Rogers luyangi
JF-Expert Member
- Sep 15, 2014
- 552
- 948
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Baharia katutosa kiaina
Poa boss twasubili jioni ifike tutambeKesho jioni naweka muendelezo msijali simulizi mdogo mdogo hii itaisha tu hata mwakani
Shusha nondo mtaalam!NILIEMDHANIA NI KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI:SINGANOJR .
AGE:18+
UTANGULIZI.
NB:SIMULIZI HII NI YA KUTUNGA
PROLOGUE../DIBAJI
Ilikuwa ni muda wa usiku saa tisa kamili ndani ya chumba kikubwa anacholala mheshimiwa Rais Senga , akiwa amepumzika na mke wake mara simu yake kubwa ya I phone 13 ilianza kuita mfuliulizo kiasi cha kumuamsha na kushangaa ni nani anampigia muda huo kwani sio kawaida yake , na mara nyingi akipokea simu usiku sana huwa ni za dharula na kuna tatizo kubwa ambalo wasaidizi wake wameshindwa kulitolea maamuzi, aliangalia jina la mpigaji na kujikuta usingizi ukimuishia, jina kwenye kioo lilionekana limeandikwa Senior(Mkubwa kazini).
“Senior kuna nini? , maana sio kawaida kunipigia muda huu”.
“Senga ulinihakikisha kuwa Edna atakuwa salama ndani ya taifa lako , lakini nini hiki kinaendelea ndani ya nchi yako”
“Naomba upunguze jazba Senior nini tatizo?”
“Vijana wangu wamenitumia ripoti kwamba Edna alitekwa”
“Nini..!! , unahakika na hio taarifa Senior?”
“Nina uhakika na vijana wangu wangu Senga , nimewapa kazi hio moja tu ya kumlinda Edna kwa siri”
“Vipi hali ya Edna kwa sasa??”.
“Ni bahati kwamba sasa hivi ana mume , kwa hilo namsifia sana , yule mtoto ana akili sana kachagua mume bora”
“Unamaanisha Roma ni mume bora kwa Edna?”.
“Ndio Senga mchunge sana huyo kijana sio mtu wa mchezo mchezo na ni mtu katili kuwahi kutokea katika huu ulimwengu, hakikisha unakuwa upande mzuri na yeye kukusaidia kwenye mpango wako, mimi yangu ni hayo tu na nikwambie Senga haupo makini kabisa Edna anatekwa huna habari , mimi niliopo ng`ambo ya pili ya nchi yako nimepata taarifa kabla yako , nimekasirishwa sana na jambo hili ,Usiku mwema nadhanni tutaongea Zaidi juu ya mipango yetu siku tukionana”Aliongea Senior na kisha kukata simu.
“Who is this Guy?”Alijiuliza mheshimiwa Senga huku akiwa ni mwenye kushangaa Senior anamfahamu vipi Roma.
“ My guess was right he is not normal , there is more hidden info about him , I have to dive deep to discover more details”.Aliwaza mheshimiwa.
Kabla haujaendelea jiulize haya maswali:
Roma ni nani katika hii simulizi , kwanini Senior anasema ni mtu katili kuwahi kutokea kwenye huu ulimwengu?.
Edna ni nani , kwanini Senior anamlinda kwa siri ?”
Senior ni nani na ni mipango gani anayo yeye pamoja na Senga Raisi wa Tanzania.
UTANGULIZIRoma mbeba mizigo ndani ya soko la Mbagala Rangi Tatu anamdhania Edna Kama mwanamke anaejiuza ,baada ya mwanadada huyu kuwekewa dawa ya usingizi kwenye kinywaji na maadui zake katika ulimwengu wa Biashara akiwa ndani ya hoteli na Roma anambeba Edna na kumpeleka Geto kwake na afanya nae mapenzi.
Edna kwa Mara ya kwanza analala na Roma pasipokujitambua na kupoteza usichana wake ,baada ya tukio Hilo anaamua kuolewa na Roma kwa mkataba wa Miezi sita ili kuepuka kuolewa na mwanaume asiempenda ,baada ya Roma kufunga ndoa na Edna anakuja kugundua kuwa mke wake anamiliki kampuni kubwa Nchini huku akiwa na utajiri wa kutisha.
Edna anamuona Roma kama mtu asiyekuwa seriasi na maisha kutokana na aina ya mfumo wa maisha yake ,maisha ya kuwa na wanawake wengi swala linalomkasirisha Edna.
