Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 104

Roma alimkaribisha kwanza Sophia mpaka kwenye masofa ya hapo sebleni , huku wakiwe mabegi pembeni, na wakati huu na Bi Wema alikuwa ashatoka jikoni na alikuwa ameketi sebuleni wakisubiri utambulisho kutoka kwa Roma.

Roma alimuelezea Edna kama alivyokuwa amepanga na Sophia , lakini kwa Edna alijikuta akishangaa , licha ya kwamba alionekana kuelewa lakini pia alibaki na maswali , kilichomfanya asiulize sana ni kutokana na kwamba hakuwa akimjua sana Roma kuhusu maisha yake ya nyuma na alichokuwa akijua tu ni kwamba Roma amelelewa huko Marekani na kuhusu taarifa za familia iliomlelea hakuwa nayo.

“Kwahio Sophia ni kama mdogo wako?”Aliuliza Bi Wema mara baada ya kuelewa utambulisho.

“Ndio Bi Wema ,Sophia ni mdogo wangu na ujio wake Tanzania ulikuwa wa ghafla sana, kwanza kanipigia akiwa tayari kashafika na sikutaka akaishi hotelini ukilinganisha na wema ambao familia yao imenitendea”Aliongea Roma kwa kudanganya na Sophia akamwangalia Roma na kujiambia kumbe Hades anajua kudanganya.

“Miss nadhani ni jambo zuri kama tutaishi na Sophia kwa muda , isitoshe Roma ni mumeo na ni sehemu ya familia”Aliongea Bi Wema Mzungu wa Roho.

Ukweli Bi Wema licha ya kwamba Edna na Roma walikuwa ni wanandoa wa mkataba lakini kwenye moyo wake alikuwa ashamkubali kabisa Roma kuwa mume wa Edna. Na alitaka na Edna pia amchukulie Roma kama mume wake , kitendo cha Roma kumleta Sophia hapo ndani ya familia alikipenda , aliona kama Edna ataendelea kukutana na baadhi ya familia ya Roma basi ukaribu wao utaongezeka.

Edna alimwangalia Roma ambaye alikuwa hana wasiwasi kabisa na kisha akageuza macho kwa Sophia na kumkagua juu hadi chini , Edna alimuona Sophia mrembo sana , na tofauti kati yake na yeye ilikuwa ndogo, na kwake ilikuwa afadhari baada ya kujua wawili hao ni kitu na mdogo wake,maana dakika kadhaa nyuma moyo wake uliogopa mpaka mwenyewe kushindwa kujielewa.

“Okey! Haina sababu ya Sophie kwenda kuishi sehemu nyingine wakati wewe ni sehemu ya familia yake”Aliongea Edna na kumfanya Roma atabasamu.

“My Wife licha ya kwamba umrembo kuliko wanawake wote ndani ya dunia hii , lakini pia umebarikiwa busara”Aliongea Roma na Edna alitabasamu , licha ya kwamba alijua Roma anampamba tu kutokana na kukubali kwa Sophia aishi hapo , ila ndani ya moyo wake aijisikia vizuri kusifiwa mbele ya Sophia.

“Sister Edna nitakuwa mtiifu na nitahakikisha sikukasirishi”Aliongea Sophie na kumfanya Edna ashangae , kilichomfanya kushangaa ni kwamba kwenye maisha yaaake hakuwahi kuitwa dada na leo ilikuwa mara yake ya kwanza.

Bi Wema alijikuta akitoa tabasamu baada ya kumuona Edna alivyobadilika baada ya kuitwa dada, na alishindwa kumuelewa Sophie kafikiria nini kumuita Edna dada na sio Wifi , ila hakutaka kujali sana kwanza kwa jinsi Sophie alivyokuwa mzuri aliona ni sawa tu kwa hao wawili kuitana dada.

“Roma unaonaje ukimwandalia Sophia chumba chake?”

“Bi Wema chumba kipi kitamfaa??”

“Nitamwandalia mimi”Aliongea Edna na kisha alimwangalia Sophie kwa kumpa ishara amfuate , huku Roma na yeye akinyanyuka kusaidia kubeba mabegi kwenda juu.

Chumba cha Sophia kilikuwa kikiangaliana na chumba cha Edna , Roma aliingiaza Mabegi na kuwaacha dada na mtu wasaidiane kuandaa chumba.

“Kesho tutaenda kununua baaadhi ya vitu ambavyo unataka viwekwe kwenye chumba chako”Aliongea Edna na Sophie alimwangalia Edna.

“Thank you Sister”Aliongea Sophie na kumfanya Edna atabasamu , hakujua kwanini Sophie kaamua kumwita Dada ila alipenda, kwani alimuona Sophia kuwa M’cute’.

Saa tatu kamili Bi Wema alikuwa ashamaliza kupika na Edna alimsaidia kuandaa chakula mezani , Sophie na yeye alikuwa ashamaliza kuoga na kubadilisha mavazi na alishashuka chini na kukaa kwenye masofa , baada ya dakika kadhaa za kuandaa , mtaalamu Roma alishuka chini kwa ajili ya kula chakula kwani njaa pia ilikuwa ikimnyanyasa.

Bi Wema alitabasamu baada ya kuona familia imeongezeka mtu mmoja ,Mama huyu hakuwa akipenda familia kuwa na watu wachache , alipenda familia ya watu wengi.

“Sophie elimu yako ni ya levo gani?”Aliuliza Edna na Roma alimwangalia Sophie ,maana licha ya kwamba amemleta hapo ndani lakini hakuwa na taarifa zozote kuhusu elimu ya Sophia.

“Nina Masters ya Uchumi”

“Kweli!!”

“Ndio Sister Edna,Mbona kama hauniamini”

“Hapana nimeshangaa , unaonekana mdogo kwa levo ya elimu yako”

“Nina ‘skills’ nyingi ambazo zitakushangaza Sister”

“Kama zipi?”

“Nina Mkanda wa Bluu (Blue Belt) kwenye mchezo wa Kung Fu”Aliongea Sophie na kumfanya Roma atake kutema chakula alichokuwa akitafuna na Sophie alimwangalia Roma na kutabasamu.

“Blue Belt kwenye ‘Kung Fu’ ndio mkanda gani?”Aliuliza Edna kwani hakuelewa na Roma alitaka kumsikiliza Sophie atakavyojibu.

“Ni levyo ya kati ya mafunzo ya kimapigano ya kichina ni sawa tu kusema levo ya uvumilivu”Aliongea Sophie na kumfanya Roma amwangalie na Sophie ni kama alifanya makusudi alimwangalia pia.

“Ilikuwaje sikufikria hili kabla , haikuwa kawaida kwa Sophie kuweza kuvumilia lile baridi kwenye ile Mashua”Roma aliwaza.

Ukweli ni kwamba kwa namna ambavyo Sophie na Shirani walivyokuwa wamepakiwa kwenye ile mashua ,lakini pia na kwa jinsi ambavyo ‘Pasific Ocean’ ocean ilivyokuwa na baridi ukijumlisha na barafu ambazo Roma alitengeneza isingekuwa rahisi kwa mtu wa kawaida kuvumilia ile baridi, na ni mtu mwenye mazoezi maalumu tu ya kimwili ndio ambaye alikuwa na uwezo huo.

Roma palepale alitengeneza miale ya rangi flani kwenye macho yake na kummulika Sophia pasipo mtu yoyote kugundua na hapo ndipo alipothibitisha ni kweli Sophia alikuwa na uwezo wa kimapigano kwa levo aliosema.

“Kwa hio Miss Sophie unajua kupigana?”AliongeaBi wema ambaye muda wote alikuwa akisikiliza lakini mazungumzo yalivyofikia hapo alijikuta akikosa uvumilivu na kuuliza.

“Ndio Bi Wema nina uwezo wa kupambana na watu kumi kwa wakati mmoja ambao hawana mafunzo ya kimapigano”

“Mimi siamini”Aliongea Edna na kumfanya Sophie atabasamu.

“Nitakuonyesha picha tukimaliza hapa”Aliongea Sophie na kweli hakutaka kuamini pasipo kuona , kwani kwa mwonekano wa Sophie , aliona ni mdada mrembo sana kuwa na uwezo wa kimapigano.

“Ujuzi wako mwingine ni upi?”Aliuliza Edna.

“Najua pia kuimba na sio kujua tu napenda kuimba na ndio maana nimerudi Tanzania nataka nijikite kwenye usanii”Aliongea na kumfanya Edna awe ni kama haamini hivi.

“Kwahio umerudi tu kwa ajili ya kuwa msanii, na kwanini usiimbe Marekani ukaja Tanzania?”

“Kwasababu napenda Bongo Fleva”Aliongea na kumfanya Edna aelewe , aliona pia sio jambo baya kwa mtu kupenda kufanya kile anachopenda.

Baada ya kumaliza kula chakula Sophie alienda na kuleta picha na kuanza kumuonesha Edna na Bi Wema , walionekana tayari washazoeana na Roma aliekuwa akishuka kutoka juu akiwa ameshikilia funguo za gari yake aliishia kutabasamu moyoni.

“Mafunzo ya Kung Fu yanaonekana kumfanya Sophie iwe rahisi kuwafanya watu waliokaribu yake kumzoea”Aliwaza Roma na kuwasogelea .

Roma alitoa taarifa kama anatoka na Edna hata hakujisumbua kugeuka Zaidi ya kunyoosha mkono tu kuitikia na Roma hakujali sana , alipanga siku hi ya leo akamtembelee mchepuko wake Rose kwani ni muda kidogo hakuwa amemtembelea tokea watoke Kisarawe , aloitaka kujua ni nini kilitokea baada ya pale.

Dakika chache tu Roma alikuwa ndani nya Mbagala , alinyoosha moja kwa moja mpaka ndani ya eneo la Club B na kuegesha gari yake , leo hii ndani ya hili eneo kulikuwa na watu wengi kidogo kutokana na kwamba magari hapo ndani yalikuwa mengi kiasi cha kumfanya Roma ashangae kidogo , kwani ilikuwa sio wikiend.

Roma aliingia ndani ya hili eneo ambalo lilikuwa limechangamka huku likiwa na harufu mchanganyiko za bia na Marashi.

