Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 339

Edna alionekana kama hakuwa akiamini kile ambacho alikuwa amekisoma alibeba tena ile bahasha na kuangalia ndani kama kuna kitu kingine zaidi ya ile karatasi na ni kweli ndani yake kulikuwa na picha mbili.

Edna alizitoa na kuanza kuangalia moja moja na alijikuta akishika moyo wake , watu wawili waliokuwa kwenye picha ya pamoja alikuwa akiwajua, mmoja akiwa ni mama yake Raheli na mwingine akiwa ni Raisi Jeremy wa Rwanda, na katika pozi ambalo walikuwa wakionekana ni dhahiri kabisa walikuwa ni wapenzi.

Edna akili yake ilipata moto na sasa ni kama anakumbuka kwa mara nyingine kitabu cha mashairi ambacho mama yake alikuwa akikisoma mara kwa mara siku zote , kitabu ambacho ndani yake kulikuwa na picha ya mwanaume ambaye hakuitambua mara moja mara baada ya kuiona , lakini sasa kwa kupitia picha zilizokuwa kwenye mikono yake anatambua kuwa ile picha pia ilikuwa ni ya Raisi Jeremy na ni yeye ambaye alishindwa tu kuitambua.

Karatasi ambayo Edna alikuwa akiisoma , ilikuwa ikionyesha majibu ya DNA kati yake yeye na Jeremy Paul ambaye ni raisi wa Rwanda na majibu hayo ndio yaliomfanya Edna kutetemeka kwani ni swala ambalo hakuwaji kulitegemea kabisa.

“Kwahio baba yangu mzazi ni Raisi Jeremy wa Rwanda?”Alijiuliza Edna huku machozi yakianza kumtoka taratibu taratibu, picha mbalimbali zilikuwa zikipita kwenye akili yake na alishindwa hata kujielewa kwa wakati huo , Edna alikumbuka namna Maisha yake na baba yake Adebayo yalivyokuwa magumu na alijikuta moyo ukiuma.

Kila kitu sasa kilikuwa kipo wazi , Edna anatambua baba yake ni Raisi Jeremy wa Rwanda , lakini jambo moja ambalo anashindwa kufahamu ukweli wake ni juu ya kuzaliwa na pacha wake aliopewa jina la Lorraine.

Edna alikaa ndani ya chumba chake kwa takribani lisaa ndipo akili yake iliporudi na kufanya kazi na hapo hapo alimkumbuka Bi Wema , aliamini Bi Wema lazima atakuwa anaufahamu ukweli juu ya baba yake mzazi kwakuwa alimlea tokea akiwa amezaliwa.

Edna alitoka haraka haraka na kushuka chini kumtafuta Bi Wema ili kumuuliza maswali juu ya Jeremy Paul wa Rwanda kuwa mzazi wake huku mkononi akiwa ameshikilia picha zile mbili ambazo zilikuja ndani ya ile bahasha.

Bi Wema ndio aliekuwa wa kwanza kumuona Edna akiwa kwenye hali ambayo sio ya kawaida.

“Edna kuna shida gani , mbona unatokwa na machozi?”Aliuliza Bi Wema huku akimsogelea Edna ,kwa upande wa Blandina aliekuwa bize na kuandaa chakula moyo wake ulidunda aliamini tayari mwanae Rpma kashayakoroga tena.

Edna alimpatia Bi Wema zile picha na baada ya bibi huyo kuzipokea na kuangalia alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa wakati mmoja na mpaka hapo Edna alimuona Bi Wema alikuwa akijua swala hilo.

“Bi Wema huyu ndio baba yangu?”Aliuliza Edna kwa huzuni na swali lile lilimfanya na Blandina kumsogelea Bi Wema na kuchukua picha iliokuwa kwenye mikono yake.

Blandina mara baada ya kuona picha moja kati ya mbili , alijikuta na yeye akivuta pumzi , picha aliokuwa ameishikilia ilikuwa imepigwa eneo la ufukweni.

Edna baada ya kuona hata Mama Mkwe wake hashituki licha ya kuona picha hio , alijikuta akishangaa na kujiuliza maswali, hata Bi Wema alijikuta akiwa ni mwenye kushangaa kuona Blandina hakuwa ni mwenye kushangaa juu ya swala hilo.

“Mama hata wewe unafahamu hili?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi.

“Edna hio picha nilipiga mimi , hapo ni Sydney Australia Bondi Beach ni miaka mingi iliopita”Aliongea na kumfanya hata Bi wema kushangaa ni kama hakuwa amesikia vizuri.

*********

Ni muda wa saa kumi na nusu mchana , Roma alishaweza kufika ndani ya nyumba ambayo wanaishi wanajeshi wake wa The Eagles na muda huo Diego na Adeline walikuwa wameketi kwenye masofa wakiwa wanamuelezea Roma kuhusu ripoti juu ya uchunguzi walioufanya kuhusiana na kifo cha Raheli.

Kwa maelezo ya Diego ni kwamba waliweza kufanya uchunguzi kwa kudukua Barua pepe binafsi ya Raheli na katika kufatilia kwa ukaribu mawasiliano ya Email yake alionekana wiki kadhaa kabla ya kifo chake aliweza kufanya mawasiliano ya mara kwa mara na Dr Robert kutoka Marekani na mazungumzo yao yalionyesha yalikuwa ni ya mgonjwa na Daktari, yaani Robert akiwa ni daktari huku Raheli akiwa ni mgonjwa, Roma alishangazwa na maneno ya Diego.

“Diego kwahio kwa maneno yako unamaanisha kwamba Raheli alikuwa na daktari binafsi?”Aliuliza Roma.

“Ndio Mfalme Pluto ,ijapokuwa Raheli alikuwa akipatiwa matibabu na Dokta Hubery, dokta wa familia , lakini wakati huo huo alikuwa na dokta binafsi ambaye ni huyu Dokta Robert ,tumeweza kufatilia ‘Profile’ ya Dokta Robert na tumegundua ni daktari ndani ya hospitali ya kimafunzo ya Mayo Clinic Marekani”Aliongea Diego na Roma alitingisha kichwa kumpa ishara ya kuendelea.

“Tulifanya mawasiliano na wenzetu waliopo Marekani kwa ajili ya kutusaidia kumhoji Dokta Robert na jambo lilikuwa Rahisi kwani dokta Robert alitupa ushirikiano wa kutosha na aliweza kutupatia faili linalohusu matibabu ya Raheli na tumeweza kugundua Raheli alikuwa amewekewa sumu kwenye mwili wake”

“Sumu!!”Roma alishangaa.

“Ndio Mfalme pluto”

“Sumu ya aina gani na kwanini awekewe sumu?”Aliuliza Roma na kumfanya Deigo kumpa ishara Adeline aliekuwa pembeni yake.

“Kabla ya kufanya uchunguzi tulikuwa tukitumia ‘reference’ kutoka kwa taarifa aliotupatia Miss Christine inayohusiana na ‘Resurrection Fluid’(Kimiminika) na tuliweza kupata taarifa ya utafiti iliofanyika juu ya hiko kimiminika”Alinyamaza kisha akaendelea.

“Mfalme Pluto kupitia taarifa iliotoka taasisi ya Innova inaonyesha kwamba ‘Ressurection Fluid’ ikitumiwa kwa mtu ambaye yupo hai inageuka na kuwa sumu mwilini, hivyo kumpelekea mhusika kuanza kupata matatizo ya ogani za mwili kufeli taratibu taratibu , ukijaribu kufanananisha na ripoti ya Dokta Robert inaonyesha Bi Raheli mwili wake ulikuwa na sumu ambayo haikuwa ikifahamika bado na ilikosa ‘Antidote’ na hiko ndio kilipelekea kifo chake”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuvuta pumzi mpaka hapo alikuwa na uhakika kwamba sasa maneno ya Christine kwa Raheli kuhusishwa na majaribioa ya kisayansi ni ya kweli.

Antidote ni dawa inayotumika kuyeyusha sumu mwilini , sasa baada ya Resurrection Fluid kuwekwa kwenye mwili wa binadamu anaeishi inashindwa kufanya kazi na kugeuka kuwa sumu ambayo haina hio ‘Antidote’ hivyo kupelekea mtu kufa kwa matatizo mbalimbali , aidha moyo kufeli kufanya kazi au figo.

“Kwahio sasa kwanini Raheli akawa sehemu ya majaribio hayo?”

“Mfalme Pluto katika kufuatilia jumbe za ‘Email’ binafsi ya Raheli tumegundua pia Raheli alikuwa na adui ambaye alikuwa akimtumia jumbe za vitisho , ijapokuwa Email hio ililikuwa ikituma jumbe pasipo ya mtumaji kufahamika , lakini tuligundua ni maswala ya kimapenzi ndio yaliokuwa yakiendelea na Miss Raheli alikuwa akishutumiwa kwa kutoka kimapenzi na mume wa mtu inaonyesha mtu ambaye alikuwa akimtumia jumbe za vitisho alikuwa ni rafiki yake wa karibu na hii ilitufanya kufatilia Maisha ya nyuma ya Raheli na tuliweza kupata hizi picha kutoka chuo cha Durban South Afrika”Aliongea Diego na kumpatia picha Roma , katika picha hizo moja tu ndio Roma aliweza kuitambua na picha hio ilikuwa ni ya Raheli ,Roma ashawahikuona picha ya Raheli mara nyingi ndio maana ilikuwa rahisi kwake kuifahamu.

Kwa maelezo ya Diego picha hio ilikuwa ni ya wadada watatu ambao walipiga pamoja siku yao ya kuhitimu , wanadada hao walikuwa ni Raheli , Nahita na Kizwe mke wa Raisi Jeremy kutoka Rwanda.

“Mfalme Pluto angalia na hii picha”Aliongea Diego na kumpatia Roma picha ya mwanaume na mwanamke wakiwa kwenye pozi la kimahaba ,ilikuwa ni picha ya First Lady wa Rwanda na Raisi Kigombola na haikuhitajika elimu kubwa kugundua kilichokuwa kikiendelea ,wawili hao walionekana kuwa wapenzi.

“Mmeipataje hii?”

“Kuna mtu ametupatia Mfalme Pluto?”Aliongea Diego na kumfanya Roma kushangaa.

“Nani kawapatia?”

“Mfalme picha hizi tumeweza kuletewa na mtoto mmoja ambaye aliagizwa wiki iliopita siku ya ijumaa, hazikuja picha tu bali ilikuja bahasha yenye karatasi zingine na ndio ambazo ziliturahishia kuweza kujua kile ambacho kilikuwa kikiendelea, inaonekana mtu ambaye ametukabidhi hakutaka kufahamika , lakini kwa namna moja ama nyingine ni kama alikuwa akifahamu tunafanya uchunguzi unaohusiana na kifo cha Miss Raheli”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuomba ambiwe hizo karatasi zingine zinahusiana na nini.

Kwa maelezo ya Diego ni kwamba karatasi hizo zilikuwa zikielezea Siri inayohusiana na Maabara ya siri iliokuwa chini ya jengo la Bima ya Taifa, katika Ripoti hio ilionyesha kwamba majaribio ya ‘Resurection Fluid’ yalifanyikia ndani ya maabara hio kwa usimamizi wa kampuni ya Innova pamoja na Maya.

Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba majaribio yaliokuwa yakihusiana na Kimiminika yalifanyikia hapa Tanzania , hivyo taarifa ambayo waliweza kuletewa na mtu asiejulikana ilikuwa ni ya siri sana , mtu alieidhinisha utafiti huo ni Raisi Kigombola kwani sahihi yake ilionekana kwenye hio karatasi.

“Diego kwahio ripoti yenu mmeikamilishaje, nini kilipelekea na Raheli kuhusika kwenye majaribio haya?”

“Mfalme Pluto baada ya kuletewa hio Nyaraka tuliona hakuna sababu ya kufanya uchunguzi zaidi kwani majibu yote yapo kwa mtu alietufikishia hizi karatasi, hivyo akili yetu tuliiwekeza kumfahamu, na bahati nzuri tuliweza kupata kupita ‘Fingerprint’(Alama za vidol) kwenye hii karatasi , ijapokuwa ilikuwa ngumu kutokana na karatasi hizi kushikwa na watu tofauti tofauti lakini ‘Fingerprint’ ya mara ya mwisho kushika hii nyaraka tuliweza kuitafuta kwenye mfumo wa ‘DataBase’ ya taifa na imeweza kutuletea jina la Suzzane Masanyika.

“Suzzane!!”

“Ndio Mfalme Pluto , Suzzane ni msaidizi wa karibu na alikuwa mwanasheria binafsi wa Marehemu Raheli na mpaka sasa anafanya kazi kama msaidizi binafsi wa Madam Persephone”Aliongea Diego na kumfanya Roma kukuna kichwa huku akionekana kuelewa.

“Mshawasiliana na huyu Suzzane?”

“Mfalme bado hatujawasiliana nae ila tunaamini anajua kila kitu , tulitaka kwanza mchango wako katika hili kabla ya kuendelea zaidi”

“Okey! Diego kama mnaamini majibu yote atakuwa nayo Suzzane basi mimi mwenyewe nitaongea nae, naamini alikuwa ananilenga mimi baada ya kuleta nyaraka hizi”Aliongea Roma na Diego alikubali..

Kwahio ripoti waliokuwa nayo wanajeshi hao haikuwa imekamilika bali iliishia kwa upande wa Roma Kwenda kuongea na Suzzane , Diego na Wenzake waliona sio vyema kwenda moja kwa moja kumhoji mfanyakazi wa karibu wa Edna pasipo kumhusisha Mfalme Pluto mwenyewe.

Roma akiwa kwenye gari akielekea nyumbani alikuwa na mawazo ya hapa na pale lakini mawazo ambayo yaliteka zaidi akili yake ni swala la Suzzane kuwa na nyaraka ya siri kama hio na kuamua kuileta kwake , kwa haraka haraka aliona huenda Suzzane alikuwa akijua mambo mengi zaidi ya yale ambayo yapo kwenye zile karatasi lakini hakuwa na namna ya kuzifanyia kazi.

Dakika kama hamsini hatimae Roma aliweza kuingiza gari yake ndani ya nyumba yao na muda ambao alikuwa akiingia ilikuwa ni saa moja moja hivi Kwenda na nusu.

Muda ambao Roma alifika ndio wakati ambao Edna alikuwa akitoka na Blandina mpaka eneo la Sebuleni kwa ajili ya kuongea kile alichokuwa akikifahamu kuhusu Raheli , mpaka akawa mpiga picha wa Raheli pamoja na Raisi Jeremy.

“Kuna nini kinaendelea, Edna mke wangu mbona macho yako mekundu?”Roma baada ya kuuliza vile Bi Wema alimpatia zile picha na Roma mara baada ya kuziangalia alifahamu sasa ni kipi kilikuwa kikiendelea.







SEHEMU YA 340.

Kwa maelezoo ya Blandina ni kwamba miaka Zaidi ya ishirini nyuma kabla ya kuzaliwa kwa Denisi ambaye ni Roma ndio kipindi ambacho Blandina aliweza kukutana na Raisi Jeremy pamoja na Raheli.

Blandina kipindi ambacho alikutana na Jeremy ni wakati alipomaliza masomo kwa ngazi ya Degree(Shahada) kwenye chuo cha Sydney, akichukua kozi ya Economics(Uchumi) na wakati huo huo kwa upande wa Raisi Senga akiwa mwaka wa mwisho wa masomo yake ya Shahada ya kwanza upande wa ‘Political’ (Siasa).

********

Raisi Kamau Kamau alisoma kwanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne katika shule ya kimataifa ya Braeburn ,katika kipindi chote hicho cha masomo rafiki yake mkubwa alikuwa ni Blandina mwanafunzi mrembo kutoka Tanzania , ukaribu wao ulikuwa mkubwa sana kiasi kwamba wanafunzi wengi waliamini walikuwa na mahusiano ya kimapenzi , lakini hilo halikuwa kweli kwani walikuwa ni marafikii tu wa karibu pasipo ya kuwa wapenzi kabisa mpaka wanamaliza kidato cha nne ndipo kwa mara ya kwanza Kamau Kamau akalala na Blandina siku ya mahafali yao.

Haikuwa ridhaa ya Blandina kulala na Kamau kutokana na kwamba kitendo hicho kilitokea baada ya Blandina kuwekewa dawa za usingizi na Kamau Kamau.

Kamau Kamau alikuwa akimpenda sana Blandina kimapenzi na sio kiurafiki , lakini kila alipokuwa akiweka hisia zake wazi kwa Blandina , mrembo huyo alikuwa akimchomolea huku akimwambia kwamba wabakie kuwa marafiki pekee , jambo ambalo Kamau Kamau hakuliafiki kabisa kwani licha ya kuendelea kuwa na urafiki na Blandina , kwenye akili yake alikuwa akipanga mengine, mipango yake ikaja kukamilika baada ya kumaliza kidato cha nne siku ya mahafali.

Tukio la kuwekewa dawa ya usingizi na kufanya mapenzi nje ya ridhaa yake na kupelekea kupoteza usichana wake lilimuuzi na kumuumiza sana Blandina na aliapia kwa majina yote hatokuja kumsamehe tena Kamau, lakini likawa swala la muda tu kwani baada ya wote Kwenda masomoni ngazi ya Shahada nchini Australia, Kamau Kamau ndio akatumia nafasi hio kuomba msamaha kwa Blandina na alifanya yote hayo kwakuwa alikuwa akimpenda Blandina sana.

Blandina kwakuwa alikuwa ugenini na mtu pekee aliekuwa akimfahamu alikuwa ni Kamau basi wakasameheana na kwanzia siku hio ndio mwanzo mpya wa kufanya mapenzi , huku Blandina akimwambia Kamau kwamba siku akipata mwanaume anaempenda wataachana, yaani kwa manenno marahisi Blandina alimchukulia Kamau kama ‘Sexmate’(Mgoni) wake tu(We sex with no String attached or friend with benefit).

Blandina alifanya hivyo kupunguza munkali wa kuhisia aliozokuwa nazo wakati akiwa masomoni wala hayakuwa mapenzi, alijitahidi sana kumpenda Kamau , lakini moyo wake ukagoma kabisa lakini kwa upande wa Kamau akatokea kumpenda sana Blandina.

Mwaka mmoja mbele yaani wakiwa mwaka wa pili ndio mwaka ambao sasa kamau aliweza kukutana na Senga ambaye alifika pia Australia kwa ajili ya masomo ya ngazi ya juu yaani Shahada.

Kamau akawa mwenyeji kwa Senga Kweka kipindi hicho na kutokana na kwamba walitokea kwenye nchi ambazo zinaunganishwa na lugha moja na ujirani , basi urafiki wao ukawa mkubwa sana kiasi kwamba kupitia urafiki huo ndio Kamau akamtambulisha Senga kwa Blandina.

Sasa alichokosea Kamau ni kumtambulisha Senga kwa Blandina kama wao ni marafiki tu na hakukuwa na la ziada , utambulisho huo ndio ukazaa hamasa ya Senga kuanza kumwangalia Blandina kwa macho ya kimapenzi , kadri siku zilivyokuwa zikienda Senga akatokea kumpenda sana Blandina , lakini haikuwa kwake tu hata kwa Blandina hivyo hivyo alitokea kumpenda Sana Senga , lakini hawakuweza kuambiana kwa kipindi hiko, kila mtu alificha hisia zake , huku upande wa Kamau pia akishangazwa na mabadiliko ya Blandina kwani hakupewa tena ‘Kitumbua’ na mrembo huyo wakati huo huo Blandina akionyesha sana kumjali Senga kuliko Kamau.

Baada ya miaka mitatu kupita ndio Raisi Kamau na Blandina wakamaliza masomo yao, huku kipindi hicho Senga yeye akiwa mwaka wa pili akiingia wa mwisho , Raisi Senga hakutaka kuzembea tena , hakutaka Blandina kurudi nchini Tanzania kabla ya kumweleza kile ambacho alikuwa akijisikia moyoni.

Siku ya mahafali ndio siku ambayo Senga akaweka wazi kile ambacho anajisikia na kumuomba Blandina wawe mapenzi , kwa upande wa Senga kusema ukweli ilikuwa ni kama kupiga bomu mochwari kwani Blandina kipindi hicho alikuwa amekufa na kuoza kwa Senga, hivyo alikubwaliwa siku hio hio bila kipingamizi na hatimae ikawa wiki moja tokea penzi lao kuanza.

“Senga nimeamua kubakia hapa hapa Australia nimepata kazi kwenye kampuni nataka nifanye nijipatie uzoefu kabla ya kurejea nchini Tanzania , nimeongea na baba na amenikubalia”Aliongea Blandina siku chache tu mara baada ya mapenzi yake na Senga kuanza , siku hio wakiwa kwenye ‘mtoko’ katika eneo maarufu la Sydeney Park wakilamba Ice Cream.

“Unasema kweli mpenzi , Daah ! Blandina siamini kabisa ni maamuzi sahihi umefanya , nilikuwa na huzuni unaniacha nakurudi Tanzania”Aliongea Senga akiwa amevalia shati lake la draft la mtumba ambalo alilinunua kwenye soko maarufu sana hapo Sydney. Usishangae sana hata Asutralia mitumba ipo kipindi hicho.

Taarifa hio ilimfurahisha sana Senga kwani alikuwa na huzuni mno kumwachia Blandina akirudi Tanzania hivyo aliikubali kwa mikono miwili maamuzi yake , upande wa Kamau baada ya kumaliza Shahada yake akarudi Kenya akimwacha Blandina Australia pasipo ya kujua mahusiano kati ya Blandina na Senga huku kichwani akiwa na mpango wa Kwenda kumchumbia Blandina mara baada tu ya kurudi Tanzania.

Blandina aliendelea kufanya kazi kwenye kampuni moja hapo Australia kwa ruhusa kutoka kwa familia yake huku Tanzania , sababu kubwa ikiwa ni kigezo cha kuongeza uzoefu , lakini haikuwa kweli nia ya kubaki Australia ilikuwa ni kuendelea kula raha na mpenzi wake Senga.

Baada ya Senga kumaliza masomo aliunganisha na ‘Masters’ hapo hapo chuoni mara baada ya kupata ufaulu mzuri , huku Blandina akiendelea na kazi.

Siku moja wakiwa kwenye fukwe ya Bondi ndio wakakutana na Raheli pamoja na Jeremy , kipindi hiki Jeremy hakuwa raisi bado bali alikuwa tayari alishaoa , ila mwanamke aliefika nae huko Australia kula bata alikuwa ni mrembo Raheli.

Kwahio urafiki wa Raisi Jeremy na Senga ulianzia Australia kwenye fukwe maarufu ya kipindi hicho ya Bondi , wakati huo huo Kamau na Senga wakifahamiana huko huko Australia.

Baada ya miaka yote ya masomo ya Senga kumalizika ndipo alipoweza kurudi nchini Tanzania , huku swala la kwanza baada ya kurudi ikawa ni kutaka kuoa na kuanza Maisha, jambo ambalo lilipingwa vikali sana na Afande kweka ambaye alikuwa baba yake.

