Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 94.

Roma ndio aliekuwa dereva usiku huu huku mke wake Edna aliekuwa amependeza akiwa amekaa pembeni ,Edna akiwa amevalia gauni la rangi nyeupe lenye maua kama michirizi huku kiunoni akafunga na mkanda wa rangi nyekundu, alikuwa amependeza , Roma nae mavazi yake yalikuwa ni suti kama kawaida na shati rangi ya bluu bila tai.

Roma aliendesha kwa maelekezo ya Edna mpaka wakaja kusimama kwenye jumba moja la Kifahari kubwa tu , na kwa kuangalia tu ndani ya eneo hili la Masaki huenda hilo jumba ndio ambalo ni kubwa sana kuliko nyumba zote ambazo wanaishi matajiri ndani ya huu mtaa.

Wakati Roma anasubiria geti la jumba hili kufunguliwa baada ya kupiga honi , nyuma yake aliona gari nyingine ya kifahari na ilionekana na yenyewe ilikuwa ikitaka kuingia ndani ya jumba hili , ilikuwa ni gari aina ya Porsche.

Geti lilifunguliwa taratibu na Roma aliingiza gari ndani ya jumba hili ambalo lilimshangaza sana Roma kwa madhanri ya hapo ndani , alipaki gari baada ya kuonyeshwa sehemu na mfanyakazi ambaye alionekana kama mlinzi na akaegesha gari yake , sehemu hii ilikuwa na magari mengi ambayo yapo ndani ya hili eneo , na jambo hili kwa harakaharaka lilimfanya Roma kugundua leo ndani ya hili jumba huenda kuna sherehe inayoendelea na sio kama alivyosema Edna kama anakuja tu kuonana na familia yenye nguvu ndani ya Tanzania.

Baada ya kugesha alishuka na kumfungulia Edna mlango na wakati huo huo ile gari iliokuwa nyuma yake pia ilikuwa eneo hilo la Maegesho na ile Roma na Edna wanapiga hatua kama mbili ,Dereva aliekuwa akiendesha gari hio alitoka na Wote Roma na Edna walimtambua , alikuwa ni Nadia Alfonso.

“Nadia alilazimisha tabasamu baada ya kuwaona Edna na Roma ambao kwa jinsi walivyokuwa wakionekana walidhihirisha uhusiano wao , yaani mume na mke.

“Mmependezana Edna”Aliongea Nadia baada ya kuwasogela na Edna alitabasamu na kumangalia Roma.

“Asante Nadia na wewe umependeza”Aliongea Edna huku Roma akimwangalia Nadia bila ya kuongea na Nadia alimwangalia Roma usoni ni kama alikuwa akisubiria Roma amsifie ila Roma hakufanya hivyo , alionekena akikumbuka baadhi ya mambo.

“Mr Roma hatujaonana tokea urudi Japani Hongera kwa kukamilisha jambo kubwa kwa kampuni”

“Asante sana Nadia , yote nimefanya tu kwa ajili ya mke wangu kipenzi”aliongea Roma huku akitabasamu na kumkonyeza Edna alietabasamu , ila kwa Nadia hakuonesha kufurahi kwa namna Roma anavyomwangalia Edna Zaidi ya kuweka abasamu bandia usoni.

Waliongozwa na mfanyakazi wa kike na kuzunguka upande wa pili wa jumba hili , hawakuingia ndani kama Roma alivyotegemea , Roma aliendelea kuangalia mandhari yakuvutia ya jumba hili.

“Nadia ,Edna karibuni”Aliongea mwanamama mmoja hivi maji ya kunde mtu mzima , makadirio ya miaka kama Arobaini na tano hivi , mwanamama huyu baada ya kuwasogelea macho yote yalikuwa kwa Roma , alimwangalia Roma kama vile alikuwa akimfananisha nah aa Roma alitambua hilo.

“Asante Mrs Mohamed”Alijibu Nadia na wakapeana mikono , alikuwa ni mwanamama ambaye alionekana mkarimu kwa jinsi alivyokuwa ameweka tabasamu usoni mwake.

“Mrs Mohamed huyu ni ndio mume wangu , anafahamika kwa jina la Roma Ramonni ,Roma huyu ni Mke wa Mohamedi tulikutana nae kwenye kusanyiko”Aliongea Edna akimtambulisha Roma.

“Unamaaisha huyu ndio mke wa yule tajiri Azizi?”

“Ndio Mr Roma naitwa Mama Nusra ,hongera kwa kupata mke mzuri kama Edna , Edna hongera nimefurahi kukutana na Mr Roma, Azizi alikuwa akiniambia kuhusu mumeo na nilitamani sana kumuona”Aliongea Mama huyu kwa furaha na kumfanya Nadia aliekuwa pembeni kuchukizwa na sifa za Mama Nusra.

“Nafurahi pia kukufahamu mama Nusra unaonekana kuwa mkarimu kweli na sikudhania Azizi atakuwa na mke kama wewe”Aliongea na kumfanya mwanamama huyu amwangalie usonni na kutabasamu.

“Ulidhania atakuwa na mke wa aina gani?”.

“Hehe..kwa anavyonekana ana hela ila Swaga hana hata mimi nimemzidi, kwanza anacheka kichafu na nilijua hatokuwa na mwanamke mrembo kama wewe ,Eti Mama Nusra umempendea nini yule mzee au ni kwasababu anapesa,”

Aliongea Roma na kumfanya Edna amfinye, maana aliona Roma anaanza kuongea ujinga lakini kwa Mama Nusra alijikuta akicheka , alionekana kujisikia vizuri sana kusifiwa kwa aina ya tofauti na Roma

Basi Edna na Roma waliongozwa mpaka upande wa Swimming Pooll , sehemu ambayo ilikuwa imepambwa , kulionekana kulikuwa na sherehe iliokuwa ikiendelea hapa ndani , kwani pia kulikuwepo na wageni japo hawakua wengi sana.

“Mr Roma.. hahahaha..tunaonana tena”Aliongea Tajiri Mohamedi , alionekana kufurahi sana kama kawaida yake na cheko lake.

“Sema Mzee unajua kucheka kichafu ,Mkeo anaweza kuingia kwenye kumi bora ya wanawake wenye huruma ndani ya Tanzania .. Anyway mimi na mke wangu tunafurahi kukutana kwa mara nyingine”Aliongea Roma na Tajiri huyu alichukulia maneno ya Roma kama sifa na alicheka tena.

“Edna kwa jinsi ulivyomzuri nilikuwa nikitegemea ,utatafuta mwanaume matawi ya juu , sikudhania utakuja kuangukia kwa mwanaume mbeba mizigo,Asie na pesa”Aliongea Tajiri Azizi na Roma alitabasamu aliona huyu mzee anamlipizia.

Wakati wakiwa wanaongea na Tajiri Azizi mara kuna mwanamke mremfu mrembo mno, mtu mzima aliwasogelea, Roma na uwezo wake wa kujua watu alijua kabisa mwanamke huyu hakuwa mtanzania.Edna alionesha kutomfahamu huyu mwanamke.

“Edna kutana na ‘First Lady’ kutoka Rwanda , Mke wa mheshimiwa Jeremy”aliongea Azizi na mwanamama huyu akaachia tabasamu na kumwangalia Edna huku akimpa mkono wa salamu.

“Nafurahi kukufahamu hakika ni kama watu wanavyokusigia , umrembo sana”Aliongea mwanamama huyu kwa kingereza na Edna alitabasamu.

“Nimefurahi pia kukutana na First lady kutoka Rwanda”Aliuongea Edna huku akiwa ametabasamu ,ila kwa Roma kuna kitu alikuwa akikiangalia kwenye uso wa huyu mwanamke , kitu ambacho mtu ambaye ni wa kawaida hawezi kukigundua , Roma aligundua huyu mwanamke anaefahamika kwa jina la ‘First lady’ hakuwa na tabasamu la dhati ni kama alikuwa akifosi na haikueleweka ni kwa namna gani aligundua.

Roma aligundua sherehe hii ilikuwa ni ya kumpongeza mtoto wa kiume wa tajiri Azizi aliekuwa amemaliza masomo yake ya ngazi ya Uzamili kutoka chuo cha Cambridge maana kulikuwa na maandishi juu ya jukwaa yalionakshiwa kwa maneno ya pongezi.

Baada ya kusalimiana na baadhi ya watu ambao wamealikwa hapa ndani , walionyeshwa meza yao ya kuketi huku wakiletewa vinywaji.

Meza aliokuwa amekaa Roma ilikuwa na jumla ya watu watatu , yaani yeye na Edna pamoja na Nadia, Edna na Nadia walionekana kuongea huku Roma akikagua mandhari ya hili eneo ni kama alikuwa akichunguza kila mtu aliekuwepo na ambaye alikuwa akiingia hapa ndani.

“Edna habari za siku”Ilikuw ani sauti iliowafanya Edna na Nadia waliokuwa wakiongea wainue macho yao na kumwangalia ni nani aliekuwa akiwasalimia na hata kwa Roma pia aligeuza shingo yake na kuangalia upande wa mtu aliesalimia.

“Denisi..!! ,Ni nzuri habari”Aliongea Edna , alikuwa ni Denisi mtoto wa raisi Senga, hata Roma alimkumbuka huyu bwana na tena alikumbuka kipindi wanaenda ikulu na Edna kuna jambo aliweza kuligundua kwenye uso wa Denisi.

“Salama kabisa , Umezidi kuwa mrembo Edna”Aliongea Denisi na leo hii alionekana kuchangamka kuliko ilivyokuwa kipindi c ha nyuma wakati Edna na Roma wapo ikulu.

Nadia alikuwa akimwangalia Denisi na Edna ni kama kuna jambo alikuwa akitafuta baina ya wawili hao , aliona wawili hawa walionekana kufahamiana kwa muda mrefu kidogo japo hakujua ni kivipi , hata kwa Roma alijua mke wake anaonekana kufahamiana na Denisi kwa muda mrefu.

Denisi p alionekana kufanya makusudi yaani licha ya kwamba Roma alikuwepo hapo kwenye Meza ila hakumsalimia na Roma hakujali ila alikerwa na namna ambavyo Denisi alikuwa akimwangalia Edna na pia namna ambavyo amemsifia ,Denisi alimwangalia Edna kwa macho ya kumtamani kabisa , licha ya kwamba wawili hawa wanaonekana kupishana umri kwani Denisi bado alikuwa mdogo kwa Edna.

Wakati Roma akiangalia namna ambayo Denisi akiongea na Edna mara alijikuta akizibwa uso na mikono laini na harakaharaka aligundua aliemziba ni mwanamke , ila alishindwa kung`amua mwanamke huyo ni nani.

“Ukinifahamu nakuachia”Ilimnong`oneza sauti masikioni na Roma alijikuta akikumbuka sauti hio lakini alishindwa kujua ni wapi aliisikia.

“Kwahio nisipokukumbuika utaendelea kuniziba hivihivi mpaka sherehe iishe”Aliongea Roma na aliemziba macho alimwachia na Roma hapo ndipo alipogeuka na kumuona msichana mrembo mwenye haiba ya utoto aliekuwa amemziba macho yake , alikuwa ni Donyi.

“Mungu wako hajajibu maombi yako tumekutana tena”Aliongea Donyi huku akivuta kiti na kuketi , alikuwa amependeza mno usiku huu.

Edna aliekuwa akiongea na Denisi alishuhudia tukio lote ,Roma kuzibwa macho na mwanamke mrembo ambaye alikuwa akimkumbuka vyema kwa kitendo cha kumkubatia Roma wakati wakiwa ndani ya jengo la My World Fashion Mall.

“Donyi Donyi unafanya nini hapa?”Aliuliza Roma.

“Na wewe unafanya nini hapa?”

“Wakubwa zako wakiuliza maswali jibu ,acha kuuliza maswali”Aliongea Roma akimfinya Donyi puani na kumfanya mwanadada huyu ampige Roma na kijibegi chake alionesha kutopenda Roma alichomfanyia.

“Unaniona kama mtoto?”

“Sio nakuoan kama mtoto , wewe ni mtoto na nikikukadiria unamiaka kumi na nane na umevunja ungo juzi tu”

“Looohh! Umekosea babu ,nina kumi na tisa”Aliongea Donyi na alionekana kumzoea kweli Roma kwa haraka , jambo ambalo lilimshangaza hata Nadia aliekuwa akiwaangalia.

“Hivi Anko jina lako unaitwa nani?”

“Naitwa Anko”Wakati Roma na Donyi wakiendelea kujibizana Sherehe ilianza na ni kama Roma alivyodhania , ilikuwa ni sherehe ya kumpongeza kijana wa kiume mkubwa wa Tajiri Azizi aliekuwa akifahamika kwa jina la Kassimu, lakini pia kulikuwa na tukio lingine la kumpongeza Mzee Atanasi, ambaye ametimiza miaka mia moja , Roma alishangazwa na jambo hili , licha ya kwamba Babu ambaye alipandihswa kwenye steji kuonekana mzee , lakini alikuwa ni mwenye afya yake nzuri..

Mzee Azizi alimpongeza kijana wake huku akiweka wazi kama mrithi wa mali zake, watu walimpongeza Atanasi na kwa jinsi kijana huyu alivyoonekana, alikuwa ni vijjana ambao walionekana kujiamini.

Kuna jambo ambalo Roma hakuelewa ila alipanga kumuuliza Edna wakati wa kurejea nyumbani.

Roma kwenye sherehe hii alipenda tukio moja tu na hilo lilikuwa ni muda wa chakula , yeye mambo mengine kwake hayakumvutia tofauti na Edna alieonekana kufurahi kuongea na baadhi ya wageni ambao walikuwa ni wafanya biashara wenzake.

Roma alikuwa ni kama mlinzi muda wote alikuwa akiangalia usalama wa Edna , licha ya kwamba alikuwa mita kadhaa tokea alipokuwa amesimama mke wake , lakini aliweza kugundua ni nani aliekuwa akimwangalia kwa macho mabaya Edna na aliweza kupata watu wawili ambao walikuwa wakimwangalia Edna kwa macho ambayo hakuyaelewa , wa kwanza alikuwa ni Denisi , huyu alionesha hali flani ya kimatamanio kwa Edna na kwa Roma alimuona Denisi kama mtu ambaye alikuwa ana mpango na Edna na hakuonesha kuheshimu Edna kama mwanamke ambaye ana mume , jambo ambalo kwake sio kama hakupenda wanaume kumwangalia Edna kwa macho ya kumtamani , alikua akijuwa mke wake ni mrembo hivyo kukodolewa macho na wanaume ni jambo la kawaida , ila macho ya Denisi yalizidi ila hakutaka kufanya lolote kwea wakati huo, aliona kuna siku lazima ambananishe tu.

Mtu mwingine aliekuwa akimwangalia Edna alikuwa ni mke wa Raisi Jeremy , alietambulishwa kwake kama First Lady huyu mwanamama Roma alimuona kama mtu ambaye hakuwa akimwangalia Edna kwa namna ya kumtakia mema , alimuangalia kwa namna flani hivi ambayo mwenyewe alitafsiri kama mtu mwenye kinyongo.

Wakati Roma akiwa ameshikilia wine yake, mara alikuja kushituliwa na mke wa Tajiri Azizi yaani Mama Nusra.

“Mr Roma kuna mtu nataka uonane nae ,nadhani hautojali nikikuiba kwa dakika”Aliongea mwanamama huyu na Roma alitingisha kichwa na kuongozana na Mama Nusra.

Waliingia ndani ya jumba hili kubwa ambalo kwa ndani lilikuwa likipendeza Zaidi ya nje ,kutokana na thamani za hali ya juu zilizokuwa zimetumika kama mapambo.

Aliongozwa mpaka kwenye chumba ambacho Roma aligundua kuwa chumba hiki sio sebule bali ni kama chumba cha kulala.

“Karibu Mr Roma”Roma alikaribishwa na Mama Nusra ndani ya chumba hiki ambacho kilikuwa ni Chumba kilichokuwa kinajitegemea , kwani kilikuwa na sebule kwa ndani ndogo na meza ya kusomea iliokuwa na tarakishi ya kampuni ya Dell, Roma macho yake yalipita harakaharaka kukagua chumba kizima na hapa ndipo alipoweza kuona picha kubwa iliotundikwa ukutani , picha hii ilikuwa ni ya Mzee Atanasi na Raisi wa kwanza wa Tanzania Julius Kambarage nyerere na wanaume wawili ambao Roma hakuwafahamu , ilikuwa ni picha ya pamoja mabayo kwa kuiangalia tu, ungegundua watu waliokuwa kwenye picha hio walionekana kuwa marafiki kutokana na mkao wao , walikuwa wameangaliana huku wakicheka.

NITARUDI WIKIEND JMOSI SAA 3 KAMILI USIKU

SIMULIZI INAENDELEA GRUPU NA WATSAPP INBOX KWA SPIDI YA 4G UNACHOPASWA KUFANYA NI KUCHIGIA KIASI KISICHOPUNGUA 2500 ILI NIKUUNGE A GRUPU , UKITAKA INBOX TU SPECIL BILA KUUNGWA GRUPU NI 3000.


NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
 
SEHEMU YA 113

Roma ilibidi amtoe Amina kwenye kifua chake kwani aliona mwanadada huyu ni kama anataka kumng`ata sasa lipsi za midomo yake ,Fayezi na mzee Kanani ni kama hawakuwa wakiamini kile ambacho kilikuwa kinatokea , waliona mpaka kufikia hatua hio jambo lishakuwa gumu , Fayezi aliwaangalia wawili hawa na hata ile hali aliokuwa nayo ilimpotea kwenye macho yake .

“Mr Rma nadhani mpaka kufikia hapo , unaonesha haupo tayari kushirikiana na sisi juu ya hili jambo?”Aliuliza Fayez.

