singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
-
- #1,821
SEHEMU YA 339
Edna alionekana kama hakuwa akiamini kile ambacho alikuwa amekisoma alibeba tena ile bahasha na kuangalia ndani kama kuna kitu kingine zaidi ya ile karatasi na ni kweli ndani yake kulikuwa na picha mbili.
Edna alizitoa na kuanza kuangalia moja moja na alijikuta akishika moyo wake , watu wawili waliokuwa kwenye picha ya pamoja alikuwa akiwajua, mmoja akiwa ni mama yake Raheli na mwingine akiwa ni Raisi Jeremy wa Rwanda, na katika pozi ambalo walikuwa wakionekana ni dhahiri kabisa walikuwa ni wapenzi.
Edna akili yake ilipata moto na sasa ni kama anakumbuka kwa mara nyingine kitabu cha mashairi ambacho mama yake alikuwa akikisoma mara kwa mara siku zote , kitabu ambacho ndani yake kulikuwa na picha ya mwanaume ambaye hakuitambua mara moja mara baada ya kuiona , lakini sasa kwa kupitia picha zilizokuwa kwenye mikono yake anatambua kuwa ile picha pia ilikuwa ni ya Raisi Jeremy na ni yeye ambaye alishindwa tu kuitambua.
Karatasi ambayo Edna alikuwa akiisoma , ilikuwa ikionyesha majibu ya DNA kati yake yeye na Jeremy Paul ambaye ni raisi wa Rwanda na majibu hayo ndio yaliomfanya Edna kutetemeka kwani ni swala ambalo hakuwaji kulitegemea kabisa.
“Kwahio baba yangu mzazi ni Raisi Jeremy wa Rwanda?”Alijiuliza Edna huku machozi yakianza kumtoka taratibu taratibu, picha mbalimbali zilikuwa zikipita kwenye akili yake na alishindwa hata kujielewa kwa wakati huo , Edna alikumbuka namna Maisha yake na baba yake Adebayo yalivyokuwa magumu na alijikuta moyo ukiuma.
Kila kitu sasa kilikuwa kipo wazi , Edna anatambua baba yake ni Raisi Jeremy wa Rwanda , lakini jambo moja ambalo anashindwa kufahamu ukweli wake ni juu ya kuzaliwa na pacha wake aliopewa jina la Lorraine.
Edna alikaa ndani ya chumba chake kwa takribani lisaa ndipo akili yake iliporudi na kufanya kazi na hapo hapo alimkumbuka Bi Wema , aliamini Bi Wema lazima atakuwa anaufahamu ukweli juu ya baba yake mzazi kwakuwa alimlea tokea akiwa amezaliwa.
Edna alitoka haraka haraka na kushuka chini kumtafuta Bi Wema ili kumuuliza maswali juu ya Jeremy Paul wa Rwanda kuwa mzazi wake huku mkononi akiwa ameshikilia picha zile mbili ambazo zilikuja ndani ya ile bahasha.
Bi Wema ndio aliekuwa wa kwanza kumuona Edna akiwa kwenye hali ambayo sio ya kawaida.
“Edna kuna shida gani , mbona unatokwa na machozi?”Aliuliza Bi Wema huku akimsogelea Edna ,kwa upande wa Blandina aliekuwa bize na kuandaa chakula moyo wake ulidunda aliamini tayari mwanae Rpma kashayakoroga tena.
Edna alimpatia Bi Wema zile picha na baada ya bibi huyo kuzipokea na kuangalia alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa wakati mmoja na mpaka hapo Edna alimuona Bi Wema alikuwa akijua swala hilo.
“Bi Wema huyu ndio baba yangu?”Aliuliza Edna kwa huzuni na swali lile lilimfanya na Blandina kumsogelea Bi Wema na kuchukua picha iliokuwa kwenye mikono yake.
Blandina mara baada ya kuona picha moja kati ya mbili , alijikuta na yeye akivuta pumzi , picha aliokuwa ameishikilia ilikuwa imepigwa eneo la ufukweni.
Edna baada ya kuona hata Mama Mkwe wake hashituki licha ya kuona picha hio , alijikuta akishangaa na kujiuliza maswali, hata Bi Wema alijikuta akiwa ni mwenye kushangaa kuona Blandina hakuwa ni mwenye kushangaa juu ya swala hilo.
“Mama hata wewe unafahamu hili?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi.
“Edna hio picha nilipiga mimi , hapo ni Sydney Australia Bondi Beach ni miaka mingi iliopita”Aliongea na kumfanya hata Bi wema kushangaa ni kama hakuwa amesikia vizuri.
*********
Ni muda wa saa kumi na nusu mchana , Roma alishaweza kufika ndani ya nyumba ambayo wanaishi wanajeshi wake wa The Eagles na muda huo Diego na Adeline walikuwa wameketi kwenye masofa wakiwa wanamuelezea Roma kuhusu ripoti juu ya uchunguzi walioufanya kuhusiana na kifo cha Raheli.
Kwa maelezo ya Diego ni kwamba waliweza kufanya uchunguzi kwa kudukua Barua pepe binafsi ya Raheli na katika kufatilia kwa ukaribu mawasiliano ya Email yake alionekana wiki kadhaa kabla ya kifo chake aliweza kufanya mawasiliano ya mara kwa mara na Dr Robert kutoka Marekani na mazungumzo yao yalionyesha yalikuwa ni ya mgonjwa na Daktari, yaani Robert akiwa ni daktari huku Raheli akiwa ni mgonjwa, Roma alishangazwa na maneno ya Diego.
“Diego kwahio kwa maneno yako unamaanisha kwamba Raheli alikuwa na daktari binafsi?”Aliuliza Roma.
“Ndio Mfalme Pluto ,ijapokuwa Raheli alikuwa akipatiwa matibabu na Dokta Hubery, dokta wa familia , lakini wakati huo huo alikuwa na dokta binafsi ambaye ni huyu Dokta Robert ,tumeweza kufatilia ‘Profile’ ya Dokta Robert na tumegundua ni daktari ndani ya hospitali ya kimafunzo ya Mayo Clinic Marekani”Aliongea Diego na Roma alitingisha kichwa kumpa ishara ya kuendelea.
“Tulifanya mawasiliano na wenzetu waliopo Marekani kwa ajili ya kutusaidia kumhoji Dokta Robert na jambo lilikuwa Rahisi kwani dokta Robert alitupa ushirikiano wa kutosha na aliweza kutupatia faili linalohusu matibabu ya Raheli na tumeweza kugundua Raheli alikuwa amewekewa sumu kwenye mwili wake”
“Sumu!!”Roma alishangaa.
“Ndio Mfalme pluto”
“Sumu ya aina gani na kwanini awekewe sumu?”Aliuliza Roma na kumfanya Deigo kumpa ishara Adeline aliekuwa pembeni yake.