Edna anajitahidi kuweka ukaribu na Roma ili kujua sababu ya mume wake macho yake kubadilika Rangi anapokuwa na hasira na kuwa ya kijani huku akiwa na roho ya ukatili mno
Idara na mamlaka za kiusalama Nchini zinashangazwa na uwezo wa Roma wa kuzungumza Lugha zaidi ya ishirini na mbili na wanaanza kutafuta taarifa zinazomuhusu Roma lakini licha ya kupata taarifa inayoonyesha Roma kusomea ndani ya chuo kikubwa Duniani Cha Harvard wanakosa taarifa zingine zinazomuhusu Roma na kuishia kujiuliza Roma ni Nani haswa
SEHEMU YA KWANZA
Ni muda wa saa moja za jioni ndani ya soko la Mbagala Rangi tatu pilika pilika zilionekana kuwa nyingi sana kwa wafanya biashara , kwani muda huu kwa wafanya biashara wengi ndani ya soko hili ndio muda ambao walikuwa wakifunga biashara zao na kurudi majumbani , hususani wale waliokuwa wakifanya biashara za nguo na vyakula.
Kikawaida ndani ya hili soko wafanyabiashara wengi walikuwa wakihifadhi mizigo yao sehemu salama kwa wale ambao walikuwa na mizigo mikubwa ambayo hawakuwa na uwezo wa kurudi nayo nyumbani , ambao pia hawakuwa na maduka maalumu ya kufanyia biashara , hivyo mara nyingi hulazimika kuhamisha mizigo yao kutoka eneo wanalo fanyia biashara mpaka sehemu ya kuhifadhia.
Kazi hii ya uhamishaji wa mizigo ni kubwa kwa wafanyabiashara hivyo huomba msaada kwa waendesha mikokoteni na wabeba mizigo kuwasaidia kuhamisha huku wakiwalipa kwa kiasi cha mizigo wanayobeba.
“Roma njoo leo unisaidie kubeba mizigo yangu basi nikahifadhi muda umeenda sana” aliongea mwanamama mmoja hivi mweupe wa wastani mnene aliekuwa akifanya biashara ya kuuza madela , vijoli pamoja na viatu vya kike ndani ya soko hili la Rangi tatu.
“Mama Nasra wala hata usiwaze , nitakuhamishia haraka haraka maana nina kazi pia ya kuhamisha na mzee Saidi”.
“Haya mwanangu nashukuru sana”Aliongea mwananamama huyu huku akimuonesha Roma mizigo ya kuingiza kwenye mkokoteni wake kwa ajili ya kwenda kuhifadhi sehemu husika.
Ndani ya dakiika kadhaa tu Roma alikuwa ameshamaliza kazi ya kuhamisha mizigo yote ya kibiashara ya Mama Nasra na kulipwa buku lake na sasa alikuwa bize na kuhamisha mizigo ya Mzee Saidi , ambaye alikuwa ni muuza Viatu vya mtumba.
Uchapakazi na uaminifu wa Roma ulikuwa ukiwafurahisha sana wafanya biashara wengi sana wa soko hili kiasi cha kupelekea mara nyingi kumtaka Roma awasaidie kila linapokuja swala la kubeba mizigo kuitoa sehemu moja kwenda nyingine , alikuwa akifanya kazi kwa haraka sana , kiasi ambacho hata wenzake abao aliokuwa akifanya nao kazi hio hio walikuwa wakimshangaa kwa uwezo na nguvu alizokuwa nazo Roma .
“Kijana Asante sana kwa kuhamisha kwa haraka haraka maana nina dharula”
“Usijali mzee wangu” Aliongea Roma kwa kuweka tabasamu usoni mwake na kisha alipokea noti yake ya shilingi elfu mbili na kisha kuingiza mfukoni.
Mpaka kufikia muda wa saa nne za usiku Roma alikuwa amesomba bidhaa nyingi za wafanya biashara na kwenda kuzihifadhi na sasa alikuwa amekaa kwenye moja ya meza tupu iliokuwa haina kitu akihesabu hela zake.
“Hatimae nimeingiza Elfu kumi na tano , ni kiasi kikubwa sana hiki kwa leo , ngoja nikale ugali na nyama ya Mbuzi kwa mama Joshua nisepe home nikalale”Alijiongelesha Roma huku akinyanyuka mahali alipkuwa ameketi na kusogelea mkokoteni wake na kuuweka pembeni sehemu ambayo mara nyingi anauhifadhi yeye pamoja na wenzake mpaka siku inayofuata .
“Oy mwanaa , leo umepiga kazi sio poa”.
“Kawaida tu Juma , japo ni kweli siku ya leo haikuwa kama jana”Aliongea Roma akiongozana na rafiki yake Juma wakielekea uelekeo mmoja . Juma ni rafiki yake Roma wa muda na walikuwa wakifanya kazi pamoja , utofauti wa Juma na Roma ni kwamba Juma yeye alikuwa ni mwenyeji wa jiji hili la Dar es salaam , akiwa amezaliwa ndani ya jiji hili na Roma alikuwa na muda wa miezi sita tu tokea aingie ndani ya jiji hili la Dar es salaam kutokea mikoani na alikuja ndani ya jiji la Dar kama moja ya vijana wengi wanaokuja kwa kisingizio cha kutafuta maisha.
