Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Dah Mkuu ungetupa kimoja cha mwisho ili tumalizie hapo kwa Roma kwanza maana duuu[emoji4]
 
SEHEMU YA 121

Grape hoteli ni moja ya hoteli maarufu sana ndani ya jiji la Dar ambayo wafanyabiashara wengi hupenda kufikia hapo kwa ajili ya mazunguzo ya kibiashara , moja ya sababu kubwa ambayo inaifanya hoteli hii kupendwa sana , ni kutokana na wateja wanavyopewa ‘high privacy’ kwa kile ambacho wanafanya pasipo kuingiliwa kwa namna yoyote ile na inasemekana moja ya mmiliki wa hoteli hii ni kigogo kutoka serikalini.

Wafanyabiashara wengi wa ulimwengu usionekana wanaita hoteli hii kama makao makuu ya ‘Underwold’ hii ikimaanisha kwamba yapo mambo mengi ambayo sio halali ambayo yanafanyika ndani ya hii hoteli na hakuna chombo chochote cha usalama ambacho kinaweza kuingia hapo ndani na kufanya ukaguzi wa aina yoyote ile.

Floor namba kumi na tisa ndio walikuja kutokea Edna na Roma na hii ni kutokana na maelekezo ya Yan Buwen, Floor hii ilikuwa ni kwa ajili ya VVIP , haikuwa na chumba chochote kwa ajili ya kulala bali kulikuwa na ukumbi mkubwa wa mikutano lakini pia ofisi ndogo mbalimbali zinazojitegemea.

“Madam Karibu sana”Aliongea General Manager wa Floor hii na Edna aliitikia kwa kichwa na ni kama walikuwa wakisubiriwa , GM aliwaongoza mpaka kwenye mlango uliokuwa na maandishi ya VIP ROOM NO 7.

Roma alikuwa akikagua eneo lolote kuhakikisha hakuna jambo ambalo linaweza kuleta shida kwa mke wake.

Edna na Roma baada ya kuingia ndani waliweza kumshuhudia mwanaume ambaye alikuwa amekaa kwenye masofa , alikuwa ni mwanaume ambaye amevalia suti na rangi nyeusi shati jeupe na tai nyekundu,Edna na Roma hawakumtambua mara moja bwana huyu katika wote wawili hawakuwahi kuonana na Yan Buwen.

“Karibu sana Miss Edna ,Naitwa Yan Buwenau unaweza kuniita Profesa Yan”Aliongea Yan Buwen kwa kuweka tabasamu.

“Ni jambo la furaha kukutana na wewe Mr Yan ana kwa ana, huyu ni ‘personal Asistatnt wangu anafahamika kwa jina la Roma Ramoni”Edna alimtambulisha Roma na Yan Buwen alimwangalia Roma na alionyesha hali ya kutofurahishwa na ujio wake na Roma aliligundua hilo , ila hakutaka kujali sana, Yan Buwen alimuonyesha Edna sehemu ya kukaa kwa mkono huyu akiweka tabasamu lake.

Kikao cha Yan Buwen na Edma kilidumu kwa Zaidi ya dakika kama kumi na tano hivi , Roma baada ya kuona Yan Buwen anazungumzia maswala ya uwekezaji , hakutaka kuingilia sana maongezi hayo, lakini pia Roma hakuona jambo lolote ambalo sio la kawaida kwa Yan Buwen.

Edna aliagana na Yan Buwen na kisha wakaingia kwenye lifr na kushuka mpaka chini na hatimae kufika eneo la maegesho ya magari , Roma alimfungulia mlango Edna na akaingia na akafuatia yeye upande wa Dereva.

“Mbona unaendesha gari uelekeo ambao sio wa nyumbani?”Aliuliza Edna baada ya kuona Roma baada ya kuelekea Kigamboni yeye alikuwa akielekea njia ya kwenda Mwenge.

“Wife mapema sana leo , tutatumia huu muda kula chakula cha usiku sehemu nzuri tulivu”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie na kisha sijui mrembo huyu alifikiria nini , ila hakutaka kusema maneno mengi , alitulia kwenye siti yake na kusubiri kuona ni wapi Roma anampeleka.

