Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 234
Baga kutokana na wivu wake na mipango yake aliokuwa nayo juu ya Mage , alishindwa kabisa kuendelea na safari , alirudi ndani ya ukumbi kwa namna ya kunyata , ili kutaka kufahamu kinachoendelea, lakini alichokiona kilimnyong`onyesha kabisa na kukunja ngumi na kurudi alikotoka.
Kiss liliendelea kwa takribani dakika tano tu , Roma alimwachia Mage na kumvuta kwenye chumba cha pembeni kilichotumika kuhifadhia vifaa na kisha akamkandamiza Mage ukutani na wakaendelea kudendeka kwa dakika mbili Zaidi na kisha akashika Mkanda wa Kombati ya jeshi ya Mage na kuanza kuifungua haraka haraka na Roma alionekana kuzijulia kombati za jeshi kwani ndani ya dakika mbili tu alikuwa ashaifikia nguo ya ndani ya Mage na kuishusha chini.
Mage hisia alizokuwa akizipata hazikuwa zikielezeka kabisa na hakuwahi kuzihisi katika Maisha yake na alijilaumu kwa miaka yote kutumia viungo bandia kujiridhisha na kukosa mambo matamu ya kiasili.
Roma hakutaka kumrembesha Mage kabisa aliamua amalizane nae moja kwa moja na ndio maana baada ya kumbakisha Mage pasipo kua na nguo alishusha suruali yake pasipo kuivua na kisha akambeba Mage juu juu na kurengesha mpini na kilichoendelea hapo ni Mage kutoa miguno ya kimahaba huku akijihisi yupo kwenye sayari ya Neptune.
Lisaa limoja mbele Roma alikuwa ashamwazibu Afande Mage kwa mikwaju ya kutosha na kutupia goli kimiani pasipo ya kuwa na wasiwasi kabisa na kwa upande wa Mage hakuelewa amepanda mlima na kushuka mara ngapi kwani network zilikuwa zikija na kupotea kwa wakati mmoja.
“Afande usiniambie ndio unaanza kunionea aibu” Aliongea Roma huku akitabasamu kifedhuli na kuchukua nguo ya ndani ya Mage na kufuta bunduki yake huku Mage akiangalia kitendo ambacho Roma anafanya mbele yake bila aibu na Mage kabla hajajibu simu ya Roma ilianza kuita mfululizo na alimpa Mage nguo yake na kupandisha suruali. Huku Mage na yeye akivaa kombati yake ya kijeshi na kuweka nguo yake nyeupe ndani ya kombati ya jeshi.
“Director ni mimi Daudi , CEO kanipa namba yako ya simu niwasiliane na wewe”ilisikika sauti upande wa pili ya mwanaume na kumfanya Roma afikirie jina la Daudi na kwakua kumbukumbu zake zilikuwa nzuri haraka haraka alikumbuka Daudi alikuwa moja ya wafanyakazi waliochaguliwa na mke wake kwa ajili ya kumsaidia katika maswala ya kampuni mpya inayokwenda kufnnguliwa.
“Ndio Daudi , nishakukumbuka unasemaje?”
“Director kuna baadhi ya mambo tumeshindwa kutoyafanyia maamuzi kwasababu yanahitajika uwepo wako”Aliongea Daudi.
“Ongea na Edna atafanya maamuzi”Aliongea Roma.
“Miss Edna kasema tukutafute wewe ndio ufanye maamuzi , yeye ana kazi zinazomuhusu”Aliongea Daudi na kumfanya Roma afikirie na kumuona Edna anajaribu kufanya nini , kwani kampuni ilikuwa ya kwake , kwanini mpaka yeye afanye maamuzi.
Ila Roma kwakuwa aliona alikuwa na bifu na mke wake , basi hakuona haja ya kukataa simu ya wito kutoka kwa Daudi , aliona kama atafanya vizuri basi hata Edna anaweza kuacha kumnunia na wakatudi katika hali ya kawaida.
“Okey Mr Daudi ninakuja baada ya masaa mawili maana niko nje ya mji”Aliongea.
“Sawa Director , tupo ndani ya jengo la Kampuni”Aliongea na Roma aliitikia na kukata simu, na kisha alimwangalia Mage aliekuwa akiona aibu mbele yake.
“Haina jana ya kuona aibu , kilichofanyika hapa kina maana kubwa kwetu , Afande Mage unaonaje ukirudi na kuendelea na upolisi”
“Nini..!! Hapana”Aliongea Mage huku akibadilika ba kurudi kwenye hali yake.
“Mimi naondoka , tutaongea vizuri ukisharudi nyumbani , kama unataka kuendelea kuwa mwanajeshi basi siwezi kukupinga .. mimi nawahi kazini simu iliopigwa ni ya muhimu sana”Aliongea Roma pasipo ya kumpa Mage nafasi ya kujielezea.
******
Masaa mawili mbele Roma alikuwa mikocheni akiingia ndani ya jengo la kampuni yao mpya ambayo anakwenda kuongoza.
Na Daudi Pamoja na Wendy walionekana walikuwa wakimsubiri , kwani walikuwa chini kabisa ya jengo hili na walitabasamu na kumsogelea Roma kwa heshima.
“Director you are here?”Aliongea Daudi huku akimpa mkono Roma na Roma alitabasamu kwa namna wawili hao walivyokuwa wakimpa heshima yake na Roma alisalimiana nao kwa bashasha na kuwaambia waelekee juu na ndani ya dakika chache tu , wote kwa Pamoja waliingia kwenye ofisi na Roma alienda kwenye kiti chake.
“What is These?”Aliuliza Roma baada ya kuona faili kibao ambazo zimerundikwa kwenye meza yake.
“Director , mpaka sasa maandalizi yamekamilika na karatasi hizo ni juu ya mapendekezo ya Projekti nane ambazo tutaanza nazo”Aliongea kwa kingereza.
Roma alichukua mafaili hayo na kuyapitia haraka haraka na kisha akayaweka yote chini na kuaangalia wasaidizi wake.
“Nimeona mnataka pia kujihusisha na utengenezaji wa filamu , jambo ambalo naona sio baya pia, lakini pia upande wa ufadhili wa Shows na wasaniii ni jambo ambalo litahitaji msaada wa nje na uhusikaji wa moja kwa moja na kiwango cha pesa kinaweza kuwa kikubwa”
“Ndio Director , ijapokuwa tumepanga kufadhili filamu , lakini pia tumepanga kutengeneza lebo ambayo itatufanya tuwe na uwezo wa kusainisha mikataba wasanii wakubwa nchini , lakini kutokana na kwamba tunaanza, tumeona kuchukua wasanii wenye vipaji vikubwa ambao hawajajulikana sana ili kupunguza gharama”
“Let me ask you a question.”Aliongea Roma na kumfanya Wendy kushangaa na kisha kumpa nafasi ya kuuliza.
“Ni ukubwa kiasi gani wa kampuni ya Vexto mpaka sasa?”Wendy hakuelewa kwanini Roma anauliza swali la namna hio , lakini aliona ajibu.
“Ukiachana na ‘Liquid Fund’ , kampuni ina thamani ya Dola bilioni therathini kwa ujumla wake wa Asset”
“Na ndani ya taifa inashika nafasi ya ngapi mpaka sasa?”
“Kwasasa ni ya kwanza kwa ukubwa na baada ya miezi kadhaa mbele malighafi kutoka Japani zitakapokamilika inaweza kuingia kwenye kumi bora ya kampuni kubwa ndani ya Afrika”Aliongea.
“Sasa kwa mtazamo wenu , mnafikiri inakuwaje kwa kampuni yenye jina kubwa kama Vexto kufungua kampuni nyingine na kufanya uwekezaji mdogo kama mlivyoainisha kwenye hizi projekti zenu?”