Roma alikuwa ni mrefu wa wastani , mwenye mwili uliokuwa umejengeka vyema kimazoezi , hakuwa handsome sana wala hakuwa mwenye sura mbaya , alikuwa ni wale wanaume ambao walikuwa wakionekana kawaida sana katika macho ya wengi na moja ya sababu kubwa iliompa Roma umaarufu ni kutokana na uchapaji kazi wake ndani ya soko hili la Rangi tatu.
Baada ya marafiki hawa kuvuka upande wa pili wa barabara hatimae walikuwa ndani ya mgahawa wa Mama Joshua kwa ajili ya kupata chakula cha usiku , waliungana na wenzao wengi waliokuwa ndani ya eneo hilo na kuagiza chakula huku wakiendelea kupiga stori za hapa na pale ili mradi kunogesha maongezi yao.
“Oya Wadau leo Club B kuna bonge la Party , leo ni full bia nusu bei”Aliongea jamaa mmoja mbeba mizigo aliekuwa maarufu sana ndani ye eneo hili la Rangi tatu aliekuwa akifahamika kwa jina la Yusuph.
“Tukitoka hapa lazima tukatembelee eneo hilo, ila hio parti inahusu nini?” aliuliza jamaaa mmoja mwembamba hivi.
“Mrembo Rose leo ni siku yake ya kuzaliwa na kuna bosi anaetoka nae hapa town ndio kaamua kumfanyia bonge la sherehe”.
“Kama ni hivyo hapo ni sawa kwa sisi kwenda kutembelea , au unaonaje Roma “ aliongea Juma akionekana ni mwenye kufurahia tukio hilo linalokwenda kutokea kwani alikuwa ni mwenye kupenda sana kunywa bia hasa zile za ofa.
“Nyie mtatangulia mimi nitarudi Getto kwanza nikaoge then nitaungana na ninyi”
“Ahaaa.. mzee unazingua , hapa hata sisi tutaenda kuoga kwanza ndio turudi kwenye Parti”aliongea Juma na kuwafanya wengine wote wamsapoti.
Naam ni muda wa lisaa limoja tu Juma akiwa ameongozana na Roma walikuwa mbele ya nyumba iliokuwa na geti jekundu Mbagala Biasi pembezoni kabisa na kilipokuwepo kituo cha Tanesko , taa kubwa za kituo hiki ziliwamulika na kufanya waonekane vyema kwa wapiti njia , kwani licha ya kwamba muda ulikuwa umeenda sana , lakini bado pilikapilika za watu wa eneo hili zilikuwa zikiendelea.
Baada ya kusimama kwa madakika kadhaa hatimae mlango mdogo wa geti hilo ulifunguliwa na mwanadada mmoja mrembo aliekuwa amevalia shungi na kuwakaribisha ndani.
“Najma vipi , ulikuwa umelala mbona umechelewa kfungua mlango?”.
“Hapana nilikuwa chumbani na hata sikusikia” aliongea mwanadada huyu kwa sauti yake iliokuwa ikisikika vyama na kisha alimwangalia Roma na kumsalimia.
“Roma mambo”
“Poa Naj , habari za siku nzima”.
“Safi tu”
“Oya Roma kajiandae chap tuondoke muda unakwenda wenzetu watatangulia kufika” aliongea Juma ilimradi tu akatishe maongezi yaliokuwa yakiendelea kati ya Roma na Najma .
Najma alikuwa ni mdogo wake Juma , alikuwa akiishi ndani ya nyumba hio ambayo ilikuwa ni yakwao walioachiwa ya urithi , ilikuwa ni nyumba kubwa tu ambayo ilikuwa wameigawa nusu wapangaji na nusu walikuwa wakiishi yeye pamoja na kaka yake.
Najma alikuwa akifundisha shule ya chekechea eneo moja lililokuwa likifahamika kwa jina la Kiramba, licha ya kwamba alikuwa akilipwa ujira mdogo , lakini alikuwa pia akionekana kuipenda kazi yake hio ya ufundishaji.
Tokea siku ambayo Roma anafika ndani ya nyumba yao na kupanga , Najma alitokea kumpenda Roma, Najma alikuwa si mwenye furaha asipomuona Roma , na kutokana na shughuli za kaka yake na Roma kuwa ni za kuwaruhusu kurudi usiku na kudamka asubuhi asubuhi , hivyo mara nyingi alikosa muda wa kuonana na Roma , hali ambayo ilimfanya kuhakikisha kila siku yeye ndio anaewafungulia mlango kila wanaporudi kutoka kazini.
Licha ya Najma kumpenda Roma kwa kaka yake ilikuwa ni tofauti , hakupenda kabisa Najma kujihusisha kimapenzi na Roma kabisa na hii yote ilisababishwa na hali ya kimaisha aliokuwa nayo Roma ,Juma alimuona Roma kama mtu ambaye hakuwa na malengo na maisha yake , hivyo aliona kitendo cha dada yake kuingia katika mapenzi na Roma dada yake asingefika mbali kimaisha na angeendelea kuishi katika hali ya maisha duni jambo ambalo hakuwa akitaka litokee kwani aliamini kwa uzuri aliokuwa nao dada yake , kama ni kupata mwanume mwenye pesa na kumuoa lisingekuwa jambo gumu , lakini asiliolijua Juma ni kwamba ni wanaume wengi sana walikuwa wakikataliwa na Najma licha ya kutaka kumhonga pesa nyingi na hata kumuahidi kumuoa ,mlimbwende huyu alikuwa amekufa na kuoza kwa mwanaume ambaye hakuwa na chochote cha kutishia jamii , mwanaume wa kawaida sana na maskinini mpangaji wao anaenda kwa jina la Roma.