“Kabla ya kufanya uchunguzi tulikuwa tukitumia ‘reference’ kutoka kwa taarifa aliotupatia Miss Christine inayohusiana na ‘Resurrection Fluid’(Kimiminika) na tuliweza kupata taarifa ya utafiti iliofanyika juu ya hiko kimiminika”Alinyamaza kisha akaendelea.
“Mfalme Pluto kupitia taarifa iliotoka taasisi ya Innova inaonyesha kwamba ‘Ressurection Fluid’ ikitumiwa kwa mtu ambaye yupo hai inageuka na kuwa sumu mwilini, hivyo kumpelekea mhusika kuanza kupata matatizo ya ogani za mwili kufeli taratibu taratibu , ukijaribu kufanananisha na ripoti ya Dokta Robert inaonyesha Bi Raheli mwili wake ulikuwa na sumu ambayo haikuwa ikifahamika bado na ilikosa ‘Antidote’ na hiko ndio kilipelekea kifo chake”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuvuta pumzi mpaka hapo alikuwa na uhakika kwamba sasa maneno ya Christine kwa Raheli kuhusishwa na majaribioa ya kisayansi ni ya kweli.
Antidote ni dawa inayotumika kuyeyusha sumu mwilini , sasa baada ya Resurrection Fluid kuwekwa kwenye mwili wa binadamu anaeishi inashindwa kufanya kazi na kugeuka kuwa sumu ambayo haina hio ‘Antidote’ hivyo kupelekea mtu kufa kwa matatizo mbalimbali , aidha moyo kufeli kufanya kazi au figo.
“Kwahio sasa kwanini Raheli akawa sehemu ya majaribio hayo?”
“Mfalme Pluto katika kufuatilia jumbe za ‘Email’ binafsi ya Raheli tumegundua pia Raheli alikuwa na adui ambaye alikuwa akimtumia jumbe za vitisho , ijapokuwa Email hio ililikuwa ikituma jumbe pasipo ya mtumaji kufahamika , lakini tuligundua ni maswala ya kimapenzi ndio yaliokuwa yakiendelea na Miss Raheli alikuwa akishutumiwa kwa kutoka kimapenzi na mume wa mtu inaonyesha mtu ambaye alikuwa akimtumia jumbe za vitisho alikuwa ni rafiki yake wa karibu na hii ilitufanya kufatilia Maisha ya nyuma ya Raheli na tuliweza kupata hizi picha kutoka chuo cha Durban South Afrika”Aliongea Diego na kumpatia picha Roma , katika picha hizo moja tu ndio Roma aliweza kuitambua na picha hio ilikuwa ni ya Raheli ,Roma ashawahikuona picha ya Raheli mara nyingi ndio maana ilikuwa rahisi kwake kuifahamu.
Kwa maelezo ya Diego picha hio ilikuwa ni ya wadada watatu ambao walipiga pamoja siku yao ya kuhitimu , wanadada hao walikuwa ni Raheli , Nahita na Kizwe mke wa Raisi Jeremy kutoka Rwanda.
“Mfalme Pluto angalia na hii picha”Aliongea Diego na kumpatia Roma picha ya mwanaume na mwanamke wakiwa kwenye pozi la kimahaba ,ilikuwa ni picha ya First Lady wa Rwanda na Raisi Kigombola na haikuhitajika elimu kubwa kugundua kilichokuwa kikiendelea ,wawili hao walionekana kuwa wapenzi.
“Mmeipataje hii?”
“Kuna mtu ametupatia Mfalme Pluto?”Aliongea Diego na kumfanya Roma kushangaa.
“Nani kawapatia?”
“Mfalme picha hizi tumeweza kuletewa na mtoto mmoja ambaye aliagizwa wiki iliopita siku ya ijumaa, hazikuja picha tu bali ilikuja bahasha yenye karatasi zingine na ndio ambazo ziliturahishia kuweza kujua kile ambacho kilikuwa kikiendelea, inaonekana mtu ambaye ametukabidhi hakutaka kufahamika , lakini kwa namna moja ama nyingine ni kama alikuwa akifahamu tunafanya uchunguzi unaohusiana na kifo cha Miss Raheli”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuomba ambiwe hizo karatasi zingine zinahusiana na nini.
Kwa maelezo ya Diego ni kwamba karatasi hizo zilikuwa zikielezea Siri inayohusiana na Maabara ya siri iliokuwa chini ya jengo la Bima ya Taifa, katika Ripoti hio ilionyesha kwamba majaribio ya ‘Resurection Fluid’ yalifanyikia ndani ya maabara hio kwa usimamizi wa kampuni ya Innova pamoja na Maya.
Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba majaribio yaliokuwa yakihusiana na Kimiminika yalifanyikia hapa Tanzania , hivyo taarifa ambayo waliweza kuletewa na mtu asiejulikana ilikuwa ni ya siri sana , mtu alieidhinisha utafiti huo ni Raisi Kigombola kwani sahihi yake ilionekana kwenye hio karatasi.
“Diego kwahio ripoti yenu mmeikamilishaje, nini kilipelekea na Raheli kuhusika kwenye majaribio haya?”
“Mfalme Pluto baada ya kuletewa hio Nyaraka tuliona hakuna sababu ya kufanya uchunguzi zaidi kwani majibu yote yapo kwa mtu alietufikishia hizi karatasi, hivyo akili yetu tuliiwekeza kumfahamu, na bahati nzuri tuliweza kupata kupita ‘Fingerprint’(Alama za vidol) kwenye hii karatasi , ijapokuwa ilikuwa ngumu kutokana na karatasi hizi kushikwa na watu tofauti tofauti lakini ‘Fingerprint’ ya mara ya mwisho kushika hii nyaraka tuliweza kuitafuta kwenye mfumo wa ‘DataBase’ ya taifa na imeweza kutuletea jina la Suzzane Masanyika.
“Suzzane!!”
“Ndio Mfalme Pluto , Suzzane ni msaidizi wa karibu na alikuwa mwanasheria binafsi wa Marehemu Raheli na mpaka sasa anafanya kazi kama msaidizi binafsi wa Madam Persephone”Aliongea Diego na kumfanya Roma kukuna kichwa huku akionekana kuelewa.
“Mshawasiliana na huyu Suzzane?”
“Mfalme bado hatujawasiliana nae ila tunaamini anajua kila kitu , tulitaka kwanza mchango wako katika hili kabla ya kuendelea zaidi”
“Okey! Diego kama mnaamini majibu yote atakuwa nayo Suzzane basi mimi mwenyewe nitaongea nae, naamini alikuwa ananilenga mimi baada ya kuleta nyaraka hizi”Aliongea Roma na Diego alikubali..
Kwahio ripoti waliokuwa nayo wanajeshi hao haikuwa imekamilika bali iliishia kwa upande wa Roma Kwenda kuongea na Suzzane , Diego na Wenzake waliona sio vyema kwenda moja kwa moja kumhoji mfanyakazi wa karibu wa Edna pasipo kumhusisha Mfalme Pluto mwenyewe.
