na Aoiline alimsukumia mbali maiti ile ya Kunguru na kuanza kuilamba midomo yake kwa damu zilizokuwa pembeni, alikuwa ni kama vile analamba asali kwa jinsi alivyonekana kufurahia.
Baada ya mkandamizo wa hewa kuondoka ndio aligeuza macho yake kwa Roma huku akiachia mkandamizo wa kawaida kama vile alikuwa akijaribu kumuogopesha Roma.
“Mr Roma huna haja ya kuniangalia hivyo na kuniona kama mchawi mnyonya damu , nimefanya hivi kwa zaidi ya miaka elfu moja , hatima yake ilikuwa ni kifo hata hivyo , kwanini nisimtumie kama kirutubisho , Au naongea uongo?”
Roma alikuwa akianza kuwa na wasiwasi juu yake , hata kama alionekana kuwa mrembo wa kuita lakini matendo yake na uwezo wake wa kijini ulimpa mashaka makubwa na kushindwa kuijua nia yake halisi juu yao.
“Nadhani tunapaswa kuendelea na safari yetu maana ushamaliza maswala yako”Aliongea Roma na kisha akamwangaliaSophia akimwambia waanze safari ya kuondoka hapo haraka iwezekanayvyo.
Sophia hakuwa na shida na alikubali kuondoka , yule Aoiline ambaye alitaka kuwa nae karibu hakumtaka tena maana alikuwa akitisha.
Aoiline palepale alitoa tabasamu la kifedhuli na kufumba na kufumbua alikuwa mbele ya Roma na kuwazuia wasiondoke.
“Mr Roma tupo karibu na jumba langu la kimalkia kwanini msiende kupunzima kwa muda”
“Hakuna shida sana juu ya hilo , safari yetu ni kuelekea kando ya ziwa la Mbingu”Aliongea Roma huku akijaribu kutafuta upenyo wa kumpita.
“Hata kama nimekudanganya kuhusu ubini wangu , lakini sikuwa nikidanganya kuhusu mambo mengine , kuna zaidi ya wiki tatu mpaka kwa mnara kufunguka , kwenda huko ni kupoteza muda wako tu”
“Mimi naweza kutokuwa na akili kama wewe lakini siwezi kuwa kichaa kabisa na kuanza kupigana na mtu kama wewe ambaye umeishi maisha marefu , lazima una nia nyingine hivyo acha kuzunguka zunguka”Aliongea Roma mpaka hapo alijua mwanamke huyo hakuwa na nia ya kuwaruhusu waondoke kirahisi.
“Mr Roma sisi majini tunaweza kufikiria pia na sio wanafiki kama binadamu , mosi nimekuja huku kwasababu nimesikia taarifa kutoka kwa watu wangu ndio maana nimekuja kujionea mwenyewekama ni kweli Baiju alikuwa akitenda mambo ya kifisadi, kitu kingine pia waliniambia kwamba kuna binadamu wageni ambao wameweza kufika katika ulimwengu wetu , Watu watatu ambao ulipigana nao katika msitu wamekuongelea vibaya sana lakini sikuwachukulia siriasi na sina nia ya kuwalipizia kisasi kwa uliowafanyia”
“Lakini bado siamini mtu kama wewe unaweza tu kunialika kwako kwa ajili ya kupumzika”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu.
“Nimeongea vya kutosha je tunaongozana au hatuongozani”
“Hatuongozani”Aliongea Roma kwa sauti huku akitingisha kichwa chake kukataa kusisitizia msimamo wake.
Aoiline alitoa pumzi ya kukatishwa tamaa huku akimwangalia Roma kwa masikito.
“Kama hutaki kuongozana na mimi basi sina budi kukulazimisha”Baada ya kuongea hivyo msisimko aliokuwa ukitoa ulibadilika kabisa na macho yake hayakuwa mazuri tena kwani yalibadilika na kuwa ya chuki.
Roma alishindwa kuelewa chuki yake inatokana na nini , aliajiambia kwanini kumbadilikia namna hio ndani ya dakika tu wakati hajamchokoza.
Roma palepale alimsukumia mbali Sophia ili tu asije akapata madhara na baada ya kumuona ameenda mbali zaidi aliita nguvu zake za kijini ili kuweza kuhimiri mkandamizio uliokuwa ukitolewa na Aoiline.
Dakika hio hio Aoiline muonekano wake wa kirembo ulikuwa umebadilika na kuwa kama vile ni jitu kubwa la kutawala , macho yake yalikuwa ni kama yale ya kutaka mtu yoyote anaemuona kumsujudia.
Roma hakutaka kumruuhusu msichana kama huyo kuendelea kumkandamiza , hakutaka tena kulinda nguvu yake ya kijini isipotee na alimsogelea Aoiline kwa nguvu zake zote.
Mpira wa moto wa bluu ulionekana katika mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto ulitegneneza maji ya kiroho ya kuosha uovu.
Aoiline alitoa tabasamu la kejeli kama vile alikuwa akidharau kile anachotaka kufanya.
Awamu hio hakutoa mikia yake bali nguo yake ilianza kutengeneza kamba kama Ribbon kutoka kwenye nguo yake ya hariri akidhamiria kupigana na hio .
Roma hakutaka kujali mbinu yake ambayo anataka kutumia na dhamira yake ilikuwa ni kutaka kumchapa na maji ya kiroho akiamini hata tone lake linaweza kumletea madhara.
Lakini nguo yake ile haikuwa nguo kama nguo kwani ilikuwa ikidhalisha kiwango kikubwa cha nishaiti isiokuwa ya kawaida na kadri ilivyokuwa ikipepea kuelekea upande wa Roma ni kama ilikuwa ikimzuia asimfikie.
Roma alijikuta akishangazwa na uwezo wake , aliweza kujua mtu anaepambana nae ndio yupo katika levo ya juu kabisa ya daraja la tisa la mafunzo ya kijini ya kuita pepo.
Kutokana na mkandamizio wake kuwa mkubwa Roma alijikuta akiamini huenda hata Athena akashindwa kabisa kudili nae.
Kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao mpizani wake Roma alianza kupoteza pambano mapema kabla hata hajaanza kushambulia kwani alishindwa hata kubadilisha nguvu zake kuleta faida katika kushambulia.
Aoiline hakuonyesha kutumia nguvu yoyote alikuwa ni kama vile anacheza na zile kamba za nguo zake za hariri na alianza kuzifanya zipeperuke hewani na zilikuwa zikitoa nguvu kubwa mno .
Roma palepale aliweza kufikiria huenda mbinu yake haikuwa ikitegemea muundo au nguvu bali alikuwa akitegemea akili yake na ufahamu . mpaka hapo alijua kwamba ulimwengu huo wenyewe ulikuwa kikwazo kwake hivyo hakuwa na namna ya kumshinda.