Katika akili ya mwanadada huyu mrembo Najma aliamini siku moja Roma atamtamkia tu kuwa anampenda na yeye pia atamkubali na watayaanza maisha yao pamoja , hio ndio Imani aliokuwa nayo Najma juu ya Roma.
Kwa upande wa Roma alikuwa akijua fika kuwa Najma alikuwa akimpenda sana kimapenzi , lakini pia alikuwa akijua sana kwamba Juma hakuwa akitaka dada yake kutoka na yeye kimapanzi kutokana na hali yake ya kimaisha , hivyo licha ya yeye kumuona Najma kama mwanamke mrembo ambayey yeye kama mwanaume rijali anapaswa kuwa naye katika mahusiano , lakini alijitahidi sana kujizuia kumuonyeshea mapenzi mwanadada huyo , kwani hakuwa ni mtu mwenye kutaka ugomzi na rafiki yake Juma , kifupi alikuwa amependa sana chumba alichopanga ndani ya nyumba hii ya Roma na dada yake.
Basi baada ya Roma na Juma kujiandaa na kubadilisha nguo hatimae walitoka kwa kupitia geti dogo na kisha kutoka ndani ya nyumba hio na kuelekea uelekeo wa Club B , kutoka Bias mpaka ilipokuwa ikipatikana Club B hapakuwa mbali sana , Club hii ilikuwa ikipatikana Chalambe nyuma kidogo kabla haujafika sehemu iliokuwa ikifahamika kama Maji Matitu , ilikuwa ni moja ya Club kubwa sana na ya kuvutia iliokuwa ikipatikana ndani ya eneo hili , lakini pia ilikuwa maarufu sana kiasi kwamba ilikuwa ikitembelewa na watu waliokuwa wakiishi ndani ya mji huu pamoa ambao waliokuwa wakiishi nje ya eneo hili , ikiwemo Chamazi , Temeke , Kisemvule na baadhi ya meneo ya karibu.
“Wadau mmechelewa sana tena Sanaa yaaniii ….. bia ya tatu hii”Aliongea Yusph huku akigida bia yake kwa mbwembwe iliokuwa na chapa la Safari Lager .
“Usijali Yusuph tutakufikia tu “Aliongea Juma huku akiangaza macho huku na kule akikagua mandhari ya hapa ndani na hata kwa upande wa Roma hivyo hivyo.
“Siku hii ya leo watu walionekana kuwa wengi , kwani makelele yalikuwa mengi , huku harufu ya Pombe ikiwa imetapakaa kwa hali ya juu ndani ya eneo hili.
“Handsome Boys karibuni niwahudumie”Ilikuwa ni sauti moja nyororo iliosikika kwa vijana hawa na kuwafanya wamuangalie aliekuwa akiongea na hapo kila mmoa alitoa macho ya uchu baada ya kumuona mwanamke wa haja. Mrembo alievalia suruali ya kitambaa iliomchora vyema umbo lake namba nane , mwanamke huyu alikuwa ni mzuri kweli , si kujaliwa tu shepu lakini pia alikuwa amejaliwa sura nzuri yenye urembo wa asili ambao huwafanya wapenda ngono wengi kummezea mate.
“Aaaaa..hhh Sister Rose sjijatarajia kukuona leo ukihudumia bhana”Aliongea Juma kwa mshangao na kumfanya Rose kutabasamu huku macho yake yote akiwa ameyaelekeza kwa Roma ambaye alionekana kama mtu ambaye hakuwa na habari na mtu aliekuwa mbele yake kwani alikuwa ni mwenye kukagua kila mtu aliekuwepo ndani ye neo hilo kama jasusi anaetafuta adui.
“Mimi nipe Safari kama Broo wangu yusuph hapo , nipe ya baridiii”Aliongea Juma huku akikaa vizuri kwenye viti hivyo virefu huku akiwa amechia tabasamu pana usoni mwake.
“Na wewe Roma vipi leo” Aliongea huku akimwangalia Roma kwa madaha kiasi kwamba wenzake wote walikuwa wakimuonea wivu kwa kuangalia na mwanamke mrembo kama Rose kwa staili hio.
“Nataka ofa leo , nipe Heinken gharama ni juu yako”Aliongea Roma pasipo kupepesa macho na kumfanya Rose atabasamu na kisha kumwambia asijali anamletea na atalipia kwa kila kinywajia atakachokunywa kwa siko hio , jamboa mbalo liliwafanya marafiki zake waone ni upendeleo , lakini wala Rose hakuwajali.