“Hubby!!!”Aliita Rose baada tu ya Roma kuingia hapa ndani, Rose alikuwa amependeza sana usiku huu , akiwa amevalia suruali yake ya kitambaa rangi ya samawati pamoja na blazia nyekundu iliokiacha kifua chake wazi.

“Bebi Rose nimekumisi sana”Aliongea Roma mara baada ya kukumbatiana na Rose pasipo kujali macho ya watu wengi yaliokuwa yakiwaangalia.

“Nimekumisi pia mpenzi”Aliongea Rose kwa sauti yake nyororo ambayo ilimsimua Roma na kisha wakaachiana.

“Kama umenimisi mbona huajanitafuta?”

“Namuogopa mkeo”Aliongea Rose na kumfanya Roma atabasamu .

“Rose mbona leo kuna watu wengi hapa kuna nini?”Rose alitabasamu na kisha akamwangalia Roma.

“Tunasherehekea ushindi leo , unaowaona hapa wengi ni vijana wangu,”Aliongea Roma huku Rose akimshika mkobo Roma na kumuongoza upande mwingine.

Club B ilikuwa ikipendwa pia na matajiri kutokana na mgawanyo wake , kwani ilikuwa pia na upande wa VIP(Very important person), upande huu wa VIP ulikuwa pia ukihusisha makutano ya kibiashara hususani wafanyabiashara wa madawa ya kulevya ambao alikuwa wakitaka kuongea maswala ya kibiashara.

“Your Majest!!!”Roma alijikuta akigeuka mara baada ya kusikia sauti ambazo alikuwa akizifahamu na hii ni baada ya kuingia upande huu wa VIP akiwa ameambatana na Rose , lakini sasa Rose alijikuta akishangaa baada ya kuwaona mabwana hawa wa kizungu wakikakamaa kama vile wamemuona kiongozi mkubwa wa nchi.

The Eagles wote ni kama walikuwa wameambizana kwani kila mmoja alikuwa hapo ndani ,huku kwa wadada wakiwa na wanaume wa kibongo na kwa wanaume wakiwa na warembo wa kitanzania , Roma aliwaangalia mmoja mmoja na kugudua kuwa mtu pekee ambaye amekosekana ndani ya hilo eneo alikuwa ni Deigo na Btam.

“Bebi mbona wako hivyo”Aliuliza Roma huku akiwaangalia hawa vijana walivyobadilika ghafla.
























NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 105

Roma hakuona haja ya kumficha tena ili hali wanajeshi hawa wapo ndani ya hili eneo lakini pia Rose alikuwa ashaona namna ambavyo wanajeshi hawa wamebadilika , lakini pia aliona anasababu ya kumwambia Rose kutokana na kwamba yeye ndie aliemsadia makazi ya vijana wake hapa Tanzania pasipo kuuliza sana maswali.

“Mnaweza kuendelea na Starehe yenu vijana msinizigantie”Aliongea Roma na kuwafanya vijana hawa washushe pumzi kwani hawakuwa ni wenye kutegemea uwepo wa Roma maeneo hayo .

Ukweli ni kwamba The Eagles baada ya kufika Tanzania hawakupenda kujifungia ndani tu , walitamani pia kula bata kama binadamu wengine , na katika sheria za jeshi lao , hawakuwa pia wakizuiwa kula bata kisheria ,hivyo hawakuona tabu ya kutafuta warembo na wanaume pia, lakini sasa k katika kuchagua maeneo ya kula bata hawakutaka maeneo ambayo walidhania watagongana na Mfalme Pluto.

Na kwa kulijua hilo walianza kutafuta maeneo ya mbali na anapoishi Roma na katika tafuta yao walijikuta wakiangukia ndani ya Club B, huku wakidhania kuwa Roma hawezi kufika hayo maeneo , lakini pia walipendezwa na amsha asmha ndani ya Club hio.

“Darling ! Unamaanisha unamiliki wanajeshi?”

“Bebi Rose cha kushangaa nini sasa hapo , si kama wewe tu unavyomiliki kundi la Tembo”

“Hata kama mpenzi , lakini kumiliki wanajeshi sio jambo dogo , tena wakizungu lazima niwe na maswali”Aliongea Rose huku akiwa amemlalia Roma kwenye mapaja wakiwa wameketi kwenye masofa , huku Roma akicheza cheza na nywele za Rose.

“Unakumbuka mara yetu ya kwanza mimi na wewe kukutana?”

“Siwezi kusahau , nadhani ndio siku ya kipekee sana kwenye maisha yangu”

“Sasa ile ndio siku yangu ya kufika hapa Tanzania kupitia uwanja wa ndege wa Mwanza na mtu wa kwanza kuongea nae hapa Tanzania ni wewe”Rose alishangaa hakuwa akilijua hilo.

“Kwahio ulitokea wapi?”

“Nilitokea Uingereza”

“kwahio hawa wanaeshi [ia wametokea Uingereza”

“Sehemu waliotokea ni mbali na Uingereza , siku moja nitakupeleka”Aliongea Roma na kumfanya Rose ajinyanyue na kumkumbatia Roma.

Rose hakutaka kuuliza maswali mengi , kwani alijiambia kwa kila nafasi ambayo Roma atakuwa anamkumbuka atakuwa anaitumia vyema kufanya nae mapenzi , ili hata wasipoonana kwa muda mrefu asiwe na hamu tena.

Walifanyana kwa Zaidi ya Masaa matatu na hii ilimfanya Rose kuchoka mno na hawakutakia kubaki hapo ndani Bar, walihamia nyumbani kwa Rose na Roma hakupanga kabisa kurudi nyumbani usiku huo.

“Vipi ulimalizaje swala la Baba yako?”Aliuliza Roma uda wa asubuhi mara baada ya kupiga cha asubuhi , sasa Roma alikuwa akinywa chai kabisa kwani hakuwa na mpango wa kurudi nyumbani , alipanga aende moja kwa moja kazini.

“Kundi lake kwa sasa lipo chini yangu , nimemfilisi mali zak zote , ila kwenye kumuua nilishindwa kwani licha ya kwamba ni adui yangu , lakini pia ni baba yangu”Aliongea Rose.

“Kwahio umeamua kufanya nini?”

“Mpaka sasa ninavyoongea yupo Kisiwa cha Heligoland”

“Unamaanisha Ujerumani?”

“Ndio babe”Roma alijikuta akishangaa kwani alikuwa akikifahamu hiki kisiwa sana kwa kuwa mbali.

“Nimeamua kumpeleka huko akaanze maisha upya , sijamuachia hata shilingi licha ya kuagiza vijana wakamuweke huko”

“Ni wazo zuri pia , nadhani atazeekea huko na hatoweza kupata nafasi ya kurudi Tanzania”

“Ndio na nimehakikisha hana aina yoyote ya mawasiliano na watu wa Tanzania kwenye kundi lake”Aliongea Rose na kumfanya Roma afikirie kidogo.

“Rose najua mpaka sasa biashara yako imekuwa kubwa na ukubwa wa biashara yako ndio wingi wa maadui, unaonaje ukitumia wanajeshi wangu”

“Lakini bebi sijui hata kwasababu gani umewaleta Tanzania kwanini niwatumie?”

“Sababu ya kuwaleta Tanzania ni kutokana na kwamba kitendo cha mimi kuwa karibu na nyie kinawaweka kwenye uhatari kutokana na upande wangu wa pili ambao watu wengi hamuufahamu na nikwambie tu , mpaka sasa nina maadu kila nchi ndani ya hii dunia”Rose alishangaa.

“Yeah! Usishangae , nina maadui wengi na ndio maana nimewaingiza The Eagles ndani ya Tanzania na madhumuni makuu ni ili wanisaidie kugundua watu wabaya wanaongia(Detect) ndani ya Tanzania”

“Mpenzi sijui historia yako ya nyuma , lakini mimi nipo tayari kukabiliana na maadui zako muda wowote, ila kwa mkeo sidhani kama ataweza”

“Ndio maana nimewaleta hapa nchini, kitendo cha mimi kuona na Edna ni Dhahiri sasa maadui zangu watakuwa wanafahamu udhaifu wangu na watamtageti, hivyo napaswa kumlinda pia”

“Kwahio umewaleta kwa ajili ya Edna tu?”Aliuliza Rose kwa wivu na Roma alitabasamu na kumfinya.

“Sijawaleta kwa ajili ya Edna pekee na ndio maana nataka wakusiadie hata kuwafundisha mapigano vijana wako ili wawe na ujuzi”Aliongea Roma na Rose aliitikia.

“Nitatafuta nafasi ya kukupeleka kwenda kuonana na mkuu wa kikosi ,Diego ,ili nikutambulishe”

“Sawa Mpenzi,Kunywa chai unaachelewa la sivyo mkeo hatokupandisha cheo”

“Bebi Rose mke wangu ashanipandisha cheo tayari”

“Kweli!!”

“Yeah!Anapanga kunifungulia kampuni niiongoze”Aliongea Roma na kumfanya Rose aone Edna anampenda sana Roma maana mpaka kuwaza kumfungulia kampuni sio swala dogo.

“Kwa hio Mpenzi ukishakabidhiwa hio kampuni si utakuwa na maamuzi ya juu kabisa?”

“Ndio , ila sinampango wa kufanya kazi nitagawa majukumu kwa wasaidizi wangu , mimi kukaa ofisini , kufanya vikao na kuandaa nyaraka kutanichosha sana , ni bora unipe kazi ya kuilipua Marekani”Rose alijikuta akitabasamu.

“Bebi unaonaje nikiwa muewekezaji kwenye kampuni yako?”

“Unataka kuwekeza?”

“Ndio ukweli ni kwamba licha ya kwamba kikundi changu kinajihusisha na Madawa ya kulevya , lakini hii biashara siipendi na napanga niache kabisa , licha ya kwamba jina la kundi langu litabaki na kikosi kizima , lakini nataka niwe tofauti na makundi mengine, nataka niwekeze kwenye biashara halali niachane na uuzaji wa madawa ya kulevya , lakini licha ya kwamba nina pesa nyingi , lakini mpaka sasa nimekosa mahali sahihi pa kuziwekeza zijiongeze , ila kwasababu unakwenda kukabidhiwa kampuni nataka tuunde umoja, nitawekeza kwa siri pasipo ya mkeo kujua”Aliongea Rose.