“Sio kwamba sitaki kutoa ushirikiano , lakini huwa mara nyingi sina tabia ya kumuangalia mtu machoni na kuongea uongo hususani kwenye swala zito kama hili ,Mtu anahitajika kufahamika katika jamii kwa sifa nzuri lakini wakati huo huo mtu anapaswa kutofautisha kati ya aibu na heshima, Amina ni mwanamke ambaye ametoa usichana wake hivyo hili sio swala la kutaka kuzimwa na pesa na kuchukuliwa kirahisi , wewe ni mwanaume unatakiwa kuelewa kanuni za maisha ndogo ndogo kama hizi”

“Kama ningekuwa simpendi Amina nisingeweka juhudi kuzuia jambo ambalo amefanya na kulisahau hili jambo katika kichwa changu na kutaka kuendelea nae”

“Haha..Unajidanganya Fayezi kwanini unataka kuficha ,Unataka katangazia watu kwamba hili jambo halijatokea wakati kila kitu kimetendeka , ulichofanya wewe ni kumsafisha kwenye macho ya watu wengi, ilihali wewe mwenyewe unakubali kwamba alitenda hili jambo , kama kweli unampenda usingeficha chochote bali ungekubali kama amefanya lakini licha ya kufanya kwake umeamua kumkubali hivyo hivyo kama binadamu asiekamilika, hayo ndio mapenzi ya dhati , ila kwa ulichofanya mimi nakuona kama mwanaume unaempenda Amina kutokana na uzuri wake wa nje tu , lakini sio kila kitu kuhusu yeye”Mrembo Amina alijikuta akiguswa na maneno ya Roma.

“Roma kwa jinsi unavyo ongea unanifanya nikupende Zaidi na tukafanye tena”Aliongea Amina pasipo kumjali baba yake wala Fayezi.

“Tulia mtoto mzuri hatuwezi kufanya muda huu”

“Mr Roma unapaswa kumheshimu Amina kama mchumba wangu , acha kuongea maswala yako ya kipuuzi”

“Wewe Fayezi bwana ni mwanaume wa kushangaza sana , ninachofanya hapa ni kujaribu kukufungua akili , huyu mrembo hakupendi hivyo kubali ukweli na ukaendelee na maisha yako , wanawake wapo wengi ambao watakufaa”

“Nasema hivi mimi labda sio Fayezi , nitahakikisha unashuhudia namuoa Amina, nina nguvu na pesa za kufanya hivyo”Roma alitabasamu.

“Hizo ni pesa zako na hazina maana yoyote kwangu wala kwa huyu mwanamke , na kama zingekuwa na maana kwako na kwake nadhani mpaka sasa tusingekuwa tunazungumza haya , lakini kama bado unataka kumuoa huyu mwanamke siwezi kuingilia , lakini unapaswa kuongea nae kwanza siku akikubali basi sitokuwa na namna ya kuingilia”

“Wewe mjinga,Mbona unaongea kwa kujiamini sana , unafikiri hatuwezi kukufanya chochote?, nakuambia hivi mimi Feisal Kanani ilimradi nina nguvu na pesa nitakufanya kitu ambacho hutokuja kusahau katika maisha yako”Aliongea tajiri Feisal kwa hasira , alishindwa kuvumilia kuangalia mambo yanayotendeka kwenye macho yake.

“Baba huruhusiwi kumfanya chochote Roma”Aliongea Mrembo huyu akimkingia kifua Roma , lakini Roma alijikuta akitabasamu na kumrudisha mrembo Amina nyuma yake na kumsogelea mzee.

“Mzee nikuambie tu , mimi sio tajiri kama nyie wa kuendesha magari na kulindwa na watu wengi lakini pia kuabudiwa kutokana na pesa zenu , mimi ninaweza kua masikini kwenye maisha yangu , lakini siwezi kuruhusu mtu anichokoze , kama kuna jambo unataka kufanya kwangu nakukaribisha, usiongee sana , msemo wangu katika maisha ninao ukubali ni ule unaosema , mwanaume anatambulika kwa juhudi za mikono yake sio kwa maneno yanayotoka kwenye midomo yake”Mzee alijikuta akichemka kwa hasira , hakuwahi kukutana na mtu anaejiamiani kama Roma kwenye maisha yake , alishindwa kufanya chochote na aliona ni kama atapasuka kwa hasira , na alijikuta akishikilia kifua chake.

“Nadhani hunijui vizuri mimi ,, nakuambbia nitakukomesha”

“Mzee nachukia kutishiwa amani sana kwenye maisha yangu ,labda nikuambie tu mwanao nilimbanjua , tena sio kwa goli moja nimepiga goli Zaidi ya tatu na wote tulifurahia tendo na tulitumia Zaidi ya masaa kama nane kumaliza , sasa hebu niambie je unauwezo wa kuchakata kama wangu?,mimi Roma Ramoni siogopi mtu , ukitaka tuliamshe tuliamshe ukinishinda nitakubali nimeshindwa lakini nikikushinda ukubali kushindwa”Mzee alijikuta akipandwa na presha na kuanza kupumua kwa tabu na kidogo tu adondoke ila alidakwa na mabodigadi wake na kumuingiza kwenye gari.

“Mr Roma ninaenda ila nitarudi kivingine”Aliongea Fayezi lakini kabla hajageuka Roma alikuwa ashamfikia na kumkaba shingoni na kufanya mabodigadi wamzingire , Fayezi alianza kutapatapa kwani mikono ilikuwa imemkaba kiasi cha kukosa pumzi , alimpiga piga ngumi Roma , lakini ni kama alikuwa akipiga gogo Roma hakuhisi maumivu yoyote.

Mabodigadi walishindwa kufanya chochote kutokana na namna ambavyo Roma amemshikilia Fayezi , ni kama walikuwa wakimuogopa Roma.

“Amina ukinipa ruhusa nimuue ili asikusumbue tena , nammaliza hapa hapa”

“Hapana Roma naomba usimuue mwachie aende zake”Aliongea Amina kwa woga , kwani aliona Fayezi anakaribia kufa na Roma alitabasamu na kumrushia kwa mabodigadi wake.

“Sipendi kutishiwa kwenye maisha yangu, nilikupa nafasi ya kunifokea unifokee kwa kumchukua mchumba wako lakini hukufanya hivyo ,lakini kunitishia ni jambo lingine kwenye maisha yangu , Na ushukuru Amina kakuokoa la sivyo nisingekuachia uhai wako , hivyo usie ukamsumbua tena maana haumdai chochote, ondoka”Aliongea Roma na Fayezi hakutaka kubakia hapo , aliingia kwenye gari akiwa na hasira na akaondoka.

Roma baada ya kumaliza kuongea hivyo ,alianza kupiga hatua kuondoka , huku akimuacha Amina aliesimama akishindwa kuelewa afanye nini , alijua mpaka hatua hio Roma amemsaidia sana hivyo hakupaswa kumfuata tena , kwani anajua ana mke.

“Kwaheri Roma,Mungu akipenda tutaoana”Aliongea Amina huku akifuta machozi kwenye macho yake na Roma alimwangalia mrembo huyo na kumkonyeza na hakutaka kubaki tena hata sekunde , alitaka awahi kazini.

*****

Jestina alijikuta akiumia sana baada ya kujua kuwa dada yake Blandina yupo hai muda wote huo Zaidi ya miaka ishirini pasipo yeye na familia yake kujua , alijilaumu kwa kutofika ndani ya kituo hiki.

“Kwahioo nia yake ya kufungua kituo hiki , ilikuwa ni kama njia kwa dada na sisi kuungana tena?”

“Naweza kusema hivyo Mrs Azizi, Blandina alikuwa akifanya maombi sana kila siku ili mmoja ya wanafamilia kuja kutembelea hiki kituo , ili apate kuonana na ninyi”Aliongea Mama Issa na kumfanya mwanamke huyu azidi kububujikwa na machozi , aliona ni roho yake ya kibinafsi ambayo ilimfanya asikumbuke kuja kutembelea hiki kituo.

Jestina hakutaka kukaa chini hata kwa dakika moja , aliomba mawasiliano ya Blandina kwa ajili ya kuwasiliana nae na Mama Issa alimpatia bila shida yoyote.

“Hii ndio namba ambayo aliandaa kwa ajili ya nyie kuwasiliana”Aliongea mama Issa na kumkabidhi namba hio.

“Asante sana mama Issa , naomba niondoke sasa , nitakuja tena baada ya kuwasiliana na dada yangu”Aliongea huyu mwanamama huku akifuta machozi na kuweka kikaratasi kile kwenye mkoba wake na kuondoka ndani ya kituo hiki.

Mama issa alijikuta akikaa chini na kuanza kulia kwa kwikwi , haikueleweka ni kwanini mwanamama huyu alikuwa akilia.

Baada ya Jestina kufika nyumbani , haraka haraka aliingia kwenye chumba cha baba yake ,Mzee Atanasi , alikuwa akitaka kumueleza kila kitu alichopata kujua siku hio ya leo.

“Kuna nini Jestina mbona unahema hivyo?”Aliuliza Mzee Atanasi baada ya kukaa kwenye kitanda , kwani alikuwa amelala , na muda huu Tajiri Azizi hakuwepo.

“Baba….hiii..hiiii”Mwanamama huyu alijikuta akianza kulia pasipo kuongea na kumfanya mzee huyu aone kuna jambo ambalo halikuwa sawa , alikuwa akijua Jestina siku hio alimuaga kwenda kutembelea kituo cha Son And Daughter Orphanage, lakini alishangazwa na namna ambavyo amerudi.

“Jestina niambie nini kimetokea , kulia kwako kunaniweka kwenye hali ya Sintofahamu, nishakuambia siku zote unapaswa kuwa imara , kwanini unaruhusu hisia zikutawale”AliongeaMzee huyu kwa kufoka baada ya kuona Jestina Analia tu bila kuongea.

“Babani Blanidna baba…”Aliongea na kuchukua mkoba wake na kutoa barua na kisha kumkabidhi Mzee Atanasi , lakini kwasababu mzee huyu hakuwa akiona vizuri alimwambia Jestina Asome hio barua.

Mpaka Jestina anamaliza kusoma barua hio ni kama mzee huyu hakuwa akiamini kile alichokisikia , ilikuwa ni barua ya kuumiza mno kwa mwanafamilia yoyote ambaye alikuwa akimpenda Blandina.

“Blandina ni mjinga , anakaaje miaka yote hio bila kutuambia yupo hai , anajua ni namna gani nilikuwa nikiumia kwa kifo chake , Mshenzi sana huyu mtoto,sikutegemea kama atafanya ujinga kama huu”Aliongea mzee Atanasi huku hasira zikiwa kwenye macho yake.

“Baba usiwe hivyo , inatupasa kufurahi yupo hai , ni kosa letu pia baba”

“Jestina naomba uniache na sitaki kumsikia, kama kweli Blandina ni mwanangu asingefanya maamuzi ya kipuuzi namna hio , naomba uniache na usije ukalitaja jina lake mbele yangu tena , kama alichagua kukaa miaka ishirini pasipo kutuambia kama yupo hai , aishi hivyo hivyo na sitaki kumuona kwenye familia yangu”Aliongea kwa hasira huyu mzee , alikuwa mzee , lakini alionyesha alichukizwa sana na maamuzi ya Blandina na Jestina aliona amuache baba yake , kwani kwa hasira aliomuona nayo , hakuwahi kuishuhudia kwenye maisha yake yote tokea akiwa mdogo.

Licha ya Jestina kuona baba yake kakasirika , hakutaka kutulia kabisa , alijiambia lazima siku hii ya leo aisikie sauti ya Blandina kwa namna yoyote ile , alijua baba yake anahasira tu za muda mfupi na muda ukipita atatulia… haraka haraka alikimbilia kwenye chumba chake na kutoa simu yake na kuanza kuingiza ile namba aliopewa na kupiga na kisha akaweka sikion, na alishukuru baada ya kusikia namba ile inaita.

*****

Roma saa tano kama na nusu ndio muda ambao alifika kazini , hali ya kampuni ilionekana kuwa tulivu mno, ni hali ya hewa ya ubaridi na marashi ya aina tofauti yaliomfaya bwana huyu kufurahi.

Baada ya kuingia ndani ya idara ya PR aliwakuta wenzake wakiwa bize , Recho alimuona Roma na kumsalimia na hakukua na stori nyingi, alikaa kwenye kiti chake na kuvuta pumzi , licha ya kwamba alionekana kuwa sawa kwa nje , ila alijua Edna saivi atakuwa na hasira nae na hivyo akili yake ilikosa utulivu,Roma hakutaka kufikiria sana , aliamua kutulia kwenye kiti chake na kuegamia , leo hii hakuwa hata na hamu ya kucheza gemu.

Saa kumi kamili alitoka na gari yake na kurudi nyumbani na alipokelewa vizuri na Bi Wema lakini kwa Sophia alimwangalia Roma na kushindwa kumuelewa , kwani tokea jana yake ndio anarudi muda huu , alishangaa ni mwanaume wa aina gani anaweza kutoka na kuiacha nyumba yake na kurudi jioni , lakini hakutaka kujali sana.

Ukweli ni kwamba licha ya taarifa ya Amina kusambaa mtandaoni lakini picha za Roma zilifichwa na pia jina lake halikuandikwa Zaidi ya Amina peke yake alieonekana , hivyo hata Sophia na Bi Wema hawakuwa wakijua kile kinachoendelea , walichokuwa wanajua ni Roma kulala nje ya Nyumbani kwa usiku mzima, na walihisi ni lazima itakuwa alilala kwa mwanamke , lakini kwa Bi Wema hakujali sana , aliona tabia za Roma zilikuwa zikisababishwa na Edna mwenyewe kwa kutomjali mume wake, mwanamama huyu aliamini kama Edna angekuwa anamhudumia Roma kwa kila kitu , basi Roma angetulia nyumbani , hivyo matendo ya Roma hakuyawazia sana.

Edna hakurudi kabisa mpaka inafika saa mbili na alimpigia simu Bi Wema kama atachelewa kurudi , ana kazi ofisini na Bi Wema alishangaa, ila hakutaka kuuliza sana , alimsihi tu asisahau kula.

Roma na yeye baada ya kujua hilo , hakutaka kuliwazia sana , alijua Edna alikuwa na hasira hivyo alikuwa akifanya hivyo kumuepuka , ili wasionane na hakutaka kufanya jambo lolote kwa muda huo , aliona ataharibu Zaidi , alichoamini tu ni kwamba Edna atakuwa salama kwani wanajeshi wake wanampa ulinzi.



































SEHEMU YA 114

BOLIVIA 1990.

Katika jambo ambalo Carlos , alikuwa amekosea ni kumuacha Ryani kumtoka kwenye macho yake, alijitukana kwa makossa aliokuwa amefanya kwani Ryani alionyesha kumzidi akili.

Misheni ya Carlos kuingia ndani ya Kambi hii ambayo ilikuwa ikiendesha project ya Pro Human ilifanikiwa kwa asilimia mia moja , na bwana huyu kutokana na utaalamu wake uliotukuka katika maswala ya kijasusi , aliweza kujipenyeza na kukubalika kama moja ya walinzi ndani ya hii kambi na alimfanya Mellisa Luiz Meneja wa hio ‘project’ kumuamini na haikuwa kumuamini tu , lakini pia alimfanya akawa mpenzi wake na hapa ndipo kosa la Melisa alilokuwa amefanya kwani Carlos alitumia udhaifu wa Mellisa wa mapenzi yake kwake na kumpa cheo kikubwa cha ulinzi ndani ya kambi hii na kufanya misheni yake kukamilika kwa asilimia mia moja.

Baada ya siku kadhaa za Carlos kutoa maendeleo ya misheni yake kwa Director Powel kwa njia ya siri , aliweza kupewa maagizo mengine ya kuhakikisha anatega mabomu ndani ya hio kambi ndani ya siku moja.

“Kazi yako ni kutega mabomu ambayo yataweza kuilipua hio kambi yote pasipo kuacha aina yoyote ya ushahidi Carlos , kuhusu namna ya kupata mabomu hayo , itakuwa juu yako , tumia utaalamu wako kutengeneza mabomu hayo , una siku nne tu , siku inayofuatia mtapokea ugeni ndani ya kambi yenu na hio ndio itakuwa siku ya kukamilisha misheni”

“Ugeni gani Director??”

“Atakuja Ryani akiwa na sura ya mjukuu wa Profesa Banosi , afahamikae kwa jina la Coheni , hakikisha unafanya nae ‘Eye Contact’ na atakupa maelekezo namna ya kukamilisha misheni na baada ya hapo utajua nini unapaswa kufanya”Aliongea Director na kisha akakata simu., na hio ilikuwa ni siku nne kabla ya Cohen na Mr Anderson kufika ndani ya kambi ya Pro Human kwa kutumia usafiri wa Chopa.

“Mellisa There is Problem , which need your attention?”Aliongea Carlos alieshikilia bunduki lake huku akiangaliana na Cohen.

“What ,Which Problem??”Aliuliza Merlisa huku akitangulia mbele na muda ule ule Cohen alimpa ishara Carlos ya vidole vinne akimaanisha kwamba anazo dakika nne za kukamilisha misheni, na Mr Anderson hakuelewa kilichokuwa kikiendelea kwani macho yake yote yalikuwa kwa vichanga ambavyo vilikuwa vikionekana kwenye Skrini.

Muda ambao Merlisa alikuwa akiingia kwenye chumba kilichokuwa ni cha kuongezea Camera ,Cohen alimsogelea Mr Anderson na kumpiga kitaalamu kwenye shingo yake na akamuweka chini akiwa hajitambui

“Upande wa Chumba cha kuongozea Kamera baada ya Merlisa kuingia ndani ya hiki chumba , alijikuta akipigwa na mshangao , kwani vijana wote walikuwa wamelala chini wakiwa hawajitambui huku kamera za Ulinzi kupitia Skirni za hapo ndani zikionesha maeneo yote ya nje na ndani ya eneo hili.