“Oya mwanangu Roma huyu Manzi anakukubali sana kitambo tu , nashangaa mzee huchangamki , au unaogopa ni vya wakubwa”Aliongea jamaa mmoja aliekuwa pembenni ya yuspuh ,jamaa huyu alikuwa akifahamika kwa jina la Samia.
“Kweli kabisa Samia , Manzi anamkubali sana Mwamba hapa , lakini jamaa anazembea zembea , ningekuwa mimi ningekuwa nisharekebisha tayari na hapa ningekuwa nakunywa bia fulu fulu bureeee”Aliongeezea Yusuph na muda huo huo alikuja Rose na kuweka vinywaji huku akimpatia kinywaji Roma.
“ Bebi kuna ,mbuzi choma nikuleteee” wote waliangaliana kwa macho ya kimshangao na ya kutamani kile kilichosemwa , lakini hawakuambiwa wao , mtu aliekuwa amepewa ofa hio alikuwa ni Roma.
“Kweli mama leo umezaliwa upya , kama ni ofa mimi sina tatizo na nipo tayari kwa kila ofa inayopatikana”Alionea Roma .
“Ofa nyingine hautaweza , siku zote umekuwa ni wa kunikimbia” aliongea Rose kwa kumnong`oneza Roma na kumfanya atabasamu , kwani alikuwa akijua alichokuwa akimaanisha Mrembo huyu.
Huu usiku kama walivyotegemea vijana hawa ndio kile walichopata , kwani walilewa chakalii kwa bia za ofa ambazo zilikuwa zimetolewa na kibosile ambaye ilikuwa ikiaminika alikuwa akitoka kimapenzi na mwanadada Rose.
Baada ya masaa matatu baada ya ya keki kukatwa na sherehe kukaribia kumalizika , huku waliokuwa wakiendelea kula mziki na kunywa bia wakiendelea , alikuja jamaa mmoja aliekuwa mhudumu wa hii Club na kumpa kijimemo Roma, ambaye licha ya kunywa bia nyingi alionekana kuwa ngangari kuliko wenzake wote , baada ya kufungua kimemo hiki , alitabasamu na kisha alinyanyuka na kuoelekea nje , na kukata kushoto na ndani ya dakika chache alikuwa nje ya chumba na kugonga , na mlango ulifunguliwa na mrembo Rose aliekuwa amevaa khanga moja tu, alionekana alikuwa ametoka kuoga.
“Karibu Mpenzi”Aliongea Rose kwa namna ya kudeka huku akimvuta Roma ndani na kuzama mzima mzima .
iNAENDELEA HIVI PUNDE .
View attachment 2319976
Shusha boss tupo mkao wa kula maana ndio jioni hiiNgoja niwashushie vipnde

SEHEMU YA 42
Kila mmoja alishangaa kwanini mzee huyu alipandwa na jaza ghafla namna hio mara baada ya kunong`onezwa jambo na muhudumu wa nyumba.
Tikayi aliekuwa amekaa pembeni na baba yake alionekana kutokuwa na wasiwasi kabisa ni kama mtu ambaye alikuwa akijua ni taarifa gani baba yake ameambiwa.
Na wakati wakiendelea kujiuliza ni kwanini mzee Yamamoto kapandwa na Jazba mara aliingia bwana mmoja mkumkukuku , bwana ambaye alikuwa amevalia shati lake rangi ya maua maua na suruali ya Jeans.
Bwana huyu ukimwangalia mara moja tu utagundua kuwa Tikayi na huyu bwana ni ndugu kimuonekano, jamaa huyu baada ya kuingia alijikokota na kudondoka kwenye miguu ya Yamammoto na kisha akaanza kulia kwa sauti na alionekana kulewa pia , jambo ambalo lilifanya hali ya hewa kuwa mbaya.
“Wu.. baba .. ninafanya nini mimi.. aaaaaah Dina kaniacha baba ..iiii .. Dina..weeee… aaaa”
Jamaa alikuwa akilia mpaka anatema mate kitendo kilichozidi kumkasiriasha mzee Yamamoto na alichokifanya ni kumpiga teke na akadondokea upande mwingine , lakini huyu bwana aliamka tena na kukamata mguu wa baba yake na kuanza kulia tena huku akiwa anamtaja mwanamkie anaeitwa Dina akilalamika ameachwa , na kila mmoja aliekuwa hapa ndani alikuwa ashajua ni nini kinaendelea kwa huyu bwana, walijua yote hayo ni sababu ya kimapenzi. Na bwana huyo alikuwa ameachwa.
“Jamani naomba mniwie radhi kwa jambo hili , huyu ni mwanangu mkubwa Tikayeshi , lakini licha ya kuwa mkubwa katika familia , ndio mpumbavu kuliko wanangu wote”Aliongea mzee huyu wa kijapani huku macho yake yakiwa mekundu kwa hasira.