“Nilisahau kukuuliza kuhusu Yezi , vipi alionana na mama Issa?”

“Ndio ameonana nae na amefurahi , kalala hukohuko”Alijibu Roma na kumfanya Edna atingishwe kichwa.

Baada ya Roma kuendesha gari kama nusu saa hatimae alikuwa akiingiza gari ndani ya Upepo Beach Garden, sehemu ambayo siku zilizopita Roma alikuja na Neema Luwazo ndani ya hilo eneo na haikueleweka kwanini Roma akachagua hilo eneo.

Edna alionyesha kupendezwa na mazingira yaliokuwa hapa ndani , ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufika na ilikuwa ikishangaza kwani matajiri wengi ndani ya Taifa la Tanzani washafika ndani ya hili eneo , lakini Edna peke yake ndio ambaye hakuwahi kufika , licha ya kwamba mrembo huyu alikuwa na pesa nyingi.

“Umepajuaje hapa Roma?”Aliuliza Edna huku akishangaa kulia na kushoto na akiangalia baadhi pia ya watu waliokuwa hapa nani wakiwa na wenza wao.

“Alinileta Neema”Alijibu Roma huku akimshika mkono Edna na kumfanya mrembo huyu aangalie namna ambavyo ameshikwa mkono na alishindwa kuutoa.

Waliongozana mpaka sehemu ambayo Roma na Neema walikaa wiki chache zilizopita,Roma alimsogezea Edna kiti na akakaa na yeye pia akakaa na wakawa wanaangaliana.

“Kijana!!!”Aliita Mzee chino na kumfanya Roma ageuke na kutabasamu baada ya kumuona huyu mzee kwa mara ya pili.

“Mzee Chino nimetokea kupenda hili eneo”Aliongea Roma na Mzee Chino alitabasamu huku akimwangalia Edna ni kama alikuwa akimfananisha.

“Mzee Chino naona unamshangaa sana mke wangu,Edna huyu ni mzee Chino ndio anaemiliki hili eneo licha ya kwamba anaonekana kama masikini”Aliongea Roma akimtambulisha Edna.

“Haha..una maneno sana kijana , ila nikupe pongezi una mke mzuri sana,Karibu Sana Miss Edna”

“Asante”Alijibu Edna akiwa na tabasamu na Eda hakuacha kugeuka geuka kuangalia hayo mazingira.

“Mzee Chino tuletee Carribean Lobster Soup”

Aliongea Roma na kumfanya Edna ashangae , kwani licha ya kwamba alikuwa akikifahamu hiko chakula , lakini hakuwahi kukionja.

“Hakuna Shida Mr Roma , ila mkeo ni kama namfananisha na mfanyabishara mmoja mkubwa Tanzania”

“Unamfananisha na nani mzee Chino?, mimi nakuona kama haujamfananisha ila ushamfahamu”

“Haha… kijana unaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kumsoma mtu ,Miss Edna nakukaribisha sana kwenye mgahawa wangu , imekuwa heshima kwangu leo kutembelewa na mfanyabiashara mkubwa ndani ya taifa hili”Aliongea Mzee Chino huku akionyesha heshima kwa Edna ,Mzee huyu alionekana kumfahamu vyema , lakini pia alifurahia leo kumuona Edna akiwa amefika ndani ya mgahawa wake.

“Asante Mzee Chino”Aliongea Edna kwa sauti yake myororo na kutabasamu.

“Mr Roma!,Wewe ni hatari”Aliongea Mzee Chino kwa utani huku akiondoka na kumfanya Roma atoe tabasamu la uchungu, alijua alichokuwa anachomaanisha Mzee Chino ila alipanga kupotezea.

“Wife ushawahi kunywa Carribean Lobster Soup ?”Aliuliza Roma baada ya Mzee Chino kuleta mabakuli mawili na kuyaweka mbele ya Edna , ambaye alikuwa akishangaa , hakuwahi kula aina hio ya chakula.

“Nishawahi kula ‘Seafood’ kama vile Sushi, lakini sijawahi kunywa hii supu ya Lobster”Aliongea Edna huku akishika kijiko na kuzungusha zungusha kama mtu ambaye hakuwa na mpango wa kula na Roma alimwangalia anachokifanya Edna na kutabasamu.

