singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #921
SEHEMU YA 167
Mage licha ya kwamba alikuwa akionekana kawaida mbele ya Roma , lakini ukweli ni kwamba mrembo huyo hakuwa kawaida kabisa, haikueleweka ilianza lini , lakini Mage alikuwa amebadilika sana yale Maisha ya kutumia viungo bandia kwa ajili ya kujiridhisha alikuwa ashaacha na swala ambalo lilikuwa limemfanya kuacha juu ya kutumia vifaa hivyo ilikuwa ni Roma.
Mage alikuwa akimuwaza Roma kila siku , licha ya kwamba Roma alikuwani mpenzi wa rafiki yake wa utotoni yaani Edna , lakini alishindwa kuhimili hisia zake , mwanzoni kwake alihisi ni chuki ambazo alikuwa nazo juu ya Roma ndio zilizokuwa zikimfanya kumuwazia Roma , lakini kadri siku zilivyokuwa zikienda aliamini haikuwa chuki bali ni mapenzi aliokuwa nayo juu ya Roma , yaani chuki zikageuka mapenzi,
Siku ya jana yake ndio alipohakikisha hisia zake kikamilifu na kuaminni kwamba alikuwa na mapenzi na Roma , kilichomfanya kuhakikisha hilo ni wakati baada ya Roma kupotea ndani ya ukumbi Pamoja na dada yake , kitendo kile kilimfanya mrembo huyu kuwa na wasiwasi mno na wasiwasi wake haukuwa kwasababu huenda Roma angekuwa kwenye matatizo , Hapana , bali wasiwasi wake ulikuwa ni kwamba huenda Magdalena pacha wake alikuwa na Roma na wanafanya mambo ya kimapenzi na hata baada ya Roma kurudi hakuridhika kabisa, kwanza alijiuliza Magdalena yuko wapi mpaka Roma kujitokeza peke yake, lakini wasiwasi wake ulijaa Zaidi baada ya dakika kadhaa kutumiwa ujumbe na Magdalenda kwamba arejee nyumbani kwani yeye ashafika.
Ilikuwa ni muda wa saa mbili za asubuhi gari ya Porsche ilisimama ndani ya eneo la Osterbay, gari hii ikiendeshwa na mwanadada mrembo Polisi Mage , baada ya kupiga honi kwa dakika moja hatimae geti lilifunguliwa na Mage akaingiza gari ndani.
“Karibu sana Miss”Aliongea mlinzi wa getini mara baada ya Mage kutoka kwenye gari na Mage aliitikia kwa kichwa na kuzunguka upande wa Buti na kutoa sanduku kubwa la kuhifadhia nguo.
“Mage..!”Ilikuwa ni sauti ya Magdalena iliokuwa ikitokea nyuma na kumfanya Mage ageuke nyuma na kumuona dada yake aliekuwa amevalia Track Suit akiwa nyuma yake na kwa jinsi alivyomuona alijua tu anatoka kuchukua mazoezi ya kukimbia na muda huio alikuwa ndio anarudi.
“Dabi Chukua hilo begi”Aliongea Mage na akimwamrisha mlinzi wa geti kuchukua Begi alilokuwa ameshikilia Mage na mlinzi kwa haraka haraka alitii na kubeba hilo begi na kuelekea ndani.
“Naona umeamua kurudi nyumbani”Aliongea Magdalena huku akimsogelea Mage.
“Ndio nimechoka kuishi mwenyewe nimeamua kurudi”Aliongea Mage huku akiladhimisha tabasamu huku akimkagua Magdalena , alikuwa ni kama aliekuwa akimfananisha dada yake na mtu, na hata Mage alishangazwa na namna ambavyo Mage alikuwa akimwangalia.
Ukumbuke kwamba Mage na Magdalena licha ya kuwa na kazi tofauti , lakini walikuwa wakifanana sana na kilichokuwa kikiwatofautisha pekee ilikuwa ni mtindo wa nywele , kwani Magdalena hakuwa na nywele ndefu na Mage alikuwa na nywele ndefu alizozibana kwa nyuma.