“Hakuna shida mzee ni jambo la kawaida kwa vijana” Aliongea moja ya wafanya kazi wa kampuni na mzee huyu aliwapa ishara walinzi wamtoe eneo hilo na bwana huyu alikokotwa na kutolewa huku akiendelea kulia kwa sauti kama toto jinga , na kwa kumuangalia tu ungejua kuwa ni sahihi kwa mzee Yamamoto kumuitwa Tikayeshi mtoto mpumbavu kuliko Watoto wake wote.
Tikayi alionekana kutabasamu na kufurahishwaa na tukio hilo , ali mwangalia baba yake alivyokuwa na hasira na kuridhishwa na hali hio.
Basi baada ya chakula wageni wale walitawanyika na hata kwa Mzee Yamamoto waliagana na Roma na kuwatakia usiku mwema huku wakiwaahidi kuonana keshi kwa ajili ya mazungumzo ya kibiashara.
Roma aliingia kwenye chumba chake na hata kwa Dorisi hivyo na wale wawakilishi wa JR pia kila mmoja aliingia kwenye chumba chake .
Roma baada ya kuingia alipunguza nguo na kisha akajilaza kitandani kuutafuta usingizi kwani muda hio ilikuwa yapata saa nne usiku.
Roma alitumia nusu saa tu kujipumzisha mara mlango uligongwa na kujikuta akishangaa nani anagonga, kwani walikuwa washaagana na hata na Dorisi pia , akiwa na singlendi yake pamoa na pensi , alisogelea mlango na kufungua na mbele yake alikuwa mhudumu wa kiume ambaye alikuwa ameshikilia sahani ambayo ilikuwa imefunikwa na kitambaa cheupe na Roma akamwagalia huyu mhudumu pasipo kumsemesha chaohcaote na kushangaa ameleta nini kwani hakuwa amegiza aina yoyote ya huduma , lakini ghafla tu muhudumu huyu wa alievalia sare za hili jumba alitoa kile kitambaa kwa kasi na kwenye ile sahani kulikuwa na kisu na alikishika haraka sana kwa ustadi na kumrushia Roma kwa madhumuni ya kumdhuru , lakini Roma ni kama vile alitegemea , kwani ile kisu kinarushwa alihepa kushoto na kisu kikapita nusu inch na umbali wa kidevu chake kiasi kwamba hata ndevu ziliguswa kiana na Roma hapo hapo akajua huyu ni mhudumu feki na ametumwa kwa ajili ya kuua.
Baada ya mhudumu huyu feki kuona Jaribio lake limefeli , alirusha ngumi lakini kwa Roma alimuona kama mtoto anaejifunza kurusha ngumi kwani aliushika mkono na kuuzungusha na kilichosikika ni mlio wa mifupa kukatika , na Mhudumu feki akaachia mguno wa maumivu , lakini Roma hakuishia hapo tu , alimpiga kwenye koo kwa mkono , kama vile alikuwa akimchinja , kwnai pigo hilo lilikuwa ni la Karate na mhudumu feki aliregea na kudondoka chini.
“Shi*t watakuwa wengi hawa ,Dorisi atakuwa kwenye matatizo”
Aliongea Roma na kuchomoka kwa spidi kuwahi kwenye chumba cha Dorisi na ile anafika tu alimuona mhudumu akiingia ndani ya chumba cha Dorisi huku akiwa na sahani kama ile ile ya mhudumu aliemuua ikiwa imefunikwa na kitambaa cheupe.
Roma alikimbia kwa kasi na kuzama na ile anafika mhhudumu alikuwa tayari ashashika kisu na kumlenga nacho Dorisi kooni na Dorisi aliishia kufumba macho huku akiwa anatetemeka mwili mzima akisubiria kifo , lakini mhudumu baada ya kufikisha sentimita mbili karibu na koo la Dorisi alidakwa mkono na kuzungushwa kwa nguvu ambayo hakuwa ameitegemea , na baada ya kugeuka tu, aliopigwa na mikono miwili kwa wakati mmoja na Roma kwenye mbavu na mhudumu yule wa kijapani aliishia kuachama na kukosa pumzi na kisha akadondoka chini kwani mbavu zilikuwa zishakatika.
Dorisi alihikuta akimkimnbilia Roma na kumkumbatia huku akianza kulia kama mtoto na Roma alimtuliza na walati huo huo aliingia ndani ya chumba cha Dorisi Tikayi.
“Mko salama?” ndio swali la kwanza kutoka kwa Tikayi huku akimwangalia Roma kwa macho ya kumsanifu.
“Naona mmetuleta Japani kwa ajili ya kutua”Aliongea Roma kwa hasira na Tikayi alianza kuomba msamaha kwa tukio hilo na wakasema kwamba hawahusiki nalo.