“Upo chini ya ulinzi Merlisa”Aliongea Carlos kwa sauti nzito ambayo Merlisa hakuwa amewahi kumsikia nayo Carlos na ni kama hakuwa akiamini kwani alijikuta akigeuka.

“Carlos..!!!”Aliongea kwa mshangao Merlisa huku akionesha hali ya wasiwasi katika macho yake.

“Usishangae Merlisa , mimi ni Carlos ndio Ajenti kutoka CIA na nipo kwenye misheni ya kuharibu kila mnachotengeneza hapa ndani”Aliongea Carlos kwa lugha ya kingereza na kumfanya mwanamama huyu kutoa machozi , alikuwa ametokea kumpenda sana Carlos kwa muda mfupi,lakini sasa baada ya kujua mwanaume aliekuwa mbele yake , alimhadaa na hakuwa akimpenda kama alivyokuwa anamwambia ila yupo kwenye misheni aliumia.

Carlos hakutaka kuongea sana na Merlisa , alimpa Amri ya kusogelea tarakishi moja iliopo hapo ndani ili kuingia kwenye mfumo wa ulinzi wa kambi hio , ili afungue mlango wa chumba ambacho vitoto vichanga vilikuwa vimehifadhiwa , na hii ilikuwa ni kumruhusu Ryani akamchukue mtoto na kutoka ndani ya hio kambi.

Merlisa hakutaka kuleta shida kabisa , aliona nia ya Carlos kumdhuru na ndio maana alitii.

“Carlos hatutakiwi kufanya hivi ni hatari mno kama watoto wale wakitoka uraiani , pasipo hatua za kiusalama juu yao kuchukuliwa “

“Shut the F*ck up Merlisa , Do as I say , Open the Door”Aliongea Carlos kwa hasira na Merlisa alianza kutetemeka , alikuwa akiogopa kufa na ndio maana alianza kucharanga batani za tarakishi na ndani ya dakika kadhaa tu , ilitokea Ramani ya eneo lote la kambi na kumfanya Carlos atabasamu.

“Make it Hury Merlisa this is no Joke”Aliongea Carlos

Hapana CIA hawajui hatari iliopo kama vile vichanga vitatoka uraiani , lazima nitafute namna”Aliwaza Merlisa na hakutaka kuleta ubishi , alifungua mlango.

Ryani aliekuwa kwenye sura ya Coheni baada ya kuona mlango umefunguka haraka haraka alitembea kwenye yale makabati ya vichanga vilivyokuwa vikirusha rusha miguu kwa nguvu mno ambayo sio ya kawaida kwa mtoto mchanga, Alihesabu vitoto vyote kumi na mbili na baada ya kifikia kwenye sanduku lililokuwa na jina la ‘The First Goddess’Alitabasamu na kilichomshangaza Ryani ni kwamba kati ya vichanga vyote kumi na mbili , mtoto wake pekee ndie embaye hakuwa akirusha miguu.

“Carlos huwezi toka hai ndani ya hii kambi unajidanganya tu , ulinzi ni mkali sana”Aliongea Merlisa

“Thanks for your Concern Merlisa , but we are not Done yet”

“Unataka nini tena Carlos?”

“Nataka u’activate All the Bomb’s, kwenye hii kambi”Aliongea Carlos na kumfanya Merlisa atoe macho.

Ukweli ni kwamba Carlos baada ya Director kumpa maelekezo ya kutengeneza mabomu , alimuelewa kwani aligundua kuwa Director Powel alikuwa akiongea kwa Code.

Katika akili ya kawaida , kwa Projekti kubwa kama hii Carlos aliaminni lazima kuna tahadhari ambazo zimechukuliwa pale mpango utakapo feli , aliamini lazima kutakuwa na mabomu ambayo yametegwa ndani ya hii kambi kama tahadhari ya kiusalama , ili kama wanachokitengeneza kikiwazidi nguvu , wanachokifanya ni kulipua tu kambi, hilo alielewa sana Mtaalamu Carlos na hivyo ndivyo pia alivyowezakufungua kodi ya Director powel , ya kutengeneza mabomu’, kwa mtu wa kawaida asingeelewa , ila kwakua Carlos alikuwa na mafunzo ya juu ya kijasusi , basi aliweza kumuelewa Powel.

Merlisa mpango wake ulikuwa ni kulipua mabomu yaliokuwa yapo kwenye hio kambi lakini kitendo cha kupewa amri na Carlos kufungua hayo mabomu basi hakuona shida kabisa kufanya hivyo m alichokifanya ni kucharanga batani za tarakishi na ndani ya dakika chache tu Ramani ya mabomu yote mazito yalionekana.

“Do you really want to Activate The Bomb’s? ,If you hit ‘Enter ‘The Bomb`s will go off in 60 second”Ulikuwa ujumbe uliosomeka kwenye Skrini ya tarakishi hii na Merlisa alimwangalia Carlos.

“Merlisa nakupenda sana na neno lolote la kimapenzi nililokuambia ni la dhati kabisa , lakini mimi ni Ajenti siruhusiwi kupenda , kabla hujabonyeza hiko kitufe nataka kukupa sekunde therathini za kujiokoa kabla ya mabomu hayo hayajalipuka”Aliongea Carlos na kumfanya Merlisa ashindwe kujua ni nini anamaanisha.

“Nitatoka na kufunga ule mlango wa kutokea baada ya kubonyeza hiko kitufe nitaufunga kwa nje , kwa uzoefu wangu kufungua kile kitasa bila ufunguo itakuchukua sekunde therathini pekee na mpaka hapo utakuwa na sekunde nyingine therathini za kutoka kwenye hii kambi kabla ya mlipuko”Aliongea Carlos na kisha alisogea kinyume nyume mpaka kwenye mlango huku siraha yake akimuelekezea Merlisa na ile anafika kwenye mlango alimuamrisha Merlisa kubonyeza ‘Enter’ huku Carlos akiangalia Skrini za ukutani maana na zenyewe zilikuwa zimekunganishwa na Tarakishi ambayo alikuwa akitumia Merlisa, na Merilisa alifumba macho kwa sekunde kama mtu ambaye alikuwa akisali na kisha akabonyeza kitufe cha ‘Enter; na palepale Carlos alitoka na kufunga mlango na kukimbia.

Carlos alifanikiwa kutoka kabla ya mlipuko lakini kwa kuchelewa na hii ni kutokana na kwamba mlango ambao alitakiwa kutumia kutokea , ambao ulikuwa ndio njia ya Rahisi kutoka kabisa ya uzio, mlango huo ulikuwa umefungwa kwa nje na alijua huenda atakuwa ni Ryani , kwani muda mchache uliopita alimpa ishara ya kutumia njia ya Mashariki ya kambi hii.

Misheni ya Carlos ikawa imefeli , kwani licha ya bwana huyu kutumia chopa kumtafuta Ryan , lakini hakumuona kabisa na Ryani alimzidi ujanja Carlos.

Hio ilikuwa nni miaka ya tisini wakati tukio hili likitokea huko nchni Bolivia kwenye msitu wa Amazoni , Ryani na mke wake Epholia walitokomea kusiko julikana na mtoto ambaye alikuwa akitengenezwa kuwa ‘Pro Human aliepewa jina na Project hio kama ‘The First Goddess’ Yaani Mungu wa kike.

Je huyu mtoto yuko wapi na ukumbuke Merlisa alisema ni hatari kwa huyu mtoto kuingia kwenye jamii ya Binadamu wa kawaida.

ITAENDELEA













SEHEMU YA 115

KENYA –NAIROBI.

Mke wa Raisi Kamau Kamau , aliekuwa akifahamika kwa jina la Maina alikuwa ameketi eneo la sebuleni akiangalia Runinga ndani ya ikulu , licha ya mwanamama huyu kuangalia kile kilichokuwa kikioneshwa na chaneli maarufu kutoka Marekani , lakini alionyesha kukosa umakini kabisa, baada ya kuona haelewi alizima runinga ile na kunyanyuka na kulisogelea Friji lililokuwa hapo sebuleni na kutoa chupa ya Wine na akaifungua na kuijaza kwenye glass na kisha alitembea kuelekea upande wa kushoto akiwa maeshikilia Wine yake mkononi,wakati huu alikuwa na sura yake bandia iliokuwa ikifahamika kwa wananchi wengi wa Taifa la Kenya.

Na wakati huu ilikuwa ni saa tisa hivi za jioni , baada ya mwanamama huyu kuingia kwenye hiki chumba , alichukua simu yake kubwa ya I phone na aliona ujumbe uliokuwa ukitoka kwa Mkuu wakituo cha kulelea Yatima cha Tanzania.

Nimefanikiwa kukabidhi”Ilikuwa ni meseji ilioandikwa kwa namna hio na mwanamama huyu alijikuta akifumba macho na kuangalia juu kwasekunde kama sitini hivi na ile anashusha uso wake chini , macho yake yalijawa na machozi baada ya kuyafumbua.

“Kamau Utanisamehe sana ,Huu ndio wakati wa mimi kutoka kwenye hiki kifungo”Aliongea mwanamama huyu na kisha akasogelea kabati lililokuwa ndani ya hiki chumba kikubwa kama cha mfalme na kufungua mlango wa kushoto , sehemu ambayo ilionekana kuhifadhia baadhi ya vitu vyake muhimu kama vile vibanio vya nywele na mikufu ya thamani , alitoa mkufu mmoja wenye kidanui chenye herufi ya nembo D na kisha akaishika mkononi na kisha alisogelea mkoba mweusi alioutundika kwenye kabati na kisha akaufungua na kutoa simu ndogo ana ya Nokia tochi na kurudi kitandani.

Maina baada ya kufika kitandani alifungua kile kidani kwa kukibanjua katikati na ikadondoka laini chini kwenye sakafu na mwanamama huyu aliinama na kuiokota na kisha akafungua ile simu ndogo na kuingiza ile laini na kuwasha ile simu.

Baada ya Maina kumaliza kuwasha tu ,simu ile ilianza kuita hapo hapo na mwanamama huyu aliangalia simu iliokuwa ikiita bila kupokea , alikuwa ni kama mtu ambaye alikuwa akijishauri kupokea ama asipokee , kwani hakuonekana kuwa na uhakika kwenye macho yake.

Blandina umejiandaa kwa Zaidi ya miaka ishirini kwa ajili yah ii siku , hupaswi kuogopa , pokea simu”Ilikuwa ni suati ambayo ilikuwa ikimshawishi kwenye kichwa chake , ambayo ilionekana kuwa na nguvu sana kuliko ile ambayo ilikuwa ikimkataza, simu ilikatika, lakini baada ya dakika moja ilianza kuita tena na mwanamama huyu alivuta pumzi na kuweka sikioni.

“Hello!!”Ilikuwa ni sauti ambayo mwanamama huyu alikuwa akiijua sana , licha ya kwamba ilikuwa miaka mingi sana bila ya kusikia hio sauti , lakini hakuwahi kabisa kuisahau Zaidi ya kuimisi tu , mwanamama huyu alijikuta akishindwa hata kuongea neno.

“Blandina najua unanisikia ni mimi mdogo wako Jestina”Ilikuwa ni sauti upande wa pili , iliosikika na kumfanya mwanamama huyu kuanza kutoa machozi mfululizo yaliokuwa yakitambaa mpaka kufikia kwenye shingo yake.

“Jestina najua ni wewe , mimi ni Blandina dada yako , sipo sehemu nzuri ya kuongea , Alhamisi ya wiki hii naomba tuonane ndani ya kituo cha Son and Daughter orphanage Bagamoyo , muda ni saa nne kamili za asubuhi”

Aliongea Maina kwa kujikaza na kisha akakata ile simu na kuizima kabisa na akaifungua na kutoa ile laini na kusogelea mlango wa chooni na akaitupa ile laini na akarudi na kiuchukua kile kidani na akakifunga kama mwanzo na kisha akarudi na kukihifadhi kwenye kabati.

Upande wa ofisini ndani ya ikulu hii ya wananchi wa Kenya , Mheshimiwa Raisi Kamau Kamau , alikuwa akiendelea na majukumu yake kama kawaida akiwa na umakini mkubwa , bwana huyu alionesha kuna nyaraka muhimu ambazo alikuwa akizisoma na kuzisaini mpaka pale mlango wake ulipofunguliwa na katibu muhtasi wake.

“Mheshimiwa Mr Deo anataka kuonana na wewe”Aliongea mwanadada moja mrefu ambaye alikuwa ni katibu muhtasi,

“Laila unaweza kumruhusu haina shida”Aliongea Kamau kwa lugha ya Kingereza na Laila aliitikia kwa kichwa na kisha akatoka ,na ndani ya dakika chache tu , aliingia bwana mmmoja hivi alievalia mavazi ya suti , mrefu mweusi alienyoa kipara, alikuwa ni kijana wa miaka kama Therathini hivi.

“Nipe ripoti Deo”

“Mheshimiwa kuna meseji kutoka Tanzania imeingia katika mfumo wetu”Aliongea Deo na Mheshimiwa alimpa ishara Deo amsogeleee kwenye meza yake na Deo alimpa mzee huyu kishikwambi alichokuwa ameshikilia mkononi mheshimiwa.

Nimefanikiwa kukabidhi”Ulikuwa ndio ujumbe uliosomeka kwenye kishkwambi , uliokuwa ukitoka kwa Mkuu wa kituo cha kulelea Yatima cha Son and Orphanage kwenda kwa Maina.

“Unaonaje?”Aliuliza Mheshimiwa.

“Unaonekana ujumbe ambao una Zaidi ya maana”

“Hata mimi naona hivyo Deo , lakini ni jambo ambalo nitalithibitisha mimi mwenyewe”Aliongea Mheshimiwa na Deo aliitikia na kisha akatoka.

“Lazima kuna jambo mke wangu anapanga kulifanya , ila nitajua,Maina huwezi kunizidi akili, mimi ndio Kamau utaishi na mimi mpaka siku mmoja wtu atakapotangulia mbele za haki”Aliwaza Mheshimiwa Kamau Kamau na kisha akarudisha macho yake kwenye karatasi zilizokuwa kwenye meza yake na kuendelea na kazi yake aliokuwa akiendelea kufanya.

“Mume wangu Alhamisi nitaelekea Tanzania”Aliongea Maina usiku baada ya kufanya tendo la ndoa na sasa walikuwa wamepumzika huku Maina akichezea chezea kifua cha Kamau.lakini kwa upande wa Kamau hapo hapo ujumbe wa meseji uliibuka kwenye kichwa chake na kengele ya hatari iligonga.

“Kuna nini mke wangu?”

“Nahitaji kuonana na watoto wa kile kituo, ni muda sasa sijafika hata kutembelea mume wangu”Aliongea Maina na kumfanya Kamau afikirie kidogo , ukweli hakuwa na tabia ya kumzuia mke wake likija swala la kutembelea watoto, kwani tokea Blandina aanze kujificha kwa sura Bandia Furaha kubwa ya blandina ni kuona watoto na ndio maana Mheshimiwa alijitahidi sana kumsapoti maina katika jitihada zake za kufungua vituo vya kulelea watoto yatima, aliona ni jambo pekee ambalo anaweza kumfanyia mke wake kama moja ya malipo kwa namna ambavyo amevumilia miaka na miaka kuishi na sura bandia mbele za watu.

“Sawa mke wangu,sina haja ya kukuzuia , ila ujue tu nakupenda sana”Aliongea Kamau na kumfanya Maina apatwe na wasiwasi kidogo , lakini aliishia kutabasamu na kujikunja kama mtoto kwenye mwili wa mume wake.



*****

Zilipita siku mbili yaani Jumatatu , jumanne na sasa ilikuwa ni jumatano kwa Roma, bwana huyu tokea tukio la kulala na Amina lipite mke wake alikuwa amezidisha kumchunia kwa asilimia mia moja , Edna hakutaka kabisa kuongea na mume wake , kwanza Edna hakuwa akirudi nyumbani muda ambao ulikuwa umezoeleka kwake kurudi na siku nyingine alikuwa akilala kabisa kazini jambo ambalo liliwashangaza sana Bi Wema na Sophia kwa mabadililo ya Edna.

Roma licha ya kujua mke wake alikuwa hataki kabisa hata kuongea na yeye na alikuwa akimkwepa makusudi , hakutaka kulazimisha , aliendelea na mishe zake kama kawaida.

Saa moja kamili za jioni Roma alikuwa Pongoni Beach akiwa na Yezi, Roma alikuwa akimenya viazi na Yezi alikuwa akikaanga na kupakua na kuweka kwenye kabati la kuhifadhia.

Yezi alikuwa akimwangalia Roma kwa namna ambavyo yupo siriasi na kujikuta moyo wake ukiwa wa moto, hakuelewa ni kipi alichojisikia moyoni mwake , lakini alikuwa akijisikia vizuri kuwa na mtu ambaye alikuwa akimsaidia na kumjali.

“Anko Aunt Edna anaendeleaje?”Aliuliza Yezi baada ya kumaliza kazi yake na kukalia kindoo karibu na Roma.

“Kaninunia, siku ya tatu leo haniongeleshi”Aliongea Roma akiwa kawaida na Yezi alishangaa kidogo.

“Yaani Anko unapata mke mzuri kama Aunt Edna halafu unamuuzi mpaka anakununia”Roma alijikuta akitoa tabasamu la uchungu , nikweli kabisa kwa jinsi Edna alivyokuwa mrembo mtu yoyote lazima angesema kama Yezi,ila kulikuwa na mambo ambayo watu hawakuwa wakijua

“Ni mambo ya mahusiano , kununiana kupo tu “Aliongea Roma akipotezea mada , ukweli aliamini Edna hasira zake zitaisha zenyewe tu na watarudi kuwa kama kawaida , licha ya kwamba Roma hakuwa akitegemea kitu kikubwa kutoka kwa Edna lakini namna mke wake alivyokuwa akimueuika , alikuwa akijisikia vibaya.