“Nimefurahi umerudi pacha.. twende ndani baba na mama watakuwa wanatusubiri”Aliongea Magdalena na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jumba hili ambalo lilikuwa la kifahari kweli.
“Jana ulirudi saa ngapi na kwanini ulipotea wewe Pamoja na Roma?”aliuliza Mage kabla hata hawajafikia mlango na kumfanya Magdalena kusimama na kumwangalia Mage.
“Kuna jambo lilitokea ni la kikazi Zaidi na lilikuwa likihusiana na kile kikombe”
“Vipi kuhusu Roma na yeye alipotea kwasababu hio hio”
“Ndio Mage ila yashapita na sitaki kuyaelezea Zaidi”Aliongea Magdalena na kuingia ndani huku akimuacha Mage akisimama nje.
“Damn it ! hii yote ni kutokana na mimi kuwa dhaifu”Alijiwazia Mage huku akikunja ngumi , kwani hakuwa ameridhika na majibu ya dada yake , alijona yeye kama dhaifu na ndio maana mambo mengi hakuwa akiyajua.
“Mage..!!!,Jamani karibu”Aliongea Mama P huku akiwa ameshikilia chupa ya chai na alionekana alikuwa akiandaa kifungua kinywa muda huo , na alifurahishwa sana baada ya kusikia kuwa Mage karudi nyumbani na siku zote lilikuwa ndio hitajio lake kubwa , hakupenda namna ambavyo Mage alikuwa akiishi peke yake kwenye Apartment.
“Asante Mum”Aliongea Mage huku wakikumbatiana kwa furaha na muda huo huo alionekana Afande Tobwe aliekuwa akishuka kutoka juu akiwa amevalia suti na kushikilia mkoba mkononi.
“Dadiii…”Aliongea Mage na kumkimbilia baba yake na kumkumbatia na kumfanya Magdalena awaangalie baba na mwana na kisha akapandisha juu kwa ajili ya kujisafisha mwili , ili arejee mezani kwa ajili ya kifungua kinywa.
“My Daughter Welcome Back Home”aliongea Afande Tobwe na kumfanya Mage atabasamu huku wakitembea wote kuelekea mezani.
“Mwana na Baba wamekutana hii nyumba itachangamka sasa na wengine kukosa nafasi”Aliongea Mama P huku akitabasamu.
“Ushaanza wivu wako na utakonda awamu hii..”Aliongea Afande Tobwe na kumfanya Mama P Kucheka kwa nguvu na wote wakaketi mezani.
Mage alioenakana kujidekeza sana mbele ya Afande Tobwe kuliko isivyokuwa kawaida na alionekana kuwa tofauti na dada yake Magdalena.
“Dadii.. nimerudi nataka kujiunga na Jeshi”Aliongea Mage na kumfanya Afdne Tobwe atamani kujimwagia juisi na hata Magdalena pia alishangazwa na maneno ya pacha wake na sio kwa Magdalena tu pia kwa Mama P alishangaa mno.
“Mage mbona unanitisha , kwanini Ghafla tu unataka kujiunga na jeshi?”Aliuliza Afande lakini muda huu Mama P alikuwa akimwangalia mwanae na kuna vitu vingi alikuwa ameviona kwa Mage na hata namna ambavyo alikuwa akiongea , alikuwa amebadilika.
“Nataka kuwa na nguvu kama Magdalena ,mambo mengi siyajui kwasababu mimi ni dhaifu…”Aliongea Mage na palepale akamwangalia Magdalena na kuanza kutoa machozi na kunyanyika na kukimbilia juu na kuwafanya wanafamilia kushangaa na mtu wa kwanza kunyanyuka na kumkibilia Mage alikuwa ni Mama P.
Mama P ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Mage akikosa ujasiri na kujiita Zaifu na kulia mbele yao , aliamini kuna jambo ambalo limemtokea mtoto wake na moyo ulimuuma mno , kwani mara nyingi hakuwa akimfatilia Mage kwa ukaribu na kujua maendeleo yake.