“Director, you’re saying…”
“Ndio , kutakuwa na uwezekano wa mambo makuu mawili , kwanza watu watatuona kama hatuna utayari wa kibiashara , lakini pili tutaonekana kama watu ambao hatuna ujasiri kwa kile tunachokifanya na pia hatujiamini, Vexto ni kampuni kubwa na kila kitu tunachofanya lazima kiendane na ukubwa wa jina la kampuni na kwa hizi Projecti zenu naamini hata wanabodi wanaweza wasilidhishwe nazo , lakini pia kwa Boss wetu Edna hatoridhishwa na maamuzi yetu kama kiongozi wa kampuni, lakini ukiachana na hayo pia washindani wetu watatuchukulia wa kawaida sana kibiashara”
“Director maneno yako yanaonekana kuwa na mantiki , ni kweli kwasababu kampuni ndio kwanza inaanza basi hata uwezekezaji wetu , lazima uwe mkubwa ili kuteka ‘Attention’ ya soko kwa ujumla wake, lakini pesa ambayo Boss Edna ametenga kwa ajili ya kampuni licha ya kutosha ,lakini kuwekeza kiasi chote kwenye projekti moja ni jambo la hatari kwa kampnni , kwani tutakosa mzunguko wa pesa”
“Ndio Director , kama tutawekeza kiasi kikubwa cha pesa itakuwa hatati kubwa”Aliongezea Daudi kuunga hoja mkono.
“Hakuna haja ya kufikiria kuhusu pesa , kuna muwekezaji ambaye yupo tayari kutuunga mkono”Aliongea Roma na kuwafanya washangae.
“Wendy utahusika na swala la kuongea na muwekezaji na nitakupatia mawasiliano namna ya kuwasiliana nae”Aliongea Roma huku akianza kumkumbuka Rose.
Daudu na Wendy baada ya kusikia kuwa kuna muwekezaji ambaye yupo tayari kwa ajili ya kuingiza hela zake kwenye kampuni walijikuta wakifurahi mno na kuanza kuona mafanikio , lakini pia hawakuacha kujiuliza Roma aliwezaje kushawishi muwekezaji haraka hivyo.
Wasicho kifahamu ni kwamb Roma alikuwa ashaongea na Rose tayari kabla hata ya kukutana nao .
“Kuhusu upande wa Lebo ambayo mmepanga kusainisha wasanii Pamoja na waigizaji mtaendelea nayo , lakini sitaki wasanii wadogo wadogo , ila kama waweka bei kubwa Zaidi mtaachana nao , kwani tunao uwezo wa kuibua vipaji sisi wenyewe kama kampuni”
“Director unamaanisha Telent Shows?”
“Ndio ninchomaanisha,, hii itakuwa rahisi Zaidi kufanyika”
“Lakini Dorector mpaka sasa kuna kampuni mbalimbali zinazofanya kitu kama hiki hiki , kwa mfano kampuni ya Benchmark Production ilio chini ya Rita Poulsen inafanya mashindano ya Bongo Star Search na wana umaarufu mkubwa jambo ambalo linaweza kutuletea shida kiushindani”Aliongea Wendy.
“Andaeni shindano ndani ya mwezi huu na aanzeni kulitangaza , kuhusu namna ya kulifanya maarufu niachieni mimi”Aliongea Roma na kufanya wawili hawa washangae mno , lakini walishindwa kupinga , ila walijiuliza ni kwa namn gani Roma ataweza kufanya shindao liwe maarufu Zaidi kuzidi la Bongo Star Search.
Ukweli Roma aliona apendekeze tukio la namna hio ili kumpa Sophia nafasi na yeye kushiriki, ili kuonyesha kipaji chake na aliona ndio njia ya haraka ya Sophia kuwa maarufu.
 
SEHEMU YA 235.
Ilikuw ani siku ya jumapili , Edna aliamka asubuhi kama kawaida , huku akichangamkiwa na Blandina mama yake Roma wakati anashuka mezani kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.
Blandina tokea ujue ukweli kwamba Edna aliolewa akiwa Bikra basi alitokea kumpenda mno na kuona pia mtoto wake ana bahati sana kupendewa na mwanamke mrembo kama Edna.
Sasa tokea siku hio alikuwa akihakikisha anamuonyeshea Edna mapenzi ya aina yake ili asijione mpweke na ahisi yupo kwenye familia sahihi na mume wake Roma nichaguo bora.
Sasa muda wa asubuhi Roma alikuwa na wanafamilia wengine kwenye meza wakijipatia kifungua kinywa , ili baada ya hapo ratiba zingine ziendelee.
“Edna bado unaendelea na utaratibu wa Kwenda kule kituoni kila siku ya jumapili?”Aliongea Blandina na kumfanya Edna atabasamu na kumwangalia mama mkwe wake.
“Ndio na nishajiandaa nataka kuelekea huko asubuhi ya leo”Aliongea Edna na kumfanya Blandina atabasamu.
“Edna mwanangu , najua sijawahi kukuambia haya , lakini nashukuru sana kwa msaada wako juu ya kuwasaidia wale Watoto, baada ya mama yako kufariki nilikuwa na wasiwasi mno ya kupata mfadhili mwingine , lakini nashukuru haujaacha kuendeleza kile ambacho mama yako na bibi yako walikuwa wakikifanya”
“Mama huna haja ya kunishukuru zaidi ya kwamba pongezi nizielekeze kwako kwani kituo kile kimekuwa sehemu ya familia yangu na nafarijika kila ninapo waona wale Watoto wakiishi kwenye mazingira safi na salama”Aliongea Edna na Blandina alijikuta akitabaamu na kujiambia yes huyu ndio mkwe.
“Leo tutaenda wote, nina siku nyingi sijaonana na Mama Issa”Aliongea huku akimwangalia Yezi na Edna aliitikia kwani hakuona ubaya na isitoshe Blandina alikuwa ni mwanzilishi wa kile kituo.
Saa tatu kamili Edna ndio aliekuwa akiendesha gari kuelekea Kiwangwa na walikuwa washanunua mahitaji maalumu tayari kwa ajili ya Watoto na ilikuwa ni kazi ya kupeleka tu.
“Edna niseme tena asante…. Nakushukuru sana mwanangu”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kupunguza mwendo.
“Mama kwanini unanishukuru hivyo”
“Edna hujui ni kiasi gani nimefurahishwa na wewe kumkubali mwanangu na kumpenda na kuvumilia madhaifu yake , mimi kama mama yake nakushukuru sana kwa kumpenda Roma na kumvumilia , hata nikiondoka kwenye huu ulimwengu najua anazaidi ya mama”Aliongea Blandina na kumfanya Edna ashindwe jinsi ya kujibu , kwanza aliona aibu na kukosa utulivu pia na alijua pia Blandina atakuwa ashaona Maisha yao wanavyoishi na mume wake Roma.
Lakini wakati huo Edna alikumbuka kuwa licha ya kwamba ni kweli anajihisi kuwa na hisia za kimapenzi na Roma , lakini ndoa yao ni ya kimkataba na ndio maana wanaishi kama sio wanandoa.
“Edna nitajitahidi kuhakikisha Roma anabadili tabia yake , nimesikia kila kitu kutoka kwa Bi Wema juu ya Roma kutoka nje ya ndoa , naomba umvumilie nitamrekebisha , nimeomba tuje wote huku kwasababu nilitaka kukuambia hivyo”Aliongea na Edna akatabasamu na kuitikia kwa kichwa na muda huu tayari walikuwa wakiingia kituoni.