SEHEMU YA 606.
“Mr Roma huu ni ushauri wangu kwako , nifuate mwenyewe kwa hiari yako au endelea kuwa kiburi na nikufunge na kuondoka na wewe”Aliongea Aoiline.
“Sina jinsi tena”Aliongea Roma katika nafsi yake , katika maisha yake hakupenda kushindwa kirahisi.
Palepale Cauldron iliweza kutokeza na kuanza kutoa moshi kiasi cha kusababisha anga kubadilika huku msisimko wa ajabu kuzingira eneo lote la msitu unaowazunguka na kufanya hata baadhi ya ndege kukimbia.
“Pumbavu kabisa , kwanini una tumia Cauldron?”
Aoiline alikuwa ashaishi muda mrefu sana , muda mfupi alikuwa akijaribu kumuita ‘Mr Roma’ kama kumchokoza lakini mara baada ya kuona dhana hio ya hatari hakutaka tena kumchukulia mwepesi.
“Bado tu unataka kupigana licha ya kuonyesha kufahamu hiki ni nini?”Roma alitumia kiasi kikubwa cha nguvu ya kijini akijiandaa kwa ajili ya kukipa nafasi kumshambulia Aoiline , lakini Aoiline alianza kutoa cheko la hali ya juu.
“Najua hilo ni tanuru la maafa na ni sehemu ya Dhana za kijini ambazo zijashawahi kuwepo lakini licha ya nguvu yake kubwa huwezi kukitumia katika nguvu yake yote kutokana na levo yako kuwa chini , ndio kwanza umeipita Dhiki unadhani unaweza kunishambulia kwa uwezo wako huo , fuata ushauri wangu kama mkubwa kwako usikitumie maana roho ya mnyama iliopo ndani yake itaishia kutawala mwili wako , Roho yake iliopo ndani haiwezi kufa na hata wale miungu hawana uwezo wa kuihimili , kwa haraka haraka naamini Roho ya mnyama hio imekuchagua lakini kama utaendeelea kukitumia ukiwa na nguvu ndogo utaishia kuwa shushu, utakuwa sio binadamu tena na wakati huo ukifikia utakuwa umechelewa kwani huwezi kurudi kuwa wewe tena”Roma alikuwa katika mshangao licha ya kwamba hakuonyesha katika uso wake, alijiuliza je ni kweli chungu hicho kinaweza kumtawala , maneno ya Aoiline yalimfanya moja kwa moja kuwa na moyo mzito.
Aoiline palepale zile kamba za hariri yake zilipotea na kisha akamsogelea Roma kwa mapozi.
“Huwezi kunishinda hata kidogo , Sijawahi kukutana na mshindani wa ukweli katika ulimwengu huu , ijapokuwa uwezo wangu sio wote kutokana na mazingira lakini gepu letu ni kubwa sana , nimekuacha mbali na sina haja ya kutumia uwezo wangu wote kukushinda ni kidogo tu”Roma alijikuta akikunja ngumi yake kwa hasira baada ya kusikia maneno yale.
“Ndio unavyoona , sio mbaya najua nafasi yangu ni ndogo kukushinda lakini sijawahi kujisalimisha kirahisi hivyo”Mwisho wa sentensi yake palepale alikielekeza Chungu chake uelekeo wa Aoiline
Aoilinepalepale alijikuta akikunja macho yake lakini kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana ni kama hakuwa na mpango wa kukikwepa.
“Mjinga sana wewe”
Ghalfa tu mikia mitano iliweza kutokea nyuma yake na kwenda kukishikilia kile chungu , nguvu yake ya mvutano ilitaka kuimeza ile mikia lakini nguvu kubwa ya kijinni aliokuwanayo Aoiline iliweza kushinda na kile chungu kilirushwa kwa nguvu kuelekea hewani kama mpira huku yale macho ya mnyama ambayo mara nyingi huonekana ndani ya chungu kile yalipotea.
Kutokana na Roma kutumia nguvu nyingi kukitawala kile chungu na wakati huo huo Aoiline na yeye kutumia uwezo wake kukidhibiti maumivu aliyapokea yeye, ilikuwa ni kama viungo vyake vya ndani vinapasuka na aliishia kutema damu.
Kitendo hicho kilimuonyesha kwamba Aoiline uwezo wake ulikuwa ni mkubwa sana kuliko isivyokuwa kawaida kwani chungu chake ambacho aliamini kilikuwa na nguvu kiliweza kudhibitiwa kwa sekunde tu bila kuonyesha ukinzani wowote.
Sophia aliekuwa akishuhudia kitendo hicho alijikuta akijawa na wasiwasi mno hasa mara baada ya kumuona Roma akitema damu na alishindwa kujizuia na kumsogelea.
“Bro vipi hali yako?”Aliongea Sophia kwa upole na Roma alijikuta akikosa nguvu na kumuegamia Sophia.
Ijapokuwa alitaka kumwambia kwamba atakuwa sawa lakini alikosa nguvu kabisa hata ya kunyanyua mdomo na aliishia kutingisha kichwa chake tu.
Uwezo wake wa kujiponyesha ulikuwa ni wa taratibu mno kutokana kuwa na nguvu kidogo ya kijini na palepale chungu kile kilipotea.
“Nilikuonya mwenyewe , kwa nguvu zako za kijini Cauldron inaweza kuwa na nguvu kwa majini pepo wa kawaida lakini kwangu hapana”
Alimwangalia Sophia ambaye alikuwa na sura iliopauka na kisha palepale hakuonyesha kutaka kupoteza muda na alirusha kamba zake za hariri na kuwafunga funga.
“Nyie wote wawili tunaondoka pamoja kuelekea Palace”
Roma alitaka kumsukuma Sophia asifungwe na zile kamba lakini hakuweza kabisa na waliishia kuburuzwa wote kama mateka.
Roma hakuwahi kukata tamaa mara baada ya kuingia katika ulimwengu huo uliojjtenga lakini alijihisi kukata tamaa mara baada ya kumuona Aoiline akipaa bila tatizo kwa spidi kubwa na umbali mrefu kirahisi kabisa licha ya kwamba alikuwa akipambana na yeye.
Aoiline alisema kwamba mazingira yalikuwa yakizuia kutumia nguvu zake ,sasa alijiuliza kama ni hivyo uwezo wake ulikuwa ikifikia wapi kama tu ataweza kutoka katika ulimwengu wa kawaida.
Roma hakuona shida kupoteza pambano lakini alimuonea huruma Sophia kutokana na ukiburi wake na mbaya zaidi asingeweza kurudisha nguvu zake ambazo zilikuwa zimepotea na hata kama ikitokea asingeweza kuwa na uwezo wa kumshinda Aoiline.
Alijikuta akikumbuka ule usemi kwamba haijalishi una nguvu kiasi gani lakini kumbuka kuna mwenzako ana nguvu kuliko wewe , ni sawa na kusema haijalishi una akili kiasi gani lakini kumbuka kuna mwingine ana akili kuliko wewe , au unaweza kusema haijalishi unajiona bora kiasi gani lakini kumbuka kuna aliebora zaidi yako hivyo kuna mazingira inapaswa kujishusha na kuukubali ukweli lakini yeye alienda kinyume na sheria hio.
Licha ya kwamba kuna misemo mingi ya kihenga lakini siku zote haifanyi kazi katika kila mazingira , anaweza akawa ameonyesha kiburi lakini dhamira yake ilikuwa ni kutaka kujaribu ndio maana hakuona aibu kushindwa ni vile tu nafsi yake ilikuwa ikijutia kumuingiza aliekuwa nae matatizoni.
Baada kupaa kuelekea mashariki kwa muda mfupi majengo yalianza kujionyesha mbele yao kwa chini.
Yalikuwa ya kitamaduni lakini makubwa na ya kuvutia , mchanganyiko huo wa kitamaduni wa makabila mbalimbali ya watu wa nje ya dunia iliwafanya kujihisi kama vile dunia ya kale imeunganiska sehemu moja, yaani waarabu , wachina , wakorea wazungu pamoja na makablila mengineyo ambayo yalikuwa yakiwakilishwa na sanifu zao za kimajengo.
Baada ya kuingia kwenye jengo moja refu ambalo lilikuwa mlimani waliweza kuona madini ya Nephriti yaliokuwa yamening’inizwa katika korido kuingia ndani kabisa ya jengo la kimalkia, ilikuwa ni kama vile ni yale majumba makubwa ya kifalme lakini ambalo limejengwa kwa mahadhi ya kisanifu tofauti tofauti .
Juu kabisa ya mlango wa kuingilia kulikuwa na ubao juu(Lintel) uliokuwa na maandishi makubwa ya kingereza na lugha isiokuwa ikieleweka , ‘Jade Fox Palace’, ni maandishi ya kubandika na hata kwa mjinga ungejua ni madini ya dhahabu yaliotumika.
Baada ya kuingia kwenye Baraza kubwa ambalo sakafu yake hiakueleweka imejengwa na madini gani kutokana na mtelezo wake palepale Aoiline aimtenganisha Sophia na Roma wakiwa wamefungwa katika staili moja lakini tofauti ni kwamba Sophia alikuwa amepoteza fahamu.
Roma akiwa amesimama katika eneo moja akiwa amefungwa na kamba za hariri palepale sehemu ambayo alikuwa amesimama ilianza kutengeneza duara kwa kuonyesha michirizi ya madini ya dhahabu na ilikuwa ni kufumba na kufumbua Roma alitumbukia ndani na kwenda kutua chini ya Gereza la Ardhini.
Roma alitaka kutoka haraka kabla shimo halijajifunga lakini alizuiwa na mwanga mkali wa dhahabu uliokuwa kama kioo.
“Wewe mtukutu hilo gereza limetengenezwa kwa madini yalitoka katika bahari Isio na mwisho , chuma chake kukuzunguka ni kile cha miaka mingi iliopita na kazi yake kubwa ni kunyonya nguvu za kijini na huu mwanga wa njano uliokuwa juu yako hauwezi hata kidogo kuupita , elewa ushauri wangu , kubali kuwa mfungwa wangu ili usipoteze nguvu zako”
Roma alijikuta akijaribu kupiga ngumi kuta za chumba na alijikuta akiona hakuna namna ya kuweza kutoboa .
“Pumbavu zako kabisa wewe Aoiline , kama unataka kulipiza kisasi cha watu wkao kwanini ipigane na mimi mpaka nife kuliko kunifungia”
Roma alikuwa na hasira alikuwa na hamu sana ya kutoka katika ulimwengu huo kuirudia familia yake , angewezaje kufikia mnara kama ndio hivyo ni mfungwa.
“Nini .. haha!, huwezi hata kushindana na mimi lakini bado unafikiria kwenda kwenye Mnara , mimi mwenyewe licha ya uwezo wangu nina asilimia hamsini tu za kupona mapigo tisini na tisa ya radi, nakushauri uache ndoto zako”
Baada ya kusema hivyo alitembea kuelekea kwenye Majilisi (Chamber au chumba) akiwa amemfunga Sophia vilevile akimburuza akiwa katika hali ya kupoteza fahamu.
Majini waliokuwa ni wahudumu na vijakazi wake walikuwa tayari wamekwisha kujipanga muda mrefu tokea anaingia na Roma .
Baada ya kuingia kwenye Majilisi wahudumu wa ngazi ya juu waliiinamisha vichwa vyao chini kwa heshima, hakuna jini ambao halikuwa na mwonekano tofauti na binadamu.
“Mchukueni na muingizeni kwenye Majilisi ya kushoto , mhudumieni vizuri lakini asiruhusiwe kutoka bila rushusa yangu , mnanielewa?”
“Ndio Bwana wetu”
Wahudumu wale hawakutaka kuuliza mtu huyo ni nani na anatokea wapi zaidi ya kutii maagizo.
Baada ya vijakazi wale kuondoka alitembea na kwenda kukaa kwenye kiti chake kilichotengenezwa kwa madini ya Dhahabu tupu huku pembeni yake kulikuwa na aina ya madini ambayo hayakuwa yakielezekza , ni kama vile ni vinundu vya Akmasi huku ndani yake kukiwa na madini mengine ambayo yalikuwa yakipumua kwa kubadilika badilika rangi.
Alifumba macho yake kwa kuvuta pumzi nyingi huku masikio yake yaliokuwa na uwezo wa kusikia mitetmeo yaliweza kunasa sauti za Roma kushindana na kuta za gereza chini ya ardhi lakini alionyesha kutojali ni kama alikuwa na uhakika asingeweza kutoka.
“God why did you send in onother headless man when I’ve almost forgotten about him?”
“Mungu kwanini ukaamua kutuma mwanaume mwingine kichaa ilihali yule nakaribia kumsahau”
Aliongea mrembo huyo akiwa anaangalia eneo la juu ambalo lilikuwa kama na kioo kinachopitisha mwanga kutoka juu angani na macho yake yalionyesha chuki na huzuni.
Kauli yake ilikuwa ikitafsirika kama vile kuna mtu aliempoteza na sasa anakaribia kumsahau lakini anamuuliza Mungu kwanini kamleta mwingine kichaa..
*******
Kulikuwa na baridi sio ya mchezo ndani ya Iringa kwasababu ilikuwa kipindi cha vuli lakini licha ya hivyo Edna hakuonekana kuathirika kwasababu alikuwa ni tofauti tokea aanze kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Ilikuwa ni muda wa jioni ndani ya jiji la Iringa, Edna alikuwa amesimama nje ya geti katika shule ya watoto maarufu iliokuwepo karibu na chuo akimsubiria mtoto wake kutoka nje ya geti kama wazazi wangine walivyokuwa wakisubiria.
Wiki mbili zilikuwa zimekwisha kupita tokea kupotea kwa Roma na hakukuwa na habari zozote za kumuhusu.
Familia ya Afande Kweka haikutaka kumruhusu Edna kurudi Dar es salaam na kujifungia akiwa mwenyewe, hivyo wakamshauri Lanlan kuandikishwa shule ya muda ndani ya jiji hilo aendelee na masomo.
Lanlan alikuwa na akili hivyo aliweza kuendana kwa haraka na mazingira ya shule mpya na hakuonyesha malalamiko yote na alipenda michezo iliokuwa ikifanyika shuleni kwao.
Ukweli ni kwamba ukoo huo wa Roma ulikuwa na utajiri mkubwa sana kutokana na kuwa na vitega uchumi vingi na haikuwa hivyo tu hata yeye mwenyewe alikuwa na hela na ingekuwa rahisi kwa Lanlan kutafutiwa mwalimu ili kufundishwa akiwa nyumbani lakini Afande Kweka hakutaka Lanlan akikaa ndani tu aliamini kuchanganyika kwa Lanlan na wenzake kutampatia msingi mzuri wa kijamii.
Edna alikuwa akielewa dhamira yao ni nini hivyo hakutaka kukataa na kuruhusu Lanlan kuanza shule lakini ukweli ndani kwa ndani mrembo huyo alikuwa na huzuni, wakati wengine wakiwa na tabasamu na tumaini yeye muda wote alikuwa akiwaza yu wapi mume wake.
Ni wiki mbili sasa hakuwa akilala usingizi mzuri na alikuwa akisumbuliwa na ndoto nyingi na alishindwa kabisa kuvuta taswira ya kila wazo baya linalomjia , maswali haya ndio yalikuwa yakikitawala kichwa cheke , vipi kama Roma asiporudi milele? , Vipi kuhusu yeye atafanya nini?.
Wanawake wa Roma kutoka Dar walikuwa wakimsumbua kwa kumpigia kutokana na kushindwa kufanya mawasiliano na Roma na Edna hakuthubutu kuwaambia ukweli kama amepotea , aliishia kudanganya kwa kuwaambia kwamba Roma yupo katika sehemu ya kujitenga akiwa kwenye mafunzo makali sana ya kimapigano.
Hakuna alieweza kushuku maneno yake , pengine ni kwasababu walikuwa wakimuamini au matamannio yao zidi ya mwanaume huyo yalikuwa makubwa kuliko wasiwasi wao.
“Mommy!!”
Sauti ya kitoto iliweza kumtoa katika hali yake ya kimawazo na Edna alionyesha tabasamu huku akichanua mikono yake kumpoktea Lanlan kwa kumbatio.
Lanlan alikuwa amevalia koti la Track suit la bluu pamoja na suruali yake kwani siku hio ilikuwa ni ya michezo shuleni
Akiwa na Lanlan mikononi mwake alitembea nae kuelekea kwenye gari huku akimuuliza maswali kama siku zote.
“Lanlan what did you learn today?”
“Leo Lanlan amecheza michezo mbalimbali ya kukimbizana na nilimshinda hadi mwalimu”Aliongea na kumfanya Edna kushindwa kuvumilia kauli yake na kutoa kicheko , Binti yake ndio mtu pekee ambaye alikuwa akimchekesha kama hivyo katika kipindi hicho cha mawazo
“Darling , you have to be easy on your teacher nextime or else it would be hard for the teacher to teach other children”Aliongea na kumfanya Lanlan kutingisha kichwa chake kukubali ushauri wa mama.
“Mama tunaenda kula sasa hivi?”
“Jua bado linawaka na tayari unawaza chakula”
“Mama Lanlan ana njaa”Aliongeana kumfanya Edna kumfinya shavu na kisha kumuingiza ndani ya gari lao la kifahari.
Mwanamke ambaye alikuwa akimwendesha Edna alikuwa ni mjeshi tena Komandoo na alipewa kazi hio maalumu kumuendesha Edna lakini kwa wakati mmoja kumpa ulinzi na mara baada tu ya kuingia ndani ya gari aliliendesha.
Wakati gari yao inaingia barabara kuu ikirudi nyuma kutokea mjini kuelekea nyumbani kwa Afande Kweka ambako ni nyuma kabla hujafika Iringa waliweza kusikia ving’ora vya gari ya kipolisi nyuma yao.
Mjeshi yule alionekana kushangaa mara baada ya kuona kuna polisi wanaomuashiria kusimamisha gari.
“Ma’ am nadhani napaswa kusimamisha”Aliongea na Edna alimpa ishara kwa kutingisha kichwa kukubali bila kufikiria mara mbili mbili.
Baada ya gari yao kusimama pembeni ya barabara walitoka polisi waliokuwa wamevalia mavazi ya kitrafiki na kuwasogelea na mmoja wao aligonga kioo na kuashiria kufungua mlango na dereva kushuka.
“Afisa nadhani sijakiuka sheria zozote za barabara”Aliongea Mjeshi mara baada ya kutoka nje ya gari.
Polisi mmoja ambaye alikuwa na chunusi nyingi usoni alimsogelea yule mjeshi na kwa spidi kubwa aliishikilia shingo yake , kilikuwa kitendo cha kushtukiza, pengine mjeda yule hakutagemea angeshambuliwa ndio maana ilikuwa rahisi kwake kupokea pigo lile kabla bata hajaweza kujitetea, ni mlio wa mifupa tu ulioweza kusikika na palepale alilegea na kudondoka chini.
Edna palepale alishituka na kugundua watu hao hawakuwa polisi kama alivyodhani , ilionekana ni majambazi ambao hawakuwa na nia nzuri kwao
“Mommy they’re bad guys!!”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kuguna.
Polisi yule mwingine hakupoteza muda kwani palele kupitia mlango wa mbele alirusha bomu la moshi kuelekea ndani ya gari na Edna alishindwa kuwa mwepesi na alijishtukia tu tayari mapafu yake yakiweza kuvuta ule moshi.
 