*******
Ukweli Nasra pia alikuwa ashawaza siku ambayo ataweza kuonana na mke wa Roma , hakujua ingekuwaje , kwani alikuwa akijua vizuri mambo ya wake kutopenda michepuko.
“Naomba tupange siku utanitambulisha tu”Aliongea Nasra na Roma alitabasamu na kukubaliana na nae.
Baada ya Roma kutoka ndani ya ofisi ya Nasra alirudi sehemu anayofanyia kazi kwa ajili ya kuendelea na shughuli ya kucheza gemu ili kupoteza muda na hatimae kurejea nyumbani.
Upande wa ofisini kwa Nasra baada ya Roma kuondoka , simu yake ya mezani ilianza kuita na aliiichukua na kuipokea.
“Sawa Boss”Aliitikia Nasra na kisha akanyanyuka na kutoka nje ya ofisi yake na alionekana kuchukua uelekeo wa ofisi ya Bosi Edna.
“Boss nimefika”Aliongea Nasra baada ya kuingia ndani ya ofisi ya Edna, Ofisi ambayo leo hii ilikuwa na mabadiliko kidogo kutokana na kuwa na maua mengi yaliokuwa yamepambwa ofisi nzima.
Ukweli ni kwamba baada ya siku kadhaa nyuma kwa Kampuni kuingia kwenye tatizo la kushuka kwa Hisa za kampuni , lakini pia taarifa mbaya ambayo ilikuwa ikisambaa mtandaoni , iliokuwa ikihusiana na Edna , lakini pia taarifa za kuugua kwa Edna , wafanyakazi wengi wa kampuni walikuwa na wasiwasi na bosi wao sana kutokana na kuugua kwake , lakini wakati huo walimuona Edna kama shujaa baada ya hali kutengemaa na tatizo kuonekana kama vile halijatokea na hayo maua yote yaliokuwa yamepambwa kwenye ofisi ya Edna yametoka kwa wafanyakazi wa kampuni hio , walionekana kumkubali sana Bosi Edna kwa juhudi zake alizokuwa akifanya kwa kampuni, kwao Edna alikuwa sio bosi tu , lakini walimuona kama shujaa, na hii yote ni kutokana na namna Edna alivyokuwa akiwajali wafanyakazi wake , kuanzia mazingira ya kazi , mpaka mishahara yao, Edna alikuwa CEO wa kuigwa , licha ya kuwa kauzu , lakini alikuwa akijali kila mfanyakazi na alihakikisha kila mfanyakazi jasho lake linathaminiwa na kampuni , Edna hakuwa mnyonyaji na alikuwa msikilizaji na mtu wa kutoa maamuzi na alikuwa akisimamisa sheria na haki katika kufanya kwake maamuzi na hilo lilimjengea heshima kubwa tokea apewe kampuni hio kutoka kwenye mikono ya mama yake.
“Nasra nitahitaji uidhinishe kiasi cha bilioni mbili kwenda Vexto Media and Entertainment”Aliongea Edna.
“Sawa bosi lakini nadhani kutokana na malengo ya kampuni na uendeshaji wake kitakuwa kiwango kidogo sana , nilipiga mahesabu na kuona Bilioni tano ndio zinaweza kutosha”
“Nalifahamu hivyo ndio maana nataka kuidhinisha kiasi hiko , nataka nione hatua atakazochukua Director kuendesha kampuni na kiasi kidogo cha pesa na isitoshe mpaka sasa tunakampuni lakini juu ya uendeshaji hatujapanga”Aliongea Edna na kumfanya Nasra kushangaa kidogo.
“Boss unapanga nani kuwa Director?”Aliongea Nasra na Edna alifikiria kidogo.
“Napanga kumuachia Roma Ramoni awe Director”Aliongea na kumfanya Nasra kutoa macho kwa mshangao , ilikuwa ni taarifa mpya kwake.