Mama Issa alikuwa na taarifa za ujio wa rafiki yake Blandina na alionekana kusimama nje ya jengo lake kwa kumsubiria kwa hamu na ile gari inaingia hapo ndani kituoni alisogelea na walikumbatiana na Blandina baada tu ya kutoka.
“Edna karibuni sana..”Aliongea Mama Issa kwa furaha huku akiwakaribisha na Edna aliacha ufunguo kwa wafanyakazi kwa ajili ya kutoa mizigo nyuma,
Stori za bapa na pale kati ya Mama Issa zilianza na Edna kama kawaida yake alijichanganya na Watoto na kuanza kucheza nao kwa furaha , alionekan kufika kwenye ulimwengu wake , kwani alicheka kama sio yeye vile na kumfanya kupendeza na Mama Issa na Blandina walifurahia kwa jinsi walivyokuwa wanamuangalia.
“Blandina hongera sana kwa kumpata mtoto wako Denisi, unajua baada ya kupewa taarifa na Jestina nilianza kufikiria siku ya kwanza Edna na Mr Roma walivyofika hapa ndani ya kituo”Aliongea Mama Issa na kumfanya Blandina amuangalie kama mtu ambaye akisubiria Blandina aendele kuongea.
“Unakumbuka kuwa kuna picha yako ambayo ipo pale ofisini kwani?”
“Ndio nakumbuka na ile picha ipo kwa kila kituo nilichofungua”Aliongea Blandina.
“Sasa siku ya kwanza Mr Roma kuangalia ile picha nilihisi mabadiliko yake ila niliyapotezea kwani nilimuona kama mtu mzuri”Aliongea Mama Issa.
“Unazungumzia mabadiliko ya aina gani?”
“Kwanza aliangalia picha yako kwa muda mrefu sana, lakini kuna kitu sio cha kawaida ambacho kilimtokea , niliona macho yake yakibadilika kwa kupitia kioo cha ofisini kwangu”Aliongea Mama Issa na kumfanya Blandina kushangaa
“Macho kubadilika , mbona sijakuelewa hapo Tabea”Aliongea na kumuita jina lake halisi.
“Sijui nielezeje , ila macho yake yalibadilika na kuwa na kiini cha rangi ya kijani , japo sikuwa na uhakika sana ila alishindwa kuendelea kuangalia picha yako na kukimbilia nje na mimi sikutaka kuuliza na nilijifanya sijaona kitu na ilibidi niitoe ile picha kwa muda nikihofia mabadiliko yake”Aliongea na kumfanya Blandina kukumbuka tukio la Roma kudhibiti wanausalama wakati anakuja kuonana na familia yake , lakini pia aliweza kukumbuka namna Roma kule Kenya namna alivyoweza kuzuia risasi.
“Tabea hata mimi nahisi Roma sio wa kawaida kabisa , lakini ninafuraha kwamba nimeonana nae kwa wakati mwingine na huzuni yangu ya kukosa mtoto imepungua kwa sasa , Namshukuru sana Edna kwa kumpokea Roma licha ya kwamba sio wakawaida”Aliongea na kumfanya Mama Issa atabasamu.
“Nampenda sana Edna na hata siku ambayo alimtambulisha Roma kwangu , nilimpenda mume wake pia , niliamini chaguo lake sio baya na kweli Imani yangu ilikuwa sahihi , huyu mtoto namuona kama baraka tokea alivyokuwa mdogo”Aliongea Mama Issa na wote wakageuka na kumwangalia Edna aliekuwa akikimbizana na Watoto kuelekea getini , lakini walishangaa pia Edna akisimama ghafla na macho yake yote kuyaelekeza getini na Watoto wote pia.
Edna alikuwa amemuaona mtoto aliekuwa amesimama kwenye geti , mtoto ambaye sura yake hakuweza kuisahau , alikuwa ni Lanlan.
“Yule mtoto ni nani?”Aliuliza Blandina baada ya kugundua Edna alikuwa akimwangalia mtoto.
“ Ni zadi ya mara tatu namuona sasa , anaishi upande wa pili na siku zote akija anasimama pale getini pasipo ya kuingia ndani”Aliongea Mama Issa na kumfanya Blandisha kushangaa.
“Ni kazuri jamani nakaona kwa mbali lakini anaonekana kufanana na Edna kabisa”
“Ni kweli hata mimi nilikuwa nikisema hivyo , kumbe hata wewe mwenzangu umeona?”Aliongea na wote wakacheka.
“Lanlan..!1”Aliita Edna huku akimsogelea Lanlan.
“Mom..!”Alita Lanlan huku akimsogela Edna kwa kusita sita , lakini Edna baada ya kusikia anaitwa Mama kwa mara nyingine na mtoto huyu moyo wake ulijihisi kitu cha ajabu.
“Lanlan njoo unikumbatie”Aliongea Edna kwa Kingereza kwani alikuwa akifahamu Lanlan hakuwa akijua Kiswahili, sasa kwa upande wa Lanlan ni kama alikuwa akisikia suati mbilimbili , sauti zinazofanana kabisa na ya mama yake mzazi na alionekana kuchanganyikiwa.
“Mom..!”Aliitakwa mara ya pili na Edna ilibidi achuchumae na kumkumbatia Lanlani ambaye machozi yanaanza kumtoka.
“Lanlan usilie tena.. niangalie machoni”Aliongea Edna huku akimwangalia Lanlan machoni na kumfuta machozi kwa mkono.
Sasa kitendo cha Lanlan kumwangalia Edna machoni , sijui nini kilitokea ila miale mnyoofu kama ya jua ilitoka kweye macho ya Lanlan na kutua kwenye macho ya Edna kitendo ambacho kilimfanya Edna kukosa nguvu na palepale alidondoka na kuzimia .
“Moo..om…”Aliita Lanlan kwa sauti na kumfanya Blandina na Mama Issa kukimbia baada ya kuona tukio lile.
*******
GENEVA -USWISI.
Ni ndani ya hoteli ya nyota tano ndani ya hoteli kubwa ya nyota tano , katika chumba cha Presidential Suite , anaonekana The First Black akiwa amekaa kwenye sofa kwa mkao ambao ni kama alikuwa akiongea na mtu , na kwa jinsi alivyokuwa akionekana ni Dhahiri kwamba wasiwasi ulikuwa umemjaa kwenye macho yake.
Na kwa watu ambao walikuwa wamemzoea The First Black , basi wangeshangaa kwa namna ambavyo alikuwa akionekana , Raisi huyu katika kutawala kwake miaka kadhaa nyuma alikuwa akijimini sana na ni mtu ambaye alikuwa akisifika kwa uongozi thabiti ambao umeleta maendeleo makubwa ndani ya Marekani na nje pia na hii ilifanya watu wengi kumkubali sana,
“Have you accomplished the task?”Ilisikika sauti ya kike chumba kizima na haikuelweka sauti hio ilikuwa ikitokea upande gani, lakini kwa mtu ambaye angeweza kuisikia angeifahamu mara moja , ilikuwa ni sauti ya Mwanamke Mrembo Athena na ilionekana alikuwa akitumia mbinu ya kuongea na The First Black pasipo kujionyesha.
“Miss sijakamilisha bado , lakini mpaka sasa hivi kuna mafanikio makubwa”Aliongea The First Black kwa wasiwasi.
“Your taking too much time for small issue like this Mr First Black , I Installed you as head of Zeros Organisation because I belived, you are smart…”
“Unachukua muda mrefu kwa jambo dogo kama hili Mr First Black , nilikufanya kuwa mkuu wa Zeros organization kwasababu niliamini una akili…”
“No.. no..”
“Sitaki uniingilie wakati nikiwa na zungumza”aliongea Athana asieonekana kwa namna ya kuamrisha na First Black mzee huyu mwenye mvi alikuwa mdogo kama Piritoni.