Roma akiwa kwenye gari akielekea nyumbani alikuwa na mawazo ya hapa na pale lakini mawazo ambayo yaliteka zaidi akili yake ni swala la Suzzane kuwa na nyaraka ya siri kama hio na kuamua kuileta kwake , kwa haraka haraka aliona huenda Suzzane alikuwa akijua mambo mengi zaidi ya yale ambayo yapo kwenye zile karatasi lakini hakuwa na namna ya kuzifanyia kazi.
Dakika kama hamsini hatimae Roma aliweza kuingiza gari yake ndani ya nyumba yao na muda ambao alikuwa akiingia ilikuwa ni saa moja moja hivi Kwenda na nusu.
Muda ambao Roma alifika ndio wakati ambao Edna alikuwa akitoka na Blandina mpaka eneo la Sebuleni kwa ajili ya kuongea kile alichokuwa akikifahamu kuhusu Raheli , mpaka akawa mpiga picha wa Raheli pamoja na Raisi Jeremy.
“Kuna nini kinaendelea, Edna mke wangu mbona macho yako mekundu?”Roma baada ya kuuliza vile Bi Wema alimpatia zile picha na Roma mara baada ya kuziangalia alifahamu sasa ni kipi kilikuwa kikiendelea.
SEHEMU YA 340.
Kwa maelezoo ya Blandina ni kwamba miaka Zaidi ya ishirini nyuma kabla ya kuzaliwa kwa Denisi ambaye ni Roma ndio kipindi ambacho Blandina aliweza kukutana na Raisi Jeremy pamoja na Raheli.
Blandina kipindi ambacho alikutana na Jeremy ni wakati alipomaliza masomo kwa ngazi ya Degree(Shahada) kwenye chuo cha Sydney, akichukua kozi ya Economics(Uchumi) na wakati huo huo kwa upande wa Raisi Senga akiwa mwaka wa mwisho wa masomo yake ya Shahada ya kwanza upande wa ‘Political’ (Siasa).
********
Raisi Kamau Kamau alisoma kwanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne katika shule ya kimataifa ya Braeburn ,katika kipindi chote hicho cha masomo rafiki yake mkubwa alikuwa ni Blandina mwanafunzi mrembo kutoka Tanzania , ukaribu wao ulikuwa mkubwa sana kiasi kwamba wanafunzi wengi waliamini walikuwa na mahusiano ya kimapenzi , lakini hilo halikuwa kweli kwani walikuwa ni marafikii tu wa karibu pasipo ya kuwa wapenzi kabisa mpaka wanamaliza kidato cha nne ndipo kwa mara ya kwanza Kamau Kamau akalala na Blandina siku ya mahafali yao.
Haikuwa ridhaa ya Blandina kulala na Kamau kutokana na kwamba kitendo hicho kilitokea baada ya Blandina kuwekewa dawa za usingizi na Kamau Kamau.
Kamau Kamau alikuwa akimpenda sana Blandina kimapenzi na sio kiurafiki , lakini kila alipokuwa akiweka hisia zake wazi kwa Blandina , mrembo huyo alikuwa akimchomolea huku akimwambia kwamba wabakie kuwa marafiki pekee , jambo ambalo Kamau Kamau hakuliafiki kabisa kwani licha ya kuendelea kuwa na urafiki na Blandina , kwenye akili yake alikuwa akipanga mengine, mipango yake ikaja kukamilika baada ya kumaliza kidato cha nne siku ya mahafali.
Tukio la kuwekewa dawa ya usingizi na kufanya mapenzi nje ya ridhaa yake na kupelekea kupoteza usichana wake lilimuuzi na kumuumiza sana Blandina na aliapia kwa majina yote hatokuja kumsamehe tena Kamau, lakini likawa swala la muda tu kwani baada ya wote Kwenda masomoni ngazi ya Shahada nchini Australia, Kamau Kamau ndio akatumia nafasi hio kuomba msamaha kwa Blandina na alifanya yote hayo kwakuwa alikuwa akimpenda Blandina sana.
Blandina kwakuwa alikuwa ugenini na mtu pekee aliekuwa akimfahamu alikuwa ni Kamau basi wakasameheana na kwanzia siku hio ndio mwanzo mpya wa kufanya mapenzi , huku Blandina akimwambia Kamau kwamba siku akipata mwanaume anaempenda wataachana, yaani kwa manenno marahisi Blandina alimchukulia Kamau kama ‘Sexmate’(Mgoni) wake tu(We sex with no String attached or friend with benefit).
Blandina alifanya hivyo kupunguza munkali wa kuhisia aliozokuwa nazo wakati akiwa masomoni wala hayakuwa mapenzi, alijitahidi sana kumpenda Kamau , lakini moyo wake ukagoma kabisa lakini kwa upande wa Kamau akatokea kumpenda sana Blandina.
Mwaka mmoja mbele yaani wakiwa mwaka wa pili ndio mwaka ambao sasa kamau aliweza kukutana na Senga ambaye alifika pia Australia kwa ajili ya masomo ya ngazi ya juu yaani Shahada.
Kamau akawa mwenyeji kwa Senga Kweka kipindi hicho na kutokana na kwamba walitokea kwenye nchi ambazo zinaunganishwa na lugha moja na ujirani , basi urafiki wao ukawa mkubwa sana kiasi kwamba kupitia urafiki huo ndio Kamau akamtambulisha Senga kwa Blandina.
Sasa alichokosea Kamau ni kumtambulisha Senga kwa Blandina kama wao ni marafiki tu na hakukuwa na la ziada , utambulisho huo ndio ukazaa hamasa ya Senga kuanza kumwangalia Blandina kwa macho ya kimapenzi , kadri siku zilivyokuwa zikienda Senga akatokea kumpenda sana Blandina , lakini haikuwa kwake tu hata kwa Blandina hivyo hivyo alitokea kumpenda Sana Senga , lakini hawakuweza kuambiana kwa kipindi hiko, kila mtu alificha hisia zake , huku upande wa Kamau pia akishangazwa na mabadiliko ya Blandina kwani hakupewa tena ‘Kitumbua’ na mrembo huyo wakati huo huo Blandina akionyesha sana kumjali Senga kuliko Kamau.
Baada ya miaka mitatu kupita ndio Raisi Kamau na Blandina wakamaliza masomo yao, huku kipindi hicho Senga yeye akiwa mwaka wa pili akiingia wa mwisho , Raisi Senga hakutaka kuzembea tena , hakutaka Blandina kurudi nchini Tanzania kabla ya kumweleza kile ambacho alikuwa akijisikia moyoni.
