Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 239

“Ndio kuna faili moja sikukukabidhi wakati nakuachia ofisi”Aliongea Meshimiwa Kigombola na kumfanya Mheshimiwa Senga kuvuta pumzi.

“Naweza kuliona hilo faili sasa hivi?”

“Ndio inawezekana na ndio maana niko hapa”Aliongea mheshimiwa na kisha akatoa Flash Disk kwenye mfuko wa koti lake na kumpatia.

“Nitakuelezea kwa kurahisisha kilicho humo ndan, kiufupi ni kwamba wakati nilipokuwa madarakani nilipokea ombi kutoka kwa Raisi wa Marekani juu ya ujenzi wa maabara ya kisasa ndani ya Tanzania”Aliongea na kumfanya mheshimiwa Senga kushangaa , hakuwahi kusikia taarifa hio.

“Maabara!!”

“Ndio Maabara ya kisasa ambayo Raisi mwenyewe kwa pesa zake aliamua kuifadhili kwa siri kwa ajili ya ujenzi wake na ilichukua miaka miwili mpaka kumalizika, dhumuni la ujenzi wa maabara hio ilikuwa ni kwa ajili ya kumpa nafasi Profesa Shelukindo kuendelea na tafiti zake akiwa hapa nchini”

“Mheshimiwa nilidhani Profesa Shelukindo alikuwa amestaafu kwenye kazi yake?”

“Hiko ndio kilichokuwa kikifahamika kwa watu wengi , lakini hilo halina ukweli wowote, moja ya sababu za Raisi wa Marekani kufika hapa Tanzania kipindi kile ni kwa ajili ya ujenzi huu wa maabara”

“Kwanini mheshimiwa alikuwa akitaka Profesa kufanya kazi hapa Tanzania na sio Marekani?”

“Hakunipa sababu wakati huo ya kueleweka, Zaidi ya kuiniambia teknolojia ambayo Profesa Shelukindo anaifanyia kazi ni muhimu Zaidi katika mapambano na The Doni”Aliongea Mheshimiwa Kigombola na Senga alishangaa mno.

“Naona umeshangaa sana juu ya jina hilo na sina shaka kwamba unamfahamu”

“Mheshimiwa The Doni simfahamu , lakini pia nimeshangazwa kwani wewe ndio niliokuwa najua kwa asilimia kubwa una mahusiano ya karibu na The Doni na ni mshitika wako , inakuwaje mkawa na mpango wa kumuangamiza The Doni?”Mheshimiwa alitabasamu kidogo.

“Unajua ndani ya taifa hili watu wengi wanaamini kwamba kila kitu ninachokifanya ni kwa ajili yangu , lakini huo sio ukweli , kila nilichokuwa nikifanya kilikuwa ni kwa maslahi mapana ya taifa , kuhusu The Doni sio mimi tu ambaye simfahamu bali hata Raisi wa Marekani pia hamfahamu, labda nikuelezee taarifa ambayo naamini mpaka sasa hauifahamu”

“The Doni unaemjua wewe sio kama yupo hapa Tanzania tu , bali ni wa dunia nzima”Aliongea Mheshimiwa na kumfanya Raisi Senga kujifuta jasho na kitambaa , hio ilikuwa ni taarifa ya kwanza kutoka kwake.

*********

“Edna simu yako inaita”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kusimama huku akieguka na kumwangalia mama mkwe wake.

Aliekuwa akipiga ni Roma kwani jina lilisomeka hivyo kwenye skrini juu na hata Blandina aliliona na hakujua ni kwanini Roma alikuwa akipiga simu.

Edna aliichukua na baada ya kuona jina ni Roma alijikuta akitamani kukata , lakini aligundua kuwa Mama yake Roma anamwangalia , hivyo hakuwa na jinsi na kupokea.

“Unasemaje?”

“Em.. Babe wife natumaini unafurahia kampani ya Watoto?”Aliongea Roma upande wa pili.

“Ongea nipo kwenye haraka”Aliongea Edna huku akipandisha kisirani.

“Kuna jambo Bi Wema alisahau kukuambia asubuhi , hivyo kaniomba nikueleze , alishatafuta kampuni ambayo itahusika na kutuhamisha”Aliongea Roma na kumfanya Edna akumbuke kwamba siku kadhaa nyuma alijadiliana na Bi Wema juu ya kuhamia Osterbay. Kwenye nyumba yake kubwa.

“Nilisahau kabisa… wewe unaonaje?”Aliongea Edna huku akishusha sauti chini.

“Kwanini unaiuliza hivyo, mimi nimekupatia taarifa hivyo”

“Lakini pia una maamuzi kwanini kila kitu lazima nikitolee maamuzi mimi , nafasi yako ni ipi?”Aliongea Edna huku akianza kukosa utulivu.

“Edna nini kinaendelea huko kituoni mbona unaongea kama haupo sawa?”Edna alifikiria kidogo na kisha akamgeukia Blandina kama vile anasoma jambo kutoka kwake.

“Kama kampuni ya uhamishaji ishafika mnaweza kuendelea na vitu muhimu vya kuhama navyo , kuhusu chumba changu vitu viachwe kama vilivyo mpaka nitakaporudi”Aliongea

“Okey nitamueleza”Aliongea Roma na kisha simu ikakatwa .

“Mama nilisahau siku ya leo tulikuwa na mpango wa kuhamia Osterbay kwenye nyumba kubwa”Aliongea Edna akimwangalia Blandina.

“Ooh!... Edna tunapaswa kurudi na kuangalia utaratibu wa uhamishaji wa vitu” Edna alifikiria maneno ya Blandina na akaona ana pointi ya msingi , lakini bado moyo wake ulikuwa ukitaka kumuona Lanlan.

“Edna yule mtoto sijui kakufanya nini , ila kwa sasa atakuwa na wazazi wake,,, najua unapenda Watoto sana na natamani siku uje upate wa kwako utakuwa mama mzuri”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kushangaa kidogo ukweli wazo la kuzaa bado halijawahi kumjia akililini na muda huo ni kama limeingia.

“Kweli , Lanlan atakuwa na wazazi wake kwasasa , sipaswi Kwenda nyumbani kwao”Aliwaza Edna na kisha akakubaliana na Blandina warejee nyumbani kwa ajili ya kusimamia uhamiaji kwenye nyumba yao ya zamani.

Dakika arobaini na tano ziliwatosha kabisa kufika nyumbani na gari kubwa la kubeba mizigo lilikuwa ndani ya nyumba yao na wafanyakazi wa kampuni ya uhamishaji walikuwa wakiendelea na kazi.

Edna alirtoa maelekezo ya baadhi ya vitu vya kawaida kuacha hapo ndani kwa mfano vifaa vva kielectronics na baadhi ya samani na hio ni kutokana nyumba ya kule Osterbay ilikuwa na kila kitu.

Roma aliekuwa akisaidiana na wafanyakazi kubeba baadhi ya vitu muhimu, alishindwa kuelewa hali aliokuwa nayo Edna , ni kama kulikuwa na kitu ambacho alikihisi wakati Edna anaingia hapo ndani ambacho hakuwa nacho tokea aonane nae kwa mara ya kwanza.

“Edna.!!”Aliita Roma baada ya kufungua mlango na kuingia ndani ya chumba cha Edna taratibu na Edna hakuongea chochote baada ya kuingia Zaidi ya kujiweka bize na anachokifanya , Edna alikuwa akipangilia baadhi ya vitu vya kuhama navyo.

“Edna nini kimetokea mlikotoka , nahisi haupo sawa kama ulivyoondoka asubuhi”Aliongea Roma lakini Edna alikuwa akiendelea na anachokifanya huku akiwa amempa mgongo Roma na alionekana kuchangua baadhi ya vitu kwenye kabati lake pasipo mpangilio maalumu ni kama mtu ammbaye alikuwa akitafuta kitu muhimu pasipo kukipata na Roma aliona jambo hilo na kuishia kutabasamu , kuna kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kutoka kwa Edna ambacho alikuwa akikihisi kutoka kwake , licha ya kumwangalia Edna kwa macho yake na kuona mwili wake hauna shida lakini kuna mabadiliko makubwa kutoka kwa Edna ni kama vile mtu anapokaribia eneo la hatari zile hisia zinazomjaa mtu ndivyo ilivyokuwa kwa Edna wakati anaingia hapo ndani akiwa na Mama yake.

Roma baada ya kuona hajibiwi alikata shauri ya kumsogelea na kumkumbatia kwa nyuma na kumfanya Edna asimame wima huku akitulia kama mtu anaefikiria hatua ya kuchukua kwa tukio ambalo kafanyiwa.

Roma alifahamu Edna angeleta shida kwa kumkumbatia kwa nyuma , lakini majibu yake yalikuwa nje ya mategemeo yake , kwani aligundua Edna alianza kulia kwa kwikwi na kumfanya Kushangaa, mbaya ni kwamba sasa staili ya namna Edna anavyolia ni tofauti na aliokuwa ameizoea , Edna alikuwa akilia kwa kwikwi huku akiwa ameshikilia moyo wake ni kama mtu ambaye amepoteza kitu kikubwa kwenye Maisha yake.

Roma ilibidi amuache Edna aendelee kulia atakavyo , alijua kulia ni sehemu ya mtu kutoa sumu moyoni na ndio maana hakutaka kumzuia Edna kutoa kilio, lakini licha ya kwamba alikuwa amemuacha Edna kulia , lakini moyo wake ulikuwa ukiuma ajabu, hakupenda kumuona Edna analia na pia alijiambia Edna ni mwanamke ambaye siku zote anajua ni imara katika kuziendesha hisia zake na ndio maana hakuwa mtu wa kuwaza sana , lakini kitendo cha Edna kulia waziwazi mbele yake, lakini pia mabadiliko ya Edna aliokuwa nayo vilimfanya kuwa na wasiwasi na kuwa na uchungu kwa wakati mmoja.

Roma ilibidi amsogelee Edna alierudi kukaa kitandani na kisha kumkumbatia na kumruhusu Edna kulilia kwenye kifua chake.

“Edna niambie ni nini kimetokea kituoni leo?”Aliuliza Roma baada ya Edna kunyamaza huku akijifuta machozi na kusimama na kuanza kuweka nguo zake kitandani.

“Hakuna kilichotokea”Aliongea Edna huku akirudiwa na hali yake, Roma alijiambia kama Edna ndani yake kulikuwa na pepo la aina yake kwani lilikuwa likimuendesha Edna kwa namna ambavyo sio ya kawaida.

Roma alijiuliza inakuwaje mtu dakika kadhaa nyuma alikuwa akilia kama mtoto , lakini sasa hivi anaonekana kama vile sio yeye na ukauzu wake kurudi kama kawaida, Roma kwa jinsi alivyomuona Edna aliamini kabisa hapo hakuna maongezi tena ya kuendelea kwani Edna asingeongea chochote.

“Unamaanisha kweli hakuna kilichotokea au unanikalia kimya”Aliuliza Roma.

“Roma.. nishasema hakuna kilichotokea”Aliongea Edna huku akiendelea na kazi yake ya kuanza kupangua nguo baadhi na kuziweka kitandani .

“Kama hakuna kilichotokea kwanini ulikuwa ukilia kama mtoto dakika moja iliopita?”Aliongea Roma na kumfanya Edna kusimama na kumgeukia Roma na kumwangalia usoni , ni kama alikuwa akitafuta jibu la kumpatia.

“Sijui.. nilijikuta natamani kulia na sababu sina”Aliongea Edna kinyonge na kisha akageukia kabati na kuendelea.

Upande wa Roma alitamani kucheka , yaani alishindwa kabisa kumuelewa Edna na alijiambia sijui ni lini ataweza kumuelewa maana aliona muda mwingine Edna hakuwa mtu wa kawaida , alijiuliza inakuwaje mtu kulia pale anapojiskika pasipo kuwa na sababu maalumu.

Roma alimwangalia Edna kwa dakika kama nne huku Edna akijifanya hajali uwepo wake na baada ya hapo aliamua kupiga hatua kutoka nje.

“Romaa..!!”Aliita Edna kabla ya Roma kufunga mlango na Roma aligeuka na kumwangalia.

“Juzi niliwaambia Daudi na Wendy wakutafute juu ya maswala ya kampuni , ila sijapata mrejesho wa kile kinachoendelea”Aliongea Edna na Roma alitabasamu.

“Boss unataka ripoti hio sasa hivi?”Aliuliza Roma kiutani , lakini Edna aliendelea kuwa na mwonekano wake uleule na kisha aktingisha kichwa.

“Unahisi siwezi kuongoza vyema kampuni , kama ulikuwa huamini kama naweza kuongoza kwanini umenipatia niongeze?”Aliongea Roma.

“Nimekuuliza kwa ajili ya kupata mipango yenu , sijawahi kufanya maamuzi ambayo nitajutia baadae , amini kwamba nayaamini maamuzi yangu” Aliongea Edna.na Roma alirudi nyuma na Kwenda kuketi kwenye kitanda.

“Njoo ukae hapa kwanza pembeni yangu”Aliongrea Roma huku akipa ishara Edna ya kusogea mpaka kitandani lakini Edna alijikuta kukosa maamuzi kwa dakika kadhaa, lakini mwishowe alisogea na kuketi kitandani.

Sasa kitendo cha Edna kuketi kitandani tu , alijikuta akifanyiwa shambulio ambaclo hakulitegemea kwani Roma alimbeba juu kama mtoto na kubwaga katikati ya kitanda , wakari Edna hajachuku hatua juu ya kipi cha kufanya , alijishutikia Roma yupo juu yako.

“Roma.. unatak.. Mhmhh..”Aliongea Lakini aliishia katikati kwani mdomo wake na wa Roma uligusana.







SEHEMU YA 240

Gari ambayo ilikuwa imekuja kwa ajili ya kuchukua vitu vya kusafirisha ilikuwa ishaondoka tayari na vitu vingi ambavyo vilichukuliwa ndani ya nyumba hio ni nguo na baadhi ya vitu vya wanafamilia vile binafsi sana.

Wakati uhamishaji unaendelea kwa upande wa Bi Wema na Blandina waliamua kuandaa kabisa chakula kwa ajili ya mchana , ili wakiondoka wawe wameshiba kabisa , kwani muda ulikuwa umeeenda sana.

Saa saba na nusu ndio muda ambao waliivisha na Bi Wema alimuagiza Sophia Kwenda kumuita dada yake Pamoja na Roma kwa ajili ya kupata chakula cha mchana.

Sophia alianza kuigonga kwenye chumba cha Roma , lakini hakukuwa na majibu na kumpeleka kufungua mlango , lakini pia hakuweza kuona mtu ndani ya chumba hiko , lakini alikuwa na uhakika Roma alikuwa ndani ya nyumba hio kwani hakumuona akitoka , hivyo alijiuliza atakuwa wapi.

Aliachana na chumba cha Roma na kupandisha ngazi kuelekea upande wa mlango wa Edna na ile anakaribia mlango wa chumba anacholala Edna , mlango haukuwa umefungwa vizuri , alijikuta akisimama baada ya kusikia miguno ya kimahaba ya Edna,

“Roma.. unatak.. Mhmhh”

Alishindwa kuona kinachoendelea ndani kwani mlango ulikuwa haujafunguka sana , hivyo baada ya kujihakikisha kuna kinachoendelea alijikuta akigeuza alikotoka na kurudi sebuleni.

“Umewaambia?”Aliuliza Blandina lakini Sophia alishindwa kujibu na Yezi aliekuwa pembeni yake aligundua kitu na kuishia kutabasamu.

“Watshuka muda si mrefu , wapo wote”Aliongea Sophia na kumfanya Blandina na Bi Wema waangaliane na kisha wakatabasamu na kuendelea na kupakua chakula.

Edna alijikuta akiwa kwenye ulimwengu mwingine, japo kitendo kilikuwa cha kushitukiza , lakini kadri Roma alivyokuwa akimpiga kiss , alijikuta hisia zake zikijikusanya na kujaa na kuanza kutoa ushirikiano huku akiwa amefumba macho.

Roma alivyoona mke wake kashaanza kutoa ushirikiano alianza kuongeza ujuzi kwa kumshika shika Edna manyonyo yake yaliosimama kwa namna ya kutekenya na Edna aliishia kujikunja kunja.

Vitendo vya kimahaba vilidumu mpaka pale Roma alipojaribu kupeleka mkono kwenye nguo ya ndani y a Edna ambayo ilikuwa imejiachia wazi kwa sababu ya gauni alilokuwa amevalia kuacha mapaja yake wazi.

Sasa ile Roma anapeleka mkono tu Edna alimzuia na ilibidi Roma amwachilie na kumwangalia usoni na kisha akatabasamu na Edna aliefumbua macho naaliangalia pembeni kwa aibu.

“Wife,,, wenzetu wanatusubiria kwa ajili ya chakula cha mchana , nahisi Sophia alikuwa hapa”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna anaejiweka sawa kwa aibu, lakini baada ya kusikia Sophia alikuwa hapo ndani ni kama alishituka.

“Sophia….!!”Alishangaa Edna huku Roma akimuonyesha Edna kwa kutumia kidole kuelekea mlangoni na Edna alijikuta akitamani ardhi ipasuke kwani mlango haukuwa umejibana vizuri.

“Umefanya makusudi..?”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma kwa macho makali na Roma alitingisha mabega.

“Unanionea wife , sema tumefanya makusudi. hehe”Aliongea Roma huku akitoka kabisa nje na kumuacha Edna akikanyaga miguu chini kama vile mtoto huku akijilaumu.

Roma yeye alishuka wa kwanza mpaka sebuleni na kuketi kwenye kiti chake cha siku zote na Edna na yeye alionekana akishuka kutoka juu na kutembea mpaka kwenye kiti chake.

“Edna mpakulie mumeo chakula”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kukamaa mwili na kisha kumwangalia Roma ambaye anaonekana kutabasamu na wengine kwenye meza macho yao yote yalikuwa kwa Edna.

Edna hakutaka kuonekana mtukutu mbele ya mama mkwe wake hivyo aliamua kufanya kama alivyoambiwa na kuchukua sahani na kuanza kumuwekea Roma chakula kwenye sahani na kisha akamsogezea.

*******

“Mheshimiwa unamaanisha nini kusema ni wa dunia nzima?”Aliuliza Mheshimiwa Senga kwa mshangao huku akisubiria jibu kwa hamu.

“Senga kila kiongozi ambaye ana,ingia hapa Ikulu baada ya kutumikia wananchi anayo siri yake ambayo hawezi kumwambia raisi anaepokea kijiti , hata mimi naamini mtangulizi wangu ,Marehemu, naamini anayo siri aliotoka nayo hapa ikulu ambayo mpaka sasa hajaniambia hivyo kwangu mimi pia kuna mambo sikukueleza”Aliongea Mheshimiwa na kumfanya Raisi Enga kutoelewa pointi ya msingi anayotaka kumaanisha.

“Mimi ni moja ya watu walioumizwa sana na namna ya Profesa Shelukindo Pamoja na familia yake walivyoteketezwa na niliumia sana mtu ambaye amehusika na kifo cha Profesa kuja nyumbani kwangu na kuanza kunilazimisha kufanya kile ambacho yeye anataka”Aliongea Mheshimiwa.

“Unamaanisha Huyu Yan Buwen , mwanasayansi kutoka China?”Aliuliza Raisi Senga.

“Ndio huyo , sikujua kama taarifa hio umeipata tayari?”

“Numeipata ndio , lakini sikuwa na uhakika nayo na nimewapa vijana wangu kuifanyia uchunguzi Zaidi, Mheshimiwa hebu niweke wazi moja kwa moja nijue ni jambo gani ambalo limekufanya kuja mpaka hapa Ikulu na kutaka kuongea na mimi”

“Moja ya sababu kubwa ilionileta hapa ni juu ya The Doni, kama nilivyosema kwamba nimeumizwa sana na kifo cha Profesa Shelukindo , lakini ombi ambalo The Doni amelitoa kwangu kulikamilisha najikuta kwenye nafasi ambayo sina chaguo lingine na ndio maana nimefika hapa Ikulu kwa ajili ya sisi kulizungumzia hili kwa mapana”Aliongea.

“Ni ombi gani?”

“Ni juu ya Yan Buwen kupata Maabara kuendeleza tafiti ambazo Profesa Shelukindo kaziacha”Aliongea na kumfanya Raisi ashangae.

“Mheshimiwa unamaanisha tumuache muuaji aendelezo tafiti za Profesa Shelukindo?”Aliuliza huku akianza kupandwa na hasira.

“Hicho ndio ninachomaanisha Senga , najua hili ni gumu kukubalika ukiliweka katika mtazamo wa kisheria na kimaadili , lakini tulipofikia mimi na wewwe hatuna budi kufanya hivyo , Yan Buwen alichokifanya ni maagizo kutoka kwa The Doni mwenyewe”

“Mheshimiwa tafiti zote za Profesa mpaka sasa hivi ni mali ya taifa na mimi kama kiongozi wa taifa hili siwezi kuruhusu Yan Buwen kuzitumia wala kuziendeleza , Mheshimiwa nadhani uliona mwenyewe v ndugu wa Profesa pale msibani siku ile?, na maumivu nilioyapata nilijiapia lazima nimkamate mhalifu na nikatoa ahadi mbele ya watu wote kuwahakikishia kumkamata yoyote aliehusika, kwanini leo hii baada ya kufanya hivyo nianze kushirikiana na muuaji?” Kigombola alionekana kutokuwa na wasiwasi , licha ya msimamo wa Senga.

“Senga kama nilivyosema mwanzo sikufahamu Profesa alichokuwa akikifanyia kazi mwanzoni na nimekuja kufahamu baada ya kukutana na huyu Yan Buwen”

“Ni kitu gani ambacho anakifanyia kazi mheshimiwa ambacho kinakupelekea mpaka kusaliti watanzania ambao walikuamini wakati ulivyokuwa ukiwaongoza?”

“Senga mimi sio mwanasayansi na hata maelezo ambayo nimepewa sikuyaelewa na sikutaka hata kuelewa Zaidi , lakini nilikaa chini na kupima faida na hasara na nimegundua kwasasa hata kama tuhitaji kumfunga Yan Buwen , jambo hilo halitofanikiwa, nadhani umesoma mikataba ya siri kati ya taifa letu na uchina , mikataba ambayo watangulizi wetu waliisaini na mingine sisi wenyewe kusaini?”Aliongea na Senga kweli alikumbuka baadhi ya mikataba ya siri ambayo imesainiwa na maraisi waliopita , lakini pia mikopo ambayo taifa la China wanadai , aliona kama Yan Buwen atakamatwa Pamoja na uraia wake wa China basi ni kauli moja tu kutoka Beijing na Yan Buwen atakuwa huru”

“Mheshimiwa unataka nifanye nini?”