Afande Kweka alitaka Senga ajiunge na jeshi mara moja ilikuendeleza ‘Legacy’ ya familia na kuacha na mambo yake ya kutaka kuoa mapema , lakini Senga akasimamia msimamo wake wa kutaka kuoa , huku akienda mbali kabisa hawezi kujiunga na jeshi, jambo hilo lilimkasirisha sana baba yake , kwani haya kuwa makubaliano yake na Senga.

Afande kweka alimtaka Senga akasome na akirudi ndio ajiunge na Jeshi lakini kutoka na Senga kukolewa na penzi la Blandina aligoma Kwenda Jeshini na akataka kuoa na hapo ndio wakatofautiana na baba yake na kufukuzwa nyumbani.

Senga hakuwa na tatizo alimchukua Blandina na wakahamia Rasmi Songea na wakaanza Maisha , huku Blandina akitumia utajiri wa nyumbani kwao kumnufaisha Senga kwani waliweza kufungua kampuni ya usafirishaji kwa kutumia mtaji ambao ulitolewa na Blandina.

Upande wa Raisi Kamau aliumia sana mara baada ya kusikia wawili hao wamefunga ndoa lakini kwakua alikuwa nchini Kenya kipindi hiko na Senga na Blandina walikuwa watanzania alishindwa kufanya chochote lakini kubwa Zaidi hakuwahi kuwa na mahusiano na Blandina licha ya kwamba walikuwa wakifanya ngono.

Raisi Kamau na yeye alioa mwanamke wa Kikuyu na kuanza Maisha na alipojaliwa Watoto wawili ndipo mke wake akafariki kwa ajali, kwahio Blandina alikuwa mke wa pili wa Raisi Kamau bala baada ya tukio la kupotea kwa ndege ya M-Airline.

Raisi Kamau hakuonyesha wazi chuki zake kwa Senga ila ukweli alikuwa akiungua sana na kumchukia kwa wakati mmoja na chuki ilizidi mara baada ya Blandina kumtamkia waziwazi kwamba alikuwa akimpenda Senga kufa kuzikana.

Baada ya miaka kadhaa kupita baada ya kupotea kwa ndege, Raisi Jeremy wa Rwanda akatumia maumivu ya Senga kumshawishi kujiunga na siasa ilikuwa na nguvu itakayomwezesha kulipiza kisasi juu ya njama iliofanyia kupoteza ndege ya M Airline.

Kipindi hicho kwakua Senga alikuwa kwenye maumivu makali ya kumpoteza mtoto wake Denisi pamoja na mke wake kipenzi Blandina , lakini pia mara baada ya Raisi Jeremy kumdokezea juu ya ajali ile ya ndege kuwa yakupangwa , basi iliamsha moto wa Raisi Senga kujiimarisha kwenye mambo ya siasa , huku akilini mwake akiwa na ile nia ya kutaka kulipiza kisasi kwa ajili ya Blandina na mtoto wake Denisi.

Upande wa Afande Kweka mara baada ya kuona Senga karudi kwake alimpa sapoti ya kutosha , huku akijiona mwamba kwani kila kilichokuwa kikiendelea kilikuwa ndani ya mipango wake alikuwa jasusi haswa mwenye Roho ngumu kwani licha ya mtoto wake kupitia kipindi kigumu yeye alikuwa akinywa kahawa kwa kutulia kabisa.

Kwanza kabisa ndie aliemtoa Denisi pamoja na Lorraine kafara kwa kuingiza kwenye mpango LADO, lakini wakati huo huo akihakikisha Blandina anaendelea kubakia nchini Kenya kwenye himaya ya Kamau, Afande Kweka hakumpenda Blandina kutokana na kwamba aliamini Senga alikuwa akipoteza mwelekeo kwa sababu yake, na ni kweli Senga kipindi hicho aliloea sana kwenye penzi la Blandina kiasi kwamba alikuwa akimuona Blandina kama ndio mzazi wake, alikuwa ni kama amewekewa Limbwata.
 
SEHEMU YA 341.

Edna sasa alielewa kwanini Blandina alisema kwamba picha hio alikuwa amepiga yeye, kumbe alishawahi kukutana na Raisi Jeremy huko Australia akiwa na mama yake wakila bata.

Roma mwenyewe alishangaa kumbe mama yake ni msomi mkubwa tu, lakini hata hivyo ilikuwa ni halali kabisa, kwani mambo ambayo Blandina aliweza kuyafanya kwa jamii kupitia sura ya Maina yalikuwa makubwa sana, kwani kama utaweza kupiga hesabu ya thamani ya vituo vyote ambavyo alivianzisha kwa nguvu zake ni Zaidi ya Dollar milioni mia moja.

Upande wa Roma yeye hakushangaa sana kwani alikua akijua mzazi wa Edna , ila mbele ya Edana alijifanyisha na yeye kushangaa , kwani alijua kama atasema alikuwa akifahamu na akakaa kimya , Edna angekasirika.

Maelezo ya Bi Wema hayakuwa na utofauti sana, kwani alishaelezwa na Raheli mwenyewe juu ya baba mzazi wa Edna, lakini sasa jumla yao wote wakajiuliza swali moja ni nani ambaye ameleta taarifa hio, na ni kwa madhumuni yapi, upande wa Roma aliamini sio Raisi Jeremy alieleta hio karatasi aliamini kuna mtu mwingine ambaye ameleta barua hio ila hakujua sababu ni nini na aliajiambia ni swala la muda tu atafahamu.

Edna sasa anajikuta akianza kuhisi huenda hata mtu aliekuwa akijiita The Protector alikuwa ni Raisi Jeremy , kwani mambo mengi ambayo aliokuwa akimsiadia yalikuwa yakihataji intelijensia ya hali ya juu.

Licha ya kwamba alihuzunishwa na jambo hilo , aliona mama yake hakuwa mtu wa kulaumiwa , kwani kulikuwa na mkataba wa yeye kutambulika kama mtoto wa Adebayo, lakini pia aliweza kufurahi na kuchukia kwa wakati mmoja kwa kumfahamu baba yake , kilichomfanya kufurahi ni kwamaba alikuwa ashatoka kwenye sintofahamu aliokuwa nayo kwa muda mrefu lakini kilichomfanya kuchukia ni kitendo cha kuwa mtoto wa nje ya ndoa lakini pia Raisi Jeremy kutoonyesha dalili yoyote ya kumtambua mbele yake.

“Bi Wema Raisi Jeremy anafahamu kama mimi ni mtoto wake wa Damu?”Aliuliza Edna.

“Juu ya hilo sifahamu , kwani mama yako alipofahamika ni mjamzito tayari alikuwa anafahamika kama mke wa Adebayo”Aliongea Bi Wema na Edna alitingisha kichwa na kisha kwa huzuni alirudi chumbani kwake.

Roma alijikuta akimuonea huruma mke wake , kwani aliweza kukumbuka maneno ya Raisi Jeremy juu ya kutokuwa na mpango wa kutomfanya Edna kuwa mtoto wake licha ya kwamba anamtambua, Alimuona mke wake hakuwa na utofauti na Yatima licha ya kwamba alikuwa na pesa nyingi, hisia ambazo zilimrudisha miaka kadhaa nyuma akiwa peke yake na Lorraine kwenye kisiwa , wakiwa hawana Baba wala Mama.

*******

Zilipita siku kumi , upande wa kwenye kampuni mashindano yalikuwa yakiendelea kama kawaida na Sophia alikuwa akifanya vyema sana kiasi cha kumpelekea kujipatia mashabiki wengi sana , kwani kwenye mitandao ya kijamii alikuwa akizungumziwa sana , huku Clip zake akiwa anaimba zikisambaa sana, watu wengi wakimtazamia kuwa mshindi wa mashindano hayo.

Mashindano yalikuwa na mvuto mkubwa sana kwani yalikuwa ya kipekee na mpangilio wake kupendwa na wengi lakini pia ndio mashindano ambayo yalikuwa yakifuatiliwa kwenye nchi nyingi sana na hio ni kutokana na kuhusika kwa Christen kwenye mashindano hayo kama jaji ambaye anatazamiwa kushiriki siku ya mwisho ya fainali, lakini pia Christen kitendo chake cha kuyapigia mashindano hayo ‘Promo’ wakati akiwa kwenye mahojiano na Vexto Tv , iliyapaisha sana duniani mashindano ya Kizazi nyota na kufanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa.

Zilikuwa zimebakia hatimae wiki tatu mpaka mashindano hayo kuhitimishwa , kwani kila wiki mashindano yalikuwa yakifanyika mara mbili na washiriki watano walikuwa wakitoka kwenye kila siku michuano.

Ikiwa ni siku ya jumamosi , kabla ya mashindano kuanza mshereheshaji Amina kanani aliweza kutoa tangazo juu ya ujio wa msanii mkubwa atakaetumbuiza siku ya fainali , msanii wa kike mrembo kutoka Korea Kusini afahamikae kwa jina la Yoon- He

Yoona- He ni moja ya wasanii maarufu ambaye anauza sana kazi zake za kisanaa ndani ya Korea na nje ya Korea , alikuwa na mashabiki wengi sana na kitu ambacho kilimfanya pia kutambulika kimataifa ni pamoja na uwezo wake katika mambo ya uigizaji , akiwa ameshiriki kwenye muvi na Tv Shows mbalimbali mbali ambazo zilifanya vizuri sokoni kimnataifa.

Licha ya kuwa msanii lakini pia inasemekeana mafanikio ya Yoon-He yalichangiwa na ukwasi wa pesa wa familia yake, kwani babu yake Yoon-He ni moja ya wafanyabiashara wakubwa walijikita katika udhalishajii wa vifaa vya kidigitali vya mambo ya nyumbani , akitajwa kama Tajiri namba kumi ndani ya Korea.

Hivyo baada ya Tangazo hilo liliibua munkari sana kwa mashabiki na wafatiliaji wengi pamoja na wale ambao walikuwa shabiki wa Yoon -He,menejimenti ya Yoon He ndio iliofanya mawasiliano na kampuni ya Vexto na kuomba ushiriki katika kuimba siku ya fainali jambo ambalo lilikubaliwa na Daudi pamoja na Amina mara moja , huku upande wa Roma kwakua hakuwa sana mpenzi wa nyimbo wala shabiki wa mtu yoyote alikubali tu ilimradi Yoon He angeongeza mapato.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana tokea mwanzo wa shindano hilo ndani ya siku chache tu , kwani faida ilikuwa ikionekana lakini pia wafatiliaji walikuwa wengi hivyo kufanya matanganzo ya kampuni ya Vexto International kufikia watu wengi sana na kufanya hata hisa za kampuni kupanda ndani ya muda mfupi , jambo ambalo lilimfurahisha sana Edna na kuona kwamba yalikuwa mawazo sahihi ya kufungua kampuni ya Habari na burudani, lakini pia lilikuwa wazo sahihi kumwachia Roma kuongoza kampuni hio.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa kwenye mawazo ya hapa na pela huku akiangalia Skrini ya tarakishi yake iliokuwa ikionyesha namna ambavyo mauzo ya hisa yamepanda kwa siku hio mara baada ya kutangazwa kwa ujio wa msanii Yoon-He.

Wakati akiendelea kuwaza alijikuta akikumbuka maneno ya mama mkwe wake siku mbili zilizopita juu ya Roma kuhamia kwenye chumba chake huku Lanlan ahamie kwenye chumba cha Qiang Xi , Edna alionekana kutafakari kidogo , huku akikumbuka siku hizo kumi zote Maisha na Roma yalikuwa mazuri sana kiasi kwamba hawakugombana na kubwa Zaidi tokea amtamkie Roma anampenda ni kama vyumba vya hisia visivyoonekana kwa darubini za kiganga kwenye moyo wake vilifunguka wazi kiasi kwamba hisia za kimapenzi zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba hata akimuona tu alikuwa akinyegeka.

Zimebaki siku tano tu kufikia tarehe ishirini na Tisa, Babu yake Lanlan asipotokea ndio siku nitakayo mlea Lanlan kama mtoto wangu na Roma kama baba yake na ndio siku ambayo Lanlan ataenda kulala na Qiang Xi na mimi kulala na Roma kama mume wangu”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake na kujikuta akitabasamu na alikuja kushituliwa na Monica ambaye aliingia hapo akiwa na faili tatu ambazo Edna anapaswa kuzisaini kabla hazijapelekwa kwenye kampuni Tanzu ili hatua Zaidi kuchukuliwa.

*******

Upande wa Raisi Senga alifanikiwa Kwenda Nigeria na kurudi salama salimini , lakini licha ya hivyo alionekana kutokuwa sawa kama alivyondoka , alionekana kuwa kwenye mawazo kiasi ambacho kilimfanya hata mke wake Damasi kujua mabadiliko ya mume wake.

“Senga ulivyoondoka sio kama ulivyorudi , unaonekana kuwa na mawazo mume wangu k ni jambo gani linaendelea?”

“Mama Ashley niko sawa ni maswala ya kikazi tu ndio yananifikirisha”Aliongea Senga kwa kujitutumua na muda huo alikuwa ndio anarudi kutoka ofisini.

Ukweli ni kwamba kilichomfanya Damasi kuwa na wasiwasi na mume wake ni kutokana na kwamba ,tokea arudi kutoka Nigeria alikoenda kikazi , hakumgusa kabisa na ndio maana Damasi alikuwa akipatwa na wasiwasi kwani haikuwa tabia ya Senga , lakini jambo lingine ni kwamba hakuwa sawa kimawazo , yaani Raisi Senga kuna muda alikuwa akiangalia sehemu basi macho yake yataganda sehemu hio mpaka ashituliwe na hiko ndio kikamfanya Damasi kuwa na mawazo.

“Senga nadhani unaelewa kauli yangu ya siku zote, licha ya kwamba wewe ni raisi wa Watanzania nikiwa mimi mmoja wapo ,lakini pia utambue mimi ni mkeo na unatakiwa kuwajibika kwangu na kwa familia”Aliongea Damasi kwa msisitizo na kisha akatoka kwenye chumba chao cha kulalaia na Kwenda upande wa Sebuleni kuendelea kuangalia Runinga.

Ikiwa ni siku nyingine baada ya Raisi Senga kuingia ofisini , asubuhi hio alionekana kuwa na ugeni ambao alionekana alikuwa akiusubuiria, ni kweli baada ya madakika kadhaa alionekana mwanaume mmoja wa kihindi mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi akiingia ndani ya ofisi ya kukutania wageni akiwa ameongozana na Katibu Muhtasi.

“Mheshimiwa Mjumbe kutoka baraza la haki za binadamu kashafika”Aliongea Katibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kumruhusu , muda ule ule mjumbe yule wa kihindi aliingia ndani ya eneo hilo na walisalimiana kwa bashasha na baada ya Raisi Senga kumkaribisha mgeni wake , palepale alitoa maagizo juu ya kikao hicho kuwa cha siri kwa muda wa dakika kadhaa na baada ya hapo baadhi ya viongozi wa Ikulu wataruhusiwa kuingia kushiriki kwenye mazungumzo pamoja na kupiga picha na kuweka mitandaoni na kwenye gazeti la kiserikali.

“Mheshimiwa nadhani hakuja haja ya maongezi Zaidi kwani kila kitu kishaongelewa, kama nilivyojitambulisha mimi ni mwanachama wa baraza la haki binadamu kutoka UN nikihudumu upande wa Afrika (Umoja wa mataifa) na nipo hapa kwa ajili ya kupata sahihi yako juu upatikanaji wa haki za LGBTQ(Mapenzi ya jinsia moja) hapa Tanzania”Aliongea yule mwanaume ambaye alijitambulisha kwa Mheshimiwa Senga kwa jina la Vishnu Gupta.

Mheshimiwa alifikitia kidogo , mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akitaka yeye asaini mkataba wa kulinda haki za mashoga hapa Tanzania , ijapokuwa makubaliano yake nchini Nigeria hayakuwa ni kwa ajili ya kutangaza hadharani kama anakubali mashoga lakini alitakuwa kutia sahihi kama mkuu wa nchi ili kuhakikisha kwamba serikali haingilii haki za mashoga nchini.

“Hakuna shida bwana Vishnu nitasaini mkataba kwani ni sehemu ya makubaliano yangu”Aliongea Raisi Senga na Vishnu alitoa karatasi na kumpatia raisi Senga na baada ya kuzisoma kwa muda mfupi hatimae aliweza kuzitia Saini , jambo ambalo lilimfanya Vishnu kutabasamu na alipeana mkono kama ishara ya makubaliano na baada ya hapo ndipo Kamera ziliruhusiwa na mazungumzo yakawa wazi , huku raisi Senga akitoa ahadi kwamba ataendelea kukomesha vitendo vyote ambavyo vnakiuka haki za kibinadamu.

Baada ya kikao kuisha mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu , licha ya kwamba alishasaini karatasi hizo ambazo zilikuwa ni ‘implicity’ kwenye utekelezaji wake , lakini bado alijiona kama mtu aliekosea watanzania , lakini pia aliejikosea yeye mwenyewe , lakini wakati huo huo Mheshimiwa Senga kuna tukio ambalo lilikuwa likijirudia rudia kwenye akili yake kiasi kwamba lilimfanya kabisa kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mke wake mpaka kupelekea malalamiko.

Mheshimiwa Senga alijikuta akijiegamiza kwenye kiti chake huku akikusanya mikono yake pamoja , alionekana kuwaza sana , haikueleweka mara moja ni nini kilichotokea kwenye Ibada ya Mpasuko Wa Mwezi kutokana na usiri mkubwa uliokuwepo , lakini jambo moja ambalo ni dhahiri ni kwmaba mheshimiwa Senga alikuwa akifanya maamuzi ambayo yapo nje ya kile anachokisimamia kama Raisi licha ya kwamba alishasaini ‘Impilicity Law’ inayohusiana na Mashoga aliamini siku sio nyingi atalazimishwa kusaini ‘Explicity Law’ inayohusiana na mashoga.

(Implicity Law ni hitimisho la kisheria ambalo linampa mtu haki ya kitu pasipo kuingiliwa licha ya kwamba sheria hio haiwekwi wazi, kwa mfano kauli ya kiongozi mmoja wa dini akisema kwamba Mapenzi ya jinsia moja sio Kosa , sio uhalifu lakini ni Dhambi hio ndio sheria isio ya moja kwa moja lakini yenye kutekelezwa , yaani huwezi kusikia kiongozi akisema hadharani kama anakukataa ushoga ilihali sheria hio ishasainiwa.

Explicity Law ni aina ya sheria ambazo ni za moja kwa moja na zinapaswa kutekelezwa kwa namna yoyote ile na mara nyingi sheria hizi kwa hapa Tanzania hupitishwa na Bunge pamoja na mahakama halafu ndio raisi atasaini ili ianze utekelezwaji wake.

Wanasheria mtatusaidia Zaidi hapo.

**********

Naam ilikuwa ni siku ya jumamosi Roma alionekana Kibaha kwa Mathiasi akikunja kushoto akiwa anendesha gari yake kuelekea upande wa mji wa kisasa , mji ambao unamilikiwa na kampuni ya Vexto Group.

Roma aliendesha gari yake kwa utaratibu huku akifurahia mazingira safi yaliokuwa yapo kandokando ya barabara hii kuelekea kwenye mji huu, kusema ukweli licha ya kwamba ilikuwa mara yake ya pili kufika kwenye huo mji lakini muonekano wake siku hio ulikuwa kama ni mpya kwake na alijiambia ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanyika mpaka kujenga makazi hayo ya kisasa kabisa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dakika kama tano aliweza kuingiza gari yake kwenye geti kubwa linarohusu magari kuingia kwenye ‘Apartment’ hizo na alikwenda moja kwa moja kuegesha kwenye Parking ya muda mfupi na akashuka na kuanza kutembea uelekeo wa jengo la Athena.

Alikuwa mahali hapo asubuhi hio kutokana na kwamba alikuwa na miadi na mrembo Suzzane , ambaye baada ya kuwasiliana nae alimwambia kwamba amfuate nyumbani kwake na Roma kwakuwa ndio alikuwa na shida ilimbidi kufanya hivyo ili kuonana na mrembo huyo.

Baada ya kufika chini kabisa ya hilo jengo alipiga simu Kwenda kwa Suzzane na alipewa maelekezo ya Kwenda mpaka Floor namba kumi na kusimama kwenye mlango wenye namba 200 ndio Apartment yake.

Tokea mrembo huyu aje kumchukua kwa mara ya kwanza kule Mbagala hakuweza tena kuongea nae moja kwa moja , kwanza Roma alimchukulai Suzzane kama mwanamke Siriasi asiependa utani , lakini pia Suzzane mara nyingi alikuwa ndani ya idara hii kwahio ilikuwa ngumu kwake sana kuonana nae mara kwa mara na kumzoea.

Dakika chache tu Roma alikuwa nje ya mlango namba 200 na alibonyeza kitufe cha kengele na kisha akasubiri mlango kufunguliwa na zilipita dakika kama mbili hivi hatimae mlango ulifunguliwa na mrembo Suzzane ambaye alikuwa amevalia gauni fupi la kumpendeza.

Suzznae alikuwa mzuri sana unaweza kumuitwa kwa jina la Black Beuty , kinachompoza ni ile hali yake ya kuwa siriasi na hata alivyosimama mbele ya Roma mara baada ya kufungua mlango alikuwa na sura yake yenye usiriasi vilevile na Roma alijiambia ilikuwa ni haki kabisa kwa mrembo huyu kuwa msaidizi wa Edna , kwani walikuwa wakiendana kwa asilimia mia moja tofauti yao tu ni kwamba Suzzane alikuwa na macho flani hivi akikuangalia ni kama anakudharau.

“Karibu”Alimkaribisha na Roma alitingisha kichwa na kisha kupita.

Roma licha ya kwamba alimpigia Suzzane , ila hakuweka swala lake wazi , alimwambia tu kuna mambo muhimu ambayo alikuwa akitaka kiuongea nae.







SEHEMU YA 341.

Edna sasa alielewa kwanini Blandina alisema kwamba picha hio alikuwa amepiga yeye, kumbe alishawahi kukutana na Raisi Jeremy huko Australia akiwa na mama yake wakila bata.

Roma mwenyewe alishangaa kumbe mama yake ni msomi mkubwa tu, lakini hata hivyo ilikuwa ni halali kabisa, kwani mambo ambayo Blandina aliweza kuyafanya kwa jamii kupitia sura ya Maina yalikuwa makubwa sana, kwani kama utaweza kupiga hesabu ya thamani ya vituo vyote ambavyo alivianzisha kwa nguvu zake ni Zaidi ya Dollar milioni mia moja.

Upande wa Roma yeye hakushangaa sana kwani alikua akijua mzazi wa Edna , ila mbele ya Edana alijifanyisha na yeye kushangaa , kwani alijua kama atasema alikuwa akifahamu na akakaa kimya , Edna angekasirika.