SEHEMU YA 607.
Gesi ile haikuwa na harufu hata kidogo wakati ikiwa inaingia kwenye mapafu yake na ilimfanya Edna kuanza kuona kizungu zungu , ijapokuwa alikuwa mwishoni mwa levo ya nusu mzunguko lakini haikusaidia kuweza kutokuathirika.
Upande wa Lanlan moshi ule haukuwa na athari kwake na palepale le alifanya maamuzi ya kufungua mlango haraka haraka kwa spidi zote na kumsogelea yule mwanaume mwenye chunusi kwa spidi kubwa akitanguliza miguu kama mpira vile.
Wale watu walishangazwa na namna ambavyo Lanlan alishindwa kuathirika na gesi ile ya kuulegeza mwili, baada ya kuona kitoto hicho kinamsogelea kwa ajili ya kumpiga alikuwa ni mwepesi sana kwani alisogea pembeni na Lanlan akapita na wakati huo huo akikamata mguu wake.
Edna aliweza kuona kila kitu lakini mwili wake haukuweza kufanya chochote hata kusogea na mara baada ya kuona namna ambavyo mmoja wapo amekwepa pigo la Lanlan kirahisi aliweza kuhisi kabisa huenda walikuwa na nguvu za ziada hata wao
Lanlan baada ya kuona kashikiliwa mguu alitumia kichwa kushambulia lakini yule mtu alimshika kwa wepesi zaidi.
“Pumbavu huu ni ukichaa , kana nguvu za kijini tena za kutosha tu , Bro mzimishe haraka”Aliongea yule mwingine.
“Gotcha”
Yule bwana mwenye chunusi alimshikilia Lanlan vizuri bila hata ya kupinda pinda na kwa ustadi wa hali ya juu kama mcheza Kungu Fu alimgusa Lanlan katika eneo muhimu la shingo na palepale akapoteza fahamu.
“Pumbavu kabisa huyu mtoto ni hatari kuliko hata mama yake , ni ,kheri tumefanikiwa na mpango wetu haujabuma”Aliongea yule bwana mwenye chunusi huku akijaribbu kuangalia mazingia kama kuna watu wanaowaangalia , lakini eneo ambalo walilichagua lilionekana kuwa kimya mno kwani hawakuonekana na dakika walizotumia zilikuwa chache mno , ilikuwa ni kama vile wamezuia magari kutopita kwani haikuwa kawaida kwa kutokuonekana hata pikipiki ikipita katika hilo eneo.
“Bro wewe mbebe huyo mwanamke na mimi nitambeba huyu mtoto , nina uhakika kuna kifaa cha GPS kwenye gari lao hivyo tunapaswa kuliacha”Aliongea
Bwana yule alikubaliana na wazo la mwenzake na kisha alitingisha kichwa katika mlango wa gari na kujaribu kama vile anamsiadia Edna kushuka na baada tu ya kumtoa alimbeba juu juu na kisha wakamuingiza kwenye gari lao la kipolisi na yule mwingine pia aliingia , muda huo Edna bado alikuwa akipambana na usingizi na alijaribu kusukuma sukuma lakini hakuwa na uwezo wowote na dakika chache mbele alisinzia…
*****
Upande wa nyumbani kwa Afande Kweka , Mzee Camillius mwenyewe alikuwa amekaa kwenye kiti chake cha kivivu huku akinywa chai ya moto akiangalia bustani yake ya Karoti.
Ilikuwa ndio tabia yake mara nyingi kama hayupo kwenye mifugo basi yupo kwenye bustani yake akikodolea mimea kama vile kuna kitu cha kufurahisha anachokiona na hakuwa akijali upepo na baridi kwani alikuwa na mavazi mazito lakini pia afya yake haikuwa mgogoro.
Dakika hio hio aliweza kusogelewa na mlinzi wa nyumba hio kwa spidi huku akiita sauti yake kwa wasiwasi.
“Marshall , Madam Edna na Lanlan gari yao imeonekana imesimama kando ya barabara na tumejaribu kuwapigia hawapatikani na Luteni Mlowe kakutwa kafariki ndani ya gari”Aliongea kwa wasiwasi na kufanya uso wa Afande Camillius kubadilika palepale kutoka katika hali yake ya amani.
“Vipi kuhusu kifaa cha GPS?”
“Signal zimepotea ni kama zimeingiliwa , Watekaji wanaonekana kuwa wabobezi”
“Kama ni hivyo hatuna muda wa kupoteza , si Afande Tobwe yupo Iringa bado , jaribu kuwasiliana nae na afanye muunganiko wa kimaagizo na mawasiliano na RCO polisi kuzuia magari kutoka nje ya Iringa, sikiliza maagizo yake na usiruhusu mtu yoyote kujua hili “Aliongea na mlinzi yule alitoa saluti na kisha alikimbia kuondoka.
Afande Kweka alisimama huku akiwa na uso usioelezeka na alionekana kama alikuwa akiongea mwenyewe huku sura yake yote ikiangalia bustani.
“Nadhani tayari siri zishavuja na maadui zako wanaitumia kama nafasi , kama hutorudi mapema nitashindwa kuhimili zaidi”Aliongea mwenyewe.
******
Jua lilikuwa tayari limekwisha kuzama na Mwezi kuchukua ufalme wake wa kuiangaza dunia , katika eneo ambalo lilikuwa kama bandari kavu kutokana na uwepo wa Makontena mengi yaliochakaa huku yakiwa yamepandiwa na uozo pamoja na miti kuota juu yake kulikuwa na ghala.
Eneo hilo lilikuwa limezungukwa na ukuta mkubwa , ni rahisi kusema ni ghala ambalo halikuwa likitumika na hata kama lilikuwa likitumika sio kwa shughuli ambazo zilikusudiwa tokea kujengwa kwake.
Ndani ya jumba bovu la mabati kama kiwanda lilikuwa limefungwa lote kwa nje huku ndani likuwa na tundu moja tu kama chanzo cha hewa safi.
Zilipita dakika chache tu eneo lote la ndani taa ziliwashwa huku mlango ukifunguliwa na hatimae walionekana Edna na Lanlan wakiwa wamefungwa katika viti wakiwa karibu karibu.
Watu waliokuwa wameingia hapo moja wapo walikuwa ni wachina na waafrika na walikuwa kama kumi na mbili hivi na walikuwa na miili iliojengeka kimazoezi.
Edna aliekuwa amefungwa katika kiti ile dawa aliowekewa ya usingizi ilikuwa imemuishia makali sasa alikuwa na fahamu zake , kwa kuangalia tu kundi la watu hao alijua kabisa ni ngumu kuweza kutoka kwani ni wengi mno.
Edna katika hali kama hio hakujali usalama wake , utashi wa mwanamke mwenye mtoto ulimvaa na kitu pekee alichokuwa akiwaza ni Lanlan kuwa salama.
Lanlan mwenyewe alikuwa macho huku akiwa na hasira nyingi na kwa nguvu zake alijaribu kufurukuta katika kiti alichokaliswa lakini bwana mwenye chunusi alikuwa amemshikilia vizuri sana , kitendo cha kuweza kushindwa kufanya chochote aliishia kutoa machozi tu ya hasira.
Lanlan katika hali kama hio akili yake iliweza kufikiria kauli ya baba yake akimlazimisha kufanya juhudi za kujimarisha katika mafunzo yake ya kuweza ku’master’ nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo, ni kama mtoto huyo mdogo ndio anajua sababu ya kuhimizwa na baba yake ilikuwa nini.
“Nyie watu ni wakina nani , hivi mnajua matokeo ya hiki mnachokifanya?”
“Bila shaka tunaelewa , wewe ni Madam kutoka ukoo wenye nguvu ndani ya taifa hili , mkwe wa Raisi Wa Jamhuri Ya Muunganno Wa Tanzania”
“Kama mnalijua hilo kwanini mnathubutu kufanya hivi?”
“Kwanini tusiweze kuthubutu , Mlengwa wetu ni moja wapo ya mwanafamilia ndani ya ukoo wa Kweka mathalanni mtu wa karibu zaidi na bwana Roma Ramoni , wewe ndio mke wake hivyo inakufanya uwe target yetu ya kwanza”
“Hamumuogopi mume wangu?”Aliuliza Edna akijaribu kujituliza.
“Madam Edna, kubali ushauri wetu na uache kuuliza maswali na kujifanyisha , tuna taarifa zote Roma Ramoni amepotea kwa zaidi ya wiki mbili sasa , hii taarifa bado haijafahamika na watu wengi na sisi tumeisikia kutoka katika chanzo cha kuaminika hivyo acha kujaribu kutufanya wajinga”
“Kama ni hivyo basi mtakuwa na sababu ya kumchukia mume wangu”
“Nitakuwa muwazi na wewe , Sisi tulishawahi kufanya kazi chini ya Kamanda Razaq kama Special Forces, tuna deni kubwa kwa Kamanda Razaq na ukoo wake wote , Roma ni shetani kabisa yule m amemuua Kamanda bila wasiwasi kwasababu tu eti ana nguvu kubwa na sapoti kubwa kutoka katika familia yake , Tupo hapa kwa ajili ya kulipiza kisasi cha Kamanda wetu”
Edna alijikuta akitoa macho na kutoa kicheko hafifu huku akiwaangalia.
“Mnajiita wanajeshi mliokuwa chini ya Kamanda Razaq , kama ni hivyo kwanini hamjatuua mpaka sasa , kwanini nyie watu mkajifanya kuwa polisi na mkatuteka?”Aliongea na kumfanya yule kiongozi wao mwenye chunusi kuwaza kidogo.
“Kama nilivyotegemea ,Mwanamke giniasi mfanyabiasara ndani ya taifa Tanzania , bado una akili kama kawaida yako licha ya kuachana na maswala ya biashara , upo sahihi tupo hapa na dhamira nyingine”Aliongea na kumfanya Edna kuhisi kitu , ni kama ashajua ni kitu gani ambacho wanataka kutoka kwake.
“Madam usijivunie bado , kutokuwaua kwetu hakumaanishi hatuna mbinu nzuri ya kimbadala kwa ajili ya kulipiza kisasi chetu , Mabraza wetu hapa wa kichina wapo katika levo za juu za mzunguko kamili katika mafunzo ya kijini lakini licha ya mipango yetu na kuwapata hawa bado ni wachache sana kuweza kupigana na ukoo wa mumeo, Roma Ramoni anajifanya kijogoo kwasababu tu ana mbinu za hali ya juu za kuvuna nishati kwa maelezo tulioyapata , kwa kumwangalia tu binti yako tunaona kitu kisicho kawaida kutoka kwake”
“Mnazunguka zunguka kwasababu hamna ujasiri wa kutuua … mpo hapa kwa ajili ya hila zenu za kuweza kupata mbinu ya mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , mpo hapa kwa mgongo wa kujifanya eti tunataka kulipiza kisasi cha Kamanda Razaq”
Bwana mwenye chunusi ambaye ni kiongizi mwili wake ulikakamaa kutokana na maneno ya Edna.
“Nendeni mkamuambie raisi Jeremy anapaswa kuacha kutumia hila zake kwangu , mimi bado ni sehemu ya ukoo wa familia ya Kweka hata kama mume wangu bado hajarudi “
“Jeremy? Hahaha.. nadhani ni kama uvumi unvyosambaa ikisemekana raisi Jeremy wa Rwanda ndio baba yako mzazi , kwanini unafikiri anaweza kufanya kitendo kama hiki kwenu nyie”
“Kwanini asiweze ,bila koneksheni nyie watu msingeweza kuwa na ujasiri wa kufanya yote haya .. hii ni Tanzania”Aliongea.
“Unachoongea hakina mashiko , nina sentensi moja tu ya kukuambia , mnatupatia mbinu hio au hamtupatii?”Aliuliza akiwa na macho makali akimwangalia Edna.
Muda huo Edna alichokuwa akijaribu kufanya ni kuvuta muda ili angalau iwe rahisi kwa watu kugundua wapo hapo
“Mnapoteza muda wenu kwani sijui chochote kuhusu nguvu za mume wangu na mbinu zake”
“Haha acha kupoteza muda au unadhani kuna mtu ambaye anaweza kuja hapa na kukusaida , ngoja tu niwe mkweli kwako hatumuogopi mtu yoyote atakae fika hapa ilimradi tu sio Roma”Aliongea kwa kejeli na kumfanya Edna kung’ata lips zake.
“Madam unaweza usielewe kitu kimoja , sababu ambayo inakufanya mpaka muda huu uendelee kuishi mbele ya macho ya watu wenye husda ni kwasababu tu umeolewa na mtu ambaye anaogopwa na kila mtu , sio kwasababu tu eti wewe ni mtoto wa nje ya ndoa wa raisi Jeremy wala sio kwasababu ni raisi wa mkampuni mkubwa kama Vexto pamoja na utajiri wako, Sasa hivi huna lolote kwetu kwani mumeo amepotea na huenda akawa amekufa huko alipo na hujui tu, hivi unafikiri tunaweza kukuogopa kuto kuukuua?”Aliongea bwana mmoja ambaye ndio aliehusika katika kumteka na meneno yake yalikwa mwiba katika moyo wa Edna.
“Hawezi kufa , Roma ni mzima”
“Nani anajali hilo . uzuri ni kwamba hayupo hata kama anaishi”
Macho yake palepale yalichanua na kuanza kumwangalia Edna na urembo wake usiovumilika na alishndwa hata kujizuia na kujiambia angalau hata kwa mara moja aguse ngozi yake ya uso na palepale alipeleka mkono huku akitetemeka tetekemeka, ni kama hakuwa akiamini anagusa shavu la mrembo Edna tajiri.
“Bad guy , don’t you dare touch mommy I’ll kill you”
“Mtu mbaya usije kuthubutu kumgusa mama , nitakuua”Lanlan aliongea huku akijaribu kufurukuka lakini bwana mmoja alimsogelea na kumlisha tambara mdomoni na kumwambia kaa kimya , hawakuweza kuvumilia kutishiwa maisha yao na mtoto mdogo kama Lanlan, hakuweza kusogea kwasababu wale watu walikuwa wamefunga kwa kulenga Meridian za mwili wake li kumzuia mtitiroko wa nishati katika mwili wake.
Lanllan aliishia kutoa machozi huku akitingicha kichwa akijaribu kutoa tambara mdomini
“Msimuumize binti yangu, ni mtoto tu hana kosa”Aliongea Edna.
Edna alijawa na hofu kubwa mara baada ya mkono wa ule mwanaume ukimsogelea kumshika , hisia kali za ukinzani kutoka kwake ziliamsha bangiri iliokuwa kwenye mikono yake na palepale ulisikika mlio wa ‘Chiii…’ kama vile ngendere anaenyongwa huku eneo lote likijaa mwanga wa kijani na wimbi lake lilikuwa na nguvu kiasi kwamba liliweza kuwapush yule mwanaume mwenye chunusi na yule mwingine, lakini kutokana na uimara wao hawakuweza kuumia.
“Shit , hicho ni nini?”Waliongea huku wakitoa macho na kundi lote lilirudi nyuma huku wakiangalia mwanga uliomzingira Edna kwa mshangao na wasiwasi wa juu.
Ule mwanga haukuwashambulia wao tu bali uliunguza mpaka zile kamba ambazo zilikuwa zimemfunga Edna na akawa huru.
Ile bangiri ni kama ilikuwa na akili kwani iliweza kumlinda Edna tu kwa kutoa mwanga ambao ulikuwa ukimzingira yeye na mtoto wake , hakika ilikuwa Dhana ya kijini kutokana na maajabu yake.
Wale majambazi hawakuelewa nini kilichopo kwenye ile bangiri , kuna hisia ziliwaambia ni siraha ya kijini lakini hawakuelewa kwanini ilikuwa na nguvu namna ile na waliogopa hata kumsogelea Edna.
Kwa maelezo ya Zenzhei Bangiri ile haikuweza kuonyesha uwezo wake wote , hivyo nguvu yake ilikuwa ikiendana na levo ya Edna katika mafunzo ya kijini , sasa haikueleweka kama Edna akifikia katika levo ya Nafsi nguvu yake itakuwaje.
Wale wachina ijapokuwa na wao walikuwa katika levo ya mzunguko kamili ilimaanisha kwamba walikuwa ni wakawaida tu na hawajapata ufunuo bado wa kutumia elementi za dunia katika kufanya mashambulizi, hivyo faida pekee waliokuwa nayo ni nguvu za miili yao , lakini katika mazingira hayo hawana uwezo wa kumsogelea Edna kwani wangeunguzwa na ule mwanga.
“Ma afande hatupaswi kuwa na hofu kwa ajili ya hichi , msisahau na sisi tuna siraha pia”
Yule bwana mwenye chunusi aliongea na palepala alichomoa bastora maarufu kama Desert Eagle na kumnyooshea Edna huku akitoa tabasamu la kejeli , wale wengine wote nao pia walitoa siraha zao zinazofanana , ule mdomo mweusi wa bastora na tundu lake ulimwambia ikitapika itamuua palepale
“Madam Edna mumeo ndio kakuachia hio siraha kwa ajili yako , Aisee nakiri ni kinga nzuri”Aliongea Jambazi mwingine mwenye kovu kwenye uso.
“Mimi shauku yangu ni kutaka kujua kama ina uwezo wa kuzuia na risasi au kama inaweza kuwalinda wote wawili kwa wakati mmoja”Aliongea na palepale alibadilisha uelekeo wa siraha yake na kumlenga Lanlan.
“Hapana”
Edna alitoa ukulele na kisha akampakua Lanlan na kumkumbatia huku akiwapa watu wale mgongo, alikuwa yupo tayari kufa yeye ila Lanlan apone.
“Madam Edna unapaswa kujua sisi kuvuta triga na kuruhusu risasi ni kitu chepesi sana na tulichosomea , hata kwa angle niliokuwepo nina shabaha ya kuweza kumchapa risasi mtoto wako hio miguu yake inayoonekana au bega , unadhani bado hio bangiri yako inaweza kumlinda ,,, vipi kama isipofanikiwa kuwalinda na risasi?”
Maneno yae yalimfanya Edna kutetemeaka na kupauka kwa wakati mmoja
Jamaa yule alionekana bingwa wa kutumia maneno vizuri sana na alimfanya Edna kujiuliza je kama bangiri hio haina uwezo wa kuzuia risasi nini kitamtokea na isitoshe ndio mara ya kwanza kupatwa na tatizo kama hilo.
Edna alijiuliza maswali mengi na aliishia kuona kwamba hawezi kuchukua Risk kwa usalama wa binti yake na katika mazingira kama hayo anapaswa kufanya maamuzi.
“Mama usilie, Lanlan haogopi kitu”Edna alishindwa kujua kama muda huo alikuwa akilia.
Lanlan bado hakuwa na uwezo wa kufanya chochote mwili wake ulilegea licha ya kufunguliwa , wale wachina walikuwa wajanja sana ni kama haikuwa mara yao ya kwanza kuteka mtu ambaye ana uwezo wa kijini kwani mtiririko wa nishati katika mwili wa Lanlan ulikuwa mdogo.
Edna alijiambia hana thamani kabisa , katika mazingira ya hatari kama hayo hata binti yake tu hawezi kumlinda , yeye ni mama wa namna gani.
“Madam Edna tuna mwisho wa uvumilivu wetu , hatuwezi kukushambulia kama upo tayari kuvua hio bangiri , kama utakataa basi tutafanya majaribio kuona kama ina uwezo wa kukinga na risasi na mimi shabaha yangu ni binti yako tu”
“Nitaivua”
Aliongea Edna kwa kufoka , kila anaposikia kauli yoyote ya mtoto wake kutaka kudhulika aliogopa sana , huenda ndio udhaifu wake mkubwa.
Edna kwa mikono iliokuwa ikimtetemeka alimuweka Lanlan chini na kisha akaivua ile bangiri na kuikweka chini kweney sakafu na palepale ule mwanga uliokuwa ukimlinda ulipotea kama vile ilikuwa ndoto.
Yule bwana mwenye chunusi mara baada ya mwanga ule kupotea alimsogelea Edna na kisha akamsukumia kwenye kiti na kisha akamuwekea bastora kwenye paji la uso wake
Edna alijua uwezo wake wa kijini ni mdogo sana , hivyo akileta ukinzani atakaepata madhara ni Lanlan hivyo aliamua kutulia
“Kacha kacha”Risasi zilipandishwa kwenye chemba ya mlipuko katika bastora ile ya yule bwana mwenye chunusi.
“Nimewaza kwa haraka haraka , kama kweli wewe madam huwezi kutuambia kuhusu mbinu ya kimafunzo ya kijini basi mtoto wako ataweza kutuelezea … mtoto huyo wa Roma tayari ana nguvu za kijinni ndani yake tena kwa umri huu mdogo ninaamini uwezo wake ni mkubwa kukuzidi …. Chubby girl tuambie mbinu ya kimafunzo ambayo baba yako amekupatia”
“Your are a bad guy , daddy will come and kill all of you”Aliongea Lanlan huku akiwa na hasira nyingi na kwa jinsi alivyokuwa akiwangaalia kwa hasira ni Roma mtupu.
“Hehee upo kama baba yako tu , tayari mkali ktika umri huo “Aliongea huku akipiga piga mashavu ya Lanlan .
“Ngoja nikuambie kitu Chubby , mama yako atakufa kama hautasema sawa”Aliongea na kumfanya Lanlan kumwangalia mama yake na machozi kuanza kumtoka , lipsi zake zilikuwa zikicheza cheza.
“Mimi sijui kitu..”
Edna alikuwa kwenye maumivu makali ya moyo lakini alipatwa na ahueni kumuona Lanlan anakumbuka maagizo ya baba yake , aliamua kumtingishia na yeye kichwa kumwambia kwamba asiongee.
“You are all badguys .. I don’t want mommy to die..”Aliongea na Lanlan pale pale aliangau kilio cha kwikwi.
“Usilie sasa mtoto mzuri, nitamuua tu mama yako”Aliongea na palepale sura ya bwana mwenye chunusi ilibadilika na kisha akamwangalia Edna na kufanya kilio cha Lanlan kukoma palepale kwa mshituko.
Kwa namna ambavyo Edna alikuwa akiangaliwa na mchezo wanaofanyiwa na hao majambazi maumivu yake yalikuwa ya juu mno ilikuwa ni kama vile moyo wake una charangwa na visu.
Alijiambia ingekuwa ngumu sana kwa maisha ya Lanlan kama ataweza kushuhudia kifo chake katika umri huo mdogo.