“Swali zuri Senga , nilikuwa nikisubiria swali kama hilo”

“Kwanza kabisa raisi mstaafu wa Marekani mpaka sasa karidhia kila kitu kuhusu tafiti zilizoachwa na Profesa Shelukindo kuendelezwa na Yan Buwen hilo ni la kwanza , swala la pili ni juu ya Yan Buwen mwenyewe”Aliongea Mheshiiwa na kumfanya Senga kutaka kusikiliza Zaidi.s

“Yan Buwen licha ya kujifanya mjanja na mtu wa kujiamini mbele yangu , lakini ana udhaifu mmoja ambao kwa mwanasayansi kama yeye ni kosa kubwa sana kwake”Aliongea.

“Nakusikiliza mheshimiwa”

“Ana tamaa ya kupitiliza”

“Mheshimiwa tamaa itatusaidiaje?”

“Hilo niachie mimi kwa sasa na nitakupa mpango mzima , ila swala ambalo naliomba kwa sasa nikuruhusu Yan Buwen aendelee na kazi yake ndani ya maabara yetu”Aliongea na kumfanya mheshimiwa Senga kufikiria kidogo.

“Mheshimiwa kabla sijakubaliana na hili nataka kwanza nielewe kitu kimoja, ni jambo gani ambalo Profesa Shelukindo alikuwa akilifanyia utafiti?”

“Sijui kwa maelezo mazuri na kukufanya uelewe ila ni swala la mambo ya ‘Ant -matter Energy”Aliongea.

“Mheshimiwa ndio nini ?”

“Mimi mwenyewe nilivyoelezwa sikufahamu Zaidi, maana sijasoma sayansi , ila kwa malezo ya haraka haraka nikwamba Ant-matter ni sawa na teknoloijia inayohusu nyuklia”

“Mheshimiwa unamaanisha Profesa Shelukindo alikuwa akitafiti maswala ya nyuklia?”

“Sio nyuklia kama nyuklia ila ni Zaidi ya nyuklia mheshimiwa Senga na kama unataka kuelewa Zaidi tunao wanasayansi ambao wana uelewa kuhsu Ant matter Energy”Aliongea

*******

Edna na Roma ndio walikokuwa wamebaki Kigamboni na Bi Wema na wanafamilia wengine wlaikuwa washaondoka na kuelekea Osterbay.

Kilichomfanya Edna kutoondoka mapema ni Najma , Najma alikuwa amempigia Edna simu kwamba anakuja kumsalimia , licha ya Edna kumwambia kwamba ndio wanahama na angekuja siku inayofauta Osterbay , lakini kwa upande wa Najma hakuridhia jambo hilo na alitaka kuonana na Edna siku hio hio.

Saa kumi na moja Roma alikuwa amekaa zake sebuleni akiendeea kuangalia Runinga kama kawaida akisubiria muda ambao mke wake amalize ili watangulizane Kwenda Osterbay, Roma hakuwa na taarifa za ujio wa Najma.

“Wife unaenda wapi? , muda wa kuondoka huu”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna ambaye anashuka kutoka juu , lakini licha ya kuongea Edna alimpotezea na kutoka nje kabisa ya nyumba.

Na ndani ya dakika kadhaa tu Edna na Najma walionekana wakiingia huku wakionekana kucheka kwa furaha.

“Karibu Najma , hapa ndio nyumbani na imekuwa bahati mbaya siku ambayo unapajua ndio nahama”Aliongea Edna kwa bashasha huku akimuonyesha Najma sehemu ya kuketi.

“Za saa hizi Mr Roma?”Alisalimia Najma huku akimwangalia Roma usoni.

“Salama Karibu Najma”Aliongea Roma kwa sauti ndogo huku akimchunguza najma , alimuona kuwa na urembo wake uleule tofauti ni kwamba , Najma alionekana kukonda.

“Wife kwahio ulikuwa ukimsubiria rafiki yako?”

“Ndio aliniambia anakuja kunisalimia, mbona unaonekana kukereka na ujio wa rafiki yangu?”Aliongea Edna kwa kumzodoa Roma.

“Em.. unafikiria mbali sana mimi nimeuliza tu “Aliongea Roma huku akinyanyuka kwa ajili ya kuelekea juu chumbani kwake na kuwaacha wawili hao waongee.

“Najma kuna zawadi nimekuandalia , tungekaa muda mrefu hapa , lakini muda umeenda sana , ngoja nikakuletee uzione”Aliongea Edna na Najma alitabasamu na kutingisha kichwa na ile Edna anaondoka alianza kuangalia mazingira ya jumba hili na kuona kweli kuna watu wanaishi pazuri

Baada ya Edna kutokomea juu , Najma alinyanyuka haraka haraka na kupandisha ngazi kuelekea juu na alivyofika gorofa ya pili alikata kulia kama mtu anetafuta chumba lakini alijikuta akitabasamu baada ya kumuona Roma.

“Najma unafanya nini huku?”Aliuliza Roma kwa mshangao kwani alikuwa amemuacha Najma akiwa eneo la chini akiongea na Edna.

Najma hakujali sana mshangao wa Roma bali alimsogelea haraka haraka na kisha akamkumbatia.

“Najma unafanya nini?”

“Shii…p!!”Alionya Najma kwa kidole na kisha akamkumbatia tena Roma kwa nguvu kwa hisia kali.

“Nimekumisi sana mpenzi…”Aliongea Najma kwa sauti huku akianza kulia kwa kwikwi na kumfanya Roma ashindwe hata kujua afanye nini , na hio yote ni kwasababu mbele yake kwenye ngazi macho ya Edna yalikuwa yakimwangalia kwa hasira kali mno.

Roma ilibidi amtoe Najma kwenye mwili wake na kitendo kile kilimfanya Najma kumwangalia Roma usoni na baada ya kugundua Roma alikuwa amebung`aa ilibidi nay eye kugeuka na kuangalia upande ambao Edna alikuwa amesimama .

“Edna…!!!”Aliongea Najma kwa kusita sita , lakini Edna kwa hasira alirudi juu kwenye chumba chake kwa kukimbia.

END OF SEASON 8
 
SEASON 9

SEHEMU YA 241

Edna alikuwa ashaandaa zawadi tayari kwa ajili ya Najma na kitendo cha kumuacha Najma sebuleni ilikuwa ni Kwenda kuchukua tu na kurejea sebuleni , lakini sasa baada ya Edna kuchukua mkoba ambao alikuwa amehifadhi zawadi kwa ajili ya Najma , ile anatoka alimuona Najma akikatiza uelekeo wa Kwenda upande wa chumba cha Roma na moyo wake ulipiga kwa nguvu kwani hakujua ni jambo gani Najma alikuwa anataka kufanya na aliona huenda Najma anataka kuja kwenye chumba chake na hajui uelekeo ndio maana ,alitembea kushuka kwa ajili ya kumuwahi , lakini sasa ile anafika kwenye korido ya Floor ya pili alijikuta akishangazwa baada ya kuona Najma kamkumbatia Roma kimahaba , moyo wake ulikuwa ni kama ukipitishwa kaa la moto kwa maumivu ya ghafla alioyahisi.

Nimekumsi sana mpenzi…”Maneno hayo yalijirudia rudia mara baada ya kuingia kwenye chumba chake na kuchukua mkoba wake na funguo ya gari na kutoka nje huku akijihisi moyo wake kutaka kumpasuka , bila sababu ya msingi alijikuta moyo wake ukiuma kwa wivu mkali na machozi na yenyewe yalishindwa kuzuilika na yalitoka mfululizo.

“Nimekumisi sana Mpenzi..” Maneno ya Najma yaligonga tena kwa Zaidi ya mara tatu.

“Siku zote walikuwa wakinidanganya hawafahamiani na kuniona mjinga , Najma kwanini umeamua kunidanganya wakati nimetokea kukupenda kama ndugu yangu…”Aliwaza Edna huku akihisi hasira zikizidi kumvaa, alihisi maumivu ya usaliti kwa mara ya kwanza kwenye Maisha yake , alikuwa akimpenda sana Najma na alitamani kufanya mambo makubwa kwa ajili yake kama rafiki , lakini kitendo cha kujua kumbe kipindi chote alikuwa akidanganywa alijihisi moyo kumuuma mno na alijiapia hatokuja kumsamehe Najma na Roma.

“Edna naomba unisame…”

“Najma naomba unyamaze na usiongee chochote tafadhali , urafiki wangu mimi na wewe unaishia hapa kwanzia leo hii..”

“Edna nisamehe naomba unisikilize..”Aliongea Najma huku machozi yakianza kumtoka mfululizo , lakini Edna hakutaka maelezo kama kawaida yake , alishuka chini haraka haraka baada ya kumpiga jicho la uhakika Roma na kisha kutokomea na mvumo wa gari ndio uliosikika dakika chache mbele.

Roma alishindwa kujua cha kufanya kwa muda huo na aliishia kuegamia ukuta na alijiambia muda uliopita mambo na mke wake yalikuwa yakianza kurudi kwenye hali ya kawaida lakini masaa mengine mbele ndio hivyo trna kila kitu kishaharibika.

“Roma nisamehe,,,sijafanya makusudi kuwagombanisha..”Aliongea Najma huku akikaa chini kwenye ngazi.

“Najma huu ulikuwa ndio mpango wako?”Aliuliza Roma kwa sauti ya kawaida lakini yenye usiriasi ndani yake.

“Roma nisame…”

“Nikusamehe vipi wakati umekuja nyumbani kwangu na kuanza kunikumbatia huku ukifahamu kabisa mke wangu yupo?”Aliuliza Roma lakini Najma aliishia kulia kama mtoto aliefiwa kiasi kwamba hata kitambaa alichofunga kichwani kudondoka chini na kuacha msuko wake wa mistari nane kuonekana.

“Najma sijui cha kufanya sasa hivi , ila inabidi uondoke”Alionea Roma.

“Hapana … Roma mpaka unisikilize ,nimemkosea Edna mimi na ananichukia ,naomba na wewe usinigeuzie mgongo tafadharii.. hii.. hii”

Roma alijikuta karoho kahuruma kumwingia na kushindwa kuelewa ni mpango gani Najma alikuwa akipanda kwa ajili yake mpaka kuja hapa nyumbani na kuanza kumkumbatia mbele ya mke wake.

Aligundua kuwa ni makusudia kabisa Najma ameyafanya, kwani alikuwa na simu na namba yake na kama kulikuwa na swala analotaka kuongea na yeye na kama ni kweli alikuwa amemmisi basi angepiga simu tu , lakini hakufanya hivyo Zaidi ya kwmaba amekuja mpaka nyumbani na kumkumbatia mbele ya mke wake.

“Okey,nyamaza na ueleze nini kimetokea”Aliongea Roma huku akimpita Najma na kushuka ngazi kuelekea chini sebuleni na Najma alishuka kinyonge.

“Sikupenda kufanya hivi Roma , nampenda sana Edna kwani rafiki wa kweli , lakini nimeghafilika na kujikuta nachukua maamuzi nilioamua kuyafanya”

*******

SIKU KADHAA NYUMA.

Ni siku ambayo tunamuona Najma akifika ndani ya nyumba anayoishi rafiki yake Nasra na kupokelewa kwa bashasha huku Najma akimuelezea Rafiki yake juu ya mambo anayopitia juu ya afya ya kaka yake Juma.

Sasa siku hii Najma alionekana kukosa usingizi kabisa na yote hayo ni juu ya mawazo aliokuwa nayo juu ya afya ya kaka yake , mrembo huyu hakuwa tayari kumuona kaka yake anapoteza Maisha , alitamani kufanya chochote kwa ajili ya kaka yake ili kupona, kuna muda aliwaza hata kutoa figo kwa ajili yake , lakini alikosa ujasiri kabisa.

Kwake kaka yake ndio ndugu pekee ambaye alikuwa amebakia hapa duniani ambaye alikuwa akiamni alikuwa akimpenda kwa dhati , licha ya madhaifu madogo madogo aliokuwa nayo kaka yake , lakini aliamini alikuwa akimpenda kwa dhati kabisa na ndio maana aliumizwa na maumivu anayopitia kaka yake kutokana na ugonjwa wake , kila saa picha ya kaka yake akilalalamika akiwa amelazwa kule hospitalini haikumtoka kichwani.

“Nasra naweza kukuazima simu yako niingie mtandaoni?”Aliuliza Najma huku akimwangalia rafiki yake Nasra ambaye alikuwa akitoka bafuni na alikuwa akijifuta maji.

“Halafu nimegundua Najma hujaja na simu yako ya siku zote”Aliongea Nasra na kumfanya Najma atoe tabasamu hafifu.

“Nimeuza shost”Aliongea Najma na kumfanya Nasra kushangaa.

“Kwanini umeuiza jamani, ndio maana umekuja kimya pasipo ya kupiga simu”Aliongea Nasra kwa kushangaa.

“Tutaongea kesho Nasra , nisaidie simu yako kuna kitu natamani kufahamu kupitia mtandao”Aliongea Najma.

Ukweli ni kwamba Najma aliuza simu yake ambayo alikuwa amepewa na Nasra kwasababu hela ya hakiba aliokuwa nayo iliisha na hospitalini pesa ilikuwa ikihitajika lakini pia aishindwa kupata msaada kwa ndugu zake , kwani kila mmoja alimwambia hana hela ya kusaidia na jambo hilo lilimuuma sana, lakini Najma hakulalamika kwani alikuwa akijua ugomvi uliokuwepo kati ya wao na ukoo wao , ugomvi ambao ulisababishwa na urithi wa nyumba ambayo walikuwa wameachiwa.

Ukoo wao wakiongzwa na baba mkubwa walitaka kuuza nyumba ya Mbagala na kuwataka Najma na Juma kurudi kijijini kuishi na ndugu , lakini Najma na Juma walikataa katakata na kuanzia hapo ndio uhasama ulipoibuka na ndugu waliwasusa, ndugu pekee aliekuwa akiwapenda kinafiki ni Shangazi yao.

Kwahio ni rahisi kusema kwamba Najma alikuwa peke yake katika kugharamikia matibabu ya kaka yake Juma na hakuwa na msaada ,mtu pekee ambaye alikuwa akimtegemea ni Nasra rafiki yake wa kitambo, lakini mrembo huyo aliona ugumu wa kumuingia Nasra moja kwa moja na kumuomba kiasi cha pesa kwa ajili ya kumsaidia kaka yake na ndio maana akauza simu yake kubwa ya I phone 12 ambayo alipewa na Nasra, lakini licha ya kuuza simu , pesa haikutosha kwani mchana wake madaktari walikuwa wakitaka pesa nyingine kwa ajili ya siku ya kesho kaka yake afanyiwe Matibabu , sasa baada ya kupewa taarifa hio na daktari Najma alijikuta akinyong`onyea kwani hakuwa na pesa nyingine na hakuwa na kitu kingine cha kuuza Zaidi ya nyumba yao.

“Hapana nitaenda kwa Nasra usiku huu kwa ajili ya kumuomba kiasi cha pesa , najua ananidai pesa nyingi lakini sija jinsi”Aliwaza Najma muda wa saa mbili usiku akiwa nyumbani kwao Bias , muda ambao ndio kwanza anafika akitokea hospitalini Mloganzila kupeleka chakula kwa ajili ya kaka yake.

Sasa baada ya wazo hilo kumjia ndio alifunga safari na usiku huo huo kuja nyumbani kwa Nasra kwa ajili ya kumwambia shida yake.

“Usijali Shost hata hivyo unabahati , nimenunua I phone 14 , nitakupa hio toleo la mwaka jana, I phone 13 , lakini hii usiuze”Aliongea Nasra huku akisogelea Dressing table na kutoa simu iliozimwa na kumpatia Nasra.

“Asante sana Shost lakini siwezi kutumia hii simu”Aliongea Najma.

“Kwanini Najma? , unapaswa kuwa na simu hasa kwa wakati kama huu”

“Nasra usinifikirie vibaya , lakini hii simu ni ya gharama kubwa na ukiangalia pia Maisha yangu na pesa ambazo zinahitajika hospitalini , siwezi Shost”Aliongea Najma na Nasra alielewa Nasra anachomaanisha , na Nasra alitabasamu na kisha akakaa karibu na Najma na kumshika mikono.

“Najma najua unachopitia na nahisi maumivu yako , lakini hauko peke yako , sisi sio marafiki tu bali ni ndugu , siwezi kusahau mema ulionitendea wakati nafika kwa mara ya kwanza hapa Dar, Najma tutapambana Pamoja mpaka mwisho kwenye hali aliokuwa nayo Juma, sawa shost?”Aliongea Nasra na Najma alitokwa machozi na alijikuta akimkumbatia rafiki yake.

“Asante sana rafiki yangu , nakupenda , asante kwa kuwa Pamoja na mimi kwenye kipindi hiki kigumu”Aliongea Najma kwa hisia na Nasra alitabasamu na alimwachia Najma na kisha akamkabidhi Najma simu ile na kuipokea.

Asubuhi kulivyokucha Nasra ndio aliekuwa wa kwanza kuamka na nusu saa baadae Najma na yeye alishtuka kutoka usingizini.

“Mbona hujaniamsha Shost?”Aliongea Najma huku akimwangalia Nasra aliekuwa bize kupika , upande wa jikoni.

“Nimekuacha upumzike kwanza, naandaa chakula cha Kwenda nacho hospitalini kabisa huna haja ya kurudi Mbagala na kuandaa”Aliongea Nasra huku akijiweka bize.

“Lete nikusadie unapaswa kujiandaa kuelekea kazini”

“Hapana tutaenda wote hospitalini , sijamuona kaka yako tokea amelazwa , kazini nitaomba ruhusa”Aliongea Nasra na Najma hakuweza kumbishia rafiki yake na walijiandaa kwa takribani lisaa lizima na kumaliza kila kitu na safari ya Kwenda Mloganzila ilianza.

“Dokta nitatoa milioni ishirini za matibabu ya awali , mpaka tutakapopata ufumbuzi mwingine”Aliongea Nasra na kumfanya Najma kushangaa.





SEHEMU YA 242

Kiasi alichotaja Nasra kilikuwa ni kikubwa mno na Najma hakuwa tayari kukubaliana na rafiki yake.

“Nasra Hapana”

“Najma usiwe na wasiwasi , kumbuka jana usiku nilichokuambia, tuko Pamoja mpaka mwisho”Aliongea Nasra huku akimshika mkono Najma.

“Sawa Miss Nasra ni maamuzi mazuri , na niwahakikishie matibabu kwa ndugu yenu yataendelea kwanzia sasa”Aliongea Dokta Issay na sura yake ya kifisadi

“Huyu mtoto mkali , ana moyo mzuri wa kumsaidia rafiki yake , lakini pia pesa anayo lazima niombe namba
”Aliwaza Dokta Issay huku akiangalia msambwanda wa Nasra ukitokomea nje ya ofisi yake.

Sasa baada ya Najma kuachana na Nasra alipanda daladala kuelekea Mbagala kwa ajili ya kuendelea na majukumu mengine Pamoja na kuandaa chakula cha mchana.

Saa chache tu alikuwa ashafika na jambo la kwanza alitoa simu aliopewa na rafiki yake na kisha akaweka laini zake alizozitoa na akawasha simu.

“Asante sana Nasra kwa msaada wako , hakika wewe ni rafiki wa kweli, sijui nitakulipa nini”Aliwaza Najma huku akikaa kwenye kochi la mbao kivivu akisubiria simu yake iwake.

Na dakika kadhaa tu simu yake mpya ya kuvutia iliwaka na kumfanya mrembo huyu kutabasamu huku akiigeuza geuza, alijiambia simu hii ni nzuri sana na ndio maana wadada wengi mjingi wapo tayari kuuza miili yao kwa ajili ya kununuliwa I phone.

Meseji mfululizo zilianza kuingia kwenye simu yake na aliangalia baadhi na kuzipotezea , lakini meseji moja ndio iliomtia kichefu chefu.

Elvice: Mrembo mbona hupatikani hewani nakupigia tokea juzi , mpango umekamilika na pesa kwa ajili ya kaka yako kubadilishiwa figo ishapatikana ni wewe tu na maamuzi yako”.

Najma alisoma meseji hio huku akianza kufikiria siku ambayo kwa mara ya kwanza amekutana na Elvice.

Elive na Najma mara yao ya kwanza ilikuwa ni ndani ya kituo cha kulelea Yatima kule Kiwangwa.

“Unaonekana unempenda sana?”Sauti ilisikika nyuma yake Nasra huku akiangalia gari aliopanda Edna na Roma ikitokomea kwenye macho yake ,hii ni siku ambayo mrembo Najma kwa mara ya kwanza alifahamu Roma mke wake alikuwa ni bilionea mrembo Edna na utambuzi huo ulimfanya kuumia sana kwani aliona hana kigezo chochote za kumzidi Edna kiasi cha kumfanya Roma kumpenda tena , yaani alijona amezidiwa kila kitu.

Najma alimwangalia Elvice aliefungwa bendeji kwenye mkono wake na mwanaume huyu licha ya kuwa handsome hakuonekana kumvutia kabisa tofauti na kwa Roma Ramoni na Najma hakutaka kujibu swali la Elvice kwani aligeuka na kurudi ndani ya ofisi yake

“Bibie nini hivyo kunikalia kimya?”Aliuliza Elvice baada ya kuingia ofisini kwa Nasra

“Kaka Samahani sikufahamu , hivyo siwezi kujibu swali lako”Aliongea Najma kwa usiriasi huku akikereka na uwepo wa Elvice kwenye ofisi yake.

…………………

Sasa kwanzia siku hio Elvice alimuandama sana Najma, lengo la kumuandama sio kwa ajili ya mapenzi , bali ni kwa ajili ya hisia za mrembo huyo Kwenda kwa Roma Ramoni , aliamini kama atamtumia vyema Najma basi Ndoa ya Roma na Edna itayumba na hii ni baada ya kupata Habari kutoka kwa Mama Issa juu ya uhusiano uliopo kati ya Edna na Najma.