“Kwahio unataka kuwekeza?”

“Ndio najua biashara ya burudani kwa Tanzania kwasasa haipo sana vizuri , ila kama utakuwa na mipango mizuri na kuitangaza kimataifa itaweza kukua haraka na faida kuwa kubwa , licha ya kwamba inaweza isiwe rahisi lakini naamini itatengeneza faida” Roma alitingisha kichwa na kuona ni jambo sawa tu kwa Rose kuwekeza kwenye kampuni, kwani pia hio itafanya kampuni kuimarika kwa upande wa kifedha.

“Umefikiria vizuri inaonekana mpenzi wangu baadae untakuja kuwa mfanyabiashara mkubwa”Aliongea Roma na kumfanya Rose atabasamu.

“Roma nataka siku tupigane?”

“Hahaha.. Rose najua una mafunzo ya kimapigano , lakini hata nisitumie uwezo wangu na uunganike na kikosi chako hamuuwezi kupambana na mimi”

“Hubby! Unajua ni kiumbe gani kina nguvu sana duniani?”Aliuliza Rose na Roma alitingisha mabega kwamba hajui.

“Kiumbe chenye nguvu sana duniani ni Mwanamke , Sisi kila mwezi tunableed’ lakini bado tunaonakena kuwa na nguvu , hivyo hata tukipigana siwezi kukubali unishinde kirahisi”Roma alitabasamu

“Hehe… Bebi Rose unatakiwa kujua mpenzi wako mimi sio wa kawaida , wanaume wengine wanaweza kulinda nyumba ili wezi wasiingie ndani kuiba ila mimi nahakikisha nalinda heshima yangu kitandani”

“Muone sasa ..mimi sijui hayo ila ninachojua wewe mwanaume ambaye huna aibu”Aliongea huku akimpokonya kikombe.

Ilikuwa ni siku ya jumamosi asubuhi wanafamilia wanne yaani Bi Wema , Roma ,Sophie na Edna walikuwa mezani wakijipatia chai ya asubuhi nzito ambayo iliandaliwa na Sophia na Bi Wema.

Roma alionekana asubuhi hii kufurahia kweli chai hio , kwani alikuwa akila kwa spidi kubwa mno kiasi kwamba ni kama kuna mtu aliekuwa akishindana nae kula, Edna alijikuta akimwangalia Roma namna anavyokula na kujikuta akishindwa kuvumilia.

“Roma kula taratibu bwana , unakulaje kama mbuzi”

“Kama mimi ni mbuzi wewe utakuwa majani”Edna alijikuta akimpotezea kwani aliona ishakuwa tabia ya Roma , huku Sophia na Bi Wema waliokuwa pembeni wakiangalia wanandoa hawa walivyokuwa wakiongeleshana.

Sophia kwanza alishangazwa na maisha ya Roma na Edna , kwani hakutegemea wanandoa kuishi vyumba tofauti tokea afikie hapo , kuna muda alijiuliza labda ni kutokana na kwamba kuna migogoro kati yao , lakini alikaa Zaidi ya siku mbili kwenye hio familia na Roma na Edna hawakuonekana kulala pamoja na hili halikumhuzunisha ila lilimfurahisha, lakini sasa kwa macho yake jinsi alivyokuwa akimwangalia Roma na Edna aliona kuna kitu ambacho kinaendelea kwa hawa wanandoa , kwani licha ya kwamba walionyesha hali ya kuwa mbali kihisia ila aliona muunganiko ambao unaweza kuwa mgumu kwake kuuvunja na sio kwa Sophia tu ,hata Bi Wema alishaanza kuona tabia za mabadiliko za Edna tokea Roma afike hapo ndani kwenye familia , alimuona Edna akianza kubadilisha baadhi ya tabia zake ambazo alikuwa ashaanza kuzizoea na aliona kabisa Edna alikuwa akifanya makusudi tu lakini ana mapenzi na Roma.

Wakati Roma akiwa anaendelea kula pasipo kujali macho ya Edna , Simu yake iliingia meseji kwa kutetema ndani ya mfuko wake , aliitoa na kuangalia ni nani ambaye katuma ujumbe asubuhi hio siku ya jumamosi.

“Anko Roma leo usiku nafungua biashara kwa pesa ulionikopesha unaonaje ukiwa mteja wangu wa kwanza”Ilikuwani meseji kutoka kwa Yezi na Roma leo alimkumbuka, kwani zilikuwa zimepita takribani siku tatu tokea aonanae na Yezi, alitabasamu na kisha akaweka kijiko chini na kujibu.

“Okey saa ngapi utafungua, nije niweke Baraka”

“Saa mbili kamili”

“Okey nitafika”Alijibu Roma huku akitabasamu m hakuelewa kwanini anatabasamu , sasa wakati Roma anaendelea kuchati Edna alikuwa akimwangalia muda wote na kwa jinsi ambavyo alimuona Roma anachati, alijua tu ni mwanamke na hakujua ni mwanamke yupi kati ya wale aliokuwa akiwajua.

“Bi Wema naenda kazini , nitachelewa kurudi leo nina miadi na mtu usiku”Aliongea Edna huku akinyanyika na kuchukua mkoba wake.

“Miss lakini leo ni wikiend , tukuletee chakula mchana?”Aliuliza Bi Wema huku Roma akiendelea na kunywa chai yake bila habari hakuona utofauti wowote.

“Nitakula huko huko usiniletee na usiku msinihesabu”Aliongea na kutokomea nje na ni mvumo wa gari tu uliosikika kwenye masikio ya Bi wema na Roma pamoja na Sophie.

“Bro ila una mke ana wivu”Aliongea Sophie na kumfanya Roma amuangalie kwani hakuelewa alichokuwa anamaanisha.

“Unamaanisha nini Sophie?”

“Hahaha..yaani unashangaza kwakweli , unashindajwe kujua mabadiliko ya mkeo”

“Ndio Roma sidhani kama Edna ana miadi ya kuonana na mtu siku ya leo”Aliongea Bi Wema na kumfanya Roma asielewe vizuri.

“Mkeo alikuona unavyochatika na kisimu chako cha Bei Rahisi , huku ukiwa na tabasamu nje nje , yaani Roma unakichwa kigumu sijawahi pata ona”Aliongea Sophie na kumfanya Roma aelewe , hakujua kama kitendo cha kuchati kilimfanya Edna kuwa na wivu , lakini pia alijiuliza Wivu wa Edna umeanza lini.



SEHEMU YA 106

I990-CIA HQ USA ,VIRGINIA

Ilikuwa ni siku ya asubuhi ndani ya makao makuu ya CIA ambayo yanapatikana ndani ya jimbo la Virginia sehemu inayofahamika kwa jina la Lenley.

Sasa asubuhi hii ndani ya makao makuu haya alionekana bwana mmoja hivi wa kizungu aliekuwa akiingia ndani ya hili eneo akiwa na gari yake aina ya Benz , bwana huyu baada ya kushuka kutoka kwenye gari sehemu alipopaki , alifuatwa na bwana mwingine ambaye alikuwa akilingana nae kiumri , kwa makadirio ya miaka kama therathini hivi , utofauti wao kati ya mtu alieingia hapo ndani na aliemfata ndani ya eneo hilo la Maegesho ni unene , jamaa aliengia alikuwa ni ni mnene kidogo kutokana na mwili wake kuonesha ulikuwa ni ule wa mazoezi , lakini aliemfuata eneo la maegesho ya magari alikuwa ni mwembamba na hakua akionyesha kama mtu ambaye alikuwa ni wa kuchukua mazoezi.

“Mr Carlos ! Karibu sana kwa mara nyingine ndani ya makao makuu ya CIA , Naitwa ajenti Smith”

“Asante sana Mr Smith kwa kunipokea”

“Your Welcome , nifuate Director anakusubiria”Aliongea bana huyu huku akianza kutembea kuelekea ndani ya jengo hili kubwa ambalo kila mtu aliekuwwepo hapa ndani alikuwa bize na majukumu, ni eneo ambalo lina ulinzi mkubwa sana.

Carlos alionesha hali ya kukagua sana hili eneo , kwa muonekano wake ni kama alikuwa hajafika ndani ya hili eneo kwa muda mrefu sana , kwani alionesha hali ya kushangaa mabadiliko ya miundo mbinu.

“Kuna mabadiliko makubwa ndani ya hili eneo tokea nilivyoondoka kwenda Vietnam”

“You seems to be surprised?”

“Very Much”

“Since then we made a lot of Upgrade , All thanks to Mr President”Aliongea huku akifungua mlango mwingine upande wa kulia kwenye Korido hii ndefu iliokuwa na idara nyingi, jamaa huyu alievalia suti yake nyeusi alitabasamu na kumpa ishara ya kuingia na Carlosi akaingia.

“Carlos nice to meet you again after year`s”

“Nice To meet you too Powell”

“Karibu uketi”Aliongea Director mkuu wa kitengo cha intellijensia na kisha akaketi.

“Mr Smith nadhani kazi yako ishaisha na sasa nitaendelea na Carlos”

“Thank you Director”Aliongea Smith na kisha akatoka na kuwaacha Director na Carlos.

“Carlos kwanza ni kupe hongera sana kwa kazi kubwa uliokuwa unafanya Vietnam”

“Nashukuru sana Director”

“lakini pia nikupe pole , kwani baada ya kurudi ulipaswa kuwa likizo , lakini kutokana na kuwepo wa jambo la muhimu sana ,ambalo limetokea sikuwa na jinsi ya kukurudisha kazini, nadhani unafahamu kabisa kwamba kazi hii inahitaji kujitoa”

“Ndio naelewa Mr Powell na nadhani itakuwa vizuri sana kama utaenda moja kwa moja , kwani baada ya kupokea tu simu yako nilijua kuna jambo la muhimu na kama nisngetaka kulifanya usingeniona hapa, nadhani unanifahamu”

“Ndio nakuelewa kabisa Carlos”Aliongea bwana Poweli ambaye alikuwa mnene kidogo , mwenye nyywere nyeupe ambazo ziliashiria uzee , kwa haraka haraka alionekana kuwa na miaka sitini hivi kupanda, Poweli ni moja ya wafanyakazi wenye umri mkubwa sana kuhudumu ndani ya kitengo cha kijasusi cha CIA na hakuonesha dalili yoyote ya kustaafu.