“Tell me about Illuminat?”Aliongea Athena au The Doni na kumfanya Mr First Black kumeza mate na hata hali ya kujiamini ikaongezeka.
“Malaika! .. tafadhati naomba nikueleze hili baada ya kukuona, nimeishi miaka mingi tokea nikiwa Director wa CIA mpaka kuwa raisi kwa kukutii , lakini kwa miaka yote hio sijapata hata nafasi ya kuona unavyofanania, kama tunataka kufanya jambo kubwa kwa dunia hii mimi na wewe naamini huu ni wakati mzuri wa kujionyesha kwangu”Aliongea The Fisr Black.
“Hahaha… kwahio unadhani unanidai kwa kazi uliofanya , unatakiwa kuelewa mimi na wewe hatudaiani , umekuwa mtu mwenye nguvu sana ndani ya Zeros Organisation kwasababu yangu , umekuwa raisi wa Marekani licha ya Ngozi yako kwasababu yangu na mpaka sasa nimekufanya kuwa mtu kuogopeka kwa sababu yangu , unafikiri kwa nilioyafanya unapaswa kunidai au unakitafuta kifo”Aliuliza Athena huku sauti yake ikidhihirisha kukasirika.
“Hapana Malaika .. naomba unisamehe , ni kwamba nimekuwa mtu wa kutamani sana kukuona , sauti yako kila siku imeendelea kuishi kwenye fikra zangu miaka na miaka na nimetengeneza taswira nyingi sana tokea siku ya kwanza naisikia sauti yako”Aliongea.
“Acha kuongea upumbavu , misheni niliokupa ukiweza kuikamilisha nitajionyesha kwako , lakini itakuwa ni kwa mapenzi yangu , kwangu wewe ni binadamu tu ambaye ninaweza kuchukua Maisha yako muda wowote , hivyo jitahadhari sana unavyotaka kupata kitu kutoka kwangu”Aliongea The Don .
“Naomba unisamehe , hili halitajirudia tena Malaika”
“Tell me about Illuminat”Aliongea kwa amri na The First Black alimeza mate na kisha akakaa vizuri.
“They are not Freemason`s”Aliongea The First Black kwa utulivu akimaanisha kwamba Illuminat sio mafreemason
“Endelea kuongea na hakikisha una Ushahidi”

SEHEMU YA 236.
2005- UNKNOWN PLACE
Ni mwaka 2005 anaonekana Athena akiwa amembeba Msichana mdogo rika la miaka kumi na moja hivi akiwa ndani ya kambi ya Kisayansi ambayo bado haikufahamika kambi hio ipo sehemu gani katika uso wa dunia.
Athena baada ya kuingia ndani ya kambi hii ya kufanyia majaribio ya kisayansi , kambi ambayo ilikuwa na teknolojia ya hali ya juu , alimuweka msichana huyo mdogo kwenye sofa ndani ya chumba ambacho kimezungukwa na Skrini nyingi zilizokuwa zikionesha maeneo mbalimbali ya dunia.
Baada ya kumuweka Msichana kwenye sofa , alimpiga kichwani eneo la utosini na palepale msichana yule alishituka kutoka usingizini.
“Where am I?”Ndio swali la kwanza lililotoka kwa mwanadada yule Kwenda kwa Athena ambaye alikuwa akimwangalia kwa kutabasamu kwa namna msichana huyo alivyokuwa akishangaa mazingira mapya aliokuwepo.
“Your in Atarctica Continent Naira” Aliongea Athena huku akimwangalia kwa kutabasamu msichana aliekuwa mbele yake.
Naira hapa alikuwa na miaka kumi na moja tu na kwa jinsi alivyokuwa akionekana ilionyesha ni Dhahiri alikuwa ndani ya maabara akifanya majaribio ya kisayansi, kwani kwa nguo zake alizovalia zilikuwa zikimtambulisha kama mwanasayansi licha ya umri wake mdogo.
Naam sasa tunajua sasa kwamba eneo ambalo Naira ameletwa na Athena ni ndani ya bara la Atarcticta bara ambalo hakuna makazi ya muda mrefu kwa binadamu kutokana na hali ya hewa yake kuwa ya baridi kali.
Naira alishangaa kuambiwa kuwa alikuwa ndani ya bara la Atarctica, kwani dakika kadhaa nyuma alikuwa ndani ya maabara chini ya Zeros Organisation akifanya kazi zake kama kawaida , lakini pia mwanamke mrembo aliekuwa mbele yake hakuwahi kuonana nae kwenye Maisha yake na jambo hilo lilimfanya kushangaa Zaidi.
“Kama kweli nipo ndani ya bara la Antarctica nimefikaje hapa?”Aliuliza Naira huku akishangaa maeneo yote ya chumba alichokuwemo na alijjiambia licha ya kambi ya Zeros aliokuwa akifanyia kazi kuwa na teknolojia kubwa , lakini hapa ndani teknolojia yake ilikuwa sio ya kawaida na akili zake za kisomi zilimwaminisha hivyo kwa asilimia kubwa.
“We teleported”Aliongea Athena huku akisogelea Friji upande wa kushoto kwake na kutoa chupa ya bia mfano wa zile za konyagi na kisha akaweka kilevi kwenye glass mbili na kumsogelea Naira na kumpa ishara ya kupokea, lakini Naira bado alikuwa akiogopa kwani mtu aliekuwa mbele yake hakuwahi kumuona , lakini pia alimwambia mambo ambayo hayawezekani.
“We..tele.. ported , how!”Aliongea kwa namna ya kubabaika na kumfanya Athena kutabasamu huku akimpa ishara ya kupokea kwanza glass ya kilevi na Naira alipokea kwa mikono miwili huku akitetemeka.
“Unaonekana kutokuniamini?” Aliuliza na Naira alishindwa kujibu lakini kwa Athena akatabasamu.
“I can utilize space laws to teleport from one point to onether with maximum speed , I can even manipulate space time”Aliongea athena akimaanisha kwamba anauwezo wa kutumia kanuni za anga kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine na spidi ya juu na pia anao uwezo wa kuendesha muda.
Licha ya meneno hayo kufika kwa msichana mdogo Naira , lakini alishindwa kuelewa na kuyapokea kwa wakati mmoja , lilikuwa ni jambo kubwa kwake na alishindwa hata kuliamini na katika Maisha yake hakuwahi kuwaza kwamba atakutana na mtu wa aina hio , licha ya kwamba ni miaka minne tu aliokuwa ameingizwa ndani ya Zeros kwa ajili ya mafunzo ya kisayansi , lakini swala la kutumia kanuni za anga kusafiri lakinii pia kuongoza muda lilikuwa kubwa kwake.
Athena pia alitambua kuwa Naira alikuwa kwenye wakati mgumu kusharabu maneno yake na ndio maana hakutaka kuongea nae Zaidi ya kumuonyesha kwa vitendo na ile Naira anapeleka Glass ya wine mdomoni palepale Athena alisimamisha muda na kisha akamsogelea Naira na kuchukua glass yake ya wine na kuishika mkononi na kisha hali ikarudi kama ilivyokuwa kawaida na Naira alijikuta akiduwaaa huku akisimama na kujiangalia mikono yake.
“Umewezaje kuchukua Glass yangu pasipo mimi kujua?”Aliuliza kwa shauku.
“Timespace manipulation”Aliongea Athena na wakati Naira anaendeelea kumwangalia , palepale akapotea alipokuwa amesimama na kilikuwa ni kitendo cha kupepesa macho mara moja Athena alikuwa nyuma yake na kumfanya Naira kuzidi kuchanganyikiwa.
“Wewe ni nani….?”Aliuliza Naira huku akijituliza.