Mage licha ya kwamba alikuwa akionekana kawaida mbele ya Roma , lakini ukweli ni kwamba mrembo huyo hakuwa kawaida kabisa, haikueleweka ilianza lini , lakini Mage alikuwa amebadilika sana yale Maisha ya kutumia viungo bandia kwa ajili ya kujiridhisha alikuwa ashaacha na swala ambalo lilikuwa limemfanya kuacha juu ya kutumia vifaa hivyo ilikuwa ni Roma.
Mage alikuwa akimuwaza Roma kila siku , licha ya kwamba Roma alikuwani mpenzi wa rafiki yake wa utotoni yaani Edna , lakini alishindwa kuhimili hisia zake , mwanzoni kwake alihisi ni chuki ambazo alikuwa nazo juu ya Roma ndio zilizokuwa zikimfanya kumuwazia Roma , lakini kadri siku zilivyokuwa zikienda aliamini haikuwa chuki bali ni mapenzi aliokuwa nayo juu ya Roma , yaani chuki zikageuka mapenzi,
Siku ya jana yake ndio alipohakikisha hisia zake kikamilifu na kuaminni kwamba alikuwa na mapenzi na Roma , kilichomfanya kuhakikisha hilo ni wakati baada ya Roma kupotea ndani ya ukumbi Pamoja na dada yake , kitendo kile kilimfanya mrembo huyu kuwa na wasiwasi mno na wasiwasi wake haukuwa kwasababu huenda Roma angekuwa kwenye matatizo , Hapana , bali wasiwasi wake ulikuwa ni kwamba huenda Magdalena pacha wake alikuwa na Roma na wanafanya mambo ya kimapenzi na hata baada ya Roma kurudi hakuridhika kabisa, kwanza alijiuliza Magdalena yuko wapi mpaka Roma kujitokeza peke yake, lakini wasiwasi wake ulijaa Zaidi baada ya dakika kadhaa kutumiwa ujumbe na Magdalenda kwamba arejee nyumbani kwani yeye ashafika.
Ilikuwa ni muda wa saa mbili za asubuhi gari ya Porsche ilisimama ndani ya eneo la Osterbay, gari hii ikiendeshwa na mwanadada mrembo Polisi Mage , baada ya kupiga honi kwa dakika moja hatimae geti lilifunguliwa na Mage akaingiza gari ndani.
“Karibu sana Miss”Aliongea mlinzi wa getini mara baada ya Mage kutoka kwenye gari na Mage aliitikia kwa kichwa na kuzunguka upande wa Buti na kutoa sanduku kubwa la kuhifadhia nguo.
“Mage..!”Ilikuwa ni sauti ya Magdalena iliokuwa ikitokea nyuma na kumfanya Mage ageuke nyuma na kumuona dada yake aliekuwa amevalia Track Suit akiwa nyuma yake na kwa jinsi alivyomuona alijua tu anatoka kuchukua mazoezi ya kukimbia na muda huio alikuwa ndio anarudi.
“Dabi Chukua hilo begi”Aliongea Mage na akimwamrisha mlinzi wa geti kuchukua Begi alilokuwa ameshikilia Mage na mlinzi kwa haraka haraka alitii na kubeba hilo begi na kuelekea ndani.
“Naona umeamua kurudi nyumbani”Aliongea Magdalena huku akimsogelea Mage.
“Ndio nimechoka kuishi mwenyewe nimeamua kurudi”Aliongea Mage huku akiladhimisha tabasamu huku akimkagua Magdalena , alikuwa ni kama aliekuwa akimfananisha dada yake na mtu, na hata Mage alishangazwa na namna ambavyo Mage alikuwa akimwangalia.
Ukumbuke kwamba Mage na Magdalena licha ya kuwa na kazi tofauti , lakini walikuwa wakifanana sana na kilichokuwa kikiwatofautisha pekee ilikuwa ni mtindo wa nywele , kwani Magdalena hakuwa na nywele ndefu na Mage alikuwa na nywele ndefu alizozibana kwa nyuma.