SEHEMU YA 506.
“Little girl , nitakupa nafasi ya mwisho , niambie mbinu yako ya mafunzo au nitamlipua mama yako..”Aliongea huku akiisogezea karibu kabisa bastora yake na uso wa Edna.
Edna asingeweza kupona kama siraha hio itamlipua kwasababu mwili wake haukuwa na nguvu kama za Roma
Lanlan alikuwa ni mtoto lakini alikuwa akielewa kama bunduki ile itakohoa basi mama yake anakufa palepale na hakutaka kufanya chochote na palepale alionyesha kufanya maamuzi yake.
“Lanlan usiongee , hawawezi kuniua , usi..”
“Boom!!!”
Sauti ya mlipuko wa risasi ilimzuia kutoendelea kuongea na bwana mwenye chunusi alionekana alilenga juu kwenye bati na kisha palepale ikiwa inafuka moshi aliigeuzia kwa Edna tena.
“Madam acha kujifanya mjuaji , hii bastora ina risasi za kutosha”
Lanlan aliogopeshwa mno na mlipuko wa bunduki na alitetemeka huku akiendelea kulia kwa kwikwi.
“Little girl ,, kama hutotuambia mapema ,,, mama yako atakufa mbele yako ukisikia mlipuko kwa mara ya pili”Aliongea lakini Edna aling’ata meno yake kwa hasira na kumwangalia Lanlan.
“Lanlan usije kuwaambia , ukifanya hivyo sitokupenda tena na nitakuacha”Lanlan aliekuwa akitaka kuongea palepale alifumba mdomo wake kwa woga mara baada ya kusikia maneno ya mama yake
“Mimi sijui”
Alijibu tena huku akiwa na wasiwasi mkubwa wa kitoto , alikuwa akitia huruma kwani sura yake ya kitoto ilibadilika na kuwa nyekundu huku akiishia kumwangalia mama yake kwa hali ya wasiwasi , aliogopa kuachwa na mama yake tena kwa mara ya pili na kuishi maisha magumu.
“Pumbavu kabisa … “Aliongea yule bwana mwenye chunusi na palepale alimsogelea Lanlan kwa ajili ya kumpiga kibao
Alikuwa akijua nguvu zake hivyo hakutaka kumlembesha na kutumia nguvu zake zote
Lanlan kwasababu nguvu zake zilikuwa zimezuliwa hakuweza kujizuia na bonge la bao lilimpata na kumtoa aliposimama na kwenda kujipigza kwenye ukuta puu.
“Hapana..!!!”
Edna alijikuta akitoa ukulele huku akiwa kama anataka kuzimia kwa maumivu .
“Ni mtoto bado , kwanini umemua kumpiga hivyo”Aliongea huku akihisi ni kama kuna mtu anaejaribbu kuwasha moto kwenye moyo wake
Ijapokuwa Lanlan alikuwa ni mwenye uwezo mkubwa lakini kibao kile ni kama maumivu yamemuingia yeye, kilio chake cha kuomba msaada kilijaza eneo lote.
“Huogopi kufa tu , Madam Edna wewe ni mbishi aisee , siwezi kujizuia tena . nimesikia binti yako ni wa kuasili hivyo hana damu ya Roma kama ni hivyo nadhani hutolaumu sisi kumpa mateso mpaka kifo kimkute mbele yako , isitoshe maisha yako yana thamani kubwa kuliko ya kwake”Baada ya kuongea hivyo alimsogelea Lanlan alipolala na kisha aliinua buti lake la kijeshi na kumbutua Lanlan na alikuwa na nguvu mno kwani Lanlan aliamba ambaa kama mpira na kwenda kutua kwenye mguu wa mwanajeshi mwingine na bwana mwingine mara baada ya kuona Lanlan kamfikia alitoa tabasamu la kifedhuli na yeye kujiandaa kuachia pigo lake.
Edna alishindwa kuvumilia na kusimama akiaka kujaribu kuwazuia lakini kwa bahati mbaya kadri alivyokuwa akijitahidi hakuweza hata kumfikia na aliishia kurudishwa kwenye kiti kwa nguvu na mikono ya majambazi wawili.
“Angalia kwa makini , haya ndio matokeo ya wewe kuuziba mdomo wako , mtoto wako anakwenda kufa kifo kibaya sana”
Jamaa yule mwingine mara baada ya kusema na yeye alimbutua tena Lanlan tumboni .
Lanlan masikini alijikuta akijipigiza kwa mara nyingine kwenye ukuta , hakutoa kilioa na aliishia kujikunyata tu kwa maumivu.
Edna alitoa kilioa mpaka koo linamkaukia na aliishia kuangalia tu namna ambavyo mtoto wake alikuwa akisurubiwa
“Pumbavu asiee hichi kitoto kina maajabu yake, bado tu kipo hai”
“Inawezekana akawa ni mtoto wa yule mwanaharamu kweli na hatuambiwi , mwili wake sio wa kawaida kabisa”
“Ni kajibonge na ukipiga kama vile ni mpira , hebu nijaribu na teke langu nione kama atavumilia”Aliongea bwana mwingine.
“Toto zuri , una bahati mbaya sana Roma Ramoni kuwa baba yako , unastahili hiki”Aliongea na pale walianza kumshambulia kwa mateke kwa zamu na kila pigo ni kama maumivu alikuwa akiyasikia Edna.
“Acheni .. acheni ,,, msipige tena binti yangu”
Machozi yaliishia kumtoka na kuloanisha mashavu yake , alikuwa kwenye maombolezo ya hali ya juu kiasi cha kushindwa kupumua ni kama kilio chake analalamika kwa Roma kuondoka na kuwaacha wenyewe.
Kila kitu ndani hapo kilianza kupotea katika macho yake , macho yake yalianza kuingiwa na ukungu huku mapigo yake ya moyo yakianza kudunda kwa kasi sana kiasi kwamba kama upo karibu yake ungeweza kusikia.
Mshipa wa damu maarufu kama ‘Jagular Vein’ na wenyewe ulianza kucheza cheza na akili yake ni kama ilihama katika mazingira hayo na kuingia katika ulimwengu uliojitenga.
Muda ule Lanlan alikuwa amechafuka na aliishia kukaa kwa kunyoosha miguu huku akimwangalia mama yake kwa huruma na aliishia kutema damu nyingi katika mdomo wake na kuchafua nguo zake.
Bwana mwenye chunusi alikuwa na roho ya kinyama kwani bila huruma alimsogelea Lanlan na kumlaza chali na kupeleka buti lake la kijeshi na kuweka mguu juu ya tumbo lake.
“Unaonaje Madam ,,, binti yako atakufa kweli kama huto…”
Aliijikuta akishidwa kuendelea na sentensi yake mara baada ya kuona kuna kitu ambacho hakikuwa sawa kuhusu Edna.
Kichwa chake kiliangalia sakafu na muonekano wake haukuonekana zaidi ya kivuli pekee .
Sio kwake tu kwa kila mtu aliekuwa hapo ndani alishituka , kwani waliweza kuhisi ubaridi zaidi ya kawaida huku hali ya hewa ikibadilika .
Wale watu waliokuwa wamemshikilia Edna wenyewe walianza kutetemeka kutokana na baridi kali iliokuwa ikisambaa katia miili yao , majambazi yote kimya wakiangalia nini kinataka kutokea.
Dakika chache tu ghafla eneo lote lilijaa mkandamizo wa hewa ambao uliwafanya kutetemeka na kukosa pumzi kwa wakati mmoja , ilikuwa ni kama vile kuna moshi uliokuwa ukiingia kutoka nje kutokana na jengo hilo kuungua.
Hatimae Edna aliinua uso wake na kuwaangalia , uso wake ulikuwa ni wa kirembo sana lakini kwa wakati mmoja macho yake yalikuwa tofauti, ni kama vile hakuwa mtu kamili kwani kiini cha macho ni kama kilikuwa kinafifia.
Edna aliwaangalia watu wale kwa dharau kubwa huku akionyesha nia dhahiri ya kimauaji , ni muonekano ambao licha ya wote hapo ndani kuwa wanajeshi msisimko wake uliwatisha.
“Mnastahili kufaa…”Sauti ambayo ni kama vile sio ya kwake ilisikika.
“Acha kutuogopesha, wewe ni..”
Kabla hata hajamaliza sentensi yake Edna palepale alichukua hatua , mikono yake ilijikunja katika angle isiokuwa ya kawaida na wale watu wawili waliokuwa wakimshikilia walijikuta wakipokea mapigo matakatifu makali sana katika matumbo yao na kiatu cha skuna.
Licha ya kwamba walikuwa na mazoezi lakini maumivu yake hayakuweza kuwa ya kuvumilika.
Ilitokea ndani ya sekunde tu kwani walianza kuvunywa mikono yao na ndio wakaunganishiwa na teke.
Edna hakuishia pale tu alikuwa fasta sana kama upepo kwani palepale aliweza kubeba bastora zao na spidi ya kukokiwa na risasi kuruhusiwa ilikuwa ni kubwa mno kiasi kwamba wale wachina waliokuwa kulia kwake walishindwa kuchukua hatua kwani palepale vichwa vyao vilifumuka baada ya kulengwa na shabaha isiokuwa ya kawaida.
Dakika ambayo wale wengine akili zao za kushambulia zinawarudia walikuwa wamechelewa kwani aliteleza kama jini na kumdhibiti mtu mwingine kwa kumvunja shingo na kumbeba juu juu na kurushia waliokuwa mbele yake ambao walikuwa wakielekeza bastora kuelekea kwake , ilikuwa ni staili ya kuwachanganya na palepale kwa spidi alishafikia na mmoja alikula mtama wa sarakasi huku mwingine akivunjwa shingo kwa staili ya kikatili mno.
Bahati mbaya sana kuna jamaa sijui kwanini kamua kuja na upanga, pengine ni sifa kwani hakuonekana kuweza kulitumia katika hilo eneo kwani ile anashtuka ashatenguliwa mkono na panga kuchukulia na koromeo lishakatwa ni matendo matatu yaliofanyika ndani ya sekunde tatu.
Ndani ya dakika chache walibakia wanne tu ambaye ni Bwana mwenye chunusi na mwenzake mwenye sare za kipolisi na wawili wengine na wawili wale wote kwa pamoja walimsogelea na ile wanamkaribia waliweza kuhisi upepo tu ukiwapita na mmoja alishika koromoe huku mmoja akishika upanga uliongia mgongoni na kutokezea kifuani eneo la moyo na kabla hata hajapata nafasi ya kujua upanga umemchomaje alikula teke la mgongo na upanga ukachomoka kwa nguvu na akadondokea mbali kama furushi huku damu kama bomba la maji ikiruka na kwa spidi kubwa Edna alishamfikia bwana mwenye chunusi na polisi mwenzake na palepale ni kama wamesogelewa na Israeli mtoa roho.
Staili ambayo alikuwa akitumia kupambana ilikuwa sio ile ya kubahatisha , ilikuwa ni kama ya ninja ambaye amefundishwa kuua tokea akiwa mdogo , ilikuwa ni ya kiasili kabisa kama mtu anazaliwa nayo.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 561.
Hata kwa Faridi mwenyewe alishangazwa na kuhusishwa katika swala hilo na mshangao wake ulimfanya Roma aamini kwamba Faridi hakuwa akijua chochote na hakuwa akiongea ukweli.
“Nadhani mtu ambaye amefanikisha hilo sio mdogo kwako kwa namna ambavyo amefanikisha kukuchezea akili na wewe kushindwa kumfahamu”.Aliongea Farid.
Roma aliona hakika mtu huyo hakuwa wa kawaida kabisa , kama kweli ameweza kutengeneza sura ya udanganyifu na kumuigiza Farid basi kweli mtu huyo ni wa levo nyingine na hapo hapo akili yake ilijiambia huenda aliemfanyia hivyo ni Raphael.
Hermes pekee ndio aliekuwa na uwezo wa kutengeneza Illusion na mtu yoyote asione utofauti, kama ingekuwa ni mtu wa kawaida ambaye alicheza na akili yake basi asingeweza kumdanganya kijinga.
Roma alikumbuka kipindi wakati alipotaka kumuua Denis ni Hermes ambaye aliingilia kwa kumtengenezea udanganyifu kwa kumuona Denisi akimuua mama yake mpaka kughairisha.
Alijiambia kama ni Hermes basi inaleta maana kutokana na uwezo wake kulingana na wa kwake , kwa kutumia siraha yake tu maarufu ya kichawi iliofahamika kwa jina la Caduceus anaweza kuwafanya hata ndugu zake kuwa katika hali ya usingizi wa ndoto.
“Nadhani nishajua nani kafanya hivyo lakini nashindwa kuelewa nia yake halisi”Aliongea Roma na Farid alitingisha kichwa kuelewa .
Balozi Ramadhani aliondoka kuelekea Dodoma na kazi iliokuwa inabaki ni Roma na Edna kutafuta njia ya kusafisha jina la Sophia na kutuliza hali ya hewa.
Mchana wote Edna alikuwa bize kushughulika na swala hilo , Roma ndio ambaye alipaswa kushughulika na swala hilo kama mkuu wa kampuni ya Vexto Media lakini kwasababu yeye amehusishwa na pia lilimuhusu Sophia aliona aingilie majukumu ya Roma kumsaidia.
Ingekuwa rahisi kudili na swala hilo kama watu waliokuwa wakisambaza ni waajiriwa wa kampuni flani , lakini kwasababu ni watu binafsi waliokuwa wakisambaza na kuongezea chumvi ilimfanya Edna kushindwa kuzuia swala hilo mara moja na kukosa kabisa namna ya kudili nalo moja kwa moja.
Kilichomchukiza zaidi watu walitumia uzushi huo kupata ‘attention’ kutoka kwa watu ili kufanya peji zao mtandaoni zifatiliwe kwa wingi.
Roma alijikuta akichukia mno kwa jinsi ambavyo Edna alikuwa akihangaika kudili na swala hilo.
Baada ya muda wa kazi kuisha Roma alimlazimisha Edna kuondoka nae kurejea nyumbani.
Edna alikuwa akipanga kufanya kazi mpaka jioni ili kushugulikia hilo swala lakini alishindwa kumshawishi Roma kumuacha ofisini na mwishowe akaamua kumkabidhi majukumu yote Benadetha kushughulika nayo.
Muda wa kutoka kazini ni kama waandishi wa habari walikuwa wakimsubiria kwani walijaa katika eneo la kuingia ndani ya kampuni hio wakiwa na kamera zao pamoja na vifaa vya kurekodi sauti , walionekana walitaka kusikia chochote kutoka kwa Edna.
Roma alimwagiza Recho kuachana nao na asitokee mfanyakazi yoyote kuongea chochote , hata hivyo hawakuwa na cha kuongea kwani kinachoendelea hakikuwa na ukweli wowote na hata kama wakanushe hakuna ambaye angeamini na wangeendelea kuuliza maswali yasio na msingi , lakini kubwa zaidi Edna hakuwa mtu wa kupenda kuongea ana kwa ana na vyombo vya habari kwani hakupenda sana umaarufu.
Ilibidi wapitie moja kwa moja kwenye Basement katika eneo la maegesiho na baada ya kuingia kwenye gari , Roma aliliondoa na kulipeleka moja kwa moja mpaka nyumbani.
Baada ya kufika nyumbani Lanlan alikuwa tayari ashatoka shuleni na alikuwa akiangalia katuni , baada ya kuwaona wazazi wake wamefika nyumbani aliwakimbilia na kumsalimia mmoja mmoja kwa kuwakumbatia na kisha akakimbia na kurudi kwenye sofa.
Alionekana kukolea kile ambacho alikuwa akiangalia na Edna na Roma waliangaliana na kuishia kutabasamu.
Edna kidogo alijisikia vizuri mara baada ya kuoga na kupata chakula cha usiku pamoja na familia yake .
Waliangalia Tv Pamoja mpaka wakati ambao Lanlan alipotelea usingizini na Qiang alimbeba na kumpeleka juu kulala wakati huo Edna alimwambia Roma amfuate hadi kwenye Yadi kuna kitu waongee.
Roma na yeye alikuwa akitarajia Edna kumwambia kile ambacho anafikiria , kwani alimuona wakati wote akiwa ni mwenye mawazo.
Baada ya kukaa kwenye viti maalumu vilivyoweka kwa nje katika Yadi , Edna alivuta pumzi nyingi na kisha kumgeukia Roma.
“Hubby si ulishaniambia utanitimizia chochote na kunisikiliza ili mradi tu sikulazimishi kuachana na wanawake wako?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushangazwa na kauli yake na kujiuliza inatokea wapi.
“Nilisema hivyo lakini sikumaanisha katika kila ombi”
“Kwahio unavunja ahadi yako?”
“Kama utaomba kuniacha ulifikiri nitaweza kukubaliana na ombi lako , sijali kama utachokoza mtu mwingine kwani nitakusapoti muda wote”
“Nilijua tu utasema hivyo”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma kwa jicho la pembeni.
“Kama ni hivyo basi naomba nikuulize , je ni kweli kwamba hutonipinga kwa maamuzi yoyote nitakayoyafanya yanayohusiana na kampuni ya Vexto?”
“Bila shaka , kampuni imeasisiwa na wazazi wako na wewe ni urithi wako , sina mpango kabisa wa kuingilia taaluma yako pamoja na uendeshaji wa kampuni”Aliongea Roma bila ya kufikiria na kumfanya Edna kuvuta pumzi nyingi na kuzishsuha.
“Vipi kama nitasema napanga kujiuzuru na kumchagua mtu mwingine kuwa CEO wa kampuni na mimi kumsaidia kwa pembeni? , Je utasapoti maamuzi yangu?”Aliuliza na kumfanya Roma kushangazwa na swali lake hilo.
“Niliweza kuhisia haya ndio maamuzi unayotaka kuchukua , lakini je ndio kitu unachopenda kufanya?”
“Nimechoka , sina nguvu tena za kudili na maswala haya zaidi na isitoshe na mimi ni binadamu, naweza kuonekana mkatili kwa watu wa nje lakini sijui namna ya kudili na marafiki zangu pamoja na familia”
“Unafanya haya yote kutokana na kilichomtokea Sophia, si ndio?”
“Hilo ni moja , iwe ni Dorisi au Nasra wote wanashikilia nafasi muhimu katika kampuni na siwezi kufanya kazi bila wao , lakini kila ninapofikiria uhusiano wako na wao , moyo wangu unakosa utulivu , kwasababu ni wafanyakazi wenzangu najitahidi kujizuia na kujiambia hakuna kitu kibaya kitakachotokea , lakini je unafikiri ni rahisi kwangu?”
Roma alijikuta akikosa neno , alijua Edna ashapotezea mambo hayo muda mrefu kumbe alikuwa akijizuia muda wote huo.