Siku ya mahafali ndio siku ambayo Senga akaweka wazi kile ambacho anajisikia na kumuomba Blandina wawe mapenzi , kwa upande wa Senga kusema ukweli ilikuwa ni kama kupiga bomu mochwari kwani Blandina kipindi hicho alikuwa amekufa na kuoza kwa Senga, hivyo alikubwaliwa siku hio hio bila kipingamizi na hatimae ikawa wiki moja tokea penzi lao kuanza.
“Senga nimeamua kubakia hapa hapa Australia nimepata kazi kwenye kampuni nataka nifanye nijipatie uzoefu kabla ya kurejea nchini Tanzania , nimeongea na baba na amenikubalia”Aliongea Blandina siku chache tu mara baada ya mapenzi yake na Senga kuanza , siku hio wakiwa kwenye ‘mtoko’ katika eneo maarufu la Sydeney Park wakilamba Ice Cream.
“Unasema kweli mpenzi , Daah ! Blandina siamini kabisa ni maamuzi sahihi umefanya , nilikuwa na huzuni unaniacha nakurudi Tanzania”Aliongea Senga akiwa amevalia shati lake la draft la mtumba ambalo alilinunua kwenye soko maarufu sana hapo Sydney. Usishangae sana hata Asutralia mitumba ipo kipindi hicho.
Taarifa hio ilimfurahisha sana Senga kwani alikuwa na huzuni mno kumwachia Blandina akirudi Tanzania hivyo aliikubali kwa mikono miwili maamuzi yake , upande wa Kamau baada ya kumaliza Shahada yake akarudi Kenya akimwacha Blandina Australia pasipo ya kujua mahusiano kati ya Blandina na Senga huku kichwani akiwa na mpango wa Kwenda kumchumbia Blandina mara baada tu ya kurudi Tanzania.
Blandina aliendelea kufanya kazi kwenye kampuni moja hapo Australia kwa ruhusa kutoka kwa familia yake huku Tanzania , sababu kubwa ikiwa ni kigezo cha kuongeza uzoefu , lakini haikuwa kweli nia ya kubaki Australia ilikuwa ni kuendelea kula raha na mpenzi wake Senga.
Baada ya Senga kumaliza masomo aliunganisha na ‘Masters’ hapo hapo chuoni mara baada ya kupata ufaulu mzuri , huku Blandina akiendelea na kazi.
Siku moja wakiwa kwenye fukwe ya Bondi ndio wakakutana na Raheli pamoja na Jeremy , kipindi hiki Jeremy hakuwa raisi bado bali alikuwa tayari alishaoa , ila mwanamke aliefika nae huko Australia kula bata alikuwa ni mrembo Raheli.
Kwahio urafiki wa Raisi Jeremy na Senga ulianzia Australia kwenye fukwe maarufu ya kipindi hicho ya Bondi , wakati huo huo Kamau na Senga wakifahamiana huko huko Australia.
Baada ya miaka yote ya masomo ya Senga kumalizika ndipo alipoweza kurudi nchini Tanzania , huku swala la kwanza baada ya kurudi ikawa ni kutaka kuoa na kuanza Maisha, jambo ambalo lilipingwa vikali sana na Afande kweka ambaye alikuwa baba yake.
Afande Kweka alitaka Senga ajiunge na jeshi mara moja ilikuendeleza ‘Legacy’ ya familia na kuacha na mambo yake ya kutaka kuoa mapema , lakini Senga akasimamia msimamo wake wa kutaka kuoa , huku akienda mbali kabisa hawezi kujiunga na jeshi, jambo hilo lilimkasirisha sana baba yake , kwani haya kuwa makubaliano yake na Senga.
Afande kweka alimtaka Senga akasome na akirudi ndio ajiunge na Jeshi lakini kutoka na Senga kukolewa na penzi la Blandina aligoma Kwenda Jeshini na akataka kuoa na hapo ndio wakatofautiana na baba yake na kufukuzwa nyumbani.
Senga hakuwa na tatizo alimchukua Blandina na wakahamia Rasmi Songea na wakaanza Maisha , huku Blandina akitumia utajiri wa nyumbani kwao kumnufaisha Senga kwani waliweza kufungua kampuni ya usafirishaji kwa kutumia mtaji ambao ulitolewa na Blandina.
Upande wa Raisi Kamau aliumia sana mara baada ya kusikia wawili hao wamefunga ndoa lakini kwakua alikuwa nchini Kenya kipindi hiko na Senga na Blandina walikuwa watanzania alishindwa kufanya chochote lakini kubwa Zaidi hakuwahi kuwa na mahusiano na Blandina licha ya kwamba walikuwa wakifanya ngono.
Raisi Kamau na yeye alioa mwanamke wa Kikuyu na kuanza Maisha na alipojaliwa Watoto wawili ndipo mke wake akafariki kwa ajali, kwahio Blandina alikuwa mke wa pili wa Raisi Kamau bala baada ya tukio la kupotea kwa ndege ya M-Airline.
Raisi Kamau hakuonyesha wazi chuki zake kwa Senga ila ukweli alikuwa akiungua sana na kumchukia kwa wakati mmoja na chuki ilizidi mara baada ya Blandina kumtamkia waziwazi kwamba alikuwa akimpenda Senga kufa kuzikana.
Baada ya miaka kadhaa kupita baada ya kupotea kwa ndege, Raisi Jeremy wa Rwanda akatumia maumivu ya Senga kumshawishi kujiunga na siasa ilikuwa na nguvu itakayomwezesha kulipiza kisasi juu ya njama iliofanyia kupoteza ndege ya M Airline.
Kipindi hicho kwakua Senga alikuwa kwenye maumivu makali ya kumpoteza mtoto wake Denisi pamoja na mke wake kipenzi Blandina , lakini pia mara baada ya Raisi Jeremy kumdokezea juu ya ajali ile ya ndege kuwa yakupangwa , basi iliamsha moto wa Raisi Senga kujiimarisha kwenye mambo ya siasa , huku akilini mwake akiwa na ile nia ya kutaka kulipiza kisasi kwa ajili ya Blandina na mtoto wake Denisi.
Upande wa Afande Kweka mara baada ya kuona Senga karudi kwake alimpa sapoti ya kutosha , huku akijiona mwamba kwani kila kilichokuwa kikiendelea kilikuwa ndani ya mipango wake alikuwa jasusi haswa mwenye Roho ngumu kwani licha ya mtoto wake kupitia kipindi kigumu yeye alikuwa akinywa kahawa kwa kutulia kabisa.
Kwanza kabisa ndie aliemtoa Denisi pamoja na Lorraine kafara kwa kuingiza kwenye mpango LADO, lakini wakati huo huo akihakikisha Blandina anaendelea kubakia nchini Kenya kwenye himaya ya Kamau, Afande Kweka hakumpenda Blandina kutokana na kwamba aliamini Senga alikuwa akipoteza mwelekeo kwa sababu yake, na ni kweli Senga kipindi hicho aliloea sana kwenye penzi la Blandina kiasi kwamba alikuwa akimuona Blandina kama ndio mzazi wake, alikuwa ni kama amewekewa Limbwata.