“Nimefurahi umerudi pacha.. twende ndani baba na mama watakuwa wanatusubiri”Aliongea Magdalena na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jumba hili ambalo lilikuwa la kifahari kweli.
“Jana ulirudi saa ngapi na kwanini ulipotea wewe Pamoja na Roma?”aliuliza Mage kabla hata hawajafikia mlango na kumfanya Magdalena kusimama na kumwangalia Mage.
“Kuna jambo lilitokea ni la kikazi Zaidi na lilikuwa likihusiana na kile kikombe”
“Vipi kuhusu Roma na yeye alipotea kwasababu hio hio”
“Ndio Mage ila yashapita na sitaki kuyaelezea Zaidi”Aliongea Magdalena na kuingia ndani huku akimuacha Mage akisimama nje.
“Damn it ! hii yote ni kutokana na mimi kuwa dhaifu”Alijiwazia Mage huku akikunja ngumi , kwani hakuwa ameridhika na majibu ya dada yake , alijona yeye kama dhaifu na ndio maana mambo mengi hakuwa akiyajua.
“Mage..!!!,Jamani karibu”Aliongea Mama P huku akiwa ameshikilia chupa ya chai na alionekana alikuwa akiandaa kifungua kinywa muda huo , na alifurahishwa sana baada ya kusikia kuwa Mage karudi nyumbani na siku zote lilikuwa ndio hitajio lake kubwa , hakupenda namna ambavyo Mage alikuwa akiishi peke yake kwenye Apartment.
“Asante Mum”Aliongea Mage huku wakikumbatiana kwa furaha na muda huo huo alionekana Afande Tobwe aliekuwa akishuka kutoka juu akiwa amevalia suti na kushikilia mkoba mkononi.
“Dadiii…”Aliongea Mage na kumkimbilia baba yake na kumkumbatia na kumfanya Magdalena awaangalie baba na mwana na kisha akapandisha juu kwa ajili ya kujisafisha mwili , ili arejee mezani kwa ajili ya kifungua kinywa.
“My Daughter Welcome Back Home”aliongea Afande Tobwe na kumfanya Mage atabasamu huku wakitembea wote kuelekea mezani.
“Mwana na Baba wamekutana hii nyumba itachangamka sasa na wengine kukosa nafasi”Aliongea Mama P huku akitabasamu.
“Ushaanza wivu wako na utakonda awamu hii..”Aliongea Afande Tobwe na kumfanya Mama P Kucheka kwa nguvu na wote wakaketi mezani.
Mage alioenakana kujidekeza sana mbele ya Afande Tobwe kuliko isivyokuwa kawaida na alionekana kuwa tofauti na dada yake Magdalena.
“Dadii.. nimerudi nataka kujiunga na Jeshi”Aliongea Mage na kumfanya Afdne Tobwe atamani kujimwagia juisi na hata Magdalena pia alishangazwa na maneno ya pacha wake na sio kwa Magdalena tu pia kwa Mama P alishangaa mno.
“Mage mbona unanitisha , kwanini Ghafla tu unataka kujiunga na jeshi?”Aliuliza Afande lakini muda huu Mama P alikuwa akimwangalia mwanae na kuna vitu vingi alikuwa ameviona kwa Mage na hata namna ambavyo alikuwa akiongea , alikuwa amebadilika.
“Nataka kuwa na nguvu kama Magdalena ,mambo mengi siyajui kwasababu mimi ni dhaifu…”Aliongea Mage na palepale akamwangalia Magdalena na kuanza kutoa machozi na kunyanyika na kukimbilia juu na kuwafanya wanafamilia kushangaa na mtu wa kwanza kunyanyuka na kumkibilia Mage alikuwa ni Mama P.
Mama P ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Mage akikosa ujasiri na kujiita Zaifu na kulia mbele yao , aliamini kuna jambo ambalo limemtokea mtoto wake na moyo ulimuuma mno , kwani mara nyingi hakuwa akimfatilia Mage kwa ukaribu na kujua maendeleo yake.