Siku nyingi zilipita pasipo ya Najma kuonyesha ushirikiano kwa Elvice Temba , lakini bwana huyo hakukata tama, aliendelea kumfuatilia Najma na hata namba yake alikuwa nayo.

“Mbona umeng`ag`ania sana hisia zangu juu ya Roma wewe?”Aliuliza Najma kwa kutumia ujumbe wa meseji akiwa ndani ya nyumba yake aliopewa na kituo.

“Kwasababau na mimii nina hisia na Edna , na Roma amenipokonya mwanamke wa ndoto zangu”meseji ilisomeka kwenye kioo na kumshangaza Najma.

“Unamaanisha unafahamiana na Edna?”

“Hilo ni jibu cha urembo , Edna sio kumfahamu tu , ila nilikuwa rafiki yake wa muda mrefu”

“Mh!, sasa imekuwaje ukaacha akaoelwa na mtu mwingine?”

“Na wewe kwanini ukaacha Roma akaoa mwanamke mwingine ilihali una urembo wa ajabu?”

“Swali juu ya swali”Aliwaza Najma huku akifikiria cha kujibu.

“Sijui labda hanipendi”

“Sio hakupendi , anakupenda ila ukute sababu ilikuwa wewe mwenyewe”

“Unamaanisha nini?”

“Fikiria mrembo , jibu lipo kwenye moyo wako”Meseji ya Elvice ilisomeka.

Najma alianza kufikiria sababu , alianza kufikiria tokea siku ambayo anaonana na Roma kwa mara ya kwanza , akafikiria kila kitu ambacho Roma amemfanyia , alifikiria na kufikiria na akakumbuka siku ambayo Roma alifika Vikindu na kumuokoa kwenye mikono ya Karim

“Shosti The Chosen one anakupenda sana , trust me”Alikumbuka pia maneno ya rafiki yake Nasra siku aliomwelezea namna alivyookolewa na mwanaume wa ndoto yake na Najma alifikia kwenye hitimisho la kwamba Roma ana mpenda sana ndio maana alikuwa tayari kumuokoa.

“Ni kweli nina hisia nae sana tu na naamini ananipenda pia”Alijibu Nasra na kusubiria jibu.

“Ewaaa..hilo ndio jibu , na mimi kwa Edna ni hivyo hivyo”

“Unamaanisha Edna hampendi Roma?”

“Nina uhakika asilimia mia Edna hana mapenzi ya dhati kwa Roma, ila Roma kafuata pesa kwa Edna niamini mimi mrembo”Meseji ilisomeka

“Inawezekana”

“Najma unapaswa kumrudisha Roma kwenye himaya yako na mimi nitamrudisha Edna wangu, hili ni swala la sisi wote kusaidiana”

“Kivipi?”

“Tutawaachanisha”

“Mh!, mimi sipo tayari kama Roma ananipenda atarudi kwangu mwenyewe”Alijibu Najma lakini Elvice aliendelea kubembeleza , lakini kwanzia siku hio jibu la Najma lilikuwa ni moja tu kwamba hayupo tayari na aliamini kama Roma anampenda atarudi kwake.

Elvice alitafuta mbinu za kumbembeleza sana tu mrembo huyo , lakini msimamo wake ulionekana kuwa imara , lakini hakukata tamaa na tumaini lake liliibuka upya baada ya kufahamu Juma kaka yake Najma yupo hoi bin Taaban na figo zimefeli na hapo akaona akiingia na gia za kumsaidia pesa Najma kwa ajili ya matibabu ya Juma basi atakubaliana na mpango wake.

…….

Najma aliangalia meseji ya Elvice kwa muda na kisha akaachana nayo .

‘Nasra kanisaidia kiasi kikubwa cha pesa , siwezi kumkosea Allah kwa mpango wa Elvice wa kutaka kugombanisha ndoa ya Roma , Hapana siwezi , Hata hivyo Roma kanisaidia sana wakati akiishi hapa nyumbani , siweizi kumlipa mabaya”Aliwaza Najma huku akipotezea kabisa mpango wa Elvice na kuendelea kujipiga picha kwa kutumia simu yake mpya na kisha aliingia sehemu ya kitufe cha kuhifadhia picha na kuanza kuangalia.

Namshukur Allah kwa kunijalia uzuri huu , naamini siku nitapata mwanaume anaenipenda na nitakaempenda , inabidi niachane na Roma , siwezi kugombanana na Edna rafiki yangu anaeonekana kunipenda”Aliwaza tena Najma huku akipitia picha alizopiga na I Phone 13 , picha za bei mbaya, ndio I phone inapicha za bei ghali, sio kama picha za Infinix(Mnisamehe).

Sasa wakati Najma akiperuzi picha zake Kwenda kushoto alijikuta moyo wake ukipiga Paah, hakuamini alichokua akikiangalia , alivuta picha iliokuwa kwenye simu hio na kuiangalia kwa umakini.

“Huyu si Roma , picha yake inafanya nini kwenye simu ya Nasra”Aliwaza Najma huku akimwangalia Roma aliekuwa kwenye usingizi akiwa kitandani kifua wazi, aliswipe haraka haraka kuangalia picha zingine na moyo wake ulinyong`onyea baada ya kuona picha ambayo Nasra amepiga akiwa na Roma kitandani.

Machozi hayakueleweka yalitoka wapi , lakini alijihisi moyo wake kumuuma sana , sana yaani , hakuwahi kufikiria rafiki yake kipenzi Nasra anaweza akawa na mahusiano na Roma.

Mrembo huyu alijiona kama anaechanganyikiwa na hata simu aliitupa pembeni huku akionekana kuiogopa na kuanza kulia.

Ilikuwa ni asubuhi , lakini saa saba ilimkuta akiwa analia kwa maumivu huku akihisi usaliti mkubwa uliofanywa na rafiki yake Nasra, maneno mbalimbali aliokuwa akiongea na Nasra yaliibuka kwenye kichwa chake na kujikuta akikasirika Zaidi.

“Ndio maana yupo tayari kwa ajili ya kunisaida hela kubwa kiasi kile kule hospitalini kumbe yote ni kwa ajili ya kunihadaa, I hate yoo Nasra”Aliongea Najma na kisha alisogelea simu yake haraka haraka na kisha alienda kwenye ujumbe wa simu uliotumwa na Elvice na kisha alipiga palepale.

“Nipo tayari kwa ajili ya mpango wako”Aliongea.

“Safi sana , Najma uzuri wako unaendana na Busara zako”Iliskika sauti upande wa pili.

“Niambie tukutane wapi?””Nitakupigia baadae usijali na nitakupa mpango mzima”Na simu palepale ikakatwa.

“Najma nitafauta mpango wa Elvice , ili nipate pesa nikulipe unachonidai na kuanzia hapo urafiki wangu na wewe unakufa , siwezi kuendelea na rafiki mnafiki kama wewe, Edna utanisamehe lakini Romaa naamini hakupendi kama kaamua kutembea na rafiki yangu , nitakusaidia uachane nae na utampata Elvice mwanaume anaekupenda kwa dhati na kuwa tayari kufanya chochote”
 
SEHEMU YA 243

Siku ileile Najma anagundua kuhusu mahusiano ya Roma na Rafiki yake Nasra , upande wa ofisini kwa Nasra alionekana kwenye mawazo, Nasra alikuwa akifikiria mambo mawili kwa wakati mmoja na jambo la kwanza ni juu ya Roma kuwa mume wa Edna na kutokufahamu kwa muda mrefu , lakini pia alikuwa akifikiria mwisho wa mwezi alioahidiana na Roma kwa ajjili ya kumpeleka kwao kuonana na mama yake.

Mrembo Nasra alikuwa yupo katikati ya maamuzi , ukweli hakutaka Kwenda nyumbani pasipo ya kusindikizwa na Roma kama walivyoahidiana na hio ni kwasababu alishatoa ahadi kwa mama yake.

Wakati akiendelea kuwaza hili na lile kuna wazo jipya ambalo liliingia kwenye akili yake na jambo hilo lilikuwa ni juu ya simu aliompatia rafiki yake Najma , alikumbuka mara ya mwisho baada ya kulala na Roma usiku kucha alijipiga picha mfululizo yeye na Roma.

“Oooh! My God nilisahau kuhamisha zile picha”Aliwaza Nasra huku akichukua simu yake kwa ajili ya kupiga , lakini alishindwa kuendelea kwani ofisi yake ilifunguliwa na moja ya mfanyakazi kutoka chini ya idara yake na kughailisha jambo lile.

“Naamini hatoangalia , lakini hata kama akiona yeye ni rafiki yangu , sijawahi kumwambia chochote kuhusu Roma na naamini atanilaumu”Aliwaza Nasra kwenye kichwa chake huku akimpa ishara mfanyakazi kuingia ndani.

*******

Roma alipata kusikiliza kila kitu alichoongea Najma mbele yake na alijikuta upande mwingine kuhisi kuwa na hatia , kwani aliamini hayo yote nyalikuwa yakitokea kwa sababu yake na wala Najma hakuwa wa kulaumiwa , lakini bado hata hivyo aliona Najma alikuwa na makosa kwa upande wake.

“Kwahio Elvice alitaka ufanye nini?”Aliuliza Roma huku akimwangalia Najma ambaye alikuwa akilia na kuona aibu kwa wakati mmoja.

“Alitaka nilale na wewe na kisha nijirekodi wakati wa kufanya mapenzi na tumtumie Edna”Aliongea Najma.

Ndio, mpango wa Elvice ambao alihitaji Najma kuufanya ni kumwita Roma hotelini na kisha ahakikishe wanafanya mapenzi na Roma huku camera ya siri ikiwarekodu na baada ya tukio hilo video itumwe kwa Edna.

“Sikia Najma sisi tutafanya kila kilichobaki , wewe cha kufanya nikuhakikisha tu unafanya mapenzi na Roma”Aliongea Elvice muda wa saa nane wakati wakiwa ndani ya mgahawa mmoja mkabala na jengo la WaterFront na siku hio Elvice hakuwa peke yake bali alikuwa na Desmond.

“Unataka kunirekodi , hilo swala linatofauti gani na kucheza michezo ya filamu za ngono?, Hapana Elvice mpango ambao nilikuwa nikitaka sio wa aina hii, huko ni kumkosea Mungu”Aliongea Nasra kwa hasira na kisha akasimama na kutaka kuondoka.

“Najma huna haja ya kuogopa , kitakachorekodiwa utakiona wewe tu na sisi hatutahusika kabisa , yaani wewe ndio utakuwa dereva wa mpango wenyewe na ukishakamilisha, mtu wa kutoa figo atakuwa chumba cha upasuaji na kaka yako atarudi katika hali yake ya kawaida”Aliongea Elvice kwa kushawishi na muda huu kwa upande wa Desmond alikuwa akimwangalia Najma kwa macho ya kiulizo , mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa mrembo mno na alishangaa kwanini mwanamke kama huyo alikuwa akiteseka , lakini aliona sio swala la kujali kwa muda huo.

“Elvice kama huo ndio mpango wenyewe sipo tayari , nitafanya ninachokijua mimi kwa ajili ya wao kuachana”Aliongea Najma huku akimwangalia Elvice kwa macho ya hasira , alimuona mwanaume huyo kama mkatili na firauni

“Najma..”Alijaribu kuita lakini Najma alikuwa akitokezea mlangoni.

“Relax Bro , huyu mrembo anaonekana ana shida na kwa jinsi ninavyomuona anaonekana amepigwa na kitu Kizito na atachukua maamuzi muda si mrefu”Aliongea Desmond na kumfanya Elvice kutuliwa.

“Kweli!!!”

“Yupo Desparate, lakini mpango wako umevuka mpaka, anaonekana kuwa hata mapenzi yenyewe hayajui vizuri , halafu leo hii unamwambia ajirekodi , nimekushangaa pia kwani nilijua mwanamke unaenikutanisha nae ni kahaba of some sort”Aliongea Desmond na Elvice alivuta pumzi na kuzishusha.

“Kwahio tunafanyaje?”

“Wewe nae unaonekana kuwa mzembe sana wa kuwajua wanawake , ujeda umekuharibu , alishasema atafanya anachokijua ili waachane na wanawake wako vizuri sana kwenye hilo”Aliongea Elvice huku akitabasamu kifedhuli.

“Kama akifanikisha , vipi kuhusu upande wetu , mtu wa kutoa figo hatuna mpaka sasa?”Aliongea Elvice na kumfanya Desmond atabasamu.

“Usiwe mjinga kijana wangu, nilifikiria upo smart upstairs lakini unaonekana kilaza bado , mwanamke kama yule ni wa kumtapeli tu” Aliongea Desmond na kumfanya Elvice aone kweli mshirika wake wa awamu hii ni shetani.

……………..

Upande wa Roma baada ya kusikiliza mpango wote wa Elvice alijikuta akipatwa na hasira mno na alitamani Elvice awe mbele yake na ampatie adhabu ya kifo.

“Roma naomba unisamehe , sikuwa nikifikiria vizuri, nilikuwa nikiheshimu ndoa yako na Edna na ndio maana nilikaa kimya lakini….”

“Lakini nini?”

“Sikujua kama una mahusiano na Nasra rafiki yangu”Aliongea Najma na kuanza kulia upya na Roma macho yalimtoka na alianza kuvuta picha siku ambayo alimuona Nasra na N ajma wakiwa Pamoja siku ya msiba wa baba yake Edna.

“Wewe na Nasra mna ukaribu wa aina gani?”Aliuliza Roma huku akiona hata aibu ya kuuliza hilo swali lakini Najma hakuweza kujibu.

“Namchukia Nasra kwa kunidanganya na kunihadaa .. Roma sikulaumu kwa hili kwasababu mimi ndio nilikuwa mjinga , licha ya kwamba ulionekana kuzikataa hisia zangu lakini niliendelea kukupenda , hata shangazi yangu na kaka yangu waliponitafutia mume nilimkataa kwasababu ya mapenzi yangu kwako…”

“Najma..”

“Roma naomba uniombee msahamaha kwa Edna , najua anaweza asinisamehe, lakini naomba uniombee msamaha , naomba pia unisamehe kwa yalitokea leo kwa kukugombanisha na mke wako naamini Mungu atawasimamia na mtayajenga … kwaheri Roma”Aliongea Nasra na kisha alinyanyuka na kukimbilia nje huku akimuacha Roma ashindwe hata kujua cha kufanya.

********

Ni siku ya jumatatu nyingine Roma aliamkia ndani ya jumba jipya ambalo yeye na famili yake walihamia , nyumba ambayo kwasasa ilikuwa inapendeza Zaidi kuliko wiki kadhaa nyuma na ilionekana Edna aliifanyia ukarabati baada tu ya msiba kuisha na Roma alimsifia kwa hilo na kuona Edna ni mwanamke ambaye anafikiria kama mwanaume muda mwingine, kwani ndani palikuwa pamependeza sana kiasi kwamba ilionekana kama haijawahi kukaliwa.

Roma aliamka akiwa na hatia moyoni , ukweli tukio lililotokea jana yake la Najma, bado hakulisahau na pia hajalitafutia ufumbuzi bado , muda wa saa mbili alishuka mpaka’ Dining’ kwa ajili ya chai ya asubuhi , lakini alishangaa baada ya kuona Edna kutokuwepo.

“Sophia Edna keshaenda kazini?”Aliuliza Roma baada ya kusalimiana na mama yake Pamoja na Bi Wema na Yezi.

“Ndio keshaondoka muda mrefu tokea saa kumi na mbili”Alijibu Bi Wema na kumfanya Roma kushangaa. Na kujiuliza saa kumi na mbili ni kazi gani hio ambayo Edna anaenda kufanya au ndio mbinu mpya ya kuchuniwa.

“Roma kabla ya kuondoka na kuelekea kwenye majukumu yako ya kazi naomba tuongee kidogo”Aliongea Blandina na Roma alifikiria kidogo na kisha alitingisha kichwa kukubaliana na mama yake.

“Sophia unapaswa uanze kujiandaa na uimbaji wako”Aliongea Roma na kumfanya Sophia kushangaa kidogo.

“Sophia unajua kuimba?”Aliuliza Blandina kwa mshangao.

“Ndio mama najua kuimba na ndoto yangu kubwa ni kuwa msanii mkubwa hapa nchini”Aliongea Sophia na kumfanya Blandina kutabasamu.

“Ni jambo zuri kwa mtu kuwa na ndoto kubwa , Sophia jitahidi , japo sijasikia hata siku moja ukiimba ila naamini unachokipaji kikubwa”Aliongea Blandina.

“Mimi nimemsikia Sophia akiimba , yupo vizuri sana anasauti nzuri na naamini atakuwa muimbaji mzuri”Aliongea Yezi na Bi Wema na yeye akaunga mkono hoja na kumfanya Roma atabasamu namna ambavyo familia ilivyochangamka na alijikuta akihuzunika baada ya kuona Mke wake Edna hakuonekana kwenye meza hio.

“ Mwezi ujao tunampango wa kuanza mashindano ya kuibua vipaji kwenye kampuni mpya ambayo ninaenda kuisimamia , Sophia inabidi uanze mazoezi ya kujiandaa”Aliongea Roma.

“Roma unakwenda kuongoza kampuni?”Aliuliza Blandina.

Ukweli mama huyu licha ya kwamba alikuwa akijua Roma sio wa kawaida lakini alichoamini ni kwamba mwanaye alikuwa masikini tu na kila kitu alikuwa akitegemea kwa mke wake Edna na hata swala la Roma kuongoza kampuni hakuwa amelisikia.

“Ndio Sister Edna kafungua kampuni nyingine na Bro Roma anakwenda kuiongoza”Aliongea Sophia na kumfanya Blandina kutabasamu , kwani mwanzoni alisikia Roma alikuwa akifanya kama mfanyakazi wa kawaida ndani ya kampuni ya mke wake , jambo ambalo kwake lilikuwa likimuumiza kichwa na kuona Edna anaweza kumdharau na alikuwa na mpango kumpatia Roma kiasi cha pesa chote alichokuwa nacho benki ili kidogo kumpandisha hadhi ya kuwa sawa na mke wake.

“Sister Edna anampenda sana Anko , ila anko wangu mimi pasua kichwa”Aliongea Yezi na kumfanya Roma amwangalie.

“Yezi toka lini ukaanza kunikandia?”

“Kwani uongo wewe ni kichwa ngumu , muda wote unamkasirisha Sister Edna na hata jana ulimkasirisha ndio maana kafika hapa mwenyewe akiwa kanuna”Aliongea Yezi bila kuficha neno na wanafamilia wote walimgeukia Roma.

“Mr Roma , ni kweli jana Miss kaja hapa akiwa kwenye hali ambayo sijawahi kumuona, kama kuna kitu kimetokea naomba ujaribu kuyamaliza”Aliongea Bi Wema kwa sauti ya upole na Roma aliona hana haja ya kumpiga Bi Wema kwani Bi Wema alikuwa ni sawa na mama kwa Edna na sio mlezi tu.

“Broo Roma kwahio mashindano yatakuwa lini?”

“Hatujapanga tarehe bado ila unapaswa kujiandaa hivyo”Aliongea Rima huku akinyanyuka kwani alikuwa ashamaliza.

Blandina na Roma walipandisha juu mpaka kwenye ‘Living lounge’ ya juu kwa ajili ya kuongea.

Hii nyumba na ya kule Kigamboni hazikuwa na utofauti mkubwa kwani zote zilikuwa na jumla ya ghorofa tatu , kinachoipa ‘credit’ hii nyumba ni upana wake, ukiangalia kwa mbele unaweza usione kama ilikuwa na ghorofa tatu., lilikuwa ni kama kasri kwa muundo wake.

“Roma nafahamu mara ya mwisho tulipoongea hukutaka tuongelee mambo yaliopita na mimi kama mama yako nilielewa japo natamani sana kujua mambo uliopitia”Aliongea Blandina hhuku akionyesha hali ya huzuni.

“Roma mimi mama yako nakushukuru sana kwa kuvumilia yote uliopitia na kuwa hai, nakushukuru sana kwa hilo na ninaahidi kuishi na wewe kwa muda wangu wote nilibakiwa hapa duniani..”Aliongea Blandina , lakini machozi na hayakumuacha salama na hili lilimshangaza Roma , na alihisi ni lazima kuna jambo ambalo limemtokea Mama yake na alikuwa akificha , ila alishindwa kuuliza.

“Mama huna haja ya kuwaza tena mambo yaliopita , kila kitu huja kwenye Maisha yetu kwasababu maalumu , hivyo naomba kwanzia sasa hivi usitoe tena machozi mbele yangu “Aliongea Roma kwa sauti ya kuwa siriasi kidogo na kumfanya Bladina kutingisha kichwa.

“Roma najua sipaswi kuingilia kwenye maswala yako ya kimahusiano wewe na Edna , lakini mimi kama mama yako kwa jinsi unavyoishi na mkeo jambo hili linaniumiza, Edna ni mwanamke mzuri sana na nikupe hongera juu ya hilo ,Edna licha ya kwamba sikuwa na ukaribu nae , lakini familia yake nilikuwa nikifahamiana nayo kwa muda mrefu na walikuwa ni watu wazuri sana kwa ujumla wake hivyo naamini kwa malezi waliompatia Edna ni mazuri, hivyo nampokea kwa mikono yote kama mwanangu pia”Aliongea Blandiana na kumfanya Roma afikirie kidogo na kushindwa hata kujibu

“Roma kama nilivyosema Nishamkubali Edna kuwa pia mwanangu kwakua ni mke wako hivyo sipo tayari kuona akiachana na wewe kwa namna yoyote ile , nafahamu kuna mambo ambayo hayako sawa kati yako na Edna hivyo ninakuomba uyashughulikie mapema kabla Edna hajachoka, unaweza usituelewe sisi wanawake lakini kuna muda uvumilivu ukitushinda na kusema basi ujue ni basi kweli”Aliongea Blandina na kumfanya Roma aone mama yake anapointi ya msingi na aliamini mama yake ashafahamu kuwa ana wanawake wengine nje ya ndoa.

“Mama huna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya hilo , kwasababu umekiri kwamba unampenda Edna kama mkwe wako na mimi nitahakikisha anaendelea kubakia kwenye Maisha yangu na yako milele”Aliongea Roma na kumfanya Blandina kutabasamu.