Maelezo ya Bi Wema hayakuwa na utofauti sana, kwani alishaelezwa na Raheli mwenyewe juu ya baba mzazi wa Edna, lakini sasa jumla yao wote wakajiuliza swali moja ni nani ambaye ameleta taarifa hio, na ni kwa madhumuni yapi, upande wa Roma aliamini sio Raisi Jeremy alieleta hio karatasi aliamini kuna mtu mwingine ambaye ameleta barua hio ila hakujua sababu ni nini na aliajiambia ni swala la muda tu atafahamu.

Edna sasa anajikuta akianza kuhisi huenda hata mtu aliekuwa akijiita The Protector alikuwa ni Raisi Jeremy , kwani mambo mengi ambayo aliokuwa akimsiadia yalikuwa yakihataji intelijensia ya hali ya juu.

Licha ya kwamba alihuzunishwa na jambo hilo , aliona mama yake hakuwa mtu wa kulaumiwa , kwani kulikuwa na mkataba wa yeye kutambulika kama mtoto wa Adebayo, lakini pia aliweza kufurahi na kuchukia kwa wakati mmoja kwa kumfahamu baba yake , kilichomfanya kufurahi ni kwamaba alikuwa ashatoka kwenye sintofahamu aliokuwa nayo kwa muda mrefu lakini kilichomfanya kuchukia ni kitendo cha kuwa mtoto wa nje ya ndoa lakini pia Raisi Jeremy kutoonyesha dalili yoyote ya kumtambua mbele yake.

“Bi Wema Raisi Jeremy anafahamu kama mimi ni mtoto wake wa Damu?”Aliuliza Edna.

“Juu ya hilo sifahamu , kwani mama yako alipofahamika ni mjamzito tayari alikuwa anafahamika kama mke wa Adebayo”Aliongea Bi Wema na Edna alitingisha kichwa na kisha kwa huzuni alirudi chumbani kwake.

Roma alijikuta akimuonea huruma mke wake , kwani aliweza kukumbuka maneno ya Raisi Jeremy juu ya kutokuwa na mpango wa kutomfanya Edna kuwa mtoto wake licha ya kwamba anamtambua, Alimuona mke wake hakuwa na utofauti na Yatima licha ya kwamba alikuwa na pesa nyingi, hisia ambazo zilimrudisha miaka kadhaa nyuma akiwa peke yake na Lorraine kwenye kisiwa , wakiwa hawana Baba wala Mama.

*******

Zilipita siku kumi , upande wa kwenye kampuni mashindano yalikuwa yakiendelea kama kawaida na Sophia alikuwa akifanya vyema sana kiasi cha kumpelekea kujipatia mashabiki wengi sana , kwani kwenye mitandao ya kijamii alikuwa akizungumziwa sana , huku Clip zake akiwa anaimba zikisambaa sana, watu wengi wakimtazamia kuwa mshindi wa mashindano hayo.

Mashindano yalikuwa na mvuto mkubwa sana kwani yalikuwa ya kipekee na mpangilio wake kupendwa na wengi lakini pia ndio mashindano ambayo yalikuwa yakifuatiliwa kwenye nchi nyingi sana na hio ni kutokana na kuhusika kwa Christen kwenye mashindano hayo kama jaji ambaye anatazamiwa kushiriki siku ya mwisho ya fainali, lakini pia Christen kitendo chake cha kuyapigia mashindano hayo ‘Promo’ wakati akiwa kwenye mahojiano na Vexto Tv , iliyapaisha sana duniani mashindano ya Kizazi nyota na kufanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa.

Zilikuwa zimebakia hatimae wiki tatu mpaka mashindano hayo kuhitimishwa , kwani kila wiki mashindano yalikuwa yakifanyika mara mbili na washiriki watano walikuwa wakitoka kwenye kila siku michuano.

Ikiwa ni siku ya jumamosi , kabla ya mashindano kuanza mshereheshaji Amina kanani aliweza kutoa tangazo juu ya ujio wa msanii mkubwa atakaetumbuiza siku ya fainali , msanii wa kike mrembo kutoka Korea Kusini afahamikae kwa jina la Yoon- He

Yoona- He ni moja ya wasanii maarufu ambaye anauza sana kazi zake za kisanaa ndani ya Korea na nje ya Korea , alikuwa na mashabiki wengi sana na kitu ambacho kilimfanya pia kutambulika kimataifa ni pamoja na uwezo wake katika mambo ya uigizaji , akiwa ameshiriki kwenye muvi na Tv Shows mbalimbali mbali ambazo zilifanya vizuri sokoni kimnataifa.

Licha ya kuwa msanii lakini pia inasemekeana mafanikio ya Yoon-He yalichangiwa na ukwasi wa pesa wa familia yake, kwani babu yake Yoon-He ni moja ya wafanyabiashara wakubwa walijikita katika udhalishajii wa vifaa vya kidigitali vya mambo ya nyumbani , akitajwa kama Tajiri namba kumi ndani ya Korea.

Hivyo baada ya Tangazo hilo liliibua munkari sana kwa mashabiki na wafatiliaji wengi pamoja na wale ambao walikuwa shabiki wa Yoon -He,menejimenti ya Yoon He ndio iliofanya mawasiliano na kampuni ya Vexto na kuomba ushiriki katika kuimba siku ya fainali jambo ambalo lilikubaliwa na Daudi pamoja na Amina mara moja , huku upande wa Roma kwakua hakuwa sana mpenzi wa nyimbo wala shabiki wa mtu yoyote alikubali tu ilimradi Yoon He angeongeza mapato.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana tokea mwanzo wa shindano hilo ndani ya siku chache tu , kwani faida ilikuwa ikionekana lakini pia wafatiliaji walikuwa wengi hivyo kufanya matanganzo ya kampuni ya Vexto International kufikia watu wengi sana na kufanya hata hisa za kampuni kupanda ndani ya muda mfupi , jambo ambalo lilimfurahisha sana Edna na kuona kwamba yalikuwa mawazo sahihi ya kufungua kampuni ya Habari na burudani, lakini pia lilikuwa wazo sahihi kumwachia Roma kuongoza kampuni hio.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa kwenye mawazo ya hapa na pela huku akiangalia Skrini ya tarakishi yake iliokuwa ikionyesha namna ambavyo mauzo ya hisa yamepanda kwa siku hio mara baada ya kutangazwa kwa ujio wa msanii Yoon-He.

Wakati akiendelea kuwaza alijikuta akikumbuka maneno ya mama mkwe wake siku mbili zilizopita juu ya Roma kuhamia kwenye chumba chake huku Lanlan ahamie kwenye chumba cha Qiang Xi , Edna alionekana kutafakari kidogo , huku akikumbuka siku hizo kumi zote Maisha na Roma yalikuwa mazuri sana kiasi kwamba hawakugombana na kubwa Zaidi tokea amtamkie Roma anampenda ni kama vyumba vya hisia visivyoonekana kwa darubini za kiganga kwenye moyo wake vilifunguka wazi kiasi kwamba hisia za kimapenzi zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba hata akimuona tu alikuwa akinyegeka.

Zimebaki siku tano tu kufikia tarehe ishirini na Tisa, Babu yake Lanlan asipotokea ndio siku nitakayo mlea Lanlan kama mtoto wangu na Roma kama baba yake na ndio siku ambayo Lanlan ataenda kulala na Qiang Xi na mimi kulala na Roma kama mume wangu”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake na kujikuta akitabasamu na alikuja kushituliwa na Monica ambaye aliingia hapo akiwa na faili tatu ambazo Edna anapaswa kuzisaini kabla hazijapelekwa kwenye kampuni Tanzu ili hatua Zaidi kuchukuliwa.

*******

Upande wa Raisi Senga alifanikiwa Kwenda Nigeria na kurudi salama salimini , lakini licha ya hivyo alionekana kutokuwa sawa kama alivyondoka , alionekana kuwa kwenye mawazo kiasi ambacho kilimfanya hata mke wake Damasi kujua mabadiliko ya mume wake.

“Senga ulivyoondoka sio kama ulivyorudi , unaonekana kuwa na mawazo mume wangu k ni jambo gani linaendelea?”

“Mama Ashley niko sawa ni maswala ya kikazi tu ndio yananifikirisha”Aliongea Senga kwa kujitutumua na muda huo alikuwa ndio anarudi kutoka ofisini.

Ukweli ni kwamba kilichomfanya Damasi kuwa na wasiwasi na mume wake ni kutokana na kwamba ,tokea arudi kutoka Nigeria alikoenda kikazi , hakumgusa kabisa na ndio maana Damasi alikuwa akipatwa na wasiwasi kwani haikuwa tabia ya Senga , lakini jambo lingine ni kwamba hakuwa sawa kimawazo , yaani Raisi Senga kuna muda alikuwa akiangalia sehemu basi macho yake yataganda sehemu hio mpaka ashituliwe na hiko ndio kikamfanya Damasi kuwa na mawazo.

“Senga nadhani unaelewa kauli yangu ya siku zote, licha ya kwamba wewe ni raisi wa Watanzania nikiwa mimi mmoja wapo ,lakini pia utambue mimi ni mkeo na unatakiwa kuwajibika kwangu na kwa familia”Aliongea Damasi kwa msisitizo na kisha akatoka kwenye chumba chao cha kulalaia na Kwenda upande wa Sebuleni kuendelea kuangalia Runinga.

Ikiwa ni siku nyingine baada ya Raisi Senga kuingia ofisini , asubuhi hio alionekana kuwa na ugeni ambao alionekana alikuwa akiusubuiria, ni kweli baada ya madakika kadhaa alionekana mwanaume mmoja wa kihindi mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi akiingia ndani ya ofisi ya kukutania wageni akiwa ameongozana na Katibu Muhtasi.

“Mheshimiwa Mjumbe kutoka baraza la haki za binadamu kashafika”Aliongea Katibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kumruhusu , muda ule ule mjumbe yule wa kihindi aliingia ndani ya eneo hilo na walisalimiana kwa bashasha na baada ya Raisi Senga kumkaribisha mgeni wake , palepale alitoa maagizo juu ya kikao hicho kuwa cha siri kwa muda wa dakika kadhaa na baada ya hapo baadhi ya viongozi wa Ikulu wataruhusiwa kuingia kushiriki kwenye mazungumzo pamoja na kupiga picha na kuweka mitandaoni na kwenye gazeti la kiserikali.

“Mheshimiwa nadhani hakuja haja ya maongezi Zaidi kwani kila kitu kishaongelewa, kama nilivyojitambulisha mimi ni mwanachama wa baraza la haki binadamu kutoka UN nikihudumu upande wa Afrika (Umoja wa mataifa) na nipo hapa kwa ajili ya kupata sahihi yako juu upatikanaji wa haki za LGBTQ(Mapenzi ya jinsia moja) hapa Tanzania”Aliongea yule mwanaume ambaye alijitambulisha kwa Mheshimiwa Senga kwa jina la Vishnu Gupta.

Mheshimiwa alifikitia kidogo , mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akitaka yeye asaini mkataba wa kulinda haki za mashoga hapa Tanzania , ijapokuwa makubaliano yake nchini Nigeria hayakuwa ni kwa ajili ya kutangaza hadharani kama anakubali mashoga lakini alitakuwa kutia sahihi kama mkuu wa nchi ili kuhakikisha kwamba serikali haingilii haki za mashoga nchini.

“Hakuna shida bwana Vishnu nitasaini mkataba kwani ni sehemu ya makubaliano yangu”Aliongea Raisi Senga na Vishnu alitoa karatasi na kumpatia raisi Senga na baada ya kuzisoma kwa muda mfupi hatimae aliweza kuzitia Saini , jambo ambalo lilimfanya Vishnu kutabasamu na alipeana mkono kama ishara ya makubaliano na baada ya hapo ndipo Kamera ziliruhusiwa na mazungumzo yakawa wazi , huku raisi Senga akitoa ahadi kwamba ataendelea kukomesha vitendo vyote ambavyo vnakiuka haki za kibinadamu.

Baada ya kikao kuisha mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu , licha ya kwamba alishasaini karatasi hizo ambazo zilikuwa ni ‘implicity’ kwenye utekelezaji wake , lakini bado alijiona kama mtu aliekosea watanzania , lakini pia aliejikosea yeye mwenyewe , lakini wakati huo huo Mheshimiwa Senga kuna tukio ambalo lilikuwa likijirudia rudia kwenye akili yake kiasi kwamba lilimfanya kabisa kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mke wake mpaka kupelekea malalamiko.

Mheshimiwa Senga alijikuta akijiegamiza kwenye kiti chake huku akikusanya mikono yake pamoja , alionekana kuwaza sana , haikueleweka mara moja ni nini kilichotokea kwenye Ibada ya Mpasuko Wa Mwezi kutokana na usiri mkubwa uliokuwepo , lakini jambo moja ambalo ni dhahiri ni kwmaba mheshimiwa Senga alikuwa akifanya maamuzi ambayo yapo nje ya kile anachokisimamia kama Raisi licha ya kwamba alishasaini ‘Impilicity Law’ inayohusiana na Mashoga aliamini siku sio nyingi atalazimishwa kusaini ‘Explicity Law’ inayohusiana na mashoga.

(Implicity Law ni hitimisho la kisheria ambalo linampa mtu haki ya kitu pasipo kuingiliwa licha ya kwamba sheria hio haiwekwi wazi, kwa mfano kauli ya kiongozi mmoja wa dini akisema kwamba Mapenzi ya jinsia moja sio Kosa , sio uhalifu lakini ni Dhambi hio ndio sheria isio ya moja kwa moja lakini yenye kutekelezwa , yaani huwezi kusikia kiongozi akisema hadharani kama anakukataa ushoga ilihali sheria hio ishasainiwa.

Explicity Law ni aina ya sheria ambazo ni za moja kwa moja na zinapaswa kutekelezwa kwa namna yoyote ile na mara nyingi sheria hizi kwa hapa Tanzania hupitishwa na Bunge pamoja na mahakama halafu ndio raisi atasaini ili ianze utekelezwaji wake.

Wanasheria mtatusaidia Zaidi hapo.

**********

Naam ilikuwa ni siku ya jumamosi Roma alionekana Kibaha kwa Mathiasi akikunja kushoto akiwa anendesha gari yake kuelekea upande wa mji wa kisasa , mji ambao unamilikiwa na kampuni ya Vexto Group.

Roma aliendesha gari yake kwa utaratibu huku akifurahia mazingira safi yaliokuwa yapo kandokando ya barabara hii kuelekea kwenye mji huu, kusema ukweli licha ya kwamba ilikuwa mara yake ya pili kufika kwenye huo mji lakini muonekano wake siku hio ulikuwa kama ni mpya kwake na alijiambia ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanyika mpaka kujenga makazi hayo ya kisasa kabisa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dakika kama tano aliweza kuingiza gari yake kwenye geti kubwa linarohusu magari kuingia kwenye ‘Apartment’ hizo na alikwenda moja kwa moja kuegesha kwenye Parking ya muda mfupi na akashuka na kuanza kutembea uelekeo wa jengo la Athena.

Alikuwa mahali hapo asubuhi hio kutokana na kwamba alikuwa na miadi na mrembo Suzzane , ambaye baada ya kuwasiliana nae alimwambia kwamba amfuate nyumbani kwake na Roma kwakuwa ndio alikuwa na shida ilimbidi kufanya hivyo ili kuonana na mrembo huyo.

Baada ya kufika chini kabisa ya hilo jengo alipiga simu Kwenda kwa Suzzane na alipewa maelekezo ya Kwenda mpaka Floor namba kumi na kusimama kwenye mlango wenye namba 200 ndio Apartment yake.

Tokea mrembo huyu aje kumchukua kwa mara ya kwanza kule Mbagala hakuweza tena kuongea nae moja kwa moja , kwanza Roma alimchukulai Suzzane kama mwanamke Siriasi asiependa utani , lakini pia Suzzane mara nyingi alikuwa ndani ya idara hii kwahio ilikuwa ngumu kwake sana kuonana nae mara kwa mara na kumzoea.

Dakika chache tu Roma alikuwa nje ya mlango namba 200 na alibonyeza kitufe cha kengele na kisha akasubiri mlango kufunguliwa na zilipita dakika kama mbili hivi hatimae mlango ulifunguliwa na mrembo Suzzane ambaye alikuwa amevalia gauni fupi la kumpendeza.

Suzznae alikuwa mzuri sana unaweza kumuitwa kwa jina la Black Beuty , kinachompoza ni ile hali yake ya kuwa siriasi na hata alivyosimama mbele ya Roma mara baada ya kufungua mlango alikuwa na sura yake yenye usiriasi vilevile na Roma alijiambia ilikuwa ni haki kabisa kwa mrembo huyu kuwa msaidizi wa Edna , kwani walikuwa wakiendana kwa asilimia mia moja tofauti yao tu ni kwamba Suzzane alikuwa na macho flani hivi akikuangalia ni kama anakudharau.

“Karibu”Alimkaribisha na Roma alitingisha kichwa na kisha kupita.

Roma licha ya kwamba alimpigia Suzzane , ila hakuweka swala lake wazi , alimwambia tu kuna mambo muhimu ambayo alikuwa akitaka kiuongea nae.

ITAENDELEA

WATSAPP 0687151346
 
SEHEMU YA 336.

Ilikuwa ni siku ya Jumanne , Roma alirudi nyumbani kwenye muda wa saa moja asubuhi maana usiku mzima hakuwa amelela nyumbani, muda ambao alirudi Edna alikuwa tayari ashaondoka na alijua hilo baada ya kutokuoona gari yake.

Roma aliingia ndani ya nyumba yao na kupokelewa na Bi Wema na Qiang XI ambao walikuwa wakiendelea na majukumu ya kuweka sawa usafi wa nyunba ,Roma alisalimiana nao na kisha moja kwa moja alielekea kwenye chumba chake na kubadilisha mavazi na baada tu ya kumaliza alipandisha juu kwenye chumba cha Edna na kisha alifungua mlango wa chumba cha mke wake ,bahati nzuri mlango ulikuwa wazi hivyo haikuwa kazi kwake kuingia.

Lanlan alikuwa amelela muda huo na ilionekana wakati Edna akiondoka hakuwa amemka bado , Roma alimwangalia Lanlan alivyolala na kutabasamu , aligeuzia macho yake juu ya meza na aliangalia Bahasha iliokuwa juu ya meza , aliichukua na kutoa karatasi ambazo zipo ndani yake na baada ya kuzisoma aligundua ni za mkataba wa ndoa yake, yeye na Edna.

Alizirudisha ndani na kisha aliangalia kulia na kushoto kama mtu anaekagua chumba hiko na kisha alionekana kuridhika , alimsogelea Lanlan alielala na kupitisha mkono wake kwenye kichwa chake kwa sekunde kwa namna ya kupeti peti na kisha alisimama na kutoka kwenye chumba hicho huku akiwa ameshikilia zile kartasi , haikueleweka alikuwa akifikiria nini , lakini ndani ya dakika chache alionekana akitoka akiwa ameshikilia ile bahasha na ile anafika sebuleni aliweza kukutana na mama yake ambaye ndio alionekana anaamka.

Roma alimsalimia mama yake ambaye alionekana kuwa na usngizi bado kutokana na kuchelewa kulala jana yake akimsubiri mtoto wake arudi , Romajana alisahau kumtaarifu kwamba harudi.

“Roma subiri kwanza unywe chai?”Aliongea Blandina mara baada ya Roma kumwambia mama yake anaenda kazini.

“Mama nitakunywa mbele ya safari , nitawahi kurudi leo”Aliongea Roma huku akitoka nje kabisa na kumuacha Blandina kuangalia mlango kwa wasiwasi. Alijiuliza Edna hakuwa amekunwa chai na Roma hivyo hakuwa amekunywa chai , hakuelewa ni kipi kinaendelea , ila aliona atulize kichwa na kuacha mambo ya wanandoa hao yawe ya kwao kutafuta suluhisho pasipo yeye kuingilia.

“Bi Wema nina wasiwasi kweli na hawa Watoto”Aliongea Blandina mara baada ya kuingia jikoni akinuia kumsaidia Bi Wema.

“Blandina huna haja ya kuwa na wasiwasi , mimi nishawazoea, haya unayo yaona hapa yataisha na amani itatawala , ninachowaza hapa ni kuhakikisha tunawafanya wawe pamoja Zaidi”Aliongea Bi Wema.

“Unamaanisha nini Bi Wema?”

“Tumlazimishe Edna kulala na mume wake Roma , hio ndio namna pekee ya kuepusha migogoro Zaidi , Lanlan atarudi kulala na Qiang Xi”Aliongea Bi Wema na kumfanya Blandina kutabasamu , aliona wazo la Bi Wema ni zuri Zaidi.

“Edna atakubali , nina wasiwasi , yule mtoto licha ya kuwa mke wa Roma lakini nashindwa kuelewa anachofikiria”Aliongea na Bi Wema kutabasamu.

“Wewe ni mama kwao ,tumia nafasi yako kuwalazimisha kulala chumba kimoja , ila waache kwanza wapatane wenyewe ndio uchukue hatua ya kuongea na Edna”Aliongea Bi Wema na Blandina aliitikia kwa kichwa , aliona mawazo ya Bi Wema sio mabaya , kama Edna anakataa kulala na Roma inabidi wamlazimishe afanye hivyo kwani aliona ni ujinga wa Edna ndio maana Roma anachepuka.

Ukweli Bi Wema asingeweza kumlazimisha Edna kulala na Roma kwani hakuwa kwenye hio nafasi , kwani yeye alikuwa ni kama mfanyakazi tu ndani ya familia hiyo na alikuwa akilipwa mshahara wake licha ya kwamba Edna alikuwa akimchukulia kama mzazi , hivyo aliona mtu pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kufanya kazi hio alikuwa ni Blandina.

Upande wa Roma hakuwa akienda kazini kwake , bali alichukua barabara ya Kwenda Posta na ndani ya dakika kama therathini tu hivi alikuwa ashafika nje ya jengo la kampuni ya Vexto , baada ya kusimamisha gari moja kwa moja alielekea kwenye lift na kubonyeza kitufe cha floor ya mwisho kabisa , ambayo ndio ofisi ya Edna ilikuwa ikipatikana , muda wote akiwa ameshikilia karatasi ya mkataba na haikueleweka alikuwa akifiria nini au alikuwa akipanga nini kufanya na hio karatasi.

Roma baada ya kutoka kwenye lift , alimfikia Monica na hakusimama Zaidi ya kumpungia tu mkono na kupita moja kwa moja kuingia kwenye ofisi ya Edna.

Edna alikuwa bize na kazi na baada ya kuona alieingia ndani ya ofisi yake ni Roma aliendelea kujiweka bize na kazi yake, Roma hakujali sana Zaidi ya kujongea na kuzunga nyuma ya meza ya Edna na kisha alizungusha kiti na kumwangalia usoni huku akiwa siriasi.