“No there is no Woman God , She Cant be God , maybe an Angel”Aliwaza kwenye kichwa chake Naira akimaanisha kwamba hakuna mwanamke Mungu , na hawezi kuwa mungu labda awe Malaika.
“Swali zuri Naira, mpaka hapo nadhani ushaanza kuamini na nitajibu maswali yako kila nitakapokuwa na muda”
“I am alien,Arrived on Earth many years Ago”Aluiongea Athena kwamba yeye ni kiumbe kutoka sayari nyingine ambaye amefika hapa duniani miaka mingi iliopita.
“Unaweza kuniita utakavyo , watu wa dini wananifahamu kama Athena kwa upande wa Ugiriki, watu kutoka Rumi wananifahamu kama Minerva , kwa Underworld t wananiita The Doni”Aliongea Athena na kumfanya Naira kushindwa kuelewa na kusharabu maneno hayo.
Athena , Minerva , The Doni , yalikuwa ni maneno yaliopita kwenye kichwa chake.
“Naira nitakujibu maswali yako taratibu kwasababu wewe ni binadamu ambaye sio wa kawaida na nimekuchagua ili kunisaida katika misheni yangu”Aliongea Athena huku akiketi na kukunja nne kwenye Sofa.
“This place will be your new home, New Lab , New Task with great cause, you are going to learn undiscovered knowledge about universe, and maybe in future you will be like me”
“Hii sehemu itakuwa ndio makazi yako mapya , maabara yako mya , kazi mpya yenye malengo makubwa , unakwenda kujifunza maarifa kuhusu ulimwengu ambayo hayajagunduliwa na labda baadae unaweza kuwa kama mimi”Aliongea Athena na kumfanya Naira kudhindwa kuelewa mara moja point ya msingi.
“Unanifahamu vipi mimi?”Aliuliza Naira kwa wasiwasi na Athena alitabasamu.
“Nakufahamu kwa muda mrefu sana , tokea ulipozaliwa na makuzi yako ndani ya Afrika , namfahamu rafiki yako kipenzi Doris Alex, namfahamu baba yako Ryan , namfahamu mama yako Epholia , nilikuwa nikikuangalia kila siku katika ukuaji wako”Aliongea Athena.
“Kwanini ulikuwa ukiniangalia?”
“Najua mama yako na baba yako hawakukueleza kwanini walikuwa ndani ya bara la Afrika na sio ndani ya nchi yao uliozaliwa”Aliongea Athena na kumfanya Naira akumbuke kuwa ni kweli hakuwahi kuelezwa na wazazi wake kwanini walikuwa ndani ya taifa la Tanzania ,na kwanini yeye pekee ndio alikuwa mtoto mwenye rangi tofauti na Watoto wengine.
Kwa maelezo ya Athena Kwenda kwa Naira ni kwamba Athena alifika ndani ya dunia hii miaka mingi iliopita kipindi kabla hata ya dini kuenea na wakati anafika hapa Duniani hakuwa peke yake bali alikuwa na kundi la watu wengine waliotoka katika sayari nyingine lakini baada ya kufika hapa duniani mategemeo yao yalikuwa nje ya matarajio, kwani walikuja kugundua kuwa miili yao haiendani na hali ya hewa na Mazingira ya binadamu , hivyo walishindwa kuendana na mazingira na walikuwa katika hatihati ya kupoteza maisha , jambo ambalo hawakauwa tayari kulikubali hata kidogo , kwani walikimbilia ndani ya dunia hii kwa ajili ya kupata makazi mapya.
Katika namna ya kutafuta mbinu za kuishi ndani ya dunia , ndipo kwa kutumia akili zao waliposhauriana kuachana na miili yao ambayo haina uwezo wa kuendana na mazingira ya dunia na kutumia miili ya binadamu kuhifadhi nafsi zao , na wakati wanapanga hayo yote walikuwa juu angani kwenye mzingo wa dunia kwenye vifaa vyao na baada ya kushauriana kwa malumbano ya siku kadhaa ndipo walipofikia makubaliano ya kuendelea na wazo la kuacha miili yao na Nafsi zao zikavae miili ya binadamu.
Athena anaendelea kuelezea kwamba , katika jaribio la kuvaa miili ya binadamu lilifanikiwa kwa asilimia kubwa lakini pia mpango wao ulitokeza dosari.
“Dosari gani zilijitokeza?”Aliuliza Naira kwa shauku.
“Tulipotezana lakini pia kupoteza rasilimali tulizokuja nazo”Aliongea Athena kwa huzuni.
“Ilikuwaje mpaka mkapotezana kama mpango ulikuwa unawezekana”
“Because we underestimated human?”Aliongea akimaanisha kwamba kwasababu tuliwadharau binadamu.
“ Kivipi?”
“Tuliwadharau binadamu kwa kuwaona kama viumbe dhaifu sana na tungeweza kutawala miili yao tutakavyo kwa kutumia nafsi zetu , lakini jambo hili lilishindikana kwa asilimia kubwa , kwani licha ya kwamba binadamu walionekana dhaifu kutokana na muonekano wao , lakini Nafsi zao zilikuwa na nguvu kuzidi za kwetu na hilo ndio kosa letu”
“Kwahio nini kilitokea?”
“Asilimia tisini za nafsi zilizoshuka duniani kwa ajili ya kuvaa miili ya binadamu zilimezwa na nafsi za binadamu kwa maneno marahisi unaweza kusema kwamba nafsi zetu zilibakia kuwa ‘Defunct’Aliongea Athena na kumfanya Naira kushangaa Zaidi.
“Na vipi asilimia moja iliobaki?”
“Swali zuri Naira , nafsi kumi na mbili tu ndio ziliweza kushindana na nafsi za binadamu na kuuteka mwili lakini licha ya hivyo tulipoteza uwezo wetu mkubwa wa kumbukumbu”Naira alishangaa Zaidi.
Athena anaendelea kusema kwamba baada ya wao kumi na mbili kuweza kufanikiwa kuteka nafsi za binaadamu na hatimae kuuteka mwili walipoteza nguvu zao , lakini pia walipoteza rasilimali zao ambazo zingewarudishia uwezo wao , lakini pia akasema kwamba wao kumi na mbili ambao waliweza kuteka miili ya binadamu na nafsi zao iliwezekana tu kutokana na kwamba walikuwa wakitokea kwenye koo moja ya kifalme katika sayari yao ambayo bado hajaiweka wazi.
“Rasilimali gani ambazo mlipoteza?”
“Swali zuri Naira , tofauti ya sayari yetu na ya kwenu ni Energy”
“Energy!!?”Aliuliza kwa mshangao.
“Yes kwenye sayari yetu tunatumia ‘Pure Energy nikimaanisha kwamba energy ambayo haitokani na maada ya aina yoyote”Aliongea.
“You mean Ant-Matter energy?” Aliuliza Naira kwa mshangao.
“Exactly”
 
SEHEMU YA 237
Naira alikuwa ni mdogo , lakini akili yake ilikuwa na uwezo mkubwa wa kuchanganua mambo , alikuwa akisikia juu ya nguvu ambayo haitokani na maada yoyote, Energy ambayo wanasayansi wengi duniani walikuwa akifanya utafiti kwa ajili ya kuigundua na namna ya kuitegeneza.
“Kama ni kweli usemayo , rasilimali mlizopoteza zinahusiana nini na Ant-matter energy?”Aliuliza Naira na kumfanya Athena kutabasamu na kumpa ishara ya kumfuata kuelekea upande wa kulia na alifungua mlango wa duara kwa namna isioelezeka na kisha akaingia ndani na hapo ndipo Naira alivyozidi kushangaa , kwani mbele yake ilikuwa ni maabara ambayo sio ya kawaida kabisa , ni kama vile alikuwa akiangalia filamu za kisayansi za kufikirika.