“Okey Carlos nitakuomba usome hio karatasi kwa dakika chache kabla hatujaendelea na mazungumzo”Aliongea na kisha Carlos alichukua hio katatasi na kuanza kusoma.

“Pro Human Project !!”

“Ndio Carlos , hili ndio jambo ambalo unakwenda kulifanyia kazi nchini Bolivia”Aliongea na kisha akampatia karatsi nyingine.

“Ryan Fredrin ni moja ya watu ambao utakwenda kufanya nao kazi, kutokana na hio kambi kuwa msituni ndio maana tumekupendekeza”

“Misheni yangu ni ipi?”

“Unachotakiwa ni kuzamia ndani ya hii kambi pasipo kujulikana , ukishaingia kazi yako kubwa ni kuandaa mazingira kwa kazi ambayo ataifanya Ryani”

“And Then?”

“Kama Ryan akifanikisha wajibu wake hakikisha unamchukua mtoto , nina uhakika Ryani ataungana na mke wake kumlinda mtoto wao na pia wanaweza wakawa na mpango wa kukimbia na mtoto wao , hakikisha swala hilo halitokei, ukishampata mtoto hakikisha unamuua Ryani pamoja na Epholia”Carlosi alishangaa.

“Okey naomba kuuliza Poweli , kwa jinsi nilivyosoma hapa ni kwamba project hii inahusisha watoto kumi na mbili , kwanini mnataka mtoto mmoja tu huyu wa Ryan na Epholia?”

“Kwasababu hii project mheshimiwa 41 President alikuwa akiifatilia kwa muda mrefu sana tokea ikiwa kwenye Preliminary Stage(hatua za Mwnzo) na mafanikio yake mpaka sasa ni asilimia 8.3%, nadhani mpaka hapo unaelewa kwanini tunahitaji mtoto mmoja kati ya kumi na mbili?”Carlos alitikia kwa kichwa.

“Kwanini Ryani ahusishwe kwenye hii misheni , kwani ninaweza kwenda kumchukua mtoto pekee bila msaada wowote”Alitabasamu.

“Only parent can identify their Child without mistake. Hivyo hayahitajiki makosa, hatuna picha ya kumtambua mtoto wa Ryan, lakini tuna inntellijensia ya mtoto wa Epholia na Ryan kutengeneza asilimia 8.3 za mafanikio”Carlos alimuelewa vyema Director.

“Kwanzia muda huu misheni ishaanza na maandalizi yako ya safari yapo tayari , utaingia Bolivia kama Interpool Ajent , the Resr will depend with your efficiency , una wiki mbili tu tunahitaji taarifa kutoka kwako”

“Yes sir”Aliongea Carlos na kisha akatoka ndani ya ofisi hio.

Hii ni kabla ya kulipuliwa kwa kambi iliokuwa kule La Paz ,Bolivia kwenye ,msitu wa Amazoni.

Swali:Je Carlos alifanikiwa, tukio hilo linauhusiano gani na simulizi

Utaendelea ufahamu kadri simulizi inavyoendelea.





*****

Roma alijisikia aibu kwa namna ambavyo Sophie alikuwa amemshushua , ila hakutaka kufikiria sana , siku hii ya leo alipanga kubakia nyumbani tu.

Sophie na Bi wema walionekana kuzoeana kwa muda mfupi sana kwani walikuwa wakicheka na kumfanya Roma aliekuwa amejipumzisha chumbani kwake awasikie na aliishia kutabasamu tu kwa ujanja wa Sophia , kwani Sophia kwa kumuangalia alikuwa mpole ila akizoeana na mtu anakua muongeaji sana.

Chakula cha mchana Roma alishuka na kula kama kawaida na kurudi chumbani kuangalia runinga kupoteza poteza muda .

Licha ya Roma kutojali maneno ya Sophia juu ya wivu wa Edna lakini alikuwa akikumbuka kabisa , aliona kama maneno hayo yana ukweli basi huenda Edna ashaanza kumpenda , alikaa chumbani kwa kufikiria kwa masaa kadhaa na alijikuta akipotelea usingizini .

Roma alijikuta akija kushituka saa moja moja aliingia bafuni akaswaki na kuoga na akashuka mpaka chini sebuleni.

“Bi wema Edna asharudi?”Aliuliza Roma baada ya kumkuta Bi Wema aliekuwa bize kuangalia Runinga.

“Hajarudi bado”

“Bi Wema leo usiniwekee chakula”Aliongea Roma na kisha alipandisha juu na ndani ya dakika chache tu Bi Wema alimuona Roma akishuka akiwa amebadili mavazi , hakutaka kuuliza Roma anaenda wapi ila alikisia.

Roma alingia kwenye gari yake na kutafuta namba ya Edna na kupiga.

“Unasemaje?”Ilikuwa ni sauti ya Kibabe iliomfanya Roma atabasamu na ukauzu wa mke wake.

“Uko wapi?”

“Ofisini! Kuna nini?”

“Hakuna”Aliongea Roma na kisha akakata simu na kuwasha gari na kutoka.

Baada ya masaa kadhaa tu Roma alikuwa akiingiza gari sehemu ya maegesho kwenye kampuni ya Vexto , alimuona Chiara na John waliokuwa ndani ya eneo hili na kuwapa ishara waondoke na walitingisha vichwa vyao na wakawasha gari yao na kuondoka.

Edna alikuwa bize mno yaani haikueleweka alianza kufanyakazi saa ngapi kwani muda wote alikuwa amekodolea tarakishi yake macho huku akiwa amevaa miwani ya kumkinga na mwanga wa bluu.

Upande wa nje Monica pia alikuwepo na Roma ile anafika ndani ya hili eneo alimkuta mwanadada huyu akiwa amesinzia alionekana kuchoka kweli , na alimuonea huruma , hakutaka kumuamsha , alimpita na kuingia moja kwa moja ofisini kwa mke wake.

“Umekuja kufanya nini?”

“Edna Monica kalala , nenda kamwambie aende nyumbani , unamtesa mtoto wa watu hata kama unamlipa”Aliongea Roma huku akikaa kwenye masofa na Edna alijikuta akikumbuka kuwa Monica alikuwa amekuja nae siku hio na alikuwa amesahau kwani muda wote alikuwa amejichimbia kufanya kazi pasipo kupumzika.,aliangalia saa na kisha akatoka mpaka nje na kumuamsha Monica na kumwambia aende nyumbani.

“Malizia kuna sehemu nataka unisindikize”Aliongea Roma mara baada ya Edna kurudi na Edna alishangaa.

“Wapi nina majukumu mengi Roma”

“Wife kwanini wewe kila siku ni mwenye kuwa na majukumu unafikiri wengine hawana majukumu”Aliongea Roma na kumfanya Edna afikirie kidogo.

“Okey tunaweza kwenda nitamalizia nyumbani”Aliongea Edna na kumfanya Roma atoe tabasamu la uchungu.

Dakika chche mbele Roma alikuwa akiingiza gari ndani ya Kigamboni Pongoni Beach , mwanzo Edna aliwazia huenda Roma anamrudisha nyumbani , lakini walivyochukua barabara nyingine alishangaa kidogo lakini hakutaka kuuliza alisubiria kuona mwisho wake ni wapi Roma anampeleka.

“Wife leo ni siku yetu ya ‘Date’ aliongea Roma na kisha akamshika Edna mkono na kuanza kutembea kueleka upande wa Beach na hii ni baada ya kuegesha gari upande wa pili wa barabara.

Edna alitaka ajitoe kwa Roma ila alishindwa kwani Roma alimshika vizuri na alijiona hana ujanja Zaidi ya kufuata , watu walikuwa wakiawaangalia na kuishia kutabasamu , kwani licha ya giza , urembo wa Edna haukujificha.

Roma alijikuta akitabasamu mara baada ya kuona maboresho ambayo Yezi alikuwa ameyafanya kwenye kibanda chake cha chipsi na kutokana na leo ilikuwa ni wikiend watu walikuwa wengi wakipita pita eneo hili na Yezi aliekuwa bize, alikuwa akionekana kwenye macho ya Roma kwa umbali.

Yezi alikuwa bize mno na kumfanya roma atabasamu na kufurahishwa na juhudi za Yezi.

“Anko Roma !”Aliita Yezi baada ya kumuona na kuwasogelea.

“Sister Edna!!!”Aliita Yezi kwa mshituko

“Yezi!!!”Roma alishangaaa.

ITAENDELEA

NICHEKI WATSAPP 0687151346 NIKUPE UTARATIBU WA KUPATA MWENDELEZO , UNLESS OTHERWISE TUONANE JUMAPILI
Duh
 
SEHEMU YA 107

Edna alijikuta akishindwa kujizuia na kumsogelea Yezi na kumkumbatia , huku Roma akiwaangalia , alijikuta wakati huo huo akikumbuka stori ya Yezi kutoroka kituo cha kulelea watoto .

“Yezi hivi unajua ni kwa kiasi gani tulikutafuta baada ya kutoroka kituoni”Aliongea Edna na kumfanya Yezi ashindwe kujibu na kuishia kulia kwa kwikwi.

Ukweli ni kwamba Yezi kuna kipindi maisha yalikuwa magumu sana kwake na kutamani kurudi , lakini alishindwa kutokana na namna ambavyo aliondoka , ule ujasiri wa kurudi ulimpotea kabisa.

Roma baada ya kusikia hivyo ndio alipata kujua sasa Yezi alikuwa ametoroka kituo cha kulelea Yatima cha Son And Daughter Orphanage.

“Aunt Edna Am Soryy najua wewe na Mama Issa mlikuwa na wakati mgumu baada ya mimi kuondoka”

“Sasa kama ulijua tutakuwa kwenye wakati mgumu kwanini umeondoka , unajua ni kiasi gani Mama Issa amekuwa ni mwenye kukuwazia tokea utoroke”Yezi alishindwa hata kujibu ,alijiona ni mwenye hatia .