“Mr Roma unafanya nini , nipo bize na kazi”Aliongea Edna huku akitaka kugeuza kiti , lakini Roma hakumpa nafasi alimshika mkono na kumnyanyua.

“Nifuate kuna sehemu twende , haijalishi unakazi gani ila tii maagizo”Aliongea Roma kwa sauti ya kibabe na hakumpa nafasi Edna ya kujitetea.

“Roma niachie , nimesema nina kazi na siwezi kuondoka ofisini” Aliongea Edna kwa ukali huku akitoa mikono yake kwa Roma.

“Kwahio hutaki Kwenda?”Aliuliza Roma huku akimwangalia Edna.

“Nishasema nina kazi Roma siwezi kuondoka na huwezi kunilazimisha”Aliongea Edna na Roma alitabasamu kifedhuli na Edna hakujua hata ilitokea vipi kwani alijikuta tayari yupo juu akielea kwenye mikono ya Roma akiwa amepakatwa.

“Nilitaka unifuate kwa hiari yako , ila naona unaniletea za kuleta”Aliongea Roma huku akimtoa Edna ndani ya ofisi akiwa amempakata , Edna licha ya kujaribu kujitoa kwenye mwili wa Roma , lakini ilishindikana na aliishia kurusha rusha miguu.

Monica aliekuwa akiongea na Dorisi eneo la mapokezi alijikuta akiduwaa mara baada ya kumshuhudia Bosi wake akiwa amepakatwa na Roma , alitaka kutoka kwenye kiti chake Kwenda kumzuia Roma , lakini Dorisi alimzuia.

“Usiingilie”Aliongea Dorisi na kumfanya Monica kumwangalia kwa mshangao.

“Nini kinaendelea , kwanini unaniambia nisiingilie wakati Roma anamteka Bosi”Aliongea Monica na Dorisi alitabasamu.

“Unaonekana kutomfahamu vyema bosi wako , unashindwaje kufahamu mahusiano ya Roma na Edna, hata kuunganisha doti umeshindwa Monica na uzoefu wako”

“Miss Dorisi unamaanisha Roma na Edna ni…”

“Ndio ni mume na mke”Aliongea Dorisi na kuchukua faili kwenye mikono ya Monica na kisha aliondoka na kumuacha Monica alieduwaa akikaa chini kwenye kiti bila kupenda kama mzigo.

“Kumbe ndio maana… kwanini sikujua hapo kabla”Aliongea mwenyewe

“Monica unawaza nini , nahitaji kuonana na CEO”Aliongea Ernest Komwe mara baada ya kufika kwenye meza ya Monica aliekuwa kwenye mawazo.

“Monica..!!!”

“Abee…!”

“Unawaza nini bwana… usiniambie unawaza tulichofanya usiku wa jana”

“Ernest kimyaa…”Aliongea Monica Kibabe mara baada ya Ernest kuingizia jambo ambalo Monica hakupenda lifahamike.

“Nimeacha kipenzi .. niambie CEO yupo nahitaji kuonana nae”

“Ametoka”Aliongea Monica kwa sauti ya upole huku akimwangalia Ernest Komwe kwa macho ya kumsanifu ilikuwa ni kama mwanamke anavyomchunguza mpenzi wake ndio ambavyo Monica alikuwa akimwangalia Ernest Komwe.

“Niachie Roma nitakufuata mwenyewe tafadhari”Aliongea Edna kwa kubembeleza mara baada ya kuona hakuna dalili ya Roma kumuweka chini mara baada ya kuingia nae kwenye Lift , hakutaka kuumbuka Zaidi , kwani kitendo cha kubebwa na Monica kuona tukio lile ilikuwa ni aibu tosha kwake na hakutaka wafanyakazi wengine wamuone mara baada ya lift kufunguka.

Roma baada ya kuona Edna anaomba sana , ilibidi amtue chini, Edna alipumua huku bado hasira zake zikiwa juu , alijiambia yaani mtukalala kwa wanawake zake pasipo ya kujali jana yake kamdhalilisha na anakuja ofisini kwake akiwa na kazi na anamkwapua tu bila ridhaa yake , alisema hawezi kuliacha hilo lipite.

“Ukifanya ujinga wa kutaka kurudi ndani nitafanya jambo kubwa Zaidi ya nililolifanya, nafikiri unajua kwamba sinaga aibu”Aliongea Roma huku akiwa hana utani kabisa.

Licha ya Roma kushikilia bahasha , lakini Edna hakugundua bahasha ile ni ile yenye mkataba wao wa ndoa na alijiuliza ni jambo gani ambal Roma alikuwa akijaribu kufanya, ila hakuelewa na ilimbidi kutii amri kwani alijiambia akifanya jambo la kurudi basi Roma hashindwi kufanya kitu kikubwa cha aibu mbele ya watu.

Dakika chache mbele waliweza kuingia kwenye gari ya Roma.

“Tunaenda wapi?”

“Utajua mbele ya safari , usiulize maswali mengi”Aliongea Roma na kisha alitoa gari kwa spidi isiokuwa ya kawaida na kumfanya Edna kufumba macho.

Roma aliendesha gari kama hana akili nzuri vile mara baada tu ya kuliingiza kwenye barabara kuu , ndani ya dakika chache tu alikuwa Mororogo Road akisonga mbele na muda huo alikuwa akipita Magomeni mapipa, dakika nyingine mbele alikuwa akipita Kijazi Interchange na alikuja kukata kulia akichukua barabra iliokuwa ikielekea hoteli ya Grand Palace.

Edna baada ya kuona Roma anaingiza gari kwenye uzio wa hoteli hio alijikuta akishangaa na kujiuliza Roma alikuwa akifanya nini , kwani sehemu hio alikuwa akiikumbuka vyema , ndio sehemu ambayo alimuomba Roma kumuoa.

Baada ya Roma kumfungulia Edna mlango alimshika mkono na kuingia nae ndani ya hoteli hio.

“Nahitaji chumba namba 708, nishafanya booking , jina Roma Ramoni”Aliongea Roma na baada ya maneno hayo kutua kwenye masikio ya Edna , moyo wake ulipiga kite , chumba ambacho Roma alitaja ni chumba kile kile alichokutana nae kwa mara ya pili.

Mhudumu wa hoteli alitoa kadi haraka haraka , alionekana kumfahamu Edna na ndio maana alifanya kwa haraka haraka huku akiwa ni kama mwenye kutetemeka.

Dakika mbili mbele Edna akishindwa kujua Roma anachokiwaza, aliingizwa kwenye chumba hiko na kukalishwa kwenye sofa.

“Nakumbuka ulikaa kwenye hili sofa, utakaa hapa hapa kama siku ile”Aliongea Roma na yeye kukaa kwenye sofa alilokalia siku ile ile miezi sita iliopita.

Roma hakujali mshangao wa Edna alichokifanya ni kutoa karatasi ya ule mkataba na kisha alimpatia Edna.

Sasa kitendo cha Edna kugundua katatasi ile ilikuwa ni ya mkataba wao wa ndoa , moyo wake ulipiga kite kwa nguvu na hakuelewa hata machozi yalitoka wapi kwani yalianza kuloanisha mboni za macho yake.

Kwahio kumbe kanileta hapa ili tuachane”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake huku akiwa ameshikilia ule mkataba wa ndoa na alijikuta bila kupenda akiurudisha kwenye meza , ila Roma hakujali , alionekana kujipanga , alitoa karamu kwenye mfuko wa shati na kumpatia Edna.

“Edna kwenye maisha yangu nina kanuni moja tu ,nikishafanya maamuzi hakuna kitu ambacho kinaweza kunifanya nikayabatilisha, lakini leo hii kwa ajili yako nipo tayari kuvunja kanuni yangu, ulivyonilazimisha miezi sita iliopita tuoane nilianza kukataa kwasababu kwenye Maisha yangu nilipanga mwanamke ambaye nitafunga nae ndoa ndio atakuwa huyo huyo kwenye Maisha yangu yote… kama niliamua kufunga ndoa nje ya ridhaa yangu na wewe, nipo tayari pia kuibatilisha ndoa yetu na kila mtu ajue Maisha yake”Aliongea Roma kwa hasira na kumfanya Edna kuzidi kulia, mtu aliekuwa mbele yake hakuamini ni yule Roma ambaye alikuwa akimjua siku zote , mwanaume ambaye hata kama hakuwa akimpa mwili wake kama mke , lakini bado alionekana kumjali , Edna hakuamini kama akisaini karatasi hio ndio utakuwa mwisho wake yeye na Roma, moyo wake uliuma, aliamini akishaachana na Roma basi huenda kati ya Dorisi au Nasra ndio watachukua nafasi yake na kuitwa mke wa Roma , moyo ulimuuma mno , moyo wake haukuwa tayari kabisa kusaini karatasi iliokuwa mbele yake kubatilisha mkataba wa ndoa..

“Edna unanipotezea muda, Saini karatasi hizo na mimi nitie sahihi yangu kila mmoja ajue mambo yake , si ndio unachotaka , nitakuacha uwe na amani”

“Roma tafadha….”

“Edna Saini, sitaki maelezo mengi”Aliongea Roma kibabe na Edna aliinua macho yake yaliojaa machozi na kumwangalia Roma na kuona kabisa hakukuwa na chembe ya utani kwenye macho yake, aliona hakuwa na jinsi Zaidi ya kusaini karatasi hizo licha ya kwmaba moyo wake ulikuwa mzito kufanya hivyo.

Kwa mara ya kwanza kwenye Maisha yake , alikosa kujiamini , Edna alishika karamu kwa kutetemeka sana, alivuta karatasi na kisha kabla ya kutia Saini alimwangalia Roma kwa mara nyingine ,alikuwa ni kama akitaka kumsikia Roma akimwambia nilikuwa nakutania , lakini Roma alionekana kuwa siriasi vilevile.

“Daah!!!... ndio naachika hivyo”Aliwaza Edna huku akichukua karatasi karibu na kutia Saini, ili kuachana na Mfalme Pluto A.k. a Hades.









SEHEMU YA 337.

Kabla ya Edna kutia Saini kwenye karatasi ile , Roma alimshika mkono na kumzuia kitendo ambacho kilimfanya Edna kumwangalia Roma.

“Edna mke wangu nilikuwa nakutania”Aliongea Roma huku akirudi kwenye hali yake ya kawaida iliozoeleka kwenye macho ya Edna kitendo ambacho kilimfanya Edna kupumua kwa nguvu ,alikuwa ni kama ametua mzigo mzito kwenye moyo wake na alijikuta akimwangalia Roma huku machozi yakimtoka zaidi.

Edna alijikuta akinyanyuka na kumkumbatia Roma kwa nguvu na kuanza kulia kwa kwikwi kama mtoto, hakuamini Roma alikuwa akifanya utani na yeye , dakika zilizopita alijikta akiwa kwenye mtihani ambao kwake hakuwahi kukutana nao, Edna alijiambia hata yale mawazo yake ya kutaka kuachana na Roma aliokuwa nayo wiki nzima yalikuwa yakitoka kwenye akili yake na sio kwenye moyo wake , hisia zake zilikuwa nyingi sana ambazo zilikuwa zikimtaka Roma abaki kwenye Maisha yake.

“Edna mke wangu nakupenda sana kuliko kitu chochote kwenye dunia hii , ijapokuwa ndoa yetu imeanzia kwenye makaratasi, lakini mimi na wewe ilipangwa tuwe mke na mume, hivyo mimi Roma Ramoni, pamoja na majina yangu yote siwezi kukuacha wewe malkia wa moyo wangu, wewe ndio mke wangu na hakuna mtu mwingine anaweza kukutoa kwenye nafasi yako kwenye moyo wangu”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna usoni.

“Nakupenda pia Roma..”Aliongea Edna kwa aibu sana ,lakini sauti yake ilisikika kwenye masikio ya Roma.

“Mke wangu sijakusikia , rudia tena”Aliongea Roma huku akitabasamu, kwa mara ya kwanza Edna alisema kila ambacho anajisikia moyoni mwake.

“Unanifanya naona aibu sasa , kama hujasikia basi”Aliongea Edna na alionekana kama mtoto.

“Hahaha,,, mke wangu unaonekana kama mtoto mdogo inakufanya uzidi kuwa mrembo”Aliongea Roma huku akimkumbatia kwa mara nyingine na kumbusu kwenye paji la uso.

Naam na hivyo ndivyo ilivyokuwa , hasira zote za mrembo Edna zikawa zimeyeyuka na kwa mara ya kwanza aliweka wazi kile anachojisikia moyoni , kwa mara ya kwanza alitamka bila kulazimishwa kwamba anampenda Hades.

Roma alimrudisha mke wake kazini mara baada ya wao wote kunywa chai ndani ya hoteli hio, alijisikia raha kweli maana alikuwa amerudisha amani na mke wake na kubwa Zaidi Edna amemtamkia mwenyewe anampenda ,jambo hilo lilikuwa likitosha sana kwake na hakuhitaji kitu kikubwa Zaidi.

“Miss Airport nimerudisha mke wangu”Aliongea Roma mara baada ya kufika kwenye meza ya secretary wa Monica, ukweli Roma hakuona haja ya kumficha tena Monica juu ya uhusiano wake na boss wake na Edna pia hakuwa na haja ya kuficha tena , kwani kitendo cha kubebwa juu juu na Roma Monica alikiona.

Monica kwa mara ya kwanza alimwangalia Roma kwa heshima na ile jeuli yake ikawa imemshuka huku akijuitia baadhi ya majibu yake mabaya aliokuwa amempatia Roma kila alipokuwa akionana nae.

Monica alikuwa mfanyakazi wa muda mrefu sana ndani ya kampuni hio ya Vexto , alikuwa amefanya kazi kama secretary wa mama yake na Edna kabla ya kifo chake na baada ya Edna kuchukua majukumu ya kikampuni ndio moja kwa moja akawa secretary wa Edna na ndio aliemuongoza Edna katika kila kitu kilichokuwa kikihusiana na kampuni , hivyo kwa lugha rahisi unaweza kusema kwamba Monica ni mfanyakazi wa kuaminika wa kampuni ya Vexto.

“Boss kwanini haukuniambia mapema jamani , najiona mjinga kwa kutogundua muda wote tokea Roma afike kufanya kazi hapa kwenye kampuni”Aliongea kwa kulalama.

“Nisamehe Sana Monica , nilipaswa kukuambia lakini niliamua kufanya siri, Roma ndio mume wangu”Aliongea Edna na Monica hakuwa kwenye nafasi ya kulalamika sana , aliamua kumuelewa Edna.

Ukweli kilichomfanya monica kutogundua mahusiano ya Edna na Roma ni kutokana na namna ambavyo Roma alikuwa akijiweka kwanza alionekana kuwa mtu ambaye hayupo siriasis na Maisha , hivyo alijiambia Edna kwa tabia yake ya uchapakazi ni ngumu sana kuwa na mwanaume suruali kama Roma anaeshindia kucheza magemu kila akifika kazini, lakini kumbe ndio hivyo tena , Roma ndio alikuwa anammiliki Edna boss.

Muda wote wa kazi Monica aliwaza sababu ambayo imempelekea Edna kumpenda Roma , lakini kila alipofikiria , aliona Roma hakuwa na hata sehemu moja ambayo ilikuwa inamvutia yeye na aliishia kujiambia ni sahihi kabisa kwa wanaume kutowaelewa wanawake.

Roma hakurejea kwenye kampuni yake bali alienda idara ya PR kucheza gemu kupoteza muda kwani nafasi yake bado ilikuwa wazi kama alivyowekeana ahadi na mke wake kwamba ataendelea kuwa mfanyakazi wa Vexto licha ya kwamba anakwenda kuongoza kampuni mpya , walipanga muda wa mchana kutoka pamoja na Kwenda Kunduchi kwa ajili ya kumsapoti Sophia.

Mashindano yaliendelea , shukrani uwepo wa Amina kila kitu kilienda vyema s , Amina aliweza kusimamia vizuri shughuli ya shoo na uzuri ni kwmaba alikuwa ndio mshereheshaji wa tukio zima , jambo ambalo liliongeza Zaidi mvuto.

Sophia kabla ya nafasi yake ya kuingia kuonana na majaji haijafika , alionekana kuwa na wasiwasi kweli , alionekana kila saa alikuwa akigeuza macho yake kukagua watu wanaongia ndani ya hoteli hio ya Maple iliokuwa maeneo ya Kunduchi Beach.

Ukweli Sophia alitaka kumuona Roma kabla ya nafasi yake kufikiwa , wakati akiwa anashangaa ghafla alitoka mbio mara baada ya kumuona mwanamke alieingia eneo hilo , alievalia mavazi ya mahadhi ya kiislamu , alikuwa ni mwanamke wa kiarabu , alikuwa ni mama yake mzazi.

“Mama siamini kama umekuja”Aliongea Sophia kwa furaha.

“Kwanini nisije kukuona mwanangu , nimetua na ndege ya asubuhi ya leo”Aliongea mama yake Sophia na walijikuta wote wakicheka mara baada ya kuangaliana walionekana kuongea kwa ishara.

Wakati wakiendelea kuongea , muda huo ikiwa ni saa saba mchana hatimae Sophia alijikuta akigeuza macho mara baada ya kumuona Edna na Roma wakiingia ndani ya eneo hilo, alishangaa, ni kama vile hakuwa akitarajia wawili hao kuja pamoja, kwani kwa vita baridi ilivyokuwa baina yao , aliamini kupatana kwao kutachukua muda , lakini kwa jinsi Edna alivyoonekana ni dhahiri kabisa ule ugomvi umeisha.

“Ednaaa…!!!”Mama yake Sophia alimsogelea Edna na kumkumbatia kwa furaha.

“Mama huyu ni Bro Roma”Aliongea Sophia akimtambulisha Roma kwa mama yake.

“Ooh!, Mr Roma hatujawahi kuonana ana kwa ana kumbe ndio wewe, sikupata kabisa nafasi ya kukushuru kwa kumuokoa mwanangu kule japani , lakini pia kumpokea na kuishi nae , Asante sana baba , nimefurahi pia kuonana na wewe”Aliongea mama huyu na kumfanya Roma kutabasamu , hakudhania mama yake Sophia atakuwa mzuri namna hio na hapo kitendalwili chake ndio kiliteguka na kuamini Sophia kila kitu alichukua kwa mama yake na kwa balozi alichangia rangi kiasi na kumfanya Sophia kuwa kidogo mweusi.

Sophia alimwangalia Edna kwa furaha na kisha alimwonyeshea dole gumba , alionekana ni kama amefurahishwa na kurudisha amani na Roma.

“Sophia kwa kipaji chako ulichonacho naamini utafanya vizuri kuliko watu wote waliopo hapa, sisi wote tunakusapoti na ndio maana tupo hapa”Aliongea Roma na Sophia alitabasamu na kisha akawaaga na Kwenda kusimama kwenye eneo lake , kwani alikuwa ni mtu wa tatu kabla ya zamu yake kufika.

Roma alimchukua Edna na Kwenda nae mpaka ndani akiwa ametangulizana na mama yake Sophia na waliingia ndani ya ukumbi huo kwa ajili ya kusubiria zamu ya Sophia kuimba ianze.

Dakika kama ishirini hatimae Sophia aliweza kupata nafasi ya kuimba na kuonyesha kipaji chake na kabla hata ya kuanza kuimba alianza kuhojiwa na Amina ambaye alikuwa ndio mshereheshaji na baada ya hapo akawaruhusu majaji kumuuliza maswali kabla ya kuwanza kuimba.

Majaji jumla yao walikuwa ni watatu , Chief jaji akiwa ni msanii mkubwa tu Tanzania wa miondoko ya Hiphop ,AY , haikueleweka ni vigezo gani vilitumika AY kupewa nafasi ya kuwa Chief jaji , lakini alionekana kufanya vyema sana. Majaji wengine wawili walikuwa ni wanawake wasanii wakonwe maarufu Tanzania ambao walikuwa na tuzo za kimataifa mmoja wapo akiwa ni Lady Jaydee.

“Miss Sophia kwanza nikupongeze kwa kuwa mrembo sana , utaimba wimbo gani leo , kuonyesha kipaji chako ili kufuzu na kuingia hamsini bora?”Aliuliza AY.

“Nitafanya Cover version ya wimbo wa Alicia Keys unaokwenda kwa jina la No One”

“Wow!! Huo ni wimbo mzuri sana Sophia ninatamani kuona ni namna gani unaweza kuwa kopi halisi ya Alicia Keys, Tunaomba utushawishi kwa kutumia kipaji chako”Aliongea Jaji na kumpa nafasi Sophia kuimba.

“I just want you close,

Where you can stay forever,

You can be sure that it will only get better,

……………..

No one, no one no one,

Can get in the way of what I m feelin,

No oe , no one no one,“

Can get in the way of what I m feelin”


Sauti aliokuwa akitumia Sophia kusema ukweli ni kama wimbo wa Alicia Keys yeye ndio alieutunga , kwani ulisikika vizuri kuliko ulivyoimbwa na mtunzi mwenyewe.

Roma ndio aliekuwa wa kwanza kusimama na kuanza kupiga makofi kwa shangwe , ukweli muda wote ambao Sophia alikuwa akiimba alikuwa ameangalia upande ambao Roma yupo , yaani ilikuwa ni kama alikuwa akimwimbia , hakika ilifurahisha kumsikiliza akiimba na kila mmoja alihusudu uimbaji wake.

Tukio lote hilo lilikuwa likionyeshwa mubashara kwa kupitia runinga , hivyo ni rahisi kusema kwa uwezo aliouonesha alikuwa amejibebea mashabiki sio ndani tu ya ukumbi lakini pia Tanzania kote kwa wale waliokuwa wakifuatilia matanganzo hayo moja kwa moja.

“Miss Sophia mimi sina cha kusema , umeonyesha kipaji kikibwa sana kukilo wenzako wote waliokutangulia , naomba nikuone tena raundi inayofuata kwenye hamsini bora , Welldone”

“Asante Chief Judge”Aliongea Sophia na zamu iliofuatiwa akapotea jaji mwingine ambaye tokea mwanzo alionekana kukandia watu kweli na kuwakatisha tamaa , alikuwa kopi halisi ya Salama Jabiri wa Bongo Star Search”

“See you Sophia on next round”Aliongea yule jaji na kumfanya Sophia kuinama kwa heshima sana kushukuru na Sophia akawa amepata asilimia zote na kupita raundi inayofuata ya hamsini bora , raundi ambayo inambidi kukaa kambi na wasanii wenzake mpaka pale mashindano yatakapoisha , au atakapoaga kama atafanya vibaya .

Edna alifurahi kumuona mdogo wake alifanya vizuri na alijiambia atamsapoti mpaka kuwa msanii mkubwa sana Afrika na duniani kwa ujumla , alijiambia Sophia ni dhahabu licha ya kwamba hakuwa akitaka pesa kutoka kwake ila alijiambia kama Sophia atapata umaarufu kupitia kampuni yake basi mauzo yataongezeka kwani itakuwa rahisi kufanya matangazo na kufikia watu wengi..