Athena hakujali mshangoa wa Naira kwani alijiambia muda si mrefu atakwenda kuzoea , alisogea mpaka katikati kwenye kifaa mfano wa jiko ambalo limefunikwa na bakuli pamoja na sinia, huku chupa lililofunika kwa juu likionekana kupumua kwa namna ya kutoa mwanga kila baada ya sekunde mbili, Athena alifungua lile chupa na kisha akatoa jiwe mfano wa goroli yenye kung`aa sana kwa rangi flani ambayo haikuwa bluu wala nyeupe ni rangi isioelezeka..
Baada ya kushika lile jiwe alimsogelea Naira aliekuwa kwenye mshangao na kumuonyesha.
“Hili jiwe ni moja ya rasilimali tulizokuja nazo hapa duniani , ambazo mpaka sasa nyingine zimepotea , binadamu wenzako wamelipa jina jiwe hili kama Godstone”Aliongea Athena na kumpatia Naira mkononi.
“What is these?”
“Naira mpaka sasa umeshikilia ‘traped Ant -Matter Energy’ , linaonekana kama jiwe kutokana na kwamba kuna teknolojia tuliotumia kutunza nguvu hio humo ndani na ndio maana jiwe hilo hata linapogusana na maada hakuna matokeo yoyote”Aliongea na kumfanya Naira kushangaa mno.
“I can`t believe , are you saying this is real , Pure energy?”Aliongea Naira kwa kubabaika na Athena alitabasamu na kutingisha kichwa huku akichukua jiwe lile na kulirudisha sehemu yake.
“Kwanini umeniambia haya yote , kwanini umenileta hapa ndani?”Aliuliza Naira.
“Swali zuri Naira , nimekuleta hapa ndani kwasababu wewe sio wa kawaida kama binadamu wengine na kuhusu hilo utalifahamu kutoka kwa wazazi wako”Aliongea Athena na kumfanya Naira kushangaa na kuzidi kuwa na maswali.
“Nafahamu wanasayansi kutoka Zeros hawakukueleza ukweli wote na ni mengi ambayo wamekuficha , lakini kama upo tayari kunisaida kwenye misheni yangu basi utajua kila kitu na Zaidi”Aliongea Athena.
“Wewe ni binadamu wa kwanza kuingia kwenye hii kambi yangu tokea nifike hapa duniani”Aliongea na kumfanya Naira kushangaa.
“Unamaanisha unaishi hapa?”
“Ndio nimeishi hapa kwa miaka mingi sana kwa sura tofauti tofauti pasipo ya kuwa na kumbukumbu”Aliongea na kumfanya Naira ushangaa Zaidi na kutaka kuuliza lakini Athena alimpa ishara ya kumwambia asiulize swali.
“Kwa maneno marahisi Naira kwanzia leo mimi na wewe tutakuwa marafiki na nitakujibu kila swali utakalo uliza kama utanisaidia kwenye misheni yangu”
“Misheni gani unataka nikusaidie?”
“Nataka kutafuta nafsi za ndugu zangu niliokuja nao ndani ya dunia hii miaka mingi nyuma”Aliongea na kumfanya Naira kuvuta pumzi na Athena hakujali sana bali alisogelea skrini ziliokuwa upande wa kulia na kisha akamuonyesha.
“Hii ni video inayoonyesha namna dunia ilivyokuwa , wakati tunafika hapa duniani”Aliongea Athena na kumuonyesha Naira.
“This was Bronze Age!?” Aliuliza Naira kwa msangao.
“Yes!, wakati tunakuja hapa duniani binadamu ndio kwanza alikuwa akianza kutumia chuma”Aliongea na kufanya Naira kushangaa na kuwa na huzuni kwa wakati mmoja kwani binadamu walikuwa wakiteseka mno.
“Baada ya ujio wetu , maarifa juu ya ulimwengu yaliongezeka kwa kasi sana na nilifikia kwenye hitimisho kwamba yote hayo yaliwezekana kutokana na nafsi zetu kuvaa miili ya binadamu” Aliongea.
“Unamaanisha maendeleo ya sayansi yalitokana na ujio wenu?”
“Ndio , maendeleo ya binadamu yalikuwa ni ya taratibu sana wakati tunafika kwenye uso wa dunia na baada ya ujio wetu binadamu alianza kupiga hatua na wansayansi wakubwa walianza kuibuka mbeleni , lakini licha ya hivyo nilishindwa kuona viashiria vyovyote vya binadamu kutumia nafsi za ndugu zangu , jambo ambalo mpaka sasa nalifanyia kazi na ndio misheni yangu”
“Kwahio unaamini wanasayansi wakubwa katika historia ya dunia , walitokana na nafsi zilizowavaa binadamu?”.
“Naamini hivyo , pia nitakuja kuthibitisha yote hayo kama nitaweza kupata rasilimali zetu tulizopoteza , lakini pia kujua namna ya kuzitumia”Aliongea na kumfanya Naira kushangaa.
“Rasilimali ni za kwenu , kwaninni unashindwa kufahamu namna ya kuzitumia?”Athena alitabasamu..
“Kati ya watu wote kumi na mbili tulifanikiwa kuteka nafsi za binadamu , hatukuwa wanasayansi kwenye sayari yetu, unaweza kunifananisha na Waafrika kwa kipindi hiki , wazungu wengi ndio wenye maarifa juu ya teknolojia za ulimwengu huu na Afrika ni watumiaji wa teknoloijia zinazotoka kwa wazungu pasipo kujua siri ilionyuma ya teknolojia hizo, hivyo hivyo kwa upande wa sayari yetu , sisi tulikuwa ni wanasiasa tu na uongozi ndio uliokuwa urithi wetu”Aliongea Athena na Naira alionekana kuelewa.
Maana ni kweli kwa hapa duniani watu wamegawanyika kutokana na taaluma zao kuna Sanaa Pamoja na sayansi , hivyo Athena katika sayari yake alikuwa upande wa Sanaa.
“Kwahio sababu ya mimi kukuleta hapa ndani ni kuhakikisha unaweza kuelewa namna ya kutumia Ant-Matter Energy, Mwanzo wa mafanikio utakayoyfanikisha ndio nitakapo pata uwezo wa kuzirudisha hai Nafsi zilizomezwa na binadamu”
“Vipi kama sitoweza kufanikiwa kugundua namna ya kutumia Godstone kuachia nguvu yake”
“Naamini kwa uwezo wako utaweza na ndio maana nimekutoa ndani ya Zeros, lakini hata hivyo nina mpango mwngine”
“Mpango gani?”
“Naira uliza swali moja tu ambalo unaamini unaweza kupata jibu ambalo litaweza kujibu maswali yako yote , una dakika nne tu ,na ndio nitajua uwezo wako wa akili”Aliongea Athena na kumfanya Naira kufikiria kwa muda huku akijiuliza ni swali gani anapaswa kuuliza kwa wakati huo, alifikiria na kufikiria na kisha akainua kichwa chake na kumuangalia Athena.
“Who is your Enemy?”Aliuliza Naira na kumfanya Athena kumsogelea Naira na kumkumbatia .
“Umeuliza swali zuri sana , hakika akili yako ni kubwa na naamini utafanikisha kazi ya kuweza kutumia Godstone”Aliongea Athena kwa furaha na kisha akamwangalia Naira.
“Adui yetu mkubwa , mimi na ndugu zangu wote ni Mungu alietuumba”Aliongea Athena na kumfanya Naira kushangaa mno.
*******
Kirendo cha kudondoka kwa ghafla kwa Edna kiliwashangaza sana Mama Issa Pamoja na Blanidna na hawakuelewa nini kimetokea, lakini hawakuwa na muda wa kujiuliza, kwani palepale walimbeba Edna na kumpeleka kwenye zahanati ya kituo hiko.