Edna alishindwa kumgombeza Zaidi Yezi, kwani ilikuwa imepita kama mwaka mmoja tokea Yezi atoroke , aliangalia mazingira ya biashara ya Yezi na kujikuta akimuonea huruma, aliona ni maisha magumu sana Yezi alipitia ukilinganisha pia yeye ni msichana.

“Umefahamiana vipi na Yezi?”Aliuliza Edna huku akimwangalia Roma na Yezi alidakia swali hilo na kujibu kwa kuelezea tukio zima.

“Kumbe ile siku hakuwa kwa wanawake wake , nilimuwazia vibaya”Aliwaza Edna.

“But Aunt hujanieleza huyu Anko ni nani kwako?”.

“Ni Mke wangu Yezi , inaonekena kukutana kwetu kulikuwa na sababu”Aliongea Roma baada ya kuona Edna anasita sita , ila Yezi alishangaa hakujua yule dada tajiri mwenye moyo mzuri ambaye alikuwa akiwasaidia watoto Yatima pasipo kujitangaza, lakini pia mwanadada ambaye alikuwa aliekuwa amkimjua kama tajiri ukijumlisha pia na urembo wa Edna, alishangaa Roma mwanaume wa kawaida kumuoa Edna.

“Hongera Anko , Aunt Edna ni mwanamke mwenye Roho nzuri sana na nni mrembo”Aliongea Yezi na kumfanya Edna aone aibu kidogo kusifiwa ila alijisikia vizuri.

Edna alionesha furaha yake ya wazi baada ya kukutana na Yezi kwa mara nyingine tokea atoroke kwenye kituo cha Son And Daughter Ophanaage ,Yezi almwelezea Edna maisha yake yote ambayo alikuwa akifanya tokea alivyotoka kituoni huku akificha kumwambia juu ya kupelekwa polisi mara kadhaa, lakini pia kujiaunga na kundi la watoto watukutu la Sherif,Roma hakutaka kuingilia mazungumzo hayo, aliacha wawili hao waongee.

Na kwa jinsi Edna alivyokuwa akionekana , ilionesha alikuwa akimpenda sana Yezi , kwa kiasi kikubwa sana.

“Vipi kuhusu Shule?”.

“Aunt Edna ushasahau nilitoroka kabla ya majibu ya kidato cha sita kutoka?”Aliongea Yezi na kumfanya Edna akumbuke na kuona amueliza swali la kijinga.

“Matokeo yako yalikuwaje, au hukufuatilia?”

“Nilifaulu kwa division Two”

“Vipi kuhusu mpango wa kwenda chuo?”

“Nilikuwa nikifikiria kujiunga chuo , lakini nilipata ugumu kurudi kituoni kufatilia vyeti vyangu”Aliuongea Yezi na Edna aliona lazima Yezi angepata ugumu , kwani kwa namna ambavyo Yezi aliondoka, kwa mtu yoyote ingekuwa ngumu kurudi tena pasipo kuwa na hatia

Edna licha ya kuona biashara ya Yezi kuwa ndogo , lakini pia mazingira kutoyapenda alishindwa kumwambia Yezi asifanye hio biashara , alimuona Yezi ni mtu mzima tayari hivyo kumwambia kipi cha kufanya wakati huo ilikuwa umepita , alitaka Yezi afanye kile ambacho anaona ni sahihi, na yeye mwenyewe atamsaidia kimawazo tu ili afanye maamuzi sahihi , kwani kwa jinsi ambavyo Yezi alimsimulia maisha yake yalivyokuwa aliona kabisa Yezi amekuwa mtu mzima ambaye amepitia changamoto za kimaisha hivyo atakuwa tayari na ukomavu wa akili katika kufanya maamuzi yanayohusu maisha yake..

“Kwahio ndio ulikuwa ulinileta kuonana na Yezi?”

“Ndio Wife , asubuhi alinitaairifu anafungua biashara yake upya , hivyo nilitaka tukamuunge mkono kama wateja wake wa kwanza”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie , alimuona Roma kuwa na Roho nzuri.

“Nilidhania asubuhi anachati na wanawake zake , nimemuwzia vibaya kwa mara mbili mfululizo”Aliwaza Edna

“Uliwezaje kumsaidia Yezi pesa na akapokea?”

“Kwanini unauliza hivyo?”

“Humjui Yezi wewe, tokea aliuvyokuwa mdogo sheria yake ilikuwa ni moja, hakupenda kupokea msaada kabisa kutoka kwa watu hususani pesa”Roma aliona maneno ya Edna kuwa na ukweli kwa namna ambavyo Yezi alizikataa pesa zake ile siku.

“Wife hio chukulia kama siri yangu na Yezi”Aliongea Roma na kumfanya Edna avute mdomo na kupotezea.

“Nimefurahi kuonana na Yezi leo, nilitokea kumpenda sana wakati akiwa ndani ya kituo”Aliongea na wakati huu walikuwa wakirejea nyumbani baada ya kupata chakula cha usiku pamoja na Yezi.

“Mke wangu hata mimi nimeona ulivyokuwa na furaha,unaonaje ukinizawadia hata busu sasa mumeo”Aliongea Roma na kumfanya Edna akose utulivu huku akianza kukumbuka ndoto yake ya siku kadhaa zilizopita

“Nataka unisadie kumshawishi Yezi arudi shule , lakini pia umpeleke akaonane na Mama Issa kwani amekuwa ni mwenye kumuwazia sana na amekuwa akiangalia picha yake mara kwa mara na nilimuonea huruma”Aliongea akiipotezea topiki

“Mama Issa anaonekana kumpenda sana Yezi?”

“Hata kama ni wewe ungempenda, Yezi aliokotwa nje ya kituo na mama Issa akiwa mdogo sana na alimlea mwenyewe mpaka kufikia umri mkubwa ni rahisi kusema ni mtoto wake kabisa , kwanini asimuwazie”

“Sasa kwanini alitoroka?”

“Yezi baada ya kuelezwa ukweli na Mama Issa namna ambavyo aliokotwa kwenye geti la kituo alianza kubadilika na hata sisi wenyewe hatukujua nini kilimpata mpaka kuamua kutoroka , lakini hayo yashapita nataka akaonanae na Mama Issa mwenyewe na wewe utachukua jukumu la kumpeleka”

Roma hakutaka kumpinga mke wake , aliona atii maagizo.

****

Saa saba mchana siku hii hii ya Jumamosi ,ndani nya kituo cha Son And Daughter Orphanage, alionekana Mke wa Tajiri Mohamedi akishuka kwenye Gari aina ya V8 nyeusi akiwa amevalia gauni lake refu lenye rangi nyeupe na nyeusi kama pundamilia na mkoba wake rangi ya khaki.

Muda huo huo wakati Mwanamama huyu akiwa amesimama kwenye hili eneo la Maegesho alisogelewa na Mama Issa na baadhi ya viongozi wa kituo hiki na kwa jinsi walivyomsogelea ni Dhahiri kabisa walikuwa na taarifa ya ujio wa mama huyu na sasa wapo hapo kwa ajili ya kumpokea.

“Karibu sana Mrs Azizi naitwa Tabea Singano Wengi wananifahamu kwa jina la Mama Issa ni mkuu wa hiki kituo”Aliongea Mama Issa huku akipeana mkono.

“Nafurahi sana kukufahamu mama Issa , mara nyingi nilikuwa nikisikia hiki kituo, kumbe ni kikubwa hivi?”Aliongea huku akigeuza macho kulia na kushoto akiangalia majengo ya kituo hiki.

“Ndio ni kituo kikubwa sana ambacho kina kila aina ya Huduma , Karibu sana ndani ya kituo chetu , tumejisikia furaha sana kusikia ujiio wako”Aliongea Mama Issa kwa ukarimu.

Mrs Azizi alimgeukia Derava wake na kumpa ishara a kwamba watoe mizigo.

“Mama Issa nimekuja na mizigo kwa ajili ya kuwasaidia watoto , najionea hata aibu kutofika ndani ya hiki kituo tokea kuanzishwa kwake , lakini naamini utakuwa ni mwanzo mzuri wa mimi kufika mara kwa mara , nimekuwa nikitembelea vituo mbalimbali , lakini nimeshindwa kufika hapa , imekuwa ajabu kweli mpaka najishangaa”Aliongea huku akitabasamu

“Huna haja ya kuzungumza hivyo , wahenga wanasema kila jambo na wakati wake na wewe kufika mahali hapa ni muda sahihi na haujachelewa kabisa , katibu sana”

Baada ya kukaribishana Mama Issa aligawa majukumu kwa ajili ya kushushwa mizigo aliokuja nayo Mrs Azizi , na wakapiga picha ya kumbukumbu na baada ya hatua hio ya kwanza kwa kila mhisani anayefika ndani ya kituo hicho kutoa msaada , hatua inayofuatwa ni kutembezwa ndani ya kituo hiko na kukutanishwa na watoto hawa wanaolelewa , Mrs Azizi alijiambia kuwa kwenye vituo vyote vya kuelelea watoto Yatima ametembelea, hiki kituo ndio kikubwa Tanzania nzima na chenye mazingira mazuri , alifurahishwa na uwepo mpaka wa ‘Swimming pool’.

“Mke wa Raisi wa Kenya amejitahidi kwakweli nampa hongera yake, ni kituo kikubwa sana”

“Ni kweli Maina amekuwa msaada mkubwa kwa jamii nyingi za kiafrika na mimi pia nampa pongezi yake kwa hilo , kwani tokea kuanzishwa kwa kituo hiki ni watoto wengi wamesaidiwa na kwa sasa wanamafanikio makubwa”Aliongea Mama Issa huku wakaongozana mpaka ofisi ya Mama Issa ilipo kwa ajili ya kupewa maelezo ya namna utaratibu wa kituo hiko huendeshwa kama ilivyodesstuli.

Waliingia ndani ya hii ofisi ya Mama Issa , lakini ajabu ni kwamba leo ile picha ya mwanamama iliokuwa ukutani haikuwepo, kama siku ile ambapo Roma alikuja hapo kwa Mara ya kwanza, na haikueleweka kwannini ilikuwa imetolewa.

