singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
-
- #1,221
SEHEMU YA 225
Kusanyiko lilikuwa ni Zaidi ya lilivyokusudiwa , kwani licha ya kwamba sababu kubwa ilikuwa ni kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa ajili ya kupanda cheo, lakini wafanyakazi walionekana kufurahia Pamoja na kufanya ukaribu wao kuongezeka, hususani kwa wafanyakazi na bosi wao Edna kwani siku zote walikuwa wakimuona kwa mbali.
“Jamani tumepoa sana , usiku huu ungekuwa mzuri kama tungekuwa na msanii wa kutuburudisha”Aliongea Ernest Komwe na kufanya kila mtu amwangalie anachotaka kusema.
“Mnaonaje mmoja wetu anaejua kuimba akatoka mpaka pale mbele na kutuburudisha ninazo instrumental Beat za nyimbo maarufu kwenye simu lakini pia nina hiki”Aliongea Ernest Komwe huku akionyesha kijispika kidogo kampuni ya Anker alichoshikilia mkononi na alifika nacho wakati wa kuja , lakini hakuna ambaye alifahamu kuwa ni kijispika.
“Nitaanza..!”Ni Sauti ya Recho ndio ambayo ilisikika na kufanya kila mtu kufurahi , Recho alionekana wine alizokunywa zishaanza kumuingia kisawa sawaa na na hata ile hofu aliokuwa nayo mbele ya Boss wake ilikuwa imemwishia.
Watu walipiga makofi baada ya Recho kusogea mbele kabisa kwenye ukumbi huu na uzuri ni kwamba ukumbi ambao walikuwa wameuchukua kwa ajili ya mkusanyiko wao ulikuwa ni binafsi , hivyo kilichokuwa kikiendelea ndani hakikuweza kusikika nje.
Wakati watu wote macho yao wakiyaelekeza kwa Recho kwa ajili ya kusikiliza kile ambacho anakwenda kuimba , Nadia Alfonso alinyanyuka kutoka sehemu alikuwa amekaa na kisha akamsogelea Roma.
“Roma tunaweza kuongea?”Aliuliza Nadia na kumfanya Roma aliekuwa akisubiria kwa hamu kumuona Recho akiimba ageuze shingo na kumwangalia Nadia.
“Nadia si unaona tupo katikati ya burudani , hatuwezi kusubiri?”Aliuliza Roma huku akimwangalia Nadia.
“Ni muhimu sana , hatuchukui muda mrefu… pleaese”Aliongea Nadia kwa namna ya kubembeleza na Roma alijikuta akivuta pumzi na kuzishusha.
Ukweli hakujua Nadia alikuwa akitaka kuongea nini na yeye , kwani tokea alivyomuacha Nadia kwenye mikono ya Stern na Alice kule Ufaransa hakuongea nae tena na hata pale alipofahamu ukaribu uliokuwepo kati ya Nadia na Depney hakuona haja ya kutafuta maelezo Zaidi na aliondoka kurejea Tanzania na kumuacha pasipo kuonana nae tena, lakini kwa jinsi Nadia alivyokuwa akionekana mbele yake aliona kabisa huwenda kuna jambo Zaidi ya lile ambalo anahisi kwenye akili yake Nadia anataka kumwambia.
Roma alimwangalia Edna ambaye alionekana muda wote macho yake yalikuwa yakimwangalia Recho ambaye ashaanza kuimba kwa madaha na kisha akamgeukia Nadia.
“Wapi unataka tukaongee?”
“Naomba unifuate”Aliongea Nadia huku akianza kupiga hatua kuelekea nje ya ukumbi huo na Roma bila ya kufikiria mara mbili mbili aliamua kunyanyuka na kumfuata.
“Nadia hatupaswi Kwenda mbali sana , sijamuaga Edna”Aliongea Roma baada ya kuona Nadia anazifuata Lift.