Edna alionekana kama hakuwa akiamini kile ambacho alikuwa amekisoma alibeba tena ile bahasha na kuangalia ndani kama kuna kitu kingine zaidi ya ile karatasi na ni kweli ndani yake kulikuwa na picha mbili.
Edna alizitoa na kuanza kuangalia moja moja na alijikuta akishika moyo wake , watu wawili waliokuwa kwenye picha ya pamoja alikuwa akiwajua, mmoja akiwa ni mama yake Raheli na mwingine akiwa ni Raisi Jeremy wa Rwanda, na katika pozi ambalo walikuwa wakionekana ni dhahiri kabisa walikuwa ni wapenzi.
Edna akili yake ilipata moto na sasa ni kama anakumbuka kwa mara nyingine kitabu cha mashairi ambacho mama yake alikuwa akikisoma mara kwa mara siku zote , kitabu ambacho ndani yake kulikuwa na picha ya mwanaume ambaye hakuitambua mara moja mara baada ya kuiona , lakini sasa kwa kupitia picha zilizokuwa kwenye mikono yake anatambua kuwa ile picha pia ilikuwa ni ya Raisi Jeremy na ni yeye ambaye alishindwa tu kuitambua.
Karatasi ambayo Edna alikuwa akiisoma , ilikuwa ikionyesha majibu ya DNA kati yake yeye na Jeremy Paul ambaye ni raisi wa Rwanda na majibu hayo ndio yaliomfanya Edna kutetemeka kwani ni swala ambalo hakuwaji kulitegemea kabisa.
“Kwahio baba yangu mzazi ni Raisi Jeremy wa Rwanda?”Alijiuliza Edna huku machozi yakianza kumtoka taratibu taratibu, picha mbalimbali zilikuwa zikipita kwenye akili yake na alishindwa hata kujielewa kwa wakati huo , Edna alikumbuka namna Maisha yake na baba yake Adebayo yalivyokuwa magumu na alijikuta moyo ukiuma.
Kila kitu sasa kilikuwa kipo wazi , Edna anatambua baba yake ni Raisi Jeremy wa Rwanda , lakini jambo moja ambalo anashindwa kufahamu ukweli wake ni juu ya kuzaliwa na pacha wake aliopewa jina la Lorraine.
Edna alikaa ndani ya chumba chake kwa takribani lisaa ndipo akili yake iliporudi na kufanya kazi na hapo hapo alimkumbuka Bi Wema , aliamini Bi Wema lazima atakuwa anaufahamu ukweli juu ya baba yake mzazi kwakuwa alimlea tokea akiwa amezaliwa.
Edna alitoka haraka haraka na kushuka chini kumtafuta Bi Wema ili kumuuliza maswali juu ya Jeremy Paul wa Rwanda kuwa mzazi wake huku mkononi akiwa ameshikilia picha zile mbili ambazo zilikuja ndani ya ile bahasha.
Bi Wema ndio aliekuwa wa kwanza kumuona Edna akiwa kwenye hali ambayo sio ya kawaida.
“Edna kuna shida gani , mbona unatokwa na machozi?”Aliuliza Bi Wema huku akimsogelea Edna ,kwa upande wa Blandina aliekuwa bize na kuandaa chakula moyo wake ulidunda aliamini tayari mwanae Rpma kashayakoroga tena.
Edna alimpatia Bi Wema zile picha na baada ya bibi huyo kuzipokea na kuangalia alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa wakati mmoja na mpaka hapo Edna alimuona Bi Wema alikuwa akijua swala hilo.
“Bi Wema huyu ndio baba yangu?”Aliuliza Edna kwa huzuni na swali lile lilimfanya na Blandina kumsogelea Bi Wema na kuchukua picha iliokuwa kwenye mikono yake.
Blandina mara baada ya kuona picha moja kati ya mbili , alijikuta na yeye akivuta pumzi , picha aliokuwa ameishikilia ilikuwa imepigwa eneo la ufukweni.
Edna baada ya kuona hata Mama Mkwe wake hashituki licha ya kuona picha hio , alijikuta akishangaa na kujiuliza maswali, hata Bi Wema alijikuta akiwa ni mwenye kushangaa kuona Blandina hakuwa ni mwenye kushangaa juu ya swala hilo.
“Mama hata wewe unafahamu hili?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi.
“Edna hio picha nilipiga mimi , hapo ni Sydney Australia Bondi Beach ni miaka mingi iliopita”Aliongea na kumfanya hata Bi wema kushangaa ni kama hakuwa amesikia vizuri.
*********
Ni muda wa saa kumi na nusu mchana , Roma alishaweza kufika ndani ya nyumba ambayo wanaishi wanajeshi wake wa The Eagles na muda huo Diego na Adeline walikuwa wameketi kwenye masofa wakiwa wanamuelezea Roma kuhusu ripoti juu ya uchunguzi walioufanya kuhusiana na kifo cha Raheli.
Kwa maelezo ya Diego ni kwamba waliweza kufanya uchunguzi kwa kudukua Barua pepe binafsi ya Raheli na katika kufatilia kwa ukaribu mawasiliano ya Email yake alionekana wiki kadhaa kabla ya kifo chake aliweza kufanya mawasiliano ya mara kwa mara na Dr Robert kutoka Marekani na mazungumzo yao yalionyesha yalikuwa ni ya mgonjwa na Daktari, yaani Robert akiwa ni daktari huku Raheli akiwa ni mgonjwa, Roma alishangazwa na maneno ya Diego.
“Diego kwahio kwa maneno yako unamaanisha kwamba Raheli alikuwa na daktari binafsi?”Aliuliza Roma.
“Ndio Mfalme Pluto ,ijapokuwa Raheli alikuwa akipatiwa matibabu na Dokta Hubery, dokta wa familia , lakini wakati huo huo alikuwa na dokta binafsi ambaye ni huyu Dokta Robert ,tumeweza kufatilia ‘Profile’ ya Dokta Robert na tumegundua ni daktari ndani ya hospitali ya kimafunzo ya Mayo Clinic Marekani”Aliongea Diego na Roma alitingisha kichwa kumpa ishara ya kuendelea.
“Tulifanya mawasiliano na wenzetu waliopo Marekani kwa ajili ya kutusaidia kumhoji Dokta Robert na jambo lilikuwa Rahisi kwani dokta Robert alitupa ushirikiano wa kutosha na aliweza kutupatia faili linalohusu matibabu ya Raheli na tumeweza kugundua Raheli alikuwa amewekewa sumu kwenye mwili wake”
“Sumu!!”Roma alishangaa.
“Ndio Mfalme pluto”
“Sumu ya aina gani na kwanini awekewe sumu?”Aliuliza Roma na kumfanya Deigo kumpa ishara Adeline aliekuwa pembeni yake.