“Pia kama ningekuwa sina uhusiano wowote na Sophia huenda ningeweza kufanya maamuzi ya kumzuia kutoonekana hadharani kwa muda kidogo, lakini siwezi kufanya hivyo kwani mimi ni Bosi wa kampuni na itaonekana namnyanyasa nikifanya hivyo , ukweli sijui namna ya kudili na hili swala nahisi kuchoka…”
Kilichokuwa kikimpa hofu zaidi Edna ni juu ya uhusiano wa Roma na Nasra pamoja na Dorisi , alifikiria je kama itafahamika katika jamii kwamba na wao wana mahusiano ya kimapenzi na mume wake si itamchafua zaidi na zaidi , alichukulia tu kwa mfano tukio la Sophia lilivyokuwa likimuumiza kichwa ndio maana alifikia maamuzi ya kutaka kuachia ngazi.
“Naelewa unachojisikia lakini hata kama utajiuzuru na kutoa nafasi yako kwa mtu mwingine hawawezi kufanya chochote na watu watasema ulikimbia”
“Najua, ndio maana mpango wangu baada ya kijiuzuru ni kuita waandishi wa habari na kisha nitawalezea uhusiano wangu na Sophia na kuwaambia hahusiki katika uzushi unaosambazwa . ni sababu nzuri kujiuzuru kwa kuwajibika ili kulinda taswira ya kampuni”
“Kwannini unataka kuwajibika , watu walioanzisha huo uzushi ndio ambao wanapaswa kuwajibika”
“Lakini angalau kuwepo na mtu wa kubeba lawama zote , sina mpango wa kuendelea kufanya kazi na kujiuzuru ndio kitu pekee ambacho naweza kufanya kwa ajili ya Sophia”
Roma alona kabisa maamuzi ambayo anataka kuchukua Edna ni ya kijinga na akifanya hivyo kwasababu ya Sophia aliamini kabisa ingemfanya na Sophia mwenyewe kukosa ujasiri wa kujitokeza hadharani tena.
Muda huo wakati wakiongea Bi Wema aliwafuata huku akionekana kuwaita.
“Miss kuna taarifa huku , njooni muone , kuna habari mbaya”Aliongea Bi Wema kwa kupaniki.
********
Muda huo huo ncha ya kaskazini mwa dunia , ndani ya maabara kubwa iliotengenezwa na Yan Buwen, hali ya hewa haikuonekana kuwa nzuri.
Vifaa vyote vya maabara vilionekana kufanya kazi , huku Skrini zikionyesha baadhi ya data ngumu kuelekeweka kupanda na kushuka.
Katika meza kubwa ya kisasa kama zile za hospitalini kulionekana mirija mingi ikiwa imeunganishwa katika mwili wa binadamu.
Upande wa kulia na kushoto wa meza hio kulikuwepo baadhi ya vifaa vilivyokuwa na maumbo ya ajabu ambayo ndani yake kulikuwa na vitu kama maji maji.
Juu kabisa ya mwili wa binadamu uliolazwa kwenye meza hio kulikuwa pia na kifaa cha muundo wa kipekee ambacho ndani yake kulikuwa na mwanga mkali wa kung’aa uliokuwa ukionekana huku ukizunguka zunguka , ilikuwa ni nishati ambayo ilionekana kuunganishwa moja kwa moja na mwili wa binadamu huyo.
Mtu wa ngozi nyeusi alielazwa katika meza alikuwa uchi wa mnyama huku miguu yake ikiwa imebananishwa na kufungwa kwa kamba ngumu maalumu ili kumzuia asisogee.
Alikuwa ni Denisi , ijapokuwa alionekana kuwa na fahamu lakini ilionyesha muda wowote angezimia, yote hayo ni kutokana na kwamba nishati iliokuwa imewekwa juu yake , ilionyesha kujiandaa kuuvamia mwili wake .
“Punguza wasiwasi , utakuwa sawa muda si mrefu , isitoshe hili linafanyika kwa faida yako”
Mwanaume aliekuwa pembeni ya meza hio ya kufanyia operesheni alionekana kutabasamu kifedhuli , alikuwa amevalia koti la maabara ambalo tayari lilikuwa na madoa mengi na alionekana ana muda mrefu hakuwa amenyoa ndevu zake kwani zilionyesha kuota kwa wingi.
Josesph Bikindi muonekano wake ulirudi na kuwa kama ule wa miezi kadhaa nyuma wakati alipokuwa akifahamika kwa jina maarufu la Lekcha.
Nguo pekee ambayo ilikuwa imeusitili mwili wake ni koti la maabara na alikuwa na mwonekano wa tofauti kidogo , kwani alionyesha kukonda tofauti na alivyokuwa siku kadhaa nyuma kabla ya kuingia katika mabara hio ya marehemu Yan Buwen.
Katika eneo la kifua chake karibu na moyo kulikuwa na kitenesi cha nishati ya Anti- matter ambayo imeshikiliana na mwili wake na huenda Roma angekuwepo moja kwa moja angejua kitenesi hicho cha nishati ni jiwe la kimungu.
Kama ilivyokuwa kwa Yan Buwen , Lckcha alitumia teknolojjia ile ile ilioachwa na kuunganisha jiwe la kimungu na mwili wake , lakini utofauti tu ni kwamba teknolojia hio yeye alikuwa ameindeleza kwa viwango vya juu na kumfanya kuwa na uwezo ambao ni mkubwa zaidi kuliko aliokuwa nao Yan Buwen.
“Unataka kufanya nini?”Alipaniki Denisi mara baada ya Lekcha kuanza kuchezesha lile boksi ambalo lilikuwa limejaa nishati.
“Hehe.. hutaki kuwa na nguvu , hii ni gunduzi yangu mpya nilioweza kuifaikisha kupitia muendelezo wa teknolojjia ya Yan Buwen…”Aliongea huku akiwa na tabasamu la kejeli kama kawaida yake.
“Hiki ni kifaa nilichokipa jina la ATD(Ant -matter transfomation device) ninachopaswa kufanya ni kukiwasha kwa kutumia jiwe la kimungu na kitaibadilisha nishati yote isio ya maada kwa kuwa na nguvu kwa zaidi ya mara mia moja, kinaweza pia kutumika kufuta Genome za mwili wako na kama kitaonyesha mafanikio kwako basi na kwangu kitafanya kazi na yatakuwa mafanikio ya teknolojia kubwa ya kuwasha link ya vinasaba vya mwili wangu na kuungana na muundo wa viambata vya nishati ya Ant-matter na kwanzia hapo nitakuwa na uwezo mkubwa wa kufanya ninachotaka”
“Unamaanisha nini?”Aliuliza Denisi kwa hofu.
“How would I know ..,, according to Yan Buwen idea the transformation on the test subject is still unknown . Well no matter how it turned out to be , I’ m sure I will benefit from it ,you won’t understand even if I explain it to you”Aliongea akimaanisha kwamba hawezi kujua kwasababu mchakato wa mabadiliko kwa mtu anaejaribiwa haujulikani , lakini anaendelea kusema licha ya matokeo ya aina yoyote ana uhakika kwamba atafaidika nyao hivyo hata kama amwelezee kila kitu hatoweza kumuelewa.
“Kwahio unataka kunitumia kama chombo cha majaribo , kwanini unataka kunifanyia hivyo , sisi si marafiki?”Aliuliza Denisi kwa wasiwasi mkubwa lakini Lekcha aliishia kucheka sana.
“Umesema marafiki, Wewe?.. wewe ni mbwa tu wangu , unafikiri unafaida kubwa kuliko yule malaya ?”
Baada ya kuongea palepale aliwasha jiwe la kimungu kwa kutmia akili yake tu na palepale mwanga ulizidi kufunika maabara hio baada ya mlipuko wa mng’ao wa mwanga wa ajabu uliotoka katika jiwe la kimungu.
Kila mlipuko wa mwanga ule wa Ant matter unavvyotokea uliakisiwa na kifaa ilichofungwa kwa kuning’inizwa juu ya mwili wa Denisi na kisha palepale kifaa kile cha ATD kilikuza nguvu ya mwanga ule na kisha kumulika katika mwili wa Denisi.
Lekcha alirudia kwa mara ya pili na awamu hio kulitokea mlipuko mkubwa zaidi wa mwanga na kisha ukasharabiwa wote na kile kifaa na kisha ukaelekezewa katika mwili wa Denisi na kumfanya asionekane kabisa kwani kifaa kile kilimulika mwili mzima mpaka kwenye kucha za miguu.
Lekcha alizidi kuinua mikono yake na kuruhusu nguvu ya jiwe la kimungu kumezwa na vifaa na kisha kuelekezewa katika mwili wa Denisi , alirudia mara nyingi mpaka ikafikia wakati sasa mwili wa Denisi ulianza kuonekana kama vile unatoa shoti za umeme wa rangi ya bluu.
Aliendelea vilevile bila kuacha , ilionekana matokeo anayoyataka bado, aliendelea kutoa nishati isio maada kumuingia Denisi huku makelele ya milipuko ya umeme kama vile nguzo inapiga shoti ilisambaa chumba kizima , lakini bado Lekcha hakuacha kufanya anachokifanya alizidi kuruhusu nishati ya ant-matter kuuvaa mwili wa Denisi kwa muda mrefu na ilifikia mwili wa Denisi hakuonekana kabisa.
Ni ndani ya nusu saa tu kulitokea mlipuko mkubwa mno kiasi kwamba kwa macho ya kawaida yasingeweza kuhimiri mn’gao wake kwani ulimkuwa mkali sana wenye wavelength za kuumiza macho.
Lekcha alirudi nyuma na kuacha kile kitendo alichokuwa akiendelea nacho na kisha macho yake yote aliangalia katikati ya maabara hio kama vile mtu anaetegemea mtu kutokea katikati ya mlupuko huo wa mng’ao.
Ni ndani ya dakika kama kumi na tano tu , ule mng’ao ulianza kujikusanya taratibu taratibu na kuanza kupungua na mpaka wote unaisha Denisi hakuweza kuonekana wala ile meza haikuonekana, ni kama vile imeyeyuka na kitu pekee kilichobakia ni mpira wenye kung’aa uliobakia sakafuni, ulikuwa ni mpira wa nishati , huenda ni nishati ya nguvu ya Ant-Matter.
Lekcha alijikuta akijawa na mshangao huku uso wake ukiwa katika hali ya tabasamu pana na alisogea kwa haraka.
Na kwa kutetemeka mikono aliunyanyua ule mpira wa nishati wenye mwanga uliokuwa ukicheza.
Baada ya kuusihikilia mkononi aliuachia hewani na palepale hakudondoka chini bali ulielea na kisha ukamsogelea katika eneo la kifua chake upande wa jiwe la kimungu.
Ilikuwa ni kama lile jiwe la kimungu lilikuwa likiuvuta kwani baada ya mpira ule wa nishati kufika katika kile kifua ulimezwa wote na kupotelea ndani ya mwili wa Lekcha.
“Haha.. I did it … I did it”Aliongea kwa furaha huku mwili wake ukianza kutetemeka , alikuwa akihisi kabisa seli za mwili wake zilikuwa zikicheza na ngozi yake alihisi ikiwa na muwasho usio kuwa wa kawaida , ni kama vile mwili wake umegeuka kuwa kidonda na sasa ulikuwa ukipita katika hatua ya kupona.
Palepale alitupa koti lake chini na kubakia uchi , lakini baada tu ya kutoa lile koti alidondoka chini na kuanza kutetemeka kwa kurusha miguu kama vile alikuwa mgonjwa wa kifafa na ghafla tu jiwe lililokuwa katika kifua chake lilitoa mwanga mkali kwa sekunde tu na kisha ukapotea na palepale mwili wa Lekcha ulianza kupitia mabadiliko kwa kasi kubwa mno kama vile ni kiumbe cha ajabu kwani hata nywele zilianza kubadilika..
Baada ya dakika tano Lekcha mwili wake ulibadilika na alifanana kwa kila kitu na Denisi , alikuwa ni Denisi mtupu.
Baada ya kutulia kabisa na kuhisi mwili wake haupo kwenye maumivu na ule muwasho wa mwili umeisha palepale alisimama na kisha akakisogelea kioo.
“Denis”Aliongea huku akitabasamu kifedhuli huku akiwa uchi , na alianza kujikagua mwili mzima akiwa kama mtu asieamini kama ameweza kubadilika na kuuvaa mwili wa Denisi.
Lekcha muda uleule hakusubiri tena hata sekunde kwani alipotea ndani ya maabara ile kama jini na alipokuja kutokezea ni nje kabisa juu ya barafu na ile anatua tu , vivuli vya watu wawili vilivyoakisiwa na mwezi vilionekana,Alikuwa ni Kizwe pamoja na Desmond.
“Denisi..!”Aliita kizwe kwa mshango na kisha alimpita Lekcha kwa mbele na kumkagua.
“Little Cripple dear , you finally succeded should I call You Denis Senga now?”
“Mpenzi wangu kilema naona umefanikiwa , vipi nikuite Denisi Senga sasa?”Aliongea Kizwe kwa kingereza.
Lekcha palepale alimsogelea kwa spidi na kabla hata Kizwe hajaelewa alijishutikia akiwa kwenye mikono ya Lekcha mwenye muonekano wa Denisi.
Kizwe alikuwa ashazoea namna ambavyo Lekcha alikuwa akimfanyia kila anapotaka huduma kutoka kwake na palepale hakuleta ubishi na alimsogezea mdomo mwanaume huyo na wakaanza kubusiana.
Desmond alisimama bila hata ya kujali kile kinachoendelea , hata hivyo licha ya kwamba mama yake alifufuliwa lakini hakuwa mama yake anaemjua , alionekana ni mtu mwingine kabisa na hakuwahi kumkubali.
“Mmefanikuwa kupata chochote?”Aliuliza Joseph Bikindi au ukipenda mwite Lekcha.
“Ni kama nilivyotarajia Jeremy ameita ndugu zake kutoka ujinini , kuna mwanaume mmoja anaeitwa Nix pamoja na Gesha , wote wana uwezo wa mafunzo ya mbingu na ardhi”Aliongea Kizwe.
“Vizuri .. tutachukulia swala hilo kwa manufaa kwetu”Alijibu Lekcha.
“Lekcha kwanini usiuvae mwili wa Jeremy na ukawa raisi wewe?”Aliuliza Kizwe.
“Acha ujinga wewe mwanamke , unafikiri hao majini ni rahisi kushindana nao , ninaweza kuwamaliza ndio lakini vipi kuhusu huko wanakotokea , unafikiri nitaweza kuwashinda wakija duniani kupambana?, kwasasa mimi ni Denisi na lazima nichukulie mwonekano wangu kama fursa”
“Unamaanisha …”Kizwe alitaka kuongea lakini palepale alijikuta akitoa tabasamu pana kama vile taa imeweshwa kwenye akili yake na kugundua anachopanga Lekcha .
“Kilema , hakika wewe ni mwenye akili sana”Aliongea Kizwe huku akitoa kicheko cha kebehi na Lekcha alimwangalia kwa kejeli mwanamke huyo na kisha akanusa nusa shingo yake lakini hakuonyesha tamaaa ya kumuhitaji Kizwe tena
“Clelia Allisanto” Jina hilo lililipuka kwenye akili yake na palepale alimtua chini Kizwe na kuonyesha tabasamu.
“Tumetumia muda mwingi sana kukaa huku Ncha ya Kaskazini…. Kituo chetu cha kwanza ni nchini Tanzania, Tuondokeni kazi ya kulipa kisasi imeanza rasmi”Aliongea Lekcha na palepale wote kwa pamoja walipotea.
Ilionekana hata Desmond alikuwa na mabadiliko makubwa kwani hakuwa wa kawaida tena.
Muda wote ambao Lekcha alikuwa akijibadilisha kuwa Denisi alikuwa akiangaliwa na mtu alievalia Mask na mavazi meusi , alikuwa ni bwana yule ambaye alipigana na Roma nchini Korea na Australia.
Lekcha hakuweza kumuona bwana huyo kutokana na kwamba alikuwa akitumia nguvu za kijini kujificha na hata baada ya Lekcha kuondoka ndani ya maabara alimfuata kwa nyuma.
Muda uleule wakati Lekcha na wenzake walivyoondoka , akitaka kugeuka na yeye kuondoka hilo eneo , kivuli cha mtu mwingine kilionekana nyuma yake .
“Your Highness Athena , you’re here”Aliongea kwa heshima huku akiinamisha kichwa chake na Athena alitingisha kichwa tu na kisha akaongea.
“He did it..”Aliongea kwa sauti yake ya kike akimaanisha , Amefanikiwa?
“Yes as you said , he activated the genetic link technology and ate Denis .He Transfomed into Denis and his power had improved greatly”Aliongea akimaanisha kwamba ameweza kufanikiwa kuwasha teknolojia ya Genetic Link na kummeza Denis, Amebadilika na kuwa Denis na nguvu zake pia zimeimarika sana.
“He is still slower , looks like he’s not as good as Yan Buwen”Aliongea akimaanisha kwamba bado yupo taratibu , na inaonekana hayupo vizuri zaidi kama Yan Buwen.
Kwa kauli yake hio ilionyesha kifo cha Yan Buwen kilikuwa hasara kubwa kwake.
“Kwa maoni yangu , Yan Buwen anaweza kuwa na kipaji na uwezo mkubwa wa akili lakini Joseph ana tamaa kubwa halafu ni mkatili , nina uhakika anaweza kuwa tishio kwetu muda si mrefu , sijui kwanini unamuacha afanye atakavyo , si tayari amefanikisha misheni ya kuendeleza utafiti wa namna ya kuwasha teknolojia ya Genetic link?”Aliuliza Bwana mwenye Mask.
“I need the results from his research but he still has values , stop asking about it”
“Nilihitaji matokeo kutoka kwa tafiti yake lakini bado ana thamani , acha kuuliza kuhusu hilo”Aliongea Athena.
“Yes Your Highness”Aliongea bwana mwenye Mask.
“Hamisha vifaa vyote ndani ya maabara katika sehemu salama na haribu kila kitu , baada ya hapo nenda nchini Tanzania na endelea kumfatilia , hakikisha Roma hakuoni asije kukumeza maana sitoweza kukukoa tena”Aliongea na kumfanya Bwana mwenye Mask kukakamaa mwili, baada ya kukumbuka tanuru la Maafa(Chaos Cauldron).
Baada ya kutingisha kichwa kuitikia palepale aliondoka hapo na kuelekea katika maabara kufanyia kazi maelekezo aliopatiwa , kwa uwezo wake ilikuwa rahisi sana kuhamisha baadhi ya vitu muhimu vyote katika sehemu salama ndani ya muda mfupi tu.
Lakini hata hivyo alizidi kumuogopa Athena , hio yote ni kutokana na kwamba mipango yake ilikuwa ipo kimahesabu zaidi .
Licha ya kuwa na uzoefu wa karne lakini alishindwa kabisa kufahami ni kipi anafikiria na mpango wake unaofuata ni upi.