Lobster kishwahili chake ni samaki aina ya Kamba ndio samaki ambaye anauzwa kwa bei kubwa sana ndani ya mahoteli , kilo moja ya Lobster inafikia Zaidi ya Elfu sabini za kitanzania.

“Kumbe tamu hivi?”Aliongea Edna kwa mshangao mara baada ya kuonja na kumfanya Roma atabasamu, alishindwa kuelewa kwanini mke wake hakuwahi kuonja chakula cha aina hio , wakati matajiri wengi hupendelea sana.

“Nichakula kitamu, lakini pia kina virutubisho vingi sana kwa ajili ya afya ya mwili , siku moja moja unapaswa kula cyakula vya aina hii”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie na kutingisha kichwa kukubaliana nae na kuendelea kula.

Ndani ya nusu saa mbele Roma na Edna walikuwa wakitembea upande wa fukwe hii Edna akiwa mbele na Roma akiwa nyuma,, Roma alijikuta akipendezwa na namna mke wake alivyokuwa akionekana ndani ya eneo hili , hususani kwa jinsi ambavyo alikuwa ameshikilia viatu vyake na kutembea.

Walitembea kwa umbali kama wa mita mia hivi na Edna akasimama huku akiangalia upande wa baharini , na sehemu waliosimama ni ile ile ambayo Roma na Neema luwazo walisimama, na Roma alijikuta akijiwazia na kumkumbuka Neema Luwazo alivyomkimbia siku ile , lakini pia namna ambavyo alimkumbatia na kuanza kubusiana,Kwa mawazo hayo ni kama Roma alipata ‘idea’ na alimsogelea Edna ambaye nywele zake zilikuwa zikipeperushwa na upepo na kisha akamkumbatia kwa nyma na kupitisha mikono kwa mbele, Edna alipata mshituko na kutaka kujitoa kwenye mikono ya Roma , ila Roma alimshikilia kwa nguvu , hakutaka kumpa nafasi hio hata kidogo

“Edna my Wife , I love you so much”Aliongea Roma na kumfanya Edna moyo wake upige kwa nguvu huku akiisikilizia pumzi ya Roma iliokuwa ikimpuliza shingoni, kwa wakati huu mrembo huyu alishindwa hata ajibu nini Zaidi ya kukodolea macho bahari ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukumbatiwa namna hio , lakini pia kuambiwa maneno hayo, hakuwa hata akijielewa kwa wakati huo na alishindwa pia kuelewa kwanini Roma ghafla tu akamwambia hayo maneno na alishindwa pia kuelewa ni hatua gani aichukue kwa wakati huo.

Roma aliemkumbatia Edna kwa nyuma alijikuta akitabasamu huku akifurahia marashi yanayotoka kwa mke wake,Ilikuwa ni picha ya kupendeza kwa namna ambavyo walikuwa wakionekana, na walisimama wakiwa wamekumbatiana kwa dakika kama mbili hivi mpaka pale Edna alipogeuza uso wake na kumwangalia Roma usoni na kadri walivyokuwa wakiangaliana ni kama kuna nguvu flani iliokuwa ikiwafanya wasogeleane.

“Moja , Mbili , Tatu..”Roma alianza kuhesabu kwenye akili yake na haikueleweka kwanini alikuwa akihesabu , lakini kabla hajatamka Nne , tayari Lipsi za Edna na Zake zilikuwa zishagusana.

Edna ambaye ilikuwa mara yake ya kwanza kufanya hivyo alijikuta automatic akitoa ulimi wake na Roma na yeye akaupokea na kilichoendelea hapo ,ilikuwa ni kunyonyana midomo , huku mrembo Edna akiwa amefumba macho na upande wa Roma hakuwa amefumba, Edna aliekuwa ameshikilia viatu vyake alijikuta akividondosha pasipo kuelewa vimedondoka muda Gani na Roma aliekuwa amepitisha mikono kwenye kiono cha Edna alizidi kumbana Edna kuelekea kwake
ITAENDELEA , KWA MWENDELEZO NICHEKI WATSAPP 0687151346
Kumekucha Roma na Edna[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Back
Top Bottom