“Mrs Azizi kama nilivyosema hujachelewa kabisa na ujio wako leo ni wakati sahihi kabisa, na kukaribisha tena ndani ya kituo chetu, nilikuwa nikiusubiria ujio wako Zaidi ya miaka ishirini na hatimae umefika ,na ndio maana nasema ni wakati sahihi”Mrs Azizi hakuelewa anachomaanisha Mama Issa.

“Ni kweli ulikuwa ukinisubiria?,Mbona naona kama kuna jambo lingine kwenye macho yako Mama Issa unataka kuniambia”

“Ni kweli kabisa umepatia, kuna jambo ambalo nataka kukuambia ,ni jambo lakni pia naweza kusema ni maagizo niliopatiwa miaka ishirini iliopita”

“Maagizo, miaka ishirini iliopita!!??”Alishangaa lakini Mama Issa hakujali alinyanyuka kwenye sofa na kusogelea meza yake na akavuta mtoto wa meza na kutoa ufunguo na kisha akasogelea kabati lililokuwepo hapo ndani upande wa kushoto lenye mlango wa mbao na kisha akalifunua na kutoa bahasha za zamani sana za kuhifadhia barua na kutoka nayo.

“Hii ni barua yako niliopewa miaka ishirini iliopita , siku ya kufunguliwa kwa hiki kituo na Madam Maina”

Mke wa tajiri Mohamedi aliangalia barua hio kwa wasiwasi , alijiuliza kama barua hio ilitakiwa kumfikia yeye kwanini hakukabidhiwa mpaka leo hii, na ni kweli barua hio ilikuwa yakwake kwani hata jina lake la Jestina lilionekana pia juu ya bahasha.

“Kwanini haukunipatia hii barua mpaka imepita miaka mingi kiasi hiki?”

“Hayo ndio maagizo niliopewa , nilitakiwa kukukabidhi siku ambayo utafika ndani ya hiki kituo cha kulelea watoto ,hata mimi Madam amenishangaza kwa maagizo hayo , lakini niliamini kuna jambo kubwa ambalo lipo kwenye hio barua”Aliongea na kumfanya Mama huyu kujawa na shauku kubwa sana ya kujua nini kimeandikwa kwenye hio barua.

“Naruhusiwa kuisoma hapa hapa , au kuna maagizo mengine?”Aliongea kwa wasiwasi

“Unaweza kuisoma hapa hapa , barua hio mpaka sasa wewe ndio mmiliki”Aliongea Mama Issa, na mke wa Tajiri huyu anaefamika kwa jina la Jestina , hakutaka kusubiria hata sekunde kujua ni nini kipo kwenye hio barua, aliifungua haraka haraka na kuanza kuisoma.

Jestina kadri alivyokuwa akisoma hio barua ilimfanya atetemeke mikono huku machozi yakiujaza uso wake , mwanamama huyu alionekana kitu ambacho alikuwa akisoma kilikuwa ni cha kuhuzunisha mno.

“Blandina dada yangu…hihiii,”Mwanamama huyu alijikuta akikosa uvumilivu kabisa na kuachia kilio cha kwikwi na kumfanya Mama Issa amsogelee na kumkumbaitia huku akimpigapiga begani kwa namna ya kumfariji, ni kama mwanamama huyu alikuwa akijua kilichokuwa kikiendelea.

Mwanamama huyu alijikuta akinyamaza na kuinua tena barua na kuanza kusoma , ni kama hakuwa akiamini alichokuwa akikisoma kwenye hio barua, lakini aliishia kujishika moyo wake na kuanza kulia tena, alionekana kuwa kwenye maumivu makali.



SEHEMU YA 108

MIAKA ISHIRINI ILIOPITA.

Ilikuwa ni mchana wa siku ya jumatano , siku ya sikukuu ya Eid al-Fitr saa saba mchana alionekana Blandina akiwa ndani ya Eneo la Bagamoyo Kiwanga, hii siku ilikuwa ndio ya ufunguzi rasmi wa kituo cha kulelea watoto cha Son and Daughter orphanage, licha ya kwamba tayari kituo hiki kilikuwa tayari kishaanza kulelea , lakini ufunguzi wake rasmi haukuwa umefanyika na siku hio ya jumatano ndio sherehe ya ufunguzi ilikuwa ikifanyika rasmi na mheshimiwa Raisi Mkapa ndio aliekuwa mgeni Rasmi katika ufunguzi wa kituo hiki.

Sherehe za ufunguzi wa hiki kituo hazikudumu muda mrefu , kwani baada ya wageni walioalikwa ndani ya hili eneo kutoa shukrani kwa Blandina aliejitolea kuenga majengo hayo ya kituo, hakukua na cha Ziada na asilimia kubwa ya watu waliokuwa wamealikwa ndani ya hiki kituo walikuwa ni wafanyabiashara na wanasiasa na sherehe hizo pia ziliambatana na Harambee kubwa iliofanyika kwenye hii siku , harambee ambayo ilikuwa ni ya kuchangia maendeleo ya kituo hicho na jambo hilo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.

Baada ya Sherehe kuisha Blandina aliongozana na Mama Issa mpaka ofisini kwa ajili ya maongezi na baadhi ya maelekezo.

“Ndio narudi Kenya hivyo Rafiki yangu”Aliongea Blandina.

“Ila Blandina sikubaliani kabisa na maamuzi yako ambayo unataka kufanya , kwaninni unaificha familia yako kama upo hai?”

“Tabea ni Zaidi ya miaka mitatu sasa nimewaficha , muumuzi yangu yananiumiza lakini kwa sasa sina jinsi”

“Huna jinsi kivipi Blandina, utaishi hivyo mpaka lini kwa kujificha , ni sababu gani inakufanya ujifiche ambayo hutaki kuniambia”

“Nitakueleza rafiki yangu kila kitu siku moja , ipo sababu kubwa ya mimi kufanya haya maamuzi”

Mama Issa alimwangalia Blandina kwa huzuni , kwani licha ya kwamba alisoma na Blandina miaka ya nyuma , lakini baada ya wao kumaliza masomo yao hawakupata kuonana tena kwa miaka , mpaka siku walivyokutana kwa bahati Nairobi, wakati Mama Issa akirudi Tanzania akitokea Nchini Uswisi alipokuwa akifanya kazi ,chini ya shirika la UNICEF.

Mama Issa hakujua kabisa maisha ya nyuma ya rafiki yake Blandina na hata pale Blandina alipompa mpango wake wa kujenga kituo cha kulelea watoto nchini Tanzania na akitaka yeye akisimamie kituo hiko hakutaka kupinga kwani pia kwa wakati huo hakuwa na kazi , lakini pia alikuwa na ndoto pia za kusaidia watoto wasiojiweza na wale ambao wapo kwenye mazingira magumu , lakini licha ya pendekezo hilo kutoka kwa Blandinda, Mama Issa alimuona Blandina kama mtu ambaye alikuwa amebadilika na hata pale mwanamama huyu alipokaa chin na kumuuliza Blandina, nini kinaendelea ,na Blandina kumueleza nusu ya ukweli, alijikuta akishangaa.

Blandina alimueleza mama Issa kama familia yake ilikuwa ikijua amefariki na ajali ya ndege na hawajui kama yupo hai , lakini pia akamwambia kuwa anataka ibakie hivyo hivyo na hapa ndipo mwanamama huyu aliposhangaa na kutakakujua sababu ni nini ya kutaka watu wake wakaribu kujua hivyo ilihali alikuwa hai , lakini Blandina hakutaka kumueleza , na kumuahidi siku moja atamuambia ni kipi kilitokea mpaka yeye kutotaka kufahamika kuwa yupo hai.

“Tabea najua una maswali mengi juu ya maamuzi yangu , lakini siwezi kukuambia kwa sasa ni ipi sahabu , hii ni barua siku mdogo wangu akifika hapa kituoni kwa ajili ya kutembelea hiki kituo ambacho tumekianzisha nataka umkabidhi hii barua, na ndio siku ambayo nitakuambia kila kitu kwanini nipo kama nilivyo, Tabea naomba unitunzie hii siri”Aliongea Blandina huku akitokwa na machozi na Tabea alimuonea huruma , alijua kuna kitu kikubwa kinachoendelea kwenye maisha ya rafiki yake ambacho ni cha kuumiza na hakuwa na jinsi kukubali ombi hilo.

“Kwahio asipokuja utaishi hivyo hivyo na siri yako miaka yote?”

“Hii ndio ahadi yangu naweka leo na wewe Tabea”Aliongea na kisha ni kama alikumbuka jambo Fulani na kutoa barua nyingine mbili kwenye begi lake na kumpatia.

“Hizi ni barua za wanafamilia wangu Tabea , yoyote atakaekuja kutembelea hiki kituo mpatie barua moja kati ya hizi kutokana na jina lake , hii ndio ahadi naweka kwako , kama wasipokuja mpaka naingia kaburini basi naamini itakuwa ni majaliwa ambayo Mungu amenipangia na kama watakuja itakuwa pia ni majaliwa ,lakini pia ndio siku ambayo sitaishi kwa kujificha tena”Tabea alishangazwa na maneno yake huku akichukua barua hizo, nah ii ni siku ambayo ilikuwa ni ya ufunguzi wa hiko kituo miaka ishirini nyuma

Tabea aliiishi kwa kusubiria mwanafamilia yoyote ndani ya familia ya Tajiri Azizi waje kutembelea kituo hicho , lakini hakuna ambaye aliweza kufika kwa takribani miaka ishirini , kuna muda mwanamama alikosa uvumilivu na kutaka kwenda kukabidhi barua hizo , lakini kila akikumbuka ahadi aliokuwa amewekeana na rafiki yake alishindwa kabisa.