SEHEMU YA 562.

Hakika ilikuwa habari mbaya sana kwa Edna na Roma kulingana na juhudi kubwa ya kumfanya Sophia kuwa maarufu.

Taarifa ambayo ilikuwa ikiwasilishwa katika runinga ilionekana ni ambayo Sophia alikuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dodoma.

Kitendo cha Sophia kufanya ‘Press conference’ bila ya kushirikisha kampuni inayomsimamia kilimshangaza Edna na Roma kwa wakati mmoja , mbaya zaidi haikuwa kikao na waandishi wa habari kukanusha tu uvumi bali alienda mbali zaidi kutangaza jambo kubwa zaidi.

Katika kikao hicho kwanza kabisa alikiri kwamba Edna ni dada yake na hata kuanzishwa kwa lebo ya kusimamia wasanii chini ya Vexto media ilianzishwa kwa ajili yake.

Baada ya kuongea hivyo waandishi hawakuonyesha hali ya kuridhika na kutaka kujua ukweli wote kuhusu yeye na Roma kama wana uhusiano wowote na hapo ndipo Sophia aliharibu kabisa kwani alikiri kwamba alikuwa na hisia za kimapenzi na Shemeji yake , lakini hakuwahi kuweka hisia zake wazi wala kujihusisha nae kwani ni mume wa dada yake.

Kauli ya Sophia ilimshutua mno Edna na hakutaka kabisa hata kuendelea kuangalia kile kilichokuwa kikiendelea kwani palepale aliondoka na kusema anaenda kulala.

Roma alishindwa kuongea chochote kutokana yeye ndio chanzo ya kila kinachoendelea hivyo alimwangalia mke wake kwa huzuni akipandisha ngazi kwenda juu kwa ajili ya kulala.

Sophia mara baada ya kutoa kauli yake hio alitoa tangazo Rasmi kwamba anaachana na maswala ya Mziki na Usanii.

Ilikuwa kauli ambayo ilishangaza kila mmoja ambaye alikuwa ni shabiki yake na hata waandishi wa habari waliokuwa wakiuliza maswali walitaka kujua kwanini Sophia kaamua kufanya maamuzi makubwa ya namna hio ilihali alishatolea swala la uhusioano wake na Shemeji yake, waliuliza je kuna sababu nyingine ya kufanya maamuzi ya kuachana na mziki, lakini licha ya maswali hayo Sophia hakutaka kujibu na alifunga mkutano huo.

Roma aliekuwa sebuleni akiangalia na Bi Wema alijikuta akiwa kwenye mshangao na kushindwa kujua kitu cha kufanya kwa wakati mmoja, alitamani kupotea hapo hapo na kwenda mpaka Dodoma.

Lakini aliona hata kama akianzisha safari hio na kufika Dodoma hakuna ambacho angeweza kufanya kama tu Sophia kaamua mwenyewe kufanya kikao bila kumshirikisha , kuna hisia zilimwambai kabisa Balozi atakuwa amehusika katika hilo.

Mjuda uleule Roma akiwa ni mwenye kuwaza cha kufanya simu yake ilianza kunguruma ikishiria ilikuwa ikiita na alipoangalia namba ambayo inampigia ni mpya na alipokea palepale na alipoweka sikioni na kusikia sauti ya mwanaume aliejitambulisha hapo hapo alijua ni nani ambaye alikuwa akiongea, alikuwa ni Balozi baba yake Sophia.

“Hades nadhani mpaka sasa umeona taarifa?”Sauti ya Balozi ilisikika.

“Nimeona taarifa ndio , lakini kwanini mmefanya maamuzi bila ya kutushirikisha mnajua ni kwa nguvu kiasi gani ambayo Edna mke wangu aliwekeza ili kumfanya Sophia kuwa maarufu”

“Hayo yalikuwa maamuzi yake , nadhani mpaka sasa unaelewa ni upi msimamo wa Sophia”

“Naelewa vipi msimamo wake ilihali sijaongea nae tokea tukio litokee”Aliongea Roma huku sauti yake ikianza kukosa uvumilivu.

“Sophia mpaka sasa hataki kuendelea na maswala ya mziki tena na ninarudi nae Japan, ukitaka kumjumuisha sehemu ya wanawake wako mfuate Japan, nilimleta Sophia kwako sio kwasababu nilitaka umfanye kuwa maarufu bali nilitaka umfanye mke wako wa pili”

“Lakini mziki ni kitu ambacho Sophia alikuwa akipenda , hatukukurupuka kumuingiza katika ulimwengu wa kistaa”

“Una uhakika ndio kitu anachokipenda au unausemea moyo wake?”

“Unataka kumaanisha nini?”

“Hades wewe ni mwanaume kwanini unazunguka zunguka ilihali unaujua ukweli , kama unahitaji kuonana na Sophia kwa mara nyingine umfuate Japan”Aliongea Balozi kitemi na palepale alikata simu yake na kumfanya Roma akijikune kichwa chake na kukosa kabisa cha kufanya.

Siku iliofuata wakati wakipata kifungua kinywa , Roma alionekana kabisa kukosa raha zote , ukweli ni kwamba usiku mzima hakulala kutokana na maamuzi alioyafanya Sophia.

“Sophia karudi Japani?”Aliuliza Edna.

“Umejuaje?”

“Kanitumia meseji jana ya usiku ya kuniomba msamaha kwa kila kitu na kuniambia kaachana na mziki”Alijibu Edna na kumfanya Roma kushangaa .

“Kwanini mimi hajaniambia chochote hata kunitumia tu ujumbe?”Aliongea Roma huku akicheka kicheko cha kukata tamaa.

“Unapanga kwenda kumfuata?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kuwa katika hali ya mshangao kidogo na kushindwa kujibu swali lake.

“Kama unataka kwenda sitokuzuia”

“Najua huwezi kunizuia kwasababu ni Sophia lakini hio ndio sababu pekee ambayo inanifanya nisiende”Aliongea na kumfanya Edna kutoa tabasamu hafifu.

“Hapa hata sijui napaswa kukasirika au kuwa na furaha”

“Usifikirie sana , hakuna ambaye amefanya kosa, baadhi ya vitu katika maisha haviendi kama tunavyopanga lakini haimaanishi kwamba haiwezekani kwa sisi kutosahau , Sophia bado ni mdogo anaweza kusahau kila kitu wakati akiendelea kujifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na Ardhi”

Ndio hata Sophia alikuwa akifanya mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na Ardhi ili asizeeke kama ilivyokuwa kwa wanawake wengine.

Hivyo Roma aliaminig nishati ya akili ambayo ageweza kuipata Sophia moja kwamoja ingemfanya kusahau yaliopita na kuanza maisha mengine.

Roma alivyokuwa akifikiria ni tofuati na Sophia alichokuwa akifikiria , Sophia alifanya mziki kwasababu tu ni sehemu ya kitu anachopenda kwasababu hakuwa na kitu kingine ambacho angeweza kufanya , malengo makuu ya Sophia ni kuwa katika mahusiano na Roma na kadri siku zilivyokuwa zikisonga alikuwa kabisa akikosa uvumilivu wa kuzishinda hisia zake , huenda hata maamuzi ya kuondoka bila kumuaga Roma ilikuwa ni sababu maalumu ya kumfanya Roma kuweza kumkumbuka.

Edna kuna kitu alichokuwa akikiona kutoka kwa Roma na alijua fika hiko ndio kilichomfanya kuwa na mwonekano wa kukosa furaha asubuhi hio.

Baada ya kula kidongo tu aliweka uma na kijiko chini na kisha akamshika Lanlan nywele na kumpa maagizo Qiang Xi kumuwahisha shule na kisha alichukua mkoba wake na kuaga anaenda kazini.

“Kwanini haraka hivyo , kuna jambo la muhimu huko kazini?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Nina miadi na lakini pia kuna vitu vya kuandaa kabla ya kikao”

“Wife ni kweli unapanga kustaafu”

“Ndio , nilishakuambia tayari jana na natarajia utasapoti maamuzi yangu”

“Lakini hauna haja ya kuharakisha kwasabu lazima kwanza uchague nani anakwenda kurithi nafasi yako , Vexto ni kampuni ya kimataifa, sio rahisi kupata mtu mwenye uwezo na ambaye ataweza kuongoza kwa ufanisi kama wewe”Aliongea Roma kushauri na kumfanya Edna kutabasamu.

“Unaweza ukaja makao makuu kama una shauku , nishachagua tayari mrithi wangu na mtu huyo atafika ndani ya kampuni baadae”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa , ijapokuwa alikuwa na hisia kwamba tayari Edna ashachagua mtu wa kumrithi lakini bado ilimfanya kama vile kawekwa gizani kwa mara nyingine.

Ukiachana na mchakato, taarifa ambayo anakwenda kutoa Edna huenda ingewashangaza wengi kwani ni ya ghafla sana , kubadilika kwa CEO wa kampunni kubwa kama hio ni jambo kubwa sana.

Edna alikuwa ashakusanya wafanyakazi wote wa juu wa kampuni siku ya jana kwa ajili ya kikao siku hio na baada ya kufika ofisini aliweza kupewa taarifa na Recho watu wote wamekusanyika katika ukumbi kwa ajili ya kikao.

Dorisi ,Nasra , Recho na Benadetha wote walikuwepo na baadhi ya wafanyakazi waliuliza sababu ya kikao hicho ni nini , lakini hawakuwa na majibu sahihi ya kuwapa kwani hawakuwa wakielewa pia kinachoendelea.

Saa nne kamili Edna aliweza kuingia katika ukumbi wa mikutano, kama kawaida yake akiwa na mwoneknao wa kujiamini na watu wote walisimamama kuonyesha ishara ya kumkaribisha .

Baada ya miaka mingi ya kufanya nae kazi pamoja na licha ya kuwa mdogo ki umri lakini alikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa wafanyakazi wake.

Roma hata yeye alikuwepo , hakuhudhuria kikao kama mfanyakazi wa kampuni lakini yeye alisimama nje ya mlango wa kuingilia akitaka kujua nani anakwenda kuwa mrithi wa Edna.

Recho ambaye muda wote alikuwa akimsaidia Edna katika majukumu yake akili yake ilikuwa kwenye wasiwasi , yeye ndio aliekuwa akijua kinachoendelea kwani siku ya jana yote ndie aliekuwa na jukumu la kupigia simu viongozi wa juu wote wa kampuni Tanzu kufika makao makuu kwa ajili ya kikao.

Sasa alijiambia kama Edna anakwenda kustaafu vipi kuhusu yeye kazi yake , inamaana na yeye anapaswa kuacha kazi kwasababu hatokuwa msaidizi tena wa Edna.

“Have a seat”Aliongea Edna kwa kingereza akiwaambia wafanyakazi hao wote kukaa chini.