Upande wa mtoto Lanlan wakati ekiendelea kulia , mlezi wake , mwanamke wa kichina alikuja haraka haraka na kumchukua na kuondoka nae huku akilia mno na kumfanya hata mlezi na yeye kutoa kilio baada ya kumfikisha Lanlan nyumbani.
“Namtaka babu , namtakam Mama… iiiii.. hiii”Aliongea huku akilia mpaka Kamasi.
“Lanlan nyamaza , usiendelee kulia…..”
“Namtaka mama ,namtaka babu”Aliongea Lanlan kwa kingereza na kumfanya Mlezi kuchanganyikiwa.
“Lanlan unamtaka nani kati ya Babu na Mama?”Aliuliza.
“Wote..”Aliongea na kumfanya Mlezi huyu wa kichina kuvuta pumzi na kukaa kwenye kiti.
Ukweli alikuwa na wasiwasi mno kwani ni Zaidi ya siku tatu hajamuona babu yake Lanlan jambo ambalo lilikuwa likimuumiza sana na kumfanya akose maamuzi kwa wakati mmoja.
Kwani mzee huyo hakuwa ameaga ameenda wapi Zaidi ya kutoonekana nyumbani kwa Zaidi ya siku tatu na kwa upande wa mlezi wa Lanlan hakuwa na uzoefu mkubwa na taifa la Tanzania na alikuwa akiijua pia tabia ya Lanlan akitaka kitu lazima akipate labda tu umpe sababu ya kuridhisha.
Upande wa Edna aliweza kurejewa na fahamu ndani ya dakika kumi tu baada ya kufikishwa zahanati.
“Edna nini kimetokea?”Aliuliza Blandina aliekuwa kwenye hali ya wasiwasi.
“Mama lanlan yuko wapi?”Aliuliza Edna huku akikaa kitako na kuzungusha kichwa akimtafuta Lanlan.
“Unamaanisha yule mtoto?, Ashachukuliwa na mlezi wake”Aliongea Blandina , lakini jibu lilionekana kutomridhisha kabisa Edna.
“Mama Issa wanaishi wapi?”Aliuliza Edna na kuwafanya wanawake hawa kushangaa , maana wao walikuwa wakitaka kujua hali yake , lakini yeye alikuwa akitaka kujua hali ya Lanlan.
“Edna mwanangu nini kimekupata , sisi wote hapa tuna wasiwasi na afya yako , kwanini umedondoka ghafla?”Aliuliza Blandina na kumfanya Edna afikirie ni kipi kimemtokea.
“Sikumbuki vizuri ila nilimulikwa na mwanga mkali machoni na nikajihisi kukosa nguvu”Aliongea Edna na kuwafanya Mama Issa na Blandina kuangaliana.
“Mwanga!, Mwanga gani?”
“Sijui , nashindwa kuelezea ila ni kama mtu aweke kioo juani na kukumulika usoni ,, sijui nini kimetokea , Mama issa nahitaji kuonana na Lanlan”Aliongea Edna huku akishuka kitandani na kuvaa viatu vyake na kutoka nje kama mwanamke aliechanganyikiwa na kuwafanya hata Mama Issa na Blandian washindwe kuelewa nini kimempata Edna.
 
SEHEMU YA 238.
“Kabla sijaendelea kuelezea naomba kuuliza swali?”Aliongea The First Black kwa wasiwasi.
“Unaweza kuuliza , lakini ni swali moja tu nakuruhusu”Ilisikika sauti ya Athena ndani ya chumba hiko cha hoteli na The First Black alivuta pumzi.
“Kwa miaka mingi nimekuwa nikiishi chini yako na kukutii kwa kila maelekzo uliokuwa ukinipatia na kuhakikisha nakupatia majibu ambayo yanakuridhisha , lakini pia niliamini katika kichwa changu unao uwezo wa kujua kila kitu ndani ya dunia hii na kutokana na hilo nimekuwa nakuheshimu sana , lakini kazi hii ya kuwafuatilia wanachama wote wa Illuminat imenishangaza, hivyo swali langu ni kutaka kujua kwanini unawatafuta hawa wanachama?”Aliuliza The First Black.
“Nikitaka kujibu swali lako kwa ufahasa , lazima uelewe historia yangu ya nyuma miaka mingi tokea kufika kwetu ndani ya uso wa dunia, nadhani unakumbuka mara ya mwisho nilikueleza kuwa sikufika kwenye dunia hii peke yangu?”
“Ndio nakumbuka?”
“Basi jibu ni kwamba nawatafuta ndugu zangu niliokuja nao na naamini kwa asilimia mia moja wamejificha chini ya hili kundi la Illuminat, nina mpango unaoendelea na ili kufanikiwa kwa mpango wangu nikuhakikisha nakuwa na kila jina la mwanachama wa Illuminat ndani ya dunia hii”Aliongea Athena.
“Asante kwa jibu lako”
“Huna haja ya kunishukuru , nimekujibu kwakua nataka majibu yangu kukusaidia katika kazi yako , hivyo huu ni wakati wako wa kunielezea Illuminat ni kundi lipi na Freemason ni kundi lipi”Aliongea .
“Mimi ni mwanachama wa Illuminat , naomba unisaheme kwa kukuficha juu ya hilo”Aliongea The First Black kwa wasiwasi mkubwa lakini muda ule ule aliijikuta akikosa hewa na kuanza kukohoa mfululizo huku akiwa ameshikilia shingo yake kama mtu anaekabwa.
“Nao..mba uni..sa.. mehe , nilikuwa na sababu ya kutokukueleza”Aliongea huku akilala kwenye sofa kwa namna ya kurusha rusha miguu kama mtu anaekata roho na tukio hilo lilidumu kwa muda wa dakika chache tu na alimuachia.
“Biuadamu tabia yenu ya kusema uongo inaniudhi sana na inanipelekea kuwachukia kila siku”Ilisikika sauti ya kike , licha ya kwamba ilikuwa ikiashria hasira , lakini bado ilikuwa nyororo.
“Nitakueleza ninachokijua kuhusu Illuminat , naomba unisamehe kwa kukuficha”Aliongea The First Black na kisha akavuta pumzi na kuweka akili yake sawa.
“Illuminat kama nilivyosema kiasili sio waanzilishi wa kundi la Freemason , bali Illuminat waliomba hifadhi ya kujificha ndani ya kundi hili la Bavarian la wajenzi huru , ambao enzi hizo walikuwa na utajiri mkubwa, sababu iliowafanya wajifiche chini ya kundi la Freemason ni kutokana na kwamba walikuwa wakiwindwa sana na serikali ya Kirumi… “Aliongea na kisha akaendelea.
Kwa maelezo yake ni kwamba Mwaka kati ya 1700 kuendelea ndani ya mamlaka ya Rumi kuliibuka wanasayansi wengi ambao walikuwa wakifanya gunduzi mbalimbali , kulikuwa na wanasayansi wabobezi katika maswala ya hesabu , kuna waliokuwa wamebobea katika maswala ya biolojia na mashine lakini pia kulikuwa na wanasayansi walibobea katika maswala ya anga.
The First Black anaelezea kwamba baada ya gunduzi hizi kufikia serikali ya kirumi ambayo ilikuwa ikiongozwa kwa misingi ya dini, walikasirishwa na baadhi ya gunduzi za wanasayansi hao kutokana na kwamba zilikuwa zikipingana na maandiko matakatifu na hili liliibua uhasama sana kwa watu wa dini na kuona wanasayansi hao wanapingana moja kwa moja na dini kutokana na tafiti zao ,na hapo ndipo serikali ilipoanza msako wa kukamatwa kwa watu waliokuwa wakijiita wanasayansi , na serikali iliwakamata na kuwatesa huku ikiwataka wanasayansi hao wabatilishe baadhi ya kauli zao.