*******
Ukweli Nasra pia alikuwa ashawaza siku ambayo ataweza kuonana na mke wa Roma , hakujua ingekuwaje , kwani alikuwa akijua vizuri mambo ya wake kutopenda michepuko.
“Naomba tupange siku utanitambulisha tu”Aliongea Nasra na Roma alitabasamu na kukubaliana na nae.
Baada ya Roma kutoka ndani ya ofisi ya Nasra alirudi sehemu anayofanyia kazi kwa ajili ya kuendelea na shughuli ya kucheza gemu ili kupoteza muda na hatimae kurejea nyumbani.
Upande wa ofisini kwa Nasra baada ya Roma kuondoka , simu yake ya mezani ilianza kuita na aliiichukua na kuipokea.
“Sawa Boss”Aliitikia Nasra na kisha akanyanyuka na kutoka nje ya ofisi yake na alionekana kuchukua uelekeo wa ofisi ya Bosi Edna.
“Boss nimefika”Aliongea Nasra baada ya kuingia ndani ya ofisi ya Edna, Ofisi ambayo leo hii ilikuwa na mabadiliko kidogo kutokana na kuwa na maua mengi yaliokuwa yamepambwa ofisi nzima.
Ukweli ni kwamba baada ya siku kadhaa nyuma kwa Kampuni kuingia kwenye tatizo la kushuka kwa Hisa za kampuni , lakini pia taarifa mbaya ambayo ilikuwa ikisambaa mtandaoni , iliokuwa ikihusiana na Edna , lakini pia taarifa za kuugua kwa Edna , wafanyakazi wengi wa kampuni walikuwa na wasiwasi na bosi wao sana kutokana na kuugua kwake , lakini wakati huo walimuona Edna kama shujaa baada ya hali kutengemaa na tatizo kuonekana kama vile halijatokea na hayo maua yote yaliokuwa yamepambwa kwenye ofisi ya Edna yametoka kwa wafanyakazi wa kampuni hio , walionekana kumkubali sana Bosi Edna kwa juhudi zake alizokuwa akifanya kwa kampuni, kwao Edna alikuwa sio bosi tu , lakini walimuona kama shujaa, na hii yote ni kutokana na namna Edna alivyokuwa akiwajali wafanyakazi wake , kuanzia mazingira ya kazi , mpaka mishahara yao, Edna alikuwa CEO wa kuigwa , licha ya kuwa kauzu , lakini alikuwa akijali kila mfanyakazi na alihakikisha kila mfanyakazi jasho lake linathaminiwa na kampuni , Edna hakuwa mnyonyaji na alikuwa msikilizaji na mtu wa kutoa maamuzi na alikuwa akisimamisa sheria na haki katika kufanya kwake maamuzi na hilo lilimjengea heshima kubwa tokea apewe kampuni hio kutoka kwenye mikono ya mama yake.
“Nasra nitahitaji uidhinishe kiasi cha bilioni mbili kwenda Vexto Media and Entertainment”Aliongea Edna.
“Sawa bosi lakini nadhani kutokana na malengo ya kampuni na uendeshaji wake kitakuwa kiwango kidogo sana , nilipiga mahesabu na kuona Bilioni tano ndio zinaweza kutosha”
“Nalifahamu hivyo ndio maana nataka kuidhinisha kiasi hiko , nataka nione hatua atakazochukua Director kuendesha kampuni na kiasi kidogo cha pesa na isitoshe mpaka sasa tunakampuni lakini juu ya uendeshaji hatujapanga”Aliongea Edna na kumfanya Nasra kushangaa kidogo.
“Boss unapanga nani kuwa Director?”Aliongea Nasra na Edna alifikiria kidogo.
“Napanga kumuachia Roma Ramoni awe Director”Aliongea na kumfanya Nasra kutoa macho kwa mshangao , ilikuwa ni taarifa mpya kwake.