“Nafurahi kusikia hivyo mwanangu, ila usisahau pia nahiraji japo kuitwa bibi”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kutabasamu kwa uchungu.

“Sidhani kama kuna mwanamke ambaye anaweza kushika ujauzito wangu?”Aliwaza Roma huku akichana na mama yake.

Roma moja kwa moja alitoka na gari yake na mpango uliokuwa kwenye kichwa chake ni Kwenda hospitali ya Mloganzila kwa ajili ya kufuatilia matibabu ya Juma , kwenye kichwa chake alijiambia ili kumaliza swala la Edna na yeye , hatua ya kwanza ni kumaliza swala la Juma na Najma kwanza , aliona hatokuwa na amanni na kumuacha Najma kupambana na afya ya kaka yake mwenyewe na aliona uhatari wa kumuacha unaweza kumeletea matatizo Zaidi , kwani swala la Elvice mpaka muda huo lilikuwa kwenye kichwa chake.

Sasa baada ya kuingiza gari ndani ya eneo la maegesho ya muda mfupi alijikuta akipigwa na mshangao kwani hakutegemea kumuona Edna ndani ya hosputali hio , tena mbaya Zaidi hakuwa peke yake , bali alikuwa amesimama na Najma Pamoja naSuzzane msaidizi wake binafsi na alijiuliza kwanini wapo wote kwani ni jana tu Edna aliweka wazi kati yake na Najma urafiki umekufa.
ITAENDELEA
SINGANOJR -0687151346 WATSAPP ONLY NICHEKI
 
hicho kitoto lailan isije kuwa ndio kitoto cha roma kwa seventeen [emoji849][emoji849][emoji849][emoji849]
 
Ndio maana ukipigiwa hupokei sio?mi nataka muendelezo,ulinitumia mpaka 273 nakupigia hupokei!
 
EHEMU YA 244
Roma baada nya kuona wanawake hao wakiwa mbele yake, alifanya maamuzi ya kutotoka kwenye gari kwanza ili kuangalia kile kinachoendelea na zilipita kama dakika tano hivi ya Edna kuongea na Najma, na kwa upande wa Najma alionekana kutingisha kichwa kama vile mtu aliekuwa mbele ya raisi nchi akipokea maagizo.
Yaani kwa maneno marahisi Roma alimuona Najma akiitikia kama vile Edna alikuwa ni bosi wake na hakuona dalili ya urafiki wao tena na alijiuliza ni kipi kinachoendelea ila alisubiria kwanza.
Roma aliwaona Edna pamoja na Suzzane wakiingia kwenye V8 na kutoka nje kabisa ya eneo hilo la hospitalini, huku wakimuacha Najma akiwa amesimama huku akiangalia gari lao lakini pia alionekana kujifuta machozi na kitambaa alichoshikilia mkononi.
Roma aliendelea kukaa kwenye gari mpaka pale alipomuona Najma akianza kupiga hatua kivivu kutoka nje kabisa ya hospitali hio na hapo ndipo Roma alipofungua mlango wa gari yake na kutoka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya hospitali hii eneo la mapokezi.
“Za saa hizi mrembo”Alisalimia Roma kwa namna ya kisheshi na mwanadada aliekuwa mbele yake alievalia mavazi ya kinesi eneo la mapokezi alitabasmau na kumwangalia Roma.
“Salama kaka , nikusaidie tafadhari”Aliongea yule nesi akiweka sura ya uprofesheno na Roma alitabasamu.
“Kuna mgonjwa wangu hapa anafahamika kwa jina la Juma Kakwera, nimekuja kumuona”Aliongea Roma na mwanadada yule alishangaa kidogo na kumwangalia mwanaume aliekuwa mbele yake.
“Ndio mgonjwa huyu yupo ndani ya hospitali yetu, naweza kujua mahusiano yako na mgonjwa tafadhari?”
“Mimi ni rafiki yake , ni braza wangu hivyo nimekuja kumuangalia”Aliongea Roma na dada alitabasamu.
“Okey , kwasasa hutoweza kupata nafasi ya kuonana nae kwani sio muda wa kuonana na wagonjwa itakubidi uje saa saba”Aliongea yule dada kwa sauti ya upole na kumfanya Roma afikirie kidogo.
“Mr Roma!”Roma alijikuta akigeuka mara baada ya kusikia sauti inamwita kutoka nyuma yake upande wa kushoto.
“Dokta.., Bora hata nimekuona”Aliongea Roma huku akitabasamu baada ya kumwangalia mwanaume aliekuwa mbele yake , alikuwa ni dokta ambaye anamtibia Juma anaefahamika kwa jina la Dokta Issay.
“Nilijua nakufananisha wakati nikiwa upande ule , kumbe ni wewe?”Aliongea Dokta kwa bashasha.
Roma asingeweza kumsahau Dokta Issay kwani washawahi kukutana , Dokta Issay na Mama Aisha ni kitu na mkwe wake, yaani mama Aisha mtoto wake wa kwanza afahamikae kwa jina la Aisha ndio ameolewa na Dokta Issay.
Mama Aisha ni yule mwanamke ambaye Edna na Roma walienda kipindi kula chakula wakati wakitoka Kibaba hadi Roma akashinda shindano la kula nyam ana kumzawaidia Edna mdoli, Sasa siku ambayo Roma alikuja Dar kwa mara ya kwanza na kukaribishwa na Mama Aisha nyumbani kwake ndipo alipoweza kukutana na Dokta Issay.
Kilicomfanya Roma kuzoeleka haraka ni kutokana na stori yake, familia ya Mama Aisha haikuamini kama ni kweli Roma alikuwa akitembea wa mguuu kuja Dar kutokea mpaka kupatiwa lift na Mama Aisha.
“Mke wangu aliniambia umeoa mwanamke mrembo sana”
“Mkeo kafahamu vipi ,mbona sijawahi kukutana nae tena toke siku ile nilivyowaacha”
“Mke wangu kaambiwa na mama yake , nasikia ulimpeleka mkeo kwenye mgahawa wake kuleMakongo juu”.
“Aah kumbw ni hivyo, ndio nilibahatika kupata mke mjini hapa mrembo na pesa zake”Aliongea Roma huku wakitembea uelekeo wa ofisi ya Dokta Issay, Ghorofa ya tano ndani ya jengo hili la Mloganzila.
“Aisee nikupe sana hongera , ijapokuwa sijawahi kuonana na mke wako ila nimesikia sifa zake kwamba ni mzuri kuliko hata mrembo wangu Aisha Shombe Shombe”Aliongea na Roma alitabasamu huku wakiingia ndani ya ofisi hii ya kitabibu.
“Sasa Dokta mimi sio mkaaji maana nahitajika kuelekea kazini, nipo hapa kwa ajili ya mgonjwa anaefahamika kwa jina la Juma Kakwera ni mgonjwa wa matatizo ya Figo”Aliongea Roma mara baada ya kuketi akikatisha Stori.
“Juma ndio ni mgonjwa wangu, una uhusiano gani na yeye?”
“Ndio rafiki alienipokea wakati nafika hapa Dar”
“Ooh!, Aisee rafiki yako naweza kusema anabahati sana”
“Usiniambie tayari ashapona?”Aliongea Roma na kumfanya Dokta Issay kutabasamu
“Sijamaanisha hivyo Mr Roma, hivi ninavyoongea na wewe nusu saa zilizopita nilikuwa na bosi Edna wa Vexto hapa na katoa kiasi cha milioni mia mbili kwa ajili ya kununua figo ili rafiki yako apatiwe matibabu”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa na sasa kuelewa kwanini alimuona Najma akiwa na mke wake, ila alijawa na shauku ya kujua ilikuwaje mpaka Edna akafikia uamuzi huo.
*******
JANA
Kitendo cha Roma na Najma kufahamiana tena sio kufahamiana tu na kuwa wapenzi juu na kumficha kilimuuma sana , Edna alijiona mjinga sana kwa kutogundua hilo mapema , alijilaumu pia kwa kumuamini Najma jambo ambalo sio kawaida yake kuamini watu kirahisi.
Edna aliendesha gari huku akikumbuka siku ya kwanza alivyoweza kukutana na Najma , alimuona kama moja ya mwanamke mpole ambae anaejiheshimu kutokana na mavazi yake , tabia ya Najma kupenda pia kucheza na Watoto ndio ilimfanya Edna kumpenda hata kuepelekea kuanza kwa urafiki wao, urafiki ambao ulikuwa haraka kutokana na kwamba Najma hakumchukulia Edna kama boss bali kama rafiki yake wa kawaida wa levo sawa na yake na namna ambavyo Najma aliweza kujiachia mbele ya Edna na vile vile kwake yeye.,
Lakini kitendo cha Najma kumdanganya ilihali alikuwa akifahamiana na Roma na tena kuwa wapenzi kabisa kilimuuma na kumuuzi mno.
Edna alifika Osterbay na kufunguliwa mlango na kuingia ndani huku akiwa amefura kwa hasira na hata kwa wanafamilia, waliokuwa bize kupangilia vitu waligundua mabadiliko aliokuwa nayo Edna na walijiuliza ni nini kimetokea kwani walikuwa wakimtegemea Edna kufika hapo akiwa na Roma , lakini ajabu ni kwmaba alifika akiwa mwenyewe na mbaya Zaidi alikuwa akionekana mwenye hasira , lakini licha ya hivyo hakuna hata mmoja aliekuwa na nafasi ya kuuliza na ukizingatia pia walikuwa bize kuweka mazingira ya nyumba yao vizuri.
Edna baada ya kuingia kwenye chumba chake ambacho hakikuwa kipya kwake kutokana na kuishi ndani ya chumba hiko tokea alipokuwa mdogo , alikaa kitandani na kisha kuinama chini kama mtu ambaye alikuwa akiwaza , alikaa kwa staili moja ya kuinama chini kwa takribani dakika kumi ndipo alipotoa simu yake kwenye mkoba na kuipangusa kwa dakika kadhaa na kuweka sikioni.
“Suzzane kuna mtu nataka taarifa zake”Aliongea Edna huku akiweka sura ya usiriasi.
“Sawa boss , nitajie jina lake”
“Kuna mwanadada alikuwa ni moja ya marafiki zangu wa karibu anaitwa Najma ni mwalimu ndani ya kituo cha Son and Daughter orphanage…”
“Boss taarifa za huyo mwanadada mbona tayari ninazo”Ilisikika sauti ya Suzzane upande wa pili na kumfanya Edna kushangaa
“Sikumbuki kama nilikuambia ufatilie taarifa zake, umemfahamu vipi”
“Samahani Boss , nilichukua tahadhari mapema baada ya kujua una urafiki nae ili kuhakikisha usalama wako”Aliongea Suzzane.
“Naona kama kawaida yako.. anyway nitumie hio taarifa kwa simu au nielezee”Aliongea Edna huku akivuta pumzi , hakutaka kumlaumu Suzzane kwa kumfatilia Najma , kwani alikuwa akimfahamu Suzzane tokea apewe kazi na mama yake ya kuwa msaidizi wake wa karibu , alikuwa akifuatilia kila mtu anaekuwa na ukaribu na yeye.
“Boss unakumbuka ile nyumba ambayo ulilala kule Mbagala?”Aliuliza Suzzane na kumfanya Edna kushangaa na kujiuliza kwanini analeta mambo ambayo hakuwa akitaka kuyakumbuka.
“Ndio nakumbuka , ila linahusiana vipi?”
“Najma na kaka yake ndio wamiliki wa ile nyumba na Mr Roma ndio alikuwa amepanga nyumbani kwao”Aliongea Suzzane na kumfanya Edna kushangaa na kuanza kuvuta picha ya siku yenyewe na baada ya kufikitia kwa sekunde alikumbuka wakati anatoka kulikuwa na mdada aliekuwa amesimama kwenye kibaraza na hakumuangalia vizuri kwanni alikuwa akijitahidi kuficha sura yake.
“Suzzane kwanini hukuniambia mapema”Aliongea Edna.
“Nisamehe Boss, sikuona haja ya kukuambia baada ya kugundua Najma ni mtu mzuri kwako”Edna alijikuta akivuta pumzi.
“Kuna taarifa nyingine Zaidi ya hio ninayohitaji kuifahamu Zaidi?”
“Ndio boss kwa uchunguzi niliofanya , niligundua Najma alikuwa na mahusiano ya karibu na Roma , licha ya kwamba wawili hao hawakuwahi kudhihirisha mahusiano yao , ila inaonekana Najma alikuwa akimpenda Roma na ndoto za kuwa na Roma zilififia baada ya wewe kufunga nae ndoa ya mkataba”Aliongea Suzzane na kumfanya Edna akae vizuri kitandani na kuanza kuwaza.
“Kwahio anachomaanisha Suzzane ni kwamba nilimwibia Najma mwanaume wake aliekuwa akimpenda na siku zote hakuwahi kunichukulia kama rafiki yake na alikuwa akitumia mbinu ya kumuweka adui karibu?”Aliwaza Edna.
Lakini Edna hakuishia kuwaza hivyo tu , alikuwa akijua Nasra alikuwa na mahusiano na Najma na urafiki wao ulikuwa mkubwa , sasa alijiuliza ilikuwaje Nasra na Najma wakampenda mwanaume mmoja , inamaana hawakuwa wakifahamu hilo au Roma ndio aliefanya wasijuane.
“Huyu mwanaume amenishinda tabia”Aliwaza tena Edna.
“Boss..”
“Ndio Suzzane kuna taarifa nyingine?”
“Ndio Boss, ni hivi Najma na Elvice walionekana kuwa Pamoja hivi karibuni na vijana wangu wameweza kunasa picha zao”
“Elvice na Najma!!”
“Ndio boss”
“Wana uhusiano wa aina gani?”
“Naendelea kufuatilia boss , ila nimefahamu Najma kaka yake ni mgonjwa na kalazwa ndani ya hospitali ya Mloganzila”Aliongea Suzzane na kumfanya Edna kushangaa kwani hakuwa akilifahamu hilo.
Suzzane alimwelezea Edna juu ya ugonjwa ambao Juma anao , lakini pia gharama za matibabu ambazo Najma alipaswa kulipia kwa ajili ya kaka yake kuendelea na matibabu.
Edna alijikuta akianza kupata picha ya kile kilichotokea , licha ya kwamba hakuwa na uhakika ila aliamini kama Najma aliweza kujifanyisha hafahamiani na Roma kwa muda , kwanini aje nyumbani ghafla tu na kukumbatiana nae mbele yake, aliamini huenda Elvice alikuwa akitumia shida za Najma kutaka kumwingiza kwenye mipango yake ovu.




SEHEMU YA 245
Siku iliofuata Edna aliamka mapema sana saa kumi na mbili za asubuhi Edna Pamoja na Suzzane walikuwa ndani ya Mbagala Rangi tatu wakiwa kwenye gari aina ya V8 na gari hio waliisimamisha mbele ya geti jekundu mtaa wa Bias Rangi tatu Tanesco.
Edna muda wote tokea anakaribia ndani ya eneo hilo , ni kama kumbukumbu za miezi iliopita zilikuwa zikimjia , licha ya kwamba siku ile hakukariri sana mazingira , lakini geti la Rangi nyekundu lililokuwa mbele yake asingeshindwa kulikumbuka.
“Boss ni hapa”Aliongea Suzzane.
“Napakumbuka Suzzane”Aliongea Edna huku akiangalia mazingira ya eneo lote na aliweza kushuhudia watu wengi waliokuwa wakitembea wakielekea kwenye shughuli zao za kila siku za kujiingizia kipato.
“Ulifuatilia gharama za matibabu?”Aliuliza Edna.
“Ndio boss na jambo zuri ni kwamba kuna mtu ambaye yupo tayari kuuza figo yake”
“Anahitaji shilingi ngapi jumla”
“Milioni mia mbili”Aliongea Suzzane huku upande wa Edna akiangalia geti la nyumba ya Najma.
“Utanisubiri kwenye gari nakuja”Aliongea Edna.
“Boss siwezi kukuacha ukaenda mwenyewe”
“Hakuna cha kunipata wewe nisubirie”Aliongea Edna huku akifungua mlango na kutoka
Na ukweli ni kwamba tokea gari yao isimame ndani ya eneo hili watu wengi waliokuwa wakipita na wale pia ambao walikuwa nje ya vibaraza vyao walikuwa wakishangaa mno , kwani ni mara chace sana kwa gari kama hio kuonekana kwenye maeneo ya uswailini kama hayo.
Sasa kitendo cha mwanamke mrembo sana kushuka kwenye hio gari kiliwashangaza na baadhi ya wanawake waliokuwa nje wakiuza mihogo lakini pia wateja waliokuwa wakinunua walimkodolea macho Edna , kwani alionekana kama vile ni Malaika.
“Nyie Mungu Fundi aisee, utazania haendi chooni vile”Aliongea baba mmoja alieshikilia kopo akipiga mswaki huku tumbo lake lenye nywele likiwa wazi na aliungwa mkono na jamaa aliekuwa akinunua mihogo.
“Wewe Baba Salehe.. ,macho kodo ,eti mungu Fyundiii, muone na mtambi wake” Mama Salehe aliekuwa akiuza vitumbua hakupenda namna Baba Salehe anavyokodolea pisi Edna.
Lakini dakika mbili mbele walishangaa Zaidi baada ya kumuona yule mwanamke akilisogelea geti la nyumba ya Najma.
Edna hakujali watu waliokuwa wanamkodolea macho , aliona ni kawaida kwani alikuwa maeneo ya uswahilini , alisogelea geti na kusukuma mlango mdogo ambao ulionekana haujafungwa kutoka ndani na kisha aliingia ndani kabisa.
Kila alivyokuwa akipiga hatua kumbukumbu zake zilianza kurudi upya kwenye kichwa chake.
“Hii ndio sehemu niliokutana na yule nyang`au”Aliwaza Edna huku akiangalia chumba alicholala na Roma kwa mara ya kwanza, Edna ni kama hakuwa akiamini amini hivi , hakuamini mara yake ya kwanza kulala na mwanaume ni ndani ya hilo eneo.
“Dada karibu”Ilisikika sauti na kumfanya Edna kugeuka nyuma.
“Asante dada.. Em.. namuulizia dada mmoja anaitwa Najma”Aliongea Edna huku akimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake na alionekana ndio alikuwa akitoka kuoga kwenye vyoo vilivyokuwa upande wa pili.
Yule mwanamke alishangaa baada ya kuona mwanamke mrembo aliekuwa mbele yake kumuulizia Najma.
Ndio kwa muonekano wa mwanamke aliekuwa mbele yake aliamini ni mtu na pesa zake na ndio maana alishangaa , kwani kila kitu kilichovaliwa na mwanamke huyo kilikuwa cha bei mbaya.
Wanasema utajiri haujifichi na ndio ambacho Edna alidhirika mbele ya mwanamke asiemfahamu.
“Naitwa Mama Debora , hali ya Najma sio nzuri tokea jana arudi hivyo hata Kwenda shuleni kwangu leo nimeshindwa ili kumsaidia”Aliongea Mama Debora huku akimpa ishara Edna kuongozana nae kuingia ndani.
Na Edna alijishauri kwa dakika kadhaa na kisha alipiga hatua kwenye ngazi zilizokuwa zikimpandisha Kwenda juu kwenye kibaraza .
“Ingia tu usivue viatu”Aliongea Mama Debo na Edna hakutaka kumsikiliza , alijiona ajishushe na alivua viatu na kisha kuingia ndani ya nyumba hii ambayo anaishi Najma .
Kusema ukweli kwa Maisha ya Edna hakuwahi kuingia kwenye nyumba za hali ya chini kama nyumba hio na hata harufu yake pia hakupendezwa nayo.
“Najma kuna mgeni wako”Aliongea Mama Debo baada ya kuingia ndani ya chumba cha Najma huku akimuacha Edna sebuleni.
“Nani?”Aliuliza Najma kivivu.
“Amka ukamuone mwenyewe”Aliongea Mama Debo na Najma kivivu alinyanyuka.
“Atakuwa Nasra , na kama ni yeye kweli namfukuza”Aliwaza Najma huku akitembea kwenye korido kuelekea upande wa Sebuleni na ile anafika alijikuta akipigwa na mshangao , kwani mtu aliekuwa hapo ndani hakumtegemea kabisa
“Edn..aaa!”
“Unashangaa kuniona nyumbani kwenu bila taarifa?”Aliongea Edna pasipo kubadili muonekano wake , licha ya kwamba alikuwa akimuonea huruma Najma lakini hakuwa amemsamehe kwa kitendo cha kumdanganya.
“Edna nao…”
“Kajiandae kuna sehemu tunapaswa Kwenda nakupa nusu saa tu”Aliongea Edna kitemi na Najma alifikiria kidogo na kisha alirudi kwa woga alikotoka kwa ajili ya kujiandaa , huku akiwa na mawazo , hakujua ni wapi ambako Edna alikuwa akitaka kumpeleka , lakini alijiambia Edna ni mtu mzuri na haawezi kumfanya kitu kibaya.
Baada ya nusu saa Najma alioga na kuva dela haraka haraka na kitambaa kichwani , haikuwa na haja kwake kujilemba na alitoka mpaka nje kwani Edna alikuwa na yeye ashatoka.
“Naamini unajiuliza nimefahamu vipi hapa unapoishi?”Aliongea Edna huku akiangalia chumba ambacho Roma alikuwa akiishi na Najma alishindwa kujibu .
“Kama kweli unampenda Roma basi nadhani huwezi kusahau miezi kadhaa iliopita.”
“Edna sio..”Aliongea Najma akitaka kujitetea lakini Edna aligeuka na kumwangalia Najma.
“Najma usiniambie hukumbuki sura yangu miez Zaidi ya mitatu iliopita nilivyotoka kwenye hiko chumba”Aliongea Edna na kumfanya Najma kutoa macho.
“Edna usiniambie..”
“Ndio ni mimi ambaye mpaka leo huenda wengi wenu hapa mnanikumbuka kwa kunidhania kahaba nilielala na Roma kwenye hiko chumba”Aliongea Edna lakini Najma aliendelea kushangaa Zaidi , lakini Edna hakutaka kuongea Zaidi ya kutembea.
“Nadhani ushajiandaa, tuondoke , nina mambo mengi ya kufanya leo”Aliongea Edna huku akipiga kutoka kabisa ndani ya nyumba hio huku Najma akifuatia nyuma.
“Dada kwaheri”Aliaga Edna.
“Karibu tena dada”Aliongea mama Debo na Edna alitingisha kichwa na kutoka.
“Mama Debora nitarudi baadae”Aliongea Najma kabla hajatoka huku akimwangalia Mama Debora.
Dakika chache mbele Najma alikuwa ndani ya gari linalonukia vizuri , lenye kiyoyozi safi , gari aina ya V8(Unaijaua vieite wewe) , Suzzane baada ya boss wake kurudi akiwa Pamoja na Najma aliondosha gari.
“Najma sitaki kujua kilichotokea kati yako na Roma na kwangu haijalishi mlikuwa na mahusiano au lah lakini pia sijali muda ambao umefahamiana na Roma, lakini kwasasa nataka uelewe kwamba Roma ni mume wangu kihalali kabisa, sitoweza kumzuia kama atakuja kwako na kutaka kuanzisha tena mahusiano na wewe, lakini ninachotaka uniahidi leo hii kama kweli ulikuwa ukinichukulia kama rafiki yako…”
“Edna naomba unisamehe….”
“Huuna haja ya kuomba msamaha Najma , nimekasirishwa sana na kitendo chako cha kunidanganya, ninachotaka uniahidi ni jambo moja tu ndio nitaangalia kama nitakusamehe”Aliongea Edna wakati gati likiendelea kuwa katika mwendo.
“Sijui kama inawezekana , lakini nataka uzipotezee hisia ulizonazo juu ya Roma , kwasababu sasa hivi ni mume wangu na sitokuwa tayari kumuona anapenda mtu mwingine Zaidi yangu”Aliongea Edna pasipo kusita na kumfanya hata Suzaane alieshikilia usukani kushangaa.
“Boss inamaana ashamkubali Roma kama mume na sio mkataba tena?”Aliwaza Suzzane.
“Najma niambie kama unaweza kufanya hivyo?”Aliongea Edna na kumfanya Najma.
“Edna sitaki kuwa muongo kwako tena , hisia nilizokuwa nazo juu ya Roma sijui nama ya kuzipotezea na huenda jambo hilo lingewezekana kwa hiari yangu ningekuwa nishafanya , jambo unaloongea kwangu haliwezekani kabisa,ninachoweza kukuahidi ni kwamba nitakaa mbali na Roma , hata kama ni Kwenda mikoani nitafanya hivyo”Aliongea Najma huku machozi yakimtirikika mfululizo , na hakujua ni kwanini alikuwa akilia , lakini moyo ulikuwa ukimuuma mno baada ya kuambiwa apotezee hisia zake , kwake kauli hio ilikuwa ni kama mtu akimwambia kuwa aachane na Roma jambo ambalo kwake halikuwa likiwezekana kabisa , kwani ni wanaume wengi aliwaacha kwa ajili ya Roma tu.
“Kwahio unamaanisha kwamba huwezi kumuacha Roma na kupotezea hisia ulizokuwa nazo juu yake?”Aliuliza Edna na Najma alikaa kimya na Edna alitafsiri kama jibu.
“Najma nikuulize swali?”Aliongea Edna na Najma alitingisha kichwa kwamba ndio.
“Kama itatokea Roma akaja kwako na akataka muanzishe mapenzi tena utamkubali?”
“Siwezi kumkataa ,… nitakubali ndio kwasababu nampenda na ndoto yangu nikuwa mume wake”Aliongea Najma na kumfanya hata Suzzane kupunguza mwendo na Edna na yeye alishangazwa na jibu hilo na kumwangalia Najma.