Sasa basi baada ya serikali kuzidi kutesa na kuua wanasayansi wengi , ilipelekea hofu kwa wanasayansi wengine ambao hawajafikiwa na serikali na kupitia hofu yao iliwafanya wakusanyike kwa siri sana kwa ajili ya kuzungumza mustakabali wao wa kuendeleza sayansi na teknolojia, baada ya kufanikiwa kukutanika kwa siri waliamua kujipatia jina kwanza ili kujiongezea hamasa na ujasiri ,na ndipo walipojipatia jina la ‘Enlightened ones’ yaan Illuminat.
The First Black anaelezea kwa kusema kwamba dhumuni ambalo liliwafanya wanasayansi hawa kukutana ni kwa ajili ya kutaka kuanzisha vita na watu wa dini kutokana na tabia yao ya kuwakamata na kuwatesa , jambo ambalo lilipingwa vikali na mwanasayansi mmoja maarufu ambaye pia alikuwa ni mtu wa dini kindakindaki , mwanasayansi ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Galilei Galilleo.
Gallileo aliwapinga wenzake kwa mpango wao wa kuanzisha vita kwa madai ya kwamba sayansi na Dini ni vitu viwili vinavyotegemeana na kwamba Sayansi ipo kwa ajili ya kuimarisha na kuipa nguvu dini , hivyo akawaasa wanasayansi wenzake wasifanye fujo bali yeye yupo tayari Kwenda kuzungumza na watu wa dini juu ya kwamba sayansi haipingi uwepo wa mungu Zaidi ya kwamba inaipa nguvu dini kimaarifa.
Sasa kwasababu Gallileo ndio aliependekeza swala hilo , wanasyanasi wakaona wajaribu kuongea na watu wa dini.
Kabla ya hapo Gallieo alikuwa tayari ashagundua kwamba dunia ilikuwa ni duara lakini pia Dunia ndio inazunguka jua na sio jua kuzunguka dunia na aliweza kugundua kutumia darubidni yake.
Sasa gunduzi yake ilikuwa ikipingana na watu wa dini waliokuwa wakiamini kwamba dunia ni tambarare na haiwezi kuwa duara na jua ndio linaiuzunguka dunia, sasa Baada ya Gallieo kutangaza gunduzi yake alianza kuwindwa na watu wa dini na alionekana kama kichaa na mtu anaeenda kinyume na mafundisho ya dini , hivyo akaingia kwenye orodha ya watu wanaotafutwa na watu wa dini.
First Black anaelezea kwa kusema kwamba kundi lote la Illuminat ambao sasa ni wanasayansi , walipendekeza Galileo Kwenda kuongea na watu wa dini juu ya pendekezo lake, na Gallielo hakupinga kwanza alikuwa akipenda sana dini licha ya kuwa mwanasayansi hivyo alifanya maamuzi ya Kwenda kuongea na watu wa dini, na alipoweka swala lake wazi , palepale alikamatwa na kuingizwa kwenye chumba cha mateso huku akilazimishwa kubatilisha kauli yake ya kwamba dunia ni duara, lakini Galileo hakuwa tayari kubatilisha kauli yake na alisimamia msimamo wake , jambo ambalo liliwaudhi watu wa kanisa na kuamua kumfunga ndani ya chumba cha gereza lenye giza mpaka umauti wake.
Sasa huku wa kundi la illuminat baada ya kuona mpango umebuma walianza kutoroka nje ya mamlaka ya kirumi na Kwenda mbali Zaidi nje ya mkono wa serikali , wakitafuta eneo zuri Zaidi kwa aijili ya kujunda upya, na katika heka heka zao ndipo walipokuja kukutana na kundi lingine linalofahmika kwa jina la Freemason na Kundi la Illuminat ndipo walipamua kujiunga nao kwa kuomba hifadhi ndanni ya kundi hilo.
Na kwanzia hapo kundi hilo la wanasayansi walitumia jina la Freemason kuendeleza Imani yao ya kuamini katika sayansi na kipindi ambacho wanakubaliwa kuingia , kundi la Freemason lilikuwa na wafuansi wengi mno kuanzia Amerika yote mpaka kufikia baadhi ya nchi za Ulaya na walikuwa washajenga mpaka Lodge za kufanyia ibada zao.
“Kwa maelezo yako Illuminat waliamua kutumia jina la Freemason kuendeleza mipango yao ya maendeleo ya kisayansi?”Aliuliza Mrembo The Doni.
“Ndio na baada ya wao kujiunga na Freemason kundi lao lilipote na kuwa Dormant”
“Kwa maelezo yako ni Dhahiri kwamba huwezi kutenganisha Freeason na Illuminat?”
“Ndio kwasababu Freemason , licha ya kwamba hatuamini uwepo wa Mungu , lakini pia Freemason tunaamini Zaidi katika utajiri na huo ndio msingi wa dunia hii”
“Kwenye vikao vyenu mnazungumza nini kuhusu mimi?”
“We Believe you are one of us”
“Tunaamini wewe ni mmoja wetu”Aliongea The First Black.
********
Mheshimiwa Senga alimkaribisha Kigombola kwa tabasamu la kinafiki mtangulizi wake mara baada ya kufika ndani ya ukumbi wa ikulu wa kuonana na wageni na kwa upande wa Mheshimiwa Kigombola , alikuwa akijua kuwa tabasamu la Senga ni la kinafiki kwasababu Mheshimiwa Kigombola hakuwa chaguo lake katika kumrithisha uongozi , ni hivyo tu kwamba wazee wachama ndio waliokuwa na nguvu Zaidi , hivyo kumfanya ashindwe kushindana nao na kuweka mtu anaemtaka yeye.
Baada ya kusalimiana kwa dakika kama kumi na tano huku vicheko vya kinafiki vikiendelea, Mheshimiwa Kigombola alienda kwenye jambo ambalo limemfaya kuja hapo ikulu.
“Nina uhakika ushapata taarifa juu ya mimi kuonana na baadhi ya viongozi wakubwa wa ulinzi , akiwemo jenerali Tozo?”Aliongea Mheshimiwa Kigombola na kumfanya Senga kushangaa kidogo na kushindwa kufahamu nia ya mtangulizi wake.
“Ndio nimeipata na imenichanganya sana mimi kama mkuu wa Nchi kuona viongozi wa chini yangu wanafanya mambo pasipo kunishirikisha”Aliongea Senga na kumfanya Mheshimiwa Mstaafu kutabasamu.
“Nazifahamu hizo hisia kwasababu hata mimi nishawahi kuwa katika nafasi yako, niende moja kwa moja , kwanza kabisa mimi ndio niliowaita kwa ajili ya kuzungumza nao na swala ambalo tumezungumza ni kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa hili”
“Wiki kadhaa nyuma nilipokea ugeni kutoka taifa la China na sikuelewa kwanini Jenerali wa jeshi la wananchi wa China aliagiza mgeni kuja moja kwa moja kwangu, lakini naweza kukisia dhumuni lao”Mheshimiwa Senga alishangaa maana hakuwa na taarifa hio.
“Mheshimiwa Senga kuna siri ambayo sikukuambia baada ya kuachia madaraka na leo hii nipo hapa kwa ajili ya kuiweka wazi”
“Siri!!!”Mheshimiwa Senga alishangaa .
ITANDELEA JUMAPILI MCHANA

0687151346 .WATSAPP NICHEKI TUONE NAMNA YA WEWE KUENDEKEA KUBURUDIKA
 
Back
Top Bottom