“Kabla ya kufanya uchunguzi tulikuwa tukitumia ‘reference’ kutoka kwa taarifa aliotupatia Miss Christine inayohusiana na ‘Resurrection Fluid’(Kimiminika) na tuliweza kupata taarifa ya utafiti iliofanyika juu ya hiko kimiminika”Alinyamaza kisha akaendelea.
“Mfalme Pluto kupitia taarifa iliotoka taasisi ya Innova inaonyesha kwamba ‘Ressurection Fluid’ ikitumiwa kwa mtu ambaye yupo hai inageuka na kuwa sumu mwilini, hivyo kumpelekea mhusika kuanza kupata matatizo ya ogani za mwili kufeli taratibu taratibu , ukijaribu kufanananisha na ripoti ya Dokta Robert inaonyesha Bi Raheli mwili wake ulikuwa na sumu ambayo haikuwa ikifahamika bado na ilikosa ‘Antidote’ na hiko ndio kilipelekea kifo chake”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuvuta pumzi mpaka hapo alikuwa na uhakika kwamba sasa maneno ya Christine kwa Raheli kuhusishwa na majaribioa ya kisayansi ni ya kweli.
Antidote ni dawa inayotumika kuyeyusha sumu mwilini , sasa baada ya Resurrection Fluid kuwekwa kwenye mwili wa binadamu anaeishi inashindwa kufanya kazi na kugeuka kuwa sumu ambayo haina hio ‘Antidote’ hivyo kupelekea mtu kufa kwa matatizo mbalimbali , aidha moyo kufeli kufanya kazi au figo.
“Kwahio sasa kwanini Raheli akawa sehemu ya majaribio hayo?”
“Mfalme Pluto katika kufuatilia jumbe za ‘Email’ binafsi ya Raheli tumegundua pia Raheli alikuwa na adui ambaye alikuwa akimtumia jumbe za vitisho , ijapokuwa Email hio ililikuwa ikituma jumbe pasipo ya mtumaji kufahamika , lakini tuligundua ni maswala ya kimapenzi ndio yaliokuwa yakiendelea na Miss Raheli alikuwa akishutumiwa kwa kutoka kimapenzi na mume wa mtu inaonyesha mtu ambaye alikuwa akimtumia jumbe za vitisho alikuwa ni rafiki yake wa karibu na hii ilitufanya kufatilia Maisha ya nyuma ya Raheli na tuliweza kupata hizi picha kutoka chuo cha Durban South Afrika”Aliongea Diego na kumpatia picha Roma , katika picha hizo moja tu ndio Roma aliweza kuitambua na picha hio ilikuwa ni ya Raheli ,Roma ashawahikuona picha ya Raheli mara nyingi ndio maana ilikuwa rahisi kwake kuifahamu.
Kwa maelezo ya Diego picha hio ilikuwa ni ya wadada watatu ambao walipiga pamoja siku yao ya kuhitimu , wanadada hao walikuwa ni Raheli , Nahita na Kizwe mke wa Raisi Jeremy kutoka Rwanda.
“Mfalme Pluto angalia na hii picha”Aliongea Diego na kumpatia Roma picha ya mwanaume na mwanamke wakiwa kwenye pozi la kimahaba ,ilikuwa ni picha ya First Lady wa Rwanda na Raisi Kigombola na haikuhitajika elimu kubwa kugundua kilichokuwa kikiendelea ,wawili hao walionekana kuwa wapenzi.
“Mmeipataje hii?”
“Kuna mtu ametupatia Mfalme Pluto?”Aliongea Diego na kumfanya Roma kushangaa.
“Nani kawapatia?”
“Mfalme picha hizi tumeweza kuletewa na mtoto mmoja ambaye aliagizwa wiki iliopita siku ya ijumaa, hazikuja picha tu bali ilikuja bahasha yenye karatasi zingine na ndio ambazo ziliturahishia kuweza kujua kile ambacho kilikuwa kikiendelea, inaonekana mtu ambaye ametukabidhi hakutaka kufahamika , lakini kwa namna moja ama nyingine ni kama alikuwa akifahamu tunafanya uchunguzi unaohusiana na kifo cha Miss Raheli”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuomba ambiwe hizo karatasi zingine zinahusiana na nini.
Kwa maelezo ya Diego ni kwamba karatasi hizo zilikuwa zikielezea Siri inayohusiana na Maabara ya siri iliokuwa chini ya jengo la Bima ya Taifa, katika Ripoti hio ilionyesha kwamba majaribio ya ‘Resurection Fluid’ yalifanyikia ndani ya maabara hio kwa usimamizi wa kampuni ya Innova pamoja na Maya.
Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba majaribio yaliokuwa yakihusiana na Kimiminika yalifanyikia hapa Tanzania , hivyo taarifa ambayo waliweza kuletewa na mtu asiejulikana ilikuwa ni ya siri sana , mtu alieidhinisha utafiti huo ni Raisi Kigombola kwani sahihi yake ilionekana kwenye hio karatasi.
“Diego kwahio ripoti yenu mmeikamilishaje, nini kilipelekea na Raheli kuhusika kwenye majaribio haya?”
“Mfalme Pluto baada ya kuletewa hio Nyaraka tuliona hakuna sababu ya kufanya uchunguzi zaidi kwani majibu yote yapo kwa mtu alietufikishia hizi karatasi, hivyo akili yetu tuliiwekeza kumfahamu, na bahati nzuri tuliweza kupata kupita ‘Fingerprint’(Alama za vidol) kwenye hii karatasi , ijapokuwa ilikuwa ngumu kutokana na karatasi hizi kushikwa na watu tofauti tofauti lakini ‘Fingerprint’ ya mara ya mwisho kushika hii nyaraka tuliweza kuitafuta kwenye mfumo wa ‘DataBase’ ya taifa na imeweza kutuletea jina la Suzzane Masanyika.
“Suzzane!!”
“Ndio Mfalme Pluto , Suzzane ni msaidizi wa karibu na alikuwa mwanasheria binafsi wa Marehemu Raheli na mpaka sasa anafanya kazi kama msaidizi binafsi wa Madam Persephone”Aliongea Diego na kumfanya Roma kukuna kichwa huku akionekana kuelewa.
“Mshawasiliana na huyu Suzzane?”
“Mfalme bado hatujawasiliana nae ila tunaamini anajua kila kitu , tulitaka kwanza mchango wako katika hili kabla ya kuendelea zaidi”
“Okey! Diego kama mnaamini majibu yote atakuwa nayo Suzzane basi mimi mwenyewe nitaongea nae, naamini alikuwa ananilenga mimi baada ya kuleta nyaraka hizi”Aliongea Roma na Diego alikubali..
Kwahio ripoti waliokuwa nayo wanajeshi hao haikuwa imekamilika bali iliishia kwa upande wa Roma Kwenda kuongea na Suzzane , Diego na Wenzake waliona sio vyema kwenda moja kwa moja kumhoji mfanyakazi wa karibu wa Edna pasipo kumhusisha Mfalme Pluto mwenyewe.