SEHEMU YA 246
Edna alishangazwa na jibu la Najma lakini pia namna alivyokuwa anajiamini mbele yake na moja kwa moja aliona mapenzi ya dhati Najma aliokuwa nayo juu ya Roma mume wake.
“Najma nataka mimi na wewe tuwekeane ahadi”Aliongea Edna na kumfanya Najma kushangaa , hakujua Edna alikuwa akitaka kuwekeana ahadi gani na yeye ila alitaka kuisikia kabla ya kutoa maamuzi.
“Nataka unihakikishie kama Roma hatokutafuta Maisha yako yote usije ukamtafuta tena, mimi nitahakikisha namfunga miguu Roma kama mke wake na wewe uahidi mbele yangu, Suzzane akiwa shahidi kama hutokuja kumtafuta Roma wala kumsogelea tena”
“Sijakuelewa vizuri Edna unachomaanisha”Aliongea Najma na kumfanya Edna kufungua mkoba wake.
“Huu ni mkataba nilioandika usiku wa jana , ukisoma kila kitu utaelewa”Aliongea Edna huku akimkabizi Najma karatasi.
Najma alijikuta akitetemeka mara baada ya kusoma kilichokuwa kimeandikwa kwenye hio karatasi.
Edna alikuwa ameandaa mkataba wa ahadi ambao ulikuwa ukimtaka Najma kutomtafuta Roma kwenye Maisha yake yote wala kumsogelea kwa nia ya kutaka kuwa nae kimapenzi labda tu Roma mwenyewe afanye hivyo kwa hiari yake , huku upande wa Edna na yeye akiweka ahadi ya kwamba atahakikisha Roma hamtafuti Najma kwa vyovyote vile na ikitokea Roma kumtafuta Najma kwa hiari yake basi Edna hatokuwa na pingamizi tena na mkataba wa ahadi utavunjika rasmi na Najma kuwa huru kuwa na Roma kimapenzi.
Maelezo hayo sio ambayo yalimfanya Najma kutetemeka bali maneno ya chini yake mwishoni kabisa.
“Huna haja ya kuwa hivyo Najma , naelewa kabisa kwamba wewe na Roma mlikutana wa kwanza kabla yangu , hivyo sitaki kuwa mkatili , kama utasaini huo mkataba basi utapata faida mbili kama nilivyoeleza , kwanza nitagharamia matibabu ya kaka yako mpaka kubadilishwa figo , pili utapata ‘Scolarship’ ya kwenda kusomea nje ya nchi, najua una Diploma hivyo ni rahisi kudahiliwa kwa vyuo vya nje na masomo yako yatagharamikiwa na ‘Foundation’ iliochini ya kampuni yangu, Edna Foundation’”Aliongea Edna na kuendelea.
“Lakini pia kama itatokea umevunja mkataba kwa kumtafuta Roma basi gharama zote nitakazolipia inabidi ulipe mara mbili yake kama penati ya kuvunja mkataba kisheria”
“Edna.. uko siriasis juu ya hili?”Aliuliza Najma na kumfanya Edna atingishe kichwa kuashiria ni hakika.
“Nilichoandika hapo ni sahihi kabisa , kama utatia sahihi yako inamaanisha kwamba umekubaliana na mkataba wangu na kwanzia siku ya leo utakuwa kwenye kifungo cha kutumikia ahadi yako , na kaka yako atapatiwa matibabu kama nilivyosema na utachagua chuo chochote nje ya nchi na taasisi yangu itagharamikia masomo yako mpaka utakapomaliza”Aliongea Edna.
Najma alisoma upya karatasi iliokuwa kwenye mikono yake na kuingia kwenye mawazo na hata walivyofika mbele ya hospitalini ya Mloganzila hakuweza kutambua.
“Najma tupo hospitalini , fanya maamuzi sasa hivi”Aliongea Edna na kumgutusha Najma aliekuwa kwenye mawazo na Najma aliagalia jengo hilo la hospitali na kuanza kumfikiria kaka yake ambaye yupo kitandani akiugulia maumivu.
Upande wa Edna ukweli jana yake usiku alifikiria sana , licha ya kwamba alitamani kumsaidia Najma , lakini kama mfanyabiashara alitaka anufaike pia na ndio maana alikuja na wazo la kuandaa mkataba wa Najma kuacha kabisa kumfikiria Roma ili amsaidie kaka yake kupona , lakini wakati huo huo amsaidie Najma Kwenda nje ya nchi akaendelee na masomo , na aliamini kama Najma atamaliza kwenye chuo kikubwa huko duniani basi ingekuwa rahisi kutoka kwenye umasikini na hata kumpandisha hadhi yake, hivyo mkataba alioandika sio kwa ajili ya kumnyonya bali kumsaidia.
“Edna nipo tayari”Aliongea Najma na kumfanya Edna kutabasamu.
“Umefanya vyema Najma , Suzzane licha ya kuwa msaidizi wangu , lakini pia ni mwanaseria na atashuhudia makubaliano yetu”Aliongea Edna na kisha akatoa kalamu na kumpatia Najma kutia Saini kwenye nafasi ilioachwa wazi.
“Sina cha kupoteza , Roma hawezi kunipenda tena na kunioa , hivyo bora niyafikirie Maisha yangu kwa sasa ya baadae, najua Edna anajaribu kunisaidia kwa namna ya kipekee hivyo siwezi kumuangusha tena, nitakuja kumlipa wema wake siku nitakapofanikiwa”Aliwaza Najma na kisha alitia sahihi na akampatia kalamu Edna na kusaini pia na Suzzane nae akasaini.
Maongezi kati ya dokta mkuu wa hospitali yalikuwa yashafanyika na utaratibu huo ulifanywa na Suzzane hivyo ilikuwa ni kwa ajili ya kuongea gharama tu na jopo la madaktari watakao husika na upasuaji.
Maongezi yalifanyika haraka haraka na Dokta Issay alifurahishwa na moyo mzuri wa Edna kumsaidia Juma na kumuona Najma kama mwanamke aliejaaliwa kuwa na marafiki wazuri.
“Najma unaonekana kuzaliwa na nyota kali sana , unatakiwa kujivunia ,wiki iliopita rafiki yako kakusaidia kiasi kikubwa cha pesa na leo hii pia Boss Edna hapa anakusaidia”Aliongea Dokta Issay na kumfanya Edna kushangaa lakini hakuuliza Zaidi ya kuagana na Dokta.
“Najma nafikiria unapaswa kumpigia Nasra simu , sijui nini kinachoendelea ila naamini ni rafiki mzuri kwako”Alimalizia Edna kuongea na Najma aliitikia kwa heshima , na Edna na Suzane waliingia kwenye gari na kumuacha Najma pasipo kujua kuwa Roma alikuwa akiwaangalia mita kadhaa kutoka waliposimama akiwa ndani ya gari.
*******
Roma baada ya kujua alichokifanya Edna hakuona haja ya kuendelea kubaki hapo hospitalini na hakutaka kabisa hata kuonana na Juma.
Aliondoka na kurudi kwenye kampuni ya mke wake na moja kwa moja alienda mpaka ndani ya ofisi ya Edna , alihitaji kujua ni nini kinaendelea.
Roma alimkuta Edna akiwa na baadhi ya mfanyakazi wa kampuni ambaye hakumtambua na aliacha wawili hao wamalize ndio aongee nae na mfanyakazi alionekana kupewa maelekzo na Edna yaliodumu kwa dakika kadhaa tu, na Roma aligundua mfanyakazi huyo ni moja ya viongozi wa moja ya kampuni za Edna ambazo zipo mikoani.
“Ngoja nikakutengenezee kahawa mke wangu kabla hatujaanza mazungumzo ya kina”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna aliekuwa akijifanyisha kuwa bize na kupuuza uwepo wake.
“Haina haja , sema shida iliokuleta ofisini kwangu Mr Roma”Aliongea Edna , lakini Roma hakujali alitoka ndani ya ofisi ya Edna na kumuuliza Monica ni wapi anaweza kutengeneza kahawa na Monica ambaye hakuwa akimpenda Roma alimuonyesha kwa ishara upande wa kushoto .
“Dakika chache mbele Roma alirudi ndani ya ofisi ya mke wake na kisha kuweka kikombe mbele yake”.
“Mke wangu nikupendae kwa moyo wote , naomba upokee kahawa aliotegeneza mume wako kama ishara ya kukusapoti kwakile unachokifanya kwa taifa hili”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna.
“Unaweza kusema sasa kilichokuleta”Aliongea Edna na kumfanya Roma afikirie kidogo , ukweli hakutaka kuongelea swala la kumuona Na Najma kule hospitalini kwani angeibua maswali.
“Edna nataka tuongee kilichotokea jana , sio kama unavyofikiria na sikupenda kukudanganya juu yangu na Najma , nilifanya hivyo…”
“Mr Roma, nipo kazini na naomba jambo lote ambalo utaongea ofisini kwangu liwe linahusiana na kazi tafadhari , Asante kwa kahawa na unaweza Kwenda kama huna jambo la ziada la kuongea”Aliongea Edna huku akiangalia tarakishi yake na kumfanya Roma avute pumzi.
“Alright kama hutaki tuongee tukiwa kazini basi tutaongea tukirudi nyumbani”Aliongea Roma na kisha aligeuka na kutoka ndani ya ofisini ya Edna.
Roma alienda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya Nasra , kuna mambo mawili matatu alitaka kuongea na mrembo huyo , kwani siku kadhaa nyuma hakuongea nae baada ya kujua kama Edna ni mke wake.
“Madam Nasra , Ninaweza kuingia?”Aliongea Roma baada ya kufnngua mlango na kumuona Nasra ambaye alionekana kuwa katika mawazo na Nasra aligeuza kiti na kumpa mgongo Roma.
Roma baada ya kuona hivyo , alijua mrembo huyo alikuwa na hasira na yeye hivyo aliona tiba pekee ni kumkumbatia na kumpiga busu na ndio alichofanya , lakini kwa Nasra alikuwa ni kama gogo , kwani hakutikisika.
“Bebi Nasra kama kuna shida ni bora ukaniambia kuliko kuninunia”Aliongea Roma na akageuza kiti cha Nasra na kumwangalia usoni , lakini ajabu mrembo huyo alikuwa akitoa machozi.
“Roma naomba nikuulize swali “Aliongea Nasra huku akimwangalia Roma usoni.
“Mhmh! Ongea Nasra na acha kulia maana machozi yako licha ya kukufanya uonekane mrembo lakini yananiumiza eti”Aliongea Roma huku akimfuta machozi Nasra kwa mkono.
“Nataka kujua nia yako ni ipi kuwa na mahusiano na mimi , huku ukijua Edna ni Zaidi ya ndugu yangu”Aliongea Nasra na kumfanya Roma asimama vizuri na kufikiria kidogo na mpaka hapo alijua kwanini mrembo huyo alionekana kutokuwa kwenye mudi nzuri.
“Nasra najua unaweza kuniona kama mwanaume mbinafsi na mwenye tabia mbaya, lakini kuhusu nilivyoanzisha mahusiano na wewe sikufikiria chochote zaidi ya kutaka kuwa na wewe, najua swala la Edna linaweza kuwa changamoto kwako na kukufanya uwaze , lakini nikuambie kwamba unawaza ujinga”Aliongea Roma na kumfanya Nasra amwangalie.
“Unasemaje nawaza ujinga , ilihali nimetembea na mume wa mtu”.
“Bebi Nasra unaonaje baadae nikija nyumbani kwako unipikie , nimemisi chakula chako na baada ya hapo tutaongea vizuri”Aliongea Roma.
“Siwezi kukaribisha mume wa mtu nyumbani kwangu tena , sitaki kumvunjia heshima Edna”
“Hehe.. tutaona kama unamaanisha hio baadae”Aliongea Roma na kisha alimsogelea Nasra na kumbusu shavuni na kutoka nje ya ofisi na ile anatoka kwenye korido macho kwa macho na Edna ambaye alionekana anatoka kwani alikuwa ametangulizana na Monica.



SEHEMU YA 247.
Edna alimwangalia Roma na kisha pasipo ya kuonyesha mabadiliko yoyote aliendelea na safari yake na kuingia kwenye lift na Roma alitabasamu na kisha alitembea mpaka kwenye ofisi ya Dorisi kwa ajili ya kumsalimia , lakini baada ya kufika ofisini kwake hakumkuta na aligeuza kuelekea kwenye idara anayofanyia kazi.
“Recho naona Ernest amekuwa na ukaribu mno na Benadetha?”Aliuliza Roma baada ya kufika kwenye meza ya Recho na hio ni baada ya kumuona Ernest Komwe, CEO msaidizi akiwa ndani ya ofisi ya Benadetha.
“Hehe.. unaona wivu kumuona mwanaume mwenzio akiongea na mrembo Benadetha?”
“Wewe nae na kakichwa kako kadogo , mimi nimeuliza na unaniuliza”Aliongea Roma na kumfanya Recho kumkagua Roma kwanzia juu mpaka chini ni kama kuna kitu anachokitafuta.
“Roma hivi wewe na Boss ni ndugu?”Aliuliza Recho na kumfanya hata Tina aliekuwa bize ainue macho yake na kumwangalia Roma.
“Kwanini unauliza hivo?”
“Unafikiri ni kawaida , kila mfanyakazi ndani ya hii kampuni anajiuliza swali la aina hio, umekuja si chini ya miezi mitatu , lakini sasa hivi mwenzetu ni Director , lakini mbaya Zaidi mnaonekana kuwa Pamoja”
“Sisi! , unaamaanisha mimi na Edna tunaoneka kuwa pamoja?”
“Ndio usichoelewa nini, mlienda Ufaransa Pamoja , lakini pia kwenye kusanyiko ile siku mlikuja Pamoja , tuna maswali ya kujua , si ndio Tina”
“Ndio Roma , tunataka utuambie ukweli leo , kama mna mahusiano tujue na kama hauna mahusiano nae utueleze mganga wako ni nani na sisi tukapate tiba”Aliongea Tina msambaa na kumfanya hata Roma kutamani kucheka na kushindwa kujua ajibu ni na aliishia kukuna kichwa.
******
Mheshimiwa Senga na Raisi mstaafu Kigombola walifikia kwenye makubaliano ya Yan Buwena kuendeleza tafiti za Marehemu Profesa Shelukindo , Raisi senga aliona hana haja ya kumzuia Mtangulizi wake katika hilo, lakini hakuacha kumpa tahadhadri ya kwamba Yan Buwen akifanya chochote ambacho kitafanya usalama wa raia kuwa hatarini basi hatovumilia juu ya hilo na mara moja Yan Buwen atakamatwa na vyombo vya sheria na Mheshimiwa Kigombola alimhakikishia Senga kwamba hakuna lolote ambalo linaweza kutokea na atakuwa karibu Zaidi na Yan Buwen.
Baada ya mheshimiwa raisi Senga kufanya kazi kwa muda mrefu mpaka muda wa chakula cha mchana , aliweza kupata smu kutoka kwa Senior.
“Ndio Senior”
“Senga nategemea kufanya ziara kwenye taifa lako ya siku mbili”Aliongea Senioit na kumfanya Senga kutabasamu.
“Nijambo jema kama utakuja Tanzania nadhani tutapata wasaa wa kuongea juu ya mipango yetu”
“Haswaa , hilo ndio linanifanya kuja Dar Es Salaam , nataka kumuona Edna pia Pamoja na mkwe wangu Roma”Aliongea na Senga alijikuta akibadili muonekano wake na ukawa usioelezeka anawaza nini.
“Senga najua unachofikiriria , ila tutaongea nikifika nchini Tanzania”
“Sawa Senior karibu sana , lakini bado hujanieleza mpango wako ni upi au unawaza kumuweka Edna wazi?”
“Hapana Senga , nataka unisaidie jambo moja kabla sijafanya safari yangu ya kuja Tanzania , nahitaji kuonana na wafanyanishara wakubwa ninaamini hio ni nafasi ya mimi kuonana na Edna”Aliongea Senior na kumfanya Senga afikirie kidogo.
“Okey Rafiki yangu , nadhani hilo linawezekana kabisa , nitawapa kazi wasaidizi wangu”
“Nitashukuru sana Senga , safari hii nitakuja kukuweka wazi mambo ambayo sikukueleza mapema , ili kuimarisha Zaidi uhusiano wetu lakini pia mipango yetu kwa maslahi mapana ya umoja wetu kitaifa”
“Ahsante Senior nategemea makubwa kutoka kwako”
“Haha.. sawa Senga nikutakie kazi njema”
“Ahsante Sana na wewe pia”Aliongea Senga na kukata simu.
“Ana mambo gani Senior anataka kuniambia au na yeye ni walewale wa kunificha , nakiri kwa sasa sina mtu wa kumuamini kabisa , napaswa kusimama mwenyewe, mwisho wa mwezi huu lazima niendele kwenye ibada ya mpasuko wa mwezi ili nijue namna ya kuongoza hili taifa na kudili na kila mmoja ambaye simuamini”Aliwaza Mheshimiwa senga.
“Mheshimiwa!!”Sauti ilimwita Mheshimiwa Senga aliekuwa kwenye mwazo na kuangalia mtu aliekuwa mbele yake, alikuwa ni Kabwe msaidizi wake.
“Nimeweza kufanya mawasiliano na Denisi na kumpatia ujumbe wa kurudi nyumbani haraka”Aliongea Kabwe.
“Shukrani Kabwe , unaweza Kwenda kama hakuna lingine muhimu”Aliongea mheshimiwa na kumfanya Kabwe kugeuka na kuondoka.
Senga licha ya kuonekana vyema kwa muonekano wa nje ila kwa ndani alikuwa akiungua , mke wake Damasi alikuwa amemchunia kutokana na Denisi kuwadanganya na Damasi alielekeza lawama zote kwake na aliona mke wake ana haki ya kumlaumu kwani siku zote alikuwa ni mwenye kufikiria uongozi pasipo kujali familia yake na matokeo yake Denisi anaamua kufanya kile anachoepnda pasipo ya yeye kuelewa.
Senga alikaa kwa dakika kadhaa na kisha alichukua simu yake na kupiga namba ambayo ilionekana kuwa ya nje ya nchi.
“Hello Dady”
“Hello My Daughter, unaendeleaje”
“Niko salama Dady how are you and mom?”
“We are fine my daughter, unarudi lini nyumbani?”
“Dady kuna tatizo…”
“Hapana tumekumiss mimi na mama yako”
“Ooh nikajua kuna tatizo , hujawahi kunipigia na kuniulizia narudi lini nyumbani baba, I real miss you and Mom too”Aliongea Ashley mtoto mkubwa wa Raisi Senga ambaye alikuwa ni mwanasayansi anaefanya kazi na Profesa Clark Stephanie.
“By the way Dady , how is Roma doing , do you keep in touch with him?”Aliuliza Ashley na kumfanya Senga kushangaa kidogo na moyo wake Kwenda kasi.
“ I don’t ,Why!, Unafahamiana na Roma?”Aliuliza Senga kwa sauti lakini hakukuwa na jibu upande wa pili na alishusha simu na kuangalia kama simu imekatwa , lakini aligundua bado ipo hewani.
“Ashley nimekuuliza swali”
“Dadii, Calm down , I was just asking if you are keeping in touch with him , you should if not dady, I know he is…”
“Baba,Punguza presha , nilikuwa na nauliza tu kama unawasiliana nae, unapaswa kufanya hivyo kama bado, najua yeye ni..”
“He is what Ashley , niambie umegundua nini?”
“Dady am sorry I Should have told you this soon , but I was worried and nor sure at the same time”
“Baba unisamehe , nilitakuwa kukueleza hili mapema , lakininilikuwa na wasiwasi na kutokuwa na uhakika kwa wakati mmoja”
Aliongea Ashley na kumfanya Senga kuvuta pumzi , kuna kitu amekingundua kwenye sauti ya Ashley.
“Niambei ni kipi unachotaka kunieleza, kinachokufanya kuwa na wasiwasi na kutokuwa na uhakika nacho kwa wakati mmoja Ashley”
“Nilifahamiana na Roma tokea naanza masomo yangu ya digrii, nilikutana nae Uingereza dady, I kept the truth hiden even when he was before you and mom, Dady forgive me, I had to pretend for some reason”Aliongea Ashley na kumfanya Senga kuvuta kidogo pumzi apate kupumua vizuri maana aliona ni mwendelezo wa maigizo kwa kila mtu anaemzunguka na aliwaza sijui na mke wake kuna jambo gani hajamwambia bado maana ndio kabakia.
“Ashley kuna mahusiano yoyote kati yako na Roma ?”Aliuliza Raisi Senga kwa wasiwasi.
“Dadiii…”
“Tell me everything Ashley”
“ Yes Dady,, we have been so far…”Aliongea Ashley na kumfanya Senga asiamini masikio yake na aliomba kile anachofikiria kisiwe sahihi.
“Dady sio kama unavyofikiria , I mean… I know he was my brother”Alimalizia Ashley.
“What..!! , You knew this even you”
“Dady I am so sorry , I know it`s not right for us to talk this over the phone , but I had the reasons, forced not to say anything when I Confirmed he was real my brother”
“Baba naomba unisamehe ,najua sio sahihi kuongelea kwenye simu , lakini nilikuwa na sababu , nililazimishwa kutoongea chochote , nilipothibitisha kama kweli ni kaka yangu”
“Ulilazimishwa nani mpaka ukashindwa kuniambia mimi na mama yako , kwanini kila mtu anafanya anavyotaka na hamnipi heshima yangu kama baba yanu”Aliongea Raisi Senga kwa hasira.
“Grandpa ndio alieniambia kwamba nisiongee chochote mpaka muda sahihi utakapofika”Aliongea Ashley na kumfanya Senga akose nguvu na alitamani apae akamtangwe risasi baba yake mzazi , kwani aliona michezo anayomfanyia imemzidi kimo.
“Huyu mzee kwanini ananizidi akili kwa kila kitu ninachokifanya , mimi ni nani kwenye Maisha yake mpaka kunifanyia mchezo mpaka na Watoto wangu”Aliwaza Senga kwa hasira huku akipangua mafaili yaliokuwa mezani na kumfanya katibu muhtasi wake kuingia baada ya kusikia vitu kudondoka.
*******
Ni muda wa saa kumi na mbili za jioni Edna alionekana akiwa ndani ya chumba chake akipangilia baadhi ya vitu vyake muhimu ambavyo alitoka navyo Kigamboni.
Wakati ekiendelea kuwa bize akipembua kitu kimoja kimoja na kukiweka katika sehemu husika , mlango wa chumbani kwake ulifunguliwa na alionekana mrembo Mage akiingia ndani ya chumba hiko.
“Edna..!”Aliita Mage na kumfanya Edna aliekuwa akipanga vitu kwenye kabati kubwa kugeuka nyuma na baada ya kugundua ni Mage alimsogelea na kumkumbatia.
“Edna nimekumisije jamani , nilivyosikia mmerudi Osterbay nimekuja mbio mbio huku kabla hata sijatulia”Aliongea Mage na Edna alitabasamu.
“Ndio tumehamia huku kwenye nyumba kubwa , karibu sana”Aliongea Edna huku Mage akiketi kwenye kitanda kikubwa cha Edna.
“Usiniambie hio nayo ni staili siku hizi”aliongea Edna huku akimwangalia Mage kichwani , Edna licha ya kumzoea Mage siku zote kutokuwa na nywele ndefu , lakini hakuzoea kumuona na kipara.
“Nilikuwa jeshini”Aliongea Mage na kumfanya Edna kushangaa
“Jeshini!, uliacha Upolisi?”
“Nilitaka kuacha ila nimeghairi , mafunzo ya jeshi yamenishinda na kukimbia”Aliongea Mage huku akidanganya , kwani ukweli ni kwamba tokea aonjeshwe utamu na Roma hakuweza kuvumilia kubaki jeshini, alitamani kurudi ili amuone Roma , lakini pia hata Roma mwenyewe alikuwa ashamwambia aachane na jeshi , hivyo alijiambia yeye ni nani hata akatae kile ambacho bebi wake amesema.
“Hahaha.. nilijua upo ngangari kama Magdalena , kumbe mtoto soft”Aliongea Edna na kumfanya Mage kucheka.
“Hiki chumba kinanikumbusha tulivyokuwa wadogo , hakina mabadiliko makubwa”Aliongea Mage na kumfanya Edna kutabasamu.
“Kimejaa kumbukumbu nyingi sana za utoto wangu”Aliongea Edna huku Mage akiendelea kuangalia , lakini macho ya Mage yalivutiwa na karatasi iliokuwa karibu yake na aliichukua na kuishikilia mkononi huku Edna akimpa mgongo.
“MARRIGE CONTRACT” neno mkataba wa ndoa ndio ambalo lilimvutia sana Mage..
“Edna huu….. mkataba usiniambie ni wa kweli?”Aliongea Mage kwa mshangao mkubwa , ni kama kitu kilichokuwa kwenye mikono yake ni feki.
Edna aligeuka haraka haraka huku akijilaumu kusahau kuhifadhi karatasi za mkataba wa ndoa yake na Roma kwenye kabati.
Edna alimwangalia Mage alieshikilia karatasi na kushindwa hata ajibu nini kwani siri yake imefichuka.
 