“Yezi nadhani unakumbuka kuwa kesho tunaenda Kiwangwa kumuona Mama yako?”Aliongea Roma.

“Ndio anko Roma nina shauku kweli ya kumuona Mama Issa”

“Kama unashauku kwanini hukurudi muda wote unamtesa mama wa watu?”

“Nilikosa ujasiri”Aliongea Yezi na Roma akatabasamu , alimuelewa Yezi anachomaanisha hivyo hakutaka kuongea Zaidi.

Roma alimsaidia Yezi mpaka muda wa kuondoka na kumsindikiza mpaka sehemu ambayo Yezi amepanga na kisha akarudi nyumbani kwa ajili ya kulala, ilikuwa ni saa nne kama na nusu wakati akiingia nyumbani na gari ya Edna haikuwepo na alijua tu huyo mwanamke atakuwa yupo bado kazini , lakini wakati anaanza kupiga hatua kuelekea ndani geti lilifunguliwa na gari ya Edna ilionekana kuingia na Roma baada yakuiona gari ya mke wake inaingia , alisimama , alitamani kuongea nae hata kidogo kabla ya kwenda kulala.

Edna alishuka kwenye gari , akiwa na mkoba wake , mrembo huyu alionyesha hali ya kuchoka mno, kiasi kwamba Roma alimuonea huruma na kujiona mwenye hatia , hakujua kilichokuwa kikiendelea kwenye akili ya Edna.

Edna alimpita Roma baada ya kumtingishia kichwa kama salamu, lakini Roma palepale alimsogelea Edna na kisha akamkumbatia kwa nyuma.

“Roma naomba uniachie , usivuke mpaka”Ilikuwa ni sauti ya kibabe ya Edna , lakini Roma hakujali , alimshika Shingo Edna na palepale Edna alilegea kwenye mikono ya Roma , alionekana tayari ashalala na haikueleweka Roma kamfanyia nini.

Roma alimbeba na kumuingiza ndani , na sebuleni walikuwepo Bi Wema na Sophia wlaiokuwa wakiangalia tamthilia ya kifilipino , na walionekana walikuwa wamenogewa sana , kwani walishindwa hata kujua Roma alipita hapo sebuleni.

Roma aliingia kwenye chumba hiki cha mke wake na kumpeleka Edna mpaka kitandani na kumlaza vizuri , alimtoa kijikoti cha suti alichovaa Edna na kumbakiza na blazia.

Roma baada ya kumaliza alimshika Edna kwenye uso wake kwa kumuwekea kiganja na akafumba macho kwa takribani dakika kumi na kisha akatoa kile kigana na kumfunika na shuka vizuri .

“Endless resorve restoration Energy ,utaamka kesho saa saba mchana , mpaka hapo utakuwa umepumzika vya kutosha na unaweza kuendelea kuninunia mke wangu , ila sitaki kukuona ukichoka namna hii”Aliongea Roma akimwangalia namna Edna alivyokuwa usingizini na kujikuta akivutiwa Zaidi na namna mke wake alivyolala.

Roma kuna jambo wakati alipoingia hakulioana na sasa alikuwa ameliona na kumfanya Acheke , jambo lenyewe ni kwamba Mdoli aliomzawadia Edna ulikuwa umening`inizwa ukiwa umefungwa Kamba shingoni kwenye uzio wa balconi kwa nje, yaani ilikuwa ni kama Edna alikuwa akiuonyonga huo Mdoli.

“Hahaha..”Roma alijikuta kicheka kwa namna ambavyo mdoli huo umenyongwa, hakutaka kuutoa , alichofanya ni kuangalia kwa dakika kadhaa na kisha akamgeukia Edna na kutabasamu na kisha akatoka na kwenda kwenye chumba chake.

“Kesho ni Alhamisi nikiamka nimpeleke Yezi Kiwangwa”Aliongea Rma baada ya kuoga na kujilaza kitandani.

ITAENDELEA KESHO.
 
SEHEMU YA 116

Roma alimaliza taratibu zake zote baada ya kuamka na ni muda wa saa mbili kamili za asubuhi alishuka mpaka sebuleni kwa ajili ya kujipaitia kifungua kinywa kilichoandaliwa na BiWema.

“Bi Wema msimuamshe Edna muacheni alale mpaka atakaposhituka mwenyewe”Aliongea Roma mara baada ya kumsalimia Sophia na Bi Wema.

“Jana Miss na wewe mlirudi saa ngapi?”

“Tulirudi mapema tu , niliwakuta mnaangalia tamthilia yenu na siku taka kuwasumbua”Aliongea Roma na kila mtu akajiweka bize kuendelea kunywa chai ,huku Sophia akiibia ibia kumwangalia Roma , haikueleweka mrembo huyu alikuwa akifikiria nini.

Roma kama alivyopanga siku ya leo hakuwa kabisa na mpango wa kwenda kazini , alipanga kumpeleka Yezi kituoni ili akamsalimie Mama Issa, alipumzika kidogo kwenye chumba chake mpaka muda wa saa tatu kama na nusu za subuhi na alimpigia simu Yezi kwamba anamfuata sehemu ambayo amepanga na amkute amejiandaa.

Dakika chache mbele Roma alikuwa ashafika na alimkuta Yezi akiwa amesimama nje alievalia suruali yake ya jeans na jezi ya Yanga.

“Ingia twende Yezi”Aliongea Roma baada ya kusimamisha gari na kumuona Yezi amezubaa zubaa, huku pia wamama wa Kiswahili waliokuwa nje ya viubaraza vyao walihusudu gari ya Roma na kujiambia kwenye nafsi yao Danga lake Yezi ni bab kubwa.

Yezi ndio aliekuwa ametawala maongezi kwenye gari na kumfanya Roma kucheka , kwani alifurahishwa na baadhi ya stori za Yezi, na hii ilifanya safari yao kuchukua muda mfupi kuliko walivyotarajia , lakini baada ya kukaribia karibu na kituo hiki Yezi alijikuta akiwa kimya na kumfanya Roma amshangae.

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi Yezi ,Mama Issa atafurahi sana kukuona siku hii ya leo”Aliongea Roma kumtia moyo Yezi , kwani aliona mabadiliko yake na Yezi alivuta pumzi na kuitikia kwa kichwa.

Roma ile anaingiza gari yake upande wa kushoto wa hiki kituo mita kama mia hivi kutoka getini, alisimamishwa na watu watatu, wote wakiwa kwenye mavazi ya suti ,wawili wakiwa ni wanaume na mmoja alikuwa ni mwanamke, Roma alishangaa kwanini kasimamishwa na watu hawa ilihali anataka kuingia kituoni.

“Tunaomba mgeuze gari mrudi na mtakuja siku ya kesho au mrudi baadae”Aliongea yule mwanamke na alionekana ndio aliekuwa ni kiongoza.

“Kwanini nirudi kesho wakati nimepanga kuja kituoni leo?”

“Mr kuna swala la kiusalama linaendelea hapa ndani na hamruhusiwi kupita”Aliongea yule mwanaume mmoja aliekuwa pembeni ya yule mwanamke, na kwa jinsi mwanaume yule alivyoongea Roma aligundua kuwa ni mkenya kutokana na rafudhi yake.

“Anko tutarudi kesho wanaonekana kuwa wanausalama”

“Yezi tulia tushakuja tayari na siwezi kurudi tena”Aliongea Roma huku akifungua mlango na kutoka nje na kuwafanya hawa wanausalama kuzidi kupandwa na hasira , maana waliona Roma analeta ngumu.

“Mr acha kujitafutia matatizo , tushasema eneo hili hauwezi kuingia siku ya leo mpaka kesho kutokana na itifaki za kiusalama”

“Kwahio unamaansha huko ndani kuna mtu mzito kutoka serikalini?”Aliuliza Roma akiwa hana hata wasiwasi.

“Mpaka hapo nadhani ushaelewa , hivyo geuza gari yako na uondoke usitulazimishe tutumie nguv”.Roma kwanza aliona hii ngumu na haikueleweka alikuwa akiwaza nini kwani alikuwa akikuna kichwa chake , aligeuka nyuma na kumwangalia Yezi ambaye alionekana kuwa na wasiwasi na hawa walinzi wote walikuwa wameshikilia Siraha za moto.

Wakati Roma akiwa amesimama pasipo kufanya jambo , ziliingia gari nyingine tatu eneo hili kwa upande wa nyuma na kuwafanya hawa walinzi wote waziangalie.

Gari moja ilikuwa nyeupe na mbili zilikuwa ni nyeusi moja ikiwa ni Mercedez Benz S-class na mbili zote zilikuwa ni gari kubwa aina ya V8, sasa barabara hii ya kuingia kituoni ilikuwa ni ndogo na ilikuwa ikiruhusu gari moja kwa wakati kupita na hivyo kitendo cha Roma kusimamisha gari yake ni kwamba alikuwa amezuia gari za nyuma yake kushindwa kupita.

“Kuna nini kinaendelea hapa?, tunataka kuingia kituoni mmezuia barabara”Aliongea bwana mmoja alievalia mavazi ya suti , alionekana alikuwa ni moja ya walinzi ambao wamekuja na gari hizo.

“Ajent Dondwe familia ya Mzee Atanasi imeshafika , nini tunapaswa kufanya?”Yule mwanamke alibonyeza kifaa chake sikioni na kuongea hayo maneno na ilionesha alikuwa akiwasiliana na waliokuwa ndani ya kituo, na baada kuongea hayo maneno alionekana kupewa maelekezo mengine na almpita Roma na kuelekea kwenye gari zilizokuwa nyuma , lakini kabla hata hajafika , alishuka mwanamama ambaye baada ya Roma kumwangalia tu alimfahamu, alikuwa ni Jestina mke wa tajiri Azizi , alijiuliza mwanamama huyu anafanya nini hapa.

“Madam unapaswa kurudi kwa siku ya leo , kuna itifaki za kiusalama zinazoendelea ndani ya hili eneo na haruhusiwi mtu yoyote kuingia kwa sasa”Aliongea yule Ajenti wa kike na kumfanya mwanamama huyu kushangaa , lakini macho yake pia alikuwa ameyaelekeza kwa Roma na yeye alijiuliza ni jambo gani ambalo limemleta Roma hapo kituoni.

“Kuna nini kinaendelea ambacho kinanifanya nisiingie ndani ya hiki kituo?”Aliuliza Jestina kwa mshangao na mpaka kufikia hali hio aliokuwa akiishuhudia , aliamini mpango wa kuonana na dada yake unakwenda kukwama.

“Lazima nionane na dada yangu kwa namna yoyote leo , najua hizi ni mbinu za kunizuia nisionane nae”Aliwaza mwanamama huyu huku akimwangalia Roma kwa sekunde na kisha akageuza na kwenda mpaka gari ya katikati , sio ile aliotoka ni ile ambayo ilikuwa ni ndogo aina ya Mercedez.

“Baba! Inaonekana walinzi wa raisi wa Kenya wanatuzuia tusionane na Blandina”Aliongea Jestina baada ya kioo kushushwa na ndani ya gari hio alionekana mzee Atanasi akiwa ameegamia kiti akiwa ameshikilia fimbo yake.

Upande wa ndani ya hiki kituo , ndani ya ofisi ya Mama Issa anaonekana Maina akiwa kwenye sura yake bandia huku akiwa amezungukwa na walinzi waliovalia suti nyeusi na mashati ya rangi yeupe , huku wakiwa wote wamevalia ‘Ear pieces’.

“Madam!, Mheshimiwa Raisi anataka urudi Kenya mara moja na hauruhusiwi kuongea na mtu yoyote ndani ya Tanzania mpaka utakapofika Kenya “Aliongea bwana mmoja hivi aliekuwa na mwili mkubwa kuliko wanausalama wote na alionekana ndio aliekuwa ni kiongozi.

“Siwezi kurudi Kenya pasipo kutimiza kile kilichonileta hapa, mwambieni hivyo Kamau”Aliongea Maina kwa hasira.

“Madam unafanya kazi yetu kuwa ngumu , tunaomba utoe ushirikiano”

“Nadhani hujayalewa maneno yangu , nishasema siwezi kutoka hapa pasipo kuoanana na mtu ambaye nimepanga kuonana nae na mtu yoyote asije akanigusa”Aliongea Maina na kufanya walinzi hawa waangaliane.

Walinzi hawa kazi yao waliona kuwa ngumu katika siku zote ambazo wamewahi kuhudumu kwa kumlinda mke wa Raisi Kamau, licha ya kwamba siku zote walinzi hawa walikuwa wakipokea maagizo kutoka kwa mke wa Raisi , lakini leo hii mara baada tu ya kuingia ndani ya kituo hiki , walipigiwa simu na mheshimiwa mwenyewe kutoka Kenya, akiwapa maagizo ya kumrudisha mke wake haraka nchini na haruhusiwi kuongea na mtu yoyote kwa usalama wake, na kwa maagizo hayo hata Mama Issa hakuruhusiwa kabisa kuongea nae na ndio maana hakuwepo kabisa kwenye hiko chumba cha ofisi.

Licha ya kwamba walinzi hawa hawakupewa maelekezo ya kutosha kutoka kwa muheshimiwa , lakini ilibidi watii oda ya raisi na mbaya Zaidi hakukuwa na maelekezo mengine ambayo yalikuwa yametolewa kwao na hii ilikuwa ni saa mbili za asubuhi muda mfupi baada ya Maina kufika hapo kituoni.

Sasa hawa walinzi walijitahidi kumueleza Maina juu ya agizo kutoka kwa mheshimiwa Raisi kumtaka Maina arudi nchini mara moja , lakini Maina hakutaka kurudi , alijua Kamau lazima atakuwa ashajua kuwa anakuja kuonana na familia yake na ndio maana alikuwa akitaka kuzuia jaribio hilo , hivyo aliona leo pasipo kutimiza azima yake anaweza asifanikiwe kabisa na ndio maana alileta ngumu na hii iliwafanya waljnzi hawa wapate ugumu wa kutekeleza maagizo , kwani licha ya kwamba walipewa oda , lakini pia walikuwa wakimheshimu mke wa raisi ,kwani walifanya nae kazi kwa muda mrefu sana hivyo unaweza ukasema kwamba walikuwa ‘Half loyal’ kwa Maina.

Baada ya Maina kuweka ngumu , hawa walinzi wa kitengo cha Secret service ilibidi wawasiliane na mheshimiwa kueleza kwamba madam hataki kurudi na jambo hili lilimkasirisha sana Mheshimiwa.

“Naona mnashindwa kufanya kazi yenu kwa weledi Njiro?”

“Hapana mheshimiwa Madam kagoma kutoa ushirikiano”

Kikawaida mke wa Raisi wa Kenya alikuwa akilindwa na walinzi wanne na ni hao ambao alikuwa akitembea nao kila mahali, na hawa walinzi alikuwepo Njiro ambaye ndio aliekuwa msaidizi wa karibu kabisa wa First Lady , lakini pia kuna walinzi wengine wawili wa kiume na msichana.

“Njiro ndani ya dakika therathini wanakuja Ajenti kutoka NIS wakiongozwa na Ajent Dondwe ,Hakikisha mke wangu haongei na mtu yoyote mpaka muda huo”Aliongea Mheshimiwa Kamau na kisha akakata simu.

NIS ni kitengo cha kijasusi cha Kenya kinachokwenda kwa kirefu cha National Intelligency Security na kitengo hiki kilikuwa na wanausalama wake ndani ya Tanzania kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wanausalama wa TISS kuwa ndani ya Taifa la Kenya.

Baada ya kama dakika arobaini na tano ndio Ajenti kutoka kitengo cha ujasusi cha Taifa la Kenya walifika ndani ya ofisi hii ya Mama Issa.

“Madam naitwa Ajenti Dondwe na hawa ni wenzangu , tupo hapa kwa ajili ya kuimarisha usalama , kwa maagizo tiliopewa ni kuhakikisha unatoka ndani ya hii nchi pasipo kuongea na mtu yoyote kwa ajili ya usalama wako”Aliongea Ajenti Dondwe mara baada ya kuingia ndani ya hii ofisi.

“Ajenti Dondwe nipo hapa Tanzania kwa ajili ya kikazi na mpaka sasa hakuna tishio lolote linalohatarisaha usalama wangu”

“Madam tunakuheshimu kama First Lady wa Taifa letu la Kenya , lakini wakati huo huo tunatii maagizo kutoka kwa raisi wa Kenya”Aliongea Dondwe akiwa siriasi.

“Ajenti Njiro hakikisha hakuna mtu anaesogelea kituo hiki kwa mita mia moja kutoka barabarani , utaungana na Ajenti niliokuja nao , nyie wawili mtabaki na mimi hapa ndani”Aluongea Dondwe na Ajenti Njiro alimwangalia Madam kwa huruma na kisha akatoka.

Kwahio licha ya kwamba Dondwe alipewa mamlaka ya kuhakikisha mke wa Raisi anarudi Kenya pasipo kuongea chochote , lakini hakuwa na mamlaka ya kumbeba kwa ulazima bila ruhusa yake , ingekuwa ni kuvunja itifaki za kiheshima kwa mke wa Raisi na ndio maana walitaka kutumia mbinu ya ushawishi kwanza na Mbinu hio haikudhaa matunda kwa takribani lisaa limoja mpaka Roma anafika hapa ndani ya kituo.