“Mr Roma hili swala halituhusu hata kidogo na tutahakikisha tunawakamata wahusika , kwani tunaamini ni watu ambao wametumwa”:
Aliongea Tikayi na muda huo huo aliingia bwana mmoja alievalia Robes za kitamaduni za Japani huku akiwa ameshika upanga kwenye mkono wake na Roma kwa kumuangalia tu aliuona huyo jamaa anajua mapigano.
“Yoshida hakikisheni mnamkamata aliehusika na hili jambo haraka , naamini ana watu wake humu ndani na bado wapo, kagua wahudumu wote mmoa mmoja” aliongea Tikayi na bwana huyu aliamrisha walinzi waliokuwa wamevalia mavazi ya majoho meusi kama yeye na kuanza kutawanyika kumtafuta muhalifu.
Dorisi na Roma walitolewa na kupelekwa kwenye chumba maalumu cha usalama Zaidi na wakati huo huo mzee Yamamoto na yeye aliingia kwa spidi na kuanza kuasihi Roma, Dorisi na wawakilishi wa JR grupu watulie mpaka pale mtuhudumiwa atakapo kamatwa huku akiomba msamaha kw akujitetea jambo hilo hawakuwa wakihusika nalo.
Wote walikusanyika na kukaa kwenye masofa haya , akiwemo Tikayi ,Yamamoto Roma ,Dorisi pamoja na wawakilishi wa JR Group , wakati wakiendelea kuongea juu ya tukio hilo ambalo halijawahi kutokea ndani ya hii nyumba kutokana na ulinzi wake , mara aliingia meneja wa nyumba , yule ambaye alimnong`oneza Yamamloto kuhusu ujio wa kilevi wa Tikayeshi.
“Kuna nini meneja?”
“Boss kuna simu yako hapa kutoka kwa mtu ambaye hatumjui na anadai humu ndani ametegesha mabomu”
“Mabomu!”Aliongea kwa kupaniki huku akichukua ile simu na kusikiliza.
“Mr Yamamoto , nyumba yako yote imejaa mabomu ambayo yataripuka baada ya nusu saa , na hata ujifanye kuyatafuta hautoweza” ilisikika sauti hio ya kijapani kwenye simu na Roma aliisikia vyema kwani na yeye alikuwa akijua kijapani.
“Unataka nini katika familia yangu”Aliongea Yamamoto kwa hasira kwa kijapani.
“Kwanza kabisa nikwambie tu kwamba mabomu yatalipuka baada ya nusu saa na hata kama ulete wataalamu wa uwezo wa juu hatoweza kufanikisha hilo ndani ya nusu saa , na mabomu hayo ni ya sumu kwa maana hio nikibonyeza kitufe ambacho nimeshikilia hapa , itawachukua dakika tano kwa kila kiumbe ndani ya nyumba kufariki”
“Sema unataka nini acha maneno mengi”
“Ni jambo rahisti tu nahitaji Yen Bilioni kumi zinifikie mahali ambapo nitawaambia na nataka Cash….” Aliongea bwana huyo , lakini muda huo huo aliingia Tikayeshi huku akilia.
“Baba .. mabomu … mabomu baba… tunakufa .. Mama wee.. babab niokoe sitaki kufa sitomuaona tena Dina mimi ,,,,aaaaaa” Alilia bwana huyu kama chizi kiasi kwamba Yamamoto alikasirishwa Zaidi na kujisemea moyoni boar ahata abadilishane na mt una gunia la Pumba heanda akapunguza hasara ya kuwa na toto jinga.
“Mtoeni huyu mpuuzi hapa” Aliongea Yamamoto na Tikayeshi alitolewa huku akiendelea kulia kwa sauti akitaja mabom na baada ya Tikayeshi kuondoka Yamamoto aliendele akusikiliza simu.
“Endelea na masharti yako nakusikiliza”
“Nishasema mzee kiasi ninachotaka , shariti la pili mtu atakae leta hizo pesa lazima awe wewe au Tikayi” mzee alitoa macho.
“Kwanini mimi au Tikayi , shida yako ni pesa na tutakupatia haina haja ya mimi kuja au Tikayi kuja”.
“Mzee nadhani haulewi nishasema nahitaj wewe uje ulete pesa hizo au Tikayi ndio alete na niwaambie tu naona kila kitu mnachokifanya hapo ndani na ikitokea mtu atatoka ama kuingia ndani ya hio nyumba bila ruhusa yangu nabonyeza kitufe na Maisha yenu yatakuwa yamefika mwisho na kama haumini mlangoni hapo kuna mtu aliesimama kama kaegeshwa” Wote waliangalia mlangoni na kuona kweli kulikuwa na mtu ambaye alikuwa ni mlinzi wa Yamamoto na wakaini ni kweli bwana huyu alikuwa akiwaona.
Mzee yamamoto jasho lilianza kumtoka , licha ya kwamba kulikuwa na baridi kali lakini jasho lilionekana kwenye uso wake , hakuwa tayari kumuachia Tikayi aende kwani alikuwa ndio mrithi pekee na ndio mtoto ambaye alikuwa na akili , kwani kaka yake alikuwa ni kama chizi.