SEHEMU YA 246
Edna alishangazwa na jibu la Najma lakini pia namna alivyokuwa anajiamini mbele yake na moja kwa moja aliona mapenzi ya dhati Najma aliokuwa nayo juu ya Roma mume wake.
“Najma nataka mimi na wewe tuwekeane ahadi”Aliongea Edna na kumfanya Najma kushangaa , hakujua Edna alikuwa akitaka kuwekeana ahadi gani na yeye ila alitaka kuisikia kabla ya kutoa maamuzi.
“Nataka unihakikishie kama Roma hatokutafuta Maisha yako yote usije ukamtafuta tena, mimi nitahakikisha namfunga miguu Roma kama mke wake na wewe uahidi mbele yangu, Suzzane akiwa shahidi kama hutokuja kumtafuta Roma wala kumsogelea tena”
“Sijakuelewa vizuri Edna unachomaanisha”Aliongea Najma na kumfanya Edna kufungua mkoba wake.
“Huu ni mkataba nilioandika usiku wa jana , ukisoma kila kitu utaelewa”Aliongea Edna huku akimkabizi Najma karatasi.
Najma alijikuta akitetemeka mara baada ya kusoma kilichokuwa kimeandikwa kwenye hio karatasi.
Edna alikuwa ameandaa mkataba wa ahadi ambao ulikuwa ukimtaka Najma kutomtafuta Roma kwenye Maisha yake yote wala kumsogelea kwa nia ya kutaka kuwa nae kimapenzi labda tu Roma mwenyewe afanye hivyo kwa hiari yake , huku upande wa Edna na yeye akiweka ahadi ya kwamba atahakikisha Roma hamtafuti Najma kwa vyovyote vile na ikitokea Roma kumtafuta Najma kwa hiari yake basi Edna hatokuwa na pingamizi tena na mkataba wa ahadi utavunjika rasmi na Najma kuwa huru kuwa na Roma kimapenzi.
Maelezo hayo sio ambayo yalimfanya Najma kutetemeka bali maneno ya chini yake mwishoni kabisa.
“Huna haja ya kuwa hivyo Najma , naelewa kabisa kwamba wewe na Roma mlikutana wa kwanza kabla yangu , hivyo sitaki kuwa mkatili , kama utasaini huo mkataba basi utapata faida mbili kama nilivyoeleza , kwanza nitagharamia matibabu ya kaka yako mpaka kubadilishwa figo , pili utapata ‘Scolarship’ ya kwenda kusomea nje ya nchi, najua una Diploma hivyo ni rahisi kudahiliwa kwa vyuo vya nje na masomo yako yatagharamikiwa na ‘Foundation’ iliochini ya kampuni yangu, Edna Foundation’”Aliongea Edna na kuendelea.
“Lakini pia kama itatokea umevunja mkataba kwa kumtafuta Roma basi gharama zote nitakazolipia inabidi ulipe mara mbili yake kama penati ya kuvunja mkataba kisheria”
“Edna.. uko siriasis juu ya hili?”Aliuliza Najma na kumfanya Edna atingishe kichwa kuashiria ni hakika.
“Nilichoandika hapo ni sahihi kabisa , kama utatia sahihi yako inamaanisha kwamba umekubaliana na mkataba wangu na kwanzia siku ya leo utakuwa kwenye kifungo cha kutumikia ahadi yako , na kaka yako atapatiwa matibabu kama nilivyosema na utachagua chuo chochote nje ya nchi na taasisi yangu itagharamikia masomo yako mpaka utakapomaliza”Aliongea Edna.
Najma alisoma upya karatasi iliokuwa kwenye mikono yake na kuingia kwenye mawazo na hata walivyofika mbele ya hospitalini ya Mloganzila hakuweza kutambua.
“Najma tupo hospitalini , fanya maamuzi sasa hivi”Aliongea Edna na kumgutusha Najma aliekuwa kwenye mawazo na Najma aliagalia jengo hilo la hospitali na kuanza kumfikiria kaka yake ambaye yupo kitandani akiugulia maumivu.
Upande wa Edna ukweli jana yake usiku alifikiria sana , licha ya kwamba alitamani kumsaidia Najma , lakini kama mfanyabiashara alitaka anufaike pia na ndio maana alikuja na wazo la kuandaa mkataba wa Najma kuacha kabisa kumfikiria Roma ili amsaidie kaka yake kupona , lakini wakati huo huo amsaidie Najma Kwenda nje ya nchi akaendelee na masomo , na aliamini kama Najma atamaliza kwenye chuo kikubwa huko duniani basi ingekuwa rahisi kutoka kwenye umasikini na hata kumpandisha hadhi yake, hivyo mkataba alioandika sio kwa ajili ya kumnyonya bali kumsaidia.
“Edna nipo tayari”Aliongea Najma na kumfanya Edna kutabasamu.
“Umefanya vyema Najma , Suzzane licha ya kuwa msaidizi wangu , lakini pia ni mwanaseria na atashuhudia makubaliano yetu”Aliongea Edna na kisha akatoa kalamu na kumpatia Najma kutia Saini kwenye nafasi ilioachwa wazi.
“Sina cha kupoteza , Roma hawezi kunipenda tena na kunioa , hivyo bora niyafikirie Maisha yangu kwa sasa ya baadae, najua Edna anajaribu kunisaidia kwa namna ya kipekee hivyo siwezi kumuangusha tena, nitakuja kumlipa wema wake siku nitakapofanikiwa”Aliwaza Najma na kisha alitia sahihi na akampatia kalamu Edna na kusaini pia na Suzzane nae akasaini.
Maongezi kati ya dokta mkuu wa hospitali yalikuwa yashafanyika na utaratibu huo ulifanywa na Suzzane hivyo ilikuwa ni kwa ajili ya kuongea gharama tu na jopo la madaktari watakao husika na upasuaji.
Maongezi yalifanyika haraka haraka na Dokta Issay alifurahishwa na moyo mzuri wa Edna kumsaidia Juma na kumuona Najma kama mwanamke aliejaaliwa kuwa na marafiki wazuri.
“Najma unaonekana kuzaliwa na nyota kali sana , unatakiwa kujivunia ,wiki iliopita rafiki yako kakusaidia kiasi kikubwa cha pesa na leo hii pia Boss Edna hapa anakusaidia”Aliongea Dokta Issay na kumfanya Edna kushangaa lakini hakuuliza Zaidi ya kuagana na Dokta.
“Najma nafikiria unapaswa kumpigia Nasra simu , sijui nini kinachoendelea ila naamini ni rafiki mzuri kwako”Alimalizia Edna kuongea na Najma aliitikia kwa heshima , na Edna na Suzane waliingia kwenye gari na kumuacha Najma pasipo kujua kuwa Roma alikuwa akiwaangalia mita kadhaa kutoka waliposimama akiwa ndani ya gari.
*******
Roma baada ya kujua alichokifanya Edna hakuona haja ya kuendelea kubaki hapo hospitalini na hakutaka kabisa hata kuonana na Juma.
Aliondoka na kurudi kwenye kampuni ya mke wake na moja kwa moja alienda mpaka ndani ya ofisi ya Edna , alihitaji kujua ni nini kinaendelea.
Roma alimkuta Edna akiwa na baadhi ya mfanyakazi wa kampuni ambaye hakumtambua na aliacha wawili hao wamalize ndio aongee nae na mfanyakazi alionekana kupewa maelekzo na Edna yaliodumu kwa dakika kadhaa tu, na Roma aligundua mfanyakazi huyo ni moja ya viongozi wa moja ya kampuni za Edna ambazo zipo mikoani.
“Ngoja nikakutengenezee kahawa mke wangu kabla hatujaanza mazungumzo ya kina”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna aliekuwa akijifanyisha kuwa bize na kupuuza uwepo wake.
“Haina haja , sema shida iliokuleta ofisini kwangu Mr Roma”Aliongea Edna , lakini Roma hakujali alitoka ndani ya ofisi ya Edna na kumuuliza Monica ni wapi anaweza kutengeneza kahawa na Monica ambaye hakuwa akimpenda Roma alimuonyesha kwa ishara upande wa kushoto .
“Dakika chache mbele Roma alirudi ndani ya ofisi ya mke wake na kisha kuweka kikombe mbele yake”.
“Mke wangu nikupendae kwa moyo wote , naomba upokee kahawa aliotegeneza mume wako kama ishara ya kukusapoti kwakile unachokifanya kwa taifa hili”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna.
“Unaweza kusema sasa kilichokuleta”Aliongea Edna na kumfanya Roma afikirie kidogo , ukweli hakutaka kuongelea swala la kumuona Na Najma kule hospitalini kwani angeibua maswali.
“Edna nataka tuongee kilichotokea jana , sio kama unavyofikiria na sikupenda kukudanganya juu yangu na Najma , nilifanya hivyo…”
“Mr Roma, nipo kazini na naomba jambo lote ambalo utaongea ofisini kwangu liwe linahusiana na kazi tafadhari , Asante kwa kahawa na unaweza Kwenda kama huna jambo la ziada la kuongea”Aliongea Edna huku akiangalia tarakishi yake na kumfanya Roma avute pumzi.
“Alright kama hutaki tuongee tukiwa kazini basi tutaongea tukirudi nyumbani”Aliongea Roma na kisha aligeuka na kutoka ndani ya ofisini ya Edna.
Roma alienda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya Nasra , kuna mambo mawili matatu alitaka kuongea na mrembo huyo , kwani siku kadhaa nyuma hakuongea nae baada ya kujua kama Edna ni mke wake.
“Madam Nasra , Ninaweza kuingia?”Aliongea Roma baada ya kufnngua mlango na kumuona Nasra ambaye alionekana kuwa katika mawazo na Nasra aligeuza kiti na kumpa mgongo Roma.
Roma baada ya kuona hivyo , alijua mrembo huyo alikuwa na hasira na yeye hivyo aliona tiba pekee ni kumkumbatia na kumpiga busu na ndio alichofanya , lakini kwa Nasra alikuwa ni kama gogo , kwani hakutikisika.
“Bebi Nasra kama kuna shida ni bora ukaniambia kuliko kuninunia”Aliongea Roma na akageuza kiti cha Nasra na kumwangalia usoni , lakini ajabu mrembo huyo alikuwa akitoa machozi.
“Roma naomba nikuulize swali “Aliongea Nasra huku akimwangalia Roma usoni.
“Mhmh! Ongea Nasra na acha kulia maana machozi yako licha ya kukufanya uonekane mrembo lakini yananiumiza eti”Aliongea Roma huku akimfuta machozi Nasra kwa mkono.
“Nataka kujua nia yako ni ipi kuwa na mahusiano na mimi , huku ukijua Edna ni Zaidi ya ndugu yangu”Aliongea Nasra na kumfanya Roma asimama vizuri na kufikiria kidogo na mpaka hapo alijua kwanini mrembo huyo alionekana kutokuwa kwenye mudi nzuri.
“Nasra najua unaweza kuniona kama mwanaume mbinafsi na mwenye tabia mbaya, lakini kuhusu nilivyoanzisha mahusiano na wewe sikufikiria chochote zaidi ya kutaka kuwa na wewe, najua swala la Edna linaweza kuwa changamoto kwako na kukufanya uwaze , lakini nikuambie kwamba unawaza ujinga”Aliongea Roma na kumfanya Nasra amwangalie.
“Unasemaje nawaza ujinga , ilihali nimetembea na mume wa mtu”.
“Bebi Nasra unaonaje baadae nikija nyumbani kwako unipikie , nimemisi chakula chako na baada ya hapo tutaongea vizuri”Aliongea Roma.
“Siwezi kukaribisha mume wa mtu nyumbani kwangu tena , sitaki kumvunjia heshima Edna”
“Hehe.. tutaona kama unamaanisha hio baadae”Aliongea Roma na kisha alimsogelea Nasra na kumbusu shavuni na kutoka nje ya ofisi na ile anatoka kwenye korido macho kwa macho na Edna ambaye alionekana anatoka kwani alikuwa ametangulizana na Monica.