“Hongera Director kwa kuandaa vyema mashindano, ni nje ya matarajio yangu”Aliongea Edna akimsifia Roma.

“Hehe.. babe inabidi unipe zawadi hata ya kiss sasa mume wako”

“Zawadi kwani lazima iwe kiss , huwezi kuomba kingine mpaka uombe mambo ya kutia aibu”Aliongea Edna kwa aibu na Roma alijikuta akicheka.

Wakati wakiendelea kuongea Roma alisimaa na kumuacha Edna na alionekana alikuwa akienda kuongea na Daudi.

“Miss Edna… !”Sauti nyororo kutokea nyuma ilisikika kwenye ngoma za masikio ya Edna na alipogeuka , aligundua ni Amina.





SEHEMU YA 338

Amina alimuomba Edna msamaha kwa kile kilichotokea wiki iliopita na kueleza kwamba haikuwa nia yake ya kumgombanisha yeye na Roma , Edna alimsikiliza Amina kwa kila alichoongea na akahitimisha kwamba anaomba kuendelea kuwa Sekretary wa Roma kwani hana nia mbaya na kampuni na kumuahidi kwamba atawezekeza nguvu zake zote kuhakikisha kampuni ya Vexto inapata umaarufu ndani ya muda mfupi kwa kupitia uzoefu wake alioupata kwa kufanya kazi na vituo vikubwa vya Habari.

“Amina umeongea kila kitu lakini sijasikia ukiongea juu ya mahusiano yako na mume wangu”Aliongea Edna akimwangalia Amina.

“Edna kuhusu hilo…”Amina alijikuta akishindwa kujua ni namna gani ya kujibu kwani alishindwa kutamka moja kwa moja kwamba hana mpango wa kumuacha Roma,

“Edna naomba usinichukie tafadhali , please , please…. Nitakutii kwa kila utakachoniambia ila naomba japo siku moja moja niwe na mume wako , nakuomba tafadhari”Aliongea Amina huku akipasha viganja na kumfanya Edna kutamani kucheka , kwa namna moja Amina alionekana kama mtoto na hiko ndio kilichomfanya Edna kutamani kucheka, lakini pia kilichomfurahisha ni namna ambavyo Amina anajitahidi kuwa mkweli kwake.

Roma alikua ashamaliza kuongea na Daudi kwani mashindano yalikuwa yamesitishwa kwa masaa kadhaa ili watu Kwenda kupata chakula cha mchana , hivyo alivyogeuka aliweza kumuona mke wake akiongea na Amina na ilibidi kwanza asimame mbali , alijua ni jambo jema sana kama Edna atapatana na Amina , aliona utakuwa mwanzo mzuri sana wa wengine pia kupatana na Edna na Maisha kuendelea bila migogoro.

“Amina sipo kwenye nafasi ya kukuzuia wala kukuruhusu kuendelea na Roma kwani yeye ndio mwamuzi mkuu , ila ninachokushauri tu ni kwamba usije ukashikwa na tamaa , mimi ndio mke wa Roma na itabakia hivyo”Aliongea Edna akiwa siriasi , huku hata yeye mwenyewe akijishangaa kwanini amekuwa mrahisi kutamka maneno hayo.

“Edna siwezi kushikwa na tamaa nitashukuru kwa kile kidogo nitakachokipata kutoka kwa Roma na sitotamani kuwa mke wa Roma, nitakuheshimu kama mke .. na juu ya yote Edna nimetokea kukupenda pia ghafla, kuongoza biashara ya mabilioni ya pesa sio jambo rahisi kwa mwanamke kufanya , lakini wewe umeshinda vyote , Edna wewe ni Role model wangu, halafu umrembo sijawahi ona”Aliongea Amina na mwanamke huyo alikuwa ‘manipulative’ sio mchezo , alijua kucheza na akili za binadamu wenzake na kujua ni kipi aongee na kwa wakati gani na maneno ya Edna licha ya kwamba hakuonyesha waziwazi kuguswa , lakini alijisikia kitu sio cha kawaida , kwanza alijiambia Roma alikuwa akimpenda yeye kuliko wanawake zake wote , hivyo yeye ni kama ndio alieshikilia mpini , hivyo hakuwa na sababu ya kuogopa michepuko ya Roma.

Sophia ndio aliekuwa wa kwanza kufika nyumbani , kwani asubuhi aliletwa na Dereva wa Edna , bwana Innocent , hivyo hata muda wa kurudi nyumbani jioni alikuwa wa kwanza, Yezi na wanafamilia wengine siku hio walikuwepo nyumbani wakiwa wameketi kwenye runinga wakiendelea kuangalia tamthilia na hata kwa Blandina alikuwa ameketi kwenye masofa akiwa ameungana na wanafamilia.

Blandina alionekana kuwa na furaha na amani sana , na hio ni mara baada ya kupokea simu kutoka kwa moja ya mkuu wa kituo cha kulelea Yatima kilichokuwa Sudani.

Unajua katika vituo vyote ambavyo Blandina alifungua , kituo cha Sudani ndio kilikuwa kikubwa kuliko vituo vingine vyote , kilikuwa na uwezo wa kubeba Watoto elfu moja kwa wakati mmoja na wote kwa pamoja kupata huduma bora kabisa, ndio kituo ambacho alipata changamoto kubwa kwenye ujenzi wake , kwani ilimbidi kutembeza bakuli la michango pamoja kuomba ufadhili kwa matajiri wengi mpaka kikajengwa na kukamilika, wakuu wote wa vituo hivyo walikuwa ni wanawake na ni marafiki zake , haikueleweka aliwezaje kuwa na marafiki wengi kiasi hiko , lakini wanawake hao wote walikuwa wakimfahamu kwa sura yake halisi na hata kwenye hivyo vituo kuna picha yake.

Sasa siku hio mchana aliweza kupata taarifa kutoka kwa rafiki yake ambaye anaongoza kituo huko Sudani baada ya kituo hiko kupata ufadhili kutoka taasisi ya Bill and Mellinda Gate Foundation kutoka Marekani katika upande wa Elimu na Chakula , taarifa hio ilikuwa njema sana kwake kiasi kwamba alijiuliza jambo hilo limewezekanaje, kwani ni kwa miaka mingi sana kituo hiko kilikosa ufadhili wa kueleweka na mara nyingi kilitegemea watu wanaotembelea na kubeba zawadi , lakini pia pamoja na hela zake alizowekeza faida ilikuwa ikienda moja kwa moja katika kituo hicho.

Sasa moja kwa moja aliamini huenda Roma ndio alivyomsaidia na ndio maana akapata ufadhili huo.

“Wamepatana”AliongeaSophia mara baada tu ya kufika sebuleni akiwa na furaha.

“Sophia unamaanisha nini?”Aliuliza Yezi.

“Bro na Sister wamepatana”Aliongea Sophia na sasa kufanya kila mmoja kuelewa alichokuwa akimaanisha ni nini.

Blandina alimwangalia Bi Wema na kisha akatabasamu na aliona maneno yake ya asubuhi bibi huyo yalikuwa ya kweli , Bi Wema alimwambia asubihi Blandina kwamba awaache watapatana na imegeuka maneno yake kuwa ya kweli, Blandina alijiambia kilichobakia hapo ni kuhakikisha Edna na Roma wanalala pamoja na ili hilo lifanikiwe anatakiwa kuongea na Edna.

Upande wa Roma baada ya kumrudhisha mke wake Kazini yeye alirejea kwenye jengo la kampuni kwa ajili ya kuendelea kucheza gemu huku akivuta muda ili saa kumi arejee nyumbani.

Lakini wakati akiwa kwenye majukumu yake ndio alipopokea simu kutoka kwa Diego.

“Mfalme Pluto tumekamilisha uchunguzi wetu na ripoti ipo tayari”Aliongea Diego mara baada tu ya Roma kupokea simu na Roma alitabasamu.

“Diego mmefanya kazi kubwa nitapitia jioni ya leo kuona hio ripoti”Aliongea Roma

Ilivyofika saa kumi Roma aliingia kwenye gari yake na safari ya kuelekea Kigamboni ilianza mara moja , alikuwa na hamu ya kujua ni nini kilimtokea mama yake Edna mpaka akawa kwenye mpango wa majaribio , ulioratibiwa na kampuni ya Maya.

*********

Upande mwingine siku hio hio Raisi Senga alikuwa akijiandaa kwa ajili ya kuanza safari yake ya Kwenda Nigeria kwa ajili ya kuhudhuria ibada ya mpasuko wa mwezi.

Sasa unachotakiwa kwanza kabisa kuelewa kuhusu ibada hii ya mpasuko wa mwezi maana yake ni kwamba ni ibada ambayo inafanyika katikati ya mwezi na ndio maana ikapewa jina la Mpasuko wa Mwezi(Rite of Moon Rift).

Hii ni sehemu ya ibada inayofanyika kila mwezi , ibada hii inakuwa na maana kubwa sana katika jamii ya siri ya Freemason, ilikuwa na maana Zaidi ya neno lenyewe la kupasuka kwa mwezi.

Moja ya matukio ambayo yanafanyika kwenye ibada hii ni kupokea wanachama wapya ambao wanataka kujiunga, ambayo wapo kwenye ngazi ya kwanza(First Degree) ambayo maana yake ni ‘Kukubaliwa’.

Sio kila mtu anaweza kujiunga na jamii hizi kutokana na kwamba kuna vigezo ambacyo vimewekwa mpaka mtu kukubaliwa na kuwa mwanachama kwa ngazi ya kwanza , kwanza kabisa kuna maombi ya kukubaliwa ambayo mtu anafanya ili aingie , maombi ambayo yanaambatana na ulipaji wa kiasi cha pesa kisichopungua milioni kumi na baada ya hapo kutaanza taratibu za aliefanya maombi kufuatiliwa ili kuangaliwa kama anakidhi vigezo, sasa moja ya kigezo kikubwa ambacho kinaangaliwa kwa mwombaji ni mchango wake kwenye jamii , lakini pia ushawishi wake kwa ujumla, kama huna ushawishi watasoma nyota yako kuangalia ni ‘Pontential’ gani ambayo mtu anayo kwenye miaka ya mbele(Nitaelezea kwa ufupi mbele)

Maswala hayo yote yanaongozwa na Lodge Grand Master kwa kutumia washirika ambao wapo kila nchi ndani ya Afrika.

Sasa sababu moja kubwa ambayo Illuminat wanakinzana na Freemason ni kwamba , Freemason yenyewe haimbagui mtu , wanachokiangalia ni uwezo wa mtu kukidhi tu vigezo , kwa mfano kama wewe ni mganga wa kutumia nguvu za giza wa kuaminika na ukakidhi vigezo unaingia huko , yaani hakuna kubaguliwa, upande wa Illuminat wenyewe hawa wanaabudu sayansi na wanaamini sayansi ndio kila kitu na ndio Mungu wa kweli na wanaamini ili mtu kukidhi vigezo na kuitwa Illuminat lazima awe na mchango chanya kwenye sayansi.

Anachotaka kukifanya Athena mpaka kumwagiza The Fisrt Black ili kufatilia wanachama wote wa Illuminat ni kwamba ,anataka kufufua upya nguvu ya kundi hili la Illuminat na kuwa wasaidizi wake wakati atakapoweza kuamsha roho za ndugu zake zilizomezwa na binadamu kwa kutumia Jiwe la Kimungu , yaani Godstone.

Sasa wiki iliopita , ikiwa ni baada ya siku nne baada ya kukutana na Blandina kule kwenye kituo cha kulelea Yatima , Raisi Senga aliweza kutembelewa na balozi wake tena kwa mara ya pili na kupewa taarifa ambayo kusema ukweli ilimfanya kuwa na amani sana.

Taarifa yenyewe ilikuwa ni inayomuhusu Blandina, taarifa hio ilikuwa ikimueleza kwamba juu ya kafara ya kiimani ambayo alipaswa kutoa imebatilishwa.

“Mheshimiwa licha ya kwamba kafara hio imebatilishwa haimaanishi kwamba hakuna namna nyingine ya kuipima Imani yako, Msingi wa Freemason sio kumwanga damu bali ni kuhakikisha wanachama wote wanakuwa na Imani thabiti , hivyo unapaswa kujiandaa kwa maelekezo mengine , kama huwezi kutoa kafara basi wewe mwenywe unatakiwa kujitoa kafara”Aliongea Balozi na kumtisha sana Raisi Senga.

“Samahani ndugu balozi unasema kwamba mimi ndio natakiwa kufa kwa niaba ya Blandina?”Aliongea Raisi Senga na kumfanya Balozi alievalia suti nyeusi kutabasamu.

“Mheshimiwa kujitoa kafara haimaanishi kifo mara zote”Aliongea na kumfanya Raisi Senga kuvuta pumzi ya ahueni

“Kwahio nini kinakwenda kunitokea , ni kafara gani ambayo ninatakiwa kutoa kama sio uhai wangu , kama mambo yakiendelea kuwa magumu hivi nitaomba kubatilisha ombi langu”

“Mheshimiwa huna haja ya kuwa na wasiwasi , kinacho kuogepesha ni kwasababu Imani hii inakwenda kuwa mpya kwako , kuhusu pia kujitoa haiwezekani kwani ushaingia hatua ya kwanza ya KUKUBALIWA na pia kuna adhabu kama utataka kujitoa na inaweza kuwa kubwa Zaidi kuliko kujitoa wewe mwenyewe kafara”Aliongea na kumfanya Mheshimiwa kuanza kujutia kwanini amejiingiza kwenye hayo mambo , kwani kila neno analotamka ndugu Balozi licha ya kwamba alikuwa akiongea kwa upole lakini maneno yake yaliambatana na ujazo wa hofu ndani yake.

“Mheshimiwa kuna aina mbili za kutoa kafara katika Imani za jamii yetu , ya kwanza ni kuthibitisha Imani yako kwa kutoa kitu unachopenda Zaidi kwenye Maisha yako na aina ya pili ya kafara ni kujitoa wewe mwenywe kwa kufanya kitu ambacho unakichukia sana kwenye Maisha yako , ambacho kinaenda kinyume na kanuni za Maisha yako, hivyo mheshimiwa kabla ya Ibada hakikisha unatambua ni jambo gani kwenye Maisha yako unalichukia sana na kamwe huwezi kulifanya”

Dunia imeumbwa katika msingi wa Uwili unaotofautiana(Kinyume nyume na kimbelembele) lakini unaovutana pamoja ,wazungu wanasema Black and White , wachina wanasema Ying And Yang ,maneno haya yanasimama kwa mfano wa kwamba, kama mtu kuna kitu anachokipenda kwenye Maisha yake sana na anaogopa kukipoteza(White) basi atakuwa na kitu anachokichukia sana kwenye Maisha yake na hata umfanye nini hawezi kukifanya(Black), kuna mifano mingi Zaidi kama vile uwepo jinsia ya kike na ya kiume.

Sasa katika jamii hizi kutoa kafara ni upande wa White yaani mtu anatoa kitu ambacho anakipenda sana na kama hawezi kutoa kitu hiko basi atachagua upande mwingine yaani Black(Kujitoa kafara) , huu ni upande ambao mtu anauchukia kufanya kwenye Maisha yake yote ,ijapokuwa kuna Zaidi ya maana kwa upande wa Black kwa mfano kama hupendi kufanya kitu unachokichukia unaweza pia kutota kafara kwa kupitia uhai wako.

Sasa mheshimiwa Senga alikuwa na mtihani wa kufahamu ni kitu gani anakichukia kwenye Maisha yake na hicho ndio atakifanya kwa namna ya kujitoa kafara yeye mwenyewe baada ya kushindwa kutoa kafara ili mradi atimize kigezo cha uthabiti wa Imani na baada ya mambo hayo yote kukamilika sasa ndio faida zitakapoonekana(Privelege’s of Brotherhood) ,lakini wakati huo akivuka sasa hatua ya kwanza ya kukubaliwa na kuingia hatua ya pili ya ‘Second Degree’.

Sasa inasemekana kwamba wanachama wengi huchagua upande mweusi(Black) upande wa kujitoa kafara na kinachofanya watu kuchagua huu upande ni kwasababu moja tu ya kwamba wanaume wote wanafanana sana kwenye kitu ambacho tunakichukia kwenye Maisha yetu kukifanya.

Wakati hayo yakiendelea upande wa huku Tanzania , upande wa Kenya ni hivyo hivyo Kamau Kamau baada ya kushindwa kumrudisha Blandina Kenya na kigezo cha kafara yake kubatilishwa alitakiwa kuchagua upande wa kujitoa kafara yeye mwenyewe kama ilivyo kwa raisi Senga.

Raisi Kamau kamau alikaa chini kwa masaa mengi sana akifikiria ni jambo gani ambalo analichukia kwenye Maisha yake , jambo ambalo hayupo tayari kulifanya na katika mahesabu yake yote kuna jambo moja kila alipokuwa akilifikiria , mapigo ya moyo yalikuwa yakienda kasi mno.

“Naomba isiwe kweli , ninachokifiria”Aliwaza Raisi Kamau usiku mmoja kabla ya siku ya kesho kufika ili kuanza safari yake kuelekea Nchini Nigeria kuhudhuria Ibada ya mpasuko wa Mwezi.

******

Ni muda wa saa kumi na moja Edna alionekana akiingiza gari lake kwenye uzio wa jumba lake la kifahali analo ishi na familia yake.

Mrembo huyu mara baada ya kuegesha gari lake na kutoa mkoba wake , alifuatwa na Derick mlinzi wa geti na akamsalimia kwa heshima.

“Madam kuna huu mzigo wako umeachwa muda si mrefu”Aliongea Derick huku akinyoosha mkono kumpatia Edna bahasha ya khaki iliokuwa kwenye mikono yake.

“Ni nani ambaye kakupatia?”

“Hajajitambulisha kwa majina lakini alisema ni mzigo wako , nilijaribu kukataa kuchukua lakini alinilazimisha na kuniambia lazima nimfikishie muhusika, nisamehe Madam kama nimefanya kosa”

“Okey hakuna shida unaweza kuendelea na majukumu yako”Aliongea Edna huku akiingia ndani akiwa ameshikilia Bahasha yake, lakini kabla hajafika ndani Lanlan alitoka spidi spidi na kumrukia Edna kwa furaha akimlaki na Edna alimbeba juu juu na Kwenda nae ndani.

Yalipita masaa kadhaa , baada ya Eda kutulia , sasa alikuwa ndani ya ofisi yake ya kujisomea na mkononi akiwa anafungua bahasha aliopatwa na Derick , bahasha ambayo inatoka kwa mtu asiemfahamu.

Edna alitoa karatasi zilizokuwa ndani ya bahasha na kuanza kuzisoma na ndani ya sekunde ishirini tu , Edna macho yalimtoka na kudondosha chini zile karatasi huku akiwa ni mwenye kutetemeka.
Episode namba 336 Edna hatakaa aisahau maishani mwake[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
SEHEMU YA 341.

Edna sasa alielewa kwanini Blandina alisema kwamba picha hio alikuwa amepiga yeye, kumbe alishawahi kukutana na Raisi Jeremy huko Australia akiwa na mama yake wakila bata.

Roma mwenyewe alishangaa kumbe mama yake ni msomi mkubwa tu, lakini hata hivyo ilikuwa ni halali kabisa, kwani mambo ambayo Blandina aliweza kuyafanya kwa jamii kupitia sura ya Maina yalikuwa makubwa sana, kwani kama utaweza kupiga hesabu ya thamani ya vituo vyote ambavyo alivianzisha kwa nguvu zake ni Zaidi ya Dollar milioni mia moja.

Upande wa Roma yeye hakushangaa sana kwani alikua akijua mzazi wa Edna , ila mbele ya Edana alijifanyisha na yeye kushangaa , kwani alijua kama atasema alikuwa akifahamu na akakaa kimya , Edna angekasirika.

Maelezo ya Bi Wema hayakuwa na utofauti sana, kwani alishaelezwa na Raheli mwenyewe juu ya baba mzazi wa Edna, lakini sasa jumla yao wote wakajiuliza swali moja ni nani ambaye ameleta taarifa hio, na ni kwa madhumuni yapi, upande wa Roma aliamini sio Raisi Jeremy alieleta hio karatasi aliamini kuna mtu mwingine ambaye ameleta barua hio ila hakujua sababu ni nini na aliajiambia ni swala la muda tu atafahamu.

Edna sasa anajikuta akianza kuhisi huenda hata mtu aliekuwa akijiita The Protector alikuwa ni Raisi Jeremy , kwani mambo mengi ambayo aliokuwa akimsiadia yalikuwa yakihataji intelijensia ya hali ya juu.

Licha ya kwamba alihuzunishwa na jambo hilo , aliona mama yake hakuwa mtu wa kulaumiwa , kwani kulikuwa na mkataba wa yeye kutambulika kama mtoto wa Adebayo, lakini pia aliweza kufurahi na kuchukia kwa wakati mmoja kwa kumfahamu baba yake , kilichomfanya kufurahi ni kwamaba alikuwa ashatoka kwenye sintofahamu aliokuwa nayo kwa muda mrefu lakini kilichomfanya kuchukia ni kitendo cha kuwa mtoto wa nje ya ndoa lakini pia Raisi Jeremy kutoonyesha dalili yoyote ya kumtambua mbele yake.

“Bi Wema Raisi Jeremy anafahamu kama mimi ni mtoto wake wa Damu?”Aliuliza Edna.

“Juu ya hilo sifahamu , kwani mama yako alipofahamika ni mjamzito tayari alikuwa anafahamika kama mke wa Adebayo”Aliongea Bi Wema na Edna alitingisha kichwa na kisha kwa huzuni alirudi chumbani kwake.

Roma alijikuta akimuonea huruma mke wake , kwani aliweza kukumbuka maneno ya Raisi Jeremy juu ya kutokuwa na mpango wa kutomfanya Edna kuwa mtoto wake licha ya kwamba anamtambua, Alimuona mke wake hakuwa na utofauti na Yatima licha ya kwamba alikuwa na pesa nyingi, hisia ambazo zilimrudisha miaka kadhaa nyuma akiwa peke yake na Lorraine kwenye kisiwa , wakiwa hawana Baba wala Mama.

*******

Zilipita siku kumi , upande wa kwenye kampuni mashindano yalikuwa yakiendelea kama kawaida na Sophia alikuwa akifanya vyema sana kiasi cha kumpelekea kujipatia mashabiki wengi sana , kwani kwenye mitandao ya kijamii alikuwa akizungumziwa sana , huku Clip zake akiwa anaimba zikisambaa sana, watu wengi wakimtazamia kuwa mshindi wa mashindano hayo.