Kituo kilizidi kuneemeka na kuongezeka ukubwa ,kilizidi kusaidia watoto wenye uhitaji wakiwa wadogo mpaka wakati ambao walifikia umri wa kujitegemea , wahisani wa kutoa msaada walikuja ndani ya hiki kituo kwa wingi akiwemo Tajiri Marium Bibi yake na Edna lakini familia pekee ya Blandina haikuweza kufika, hata baada ya miaka ambayo Blandina mume wake anashinda kiti cha uraisi nchini Kenya hakuna familia yoyote iliowahi kufika ndani ya hiki kituo , Blandina alisubiria familia yake kufika ili ajiweke huru aache kuishi kwa kujificha , lakini waapi , Tabea na yeye aliishi kwa kusubiria familia ya Atanasi ije kutembelea kituo ili siri imtoke moyoni , lakini waapi , wanafamilia hao ni kama kuna nguvu ambayo ilikuwa ikiwafanya wasifike ndani ya hiko kituo , kwani hata magari yao yalikuwa yakipita kabisa nje ya kituo hiko.

Blandina akaishi kwa miaka Zaidi ya ishirini bila kutambulika kama yuko hai na familia yake ilikuwa ishamsahau kabisa na walishamfanyia hata matanga na kubakia kama kumbukumbu.

Blandina kuna muda alitaka kwenda kuonana na familia yake kabla ya Baba yake kuiaga dunia , alihofia sana huyu mwanamama kama baba yake atafariki kabla ya wao kuonana na kujitambulisha kwake kama yu hai , lakini ahadi yake aliojiwekea kwenye moyo wake ilikuwa na nguvu kiasi kwamba alishindwa kuchukua hatua kabisa, Dhamiri na kiapo alichojiwekea mwanamama huyu ni kama Mungu alikikubali kwa asilimia mia moja na ahadi hio ikamfunga..

Naam baada ya miaka Zaidi ya ishirini imepita na sasa ile siku ambayo Tabea alikuwa akiisubiria ilikuwa imefika na leo siku ya Jumamosi hatimae anatua siri ambayo ameitunza kwa miaka mingi kwenye kifua chake .

****

Ilikuwa ni usiku wa jumapili Saa mbili za jioni Roma alionekana ndani ya gari yake aina ya Audi maeneo ya Moroco,Roma usiku huu hakutaka kubaki kabisa nyumbani kutokana na kwamba siku nzima alikuwa tu nyumbani hakutoka , leo hii bwana huyu kwenye kichwa chake alikuwa amepanga apate sehemu ya kutuliza kichwa usiku huu, na mchana yote alikuwa akitafuta mtandaoni ni sehemu gani nzuri kwa ajili ya bata la usiku na sehemu aliokuwa amepata ilikuwa ni Maisha Basement Club , club ambayo ilikuwa ikipatikana ndani ya Makumbusho ndani ya jengo la LAPF tower.

Baada ya kuendesha kwa dakika kama kumi hivi hatimae aliingiza gari yake ndani ya hili eneo, na watu siku hii walionekana kuwa wengi sana jambo ambalo lilimfurahisha kwani hakutaka eneo tulivu , alitaka eneo ambalo litamrusha roho,Warembo kama kawaida walimuangalia Roma kwa macho ya Matamanio kwani waliona gari nzuri aliokuja nayo.

Ndani ya club hii walionekana warembo mbalimbali waliovalia nusu uchi walioo kuwa wakiingia na wale ambao walikuwa wakitoka.

Baada ya kuzama ndani kabisa ya Club hii kubwa tu ndani ya jiji la Dar aliangalia upande wa kushoto na kulia kuona ni sehemu gani kukaa , huku akisikilizia makelele ya mziki yaliokuwa hapa ndani huku watu waliokaa zaidi ya wawili kwa jinsia zote wakiendelea kuburudika.

Roma alipenda sana hili eneo kwa kusukuma muda uende kisha arudi nyumbani , leo hii hakuwa na mpango kabisa wa kuwa na mwanamke , alipanga apate bia mbili tatu na kisha aondoke.

Alichagua upande wa kulia wa hii bar , sehemu ambapo haakuwa na watu wengi sana na kisha akaketi na dakika moja tu baada ya kukaa alikuja muhudumu na Roma aliagiza Heinken na muhudumu huyu wa kiume alitabasamu na kuondoka kuleta kinywaji alichoagizwa.

Ndani ya dakika chache tu Roma alikabidhiwa kinywaji chake huku akinywa taratibu bila habari huku akichora baadhi ya watu waliokuwa wakiingia hapa ndani na ni kama kuna kitu alichokuwa akitafuta.

Sasa ile wakati anamaliza bia yake na kumuita mhudumu kwa ajili ya kumuongeza bia nyingine ,mara aliingia mwanamke Shombe Shombe wa Kiarabu ndani ya hili eneo na kufanya hali ya hewa ibadilike kwani wanaume wote waliokuwa hapa ndani walimkodolea macho kutokana na urembo wa mwanamke huyo.

Yule mwanadada ni kama alikuwa akijua ni wapi anaelekea , kwani alinyoosha moja kwa moja mpaka upande ambao yupo Roma huku akiwa na tabasamu , kwa muonekano wake ni kama alikuwa akiwaambia watu kama nina miadi na mtu, na Roma alimwangalia mrembo huyu kwa macho ya kujiuliza mbona kama anamfuata yeye na makisio yake yalikuwa ni kweli , kwani yule mrembo ambaye alikuwa amevaa kinguo kifupi cha plastiki na kufanya umbile lake alilojaaliwa nalo kuonekana vizuri kwa wanaume hawa na kuamsha matamanio yao kusogea moja kwa moja mpaka kwenye meza yake na kisha akaketi, na hakujali namna ambavyo Roma alikuwa akimwangalia.
 
SEHEMU YA 109

“Hi!”Alisalimia yule mrembo mara baada ya kumfikia Roma na Romaa alitikia huku akimwangalia huyu mwanamke kwa kumchunguza , alionekana mrembo kwenye macho ya Roma , lakini kwa jinsi ambavyo amevaa ilionesha huyu mwanamke alikuja hapo ndani kuuza , hivyo ndio namna ambavyo Roma alimuona.

“Utapendelea nini miss?”Aliuliza mhudumu ambaye alimhudumia Roma dakika kadhaa zilizopita , aliuliza kwa lugha ya Kiswahili.

“Brandy Alexanda or Alexandra” Huyu mwanadada alimjibu kwa lugha ya kingereza safi kile cha kumungunya , na kwa Roma alijjua tu huyu mwanadada kwa rafudhi yake atakuwa ameishi sana Uingereza kutokana na namna yake alivyokuwa anaongea , alikuwa akiongea kama Mzawa.

“Whaat….What!”Mhudumu alionesha hali ya kutokuwa vizuri kwenye swala zima la kuongea kingereza , kwani hakumuelewa yule mwanadada mrembo.

“Amesema leta bia yoyote yenye chapa ya Alexanda au Alexardra”Alirekebisha Roma kwa Kiswahili na Mhudumu alimshukuru Roma kwa kumsaidia maana alikuwa akitoka jasho.

Ndani ya sekunde chache tu Mhudumu alirudi akiwa ameshikilia ‘cocoa colored cocktail’ na kumpatia huyu mwanadada na akapokea na akamgeukia Roma na kumpa tabasamu mwanana.

“Sorry about that, I’ve been overseas for the last few years, so I don’t know how to call for drinks in this country. However, not many people know the name Alexandra, looks like Mister is well-educated when it comes to drinks.”

“Samahani juu kilichotokea , nilikuwa nje ya nchi kwa miaka mingi kidogo hivyo sijui namna ya kuagiza kinywaji ndani ya hili taifa, Hatahivyo sio watu wengi ambao wanajua kutamka Alexandra ,Inaonyesha Mr umeelimika kidogo likija swala la Vinywaji?”Aliongea Mrembo huyu kwa kingereza safi na kumfanya Roma Atabasamu , alipendezwa na namna mrembo huyu alivyokuwa akiongea na alikumbuka mbali.

“To commemorate the King of Britain Edward the 7th and Queen Alexandra’s marriage, that cocktail was made as a present for the queen. Many women like the taste of that drink. If a man has the heart to understand women, then for a man to know all this is nothing special.”

“Kuadhimisha ndoa ya Mfalme wa Uingereza Edward wa 7 na Malkia Alexandra, kinywaji hiko ilitengenezwa kama zawadi kwa malkia. Wanawake wengi wanapenda ladha ya kinywaji hicho. Ikiwa mwanamume ana moyo wa kuelewa wanawake, basi kwa mwanamume kujua haya yote sio kitu cha kipekee sana”Aliongea Roma huku akiinua chupa yake na kugonga Chears

“But amongst the men who entered this place, you’re the only man who didn’t go looking for a woman.”

“Lakini kati ya wanaume walioingia mahali hapa, wewe ndiye mwanaume wa pekee ambaye hauna mwanamke.”Aliongea huyu mrembo na kumfanya Roma azungushe kichwa kuangalia watu waliokuwa hapa ndani na kuona ni kweli yeye pekee ndio aliekuwa yupo peke yake na hii ilimfanya kujua ni kwannini huyu mrembo alikuja moja kwa moja mpaka kwenye meza yake.

“Even if I didn’t look, didn’t you come over?”

“Sijaenda kutafuta lakini si tayari umekuja?”Aliongea Roma huku akitabasamu na mwanadada huyu alitabasamu pia na kisha akanyoosha mkono wake.

“Naitwa Amina”Roma alijikuta akitabasamu na kwa jinsi alivyomuona huyu mwanamke alijikuta akivutiwa nae na ule mpango wake aliokuwa nao wa kutotafuta mwanamke usiku huu aliutupilia mbali na kujiambia huyu mwanamke usiku huu hamuachi , anafaa kwa matumizi ya usiku huo.

“What a unique introduction.Naitwa Roma Ramoni”

“Your introduction is even more special, but at least it’s much more interesting than other men I met this night, Congratulations, you’ve aroused my interes”

Utambulisho wako pia unaonekana kuwa wa kipekee Zaidi na angalau unavutia kuliko wa wanaume wote ambao nimeweza kukutana nao usiku huu , Hongera umeyaamsha matamanio yangu”Aliongea huyu mrembo kwa namna ya kutongoza flani hivi

“What interest?, You want to know my body is made of? If you’re willing to trade at an equal price, perhaps we can reach a mutual understanding”

“Matamanio gani?,Unataka kujua mwili wangu umeumbwaje , kama upo tayari kuniuzia kwa bei ya kawaida , huenda tukafikia maelewano”Aliongea Roma ila mrembo huyu hakukasirika.