“Roma hatuchukui muda mrefu naomba unifuate”Aliongea Nadia huku akibonyeza Lift na kusubiria ifunguke na ndani ya dakika moja ilifunguka na Roma ilibidi aingie kwenye Lift hio Pamoja na Nadia.
“Roma nafahamu unayo maswali mengi ya kilichotokea Paris and I real need to Explain it”Aliongea Nadia.
“Nadia kama unataka kuongea juu ya hili nikuambie tu, huna haja ya kujielezea kabisa , ijapokuwa sijui ukweli wote lakini naaminini halina maana tena kwani Depney alishafariki na ulishuhudia kwa macho yako”Aliongea Roma na muda huo huo Lift ilifunguka juu kabisa kwenye korido yenye vyumba vingi vya kulala.
“Kwahio kweli hutaki nikijielezea…?”Aliongea Nadia huku wakitembea ki upande upande.
“Nadia nishakuambia hauna haja ya kujielezea na sidhani ndio swala ambalo ni muhimu ambalo unataka kuniambia”Aliongea
“Ndio kuna swala lingine muhimu, ila najihisi uhitaji wa kujielezea natumaini utanipa nafasi , I need you to see the reason”Aliongea Nadia na muda huu walikuwa washafika kwenye mlango wa chumba namba 117 ndani ya hoteli hii na Nadia alitoa kadi yake kwenye mkoba wake na kuchomeka kwa kutumia mkono wa kushoto.
Ndio Nadia alikuwa akitumia mkono wa kushoto hata kwenye maswala ya kuandika na mkono wake wa kulia haukuwa na nguvu kabisa.
Baada ya mlango kufunguka Nadia alimpa ishara Roma kuingia na Roma ni mtu ambaye alikuwa akijiamini na hakusita sita kwani aliingia na akafuatia Nadia.
Ni chumba aina ya Super Deluxe , See View na Roma aliendezwa na mpangilio na uzuri wa chumba , mbele kabisa ya chumba hiki alionekana mwanamke ambaye amevalia taulo akiwa amesimama akiangalia upande wa baharini , alikuwa ni mwanamke wa Kizungu na kwa haraka haraka Roma kwa kuangalia nywele zake aligundua kabisa mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa si chini ya miaka sitini na tano ki umri.
“Madam Roma has arrived”Aliongea Nadia kwa Kingereza na Roma alienda moja kwa moja kukaa kwenye masofa huku akimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake , akisubiria ageuka amuone.
“Thank you Nadia for this, now we can talk”Aliongea yule mwanamke kwa sauti yake ya kiutu uzima na akageuka na kisha akatembea kwa kujiamini na kumsogelea Roma.
“Mr Roma naitwa Joyce Donald naomba nitangulize radhi kwa kuingilia ratiba yako usiku huu”Aliongea yule mwanamke wa Kizungu huku akinyoosha mkono kumpatia Roma kama salamu , lakini Roma hakuupokea.
“Joyce umeingilia ratiba zangu usiku huu, lakini siwezi kuendelea kupoteza muda kama utaendelea kujitambulisha kwangu kwa jina feki na sura bandia”Aliongea Roma kwa pasipo kubadili miuonekano wake na kumfanya Joyce kushangaa kidogo na kisha akatabasamu.
“Hakika wewe ni Hades mwenye kusikika na sifa nyingi , sikuweza kudhania unaweza kunitambua kwa sura bandia ilihali ni mara yetu ya kwanza kuonana , tafadhari naomba uniwie radhi na nitajirambulisha kwa majina yangu halisi”Aliongea kwa Kingereza huku akiketi na kukunja nne kwenye sofa na kumfanya hadi mapaja yake kuwa wazi kutoka na kuvaa taulo tu , lakini kwake hakuona shida.
Upande wa kule ukumbini licha ya kwamba Edna alikuwa bize akimwangalia Recho aliekuwa akiimba , lakini wakati Nadia alivyonyanyuka na kumsogelea Roma aliona kitendo hiko na hata wakati wanatoka pia aliona na Edna baada ya kupita kama dakika nne za Roma na Nadia kutoka na yeye alinyanyuka na kuusogelea mlango wa kutokea na kufanya baadhi ya wafanyakazi wamwangalie , lakini hawakujali kwani waliamini huenda Edna anaenda maliwatoni.