Mashindano yalikuwa na mvuto mkubwa sana kwani yalikuwa ya kipekee na mpangilio wake kupendwa na wengi lakini pia ndio mashindano ambayo yalikuwa yakifuatiliwa kwenye nchi nyingi sana na hio ni kutokana na kuhusika kwa Christen kwenye mashindano hayo kama jaji ambaye anatazamiwa kushiriki siku ya mwisho ya fainali, lakini pia Christen kitendo chake cha kuyapigia mashindano hayo ‘Promo’ wakati akiwa kwenye mahojiano na Vexto Tv , iliyapaisha sana duniani mashindano ya Kizazi nyota na kufanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa.

Zilikuwa zimebakia hatimae wiki tatu mpaka mashindano hayo kuhitimishwa , kwani kila wiki mashindano yalikuwa yakifanyika mara mbili na washiriki watano walikuwa wakitoka kwenye kila siku michuano.

Ikiwa ni siku ya jumamosi , kabla ya mashindano kuanza mshereheshaji Amina kanani aliweza kutoa tangazo juu ya ujio wa msanii mkubwa atakaetumbuiza siku ya fainali , msanii wa kike mrembo kutoka Korea Kusini afahamikae kwa jina la Yoon- He

Yoona- He ni moja ya wasanii maarufu ambaye anauza sana kazi zake za kisanaa ndani ya Korea na nje ya Korea , alikuwa na mashabiki wengi sana na kitu ambacho kilimfanya pia kutambulika kimataifa ni pamoja na uwezo wake katika mambo ya uigizaji , akiwa ameshiriki kwenye muvi na Tv Shows mbalimbali mbali ambazo zilifanya vizuri sokoni kimnataifa.

Licha ya kuwa msanii lakini pia inasemekeana mafanikio ya Yoon-He yalichangiwa na ukwasi wa pesa wa familia yake, kwani babu yake Yoon-He ni moja ya wafanyabiashara wakubwa walijikita katika udhalishajii wa vifaa vya kidigitali vya mambo ya nyumbani , akitajwa kama Tajiri namba kumi ndani ya Korea.

Hivyo baada ya Tangazo hilo liliibua munkari sana kwa mashabiki na wafatiliaji wengi pamoja na wale ambao walikuwa shabiki wa Yoon -He,menejimenti ya Yoon He ndio iliofanya mawasiliano na kampuni ya Vexto na kuomba ushiriki katika kuimba siku ya fainali jambo ambalo lilikubaliwa na Daudi pamoja na Amina mara moja , huku upande wa Roma kwakua hakuwa sana mpenzi wa nyimbo wala shabiki wa mtu yoyote alikubali tu ilimradi Yoon He angeongeza mapato.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana tokea mwanzo wa shindano hilo ndani ya siku chache tu , kwani faida ilikuwa ikionekana lakini pia wafatiliaji walikuwa wengi hivyo kufanya matanganzo ya kampuni ya Vexto International kufikia watu wengi sana na kufanya hata hisa za kampuni kupanda ndani ya muda mfupi , jambo ambalo lilimfurahisha sana Edna na kuona kwamba yalikuwa mawazo sahihi ya kufungua kampuni ya Habari na burudani, lakini pia lilikuwa wazo sahihi kumwachia Roma kuongoza kampuni hio.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa kwenye mawazo ya hapa na pela huku akiangalia Skrini ya tarakishi yake iliokuwa ikionyesha namna ambavyo mauzo ya hisa yamepanda kwa siku hio mara baada ya kutangazwa kwa ujio wa msanii Yoon-He.

Wakati akiendelea kuwaza alijikuta akikumbuka maneno ya mama mkwe wake siku mbili zilizopita juu ya Roma kuhamia kwenye chumba chake huku Lanlan ahamie kwenye chumba cha Qiang Xi , Edna alionekana kutafakari kidogo , huku akikumbuka siku hizo kumi zote Maisha na Roma yalikuwa mazuri sana kiasi kwamba hawakugombana na kubwa Zaidi tokea amtamkie Roma anampenda ni kama vyumba vya hisia visivyoonekana kwa darubini za kiganga kwenye moyo wake vilifunguka wazi kiasi kwamba hisia za kimapenzi zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba hata akimuona tu alikuwa akinyegeka.

Zimebaki siku tano tu kufikia tarehe ishirini na Tisa, Babu yake Lanlan asipotokea ndio siku nitakayo mlea Lanlan kama mtoto wangu na Roma kama baba yake na ndio siku ambayo Lanlan ataenda kulala na Qiang Xi na mimi kulala na Roma kama mume wangu”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake na kujikuta akitabasamu na alikuja kushituliwa na Monica ambaye aliingia hapo akiwa na faili tatu ambazo Edna anapaswa kuzisaini kabla hazijapelekwa kwenye kampuni Tanzu ili hatua Zaidi kuchukuliwa.

*******

Upande wa Raisi Senga alifanikiwa Kwenda Nigeria na kurudi salama salimini , lakini licha ya hivyo alionekana kutokuwa sawa kama alivyondoka , alionekana kuwa kwenye mawazo kiasi ambacho kilimfanya hata mke wake Damasi kujua mabadiliko ya mume wake.

“Senga ulivyoondoka sio kama ulivyorudi , unaonekana kuwa na mawazo mume wangu k ni jambo gani linaendelea?”

“Mama Ashley niko sawa ni maswala ya kikazi tu ndio yananifikirisha”Aliongea Senga kwa kujitutumua na muda huo alikuwa ndio anarudi kutoka ofisini.

Ukweli ni kwamba kilichomfanya Damasi kuwa na wasiwasi na mume wake ni kutokana na kwamba ,tokea arudi kutoka Nigeria alikoenda kikazi , hakumgusa kabisa na ndio maana Damasi alikuwa akipatwa na wasiwasi kwani haikuwa tabia ya Senga , lakini jambo lingine ni kwamba hakuwa sawa kimawazo , yaani Raisi Senga kuna muda alikuwa akiangalia sehemu basi macho yake yataganda sehemu hio mpaka ashituliwe na hiko ndio kikamfanya Damasi kuwa na mawazo.

“Senga nadhani unaelewa kauli yangu ya siku zote, licha ya kwamba wewe ni raisi wa Watanzania nikiwa mimi mmoja wapo ,lakini pia utambue mimi ni mkeo na unatakiwa kuwajibika kwangu na kwa familia”Aliongea Damasi kwa msisitizo na kisha akatoka kwenye chumba chao cha kulalaia na Kwenda upande wa Sebuleni kuendelea kuangalia Runinga.

Ikiwa ni siku nyingine baada ya Raisi Senga kuingia ofisini , asubuhi hio alionekana kuwa na ugeni ambao alionekana alikuwa akiusubuiria, ni kweli baada ya madakika kadhaa alionekana mwanaume mmoja wa kihindi mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi akiingia ndani ya ofisi ya kukutania wageni akiwa ameongozana na Katibu Muhtasi.

“Mheshimiwa Mjumbe kutoka baraza la haki za binadamu kashafika”Aliongea Katibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kumruhusu , muda ule ule mjumbe yule wa kihindi aliingia ndani ya eneo hilo na walisalimiana kwa bashasha na baada ya Raisi Senga kumkaribisha mgeni wake , palepale alitoa maagizo juu ya kikao hicho kuwa cha siri kwa muda wa dakika kadhaa na baada ya hapo baadhi ya viongozi wa Ikulu wataruhusiwa kuingia kushiriki kwenye mazungumzo pamoja na kupiga picha na kuweka mitandaoni na kwenye gazeti la kiserikali.

“Mheshimiwa nadhani hakuja haja ya maongezi Zaidi kwani kila kitu kishaongelewa, kama nilivyojitambulisha mimi ni mwanachama wa baraza la haki binadamu kutoka UN nikihudumu upande wa Afrika (Umoja wa mataifa) na nipo hapa kwa ajili ya kupata sahihi yako juu upatikanaji wa haki za LGBTQ(Mapenzi ya jinsia moja) hapa Tanzania”Aliongea yule mwanaume ambaye alijitambulisha kwa Mheshimiwa Senga kwa jina la Vishnu Gupta.

Mheshimiwa alifikitia kidogo , mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akitaka yeye asaini mkataba wa kulinda haki za mashoga hapa Tanzania , ijapokuwa makubaliano yake nchini Nigeria hayakuwa ni kwa ajili ya kutangaza hadharani kama anakubali mashoga lakini alitakuwa kutia sahihi kama mkuu wa nchi ili kuhakikisha kwamba serikali haingilii haki za mashoga nchini.

“Hakuna shida bwana Vishnu nitasaini mkataba kwani ni sehemu ya makubaliano yangu”Aliongea Raisi Senga na Vishnu alitoa karatasi na kumpatia raisi Senga na baada ya kuzisoma kwa muda mfupi hatimae aliweza kuzitia Saini , jambo ambalo lilimfanya Vishnu kutabasamu na alipeana mkono kama ishara ya makubaliano na baada ya hapo ndipo Kamera ziliruhusiwa na mazungumzo yakawa wazi , huku raisi Senga akitoa ahadi kwamba ataendelea kukomesha vitendo vyote ambavyo vnakiuka haki za kibinadamu.

Baada ya kikao kuisha mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu , licha ya kwamba alishasaini karatasi hizo ambazo zilikuwa ni ‘implicity’ kwenye utekelezaji wake , lakini bado alijiona kama mtu aliekosea watanzania , lakini pia aliejikosea yeye mwenyewe , lakini wakati huo huo Mheshimiwa Senga kuna tukio ambalo lilikuwa likijirudia rudia kwenye akili yake kiasi kwamba lilimfanya kabisa kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mke wake mpaka kupelekea malalamiko.

Mheshimiwa Senga alijikuta akijiegamiza kwenye kiti chake huku akikusanya mikono yake pamoja , alionekana kuwaza sana , haikueleweka mara moja ni nini kilichotokea kwenye Ibada ya Mpasuko Wa Mwezi kutokana na usiri mkubwa uliokuwepo , lakini jambo moja ambalo ni dhahiri ni kwmaba mheshimiwa Senga alikuwa akifanya maamuzi ambayo yapo nje ya kile anachokisimamia kama Raisi licha ya kwamba alishasaini ‘Impilicity Law’ inayohusiana na Mashoga aliamini siku sio nyingi atalazimishwa kusaini ‘Explicity Law’ inayohusiana na mashoga.

(Implicity Law ni hitimisho la kisheria ambalo linampa mtu haki ya kitu pasipo kuingiliwa licha ya kwamba sheria hio haiwekwi wazi, kwa mfano kauli ya kiongozi mmoja wa dini akisema kwamba Mapenzi ya jinsia moja sio Kosa , sio uhalifu lakini ni Dhambi hio ndio sheria isio ya moja kwa moja lakini yenye kutekelezwa , yaani huwezi kusikia kiongozi akisema hadharani kama anakukataa ushoga ilihali sheria hio ishasainiwa.

Explicity Law ni aina ya sheria ambazo ni za moja kwa moja na zinapaswa kutekelezwa kwa namna yoyote ile na mara nyingi sheria hizi kwa hapa Tanzania hupitishwa na Bunge pamoja na mahakama halafu ndio raisi atasaini ili ianze utekelezwaji wake.

Wanasheria mtatusaidia Zaidi hapo.

**********

Naam ilikuwa ni siku ya jumamosi Roma alionekana Kibaha kwa Mathiasi akikunja kushoto akiwa anendesha gari yake kuelekea upande wa mji wa kisasa , mji ambao unamilikiwa na kampuni ya Vexto Group.

Roma aliendesha gari yake kwa utaratibu huku akifurahia mazingira safi yaliokuwa yapo kandokando ya barabara hii kuelekea kwenye mji huu, kusema ukweli licha ya kwamba ilikuwa mara yake ya pili kufika kwenye huo mji lakini muonekano wake siku hio ulikuwa kama ni mpya kwake na alijiambia ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanyika mpaka kujenga makazi hayo ya kisasa kabisa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dakika kama tano aliweza kuingiza gari yake kwenye geti kubwa linarohusu magari kuingia kwenye ‘Apartment’ hizo na alikwenda moja kwa moja kuegesha kwenye Parking ya muda mfupi na akashuka na kuanza kutembea uelekeo wa jengo la Athena.

Alikuwa mahali hapo asubuhi hio kutokana na kwamba alikuwa na miadi na mrembo Suzzane , ambaye baada ya kuwasiliana nae alimwambia kwamba amfuate nyumbani kwake na Roma kwakuwa ndio alikuwa na shida ilimbidi kufanya hivyo ili kuonana na mrembo huyo.

Baada ya kufika chini kabisa ya hilo jengo alipiga simu Kwenda kwa Suzzane na alipewa maelekezo ya Kwenda mpaka Floor namba kumi na kusimama kwenye mlango wenye namba 200 ndio Apartment yake.

Tokea mrembo huyu aje kumchukua kwa mara ya kwanza kule Mbagala hakuweza tena kuongea nae moja kwa moja , kwanza Roma alimchukulai Suzzane kama mwanamke Siriasi asiependa utani , lakini pia Suzzane mara nyingi alikuwa ndani ya idara hii kwahio ilikuwa ngumu kwake sana kuonana nae mara kwa mara na kumzoea.

Dakika chache tu Roma alikuwa nje ya mlango namba 200 na alibonyeza kitufe cha kengele na kisha akasubiri mlango kufunguliwa na zilipita dakika kama mbili hivi hatimae mlango ulifunguliwa na mrembo Suzzane ambaye alikuwa amevalia gauni fupi la kumpendeza.

Suzznae alikuwa mzuri sana unaweza kumuitwa kwa jina la Black Beuty , kinachompoza ni ile hali yake ya kuwa siriasi na hata alivyosimama mbele ya Roma mara baada ya kufungua mlango alikuwa na sura yake yenye usiriasi vilevile na Roma alijiambia ilikuwa ni haki kabisa kwa mrembo huyu kuwa msaidizi wa Edna , kwani walikuwa wakiendana kwa asilimia mia moja tofauti yao tu ni kwamba Suzzane alikuwa na macho flani hivi akikuangalia ni kama anakudharau.

“Karibu”Alimkaribisha na Roma alitingisha kichwa na kisha kupita.

Roma licha ya kwamba alimpigia Suzzane , ila hakuweka swala lake wazi , alimwambia tu kuna mambo muhimu ambayo alikuwa akitaka kiuongea nae.







SEHEMU YA 341.

Edna sasa alielewa kwanini Blandina alisema kwamba picha hio alikuwa amepiga yeye, kumbe alishawahi kukutana na Raisi Jeremy huko Australia akiwa na mama yake wakila bata.

Roma mwenyewe alishangaa kumbe mama yake ni msomi mkubwa tu, lakini hata hivyo ilikuwa ni halali kabisa, kwani mambo ambayo Blandina aliweza kuyafanya kwa jamii kupitia sura ya Maina yalikuwa makubwa sana, kwani kama utaweza kupiga hesabu ya thamani ya vituo vyote ambavyo alivianzisha kwa nguvu zake ni Zaidi ya Dollar milioni mia moja.

Upande wa Roma yeye hakushangaa sana kwani alikua akijua mzazi wa Edna , ila mbele ya Edana alijifanyisha na yeye kushangaa , kwani alijua kama atasema alikuwa akifahamu na akakaa kimya , Edna angekasirika.

Maelezo ya Bi Wema hayakuwa na utofauti sana, kwani alishaelezwa na Raheli mwenyewe juu ya baba mzazi wa Edna, lakini sasa jumla yao wote wakajiuliza swali moja ni nani ambaye ameleta taarifa hio, na ni kwa madhumuni yapi, upande wa Roma aliamini sio Raisi Jeremy alieleta hio karatasi aliamini kuna mtu mwingine ambaye ameleta barua hio ila hakujua sababu ni nini na aliajiambia ni swala la muda tu atafahamu.

Edna sasa anajikuta akianza kuhisi huenda hata mtu aliekuwa akijiita The Protector alikuwa ni Raisi Jeremy , kwani mambo mengi ambayo aliokuwa akimsiadia yalikuwa yakihataji intelijensia ya hali ya juu.

Licha ya kwamba alihuzunishwa na jambo hilo , aliona mama yake hakuwa mtu wa kulaumiwa , kwani kulikuwa na mkataba wa yeye kutambulika kama mtoto wa Adebayo, lakini pia aliweza kufurahi na kuchukia kwa wakati mmoja kwa kumfahamu baba yake , kilichomfanya kufurahi ni kwamaba alikuwa ashatoka kwenye sintofahamu aliokuwa nayo kwa muda mrefu lakini kilichomfanya kuchukia ni kitendo cha kuwa mtoto wa nje ya ndoa lakini pia Raisi Jeremy kutoonyesha dalili yoyote ya kumtambua mbele yake.

“Bi Wema Raisi Jeremy anafahamu kama mimi ni mtoto wake wa Damu?”Aliuliza Edna.

“Juu ya hilo sifahamu , kwani mama yako alipofahamika ni mjamzito tayari alikuwa anafahamika kama mke wa Adebayo”Aliongea Bi Wema na Edna alitingisha kichwa na kisha kwa huzuni alirudi chumbani kwake.

Roma alijikuta akimuonea huruma mke wake , kwani aliweza kukumbuka maneno ya Raisi Jeremy juu ya kutokuwa na mpango wa kutomfanya Edna kuwa mtoto wake licha ya kwamba anamtambua, Alimuona mke wake hakuwa na utofauti na Yatima licha ya kwamba alikuwa na pesa nyingi, hisia ambazo zilimrudisha miaka kadhaa nyuma akiwa peke yake na Lorraine kwenye kisiwa , wakiwa hawana Baba wala Mama.

*******

Zilipita siku kumi , upande wa kwenye kampuni mashindano yalikuwa yakiendelea kama kawaida na Sophia alikuwa akifanya vyema sana kiasi cha kumpelekea kujipatia mashabiki wengi sana , kwani kwenye mitandao ya kijamii alikuwa akizungumziwa sana , huku Clip zake akiwa anaimba zikisambaa sana, watu wengi wakimtazamia kuwa mshindi wa mashindano hayo.

Mashindano yalikuwa na mvuto mkubwa sana kwani yalikuwa ya kipekee na mpangilio wake kupendwa na wengi lakini pia ndio mashindano ambayo yalikuwa yakifuatiliwa kwenye nchi nyingi sana na hio ni kutokana na kuhusika kwa Christen kwenye mashindano hayo kama jaji ambaye anatazamiwa kushiriki siku ya mwisho ya fainali, lakini pia Christen kitendo chake cha kuyapigia mashindano hayo ‘Promo’ wakati akiwa kwenye mahojiano na Vexto Tv , iliyapaisha sana duniani mashindano ya Kizazi nyota na kufanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa.

Zilikuwa zimebakia hatimae wiki tatu mpaka mashindano hayo kuhitimishwa , kwani kila wiki mashindano yalikuwa yakifanyika mara mbili na washiriki watano walikuwa wakitoka kwenye kila siku michuano.

Ikiwa ni siku ya jumamosi , kabla ya mashindano kuanza mshereheshaji Amina kanani aliweza kutoa tangazo juu ya ujio wa msanii mkubwa atakaetumbuiza siku ya fainali , msanii wa kike mrembo kutoka Korea Kusini afahamikae kwa jina la Yoon- He

Yoona- He ni moja ya wasanii maarufu ambaye anauza sana kazi zake za kisanaa ndani ya Korea na nje ya Korea , alikuwa na mashabiki wengi sana na kitu ambacho kilimfanya pia kutambulika kimataifa ni pamoja na uwezo wake katika mambo ya uigizaji , akiwa ameshiriki kwenye muvi na Tv Shows mbalimbali mbali ambazo zilifanya vizuri sokoni kimnataifa.

Licha ya kuwa msanii lakini pia inasemekeana mafanikio ya Yoon-He yalichangiwa na ukwasi wa pesa wa familia yake, kwani babu yake Yoon-He ni moja ya wafanyabiashara wakubwa walijikita katika udhalishajii wa vifaa vya kidigitali vya mambo ya nyumbani , akitajwa kama Tajiri namba kumi ndani ya Korea.

Hivyo baada ya Tangazo hilo liliibua munkari sana kwa mashabiki na wafatiliaji wengi pamoja na wale ambao walikuwa shabiki wa Yoon -He,menejimenti ya Yoon He ndio iliofanya mawasiliano na kampuni ya Vexto na kuomba ushiriki katika kuimba siku ya fainali jambo ambalo lilikubaliwa na Daudi pamoja na Amina mara moja , huku upande wa Roma kwakua hakuwa sana mpenzi wa nyimbo wala shabiki wa mtu yoyote alikubali tu ilimradi Yoon He angeongeza mapato.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana tokea mwanzo wa shindano hilo ndani ya siku chache tu , kwani faida ilikuwa ikionekana lakini pia wafatiliaji walikuwa wengi hivyo kufanya matanganzo ya kampuni ya Vexto International kufikia watu wengi sana na kufanya hata hisa za kampuni kupanda ndani ya muda mfupi , jambo ambalo lilimfurahisha sana Edna na kuona kwamba yalikuwa mawazo sahihi ya kufungua kampuni ya Habari na burudani, lakini pia lilikuwa wazo sahihi kumwachia Roma kuongoza kampuni hio.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa kwenye mawazo ya hapa na pela huku akiangalia Skrini ya tarakishi yake iliokuwa ikionyesha namna ambavyo mauzo ya hisa yamepanda kwa siku hio mara baada ya kutangazwa kwa ujio wa msanii Yoon-He.

Wakati akiendelea kuwaza alijikuta akikumbuka maneno ya mama mkwe wake siku mbili zilizopita juu ya Roma kuhamia kwenye chumba chake huku Lanlan ahamie kwenye chumba cha Qiang Xi , Edna alionekana kutafakari kidogo , huku akikumbuka siku hizo kumi zote Maisha na Roma yalikuwa mazuri sana kiasi kwamba hawakugombana na kubwa Zaidi tokea amtamkie Roma anampenda ni kama vyumba vya hisia visivyoonekana kwa darubini za kiganga kwenye moyo wake vilifunguka wazi kiasi kwamba hisia za kimapenzi zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba hata akimuona tu alikuwa akinyegeka.

Zimebaki siku tano tu kufikia tarehe ishirini na Tisa, Babu yake Lanlan asipotokea ndio siku nitakayo mlea Lanlan kama mtoto wangu na Roma kama baba yake na ndio siku ambayo Lanlan ataenda kulala na Qiang Xi na mimi kulala na Roma kama mume wangu”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake na kujikuta akitabasamu na alikuja kushituliwa na Monica ambaye aliingia hapo akiwa na faili tatu ambazo Edna anapaswa kuzisaini kabla hazijapelekwa kwenye kampuni Tanzu ili hatua Zaidi kuchukuliwa.

*******

Upande wa Raisi Senga alifanikiwa Kwenda Nigeria na kurudi salama salimini , lakini licha ya hivyo alionekana kutokuwa sawa kama alivyondoka , alionekana kuwa kwenye mawazo kiasi ambacho kilimfanya hata mke wake Damasi kujua mabadiliko ya mume wake.