Roma akiwa kwenye gari akielekea nyumbani alikuwa na mawazo ya hapa na pale lakini mawazo ambayo yaliteka zaidi akili yake ni swala la Suzzane kuwa na nyaraka ya siri kama hio na kuamua kuileta kwake , kwa haraka haraka aliona huenda Suzzane alikuwa akijua mambo mengi zaidi ya yale ambayo yapo kwenye zile karatasi lakini hakuwa na namna ya kuzifanyia kazi.
Dakika kama hamsini hatimae Roma aliweza kuingiza gari yake ndani ya nyumba yao na muda ambao alikuwa akiingia ilikuwa ni saa moja moja hivi Kwenda na nusu.
Muda ambao Roma alifika ndio wakati ambao Edna alikuwa akitoka na Blandina mpaka eneo la Sebuleni kwa ajili ya kuongea kile alichokuwa akikifahamu kuhusu Raheli , mpaka akawa mpiga picha wa Raheli pamoja na Raisi Jeremy.
“Kuna nini kinaendelea, Edna mke wangu mbona macho yako mekundu?”Roma baada ya kuuliza vile Bi Wema alimpatia zile picha na Roma mara baada ya kuziangalia alifahamu sasa ni kipi kilikuwa kikiendelea.
SEHEMU YA 340.
Kwa maelezoo ya Blandina ni kwamba miaka Zaidi ya ishirini nyuma kabla ya kuzaliwa kwa Denisi ambaye ni Roma ndio kipindi ambacho Blandina aliweza kukutana na Raisi Jeremy pamoja na Raheli.
Blandina kipindi ambacho alikutana na Jeremy ni wakati alipomaliza masomo kwa ngazi ya Degree(Shahada) kwenye chuo cha Sydney, akichukua kozi ya Economics(Uchumi) na wakati huo huo kwa upande wa Raisi Senga akiwa mwaka wa mwisho wa masomo yake ya Shahada ya kwanza upande wa ‘Political’ (Siasa).
********
Raisi Kamau Kamau alisoma kwanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne katika shule ya kimataifa ya Braeburn ,katika kipindi chote hicho cha masomo rafiki yake mkubwa alikuwa ni Blandina mwanafunzi mrembo kutoka Tanzania , ukaribu wao ulikuwa mkubwa sana kiasi kwamba wanafunzi wengi waliamini walikuwa na mahusiano ya kimapenzi , lakini hilo halikuwa kweli kwani walikuwa ni marafikii tu wa karibu pasipo ya kuwa wapenzi kabisa mpaka wanamaliza kidato cha nne ndipo kwa mara ya kwanza Kamau Kamau akalala na Blandina siku ya mahafali yao.
Haikuwa ridhaa ya Blandina kulala na Kamau kutokana na kwamba kitendo hicho kilitokea baada ya Blandina kuwekewa dawa za usingizi na Kamau Kamau.
Kamau Kamau alikuwa akimpenda sana Blandina kimapenzi na sio kiurafiki , lakini kila alipokuwa akiweka hisia zake wazi kwa Blandina , mrembo huyo alikuwa akimchomolea huku akimwambia kwamba wabakie kuwa marafiki pekee , jambo ambalo Kamau Kamau hakuliafiki kabisa kwani licha ya kuendelea kuwa na urafiki na Blandina , kwenye akili yake alikuwa akipanga mengine, mipango yake ikaja kukamilika baada ya kumaliza kidato cha nne siku ya mahafali.
Tukio la kuwekewa dawa ya usingizi na kufanya mapenzi nje ya ridhaa yake na kupelekea kupoteza usichana wake lilimuuzi na kumuumiza sana Blandina na aliapia kwa majina yote hatokuja kumsamehe tena Kamau, lakini likawa swala la muda tu kwani baada ya wote Kwenda masomoni ngazi ya Shahada nchini Australia, Kamau Kamau ndio akatumia nafasi hio kuomba msamaha kwa Blandina na alifanya yote hayo kwakuwa alikuwa akimpenda Blandina sana.
Blandina kwakuwa alikuwa ugenini na mtu pekee aliekuwa akimfahamu alikuwa ni Kamau basi wakasameheana na kwanzia siku hio ndio mwanzo mpya wa kufanya mapenzi , huku Blandina akimwambia Kamau kwamba siku akipata mwanaume anaempenda wataachana, yaani kwa manenno marahisi Blandina alimchukulia Kamau kama ‘Sexmate’(Mgoni) wake tu(We sex with no String attached or friend with benefit).
Blandina alifanya hivyo kupunguza munkali wa kuhisia aliozokuwa nazo wakati akiwa masomoni wala hayakuwa mapenzi, alijitahidi sana kumpenda Kamau , lakini moyo wake ukagoma kabisa lakini kwa upande wa Kamau akatokea kumpenda sana Blandina.
Mwaka mmoja mbele yaani wakiwa mwaka wa pili ndio mwaka ambao sasa kamau aliweza kukutana na Senga ambaye alifika pia Australia kwa ajili ya masomo ya ngazi ya juu yaani Shahada.
Kamau akawa mwenyeji kwa Senga Kweka kipindi hicho na kutokana na kwamba walitokea kwenye nchi ambazo zinaunganishwa na lugha moja na ujirani , basi urafiki wao ukawa mkubwa sana kiasi kwamba kupitia urafiki huo ndio Kamau akamtambulisha Senga kwa Blandina.
Sasa alichokosea Kamau ni kumtambulisha Senga kwa Blandina kama wao ni marafiki tu na hakukuwa na la ziada , utambulisho huo ndio ukazaa hamasa ya Senga kuanza kumwangalia Blandina kwa macho ya kimapenzi , kadri siku zilivyokuwa zikienda Senga akatokea kumpenda sana Blandina , lakini haikuwa kwake tu hata kwa Blandina hivyo hivyo alitokea kumpenda Sana Senga , lakini hawakuweza kuambiana kwa kipindi hiko, kila mtu alificha hisia zake , huku upande wa Kamau pia akishangazwa na mabadiliko ya Blandina kwani hakupewa tena ‘Kitumbua’ na mrembo huyo wakati huo huo Blandina akionyesha sana kumjali Senga kuliko Kamau.
Baada ya miaka mitatu kupita ndio Raisi Kamau na Blandina wakamaliza masomo yao, huku kipindi hicho Senga yeye akiwa mwaka wa pili akiingia wa mwisho , Raisi Senga hakutaka kuzembea tena , hakutaka Blandina kurudi nchini Tanzania kabla ya kumweleza kile ambacho alikuwa akijisikia moyoni.
Siku ya mahafali ndio siku ambayo Senga akaweka wazi kile ambacho anajisikia na kumuomba Blandina wawe mapenzi , kwa upande wa Senga kusema ukweli ilikuwa ni kama kupiga bomu mochwari kwani Blandina kipindi hicho alikuwa amekufa na kuoza kwa Senga, hivyo alikubwaliwa siku hio hio bila kipingamizi na hatimae ikawa wiki moja tokea penzi lao kuanza.