“I suspect that such words may not be from the true you, and that’s what sparked my interest. To simply put, I wanted to see if the man in front of me could meet the requirements to be my intimate male companion.”

“Amina ,the truth in this world doesn’t exist, if you’re willing to, I feel that you should make a judgement based on the sharp intuition you ladies have”

“Amina, neno ukweli katika ulimwengu huu halipo, ikiwa uko tayari, nahisi unapaswa kutoa uamuzi kulingana na hisia za kimaamuzi ambazo mnazo nyie wanawake”Kwa jinsi Roma alivyomuona huyu mrembo ni Dhahiri kabisa alikuwa hapa ndani kwa ajili ya kutafuta mwanaume , lakini anashindwa kuongea moja kwa moja.

“Could you explain? I don’t really understand what you mean, Mr. Roma.”

Roma kwanza alitabasamu hakuelewa ni kii huyu mrembo hakuwa akielewa mpaka kufikia hatua hio , aliona ni kama alikuwa akijifanyisha tu.

“Amina! Unajua ni nani aliegundua Redio?”

“Mtu yoyyote aliesoma lazima atakuambia ni Marconi”Alijibu lakini mrembo huyu alimuona Roma kama mtu ambaye hakukubaliana na jibu.

“Kwahio unamaanisha nimekosea?”

“Kulingana na nchi nyingi za magharibi, ni kweli Marconi ndiye aliyevumbua redio. lakini, katika vitabu vya kiada vya Urusi ya Kisoviet ya Zamani , ilikuwa ni Popov; huko Ujerumani, ni Hertz; Bara la Amerika, ni Dreyfus. Ili kukurahisishia tu, Popov wa Urusi alikuwa amefanikiwa kutafiti teknolojia ya redio miaka kadhaa kabla ya Marconi, lakini kwa sababu alihitaji ufadhili wa kiasi cha rubles(hela ya Urusi) 1000, jeshi la Urusi lilikataa moja kwa moja uvumbuzi wake. Na baada ya miaka Kadhaa mbele Marconi alipokea Tuzo ya Nobel Prize baada ya kutangaza kugundua Redio”

“Roma ingawa sijui maneno unayoyasema ni kweli au La , ila hakuna mwanaume ambaye nishawahi kukutana nae anaongea kwa Swaga kama wewe”Aliongea huku akimkonyeza Roma na Roma alitabasamu.

“Kwahio vipi sasa , unakubali au?”

“Congratulations, tonight I’m yours.”

“Hehe..Happy to serve you”Aliongea Roma na kujiona mshindi baada ya kufanikiwa kupata hio pisi na aliona usiku wake unakwenda kuwa wa maana sana.

Wakati sasa Roma anamalizia bia yake ili aondoke na mrembo Amina akajivinjari nae usiku , waliingia wanaume wanne ndani ya hii Bara huku wakiangalia kulia na kushoto na ile wanaangalia mbele waliona walichokuwa wanakitafuta na kusogea kwa spidi mpaka kwenye meza aliokaa Roma.

“Amina Bosi ametuagiza urudi nyumbani sasa hivi na tupo hapa kwa ajili ya kukuchukua”Aliongea mwanaume mmoja hivi mwenye mwili wa mazoezi na alionekana kama bodigadi, alievalia suruali nyeusi cchini kama za jeshi na tisheni ya kubana kifua chake , alikuwa amevimba kifua kwa mazoezi makali.

Mrembo huyu aliwaangalia mabaunsa hawa huku akiwa amejawa na wasiwasi kwenye macho yake na kisha akamgeukia Roma.

“Mr Roma utanicha niondoke na hawa watu au utanitoa mahali hapa ukaufurahie urembo wangu usiku kucha?”Aliongea kwa kingereza chake na Roma akaweka chupa ya bia yake chini na kisha akatoa kiasi cha pesa kwa bia aliokuwa ametumia mrembo huyu na ya kwake na kuweka mezani na kuzuia na chupa na kisha akatabasamu, alijiambia ni mwanaume mjinga pekee anaeweza kuacha mrembo kama huyo aliejirengesha kwake.

“If Miss Amina can bless me with a kiss, I believe tonight we would have such a great time that it would be remembered for a lifetime”

Aliongea Roma na Amina alionekana kuwa romantic kweli kwani alimsogelea Roma na kumbusu shavuni na kumfanya Bodigadi yule kupandwa na hasira na kumsogelea Roma huku akidhamiria kumtoa Amina, lakini Amina hakujua namna ambavyo alibadilsihwa upande na Roma.

“Wewe mpuuzi unakitaka kifo”Aliongea lile baunsa na kurusha ngumi kuelekea usoni kwa Roma , lakini ni kama Roma alimtegemea , kwani ile inamfikia usawa wa uso, alidaka mkono wake sehemu ya muunganiko wa kiganja na mkono na kabla bwana yule hajarusha teke Roma alimkunja kwa nguvu kiganja cha mkono wake na kukipindisha kueleka upande mwingine na kumfanya baunsa atoe ukulele.

Mrembo Amina alijikuwa akishangazwa na tukio hilo , Wale wengine baada ya kuona mwenzao ameshikiliwa kwa namna ile na kutoa ukulele walisogea kwa kasi kwa ajili ya kumchangia Roma, lakini kabla hawajamfikia , Roma alimyanyua kwa nguvu yule Baunsa na kuwarushia wale na kuwafanya wote wadondoke nae huku kuvunjika kwa viti hapa ndani kukisambaa na kufanya watu waanze kusogea.

Roma hakutaka kuleta vurugu Zaidi ,alijua walinzi watakuja muda si mrefu , alimshika Amina mkono na kuwakwepa wale mabaunsa na kutoka nje haraka huku watu wakiwashangaa , lakini wakimshangaa Zaidi Roma kwani kwa namna ambavyo alimrusha yule bodigadi ni kama mpira.

“You belong to me, and not the other way around. Obediently stay in your seat and buckle up, don’t delay what’s important”Aliongea Roma kwa kumuamrisha Amina na kisha akaliwasha gari.

Mabaunsa yalinyanyuka harakaharaka na kukimbilia nje , lakini walikuwa wamechelewa kwani ile wanatoka gari ilikuwa ikitokomea barabarani upande wa Moroco , waliifukuzia na Roma aliwaona kwenye kioo namna ambavyo wanakuja na akatabasamu , alichukua barabara ya Magomeni na ndani ya dakika chache tu aliwaacha mbali sana baada ya kufika makutano ya barabara ya Karume na Kariakoo , aliendelea kuendesha gari huku mrembo huyu akimshangaa Roma na kuzidi kuvutiwa , alionesha kupenda wanaume wenye nguvu.

Roma baada ya kuendesha gati kwa madakika kadhaa alikuwa akiingia daraja la kuingia kigamboni , alilipia ushuru na kupita na alikuwa na mpango wa kutafuta Hoteli , Kwa jinsi alivyomuona mrembo huyu , aliona hapaswi kuchukua hoteli ya kawaida , kuna Hoteli aliokuwa akiikumbuka iliokuwa karibu na Nyumba ya Rose ,ndio alipanga kwenda ndani ya hoteli hio.

Dakika chache mbele alikuwa ndani ya Cloud Hotel , ilikuwa ni hoteli nzuri ya kisasa ambayo ilikuwa ikivutia kwa kiasi kikubwa , Roma alibenjua mkebe wa Gari na kutoa hela za Dola alizokuwa amehifadhi na kisha alifungua mlango na wakatoka baada ya kuegesha gari sehemu maalumu.

Roma baada ya kukabidhiwa chumba chao na kuingia ndani alijikuta akipandwa na mzuka hatari , kiasi kwamba huyu mrembo alijikuta akishindwa kujizuia na kucheka

“There’s no need to be in such a rush, right? It’s not like I’m going to run away tonight.”

“Haina haja ya kuwa na haraka sana , sio kama nitakukimbia usiku huu “

“You demoness, isn’t this fire caused by you?”Aliongea Roma huku akimkumbatia kwa nyuma.

Moto ulionekana kuwapanda kweli , ila kwa Roma aligundua ugeni kwa huyu mrembo hakujua kwanini mrembo aneonekana kutokuwawa mzoefu hivi hakuwa mtundu kwenye mapenzi.

Baada ya kuvuana nguo , alimbeba juu juu na kisha akaelekea nae bafuni na umtumbukiza kwenye ‘bath tub’ na Roma akafuatia, na ndani ya madakika walikuwa kwenye kitanda hiki kikubwa cha sita kwa sita

“Wewe ni bikra?”Aliuliza Roma baada ya kuona ugumu.

“Endelea tu usijali sana Mr Roma”Aliongea Mrembo huyu na Roma hakujali , alijiambia si umetaka mwenyewe ngoja ni kuoneshe.

Ilikuwa ni muda wa Asubuhi ,Roma akiwa amelala wakiwa wamekumbatiana na mrembo Amina , Mara mlango wao uligongwa kwa nguvu kiasi cha kumfanya Roma ashituke na kupandwa na hasira na kujiuliza mpuuzi gani huyo anagonga mlango namna hio.

“Wewe Mbakaji Fungua , Utaozea jela nakuambia”Ilisikika sauti ya kibabe nje na kumfanya Roma aone wanaogonga hawana heri , Amina alikuwa ashaamka na yeye na Roma alimgeukia na kumwangalia na Amina akamtingishia Mabega kuashiria haujui kinachoendelea na Roma alijifunga taulo na kuusogelea mlango.

Unajua nini kitarokea

ITAENDELEA.
 
Yaaani ni kama picha ndio kwanza linaanza...daaah niko pale j5 nimekaa seat ya mbele.
 
Yaaani ni kama picha ndio kwanza linaanza...daaah niko pale j5 nimekaa seat ya mbele.
Hadithi nzuri sana ila unavuta sana mkuu.eneo moja linachukua pakubwa sana.kwa mfano leo hujatundea haki kwa kweli.
 
Back
Top Bottom