“Senga ulivyoondoka sio kama ulivyorudi , unaonekana kuwa na mawazo mume wangu k ni jambo gani linaendelea?”

“Mama Ashley niko sawa ni maswala ya kikazi tu ndio yananifikirisha”Aliongea Senga kwa kujitutumua na muda huo alikuwa ndio anarudi kutoka ofisini.

Ukweli ni kwamba kilichomfanya Damasi kuwa na wasiwasi na mume wake ni kutokana na kwamba ,tokea arudi kutoka Nigeria alikoenda kikazi , hakumgusa kabisa na ndio maana Damasi alikuwa akipatwa na wasiwasi kwani haikuwa tabia ya Senga , lakini jambo lingine ni kwamba hakuwa sawa kimawazo , yaani Raisi Senga kuna muda alikuwa akiangalia sehemu basi macho yake yataganda sehemu hio mpaka ashituliwe na hiko ndio kikamfanya Damasi kuwa na mawazo.

“Senga nadhani unaelewa kauli yangu ya siku zote, licha ya kwamba wewe ni raisi wa Watanzania nikiwa mimi mmoja wapo ,lakini pia utambue mimi ni mkeo na unatakiwa kuwajibika kwangu na kwa familia”Aliongea Damasi kwa msisitizo na kisha akatoka kwenye chumba chao cha kulalaia na Kwenda upande wa Sebuleni kuendelea kuangalia Runinga.

Ikiwa ni siku nyingine baada ya Raisi Senga kuingia ofisini , asubuhi hio alionekana kuwa na ugeni ambao alionekana alikuwa akiusubuiria, ni kweli baada ya madakika kadhaa alionekana mwanaume mmoja wa kihindi mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi akiingia ndani ya ofisi ya kukutania wageni akiwa ameongozana na Katibu Muhtasi.

“Mheshimiwa Mjumbe kutoka baraza la haki za binadamu kashafika”Aliongea Katibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kumruhusu , muda ule ule mjumbe yule wa kihindi aliingia ndani ya eneo hilo na walisalimiana kwa bashasha na baada ya Raisi Senga kumkaribisha mgeni wake , palepale alitoa maagizo juu ya kikao hicho kuwa cha siri kwa muda wa dakika kadhaa na baada ya hapo baadhi ya viongozi wa Ikulu wataruhusiwa kuingia kushiriki kwenye mazungumzo pamoja na kupiga picha na kuweka mitandaoni na kwenye gazeti la kiserikali.

“Mheshimiwa nadhani hakuja haja ya maongezi Zaidi kwani kila kitu kishaongelewa, kama nilivyojitambulisha mimi ni mwanachama wa baraza la haki binadamu kutoka UN nikihudumu upande wa Afrika (Umoja wa mataifa) na nipo hapa kwa ajili ya kupata sahihi yako juu upatikanaji wa haki za LGBTQ(Mapenzi ya jinsia moja) hapa Tanzania”Aliongea yule mwanaume ambaye alijitambulisha kwa Mheshimiwa Senga kwa jina la Vishnu Gupta.

Mheshimiwa alifikitia kidogo , mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akitaka yeye asaini mkataba wa kulinda haki za mashoga hapa Tanzania , ijapokuwa makubaliano yake nchini Nigeria hayakuwa ni kwa ajili ya kutangaza hadharani kama anakubali mashoga lakini alitakuwa kutia sahihi kama mkuu wa nchi ili kuhakikisha kwamba serikali haingilii haki za mashoga nchini.

“Hakuna shida bwana Vishnu nitasaini mkataba kwani ni sehemu ya makubaliano yangu”Aliongea Raisi Senga na Vishnu alitoa karatasi na kumpatia raisi Senga na baada ya kuzisoma kwa muda mfupi hatimae aliweza kuzitia Saini , jambo ambalo lilimfanya Vishnu kutabasamu na alipeana mkono kama ishara ya makubaliano na baada ya hapo ndipo Kamera ziliruhusiwa na mazungumzo yakawa wazi , huku raisi Senga akitoa ahadi kwamba ataendelea kukomesha vitendo vyote ambavyo vnakiuka haki za kibinadamu.

Baada ya kikao kuisha mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu , licha ya kwamba alishasaini karatasi hizo ambazo zilikuwa ni ‘implicity’ kwenye utekelezaji wake , lakini bado alijiona kama mtu aliekosea watanzania , lakini pia aliejikosea yeye mwenyewe , lakini wakati huo huo Mheshimiwa Senga kuna tukio ambalo lilikuwa likijirudia rudia kwenye akili yake kiasi kwamba lilimfanya kabisa kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mke wake mpaka kupelekea malalamiko.

Mheshimiwa Senga alijikuta akijiegamiza kwenye kiti chake huku akikusanya mikono yake pamoja , alionekana kuwaza sana , haikueleweka mara moja ni nini kilichotokea kwenye Ibada ya Mpasuko Wa Mwezi kutokana na usiri mkubwa uliokuwepo , lakini jambo moja ambalo ni dhahiri ni kwmaba mheshimiwa Senga alikuwa akifanya maamuzi ambayo yapo nje ya kile anachokisimamia kama Raisi licha ya kwamba alishasaini ‘Impilicity Law’ inayohusiana na Mashoga aliamini siku sio nyingi atalazimishwa kusaini ‘Explicity Law’ inayohusiana na mashoga.

(Implicity Law ni hitimisho la kisheria ambalo linampa mtu haki ya kitu pasipo kuingiliwa licha ya kwamba sheria hio haiwekwi wazi, kwa mfano kauli ya kiongozi mmoja wa dini akisema kwamba Mapenzi ya jinsia moja sio Kosa , sio uhalifu lakini ni Dhambi hio ndio sheria isio ya moja kwa moja lakini yenye kutekelezwa , yaani huwezi kusikia kiongozi akisema hadharani kama anakukataa ushoga ilihali sheria hio ishasainiwa.

Explicity Law ni aina ya sheria ambazo ni za moja kwa moja na zinapaswa kutekelezwa kwa namna yoyote ile na mara nyingi sheria hizi kwa hapa Tanzania hupitishwa na Bunge pamoja na mahakama halafu ndio raisi atasaini ili ianze utekelezwaji wake.

Wanasheria mtatusaidia Zaidi hapo.

**********

Naam ilikuwa ni siku ya jumamosi Roma alionekana Kibaha kwa Mathiasi akikunja kushoto akiwa anendesha gari yake kuelekea upande wa mji wa kisasa , mji ambao unamilikiwa na kampuni ya Vexto Group.

Roma aliendesha gari yake kwa utaratibu huku akifurahia mazingira safi yaliokuwa yapo kandokando ya barabara hii kuelekea kwenye mji huu, kusema ukweli licha ya kwamba ilikuwa mara yake ya pili kufika kwenye huo mji lakini muonekano wake siku hio ulikuwa kama ni mpya kwake na alijiambia ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanyika mpaka kujenga makazi hayo ya kisasa kabisa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dakika kama tano aliweza kuingiza gari yake kwenye geti kubwa linarohusu magari kuingia kwenye ‘Apartment’ hizo na alikwenda moja kwa moja kuegesha kwenye Parking ya muda mfupi na akashuka na kuanza kutembea uelekeo wa jengo la Athena.

Alikuwa mahali hapo asubuhi hio kutokana na kwamba alikuwa na miadi na mrembo Suzzane , ambaye baada ya kuwasiliana nae alimwambia kwamba amfuate nyumbani kwake na Roma kwakuwa ndio alikuwa na shida ilimbidi kufanya hivyo ili kuonana na mrembo huyo.

Baada ya kufika chini kabisa ya hilo jengo alipiga simu Kwenda kwa Suzzane na alipewa maelekezo ya Kwenda mpaka Floor namba kumi na kusimama kwenye mlango wenye namba 200 ndio Apartment yake.

Tokea mrembo huyu aje kumchukua kwa mara ya kwanza kule Mbagala hakuweza tena kuongea nae moja kwa moja , kwanza Roma alimchukulai Suzzane kama mwanamke Siriasi asiependa utani , lakini pia Suzzane mara nyingi alikuwa ndani ya idara hii kwahio ilikuwa ngumu kwake sana kuonana nae mara kwa mara na kumzoea.

Dakika chache tu Roma alikuwa nje ya mlango namba 200 na alibonyeza kitufe cha kengele na kisha akasubiri mlango kufunguliwa na zilipita dakika kama mbili hivi hatimae mlango ulifunguliwa na mrembo Suzzane ambaye alikuwa amevalia gauni fupi la kumpendeza.

Suzznae alikuwa mzuri sana unaweza kumuitwa kwa jina la Black Beuty , kinachompoza ni ile hali yake ya kuwa siriasi na hata alivyosimama mbele ya Roma mara baada ya kufungua mlango alikuwa na sura yake yenye usiriasi vilevile na Roma alijiambia ilikuwa ni haki kabisa kwa mrembo huyu kuwa msaidizi wa Edna , kwani walikuwa wakiendana kwa asilimia mia moja tofauti yao tu ni kwamba Suzzane alikuwa na macho flani hivi akikuangalia ni kama anakudharau.

“Karibu”Alimkaribisha na Roma alitingisha kichwa na kisha kupita.

Roma licha ya kwamba alimpigia Suzzane , ila hakuweka swala lake wazi , alimwambia tu kuna mambo muhimu ambayo alikuwa akitaka kiuongea nae.

ITAENDELEA

WATSAPP 0687151346
 
SEHEMU YA 341.

Edna sasa alielewa kwanini Blandina alisema kwamba picha hio alikuwa amepiga yeye, kumbe alishawahi kukutana na Raisi Jeremy huko Australia akiwa na mama yake wakila bata.

Roma mwenyewe alishangaa kumbe mama yake ni msomi mkubwa tu, lakini hata hivyo ilikuwa ni halali kabisa, kwani mambo ambayo Blandina aliweza kuyafanya kwa jamii kupitia sura ya Maina yalikuwa makubwa sana, kwani kama utaweza kupiga hesabu ya thamani ya vituo vyote ambavyo alivianzisha kwa nguvu zake ni Zaidi ya Dollar milioni mia moja.

Upande wa Roma yeye hakushangaa sana kwani alikua akijua mzazi wa Edna , ila mbele ya Edana alijifanyisha na yeye kushangaa , kwani alijua kama atasema alikuwa akifahamu na akakaa kimya , Edna angekasirika.

Maelezo ya Bi Wema hayakuwa na utofauti sana, kwani alishaelezwa na Raheli mwenyewe juu ya baba mzazi wa Edna, lakini sasa jumla yao wote wakajiuliza swali moja ni nani ambaye ameleta taarifa hio, na ni kwa madhumuni yapi, upande wa Roma aliamini sio Raisi Jeremy alieleta hio karatasi aliamini kuna mtu mwingine ambaye ameleta barua hio ila hakujua sababu ni nini na aliajiambia ni swala la muda tu atafahamu.

Edna sasa anajikuta akianza kuhisi huenda hata mtu aliekuwa akijiita The Protector alikuwa ni Raisi Jeremy , kwani mambo mengi ambayo aliokuwa akimsiadia yalikuwa yakihataji intelijensia ya hali ya juu.

Licha ya kwamba alihuzunishwa na jambo hilo , aliona mama yake hakuwa mtu wa kulaumiwa , kwani kulikuwa na mkataba wa yeye kutambulika kama mtoto wa Adebayo, lakini pia aliweza kufurahi na kuchukia kwa wakati mmoja kwa kumfahamu baba yake , kilichomfanya kufurahi ni kwamaba alikuwa ashatoka kwenye sintofahamu aliokuwa nayo kwa muda mrefu lakini kilichomfanya kuchukia ni kitendo cha kuwa mtoto wa nje ya ndoa lakini pia Raisi Jeremy kutoonyesha dalili yoyote ya kumtambua mbele yake.

“Bi Wema Raisi Jeremy anafahamu kama mimi ni mtoto wake wa Damu?”Aliuliza Edna.

“Juu ya hilo sifahamu , kwani mama yako alipofahamika ni mjamzito tayari alikuwa anafahamika kama mke wa Adebayo”Aliongea Bi Wema na Edna alitingisha kichwa na kisha kwa huzuni alirudi chumbani kwake.

Roma alijikuta akimuonea huruma mke wake , kwani aliweza kukumbuka maneno ya Raisi Jeremy juu ya kutokuwa na mpango wa kutomfanya Edna kuwa mtoto wake licha ya kwamba anamtambua, Alimuona mke wake hakuwa na utofauti na Yatima licha ya kwamba alikuwa na pesa nyingi, hisia ambazo zilimrudisha miaka kadhaa nyuma akiwa peke yake na Lorraine kwenye kisiwa , wakiwa hawana Baba wala Mama.

*******

Zilipita siku kumi , upande wa kwenye kampuni mashindano yalikuwa yakiendelea kama kawaida na Sophia alikuwa akifanya vyema sana kiasi cha kumpelekea kujipatia mashabiki wengi sana , kwani kwenye mitandao ya kijamii alikuwa akizungumziwa sana , huku Clip zake akiwa anaimba zikisambaa sana, watu wengi wakimtazamia kuwa mshindi wa mashindano hayo.

Mashindano yalikuwa na mvuto mkubwa sana kwani yalikuwa ya kipekee na mpangilio wake kupendwa na wengi lakini pia ndio mashindano ambayo yalikuwa yakifuatiliwa kwenye nchi nyingi sana na hio ni kutokana na kuhusika kwa Christen kwenye mashindano hayo kama jaji ambaye anatazamiwa kushiriki siku ya mwisho ya fainali, lakini pia Christen kitendo chake cha kuyapigia mashindano hayo ‘Promo’ wakati akiwa kwenye mahojiano na Vexto Tv , iliyapaisha sana duniani mashindano ya Kizazi nyota na kufanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa.

Zilikuwa zimebakia hatimae wiki tatu mpaka mashindano hayo kuhitimishwa , kwani kila wiki mashindano yalikuwa yakifanyika mara mbili na washiriki watano walikuwa wakitoka kwenye kila siku michuano.

Ikiwa ni siku ya jumamosi , kabla ya mashindano kuanza mshereheshaji Amina kanani aliweza kutoa tangazo juu ya ujio wa msanii mkubwa atakaetumbuiza siku ya fainali , msanii wa kike mrembo kutoka Korea Kusini afahamikae kwa jina la Yoon- He

Yoona- He ni moja ya wasanii maarufu ambaye anauza sana kazi zake za kisanaa ndani ya Korea na nje ya Korea , alikuwa na mashabiki wengi sana na kitu ambacho kilimfanya pia kutambulika kimataifa ni pamoja na uwezo wake katika mambo ya uigizaji , akiwa ameshiriki kwenye muvi na Tv Shows mbalimbali mbali ambazo zilifanya vizuri sokoni kimnataifa.

Licha ya kuwa msanii lakini pia inasemekeana mafanikio ya Yoon-He yalichangiwa na ukwasi wa pesa wa familia yake, kwani babu yake Yoon-He ni moja ya wafanyabiashara wakubwa walijikita katika udhalishajii wa vifaa vya kidigitali vya mambo ya nyumbani , akitajwa kama Tajiri namba kumi ndani ya Korea.

Hivyo baada ya Tangazo hilo liliibua munkari sana kwa mashabiki na wafatiliaji wengi pamoja na wale ambao walikuwa shabiki wa Yoon -He,menejimenti ya Yoon He ndio iliofanya mawasiliano na kampuni ya Vexto na kuomba ushiriki katika kuimba siku ya fainali jambo ambalo lilikubaliwa na Daudi pamoja na Amina mara moja , huku upande wa Roma kwakua hakuwa sana mpenzi wa nyimbo wala shabiki wa mtu yoyote alikubali tu ilimradi Yoon He angeongeza mapato.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana tokea mwanzo wa shindano hilo ndani ya siku chache tu , kwani faida ilikuwa ikionekana lakini pia wafatiliaji walikuwa wengi hivyo kufanya matanganzo ya kampuni ya Vexto International kufikia watu wengi sana na kufanya hata hisa za kampuni kupanda ndani ya muda mfupi , jambo ambalo lilimfurahisha sana Edna na kuona kwamba yalikuwa mawazo sahihi ya kufungua kampuni ya Habari na burudani, lakini pia lilikuwa wazo sahihi kumwachia Roma kuongoza kampuni hio.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa kwenye mawazo ya hapa na pela huku akiangalia Skrini ya tarakishi yake iliokuwa ikionyesha namna ambavyo mauzo ya hisa yamepanda kwa siku hio mara baada ya kutangazwa kwa ujio wa msanii Yoon-He.

Wakati akiendelea kuwaza alijikuta akikumbuka maneno ya mama mkwe wake siku mbili zilizopita juu ya Roma kuhamia kwenye chumba chake huku Lanlan ahamie kwenye chumba cha Qiang Xi , Edna alionekana kutafakari kidogo , huku akikumbuka siku hizo kumi zote Maisha na Roma yalikuwa mazuri sana kiasi kwamba hawakugombana na kubwa Zaidi tokea amtamkie Roma anampenda ni kama vyumba vya hisia visivyoonekana kwa darubini za kiganga kwenye moyo wake vilifunguka wazi kiasi kwamba hisia za kimapenzi zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba hata akimuona tu alikuwa akinyegeka.

Zimebaki siku tano tu kufikia tarehe ishirini na Tisa, Babu yake Lanlan asipotokea ndio siku nitakayo mlea Lanlan kama mtoto wangu na Roma kama baba yake na ndio siku ambayo Lanlan ataenda kulala na Qiang Xi na mimi kulala na Roma kama mume wangu”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake na kujikuta akitabasamu na alikuja kushituliwa na Monica ambaye aliingia hapo akiwa na faili tatu ambazo Edna anapaswa kuzisaini kabla hazijapelekwa kwenye kampuni Tanzu ili hatua Zaidi kuchukuliwa.

*******

Upande wa Raisi Senga alifanikiwa Kwenda Nigeria na kurudi salama salimini , lakini licha ya hivyo alionekana kutokuwa sawa kama alivyondoka , alionekana kuwa kwenye mawazo kiasi ambacho kilimfanya hata mke wake Damasi kujua mabadiliko ya mume wake.

“Senga ulivyoondoka sio kama ulivyorudi , unaonekana kuwa na mawazo mume wangu k ni jambo gani linaendelea?”

“Mama Ashley niko sawa ni maswala ya kikazi tu ndio yananifikirisha”Aliongea Senga kwa kujitutumua na muda huo alikuwa ndio anarudi kutoka ofisini.

Ukweli ni kwamba kilichomfanya Damasi kuwa na wasiwasi na mume wake ni kutokana na kwamba ,tokea arudi kutoka Nigeria alikoenda kikazi , hakumgusa kabisa na ndio maana Damasi alikuwa akipatwa na wasiwasi kwani haikuwa tabia ya Senga , lakini jambo lingine ni kwamba hakuwa sawa kimawazo , yaani Raisi Senga kuna muda alikuwa akiangalia sehemu basi macho yake yataganda sehemu hio mpaka ashituliwe na hiko ndio kikamfanya Damasi kuwa na mawazo.

“Senga nadhani unaelewa kauli yangu ya siku zote, licha ya kwamba wewe ni raisi wa Watanzania nikiwa mimi mmoja wapo ,lakini pia utambue mimi ni mkeo na unatakiwa kuwajibika kwangu na kwa familia”Aliongea Damasi kwa msisitizo na kisha akatoka kwenye chumba chao cha kulalaia na Kwenda upande wa Sebuleni kuendelea kuangalia Runinga.

Ikiwa ni siku nyingine baada ya Raisi Senga kuingia ofisini , asubuhi hio alionekana kuwa na ugeni ambao alionekana alikuwa akiusubuiria, ni kweli baada ya madakika kadhaa alionekana mwanaume mmoja wa kihindi mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi akiingia ndani ya ofisi ya kukutania wageni akiwa ameongozana na Katibu Muhtasi.

“Mheshimiwa Mjumbe kutoka baraza la haki za binadamu kashafika”Aliongea Katibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kumruhusu , muda ule ule mjumbe yule wa kihindi aliingia ndani ya eneo hilo na walisalimiana kwa bashasha na baada ya Raisi Senga kumkaribisha mgeni wake , palepale alitoa maagizo juu ya kikao hicho kuwa cha siri kwa muda wa dakika kadhaa na baada ya hapo baadhi ya viongozi wa Ikulu wataruhusiwa kuingia kushiriki kwenye mazungumzo pamoja na kupiga picha na kuweka mitandaoni na kwenye gazeti la kiserikali.

“Mheshimiwa nadhani hakuja haja ya maongezi Zaidi kwani kila kitu kishaongelewa, kama nilivyojitambulisha mimi ni mwanachama wa baraza la haki binadamu kutoka UN nikihudumu upande wa Afrika (Umoja wa mataifa) na nipo hapa kwa ajili ya kupata sahihi yako juu upatikanaji wa haki za LGBTQ(Mapenzi ya jinsia moja) hapa Tanzania”Aliongea yule mwanaume ambaye alijitambulisha kwa Mheshimiwa Senga kwa jina la Vishnu Gupta.

Mheshimiwa alifikitia kidogo , mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akitaka yeye asaini mkataba wa kulinda haki za mashoga hapa Tanzania , ijapokuwa makubaliano yake nchini Nigeria hayakuwa ni kwa ajili ya kutangaza hadharani kama anakubali mashoga lakini alitakuwa kutia sahihi kama mkuu wa nchi ili kuhakikisha kwamba serikali haingilii haki za mashoga nchini.

“Hakuna shida bwana Vishnu nitasaini mkataba kwani ni sehemu ya makubaliano yangu”Aliongea Raisi Senga na Vishnu alitoa karatasi na kumpatia raisi Senga na baada ya kuzisoma kwa muda mfupi hatimae aliweza kuzitia Saini , jambo ambalo lilimfanya Vishnu kutabasamu na alipeana mkono kama ishara ya makubaliano na baada ya hapo ndipo Kamera ziliruhusiwa na mazungumzo yakawa wazi , huku raisi Senga akitoa ahadi kwamba ataendelea kukomesha vitendo vyote ambavyo vnakiuka haki za kibinadamu.

Baada ya kikao kuisha mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu , licha ya kwamba alishasaini karatasi hizo ambazo zilikuwa ni ‘implicity’ kwenye utekelezaji wake , lakini bado alijiona kama mtu aliekosea watanzania , lakini pia aliejikosea yeye mwenyewe , lakini wakati huo huo Mheshimiwa Senga kuna tukio ambalo lilikuwa likijirudia rudia kwenye akili yake kiasi kwamba lilimfanya kabisa kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mke wake mpaka kupelekea malalamiko.

Mheshimiwa Senga alijikuta akijiegamiza kwenye kiti chake huku akikusanya mikono yake pamoja , alionekana kuwaza sana , haikueleweka mara moja ni nini kilichotokea kwenye Ibada ya Mpasuko Wa Mwezi kutokana na usiri mkubwa uliokuwepo , lakini jambo moja ambalo ni dhahiri ni kwmaba mheshimiwa Senga alikuwa akifanya maamuzi ambayo yapo nje ya kile anachokisimamia kama Raisi licha ya kwamba alishasaini ‘Impilicity Law’ inayohusiana na Mashoga aliamini siku sio nyingi atalazimishwa kusaini ‘Explicity Law’ inayohusiana na mashoga.