“Senga nimeamua kubakia hapa hapa Australia nimepata kazi kwenye kampuni nataka nifanye nijipatie uzoefu kabla ya kurejea nchini Tanzania , nimeongea na baba na amenikubalia”Aliongea Blandina siku chache tu mara baada ya mapenzi yake na Senga kuanza , siku hio wakiwa kwenye ‘mtoko’ katika eneo maarufu la Sydeney Park wakilamba Ice Cream.
“Unasema kweli mpenzi , Daah ! Blandina siamini kabisa ni maamuzi sahihi umefanya , nilikuwa na huzuni unaniacha nakurudi Tanzania”Aliongea Senga akiwa amevalia shati lake la draft la mtumba ambalo alilinunua kwenye soko maarufu sana hapo Sydney. Usishangae sana hata Asutralia mitumba ipo kipindi hicho.
Taarifa hio ilimfurahisha sana Senga kwani alikuwa na huzuni mno kumwachia Blandina akirudi Tanzania hivyo aliikubali kwa mikono miwili maamuzi yake , upande wa Kamau baada ya kumaliza Shahada yake akarudi Kenya akimwacha Blandina Australia pasipo ya kujua mahusiano kati ya Blandina na Senga huku kichwani akiwa na mpango wa Kwenda kumchumbia Blandina mara baada tu ya kurudi Tanzania.
Blandina aliendelea kufanya kazi kwenye kampuni moja hapo Australia kwa ruhusa kutoka kwa familia yake huku Tanzania , sababu kubwa ikiwa ni kigezo cha kuongeza uzoefu , lakini haikuwa kweli nia ya kubaki Australia ilikuwa ni kuendelea kula raha na mpenzi wake Senga.
Baada ya Senga kumaliza masomo aliunganisha na ‘Masters’ hapo hapo chuoni mara baada ya kupata ufaulu mzuri , huku Blandina akiendelea na kazi.
Siku moja wakiwa kwenye fukwe ya Bondi ndio wakakutana na Raheli pamoja na Jeremy , kipindi hiki Jeremy hakuwa raisi bado bali alikuwa tayari alishaoa , ila mwanamke aliefika nae huko Australia kula bata alikuwa ni mrembo Raheli.
Kwahio urafiki wa Raisi Jeremy na Senga ulianzia Australia kwenye fukwe maarufu ya kipindi hicho ya Bondi , wakati huo huo Kamau na Senga wakifahamiana huko huko Australia.
Baada ya miaka yote ya masomo ya Senga kumalizika ndipo alipoweza kurudi nchini Tanzania , huku swala la kwanza baada ya kurudi ikawa ni kutaka kuoa na kuanza Maisha, jambo ambalo lilipingwa vikali sana na Afande kweka ambaye alikuwa baba yake.
Afande Kweka alitaka Senga ajiunge na jeshi mara moja ilikuendeleza ‘Legacy’ ya familia na kuacha na mambo yake ya kutaka kuoa mapema , lakini Senga akasimamia msimamo wake wa kutaka kuoa , huku akienda mbali kabisa hawezi kujiunga na jeshi, jambo hilo lilimkasirisha sana baba yake , kwani haya kuwa makubaliano yake na Senga.
Afande kweka alimtaka Senga akasome na akirudi ndio ajiunge na Jeshi lakini kutoka na Senga kukolewa na penzi la Blandina aligoma Kwenda Jeshini na akataka kuoa na hapo ndio wakatofautiana na baba yake na kufukuzwa nyumbani.
Senga hakuwa na tatizo alimchukua Blandina na wakahamia Rasmi Songea na wakaanza Maisha , huku Blandina akitumia utajiri wa nyumbani kwao kumnufaisha Senga kwani waliweza kufungua kampuni ya usafirishaji kwa kutumia mtaji ambao ulitolewa na Blandina.
Upande wa Raisi Kamau aliumia sana mara baada ya kusikia wawili hao wamefunga ndoa lakini kwakua alikuwa nchini Kenya kipindi hiko na Senga na Blandina walikuwa watanzania alishindwa kufanya chochote lakini kubwa Zaidi hakuwahi kuwa na mahusiano na Blandina licha ya kwamba walikuwa wakifanya ngono.
Raisi Kamau na yeye alioa mwanamke wa Kikuyu na kuanza Maisha na alipojaliwa Watoto wawili ndipo mke wake akafariki kwa ajali, kwahio Blandina alikuwa mke wa pili wa Raisi Kamau bala baada ya tukio la kupotea kwa ndege ya M-Airline.
Raisi Kamau hakuonyesha wazi chuki zake kwa Senga ila ukweli alikuwa akiungua sana na kumchukia kwa wakati mmoja na chuki ilizidi mara baada ya Blandina kumtamkia waziwazi kwamba alikuwa akimpenda Senga kufa kuzikana.
Baada ya miaka kadhaa kupita baada ya kupotea kwa ndege, Raisi Jeremy wa Rwanda akatumia maumivu ya Senga kumshawishi kujiunga na siasa ilikuwa na nguvu itakayomwezesha kulipiza kisasi juu ya njama iliofanyia kupoteza ndege ya M Airline.
Kipindi hicho kwakua Senga alikuwa kwenye maumivu makali ya kumpoteza mtoto wake Denisi pamoja na mke wake kipenzi Blandina , lakini pia mara baada ya Raisi Jeremy kumdokezea juu ya ajali ile ya ndege kuwa yakupangwa , basi iliamsha moto wa Raisi Senga kujiimarisha kwenye mambo ya siasa , huku akilini mwake akiwa na ile nia ya kutaka kulipiza kisasi kwa ajili ya Blandina na mtoto wake Denisi.
Upande wa Afande Kweka mara baada ya kuona Senga karudi kwake alimpa sapoti ya kutosha , huku akijiona mwamba kwani kila kilichokuwa kikiendelea kilikuwa ndani ya mipango wake alikuwa jasusi haswa mwenye Roho ngumu kwani licha ya mtoto wake kupitia kipindi kigumu yeye alikuwa akinywa kahawa kwa kutulia kabisa.
Kwanza kabisa ndie aliemtoa Denisi pamoja na Lorraine kafara kwa kuingiza kwenye mpango LADO, lakini wakati huo huo akihakikisha Blandina anaendelea kubakia nchini Kenya kwenye himaya ya Kamau, Afande Kweka hakumpenda Blandina kutokana na kwamba aliamini Senga alikuwa akipoteza mwelekeo kwa sababu yake, na ni kweli Senga kipindi hicho aliloea sana kwenye penzi la Blandina kiasi kwamba alikuwa akimuona Blandina kama ndio mzazi wake, alikuwa ni kama amewekewa Limbwata.