SEHEMU YA 247.
Edna alimwangalia Roma na kisha pasipo ya kuonyesha mabadiliko yoyote aliendelea na safari yake na kuingia kwenye lift na Roma alitabasamu na kisha alitembea mpaka kwenye ofisi ya Dorisi kwa ajili ya kumsalimia , lakini baada ya kufika ofisini kwake hakumkuta na aligeuza kuelekea kwenye idara anayofanyia kazi.
“Recho naona Ernest amekuwa na ukaribu mno na Benadetha?”Aliuliza Roma baada ya kufika kwenye meza ya Recho na hio ni baada ya kumuona Ernest Komwe, CEO msaidizi akiwa ndani ya ofisi ya Benadetha.
“Hehe.. unaona wivu kumuona mwanaume mwenzio akiongea na mrembo Benadetha?”
“Wewe nae na kakichwa kako kadogo , mimi nimeuliza na unaniuliza”Aliongea Roma na kumfanya Recho kumkagua Roma kwanzia juu mpaka chini ni kama kuna kitu anachokitafuta.
“Roma hivi wewe na Boss ni ndugu?”Aliuliza Recho na kumfanya hata Tina aliekuwa bize ainue macho yake na kumwangalia Roma.
“Kwanini unauliza hivo?”
“Unafikiri ni kawaida , kila mfanyakazi ndani ya hii kampuni anajiuliza swali la aina hio, umekuja si chini ya miezi mitatu , lakini sasa hivi mwenzetu ni Director , lakini mbaya Zaidi mnaonekana kuwa Pamoja”
“Sisi! , unaamaanisha mimi na Edna tunaoneka kuwa pamoja?”
“Ndio usichoelewa nini, mlienda Ufaransa Pamoja , lakini pia kwenye kusanyiko ile siku mlikuja Pamoja , tuna maswali ya kujua , si ndio Tina”
“Ndio Roma , tunataka utuambie ukweli leo , kama mna mahusiano tujue na kama hauna mahusiano nae utueleze mganga wako ni nani na sisi tukapate tiba”Aliongea Tina msambaa na kumfanya hata Roma kutamani kucheka na kushindwa kujua ajibu ni na aliishia kukuna kichwa.
******
Mheshimiwa Senga na Raisi mstaafu Kigombola walifikia kwenye makubaliano ya Yan Buwena kuendeleza tafiti za Marehemu Profesa Shelukindo , Raisi senga aliona hana haja ya kumzuia Mtangulizi wake katika hilo, lakini hakuacha kumpa tahadhadri ya kwamba Yan Buwen akifanya chochote ambacho kitafanya usalama wa raia kuwa hatarini basi hatovumilia juu ya hilo na mara moja Yan Buwen atakamatwa na vyombo vya sheria na Mheshimiwa Kigombola alimhakikishia Senga kwamba hakuna lolote ambalo linaweza kutokea na atakuwa karibu Zaidi na Yan Buwen.
Baada ya mheshimiwa raisi Senga kufanya kazi kwa muda mrefu mpaka muda wa chakula cha mchana , aliweza kupata smu kutoka kwa Senior.
“Ndio Senior”
“Senga nategemea kufanya ziara kwenye taifa lako ya siku mbili”Aliongea Senioit na kumfanya Senga kutabasamu.
“Nijambo jema kama utakuja Tanzania nadhani tutapata wasaa wa kuongea juu ya mipango yetu”
“Haswaa , hilo ndio linanifanya kuja Dar Es Salaam , nataka kumuona Edna pia Pamoja na mkwe wangu Roma”Aliongea na Senga alijikuta akibadili muonekano wake na ukawa usioelezeka anawaza nini.
“Senga najua unachofikiriria , ila tutaongea nikifika nchini Tanzania”
“Sawa Senior karibu sana , lakini bado hujanieleza mpango wako ni upi au unawaza kumuweka Edna wazi?”
“Hapana Senga , nataka unisaidie jambo moja kabla sijafanya safari yangu ya kuja Tanzania , nahitaji kuonana na wafanyanishara wakubwa ninaamini hio ni nafasi ya mimi kuonana na Edna”Aliongea Senior na kumfanya Senga afikirie kidogo.
“Okey Rafiki yangu , nadhani hilo linawezekana kabisa , nitawapa kazi wasaidizi wangu”
“Nitashukuru sana Senga , safari hii nitakuja kukuweka wazi mambo ambayo sikukueleza mapema , ili kuimarisha Zaidi uhusiano wetu lakini pia mipango yetu kwa maslahi mapana ya umoja wetu kitaifa”
“Ahsante Senior nategemea makubwa kutoka kwako”
“Haha.. sawa Senga nikutakie kazi njema”
“Ahsante Sana na wewe pia”Aliongea Senga na kukata simu.
“Ana mambo gani Senior anataka kuniambia au na yeye ni walewale wa kunificha , nakiri kwa sasa sina mtu wa kumuamini kabisa , napaswa kusimama mwenyewe, mwisho wa mwezi huu lazima niendele kwenye ibada ya mpasuko wa mwezi ili nijue namna ya kuongoza hili taifa na kudili na kila mmoja ambaye simuamini”Aliwaza Mheshimiwa senga.
“Mheshimiwa!!”Sauti ilimwita Mheshimiwa Senga aliekuwa kwenye mwazo na kuangalia mtu aliekuwa mbele yake, alikuwa ni Kabwe msaidizi wake.
“Nimeweza kufanya mawasiliano na Denisi na kumpatia ujumbe wa kurudi nyumbani haraka”Aliongea Kabwe.
“Shukrani Kabwe , unaweza Kwenda kama hakuna lingine muhimu”Aliongea mheshimiwa na kumfanya Kabwe kugeuka na kuondoka.
Senga licha ya kuonekana vyema kwa muonekano wa nje ila kwa ndani alikuwa akiungua , mke wake Damasi alikuwa amemchunia kutokana na Denisi kuwadanganya na Damasi alielekeza lawama zote kwake na aliona mke wake ana haki ya kumlaumu kwani siku zote alikuwa ni mwenye kufikiria uongozi pasipo kujali familia yake na matokeo yake Denisi anaamua kufanya kile anachoepnda pasipo ya yeye kuelewa.
Senga alikaa kwa dakika kadhaa na kisha alichukua simu yake na kupiga namba ambayo ilionekana kuwa ya nje ya nchi.
“Hello Dady”
“Hello My Daughter, unaendeleaje”
“Niko salama Dady how are you and mom?”
“We are fine my daughter, unarudi lini nyumbani?”
“Dady kuna tatizo…”
“Hapana tumekumiss mimi na mama yako”
“Ooh nikajua kuna tatizo , hujawahi kunipigia na kuniulizia narudi lini nyumbani baba, I real miss you and Mom too”Aliongea Ashley mtoto mkubwa wa Raisi Senga ambaye alikuwa ni mwanasayansi anaefanya kazi na Profesa Clark Stephanie.
“By the way Dady , how is Roma doing , do you keep in touch with him?”Aliuliza Ashley na kumfanya Senga kushangaa kidogo na moyo wake Kwenda kasi.
“ I don’t ,Why!, Unafahamiana na Roma?”Aliuliza Senga kwa sauti lakini hakukuwa na jibu upande wa pili na alishusha simu na kuangalia kama simu imekatwa , lakini aligundua bado ipo hewani.
“Ashley nimekuuliza swali”
“Dadii, Calm down , I was just asking if you are keeping in touch with him , you should if not dady, I know he is…”
“Baba,Punguza presha , nilikuwa na nauliza tu kama unawasiliana nae, unapaswa kufanya hivyo kama bado, najua yeye ni..”
“He is what Ashley , niambie umegundua nini?”
“Dady am sorry I Should have told you this soon , but I was worried and nor sure at the same time”
“Baba unisamehe , nilitakuwa kukueleza hili mapema , lakininilikuwa na wasiwasi na kutokuwa na uhakika kwa wakati mmoja”
Aliongea Ashley na kumfanya Senga kuvuta pumzi , kuna kitu amekingundua kwenye sauti ya Ashley.
“Niambei ni kipi unachotaka kunieleza, kinachokufanya kuwa na wasiwasi na kutokuwa na uhakika nacho kwa wakati mmoja Ashley”
“Nilifahamiana na Roma tokea naanza masomo yangu ya digrii, nilikutana nae Uingereza dady, I kept the truth hiden even when he was before you and mom, Dady forgive me, I had to pretend for some reason”Aliongea Ashley na kumfanya Senga kuvuta kidogo pumzi apate kupumua vizuri maana aliona ni mwendelezo wa maigizo kwa kila mtu anaemzunguka na aliwaza sijui na mke wake kuna jambo gani hajamwambia bado maana ndio kabakia.
“Ashley kuna mahusiano yoyote kati yako na Roma ?”Aliuliza Raisi Senga kwa wasiwasi.
“Dadiii…”
“Tell me everything Ashley”
“ Yes Dady,, we have been so far…”Aliongea Ashley na kumfanya Senga asiamini masikio yake na aliomba kile anachofikiria kisiwe sahihi.
“Dady sio kama unavyofikiria , I mean… I know he was my brother”Alimalizia Ashley.
“What..!! , You knew this even you”
“Dady I am so sorry , I know it`s not right for us to talk this over the phone , but I had the reasons, forced not to say anything when I Confirmed he was real my brother”
“Baba naomba unisamehe ,najua sio sahihi kuongelea kwenye simu , lakini nilikuwa na sababu , nililazimishwa kutoongea chochote , nilipothibitisha kama kweli ni kaka yangu”
“Ulilazimishwa nani mpaka ukashindwa kuniambia mimi na mama yako , kwanini kila mtu anafanya anavyotaka na hamnipi heshima yangu kama baba yanu”Aliongea Raisi Senga kwa hasira.
“Grandpa ndio alieniambia kwamba nisiongee chochote mpaka muda sahihi utakapofika”Aliongea Ashley na kumfanya Senga akose nguvu na alitamani apae akamtangwe risasi baba yake mzazi , kwani aliona michezo anayomfanyia imemzidi kimo.
“Huyu mzee kwanini ananizidi akili kwa kila kitu ninachokifanya , mimi ni nani kwenye Maisha yake mpaka kunifanyia mchezo mpaka na Watoto wangu”Aliwaza Senga kwa hasira huku akipangua mafaili yaliokuwa mezani na kumfanya katibu muhtasi wake kuingia baada ya kusikia vitu kudondoka.
*******
Ni muda wa saa kumi na mbili za jioni Edna alionekana akiwa ndani ya chumba chake akipangilia baadhi ya vitu vyake muhimu ambavyo alitoka navyo Kigamboni.
Wakati ekiendelea kuwa bize akipembua kitu kimoja kimoja na kukiweka katika sehemu husika , mlango wa chumbani kwake ulifunguliwa na alionekana mrembo Mage akiingia ndani ya chumba hiko.
“Edna..!”Aliita Mage na kumfanya Edna aliekuwa akipanga vitu kwenye kabati kubwa kugeuka nyuma na baada ya kugundua ni Mage alimsogelea na kumkumbatia.
“Edna nimekumisije jamani , nilivyosikia mmerudi Osterbay nimekuja mbio mbio huku kabla hata sijatulia”Aliongea Mage na Edna alitabasamu.
“Ndio tumehamia huku kwenye nyumba kubwa , karibu sana”Aliongea Edna huku Mage akiketi kwenye kitanda kikubwa cha Edna.
“Usiniambie hio nayo ni staili siku hizi”aliongea Edna huku akimwangalia Mage kichwani , Edna licha ya kumzoea Mage siku zote kutokuwa na nywele ndefu , lakini hakuzoea kumuona na kipara.
“Nilikuwa jeshini”Aliongea Mage na kumfanya Edna kushangaa
“Jeshini!, uliacha Upolisi?”
“Nilitaka kuacha ila nimeghairi , mafunzo ya jeshi yamenishinda na kukimbia”Aliongea Mage huku akidanganya , kwani ukweli ni kwamba tokea aonjeshwe utamu na Roma hakuweza kuvumilia kubaki jeshini, alitamani kurudi ili amuone Roma , lakini pia hata Roma mwenyewe alikuwa ashamwambia aachane na jeshi , hivyo alijiambia yeye ni nani hata akatae kile ambacho bebi wake amesema.
“Hahaha.. nilijua upo ngangari kama Magdalena , kumbe mtoto soft”Aliongea Edna na kumfanya Mage kucheka.
“Hiki chumba kinanikumbusha tulivyokuwa wadogo , hakina mabadiliko makubwa”Aliongea Mage na kumfanya Edna kutabasamu.
“Kimejaa kumbukumbu nyingi sana za utoto wangu”Aliongea Edna huku Mage akiendelea kuangalia , lakini macho ya Mage yalivutiwa na karatasi iliokuwa karibu yake na aliichukua na kuishikilia mkononi huku Edna akimpa mgongo.
“MARRIGE CONTRACT” neno mkataba wa ndoa ndio ambalo lilimvutia sana Mage..
“Edna huu….. mkataba usiniambie ni wa kweli?”Aliongea Mage kwa mshangao mkubwa , ni kama kitu kilichokuwa kwenye mikono yake ni feki.
Edna aligeuka haraka haraka huku akijilaumu kusahau kuhifadhi karatasi za mkataba wa ndoa yake na Roma kwenye kabati.
Edna alimwangalia Mage alieshikilia karatasi na kushindwa hata ajibu nini kwani siri yake imefichuka.

SEHEMU YA 248.
LONDON—KENSIGNTON PALACE.
Ni ndani ya jumba la Kifalme ndani ya jiji la London Uingereza , anaonekana mrembo Ashley akiingia ndani ya jumba hilo akiwa amesindikizwa na walinzi wawili wa kike.
Ashley licha ya kwamba haikuwa mara yake ya kwanza kufika ndani ya hili eneo lakini hakuweza kuzoea mazingira ya ndani ya jengo hili na kama siku moja ataingia mwenyewe pasipo muongozo maalumu basi angeweza kupotea.
Mitindo ya kizamani ya upambaji wa jumba hili ndio moja ya vitu vilivyomvutia Zaidi Ashley.
Alitembea akiwa na mlinzi mpaka ghorofa ya tatu na kukaribishwa eneo la sebuleni na ‘House Keeper ‘ huku akiambiwa asubiri.
Dakika chache mbele baada ya kusubiri alionekana Profesa Clark Stephanie alievalia gaunni la Rangi nyeupe la maua maua na visendo vya rangi nyeupe akishuka kutoka juu ya ghorofa.
“Ashley you are here”Aliongea Profesa Clark na kumfanya Ashley kusimama na alisogeleana na Clark na kukumbatiana.
“Let us sit and talk, Shall we?”Aliongea Clark na Ashley aliitikia kwa kichwa na kuketi kwenye masofa hayo ya kifahari.
“Kwanini unataka kurudi Tanzania katikati ya project Ashley?”Aliuliza Profesa Clark huku akimwangalia Clark.
“Nina matatizo ya kifamilia. Profesa I told my father about Roma, I am so stupid , I should have told him in person not over the phone”Aliongea Ashley na kumfanya Clark kushangaa kidogo.
“Kwahio tatizo liko wapi kama ushamwambia tayari , hili ni jambo ambalo alipaswa kujua tokea miaka minne iliopita na mimi nilikuzuia kwasababu maalumu”
“Ndio naelewa Profesa , ulinieleza nikae kimya , lakini bado nahisi kuikosea familia yangu , Hususani baba inaonekana anafahamu tayari kuhusu Roma and he wasn’t surprised at all , it looks like he knew it from Grandpa….”Aliongea Ashley huku akionekana kujutia , mrembo huyu licha ya kwamba anayo PhD lakini bado alionekana sio mwenye uwezo mkubwa wa kuongoza hisia zake.
“Ashley I kbow that feelings, and you should go and explain it, you are not going to concentrate with Project anyway with that situation”Aliongea Clark na kumfanya Ashley kutabasamu.
“Professor naweza kuelezea kila kitu kuhusu Roma , kuanzia siku ambayo nilitambua kuwa ni kaka yangu?”Aliuliza Profesa na kumfanya Clark afikirie.
“Ndio unaweza kuelezea , lakini ukumbuke tulimficha Hades juu ya uhusiano wako na yeye kwa muda mrefu”
“Naelewa Profesa , nampenda sana kaka yangu , ijapokuwa mama sio mmoja lakini tunashea damu moja, natamani kumuona Roma akimtambua baba”Aliongea Ashley na kumfanya Clark kumsogelea na kumshika mkono.
“Ashley unajua ni sababu gani nilikuchukua kipindi kile na kuwa mwanafunzi wangu na ukawa mtu wa kwanza kuingia kwenye maabara yangu?”Aliuliza Porfesa na Clark alitingisha kichwa kwamba hajui.
“Because you are Empaths”Aliongea Profesa akimaanisha kwamba Ashley ni mtu ambaye ana uwezo wa kuhisi maumivu na hisia za wengine wanaomzunguka.
“There is no static logic when it comes to family matter`s , all Decisions are always influenced with our own intuition and Intuition is common sense so you should do what feels right for your family”
“Hakuna mantiki maalumu likija swala la kifamilia , maamuzi yote yanaathiriwa na uangavu wetu wenyewe na uangavu ndio akili ya kawaida , hivyo unapaswa kufanya kilichobora kwa familia yako”Aliongea Profesa na Ashley alitabasamu na kisha waliagana.
*******
Mage alijikuta moyo wake ukijawa na furaha mno, hakuamini kama ndoa ya Edna na Roma ilikuwa ni feki , mrembo huyu licha ya kwamba alikuwa akimpenda Roma lakini alijawa na hatia kwani Roma alikuwa ni mume wa Edna , lakini leo hii ni kama alitua mzigo kwenye moyo wake baada ya kugundua kuwa Roma na Edna ndoa yao si kwasababu ya mapenzi bali ni ya kimkataba tu, alisoma vyema mkataba huo na aligundua ni kama mwezi tu uliokuwa umebaki kwa Roma na Edna kumaliza siku zao walizoahidiana kua Pamoja kama mke na mume..
Edna yeye kwasababu alimchukulia Mage kama rafiki yake , hakuona haja ya kumficha na alimweleza namna ambavyo walifunga ndoa na Roma , kwamba yote ilikuwa ni kumuepuka marehemu baba yake kumlazimisha kuolewa na mtu asiempenda.
“Edna niambie ukweli, Unampenda Roma?”Aliuliza Mage huku akimwangalia Edna kwa shauku.
“Kwanini unauliza hivyo?”
“Nataka kujua kama unampenda Roma licha ya kwamba umefunga nae ndoa ya kimkataba”Edna ukweli hakuwahi kujiuliza swali kama hilo na hata alipoulizwa alishindwa kuwa na majibu ya moja kwa moja.
“Sister Edna kuna hii kadi imeletwa kwa ajili yako”Aliongea Yezi aliengia chumba cha Edna na kufanya mazungumzo kati ya Mage na Edna kuvurugika.
Edna alichuku kadi iliokuwa ipo kwenye mikono yake na kuanza kuisoma , ilikuwa ni kadi iliokuwa ikionyesha mwaliko wa kuhudhuria kikao cha wafanyabiashara wakubwa nchini na Raisi wa Rwanda , mheshimiwa Paul Jeremy.
“Asante mdogo wangu”Aliongea Edna na Yezi alitabasamu
“Edna ngoja nirudi nyumbanni Baba na Mama wananisubiria, ndio kwanza nimerudi sasa hivi na sijawapa maelezo mazuri kwanini nimekimbia mafunzo ya jeshi”Aliongea Mage huku akinyanyuka na Edna aliafana na Mage na kuahidiana watatembeleana mara kwa mara kwani ni majirani.
“Safari yangu imejawa na bahati kubwa , nimefika tu nyumbani na nimegundua Edna na Roma hawaja oana kwa mapenzi, Roma ukishaachana na Edna utanioa mimi”Aliwaza Mage wakati akitoka kwenye geti la nyumba ya Edna.
Upande wa Edna baada ya Mage kuondoka aliingia kwenye mawazo, huku akiangalia karatasi ya mkataba wa ndoa, mrembo huyu alionekana kujiuliza maswali mengi na kukummbuka mengi ambayo Roma na yeye wamefanya.
Alijikuta akikumbuka kitendo walichofanya na Roma kule Kigamboni jana yake na alijikuta akitabasamu na kujionea aibu na kuuhifadhi mkataba ule kwenye Droo ya kabati.
*******
Kuanzia saa moja kamili mpaka saa mbiili na nusu Roma na Nasra walionekana kuhemeana kama vile ni mabeberu huku kila mmoja akionekana kutoa jasho jingi na shughuli iliofanyika hapo kitandani ilionekana pevu , na haikueleweka ule msimamo wa Nasra alioongea mchana uliishia wapi , kwani tunachoona mrembo huyu sio tu kumkaribisha Roma nyumbani kwake , lakini pia alimpatia kabisa na kitumbua.
“Bebi Nasra usiniambie ulijaza asali kabla ya mimi kuja?”Aliuliza Roma aliemkumbatia Nasra kwa nyuma huku wote wakiwa uchi.
“Ushaanza kuongea ujinga”Aliongea Nasra kwa aibu lakini na kufurahi kwa wakati mmoja kwani aliamini Roma atakuwa amefurahi.
“Hehe.. haina haja ya kuona aibu cha urembo”Aliongea Roma na kumbeba Nasra juu juu na kuzama nae bafuni na kilichosikika ni vicheko vya Nasra , na haikueleweka alikuwa akitekenywa au ni kipi kilichokuwa kikiendelea ,ila jambo moja la uhakika ni kwamba Nasra alikuwa ashayavulia maji nguo na hakuwa na budi kuyaoga , hakumuwaza tena Edna na alikuwa ni kama Dorisi tu, wote walijiambia watashea mwanaume mmoja yaani Roma au mfalme Pluto.
“Najma niambie kuhusu urafiki wako na Najma”Aliongea Roma na kumfanya Nasra kudondosha kijiko chini kwa mshangao.
“Roma una..”
“Nasra huna haja ya kupata mshituko, ndio nafahamiana na Najma, yeye na kaka yake ndio watu pekee waliokuwa kama ndugu kwangu nilivyofika hapa Dar”Aliongea Roma na baada ya kumaliza sentensi yake machozi yalikuwa yamemjaaa Nasra na Roma alishangazwa na hilo.
“Roma usiniambie mwanaume ambaye Najma anampenda ni wewe?”Aliuliza Nasra kwa wasiwasi na Roma hakuona haja ya kuficha na alimueleza ndio.
“Nasra subiri..”
“Roma naomba uondoke nyumbani kwangu”Nasra alibadilika ndani ya dakika chache huku akihisi kifua chake kupanda na kushuka kwa wakati mmoja.
“Roma naomba uongoke tafadhari..”Aliongea Nasra huku akikimbilia chumbani kwake na Roma alishangazwa na mabadiliko ya Nasra ,ila alishindwa kuendelea kukaa hapo ndani, aliona ni bora kuondoka na atakuja kumtafuta akishatulia.
Nasra alijikuta akilia ndani ya chumba chake kwa muda mrefu ,mpaka pale aliponekana akitoka akiwa na mkoba na funguo za gari na kwa jinsi alivyoonekana ni Dhahiri alikuwa akienda nyumbani kwa rafiki yake Najma..
Sasa wakati anaingia kwenye gari yake tun a kuliwasha , simu yake ilitoa mlio wa kuingia kwa ujumbe wa meseji na aliinua haraka hara na kisha kuangalia ujumbe huyo na alijikuta akinyong`onyea kwenye siti yake.
“Najma Am rel sorry sikufahamu , this is all because of Roma . Roma I hate you”Aliongea Nasra huku machozi yakimtoka.