Chumba chote kilibakia kuwa chini ya ukimya wa hali ya juu sana na macho yao yote walikuwa wameyaelekezea kwa Edna.

Edna upande wake alitulia kwa dakika kadhaa na kisha akaonyesha tabasamu ili kuondoa hali ya hewa ya wasiwasi kwa wafanyakazi hao.

“Najua mna wasiwasi mkubwa na kama mmechanganyikiwa na kujaribu kufanya makisio na kupelekea kuwa katika hali ya wasiwasi lakini yote hayo hayatozuia mimi kutoa tangazo langu , Ninaachia ngazi katika nafasi yangu kama raisi wa makampuni yote ya Vexto”Aliongea Edna na kufanya watu wote kuwa katika hali ya mshangao na kauli yake.

“Raisi Edna nini kinaendelea , kampuni yetu inafanya vizuri tutawezaje kuendelea bila ya wewe?”Aliuliza mmoja ya wafanyakazi alieshindwa kuzuia mshangao wake.

“Ndio CEO, tuambie matatizo yako, tumepitia magumu mengi kuifikisha kampuni katika hatua hii tukiwa pamoja , hakuna lingine la kutuogopesha”Alichangia mwingine na mwingine akadiakia hivyo hivyo na mwishowe likaibuka Zogo la wafanyakazi wote kutaka Edna atengue kauli yake na Edna alisimamia katika msimamo wake.

“Ninajiuzuri kama CEO lakini haimaanishi kwamba naitelekeza Vexto , Bibi yangu na mama yangu waliyatoa maisha yao kwa ajili ya maendeleo ya kampuni hii na ishakuwa kama sehemu ya familia yangu , siwezi kuitekeleza familia yangu , ninachosema ni kwamba najiuzuru katika nafasi yangu lakini bado nitakuwa na asilimia hamsini za hisa zote za kampuni na nitaendelea kubakia kama mwenyekiti wa bodi .. sababu ya mimi kujiuzuru ni kwasababu ya maswala binafsi , siwezi kfuanya kazi kila siku kama nilivyokuwa nafanya kipindi cha nyuma”Aliongea na wafanyakazi hao walijikuta wakipata ahueni kidogo kwa maneno yake lakini bado walikuwa katika hali ya mshangao na kutoridhika.

“Raisi Edna unataka kubakia kama mwenyekiti wa bodi kwasababu umechoshwa na kazi?”Aliuliza mwanamke mmoja.

“Kuna sababu nyingi ambazo zimepelekea kufanya maamuzi haya , naamini wote mnajua kwamba nimeolewa na pia nina mtoto tayari , ninataka kutumia muda mwingi kuwa na binti yangu ili kumwangalia kwa ukaribu akiendelea kukua na isitoshe mume wangu hapendi nikifanya kazi kwa muda mrefu, nadhani ni wakati wa mimi kuwa karibu na familia yangu , nimechoka sana na nadhani napaswa kujipa muda wa mapumziko , ninaweza kabisa kustaafu hata uwenyekiti na kumpa mtu mwingine kushika nafasi yangu”Aliongea na kufanya chumba chote kuwa kimya na watu kuangaliana .

“Madam , kama unajiuzuru nani anakwenda kushika wadhifa wako , mrithi lazima awe na uelewa wa namna kampuni ya Vexto inavyoendeshewa pamoja na sera zake ili kuwa na ufanisi , lazima awe pia na uwezo wa kutushawishi na sisi tumkubali kama kiongozi wetu”Aliongea mwingine na kumfanya Edna kuangalia saa ya ukutani.

“Mrithi wangu atakuwa hapa muda si mrefu , tafadhari subirini kwa muda kidogo”Aliongea.

Muda huo Roma aliekuwa nje ya mlango akitaka kujua nani anakwenda kuwa mrithi wa Edna , alijikuta akipatwa na mshangao mara baada ya kuona sura za watu wawili zikitokea kwenye Lift .

Alikuwa ni mwanaume ambaye amevalia suri safi ya bei ghali na tai nyekndu na kumpelekea kuonekana ni mtaaluma maridadi na kwa upande wa mwanamke alionekana kuwa na sura ya kawaida lakini alikuwa ni mwenye tumbo kubwa akiashiria ni mjamzito , lakini licha ya hivyo alitembea kwa muondoko wa kuonyesha kujiamini huku akitoa Aura kama ya mfanyabiashara mkubwa.

“Ernest Komwe na Monica !!?”Roma alijikuta akiongea katika nafsi yake kwani hakutegemea watu hao ndio ambao Edna alikuwa akizungumzia kwenda kumrithi.

“It’s been a while Mister Roma , I hope you are not irked by our appearance”

“Imekuwa kipindi kirefu Mr Roma , natumaini hujakerwa na kuonekana kwetu?”Aliongea Ernest Komwe akiweka tabasamu huku akionyesha heshima mbele ya Roma , alikuwa makini sana na ni kama mtu ambaye aliogopa kumkosea Roma.

Upande huo wafanyakazi wote waliweza kumuona Ernest akisalimiana na Roma walijikuta wakishangaaa mno.

Hawakushangaa kumuona Ernest Komwe tu , bali pia walishangaa kumuona Monica kwani taarifa walizokuwa nazo ni kwamba watu hao walihamia Marekani.

Nasra, Dorisi na Benadetha mara baada yakumuona Ernest walijikuta sura zao zikikunjamana.

Roma aliishia kuangalia mkono wa Ernest Komwe na kumfanya Edna kumwangalia Roma kwa mwonekano wa kuomba asifanye chochote kibaya.

Roma hakupokea hata mkono wa Ernest zaidi ya kutoa tabasamu la machungu na kisha aligeuza na kuondoka kuzifuata Lift na kupotelea ndani.

Kutokana na yaliotokea hakuwa kabisa na hamu ya kuongea na Ernest wala kuendelea kusikiliza kikao hicho ndio maana akaondoka.

Alijiambia ndio maana Edna alikuwa akimuomba kumsapoti kwa maamuzi yoyote kumbe mtu ambaye aliona anafaa kumrithi ni binamu yake Ernest.

Licha ya hivyo Roma alikubali maamuzi ya Edna , kwanza kabisa Ernest ashafanya kazi ndani ya kampuni ya Vexto kwa muda mrefu na ana uelewa na maswala yote ya kampuni lakini pia alikuwa ni mwenye uwezo mkubwa , pili ingekuwa ngumu kwa Ernest kumsaliti Edna kutokana na kwamba alishuhudia uwezo halisi na ukatiri wa Roma , mwisho kabisa uwepo wa Monica pembeni yake ungeongeza ufanisi mkubwa kwani Monica alihudumu katika kampuni ya Vexto kwa vipindi vya mabosi wote wawili yaani Rahel pamoja na Edna mwenyewe hivyo uzoefu wake ulikuwa mkubwa.

Lakini jambo la umuhimu sana Ernest alikuwa ni binadamu yake , huenda aliona ngumu kuchagua mtu wa nje ya familia kuongoza kampuni.

Roma aliona pia mpaka Edna kufikia maamuzi hayo huenda alikuwa na mawasiliano ya karibu na Ernest , kwani isingekuwa kitendo cha kufanya maamuzi jana na baada ya hapo kumrihisha kampuni.

Baada ya Roma kuondoka Edna alionyesha hali ya wasiwasi , lakini aliweza kujizuia na kisha akawakaribisha Monica na Ernest kungia ndani ya chumba hicho cha mikutano.

Monica na Ernest walijisikia vibaya kutokana na Roma kuondoka bila kuonyesha furaha ya kuwaona , lakini na wao walijitahidi kutoonyesha hali ya kuathirika na kusalimia kila mmoja aliekuwa ndani ya ukumbi huo.

Baada ya muda wa kusalimiana kwa wale waliokuwa wakimjua Ernest na Monica hatimae Edna aliamua kuwatuliza ili kuendelea na kikao.

“Jamani mpo sahihi huyu ni Ernest , alikuwa ni CEO Msaidizi , jina lake la mwanzo la ukoo alikuwa akiitwa Komwe lakini sasa hivi anafahamika kwa jina la Ernest Kayage, nadhani kila mmoja anafahamu uwezo wake katika kazi hivyo kurudi kwake akiwa ameambatana na Bi Monica ni jambo la bahati sana , Baaada ya kustaafu kwangu nafasi yangu itachukuliwa na Ernest Kayage na Monica atakuwa msaidizi wake , Recho msaidizi wangu atachukua nafasi ya Benadetha kama mkuu wa kitendo cha idara ya uhusiano na masoko na Benadetha atapandishwa cheo na kuwa CEO msaidizi namba mbili akisaidiana na Nasra”Aliongea Edna na kufanya kila mmoja kushangazwa na taarifa hio ya ubadilikaji wa vyeo.

Nasra, Dorisi , Benadetha na Recho walipatwa na mshangao , aliekuwa kwenye mshangao zaidi wa kutokuamini ni Recho baada ya kusikia kwamba anapandishwa cheo na kuwa mkuu wa idara, kila kitu kwake kilikuwa kama ndoto.

Edna muda wote aliaminika katika maamuzi yake na hata baada ya kutamka mabadiliko hayo madogo hakuna ambaye alipinga kwani walimuamini.

Baada ya mkutano kuisha Dorisi na Nasra walimsogelea Edna haraka haraka wakionekana kuwa na maswali.

“Edna ulimwambia Roma kabla ya kufanya haya maamuzi?”Aliuliza Nasra.

“Aliniambia atanisapoti kwa kila maamuzi nitakayochukua lakini nadhani sasa hivi amekasirika”

“Ndio lazima akasirike , unajua kabisa kilichotokea kati yake na Ernest na sasa hivi..”Aliongea lakini muda huo huo na Ernest aliwasogelea na alioekana kusikia maongezi yao.

“Samahani sana Makamu Nasra , najua tunaonekana kama tumekosa aibu kwa kitendo cha sisi kurudi licha ya mabaya tulioyafanya”

“Vizuri kama unaelewa , Edna anakuchukulia kama binamu ndio maana Roma alikuacha hai , la sivyo tusingekumbuka jina lako muda huu”Aliongea Dorisi akionyesha hajafurahishwa, Monica na Ernest waliangaliana wakikosa neno la kuongezea kupinga kauli yake.

“Hayo yote ni mambo yaliopita na tuachane nayo , hakikisha unafanya vizuri kusimamia Vexto wakati ambao sitokuwepo , sikutaka tu kuona ndugu wa mama yangu wakiishi uhamishoni kwa muda mrefu bila msaada”Aliongea na kumfanya Nasra na Dorisi kuangaliana kwa ishara.

“Edna kama wewe unaondoka na mimi sina sababu ya kubakia hapa kuendelea na kazi , nitatafuta mtu wa kumpendekeza kurithi nafasi yangu”Aliongea Nasra.

“Nilijua tu utaongea hivyo , vipi na wewe Dorisi una mpango wa kuacha pia?”Aliuliza Edna na Dorisi alitingisha kichwa.

“Nitaondoka baada ya kukamilisha majukumu yangu , sitaku kuachwa hapa peke yangu na kuwa nyuma ya mazoezi”Aliongea akimaanisha kwamba hawezi kuendelea na kazi na kushindwa kuendeleza mazoezi ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi.

Monica na Ernest walishindwa kuelewa Dorisi amemaanisha nini kwani kauli yake ilionekana kuwa na zaidi ya maana.

“Juu ya yote Monica Hongera , naona unatarajia mtoto”Aliongea Dorisi.

“Asante sana Dorisi”Alijibu Monnica huku akiweka tabasamu na Nasra na yeye pia alimpa hongera.







SEHEMU YA 563.

Ni muda wa mchana baada ya kikao , Roma hakuwa ameondoka bado ndani ya jengo la kampuni na hata wakati wa Dorisi , Nasra na Edna wanashuka katika Kantini ya kampuni kwa ajili ya chakula waliweza kumkuta.

“Hubby unaonaje ukiungana na sisi kwa ajili ya chakula cha mchana , unaweza kuchagua chochote utakachopenda na sisi tutakula hicho hicho”Aliongea Edna mara baada ya kukutana na Roma njiani lakini Roma hakutaka kuongea nae na kuanza kupiga hatua za kutaka kuondoka akionyesha hali ya kukasirika.

Edna alionyesha kuwa na hofu kwenye macho yake na jambo lile liliwashangaza wafanyakazi waliokuwa wakiona kinachoendelea na hawakutegemea kuona mwanamke mrembo kama Edna kumuogopa mume wake, Edna hakutaka kumpa nafasi Roma ya kuondoka na alimzuia kwa kumshika mkono.

“Unafanya nini , si ulisema wewe mwenyewe siku zote utakuwa ni mwenye kunisapoti? Sikukuomba kuachana na wanawake wako kama tulivyokubaliana lakini kwanini … na isitoshe hili haliwezi kutuletea matatizo , unadhania naweza kumuacha binamu yangu kuzurula huko ugenini bila msaada wowote licha ya yaliowatokea?”Aliuliza Edna na upande wa Roma alijifanyisha kutoridhika.

“Kama nilijua utawarudish kwanini nilitumia juhudi kubwa kuwafukuza kwenda nje ya nchi , naona kabisa binamu wako ni muhimu zaidi kuliko mimi mume wako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kukamatika maana alikuwa akimjaribu kuishi ndani ya ahadi yake lakini ilishindikana

“Basi sawa , nakubali nimefanya kosa na sijakutendea vizuri , ni kipi naweza kufanya ili unisamehe?”Aliongea Edna na kumfanya Roma moyo wake kutabasamu ndani kwa ndani , ukweli ni kwamba hakuwa na hasira ila alikuwa akitaka kutumia nafasi hio kuweka mpango wake wazi.

“Okey kwasababbu unaonyesha kubembeleza basi kitu unachopaswa kunifanyia ni kuniruhusu kwenda Cicilly kuwasindikiza Rose na Magdalena wiki ijayo … hivyo sitopata muda wa kukaa na wewe pamoja na Lanlan…”Aliongea Roma lakini palepale sura ya Edna ilijikunja na aliishia njiani kutokumalizia sentensi yake.

“Lakini kama hukubaliani na pendekezo langu , bado tunaweza kujadiliana.. si wewe umesema ni kipi unataka ufanye ili nikusamehe”Aliongea Roma huku akibadili sauti yake.

“Okey hakuna shida unaweza kwenda , hatuwezi kufa au kupotea kwasababu haupo na isitoshe ninaweza tu kumwambia Lanlan baba yake amechagua kusindikiza shangazi zake bada ya yeye”

“Kwanini unataka kumwambia mtoto hivyo ? Nina uhakika Chubby wangu lazima atatafsiri vibaya”

“Hakuna cha kutafsiri vibaya , unaenda kusindikiza wanawake wengine”Aliongea huku akimwangalia kwa macho makali na kumfanya Roma ayakwepeshe ya kwake.

“Sio kama unavyofikiria , marafiki zangu wengi waliopo Cicilly wanataka niende nikaangalie , siwezi kuwapotezea , nipe angalau wiki moja tu na nitawahi kurudi haraka iwezekanavyo baada ya kumaliza kazi yangu”

“Kama ni hivyo kwanini ni Rose na Magdalena ambao wanaweza kwenda huko na sio mimi na Lanlan?”

“Edna haiwezekani , unajua mwenyewe kinachokwenda kutokea huko ni kama vita kati ya wanajeshi na wanajeshi na nadhani mwenyewe unajua tabia ya Lanlan”Aliongea Roma na kumfanya Edna angalau kuelewa maana yake na kujituliza lakini bado hakuridhika.

Wakati Roma akiendelea na maongezi yake na Edna mara palepale simu yake ilianza kuita na alivyoangalia mtu anaepiga ni mama yake mzazi.

Roma palepale alipokea kutaka kujua tatizo ni nini maana mama yake hakuwa na tabia ya kupiga muda kama huo na isitoshe jana usiku tu aliwasiliana nae.

Baada ya kusalimiana ndio muda ambao Blandina alimweleza Roma kuhusu Najma kupata kazi katika wizara kama Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam.