“Okey tupe dakika kumi na tano tukuandalie Cash”
“Dakika kumi zinatosha hakuna maongezi na narudia , naona kila kitu kinachoendelea hapo ndani mpaka panya wanaoingia na kutoka, hivyo nikiona mtu anatoka ambaye sio wewe au Tikayi nabonyeza kutufe na kuwalipua”.
“Sawa tupe dakika kumi tukuandalie Cash”
“Nitapiga baada ya dakika kumi , muwe na Cash na ndipo nitawapa eneo mnalotakiwa kuja”
Baada ya simu kukatwa Yamamoto alimuuliza Tikayi kama wanashilingi ngapi hapa ndani na Tikayi alisema wana Yen bilioni kumi na nusu, mzee baada ya jibu hilo alipata ahueni na kumuagiza Tikayi akaziweke kwenye begi na baada ya dakika kama saba hivi Tikayi alirudi akiwa ameshikilia begi zito likiwa na vibunda vya hela .
“Nitaenda mimi baba”Aliongea Tikayi na kufanya watu wote hapo ndani washangae.
“Hapana Tikayi , hao majambazi siwaamini kabisa wanaweza wakakufanya kitu , kibaya na wewe ndio mrithi pekee ambaye napanga kukuachia kuiongoza Yamakuza , hapana siwezi kukuruhusu kwenda”
Aliongea Yamamoto lakini Tikayi aling`ang`ania kwenda na baada ya malumbanio ya dakika mbili Mzee huyu alikubali Tikayi aende lakini akimsihi kuwa makini.
Baada ya dakika kumi Jambazi lilipiga simu na kutoa maelekezo ya sehemu ambayo alitakiwa kwenda , ni sehemu moja iliokuw aikifahamika kwa JPN.
Jambazi aliendelea kuwapiga mkwara kwamba hakuna mtu kutoka Zaidi ya Tikayi, na mzee Yamamoto licha ya kwamba alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa , alikubaliana na Jambazi , kwani hakuwa akitaka kuona watu wote waliokuwa humu ndani wanakufa kisa pesa,
Baada ya Tikayi kutoka akielekea mahali ambapo majambazi hayo ndio walisema wapo , Roma hakubaki hapo kwenye chumba cha usalama , alitoka na kuelekea kwenye chumba chake na baada tu ya kufika , aliangalia nje kwa kutumia dirishani kwa sekunde kadhaa na kisha akatabasamu na kufungua dirisha , alirudi na kuvaa shati na suruali na kisha akarudia dirisha na alionekana alikuwa akijiandaa kuruka.
“Unataka kuniacha sio?, ndani ya hii nyumba unajiokoa mwenywe ”Ilikuwa ni sauti ya Dorisi iliomfanya Roma aliekuwa amepandisha mguu kwenye dirisha ageuke na kumwangalia Doris.
“Doris narudi ,baki hapa naamini hakuna kitakacho kutokea” Aliongea Roma
“Hapana tunaenda wote na sipo tayari kubaki”Aliongea huku akionekana yupo siriasi na Roma alifikiria kwa sekunde na kisha akamgeukia.
“Utaweza kuruka hapa?”
“Hapana”
“Sasa utaendaje na mimi kama hapa huuezi kuruka” Dorisi hakuwa na jibu na Roma alifkiria jambo na kisha akamwangalia.
“ Natangulia kwenda chini , utajirusha na mimi nitakudaka”Aliongea lakini Dorisi alitoa mshangao , kwani alipochungulia umbali kutoka walipo mpaka chini aliogopa.
“Kama huwezi mimi nitaondoka mwenyewe”
“Okey nitajirusha kama kweli utanidaka”.
“Usijali nitakudaka”Aliongea Roma na kumwnaglaia tena Dorisi.
“Nitahesabu mpaka nne usipojirusha naondoka”.
Baada ya kuongea Roma alijirusha chini na kwenda kutua kwenye bustani bila ya kupiga kelele ya aina yoyote ile , alionekana kuwa mtaalamu kweli na baada ya kutua aligeuka na kuangalia juu huku akimpa ishara Dorisi ajirushe , ila Dorisi alikuwa akitetemeka ,Roma baada ya kuona Dorisi anatetemeka na hayuko tayari kujirusha , alimuonesha vidole kwa ishara na kuanza kuhesabu , na ile anafika tatu Dorisi alimpa ishara ya kujirusha na hakuwa na jinsi alikuwa akiogopa kufa mabomu na hakutaka kubaki mwenyewe hapo ndani na ndio maana alitaka kuondoka na Roma , alifumba macho na kujiachia kwa ujasiri na ile anafika chini alikuwa kwenye mikono ya Roma , huku akihema kwa kasi sana na Roma alimtuliza na kumwambia apunguze presha.
UNAJUA NINI KIMETOKEA ..TUKUTANE WIKIEND
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 60 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA
NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
View attachment 2340933
[emoji3][emoji3][emoji3]umempenda sanna Afande mage