(Implicity Law ni hitimisho la kisheria ambalo linampa mtu haki ya kitu pasipo kuingiliwa licha ya kwamba sheria hio haiwekwi wazi, kwa mfano kauli ya kiongozi mmoja wa dini akisema kwamba Mapenzi ya jinsia moja sio Kosa , sio uhalifu lakini ni Dhambi hio ndio sheria isio ya moja kwa moja lakini yenye kutekelezwa , yaani huwezi kusikia kiongozi akisema hadharani kama anakukataa ushoga ilihali sheria hio ishasainiwa.

Explicity Law ni aina ya sheria ambazo ni za moja kwa moja na zinapaswa kutekelezwa kwa namna yoyote ile na mara nyingi sheria hizi kwa hapa Tanzania hupitishwa na Bunge pamoja na mahakama halafu ndio raisi atasaini ili ianze utekelezwaji wake.

Wanasheria mtatusaidia Zaidi hapo.

**********

Naam ilikuwa ni siku ya jumamosi Roma alionekana Kibaha kwa Mathiasi akikunja kushoto akiwa anendesha gari yake kuelekea upande wa mji wa kisasa , mji ambao unamilikiwa na kampuni ya Vexto Group.

Roma aliendesha gari yake kwa utaratibu huku akifurahia mazingira safi yaliokuwa yapo kandokando ya barabara hii kuelekea kwenye mji huu, kusema ukweli licha ya kwamba ilikuwa mara yake ya pili kufika kwenye huo mji lakini muonekano wake siku hio ulikuwa kama ni mpya kwake na alijiambia ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanyika mpaka kujenga makazi hayo ya kisasa kabisa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dakika kama tano aliweza kuingiza gari yake kwenye geti kubwa linarohusu magari kuingia kwenye ‘Apartment’ hizo na alikwenda moja kwa moja kuegesha kwenye Parking ya muda mfupi na akashuka na kuanza kutembea uelekeo wa jengo la Athena.

Alikuwa mahali hapo asubuhi hio kutokana na kwamba alikuwa na miadi na mrembo Suzzane , ambaye baada ya kuwasiliana nae alimwambia kwamba amfuate nyumbani kwake na Roma kwakuwa ndio alikuwa na shida ilimbidi kufanya hivyo ili kuonana na mrembo huyo.

Baada ya kufika chini kabisa ya hilo jengo alipiga simu Kwenda kwa Suzzane na alipewa maelekezo ya Kwenda mpaka Floor namba kumi na kusimama kwenye mlango wenye namba 200 ndio Apartment yake.

Tokea mrembo huyu aje kumchukua kwa mara ya kwanza kule Mbagala hakuweza tena kuongea nae moja kwa moja , kwanza Roma alimchukulai Suzzane kama mwanamke Siriasi asiependa utani , lakini pia Suzzane mara nyingi alikuwa ndani ya idara hii kwahio ilikuwa ngumu kwake sana kuonana nae mara kwa mara na kumzoea.

Dakika chache tu Roma alikuwa nje ya mlango namba 200 na alibonyeza kitufe cha kengele na kisha akasubiri mlango kufunguliwa na zilipita dakika kama mbili hivi hatimae mlango ulifunguliwa na mrembo Suzzane ambaye alikuwa amevalia gauni fupi la kumpendeza.

Suzznae alikuwa mzuri sana unaweza kumuitwa kwa jina la Black Beuty , kinachompoza ni ile hali yake ya kuwa siriasi na hata alivyosimama mbele ya Roma mara baada ya kufungua mlango alikuwa na sura yake yenye usiriasi vilevile na Roma alijiambia ilikuwa ni haki kabisa kwa mrembo huyu kuwa msaidizi wa Edna , kwani walikuwa wakiendana kwa asilimia mia moja tofauti yao tu ni kwamba Suzzane alikuwa na macho flani hivi akikuangalia ni kama anakudharau.

“Karibu”Alimkaribisha na Roma alitingisha kichwa na kisha kupita.

Roma licha ya kwamba alimpigia Suzzane , ila hakuweka swala lake wazi , alimwambia tu kuna mambo muhimu ambayo alikuwa akitaka kiuongea nae.







SEHEMU YA 341.

Edna sasa alielewa kwanini Blandina alisema kwamba picha hio alikuwa amepiga yeye, kumbe alishawahi kukutana na Raisi Jeremy huko Australia akiwa na mama yake wakila bata.

Roma mwenyewe alishangaa kumbe mama yake ni msomi mkubwa tu, lakini hata hivyo ilikuwa ni halali kabisa, kwani mambo ambayo Blandina aliweza kuyafanya kwa jamii kupitia sura ya Maina yalikuwa makubwa sana, kwani kama utaweza kupiga hesabu ya thamani ya vituo vyote ambavyo alivianzisha kwa nguvu zake ni Zaidi ya Dollar milioni mia moja.

Upande wa Roma yeye hakushangaa sana kwani alikua akijua mzazi wa Edna , ila mbele ya Edana alijifanyisha na yeye kushangaa , kwani alijua kama atasema alikuwa akifahamu na akakaa kimya , Edna angekasirika.

Maelezo ya Bi Wema hayakuwa na utofauti sana, kwani alishaelezwa na Raheli mwenyewe juu ya baba mzazi wa Edna, lakini sasa jumla yao wote wakajiuliza swali moja ni nani ambaye ameleta taarifa hio, na ni kwa madhumuni yapi, upande wa Roma aliamini sio Raisi Jeremy alieleta hio karatasi aliamini kuna mtu mwingine ambaye ameleta barua hio ila hakujua sababu ni nini na aliajiambia ni swala la muda tu atafahamu.

Edna sasa anajikuta akianza kuhisi huenda hata mtu aliekuwa akijiita The Protector alikuwa ni Raisi Jeremy , kwani mambo mengi ambayo aliokuwa akimsiadia yalikuwa yakihataji intelijensia ya hali ya juu.

Licha ya kwamba alihuzunishwa na jambo hilo , aliona mama yake hakuwa mtu wa kulaumiwa , kwani kulikuwa na mkataba wa yeye kutambulika kama mtoto wa Adebayo, lakini pia aliweza kufurahi na kuchukia kwa wakati mmoja kwa kumfahamu baba yake , kilichomfanya kufurahi ni kwamaba alikuwa ashatoka kwenye sintofahamu aliokuwa nayo kwa muda mrefu lakini kilichomfanya kuchukia ni kitendo cha kuwa mtoto wa nje ya ndoa lakini pia Raisi Jeremy kutoonyesha dalili yoyote ya kumtambua mbele yake.

“Bi Wema Raisi Jeremy anafahamu kama mimi ni mtoto wake wa Damu?”Aliuliza Edna.

“Juu ya hilo sifahamu , kwani mama yako alipofahamika ni mjamzito tayari alikuwa anafahamika kama mke wa Adebayo”Aliongea Bi Wema na Edna alitingisha kichwa na kisha kwa huzuni alirudi chumbani kwake.

Roma alijikuta akimuonea huruma mke wake , kwani aliweza kukumbuka maneno ya Raisi Jeremy juu ya kutokuwa na mpango wa kutomfanya Edna kuwa mtoto wake licha ya kwamba anamtambua, Alimuona mke wake hakuwa na utofauti na Yatima licha ya kwamba alikuwa na pesa nyingi, hisia ambazo zilimrudisha miaka kadhaa nyuma akiwa peke yake na Lorraine kwenye kisiwa , wakiwa hawana Baba wala Mama.

*******

Zilipita siku kumi , upande wa kwenye kampuni mashindano yalikuwa yakiendelea kama kawaida na Sophia alikuwa akifanya vyema sana kiasi cha kumpelekea kujipatia mashabiki wengi sana , kwani kwenye mitandao ya kijamii alikuwa akizungumziwa sana , huku Clip zake akiwa anaimba zikisambaa sana, watu wengi wakimtazamia kuwa mshindi wa mashindano hayo.

Mashindano yalikuwa na mvuto mkubwa sana kwani yalikuwa ya kipekee na mpangilio wake kupendwa na wengi lakini pia ndio mashindano ambayo yalikuwa yakifuatiliwa kwenye nchi nyingi sana na hio ni kutokana na kuhusika kwa Christen kwenye mashindano hayo kama jaji ambaye anatazamiwa kushiriki siku ya mwisho ya fainali, lakini pia Christen kitendo chake cha kuyapigia mashindano hayo ‘Promo’ wakati akiwa kwenye mahojiano na Vexto Tv , iliyapaisha sana duniani mashindano ya Kizazi nyota na kufanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa.

Zilikuwa zimebakia hatimae wiki tatu mpaka mashindano hayo kuhitimishwa , kwani kila wiki mashindano yalikuwa yakifanyika mara mbili na washiriki watano walikuwa wakitoka kwenye kila siku michuano.

Ikiwa ni siku ya jumamosi , kabla ya mashindano kuanza mshereheshaji Amina kanani aliweza kutoa tangazo juu ya ujio wa msanii mkubwa atakaetumbuiza siku ya fainali , msanii wa kike mrembo kutoka Korea Kusini afahamikae kwa jina la Yoon- He

Yoona- He ni moja ya wasanii maarufu ambaye anauza sana kazi zake za kisanaa ndani ya Korea na nje ya Korea , alikuwa na mashabiki wengi sana na kitu ambacho kilimfanya pia kutambulika kimataifa ni pamoja na uwezo wake katika mambo ya uigizaji , akiwa ameshiriki kwenye muvi na Tv Shows mbalimbali mbali ambazo zilifanya vizuri sokoni kimnataifa.

Licha ya kuwa msanii lakini pia inasemekeana mafanikio ya Yoon-He yalichangiwa na ukwasi wa pesa wa familia yake, kwani babu yake Yoon-He ni moja ya wafanyabiashara wakubwa walijikita katika udhalishajii wa vifaa vya kidigitali vya mambo ya nyumbani , akitajwa kama Tajiri namba kumi ndani ya Korea.

Hivyo baada ya Tangazo hilo liliibua munkari sana kwa mashabiki na wafatiliaji wengi pamoja na wale ambao walikuwa shabiki wa Yoon -He,menejimenti ya Yoon He ndio iliofanya mawasiliano na kampuni ya Vexto na kuomba ushiriki katika kuimba siku ya fainali jambo ambalo lilikubaliwa na Daudi pamoja na Amina mara moja , huku upande wa Roma kwakua hakuwa sana mpenzi wa nyimbo wala shabiki wa mtu yoyote alikubali tu ilimradi Yoon He angeongeza mapato.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa sana ambayo yamepatikana tokea mwanzo wa shindano hilo ndani ya siku chache tu , kwani faida ilikuwa ikionekana lakini pia wafatiliaji walikuwa wengi hivyo kufanya matanganzo ya kampuni ya Vexto International kufikia watu wengi sana na kufanya hata hisa za kampuni kupanda ndani ya muda mfupi , jambo ambalo lilimfurahisha sana Edna na kuona kwamba yalikuwa mawazo sahihi ya kufungua kampuni ya Habari na burudani, lakini pia lilikuwa wazo sahihi kumwachia Roma kuongoza kampuni hio.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa kwenye mawazo ya hapa na pela huku akiangalia Skrini ya tarakishi yake iliokuwa ikionyesha namna ambavyo mauzo ya hisa yamepanda kwa siku hio mara baada ya kutangazwa kwa ujio wa msanii Yoon-He.

Wakati akiendelea kuwaza alijikuta akikumbuka maneno ya mama mkwe wake siku mbili zilizopita juu ya Roma kuhamia kwenye chumba chake huku Lanlan ahamie kwenye chumba cha Qiang Xi , Edna alionekana kutafakari kidogo , huku akikumbuka siku hizo kumi zote Maisha na Roma yalikuwa mazuri sana kiasi kwamba hawakugombana na kubwa Zaidi tokea amtamkie Roma anampenda ni kama vyumba vya hisia visivyoonekana kwa darubini za kiganga kwenye moyo wake vilifunguka wazi kiasi kwamba hisia za kimapenzi zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba hata akimuona tu alikuwa akinyegeka.

Zimebaki siku tano tu kufikia tarehe ishirini na Tisa, Babu yake Lanlan asipotokea ndio siku nitakayo mlea Lanlan kama mtoto wangu na Roma kama baba yake na ndio siku ambayo Lanlan ataenda kulala na Qiang Xi na mimi kulala na Roma kama mume wangu”Aliwaza Edna kwenye kichwa chake na kujikuta akitabasamu na alikuja kushituliwa na Monica ambaye aliingia hapo akiwa na faili tatu ambazo Edna anapaswa kuzisaini kabla hazijapelekwa kwenye kampuni Tanzu ili hatua Zaidi kuchukuliwa.

*******

Upande wa Raisi Senga alifanikiwa Kwenda Nigeria na kurudi salama salimini , lakini licha ya hivyo alionekana kutokuwa sawa kama alivyondoka , alionekana kuwa kwenye mawazo kiasi ambacho kilimfanya hata mke wake Damasi kujua mabadiliko ya mume wake.

“Senga ulivyoondoka sio kama ulivyorudi , unaonekana kuwa na mawazo mume wangu k ni jambo gani linaendelea?”

“Mama Ashley niko sawa ni maswala ya kikazi tu ndio yananifikirisha”Aliongea Senga kwa kujitutumua na muda huo alikuwa ndio anarudi kutoka ofisini.

Ukweli ni kwamba kilichomfanya Damasi kuwa na wasiwasi na mume wake ni kutokana na kwamba ,tokea arudi kutoka Nigeria alikoenda kikazi , hakumgusa kabisa na ndio maana Damasi alikuwa akipatwa na wasiwasi kwani haikuwa tabia ya Senga , lakini jambo lingine ni kwamba hakuwa sawa kimawazo , yaani Raisi Senga kuna muda alikuwa akiangalia sehemu basi macho yake yataganda sehemu hio mpaka ashituliwe na hiko ndio kikamfanya Damasi kuwa na mawazo.

“Senga nadhani unaelewa kauli yangu ya siku zote, licha ya kwamba wewe ni raisi wa Watanzania nikiwa mimi mmoja wapo ,lakini pia utambue mimi ni mkeo na unatakiwa kuwajibika kwangu na kwa familia”Aliongea Damasi kwa msisitizo na kisha akatoka kwenye chumba chao cha kulalaia na Kwenda upande wa Sebuleni kuendelea kuangalia Runinga.

Ikiwa ni siku nyingine baada ya Raisi Senga kuingia ofisini , asubuhi hio alionekana kuwa na ugeni ambao alionekana alikuwa akiusubuiria, ni kweli baada ya madakika kadhaa alionekana mwanaume mmoja wa kihindi mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi akiingia ndani ya ofisi ya kukutania wageni akiwa ameongozana na Katibu Muhtasi.

“Mheshimiwa Mjumbe kutoka baraza la haki za binadamu kashafika”Aliongea Katibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kumruhusu , muda ule ule mjumbe yule wa kihindi aliingia ndani ya eneo hilo na walisalimiana kwa bashasha na baada ya Raisi Senga kumkaribisha mgeni wake , palepale alitoa maagizo juu ya kikao hicho kuwa cha siri kwa muda wa dakika kadhaa na baada ya hapo baadhi ya viongozi wa Ikulu wataruhusiwa kuingia kushiriki kwenye mazungumzo pamoja na kupiga picha na kuweka mitandaoni na kwenye gazeti la kiserikali.

“Mheshimiwa nadhani hakuja haja ya maongezi Zaidi kwani kila kitu kishaongelewa, kama nilivyojitambulisha mimi ni mwanachama wa baraza la haki binadamu kutoka UN nikihudumu upande wa Afrika (Umoja wa mataifa) na nipo hapa kwa ajili ya kupata sahihi yako juu upatikanaji wa haki za LGBTQ(Mapenzi ya jinsia moja) hapa Tanzania”Aliongea yule mwanaume ambaye alijitambulisha kwa Mheshimiwa Senga kwa jina la Vishnu Gupta.

Mheshimiwa alifikitia kidogo , mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akitaka yeye asaini mkataba wa kulinda haki za mashoga hapa Tanzania , ijapokuwa makubaliano yake nchini Nigeria hayakuwa ni kwa ajili ya kutangaza hadharani kama anakubali mashoga lakini alitakuwa kutia sahihi kama mkuu wa nchi ili kuhakikisha kwamba serikali haingilii haki za mashoga nchini.

“Hakuna shida bwana Vishnu nitasaini mkataba kwani ni sehemu ya makubaliano yangu”Aliongea Raisi Senga na Vishnu alitoa karatasi na kumpatia raisi Senga na baada ya kuzisoma kwa muda mfupi hatimae aliweza kuzitia Saini , jambo ambalo lilimfanya Vishnu kutabasamu na alipeana mkono kama ishara ya makubaliano na baada ya hapo ndipo Kamera ziliruhusiwa na mazungumzo yakawa wazi , huku raisi Senga akitoa ahadi kwamba ataendelea kukomesha vitendo vyote ambavyo vnakiuka haki za kibinadamu.

Baada ya kikao kuisha mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu , licha ya kwamba alishasaini karatasi hizo ambazo zilikuwa ni ‘implicity’ kwenye utekelezaji wake , lakini bado alijiona kama mtu aliekosea watanzania , lakini pia aliejikosea yeye mwenyewe , lakini wakati huo huo Mheshimiwa Senga kuna tukio ambalo lilikuwa likijirudia rudia kwenye akili yake kiasi kwamba lilimfanya kabisa kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mke wake mpaka kupelekea malalamiko.

Mheshimiwa Senga alijikuta akijiegamiza kwenye kiti chake huku akikusanya mikono yake pamoja , alionekana kuwaza sana , haikueleweka mara moja ni nini kilichotokea kwenye Ibada ya Mpasuko Wa Mwezi kutokana na usiri mkubwa uliokuwepo , lakini jambo moja ambalo ni dhahiri ni kwmaba mheshimiwa Senga alikuwa akifanya maamuzi ambayo yapo nje ya kile anachokisimamia kama Raisi licha ya kwamba alishasaini ‘Impilicity Law’ inayohusiana na Mashoga aliamini siku sio nyingi atalazimishwa kusaini ‘Explicity Law’ inayohusiana na mashoga.

(Implicity Law ni hitimisho la kisheria ambalo linampa mtu haki ya kitu pasipo kuingiliwa licha ya kwamba sheria hio haiwekwi wazi, kwa mfano kauli ya kiongozi mmoja wa dini akisema kwamba Mapenzi ya jinsia moja sio Kosa , sio uhalifu lakini ni Dhambi hio ndio sheria isio ya moja kwa moja lakini yenye kutekelezwa , yaani huwezi kusikia kiongozi akisema hadharani kama anakukataa ushoga ilihali sheria hio ishasainiwa.

Explicity Law ni aina ya sheria ambazo ni za moja kwa moja na zinapaswa kutekelezwa kwa namna yoyote ile na mara nyingi sheria hizi kwa hapa Tanzania hupitishwa na Bunge pamoja na mahakama halafu ndio raisi atasaini ili ianze utekelezwaji wake.

Wanasheria mtatusaidia Zaidi hapo.

**********

Naam ilikuwa ni siku ya jumamosi Roma alionekana Kibaha kwa Mathiasi akikunja kushoto akiwa anendesha gari yake kuelekea upande wa mji wa kisasa , mji ambao unamilikiwa na kampuni ya Vexto Group.

Roma aliendesha gari yake kwa utaratibu huku akifurahia mazingira safi yaliokuwa yapo kandokando ya barabara hii kuelekea kwenye mji huu, kusema ukweli licha ya kwamba ilikuwa mara yake ya pili kufika kwenye huo mji lakini muonekano wake siku hio ulikuwa kama ni mpya kwake na alijiambia ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanyika mpaka kujenga makazi hayo ya kisasa kabisa kwa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dakika kama tano aliweza kuingiza gari yake kwenye geti kubwa linarohusu magari kuingia kwenye ‘Apartment’ hizo na alikwenda moja kwa moja kuegesha kwenye Parking ya muda mfupi na akashuka na kuanza kutembea uelekeo wa jengo la Athena.

Alikuwa mahali hapo asubuhi hio kutokana na kwamba alikuwa na miadi na mrembo Suzzane , ambaye baada ya kuwasiliana nae alimwambia kwamba amfuate nyumbani kwake na Roma kwakuwa ndio alikuwa na shida ilimbidi kufanya hivyo ili kuonana na mrembo huyo.

Baada ya kufika chini kabisa ya hilo jengo alipiga simu Kwenda kwa Suzzane na alipewa maelekezo ya Kwenda mpaka Floor namba kumi na kusimama kwenye mlango wenye namba 200 ndio Apartment yake.

Tokea mrembo huyu aje kumchukua kwa mara ya kwanza kule Mbagala hakuweza tena kuongea nae moja kwa moja , kwanza Roma alimchukulai Suzzane kama mwanamke Siriasi asiependa utani , lakini pia Suzzane mara nyingi alikuwa ndani ya idara hii kwahio ilikuwa ngumu kwake sana kuonana nae mara kwa mara na kumzoea.

Dakika chache tu Roma alikuwa nje ya mlango namba 200 na alibonyeza kitufe cha kengele na kisha akasubiri mlango kufunguliwa na zilipita dakika kama mbili hivi hatimae mlango ulifunguliwa na mrembo Suzzane ambaye alikuwa amevalia gauni fupi la kumpendeza.

Suzznae alikuwa mzuri sana unaweza kumuitwa kwa jina la Black Beuty , kinachompoza ni ile hali yake ya kuwa siriasi na hata alivyosimama mbele ya Roma mara baada ya kufungua mlango alikuwa na sura yake yenye usiriasi vilevile na Roma alijiambia ilikuwa ni haki kabisa kwa mrembo huyu kuwa msaidizi wa Edna , kwani walikuwa wakiendana kwa asilimia mia moja tofauti yao tu ni kwamba Suzzane alikuwa na macho flani hivi akikuangalia ni kama anakudharau.

“Karibu”Alimkaribisha na Roma alitingisha kichwa na kisha kupita.

Roma licha ya kwamba alimpigia Suzzane , ila hakuweka swala lake wazi , alimwambia tu kuna mambo muhimu ambayo alikuwa akitaka kiuongea nae.

ITAENDELEA

WATSAPP 0687151346
341 umeirudia mkuu
 
Nahisi hata Bwana Rais aliliwa kiboga
mwenyewe nimewaza hivyo hivyo,
ila haya mambo ya secret societies bana ni balaa sana, wengi wa watu wanaotajwa kuwa member huko wana character za ajabu ajabu.........(hili la upinde wengi huhusishwa nalo sana)
 
Back
Top Bottom