SEHEMU YA 249
Ni muda wa saa mbili usiku , familia nzima ilikuwa mezani kasoro Roma peke yake ambaye aliaga tokea saa kumi na mbili kama anatoka na bado hakuwa amerudi.
Edna alikuwa akila chakula mdogo mdogo pasipo ya kuwa mchangiaji wa stori , alionekana kuwa mpole kuliko isivyokuwa kawaida , jambo hilo lilimfanya Blandina moyo wake kuuma , kama mama aliona Edna anateseka na kutokuwepo kwa Roma na alishindwa cha kufanya kumfariji Edna.
Wanafamilia walikula chakula mdogo mdogo huku stori za hapa na pale zikiendelea na Edna ndio aliekuwa wa kwanza kumaliza kula chakula na alirudi kwenye chumba chake cha kujisomea , chumba ambacho miaka kadhaa nyuma kilikuwa kikitumiwa na Bibi yake Pamoja na mama yake , ni chumba kikubwa kweli chenye vitabu vingi kuliko kile cha kule Kigamboni na vitabu vilionekana kupangiliwa kwa usafi wa hali ya juu.
Upande wa kushoto kulikuwa na tarakishi kubwa ya kampuni ya Apple na meza kubwa , kwa muonekano wake ni kama ofisi, na kama Edna ataamua kufanyia kazi zake hapo ndani basi isingeleta shida yoyote kwani kila kitu cha kiofisi kipo.
Moja ya sababu kubwa ambayo humfanya Edna kupotezea mawazo mabaya ni uwezo wake mkubwa wa akili , Edna ni mtu anaependa utulivu, ni aina ya watu wenye haiba ya ukimya na upole na mara nyingi hata jambo likimuudhi hatoongea chochote Zaidi ya kukaa kimya na kutafuta jambo la kufanya ili kumfanya kuwa bize, na Edna ndicho alichofanya baada ya kuingia kwenye chumba hiko , kwani alianza kufanya kazi ambazo hakuzimaliza ofisini kujiweka bize.
Nusu saa mbele mlango ulifunguliwa na alionekana Blandina aliebeba juisi na kuingia ndani ya chumba hiko na kumwangalia Edna aliekuwa bize na kazi.
“Edna mwanangu , unapendeza unavyoonekana kuwa bize na kazi”Aliongea Blandina huku akikagua chumba hiko na alimpatia na juisi.
“Ahsante mama”Aliongea Edna huku akitabasamum haikueleweka Blandina alitaka kuongea nini na Edna ila hakuweza kuongea na alimuacha Edna kuendelea na kazi huku akimwambia kuwa akichoka akapumzike asijitese kufanya kazi muda mrefu na Edna aliitikia kuwa atafanya hivyo , huku akijisikia vizuri, kwani aliona Mama mkwe wake anaonekana kumpenda na kumjali.
Saa sita kamili za usiku ndio muda ambao Roma alirudi na kabla hajaenda kwenye chumba chake alielekea kwanza kwenye chumba cha Edna na kujaribu kusukuma mlango na alitabasamu baada ya kugundua haujafungwa kwa Ndani.
Roma aliingia kwenye chumba hiki cha mke wake kimya kimya na kumwangalia Edna ambaye alionekana kuwa katika usingizi mzito, Roma alimfunika vizuri Edna na kisha alimwangalia usoni , alipendezwa na namna ambavyo Edna alikuwa amefumba macho na kuwa usingizini kwani alionekana kama mtoto.
“Nakupenda sana Edna mke wangu.., unaonekana kuwa mrembo Zaidi unapolala, Usiku mwema”Aliongea Roma kwa kunong`ona na kisha akambusu Edna kwenye paji la uso na kutoka nje ya chumba hiko, lakini ile anafunga mlango kwa nje , Edna alionekana hakuwa amelala na alimsikia Roma vizuri na kuishia kutabasamu na kufumba macho na kuendelea kulala.
Ukweli ni kwamba Edna baada ya kumaliza kufanya kazi zake na kurudi ndani ya chumba chake kwa ajili ya kupumzika hakulala , alikuwa macho mpaka wakati alipoona gari ya Roma ikiingia na kusimama maegeshoni ndio muda ambao alipanda kitandani kulala , kwani alionekana kuridhika baada ya kumuona mume wake kasharudi salama.
Sasa haikueleweka kama Roma asingerudi na kuendelea kutafuna kitumbua cha Nasra ingekuwaje, tushukuru kukasirika kwa Nasra kwani mrembo Edna aliweza kumuona mume wake akirudi kutoka kwa mchepuko wake na kupumzika.
********
“Najma naomba unisamehe rafiki yangu , sikufahamu kabisa kama The chosen one ndio Roma”Aliongea Nasra baada tu ya kufika Mbagala na Najma alikuwa na hasira mno kwani hakutaka kabisa hata kumkaribisha ndani rafiki yake.
Lakini licha ya hivyo Najma alikuwa ashaanza kumhurumia Nasra, ambaye alionekana kujutia na Najma pia aliona makosa ni ya kwake kwani licha ya kumpenda Roma na kumwambia Nasra kuhusu The Chosenn one lakini hata siku moja hakuwahi kumuonyesha Nasra sura ya Roma.
“Najma mwenyewe sikufahamu kama Roma ni mume wa Edna ndio nimefahamu juzi , kama ningejua mapema…”Aliongea Nasra na kuanza kulia , Nasra hakuwa tayari kukosana na Najma , alikuwa akimchukulia Najma kama ndugu yake wa pekee hapa mjini na ndio maana alikuwa tayari kufanya chochote kile kwa ajili ya kupewa msamaha , kwa upande wa Najma pia ilikuwa hivyo hivyo , licha ya kwamba alikuwa na hasira na Nasra lakini hakuwa tayari kumpoteza.
Nasra alieleza tokea siku ya kwanza anakutana na Roma kwenye usaili , lakini pia siku ambayo alijikuta akiwa uchi mbele ya Roma pasipo kutambua nini kilitokea na namna ambavyo mahusiano yake na Roma yalivyoanza na namna ambavyo hakuweza kutambua Roma ni mume wa Edna , mpaka siku ambayo pia Nasra alimpigia magoti Edna kwa ajili ya kumuomba msamaha , mrembo huyu alimweleza rafiki yake kila kitu na hio yote ni kutaka kumfanya Najma kumuamini tena.
Najma aliona ukweli katika maneno ya rafiki yake na hakuona haja ya kutokumsamehe , alimsogelea na kumkumbatia na wakaanza kulia Pamoja baada ya kusameheana.
Ni asubuhi Nasra alionekana akitoa gari yake ndani ya eneo la Bias akiitafuta barabara kuu kwa ajili ya kurudi nyumbani kwake na kujiandaa kwa ajili ya Kwenda kazini , njia nzima mrembo huyu alionekana kufikiria yale ambayo waliongea jana usiku na rafiki yake Najma.
Hakuamini kama Edna ameamua kumsaidia Najma kwa ajili ya kaka yake kupatiwa matibabu , hela ambazo Edna ametoa kwa ajili ya matibabu zilikuwa nyingi sana na ndio maana Nasra alijikuta akimfikiria Edna.
Ukweli ni kwamba Nasra hakufahamu kama kuna ahadi Najma na Edna wamekubaliana na Najma hakumueleza Nasra kutokana na kwamba mkataba wake na Edna ulikuwa ni siri na maelekezo hayo alipewa na Edna , hivyo aliamua kukaa kimya na kutokumuambia Nasra na ndio maana asubuhi hio Nasra alikuwa ni mwenye kujiuliza Edna ni kiumbe gani mwenye roho nzuri mpaka kutoka kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya matibabu ya kaka yake na Najma , alimuona Edna kama Malaika.
“Ngoja nikifika ofisini lazima nimpe shukrani zangu kwa kumsaidia rafiki yangu Najma”Aliwaza Nasra huku akizidi kukanyaga pedeli kuelekea Mikocheni nyumbani kwake.
*********
“Camillius wageni wetu washafika”Aliongea Zenzhei akimwamsha Afande kweka ambaye alionekana kupumzika ndani ya chumba chake.
“Asante Zenzhei , waelekeze chumba cha kukutania wageni ninakuja muda si mrefu , unaweza pia kuendelea na taratibu zingine”Aliongea Afande kweka na Zenzhei aliitikia na kutoka ndani ya chumba cha Afande Kweka kwa ajili ya kuelekeza wageni wake.
Ni ndani ya nyumba ya pili yake ndani ya uzio wa jumba hili analoishi afande kweka , mita kadhaa kuna nyumba nyingine ambayo mara nyingi Afande kweka hupenda kufanyia vikao ambayo vinahusu watu wengi lakini pia vya siri sana.
Sasa ndani ya jumba hili wanaonekana watu wanne jumla ambao ndio wageni wanaopaswa kuonana na Afande kweka , wageni hawa wa kwanza alikuwa ni Mellissa Luiz, wa pili ni Nadia Alfonso , wa tatu ni Zoe Kovac na mwingine ni mwanaume mzungu alievalia suti ya rangi ya samawati ambaye hakufahamika jina lake, ambaye kwa muonekano wake si chini ya miaka hamsini hivi.
Zenzhei Pamoja na wahudumu wa kasri hili la Afande kweka walionekana kuwa bize wakiwapa huduma wageni hawa ili kuwafanya wajisikie wapo nyumbani.
Baada ya kama nusu saa hivi alionekana afande kweka akiingia ndani ya ukumbi huo wa mikutano akiwa amevalia suti yake ya rangi nyeusi , licha ya kwamba alioekana kuwa mzee lakini afya yake ilikuwa imara kwani alitembea pasipo kutumia mkongojo.
“Karibuni sana wageni naitwa Camillius Kweka, ni Jenerali mstaafu wa jeshi la wananchi wa Tanzania, lakini pia mimi ndio baba kwa Raisi wa taifa hili”Aliongea Camillius akijitambulisha mbele ya wageni wake baada ya kukaa kwenye kiti.
“Tunashuru sana kukufahamu Afande Kweka , nitaanza kujitambulisha mimi”
“Kwa majjina nafahamika kama Mellisa Luiz ni jasusi mstaafu kutoka CIA na Dhoruba Nyekundu”Aliongea Mellisa kwa kingereza akijitambulisha na kisha akatambulisha kila mmoja alieambatana nae , lakini baada ya kufika kwa mzungu yule ambaye alionekana kuwa mtu mzima kama ilivyo kwa Mellisa , alimpa ishara ya kujitambulisha mwenyewe.
“Kwa majina nafahamika kama Phill Knight , I am Former undercover Agent with Zeros Organisation”Aliongea yule mwanaume kwa kujitambulisha kwa jina la Phill Knight akiwa ni jasusi mstaafu kutoka taasisi ya Zero.
“Karibu sana Phill Knight Tanzania , wote karibuni kwa mara nyingine Tanzania na huu ni mwanzo mzuri wa sisi kufahamiana , Comrade aliponipigia simu juu ya ujio wenu hapa Tanzania nilishangaa , lakini nimeshangazwa pia na namna mnavyoonekana kujiamini hii ni ishara kubwa kwa ushindi wa mapambano yetu tunayokwenda kuanza nayo”
“Huyu ni Zenzhei , ni msaidizi wangu lakini pia ni mwanachama mwenzetu , anaonekana kama binadamu wa kawaida , lakijni asili yake ni kutoka ulimwengu wa Majini kutoka miliki ya Hongmeng China, lakini pia ni moja ya Ninja waliopata mafunzo chini ya Yamaguchi”Aliongea Afande Kweka na kumfanya kila mmoja kushangaa.
“Afande kweka , sijawahi kumuona mtu kutoka jamii ya kijini kwenye mazingira ya kawaida ya dunia , kumbe stori juu ya miliki ya kijini ni kweli sio hadithi?”Aliongea Mellisa kwa namna ya kushangaa.
“Unaonekana kushangaa Miss Mellisa, Sio Hongmeng tu ndio miliki za kijini duniani , kwa ufupi ni kwamba Hongmeng ni kama sehemu tu ya taifa ndani ya ulimwengu wa Kijini na yapo makabila mengine yenye miliki katika ulimwengu wa Majini, Sisi kwa upande wetu Hongmeng ni kama walinzi wakuu ndani ya taifa la China”Aliongea Zenzhei na kumfanya Mellisa na wengine kuduwaa kwa mshangao ni Habari mpya kwao.
“Jamani nadhani leo hii hatupo hapa kwa ajili ya kuzungumzia miliki za kijini, ila ni kwa ajili ya kuongelea sehemu ya ajenda mlizofika nazo hapa nchini na kutaka kujadiliana na mimi”Aliongea Afande Kweka na Mellisa alitingisha kichwa.
“Afande kabla ya kikao chetu kuanza , nitajaribu kukueleza kwa ufupi ni kipi kilitokea miaka kumi na moja iliopita na kumfanya Phill Knight kuwa sehemu ya wanachama wetu”Aliongea Mallisa Luiz na kuanza kueleza stori ya Phill.

SHEMU YA 250
((((11 YEARS AGO(MIAKA KUMI NA MOJA ILIOPITA ANAELEZEA MELLISA)
Ni tarehe ishirini na tatu kuamkia ishirini na nne mwezi wa kumi na mbili ndani ya jimbo la Texasi jijjini Dallas , ndani ya makazi ya watu, sehemu inayofahamika kwa jina la Greenville Avenue muda wa saa sita usiku.
Mwanamama wa umri wa miaka arobaini hivi aliekuwa akifahamika kwa jina la Mary , alionekana akishituka kutoka usingizini , baada ya kulala muda mrefu, mwanamama huyu baada ya kishituka alijikuta akipapasa mkono wake upande wa kushoto pasipo kugeuka kwa nia ya kutafuta mwili wa mime wake Phill, lakini mwanamama huyu baada ya kupapasa juu na chini mkono wake haukuambulia kitu na hii ilimfanya anyanyuke na kukaa kitako na kugeuza macho yake kulia, na hapo alijikuta akitoa shuka taratibu baada ya kumuona mume wake aliekuwa amepitiwa na usingizi katika meza yake ya kusomea huku pembeni ilionekana Printer ambayo na yenyewe ilionekana kuwa imewashwa pamoja na tarakishi.
Bi Mary alionekana kumuonea huruma mume wake kwa kitendo cha kupotelea usingizi akiwa mezani anasoma,mwanamama huyu ambaye alikuwa amevalia nguo za kulalia alitembea kusogea upande ambao mume wake amelala kwenye meza ,na kabla hajamgusa ili aamke , mara Printer ilianza kutoa mlio wa sauti ya Kuprint karatasi.
Bi Mary alijikuta akighairisha zoezi lake na kisha kuchukua baadhi ya karatasi ambazo zilikuwa zikitemwa na Printer hio, karatasi ya kwanza ndio iliomshangaza mwanamama huyu:
Kwanza kabisa karatasi hio ilikuwa na ‘watermark’ ya neno ‘Confidential’ , ilionekana ilikuwa ni nyaraka ya siri ambayo Mume wake Phill alikuwa akiisubiria kiasi kwamba alijikuta akisinzia kwenye meza.
Bi Mary alijikuta akianza kutetemeka mikono kadiri alivyokuwa akisoma karatasi hio , huku mume wake akiwa bado amelala , mwana mama huyu alielewa kabisa taarifa hio ni nyeti , lakini kutokana na taarifa yenyewe kumshangaza alijikuta akiendelea kusoma, alimaliza katatasi ya kwanza akachukua nyingine akaimaliza , huku kila karatasi anayosoma ikimuacha mdomo wazi , alisoma nukta hadi nukta mwanamama huyu ambaye kazi yake kubwa ni kuuza maua.
Baada ya Bi Mary kumaliza kusoma , alijikuta mwili wake ukikosa nguvu , alichukua karatasi alizokuwa ameshikilia na akazirudisha kwenye mdomo wa Printer na baada ya kumaliza kusoma , alijikuta hata kile ambacho kimemsogeza kwenye meza aliolala mume wake Phill ,alisahau m alijongea na kurudi kwenye kitanda na kisha akajilaza na kujifunika shuka.
“Evidence regarding killing of Professor Banos and M-Airline Plane dissapearencce”
“Detailed Plan to Eliminate the World coming Enemy”
“Project LADO success Rate”
“Twelve Greek God`s to faight against the Wold Coming Enemy”
Hivyo ndio vichwa vya habari ambavyo Bi Mary alikuwa amevisoma na alikuwa akivifikiria akiwa ndani ya Blanketi huku machozi yakiwa yameujaza uso wake, hakuwamini kabisa kwa kile alichokiona.
Kulivyokucha Mary alijitahidi kuwa wa kawaida mbele ya mume wake amaye tayari alikuwa amevaa suti kwa ajili ya kuelekea kazini , ambayo Bi Mary siku zote alikuwa akijua mume wake alikuwa ni Mhandisi ndani ya kampuni ya kutengeneza magreda ya kuchimbia barabara.
Bi Mary aliwaangalia watoto wake watatu kwa namna ya kuwaonea huruma , na kisha akamgeukia mume wake Phill ambaye alionekana kutabasamu muda wote.
“Mary Yo seem to be off today , what the matter , Tomorrow is Christmas , why you are not happy like everyone else, Come on tell me”
“No Phill , I am fine ,Why?”
“Its nothing Mary if you are fine , then it`s okay , I will be off to work now”Aliongea bwana huyu na kisha alimsogelea mke wake na kumbusu shavuni na kisha akahamia kwa watoto wake wote ambao mmoja wa kike alikuwa na miaka kumi na mbili mwingine kumi na mmoja mine.
Baada ya dakika kadhaa za Phili kutoweka kwenye macho ya Mary , alikimbilia chumbani kwake na kuanza kutafuta zile karatasi sehemu ambazo alikuwa akiamini atazipata , lakini hakuweza kuzipata.
“Atakuwa ameenda nazo”Alijiongelesha huku akijilaumu kwanini hakupiga picha
“Pastor Edwardo , I have something very important to discuss with you”Aliongea akimaanisha kwamba anajambo la kuongea na mchungaji aliemtaja kwa jina la Edwardo na hii ni baada ya kusalimiana.
“Unaonaje mara baada ya mkesha wa leo , litakuwa jambo zuri , maana mchana wa leo ratiba zimebanana”Ilisikika sauti upande wa pili na Mary akakubaliana na Pastor.
“Sijui kama ninachofanya ni sahihi , lakini naamini ni vyema nikiongea na kiongozi wa dini , Phill sio wa kunidanganya mimi kwa Zaidi ya miaka ishirini tokea tuone, he is undercover agent with Zeros Organisation all this time?, Damn you Phill”Alijiongelesha mwanamama huyu huku akianza kutoa machozi ,alionekana taarifa ya jana usiku aliosoma ilikuwa ni kubwa kwake na yenye kumuumiza.
Usiku wa saa sita hivi kwenda saa saba za usiku ndipo tukio la kutisha lilipotokea na mkurdish Afshar alivyofanya yake ya kuwarushia risasi waumini wa kanisa la The Forgivven.
Upande wa Pastor na Mary walikufa wakiwa ndani ya chumba ambacho kilikuwa kinatumiaka kama ofisi ya mchungaji ndani ya kanisa hili la The Forgiven.))).
…………………
Afande Kweka alijikuta akishangazwa na stori hio sana na sio kwake tu hata kwa Zenzhei na Nadia pia walionekana kushitushwa na Habari hio.
“Kwahio bwana Phill baada ya kupoteza familia yako yote ni nini ambacho kilitokea?”
“Zeros organization wakishirikiana na CIA walinikamata na kunipeleka kwenye moja ya Blacksite na kuanza kunipa mateso makali ambayo sitoweza kuyasahau maishani , wakitaka nieleze kwanini nilidukua taarifa ambazo hazikuwa zikinihusu na ni nani ambaye nashirikiana nae ”Aliongea Phill na kumfanya Afande Senga kujawa na shauku.
“Unamaanisha kwamba taarifa ambazo Mary mke wako alisoma zilikuwa hazikuhusu , nilidhani wewe ni Undercover Agent kutoka Zeros Organisation?”Aliuliza afande Kweka na Phili alitabasamu.
“Ni kweli mimi nilikuwa ni Undercover ajent wa CIA , lakini pia wa Zeros Organisation , licha ya kwamba nilikuwa nikifanya kazi kwao haimaanishi kwamba nilikuwa na ruhusa ya kupata taarifa za kile ambacho kilikuwa kinaendlea ndani ya CIA Pamoja na Zeros kwani kazi zangu zilikuwa ni nje ya ofisi kama ujuaavyo Ajent wa CIA wengi”Aliongea.
“Unamaanisha nini?”
“Afande Kweka ninachomaanisha ni kwamba mkataba ambao ulinifanya nikachelewa kulala mpaka mke wangu kuupata na kuusoma haikuwa sehemu ya kazi yangu , bali kuna mtu kutoka ndani ya kitengo alinipa taarifa kwamba kuna siri kubwa anataka kunitumia”
“Mtu!!, Unamaanisha kutoka ndani ya Zeros au CIA?”
“Sifahamu ni kutoka kwa kundi lipi kwani yote nilikuwa nikifanyia kazi kwa wakati mmoja, ila mtu huyo nina uhakika alikuwa ndani kati ya idara hizo mbili na hakujitambulisha kwangu jina na aliniambia ni kutokana na usalama”
“Alikuwa akitaka nini kwako, na kwanini aliamua kukuchagua wewe na kukutumia nyaraka za siri”
“Aliniambia kwamba atanipa maelekezo mengine baada ya kusoma hizo nyaraka , lakini cha kusikitisha ni kwamba familia yangu na waumini wa kanisa la Forgiven waliteketezwa kwa kuuwawa kikatili kwa ajili ya siri hio feki”Aliongea na kumfanya Kweka kushangaa
“Kwanini unasema ni feki , ilihali ilipelekea vifo vya watu wengi kwa ajili ya kuzuia isisambae?”
“Afande Kweka hilo sifahamu mpaka sasa na ndio maana nipo hapa katika haya mazungumzo, nahitaji pia kujua kwanini watu walikufa licha ya taarifa ile kuwa asilimia hamsini ni uongo”
“Wewe ulitambua vipi kwamba taarifa hio ilikuwa ni feki?”
“Seventeen ndio alietuambia taarifa hio kuwa feki”Aliongea Mallisa na kumfanya Afande kweka kutoelewa , kwanza hakuwahi kusikia jina la Seventeen.
“Seventeen!!”
“Ndio Afande Seventeen ni mwanamke ambaye alikuwa na mahusiano na mjukuu wako Roma na ndio alietuambia taarifa hio kuwa feki lakini sio kwa asilimia mia moja, asilimia hamsini ya taarifa hio ni feki na nusu yake ni ukweli”Aliongea Mellisa na kumfanya Afande kweka kushangaa Zaidi.
“Mnaonaje mkiniambia hio asilimia ya ukweli ni ipi na huyo Seventeen ni nani kwa ujumla wake?”
1.Detailed Plan to Eliminate the World coming Enemy
2. Twelve Greek God`s to faight against the Wold Coming Enemy
“Hizo nyaraka mbili ni feki Afande , kwanza kabisa hakuna mpango wowote uliondaliwa kwa ajili ya kupambana na adui anaekuja kama ilivyoandikwa , lakini pia hakuna miungu kumi na mbili ambayo itapambana na Adui anaekuja , bali ilitakiwa kuandikwa kwamba One god to fight against eleven Greek gods”Aliongea Mellisa akimaanisha kwamba kati ya mungu mmoja atapamabana na miungu kumi na moja.
“Kama maelezo yako ni sahihi je huyo mmoja atakaeweza kupambana na miungo yote kumi na moja ni nani na kwanini mmojaapambane na wenzake?”Aliuliza Zenzhei ambaye alionekana kuwa katika mshangao pia.
“Ni Mfalme Pluto, Hades”
“Roma!, unamaanisha mjukuu wangu?”
“Ndio mjukuu wako ndie anaetakiwa kupambana na miungu yote kumi na moja kwani ni tishio kwa ulimwengu huu na ni yeye pekee ambaye anaweza kufanya hivyo”Aliongea Mellisa na kumfanya Afande Kweka kuvuta pumzi , bado alionekana kutoelewa.
“Kwanini mnaamini kwamba Roma ndio mtu pekee ambaye anaweza kupamana na hio miungu ambayo hata sielewi inahusiana na ninikwani nasikia stori zake tu na mmefahamu vipi kwamba Roma ndio muhusika kwa kupambana nah io Miungu?”
“Seventeen ndio alietueleza hivyo kwa Ushahidi mkamilifu”
“Ushahidi , unamaanisha kwmaba mmekuja na Ushahidi”
“Hpana afande , Roma mwenyewe ndio Ushahidi,,”Ilisikika sauti kutoka nje na kumfanya kila mmoja kugeuza shingo.
“Comrade!!”Aliongea Afande Senga akiwa katika hali ya mshangao , hakuamini rafiki yake wa miraka mingi alikuwa mbele yake.
ITAENDELEA MWAKANI , HAOOY NEW YEAR TO YOU ALL ,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…