Baada ya Dondwe kupata taarifa ya ujio wa mke wa Tajiri Azizi akiwa na familia yake , uso wake ulizidi kuwa mweusi kutokana na wasiwasi , bwana huyu alikuwa na maelekezo ya kuzuia familia hio kukutana kwa namna yoyote na Maina, licha y a kwamba alishindwa kuelewa nini kinaendelea aliona ni wajibu wake kutii kile ambacho ameagizwa na mkuu wake wa nchi , Wakati akiendelea kuwaza cha kufanya simu yake ilianza kuita na kuitoa mfukoni.

“Dondwe mmefikia wapi mpaka sasa?”Aliuliza Mheshimiw Kamau aliekuwa kwenye hali ya wasiwasi.

“Madam Kagoma kabisa kutoa ushirikiano mheshimiwa , nahitaji amri yako nitumie nguvu”Aliongea Dondwe na kimya kikatawala kwa sekunde kama tano.

“Mpe Maina simu”Aliongea Kamau na Dondwe alifanya kama alivyoelekezwa .

“Kamau kwannini unanifanyia hivi?”

“Maina Jambo ambalo unataka kufanya linaniweka katika wakati mgumu , hebu nifikirie japo kidogo ni madhara gani yatatokea ukifanya hivyo”

“Kamau labda haujawahi kunifahamu , nilishafanya maamuzi tokea siku ya kwanza naingia ndani ya ikulu ya Wananchi wa kenya hii siku ikifika lazima niweke ukweli wote wazi”Aliongea Maina kwa hasira.

“Blandina mke wangu , najua mateso yako lakini hebu nifikirie kidogo kama kweli unanipenda , Please Blandina nipe muda wa miaka miwili”Licha ya mheshimiwa kuonekana kutumia kila mbinu ya kumshawishi Maina , lakini mwanamama huyu alishupaza shingo , alikuwa ashafanya maamuzi tayari mpaka kwa kufikia hapo.

Kamau wewe ni mbinafsi sana, lazima nionane na familia yangu , niashachoka”Aliwaza Mke wa raisi baada ya kukata simu na Dondwe kuichukua na muda huo huo iliita tena.

“Dondwe mnaruhusa yangu tumieni njia yoyote hata kumzimisha”

“Sawa Mheshimiwa”Alijibu Dondwe na kisha alikata simu na kumuangalia mke wa Raisi.

“Madam naomba utoe ushirikiano wako , kabla hatua kali Zaidi hazijafanyika kuhakikisha unatoka ndani ya hili taifa”Aliongea Dondwe na Maina alijikuta akijawa na wasiwasi , aliomba hata malaika atokee amuokoe katika hio hali .

Dondwe baada ya kuona hakuna dalili ya Madam President kutii agizo, alimsogeleea.

“Unataka kufanya nini dondwe , nakuambia usije ukanigusa”

“Samahani madam”Aliongea dondwe na palepale akamfinya shingoni Madam President na akazima na akawapa ishara ajenti wenzake wambebe.







SEHEMU YA 117

Roma alielezwa kwa ufupi sana na mke wa Tajiri Azizi juu ya sababu ya wao kuja ndani ya hiki kituo kwa siku hii ya leo.

“Kwahio mmepanga kuonana na mke wa Raisi wa Kenya ndani ya hiki kituo?”Aliuliza Roma ili aelewe vizuri na mama huuyu alitingisha kichwa , licha ya kwamba amemuelezea Roma , lakini ukweli ni kwamba mwanamama huyu hakuwa na matumaini yoyote na aliona kama jambo hili likishindikana ampigie mume wake simu ili kumuomba msaada , licha ya kwamba hawakuwa wamempa taarifa juu ya jambo hilo.

“Kama mnamiadi nae basi nadhani hawa walinzi wanafanyakosa kubwa la kuwazuia”Aliongea Roma na kumfanya mwanamama huyu asimuelewe Roma alichokuwa akimaanisha.

Njiro aliekuwa amesimama mita kadhaa , alikuwa na wasiwasi mno , katika maisha yake ya kazi ya usalama hakuwahi kukutana na hali kama hio ambayo inamfanya kushindwa kuwa na maamuzi ya moja kwa moja , mwanamke huyu alikuwa kwenye dilema.

“Eti dada unaitwa Ajenti Nani?”Aliuliza Roma baada ya kumsogelea.

“Hupaswi kufahamu jina langu , unachopaswa ni kuondoka hapa”

“Wewe unaongea kama nani?”Aliuliza Roma lakini Njiro alishindwa kumuelewa.

“Unamanisha nini?”

“Namaanisha kwamba hapa ni Tanzania , hivyo huwezi kutuambia cha kufanya kwenye nchi yetu si Ndio Mrs Azizi?”Aliuliza Roma na kumfanya Jestina atingishe kichwa.

“Acha kibuli wewe mwanaume , nadhani haunitambui vizuri , kama unataka uondoke huna meno endelea kunigomea”Aliongea Njiro kwa dharau na kumfanya Roma atabasamu na kumpima huyu mwanamke kwa sekunde.

Yezi aliekuwa kwenye gari alikuwa akitetemeka sana , alitamani kumwambia Roma waondoke waache kuleta fujo na watarudi hata siku nyingine.

“Fyuu…!!!,, Fyuu.. Fyuu. Fyuu”Haikueleweka mara moja ni spidi ya aina gani aliotumia Roma kwani aliwapiga wanausalama wote shingoni ndani ya sekunde nne, jambo la kushangaza ni kwamba licha ya hawa wanajeshi kupigwa ndani ya sekunde nne , walidondoka chini wote kwa wakati mmoja wakiwa hawajitambui na ni Dhahiri kwamba hata kama watakaposhituka baadae hawataelewa ni nini kilitokea kwao.

Kila mmoja alieshuhudia kile kilichotokea alishangaa mno sio Yezi , sio mke wa tajiri Azizi , sio Mlinzi , sio mzee Atanasi , wote hawakuelewa nini kilichotokea Zaidi ya kuona kitendo cha Roma kupotea na ile anaibuka wanausalama wote walidondoka chini, ni rahisi kusema hawakuona tukio la Roma kuwagonga shingoni wale walinzi kwani alitumia spidi kubwa sana na ukizingatia pia Walinzi walikuwa wameachana kwa mita kama moja hivi umbali.

“Roma umewafanya nini?”Aliuliza Mrs Azizi kwa mshangao , lakini Roma hakuwa na jibu.

“Mrs Azizi nadhani sio muda wa maswali huu”Aliongea Roma na kuwabeba wale walinzi na kuwaweka pembeni ya barabara na kisha akaingia kwenye gari na kuendesha pasipo kumjali Yezi ambaye yupo kwenye mshangao.

Dondwe baada ya kumzimisha Maina na vijana wake kumbeba alibonyeza kitufe chake shingoni ili kuwasiliana na wanausalama wenzake wa nje , lakini ajabu alikosa mawasiliano na kuanza kuingiwa na wasiwasi.

“Nyie wawili mshikilieni vizuri mkamuingize kwenye gari , tunaondoka ndani ya hili eneo”Aliongea Dondwe huku akimpa ishara mwanausalama mmoja atoe siraha yake na awe makini , huku na yeye akitoa yake.

Ndani ya hili eneo , hapakuwa na mtu kabisa na ilionekana tahadhari zilikuwa zimechukuliwa , kwani haikuwa kama ilivyozoeleka licha ya kwamba leo ilikuwa ni siku ya katikati ya wiki , watoto wote walionekaa kuwa ndani ya majengo yao na hata Mama Issa pia hakuonekana.

Ile Dondwe anafungua mlango wa geti kwa kulisikuma ili kuruhusu gari za ndani zitoke alishangaa kumuona Roma aliekuwa amesimama na ilionekana alikuwa na yeye anataka kufungua geti.

“Mr Usalama! ,Mke wa Raisi yuko wapi wageni wake washafika”Aliongea Roma pasipo kujali huku akinyooshea vidole gari zilizokuwa nyuma ya gari yake ,Dondwe alijikuta akiangalia mbali Zaidi ya magari na hapa ndipo alipoweza kushuhudia vijana wake wakiwa chini pembezoni mwa barabara.

“Kacha Kacha”.Dondwe alikoki siraha yake huku akimnyooshe Roma.

“Nyoosha mikono juu na kaa pembeni , ukisogea hatua moja tu nakuchangua ubongo wako”Aliongea Dondwe lakini Roma hakujali yaani ni kama alimuona Dondwe kashikilia ‘toy’.

“Mr Usalama licha ya kwamba sipendi bunduki , lakini vile vile siziogopi , ninachotaka ni Amani itawale bila ya kutumia nguvu”Aliongea Roma na wakati huo huo gari zilizokuwa ndani zilisogelea geti na zenyewe zikitaka kutoka na akashuka na mwanausalama mwingine akiwa na siraha yake mkononi.

Mrs Azizi alijikuta akiwa ni mwenye wasiwasi kweli, hakuwa akiona kinachoendelea mbele kutokana na kwamba gari ya Roma ilikuwa imewazibia,Roma baada ya kuona Dondwe hayiupo tayari kumsikiliza alitumia sipidi ile ile ya mwanzo kumdhibiti Dondwe na mwenzake na baada ya kuona amefanikiwa , aliwatoa njiani na kisha akasogelea gari iliokuwa ikiwashwasha taa za mbele ikiashria inataka kutoka.

Wale walinzi kwa jinsi walivyoshuhudia namna ambavyo Dondwe na mwenzao walivyonyamazishwa na Roma walijikuta wakiwa kwenye mshituko na hawakuelwa ni jambo gani la kufanya wakiti huo.

Roma alimpa ishara dereva asogeze gari lake pembeni na kisha ashuke na dereva mwanausalama alitii, na kusogeza pembeni na kisha akazima gari na Roma akawapa ishara watoke kwenye gari.

“Okey! Madam President yuko wapi?”Aliuliza Roma lakini wanausalama hawa walishindwa kujibu na hii ni kutokana na kwamba walikuwa kwenye mshituko bado na kuogopa kwa wakati mmoja.

Ni baada ya nusu saa hali ndani ya kituo ilirudi kawaida na Mama Issa alionekana kuwa na furaha kubwa baada ya kuonana na Yezi , mwanamama huyu alikuwa amekaa na Yezi eneo la nje , sehemu ya kupumzikia kwenye majengo haya ya utawala huku wakiongea kwa furaha, kwa jinsi walivyokuwa wakiongea nni kama hakukuwa na tukio lililokuwa limetokea dakika kadhaa nyuma.

Wanausalama wote walikuwa wamefungwa na Kamba ngumu miguuni na mikononi na Roma , akisaidiana na mlinzi wa mke wa tajiri Azizi na wote walikuwa wanajitambua kwani ile Roma anamaliza kuwafunga aliwaamsha.

Dondwe na Njiro hawakuelewa ni nini kimetokea na walishindwa hata kuongea Zaidi ya kumwangalia Roma aliekuwa hana hata habari nao huku wakiwa na maswali mengi kwenye vichwa vyao , lakini sio maswali tu woga uliwajaa na wasiwasi kwa wakati mmoja , mpaka muda huo hawakujua Mke wa Raisi yuko wapi.

****

“Blandina nisikilize, kama hutaji nimwonyeshe hizi Picha Senga unatakiwa kukubali ninachokuambia”

“Kamau sikujua una roho ya kinyama namna hii?”

“Sina roho mbaya Blandina wewe ndio ulienilazimisha mimi kufanya haya yote , kumbuka tulipotoka mimi na wewe , nilikupenda wa kwanza , nikakufanyia kila kitu , lakini alipotokea tu Senga ukaamua kuniacha, unajua ni maaumivu gani nilipitia , huna haja ya kunilaumu kwa maamuzi yangu”

“Sikuwahi kukubalia Kamau kwa sisi kuwa wapenzi , kufanya kwetu mapenzi ilikuwa ni msukumo wa kimwili tu , lakini sikuwahi kukupenda Kamau na nilikuambia kabisa siku nikipata mwanaume ninaempenda tunaacha”

“Blandina kama haupo tayari uniambie sitaki kusikia ngonjera zako mabazo hazina ukweli , hii ni nafasi pekee niliokuwa nayo , nimetoka Kenya mpaka hapa Lampur kwasababu ya hii nafasi , siwezi kuichezea hata kidogo, kama hutaki niambie nimtumie Senga hizi picha , nadhani baada ya hapa mtaendelea kupendana sana”

“Usinifanyie hivyo Kamau, Sitaki kumsaliti Senga najua tuna hisitoria mimi na wewe lakini hayo yashapita naomba usimtumie Senga hizo picha”

“Sikia Blandina nafanya yote haya kwasababu nakupenda sana naomba kesho ughairishe kwenda China tutumie nafasi ya kesho na kesho kutwa na baada ya hapo nitakuacha na maisha yako, Blandina na nakuapia hizi picha nitafuta kama utakubali na sitokusumbua”

“Siwezi kufanya hivyo , Denisi ni mgonjwa na taratibu za kiusafiri zishafanyika tayari , siwezi kughairisha”

“Najua Denisi ni mgonjwa na ndio maana kesho ataondoka na Bite na wewe utabaki , ila sikulazimishi Blandina ,nikuambie tu muda utakao ingia kwenye ndege ndio muda ambao nitahakikisha hizi picha zinamfikia Senga”

Naam hayo ni mazungumzo ambayo yalikuwa yakifanyika ndani ya mgahawa mmoja katikati ya jiji la Kual Lampur , mazungumzo haya yalikuwa ni kati ya Blandina na Kamau Kamau na ilikuwa ni miaka Zaidi ya Ishirini iliopita wakati Blandina akiwa nchini Malaysia kwa ajili ya matibabu ya Denisi.

Baada ya siku kupita baada ya mazungumzo hayo kufanyika yaani saa saba mchana ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa uliokuwa ndani ya jiji hili la Kual Lampur , alionekana Blandina pamoja na mwanadada mmoja hivi mrefu mwemambamba ,Maji ya kunde aliekuwa akifahamika kwa jina la Bite wakiingia ndani ya jengo la wasafiri lililokuwa na maandishi makubwa ya ‘Departure’. Blandina alikuwa amemshikilia mkono mtoto mdogo wa miaka kama mitano hivi.

“Denis utatangulia na Mama Mdogo Bite, sawa mwanangu”

“Hapana mama twende wote”

“Nisikilize Denisi Mama yako ,utaenda na Mama mdogo kama tulivyoongea jana sawa?”Aliongea Blandina huku akimgusa Denisi kichwani kwa kumbembeleza.

“Bite nina dharula inayonitaka kubaki hapa Malaysia ile kesho nitafika , naomba utangulie ,taratibu zote za mapokezi zishafanyika kwa upande wa China”

“Sawa ila inabidi iwe kesho kweli , Denisi ni mgonjwa na anakuhitaji wewe Zaidi kuliko mtu yoyote”Aliongea Bite na kumfanya Blandina ajisikie vibaya, alikuwa ni mwenye huzuni mno kumuachia Denisi kwenda China peke yake.

“Nisamehe mwanangu , najua hali yako kwa sasa sio mbaya , ila nafanya haya yote kulinda ndoa yangu , nakupenda sana Denisi”Aliwaza Blandina wakati akiwaangalia Bite na Denisi wakitokomea kwenye mlango kuelekea kupanda ndege ya Shirika la M Airline.

“Blanidna hupaswi kuwa na mawazo tena , baada ya leo kesho utasafiri kwenda kumuona mwanao”Blamdina alijikuta akigutushwa na sauti ilio nyuma yake , sauti aliokuwa akiijua vyema kama ni ya Kamau.

Blandina hakutaka kuongea neno , alijikuta chozi likimtoka huku akitangulia mbele kutoka ndani ya jengo hili la uwanja wa ndege,moyo wake ulikuwa ukimuuma mno mpaka yeye alijishangaa.

Bite alijikuka akichangamka mara baada ya kukutana na mwanamke wa kiafrika ambaye alikuwa amekaa siti ya pembeni na yeye , mwanamke ambaye alikuwa amebeba mtoto mdogo.

“Mnaenda China kufanya nini?”Aliuliza yule mwanadada ambaye alijitambulisha kwa jina la Regina.

“Ni kwa ajili ya Denisi , ni mgonjwa “Alijibu Bite.

“Pole jamani , nini Zaidi?”

“Ana saratani ya Ubongo”Alijibu Bite na kumfanya mwanamama Regina amuonee huruma Denisi, alishangazwa na mtoto mdogo namna hio kuwa na saratani ya Ubongo.

“Na wewe mtoto wako anaitwa nani?”

“Lorraine”Alijibu huku akitabasamu.

“Una katoto kazuri mno”.

“Asante”Wadada hawa wawili yaani Regina na Bite waliacha kuongea mara baada ya kuambiwa wafunge mikanda kwani Ndege inataka kupaa.

Regina alikuwa na yeye akielekea nchini China akiwa na mtoto Lorraine na Bite alikuwa akielekea nchini China kumpeleka Denisi kwenye matibabu.

“Blandina najua unaniona kama mnyama , lakini baada ya tukio linaloenda kutokea muda mfupi ujao utanishukuru” Aliwaza Kamau Kamau wakati akiwa na Blandina kwenye Taxi. Na hio ilikuwa ni miaka Zaidi ya ishirini nyuma.

Kamau Kamau alionekana kujua kuna jambo ambalo linaenda kutokea muda mchache unaokuja , je kama ni kweli alifahamu vipi kutokana na tukio lenyewe na ilikuwaje Blandina akabakia kwake.

ITAENDELEA NEXT EPISODE MUDA WOWOTE KABLA YA SAA TATU





SEHEMU YA 118

Mheshimiwa Raisi Kamau alionekana kuwa na wasiwasi mwingi mno na hii ni baada ya kukosekana hewani kwa Dondwe na kumfanya kutofahamu ni nini kinaendelea nchini Tanzania.