Roma alifurahishwa na taarifa hio , lakini ilimshangaza kwa wakati mmoja mara baada ya kusikia mtu aliewezesha Najma kupata nafasi hio ni raisi Senga na kwa namna ambavyo mama yake alikuwa akisikika ni kama alikuwa na maelewano mazuri na baba yake mzazi, ijapokuwa alikuwa na hisia za aina hio , lakini bado alishangaa kuona mama yake amepiga hatua , lakini hata hivyo alifurahi kwa ajili yake

“Roma baba yako anajitahidi kuanza kujenga ukaribu na wewe , nadhani itakuwa jambo zuri kama utampigia simu na kumshukuru kwa kumsaidia Sophia , isitoshe ni mwanamke wako pia”Roma alifikiria kidogo maelezo yake na kutaka kumuuliza mama yake ni lini akawa na mahusiano ya karibu na Senga lakini alijizuia.

“Mama ni jambo dogo kama hilo amefanya na halihusiani kabisa na mimi kumsogelea , yeye ndie aliekuwa wa kwanza kunikataa kwanini nimfuate na kujipendekeza kwake”Aliongea Roma.

“Najua ndio , lakini ni hasira tu , Senga baba yako amepitia magumu mengi kukuomboleza, huwezi jua lakini alikuwa akikupenda sana wakati ulivyokuwa mdogo na alifanya kila kitu kukuona una furaha, isitoshe ni jambo zuri kama atakutambua , naamini pia uhusiano wako na Denisi utaimarika, ni muda sasa alikuwa na mawazo juu ya Denisi na amekwisha kurudi nyumbani, Roma nakushauri kuepuka ugomvi na Denisi”

“Mama umesema Denisi amerudi?”

“Ndio amerudi baada ya kutokuonekaan kwa mwezi mmoja”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kuhisi kitu cha hatari lakini alipotezea.

Baada ya maongezi ya muda mrefu kidogo Roma alikata simu na Edna alionekana akitaka kujua nini walikuwa wakiongea mara baada ya kusikia jina la Denisi.

“Nimesikia kuhusu Denisi , vipi amerudi?”Aliuliza Edna , alikuwa akijua kutoweka kwa Denisi kupitia Ashley ambaye alikuwa akiongoza projekti yake ya dawa aliongia nayo mkataba na Profesa Clark.

Ashley alikuwa na mwezi mmoja tokea arudi nchini Tanzania na aliteuliwa rasmi kama mkemia mkuu wa serikali na baba yake na kutokana na mafanikio yake hakuna mtu aliepinga nafasi yake, lakini licha ya hivyo Roma hakuwahi kukutana na Ashley tokea arudi nchini , huenda ni kwasababu ya ubize wake ndio maana.

“Mama amesema kwamba Denisi amerudi na kwa maelezo yake anasema hatoondoka tena na mpango wake ni kubadilika na kuwa mtoto mwema na ameweza hata kwenda nyumbani kwa Afande Kweka na kumuomba amuunganishe na jeshi kwani anataka kulitumikia taifa”Aliongea Roma.

“Kama ni hivyo kwanini uso wako upo hivyo , je una kwenda kumuua?”Aliuliza Roma na alishindwa kujibu swali lake , ukweli ni kwamba Roma hakuwa kabisa na mpango wa kumua tena Denisi tena , na hakujali pia makuzi yake yalikuwaje na isitoshe kwa muda huo hakutaka mitafaruku zaidi kwani alipenda amani ndani ya familia yake.

Lakini licha ya hivyo alihisi kuna kitu kinaendelea kuhusu kuonekana kwa Ghafla kwa Denisi na kuanza kutaka kujiunga na jeshi, ijapokuwa hakuwa na sababu ya msingi ya kujisikia hivyo lakini hisia zake zilimwambia kabisa kuna kitu hakipo sawa kuhusu Denisi.

“Tutaona pia namna itakavyokuwa , si unakumbuka mzee Kweka alituhitaji tukusanyike Iringa siku zijazo kama familia , nadhani nitapata fursa ya kujua mchezo anaopanga kucheza., siwezi kuogopa kumuua kama kuna kitu kibaya anachopanga lakini siwezi kufanya hivyo mbele ya Lanlan na kuja kufahamu kwamba nilimuua mdogo wangu”Aliongea Roma.

Roma siku ambayo alienda kumchukua Lanlan mara baada ya kurudi Dubai aliweza kuambiwa na Afande Kweka kufika Iringa mwanzo wa mwezi unaokuja.

Afande Kweka alikuwa akihamia rasmi Iringa na kufanya makazi ya kudumu, alitaka angalau kukaa karibu na mifugo yake na kuufurahia uzee wake, Roma hakuuliza sana juu ya safari hio ya kwenda Iringa.

Ukweli ni kwamba siku hio ilipangwa maalumu na Afande Kweka kuwakutanisha rasmi Raisi Senga na Roma ili kumaliza tofauti zao na hio ni mara baada ya Raisi Senga kufika nyumbani na kuweka nia yake wazi na kuomba baba yake mzazi kumsaidia katika kuirudisha familia yake katika mstari.

Edna aliridhishwa na kauli ya Roma kwamba hawezi kumruhusu Lanlan kushuhudia yeye mwenyewe akimuua mdogo wake.

“Naona mume wangu umezidi kuwa na busara”Aliongea Edna huku akitoa pumzi ya ahueni lakini kauli yake ilimfanya Roma kuona aibu kidogo za kiume , tokea aoe na hatimae kuwa na mtoto alianza kuzingatia mambo mengi .

“Turudi kwenye topiki yetu mke wangu , naomba uniruhusu niondoke angalau kwa siku saba , ninakuahidi nitarudi mapema na wote kwa pamoja tutaenda Iringa, nyie wawili mtachceza mtakavyo mara baada ya kufik, sawa babe?”Aliongea kwa kubembeleza.

“Ole wako uchelewe kurudi na kutumia siku nyingi na kututelekeza mimi na mtoto , nakuambia hutoweza kuvumilia matokeo yake”Aliongea Edna , hata hivyo alijua asingeweza kumzuia , alifurahi kwamba alikuwa akiombwa ruhusa hivyo hakutaka kuleta mambo mengi.

******

Katika siku zilizofuata Edna tayari alianza taratibu za kuhamisha uongozi wake kwenda kwa Ernest na kumkabidhi kila kitu.

Upande wa Roma na yeye baada ya kuona Edna kaacha kazi na yeye hivyo hivyo aliacha na nafasi yake akampatia Daudi.

Edna rasmi akawa sio CEO tena wa kampuni ya Vexto na maswali mengi katika vyombo vya habari yaliibuka lakini kampuni iliishia kutoa maelezo kwa ufupi kwamba Edna alijiuzuru kwa sababu za kifamilia.

Ilikuwa ikishangaza kwani Edna alikuwa amejijengea jina kubwa sana katika ulimwengu wa kibiashara ndani na nje ya nchi.

Upande wa Edna alionekana kufurahia maamuzi yake na alitumia muda mwingi nyumbani kujifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi huku akipewa maelekezo na Rufi kutokana na uelewa wake ulioambatana na uzoefu.

Bi Wema alifurahi sana kuona namna ambavyo Edna alijenga ukaribu na Rufi mtoto wake, hata ile hali ya uzee aliokuwa nayo ilianza kutoweka na sasa alianza kuwa kijana zaidi , huenda mawazo ya kumkumbuka mwanae yalimtesa miaka na miaka na baada ya kurudi alijisikia vizuri zaidi.

Upande wa Amina baba yake alikuwa akiendelea vizuri na hio ni mara baada ya kupewa kidonge cha kijini na Roma, ijapokuwa ugonjwa wake haukuwa umepona lakini hali yake iliimarika kidogo lakini licha ya hivyo hakuweza kurudi kwenye kampuni tena.

Amina mara baada ya kusikia Edna kajiuzuru na yeye alitamani kufanya hivyo lakini hakuwa na mtu wa kumrithisha hivyo aliachana na mawazo hayo na kuendelea kufanya kazi huku akifanya mazoezi ya kuvua nishati za mbingu na Ardhi.

Upande wa Qiang Xi na yeye alikuwa na wasiwasi mara baada ya Edna kujizuru kwa kugopa kwamba kazi yake ya kumlea Lanlan moja kwam moja ingehamia kwa Edna , lakini Edna alijua wasiwasi wake na kumwambia hana haja ya kuwa na wasiwasi na Edna alimwambia kama atakuwa na mpango wa kutaka kurudi nchini China basi atahakikisha anamsaidia namna ya kwenda kuanza maisha , lakini mrembo huyo wa kichina aligoma na kusema anataka kubakia Tanzania kwa muda.

Kauli yake hio ni kama ilieleweka , walijua tu lazima Qiang Xi alikuwa akitegemea Master wake atarudi Tanzania kumuona Lanlan na yeye ndio maana hakutaka kuondoka , isitoshe pia aliogopa kwamba kuna baadhi ya majukumu hakuwa ametimiza kwa ajili ya Lanlan kama alivyoagizwa na Master wake.

Siku ya jumapili ndio siku ambayo Roma alianza safari yake ya kuelekea katika visiwa vya wafu.

Magdalena na Rose licha ya kwamba walisuburia kwa wiki tu , lakini kutokana na shauku yao ilimwafanya kuona kama wamesubiri muda mrefu na hawakuamini siku ya kesho ndio hio ambayo wanatarajia kuona mkutano huo wa kaisari au Baraza la kaisari ambalo hukutanisha vikosi vya wanajeshi wa kulipwa kutoka makundi mengi duniani.

Siku walizoishi katika visiwa vya wafu , ukiachana na kufanya mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi lakini pia waliweza kuzoeana na raia wanaoishi katika visiwa hivyo.

Ijapokuwa walikuwa wakipata shida ya kuwasiliana kutokana na baadhi ya wengi wao kujua kitaliano , lakini kutokana na kwamba walikuwa katika levo ya Nafsi uwezo wao wa kujifunza lugha mpya ulikuwa mkubwa mno.

Lakini pia asilimia kubwa ya wakazi wa visiwa hivyo kuwa ni wanajeshi wastaafu basi ilikuwa rahisi kwao kupata watu ambao walikuwa wakizungumza lugha ya kingereza na kuelewana, walichofurahi zaidi hawakuonyeshewa ubaguzi kutokana na rangi zao.

Ron kwasababu ndio aliekuwa ana kwenda kuwa mwenyeji katika kipindi chote watakachokuwepo Cicily basi aliweza kufanya maandalizi yote ya safari.

Baada ya Roma kufika tu Ron tayari amekwisha kuandaa Ndege binafsi iliokuwa ikimsubiri yeye na wanawake wake kupanda na kuondoka visiwani hapo.

Kutoka Visiwa vya wafu mpaka Cicilly ulikuwa ni umbali wa nusu saa tu na kama wangependa kusafiiri kwa mbinu za kijini basi ingekuwa ni kufumba na kufumbua , lakini kutokana na kwamba ilikuwa kama safari ya kimatembezi basi waliona watumie ndege.

Cicilly kilikuw ani kisiwa cha watu wengi na kilikuwa Kusini Magharibi mwa bahari ya Pasifiki.

Kama ilivyoelezwa katika historia , Ugiriki ya kale , Warumi , Wabzantine(Byzantines), Vikings(Norman) na wengineo ndio ambao walitawala kisiwa hicho hapo kabla , baada ya mgawanyiko wa tawala ya kifalme ya Cicily wahispania na wao walikitawala na baada ya hapo ndipo utawala wa Italy ulikichukua na kuanzia hapo ndipo Cicily ilipoweza kujiendesha yenyewe.

Ni sehemu katika Italy ambayo ni maarufu sana kutokana na kwamba ndio mahali ambapo makundi ya Kimafia duniani yalitokea kwa wingi na kutawala eneo lote ,

Familia za kimafia walikuwa ni kama serikali kivuli ndani ya miji ya visiwa hivyo na walienda sambamba na serikali na hawakuweza kutokomezwa kutokana na makundi hayo kupandikiza watu wao serikalini.

Katika eneo hilo sheria ya kiserikali haikufanya sana kazi au kufuatwa na sheria ambazo zimetungwa na makundi hayo ya kimafia ndio ambazo zilikuwa na nguvu.

Familia ya Constantine ndio familia ambayo anatokea Ron na ndio moja wapo ya familia ambayo ilikuwa ikiogopeka kwa kumiliki kundi kubwa la Mafia Gang.

Lakini hata hivyo Ron alikuwa tayari ashaachia ngazi kama kiongozi wa familia hio na kuhamishia maisha yake katika visiwa vya wafu lakini licha ya hivyo ukubwa wake ndani ya familia bado ulikuwa ukichukuliwa siriasi na alikuwa akiheshimika.

Wakiwa katika ndege Magdalena na Rose waliweza kushangazwa na tamaduni nyingi ambazo Ron aliwaambia kuhusiana na watu wa Cicily lakini shauku yao yote ilikuwa kwenye umoja wa makundi ya kimafia ufahamikao kwa jina la Mafia Alliance.

“Mr Ron nimeweza kusikia kutoka kwa watu kule kisiwani kwamba ulikuwa raisi wa Mafia Allianace? Tuambie ni kwa namna gani uliweza kupata cheo hicho , inashangaza sana?”Aliongea Rose kwa shauku kubwa , kundi lake la Tembo lilikuwa kama chawa kwa makundi ya kimafia ya Itali, watu wa huko walikuwa ni Ma’gangstar wa kihistoria.

“Lady Rose hayo yote ni kwasababu ya Mfalme Pluto , ukweli ni kwamba kama asingetusaidia huenda makundi yote ya kimafia ndani ya Cicily yangetokomezwa”

“Roma ndio kafanya hivyo ?”Aliuliza Magdalena kwa shauku.

“Ukweli ni kwamba wale watu waliokuwa na nguvu ndani ya makundi yetu walikuwa wakipungua siku hadi siku hivyo kupunguza ukubwa wa shughuli zetu na zaidi ya yote watu wa dunia walianza kutuchoka na kipindi hicho serikali ilichukulia jambo hilo kama fursa na wakasambaza wanajeshi wa vitengo maalumu kupambana na sisi , ijapokuwa kipindi hicho tuliweza kupata taarifa mapema ya mpango wa serikali lakini ilikuwa ngumu kwetu kuweka ukinzani , unachotakiwa kuelewa ni kwamba kama serikali ikiamua lake hawachukui tahadhari za aina yoyote, kipindi ambacho tunakaribiwa kushindwa kwa kukosa siraha na watu wa kupambana ndio kipindi ambacho Ghafla tu mfalme Pluto alitokeza”Aliongea huku akionyesha hali ya kukumbuka kipindi kilichopita.

“Nakumbuka kabisa kipindi hicho Mfalme Pluto alitokeza mbele ya maadui zetu na kuharibu siraha zao na kuharibu magari yao ndani ya muda mfupi tu , wanajeshi waliotumwa kipindi hicho walikuwa ni kutoka kambi ya kijeshi ya Uingereza iliokuwa pembeni ya Rome na walisifika kwa uhodari wao lakini Mfalme Pluto aliweza kubadili hali ya hewa kwa kumuua Kamanda wao na mkono mmoja tu , baada ya tukio hilo kundi letu lote lilipata nguvu upya na tuliweza kupambana mpaka tukashinda na baada ya machafuko kuisha ndio nilivyoweza kupata cheo cha uraisi wa Mafia Alliance kama hsehima , lakini ukweli ni kwamba sikufanya chochote..”Aliongea huku akimwangalia Roma kwa namna ya kumkubali, Rose na Magdalena na wao walimwangalia kwa macho ya kiulizo

Muda huo Roma hakuwa ni mwenye kujali stori zao kwani alikuwa bize kula matunda ya zabibu yaliokuwa kwenye sahani na baada ya kugundua anaangaliwa aliwasogezea sahani.

Upande wa Magdalena na Rose waliweza kuona kuna utofaut mkubwa kati ya matarajio yao na uhalisia wanao uona na pengine wanaokwenda kuushuhudia.

Kuna nini huko kwenye Kaisari Conference , je unadhani wanaenda tu kuangalia mapambano tu na Roma anawasindikiza tu warembo hao , jibu linakuja.
[emoji2923][emoji373][emoji2923][emoji373][emoji1635][emoji512]
 
Back
Top Bottom