Edna baada ya kutoka nje kabisa , alikumbana na Korido ndefu ambayo haikuonekana kuwa na mtu anaefanana na Roma wala Nadia , alijiuliza Roma kaelekea wapi.
Ukweli hali ya wivu ilimwingia baada ya kumuona Nadia akitoka na Roma hivyo aliamini huenda kuna jambo la kishenzi ambalo Nadia na Roma walikuwa wakipanga kulifanya na ndio maana alitoka kwa ajili ya kuangalia usalama wa mume wake , lakini sasa anajikuta kuwa na wasiwasi Zaidi baada ya kutokumuona Roma ndani ya hilo eneo.
Baada ya kuangalia kulia na kushoto pasipo ya kuona dalili ya Roma alianza kupiga hatua kuelekea upande wa Lift na haikueleweka alikuwa akipanga kufanya nini, lakini alienda na akabonyeza kitufe na lift ilionekana kutokuwa na mtu kwani ilifunguka na aliingia.
“Damn you Roma , umeelekea wapi na yule mwanamke”Aliwaza Edna huku hasira na wivu vikianza kuutekenya moyo wake , Edna hakuwa tayari kumuona Roma akiongeza mchepuko mwingine na ndio maana mpango wake wa kuja kwenye hilo kusanyiko nje ya utaratibu yake ni kumchunga Roma , lakini muda huo alijikuta akiwa amepigwa chenga.
“Ding!”Lift iligonga kengere kuashilia inafunguka eneo la Ground Floor na Edna aliangalia mbele baada ya mlango kuachiana , lakini alijikuta akishangaa baada ya kumuona mwanaume aliekuwa mbele yake.
“Edna… how Unfortunates!”Ilikuwa ni sauti ya mwanaume , nzito iliosikika mbele ya Edna.
Kusanyiko lilikuwa ni Zaidi ya lilivyokusudiwa , kwani licha ya kwamba sababu kubwa ilikuwa ni kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa ajili ya kupanda cheo, lakini wafanyakazi walionekana kufurahia Pamoja na kufanya ukaribu wao kuongezeka, hususani kwa wafanyakazi na bosi wao Edna kwani siku zote walikuwa wakimuona kwa mbali.
“Jamani tumepoa sana , usiku huu ungekuwa mzuri kama tungekuwa na msanii wa kutuburudisha”Aliongea Ernest Komwe na kufanya kila mtu amwangalie anachotaka kusema.
“Mnaonaje mmoja wetu anaejua kuimba akatoka mpaka pale mbele na kutuburudisha ninazo instrumental Beat za nyimbo maarufu kwenye simu lakini pia nina hiki”Aliongea Ernest Komwe huku akionyesha kijispika kidogo kampuni ya Anker alichoshikilia mkononi na alifika nacho wakati wa kuja , lakini hakuna ambaye alifahamu kuwa ni kijispika.
“Nitaanza..!”Ni Sauti ya Recho ndio ambayo ilisikika na kufanya kila mtu kufurahi , Recho alionekana wine alizokunywa zishaanza kumuingia kisawa sawaa na na hata ile hofu aliokuwa nayo mbele ya Boss wake ilikuwa imemwishia.
Watu walipiga makofi baada ya Recho kusogea mbele kabisa kwenye ukumbi huu na uzuri ni kwamba ukumbi ambao walikuwa wameuchukua kwa ajili ya mkusanyiko wao ulikuwa ni binafsi , hivyo kilichokuwa kikiendelea ndani hakikuweza kusikika nje.
Wakati watu wote macho yao wakiyaelekeza kwa Recho kwa ajili ya kusikiliza kile ambacho anakwenda kuimba , Nadia Alfonso alinyanyuka kutoka sehemu alikuwa amekaa na kisha akamsogelea Roma.