Bwana huyu alijilaumu sana kumruhusu Maina kwenda Tanzania pasipo kuchukua tahadhari zozote.

Ukweli ni kwamba baada ya Maina kupanda ndege na baada ya masaa mawili kupita ndipo mheshimiwa alipopewa ujumbe na Deo kuwa inawezekana Madam anaenda kuonana na mke wa tajiri Azizi.

Baada ya mheshimiwa Kamau kupata hii taarifa , alitafuta namna ya kuhakikisha taarifa hio na hapo ndipo alipompigigia mtu wake aliempandikiza ndani ya familia ya Tajiri Azizi na ni kweli alipewa taarifa kwamba Mke wa Tajiri Azizi yaani Jestina alikuwa na ratiba ya kwenda kituo cha kulelea yatima cha Son And Daughter Orphanage, na mpaka hapo ndipo Kamau alipopata kujua jambo ambalo Maina alikuwa akilifanya , alishangaa sana na kuona ni kwanini Maina hakumshirikisha.

“Inanipasa kutulia naamini Blandina anataka tu kuonana na familia yake , na hatoongea Zaidi ya anayoyajua , napaswa kumuamini”Aliwaza Mheshimiwa Kamau huku akichukua maji kwenye glasi na kunywa kidogo ili kujituliza , lakini licha ya kujiambia maneno hayo bado bwana huyu alikosa utulivu kwenye akili yake.

*****

“Mheshimiwa Maina amefanikiwa kuonana na familia yake leo”Aliongea Linda mlinzi wa raisi Jeremy na kumfanya mzee huyu kutabasamu.

“Iliwezekana vipi Kamau akashindwa kumzuia mke wake?”

“Kwa taarifa za watu wetu nchini Tanzania wanasema raisi Kamau alijitahidi kuzuia , ila alishindwa kutokana na Roma kuingilia”Jeremy alitoa macho na kumwangalia Linda ni kama hajasikia vizuri.

“Ilikuwaje Roma akawa ndani ya hiko kituo?”

“Mpaka sasa sijapata taarifa Zaidi Mheshimiwa”.

“Hili swala sikudhania litatokea mapema hivi nadhani ni muda sasa wa kuanzisha mpango wangu niliokuwa nao miaka mingi , lakini bado namuonea huruma Senga”Aliongea Jeremy.

“Lakini Mheshimiwa Naamini Mheshimiwa Kamau hakuna anachokifahamu kuhusu mpango LADO”

“Linda unachoongea ni kweli na mimi nataka kuamini hivyo na nimekuwa nikijitahidi miaka na miaka kuamini hivyo , lakini mienendo ya Kamau haijawahi kunifanya nimwamini , kumbuka Kamau ndio mtu pekee aliekataa kuingia kwenye mpango TASAC licha ya kumlazimisha”

“Naelewa Mheshimiwa lakini bado naona ni swala ambalo linakosa muunganiko , maana swala la kupotea kwa ile ndege ni swala ambalo ni zito mno kwa mtu kama Kamau kulifahamu”Aliongea Linda na kumfanya Mheshimiwa Jeremy awaze kidogo.

“Nadhani swala hili tuangalie DS ya Tanzania watalitolea vipi maamuzi swala la Blandina, Endelea kufuatilia ni sababu gani Roma alikuwepo kwenye kituo cha Son And Daughter Orphanage”

“Sawa Mheshimiwa” Aliongea Linda na kisha akatoka.

DS ni kirefu cha maneno ya ‘Deep State’ au kwa Kiswahili unaweza kusema Serikali ya ndani,DS ni kikundi cha watu ndani ya nchi ambacho kinakuwa na nguvu ya kufanya maamuzi ya kisela katika Nyanja zote , hawa DS ni rahisi kusema wanauwezo wa kuamua ndani ya taifa raisi awe nani kutokana na nguvu yao na mara nyingi wanafanya kazi kwa siri sana.

******

Edna alijikuta akijishangaa kulala muda mrefu mno kuliko isivyokuwa kawaida , saa saba na nusu mrembo huyu alishituka kutoka usingizini na kuanza kukumbuka ni muda gani alilala maana alikuwa na nguvo alizovaa jana yake.

Ni Roma yule Shetani Sijui alinifanyia nini?”Mrembo huyu alionekana kukumbuka tukio lililotokea , alikumbuka namna ambavyo Roma alimkumbatia kwa nyuma na kwanzia hapo hakuelewa nini kiliendelea.

Edna alijinyanyua kivivu kitandani na kuangalia saa kupitia simu na hapa ndipo aliposhituka , hakuamini ilikuwa ni saa saba mchana , kwani licha ya kwamba alijua amelala muda mrefu , lakini hakujua kuwa siku ilikuwa ikikaribia kuisha , alikumbuka simu yake nyingine iliokuwa kwenye mkoba wake na kuitoa haraka na kuangalia ni nani kapiga na kweli kulikuwa na ‘missed calls’ nane kutoka kwa Monica lakini pia kulikuwa na ujumbe wa maandishi.

“Madam muwekezaji Yan Buwen kutoka China keshafika nchini , Nakupigia hupatikani nimesogeza ratiba ya wewe kuonana nae saa moja za leo jioni”

Ulikuwa ujumbe kutoka kwenye simu ya Edna hakukuwa na jumbe nyingine za muhimu Zaidi na kumfanya mwanamke huyu kuvuta pumzi ya afadhali.

“Miss umeamka?”Ilikuwa ni sauti ya Bi Wema aliekuwa akiandaa chakula mezani na kwa harufu tu ya chakula ilimfanya Edna kuhisi njaa.

“Nimelala sana Bi Wema leo , kwanini hamkuniamsha?”

“Roma alituambia tusikuamshe mpaka utakapo amka mwenyewe na sisi tuliona ni sawa maana ulifanya kazi sana wiki hii pasipo kupumzika”Aliongea Bi Wema na Edna hakubadili muonekano wake , ila alikuwa akiwazia ni nini Roma alimfanya mpaka kulala muda mrefu, alijua Roma sio mtu wa kawaida lakini hakudhania kama anaweza kumfanya pia mtu kulala muda mrefu.

“Miss Mbona haukuniambia kama Yezi amepatikana?”Aliongea Bi Wema na kumfanya Sophia ajiulize Yezi ni nani.

“Ndio Bi Wema nilisahau , mambo yalikuwa mengi ,Roma ndio kakuambia?”

“Ndio kaniambia leo asubuhi na kampeleka kituoni kuonana na Mama Issa”Edna alishangaa kwasababu hakuwa na hio taarifa.

******

Upande mwingine ndani ya hoteli ya Serena alionekana bwana mmoja hivi wa Kichina aliekuwa amevalia taulo la rangi nyeupe ndani ya hoteli hii akiwa ameshikilia glasi ya wine huku akiwa amevalia miwani yake , kwa kumuangalia tu bwana huyu utafahamu umri wake haukua ukizidi miaka Arobaini.

Wakati bwana huyu akiangalia mandhari ya nje yajiji hili , simu yake ya chumba iliita mfululizo na kumfanya ageuke na kuisogelea na kisha aliipokea.

“Mr Yan Una mgeni eneo la mapokezi anafahamika kwa jina la Scorpion”Aliongea mwanadada wa mapokezi na kumfanya Bwana huyu atabasamu na kisha alijibu kwa Kingereza kama amruhusu aje.

Baada ya kama dakika tano aliingia mlinzi wa kike wa mheshimiwa Kigombola aliekuwa akifahamika kwa jina la Scorpion , alikuwa amevalia mavazi yake ya suti nyeusi akiwa na miwani ya jua , licha ya mwanadada huyu kuwa na sura ngumu lakini leo hii alipendeza.

“Karibu sana Sciorpion , ni muda mrefu hatujawahi kuonana tokea uje Tanzania”Aliongea Yan Buwen huku akitabasamu lakini Scorpion hakutoa aina yoyote ya tabasamu mlinzi huyu alikuwa kauzu hatari.

“Umekuja Tanzania kufanya nini Yan Buwen?”Aliuiza Scorpion kwa sauti ya kibabe.

“Nadhani unajua kwanini nipo hapa Tanzania mpaka muda huu”

“Kama umekuja kwa ajili ya jiwe la Kimungu sahau , washalichukua Yamata”

“Hahaha..Scorpion Baada ya kuja Tanzania naona uwezo wako wa akili umeshuka kwa Zaidi ya asilimia hamsini , Watanzania wamekudumaza kama walivyodumaa”Aliongea Yan Buwen kwa kejeli.

“Unamaanisha nini?”

“Yamata wamepewa jiwe feki , hivi unamchukuliaje Hades wewe, ndio maana nakuambia uwezo wako umedumaa , ulivyokuwa chini yangu haukuwa hivyo Scorpion”Aliongea Yan Buwen na kumfanya Scorpion ashangae.

“Una uhakika ni jiwe feki?”

“Ndio maana nipo hapa Tanzania, The Don anataka hilo jiwe kwa namna yoyote na niimekuita tuonane ili unisaidie kuandaa mpango wa kupata jiwe hilo”.

“Mpango Gani unapanga ili hali unajua hatuna uwezo wa kupambana na Hades”

“Hatuna haja ya kupambana na Hades ,The Doni mwenyewe atapambana nae”Aliongea Yan Buwen kwa tabasamu na alionekana kuwa na shauku kubwa.

“Sasa kama The Don ndio anakwenda kupambana na Hades tunaandaa mpango wa nini?”Aliuliza Scorpion na Yan Buwen alikunywa kidogo kinywaji chake halafu akatabasamu.

“Yapo mambo mengi haufahamu Scorpion na siku sio nyingi utakuja kugundua angalau nusu yake , ujio wangu hapa Tanzania ni kutaka kuhakikisha kama jiwe hilo lipo hapa au Hades kalificha nje ya Tanzania , hio ndio sababu ya mimi kufika hapa Tanzania , lakini pia nadhani mpaka sasa haujafahamu kwanini The Don alikupa maagizo kukaa karibu na mheshimiwa Kigombola?”Scorpion alitngisha kichwa kuonyesha hajui.

“Okey ukikamilisha kazi nitakayokupa siku ya leo, nitakuambia kila kitu”Aliongea na kisha akanyanyuka na kutoa picha na kumpatia Scorpion”

“Nahitaji kusikia kifo cha huyo mtu kabla ya kesho asubuhi”Aliongea Yan buwen na Scorpion aliangalia hio picha na kisha akavuta pumzi.

“Kwahio hili ni dili , nakamilisha kifo cha huyo mtu na utaniambia kwanini The Don kanileta Tanzania”.

“Hahaha…Scorpion , hupaswi kuwa na wasiwasi licha ya kwamba naonekana kama mtu ambaye siaminiki , lakini kuhusu hilo nitakutimizia , Ndani ya dunia hii ni mimi pekee ambaye namfahamu The Don kwa kumuona Hata raisi wa Marekani anamsikia tu … hahahaha”

ITAENDELEA MONDAY.
 
NICHEKI WATSAPP 0687151346 KUOATA UTARATIBU WA MWENDELEZO , SISI HUKU WATSAPP TUPO SEHEMU YA 170
 
SEHEMU YA 116

Roma alimaliza taratibu zake zote baada ya kuamka na ni muda wa saa mbili kamili za asubuhi alishuka mpaka sebuleni kwa ajili ya kujipaitia kifungua kinywa kilichoandaliwa na BiWema.

“Bi Wema msimuamshe Edna muacheni alale mpaka atakaposhituka mwenyewe”Aliongea Roma mara baada ya kumsalimia Sophia na Bi Wema.

“Jana Miss na wewe mlirudi saa ngapi?”

“Tulirudi mapema tu , niliwakuta mnaangalia tamthilia yenu na siku taka kuwasumbua”Aliongea Roma na kila mtu akajiweka bize kuendelea kunywa chai ,huku Sophia akiibia ibia kumwangalia Roma , haikueleweka mrembo huyu alikuwa akifikiria nini.

Roma kama alivyopanga siku ya leo hakuwa kabisa na mpango wa kwenda kazini , alipanga kumpeleka Yezi kituoni ili akamsalimie Mama Issa, alipumzika kidogo kwenye chumba chake mpaka muda wa saa tatu kama na nusu za subuhi na alimpigia simu Yezi kwamba anamfuata sehemu ambayo amepanga na amkute amejiandaa.

Dakika chache mbele Roma alikuwa ashafika na alimkuta Yezi akiwa amesimama nje alievalia suruali yake ya jeans na jezi ya Yanga.

“Ingia twende Yezi”Aliongea Roma baada ya kusimamisha gari na kumuona Yezi amezubaa zubaa, huku pia wamama wa Kiswahili waliokuwa nje ya viubaraza vyao walihusudu gari ya Roma na kujiambia kwenye nafsi yao Danga lake Yezi ni bab kubwa.

Yezi ndio aliekuwa ametawala maongezi kwenye gari na kumfanya Roma kucheka , kwani alifurahishwa na baadhi ya stori za Yezi, na hii ilifanya safari yao kuchukua muda mfupi kuliko walivyotarajia , lakini baada ya kukaribia karibu na kituo hiki Yezi alijikuta akiwa kimya na kumfanya Roma amshangae.

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi Yezi ,Mama Issa atafurahi sana kukuona siku hii ya leo”Aliongea Roma kumtia moyo Yezi , kwani aliona mabadiliko yake na Yezi alivuta pumzi na kuitikia kwa kichwa.

Roma ile anaingiza gari yake upande wa kushoto wa hiki kituo mita kama mia hivi kutoka getini, alisimamishwa na watu watatu, wote wakiwa kwenye mavazi ya suti ,wawili wakiwa ni wanaume na mmoja alikuwa ni mwanamke, Roma alishangaa kwanini kasimamishwa na watu hawa ilihali anataka kuingia kituoni.

“Tunaomba mgeuze gari mrudi na mtakuja siku ya kesho au mrudi baadae”Aliongea yule mwanamke na alionekana ndio aliekuwa ni kiongoza.

“Kwanini nirudi kesho wakati nimepanga kuja kituoni leo?”

“Mr kuna swala la kiusalama linaendelea hapa ndani na hamruhusiwi kupita”Aliongea yule mwanaume mmoja aliekuwa pembeni ya yule mwanamke, na kwa jinsi mwanaume yule alivyoongea Roma aligundua kuwa ni mkenya kutokana na rafudhi yake.

“Anko tutarudi kesho wanaonekana kuwa wanausalama”

“Yezi tulia tushakuja tayari na siwezi kurudi tena”Aliongea Roma huku akifungua mlango na kutoka nje na kuwafanya hawa wanausalama kuzidi kupandwa na hasira , maana waliona Roma analeta ngumu.

“Mr acha kujitafutia matatizo , tushasema eneo hili hauwezi kuingia siku ya leo mpaka kesho kutokana na itifaki za kiusalama”

“Kwahio unamaansha huko ndani kuna mtu mzito kutoka serikalini?”Aliuliza Roma akiwa hana hata wasiwasi.

“Mpaka hapo nadhani ushaelewa , hivyo geuza gari yako na uondoke usitulazimishe tutumie nguv”.Roma kwanza aliona hii ngumu na haikueleweka alikuwa akiwaza nini kwani alikuwa akikuna kichwa chake , aligeuka nyuma na kumwangalia Yezi ambaye alionekana kuwa na wasiwasi na hawa walinzi wote walikuwa wameshikilia Siraha za moto.

Wakati Roma akiwa amesimama pasipo kufanya jambo , ziliingia gari nyingine tatu eneo hili kwa upande wa nyuma na kuwafanya hawa walinzi wote waziangalie.

Gari moja ilikuwa nyeupe na mbili zilikuwa ni nyeusi moja ikiwa ni Mercedez Benz S-class na mbili zote zilikuwa ni gari kubwa aina ya V8, sasa barabara hii ya kuingia kituoni ilikuwa ni ndogo na ilikuwa ikiruhusu gari moja kwa wakati kupita na hivyo kitendo cha Roma kusimamisha gari yake ni kwamba alikuwa amezuia gari za nyuma yake kushindwa kupita.

“Kuna nini kinaendelea hapa?, tunataka kuingia kituoni mmezuia barabara”Aliongea bwana mmoja alievalia mavazi ya suti , alionekana alikuwa ni moja ya walinzi ambao wamekuja na gari hizo.

“Ajent Dondwe familia ya Mzee Atanasi imeshafika , nini tunapaswa kufanya?”Yule mwanamke alibonyeza kifaa chake sikioni na kuongea hayo maneno na ilionesha alikuwa akiwasiliana na waliokuwa ndani ya kituo, na baada kuongea hayo maneno alionekana kupewa maelekezo mengine na almpita Roma na kuelekea kwenye gari zilizokuwa nyuma , lakini kabla hata hajafika , alishuka mwanamama ambaye baada ya Roma kumwangalia tu alimfahamu, alikuwa ni Jestina mke wa tajiri Azizi , alijiuliza mwanamama huyu anafanya nini hapa.

“Madam unapaswa kurudi kwa siku ya leo , kuna itifaki za kiusalama zinazoendelea ndani ya hili eneo na haruhusiwi mtu yoyote kuingia kwa sasa”Aliongea yule Ajenti wa kike na kumfanya mwanamama huyu kushangaa , lakini macho yake pia alikuwa ameyaelekeza kwa Roma na yeye alijiuliza ni jambo gani ambalo limemleta Roma hapo kituoni.

“Kuna nini kinaendelea ambacho kinanifanya nisiingie ndani ya hiki kituo?”Aliuliza Jestina kwa mshangao na mpaka kufikia hali hio aliokuwa akiishuhudia , aliamini mpango wa kuonana na dada yake unakwenda kukwama.