“Roma tunaweza kuongea?”Aliuliza Nadia na kumfanya Roma aliekuwa akisubiria kwa hamu kumuona Recho akiimba ageuze shingo na kumwangalia Nadia.
“Nadia si unaona tupo katikati ya burudani , hatuwezi kusubiri?”Aliuliza Roma huku akimwangalia Nadia.
“Ni muhimu sana , hatuchukui muda mrefu… pleaese”Aliongea Nadia kwa namna ya kubembeleza na Roma alijikuta akivuta pumzi na kuzishusha.
Ukweli hakujua Nadia alikuwa akitaka kuongea nini na yeye , kwani tokea alivyomuacha Nadia kwenye mikono ya Stern na Alice kule Ufaransa hakuongea nae tena na hata pale alipofahamu ukaribu uliokuwepo kati ya Nadia na Depney hakuona haja ya kutafuta maelezo Zaidi na aliondoka kurejea Tanzania na kumuacha pasipo kuonana nae tena, lakini kwa jinsi Nadia alivyokuwa akionekana mbele yake aliona kabisa huwenda kuna jambo Zaidi ya lile ambalo anahisi kwenye akili yake Nadia anataka kumwambia.
Roma alimwangalia Edna ambaye alionekana muda wote macho yake yalikuwa yakimwangalia Recho ambaye ashaanza kuimba kwa madaha na kisha akamgeukia Nadia.
“Wapi unataka tukaongee?”
“Naomba unifuate”Aliongea Nadia huku akianza kupiga hatua kuelekea nje ya ukumbi huo na Roma bila ya kufikiria mara mbili mbili aliamua kunyanyuka na kumfuata.
“Nadia hatupaswi Kwenda mbali sana , sijamuaga Edna”Aliongea Roma baada ya kuona Nadia anazifuata Lift.
“Roma hatuchukui muda mrefu naomba unifuate”Aliongea Nadia huku akibonyeza Lift na kusubiria ifunguke na ndani ya dakika moja ilifunguka na Roma ilibidi aingie kwenye Lift hio Pamoja na Nadia.
“Roma nafahamu unayo maswali mengi ya kilichotokea Paris and I real need to Explain it”Aliongea Nadia.
“Nadia kama unataka kuongea juu ya hili nikuambie tu, huna haja ya kujielezea kabisa , ijapokuwa sijui ukweli wote lakini naaminini halina maana tena kwani Depney alishafariki na ulishuhudia kwa macho yako”Aliongea Roma na muda huo huo Lift ilifunguka juu kabisa kwenye korido yenye vyumba vingi vya kulala.
“Kwahio kweli hutaki nikijielezea…?”Aliongea Nadia huku wakitembea ki upande upande.
“Nadia nishakuambia hauna haja ya kujielezea na sidhani ndio swala ambalo ni muhimu ambalo unataka kuniambia”Aliongea
“Ndio kuna swala lingine muhimu, ila najihisi uhitaji wa kujielezea natumaini utanipa nafasi , I need you to see the reason”Aliongea Nadia na muda huu walikuwa washafika kwenye mlango wa chumba namba 117 ndani ya hoteli hii na Nadia alitoa kadi yake kwenye mkoba wake na kuchomeka kwa kutumia mkono wa kushoto.
Ndio Nadia alikuwa akitumia mkono wa kushoto hata kwenye maswala ya kuandika na mkono wake wa kulia haukuwa na nguvu kabisa.
Baada ya mlango kufunguka Nadia alimpa ishara Roma kuingia na Roma ni mtu ambaye alikuwa akijiamini na hakusita sita kwani aliingia na akafuatia Nadia.
Ni chumba aina ya Super Deluxe , See View na Roma aliendezwa na mpangilio na uzuri wa chumba , mbele kabisa ya chumba hiki alionekana mwanamke ambaye amevalia taulo akiwa amesimama akiangalia upande wa baharini , alikuwa ni mwanamke wa Kizungu na kwa haraka haraka Roma kwa kuangalia nywele zake aligundua kabisa mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa si chini ya miaka sitini na tano ki umri.