“Lazima nionane na dada yangu kwa namna yoyote leo , najua hizi ni mbinu za kunizuia nisionane nae”Aliwaza mwanamama huyu huku akimwangalia Roma kwa sekunde na kisha akageuza na kwenda mpaka gari ya katikati , sio ile aliotoka ni ile ambayo ilikuwa ni ndogo aina ya Mercedez.

“Baba! Inaonekana walinzi wa raisi wa Kenya wanatuzuia tusionane na Blandina”Aliongea Jestina baada ya kioo kushushwa na ndani ya gari hio alionekana mzee Atanasi akiwa ameegamia kiti akiwa ameshikilia fimbo yake.

Upande wa ndani ya hiki kituo , ndani ya ofisi ya Mama Issa anaonekana Maina akiwa kwenye sura yake bandia huku akiwa amezungukwa na walinzi waliovalia suti nyeusi na mashati ya rangi yeupe , huku wakiwa wote wamevalia ‘Ear pieces’.

“Madam!, Mheshimiwa Raisi anataka urudi Kenya mara moja na hauruhusiwi kuongea na mtu yoyote ndani ya Tanzania mpaka utakapofika Kenya “Aliongea bwana mmoja hivi aliekuwa na mwili mkubwa kuliko wanausalama wote na alionekana ndio aliekuwa ni kiongozi.

“Siwezi kurudi Kenya pasipo kutimiza kile kilichonileta hapa, mwambieni hivyo Kamau”Aliongea Maina kwa hasira.

“Madam unafanya kazi yetu kuwa ngumu , tunaomba utoe ushirikiano”

“Nadhani hujayalewa maneno yangu , nishasema siwezi kutoka hapa pasipo kuoanana na mtu ambaye nimepanga kuonana nae na mtu yoyote asije akanigusa”Aliongea Maina na kufanya walinzi hawa waangaliane.

Walinzi hawa kazi yao waliona kuwa ngumu katika siku zote ambazo wamewahi kuhudumu kwa kumlinda mke wa Raisi Kamau, licha ya kwamba siku zote walinzi hawa walikuwa wakipokea maagizo kutoka kwa mke wa Raisi , lakini leo hii mara baada tu ya kuingia ndani ya kituo hiki , walipigiwa simu na mheshimiwa mwenyewe kutoka Kenya, akiwapa maagizo ya kumrudisha mke wake haraka nchini na haruhusiwi kuongea na mtu yoyote kwa usalama wake, na kwa maagizo hayo hata Mama Issa hakuruhusiwa kabisa kuongea nae na ndio maana hakuwepo kabisa kwenye hiko chumba cha ofisi.

Licha ya kwamba walinzi hawa hawakupewa maelekezo ya kutosha kutoka kwa muheshimiwa , lakini ilibidi watii oda ya raisi na mbaya Zaidi hakukuwa na maelekezo mengine ambayo yalikuwa yametolewa kwao na hii ilikuwa ni saa mbili za asubuhi muda mfupi baada ya Maina kufika hapo kituoni.

Sasa hawa walinzi walijitahidi kumueleza Maina juu ya agizo kutoka kwa mheshimiwa Raisi kumtaka Maina arudi nchini mara moja , lakini Maina hakutaka kurudi , alijua Kamau lazima atakuwa ashajua kuwa anakuja kuonana na familia yake na ndio maana alikuwa akitaka kuzuia jaribio hilo , hivyo aliona leo pasipo kutimiza azima yake anaweza asifanikiwe kabisa na ndio maana alileta ngumu na hii iliwafanya waljnzi hawa wapate ugumu wa kutekeleza maagizo , kwani licha ya kwamba walipewa oda , lakini pia walikuwa wakimheshimu mke wa raisi ,kwani walifanya nae kazi kwa muda mrefu sana hivyo unaweza ukasema kwamba walikuwa ‘Half loyal’ kwa Maina.

Baada ya Maina kuweka ngumu , hawa walinzi wa kitengo cha Secret service ilibidi wawasiliane na mheshimiwa kueleza kwamba madam hataki kurudi na jambo hili lilimkasirisha sana Mheshimiwa.

“Naona mnashindwa kufanya kazi yenu kwa weledi Njiro?”

“Hapana mheshimiwa Madam kagoma kutoa ushirikiano”

Kikawaida mke wa Raisi wa Kenya alikuwa akilindwa na walinzi wanne na ni hao ambao alikuwa akitembea nao kila mahali, na hawa walinzi alikuwepo Njiro ambaye ndio aliekuwa msaidizi wa karibu kabisa wa First Lady , lakini pia kuna walinzi wengine wawili wa kiume na msichana.

“Njiro ndani ya dakika therathini wanakuja Ajenti kutoka NIS wakiongozwa na Ajent Dondwe ,Hakikisha mke wangu haongei na mtu yoyote mpaka muda huo”Aliongea Mheshimiwa Kamau na kisha akakata simu.

NIS ni kitengo cha kijasusi cha Kenya kinachokwenda kwa kirefu cha National Intelligency Security na kitengo hiki kilikuwa na wanausalama wake ndani ya Tanzania kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wanausalama wa TISS kuwa ndani ya Taifa la Kenya.

Baada ya kama dakika arobaini na tano ndio Ajenti kutoka kitengo cha ujasusi cha Taifa la Kenya walifika ndani ya ofisi hii ya Mama Issa.

“Madam naitwa Ajenti Dondwe na hawa ni wenzangu , tupo hapa kwa ajili ya kuimarisha usalama , kwa maagizo tiliopewa ni kuhakikisha unatoka ndani ya hii nchi pasipo kuongea na mtu yoyote kwa ajili ya usalama wako”Aliongea Ajenti Dondwe mara baada ya kuingia ndani ya hii ofisi.

“Ajenti Dondwe nipo hapa Tanzania kwa ajili ya kikazi na mpaka sasa hakuna tishio lolote linalohatarisaha usalama wangu”

“Madam tunakuheshimu kama First Lady wa Taifa letu la Kenya , lakini wakati huo huo tunatii maagizo kutoka kwa raisi wa Kenya”Aliongea Dondwe akiwa siriasi.

“Ajenti Njiro hakikisha hakuna mtu anaesogelea kituo hiki kwa mita mia moja kutoka barabarani , utaungana na Ajenti niliokuja nao , nyie wawili mtabaki na mimi hapa ndani”Aluongea Dondwe na Ajenti Njiro alimwangalia Madam kwa huruma na kisha akatoka.

Kwahio licha ya kwamba Dondwe alipewa mamlaka ya kuhakikisha mke wa Raisi anarudi Kenya pasipo kuongea chochote , lakini hakuwa na mamlaka ya kumbeba kwa ulazima bila ruhusa yake , ingekuwa ni kuvunja itifaki za kiheshima kwa mke wa Raisi na ndio maana walitaka kutumia mbinu ya ushawishi kwanza na Mbinu hio haikudhaa matunda kwa takribani lisaa limoja mpaka Roma anafika hapa ndani ya kituo.

Baada ya Dondwe kupata taarifa ya ujio wa mke wa Tajiri Azizi akiwa na familia yake , uso wake ulizidi kuwa mweusi kutokana na wasiwasi , bwana huyu alikuwa na maelekezo ya kuzuia familia hio kukutana kwa namna yoyote na Maina, licha y a kwamba alishindwa kuelewa nini kinaendelea aliona ni wajibu wake kutii kile ambacho ameagizwa na mkuu wake wa nchi , Wakati akiendelea kuwaza cha kufanya simu yake ilianza kuita na kuitoa mfukoni.

“Dondwe mmefikia wapi mpaka sasa?”Aliuliza Mheshimiw Kamau aliekuwa kwenye hali ya wasiwasi.

“Madam Kagoma kabisa kutoa ushirikiano mheshimiwa , nahitaji amri yako nitumie nguvu”Aliongea Dondwe na kimya kikatawala kwa sekunde kama tano.

“Mpe Maina simu”Aliongea Kamau na Dondwe alifanya kama alivyoelekezwa .

“Kamau kwannini unanifanyia hivi?”

“Maina Jambo ambalo unataka kufanya linaniweka katika wakati mgumu , hebu nifikirie japo kidogo ni madhara gani yatatokea ukifanya hivyo”

“Kamau labda haujawahi kunifahamu , nilishafanya maamuzi tokea siku ya kwanza naingia ndani ya ikulu ya Wananchi wa kenya hii siku ikifika lazima niweke ukweli wote wazi”Aliongea Maina kwa hasira.

“Blandina mke wangu , najua mateso yako lakini hebu nifikirie kidogo kama kweli unanipenda , Please Blandina nipe muda wa miaka miwili”Licha ya mheshimiwa kuonekana kutumia kila mbinu ya kumshawishi Maina , lakini mwanamama huyu alishupaza shingo , alikuwa ashafanya maamuzi tayari mpaka kwa kufikia hapo.

Kamau wewe ni mbinafsi sana, lazima nionane na familia yangu , niashachoka”Aliwaza Mke wa raisi baada ya kukata simu na Dondwe kuichukua na muda huo huo iliita tena.

“Dondwe mnaruhusa yangu tumieni njia yoyote hata kumzimisha”

“Sawa Mheshimiwa”Alijibu Dondwe na kisha alikata simu na kumuangalia mke wa Raisi.

“Madam naomba utoe ushirikiano wako , kabla hatua kali Zaidi hazijafanyika kuhakikisha unatoka ndani ya hili taifa”Aliongea Dondwe na Maina alijikuta akijawa na wasiwasi , aliomba hata malaika atokee amuokoe katika hio hali .

Dondwe baada ya kuona hakuna dalili ya Madam President kutii agizo, alimsogeleea.

“Unataka kufanya nini dondwe , nakuambia usije ukanigusa”

“Samahani madam”Aliongea dondwe na palepale akamfinya shingoni Madam President na akazima na akawapa ishara ajenti wenzake wambebe.







SEHEMU YA 117

Roma alielezwa kwa ufupi sana na mke wa Tajiri Azizi juu ya sababu ya wao kuja ndani ya hiki kituo kwa siku hii ya leo.

“Kwahio mmepanga kuonana na mke wa Raisi wa Kenya ndani ya hiki kituo?”Aliuliza Roma ili aelewe vizuri na mama huuyu alitingisha kichwa , licha ya kwamba amemuelezea Roma , lakini ukweli ni kwamba mwanamama huyu hakuwa na matumaini yoyote na aliona kama jambo hili likishindikana ampigie mume wake simu ili kumuomba msaada , licha ya kwamba hawakuwa wamempa taarifa juu ya jambo hilo.

“Kama mnamiadi nae basi nadhani hawa walinzi wanafanyakosa kubwa la kuwazuia”Aliongea Roma na kumfanya mwanamama huyu asimuelewe Roma alichokuwa akimaanisha.

Njiro aliekuwa amesimama mita kadhaa , alikuwa na wasiwasi mno , katika maisha yake ya kazi ya usalama hakuwahi kukutana na hali kama hio ambayo inamfanya kushindwa kuwa na maamuzi ya moja kwa moja , mwanamke huyu alikuwa kwenye dilema.

“Eti dada unaitwa Ajenti Nani?”Aliuliza Roma baada ya kumsogelea.

“Hupaswi kufahamu jina langu , unachopaswa ni kuondoka hapa”

“Wewe unaongea kama nani?”Aliuliza Roma lakini Njiro alishindwa kumuelewa.

“Unamanisha nini?”

“Namaanisha kwamba hapa ni Tanzania , hivyo huwezi kutuambia cha kufanya kwenye nchi yetu si Ndio Mrs Azizi?”Aliuliza Roma na kumfanya Jestina atingishe kichwa.

“Acha kibuli wewe mwanaume , nadhani haunitambui vizuri , kama unataka uondoke huna meno endelea kunigomea”Aliongea Njiro kwa dharau na kumfanya Roma atabasamu na kumpima huyu mwanamke kwa sekunde.

Yezi aliekuwa kwenye gari alikuwa akitetemeka sana , alitamani kumwambia Roma waondoke waache kuleta fujo na watarudi hata siku nyingine.

“Fyuu…!!!,, Fyuu.. Fyuu. Fyuu”Haikueleweka mara moja ni spidi ya aina gani aliotumia Roma kwani aliwapiga wanausalama wote shingoni ndani ya sekunde nne, jambo la kushangaza ni kwamba licha ya hawa wanajeshi kupigwa ndani ya sekunde nne , walidondoka chini wote kwa wakati mmoja wakiwa hawajitambui na ni Dhahiri kwamba hata kama watakaposhituka baadae hawataelewa ni nini kilitokea kwao.

Kila mmoja alieshuhudia kile kilichotokea alishangaa mno sio Yezi , sio mke wa tajiri Azizi , sio Mlinzi , sio mzee Atanasi , wote hawakuelewa nini kilichotokea Zaidi ya kuona kitendo cha Roma kupotea na ile anaibuka wanausalama wote walidondoka chini, ni rahisi kusema hawakuona tukio la Roma kuwagonga shingoni wale walinzi kwani alitumia spidi kubwa sana na ukizingatia pia Walinzi walikuwa wameachana kwa mita kama moja hivi umbali.

“Roma umewafanya nini?”Aliuliza Mrs Azizi kwa mshangao , lakini Roma hakuwa na jibu.

“Mrs Azizi nadhani sio muda wa maswali huu”Aliongea Roma na kuwabeba wale walinzi na kuwaweka pembeni ya barabara na kisha akaingia kwenye gari na kuendesha pasipo kumjali Yezi ambaye yupo kwenye mshangao.

Dondwe baada ya kumzimisha Maina na vijana wake kumbeba alibonyeza kitufe chake shingoni ili kuwasiliana na wanausalama wenzake wa nje , lakini ajabu alikosa mawasiliano na kuanza kuingiwa na wasiwasi.

“Nyie wawili mshikilieni vizuri mkamuingize kwenye gari , tunaondoka ndani ya hili eneo”Aliongea Dondwe huku akimpa ishara mwanausalama mmoja atoe siraha yake na awe makini , huku na yeye akitoa yake.

Ndani ya hili eneo , hapakuwa na mtu kabisa na ilionekana tahadhari zilikuwa zimechukuliwa , kwani haikuwa kama ilivyozoeleka licha ya kwamba leo ilikuwa ni siku ya katikati ya wiki , watoto wote walionekaa kuwa ndani ya majengo yao na hata Mama Issa pia hakuonekana.

Ile Dondwe anafungua mlango wa geti kwa kulisikuma ili kuruhusu gari za ndani zitoke alishangaa kumuona Roma aliekuwa amesimama na ilionekana alikuwa na yeye anataka kufungua geti.

“Mr Usalama! ,Mke wa Raisi yuko wapi wageni wake washafika”Aliongea Roma pasipo kujali huku akinyooshea vidole gari zilizokuwa nyuma ya gari yake ,Dondwe alijikuta akiangalia mbali Zaidi ya magari na hapa ndipo alipoweza kushuhudia vijana wake wakiwa chini pembezoni mwa barabara.

“Kacha Kacha”.Dondwe alikoki siraha yake huku akimnyooshe Roma.

“Nyoosha mikono juu na kaa pembeni , ukisogea hatua moja tu nakuchangua ubongo wako”Aliongea Dondwe lakini Roma hakujali yaani ni kama alimuona Dondwe kashikilia ‘toy’.

“Mr Usalama licha ya kwamba sipendi bunduki , lakini vile vile siziogopi , ninachotaka ni Amani itawale bila ya kutumia nguvu”Aliongea Roma na wakati huo huo gari zilizokuwa ndani zilisogelea geti na zenyewe zikitaka kutoka na akashuka na mwanausalama mwingine akiwa na siraha yake mkononi.

Mrs Azizi alijikuta akiwa ni mwenye wasiwasi kweli, hakuwa akiona kinachoendelea mbele kutokana na kwamba gari ya Roma ilikuwa imewazibia,Roma baada ya kuona Dondwe hayiupo tayari kumsikiliza alitumia sipidi ile ile ya mwanzo kumdhibiti Dondwe na mwenzake na baada ya kuona amefanikiwa , aliwatoa njiani na kisha akasogelea gari iliokuwa ikiwashwasha taa za mbele ikiashria inataka kutoka.

Wale walinzi kwa jinsi walivyoshuhudia namna ambavyo Dondwe na mwenzao walivyonyamazishwa na Roma walijikuta wakiwa kwenye mshituko na hawakuelwa ni jambo gani la kufanya wakiti huo.

Roma alimpa ishara dereva asogeze gari lake pembeni na kisha ashuke na dereva mwanausalama alitii, na kusogeza pembeni na kisha akazima gari na Roma akawapa ishara watoke kwenye gari.

“Okey! Madam President yuko wapi?”Aliuliza Roma lakini wanausalama hawa walishindwa kujibu na hii ni kutokana na kwamba walikuwa kwenye mshituko bado na kuogopa kwa wakati mmoja.

Ni baada ya nusu saa hali ndani ya kituo ilirudi kawaida na Mama Issa alionekana kuwa na furaha kubwa baada ya kuonana na Yezi , mwanamama huyu alikuwa amekaa na Yezi eneo la nje , sehemu ya kupumzikia kwenye majengo haya ya utawala huku wakiongea kwa furaha, kwa jinsi walivyokuwa wakiongea nni kama hakukuwa na tukio lililokuwa limetokea dakika kadhaa nyuma.

Wanausalama wote walikuwa wamefungwa na Kamba ngumu miguuni na mikononi na Roma , akisaidiana na mlinzi wa mke wa tajiri Azizi na wote walikuwa wanajitambua kwani ile Roma anamaliza kuwafunga aliwaamsha.

Dondwe na Njiro hawakuelewa ni nini kimetokea na walishindwa hata kuongea Zaidi ya kumwangalia Roma aliekuwa hana hata habari nao huku wakiwa na maswali mengi kwenye vichwa vyao , lakini sio maswali tu woga uliwajaa na wasiwasi kwa wakati mmoja , mpaka muda huo hawakujua Mke wa Raisi yuko wapi.

****

“Blandina nisikilize, kama hutaji nimwonyeshe hizi Picha Senga unatakiwa kukubali ninachokuambia”

“Kamau sikujua una roho ya kinyama namna hii?”

“Sina roho mbaya Blandina wewe ndio ulienilazimisha mimi kufanya haya yote , kumbuka tulipotoka mimi na wewe , nilikupenda wa kwanza , nikakufanyia kila kitu , lakini alipotokea tu Senga ukaamua kuniacha, unajua ni maaumivu gani nilipitia , huna haja ya kunilaumu kwa maamuzi yangu”

“Sikuwahi kukubalia Kamau kwa sisi kuwa wapenzi , kufanya kwetu mapenzi ilikuwa ni msukumo wa kimwili tu , lakini sikuwahi kukupenda Kamau na nilikuambia kabisa siku nikipata mwanaume ninaempenda tunaacha”

“Blandina kama haupo tayari uniambie sitaki kusikia ngonjera zako mabazo hazina ukweli , hii ni nafasi pekee niliokuwa nayo , nimetoka Kenya mpaka hapa Lampur kwasababu ya hii nafasi , siwezi kuichezea hata kidogo, kama hutaki niambie nimtumie Senga hizi picha , nadhani baada ya hapa mtaendelea kupendana sana”

“Usinifanyie hivyo Kamau, Sitaki kumsaliti Senga najua tuna hisitoria mimi na wewe lakini hayo yashapita naomba usimtumie Senga hizo picha”

“Sikia Blandina nafanya yote haya kwasababu nakupenda sana naomba kesho ughairishe kwenda China tutumie nafasi ya kesho na kesho kutwa na baada ya hapo nitakuacha na maisha yako, Blandina na nakuapia hizi picha nitafuta kama utakubali na sitokusumbua”

“Siwezi kufanya hivyo , Denisi ni mgonjwa na taratibu za kiusafiri zishafanyika tayari , siwezi kughairisha”

“Najua Denisi ni mgonjwa na ndio maana kesho ataondoka na Bite na wewe utabaki , ila sikulazimishi Blandina ,nikuambie tu muda utakao ingia kwenye ndege ndio muda ambao nitahakikisha hizi picha zinamfikia Senga”

Naam hayo ni mazungumzo ambayo yalikuwa yakifanyika ndani ya mgahawa mmoja katikati ya jiji la Kual Lampur , mazungumzo haya yalikuwa ni kati ya Blandina na Kamau Kamau na ilikuwa ni miaka Zaidi ya Ishirini iliopita wakati Blandina akiwa nchini Malaysia kwa ajili ya matibabu ya Denisi.

Baada ya siku kupita baada ya mazungumzo hayo kufanyika yaani saa saba mchana ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa uliokuwa ndani ya jiji hili la Kual Lampur , alionekana Blandina pamoja na mwanadada mmoja hivi mrefu mwemambamba ,Maji ya kunde aliekuwa akifahamika kwa jina la Bite wakiingia ndani ya jengo la wasafiri lililokuwa na maandishi makubwa ya ‘Departure’. Blandina alikuwa amemshikilia mkono mtoto mdogo wa miaka kama mitano hivi.

“Denis utatangulia na Mama Mdogo Bite, sawa mwanangu”

“Hapana mama twende wote”

“Nisikilize Denisi Mama yako ,utaenda na Mama mdogo kama tulivyoongea jana sawa?”Aliongea Blandina huku akimgusa Denisi kichwani kwa kumbembeleza.

“Bite nina dharula inayonitaka kubaki hapa Malaysia ile kesho nitafika , naomba utangulie ,taratibu zote za mapokezi zishafanyika kwa upande wa China”

“Sawa ila inabidi iwe kesho kweli , Denisi ni mgonjwa na anakuhitaji wewe Zaidi kuliko mtu yoyote”Aliongea Bite na kumfanya Blandina ajisikie vibaya, alikuwa ni mwenye huzuni mno kumuachia Denisi kwenda China peke yake.

“Nisamehe mwanangu , najua hali yako kwa sasa sio mbaya , ila nafanya haya yote kulinda ndoa yangu , nakupenda sana Denisi”Aliwaza Blandina wakati akiwaangalia Bite na Denisi wakitokomea kwenye mlango kuelekea kupanda ndege ya Shirika la M Airline.

“Blanidna hupaswi kuwa na mawazo tena , baada ya leo kesho utasafiri kwenda kumuona mwanao”Blamdina alijikuta akigutushwa na sauti ilio nyuma yake , sauti aliokuwa akiijua vyema kama ni ya Kamau.

Blandina hakutaka kuongea neno , alijikuta chozi likimtoka huku akitangulia mbele kutoka ndani ya jengo hili la uwanja wa ndege,moyo wake ulikuwa ukimuuma mno mpaka yeye alijishangaa.

Bite alijikuka akichangamka mara baada ya kukutana na mwanamke wa kiafrika ambaye alikuwa amekaa siti ya pembeni na yeye , mwanamke ambaye alikuwa amebeba mtoto mdogo.

“Mnaenda China kufanya nini?”Aliuliza yule mwanadada ambaye alijitambulisha kwa jina la Regina.

“Ni kwa ajili ya Denisi , ni mgonjwa “Alijibu Bite.

“Pole jamani , nini Zaidi?”

“Ana saratani ya Ubongo”Alijibu Bite na kumfanya mwanamama Regina amuonee huruma Denisi, alishangazwa na mtoto mdogo namna hio kuwa na saratani ya Ubongo.

“Na wewe mtoto wako anaitwa nani?”

“Lorraine”Alijibu huku akitabasamu.

“Una katoto kazuri mno”.

“Asante”Wadada hawa wawili yaani Regina na Bite waliacha kuongea mara baada ya kuambiwa wafunge mikanda kwani Ndege inataka kupaa.

Regina alikuwa na yeye akielekea nchini China akiwa na mtoto Lorraine na Bite alikuwa akielekea nchini China kumpeleka Denisi kwenye matibabu.

“Blandina najua unaniona kama mnyama , lakini baada ya tukio linaloenda kutokea muda mfupi ujao utanishukuru” Aliwaza Kamau Kamau wakati akiwa na Blandina kwenye Taxi. Na hio ilikuwa ni miaka Zaidi ya ishirini nyuma.

Kamau Kamau alionekana kujua kuna jambo ambalo linaenda kutokea muda mchache unaokuja , je kama ni kweli alifahamu vipi kutokana na tukio lenyewe na ilikuwaje Blandina akabakia kwake.

ITAENDELEA NEXT EPISODE MUDA WOWOTE KABLA YA SAA TATU





SEHEMU YA 118

Mheshimiwa Raisi Kamau alionekana kuwa na wasiwasi mwingi mno na hii ni baada ya kukosekana hewani kwa Dondwe na kumfanya kutofahamu ni nini kinaendelea nchini Tanzania.

Bwana huyu alijilaumu sana kumruhusu Maina kwenda Tanzania pasipo kuchukua tahadhari zozote.

Ukweli ni kwamba baada ya Maina kupanda ndege na baada ya masaa mawili kupita ndipo mheshimiwa alipopewa ujumbe na Deo kuwa inawezekana Madam anaenda kuonana na mke wa tajiri Azizi.

Baada ya mheshimiwa Kamau kupata hii taarifa , alitafuta namna ya kuhakikisha taarifa hio na hapo ndipo alipompigigia mtu wake aliempandikiza ndani ya familia ya Tajiri Azizi na ni kweli alipewa taarifa kwamba Mke wa Tajiri Azizi yaani Jestina alikuwa na ratiba ya kwenda kituo cha kulelea yatima cha Son And Daughter Orphanage, na mpaka hapo ndipo Kamau alipopata kujua jambo ambalo Maina alikuwa akilifanya , alishangaa sana na kuona ni kwanini Maina hakumshirikisha.

“Inanipasa kutulia naamini Blandina anataka tu kuonana na familia yake , na hatoongea Zaidi ya anayoyajua , napaswa kumuamini”Aliwaza Mheshimiwa Kamau huku akichukua maji kwenye glasi na kunywa kidogo ili kujituliza , lakini licha ya kujiambia maneno hayo bado bwana huyu alikosa utulivu kwenye akili yake.

*****

“Mheshimiwa Maina amefanikiwa kuonana na familia yake leo”Aliongea Linda mlinzi wa raisi Jeremy na kumfanya mzee huyu kutabasamu.

“Iliwezekana vipi Kamau akashindwa kumzuia mke wake?”

“Kwa taarifa za watu wetu nchini Tanzania wanasema raisi Kamau alijitahidi kuzuia , ila alishindwa kutokana na Roma kuingilia”Jeremy alitoa macho na kumwangalia Linda ni kama hajasikia vizuri.

“Ilikuwaje Roma akawa ndani ya hiko kituo?”

“Mpaka sasa sijapata taarifa Zaidi Mheshimiwa”.

“Hili swala sikudhania litatokea mapema hivi nadhani ni muda sasa wa kuanzisha mpango wangu niliokuwa nao miaka mingi , lakini bado namuonea huruma Senga”Aliongea Jeremy.

“Lakini Mheshimiwa Naamini Mheshimiwa Kamau hakuna anachokifahamu kuhusu mpango LADO”

“Linda unachoongea ni kweli na mimi nataka kuamini hivyo na nimekuwa nikijitahidi miaka na miaka kuamini hivyo , lakini mienendo ya Kamau haijawahi kunifanya nimwamini , kumbuka Kamau ndio mtu pekee aliekataa kuingia kwenye mpango TASAC licha ya kumlazimisha”

“Naelewa Mheshimiwa lakini bado naona ni swala ambalo linakosa muunganiko , maana swala la kupotea kwa ile ndege ni swala ambalo ni zito mno kwa mtu kama Kamau kulifahamu”Aliongea Linda na kumfanya Mheshimiwa Jeremy awaze kidogo.

“Nadhani swala hili tuangalie DS ya Tanzania watalitolea vipi maamuzi swala la Blandina, Endelea kufuatilia ni sababu gani Roma alikuwepo kwenye kituo cha Son And Daughter Orphanage”

“Sawa Mheshimiwa” Aliongea Linda na kisha akatoka.

DS ni kirefu cha maneno ya ‘Deep State’ au kwa Kiswahili unaweza kusema Serikali ya ndani,DS ni kikundi cha watu ndani ya nchi ambacho kinakuwa na nguvu ya kufanya maamuzi ya kisela katika Nyanja zote , hawa DS ni rahisi kusema wanauwezo wa kuamua ndani ya taifa raisi awe nani kutokana na nguvu yao na mara nyingi wanafanya kazi kwa siri sana.

******

Edna alijikuta akijishangaa kulala muda mrefu mno kuliko isivyokuwa kawaida , saa saba na nusu mrembo huyu alishituka kutoka usingizini na kuanza kukumbuka ni muda gani alilala maana alikuwa na nguvo alizovaa jana yake.

Ni Roma yule Shetani Sijui alinifanyia nini?”Mrembo huyu alionekana kukumbuka tukio lililotokea , alikumbuka namna ambavyo Roma alimkumbatia kwa nyuma na kwanzia hapo hakuelewa nini kiliendelea.

Edna alijinyanyua kivivu kitandani na kuangalia saa kupitia simu na hapa ndipo aliposhituka , hakuamini ilikuwa ni saa saba mchana , kwani licha ya kwamba alijua amelala muda mrefu , lakini hakujua kuwa siku ilikuwa ikikaribia kuisha , alikumbuka simu yake nyingine iliokuwa kwenye mkoba wake na kuitoa haraka na kuangalia ni nani kapiga na kweli kulikuwa na ‘missed calls’ nane kutoka kwa Monica lakini pia kulikuwa na ujumbe wa maandishi.

“Madam muwekezaji Yan Buwen kutoka China keshafika nchini , Nakupigia hupatikani nimesogeza ratiba ya wewe kuonana nae saa moja za leo jioni”

Ulikuwa ujumbe kutoka kwenye simu ya Edna hakukuwa na jumbe nyingine za muhimu Zaidi na kumfanya mwanamke huyu kuvuta pumzi ya afadhali.

“Miss umeamka?”Ilikuwa ni sauti ya Bi Wema aliekuwa akiandaa chakula mezani na kwa harufu tu ya chakula ilimfanya Edna kuhisi njaa.

“Nimelala sana Bi Wema leo , kwanini hamkuniamsha?”

“Roma alituambia tusikuamshe mpaka utakapo amka mwenyewe na sisi tuliona ni sawa maana ulifanya kazi sana wiki hii pasipo kupumzika”Aliongea Bi Wema na Edna hakubadili muonekano wake , ila alikuwa akiwazia ni nini Roma alimfanya mpaka kulala muda mrefu, alijua Roma sio mtu wa kawaida lakini hakudhania kama anaweza kumfanya pia mtu kulala muda mrefu.

“Miss Mbona haukuniambia kama Yezi amepatikana?”Aliongea Bi Wema na kumfanya Sophia ajiulize Yezi ni nani.

“Ndio Bi Wema nilisahau , mambo yalikuwa mengi ,Roma ndio kakuambia?”

“Ndio kaniambia leo asubuhi na kampeleka kituoni kuonana na Mama Issa”Edna alishangaa kwasababu hakuwa na hio taarifa.

******

Upande mwingine ndani ya hoteli ya Serena alionekana bwana mmoja hivi wa Kichina aliekuwa amevalia taulo la rangi nyeupe ndani ya hoteli hii akiwa ameshikilia glasi ya wine huku akiwa amevalia miwani yake , kwa kumuangalia tu bwana huyu utafahamu umri wake haukua ukizidi miaka Arobaini.

Wakati bwana huyu akiangalia mandhari ya nje yajiji hili , simu yake ya chumba iliita mfululizo na kumfanya ageuke na kuisogelea na kisha aliipokea.

“Mr Yan Una mgeni eneo la mapokezi anafahamika kwa jina la Scorpion”Aliongea mwanadada wa mapokezi na kumfanya Bwana huyu atabasamu na kisha alijibu kwa Kingereza kama amruhusu aje.

Baada ya kama dakika tano aliingia mlinzi wa kike wa mheshimiwa Kigombola aliekuwa akifahamika kwa jina la Scorpion , alikuwa amevalia mavazi yake ya suti nyeusi akiwa na miwani ya jua , licha ya mwanadada huyu kuwa na sura ngumu lakini leo hii alipendeza.

“Karibu sana Sciorpion , ni muda mrefu hatujawahi kuonana tokea uje Tanzania”Aliongea Yan Buwen huku akitabasamu lakini Scorpion hakutoa aina yoyote ya tabasamu mlinzi huyu alikuwa kauzu hatari.

“Umekuja Tanzania kufanya nini Yan Buwen?”Aliuiza Scorpion kwa sauti ya kibabe.

“Nadhani unajua kwanini nipo hapa Tanzania mpaka muda huu”

“Kama umekuja kwa ajili ya jiwe la Kimungu sahau , washalichukua Yamata”

“Hahaha..Scorpion Baada ya kuja Tanzania naona uwezo wako wa akili umeshuka kwa Zaidi ya asilimia hamsini , Watanzania wamekudumaza kama walivyodumaa”Aliongea Yan Buwen kwa kejeli.

“Unamaanisha nini?”

“Yamata wamepewa jiwe feki , hivi unamchukuliaje Hades wewe, ndio maana nakuambia uwezo wako umedumaa , ulivyokuwa chini yangu haukuwa hivyo Scorpion”Aliongea Yan Buwen na kumfanya Scorpion ashangae.

“Una uhakika ni jiwe feki?”

“Ndio maana nipo hapa Tanzania, The Don anataka hilo jiwe kwa namna yoyote na niimekuita tuonane ili unisaidie kuandaa mpango wa kupata jiwe hilo”.

“Mpango Gani unapanga ili hali unajua hatuna uwezo wa kupambana na Hades”

“Hatuna haja ya kupambana na Hades ,The Doni mwenyewe atapambana nae”Aliongea Yan Buwen kwa tabasamu na alionekana kuwa na shauku kubwa.

“Sasa kama The Don ndio anakwenda kupambana na Hades tunaandaa mpango wa nini?”Aliuliza Scorpion na Yan Buwen alikunywa kidogo kinywaji chake halafu akatabasamu.

“Yapo mambo mengi haufahamu Scorpion na siku sio nyingi utakuja kugundua angalau nusu yake , ujio wangu hapa Tanzania ni kutaka kuhakikisha kama jiwe hilo lipo hapa au Hades kalificha nje ya Tanzania , hio ndio sababu ya mimi kufika hapa Tanzania , lakini pia nadhani mpaka sasa haujafahamu kwanini The Don alikupa maagizo kukaa karibu na mheshimiwa Kigombola?”Scorpion alitngisha kichwa kuonyesha hajui.

“Okey ukikamilisha kazi nitakayokupa siku ya leo, nitakuambia kila kitu”Aliongea na kisha akanyanyuka na kutoa picha na kumpatia Scorpion”

“Nahitaji kusikia kifo cha huyo mtu kabla ya kesho asubuhi”Aliongea Yan buwen na Scorpion aliangalia hio picha na kisha akavuta pumzi.

“Kwahio hili ni dili , nakamilisha kifo cha huyo mtu na utaniambia kwanini The Don kanileta Tanzania”.

“Hahaha…Scorpion , hupaswi kuwa na wasiwasi licha ya kwamba naonekana kama mtu ambaye siaminiki , lakini kuhusu hilo nitakutimizia , Ndani ya dunia hii ni mimi pekee ambaye namfahamu The Don kwa kumuona Hata raisi wa Marekani anamsikia tu … hahahaha”

ITAENDELEA MONDAY.
Shukrani sana mkuu
 
Back
Top Bottom