“Madam Roma has arrived”Aliongea Nadia kwa Kingereza na Roma alienda moja kwa moja kukaa kwenye masofa huku akimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake , akisubiria ageuka amuone.
“Thank you Nadia for this, now we can talk”Aliongea yule mwanamke kwa sauti yake ya kiutu uzima na akageuka na kisha akatembea kwa kujiamini na kumsogelea Roma.
“Mr Roma naitwa Joyce Donald naomba nitangulize radhi kwa kuingilia ratiba yako usiku huu”Aliongea yule mwanamke wa Kizungu huku akinyoosha mkono kumpatia Roma kama salamu , lakini Roma hakuupokea.
“Joyce umeingilia ratiba zangu usiku huu, lakini siwezi kuendelea kupoteza muda kama utaendelea kujitambulisha kwangu kwa jina feki na sura bandia”Aliongea Roma kwa pasipo kubadili miuonekano wake na kumfanya Joyce kushangaa kidogo na kisha akatabasamu.
“Hakika wewe ni Hades mwenye kusikika na sifa nyingi , sikuweza kudhania unaweza kunitambua kwa sura bandia ilihali ni mara yetu ya kwanza kuonana , tafadhari naomba uniwie radhi na nitajirambulisha kwa majina yangu halisi”Aliongea kwa Kingereza huku akiketi na kukunja nne kwenye sofa na kumfanya hadi mapaja yake kuwa wazi kutoka na kuvaa taulo tu , lakini kwake hakuona shida.
Upande wa kule ukumbini licha ya kwamba Edna alikuwa bize akimwangalia Recho aliekuwa akiimba , lakini wakati Nadia alivyonyanyuka na kumsogelea Roma aliona kitendo hiko na hata wakati wanatoka pia aliona na Edna baada ya kupita kama dakika nne za Roma na Nadia kutoka na yeye alinyanyuka na kuusogelea mlango wa kutokea na kufanya baadhi ya wafanyakazi wamwangalie , lakini hawakujali kwani waliamini huenda Edna anaenda maliwatoni.
Edna baada ya kutoka nje kabisa , alikumbana na Korido ndefu ambayo haikuonekana kuwa na mtu anaefanana na Roma wala Nadia , alijiuliza Roma kaelekea wapi.
Ukweli hali ya wivu ilimwingia baada ya kumuona Nadia akitoka na Roma hivyo aliamini huenda kuna jambo la kishenzi ambalo Nadia na Roma walikuwa wakipanga kulifanya na ndio maana alitoka kwa ajili ya kuangalia usalama wa mume wake , lakini sasa anajikuta kuwa na wasiwasi Zaidi baada ya kutokumuona Roma ndani ya hilo eneo.
Baada ya kuangalia kulia na kushoto pasipo ya kuona dalili ya Roma alianza kupiga hatua kuelekea upande wa Lift na haikueleweka alikuwa akipanga kufanya nini, lakini alienda na akabonyeza kitufe na lift ilionekana kutokuwa na mtu kwani ilifunguka na aliingia.
“Damn you Roma , umeelekea wapi na yule mwanamke”Aliwaza Edna huku hasira na wivu vikianza kuutekenya moyo wake , Edna hakuwa tayari kumuona Roma akiongeza mchepuko mwingine na ndio maana mpango wake wa kuja kwenye hilo kusanyiko nje ya utaratibu yake ni kumchunga Roma , lakini muda huo alijikuta akiwa amepigwa chenga.
“Ding!”Lift iligonga kengere kuashilia inafunguka eneo la Ground Floor na Edna aliangalia mbele baada ya mlango kuachiana , lakini alijikuta akishangaa baada ya kumuona mwanaume aliekuwa mbele yake.
“Edna… how Unfortunates!”Ilikuwa ni sauti ya mwanaume , nzito iliosikika mbele ya Edna.